Category Archive Home

NITAFANYA YERUSALEMU KUWA JIWE LA KUWALEMEA .

Nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote;


Kitakachochochea vita kuu mbili kuu ambazo tunazitazamia kuja huko mbeleni..ambayo ya kwanza ni ile vita ya Gogu na Magogu inayozungumziwa katika kitabu cha Ezekieli 38 & 39. Na ya pili ni ile ya Harmagedoni inayozungumziwa katika Ufunuo 16:15 na Ufunuo 19:11-21 ambayo hiyo itakuwa ni Mungu mwenyewe. Ipo nyingine ya Tatu ambayo itakuja kutokea baada ya ile miaka 1000 ya utawala wa Kristo kuisha, ambayo nayo itahusisha Magogu, lakini hiyo hatutaizungumzia leo hapa.

Hiyo ya kwanza inasema mfalme wa kaskazini atashuka akiyangoza baadhi ya mataifa ya kando kando, yatakusanyika  lengo lao likiwa ni kuindoa Israeli katika ramani ya dunia..Na kwasasa tunajua mfalme huyo wa Kaskazini atakuwa si mwingine Zaidi ya Taifa la URUSI, (ndio Gogu na Magogu), kwasababu hilo ndilo lipo upande wa kaskazini mwa Israeli, na ndio lenye nguvu kwa ukanda ule wote..Hivyo Siku za usoni, tendo hilo litafanyika, lakini hawatashinda, kwani watauawa kwa mauaji ya halaiki, biblia inasema kutakuwa na mizoga ya miili ya watu itafagiliwa kwa muda wa miezi saba pale Israeli.. na silaha zao watazitumia kama nishati kwa muda wa miaka 7 kwa jinsi zitakavyokuwa nyingi..

Ezekieli 39:12 “Na kwa muda wa miezi saba nyumba ya Israeli watakuwa wakiwazika, wapate kuisafisha nchi.

13 Naam, watu wote wa nchi hiyo watawazika; itakuwa ni sifa kwao katika siku ile nitakapotukuzwa, asema Bwana MUNGU.

14 Nao watawachagua watu wa kufanya kazi ya daima, watakaopita kati ya nchi, ili kuwazika waliosalia juu ya uso wa nchi, ili kuisafisha; miezi saba itakapokwisha kupita watatafuta”

Na wakati huo ndio utakaokuwa mwisho wa Taifa la Urusi halitakuwepo tena.

Na vita nyingine ni ile ya Harmagedoni, hii itaongozwa na mataifa yatokayo katika mawio ya jua, mataifa ya Mashariki ya mbali, nayo yatakuwa si mengine Zaidi ya korea, Japani, China, Tawani..haya ndio yatakayoingoza vita hiyo, na safari hii haitakuwa mataifa machache tu, hapana bali itakuwa ni mataifa yote duniani yaliyosalia yataungana na hawa viongozi wao kwa ajili ya kuipoteza tena Israeli.

Unaweza ukajiuliza ni kwanini jambo hili litokee tu kwa Israeli?.. Kwani Wana ugomvi gani hasaa mkubwa mpaka ifikie hatua mataifa yote ulimwenguni yanaungana kwenda kukishambulia ki-nchi kidogo kama kile chenye ukubwa usiozidi hata mji wa Daresalaam.

Kama ukifuatilia utagundua Israeli kwasasa hawaingilii siasa zozote…au mambo ya mataifa mengine, kama yanavyofanya sasahivi mataifa makubwa kama vile Marekani, au mataifa ya Ulaya, ambayo hayo kimsingi ndio yangepaswa yawe na sababu za kutosha za kuwa na maadui.

Lakini Israeli, haifanyi chochote lakini inachukiwa,..Watu hawajui kuwa jambo hilo linatoka kwa BWANA. Ikiwa leo hii hata bado neema haijawarudia wayahudi, tayari ni maadui wa mataifa mengi, Fikiria siku ambapo watarudiwa ni nini kitatokea?

Hili shinikizo lilipo sasa litazidi hata Zaidi ya mara mia kwa jinsi siku zinavyozidi kusogea, Mungu atanyanyua visa, mbalimbali ambavyo vitayafanya mataifa yote sasa yawe na kusudi moja la kuingamiza Israeli.. Ni Mungu mwenyewe atayachochea haya mataifa kwa namna isiyo ya kawaida, atayachochoe, kweli kweli mpaka hilo Neno litatimia linalosema…

Zekaria 12:2 “Angalia, mimi nitafanya Yerusalemu kuwa kikombe cha kuyumba-yumba kwa watu wa kabila zote, wazungukao pande zote; tena kitakuwa juu ya Yuda pia wakati wa kuhusuriwa Yerusalemu”.

3 Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake.

Unaona, hiyo ndio itakayopelekea sasa mataifa yote duniani kufikia Kiama chao..

Watakusanyika pale Harmagedoni..Sasa kumbuka wakati huo Taifa la Israeli litakuwa litakuwa limeshamwamini Masihi wao Yesu Kristo, hivyo watapaza sauti zao na kumlilia, aje kuwapigania kama alivyowapigania enzi za kale. Wakati huo ambapo mataifa yote sasa yameshaizunguka nchi hiyo ndogo,.. ndipo watakapomwona mwa Adamu akishuka na mawingu kutoka mbinguni kwa nguvu na utukufu mwingi akiwa na majeshi wa watakatifu wake ambao alishawanyakua.

Na hapo ndipo mataifa yote yatakapoomboleza, lakini utakuwa ndio mwisho wao, Bwana atawauwa wote kwa upanga utokao katika kinywa chake..

Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana.

17 Kisha nikaona malaika mmoja amesimama katika jua; akalia kwa sauti kuu, akiwaambia ndege wote warukao katikati ya mbingu, Njoni mkutane kwa karamu ya Mungu iliyo kuu;

18 mpate kula nyama ya wafalme, na nyama ya majemadari, na nyama ya watu hodari, na nyama ya farasi na ya watu wawapandao, na nyama ya watu wote, waungwana kwa watumwa, wadogo kwa wakubwa.

19 Kisha nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana kufanya vita na yeye aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake”.

Wakati huo upo karibu sana, leo hii kila mmoja wetu anashuhudia kinachoendelea mashariki ya kati, kama wewe si mfuatiliaje wa taarifa za habari..anza kufuatilia habari hususani za mashariki ya kati… jifunze, au ulizia ufahamu mambo yanayoendelea ulimwenguni.. Idadi ya mataifa yanayoipinga nchi ya Israeli inazidi kuongozeka, dini zinazolichukia taifa la Israeli nazo zinaongezeka.

Hilo lote ni shinikizo kutoka kwa Bwana mwenyewe..Kutuonyesha kuwa mwisho upo karibuni sana..

Nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote;

Na kabla hayo yote hayajatokea Utatangulia unyakuo wa kanisa kwanza..Ambao dalili zote zinaonyesha wakati wowote kuanzia sasa parapanda italia..na wafu wote waliokufa katika Kristo watafufuka na kwenda katika karamu ya mwanakondoo mbinguni..

Ila wale waliobakia mlango wa neema hautakuwa kwao tena, bali kwa wateule wa Mungu wayahudi..Leo hii unasubiri nini usimruhusu Kristo aingie maishani mwako akubalishe, usidanganywe na uvumi kama uvumi wa amani unaouna sasa hivi, huo ni kuwapumbaza watu waone kama tuna mamilioni ya miaka hapa duniani.. biblia inasema…

1Wathesalonike 5:1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Unaona? Tubu dhambi zote, umgeukie Kristo ndani ya wakati huu mfupi tuliobakiwa nao kabla ya parapanda kulia, tengeneza mambo yako kwasababu injili tuliyonayo sasa si ile tena ya zamani ya kuvutwa kwa maneno laini, tuliyonayo sasa ni ile ya mtakatifu na aendelee kujitakasa na mwenye dhambi aendelee kufanya dhambi..Kwani wakati wa mavuno upo karibu sana…Hivyo maombi yangu ni mimi na wewe tuangukie katika kundi la wanaojitakasa..

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MTINI, WENYE MAJANI.

Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je kuzalishwa na mkunga wa kiume ni dhambi?

Je kuzalishwa na mkunga wa kiume ni dhambi?..Je Mungu anaweza kutumia chochote kupitisha uponyaji wake?..Je jina la Yesu Kristo lina nguvu ya kuponya kabisa bila kutegemea daktari?

Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa tatizo lolote au ugonjwa wowote ambao mtu anaweza kuupata..Mungu anauwezo wa kuuondoa pasipo mkono wa mwanadamu yoyote kuhusika…Na hiyo inatokana na Imani mtu aliyonayo kwa Mungu..Ukiamini kwa moyo wako wote, basi yote yanawezekana.

