Mungu amejifunua katika Ofisi kuu 3, (Baba, Mwana na Roho Mtakatifu).
Lakini katika dhihirisho zote hizi tatu (3) Mungu anabaki kuwa mmoja na si watatu.
Sasa swali ni je kama ni mmoja kwanini ajifunua hivyo katika utatu?
Jibu rahisi ni kwamba, Mungu kajidhihirisha hivyo kwa lengo la kumkamilisha Mwanadamu na si kujitambulisha yeye. Na kwanini mwanadamu akamilishwe kupitia dhihirisho hizo tatu?..Ni kwasababu alikuwa amepotea na kujitenga mbali naye kwasababu ya dhambi.
(Dhambi zinatutenganisha sisi na Mungu) Kama maandiko yanavyosema…katika Isaya 59:2.
Mwanzo katika Edeni Mungu alikuwa karibu sana na MTU, aliweza kumwona, kumsikia, na hata kuzungumza naye (Mwanzo 3:8). Lakini baada ya dhambi kuingia ule ukaribu na Mungu ukapotea, Adamua akawa hawezi kumwona tena Mungu wala kumsikia kama alivyokuwa anamsikia mwanzo…Ile dhambi ikamtenga mbali na Mungu. (Isaya 59:2).
Na Mungu kwa upendo wake kwetu, akaanza mpango wa kuturejesha karibu naye tena. Tumwone tena, tuseme naye, tutembee naye na tumhisi ndani yetu kama mwanzo. Lakini matengenezo hayo si ya mara moja kama maharibifu. (kuharibu mahusiano ni mara moja, lakini kujenga inagharimu muda mrefu).
Na neno la ahadi ni kwamba siku moja MASKANI ya MUNGU itakuwa pamoja na wanadamu kuliko hata ilivyokuwa EDENI.
Ufunuo 21:3 “Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, NAYE ATAFANYA MASKANI YAKE PAMOJA NAO, NAO WATAKUWA WATU WAKE. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao”.
Sasa mahusiano hayo yaliyoharibika Mungu alianza kuyatengeneza hatua kwa hatua..na sasa tupo katika hatua ya mwisho wa matengenezo hayo.. Hebu tuzitazame hizo hatua moja baada ya nyingine.
1.MUNGU JUU YETU. (Kama Baba)
Hii ni hatua ambayo Mungu alianza kuongea na watu kwa njia ya Maono na Ndoto, lakini akawa haonekani. Na alisema na watu wachache tu walioitwa manabii. Huu ni wakati ambao MUNGU alijidhihirisha kama NENO tu!.. (Maana yake MANENO YAKE ndiyo yaliyokuwa yanafahamika tu lakini yeye mwenyewe haonekani kwa macho).
Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu”.
2. MUNGU PAMOJA NASI (Kama Mwana).
Huu ni wakati ambao Mungu aliuvaa mwili, ili yale MANENO aliyokuwa anasema na watu kwa njia ya maono na ndoto basi ayaseme kwa mdomo wa damu na Nyama na kuyafafanua na kuyafundisha ili watu wamwone na kumwelewa.. Na mwili ambao aliuvaa ndio ukaitwa YESU.
Yohana 1:14 “Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.
Umeona?..Mungu anaanza kumsogelea tena mwanadamu kwa karibu.. Kwahiyo YESU ni Mungu aliyeuvaa mwili kwa lengo hilo la kuyasema yale maneno ya Mungu yaliyokuwa yanayosikika kwa ndoto na maono kupitia manabii..
Kuzidi kuuthibitisha uungu wa YESU basi soma mistari ifuatayo (Yohana 20:28, 1Yohana 1:1-2, Tito 2:13, Isaya 9:6 na 1Timotheo 3:16).
Lakini isingetosha tu Mungu aonekane katika mwili na kuyahubiri maneno yake kwa mdomo kama alivyokuwa anaongea na Adamu pale Edeni na huku bado mwanadamu hajui kanuni ya kuishi katika mapenzi ya Mungu…Hivyo akaongeza mpango wa pili juu yake wa kumfundisha mwanadamu njia na kanuni za kuishi kimatendo, kwahiyo ikambidi aishi kama mwanadamu ambaye anamcha Mungu.
Lengo si kutafuta ukamilifu yeye, bali ni kutufundisha sisi ukamilifu, ndio maana akaishi chini ya wazazi ili awafundishe watoto namna ya kuishi maisha ya kumcha Mungu, na tena akawa mtu mzima ili awafundishe watu wazima kanuni za kumcha Mungu, ndio maana akawa anaomba, akawa anafunga, akawa anamwambudu Mungu kana kwamba kuna Mungu juu n.k.
