Category Archive Maana ya maneno

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

Swali: Wenye kutia Kalafati ni watu gani?

Jibu: Neno “Kalafati” limeonekana mara mbili tu katika biblia, katika Ezekieli 27:9 na Ezekieli 27:27.

Na maana yake ni “Kamba nyembamba iliyotengenezwa kwa pamba” ambayo inawekwa katikati ya mianya ya mbao za merikebu, ili kuzuia maji yasipenye katika ile miunganiko. (Tazama picha juu)

Hivyo watu wanaofanya hiyo kazi ndio waliotajwa hapo katika Ezekieli 27:9,

Ezekieli 27:9 “Wazee wa Gebali na wenye akili wake walikuwa ndani yako, WENYE KUTIA KALAFATI; merikebu zote za bahari na mabaharia wao walikuwa ndani yako, ili kubadiliana biashara yako”.

Lakini habari hii inahusu nini?

Ukisoma kitabu hicho cha Ezekieli mlango wa 27 kuanzia mstari wa kwanza, utaona ni unabii unamhusu mfalme wa Tiro. (Kwa urefu kuhusu Taifa la Tiro fungua hapa >>>Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa? 

Lakini hapa ni unabii wa Mfalme wa Tiro, Kwamba kwa kiburi chake na biashara zake nyingi alizozifanya juu ya nchi na katika bahari kupitia merikebu zake, siku inakuja ambapo ataanguka na kushuka chini kwasababu ya dhambi zake nyingi.

Na biashara za baharini alizokuwa anazifanya kupitia merikebu zake kubwa ambazo ndani yake kulikuwa na wana-maji, na “watiao Kalafati” na manahodha, zitaanguka na shughuli zao hizo zitaisha!

Ezekieli 27:27 “Mali zako, na bidhaa yako, na utajiri wako, wana-maji wako, na rubani zako, na WENYE KUTIA KALAFATI WAKO, na wafanya biashara wako, na watu wako wa vita wote, walio ndani yako, pamoja na jeshi lako lote lililo ndani yako, wataanguka katika moyo wa bahari katika siku ya kuangamia kwako”.

Ufunuo kamili pia kwa anguko la ulimwengu pamoja na dini zake za uongo katika siku za mwisho..

Ufunuo Ufunuo 18:2  “Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza;

3  kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake………………..

9  Na hao wafalme wa nchi, waliozini naye na kufanya anasa pamoja naye, watalia na kumwombolezea; wauonapo moshi wa kuungua kwake;

10  wakisimama mbali kwa hofu ya maumivu yake, wakisema, Ole, ole, mji ule ulio mkuu, Babeli, mji ule ulio na nguvu! Kwa kuwa katika saa moja hukumu yako imekuja.

11  Nao wafanya biashara wa nchi walia na kumwombolezea, kwa sababu hapana mtu anunuaye bidhaa yao tena;

12  bidhaa ya dhahabu, na fedha, na kito chenye thamani, na lulu, na kitani nzuri, na nguo ya rangi ya zambarau, na hariri, na nguo nyekundu; na kila mti wa uudi, na kila chombo cha pembe, na kila chombo cha mti wa thamani nyingi, na cha shaba, na cha chuma, na cha marimari;

13  na mdalasini, na iliki, na uvumba, na marhamu, na ubani, na mvinyo, na mafuta ya mzeituni, na unga mzuri, na ngano, na ng’ombe, na kondoo, na farasi, na magari, na miili na roho za wanadamu.

14  Na matunda yaliyotamaniwa na roho yako yamekuondokea; na vitu vyote vilivyo laini na vitu vya fahari vimekupotea; wala watu hawataviona tena kamwe.

15  Na wafanya biashara ya vitu hivyo, waliopata mali kwake, watasimama mbali, kwa hofu ya maumivu yake; wakilia na kuomboleza”

Je Umeokoka kwa kumwamini Bwana Yesu Kristo na kubatizwa, sawasawa na Marko 16:16?. Fahamu kuwa tunaishi katika siku za mwisho na Kristo amekaribia kurudi.

