UFANYE WEMA WAKO KATIKA MAARIFA.

UFANYE WEMA WAKO KATIKA MAARIFA.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, Karibu tujifunze biblia..

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, NA KATIKA WEMA WENU MAARIFA”

Wema usiokuwa na Maarifa bado haujakamilika.. Ni kweli unaweza kufanya Wema na nia yako ikawa ni njema, lakini wema huo usipoufanya katika maarifa, huenda ukakuletea madhara hata wewe mwenyewe uliofanya huo wema.

Hebu tuangalie mtu mmoja katika biblia ambaye aliufanya wema wake katika maarifa yote, na huyo si mwingine zaidi ya Yule Msamaria-mwema.

Hebu tusome habari yake na kisha tutafakari…

Luka 10: 30 “ Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.

31  Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.

32  Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.

33  Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,

34  akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.

35  Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa”

Tunaona Msamaria huyu alipopita njiani na kukuta mtu kalala kando, hakukurupuka  na kumpeleka nyumbani kwake, akalale na watoto wake au ndugu zake.. Badala yake alimchukua na kumpeleka katika nyumba ya kulala wageni (yaani Guest-house), na akiwa huko huenda aliendelea na hatua nyingine za kuripoti habari yake katika vyombo vilivyohusika, ili kama ikiwezekana apate msaada zaidi wa kuwapata watu wa nyumbani kwake.

Sasa kwanini hakumpeleka nyumbani kwake moja kwa moja?, si kwasababu hakuwa na huo uwezo, au labda ni mbali.. La! Bali ni kwasababu alitumia maarifa katika Wema wake, kwasababu Yule mtu alikuwa hamjui, hivyo kumchukua na kumpeleka nyumbani moja kwa moja, ingeweza kuwa hatari kwasababu huenda akafa, na matatizo yakawa kwa Yule aliyemsaidia, au huenda si mtu mzuri wakati wa kulala usiku akapata nafuu na kuamka na kumdhuru Yule aliyemsaidia.

Hivyo suluhisho la akili na hekima si kumpeleka nyumbani, bali katika nyumba ya kulala wageni.

Hali kadhalika na sisi tunapaswa tufanye wema wetu katika MAARIFA.. Si kila anayehitaji msaada basi ni wa kumpatia kile anachokihitaji yeye, bali tunapaswa tupime namna ya kumsaidia katika maarifa..

1 . Mtu  usiyemjua akikuomba fedha ya hitaji Fulani, ni vizuri usimpe hiyo fedha bali ukamnunulia hilo hitaji lake na kumpatia.

2. Ukimkuta mtu usiyemjua yupo katika hali ya kuhitaji msaada wa kimalazi.. usimchukue moja kwa moja na kumpeleka kwako, jitahidi umtafutie mahali pa kulala hususani kama gesti, angalau kwa siku moja, huku unaendelea kufuatilia taarifa zake na kuziripoti, na ukishajiridhisha vya kutosha ndipo umwamishie kwako.

3. Mtu usiyemjua akikuomba nguo, kama una uwezo basi mnunulie yake mpya, lakini usiitoe ile ya mwilini mwako na kumpatia, kwasababu shetani anaweza kuitumia hiyo kama mlango wa kukuletea matatizo maishani mwako. Lakini kama mtu unamjua au umejiridhisha kabisa kuwa ni mhitaji asiye na tashwishi basi waweza kumpa moja kwa moja nguo inayotoka moja kwa moja.

4. Mtu usiyemjua akikuomba Lift ya gari, au pikipiki, au baiskeli..kama una uwezo mlipie nauli apande katika chombo kingine, kwasababu humjui mtu huyo ni nani, na hivyo ni rahisi kutumiwa na adui kuleta dhara lolote lile.

5. Mtu usiyemjua akikuomba chakula kutoka katika sahani yako, usimpe kile chakula, badala yake mnunulie cha kwake binafsi, (sio uchoyo kufanya hivyo, bali ni hekima) kwasababu shetani anaweza kumtumia kama chombo cha kukuletea matatizo, kwasababu unaweza kumpa na kumbe kile chakula hakiendani na mwili wake, hivyo kikamletea madhara au hata kifo, jambo ambalo linaweza kutafsirika kwamba umemwekea sumu au dhara lolote, na kukuingiza wewe matatizoni pasipo sababu yoyote, hivyo ni lazima katika WEMA wako uweke na maarifa. (Kumbuka usiache kutenda wema, bali utende katika maarifa).

Na mambo mengine yote mema unayoyafanya kwa Mtu au watu, hakikisha unayafanya katika maarifa yote, ndivyo biblia inavyotufundisha.

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, NA KATIKA WEMA WENU MAARIFA

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?

Nuru yetu inapaswa iangaze au isiangaze kulingana na Mathayo 5:16 na Mathayo 6:1?

MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuiaua Nchi ni kufanya nini? (Waamuzi 18:2).

