Boazi na Ruthu.
Atukuzwe Yesu Kristo Bwana wetu na mwokozi wetu, Nakukaribisha tuzidi kuzitafakari siri za ufalme wa mbinguni.
Awali ya yote tukumbuke kuwa mahusiano ambayo Yesu anayatengeneza kwa kila mwaminio sio mahusiano kama ya rafiki na rafiki, au ndugu na ndugu, hapana, bali kama ya Bwana-arusi na Bibi-arusi.
Ni vema hilo ukalifahamu mapema, kwasababu kitakachotufanya tuende mbinguni, ni Ndoa, na sio urafiki. Hivyo yeye kama Mfalme ndio Bwana-arusi, na sisi ni Bibi-arusi wake. Tunapojiunganisha naye, ni lazima tuonyeshe tabia za bibi-arusi wa kweli, vinginevyo hatutapata kibali cha kuwepo katika karamu ya Arusi yake, atakayoifanya mbinguni kwa wateule wake kwa tukio linalojulikana kama Unyakuo.
Mimi na wewe hatua budi kuhakikisha tunakuwa bibi-arusi safi wa Kristo, na sio masuria, ili tupate kibali cha kukubaliwa na yeye siku ile ya mwisho.
Leo wa neema za Bwana, tutajifunza kwa kupitia maisha ya Boazi na Ruthu. Kumbuka hadithi zote unazozisoma katika biblia zina ufunuo wa Kristo na kanisa lake. Hivyo usomapo hakikisha unamwomba Roho Mtakatifu akufunulie, ili biblia kwako isiwe kama vitabu vingine vya hadithi.
Sasa kama wewe ni mwanafunzi wa Biblia utakuwa umeshawahi isoma habari ya Ruthu. (Kama hujasoma nashauri ukakisome kwanza hicho kitabu, ndipo utaelewa vema, kiini cha somo hili, kwasababu hatutakichambua chote).
Utakumbuka, Boazi alikuwa ni shemeji wa yule mwanamke mjane aliyeitwa Naomi. Biblia inasema Boazi alikuwa ni tajiri sana, na mkuu katika mji ule. Lakini huyu Naomi alikuwa pia na mkwe wake aliyeitwa Ruthu.
Ruthu naye alikuwa mjane, kwani alifiwa na mume wake kabla hajapata mtoto. Hivyo wote wawili walikuwa ni wajane yaani Naomi na Ruthu, isipokuwa Ruthu alikuwa bado ni kijana aliyekidhi vigezo vya kuoelewa tena, lakini Naomi alikuwa ameshakuwa mkongwe hawezi kuolewa tena.
Lakini siku moja Naomi, akaona si vema mkwe wake Ruthu abakie kama yeye. Akaanda mazingira ya kumpatia mkwe wake mume mwingine, ndipo akachunguza na kuona kuwa Boazi ndiye amfaaye. Hivyo akaunda mpango aliokuwa na uzoefu nao, akamfundisha Ruthu namna ya kumwingia, na kwa kupitia njia ile basi Ruthu atapata kibali, kwa mtu huyu tajiri na mkuu wa mahali pale.
Embu tuutazame mpango wenyewe, tunaousoma katika ile sura ya 3, kisha tuone kanuni na sisi ya kukubaliwa na Kristo.
Ruthu 3:1 “Kisha Naomi akamwambia mkwewe, Je! Mwanangu, si vizuri nikutafutie raha, ili upate mema? 2 Basi na huyu Boazi, je! Siye wa mbari yetu, ambaye ulikuwapo pamoja na wasichana wake? Tazama, usiku wa leo atakuwa akipepeta shayiri pale ugani.
3 Basi wewe oga, ujipake mafuta ujivike mavazi yako, kisha uende kwenye uga; walakini usijionyeshe kwake mtu yule, ila atakapokwisha kula na kunywa.
4 Nayo itakuwa wakati atakapolala, utapaangalia mahali alalapo, nawe uingie, uifunue miguu yake ujilaze hapo; na yeye atakuambia utakalofanya.