Hivyo maisha yake yakawa njia ili sisi tufahamu njia (soma Yohana 14:6). Lakini yeye hakuwa mtu, bali ni Mungu ndani ya mwili wa Mtu kwa lengo la kutufundisha njia..
Wafilipi 2:5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu”
Wafilipi 2:5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu”
Lakini pia isingetosha yeye ahubiri maneno yale kwa kinywa chake, na awe mwalimu wa kutufundisha sisi na ili hali bado tuna laana ya dhambi tuliyoirithi toka kwa wazazi wetu wa kwanza Adamu na Hawa
Hivyo akaongeza mpango mwingine wa tatu (2) juu ya hiyo miwili, kwamba autoe mwili wake huo kuwa sadaka ya dhambi baada ya kumaliza huduma kazi hizo mbili.. Hiyo ndio sababu kwanini Kristo afe msalabani..Ni ili sisi tupate ondoleo la dhambi.
3. MUNGU NDANI YETU (Kama Roho Mtakatifu).
Baada ya kurejesha uhusiano namna hiyo, kwamba sasa tunamwona MUNGU na tumeondolewa dhambi na kile kizuizi kulichokuwa kinatutenga sisi na Mungu, na ile laana ya Adamu tuliyokuwa tunaibeba. Mungu aliongeza mpango mwingine wa Mwisho ambao kupitia huo tutakuwa karibu na Mungu moja kwa moja, kwamba tutamsikia na kumwona na kumwelewa sana.
Na mpango huo si mwingine Zaidi ya yeye kuingia ndani yetu, kama ROHO, ili atusaidie madhaifu yetu..Ni sawa na mchezaji aliye katika michezo anayepewa kinywaji cha kuongeza nguvu na kusisimua misuli ili ashinde katika mchezo ule.
Na Roho Mtakatifu ni MUNGU katika ROHO, ambaye anaingia ndani yetu na KUSISIMUA uwezo wetu wa kumwelewa MUNGU, UWEZO wetu wa KUSHINDA DHAMBI, uwezo wetu wa KUMCHA MUNGU, Uwezo wetu wa kukumbuka n.k (Yohana 14:26 na Yohana 16:12-13).
Sasa kuthibitisha kuwa Roho Matakatifu ndiye yule yule Mungu soma 2Wakorintho 3:17.
Hii ni zawadi kubwa na kipekee sana, na ya mwisho inayomsogeza Mtu karibu na Mungu kuliko zote.
Sasa swali la ziada ni hili; Kwanini KRISTO aondoke!
Sababu ya KRISTO kuondoka na kwenda juu mbinguni ni kwenda kutuandalia sisi makao (Yaani ile YERUSALEMU MPYA), Makao ya watakatifu. (soma Yohana 14:2, Ufunuo 3:12 na Ufunuo 21:2).
Na makao hayo anayokwenda kutuandalia ni ili wakati utakapofika tukae naye milele, katika mbingu mpya na nchi mpya. (Maskani yake iwe pamoja nasi)…Hapo yale yaliyoharibika Edeni yatakuwa yametengenezwa upya tena katika utukufu Mkuu kuliko ule wa kwanza.
Ufunuo 21:3 “Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. 5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli”.
Ufunuo 21:3 “Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.
5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli”.
Je umeuona mpango wa Mungu??…na je umeyaona pia madhara ya dhambi??… Dhambi ilitutenga mbali na Mungu na mpaka sasa inatutenga mbali na Mungu..
Na kanuni pekee ya kumkaribia MUNGU ni kwa kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha (Mithali 28:13). Unapotubu kwa kumaanisha kuziacha unamkaribisha YESU maishani mwako ambaye humwoni kwa macho sasa, lakini siku moja utamwona… Lakini zawadi kubwa atakayokupa ambayo itakufanya ujihisi upo naye hata kama humwoni ni ROHO MTAKATIFU (ambaye kiuhalisia ni yeye mwenyewe katika mfumo wa Roho).
Na huyo Roho Mtakatifu atakulinda na ulimwengu, mpaka siku ya mwisho, ambayo BWANA YESU ATAKUJA na kutupa TAJI ZA UZIMA, na kukaa naye milele katika maisha ya furaha, yasiyo na mwisho, wala dhiki wala mateso, wala uchungu, wala vilio..kwasababu mambo ya kwanza yatakuwa yameshapita.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?
KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000
Kwa namna gani tumefanyika Makuhani na Ufalme?.(Ufunuo 1:6)
REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.
KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.
Rudi nyumbani
Print this post
(Masomo maalumu yahusuyo matoleo na sadaka).
Karibu tujifunze bible, Neno la Mungu wetu lililo mwanga wa Njia yetu na Taa iongozayo miguu yetu (Zab. 119:105).
Kuna umuhimu mkubwa sana wa kutoa Sadaka katika agano jipya, na shetani anafanya kila awezalo kuwazuia watu wasitoe sadaka kwa Mungu, kwani anaijua Nguvu iliyopo katika sadaka kwa mkristo.
Na moja ya njia anayotumia kuwafanya watu wasimtolee Mungu, ni kuwanyanyua watu/watumishi wake ambao watalichafua eneo hilo kwa aidha kuwalazimisha watu, au kuwatapeli, au kutumia uongo kwa kivuli cha biblia.
Na mtu aliye dhaifu kiimani, akishaona kasoro hizo basi moja kwa moja anakata shauri au anaadhimia kutotoa kabisa sadaka mahali popote kwa kuamini kuwa ni utapeli tu ndio unaoendelea, hivyo adui anakuwa ameshinda juu ya huyo mtu katika eneo la utoaji.
Lakini jambo ni moja tu!.. SADAKA INA NGUVU, na kila MKRISTO (pasipo kujali wadhifa wake, iwe mchungaji au mwanafunzi) NI LAZIMA AJIFUNZE KUTOA SADAKA ili KUFUNGUA MILANGO YA BARAKA na KUONDOA VIKWAZO.
Sasa zipo faida nyingi za SADAKA, lakini leo nataka tuizungumzie hii moja, ambayo ni muhimu sana kuijua…Nayo si nyingine Zaidi ya “KUHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU”. Si kila madhabahu inaharibiwa kwa kuomba tu!, la! Nyingine ni lazima zihusishe matoleo/Sadaka.
Hebu tusome habari ya Gideoni kidogo.
Waamuzi 6:25 ”Ikawa usiku uo huo Bwana akamwambia, MTWAE NG’OMBE WA BABA YAKO, yaani ng’ombe wa pili, wa miaka saba, UKAIANGUSHE MADHABAHU YA BAALI, aliyo nayo baba yako, UKAIKATE ASHERA ile iliyo karibu nayo; 26 UKAMJENGEE BWANA, MUNGU WAKO, MADHABAHU juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; UKAMTWAE YULE NG’OMBE WA PILI NA KUMTOA AWE SADAKA YA KUTEKETEZWA, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata”
Waamuzi 6:25 ”Ikawa usiku uo huo Bwana akamwambia, MTWAE NG’OMBE WA BABA YAKO, yaani ng’ombe wa pili, wa miaka saba, UKAIANGUSHE MADHABAHU YA BAALI, aliyo nayo baba yako, UKAIKATE ASHERA ile iliyo karibu nayo;
26 UKAMJENGEE BWANA, MUNGU WAKO, MADHABAHU juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; UKAMTWAE YULE NG’OMBE WA PILI NA KUMTOA AWE SADAKA YA KUTEKETEZWA, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata”
Hapo kuna hatua 4 Gideoni alizoambiwa na Mungu azifanye, ambazo zimebeba funzo kubwa..
1.MTWAE NG’OMBE WA BABA
Kwanini Amtwae Ng’ombe wa Baba yake?.. Kwasababu madhabahu ile ya baali ilikuwa imemshika sana baba yake (ilikuwa na nguvu juu ya nyumba ya baba yake yote). Ikifunua kuwa na sisi tunapotaka kushughulika na madhabahu za mababa, ni lazima tutafute sadaka kwajili yao, tena zile zinazowagusa kama hiyo ya Gideoni.
2. UKAIANGUSHE MADHABAHU YA BAALI.
Baada ya Gideoni kumtwaa Ng’ombe wa baba yake, hatua iliyofuata ni kuangusha ile madhababu ya baali na ashera iliyomshika baba yake (kwa kuivunja vunja na kuiponda ponda). Na sisi baada ya kuandaa sadaka hatua inayofuata ni kuzivunja hizo madhabahu kwa damu ya YESU kwa njia ya maombi na kwa KUZIONDOA KABISA KIMWILI KAMA ZINAONEKANA..
Kama kuna miti fulani inatumika kiibada hapo ulipo unaikata, kama ni mazindiko yamewekwa juu ya dari unayaondoa, wala usiogope, na tena wakati mwingine usimwambie mtu..wewe yaondoe kimya kimya kama alivyofanya Gideoni..ukienda kutafuta ruhusa hawatakuruhusu..zaidi utanyanyua vita vikali..