Kwa msaada Zaidi katika kumpokea Kristo fuatiliza sala hii ya Toba >>KUONGOZWA SALA YA TOBA  au wasiliana nasi kwa namba zetu zilizoanishwa mwisho wa somo hili.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

Rudi nyumbani

Print this post

Makasia ni nini? (Yona 1:13).

Swali: Kuvuta Makasia maana yake nini?


Likiwa moja linatiwa ”Kasia”, yakiwa mengi ni “Makasia” … Hizi ni  “Zana” ya kukisaidia chombo kutembea juu ya maji. Zana hii kwa mwonekano ni kama “Mwiko mkubwa”, (tazama picha juu), ambapo mabaharia walipoyavuta basi chombo kilisogea mbele..

Yona 1:13 “Lakini wale watu WAKAVUTA MAKASIA kwa nguvu, ili wapate kurudi pwani, wasiweze; kwa maana bahari ilizidi kuwachafukia sana”.

Unaweza kusoma Zaidi kuhusu makasia katika mistari ifuatayo; Marko 6:48, Yohana 6:19,  Isaya 33:21, na Ezekieli 27:6.

Je ni nini tunajifunza katika habari ya Yona na mabaharia hawa kuvuta makasia kurudi pwani?.. Fungua hapa >>>YONA: Mlango 1

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

YONA: Mlango wa 2

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

YONA: Mlango wa 3

YONA: Mlango wa 4

Rudi nyumbani

Print this post

Upepo wa Mbisho maana yake nini? (Mathayo 14:24)

Swali: Pepo za Mbisho ni nini?


Jibu: Turejee kuanzia mstari wa 23.

Mathayo 14:23 “Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake.

24  Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; MAANA UPEPO ULIKUWA WA MBISHO.

25  Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.

26  Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu”.

Maana ya neno “Mbisho” ni “Ukinzani”. Hivyo hapo aliposema “Upepo ulikuwa wa Mbisho”, maana yake upepo ulikuwa ni wa ukinzani, (yaani ulikuwa unavuma kinyume na uelekeo waliokuwa wanauendea).

Utasoma tena aina ya upepo huu ikitajwa katika Matendo 27:4,

Matendo 27:4 ”Kutoka huko tukatweka, tukasafiri chini ya Kipro ili kuukinga upepo, kwa maana PEPO ZILIKUWA ZA MBISHO”.

Safari yoyote ya majini, ikikutana na pepo za mbisho, safari hiyo inakuwa ni ngumu sana.. Kwasababu upepo utakuwa unavuma kinyume na ile merikebu na hivyo kuchelewesha safari au hata kuirudisha nyuma.

Lakini pepo za Mbisho zinafunua nini kiroho?

Pepo za mbisho kiroho ni kila aina ya matatizo, na shida na dhiki na vikwazo kutoka kwa yule adui vinavyokawisha au kurudisha nyuma safari yetu ya Imani hapa duniani.

Ndio maana utaona katika habari hiyo ya Mathayo 14:23-36, kabla wanafunzi wa Bwana YESU kufika nchi ya Wagerasi kwaaijli ya huduma ya kufundisha na kuponya wagonjwa na kuwafungua walioteswa na shetani, adui aliwatumia “Upepo huu wa mbisho”, lengo ni ili wasifanikiwe safari yao hiyo.

Lakini BWANA YESU alipoingia ndani ya chombo kile ule upepo ukakoma na misuko suko yake, kufunua kuwa zile zilikuwa ni hila za ibilisi.

Hivyo hata sisi tunapokutana na pepo za namna hii katika Imani, suluhisho ni kuzikemea kwa Imani na kwa jina la YESU, na zitatii.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

Rudi nyumbani

Print this post

Mata ni nini (Mwanzo 27:3).

Mata ni kitu gani na imebeba  ujumbe gani kiroho?


Jibu: Turejee,

Mwanzo 27:2 “Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa kwangu.

3 Basi, nakuomba, chukua MATA yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo;  4 ukanifanyie chakula kitamu namna ile niipendayo, ukaniletee, ili nile; na roho yangu ikubariki, kabla sijafa”.