5 Akamwambia, Hayo yote unenayo mimi nitayafanya.
6 Basi akashuka mpaka ugani; akafanya yote kama vile mkwewe alivyomwagiza”
Ukichunguza hapo utaona, Ruthu anapewa hatua tano za kupitia.
Naomi alijua uchafu, haupatani na bibi-arusi yoyote. Hakuna mume anayependa mwanamke mchafu, ni sharti awe msafi tena kwelikweli. Ndipo hapo sasa utaona akamwambia Ruthu akaoge kwanza awe safi. Ikifunua kuwa mkristo yoyote kabla ya kukubaliwa na Kristo, ni sharti kwanza awe safi kwa maji, yaani Ubatizo, ambao unaleta ondoleo la dhambi zake. Kama hujabatizwa, ni sharti ubatizwe katika maji ya kuzama, na kwa jina la Yesu Kristo, ili dhambi zako ziondolewe, Ndipo ukidhi hatua ya pili ya kumkaribia Kristo.
Kuoga tu peke yake haikutosha aliambiwa pia ajipake mafuta, Ikifunua kuwa Mkristo yoyote ni lazima awe na mafuta rohoni mwake. Na mafuta hayo ni Roho Mtakatifu. Ukikosa Roho Mtakatifu kamwe huwezi kukubaliwa na Kristo.
Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”
Ruthu alikuwa na mavazi yake ya kawaida, lakini hapa Naomi anampa shauri avae mavazi mengine yanayofanana na ya bibi-arusi, meupe safi, aonekane tofauti na wanawake wengine, apendeze, avutie machoni pa Boazi atakapoenda kujionyesha kwake.
Maana yake ni kuwa kila mkristo lazima awe na vazi la arusi, na vazi lenyewe ni Utakatifu. Kama tunavyosoma katika Ufunuo 19:8.Ukipoteza utakatifu, kamwe Kristo hawezi kukupokea, haijalishi utasema nimeokoka.
Ugani ni mahali wanapopepeta nafaka, Hivyo Boazi alikuwa ni mtu wa kazi, muda wote utamkuta yupo kazini kwake, si mtu aliyekuwa mlegevu, Ukitaka kumpata sharti na wewe pia uingie ugani kwake. Hivyo Ruthu ilimpasa aende vilevile, lakini alipewa maagizo kwamba iwe kwa siri, asijulikane na mtu yoyote yule.
Ikifunua kuwa, pamoja na kwamba, utakuwa umeokoka, huna budi kujishughulisha na kazi ya Bwana. Na wewe pia uwepo shambani mwake, lakini ukiwa na vazi lako la thamani(yaani Utakatifu). Na wakati uwapo huihitaji, kutenda kazi yake kama mtu wa mshahara bali kama mtumwa asiyekuwa na faida, uhakikishe upo kama mtu asiyetambulika na Kristo. Unatumika ndipo baadaye yeye mwenyewe aone vema kujifunua kwako.
Luka 17:5 Mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani.
6 Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.
7 Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng’ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula?
8 Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa?
9 Je! Atampa asante yule mtumwa, kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa? 10 Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya
Na hatua ya mwisho aliyopewa Ruthu na Naomi ni kujilaza miguuni pa Boazi. Maana yake ni kujivika unyenyekevu, Unakubali kulala kwenye miguu yenye mavumbi ya Bwana wako. unathamini cha Bwana ambacho kinadharauliwa, unathamini watu wa Mungu, .. Hapo ndipo pawe makazi yako daima, penye unyenyekevu.
Hivyo baada ya kutimiza, hatua zote hizo 5, yaani kuoga, kujipaka mafuta, kuvaa vazi la bibia-arusi, kudumu ugani na kulala chini ya miguu ya Yesu. Fahamu kuwa Kristo atajidhihirisha kwako, kama Boazi wa Ruthu.