Jibu: Tusome,

Waamuzi 18:2 “Basi wana wa Dani wakatuma watu wa jamaa zao, watu watano katika hesabu yao yote, watu mashujaa, kutoka Sora, na kutoka Eshtaoli, ili kuipeleleza hiyo nchi, KUIAUA; wakawaambia, Haya, endeni mkaikague nchi hii; basi wakaifikilia nchi ya vilima vilima ya Efraimu, hata nyumba ya huyo Mika, Wakalala huko”

Kuiaua nchi maana yake ni KUITEMBELEA NCHI au KUIZURU. Kwahiyo watu wanaozunguka zunguka ndani ya nchi kwa lengo la kuipeleleza au kwa lengo la utalii, maana yake ni WAMEIAUA HIYO NCHI.

Mungu wetu anaiaua dunia hii tunayoishi, kutafuta watu wanaomcha yeye, kuwatia nguvu na kuonyesha uweza wake juu yao.

2Nyakati 16:9 “Kwa maana macho ya Bwana hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake…”

Lakini pia adui yetu shetani ANAIAUA dunia nzima kutafuta mwenye haki mmoja amwangushe..

Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. 

7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

 8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu”

Hivyo hatuna budi kuutunza ukamilifu wetu ili tusije tukanaswa katika mitego ya shetani na hatimaye kuanguka kabisa.

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.

Rudi nyumbani

Print this post

Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)          

Huu ni mwendelezo wa Mafundisho maalumu yawahusuyo wanawake.

Mithali 11:16          

[16]Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; ..”

Ujumbe huu ni kwako wewe binti/Mama/ ambaye unapenda kuheshimiwa na Mungu pamoja na wanadamu.

Kumbuka  heshima inatafutwa na si wote wanayo, kwasababu inagharama yake kuipata…heshima sio uzuri, heshima sio elimu, sio u-kisasa, wala sio pesa..Ni thamani yako ya ndani, inayoonwa na wengine.

Dada Ukitaka kufahamu ni nini kitakupa heshima usiwafuate mabinti wenzako,la! Hata na  akili zako pia usizifuate, Bali mtafute aliyekuumba ili akupe siri ni nini kitakuthaminisha hapa duniani kwa wanadamu.

Inatia huruma kuona, mabinti wengi wanadhani wanaheshimiwa kwa urembo wao..hivyo hubuni kila namna ya kujipamba, na kujichubua ngozi zao, wanavaa mawigi na makucha ya bandia, kisha kwa ujasiri wanatembe mbele ya watu..wakidhani kuwa ndio wanaonekana watu wa maana sana kwenye jamii..Ukifanya hivyo Binti umepotea!

Wanadhani kuonyesha miili yao barabarani, na kujifanya wakisasa ni heshima, dada hapo huheshimiwi unasanifiwa tu. Unachofanya ni kujiongezea nafasi tu ya kuwa kiburudisho cha macho ya wahuni..na ndio maana watakupigia miluzi na kukutazama tazama.mara mbili ili kesho urudie kufanya hivyo tena, wajiburudishe macho yao, lakini zaidi ya hapo wewe ni FELIA…

Hivyo fahamu heshima yako inatoka wapi..

Biblia inaeleza heshima ya mwanamke inakuja katika mambo haya  saba

  1. Kumcha Bwana
  2. Adabu
  3. Upole
  4. Kiasi
  5. Utulivu
  6. Kujisitiri
  7. Utiifu

Yote haya utayasoma katika vifungu hivi:

Mithali 31:30

[30]Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili;  Bali mwanamke AMCHAYE BWANA, ndiye atakayesifiwa.

1 Timotheo 2:9-11

[9]Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa MAVAZI YA KUJISITIRI, pamoja na ADABU nzuri, na MOYO WA KIASI; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

[10]bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

[11]Mwanamke na ajifunze katika UTULIVU, AKITII kwa kila namna.

1 Petro 3:3-4

[3]Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

[4]bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya UPOLE NA UTULIVU, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

Ukiyazingatia haya binti/mwanamke, heshima itakufuata yenyewe…na lolote ulitamanilo kwa Mungu utalipata tu..Kama ni mume bora Mungu atakuletea, tena zaidi ya matarajio yako kama Ruthu alivyoletewa Boazi, 

Kama ni kibali, utakipata tena cheo kikubwa zaidi ya wengi, ikiwa ni utumishi, Bwana ataizidisha karama yako pakubwa sana..Na zaidi ya yote una uzima wa milele. Hata ukienda mbinguni unawekwa kundi moja na akina Sara na Ana na Debora, Mariamu, na wanawake wote mashujaa walioishindania imani ipasavyo.

Lakini kinyume chake ni kweli, usipoyashika hayo, utafanana tu na Yezebeli na ukienda kuzimu utawekwa kundi moja na yeye.

Usiiuze heshima yako.

Jithamini.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

USHAURI KWA MWANAMKE WA KIKRISTO.

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?

