Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, Karibu tujifunze maneno ya uzima.
Katika agano la kale ilikuwa ni sheria, ili sadaka ya upatanisho, au ya dhambi ambayo ilihusisha kafara za wanyama, kuwa kamili, ni lazima uhusishwe na sehemu kuu mbili, ya kwanza ni ndani ya kambi, na ya pili ni nje ya kambi.
Ndani ya kambi au ndani ya lango, ndio ilichukuliwa damu ya mnyama huyo na kuingizwa kwa ajili ya upatanisho kwa kunyunyizwa. Lakini ilikuwa ni sharti pia viungo, ngozi na vinyesi, vya mnyama huyo vikateketezwe mbali nje ya kambi. Na kama jambo hilo lisipofanyika, haijalishi damu ya kunyunyiza ya mnyama huyo itakuwa ni njema kiasi gani, utapatanisho hauwezi kutokea.
Ndani ya kambi ni mahali patakatifu, lakini je! Ya kambi ni mahali pa uovu.
Sasa tukirudi kwenye agano jipya, tunaona mwokozi wetu Yesu Kristo, anafananisha na mnyawa huyo wa upatanisho, Hivyo ilimbidi, ahusishwe pia na sehemu zote mbili, yaani ndani ya kambi na nje ya kambi.
Alimwaga damu yake, ambayo kwa kupitia hiyo, ameingia nayo patakatifu pa patakatifu kule mbinguni, kutuombea sisi, Lakini hilo lisingewezekana, kama asingeteketezwa nje ya kambi.
Ndio Hapo tunaona Bwana wetu, ilimpasa, aache enzi na mamlaka mbinguni, (Atoke nje ya kambi), akutane na waovu huku duniani, ateketezwe kabisa mahali pa aibu pa waovu pale Golgota, ili sasa damu yake ipatikane kufanya upatanisho wetu kule mbinguni, kwa Baba ambapo ndio ndani ya kambi.
Na matokeo yake ndio haya tunayoyaona sasa hivi, sote kupata neema na ondoleo la dhambi zetu.
Lakini sasa maandiko yanasema..
Waebrania 13:11 Maana wanyama wale ambao damu yao huletwa ndani ya patakatifu na kuhani mkuu kwa ajili ya dhambi, viwiliwili vyao huteketezwa nje ya kambi.
12 KWA AJILI HII YESU NAYE, ILI AWATAKASE WATU KWA DAMU YAKE MWENYEWE, ALITESWA NJE YA LANGO.
13 BASI NA TUTOKE TUMWENDEE NJE YA KAMBI, TUKICHUKUA SHUTUMU LAKE.
14 Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.
Umeona hapo? Kumbe na sisi, hatuna budi kumfuata Yesu nyayo zake, kwasababu alisema mimi nilipo na mtumishi wangu atakuwepo. Sasa hapo anasema, na sisi tutoke nje ya kambi, tuchukue shutumu lake. Akiwa na maana, tukubali kujitoa sadaka na sisi, nje ya lango, waovu walipo ili tuwavute wengine kwa mwokozi.
Kama mashahidi wa kweli wa Kristo, ni lazima tuwe tayari kuhatarisha maisha yetu, kwa ajili ya wengine. Tusiwe tu ndani ya lango, walipo watakatifu, ni kweli ni vizuri kufanya semina za ndani makanisani zina nafasi yake, ni vizuri kuhubiri mikutano ya ndani. Lakini je! Tunaweza tukawa tayari pia kwenda katikati ya watu wa dini nyingine kuwahubiria Kristo, tukawa tayari kwenda mahali pa jamii zenye vita na kuzitangaza habari za Yesu. Kanisa la Kwanza la mitume lilikuwa tayari kutoka nje ya kambi, kukutana na ukinzani wa wayahudi, kuburutwa, kupigwa mawe hata kuawa, walikuwa tayari kuwaendea wapagani sugu, na jamii za wachawi kuwatangazia Kristo. Vivyo hivyo na sisi hatuna budi kutoka nje ya kambi, kuliendea na kundi lingine ambalo halijamjua Kristo.