Kumbuka maagizo hayo yote, Ruthu hakujiamulia tu, bali aliyapokea, kwa mkwe wake mzoefu aliyeitwa Naomi. Na sisi Naomi wetu ni Mitume na Manabii, yaani Biblia Takatifu. Tukiipenda, kuyashika yaliyoandikwa mule, basi tutakuwa bibi-arusi wa Kristo kwelikweli. Mtume Paulo aliandika hivi;
2Wakorintho 11:2 “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.
3 Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo”.
Zingatia: Kama wewe si bibi-arusi, huwezi kwenda kwenye Unyakuo. Hizi ni siku za mwisho, wakati wowote Yesu anarudi, Je! umejiandaaje? Utajibu nini siku ile, utakapoulizwa kwanini hukuitii injili? Wakati ni mchache sana tunaishi katika dakika za nyongeza tu, Tengeneza maisha yako sasa, huu sio wakati wa kuhubiriwa injili ya kubembelezwa, ni wewe mwenyewe uone uhalisia utubu. Yesu yupo mlangoni.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
KWANINI UNAPASWA UWE BIBI ARUSI NYAKATI HIZI ZA MAJERUHI?
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:
ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.
INAYOENDELEA SASA NI HUDUMA YA RUTHU.
EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuzidi kuyatafakari maneno ya uzima.
Je! Unahabari kuwa watakaonyakuliwa wameshaanza kuandaliwa? Je! Wewe upo katika hatua ipi?
Biblia inasema zipo hatua ambazo Bwana atatumia kushuka kabla haijaja siku ile yenyewe ya sisi kutwaliwa kwenda mbinguni. Hivyo haitakuwa tendo la kushtukiza kwa wale ambao tayari yameshaingizwa katika hatua hizo.
Angalia ni nini Bwana anasema hapa..
1Wathesalonike 4:16 “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na MWALIKO, na SAUTI YA MALAIKA MKUU, na PARAPANDA YA MUNGU; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. 17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. 18 Basi, farijianeni kwa maneno hayo.”
Tafakari kwa makini hayo maneno, Bwana hasemi atashuka na “Parapanda” nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu. Hapana Bali anasema, ataanza kwanza na MWALIKO, kisha SAUTI YA MALAIKA MKUU na ndipo Parapanda ya Mungu mwisho. Tofauti na sisi tunavyofikiri, kuwa ni parapanda tu ndio tutakaoisikia ndipo tunyakuliwe.
Ndugu, tafsiri ya hayo maandiko ni kuwa huwezi kuisikia parapanda ya Mungu, kama hujaitikia hatua ya mwaliko na hatua ya sauti ya malaika mkuu. Hivyo Embu tukautazame huo mwaliko ni upi na hiyo sauti ya malaika mkuu ni ipi?
Awali ya yote tukumbuke kuwa lengo la kunyakuliwa sisi ni ili kwenda kula karamu ya arusi ya mwanakondoo mbinguni, aliyoiandaa Yesu Kristo kwa ajili yetu, kama alivyosema katika Yohana 14:1-4 na Ufunuo 19:9. Hivyo kama tunavyojua hakuna sherehe yoyote isiyokuwa na mwaliko. Hakuna mtu anayejikuta tu kwenye arusi ya mtu bila kualikwa, hakujawahi kuwa na utaratibu huo. Na ndivyo Yesu naye, kabla ya kutupelekea huko mbinguni alipotuandalia vinono, ni sharti kwanza atualike. Hapo ndipo akatumia mfano mmoja wa Mfalme aliyemfanyia mtoto wake karamu kubwa. Lakini katika kuwaalika watu wake, kukawa na mwitikio tofauti tofauti,
Embu tuisome habari hiyo tupate kuielewa vizuri; (Soma kwa utulivu) kwasababu hapa ndipo palipo na msingi.
Mathayo 22:1 “Yesu akajibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema, 2 Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.
3 Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.
4 Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.
5 Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;
6 nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.
7 Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.
8 Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.
9 Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.
10 Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.
11 Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.
12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.
13 Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
14 Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.