Rudi nyumbani

Print this post

Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala Mwangalie sana

SWALI: Mstari huu unamaana gani?

Mithali 23:1-3

[1]Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala, Mwangalie sana yeye aliye mbele yako.

[2]Tena ujitie kisu kooni, Kama ukiwa mlafi.

[3]Usivitamani vyakula vyake vya anasa; Kwa maana ni vyakula vya hila.


JIBU: Sulemani akiwa kama mfalme alielewa sana tabia za wafalme zilivyo na hivyo kwa uzoefu wake hapa anatoa mapendekezo yake kwa mtu yeyote ambaye ataitwa na mfalme au mtu yeyote mkuu kula chakula pamoja nao.

Anasema chukua tahadhari “Mwangalie sana”..uwe na kiasi na hizo zawadi zake akupazo, hapo ametumia lugha ya vyakula, lakini yaweza kuwa uongozi, fursa, pesa, n.k..anasema uwe na kiasi, kwasababu nyingi za hizo huwa ni za hila.

Kwasababu mfalme hawezi kumwalika mtu, kama haoni kuna faida fulani anaweza kuipata kwake, ingekuwa ni hivyo angekuwa anamwalika kila mtu tu, ikulu na kushiriki naye.

Mfano wa wazi tunauona, kwa malkia Esta alipomwalika Hamani, kama Hamani angelielewa andiko hili, angetafakari mara mbili mbili ni kwanini apewe tu yeye kipaumbele cha juu zaidi ya wengine..Lakini alikuwa anacheka na kufurahia tu mialiko, na matokeo yake yakawa ni kujipeleka mwenyewe kitanzini.

Ni kawaida ya shetani akishaona una hatari ya kuupindua ufalme wake, haji kwa hasira au kiboko, atakuja kwa anasa, alifanya hivyo kwa Bwana Yesu, na kumwambia “hivi vyote nitakupa, endapo utaanguka na kunisujudia”..Bwana akamkemea, na kumfukuza, wakati mwingine mfalme Belshaza alimwita Danieli, amtabirie vizuri juu ya ufalme wake akamuahidi atakuwa mtu wa tatu kwenye ufalme wake, Danieli hakupumbazika na kukaa pamoja naye katika utawala wake wa dhambi, kinyume chake akakataa akatabiri na kuondoka zake..Lakini usiku huo huo kumbe ndio ulikuwa mwisho wa mfalme Belshaza, akavamiwa na wamedi, na kuuawa, sasa kama Danieli angekutwa pale anafanya anasa nao naye pia habari yake ingeishia pale.

Watumishi wengi wa Mungu wakubwa, wamepoozwa moto wao wa injili au utumishi wao kwa ujumla na watu wakuu au wa mamlaka, kwa kukosa kwao kiasi. 

Hivyo mstari huu unatupa tahadhari, katika ngazi yoyote ile,  iwe ni ngazi ya chini, katika kampuni,au shirika,  au katika serikali, tualikwapo, tuwe makini, kuchunguza ni mashauri gani yapo nyuma yake.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

NUHU WA SASA.

Rudi nyumbani

Print this post

YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.

Maandiko yanasema kuwa Bwana Yesu hakuwahi kumbatiza mtu yeyote kwa maji katika huduma yake yote…

Yohana 4:1 “Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza,

(lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake)

Umeona?.. kila mahali Bwana Yesu alipofika aliwaachia wanafunzi wake wabatize!.. lakini yeye mwenyewe hakubatiza mtu yeyote kwa maji. Sasa hiyo haimaanishi kuwa ubatizo wa maji hauna maana!. (mbele kidogo tutaelewa zaidi umuhimu wake).

Sasa kufuatia mwenendo huo wa Bwana Yesu kutombatiza mtu yeyote, ni kuonyesha kuwa anao ubatizo mwingine ambao atawabatiza nao watu, ambao hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kuufanya!… Ubatizo wa maji mwanadamu anaweza kuufanya kwa mwanadamu mwenzake, Lakini ubatizo huo ambao Bwana Yesu atakwenda kuwabatiza nao watu hakuna anayeweza kuufanya zaidi yake yeye mwenyewe.. Na ubatizo huo si mwingine zaidi ya ule wa Roho Mtakatifu.

Tunapobatizwa kwa Maji, miili yetu inazama kwenye maji mengi na kuibuka juu, kama ishara ya kufa na kufufuka na Kristo.. Lakini tunapobatizwa kwa Roho Mtakatifu ni kitendo cha Bwana Yesu kuzichukua roho zetu na kuzizamisha katika Roho Mtakatifu, Ni tendo kuu sana ambalo hakuna mwanadamu yeyote wala malaika yeyote anayeweza kulifanya.. kama maandiko yanavyosema katika Yohana 3:16.

Luka 3:16 “Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO”

Hiyo ikimaanisha kuwa kama vile ubatizo wa maji ulivyo wa muhimu vile vile na ubatizo wa Roho Mtakatifu ni wa muhimu sana..Ni lazima tubatizwe na watu katika Maji na vile vile tubatizwe na Bwana Yesu katika Roho Mtakatifu.

