Title November 2023

Je Yuda alienda wapi, ni mbinguni au jehanamu?

Hili ni moja ya maswali yanayoleta mkanganyiko miongoni mwa wakristo wengi? Baadhi wanaamini kile kitendo tu cha yeye kujutia makosa yake mpaka kupelekea kutoona faida ya kuishi hadi kwenda kujinyonga ni toba tosha, baadhi wanaamini tayari alikuwa ni mtume aliyechakuliwa na Yesu, hivyo hata iweje hawezi kwenda kuzimu, kwasababu Mungu hachagui vilivyo dhaifu. Lakini baadhi bado wanashikilia kuwa alikwenda kuzimu, kwasababu alikuwa mwizi na mwisho wa kifo chake ilikuwa ni kujinyonga. Na hiyo ni uthibitisho kuwa alipotea.

Lakini tuangalie maandiko yanatupa alama gani kuhusiana na hatma ya Yuda, ndipo tutakapoitimisha kwamba Yuda alikwenda wapi.

Bwana Yesu alisema maneno haya kwa Yuda;

Mathayo 26:24  Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa.

Pa kutilia umakini ni hilo Neno alilohitimisha nalo,  “Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa”.linatupa picha mbaya kwamba mtu huyo alikuwa  hana faida yoyote duniani, maisha yake ni kama bure.

Lakini pia, kuna maneno mengine ambayo Bwana Yesu aliyasema katika sala yake; Alisema..

Yohana 17:12  Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.

Kuonyesha kuwa Yuda alipotea.

Lakini andiko lingine, tunalisoma katika kitabu cha matendo ya mitume, wakati mitume wanapiga kura kuchagua mtume atakayesimama mahali pa Yuda. Nao pia walisema maneno haya;

Matendo 1:24  Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili, 25  ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. 26  Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.

Utaona hapo anasema “aende zake mahali pake mwenyewe”. Ikimaanisha kuwa Yuda hakwenda mbinguni bali mahali pake, na huko si kwingine zaidi ya  kuzimu.

Hivyo kwa vifungu hivyo vyote, hatuoni mahali popote maandiko yanatupa viashiria kuwa Yuda alikwenda mahali pazuri, ukizingatia kuwa katika hatua zake za mwisho hadi kujinyonga, biblia inatuambia aliingiwa na “shetani”. Maana yake ni kuwa shetani alifanya kiti cha enzi ndani yake, hivyo maamuzi yote aliyokuwa anayafanya yalisukumwa na yule mwovu, sio Mungu. Kwahiyo hakuna kitendo cha ki-Mungu alichokifanya Yuda tangu wakati ule.

Hili ni fundisho kubwa sana, hususani kwa watumishi wa Mungu. Bwana kukuita haimaanishi kuwa huwezi potea. Au huwezi ingiliwa na shetani. Petro aliteleza mara kadhaa, na alivamiwa na shetani kinywani mwake, lakini hakukubali kumpa adui nafasi, vivyo hivyo na wewe, hupaswi kusema mimi nina kanisa kubwa, mimi ninahubiri, mimi nimetokewa na Yesu. Kumbuka Yuda aliishi na Yesu kwa zaidi ya miaka mitatu, sio kutokewa nusu saa, lakini alianguka, kwasababu aliipa dhambi nafasi katika maisha yake.

Nasi pia tunapaswa tusimame, dhambi isichukue nafasi yoyote mioyoni mwetu. Kwasababu hiyo inaanza kama tamaa, kisha inachukua mimba, kisha inazaa mauti. Kaa mbali na dhambi.

Bwana atusaidie..

Je! Umeokoka? Je unahabari kuwa hizi ni siku za mwisho, na Yesu yupo mlangoni kurudi?. Umejiandaaje, unaishije, unatazamia nini baada ya haya maisha? Ni heri utubu dhambi zako sasa, umrejee Bwana, usamehewe dhambi zako, Kumbuka adui anakuwinda sana, usiishi maisha kama ya wanyama, wewe ni wa thamani, mbele za Mungu wako.  ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi waweza fungua hapa kwa msaada wa mwongozo wa sala ya Toba >>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Je ni kweli Yuda hakuwa na dhambi kwa kumsaliti Bwana, kwasababu tayari ilikuwa imeshatabiriwa?