“Mata” Ni jina jingine la “Silaha”. Kwahiyo badala ya kutumia neno “silaha” ni sahihi pia kutumia neno “Mata”.

Kwahiyo mstari huo wa tatu (3) ni sahihi kuuweka hivi,… “chukua SILAHA yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo ”

Na silaha hiyo inaweza kuwa mkuki, mshale au upanga, lakini katika andiko hilo silaha (Mata), iliyomaanishwa pale ni “Mshale”. Na kwanini ni mshale na si upanga wala mkuki?.. ni kwasababu kuna Podo imetajwa pale na upinde..

Maana yake huwezi kubeba upanga na upinde bila mshale, hivyo ni wazi kuwa Mata iliyomaanishwa pale ni mshale, kwasababu kuna upinde na Podo.

Sasa kwa maarifa kuhusu “Podo” na ufunuo wake kiroho waweza fungua hapa >>> Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

Sasa hizi zote ni silaha za mwili, lakini biblia inatufundisha kuwa zipo silaha za roho ambazo kila mkristo ni lazima azivae, na silaha hizo tunazisoma katika kitabu cha Waefeso 6:10-18, ambazo ni Chapeo ya Wokovu, Dirii ya Haki, Ngao ya Imani, Kweli, Upanga wa Roho, na Utayari miguuni pamoja na sala na maombi.

Na kwa silaha hizo pekee ndio tutaweza kumshinda adui yetu shetani, kwa mapana kuhusiana na silaha hizi jinsi ya kuvizaa na namna zinavyotenda kazi fungua hapa >>>MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UTHABITI WA AGANO LA MUNGU KWA MKRISTO.

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

KWANINI UPIGE MISHALE CHINI?

NDUGU,TUOMBEENI.

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

Rudi nyumbani

Print this post

Kiti cha Musa ni kipi? (Mathayo 23:2)

Swali: Biblia ina maana gani kusema Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa? Je hiki kiti cha Musa ndio kipi?



Jibu: Turejee,

Mathayo 23:2 “Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa”

“Kiti cha Musa” maana yake ni “Nafasi ya Musa”.. Leo hii tukisema mtu kaketi katika kiti cha Uraisi, maana yake ni kuwa “kachukua nafasi ya Uraisi”.

Sasa Musa alikuwa na nafasi gani?

Musa alikuwa na nafasi kuu mbili (2) mbele za wana wa Israeli.

   1) UALIMU.

Mtu wa Kwanza kuwafundisha wana wa Israeli HUKUMU, AMRI NA SHERIA za Mungu alikuwa ni MUSA.

Kumbukumbu 4: 14 “Bwana akaniamuru wakati ule NIWAFUNDISHE maagizo na hukumu, mpate kuzitenda katika nchi ile mtakayoivukia ili kuimiliki.

15 Jihadharini nafsi zenu basi; maana hamkuona umbo la namna yo yote siku ile Bwana aliyosema nanyi kutoka kati ya moto;

16 msije mkajiharibu nafsi zenu, mkajifanyia sanamu ya kuchonga, mfano wa sura yo yote, mfano wa mwanamume au mwanamke”.

Na mahubiri yake yaliendelea kuwa msingi wa marejeo kwa vizazi na vizazi mbeleni.

2) UONGOZI.

Hii ni nafasi ya pili aliyokuwa nayo Musa mbele ya wana wa Israeli:
Maandiko yanasema Mungu alimfanya Musa kuwa “Mkuu sana” mbele ya Misri na mbele ya wana wa Israeli. Kiasi kwamba maamuzi ya mwisho yalikuwa yanatoka kwake, kwa lugha nyepesi alikuwa ni kama Mfalme.

Kutoka 11:3 “…Zaidi ya hayo, huyo Musa ALIKUWA NI MKUU SANA katika nchi ya Misri, machoni pa watumishi wa Farao, na machoni pa watu wake”.

Soma pia Kutoka 18:13-24, utaona nafasi ya Musa katika kuwaamua Israeli.