Hatuna budi kuwa tayari hata kuhatarisha afya zetu, fedha zetu, kazi zetu, vyeo vyetu, elimu zetu inapobidi ili wengine waokoke, wamjue Kristo. Huko ndiko kutoka nje ya kambi. Bwana Yesu ilimpasa aache enzi na mamlaka juu mbinguni, awaendee makahaba na watoza ushuru, awaendee waliosumbuliwa na ibilisi na mapepo, na sio kwa makuhani na waandishi, ijapokuwa na hao pia alikuja kuwafia, lakini nguvu zake nyingi zilikuwa kwa wenye dhambi.
Bwana atupe neema hiyo.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
(Masomo maalumu kwa watumishi wa Mungu).
Katika agano la Kale, Mungu aliwafundisha Haruni (aliyekuwa kuhani mkuu) pamoja na wanawe wote, jinsi ya kuwabarikia wana wa Israeli, na kupitia sala hiyo, au matamko hayo wana wa Israeli walibarikiwa kweli kweli.
Sala hiyo pia inaweza kutumika na watumishi wa Mungu leo, kulibarikia kundi la MUNGU, kwani nao pia ni makuhani kwa Mungu sawasawa na Ufunuo 1:6
Sala hiyo tunaisoma katika Hesabu 6:22-27.
Hesabu 6:22 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
23 Nena na Haruni na wanawe, uwaambie, HIVI NDIVYO MTAKAVYOWABARIKIA WANA WA ISRAELI; MTAWAAMBIA
24 Bwana akubarikie, na kukulinda;
25 Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;
26 Bwana akuinulie uso wake, na kukupa Amani
27 Ndivyo watakavyoweka jina langu juu ya wana wa Israeli; nami nitawabarikia”
Na baraka hizo ni lazima zitamkwe baada ya watu kufundishwa kanuni za kubarikiwa, na kupokea Amani ya kiMungu na ulinzi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)
Kutoka 14:13 “Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.
14 BWANA ATAWAPIGANIA NINYI, NANYI MTANYAMAZA KIMYA”.
Matokeo ya kupiganiwa na Bwana ni “Mwisho wa Manung’uniko, malalamiko, masononeko, huzuni na maumivu”.
Ndicho kilichowatokea wana wa Israeli pale walipoliona jeshi la Farao likija nyuma yao, na mbele yao kuna kizuizi cha bahari, (nyuma mauti inakuja, mbele mauti inawangojea).. wakaogopa mno na kupaniki na kuanza kumlaumu Musa, wakasahau mambo makuu waliyotendewa na Mungu masaa kadhaa na siku kadhaa nyuma, jinsi alivyompiga Farao kwa mapigo makuu.
Sasa ni rahisi sana kuwalaumu wana wa Israeli kuwa ni wajinga na wasiokumbuka!.. Lakini majaribu kama hayo hayo yanatukuta wengi leo na tunakuwa tunasahau fadhili za Mungu alizotutendea siku kadhaa au miaka kadhaa nyuma.
Hivyo unapotazama na kuona mauti mbele yako na nyuma yako unaona Giza, kiasi kwamba unajikuta unakosa utulivu na hata wakati mwingine kujiona upo katika hatari ya kutoa maneno mabaya kutoka katika kinywa chako… unapofikia hiyo hatua, basi huo si wakati wa kunung’unika, wala kulalamika, ni wakati wa wewe kumwomba MUNGU AKUPE UTULIVU.