JINSI BWANA ALIVYOWACHAGUA MITUME WAKE.

YUDA ISKARIOTE! MTUME ALIYECHAGULIWA NA BWANA YESU.

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

Kitabu hiki katika lugha ya kiebrania kinasomeka kama “Devarim” ambayo tafsiri yake ni “Maneno”

Na ndio maana mstari wa kwanza kabisa un itaanza Kwa kusema. “Haya ndiyo maneno”

Kumbukumbu la Torati 1:1

[1]Haya ndiyo maneno Musa aliyowaambia Israeli wote ng’ambo ya Yordani barani, katika Araba lililoelekea Sufu, kati ya Parani, na Tofeli, na Labani, na Hazerothi, na Dizahabu.

Lakini katika tafsiri ya kigiriki Cha kale (septuagint),  kilisomeka kama “deuteronomioni” chenye maana ya “Mrudio wa sheria” ambapo Kwa sisi kinasomeka kama “kumbukumbu la sheria/torati”. 

Ni kitabu Cha Tano ambacho kiliandikwa na Musa karibia na mwisho wa Ile miaka 40, wakati walipokuwa ng’ambo ya Yordani katika nchi ya Moabu.

Lengo la kuandikwa kitabu hicho ni kukumbushwa sheria na maagizo ya Mungu, kwasababu kundi kubwa la Wana wa Israeli lililopokea sheria Kule mlima Sinai mwanzoni, lilifia jangwani, hivyo kile kizazi kipya Hakikuwa na msingi imara juu ya sheria za Mungu. Na ndio hapa Musa anaagizwa na Mungu awakumbushe Wana wa Israeli sheria yake.

Kitabu hiki kimeanza kuwakumbushia safari Yao Toka Misri, pia kikagusia jukumu lao la kumpenda Mungu na kuzishika sheria zake. Ikafuatana na baraka na laana ambazo zitampata mtu katika kutii au kutokutii, na mwisho kifo cha Musa.

Je ni Nini tunajifunza kuwepo kwa kitabu hiki ? 

Bwana anataka na sisi tuweke kumbukumbu la agano lake mioyoni mwetu, Kwa vizazi vijavyo tupende kuwafundisha vizazi vinavyochipukia Neno la Mungu, tusiwaache tukadhani wataelewa tu wenyewe kisa biblia ipo, bila kukumbushwa Kwa kufundishwa.

Musa alifanya vile ndio maana kizazi kile kikawa imara baada ya pale.

Na sisi tuwe watu wenye tabia hii, Sio kwa watoto tu hata Kwa kondoo wa Bwana kanisani. Mara Kwa mara tuwakumbushe maagizo ya Mungu.

Kwa maelezo ya ziada kuhusu kitabu hichi pitia hapa >>> https://wingulamashahidi.org/2019/05/13/vitabu-vya-biblia-sehemu-ya-2/

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya ki-Mungu?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Nini maana ya “Atamwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake”. (2Wathesalonike 2:8).

Rudi nyumbani

Print this post

Kuota upo uwanjani (uwandani)

Nini maana ya kuota upo uwanjani/uwandani?

Jibu: Kiroho uwanja au uwanda unawakilisha mahali pa mapambano.Wanamichezo wote wanaoshindania tuzo, huwa mashindano hayo yanafanyikia viwandani/uwandani.

Kwahiyo unapoota kuwa upo Uwandani na shughuli zako hazihusiani na viwanja, basi fahamu kuwa upo katika mapambano. Na mapambano hayo yanaweza kuwa mazuri au mabaya.
Mapambano Mazuri:

Mapambano mazuri ni yale ya imani, hivyo kama umeokoka vizuri na umesimama kisawasawa na ukapata ndoto au ono unashindana na watu wengi au wachache katika uwanja/uwanda basi fahamu kuwa huenda Mungu anakuonyesha, au kukukumbush vita vya kiimani vilivyopo mbele yako. Hivyo huna budi kupiga mbio..sawasawa na kile kitabu cha Waebrania 12:1

Waebrania 12:1”Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”.

Soma pia Wafilipi 1:30, Wafilipi 1:27, na 1Wakorintho 9:24.