Lakini pamoja na hayo..pia Mungu anaweza kutumia chochote kupitisha uponyaji wake…Anaweza kumtumia mwanadamu, anaweza kutumia chakula au chochote kile.

Mtu anaweza akaugua akala aina fulani ya chakula akapona..sasa kiuhalisia sio chakula kilichomponya bali ni ule uponyaji Mungu aliouweka ndani ya kile chakula ndio uliomfungua…

Kadhalika anaweza kumtumia mwanadamu kumponya mtu…anawapa maarifa fulani wanadamu ambayo kwa hayo mtu anaweza kupata uponyaji kwamfano..Mtu anaweza kuugua ugonjwa fulani..labda uvimbe umeota tumboni…na madaktari wakahusika katika kuuondoa uvimbe ule kwa njia ya OPERATION na mtu akawa mzima kabisa.,Sasa hiyo ni nguvu ya uponyaji Mungu aliyoiweka kwenye maarifa ya wanadamu n.k

Sasa tukirudi katika suala la Wakunga wa kiume (kuzalishwa na mkunga wa kiume)

Ni wazi kuwa nyakati za zamani sana hakukuwepo kabisa kwa wakunga wa kiume…au kama walikuwepo walikuwa wachache sana..Lakini kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda wanaongezeka sana..Hiyo ni kutokana na matatizo ya wanawake kuongezeka…Magonjwa ya wanawake yanapozidi kuongezeka madaktari nao wanalazimika kuongezeka na idadi kubwa madaktari wanaoongezeka ni wanaume…Hivyo wanaume wengi wanajikita kuingia kusomea mfumo wa kibaolojia wa mwanamke zaidi ya wanawake wenyewe..huku wanawake wakiwa wachache kutokana na sababu mbalimbali.

Kwasababu hiyo basi sio dhambi kuwepo kwa madaktari wa kiume katika kushughulikia matatizo ya wanawake pale wanawake wanapokosekana kwasababu..lengo la wao kuwepo sio kuongeza matatizo bali kupunguza. Hakuna mtu yeyote anayekwenda hospitalini asiyekuwa na tatizo lolote, wote wanaokwenda wanakwenda kutafuta msaada.

Hivyo kuzalishwa na mkunga wa kiume sio dhambi wala kufanyiwa operation na mwanamume sio dhambi..Zipo operation za uzazi, ambazo kizazi kinalazimika kuchanwa kuondolewa ugonjwa usiopaswa kuwemo humo..Na operation kama hizo huwa zinamlazimisha mgonjwa kuvuliwa nguo zote na kuwa kama alivyozaliwa ili matibabu hayo yaweze kufanyika..na madaktari bingwa wanaofanya hizo operation wengi ni wanaume wakiwa pamoja na manesi wa kike…Hivyo kwa mgonjwa wa kike kutibiwa kwa viwango hivyo  na daktari wa kiume sio dhambi..wala wa kiume pia kutibiwa kwa viwango hivyo na daktari wa kike ambavyo vitamlazimisha kuwa tupu kabisa mbele ya matatibu sio dhambi…Kwasababu lengo ni kupata matibabu na si kitu kingine.

Na matibabu kama hayo yanafanyika  kwa madaktari wa hospitalini tu kwasababu wengi wakiwa katika vyumba vya uchunguzi au operation wanakuwa zaidi ya daktari mmoja tena wa jinsia tofauti, ili kuzuia uzalilishaji na vitu kama hivyo…. na sio kwa waganga wa kienyeji…wala kwa madaktari binafsi wa mitaani ambao wanakuita tu binafsi na kukwambia uvue hichi au kile wakuchunguze..Hao kwa namna yoyote hawapaswi kuruhusiwa kufanya uchunguzi au matibabu ya namna hiyo.

Lakini yote katika yote..Bwana Yesu ndiye mponyaji mkuu..operesheni wakati mwingine zinafeli pamoja na gharama zake zote hizo kubwa…lakini Yesu Kristo hajawahi kushindwa…

Vyakula wakati mwingine vinashindwa kutuponya lakini Yesu Kristo hajawahi kushindwa..Yapo magonjwa ambayo madaktari hawayaelewi chanzo chake lakini Yesu Kristo anayajua.

Madaktari wanatibu kwa gharama kubwa za fedha, na wakati mwingine gharama za kutolewa nguo zote, au nywele zote au kiungo fulani kukatwa ndipo matibabu yaweze kufanyika..lakini Yesu Kristo anafanya bila hayo yote.

Ikiwa unaumwa ugonjwa wowote ule..Nataka na unakaribia kwenda kwenye operesheni…nataka nikuambie Yesu Kristo anaweza kukuponya kabla hujamkaribia  huyo daktari..

Weka mkono mahali unapoumwa..kama ni kifuani, kichwani, tumboni..kama ni ugonjwa ambao huelewi chanzo chake weka kichwani…Yesu anajua chanzo chake..

Sasa baada ya kuweka kichwani..unaposoma sala hii ugonjwa wako unakwenda kuhama sasahivi na kutoweka kabisa..Amini tu.

“Bwana Yesu namwombe mtu ambaye simjui ni nani, wala jina lake, wala ugonjwa wake wala mahali alipo, lakini wewe unamjua jina lake, mahali alipo na tatizo alilonalo..namwombea kwa Imani katika jina lako  lenye nguvu (Jina la Yesu). Kwamba kila ugonjwa na kila pandikizo lililopandikizwa ndani yake na yule adui likapate kutoweka sasahivi katika JINA LA YESU KRISTO! Amen”.

Ikiwa umeisoma hii sala niliyokuombea…Huo ugonjwa umeshaondoka na kama ugonjwa huo ulivyoondoka ndani yako…Ugonjwa wa rohoni pia unapaswa uondoke pia..Na ugonjwa wa rohoni ni dhambi.

Hizo zinaondoka ndani yako kwa kumkiri sasa Yesu Kristo ambaye amekuponya ugonjwa wako..Na baada ya kumkiri kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako..mwambie akusamehe dhambi zote ulizowahi kuzitenda huko nyuma…na wewe mwenyewe dhamiria kuziacha…kama ulikuwa ni mwasherati..umeona utukufu wa Mungu..hivyo usifanye uasherati tena…vivyo hivyo na dhambi nyingine zote. Usizifanye tena,  yasije yakakupata mabaya kuliko hayo uliyokuwa nayo.

Na baada ya kutubu haraka sana nenda katafute ubatizo. Kumbuka ubatizo sahihi ni wa muhimu sana. Na ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa Jina la Yesu Kristo.(kulingana na Matendo 2:38). Na Roho Mtakatifu atakayeingia ndani yako atakuongoza na kukutia katika kweli yote.

Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali share na wengine.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?

JE! MUNGU NI NANI?

Biblia ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

kilemba cha neema, Je! Umemvika mwanao ?


Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe..Karibu tujikumbushe mambo muhimu katika maisha yetu..Na hayo si mengine zaidi ya maonyo ya Neno la Mungu…Leo kwa Neema za Bwana tutajikumbusha majukumu machache ya wazazi juu ya watoto wetu..

Biblia inasema katika…

Kutoka 20: 12 “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako”.

Neno hili ni Neno la Mungu kwa watoto wote ambao wanao wazazi…Na hata kama hawana wazazi labda wamefariki au hawaishi nao kwa namna moja au nyingine…Basi nafasi hiyo ya Baba na Mama itachukuliwa na walezi wao…Hao wanasimama kama Baba zao na Mama zao kihalali kabisa mbele za Mungu..hata kama wapo katika vituo vya malezi vya mayatima…hao walezi wao wanachukua nafasi hiyo ya Baba na Mama…wana amri kutoka kwa Mungu kuheshimiwa kama wazazi halisi…Kwasababu kuna Baraka kubwa sana katika kuwaheshimu wazazi na kuwasikiliza..

Kadhalika haijalishi mzazi ni mwovu kiasi gani lakini ni lazima kumheshimu, na kumtii haijalishi yeye hajiheshimu kiasi gani ni wajibu wa kila mtoto kumheshimu mzazi wake..Kwasababu ndio amri ya kwanza yenye ahadi…

Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.

2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,

3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”

Kupata heri na kuishi siku nyingi ni vitu viwili tofauti…Unaweza kuishi siku nyingi lakini maisha yasiwe ya heri..Hivyo, vyote viwili vinapaswa viende pamoja…

Jukumu la mzazi kwa mtoto.