Na unamwomba UTULIVU kwa wewe kumsihi asimame AKUPIGANIE VITA VILIVYOPO MBELE YAKO, Na ikiwa moyo wako umenyooka mbele zake basi utaona mkono wake akikupigania kama alivyowapigania waIsraeli NAWE UTAKAA KIMYA, ile huzuni itayeyuka, ile aibu itapotea, ile kiu ya kusema maneno mabaya na ya makufuru itayeyuka, nawe utajaa nyimbo za shangwe na sifa na shukrani kama wana wa Israeli walizoziimba baada ya bahari kupasuka na kuwameza maadui zao.
Kutoka 15:1 “Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia Bwana wimbo huu wakanena, na kusema, Nitamwimbia Bwana, kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.
2 Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.
3 Bwana ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lake.
4 Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini, Maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.
5 Vilindi vimewafunikiza, Walizama vilindini kama jiwe.
6 Bwana, mkono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo, Bwana, mkono wako wa kuume wawasetaseta adui.
7 Kwa wingi wa ukuu wako wawaangusha chini wanaokuondokea, Wapeleka hasira yako, nayo huwateketeza kama mabua makavu.
8 Kwa upepo wa mianzi ya pua yako maji yalipandishwa, Mawimbi yakasimama juu wima mfano wa chungu, Vilindi vikagandamana ndani ya moyo wa bahari.
9 Adui akasema, Nitafuatia, nitapata, nitagawanya nyara, Nafsi yangu itashibishwa na wao; Nitaufuta upanga wangu, mkono wangu utawaangamiza.
10 Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza; Wakazama kama risasi ndani ya maji makuu”.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je Farao alikufa kwenye maji pamoja na jeshi lake au alipona?
Mwanzo1:26 “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba
Mnyumbuliko:
>Tumfanye – Mungu analishirikisha jeshi lake la Mbinguni wazo lake la uumbaji, kama alivyofanya katika 2Nyakati 18:18-19
> Kwa sura – Mwonekano wa nje kama kichwa, kiwiliwili na miguu.
> Mfano wetu – Utu wa ndani kama Roho, na nafsi.
> Wakatawale – Wakawatiishe, wakawatumie, na kuwaongoza.
Somo kamili kuhusiana na kuumbwa kwa sura na mfano wa Mungu fungua hapa >>Nini maana ya tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mungu alikuwa anaongea na nani aliposema na “Tumfanye mtu kwa mfano wetu (Mwanzo 1:26)?
TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.
Mathayo 5:21 Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu. 22 Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto.
JIBU: Katika vifungu hivi tunaona Bwana Yesu anatoa mtazamo mpya kuhusiana na dhambi ya uuaji. Hapo mwanzo ilidhaniwa kuwa pale mtu anapochukua hatua ya kumchinja ndugu yake, au kumpiga mpaka kufa kama alivyofanya Kaini, ndio umehitimu kuwa muuaji. Lakini Bwana Yesu anasema..
Kitendo tu cha kumwonea hasira ndugu yako, kumfyolea, na kumwapiza, tayari ni kosa la uuaji.
Sasa alikuwa na maana gani kwa maneno hayo matatu. “Hasira, kufyolea na kuapiza?”
Hasira kwa ndugu, huzaa mambo kama kinyongo, uchungu, na wivu. Kwahiyo kama mtu akiwa na mambo kama hayo kwa ndugu yake, mbele ya Kristo amestahili kuhukumiwa.
Lakini pia akimfyolea. Kumfyolea ni kumwita mwenzako mjinga wewe, au mpumbavu wewe. Ukilenga mtu asiye na akili, Kwa urefu wa tafsiri hii fungua hapa>> RACA Hilo nao ni kosa lililostahili kuketishwa kwenye mabaraza ya wazee, utoe hesabu.
Lakini mbaya zaidi kumwapiza. Hichi ni kitendo cha kumtamkia kabisa maneno ya laana. Kana kwamba ni mtu mwovu sana aliyepindukia. Kwamfano kumwita ndugu yako mwana-haramu wewe, au kumwita ‘shoga wewe’, kumwita msenge(neno lenye maana mtu anayeshiriki uovu kinyume na jinsia yake), kumwita pepo, kafiri wewe, n.k. maneno ambayo hayawezi kutamkika, ni sawa na tusi kwa mwenzako. Huko ndio kuapiza.