Sasa baada ya Musa kuondoka (yaani kufa), Mafarisayo na Waandishi wakajiweka katika nafasi yake, maana yake wao ndio wakawa WAALIMU kama alivyokuwa Musa, na pia wakajiweka kuwa VIONGOZI kama alivyoukwa Musa, kiasi kwamba maamuzi ya mwisho yalikuwa yanatoka kwao.

Lakini ni heri kama wangekuwa wameketi kwenye nafasi hiyo ya Musa, na wakawa kama Musa..(yaani wacha Mungu kama Musa, au wapole kama Musa)..

Lakini wao walikuwa ni kinyume chake, walikuwa wanawatawala watu na kuwahukumu kwa sheria ya Musa lakini wao wenyewe ni wanafki mioyoni mwao.. mioyo yao ilikuwa ipo mbali na Mungu ingawa kwa nje wanaonekana ni waamuzi wazuri na viongozi wazuri wenye kusifiwa, lakini ndani yao wamejaa unafiki!.

Na Bwana YESU anatuonya tusiwe kama wao..

Mathayo 23:2 “Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa”

3 basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi

4 Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.

5 Tena matendo yao yote huyatenda ili kutazamwa na watu; kwa kuwa hupanua hirizi zao, huongeza matamvua yao;

6 hupenda viti vya mbele katika karamu, na kuketi mbele katika masinagogi,

7 na kusalimiwa masokoni, na kuitwa na watu, Rabi.

8 Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu.

9 Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni.

10 Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo.

11 NAYE ALIYE MKUBWA WENU ATAKUWA MTUMISHI WENU.

12 Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa”.

Je YESU KRISTO ni Bwana na Mwokozi wa maisha yako?..Je una uhakika jina lako lipo katika kitabu cha uzima?.. Kama bado YESU hayupo maishani mwako ni heri ukampokea leo, maana saa ya wokovu na wakati uliokubali ni sasa.
Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI KIZAZI KIPI WEWE UPO?

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.

Rudi nyumbani

Print this post

Yahu ni nani? (Wimbo 8:6).

Jibu: Turejee,

Wimbo 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni MIALI YA YAHU”.

“YAHU” ni jina lingine la “YAHWE” ambalo ndilo “YEHOVA”.

Kutoka 6:2 “Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; 

3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao”.

Kwahiyo YAHU, YAHWE na YEHOVA ni jina Moja!

Lakini hapo katika Wimbo 8:6 maandiko yanasema kuwa “upendo una nguvu kama mauti”.. maana yake kama vile mauti ilivyo na nguvu kiasi kwamba wanaokufa ni ngumu kurudia uzima! Vile vile Upendo wa Mungu kwetu ni mkuu kiasi kwamba akitupenda ametupenda!, hakuna wakati atatuchukia, anaweza asipendezwe na sisi lakini si kutuchukia!.

Warumi 8:35 “Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?………

38  Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39  wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Lakini pia anasema wivu ni mkali kuliko Ahera..Ahera ni “Kaburi”, Kwa urefu Zaidi fungua hapa >>>Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.

Na miali yake ni miali ya YAHU. Maana yake ni kuwa Mungu ana upendo lakini pia anawivu, huwezi kamwe kutanganisha vitu hivi viwili, UPENDO na WIVU.

Kwahiyo kama Mungu ametupenda, basi hapendi kuona tunaabudu miungu mingine, tukifanya hivyo tunamtia yeye wivu, umbao unaweza kutupeleka kaburini (Ahera).

Kutoka 20:3 “Usiwe na miungu mingine ila mimi.

4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, NI MUNGU MWENYE WIVU; NAWAPATILIZA WANA MAOVU YA BABA ZAO, HATA KIZAZI CHA TATU NA CHA NNE CHA WANICHUKIAO, 

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.

YAHU atusaidie tusimtie Wivu, lakini tumpende, na vile vile upendo wake utubidiishe katika kuyafanya mapenzi yake.

Maran atha.

Mafundisho Mengine:

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

IJUE HEKIMA YA MUNGU KATIKA KUKUINUA KIMAISHA.

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

Rudi Nyumbani:

 

Print this post

Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

Falaki ni nini katika biblia?