Gideoni angeenda kumpa kwanza taarifa baba yake kwamba ile madhabahu ya baali anaenda kuivunja baba yake asingemwelewa kabisa, kwani zile roho zilikuwa zimemshika baba yake na alikuwa anaiogopa sana ile miungu.. Vile vile madhabahu za mababa/na mababu zimewashika na kuwaogopesha wanaoziabudu.
Hivyo wewe vaa ujasiri kuwasaidia, kwani baada ya hapo watamshukuru Mungu wako kwa mambo yatakayofanyika baada ya hapo.
3.UKAMJENGEE BWANA MADHABAHU.
Baada ya Gideoni kuvunja ile madhabahu akaijenga madhabahu ya BWANA pale pale. Na sisi baada ya maombi na kusafisha kila uchafu..tunalisimamisha jina la Bwana mahali pale, kwa kuanzisha ibada, au kanisa…Wengi baada ya maombi hakuna tena kinachoendele, jambo ambalo ni la hatari sana!..
Ni lazima jina la Bwana liendelee kutamkwa mahali pale, ili madhabahu ya adui isisimamishwe tena, kama ni nyumbani au kijijini. (Maombi ya asubuhi na jioni lazima yafanyike, vile vile nyakati za kujifunza Neno la Mungu lazima ziendelee, na watu waendelee kumtafuta Mungu).. Sio kuomba tu na kuacha!.
4. UKAMTOE NG’OMBE KUWA SADAKA.
Baada ya Gideoni kujenga madhabahu akamtoa yule Ng’ombe wa baba yake awe sadaka na hapo ndipo ukawa mwisho wa Nguvu ya ile madhabahu ya baali kutenda kazi…ikamwachia baba yake moja kwa moja, hata alipokuja na kusikia kuwa ile madhabahu ya ashera imevunjwa na mwanae wala hakuogopa kwani tayari vifungo vya uoga vilikuwa vimeshamwachia…. na hata yeye (Gideoni) naye pia alifunguliwa kwa ujumla.. Na hapo ndio ukawa mwanzo wa ushujaa wa Gideoni!.
Vile vile na sisi tunapomaliza maombi na kuhitimisha kuvunja madhabahu…Ile sadaka inapaswa itumike kujenga kanisa la pale, au kuimarisha ibada za pale, ikiwa na maana kwamba kama fedha basi zitumike kununua biblia, au vitabu vya nyimbo, au kama ni kiwanja kimetolewa kama sadaka basi kitumike kujenga kanisa ili watu wa Mungu waendelee kumwabudu Mungu wa kweli pale.
Lakini ikiwa hakuna namna ya wewe kufika mahali pale ambapo madhabahu hizo zimesimamishwa, aidha kutokana na umbali.. basi baada ya maombi toa sadaka katika madhabahu nyingine yoyote ya Mungu aliye hai na italeta matokeo yale yale. Lakini kumbuka USIOMBE TU, BILA KUTOA!..TOA TOA TOA!!!!!
MADHABAHU NI NINI?
YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.
UDHAIFU WA SADAKA!
Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?
MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.
Rudi Nyumbani
Manabii Wanaume katika biblia walikuwa wengi kiidadi kuliko manabii wanawake.
UFUATAO NI UFUPISHO KWA NJIA YA JEDWALI:
Kutazama Jadwali zima, basi Slide kuelekea upande wa kushoto.
Mbali na hawa walioorodheshwa katika Jedwali hilo hapo juu, walikuwepo pia Manabii wengine ambao hawakuonekana wakitajwa katika kutoa Nabii za Nchi au Taifa.. Mfano wa hao tunawaona katika Jedwali lifuatalo.
MAJINA YA MANABII WANAWAKE
MAJINA YA MITUME WA BWANA YESU
WAFALME NA MALKIA WALIOTAWALA YUDA
WAFALME WALIOTAWALA ISRAELI.
Orodha ya Manabii wa kike katika biblia.
Jumla ya Manabii wa kike (wanawake) waliotajwa katika biblia ni 11, Kati ya hao manabii Tisa (9) walikuwa wa KWELI na Wawili (2) walikuwa wa UONGO.
LIFUATALO NI JEDWALI LA UFUPISHO..
Kulitazama jedwali zima, basi ‘SLIDE’ kuelekea kushoto.
UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.
Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.
Nini maana ya “Torati na manabii”?