Sasa Kitu cha Muhimu cha kufahamu kwa mzazi ni kwamba…Hatima ya mtoto, mzazi anaweza kuchangia kwa asilimia kubwa kuitengeneza au kuiharibu…Mzazi anaweza kukazana kweli kumpenda mwanawe, kumlipia karo, kumtafutia shule bora..kumpatia lishe bora, kumlinda..kumhakikishia bima ya afya n.k Lakini kama hatamtengenezea mwanawe mazingira ya kumheshimu au kumtii.. huyo mtoto hawezi kupata heri yoyote huko anakokwenda, wala hawezi kuishi maisha marefu…haijalishi atapatiwa elimu nzuri kiasi gani sasa…au atakuwa na afya nzuri kiasi gani sasa au maarufu kiasi gani…Maisha yake yatakatika katikati na yatakuwa ya tabu.

Hivyo mzazi ukilijua hilo utahakikisha mwanao anakuheshimu na kukutii…

Hayo ndio mambo ya kwanza ya kuzingatia kabla hata ya kwenda kuangalia ufaulu wake wa darasani…usifurahie anapofaulu sana na huku adabu yake inazidi kwenda chini..furahia pale heshima yake na utii wake unapozidi kupanda kwasababu unajua..hata kama atapepesuka kiafya sasa..hatakufa!..ataishi muda mrefu kwasababu Neno la Mungu linasema hivyo..hata kama hana heri sasa, lakini atakuja kuwa na heri baadaye katika kipindi cha maisha yake yote..

Hivyo kazana kumfundisha awe na tabia ya kukusikiliza…chochote utakachomwambia akutii na afanye kwa kupenda na si kwa kulazimishwa lazimishwa..mfunze tabia nzuri na heshima na utiii kwako na kwa watu wengine, mvishe mavazi ya adabu na mfundishe kuwa mtii….Mjaribu mara kwa mara kuangalia utii wake umefikia wapi ukiona umepungua tafuta namna ya kuurudisha…..mtume dukani mrudishe hata mara mbili au tatu, mpime..ujue kiwango cha utii alichonacho na heshima.

Mpime mwanao;

Mpime anapokuwa na wageni na watu wengine anakuwa na tabia gani zisizofaa na zile zinazofaa mpongeze…ukiona kasoro tumia fimbo kidogo, maana biblia inasema ukimpiga hatakufa…Wengi hawatumii fimbo wakidhani wanamharibia ujasiri mtoto, fimbo isiyokuwa na mafunzo sahihi ndiyo inayomharibia ujasiri..lakini fimbo yenye ujumbe wa kujenga ndiyo inayomjenga zaidi mtoto…

Na Mungu alivyowaumba watoto hawana kinyongo ili kwamba waweze kutengenezeka..ukimwadhibu sasahivi baada ya nusu saa mnacheka na kufurahi, ule upumbavu utakuwa umendoka lakini upendo wake kwako bado upo…..ukimwacha sasa bila kumfunza atakapokuwa mtu mzima hali za kuwa na vinyongo na uchungu zitakapomjia itakuwa ni ngumu kumtengeneza….kila utakalomwambia atakuwa anakwambia unamnyanyasa,..mara unaingilia uhuru wake..mara hujali hisia zake, mara wewe ni mkoloni, mara unamwaibisha n.k

Mfundishe biblia;

Pia katika utoto aliopo, mfundishe biblia..mpe mistari kadhaa ya kuikariri na kuishika kwasababu watoto wengi bado hawajaweza kuipambanua mistari..wape tu waikariri itawasaidia ukubwani..kuliko kukariri nyimbo za kidunia..pia wafundishe nyimbo za kuabudu, na kumsifu Mungu na wafundishe sala za kuomba muda wote na habari za Yesu ambazo ndizo za muhimu kuliko zote..Na wapime je hivyo unavyowafundisha au wanavyofundishwa na wengine wanavizingatia.??

Ukimpima mtoto vizuri na kujua kuwa anakutii na kukuheshimu na anaheshima kubwa ambayo mpaka watu wa nje wanaishuhudia na kusema Yule mtoto anaheshima na adabu…Basi, kuna Baraka ambazo Mungu anaziachia ambazo ulimwengu hauwezi ukaziona..hapo ndipo nyota njema ya mtoto inapoanzia..

Biblia inasema hayo mafunzo hatayaacha hata atakapokuwa mzee…

Mithali 22: 6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”…

Wengi wanaogopa kuwafundisha wanao adabu na heshima kwasababu wanahisi wakishafikisha umri Fulani labda wa kuvunja ungo au kubalehe watakengeuka..Huo ni uongo wa shetani!!…Watoto wengi wanakengeuka ukubwani kwasababu wazazi wao ambao hapo kwanza walikuwa wanawalea vizuri leo wamekengeuka!..sasa kama mzazi kakengeuka mtoto atasalimikaje?..Mzazi alikuwa anakwenda kanisani na mwombaji sasa hafanyi hivyo tena..mtoto ataendeleaje kwenda kanisani?…Mtoto alikuwa amezoea nyumbani ni mahali pa ibada sasa nyumbani kunapigwa kila siku kwenye TV, nyimbo za kidunia, mtoto ataendeleaje kuwa mtakatifu?….Lakini kama mzazi akibaki vile vile Yule mtoto kamwe hawezi kukengeuka hata atakapokuwa mzee..biblia sio kitabu cha Uongo!… Haiwezi kusema mtoto hataiacha ile njia halafu aje kuiacha!..sasa Mungu atakuwa ni mwongo.

Sasa faida nyingine ya mwisho na kuu ambayo mtoto anaweza kuipata kutoka kwako mzazi kwa kumfanya akutii na hata akusikilize na kukuheshimu katika viwango vya juu ni KUVIKWA KILEMBA CHA NEEMA KICHWANI PAKE?.

Faida hiyo ya kuvikwa KILEMBA CHA NEEMA KICHWANI PAKE.Biblia inaisema katika..

Mithali 1: 8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

9 Kwa maana hayo yatakuwa KILEMBA CHA NEEMA KICHWANI PAKO, Na mikufu shingoni mwako”.

Hii ni Baraka kubwa sana ambayo wazazi wengi hawaijui…Hapa duniani tunaishi kwa Neema,…Hivyo Neema ya Kristo inapokuwa nyingi juu yetu..ndipo tunapokuwa na nafasi zaidi ya kumkaribia Mungu, ndipo tunapokuwa na nafasi kubwa zaidi ya kuwa watumishi wa Mungu…Na utumishi wa Mungu sio tu ule wa kuhubiri madhabahuni hapana! bali hata ule wa Danieli ni utumishi wa Mungu..Pale Mungu anapokuweka katika ngazi Fulani ya juu na huko anakutumia kuwatunza watu wake..Hivyo Neema kama hiyo ni njema kwa mtu yeyote…Mtu anayemtumikia Mungu,.. Mungu atamheshimu biblia inasema hivyo (katika Yohana 12:26).

Mfundishe kwa bidii kukutii;

Sasa ni nani asiyetaka kuheshimiwa na Mungu?..Je! unataka mwanao aheshimiwe na Mungu?…Kwa kuvikwa neema ya kuwa mtumishi wake?…Ni kwa kumfanya akutii na kukuheshimu..huku na wewe ukionyesha kielelezo cha kumcha Mungu maisha yako yote ili usimwangushe..

Kuwa na mtoto ni Baraka!..Hususani kama umemvisha kilemba hicho cha neema….Neno la Mungu linasema wapeni watu vitu nanyi mtapewa kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika ndivyo watu watakavyowapa kifuani mwenu…..Na wewe umempa mwanao hicho kipimo cha Neema ya Mungu juu ya kichwa chake kubwa namna hiyo…Bwana atamtumia huyo huyo kukulipa..kukurudishia kipimo cha kujaa na kushindiliwa nakusukwasukwa hata kumwagika katika siku za mbeleni..Na kwasababu mwanao au wanao watakuwa wanatembea na hiyo NEEMA kubwa sana kichwani mwao basi kila watakalomwomba Mungu, Mungu na kila watakalolifanya litafanikiwa katika maisha yao.

Bwana akubariki.

Kama wewe mzazi hujaokoka!..Tambua kuwa huwezi kuwavika wanao KILEMBA HICHO CHA NEEMA vichwani mwao..Wataharibikiwa na kuwa na maisha mabaya..kwasababu maisha yako wewe ni mabaya!..Hivyo ni vizuri leo hii ukamgeukia Kristo akuoshe dhambi zako kweli kweli kwa damu yake..Ili uwe mzazi/mlezi bora…Unachopaswa kufanya ni kutubu kuanzia leo na kumwambia Bwana akusamehe..akusamehe, uasherati wako kama ulikuwa unaufanya..akusamehe kwa kutowajali wanao,..akusamehe kwa kila uchafu uliokuwa unaufanya..na hivyo unamwahidi kwamba utafanya tena..