Lakini kama umejiona upo uwandani peke yako, basi kuna jambo la lingine Mungu anataka kusema nawe. Na hilo huenda ni jambo la tahadhari.

Na tahadhari yenyewe ni kama ile ya Kaini.

Wakati Kaini alipotaka kumwua Habili, alimtenga na kumpeleka uwandani. Na hiyo ni kanuni ya adui anapotaka kumdhuru mtu, anampeleka kwanza uwandani, mahali ambapo hapana watu, wala msaada wa kitu chochote..

Hivyo unapojiona upo uwandani/uwanjani peke yako, au upo na mtu mmoja, basi fahamu kuwa adui anatafuta kukuharibu au kuharibu mambo yako ya kiroho na kimwili.

Mwanzo 4:8 “Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani].
Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua”.

Kwahiyo uotapo ndoto hiyo, kama hujaokoka zingatia kuokoka, na pia kama una wokovu usio thabiti (maana yake wewe ni vuguvugu) basi zingatia kuwa moto, ili adui asipate nafasi ya kukumaiza.

Lakini kama tayari upo dhani ya wokovu ulio thabiti, basi zingatia Maombi, omba maombi ya kuharibu hila zote na njama za adui, na kutakuwa shwari.
Bwana akubariki.

Tafadhalishea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

KUOTA UPO UCHI.

Kuota unasubiriwa mahali fulani uhutubie, halafu unachelewa.

Kuota mbwa kunamaanisha nini?

UZAO WA NYOKA.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

USILIPIZE KISASI.

Kwanini hatupaswi kujilipiza kisasi?… Kwasababu maandiko yanatufundisha kuwa kisasi ni juu yake yeye atalipa.

Warumi 12:19 “Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, KISASI NI JUU YANGU MIMI; MIMI NITALIPA, ANENA BWANA.

20 Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake”.

Tabia ya kujilipiza kisasa Bwana Mungu aliikataa tangu Mwanzo na Bwana Yesu akaja kuithibitisha tena katika Mathayo 5.

Tunaona baada ya Kaini kumwua ndugu yake Habili kwasababu ya wivu, Mungu alimlaani Kaini kwa kosa lile..

Lakini Mungu hakumwua Kaini bali alimlaani juu ya ardhi kwamba ataendelea kuishi lakini ardhi itamkataa… Kila kilimo atakachokifanya juu ya ardhi hakitafanikiwa, ndio maana baada ya pale hatuoni Kaini na uzao wake wakiendelea na kazi yake ya ukulima badala yake tunasoma wanaanza kutengeneza vyuma, na wapiga filimbi (Mwanzo 4:17-22).

Sasa baada ya Bwana Mungu kumlaani Kaini alijua kabisa kuna watu watakuja kusikia habari zake kwamba ni mwuaji, na pia kalaaniwa na Mungu, hivyo watataka wajichukulie hukumu aidha ya kumwua au kumnyanyasa…

Sasa Mungu kwa kulijua hilo, akamwekea Kaini alama, ili kila mtu atakayemwona asimguse…

Na alama hiyo ikaendelea kuwepo juu ya Kaini na uzao wake, iliyowatofautisha uzao wa Kaini na uzao mwingine.

Na Bwana akasema mtu atakayemwua Kaini, basi atalipwa kisasi mara 7,

Mwanzo 4:13 “Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.

14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.

15 BWANA akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. BWANA akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga”

Hivyo watu walivyosikia hivyo wakaogopa kumnyooshea mikono yao Kaini, kwasababu walijua kuna adhabu kubwa sana katika kufanya hayo…

Umeona?..Kumbe kisasi na hasira ndani ya maisha ya mtu ni machukizo makubwa sana mbele za Mungu..
Ndivyo maandiko yanasema…

Mithali 24:17 “Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

18 BWANA asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.

Ikiwa na maana kuwa kama adui yako amekutenda mabaya na wewe usimrudishie yale mabaya, mwombee Bwana ambadilishe, itakuwa heri kwako…na utasikia ule mzigo umeondoka ndani yako…

Lakini kama ukifikiri kwamba njia ya kuondoa mzigo (uchungu) ndani yako ni wewe kujilipiza kisasi, nataka nikuambie kuwa ndio utauongeza badala ya kuupunguza, kwasababu utakayemlipa kisasi utakuwa umeweka uadui naye hivyo shetani anaweza kumtumia tena kufanya jambo lingine kwa wakati mwingine kwa njia nyingine…lakini lililo baya zaidi ni kwamba utakuwa umekosana na Mungu pia.