Jibu: Turejee,

Isaya 47:12 “Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda. 

13 Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na WASIMAME HAO WAJUAO FALAKI, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata”.

“Falaki” ni “elimu ya nyota na sayari na jua”.

Wanaofanya Falaki, wanaamini kuwa  “mpangilio wa nyota, mwezi na jua na sayari angani, unaathiri tabia ya nchi na tabia ya mtu/watu”. Jambo ambalo kwa sehemu moja ni kweli na sehemu nyingine uongo!.

Ni kweli Mpangilio wa Jua na mwezi, unaweza kuathiri tabia ya nchi, kama  vile vipindi vya mvua, kiangazi, au kipupwe….ipo miezi ambayo mvua inanyesha, na miezi ambayo mvua hainyeshi, ipo miezi ya kiangazi na miezi ya kipupwe…Majira ya mwezi wa 6 na 7 ni Kipindi ambacho jua linakuwa mbali na dunia na kweli nchi inaathirika na baridi kali, katika ukanda wa kusini wa dunia.

Vile vile tabia za mimea zinaathiriwa na majira na nyakati, yanayotokana na mpangilio wa mwezi na jua angani, mfano tabia za miembe kuzaa maembe zinaathiriwa na mwezi wa 12, kwamba yanapofika majira ya mwezi huo wa 12 mpaka wa 1 basi miti yote ya miembe inazaa sana, tofauti na kipindi kingine chote (kwahiyo kwa sehemu ni kweli).

Sasa kwa mantiki hiyo wana-falaki wanaamini kuwa kama mpangilio wa jua, mwezi na nyota angani unaweza kuathiri mazingira na hali ya hewa, basi vile vile mpangilio huo huo unaweza kuathiri tabia za watu, na hisia zao, na maamuzi yao na hata hatima yao!.

Kwamba kila tarehe na mwezi unabeba matukio yake kulingana na mtu na mtu, na pia kulingana na tarehe aliyozaliwa, vile vile mpangilio wa nyota na mwezi unaweza kuelezea ni kitu gani mtu atafanya, au atakitenda, au kitampata, vile vile ni bahati gani ipo mbele yake au hatari gani inamkabili.

Kwahiyo wote waliohitaji kujua mambo yatakayowapata mbeleni waliwatafuta hawa wana-Falaki, au kwa lugha nyingine wanajimu kujua hatima zao.

Lakini swali ni je! Elimu hii ina ukweli wowote na je wakristo ni sahihi kuitafuta, ili kujua hatima zetu kupitia falaki?

Jibu ni LA! Elimu hii haina ukweli wowote, mpangilio wa sayari na nyota, na mwezi hauwezi kuelezea tabia, hisia, maamuzi au hatima ya Mwanadamu!…mpangilio huo unaweza kufaa katika utabiri wa hali ya hewa na misimu ya kupanda na kuvuna (tena kwa sehemu ndogo) lakini hauwezi kutabiri maisha ya mtu.

Maisha ya mtu hayatabiriwi wala kusomwa kwa kutazama jua, au mwezi au nyota au sayari, kama ndivyo kulikuwa hakuna haja ya Kristo kuja, au hata kama angekuja basi angetuhubiria sana hiyo elimu, bali maisha ya mtu yanatabiriwa kwa KULITAZAMA NENO LA MUNGU peke yake!.

Ukitaka kujua kesho yako itakuwaje, isome biblia, itakuambia sio tu kesho utakuwa wapi, bali MILELE UTAKUWA WAPI!!!.

Utauliza vipi wale Mamajusi, mbona walioiona nyota ya Bwana YESU kutoka mashariki?.

Mungu alipenda kutumia ishara ya nyota kuelekeza utukufu wa mwanae alipozaliwa, lakini hakuwa anahubiri elimu ya nyota pale!, ni sawa na alivyotumia ishara ya Nguzo ya wingu au nguzo ya moto juu ya wana wa Israeli walipokuwa jangwani,.. ilikuwa ni kwa lengo la kuelekeza utukufu wa wana wake mahali walipo, lakini hakuwa anahubiri elimu za mawingu na moto, kwamba zikasomwe kwa bidii ili kuelezea utukufu juu ya mtu/watu.