Wapo watu wanaosema kuwa ubatizo wa Roho Mtakatifu sio wa muhimu, bali ule wa maji tu unatosha, na wapo wanaosema ubatizo wa Roho Mtakatifu ndio wa muhimu, hivyo mtu akishaupata ubatizo wa Roho Mtakatifu hakuna haja tena ya ubatizo wa maji. Nataka nikuambie kuwa hiyo imani ni imani potofu ambayo imetengenezwa na ufalme wa giza kuwaua watu kiroho, maandiko yanasema “…Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu (Yohana 3:5) ”

Kuzaliwa kwa maji ni ubatizo wa Maji, na kuzaliwa kwa Roho ni ubatizo wa Roho Mtakatifu (Haihitaji elimu kubwa kuelewa hili, ni tafakari nyepesi kabisa).

Na zaidi ya yote tunazidi kuthibitisha kuwa ubatizo wa maji ni wa muhimu hata baada ya kuupokea ule wa Roho Mtakatifu, wakati ule Petro alipofika nyumbani kwa Kornelio, maandiko yanasema baada ya wale watu wa nyumbani kwa Kornelio kushukiwa na Roho Mtakatifu, bado Mtume Petro aliwaagiza wakabatizwe katika maji na kwa jina la Yesu Kristo.

Matendo 10:44  “Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno.

45  Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu.

46  Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu,

47  Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?

48  Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha”

Umeona?, hao watu walitangulia kubatizwa na Bwana Yesu mwenyewe kwa  ubatizo wa Roho mtakatifu, lakini bado walikwenda kubatizwa tena na akina Petro kwa ubatizo wa Maji. Kwasababu Petro alijua kuwa hawa wasipozaliwa kwa Maji na kuwaacha tu wawe wamepokea ubatizo wa Roho hawataweza kuuona ufalme wa Mungu, sawasawa na maneno ya Bwana.

Je! na wewe umebatizwa kwa Maji?.. Kama bado na umeshasikia ukweli namna hii, upo hatarini sana…Na kumbuka kama ulibatizwa uchangani, basi huna budi kubatizwa upya kwa sababu hukuwa umejitambua wakati huo, zaidi sana kama pia ulibatizwa kwa maji machache, ni lazima ubatizwe upya kwa maji mengi (Yohana 3:23)

Na je! umeshabatizwa pia kwa Roho Mtakatifu?.. kama Bado msihi Bwana naye ni mwaminifu atakupa Roho wake mtakatifu, kwasababu yeye anatamani uwe naye kuliko wewe unavyotamani.. lakini ni sharti kwanza utubu kwa kumaanisha kuacha dhambi zako zote na kubatizwa kwa maji kama tayari umeshausikia ukweli, kwa kukamilisha mambo hayo, maandiko yanasema Yule Roho ni kwaajili yetu, na kwa vizazi vyetu, Bwana Yesu anatubatiza kwa huyo bureeeeeeeeee..

Matendo 2:37  “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39  Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

NUNUA MAJI YA UZIMA.

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

Rudi nyumbani

Print this post

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

Jibu: Tusome,

1Samweli 28:24 “Naye yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona nyumbani; akafanya haraka kumchinja; akatwaa na unga, akaukanda, akafanya MKATE WA MOFA kwa unga huo”.

Mkate wa Mofa ni mkate uliotengenezwa bila kuwekwa “Hamira”.  Hamira kwa lugha ya kibiblia inaitwa “Chachu” kazi yake ni kuchachusha au kuumua unga uliokandwa, kama biblia inavyosema katika..

Mathayo 13:33  “Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia”

Na tena biblia inasema.. “Chachu kidogo huchachua donge zima (Wagalatia 5:9)”

Kwahiyo Mikate ya Mofa ni mikate iliyotengenezwa bila kuwekwa hamira, mfano wa chapati. Kwa  wayahudi baada ya sikukuu ya pasaka kupita, sikukuu iliyokuwa inafuata ilikuwa ni sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu (yaani Mofa),  Ndani ya siku 7 Wana wa Israeli waliambiwa wale mikate ya Mofa, na mtu yeyote ambaye alionekana anakula mikate mingine zaidi ya hiyo, aliuawa kulingana na sheria ya torati.

Na ndani ya kipindi hicho pia mtu yeyote akionekana na Viungo vya Hamira ndani kwake, hata kama atakuwa hajaviweka kwenye unga, kitendo tu cha kuiweka ndani ilikuwa pia adhabu yake ni kifo

Kutoka 12: 15 “Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba; siku hiyo ya kwanza mtaondoa chachu yote isiwe katika nyumba zenu kabisa; kwa kuwa mtu ye yote atakayekula mkate uliochachwa tangu siku hiyo ya kwanza hata siku ya saba, nafsi hiyo atakatiliwa mbali na Israeli”.