Sasa nini kifanyike ili kuishinda nguvu ya kisasi ndani yako?

1. Wokovu.

Wokovu ndio mlango wa Imani. Ni lazima kumwamini Yesu na kumkiri.


2. Maombi (yanayoambatana na mifungo).

Baada ya kuokoka ni lazima uwe mtu wa maombi. Maombi yatakufanya uwe na nguvu za kiroho ambazo zitakusaidia wewe kushinda dhambi.

3 .Kusoma Neno.

Neno la Mungu (biblia) litakusaidia kukujenga utu wako wa ndani. Kwamfano Neno lifuatalo ukilijua litakusaidia wewe kutolipiza kisasi.

Mhubiri 7:21 “Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Mambo haya matatu ukiyazingatia sana basi Nguvu ya kisasi haiwezi kufanya kazi ndani yako, utakuwa mtu wa kusamehe na kuombea wanaokuudhi, na mengine kumwachia Bwana, na hivyo utu wako wa ndani utajengeka sana.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

KISASI NI JUU YA BWANA.

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

SADAKA INAKOMESHA LAANA!

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

Rudi nyumbani

Print this post

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Safari ya wokovu ya mkristo inafananishwa na safari ya Wana wa Israeli kutoka Misri kwenda Kaanani. 

Na kama vile maandiko yanavyotuonyesha walikombolewa wote Kwa damu ya Mwana kondoo, Kisha Wakabatizwa katika bahari ya Shamu, wakawa chini ya wingu la Roho Mtakatifu kule jangwani,.. Lakini katika hayo yote bado tunaambiwa wengi wao hawakuweza kuiona Ile nchi ya ahadi. Isipokuwa wawili tu, (yaani Yoshua na Kalebu), waliotoka nchi ya Misri.

Biblia inatuonyesha walipishana na majaribu 5, ambayo yaliwafanya waangamie jangwani. Na majaribu yenyewe tunayasoma katika 1Wakorintho 10:1

1 Wakorintho 10:1-12

[1]Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; [2]wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;

[3]wote wakala chakula kile kile cha roho; [4]wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. [5]Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.

[6]Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani. [7]Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.

[8]Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. [9]Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

[10]Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu. [11]Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. [12]Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.

Kama tunavyosoma hapo. Makosa hayo yalikuwa ni haya;

  1. Kutamani mabaya
  2. Kuabudu sanamu
  3. Kufanya uasherati
  4. Kumjaribu Mungu
  5. Kunung’unika

1) Kutamani mabaya

Mungu aliwapa MANA kama chakula pekee ambacho wangekula jangwani, wao na mifugo Yao, lakini, baadaye waliikinai wakataka NYAMA, na vyakula vingine (Hesabu 11:4-35), matokeo yake ikiwa Mungu kuwaua, wengi wao.

Kama wakristo tuliookoka MANA yetu ni NENO LA MUNGU, Hatupaswi kulikinai, tukakimbilia chakula kingine kisicho Cha kiMungu. Tukataka tuongozwe na mifumo ya kidunia. Ndugu ni hatari mbaya sana. Kumbuka Ile mana ijapokuwa kilikuwa ni chakula Cha aina Moja, lakini hawakuwahi kuumwa, Wala kudhoofika, Wala miguu yao kupasuka, tofauti na walivyokuwa Misri penye vyakula vingi, lakini vimegubikwa na magonjwa. 

Ndugu Lipokee Neno la Mungu, ishi Kwa hilo, hata kama halitavutia (kidunia), lakini limebeba virutubisho vyote vya kimwili na kiroho. Wanaotembea Kwa Neno la Mungu, hawatikisiki hustawi milele.

2) kuabudu sanamu:

Walipomwona Musa amekawia mlimani, na Mungu hazungumzi chochote Kwa wakati ule  wakajiundia sanamu zao za ndama waziabudu. Wakacheza, wakala na kinywa (Kutoka 32). Hii ni kuonesha kuwa kitu chochote kinachokufanya ushangilie  tofauti na Mungu wako, ni ibada ya sanamu.