Adhabu yake Kristo anaifananisha na kutupwa katika jehanamu ya moto.
Hivyo hatupaswi kudhani kuwa, kuua ni mpaka tumwage damu, lakini twaweza kufanya hivyo tokea moyoni mwetu hadi vinywani mwetu, kabla hata hatujafikia kwenye kitendo chenyewe.
Tujazwe Roho Mtakatifu, tuwezi kuzishinda tabia hizi mbaya za mwili.
Katika agano la kale ilikuwa sio tu kumpiga mzazi wako, ilikupasa kifo (Kutoka 21:15), lakini pia kumwapiza huku, adhabu yake ilikuwa ni moja tu na hilo kosa la kwanza yaani kifo.
Kutoka 21:17 “Yeye amwapizaye baba yake au mama yake, sharti atauawa”
Shalom.
Je! Umeokoka? Fahamu kuwa usipomwamini Kristo, na kupokea msamaha wake wa dhambi, hauna uzima wa milele ndani yako. Kwasababu kamwe hutakaa umpendeze Mungu kwa nguvu zako au matendo yako mwenyewe. Na sababu ya Yesu kufa msalabani kwa ajili yako kukusaidia, kupokea msamaha wa dhambi, lakini pia nguvu ya kushinda mambo mabaya kwa Roho wake Mtakatifu tuliopewa. Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu akuokoe leo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo ya wokovu, Bwana akubariki >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Amen
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Bwana alimaanisha nini kusema “atazamaye mwanamke kwa kumtamani” amezini naye?
Je ni sahihi kumwita mtu “Mkuu”?
Swali: Tunaona sehemu moja Bwana YESU akimshuhudia Yohana Mbatizaji kuwa yeye ndiye Eliya ajaye (Mathayo 11:14), lakini sehemu nyingine Yohana Mbatizaji anakataa jambo hilo kuwa yeye si Eliya, (Yohana 1:19-21) je ni yupi yupo sahihi, Bwana Yesu au Yohana Mbatizaji?.. au je biblia inajichanganya?
Jibu: Turejee mistari hiyo..
Mathayo 11:13 “Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
14 Na ikiwa mnataka kukubali, yeye ndiye Eliya atakayekuja”.
Ni kweli hapa Bwana YESU anasema “Yohana Mbatizaji ndiye Eliya ajaye”. Lakini kumbuka kuwa Bwana YESU hakumlenga Eliya kama Eliya, kwamba atarudi tena na kutokea duniani kuhubiri!.. La! Bali alimaanisha “roho ya Eliya/ huduma ya Eliya” ipo ndani ya Yohana Mbatizaji.
Ni sawa na kwenye ule mfano wa Lazaro na Tajiri Bwana YESU aliowaambia watu, pale Ibrahimu aliposema “Wanaye Musa na Manabii (Luka 16:29)” hakumaanisha Musa yupo sasahivi, bali alimaanisha kuwa watumishi wa Mungu wanaohubiri leo ndio akina Musa..
Hivyo Bwana YESU aliposema Yohana Mbatizaji ndiye Eliya alimaanisha ile roho iliyokuwa inatenda kazi ndani ya Eliya sasa ipo juu ya Yohana Mbatizaji. Sawasawa na ujumbe wa Malaika, aliompa Zakaria baba yake Yohana, kuwa mtoto atakayezaliwa atatangulia mbele za Bwana katika roho ya Eliya, lakini hatakuwa Eliya.
Luka 1:13 “Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana.
14 Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye.
16 Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao.