Vile vile leo hii shetani anapenyeza elimu hii ya Nyota(Falaki) ndani ya kanisa kwa kasi sana!. Elimu hii inatoka kwa waganga na inahamia kanisani kwa kasi sana..Watu hawasomi tena biblia wanatafuta kusomewa nyota zao! Hawaombi tena kulingana na Neno wanaombea nyota kwa kurejea elimu ya falaki.

Ndugu usidanganyike!..Elimu ya nyota (Falaki) ni elimu ya shetani asilimia mia.

Kama unataka kusafisha hatima yako itii biblia, wala usitafute maombi ya kutakasiwa nyota!, hiyo ni elimu nyingine!… Vile vile ukitaka kujua kesho yako itakuwaje kasome biblia, usitafute utabiri wa kusomewa nyota kutoka kwa yoyote yule iwe mganga au anayejiita mtumishi wa Mungu.. Biblia pekee ndiyo itakayokuonyesha tabia yako na kukupa utabiri sahihi wa maisha yako ya kesho na ya milele.

Je umemwamini Yesu?, je umebatizwa ubatizo sahihi? Je umepokea Roho Mtakatifu?.

Bwana Yesu anarudi.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MSHIKE SANA ELIMU.

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MIEZI 13 YA KIYAHUDI.

Rudi nyumbani

Print this post

Gudulia ni nini? (1Samweli 26:11).

Jibu: Tusome,

1Samweli 26:11 “Hasha! Nisiunyoshe mkono wangu juu ya masihi

12 Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile GUDULIA LA MAJI, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia”.

Gudulia ni chombo maalumu kilivyotengenezwa kwa lengo la kuhifadhia maji ya kunywa ya watu wachache, kwa lugha ya sasa hivi tunayaita “majagi”

Magudulia/majagi ya zamani yalitengenezwa kwa malighafi tofauti na ya zama hizi. Zamani majagi/magudulia waliyatengeneza kwa kutumia udongo wa (mfinyanzi tazama picha juu), lakini sasa yanayotumika mengi yao yametengenezwa kwa glasi au plastiki.(tazama picha chini).

Gudulia ni nini?

Mistari mingine inayotaja chombo hiki (gudulia) ni pamoja na 1Wafalme 19:6, Yeremia 19:1 na Yeremia 19:10.

Je umemwamini Bwana Yesu?, je unajua kuwa tunaishi katika majira ya kurudi kwa YESU mara ya pili, na wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea?.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Shilo ni wapi?

TWEKA MPAKA VILINDINI.

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

JINSI YA KUISHINDA HALI YA MSONGO WA MAWAZO.

Rudi nyumbani

Print this post

Uadilifu ni nini kibiblia?

Uadilifu ni neno pana linalomaanisha, nidhamu, utu, auminifu, yaani kutenda kile ambacho jamii husika inataka wewe ukitende.

Kibiblia uadilifu ni utiifu katika sheria ya Mungu. Vilevile uaminifu na nidhamu katika mambo yote ya ki-Mungu.  Mtu wa namna hiyo anaitwa mwadilifu, au mcha Mungu.

Kwamfano watu ambao walikuwa waadilifu katika biblia ni kama Yusufu, Ayubu, Danieli pamoja na wengine, ambao waliweza kutembea katika sheria za Mungu bila lawama yoyote.

Baadhi ya vifungu ambavyo utakutana na Neno hilo ni hivi;

2Nyakati 26:3 Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na miwili; na jina la mamaye aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.  4 Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Amazia babaye

Zaburi 64: 10 “Mwenye haki atamfurahia Bwana na kumkimbilia, Na wote wenye moyo wa adili watajisifu”

Zaburi 112: 2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.  3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele.  4 Nuru huwazukia wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki

Soma pia 2Nyakati 27:2,29:2 Zaburi 140:13.

Lakini cha kujua kuhusu tabia hii, ni kwamba Bwana Yesu alisema ni wajibu pia wa kila kiongozi wa kiroho/ Mhubiri kufundisha mafundisho ya adili, zaidi ya mafundisho ya utoaji.