Rafiki kuwa makini Kwa wakati wa Leo mkristo kushabikia mipira, kwenda Disko, kutumikia Mali, kufuatilia vipindi vya sinema kulikopitiliza, chattings, kupenda anasa. Ni ibada za sanamu waziwazi.

 Kwasababu gani?. Kwasababu ndio bubujiko lako la roho lilipo kama ilivyokuwa Kwa Wana wa Israeli, Kwa sanamu zile. Ikapelekea watu wengi kufa siku Ile. Ibada Yako iwe Kwa Bwana. Mungu ni mwenye wivu. Mpira ukichukua nafasi zaidi ya Mungu wako ni kosa.

3) Kufanya uasherati

Walipokuwa jangwani Mungu aliwakataza wasitangamane na wageni, kwasababu watawageuza mioyo na kuiabudu miungu Yao. Lakini wao walipowaona wanawake wa taifa la Moabu, wakaenda kuzini nao, Kisha wakageuzwa mioyo wakaabudu miungu Yao. Hiyo ikawa sababu ya Mungu kuwaua waisraeli wengi sana idadi yake 23,000.

Na sisi kama wakristo tulishapewa tahadhari kwenye maandiko. Tusifungwe nira na wasioamini isivyo sawasawa (2Korintho 6:14-18). Kwasababu hakuna ushirika kati ya Nuru na Giza. Hivyo hatuna budi kuwa makini na ulimwengu, tushirikiane nao kwenye mambo ya kijamii na ya msingi, pale inapokuwa na ulazima, lakini ya kiroho, hatupaswi hata kidogo kuwa na urafiki nao kwasababu ni rahisi kugeuzwa moyo na kuambatana nao kitabia, na matokeo yake tukamwasi Mungu.

Sulemani aligeuzwa moyo, Wana wa Mungu tunaosoma kwenye Mwanzo 6 nao pia waligeuzwa mioyo Kwa jinsi hiyo hiyo, na wewe pia usipojiwekea mipaka na watu ambao ni wa kidunia, Unaweza kupoteza taji lako. Pendelea zaidi kuwa na kampani ya waliookoka. Ni Kwa usalama wako. Usijikute unafanya uasherati wa kiroho.

4) Kumjaribu Bwana

Wana wa Israeli walimjaribu Bwana, wakati Fulani wakamnun’gunikia Mungu na Musa, wakisema chakula hiki dhaifu, wakitaka Kwa makusudi Bwana awafanyie Tena muujiza mwingine, Mungu akakasirishwa nao, akawaangamiza Kwa nyoka (Hesabu 21:4-9).

Kama mkristo tambua kuwa Mungu haendeshwi kama “robot”. Kwamba ni lazima afanye jambo Fulani Kila tutakapo ndio tuthibitishe yeye yupo na sisi. Ndugu ukristo wa hivi ni hatari, wengi wameishia kuanguka kwasababu hii. Jaribu kama hili aliletewa Bwana Yesu na shetani jangwani. Ajitupe kutoka kinarani, kwasababu maandiko yanasema Mungu atamuagizia malaika wake wamchukue salama. lakini Bwana Yesu alimwambia shetani usimjaribu Bwana Mungu wako.

Kamwe usimwendeshe Mungu, mwache yeye ayaendeshe maisha Yako. Tuwe na hofu na Mungu wetu.

5) Kunung’unika.

Wana wa Israeli tangu mwanzo wa safari Yao Hadi karibia na mwisho, waligubikwa na manung’uniko tu,(Kutoka 23:20-21) wengi wao hawakuwa watu wa shukrani. Ijapokuwa walilishwa mana, waliouna utukufu wa Mungu Kwa wingi. Lakini bado manung’uniko yalizidi shukrani.

Biblia inatuasa sisi tuliookoka tuwe watu wa Shukrani (Wakolosai 3:15), Kwa kazi aliyoimaliza Yesu pale msalabani ya kuondolewa dhambi ni fadhili tosha zaidi hata ya wale Wana wa Israeli kule jangwani. Hata tukikosa Kila kitu, maadamu tumeahidiwa uzima wa milele. Hatuhitaji kuwa na hofu na jambo lolote. Wokovu wetu ndio uwe faraja.