17 NAYE ATATANGULIA MBELE ZAKE KATIKA ROHO YA ELIYA, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa.”
Hapo mstari wa 17 unasema, “Atatangulia katika roho ya Eliya”…na si kwamba atakuwa Eliya mwenyewe yule aliyepaa.. (Yule alishaondoka na hawezi kurudi tena).. Hivyo Yohana Mbatizaji, alijijua kuwa roho ya Eliya inatenda kazi ndani yake, lakini yeye si Eliya, na ndio maana walipomwuliza kama yeye ni Eliya akajibu siye.
Kwanini alijibu vile?..kwasababu ni kweli hakuwa Eliya, isipokuwa Huduma ya Eliya/roho iliyokuwa juu ya Eliya inatenda kazi ndani yake.
Yohana 1:19 “Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?
20 Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.
21 Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La”.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kuwa Yohana Mbatizaji hakuwa Eliya aliyerudi… bali ni mtu ambaye roho ya Eliya ilikuwa inatenda kazi ndani yake. Hivyo biblia haijichanganyi mahali popote.
Je umeokoka?.. Kama bado basi fahamu kuwa unyakuo wa kanisa upo karibu sana, na Kristo amekaribia kulichukua kanisa lake. Hivyo fanya uamuzi sahihi leo wa kumkabidhi Bwana YESU maisha yako kabla ya ule mwisho.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.
Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?
Je! ile habari ya Herode kutaka kumwua Yohana mbatizaji inajichanganya?(Mathayo 14:5 na Marko 6:20).
Jibu:Turejee,
Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.
13 KWA MAANA MANABII WOTE NA TORATI WALITABIRI MPAKA WAKATI WA YOHANA”.
Mstari huo haumaanishi kuwa Torati yote na Manabii wote walimtabiri Yohana Mbatizaji.. kwamba atakuja kutokea na kuhubiri, na kwamba atakuwa nabii mkuu kuliko wote. Hapana, bali ilimaanisha kuwa Torati iliendelea kuwepo na kufanya kazi, na manabii waliendelea kutokea na kutoa unabii, mpaka wakati wa Yohana kutokea duniani.. na baada ya Yohana ndipo likaanza agano lingine jipya la ufalme wa Mungu kutangazwa na kila mtu kujiingiza kwa nguvu.
Maneno hayo yamewekwa katika Kiswahili kirahisi Zaidi katika kitabu cha Luka..
Luka 16:16 “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”.
Sasa kufahamu nini maana ya Torati na Manabii fungua hapa >>>Nini maana ya “Torati na manabii”?
Lakini ni kwanini aseme tangu wakati wa Yohana ufalme wa Mungu unapatikana kwa nguvu na watu wanajiingiza kwa nguvu??..Ni kuonyesha kuwa hapo kwanza ilikuwa haiwezekani mtu kujiingiza katika ufalme wa Mungu..ilihitaji kuingizwa.. na waliokuwa wamesimama kama waingizaji wa watu katika ufalme wa Mungu ni Manabii na Torati..
Watu walisubiri maagizo ya Mungu kupitia Nabii au kuhani ndipo wapatanishwe na Mungu… lakini baada ya Bwana YESU kufa na kufufuka kiti cha rehema kimefunguliwa.. Watu hawahitaji tena manabii wala makuhani kumkaribia Mungu… (Maana yake kila mtu ana uwezo wa kumkaribia Mungu kupitia damu ya YESU).
Hatuhitaji tena kwenda Yerusalemu kwa makuhani ndipo tumsikie Mungu, hatuhitaji tena sanduku la agano, hatuhitaji tena nabii atokee ndipo atupe maagizo ya Mungu.. bali kupitia Roho Mtakatifu ndani yetu tunamkaribia yeye.
Kwa kadiri tunavyotia bidii ndivyo tunavyoukaribia na kuuteka ule ufalme..na wenye hekima na bidii ndio wanaoukaribia Zaidi ule ufalme.