Luka 11:42  Lakini, ole wenu, Mafarisayo, kwa kuwa mwatoa zaka za mnanaa na mchicha na kila mboga, na huku mwaacha mambo ya adili, na upendo wa Mungu; iliwapasa kuyafanya hayo ya kwanza, bila kuyaacha hayo ya pili.

Mafundisho ya adili, ni kama vile, utakatifu, auminifu, haki, utu wema, amani, umoja na kiasi, uvumilivu, fadhili, upole, unyenyekevu. na yote yanayofanana na hayo. Kwasababu ndicho Bwana anataka kukiona ndani ya mioyo ya watu wake, wawe waadilifu kama yeye alivyo mwadilifu (Zaburi 25:8).

Je! Wewe ni mwadilifu? Kumbuka huwezi kuwa hivyo kama upo nje ya Kristo. Yeye ndio pekee anayeweza kukupa nguvu ya kutenda mema. Hivyo ili uitwe mwadilifu sharti kwanza umpokee Yesu akuokoe, akusamehe dhambi zako. Ndipo Bwana akupe nguvu ya kumcha yeye.

Ikiwa upo tayari leo kuokoka, basi fungua hapa kwa mwongozo wa Sala ya Toba. >> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

IMANI YENYE MATENDO;

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Ebenezeri/ Ebeneza maana yake ni nini?

Maana ya Neno Ebenezeri ni jiwe la msaada.

Wakati ule Israeli wanamlilia Bwana awarudie, Wafilisti walipata taarifa wakakusanyika pamoja ili wawaangamize, Israeli walivyoona hivyo wakaogopa sana, wakamsihi Samweli awalilie kwa Bwana ili wasaidiwe kwasababu wanakwenda kuangamia. Na Mungu akasikia kilio chao, akawatetea, kwa kutoa ngurumo kubwa sana, zilizowadhoofisha wafilisti, hivyo wakapigwa na kuharibiwa, mpaka miji ambayo wafilisti walikuwa wameiteka ikarudishwa yote kwa Israeli. Ndipo Samweli akachukua jiwe kubwa akalisimamisha Kati ya Mispa na Sheni, akaliita Ebenezeri, akasema hata sasa Bwana ametusaidia.

1Samweli 7:12 Ndipo Samweli akatwaa jiwe, na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri, akisema, Hata sasa Bwana ametusaidia.

Lakini la kujiuliza kwanini Samweli anyanyue jiwe, na sio kitu kingine labda nguzo au bendera? Na pia alikuwa na maana gani kusema “Hata sasa Bwana ametusaidia”? Na sio maneno mengine?

JIBU: Alinyanyua jiwe kwasababu alipata ufunuo wa aliyemsaidia, na huyo si mwingine zaidi ya  Kristo ambaye ndio jiwe letu (Warumi 9:33). Alitambua ni yeye ndiye aliyewapigania vita kwa kunguruma, Kwasababu ndiye simba wa Yuda.

Lakini pia kwanini aseme “Hata sasa Bwana ametusaidia” ni kwasababu alitambua kuwa Mungu ni msaada wao sikuzote, hadi ule wakati walioufikia bado alikuwa ni msaada wao, ndio maana akasema “Hata sasa Bwana ametusaidia”, yaani sio tu jana, au zamani bali hata sasa Bwana yupo pamoja nasi.

Ikiwa na maana kuwa hata na sisi tukiwa ndani ya Kristo wakati wote atatulinda,  sio jana tu peke yake, hadi leo na hata kesho. Ni furaha iliyoje kuwekwa chini ya huu mwamba Yesu Kristo?

Je! Kristo ni jiwe lako? Je! Ni Ebenezeri wako? Kama sio, embu mkaribishe leo maishani mwako akuokoe, upate uzima wa milele. Akulinde mbali na Yule mwovu. Ikiwa upo tayari kutubu na kumpokea Yesu basi fungua hapa kwa msaada wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

LIONDOE JIWE.

Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako.

Rudi nyumbani

Print this post