Nini maana ya Mithali 11:17 inaposema;
Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake; Aliye mkali hujisumbua mwili wake.
JIBU: Mwenye rehema ni mtu wa huruma, mwenye kusamehe, mwenye kuachilia hata kama tendo alilofanyiwa linastahili adhabu kwa yule mwingine.
Biblia inasema mtu kama huyo huipa faida nafsi yake. Huitendea mema nafsi yake. Ambayo huipata kwanza hapa hapa duniani, kwasababu Bwana alisema kipimo kile tupimacho ndicho tutakachopimiwa na watu.
Marko 4:24 Akawaambia, Angalieni msikialo; kipimo kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa, na tena mtazidishiwa.
Maana yake ni anajijengea wigo mpana wa yeye naye kukutana na rehema nyingi mbeleni.
Vilevile anapata faida katika ulimwengu ujao, Bwana alisema..
Mathayo 5:7 Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.
Lakini anasema pia, mtu mkali hujisumbua mwili wake. Mtu mkali ni kinyume cha mtu mwenye rehema, ni mtu asiye na huruma, mwenye visasi, asiyejali, mkorofi, akiudhiwa anarudisha Maudhi, akikosewa kidogo, analipiza mara mbili, maneno yake hayana staha, kugombeza wengine kwake ni jambo la kawaida n.k.
Sasa matokeo ya mtu wa namna hii ni kuadhibiwa na Mungu, aidha hapa hapa duniani, au kule aendapo.
Bwana alisema…auaye kwa upanga, atauwawa kwa upanga, ukimtendea mtu kwa ukali na wewe ukali utakurudia, ukimpiga mwingine kwasababu kakuudhi kidogo, na wewe utapigwa mahali fulani kwasababu ulimuudhi mwingine.. (hicho huitwa kisasi cha Mungu).
Hivyo tendea mema nafsi yako, lakini pia mwili wako, kwa kumpenda Bwana. Na kuwa mwema.
KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.(Opens in a new browser tab)
Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)
(Opens in a new browser tab)NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.(Opens in a new browser tab)
Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?(Opens in a new browser tab)
SWALI: Nini maana ya Mithali 20:11 inaposema;
Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake; Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.
JIBU: Mwandishi anatuonyesha kuwa tabia ya mwanadamu yoyote, huwa haijifichi kufuatana na umri wake, kwamba yaweza kukaa ndani tu kipindi cha utotoni isionekane ikaja kudhihirika ghafla ukubwani. Hapana, anasema “Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake; Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili”.
Ikiwa na maana katika utoto ule ule unaweza kuuchunguza mwenendo wa mtoto, ukautambua. Na hiyo itakupa fursa ya kuurekebisha ukiwa ni mbaya, au kuuimarisha ukiwa ni mzuri, akiwa katika vipindi kile kile. Usione mwanao anayotabia ya udokozi, ukasema huyu ni mtoto tu, haelewi anachokifanya. Hapana unapaswa umrekebishe mapema, kwasababu hicho kitu kipo ndani yake, Ukiona mtoto anapenda kutazama biblia, anapenda kukaa kanisani, anapenda kusikiliza nyimbo za injili. Usiseme, huyu ni mtoto, ukampuuzia tu, kwa kuishia kusema ‘ubarikiwe mwanangu’ kinyume chake, mwendelezee mazingira hayo, kwasababu mwelekeo wa maisha yake, ni huko.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo, tabia zake zilianza kuonekana tangu utotoni, wazazi wake walimstaajabia, kumwona katika umri ule mdogo, yupo hekaluni, amekaa na waalimu na wakuu wa dini akiwauliza maswali, Kinyume chake wazazi wake hawakumkemea, bali waliyaweka yote mioyoni mwao, na kukubali kuutambua mwelekeo wa mtoto wao.
Hii ni kufundisha nini?
Lipo funzo la rohoni, lakini pia la mwilini.
La mwilini ni kuwa yatupaswa tuwatazame watoto, bila kupuuzia kitendo chochote wanachokidhihirisha katika umri ule wa chini. Ikiwa ni chema tukipalilie, ikiwa ni kibaya, tukikemee, na kushughulika nacho kwelikweli kabla hakijaweka mizizi. Hivyo hakuna mzazi au mlezi anaweza kusema, huyu mwanangu kabadilika tu ghafla. Ukweli ni kwamba mabadiliko yalianza kuwepo tangu zamani, isipokuwa kwa namna moja au nyingine tulipuuzia, tulipoyaona ndani yao tukadhani ni tabia za utoto tu. Wazazi wanaowajenga wanao katika maadili na vipawa tangu utotoni, ukiwatazama watoto wao wanapokuwa watu wazima, huwa wanakuwa na ufanisi na ujuzi wa hali ya juu sana, zaidi ya wale ambao watajijengea wenyewe wanapokuwa watu wazima. Hivyo mzazi jali maisha ya kiroho ya mwanao.