Soma pia Walawi 23:5-6.

Lakini je! Mkate wa Mofa unawakilisha nini kiroho?

Mkate wa Mofa unawakilisha Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo,  Na ndio uliotumika na wakristo wa kanisa la kwanza katika kushiriki Meza ya Bwana, na ndio unapaswa utumike hata sasa katika kushiriki meza ya Bwana, na si biskuti au maandazi!.

Luka 22:19  “Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu”.

Sasa kwanini Bwana Yesu achague mkate wa Mofa, kuwakilisha Mwili wake?

Ni kwasababu Mwili wa Bwana Yesu haubadiliki wala hauwezi kubadilishwa maumbile. Hamira/chachu kazi yake ni kubadilisha maumbile ya vitu, ndio maana inapowekwa kwenye unga uliokandwa baada ya muda Fulani utakuta ule unga umeumuka!

  Sasa mwili wa Kristo hauumushwi, wala hauwezi kubadilishwa kimaumbile..bali siku zote ni ule ule!(Waebrania 13:8).. Maana yake kanuni za Bwana Yesu ni zile zile, hazibadilishwi na mazingira wala na mtu, Neno lake ni lile lile jana na leo na hata milele.

Hatuwezi kutia hamira Neno la Mungu, Neno la Mungu likisema ulevi ni dhambi!, hatuwezi kuliwekea hamira hapo na kusema ulevi sio dhambi!..likisema “mtu anapaswa avae mavazi ya kujisitiri” hatuwezi kulitia hamira kwa kusema “Mungu haangalii roho bali anaangalia mwili (1Timotheo 2:9)”

Na mambo mengine yote, biblia iliyoyataja ni lazima tuyazingatie yabaki kama yalivyo bila kuumuliwa na hamira za mafundisho ya uongo.

Bwana Yesu atusaidie katika hayo.

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo aliye Bwana na mwokozi wetu. Utukufu na uweza ni vyake milele na milele. AMEN.

Leo tuone ni nini Bwana anasema nasi tena nyuma ya  tukio la Hajiri kijakazi wa Sarai alipomtoroka bibi yake..

Kama tuonavyo katika maandiko mateso yalipozidi, alikimbilia jangwani..lakini akiwa kule jangwani, alilia sana  Bwana, amsaidie kwasababu kama tujuavyo jangwani ni mahali ambapo hakuna mahitaji yoyote ya kijamii..ukizingatia na yeye alikuwa mjamzito, hawezi kujihudumia kwa lolote.

Lakini upo uamuzi ambao hajiri aliuchukua ambao kama asingeuchukua kwa wakati ule, haijalishi angemlilia Mungu namna gani asingepata msaada wowote, wala asingeisikia sauti ya Mungu, ilipokuwa inamtafuta kusema naye kule jangwani..

Na uamuzi wenyewe ulikuwa ni ule wa kukimbilia kwenye CHEMCHEMI YA MAJI. 

Mwanzo 16:6-12

[6]Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake.

[7]MALAIKA WA BWANA AKAMWONA KWENYE CHEMCHEMI YA MAJI katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri.

[8]Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai.

[9]Malaika wa BWANA akamwambia, Rudi kwa bibi yako, ukanyenyekee chini ya mikono yake.

[10]Malaika wa BWANA akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi.

[11]Malaika wa BWANA akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana BWANA amesikia kilio cha mateso yako.

[12]Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.

Ni vizuri tukaona kitu hapo…kumbe malaika alikuwa anamtafuta hamwoni…lakini alipofika katika ile chemchemi ya maji ndipo akamwona Hajiri kisha akazungumza naye na kumpa maagizo.

Hata sasa, watu wengi wanamlilia Mungu kweli awasaidie, wapo katika majangwa ya namna mbalimbali, na Mungu kweli anawasikia, lakini pale ambapo malaika wa Bwana wanatumwa kuwapa majibu yao hawawaoni, kwasababu hawapo katika chemchemi ya maji…wapo kwenginepo.

Na maandiko yanasema Yesu ndiye chemchemi ya maji ya uzima..

Yohana 4:13-14

[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

Ni mara ngapi tunakuwa wepesi wa kumlilia Mungu atusaidie, lakini kumuishi Kristo katika maisha yetu inakuwa ngumu.

Hatuna Muda wa kusoma Neno, hatuna muda wa kuomba, hatuna muda wa kufanya ibada, na kushuhudia habari njema, hatuna muda wa kudumu katika chemchemi ya maji ya uzima..lakini wakati huo huo tunalia Bwana tusaidie! Bwana tutetee! Bwana tubariki!, Bwana tuponye..tukiwa katika biashara zetu, katika vijiwe vyetu, katika mitandao ya kijamii tunachat, katika tv, tunaangalia movie, na tamthilia, katika party na starehe, tunakesha kila mwisho wa wiki, lakini kukesha kanisani mara moja kwa wiki hatuwezi. 

