Title April 2024

FAHAMU KURUDI KWA YESU KUKO KWA NAMNA NGAPI?

Wengi, tumeshasikia kuwa Yesu atarudi, lakini mpaka mtu anasema atarudi, maana yake ni kuwa alishawahi kuja hapo nyuma. Na kama tunavyojua Bwana wetu Yesu Kristo alikuja mara moja tu, miaka karibu elfu mbili iliyopita, akaishi, akafa,akazikwa, akafufuka, akapaa mbinguni. Lakini wakati wote alipokuwa hapa duniani aliwaahidi wanafunzi wake kuwa atarudi tena.

Hivyo somo hili, ni muhimu kufahamu,  namna ambazo Yesu alisema atarudi, ili usikose maarifa, kwasababu wengi hapa wanakosa shabaha katika kutambua kauli za Yesu. Naomba Soma kwa utulivu somo hili mpaka mwisho.

Sasa kuhusu kurudi kwake duniani, alizungumza katika nyakati tofuati tofauti kurudi kwa namna mbili.

  1. Namna ya kwanza, ni kama Roho
  2. Namna ya pili ni kama Mwizi

Tuangalie kwa undani, namna hizi mbili. Husasani tutailenga hiyo ya pili.

Je! ni kwa namna gani, alirudi kama Roho,Aliwaambia hivi mitume wake;

Yohana 14:18  “Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. 19  Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.

20  Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu”.

Soma pia, katika Yohana 16:16, amerudia maneno hayo hayo,

Unaona? Mitume walidhani hawatamwona tena, lakini siku ile aliyopaa mbinguni,siku kumi baadaye, biblia inasema walikuwa wamekusanyika wote mahali pamoja, akawajilia Roho Mtakatifu akawakalia wote, wakajazwa Roho Mtakatifu. Na kama tunavyojua tangu huo wakati na kuendelea, kila mmoja alijua anaye Yesu moyoni mwake, hakuna mtu aliyeuliza Yesu yupo wapi.

Uyatima uliondoka kabisa, kabisa, ndipo wakatambua maana ya yale maneno. Hivyo tumeshaona kurudi kwake kwa kwanza duniani, kulikuja kwa namna hiyo ya Roho Mtakatifu, na mpaka sasa Kristo yupo ndani ya mioyo ya waliomwamini, na kupokea Roho Mtakatifu.

Lakini pia katika maneno yake mengine, alisema atarudi kama mwizi.

Soma,

Mathayo 24:43  Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.

44  Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.

Unaona tena?, Hajasema, atarudi kama askari, au mfanya biashara, bali kama mwizi. Sasa ni vema tujue sifa za mwizi, ni zipi kibiblia, ndipo tuelewe jinsi kurudi kwake kwa namna hiyo kutakavyokuwa.

Ukisoma Yohana 10:10  Yesu anasema hivi;  Mwivi haji ila AIBE na KUCHINJA na KUHARIBU; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele”.

Kumbe mwizi hasaa, anayezungumziwa ni mfano wa jambazi, na sio wale wadokozi, ni wale wanaobeba silaha, ili kuharibu na kuua wanaowaona, wachukue mali yao waondoke.

Na Yesu ndivyo atakavyokuja katika siku za mwisho hizi, atatimiza sifa hizo zote tatu.

1.) Jambo la kwanza Atakuja saa tusiyodhani, Kisha ATAIBA kitu chake cha thamani duniani. Ni hicho si kingine zaidi ya watakatifu wake. Hapo ndio suala la unyakuo linapoibukia.

Mathayo 24:40  Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa; 41  wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.

2) Lakini pamoja na hilo, kuja kwake kutaambatana na KUCHINJA.

Maana yake ni kwamba, kama unyakuo utakupita, dunia itakuwa inajiandaa kuingia katika siku ile ya mapigo ya ghadhabu ya Mungu, ambayo mwisho wake utaishia na Kristo kuonekana katika umbile la kibinadamu kabisa, kuwaua mataifa yote ambayo yatakusanyika kupigana naye katika ile vita kuu ya Harmagedoni.

Ufunuo 19:11  Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12  Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13  Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14  Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15  NA UPANGA MKALI hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16  Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANAWA MABWANA.

Huu ni wakati ambao Yesu, atauangamiza  ulimwengu, mfano wa mwizi, asiyekuwa na huruma. Usitamani uwepo wakati huo ndugu, ni majuto vilio na kusaga meno.

3) Lakini mwisho kabisa, ATAHARIBU.