Vilevile rohoni, wapo ambao ni wachanga kiroho. Ikiwa na maana katika kanisa ni wale ambao wameokoka hivi karibuni. Halikadhalika hawa nao utaweza kutambua karama zao, sio mpaka wawe wakomavu kiroho. Aliye Mwinjilisti, utaona anapenda kushuhudia, lakini pia anauwezo wa kuwavuta wengine kwa Bwana. Aliye mwalimu, utaona anapenda sana kujifunza, aliye nabii, utaona karama za maono, ndoto, huwa zinamjia mara kwa mara, hata kwa namna ambazo hazielewi elewi, mwimbaji atapenda wakati mwingi kujifunza kuimba hata kama hawezi. Hivyo, kila mmoja wetu, kitu ambacho Mungu amekiweka ndani yake, hujidhihirisha mapema sana pindi ameokoka. Sio mpaka awe amekomaa sana kiroho kama wengi wanavyodhani.
Pindi unapookoka, kipindi hicho hicho karama yako inaanza kufanya kazi, unapachopaswa tu, ni kujishughulisha na utumishi wa Bwana, ndivyo utakavyoruhusu mambo hayo kutokea kwa wepesi na urahisi zaidi?
Mafundisho mengine
MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.
(TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!
Uasherati wa Kiroho maana yake nini?(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)
MAANA WEWE, BWANA HUKUWAACHA WAKUTAFUTAO”.(Opens in a new browser tab)
Mitume wa BWANA YESU walikuwa 12, ambapo baadaye walisalia 11 baada ya YUDA ISKARIOTE, aliyemsaliti BWANA kufa kwa kujinyonga!.. Nafasi yake ilichukuliwa na MATHIYA, na hivyo kukamilisha idadi ya Mitume 12
IFUATAZO NI TAKWIMU YA MITUME WA BWANA.
Kutazama column za ziada slide jedwali lifuatalo kuelekea upande wa kushoto.
Bwana alimaanisha nini katika Mathayo 5:20 aliposema..
[20]Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
Ni haki ipi hiyo.
JIBU: Katika andiko hilo tunaona Bwana akiainisha kigezo cha mtu kuingia kwenye ufalme wa Mungu..kwamba kigezo chenyewe ni “HAKI” …
Haki ni kitu kinachomstahilisha mtu kupokea kitu fulani. Kwamfano tunasema mtoto ana haki ya kulindwa…ikiwa na maana kilichomsababishia apate haki ya kulindwa ni ile hali ya utoto wake.
Mfano mwingine, tunasema ni mtu mzima ana haki ya kuoa au kuolewa na mtu amtakaye, katika wakati auchaguaye yeye. Tafsiri yake ni kwamba kinachompa haki ya kuwa hivyo ni kwasababu yeye ni “mtu-mzima”. Angekuwa mtoto asingekuwa na haki hiyo.
Sasa tukirudi katika habari hiyo tunaona kilichowafanya waandishi na mafarisayo wajihesabie haki kwamba wao ni warithi wa ufalme wa mbinguni. Ilikuwa ni kuitimiza sheria kwa matendo yao. Ambayo kimsingi wao wenyewe hawakuweza kuishika..kwa nje walionekana sawa lakini ndani walikuwa mbali na sheria yao. Kwasababu hakuwahi kutokea mtu hata mmoja aliyeweza kumpendeza Mungu kwa matendo yake, yeye mwenyewe.
Hivyo njia yao ya kupata haki, ambayo ni kwa matendo ya sheria haikuwa sawa. Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake na wale waliomsikia kwamba haki “ yao” isipozidi ya mafarisayo na waandishi kamwe hawataweza kuuingia ufalme wa mbinguni.
Swali je ya kwao inapaswa iweje. Je ya matendo ya sheria zaidi ya yale au vinginevyo?
Haki Yesu aliyoileta ambayo itampelekea mtu kurithi uzima wa milele ni kwa njia yake yeye mwenyewe .Ambayo sisi tunahesabiwa haki kwa kumwamini, kama mwokozi wa maisha yetu. Bila kutegemea matendo yetu ya haki. Yaani ni haki tuipatayo kwa neema.