Baada ya kutubu kabatizwe katika ubatizo sahihi kwaajili ya ondoleo la dhambi (Matendo 2:38)..Kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa mwili wote kwenye maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo. Baada ya kufanya hivyo Roho Ambaye atakuwa ndani yako atakuongoza kufanya mengine yote yaliyosalia na kukupa uelewa wa ajabu wa kuyaelewa maandiko na kukusaidia kushinda dhambi ambazo kwa nguvu zako ulikuwa huwezi.

Kumbuka pia Yesu Kristo atarudi..Biblia inasema “Itatufaidia nini tuupate ulimwengu mzima na kisha tupate hasara za nafsi zetu’’..Hivyo uwe unalitafakari hilo kila siku.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Maran atha!..Shalom.

Mada Nyinginezo:

LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

KIMBIA! KIMBIA! KIMBIA!

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

BONDE LA KUKATA MANENO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

Ulinzi wa daima (eternal security) ni neno la kimaandiko?


JIBU: Ulinzi wa daima, kama inavyojulikana kwa lugha ya kiingereza“eternal security”, linamaana kwamba mtu akishamwamini Kristo akaokoka, basi mtu huyo anakuwa tayari anao ulinzi wa milele wa wokovu wake, na kwamba hawezi kuanguka tena kwenda kuzimu hata iweje, kwani wewe tayari ni milki ya Mungu milele. “Once saved, forever saved”.

Wanaoamini hivyo wanasema, suala la wokovu ni la Mungu mwenyewe, anamwokoa mtu kwa neema na si kwa matendo yake mwenyewe. Na hivyo hata mtu anapochukua uamuzi wa kuupokea wokovu, hata hayo yaliyobakia pia ya kumlinda mtu huyo hadi siku wa mwisho yanakuwa ni ya Mungu..

Lakini Je! Mtazamo huo unatafsiriwa ipasavyo?

Ni kweli ulinzi wa daima/milele ni neno la kimaandiko, kwamba ni kweli mtu akishaokolewa, Saa hiyo hiyo Mungu anampa uhakika wa uzima wa milele, anakuwa ametiwa muhuri hadi siku ya ukombozi wake, (Soma Waefeso 4:30, Warumi 8:33-34, Warumi 8:38-39)..Lakini ahadi hiyo ni kama mtu akidumu katika hiyo neema tu!. Ikiwa atafanya hivyo Mungu hawezi kumwacha akaangamia, atamshikilia mkono kila anapokwenda kuhakikisha haanguki.. Lakini kama hatataka yeye mwenyewe kudumu katika neema (Imani) hiyo, wazo hilo ni la uongo.

Ni sawa umemshika mtoto mkono na kumwambia atembee huku umemshika mkono na ukamwakikishia kwamba akiwa katika mikono yako kamwe hataanguka atakuwa salama daima..Lakini Yule mtoto akasikiliza ushauri wa mtu mwingine kwamba anaweza kutembea peke yake hivyo kwa hiyari yake mwenyewe akakataa na kusema sitaki kushikwa na wewe na akatoka mikononi mwako kwa nguvu je! Akianguka atakulaumu..na kumwambia ulimwahidia hataanguka daima atakuwa salama?..Kitu kisichofahamika na wengi ni kwamba Mungu hawezi kuvuka maamuzi yetu..Huwa hatulazimishi kufanya kitu kama sisi wanadamu tunavyolazimishana..

Hivyo tunapookolewa, hatukai tu tukijitumainisha kuwa tumeshashinda vita moja kwa moja, na kwamba tupo mikononi mwa Mungu salama…Tunapaswa tufahamu kuwa ndio kwanza tumeanza vita kwasababu Adui yetu shetani atataka kutufanya tuamue kuiacha imani..

Mapambano yanaendelea;

Na ndio maana kuanzia huo wakati (baada ya kuokoka) mambo huwa hayawahi marahisi wakati mwingine tunakumbana na vita na majaribu mengi kutoka kwa adui, na misukosuko mingi ili tu tuiache imani,..Hivyo kama shetani angekuwa anajua kuwa kama mtu ameupata wokovu ndio kaupata milele, basi asingekuwa na haja ya sisi kutufuatilia tuiache Imani baada ya hapo, maana kwake yeye ingekuwa ni kazi bure.,Lakini kinyume chake kila siku anatupiga vita kwasababu anajua kuwa uwezakano wa kukipoteza kile tulichonacho upo!…Anajua pia bado kuna uwezekano wa kuupoteza ulinzi huo wa milele.

Hivyo ikiwa kama tutadumu katika mapenzi ya Mungu basi uhakika wa wokovu huo ni lazima.. Lakini ikiwa hatutailinda neema tuliyopewa kwa bidii, tukawa wazembe, yaani tunaishi tu kama tunavyotaka, uwezekano mkubwa wa kuupoteza wokovu wetu upo.

Mtume Paulo alikuwa ni mtu aliyetokewa na Kristo, aliyejitoa kweli kwa Mungu, aliyehubiri injili kwa mataifa mengi, maelfu au pengine mamilioni ya watu waliokolewa kwa kupitia huduma yake..Lakini kuna wakati alisema..

1Wakorintho 9:26 “Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Unaona, alishaona kumbe anaweza akawa sio tu mkristo peke yake, bali akawa hata mtumishi wa Mungu aliyeitwa, lakini mwisho wa siku akawa ni mtu wa kukataliwa (akaenda Jehanamu ya moto).

Hatari ya kutoishindania imani;

Paulo alisema vile kwa kumaanisha, sio kama kujionyesha kuwa ni yeye ni mnyenyekevu..Aliona uwezekano huo wa kupotea bado upo kwa asilimia kubwa!.

Wapo watumishi leo hii, ni wazinzi, wanadhani bado wanao ulinzi wa daima ndani yao..Wapo wachungaji ni wanywaji pombe na wavutaji sigara, wanadhani bado wanao ulinzi wa daima ndani yao..Kwamba hata wakifa watakwenda mbinguni kwasababu maandiko yanatuambia tunaokolewa kwa neema.

Nataka nikuambie, Hata Yuda, aliyechaguliwa na Kristo, mwenyewe,..Na alianza vizuri lakini hakuilinda neema aliyopewa na mwisho wa siku akaangukia katika mikono ya shetani. Sasa kama Yuda aliyetembea na Yesu miaka 3 na nusu alikengeuka…Mimi na wewe ni nani ambao hata hatujawahi kumwona Yesu tujidanganye kuwa tukishaokolewa tumeokolewa?.

Hivyo usipoithamini neema uliyopewa bure kwa damu ya Yesu Kristo, hujibidiishi kuilinda Imani yako, huko nyuma ulimaanisha kuokoka kweli, lakini leo hii, unakwenda Disko,.. unavaa nguo za uchi uchi, unatazama picha chafu mitandaoni, unasikiliza miziki ya kidunia, unakula rushwa, unakwenda kwa waganga..Nataka nikuambie kwako ulinzi huo wa daima (eternal security) ulishaondoka!!..Na hata ukifa leo hii utakwenda kuzimu na adhabu yako itakuwa kubwa Zaidi ya wale ambao hawakumjua Kristo, Haijalishi wewe ni kiongozi mzuri wa kanisani kiasi gani,..haijalishi umeshahubiri kiasi gani, haijalishi umewaleta wengi kwa Kristo kiasi gani…Usipoyafanya mapenzi ya Mungu, utapotea tu.

Ezekieli 3:20 “Tena mtu mwenye haki aiachapo haki yake, na kutenda uovu, nami nikiweka kikwazo mbele yake, atakufa; kwa sababu hukumwonya, atakufa katika uovu wake, wala matendo yake ya haki aliyoyatenda hayatakumbukwa;”

Na ndio maana biblia inasema:

2Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”.

Uthamini wokovu wako, ili Mungu apate nafasi ya kukulinda..

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

CHUJIO HILI NI LA AJABU SANA!

INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

 

KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

BIRIKA LA SILOAMU.

BIRIKA LA SILOAMU…Bwana Yesu alisema..”Mtu akiona kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.

Shalom, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu ambalo ni mwanga wa njia zetu, na taa iongozayo miguu yetu.

Yohana 9:6 “Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho,

7 akamwambia, Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, (maana yake, Aliyetumwa). Basi akaenda na kunawa; akarudi anaona”

Bwana wetu Yesu angeweza kumponya mtu huyu pasipo hata kumwambia akanawe katika birika la Siloamu.. Tafsiri ya birika ilivyotumika hapo sio birika la kuwekea chai au maji ya moto..hapana! bali birika maana yake ni Bwawa dogo lililotengenezwa kwa kusudi maalumu…ni kama swimming pool kwa lugha ya kiingereza..