Tunafahamu kuwa mwizi, huvunja, mahali ili aingie, huvuruga kila kitu anachokiona, vivyo hivyo na hii dunia itafumuliwa yote, mifumo yote itaangushwa, itafinyangwa upya, yote hayo yatatokea katika siku hiyo hiyo ya Bwana, ambayo itaharibu kila kitu.

2Petro 3:10  Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 11  Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 12  mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?

Soma pia,(Ufunuo 16:17-21), kuongeza maarifa..

Hivyo ndugu, wakati huu wa Yesu kurudi kama mwizi umekaribia sana, ambao utaanza  Kwanza kwa tukio la unyakuo. Bwana anatutaka sisi tukeshe(rohoni), asitukute tumelala. Ili Siku hiyo isitujilie ghafla, tukabaki hapa duniani.

1Wathesalonike 5:1  Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2  Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3  Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.

4  Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.

5  Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.

6  Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

7  Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 8  Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.

Bwana atupe macho ya kuona haya.

Je! Umempokea Yesu maishani mwako, Je! Ameziondoa dhambi zako? Kama jibu ni la, unasubiri nini? Hujui kesho kama utakuwepo, hujui kama leo atarudi. Hivyo tubu sasa, mwamini Yeye upate ondoleo la dhambi zako, kisha utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Ikiwa utapenda kupokea wokovu basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii bure. Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

KAMA MWIZI USIKU WA MANANE.

Kuna tofauti gani kati ya “Mwivi” na “Mwizi”?

Fahamu Namna ya Kuomba.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 30:33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi

SWALI: Naomba kuelewa tafsiri ya mithali 30:32-33, isemayo;

Mithali 30:32 Ikiwa umefanya kipumbavu kwa kujikuza; Au ikiwa umewaza mabaya; Basi weka mkono wako juu ya kinywa chako. 

33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi; Na kupiga pua hutokeza damu; kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.

JIBU: Hekima inatueleza matokeo ya kila tendo linapofanyiwa kazi liwe ni zuri au baya litaleta majibu fulani tu. Hapa anatumia mfano wa siagi ambayo inatolewa katika maziwa.  Kwa kawaida siagi huwa imejificha ndani ya maziwa, hivyo ili kuipata tu ile siagi, ni kitendo cha kuipiga basi hutokea kwa juu yote,

Sasa kupiga hapo sio kuyachapa maziwa hapana, bali kuyakoroga, ndani chombo Fulani maalumu kwa muda mrefu, baadaye maziwa na siagi hujitenga vyenyewe.

Halikadhalika, pia damu huwa ipo ndani ya pua, lakini haiwezi kutoka yenyewe tu bila kuisumbua pua kwa kuipiga. Kwamfano mtu akikupiga ngumi ya pua ni wazi kuwa damu itatoka tu.

Ndivyo anavyofananisha na ugomvi, kwamba ni jambo ambalo lipo tu, wakati wowote katikati yetu. Mfano tu wa siagi ndani ya maziwa na damu ndani ya pua. Lakini mpaka ugomvi huo ujitokeze, unahitaji kuchochewa, kukorogwa, korogwa, kupigwa pigwa.

Anasema hasira inapoanza, aidha kwa kuzungumza maneno mabaya, mwenzako akakereka, haraka sana, weka mkono wako kinywani, usiendelee kuzungumza, kwasababu kitakachofuata ukiendelea sana ni ugomvi, yaani mapigano, na kudhuriana.

Mauaji, visasi, chuki, asilimia kubwa vimetokana na hasira zilizochochewa.

Lakini, uwezo huu wa kujizuia, una nguvu endapo mtu yupo ndani ya Kristo. Je! Umemwamini? Kama bado na upo tayari kumpokea leo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu chini.

Bwana akubariki

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

Kwanini iwe ni nchi ibubujikayo maziwa na asali?

Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

Rudi Nyumbani

Print this post

BWANA NITIE NGUVU TENA. (Waamuzi 16:28)

Waamuzi 16:28 “Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili”.

Samsoni haombi kujilipiza kisasi kwaajili ya Nywele zake zilizokatwa, bali kwajili ya “MACHO YAKE MAWILI”.. Maana yake macho yake yalikuwa ni bora kuliko nguvu zake… Laiti angeambiwa achague nguvu ziondolewe na macho yabaki, ni Dhahiri kuwa angechagua macho  yabaki.. Na huo ungeweza kuwa uchaguzi wa kila mtu.