Tusahau kumwona malaika wa Bwana, akileta majibu ya maombi yetu..kwasababu macho yao hayaoni mahali pengine zaidi ya penye chemchemi ya maji ya uzima. Ndivyo walivyoumbwa, Kamwe malaika hawezi kukufuata kwenye kijiwe chako, au kwenye mihangaiko yako, kukupa majibu ya maombi yako. Atakuona tu, pindi uwapo uweponi mwa Kristo, hilo tu!…hawana shughuli na mambo ya ulimwengu huu.

Tumaanishe sasa kumrudia Bwana, kwa mioyo yetu yote..tujifunze kudumu uwepo mwa Kristo, Kuna faida nyingi. Ondoa uvivu wako katika masuala ya wokovu wa Roho yako. Ikiwa utaamka kila siku alfajiri kwenda kazini, kwanini uone uvivu kuhudhuria mikesha na ibada?

Bwana atusaidie…

Je umeokoka? Je! Unatambua ya kuwa tunaishi katika kizazi ambacho kinaweza kushuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa Kristo duniani? Kwasababu dalili zote zimeshatimia. Na kanisa tunaloishi ndio la mwisho lijulikanalo kama Laodikia?

Umejiwekaje tayari, ikiwa upo tayari kumkabidhi Kristo maisha yako. Na unahitaji mwongozo huo, au utapenda kupata ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi 

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

+255693036618/ +254789001312

Bwana akubariki shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WEWE U MUNGU UONAYE.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NUNUA MAJI YA UZIMA.

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Rudi nyumbani

Print this post

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

(1Samweli 23:1-14)

Keila ni moja ya miji midogo  iliyokuwa Israeli, lakini kuna wakati ulipitia taabu kubwa sana ya kuvamiwa na wafilisti, wakateswa wakaibiwa nafaka zao, hivyo wakiwa katika mahangaiko hayo, na mateso hakuna wa kuwasaidia, Maandiko yanatuonesha akatokea Daudi katika maficho yake, alipokuwa anamkimbia Sauli..Akapita katikati ya mji huo,akasikia, kuwa wafilisti wapo huko wanawatesa watu wa Keila.

Lakini Daudi aliguswa sana moyo, hakujali Maisha yake na kuendelea na safari yake ya mafichoni bali alichokifanya ni kukiita kikosi chake kidogo, na kukiambia adhima yake ya kuwasaidia, japokuwa watu wake walikuwa wachache, walijitia nguvu, ndipo Daudi akaenda kumuuliza Mungu, kama akiwapigania watu wa Keila atashinda au hatashinda, Mungu akamwambia, hakika atashinda, akauliza tena na mara nyingine Mungu akamjibu hivyo hivyo kuwa watashinda.

Tengeneza picha, wenyeji wa mtu huyo wanasikia, Shujaa Daudi amekuja kuwasaidia, walifurahi kiasi gani, Na ndivyo ilivyokuwa Daudi akaenda kuwapigania watu hao, akashinda na kurejesha mateka yote, tena  na Zaidi akawarejeshea. 

Wanawake, wazee, vijana wa Keila wakahuika mioyo yao, wakafurahia kuona ng’ombe zao, ngano zao, watumwa wao, mali zao zimerudi.. Waliruka ruka na kucheza, na kumpenda sana Daudi.

Lakini habari mbaya ziliwafikia kwa ghafla watu wa Keila, biblia inasema, Sauli aliyekuwa anamwinda Daudi alipata taarifa kuwa adui yake amefika Keila, kuwasaidia watu wale. Hivyo, akatuma vikosi vyake, kwenda kumkamata. Lakini safari hii sio tena kumtafuta, bali kwenda kuwafuata wakuu wa mji huo, na kuwaambia wamkamate Daudi wamfikishe kwa Sauli ili amuue.

Lakini kabla Sauli hajatuma vikosi vyake, Daudi naye akapata taarifa kuwa Sauli amejua yupo kule, hivyo alichokifanya ni kwenda kumuuliza Mungu kama ilivyokawaida yake, kuhusiana na jambo hilo kama kweli watu wa Keila watamtoa na kumpa Sauli au La..

Matarajio ya Daudi yalikuwa ni hapana, akiamini kuwa wale watu aliowaokoa kwa mkono mkuu, watampa hifadhi watamficha, hawawezi kumsaliti, Lakini Bwana akamwambia Daudi kuwa, hao watu watakutoa kwa Sauli. Hapo Daudi akawa hana jinsi Zaidi ya kuingia tena maporini kwenda kutafuta mahali pa kujificha.

1Samweli 23:7 “Kisha Sauli aliambiwa ya kwamba Daudi amefika Keila. Sauli akasema, Mungu amemtia mkononi mwangu; kwa maana amefungwa ndani, kwa vile alivyoingia katika mji wenye malango na makomeo. 

8 Basi Sauli akawaita watu wote waende vitani, ili waishukie Keila, na kumhusuru Daudi na watu wake.  9 Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera. 