Bwana atusaidie.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
Swali: Je biblia inajichanganya kwa habari ya Bwana YESU kumjibu Pilato? Maana katika (Yohana 18:33-34) inasema alimjibu lakini katika (Mathayo 27:13-14).. inasema hakujibu chochote alipoulizwa? Je lipi ni sahihi?
Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa biblia haijichanganyi mahali popote pale, isipokuwa kinachojichanganya ni tafakari zetu, na fahamu zetu… Lakini biblia ni kitabu kikamilifu na kilichovuviwa na Roho Mtakatifu wa Mungu, hivyo hakina kasoro yoyote.
Sasa tukirejea habari hiyo katika Yohana 18:33-37.
Yohana 18:33 “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?
34 Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?
35 Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?
36 Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.
37 Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu”
Hapa ni kweli tunasoma Bwana YESU alimjibu Pilato alipoulizwa kuhusu habari zake mwenyewe… Lakini tukirejea kitabu cha Mathayo ni kama tunasoma habari tofauti kidogo.
Mathayo 27:11 “Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, WEWE WASEMA.
12 Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno.
13 Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?
14 Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”.
Hapa tunasoma Bwana YESU hamjibu Pilato.. Sasa swali je! Biblia inajichanganya??..Jibu ni la! Haijichanganyi.
Tukisoma vizuri habari hizo mbili zinaelezea kisa kimoja lakini katika mazingira manne tofauti..
Wakati Bwana anafikishwa kwa Pilato, alitangulia liwali kumhoji Bwana YESU kama yeye ndiye mfalme wa Wayahudi hapo alijibu “wewe wasema (maana yake ndio mimi ndiye)” Huyo ni Liwali anahoji na anajibiwa na Bwana bila maficho yoyote.
Mathayo 27:11 “Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, WEWE WASEMA…”
Lakini wakati ambao Wazee wa makuhani wanamshitaki Bwana YESU kwa Pilato yeye hakujibu chochote..
Kumbuka hapa wazee wa makuhani hawakuwa wanamhoji kuhusiana na swali alilouliza Liwali kwamba kama yeye ni mfalme wa Wayahudi…LA! Bali wazee wa makuhani wenyewe walikuwa wanamshitaki kwa mambo mengine ikiwamo habari ya kulivunja hekalu pamoja na kujiita mwana wa Mungu.. Soma Mathayo 26:62-68..Na sasa wanataka wamsikie Bwana YESU akijitetea mbele ya Pilato. Lakini Bwana YESU hakujibu chochote.
Mathayo 27:12 “Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno”.
Pilato aliposimama na kumwuliza Bwana YESU ajitetee, mbele ya wazee wa makuhani kuhusiana na mashtaka hayo (ya kulivunja hekalu na kujiita mwana wa Mungu).. yeye hakujibu chochote mpaka Liwali akashangaa!!..
Mathayo 27:13 “Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?
14 Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”
Na kwanini Bwana YESU hakumjibu hapa Pilato lolote?.. JIbu ni kwasababu Wazee wa Makuhani ambao waliokuwa ni wanafiki walikuwepo pale wakitafuta neno litokalo kinywani mwake ili waanze kuzusha maneno mengi juu yake..hivyo Bwana hakumjibu Pilato wala makuhani.
Pilato alipoona hapati jibu lolote kuhusiana na mashtaka ya wayahudi juu ya Bwana.. alimchukua Bwana YESU ndani ya Praitorio na kumwoji akiwa peke yake swali lile lile aliloulizwa na Liwali! (Je wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi?)..na Bwana YESU akampa jibu kama lile lile alilompa Liwali.
Yohana 18:33 “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?
34 Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?…”
Umeona?… Kwahiyo biblia haijichanganyi yenyewe.. Ni kwamba Bwana YESU hakujibu mashtaka ya Wazee wa Wayahudi lakini alijibu maswali ya Pilato na Liwali.
Na kwanini Bwana YESU asijibu mashtaka ya wazee wa makuhani? Na amjibu Liwali pamoja na Pilato peke yao?…ni kwasababu wale wazee walikuwa wamemkusanyikia kwa shari, wapate kumwongezea dhiki….