Macho ni Zaidi ya mikono, ni Zaidi ya miguu, ni Zaidi ya nguvu za mwili.. Na ndicho shetani alikitafuta kwa SAMSONI.. Macho yake!!!!… lakini ni jinsi gani angeyatoa?? Inahitajika kuziondoa kwanza nguvu zake za mwili.. Shetani alikuwa haziogopi nguvu za Samsoni, alichokuwa anakiogopa ni macho yake…

Kwani baada ya kumtoa macho alizitumia nguvu zake kusaga ngano za wafilisti…

Na leo hii adui anatafuta macho ya watu kama shabaha yake ya kwanza.. na macho anayoyatafuta si ya kimwili, bali yale ya kiroho..na anaanza kwanza kwa kudhoofisha nguvu za kiroho za mtu na kisha anamaliza kwa kumpofusha Macho ya kiroho … (hapo anakuwa amemaliza kazi!).. na hapo anaanza kumtumikisha kama alivyomtumikisha Samsoni.

2Wakorintho 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.

Lakini habari njema ni kwamba ipo NEEMA kuu juu yetu Zaidi ya ile iliyokuwa juu ya Samsoni. Kwani Samsoni alipomwomba Mungu amrejezee Nguvu zake alirejeshewa kweli na kuwaaharibu maadui zake lakini bado aliendelea kuwa kipofu..

Lakini katika wakati huu wa agano jipya tunaponyenyekea kwa Baba na kuomba msaada, kwa kumaanisha kabisa mbele zake, basi zile nguvu zetu adui alizoziteka zinarejea tena upya na pia macho yetu yanatiwa nuru.. Hiyo ndio faida ya kuwa ndani ya KRISTO.

Je nguvu zako za Kuomba zimeisha???, nguvu zako za kufunga zimeisha??..Nguvu za kumtumikia Mungu zimeisha??…. Kama ndio jua hiyo pia ni dalili ya kupofushwa macho na Ibilisi… Hivyo huwezi kuona mbele wala kutafakari yaliyopita… unahitaji msaada wa Mungu, kwa nguvu zako huwezi!!!

Huu ni wakati wa wewe kunyenyekea kwa Mungu kama Samsoni ili Bwana azirejeshe nguvu zako upya na macho yako yatiwe nuru.

Waamuzi 16:28 “Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili”.

Omba kwa kumaanisha, na ikiwezekana funga! Ili Toba yako iwe na nguvu.. Na matokeo utayaona!

Waefeso 1:18  “macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

KITENDAWILI CHA SAMSONI

UMEFUNULIWA AKILI?

BUSTANI YA NEEMA.

Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?

Rudi Nyumbani

Print this post

MADHARA YA KIBURI KATIKA MAISHA YA MTU.

Kiburi ni hali ya moyo wa mtu kuinuka kutokana na kitu fulani alichonacho, au alichokipata au atakachokipata ambacho kinamtofautisha au kitamtofautisha yeye na mwingine.

Hali hii inamfanya mtu anakuwa na majivuno, dharau na jeuri na asiyetii na hata kukosa staha.

Mtu huyu anakuwa ni mgumu kushaurika, na wakati wote yeye ndio anajiona yupo sahihi  na wengine wote wana kasoro.

Vifuatavyo ni vitu vichache ambavyo vinatengeneza kiburi ndani ya mtu.

1.MALI

Hiki ni kitu cha kwanza ambacho kinatengeneza kiburi ndani ya mtu, na kiburi chenyewe ni “kiburi cha uzima” tunachokisoma katika 1Yohana 2:16.

Hapa mtu anakuwa anaamini anao uzima au maisha kupitia vile alivyonavyo.. Hivyo hahitaji kuambiwa kingine chochote ambacho kitampa yeye uzima, tayari yeye anakuwa anaamini mali alizonazo ndizo jawabu la mambo yote..hivyo hata ukimpelekea Neno la Mungu ambalo ndilo uzima hawezi kukusikiliza…

Na kiburi hiki pia kwa sehemu kipo kwa watu wasio na mali, wanaozisaka wakiamini kuwa watakapozipata zintawapa majibu yote…na hawa ndio wale ukiwapelekea Neno la Mungu wanadharau na kukejeli na kuulizia pesa.

Lakini Bwana YESU alisema kuwa uzima wa mtu haupo katika wingi wa vitu mtu alivyonavyo..(Luka 12:15).

2. ELIMU

Maarifa hususani ya kidunia ni mlango wa pili wa kuzalisha kiburi ndani ya mtu.