Katika Yerusalemu zamani za agano la kale, lilikuwepo birika hilo ambalo lilitengenezwa mara ya kwanza na Mfalme wa Israeli aliyeitwa Hezekia, ukisoma 2Wafalme 20:20 utaliona jambo hilo,..lakini birika hilo lilikuja kubomolewa na Mfalme wa Babeli Nebukadneza, lakini baadaye lilikuja kutengenezwa tena na Nehemia…na likaendelea kuwepo mpaka wakati wa kipindi cha Bwana Yesu…ingawa lilikuja kufanyiwa ukarabati tena na Herode.

Biblia inasema.

Yohana 7: 37 “Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.

38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

39 Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa”.

Utaona mahali pengine pia Bwana Yesu alitumia mfano wa maji ya kisimani kufundisha juu ya maji ya rohoni..

Yohana 4: 6 “Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.

7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.

8 Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.

9 Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria).

10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai.

11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai?

12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?

13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.

16 Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa”

Je umeyapata hayo maji?..Roho Mtakatifu ndiye maji ya Uzima..anakata kiu ya dhambi, kiu ya uasherati, kiu ya rushwa,kiu ya wizi na kila aina ya uchafu, maji hayo yanapatikana bure…

Bwana Yesu alisema mwenye hivyo…

Ufunuo 21: 6 “Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure”

Ufunuo 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.

Pengine umesikia habari hizi za maji ya uzima mara nyingi sana zisizohesabika…lakini nataka nikuambie ukiyadharau haya maji leo yanayopatikana bure utayatamani siku ile katika ziwa la moto na utayakosa kama yule Tajiri aliyemwomba Lazaro achovye kidole chake kwenye maji hayo ili auburudishe ulimi wake akakosa…Na ndivyo siku ile utayatamani maji hayo utayakosa…usikazane kutafuta maji ya upako, au kutafuta kuzamishwa kwenye mabwawa yajulikanayo kama mabwawa ya upako..tafuta MAJI YA UZIMA…Bwana atusaidie tuyapate maji haya kwa wingi..ili tuwe na Uzima…Tunamshukuru sana Bwana wetu Yesu Kristo wa kutuletea maji haya ya uzima..jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

UMEPATANISHWA NA MAADUI ZAKO?

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

KIJITO CHA UTAKASO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

BWANA ANAPOTUKASIRIKIA, ANA LENGO ZURI NA SISI.

BWANA ANAPOTUKASIRIKIA ANA LENGO ZURI NA SISI NDANI YA MOYO WAKE.

Marko 3:5 “Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.

6 Mara wakatoka wale Mafarisayo, wakawa wakifanya shauri juu yake pamoja na Maherodi, jinsi ya kumwangamiza”

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima. Neno la Mungu ndio chakula kitupacho uzima wa milele,. hivyo tunapochukua muda kulitafakari kila siku,. basi tunafanya jambo ambalo faida yake hatutaiona hapa peke yake, bali hata miaka miaka trilioni moja mbele.

Leo kwa neema za Mungu tutaangazia jambo moja kwa ufupi juu ya Hasira ya Kristo..Tukiyatafakari hayo maneno hapo juu tunaona kuna wakati Bwana alikwenda kwenye sinagogi na kukutana na mtu ambaye alikuwa na mkono uliopooza…

Lakini alipotaka kumponya, aligundua kuwa Mafarisayo na Maherodi walikuwa wanamzivia ili wamjaribu kama atamponya mkono wake siku ya sabato, ili wapate kumshitaki..Lakini yeye alipogundua hilo akakasirika sana, akatulia kwa muda akiwaangalia wale watu kwa hasira..kuanzia kushoto kwake mpaka kulia kwake, wale waliokuwa mbele yake, hadi wale waliokuwa nyuma yake… wote aliwaangalia kwa makusudi ili wauone uso wa Kristo ulivyojaa hasira..

Embu tafakari mfano na wewe ungekuwa upo na wale mafarisayo, ungemwonaje Kristo?..

Ni rahisi kusema huyu mtu kashaanza kutuchukia,. Au huyu mtu anakinyongo Fulani ndani yake kwa ajili yetu, lakini tunasoma biblia inasema, ndani ya moyo wake,. Alikuwa na huzuni kubwa kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao.. Alikuwa anawaonea huruma ndani ya moyo wake, alikuwa anawapenda upeo na hivyo hataki wapotee na ndio maana japokuwa uso wake ulikuwa umejaa hasira nyingi,.. Lakini moyoni mwake alikuwa unadondosha machozi mengi ya huzuni.. Hiyo ndio hasira ya kweli ya ki-Mungu.

Mungu anapokukemea kwa ajili ya dhambi zao, usidhani kuwa Mungu anakuchukia, au anakutesa, au ni mkatili,. uso wa Mungu unapogeuka kwako, usidhani kuwa Mungu hakupendi, lakini badala yake anafanya hivyo kwasababu anataka ugeuke usipotee, moyoni mwake anakuthamini kushinda wewe unavyodhani..(kumbuka tena Bwana anapotukasirikia ana lengo zuri na sisi)

Mungu anapokuambia, uzinzi unaofanya utakupeleka kuzimu, usidhani anakuchukia,. Anapokuambia, rushwa unayokula, ushirikina unaoufanya, matambiko na kafara unazozitoa, moja ya hizi siku utakwenda kuchomwa katika moto usiozimika,. Sio kwamba anakuchukia, anapokuadhibu kwa dhambi zako, na kumwona Mungu kwako kama ni mkatili mwenye uso wa hasira sikuzote kwako..Furahia ni kwasababu anakupenda, na anataka ubadilike..wakati mwingine anakunyang’anya hata baadhi ya vitu ulivyonavyo, au unamwomba hakupi hata kimoja,. Sio kwasababu hakujali, au hakuoni, hapana, Kaonyesha uso wa hasira nyingi kwako kwasababu njia zako ni mbaya..

Biblia inasema..

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.

22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”.

Unaona hapo? Anasema “Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi”..

Mungu akikupenda hata acha kuonyesha uso wa hasira kwako, hataacha kukuonya juu ya dhambi zako, kama vile leo hii anavyokuonya.. Anakueleza ukiendelea kuvaa nguo za nusu uchi utaishi jehanamu ya moto,. ukiendelea kutazama pornography utaishi jehanamu ya moto, ukiendelea kwenda disko utakufa siku moja na kushukia kuzimu…kwasababu anasema wote niwapendao! anawakemea.

Hivyo usishupaze shingo yako,. bali utubu leo hii, mgeukie Bwana wako, ili uugeuze uso wake wa hasira na kuwa wa furaha. Unachotakiwa kufanya ni kujisalimisha kwa Bwana, ukiwa na mzigo wa dhambi zako, na kumwambia, nisamehe nimekosa Mungu wangu na leo hii ninataka kuanza upya tena..Ninaacha hiki, ninaacha kile kwa kumaanisha kabisa..

Kisha ukishafanya hivyo, anza kuonyesha kweli kuwa umetubu.

kwa kuanza kujishughulisha na mambo ya Mungu na kukaa mbali na dhambi ulizokuwa unazifanya hapo kabla,. kama ni nguo za kizinzi unazichoma, kama ulikuwa unaishi na mke/mume ambaye si wako unamuacha.. kama ulikuwa unakwenda bar, unaacha, kama ulikuwa unatazama picha chafu mitandaoni unazifuta,.. kama ulikuwa unafanya uasherati na girlfriend au boyfriend hamjaona, unaacha, kisha unaanza kutafuta ndugu wa kikristo na kukaa nao,..

Sasa Mungu akishaiona Imani kama hiyo, na toba yako iliyoambatana na matendo kama hayo,. yeye mwenyewe kuanzia huo wakati anachukua jukumu la kukufanya kuwa mwana wake kweli kweli, atakupa uwezo wa ajabu wa kuweza kuyashinda hata yale ambayo ulikuwa huwezi kuyaacha..Na mwisho wa siku utajikuta umeshaimarika ndani ya Kristo kwa viwango vya juu sana.

Lakini pia kumbuka, mara baada ya kutubu kwako unapaswa ukabatizwe,. na ubatizo sahihi ni ule wa kuzamwishwa katika maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38,.Ubatizo sahihi ni muhimu, fanya hivyo na hapo utakuwa umezaliwa mara ya pili.

Kumbuka anasema wote niwapendao nawakemea au kwa lugha wote niwapendao niwaeleza ukweli..Hivyo umeusikia leo ukweli. Kubali na kugeuka.

Marko 3:5 “Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao”

Ubarikiwe. Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Maswali na Majibu

UPAKO NI NINI?

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI AU KUTOA TALAKA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

 Habari ya UZIMA? Naomba unisaidie tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu Kwa Sisi Tumwaminio/wafuasi wake. Je! Damu ya Yesu inakazi ya Kutulinda sisi au Mali zetu pale tunapoomba kupitia Damu? Ni sahihi kuomba hivyo? Je! Damu ya Yesu inatumikaje Kwa sisi wakristo?