Maswali yao si ya lengo la kutaka kujua, bali kutafuta sababu za kumshitaki..kwani tayari alishawajibu huko nyuma lakini bado waliendelea kumtafuta kwa maswali mengine mengi (Mathayo 26:62-68).
Kwahiyo na sisi tunachoweza kujifunza ni utulivu na kunyamaza katika vipindi ambavyo adui anatumia vinywa vya watu kutujaribu.. Ukishajibu swali mara ya kwanza, na mtu haelewi badala yake anatafuta tu kasoro, basi kinachofuata baada ya hapo ni kukaa kimya.
Kwasababu yapo maswali ambayo ukijibu hayatamsaidia yule anayeuliza badala yake yatampa kila sababu za kukusumbua wewe ziaidi, kwasababu lengo lake si kutaka kujua bali ni kubishana au kukudhuru wewe au kukushambulia. Hivyo ni muhimu kuwa makini.
Tito 3:9 “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana.
10 Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae”
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.
Jina la Bwana na Mwokozi Mkuu YESU KRSTO libarikiwe daima!
Kuna tofauti ya kumjua YESU WA KIDINI na yule wa UFUNUO (Yaani Yesu aliyefunuliwa maishani mwako na yule uliyempokea kwa wazazi au kwa mhubiri fulani) Utauliza kivipi?..Hebu tumwangalie mtu mmoja katika biblia ambaye hapo kwanza alimjua YESU wa kidini lakini baadaye akaja kumpokea wa KIUFUNUO, Na ikawa heri kwake!. Na mtu huyo si mwingine Zaidi ya Petro.
Yohana 1:40 “Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.
41 Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, TUMEMWONA MASIHI (MAANA YAKE, KRISTO).
42 Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe)”
Hapa Petro anamjua na kumpokea YESU kwa kuambiwa TU!!!…Anaambiwa na Adrea kaka yake habari za YESU, hivyo Petro anaamini na akampokea YESU wa kidini, akawaa mfuasi wa YESU tu, lakini bado hajafunuliwa ndani yake!. Akamjua tu kulingana na dini ya kiyahudi kuwa atakuja Masihi na hivyo amemwona! Na si Zaidi.
Baada ya kipindi kirefu kupita, Petro ampokea YESU wa ufunuo na hapo inakuwa heri kwake.
Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”.
Umeona hapo?… Petro amemjua YESU KIUFUNUO!.. aliyefunuliwa na Baba wa mbinguni, na si yule aliyeambiwa na kaka yake Andrea.
Kumbuka tayari alikuwa ameshajua kuwa YESU ndiye Kristo, kwani Andrea alishamwambia… Lakini ni kidini tu!..alipotulia na kumruhusu Roho Mtakatifu afanye kazi ndani yake ndipo akajua huyu wa kidini hatoshi, na kumbe YESU NA ZAIDI NA ALIVYOKUWA ANAMFIKIRIA..
Na utaona baada ya hapo ndipo Bwana anampa Petro funguo za Ufalme wa Mungu, baada tu ya kumpata YESU WA UFUNUO.
Mathayo 16:17 “Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.
19 NAMI NITAKUPA WEWE FUNGUO ZA UFALME WA MBINGUNI; NA LO LOTE UTAKALOLIFUNGA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGWA MBINGUNI; NA LO LOTE UTAKALOLIFUNGUA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGULIWA MBINGUNI”
Ni Kwanini leo hii, wengi funguo za ufalme wa Mungu hawana???… Sababu kuu ni YESU WALIYE NAYE MAISHANI MWAO si wa ufunuo bali wa kidini… Kama ni wa kidini huyo hawezi kufungua lolote ndani yao, lakini kama ni yule wa UFUNUO huyo anafungua mbingu na nchi!.
Sasa swali tunampataje YESU WA UFUNUO.