Hapa ni pale mtu kapata elimu ambayo ni ya juu kuliko wengi..moyo wake unanyanyuka na kuona wengine wote hawawezi kumzidi akili au uwezo wa kutafakari..

Hivyo anapoletewa Neno la Mungu basi anaanza kumpima yule aliyemletea na anapogundua kuwa ana elimu ndogo ya kidunia kuliko yake, basi hamsikilizi akiamini kuwa atakuwa na upambanuzi hafifu…pasipo kujua kuwa elimu ya mbinguni haipatikani katika shule za wanadamu..kwani hata Mitume wa Bwana Yesu hawakusoma isipokuwa Mathayo tu..lakini leo mafunuo yao tunayasoma na kutusaidia.

3. KIPAWA/KARAMA

Kipawa/kipaji/Karama mtu alichonacho ni mlango wa tatu wa kuzalisha kiburi ndani ya mtu.

Hapa ni pale mtu anapotambua kuwa anao uwezo pengine wa kuimba kuliko wengine, anauwezo wa kufundisha kuliko wengine, ana uwezo wa kutenda jambo fulani kuliko wengine, na badala atumie uwezo huo kujaza pale palipopunguka, kinyume chake anautumia uwezo huo kujisifia au kujionyesha yeye ni bora na hivyo hata kusikiliza wengine au kushawishwa na wengine inakuwa ni ngumu.

4. CHEO/NAFASI.

Cheo au nafasi ni mlango wa nne wa kiburi kuzalika ndani ya mtu..

Hapa ni pale mtu anapopata nafasi fulani katika kanisa, au jamii au kazi…na kuona wote walio chini yake hawawezi kumwongezea chochote.

5. MWONEKANO

Huu ni mlango wa tano ambao unatengeneza kiburi ndani ya mtu..

Hapa ni pale mtu inatokea kujiona anavutia kimwonekano kuliko wengine, na kuamini kuwa yeye ni mzuri/mrembo zaidi ya wote na hakuna wa kumzidi..

Na kiburi hiki kinazalika pale anapopokea maoni ya kusifiwa na mtu mmoja au wawili.. Mtu kama huyu anapotokea mtu mwingine na kutaka kuzungumza naye inakuwa ni ngumu kumsikiliza kwasababu alijiona kama atachafuliwa mwonekano wake.

Sasa yafuatayo ni madhara ya kiburi juu ya mtu kibiblia.

1.Kiburi kinaondoa Neema ya Mungu.

Petro 5:5 “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema”.

Neema ya Mungu inapokuwa juu ya mtu inamwongezea kibali kwake Mungu na kwa wanadamu…

Mtu mwenye neema ya Mungu tele juu yake, inakuwa ni vyepesi kwake kushinda dhambi tofauti na yule ambaye amepungukiwa neema, vike vile inakuwa vyepesi kwake kufanya jambo likafanikiwa.

2. Kiburi kinamletea mtu Aibu.

Mithali 11:2 “Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu…”

Watu wengi wenye kiburi wanaishia kuabika, kutokana na majivuno yao na dharau zao hivyo mwisho wake huwa hawapati vile wanavyovitafuta na hivyo wanakuja kuaibika baadaye.

3. Kiburi kinaharibu Nyumba

Mzazi mmoja au wote wanapokuwa na kiburi wanaiharibu familia yao wenyewe…

Mithali 15:25 “BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi..”

4. Kiburi kinamshusha mtu chini (kimaisha).

Wote wenye kiburi Mungu anawashusha chini..

Mithali 29:23 “Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa”.

5. Kiburi kitamshusha mtu kuzimu.

Wote wenye kiburi hawataurithi uzima wa milele.

Isaya 2:12 “Kwa maana kutakuwa siku ya BWANA wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini……..

17 Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo”

Tabia nyingine ya mtu wenye kiburi pia ni mashindano na ubishi

Mithali 21:24 “Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo majivuno ya kiburi chake”.

Mithali 13:10 “Kiburi huleta mashindano tu…”

Jihadhari na kiburi..Na tunajihadhari nacho kwanza kwa kuokoka kisha kujazwa Roho Mtakatifu katika maisha yetu na kujitahidi kwa bidii kukaa mbali na mazingira yote yanayochochea kiburi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kiburi cha Uzima ni nini? (1Yohana 2:16)

MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI.

Unyenyekevu ni nini?

Babeli ni nchi gani kwasasa?