JIBU: Ili kuelewa tofuati ya utendaji kazi wa damu ya YESU na Jina Jina la Yesu, Ni vizuri kwanza tukajifunza katika maisha ya kawaida…Katika maisha ya kawaida mtu anayo DAMU na vilevile analo JINA…Jina la mtu linaelezea utambulisho wa mtu yule, cheo alicho nacho, heshima aliyo nayo, nguvu aliyo nayo na mamlaka aliyonayo.. Kwamfano katika nchi yoyote mtu mwenye jina kubwa na lenye nguvu kuliko wote ni Raisi wa nchi hiyo…

Vilevile katika upande wa pili DAMU ya mtu inaelezea Uzima wa huyo mtu, asili ya mtu huyo, Undugu alionao na wanafamilia wenzake, na inaelezea pia Urithi alionao..yaani watu atakaowarithisha mali zake.

Na kila Raisi wa nchi au Mfalme, anayo DAMU na vilevile analo JINA.

Sasa tukirudi katika mamlaka ya kimbinguni ambayo hiyo ni kuu kuliko ya kiduniani…Tunaye Mfalme mmoja, naye ni Yesu Kristo (Huyo ni Zaidi ya Raisi yeyote wa nchi)…Na huyu analo JINA vilevile na anayo DAMU.

Kama tulivyosema damu inaelezea undugu wa mtu, yaani uana-familia.….na Bwana Yesu pia anao ndugu zake wa damu,..ambao ni wale wote waliozaliwa mara ya pili…Hao wanayo mamlaka ya kumsogelea katika meza yake na kula naye, na kumwomba lolote kwa jina lake na kupewa…Mtoto wa mfalme akiomba apewe jimbo fulani kutoka kwa Baba yake…haitachukua mlolongo mrefu kupewa haja ya moyo wake..mara moja tu baba yake atamwandikia hati ya nakala kwa jina lake na kuipeleka mahali husika kupata anachokihitaji…Na huyo mtoto kwa jina la Baba yake anaweza kupata lolota katika nchi…..Lakini hebu mtu wa kawaida tu amsogelee mfalme wa nchi na kumwomba apewe hicho kipande cha ardhi uone mlolongo wake!…anaweza kufukuzwa au hata asipofukuzwa basi ombi lake linaweza kuchukua muda mrefu sana kujibiwa…

Sasa yote hayo ni kutokana na nini?

Ni kutokana na kwamba mtoto wa Mfalme anatumia DAMU kupata lolote kwa JINA la Baba yake…wakati wengine wanatumia bahati tu!..kwamba ombi lao likikubaliwa ni kama wamepata bahati tu!..wangeweza kukataliwa…lakini mtoto wa Mfalme anauhakika kwasababu anatumia damu.

Kwahiyo tukirudi kwenye swali: Tofauti kati ya damu ya Yesu na jina la Yesu ni ipi? Tumeshaiona hapo juu na …na je ni sahihi kuomba kutumia damu ya Yesu kutulinda sisi na mali zetu? (damu ya Yesu inatumikaje)

Jibu: Mtu aliyeokoka tayari damu ya Yesu inanena mema juu yake..kama kwa hiyo mifano tuliyoiona hapo juu…Haihitaji kumweleza sana Baba wa mbinguni kwamba unahitaji ulinzi..kitendo tu cha kuwa mwanawe wa damu tayari ni jukumu lake kukulinda wewe na mali zako..na kwa jina lake kupewa chochote katika huu ulimwengu..Tofauti na mtu ambaye hajaokoka…huyo si mwana wa Mungu,..huyo hana uhusiano wowote na damu ya Mungu…Kwahiyo hata akiomba lolote kwa jina la Yesu kwake ni bahati nasibu kupata anachokiomba…

Je umeokoka?…

Umefanyika kuwa mwana wa Mungu?..umekuwa damu moja na Mungu?..Kama hujaokoka basi fahamu kuwa ni ngumu wewe kupokea upendeleo wowote kutoka kwa Mungu..Kwasababu Mungu anawaangalia kwanza wanawe kuwapatia mema (Soma Warumi 8:28-29)..na hao ndio atakaowarithisha uzima wa milele…hawezi kuwarithisha watu wasio wanawe…hata wewe mwenyewe ni ngumu kumrithisha mtoto asiye wako mali zako na kuwaacha wanao bila urithi…

Sasa kwanini uwe kama Yatima siku ile?..wakati wenzako wanairithi mbingu…wewe unarithi ziwa la moto kutoka kwa baba yako ibilisi?..mwache shetani aende kuzimu mwenyewe wewe mgeukie Kristo, mwenye urithi udumuo.

Hivyo unachopaswa kufanya ni kutubu kama hujatubu, kama ulikuwa ni mwasherati unatubu kwa kuacha kufanya hivyo, kama ulikuwa unaweka make-up unaacha, kwasababu mabinti wa Mungu waliozaliwa kwa damu ya Mungu hawafanyi hivyo, ..kama ulikuwa unasuguliwa kucha na wanaume saloon, utubu na kuacha,.., kama ulikuwa unavaa vimini, unapamba uso, unavaa surali, unatubu na kuacha kama ulikuwa ni mlevi, mvutaji wa sigara na mfanyaji masturbation na mtazamaji wa picha chafu katika mitandao unatubu na kuacha, kama ulikuwa ni mwizi vivyo hivyo…

Na baada ya kutubu kwa kudhamiria kabisa na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu. …utakuwa umezaliwa mara ya pili na kuhesabika mwana-familia wa familia ya kimbinguni. Na hivyo kuwa mrithi, na ile damu ya thamani isiyoisha muda wa matumizi, damu ya Yesu Kristo itaanza kunena mema juu yako.

Na hivyo hata ukiitamka jambo lolote kwa jina lake utapata.

Bwana akubariki.

Tafadhali share na wengine. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

Je! ni dhambi kuimba wimbo wa Taifa hata kama umetungwa kidunia?.Na je ni dhambi kwa watoto wa kikristo kuimba zile nyimbo za chekechea?

JIBU: Nyimbo karibia zote za kitaifa hazijatungwa kidunia… Nyingi zilitungwa wakati au baada kidogo ya uhuru wa Taifa husika..Zilikuwa ni nyimbo za Kumshukuru Mungu na kulitakia amani, baraka na mafanikio Taifa husika. Hivyo nyimbo nyingi zilitungwa kama sala iliyo katika mfumo wa kama wa wimbo hivi.

Hakuna wimbo wowote wa Taifa lolote duniani..unaiombwa kwa lengo la kunyanyua hisia za uasherati, wala kutukana kama nyimbo zinazotungwa siku hizi, wala kwa lengo la kujiburudisha, wala kutafuta fedha, wala kujulikana…Hata wengi wa watunzi wa nyimbo hizo hazikuwa mali zao wenyewe kwamba wana hati miliki nazo..bali zilikuwa ni mali za Taifa.

Lengo lingine pia la nyimbo hizo, zimetungwa kuinua morali ya kufanya kazi, kuishi kwa umoja, upendo na kuliheshimu Taifa.

Hivyo hakuna ubaya wowote wa kuimba wimbo wa Taifa mahali popote.

Na sio tu nyimbo za Taifa, bali hata nyimbo za Chekechea (Nursery) kwa watoto wa kikristo.

nyimbo za chekechea

Mtoto wa kikristo si dhambi kushiriki nyimbo za shuleni na watoto wengine..Maadamu nyimbo hizo zimejulikana ni za kimaadili na za kujifunza na zipo katika mtaala wa shule!..Lakini nyingine zozote zilizosalia za kidua ambazo si za kielimu wala si za kiheshima, wala hazipo katika mtaala wowoe wa kishule watoto wa kikristo hawaruhusiwi kushiriki wa vyovyote vile.

Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NYIMBO ZA WOKOVU

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

TENZI ZA ROHONI

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAMNGOJEAO BWANA WATAPATA NGUVU MPYA.

Wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya.


Ipo ahadi kubwa sana ambayo Mungu kaitoa kwa wale walioamua kuiacha dunia na kumfuata yeye kwa gharama zote. Na ahadi yenyewe ni “kupokea nguvu mpya kipindi baada ya kipindi”. Mungu anafahamu kabisa safari ya wokovu ni ngumu kama ilivyosafari nyingine yeyote ya haya maisha…kuna milima na mabonde, kuna kuchukiwa na kudharauliwa, kuna kuonekana umerukwa na akili na kutokuthaminiwa, kuna kutengwa na kuudhiwa, kuna kupungukiwa na kuvunjwa moyo, kuna msiba na dhiki n.k. vyote hivyo mtu yeyote aliyeamua kumfuata Kristo, kwa namna moja au nyingine atakumbana navyo…

Lakini utajiuliza pamoja na hali kama hizo ni kwanini bado watu waliookoka wengi ki-kweli kweli wanaweza kustahimili?..Ni rahisi mtu kwa kidunia kuvunjika moyo au kukatishwa tamaa na mambo kama hayo lakini kwa mkristo aliyedhamiria kumfuata Yesu, ndio kwanza anazidi kuwa karibu na Mungu wake..Hiyo yote ni kwasababu ipo nguvu inayoachiliwa ndani yake kipindi baada ya kipindi..