Hivyo, wote wanaoipokea haki hiyo basi uzima wa milele ni wao. Na kwasababu ndio njia ambayo sisi tutamfikia Mungu. Basi neema yenyewe inatufundisha pia kuyazaa matunda ya Roho. Na hivyo tunaitimiza sheria ya Mungu mioyoni mwetu bila unafiki. Mbali na mafarisayo ambao walitegemea akili zako na nguvu zao.
Hata sasa ikiwa unategemea jitihada zako, zikupe haki mbele za Mungu, ndugu umepotea. Hutaweza Itegemee neema ya Mungu. Na hiyo itakusaidia kuyatimiza hayo mengine kwa Roho Mtakatifu.
TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.
FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.
Nini maana ya kumsulibisha mwana wa Mungu mara ya pili?
Masomo maalumu kwa wazazi/walezi.
Je unazijua kanuni za kuwabariki watoto wako?.. Wengi tunaijua kanuni moja tu ya kuwatamkia Baraka!..Hiyo ni sahihi kabisa na ipo kibiblia..(kwasababu maneno ya kinywa yana nguvu).
Lakini ni vizuri kufahamu jambo moja, kama Maneno yako hayataambatana na matendo yako, uwezekano wa hayo uliyoyasema kutokea bado utakuwa ni mdogo sana.
Kama unataka mtoto wako apate Baraka zote ulizozitamka juu yake, (na kwa njia ya maombi) ikiwemo Baraka katika kumjua Mungu, kuwa na afya na mafanikio, basi ongezea yafuatayo..
1.MFUNDISHE SHERIA ZA MUNGU.
Wafundishe watoto wako sheria za Mungu, huku wewe mwenyewe ukiwa kielelezo cha kuzifanya, ili wasione kama ni sheria tu za MUNGU bali hata zako wewe mzazi!.. Mtoto wako anapaswa azione sheria za Mungu kama ni za kwako wewe. Lakini asipoona wewe mwenyewe ukizifanya hata yeye hataweza kukusikiliza wala kuzitenda, hata kama kwa mdomo atakuitikia.
Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako, 9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.
Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,
9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.
2. USIMNYIME MAPIGO.
Yapo makosa yanayoweza kurekebishwa kwa maneno peke yake na mtoto akajengeka na kubadilika, lakini yapo yanayohitaji kurekebishwa kwa maneno pamoja na kiboko, hususani yale ya kujirudia rudia tena ya makusudi.
Biblia inasema ukimpiga hatakufa bali utakuwa umemwokoa roho yake na kuzimu.. (Hapo utakuwa umembariki pakubwa Zaidi ya kumtamkia tu baraka za maneno halafu hufanyi chochote).
Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. 14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.
Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.
3. MFUNDISHE KUSHIKA ELIMU
Badala ya kumtakia tu Baraka kwa kinywa (au kumwombea tu katika chumba chako cha ndani), tenga muda wa kumfundisha Umuhimu wa Elimu (kwanza ya Mungu) na pili ya dunia… Hapo utakuwa umembariki kwa vitendo na si mdomo tu.
Mithali 4:13 “Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako”
4. MFUNDISHE KUSHIKA SHERIA ZA NCHI na KUWAHESHIMU WENYE MAMLAKA (Wafalme).
Badala ya kumtamkia tu mafanikio, na kumwombea.. tenga muda kumfundisha umuhimu wa kuwatii wenye mamlaka na kuzingatia sheria ya nchi, hiyo itakuwa Baraka kwake katika siku zijazo za maisha yake.
Mithali 24:21 “Mwanangu, mche Bwana, NA MFALME; Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;
5. MFUNDISHE KATIKA NJIA INAYOMPASA
Ni njia gani inampasa katika umri wake na jinsia yake?.. Je! Katika umri wake huo anapaswa amiliki simu??..je katika umri wake anapaswa asemeshwe maneno hayo unayomsemesha?..je katika umri wake anapaswa atazame hayo anayoyatazama katika TV?.. je katika umri wake huo anapaswa awepo hapo alipo?..anapaswa afanye hicho anachokifanya?.Je! Kwa jinsia yake anapaswa kuvaa hayo mavazi unayomvika??..
Ni muhimu sana kujua mambo yampasayo mwanao/wanao kwa rika walilopo na jinsia zao…
Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”
Ukiyafanya hayo na mengine kama hayo pamoja na MAOMBI umwombeayo kila siku, basi utakuwa umembariki mwanao/wanao kweli kweli.
JE! UMEYABATILISHA MAMBO YA KITOTO?
FIMBO YA HARUNI!
MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?
NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?
MAOMBI YA KUOMBEA WATOTO.
Swali: Mafuta Mabichi yapoje, na yanafunua nini kiroho?
Jibu: Tureje..
Zaburi 92:10 “Bali pembe yangu umeiinua kama pembe ya nyati, Nimepakwa MAFUTA MABICHI”.
Mafuta mabichi yanayozungumziwa hapo si mafuta ambayo hayajapitishwa kwenye moto yakaiva na kuchemka… La!.. bali ni mafuta yaliyo mapya (yaani freshi) ambayo yayajakaa muda mrefu.
Nyakati za biblia na hata sasa wayahudi wanatumia mafuta ya Mizeituni kwa matumizi ya chakula na ibada.
Asilimia kubwa ya vyakula vya wayahudi na baadhi ya jamii za mashariki ya kati wanatumia mafuta ya Mizeituni kama kiungo cha mboga, na wakati jamii nyingine mbali na hizo wanatumia mafuta ya Alizeti au mimea mingine katika mapishi.
Chakula kilichoandaliwa kwa mafuta mabichi (yaani mapya) ya Mizeituni kinakuwa ni kitamu na chenye ladha… utaona hata ile MANA jangwani, ladha yake ilifananishwa na ladha ya mafuta mapya. (soma Hesabu 8:11).
Vile vile katika shughuli za kiibada, pale ambapo mtu anatawazwa kuwa mfalme basi alipakwa Mafuta haya ya mizeituni kama ishara ya kuruhusiwa kuchukua madaraka hayo,
1Samweli 9:15 “Basi Bwana alikuwa amemfunulia Samweli, siku moja kabla Sauli hajamwendea, akisema, 16 Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini, NAWE MTIE MAFUTA ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti; maana nimewaangalia watu wangu, kwa sababu kilio chao kimenifikilia”
1Samweli 9:15 “Basi Bwana alikuwa amemfunulia Samweli, siku moja kabla Sauli hajamwendea, akisema,
16 Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini, NAWE MTIE MAFUTA ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti; maana nimewaangalia watu wangu, kwa sababu kilio chao kimenifikilia”
Soma pia1Wafalme 16:12, 1Wafalme 1:34, na 1Wafalme 19:15-16 utaona jambo hilo hilo..
Vile vile makuhani walitiwa mafuta kama ishara ya kuchaguliwa na Mungu kutumika katika nyumba yake.
Zaburi 133:2 “Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake”.
Sasa ilikuwa ni heshima na jambo jema kutiwa mafuta ambayo ni mapya.. Kwani Mafuta ya Mizetuni kama yamehifadhiwa vizuri yanadumu kwa miaka 2 tu, ukipita huo muda yanaharibika na kutoa harufu nyingine. Kwahiyo chakula kilichoandaliwa kwa mafuta yaliyokaa kinakuwa hakina ladha na pia kinatoa harufu mbaya…
Vile vile mtu aliyepakwa mafuta yaliyokaa sana au kuharibika si jambo la utukufu… lakini mafuta mabichi ilikuwa ni jambo la utukufu kwasababu ni freshi.
Sasa mafuta mabichi (yaani mapya) na yale yaliyokaa (yaani ya zamani) yanawakilisha nini sasa kiroho?..
Mafuta yanamwakilisha ROHO MTAKATIFU. Hivyo mafuta yaliyokaa (ya zamani) yanawakilisha utendaji kazi wa Roho Mtakatifu katika Agano la kale… na Mafuta mapya ni utendaji wa ROHO MTAKATIFU katika agano jipya.
Na sisi tunayahitaji mafuta mabichi katika UTUMISHI WETU, na si yale yaliyokaa… kwasababu hayatatufaa sana..
Mafuta mapya yanatufundisha kuwa wakamilifu zaidi na katika kuyafanya mapenzi ya Mungu..kuliko yale ya zamani.
Mathayo 5:27 “Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake. 29 Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum. 30 Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum. 31 Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; 32 lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini. 33 Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako; 34 lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu”.
Mathayo 5:27 “Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;
28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
29 Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.
30 Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.
31 Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka;
32 lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.
33 Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;
34 lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu”.
Je umempokea YESU KRISTO, aliye mjumbe wa Agano jipya?, kumbuka huwezi kuwa na ROHO MTAKATIFU, kama YESU KRISTO hayupo ndani ya maisha yako.
Wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza
Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?
MAANA YA KRISTO/ JINA KRISTO LINA MAANA GANI?
Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?
Mfano wa wanawali kumi(Mathayo 25), unaelewekaje?