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Rudi Nyumbani

Print this post

NA SISI TUTOKE TUMWENDEE NJE YA KAMBI.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, Karibu tujifunze maneno ya uzima.

Katika agano la kale ilikuwa ni sheria, ili sadaka ya upatanisho, au ya dhambi ambayo ilihusisha kafara za wanyama, kuwa kamili, ni lazima uhusishwe na sehemu kuu mbili, ya kwanza ni ndani ya kambi, na ya pili ni nje ya kambi.

Ndani ya kambi au ndani ya lango, ndio ilichukuliwa damu ya mnyama huyo na kuingizwa kwa ajili ya upatanisho kwa kunyunyizwa. Lakini ilikuwa ni sharti pia viungo, ngozi na vinyesi, vya mnyama huyo vikateketezwe mbali nje ya kambi. Na kama jambo hilo lisipofanyika, haijalishi damu ya kunyunyiza ya mnyama  huyo itakuwa ni njema kiasi gani, utapatanisho hauwezi kutokea.

Ndani ya kambi ni mahali patakatifu, lakini je! Ya kambi ni mahali pa uovu.

Sasa tukirudi kwenye agano jipya, tunaona mwokozi wetu Yesu Kristo, anafananisha na mnyawa huyo wa upatanisho, Hivyo ilimbidi, ahusishwe pia na sehemu zote mbili, yaani ndani ya kambi na nje ya kambi.

Alimwaga damu yake, ambayo kwa kupitia hiyo, ameingia nayo  patakatifu pa patakatifu kule mbinguni, kutuombea sisi, Lakini hilo lisingewezekana, kama asingeteketezwa nje ya kambi.

Ndio Hapo tunaona Bwana wetu, ilimpasa, aache enzi na mamlaka mbinguni, (Atoke nje ya kambi), akutane na waovu huku duniani, ateketezwe kabisa mahali pa aibu pa waovu pale Golgota, ili sasa damu yake ipatikane kufanya upatanisho wetu kule mbinguni, kwa Baba ambapo ndio ndani ya kambi.

Na matokeo yake ndio haya tunayoyaona sasa hivi, sote kupata neema na ondoleo la dhambi zetu.

Lakini sasa maandiko yanasema..

Waebrania 13:11  Maana wanyama wale ambao damu yao huletwa ndani ya patakatifu na kuhani mkuu kwa ajili ya dhambi, viwiliwili vyao huteketezwa nje ya kambi.

12  KWA AJILI HII YESU NAYE, ILI AWATAKASE WATU KWA DAMU YAKE MWENYEWE, ALITESWA NJE YA LANGO.

13  BASI NA TUTOKE TUMWENDEE NJE YA KAMBI, TUKICHUKUA SHUTUMU LAKE.

14  Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.

Umeona hapo? Kumbe na sisi, hatuna budi kumfuata Yesu nyayo zake, kwasababu alisema mimi nilipo na mtumishi wangu atakuwepo.  Sasa hapo anasema, na sisi tutoke nje ya kambi, tuchukue shutumu lake. Akiwa na maana, tukubali kujitoa sadaka na sisi, nje ya lango, waovu walipo ili tuwavute wengine kwa mwokozi.

Kama mashahidi  wa kweli wa Kristo, ni lazima tuwe tayari kuhatarisha maisha yetu, kwa ajili ya wengine. Tusiwe tu ndani ya lango, walipo watakatifu, ni kweli ni vizuri kufanya semina za ndani makanisani zina nafasi yake, ni vizuri kuhubiri mikutano ya ndani. Lakini je! Tunaweza tukawa tayari pia kwenda katikati ya watu wa dini nyingine kuwahubiria Kristo, tukawa tayari kwenda mahali pa jamii zenye vita na kuzitangaza habari za Yesu. Kanisa la Kwanza la mitume lilikuwa tayari kutoka nje ya kambi, kukutana na ukinzani wa wayahudi, kuburutwa, kupigwa mawe hata kuawa, walikuwa tayari kuwaendea wapagani sugu, na jamii za wachawi kuwatangazia Kristo. Vivyo hivyo na sisi hatuna budi kutoka nje ya kambi, kuliendea na kundi lingine ambalo halijamjua Kristo.

Hatuna budi kuwa tayari hata kuhatarisha afya zetu, fedha zetu, kazi zetu,  vyeo vyetu, elimu zetu inapobidi ili wengine waokoke, wamjue Kristo. Huko ndiko kutoka nje ya kambi. Bwana Yesu ilimpasa aache enzi na mamlaka juu mbinguni, awaendee makahaba na watoza ushuru, awaendee waliosumbuliwa na ibilisi na mapepo, na sio kwa makuhani na waandishi, ijapokuwa na hao pia alikuja kuwafia, lakini nguvu zake nyingi zilikuwa kwa wenye dhambi.