10 Ndipo Daudi akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mimi mtumwa wako nimesikia hakika ya kuwa Sauli anataka kuja huku Keila, ili kuuharibu mji kwa ajili yangu. 

11 Je! Watu wa Keila watanitoa, nitiwe mkononi mwake? Je! Sauli atashuka, kama mtumwa wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, nakusihi, umwambie mtumwa wako. Naye Bwana akamjibu, Atashuka. 

12 Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? Bwana akasema, Watakutia. 

13 Basi Daudi na watu wake, ambao wapata kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda po pote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akaacha kutoka nje. 

14 Basi Daudi alikuwa akikaa nyikani ngomeni, akakaa katika nchi ya milima milima kwenye nyika ya Zifu. Naye Sauli alikuwa akimtafuta kila siku, lakini Mungu hakumtia mikononi mwake.”

Maana yake ni nini habari hii?

Wenyeji waliona ni heri mmoja wao aangamie lakini mji wote upone mikononi mwa jeshi la Sauli. Hawakujali msaada mkubwa aliowapatia, wakamwogopa mtu ambaye hakuwajali hata kidogo walipokuwa katika mateso yao. Mfano Dhahiri wa watu wa kipindi kile cha Bwana Yesu.. 

Hawakujali miujiza waliyotendewa, hawakujali wafu waliofufuliwa, pepo waliotolewa, vipofu walioona, habari njema za faraja zilizohubiriwa na Yesu, Watoto wao walioponywa. Lakini Waliposikia tu kuna hatari ya Herode kuja kuwaangamiza.. Wakasema ni heri Mmoja afe ili taifa zima lisiangamie.

Yohana 11:47  “Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi.

48  Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu.

49  Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;

50  wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima”

Wakamsulibisha mwokozi wao.. Hata Sasa hatushangai kuona, watu wakimfurahia Kristo anapowasaidia tu nyakati za mateso yao, anapowabariki, anapowalinda, anapowaponya.. Lakini ikija tu tufani ndogo ya ibilisi kwa ajili ya Kristo, tayari wanamsaliti, wanautupilia mbali wokovu, akiambiwa anafukuzwa kazi kisa Yesu wake, anasahau, mema yote aliyofanyiwa na Bwana siku zote za Maisha yake. Anamwacha. Akiona umri umeenda haolewi, anasema huku kuvaa magauni ya nini tena, ngoja nivae vimini nitembee nusu uchi, ili nipate mchumba.

Tusiwe kama watu Keila, ambao walimsaliti shujaa wao kisa mtu asiyewajali, tusimwache Yesu kisa vitisho vya shetani vidogo vinavyopita mbeleni yetu. Kisa wazazi hawapendezwi na Imani yetu. Tukumbuke yeye ndio jemedari wetu, kama alitupigania vipindi vya nyuma atatupigania hata sasa.

Tumpende Bwana Mungu wetu kwa mioyo yetu yote, kwa nguvu zetu zote, kwa roho zetu zote, na kwa akili zetu zote.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Naivera ni nini? Kwanini Daudi aliihitaji alipomtafuta Mungu?

Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

Haya ni Mafundisho maalumu kwa ajili ya wanawake..

JIBU: Ni vema kujua mfungo ni nini na madhumuni yake ni yapi.

Mfungo ni kitendo cha kujizuia kufanya jambo fulani la lazima kwa kipindi fulani kwa lengo la kumkaribia Mungu zaidi..

Kwamfano mfungo hasaa hulenga kujizuia kula au kunywa , wengine huzuia usingizi, wengine kazi, wengine mawasiliano n.k. inategemea unalenga nini.

Hivyo pale unapojizuia kula au kunywa lengo lako ni upate utulivu wa kuwa karibu zaidi na Mungu katika maombi na kumtafakari.

Kwahiyo kwa jinsi unavyojiweka mbali zaidi na masuala ya mwili ndivyo unavyoupa zaidi mfungo wako nguvu.

Hivyo tukirudi katika swali je tunaruhisiwa kushiriki tendo la ndoa tuwapo katika mfungo? 

Jibu ni kuwa hakuna katazo lolote..kwasababu shabaha ya mfungo wako lilikuwa katika kujizuia kula au kunywa..

Lakini ikiwa utapenda kuzuia pia tendo la ndoa, ni vizuri lakini hapo ni jambo la makubaliano na mwenzi wako, ikiwa ataliridhia kwa wakati huo msifanye tendo la ndoa, ili mwelekeze fikra zenu zote kwa Bwana…hapana shida. Ni vema.

Lakini ikiwa mmoja wenu hajaridhia, hapo hupaswi kuzuia, kwasababu uolewapo au uoapo, huna amri juu ya mwili wako, isipokuwa mwenzako, kwahiyo akikataa hupaswi kupinga.Ni lazima ufanye.

Biblia inasema..

1 Wakorintho 7:3-5

[3]Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

[4]Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

[5]Msinyimane isipokuwa MMEPATANA kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.