Biblia inasema..

Isaya 40:28 “Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.

29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.

30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;

31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.

Kama sio neema hiyo, hakuna hata mmoja wetu angeweza kumwamini na kumtuamini Mungu asiyemwona sikuzote za maisha yake..Lakini kwasababu ipo nguvu anayoiachia ndani ya wale wanaomngojea wanajikuta tu wanazidi kumtafuta Mungu, safari yao ya wokovu wanaiona kama vile imeanza jana..

Hiyo ndio tofauti na mtu aliyeokoka na yule ambaye hajaokoka..Yule ambaye hajaokoka, anaweza akawa anajisumbua katika jambo Fulani, au katika shughuli yake,.. au katika elimu yake, lakini upo wakati atachoka, ataboreka, atazimia na kusema ngoja nipumzike kwanza, nitakuja kuendelea baadaye, lakini kwa mtu aliyejitwika msalaba wake na kumfuata Kristo, pale ambapo ataonekana anakaribia kuzimia hapo ndipo Mungu anapompa nguvu mpya, anapompa uwezo mpya.

Hufanya njia pale pasipo na Njia:

Pale ambapo watu watasema sasa huyu ndio basi, kwa hali hii, anayoipitia hamalizi huu mwaka atakuwa amesharudi tu huku kwenye dunia, lakini wanashangaa mwaka unapita, miaka inapita,.. ndio kwanza anazidi kumpenda na kumtafuta Mungu wake Zaidi ya hapo mwanzo..Kwasababu gani, Ni kwasababu Mungu anahakikisha anawapa nguvu mpya wale wao waliodhamiria kujitwika msalaba wao na kumfuata..kama maandiko yanavyosema:

watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.

Ukristo ni safari ya kuwezeshwa, ukiona mtu anasema nimeishiwa pumzi njiani siwezi kuendelea mbele nimezidiwa na tamaa za ulimwengu, fahamu kuwa mtu huyo tangu mwanzo alikuwa bado hajadhamiria kumfuata Kristo kwa moyo wake wote.. Kwasababu ni kitu ambacho hakiwezekani kuishiwa pumzi katikati angali kila wakati unawezeshwa, unapokea nguvu mpya, sasa huko kuishiwa pumzi kunatoka wapi?.

Leo hii unaweza ukajiuliza hivi kweli nikiokoka, nitaweza kuishi bila uzinzi kwa muda mrefu?, nitaweza kuacha kunywa pombe kwa kipindi kirefu,.. nitaweza kuvumilia kutovuta sigara kwa miaka 2 kweli, nikiamua kumfuata Kristo nitaweza kujizuia kutokuweka make-up maisha yangu yote, na kutokuvaa suruali,.. nitaweza kutokwenda Disko, nitaweza kutokufanya Musturbation…Nataka nikuambie kwa akili zako na nguvu zako chache hutaweza, lakini ukiamua kwa kudhamiria kweli kumfuata Kristo kwa moyo wako wote, ukasema leo hii naanza upya kupiga mwendo na Kristo, hilo jambo ni rahisi sana kulishinda kuliko unavyodhani..

Utapokea nguvu mpya:

Kabla hata hujakaribia kuishiwa pumzi Bwana atakuwa pembeni yako kukutia nguvu mpya..Kila siku itakuwa fresh kwako, wiki itapita, mwezi utapita, mwaka utapita, miaka itapita na bado ile hamu ya kufanya hayo mambo haipo ndani yako, ..Hiyo ni neema kubwa Mungu aliyowahaidia wale wote watakaomngojea…Hapo ndipo tunapouna wepesi wa wokovu, vinginevyo hakuna ambaye angeweza kuushinda huu ulimwengu, si mchungaji, si mwinjilisti..hakuna atakayeweza kuushinda ulimwengu.

Hata kama utapitia hali ambayo unaona kesho au kesho kutwa haifiki, lakini maadamu upo kwa Bwana, na unamtazama yeye, utaona tu jinsi atakavyokufanyia njia mahali ambapo hapana njia na wewe mwenyewe utajikuta unamwimbia, EBENEZA MWAMBA WANGU!..

Hata katika magonjwa, au dhiki, katikati yake atakufungulia mifereji ya faraja na uponyaji, nawe utasema ni heri Mungu nilichagua kukufuata maana ninauona mkono wako ukinizunguka!..Hali hiyo hiyo utaendelea nayo mpaka utakapomaliza mwendo wako hapa duniani kama unyakuo hautakukuta..hata Katika raha atakuwa na wewe pia kukuongezea raha Zaidi..

Je na kwa mwenye dhambi ni hivyo hivyo?

Lakini ikiwa upo mbali naye, na unasema kuishi maisha ya wokovu haiwezekani hapa duniani..Nataka nikuambie utajikuta unaendelea kusema hivyo mpaka unakufa na dhambi zako,..

Bwana Yesu aliwaambia mafarisayo katika Yohana 8:24 ‘Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu’.

Kuna madhara makubwa sana kufa katika dhambi…Ukifika kule mbele ya kiti cha hukumu wataletwa watu wa kizazi chako walioweza kukishinda hicho kinachokushinda wewe leo hii,..Nao wataulizwa ilikuaje kuaje nyie mliweza kuushinda uzinzi katika dunia iliyojaa vishawishi namna ile? na wakati hawa wengine wameshindwa?..Nao watajibu kwa ku-unukuu mstari huo;

Isaya 40:29-31

 ‘29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.

30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;

31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.

Hapo utakosa cha kujibu, ukijua kuwa kumbe na wewe ulikuwa na fursa kama hiyo lakini uliikataa.

Hivyo usisibiri upendeleo wa kipekee kama huo ukupite, acha kufikiria fikiria kwa juhudi zako utawezaje. Leo hii dhamiria kutubu dhambi zako zote, hapo ulipo tenga muda mchache ukiwa peke yako piga magoti, anza kumweleza Mungu mambo yako maovu yote uliyomtendea,… kisha mwambie Naomba msamaha,..Fanya hivyo kwa kumaanisha kabisa kutoka moyoni mwako kwasababu yupo hapo kukusikia, na yupo hapo kukusamehe dhambi zako zote..

Na Ile damu yake Yesu Kristo itakusafisha kabisa, na uthibitisho wake ni kuwa, baada ya Toba Amani ya ajabu na utulivu wa kipekee utaingia ndani yako, ukishaona hivyo, dhamiria sasa kuacha kufanya yale yote uliyokuwa unafanya nyuma yasiyompendeza Mungu, kwasababu Mungu kashakukaribia….kama ulikuwa ni mlevi kaa mbali na walevi na pombe, ulikuwa ni mzinzi kaa mbali na wazinzi na acha uzinzi, Na Mungu akishaona mwitikio wako, na kwamba umegeuka kivitendo sawasawa na toba yako, Sasa ile nguvu yake ya kukufanya uzidi kupiga mbio upae juu Zaidi kwa mbawa za tai, itaanza kuachiliwa ndani yako..Na kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda ndivyo utakavyojiona tamaa ya vile vitu ulivyokuwa unavifanya vinakufa ndani yako, na mwisho wa siku vitapotea kabisa..

Hatua inayofuata baada ya toba:

Hivyo ukishatubu bila kupoteza muda hakikisha unatafuta kanisa, ukabatizwe, katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38 ili kuukamilisha wokovu wako.

Kumbuka ubatizo sahihi ni muhimu sana..Vilevile anza kujumuika na wakristo wenzako, wale unaoona wamesimama kweli kweli na anza kusoma Neno kwa bidii na kusali..Yaliyosalia Roho Mtakatifu atakuongoza kuyatenda..jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Shalom.

Mada Nyinginezo:

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

MNGOJEE BWANA

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?

Je! Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?


JIBU: Tukisoma kitabu cha Ufunuo ni kweli tunamwona mnyama aliyetajwa mwenye vichwa saba na pembe kumi..Tofauti na idhaniwavyo na wengi kwamba zile pembe kumi zimejigawanya kwenye vichwa vyote 7..na kwamba kuna vichwa vingine labda vitakuwa vimepata pembe mbili mbili au zaidi…Lakini ukweli ni kwamba ni kichwa kimoja tu ndicho kilichokuwa na pembe zote 10..Hivyo vingine havikuwa na pembe yoyote.