Bwana atupe neema hiyo.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

UWEZA WA MUNGU NJE YA WAKATI.

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

USIWE ADUI WA BWANA

Rudi Nyumbani

Print this post

Sala ya baraka (Hesabu 6:24-26).

(Masomo maalumu kwa watumishi wa Mungu).

Katika agano la Kale, Mungu aliwafundisha Haruni (aliyekuwa kuhani mkuu) pamoja na wanawe wote, jinsi ya kuwabarikia wana wa Israeli, na kupitia sala hiyo, au matamko hayo wana wa Israeli walibarikiwa kweli kweli.

Sala hiyo pia inaweza kutumika na watumishi wa Mungu leo, kulibarikia kundi la MUNGU, kwani nao pia ni makuhani kwa Mungu sawasawa na Ufunuo 1:6

Sala hiyo tunaisoma katika Hesabu 6:22-27.

Hesabu 6:22 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

23 Nena na Haruni na wanawe, uwaambie, HIVI NDIVYO MTAKAVYOWABARIKIA WANA WA ISRAELI; MTAWAAMBIA

24 Bwana akubarikie, na kukulinda;

25 Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;

26 Bwana akuinulie uso wake, na kukupa Amani

27 Ndivyo watakavyoweka jina langu juu ya wana wa Israeli; nami nitawabarikia”

Na baraka hizo ni lazima zitamkwe baada ya watu kufundishwa kanuni za kubarikiwa, na kupokea Amani ya kiMungu na ulinzi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

FIMBO YA HARUNI!

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

HARUNI

Rudi Nyumbani

Print this post

Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya (Kutoka 14:14)

Kutoka 14:13 “Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.

14 BWANA ATAWAPIGANIA NINYI, NANYI MTANYAMAZA KIMYA”.

Matokeo ya kupiganiwa na Bwana ni “Mwisho wa Manung’uniko, malalamiko, masononeko, huzuni na maumivu”.

Ndicho kilichowatokea wana wa Israeli pale walipoliona jeshi la Farao likija nyuma yao, na mbele yao kuna kizuizi cha bahari, (nyuma mauti inakuja, mbele mauti inawangojea).. wakaogopa mno na kupaniki na kuanza kumlaumu Musa, wakasahau mambo makuu waliyotendewa na Mungu masaa kadhaa na siku kadhaa nyuma, jinsi alivyompiga Farao kwa mapigo makuu.

Sasa ni rahisi sana kuwalaumu wana wa Israeli kuwa ni wajinga na wasiokumbuka!.. Lakini majaribu kama hayo hayo yanatukuta wengi leo na tunakuwa  tunasahau fadhili za Mungu alizotutendea siku kadhaa au miaka kadhaa nyuma.

Hivyo unapotazama na kuona mauti mbele yako na nyuma yako unaona Giza, kiasi kwamba unajikuta unakosa utulivu na hata wakati mwingine kujiona upo katika hatari ya kutoa maneno mabaya kutoka katika kinywa chako… unapofikia hiyo hatua, basi huo si wakati wa kunung’unika, wala kulalamika, ni wakati wa wewe kumwomba MUNGU AKUPE UTULIVU.

Na unamwomba UTULIVU kwa wewe kumsihi asimame AKUPIGANIE VITA VILIVYOPO MBELE YAKO, Na ikiwa moyo wako umenyooka mbele zake basi utaona mkono wake akikupigania kama alivyowapigania waIsraeli NAWE UTAKAA KIMYA, ile huzuni itayeyuka, ile aibu itapotea, ile kiu ya kusema maneno mabaya na ya makufuru itayeyuka, nawe utajaa nyimbo za shangwe na sifa na shukrani kama wana wa Israeli walizoziimba baada ya bahari kupasuka na kuwameza maadui zao.

Kutoka 15:1 “Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia Bwana wimbo huu wakanena, na kusema, Nitamwimbia Bwana, kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.

2 Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.

3 Bwana ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lake.

4 Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini, Maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.