Epuka Maisha ya manung’uniko.

Bwana akubariki.

Ikiwa tutashinda majaribu haya MATANO katika safari yetu ya wokovu. Basi tutalipokea taji timilifu Kwa Bwana  siku Ile mfano wa Yoshua na Kalebu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

Umoja wa Roho Mtakatifu upo katika vifungo 7, ambavyo kama kanisa ni lazima tujifunge katika vifungo hivyo.

Lakini kabla ya kuvitazama hivi vifungo 7 vya Roho Mtakatifu, ni vizuri tuweke msingi kidogo kumhusu Roho Mtakatifu.

Biblia inatufundisha kuwa kuna Roho 7 za Mungu, ambazo ndizo zinazotajwa kama Macho 7 ya Mungu.

Ufunuo 5:6  “Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale wenye uhai wanne, na katikati ya wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye pembe saba na macho saba, AMBAZO NI ROHO SABA ZA MUNGU zilizotumwa katika dunia yote”

Vile vile inazitaja Roho hizi 7 kama TAA SABA ZA MUNGU, ikiwa na Maana kuwa hizo ndizo mwanga mbele ya kiti cha Enzi.

Ufunuo 4:5 “Na katika kile kiti cha enzi kunatoka umeme na sauti na ngurumo. NA TAA SABA ZA MOTO ZILIKIWAKA MBELE YA KILE KITI CHA ENZI, NDIZO ROHO SABA ZA MUNGU”.

Hii yote ikimaanisha kuwa Roho Mtakatifu anatenda kazi katika Nafasi zake 7, au hatua zake 7 katika kuwakamilisha watu wake, lakini haina maana kuwa Roho Mtakatifu wapo 7.

Kwa msingi huo basi twende tukazitazame jinsi anavyolikamilisha kanisa katika kifungo cha UMOJA katika hatua zake saba.

Tusome,

Waefeso 4:3 “ na kujitahidi kuuhifadhi UMOJA WA ROHO katika kifungo cha amani.

MWILI MMOJA, na ROHO MMOJA, kama na mlivyoitwa katika TUMAINI MOJA la wito wenu.

BWANA MMOJA, IMANI MOJA, UBATIZO MMOJA.

MUNGU MMOJA, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.

Tutazame moja baada ya nyingine:

1.MWILI MMOJA.

Mwili unaozungumziwa hapa ni Mwili wa Yesu, (Soma Waefeso 4:12 na Wakolosai 3:15), na Mwili huu unajengwa kupitia Vipawa na Karama ambazo Roho Mtakatifu ameziweka ndani yetu, ambapo kila mmoja ni kiungo ndani ya mwili huo.. Hivyo ili tuufikie umoja wa Roho kama kanisa ni lazima tuenende katika msingi huu kwamba kanisa linaongozwa katika karama za Roho Mtakatifu, na si itikadi, mapokeo au siasa.

1Wakorintho 12:13  “Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.

14  Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi”.

2. ROHO MMOJA.

Anaposema Roho mmoja, zipo roho nyingi, hata shetani naye ni roho.. ikiwa na maana kuwa ndani ya kanisa ni lazima tuwe na Roho mmoja anayezaa matunda yanayofanana kwa wote. Na matunda ya Roho ni yale yanayotajwa katika Wagalatia 5:22, kupitia hayo, tutakuwa tumekamilka katika kifungo cha pili cha Roho. Ndio maana biblia inatufundisha kuzichunguza roho, kwamaana zipo roho nyingi..

2Wakorintho 11:4 “Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea ROHO NYINGINE MSIYOIPOKEA, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye”

3. TUMAINI MOJA

Tumaini linalozungumziwa hapa ni “Tumaini la Utukufu ujao”.. Kwamba kila aliyeokoka analo tumaini la kuingia katika utukufu wa Mungu ujao,(Mbingu mpya na nchi mpya). Hili ni tumaini ambalo Kanisa lazima liufikie, na si kila mmoja anaamini analoliamini, kwasababu wapo wengine wanaosema hakuna ufufuo, mtu akifa amekufa!, jambo ambalo ni kinyume kabisa na maandiko. Ufufuo upo, na watakatifu watafufuliwa na kuingia katika utukufu wa milele.