Na kama ukitafakari kwa makini kwa msaada wa Roho utagundua kuwa vile vichwa saba ni Wanyama saba katika mwili mmoja na sio tu vichwa kama vichwa vilivyojiotea kwenye mwili mmoja…bali ni Wanyama saba tofauti wanaoshiriki mwili mmoja (yaani wana-share mwili mmoja)..

Ufunuo 17: 11 “Na yule mnyama aliyekuwako naye hayuko, yeye ndiye wa nane, naye ni mmoja wa wale saba, naye aenenda kwenye uharibifu”.

Sasa hiyo imekaaje kaaje?..Inawezekana Wanyama Zaidi ya mmoja kushiriki mwili mmoja?..

Hiyo inawezekana asilimia 100..wapo ng’ombe mapacha wanaozaliwa wakiwa na mwili mmoja lakini vichwa viwili tofauti, kadhalika wapo nyoka wanaozaliwa hata watatu au wanne wakiwa na wanashea mwili mmoja…Na Zaidi ya yote wapo pia wanadamu ambao wanaozaliwa wakiwa wameungana…Kuna mapacha wanaoishi leo duniani ambao wameungana kila kitu isipokuwa kichwa tu…yaani ukikutana nao unaweza kusema umekutana na mtu mmoja mwenye vichwa viwili lakini kumbe ni watu wawili waliozaliwa wameungana wanaoshea mwili mmoja..Na watu hao walioungana kila mmoja anatafakari kivyake na ana malengo yake na mipango yake, na matamanio yake.

Na katika tukio hilo la Ufunuo ni vivyo hivyo..Biblia imemtaja mnyama huyo kuwa mwenye vichwa saba..Lakini kiuhalisia ni Wanyama saba tofauti wenye mwili mmoja…Na kila mnyama (yaani kichwa kina mambo yake)…Na pia ni mnyama mmoja tu kati ya hao wote mwenye pembe kumi (yaani ni kichwa kimoja tu chenye pembe hizo kumi).

Sasa hao Wanyama saba au vichwa saba ni nini?

Biblia inasema ni wafalme saba..

Ufunuo 17:9 “Hapo ndipo penye akili zenye hekima. Vile vichwa saba ni milima saba anayokalia mwanamke huyo

10 Navyo ni wafalme saba. Watano wamekwisha kuanguka, na mmoja yupo, na mwingine hajaja bado. Naye atakapokuja imempasa kukaa muda mchache. ”.

Falme hizo kama zinavyojidhihirisha katika taifa la Mungu kwenye biblia ni MISRI, ASHURU, BABELI, UMEDI & UAJEMI, UYUNANI, RUMI YA KIPAGANI na RUMI YA KIDINI..Hizi ndizo falme hizo saba au Wanyama hao 7..Falme hizi ni Mataifa aliyotumia shetani kuutesa uzao wa Mungu kwa ujumla wake…

Mataifa Matano ya kwanza yaliwatesa wana wa Israeli peke yao, wakiwa Misri, na mengine baada ya kuchukuliwa tena mateka babeli..lakini haya mawili ya mwisho yaliwatesa wana wa Israeli pamoja na Kanisa la Kristo…Na hicho kichwa ndicho cha mwisho na ndiye mnyama wa 7 ambaye ni RUMI YA KIDINI,.. nacho ndicho chenye pembe zote saba.. mnyama huyu ndiye ambaye yupo sasa na anazidi kuongezeka nguvu siku baada ya siku,.atakapofikia kilele chake atazitumia pembe zake 10 ambayo ni mataifa yanayounda umoja wa ulaya (EU) kuhimiza ile chapa ya mnyama. Kwasasaba umoja huo una wanachama Zaidi ya 10..

Lakini unabii unaonyesha yatakuja kubakia 10 tu yenye nguvu kwenye umoja huo. Na Kwa pamoja yatashirikiana na mnyama huyo, (Rumi ya kidini Iliyopo chini ya kiongozi wa kanisa katoliki ,Papa) kuishawishi dunia kuendesha zoezi la kuwatia watu chapa. Kwa kipindi kifupi sana kisichozidi miaka mitatu na nusu, Chapa itakuwa imeshawafikia watu wote duniani…Watakaoikataa watakamatwa na kupelekwa kwenye kambi maalumu za mateso…

Wakati huo unyakuo utakuwa umeshapita…Watakatifu wameondolewa duniani,.kuepushwa na ghadhabu ya Mungu na majaribu ya mpinga-kristo.

Ukali wa dhiki kuu.

Na huko katika magereza hayo ya mateso, watu watakitafuta kifo hawatakiona kama unabii unavyosema.. “kwasababu mtu anayekutesa siku zote hataki ufe haraka..lengo lake uteseke kwa muda mrefu”..Ndicho kitakachotokea siku hiyo..watu watateswa lakini hawatauawa kwa haraka (Yatakuwa ni mara 100 zaidi ya yale ya Hitler, ambayo alikuwa anawapiga watu kwa nyundo yenye uzani mdogo kichwani mara nyingi aangalie ni kwa kiwango gani watu wanasikia maumivu, na kiwango cha watu kustahimili vifo wanapouliwa taratibu..mtu huyo anapigwa nyundo hata saa 4 mpaka anazirai, na mwisho wa siku kufa..

Au wanamfanyia mtu operation bila ganzi huku anatazamwa uwezo wake wa kumudu maumivu, au wanawatia watu kwenye barafu kali wakiwa uchi kwa masaa kadhaa kila siku)…ndivyo atakavyofanya mpinga-kristo na ziadi wakati huo wa dhiki kuu, na mateso hayo yatadumu kwa muda mrefu sana kwenye kambi hizo..kwa miaka sio chini ya mitatu na nusu..baadaye ndipo watawaua..wakati wengine waliosalia huko nje wakiendelea kufurahia Maisha baada ya kuipokea chapa…Hivyo dhiki kuu haitawahusu watu wote, bali tu wale watakaoikataa chapa…

Dhiki ya mataifa.

Baada ya wale waliokataa chapa kufa wote…Itakuwa ni zamu ya wale walioikubali chapa kupitia dhiki na wao…Dhiki hiyo ni ghadhabu ya Mungu mwenyewe atakayoimwaga juu ya wale wote walioipokea chapa…Ghafla tu wakati wanaona dunia ni tamu mambo yataanza kubadilika…Bahari itakuwa damu, mito na chemchemu zote zikuwa damu, majipu na magonjwa ya ajabu yataanza kuwatokea, roho za mapepo wabaya zitaachiwa juu ya wanadamu, kutokuelewana kutaanza kutokea,vita vya wenyewe kwa wenyewe vitazuka, mvua ya mawe makubwa kama talanta zitaanza kushuka juu ya wanadamu,.. jua litashushwa chini kuwaunguza wanadamu kwa kipindi kirefu..na mwisho jua na mwezi na nyota vitatiwa giza, tetemeko kubwa duniani litatokea, kila visiwa kitapotea na kuzama kwenye bahari ya damu, na milima itafumuka..

Wanadamu wote walioipokea chapa watakufa kifo kibaya kuliko hata cha wale walioikataa chapa..na baada ya kifo hicho wote wataelekea jehanamu ya moto..Na kabla hawajamalizika wote kufa, wale wa mwisho mwisho kufa wachache sana ambao ni washirika wa vita vya Harmagedono ndani ya giza hilo kuu watamwona Kristo akija katika mawingu wataomboleza sana , lakini biblia inasema wataangamizwa kwa upanga utokao katika kinywa chake..

Biblia inasema

Mathayo 24:29 “Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;

30 ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi”

Je! Unatamani kuwepo kwenye dhiki kuu?.. mimi sitamani..Natumai hata na wewe pia hutamani, Lakini unafahamu kuwa huo wakati upo karibu sana yamkini mambo hayo yatatokea katika kizazi chetu? Je! umempa Kristo Maisha yako?..Una uhakika wa kwenda kwenye unyakuo?…au bado upo kwenye ulimwengu?..kama bado ni mwasherati endapo parapanda italia leo utabaki hapa kukutana na hayo yote tuliyoyasoma hapo juu..

Kama hujaokoka na unataka kuokoka, fanya hivyo sasahivi.. Hapo ulipo tubu..na mwambie Bwana unataka kufanyika kuwa kiumbe kipya..baada ya kutubu tafuta kanisa ushiriki na wengine wenye Imani moja na wewe.. Na baada ya hapo pia hakikisha unabatizwa katika ubatizo sahihi kama hujabatizwa…Ubatizo sahihi ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo..Na Roho Mtakatifu atakusaidia kufanya yaliyosalia katika Maisha yako, na kukuweka katika mstari wa wale watakaonyakuliwa na kuepushwa na hukumu ya Mungu ya milele.

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 13

UFUNUO: Mlango wa 17

UFUNUO: Mlango wa 16.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

Rudi Nyumbani:

Print this post