5 Vilindi vimewafunikiza, Walizama vilindini kama jiwe.

6 Bwana, mkono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo, Bwana, mkono wako wa kuume wawasetaseta adui.

7 Kwa wingi wa ukuu wako wawaangusha chini wanaokuondokea, Wapeleka hasira yako, nayo huwateketeza kama mabua makavu.

8 Kwa upepo wa mianzi ya pua yako maji yalipandishwa, Mawimbi yakasimama juu wima mfano wa chungu, Vilindi vikagandamana ndani ya moyo wa bahari.

9 Adui akasema, Nitafuatia, nitapata, nitagawanya nyara, Nafsi yangu itashibishwa na wao; Nitaufuta upanga wangu, mkono wangu utawaangamiza.

10 Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza; Wakazama kama risasi ndani ya maji makuu”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je Farao alikufa kwenye maji pamoja na jeshi lake au alipona?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

USIMWABUDU SHETANI!

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Makasia ni nini? (Yona 1:13).

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwanzo 1:26-27 (Tumfanye mtu kwa mfano wetu).

Mwanzo1:26 “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba

Mnyumbuliko:

>Tumfanye – Mungu analishirikisha jeshi lake la Mbinguni wazo lake la uumbaji, kama alivyofanya katika 2Nyakati 18:18-19

> Kwa sura – Mwonekano wa nje kama kichwa, kiwiliwili na miguu.

> Mfano wetu – Utu wa ndani kama Roho, na nafsi.

> Wakatawale – Wakawatiishe, wakawatumie, na kuwaongoza.

Somo kamili kuhusiana na kuumbwa kwa sura na mfano wa Mungu fungua hapa >>Nini maana ya tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mungu alikuwa anaongea na nani aliposema na “Tumfanye mtu kwa mfano wetu (Mwanzo 1:26)?

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

DANIELI: Mlango wa 9

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuapiza ni nini? (Mathayo 5:21-22)

Mathayo 5:21  Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu. 22  Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto.

JIBU: Katika vifungu hivi tunaona Bwana Yesu anatoa mtazamo mpya kuhusiana na dhambi ya uuaji. Hapo mwanzo ilidhaniwa kuwa pale mtu anapochukua hatua ya kumchinja ndugu yake, au kumpiga mpaka kufa kama alivyofanya Kaini, ndio umehitimu kuwa muuaji. Lakini Bwana Yesu anasema..

Kitendo  tu cha kumwonea hasira ndugu yako, kumfyolea, na kumwapiza, tayari ni kosa la uuaji.

Sasa alikuwa na maana gani kwa maneno hayo matatu. “Hasira, kufyolea na kuapiza?”

Hasira kwa ndugu, huzaa mambo kama kinyongo, uchungu, na wivu. Kwahiyo kama mtu akiwa na mambo kama hayo  kwa ndugu yake, mbele ya Kristo amestahili kuhukumiwa.

Lakini pia akimfyolea. Kumfyolea ni kumwita mwenzako mjinga wewe, au mpumbavu wewe. Ukilenga mtu asiye na akili, Kwa urefu wa tafsiri hii fungua hapa>> RACA Hilo nao ni kosa lililostahili kuketishwa kwenye mabaraza ya wazee, utoe hesabu.

Lakini mbaya zaidi kumwapiza. Hichi ni kitendo cha kumtamkia kabisa maneno ya  laana. Kana kwamba ni mtu mwovu sana aliyepindukia. Kwamfano kumwita ndugu yako mwana-haramu wewe, au kumwita ‘shoga wewe’, kumwita msenge(neno lenye maana mtu anayeshiriki uovu kinyume na jinsia yake), kumwita pepo, kafiri wewe, n.k. maneno ambayo hayawezi kutamkika, ni sawa na tusi kwa mwenzako. Huko ndio kuapiza.

Adhabu yake Kristo anaifananisha na kutupwa katika jehanamu ya moto.

Hivyo hatupaswi kudhani kuwa, kuua ni mpaka tumwage damu, lakini twaweza kufanya hivyo tokea moyoni mwetu hadi vinywani mwetu, kabla hata hatujafikia kwenye kitendo chenyewe.

Tujazwe Roho Mtakatifu, tuwezi kuzishinda tabia hizi mbaya za mwili.

Katika agano la kale ilikuwa sio tu kumpiga mzazi wako, ilikupasa kifo (Kutoka 21:15), lakini pia kumwapiza huku, adhabu yake ilikuwa ni moja tu na hilo kosa la kwanza yaani kifo.

Kutoka 21:17 “Yeye amwapizaye baba yake au mama yake, sharti atauawa”

Shalom.