Tunampata YESU wa ufunuo kwanza kwa kuweka mbali mapokeo, na udini, na udhehebu na ujuaji na kumruhusu ROHO MTAKATIFU afanye ndani yako kwa unyenyekevu wote..huku ukiwa umejikana nafsi yako na kujitwika msalaba wako… Kidogo kidogo utaanza kumwona YESU kwa UFAHAMU MWINGINE, Na utayagundua mengi kumhusu yeye, na hayo mambo mapya utakayoyapata kumhusu YESU ndiyo mafunuo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?
Petro na Adrea waliitwa na Bwana wakati gani?
HERI, WALE MUNGU ASIOWAHESABIA MAKOSA YAO.
Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
SWALI: Nini Maana ya Isaya 24:16-18, inapomzungumzia mwenye haki, na anaposema Kukonda kwangu!
Isaya 24:16 Toka pande za mwisho wa dunia tumesikia nyimbo, Atukuzwe mwenye haki. Ndipo niliposema, Kukonda kwangu! Kukonda kwangu! Ole wangu! Watenda hila wametenda hila, naam, watendao hila wametenda hila sana.
17 Hofu, na shimo, na mtego, vi juu yako, Ee mwenye kukaa duniani.
18 Itakuwa kila akimbiaye sauti ya hofu ataanguka katika shimo; na kila apandaye na kutoka shimoni atanaswa na mtego; kwa maana madirisha yaliyo juu yamewekwa wazi, na misingi ya dunia inatikisika
JIBU: Vifungu hivyo vinazungumzia unabii wa Masihi (Yesu Kristo) mwokozi wetu.
Katika mstari wa 16, nabii Isaya anaonyeshwa maono, ya nyimbo za “mwenye haki” ambaye si mwingine zaidi ya Kristo, Kwamba atukuzwe. Jambo ambalo ni la furaha, Kristo kuja duniani, ni tendo ambalo lilishangaliwa sio tu na malaika (Luka 2:8-14), lakini pia na wanadamu (Yohana 12:12-13).
Lakini tunaona katika sentensi inayofuata nabii Isaya, anaonyesha masikitiko yake, kwa kusema Kukonda kwangu! Kukonda kwangu! Ole wangu, watenda hila wametenda hila. Akifunua kimifano hali ya taabu na huzuni inayompelekea hata kupoteza afya kwasababu ya mienendo ya watu waovu baada ya pale. Yaani badala wampokee mwokozi, wengi walimpinga na kumkataa, wakamsulubisha, na kuukata wokovu, ulioletwa na huyo mwenye haki.
Hivyo katika vifungu vinavyofuata 17-18, Anaeleza hukumu itakayowapata waliopo duniani, kwa kosa la kumkataa masihi, akilenga hasaa siku ile kuu ya Bwana, siku ya mwisho ya ghadhabu ya Mungu ambayo hii dunia itaharibiwa kabisa pamoja na watu waovu. Ambapo kwa urefu wake, inaelezwa pia katika vifungu vinavyofuata.
Unabii ambao ni kweli kabisa, unapompinga Kristo leo, aliye mwenye haki, aliyekuja kukuondolea dhambi zako, huwezi kuikwepa jehanamu ya moto, kwasababu matendo yako pekee hayawezi kukufanya mkamilifu, vilevile katika siku za mwisho ikiwa utakuwepo duniani, huwezi kuyakwepa mapigo ya Mungu juu yako.
Hivyo mpendwa ni heri ukampokea Yesu leo, akusamehe dhambi zako. Jina lako liandikwe kwenye kitabu cha uzima. Mwisho umekaribia sana, Jiulize ukifa leo katika hali ya dhambi utaenda kuwa mgeni wa nani huko ng’ambo ufikapo?
Ikiwa upo tayari kuupokea wokovu leo, upate msamaha wa dhambi zako basi fungua hapa kwa mwongozo huo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela.
“Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).