Wakolosai 1:26  “siri ile iliyofichwa tangu zamani zote na tangu vizazi vyote, bali sasa imefunuliwa kwa watakatifu wake;

27  ambao Mungu alipenda kuwajulisha jinsi ulivyo utajiri wa utukufu wa siri hii katika Mataifa, NAO NI KRISTO NDANI YENU, TUMAINI LA UTUKUFU”

4. BWANA MMOJA

Yupo Bwana mwingine (yesu mwingine), anayehubiriwa tofauti na yule wa kwenye maandiko matakatifu.

2Wakorintho 11:4 “Maana yeye AJAYE AKIHUBIRI YESU MWINGINE ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye”.

Yesu mwingine ni yule anayesema Mungu haangalii mwili anaangalia Roho, ni yule anayesema mchukie adui yako, n.k. Lakini yule halisi anasema Mwombee adui yako, waombeeni wale wanaowaudhi, na wasameheni wale wanaowaudhi (Mathayo 5:43).

5. IMANI MOJA

Imani moja ni sahihi ni ile inayosema mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu ni mmoja (naye ni YESU KRISTO), Lakini Imani nyingine inasema “watakatifu waliokufa pia wanaweza kuwa wapatanishi” hivyo wanaweza kutuombea…

1Timotheo 2:5  “Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu”.

Vile vile inasema, mwombezi wetu kwa Baba ni yeye mmoja Yesu Kristo ( 1Yohana 2:1) na wala hakuna mwingine, lakini Imani nyingine inasema waombezi wanaweza kuwa wengi mbinguni. Hivyo kanisa ni lazima lifikie umoja wa Imani ya kweli ya kwenye biblia, kwamba mpatanishi ni mmoja na mwombezi ni mmoja, ambaye ni Yesu Kristo, na wala hakuna mwingine wa kumsaidia.

6. UBATIZO MMOJA.

Ubatizo mmoja wa kimaandiko ni ule wa Maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38, Matendo 10:48, Matendo 19:5). Ni lazima kanisa lifikie huu umoja, na si kila mmoja kuamini ubatizo wake.

7. MUNGU MMOJA.

Mungu mmoja wa kweli  ni yule aliyeumba mbingu na nchi, ambaye ni Baba wa yote, aliyeko juu mbinguni na si sanamu, wala miti, wala wanadamu. Hivyo ni lazima ndani ya mwili wa Kristo wote tufikie umoja huu wa kumwamini na kumwabudu Mungu mmoja, na kuchanganya ibada na miungu mingine au sanamu.

Adui anafanya kazi kwa nguvu, kuuvunja UMOJA HUU WA ROHO, kwasababu anajua ndio NGUVU YA KANISA, anataka kuweka umoja wake mwingine wa kidunia ndani ya kanisa, na kuutafsiri kama ndio umoja wa roho. Hivyo hatuna budi kuwa makini na kuyaishi maandiko.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

JE UNAMHUBIRI KRISTO KATIKA KWELI YOTE?.

Roho Mtakatifu ni nani?.

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

TUMAINI NI NINI?

Dinari ni nini na Rupia ni nini (Mathayo 20:2,Ufunuo 6:6)

Rudi nyumbani

Print this post

JE NI KIKOMBE KIPI UTAKINYWEA SIKU ILE?

Rohoni vipo vikombe viwili ambavyo Mungu ameviandaa kwa wanadamu.

  1. Kikombe Cha kwanza kinajulikana kama kikombe Cha ghadhabu ya Mungu.
  2. Na kikombe Cha pili kama kikombe Cha baraka/ wokovu.

KIKOMBE CHA GHADHABU

Kama hufahamu, Mungu Huwa anajiwekea “akiba” ya hasira yake. Ikiwa na maana si mwepesi kutimiliza hasira yake Kwa haraka, Huwa anaikusanya na siku ikifika kipimo chake Kisha akaimimina hapo huwa hapana Rehema Tena. Ni kilio na kusaga meno!.

Soma

Nahumu 1:2-3

[2]BWANA ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; BWANA hujilipiza kisasi, naye ni mwingi wa hasira; BWANA hujilipiza kisasi juu ya adui zake, huwawekea adui zake akiba ya hasira.