Je! Umeokoka? Fahamu kuwa usipomwamini Kristo, na kupokea msamaha wake wa dhambi, hauna uzima wa milele ndani yako. Kwasababu kamwe hutakaa umpendeze Mungu kwa nguvu zako au matendo yako mwenyewe. Na sababu ya Yesu kufa msalabani kwa ajili yako kukusaidia, kupokea msamaha wa dhambi, lakini pia nguvu ya kushinda mambo mabaya kwa Roho wake Mtakatifu tuliopewa. Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu akuokoe leo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo ya wokovu, Bwana akubariki >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Amen

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bwana alimaanisha nini kusema “atazamaye mwanamke kwa kumtamani” amezini naye?

Je ni sahihi kumwita mtu “Mkuu”?

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

UFANYE MOYO WA MUNGU UWAELEKEE WATU WAKE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je biblia inajichanganya kwa habari za Yohana kuwa Eliya?

Swali: Tunaona sehemu moja Bwana YESU akimshuhudia Yohana Mbatizaji kuwa yeye ndiye Eliya ajaye (Mathayo 11:14), lakini sehemu nyingine Yohana Mbatizaji anakataa jambo hilo kuwa yeye si Eliya, (Yohana 1:19-21) je ni yupi yupo sahihi, Bwana Yesu au Yohana Mbatizaji?.. au je biblia inajichanganya?

Jibu: Turejee mistari hiyo..

Mathayo 11:13 “Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana.

14  Na ikiwa mnataka kukubali, yeye ndiye Eliya atakayekuja”.

Ni kweli hapa Bwana YESU anasema “Yohana Mbatizaji ndiye Eliya ajaye”. Lakini kumbuka kuwa Bwana YESU hakumlenga Eliya kama Eliya, kwamba atarudi tena na kutokea duniani kuhubiri!.. La! Bali alimaanisha “roho ya Eliya/ huduma ya Eliya” ipo ndani ya Yohana Mbatizaji.

Ni sawa na kwenye ule mfano wa Lazaro na Tajiri Bwana YESU aliowaambia watu, pale Ibrahimu aliposema “Wanaye Musa na Manabii (Luka 16:29)” hakumaanisha Musa yupo sasahivi, bali alimaanisha kuwa watumishi wa Mungu wanaohubiri leo ndio akina Musa..

Hivyo Bwana YESU aliposema Yohana Mbatizaji ndiye Eliya alimaanisha ile roho iliyokuwa inatenda kazi ndani ya Eliya sasa ipo juu ya Yohana Mbatizaji. Sawasawa na ujumbe wa Malaika, aliompa Zakaria baba yake Yohana, kuwa mtoto atakayezaliwa atatangulia mbele za Bwana katika roho ya Eliya, lakini hatakuwa Eliya.

Luka 1:13 “Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana.

14  Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.

15  Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye.

16  Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao.

17  NAYE ATATANGULIA MBELE ZAKE KATIKA ROHO YA ELIYA, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa.”

Hapo mstari wa 17 unasema, “Atatangulia katika roho ya Eliya”…na si kwamba atakuwa Eliya mwenyewe yule aliyepaa.. (Yule alishaondoka na hawezi kurudi tena).. Hivyo Yohana Mbatizaji, alijijua kuwa roho ya Eliya inatenda kazi ndani yake, lakini yeye si Eliya, na ndio maana walipomwuliza kama yeye ni Eliya akajibu siye.

Kwanini alijibu vile?..kwasababu ni kweli hakuwa Eliya, isipokuwa Huduma ya Eliya/roho iliyokuwa juu ya Eliya inatenda kazi ndani yake.

Yohana 1:19 “Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?

20  Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.

21  Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kuwa Yohana Mbatizaji hakuwa Eliya aliyerudi… bali ni mtu ambaye roho ya Eliya ilikuwa inatenda kazi ndani yake. Hivyo biblia haijichanganyi mahali popote.

Je umeokoka?.. Kama bado basi fahamu kuwa unyakuo wa kanisa upo karibu sana, na Kristo amekaribia kulichukua kanisa lake. Hivyo fanya uamuzi sahihi leo wa kumkabidhi Bwana YESU maisha yako kabla ya ule mwisho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

Je! ile habari ya Herode kutaka kumwua Yohana mbatizaji inajichanganya?(Mathayo 14:5 na Marko 6:20).

ROHO YA ELIYA KATIKA AGANO JIPYA INATENDAJE KAZI?.

YOHANA MBATIZAJI

Rudi Nyumbani

Print this post