Vilevile ikiwa nyote hamjaridhia…pia bado hakuharibu mfungo wenu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kushiriki tendo la ndoa, ndani ya mfungo, hakubatilishi mfungo wa mtu. Isipokuwa tu maandiko yanatuelekeza  iwe ni kwa kiasi ili mpate na muda wa kusali 

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

VYA MUNGU MPENI MUNGU.

Tunajua kuwa vya Kaisari tunavyopaswa tumpe ni “kodi” lakini je! Na Vya Mungu ambavyo tunapaswa tumpe ni vipi kulingana na Luka 20:25?

Tuanze kusoma mstari wa 21 ili tuelewe vizuri zaidi..

Luka 20:21 “Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli

22  Je! Ni halali tumpe Kaisari kodi, au sivyo?

23  Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,

24  Nionyesheni dinari. INA SURA NA ANWANI YA NANI? Wakamjibu, Ya Kaisari.

25  Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, NA VYA MUNGU MPENI MUNGU.

26  Wala hawakuweza kumshitaki kwa maneno yake mbele ya watu; wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa”.

Nataka tujifunze ni vigezo gani Bwana Yesu alitumia hapo kuhalalisha kuwa Kodi ni haki ya Kaisari, hiyo itatusaidia na sisi kujua vilivyo vya Mungu ni vipi?.. Na tunaona hakutumia kitu kingine chochote isipokuwa ile “Sura” inayoonekana kwenye ile sarafu pamoja na ‘Anwani” inayosomeka pale. Kwani Dinari ile ilikuwa na sura ya Kaisari na Anwani ya Kaisari, hivyo ni haki kuwa mali ya Kaisari.

Sasa kama vya Kaisari vilitambulika kwa sura iliyokuwa inaonekana juu ya Sarafu, ni wazi kuwa na vya Mungu vitatambulika kwa njia hiyo hiyo, Maana yake chochote chenye Sura ya Mungu hicho ni cha Mungu, na anapaswa apewe.. Sasa hebu tusome maandiko yafuatayo..

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.

Umeona?..Kumbe! sisi tumeumbwa kwa Mfano wa Mungu, Nyuso zetu ni nyuso za Mungu, na kama tumeumbwa kwa mfano na Sura ya Mungu basi ni wazi kuwa sisi (yaani miili yetu na roho zetu) ni mali ya Mungu na si yetu! na hivyo ni LAZIMA TUMPE MUNGU VILIVYO VYAKE…Biblia inasema hivyo kuwa sisi si mali yetu wenyewe..

1Wakorintho 6:19  Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? WALA NINYI SI MALI YENU WENYEWE

Na tena inasema Miili yetu ni MALI INAPASWA ITOLEWE KWA BWANA..

1Wakorintho 6:13  “Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. LAKINI MWILI SI KWA ZINAA, BALI NI KWA BWANA, naye Bwana ni kwa mwili”

Hiyo ikiwa na maana kuwa ni lazima tuitoe miili yetu kwa Bwana, ni lazima tumpe MUNGU vilivyo vyake, Tusipofanya hivyo tutakuwa tunafanya makosa makubwa sana..

Sasa tunampaje Mungu vilivyo vyake?

1.KWA KUOKOKA!

Kuokoka maana yake ni kumkabidhi Bwana roho zetu, kwa kutubu dhambi na kubatizwa kwa maji na kwa Roho.(Marko 16:16). Unapomwamini Bwana Yesu na kumkabidhi maisha yako, hapo umempa Mungu vilivyo vyake, na hivyo utakuwa umeyafanya mapenzi ya Mungu.. kwasababu Utu wako wa ndani umeumbwa kwa mfano wake.

2. KWA KUJITENGA NA DHAMBI.

1Wakorintho 6:13  “…LAKINI MWILI SI KWA ZINAA, BALI NI KWA BWANA, naye Bwana ni kwa mwili” Hapa maandiko yanaonesha dhahiri kuwa “mwili si kwa zinaa bali kwa Bwana ” maana yake mtu anayefanya zinaa inaiharibu mali ya Mungu, ambayo ni mwili wake.. Kwasababu mwili wake umeumbwa kwa mfano wa MUNGU, una anwani ya Mungu!!..

Hivyo si ruhusa kuuharibu kwa zinaa, au kwa pombe, au kwa sigara, au kwa kuuandika tattoo au kwa kuuvisha jinsi mtu atakavyo (nguo za kubana au zisizo za maadili) au kwa mambo mengine yote yanayofanana na hayo..

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba.. Vya Mungu anavyopaswa apewe ni ROHO ZETU, na MIILI YETU. Kwasababu vitu hivyo vina sura na anwani ya Mungu mwenyewe, kama vile dinari iliyokuwa na sura na anwani ya Kaisari.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Nuru yetu inapaswa iangaze au isiangaze kulingana na Mathayo 5:16 na Mathayo 6:1?

Rudi nyumbani

Print this post