[3]BWANA si mwepesi wa hasira, ana uweza mwingi, wala hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; BWANA ana njia yake katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.

Mifano halisi ya hasira ya Mungu tunaiona kipindi Cha gharika, kipindi Cha sodoma na Gomora. Na ameahidi pia katika siku za mwisho ataleta hukumu hiyo Kwa ulimwengu mzima, na itatimilika yote katika lile ziwa la moto.(2Petro 3:7-5)

Utapata majibu Kwanini Leo,  Mungu anaonekana kama vile yupo kimya Kwanini uovu unaendelea hachukui hatua stahiki duniani, fahamu ni kwamba anangoja kipimo chake kijae, kikombe kijae ili waovu wanywe ghadhabu yake yote. Ndivyo alivyowaambia Ibrahimu kuhusu kuangamia Kwa wakaanani, alikuwa anasubiria uovu wao utumie (Mwanzo 15:16), na siku ilipofika Yoshua aliwaangamiza wote.

Hivyo mtu unapokuwa mwovu unakijaza kikombe Cha ghadhabu ya Mungu, Na kama dhiki kuu itakupita basi utakatana na kikombe hicho siku Ile ya hukumu, utakinywa Kwa kutupwa kwenye lile ziwa la moto.

Ufunuo wa Yohana 14:10

[10]yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.

KIKOMBE CHA BARAKA.

Lakini pia watakatifu nao Bwana anawawekea akiba ya Baraka na mema. Kwa maisha ya haki wanayoishi sasa hapa duniani, usidhani kuwa hayo mema unayotendewa ndio malipo stahiki Kutoka Kwa Mungu wako,hapana..Bwana anakijaliza kikombe Cha watakatifu na siku Ile tutakinywea na Yesu Kristo kule mbinguni kwenye Karamu ya Mwana kondoo. Haleluya.

Mathayo 26:27-29

[27]Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki;

[28]kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

[29]Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.

Hapo ndipo tutakapoona wema wote wa Mungu maishani mwetu. Tutakinywea kikombe hicho, tutamiminiwa thawabu na Raha isiyo na kifani. Hapo ndipo tutakapojua ni jinsi gani Mungu anavyotujali. Usikose mbingu ndugu, kosa vyote lakini Unyakuo usikupite.

Ndugu ukiona unamtumikia Mungu Leo huoni faida yoyote, kama vile huoni malipo yoyote, ,tambua kuwa Bwana anaona..anaweka tu akiba, utaipokea Raha siku Ile itakapofika.

Unapojitesa kuishi maisha ya haki, halafu unaona kama vile Mungu hakujali..usijidanganye kikombe unakijazilisha tu. Wakati wa kukinywea utafika.

Soma haya maneno ya faraja Mungu aliyoyatamka Kwa watu wake..

Malaki 3:13-18

[13]Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema BWANA. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani?

[14]Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa kwenda kwa huzuni mbele za BWANA wa majeshi?

[15]Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.

[16]Ndipo wale waliomcha BWANA waliposemezana wao kwa wao. Naye BWANA akasikiliza, akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha BWANA, na kulitafakari jina lake.

[17]Nao watakuwa wangu, asema BWANA wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye.

[18]Ndipo mtakaporudi, nanyi mtapambanua kati ya wenye haki na waovu, na kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.

Bwana atupe macho ya kumwelewa yeye. Kijazilishe kikombe Cha wokovu wako. Ili siku Ile ushiriki mema yote.

Ubarikiwe.

Je umeokoka? Kama bado unasubiri Nini Leo usifanye hivyo. Ikiwa upo tayari kumgeukia Yesu na kumfanya mwokozi wa maisha Yako, akusamehe dhambi zako. Basi ni wewe tu kufungua moyo wako na kuikubali msamaha huo.Ikiwa upo tayari kufanya.hivyo basi fungua hapa Kwa mwongozo huo.

Bwana akubariki..

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

SIKU YA MAONYESHO MAKUU YA BWANA YESU, IPO KARIBU.

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA.

Kwanini Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wasikisaze chakula?

IEPUKE GHADHABU YA MUNGU.

USIIHARIBU TABIA YAKO KWA MAZUNGUMZO YAKO.

Rudi nyumbani

Print this post