Ukitafakari hapo, utajiuliza, iweje mfalme akualike kwenye sherehe yake halafu usiende?..Ni heri angekuwa mtu wa kawaida, lakini walioalikwa hawakulijali hilo, kwamba yule ni mfalme na sio mtu wa kawaida, hawana budi kuahirisha shughuli zao waende, kwani wamepewa heshima kubwa, lakini kwao mambo yalikuwa tofauti, wakapuuzia na kibaya zaidi wakawapiga na kuwaua baadhi ya watumwa wake.
Sasa hawa wanalinganishwa na wayahudi, ambao ndio waliokuwa wa kwanza kupewa mwaliko huu ya injili, lakini waliwaangamiza, manabii wengi wa Mungu, mpaka ikafikia hatua ya Kristo akawakataa kabisa, akawakatilia mbali (Soma Mathayo 23:37-39). Hivyo Mungu akahamishia mpango wake wa wokovu kwa watu wa mataifa, ambao ndio mimi na wewe.
Ambao tunalinganishwa sasa na hao waovu, na vilema, waliookotwa huko mabarabarani wakaalikwa kwenye karamu. Maandiko yanatuambia kundi hilo halikukataa mwaliko kama lile la kwanza. Bali lilikubali lote, Lakini sasa ndani ya ukumbi, akaonekana mmoja ambaye alikuwa tofauti na wenzake, yeye hakuwa na “vazi la arusi”. Utajiuliza ni kwanini akose vazi lile? Ni kwanini asifanane na wenzake? Utagundua kuna jambo alilipuuzia, ambalo angepaswa alifanye kabla ili akidhi vigezo vya yeye kuila karamu.
Sasa kabla hatujatazama vazi hilo ni nini? Maana ya mfano huo ni mwaliko wa wokovu ambao tunahubiriwa sisi sote. Ukweli ni kwamba leo hii lipo japo kubwa la watu katika kanisa “wanaokiri wokovu”, wengi wao wamebatizwa, wanashiriki ibada kama kawaida kanisani, wanatoa zaka, wote wanakiri kuwa wanamsubiria Yesu aje kuwanyakua. Lakini je! Ni wote watakaonyakuliwa? La! Bwana anasema..Siku ile Mmoja atanyakuliwa mmoja ataachwa!(Mathayo 24:40-41) .. Maana yake ni kwamba hupaswi kuridhika tu kuitwa mkristo, lipo jambo la ziada unapaswa ufanye ili ukidhi vigezo vya kuiila karamu ya mwanakondoo mbinguni. Usiridhike tu kusema mimi ni mshirika, mimi ni muumini, acha kabisa hayo mawazo, katika siku hizi za mwisho tunazoishi, yule mtu aliketi kabisa ukumbini, akaona vinono vyote lakini hakula hata kimoja..Sasa embu tuitazame hatua ya pili,
Bwana anasema atashuka na..”Sauti ya malaika mkuu”. Maana yake ni kwamba kabla ya kuisikia parapanda, ni sharti uisikie hii sauti ya malaika mkuu. Tukirudi katika hiyo habari, ni kwamba yule mtu ambaye hakuwa na mavazi ya arusi, hakuisikia/aliipuzia sauti ya mjumbe aliyesimama pale mlangoni kuwapa maelekezo ya namna ya kukubaliwa katika karamu. Wakati wenzake wanamsikiliza, walipoambiwa wakaoge, wabadili mavazi yao ya kihuni, ya ki-utupu, ya ki-zinzi, ya ki-dunia. Wavae mavazi meupe ya sherehe, yeye akaona ule ni mzigo mzito sana, anamnyima uhuru wake, akataka kwenda kipekee pekee na staili zake, maadamu ameshapewa heshima ya kualikwa na mfalme. Hawezi kuzuiliwa. Hivyo akaendelea kustarehe vilevile pale ukumbini, akimsubiria mfalme, kuja kuwapongeza wageni wake waliomtii. Lakini alipofika kwake, akidhani, sasa ni wakati wa kupongezwa, akashangaa amebadilikiwa uso, badala ya kupongezwa, ndio kwanza anafungwa Kamba kama vile vibaka, kisha anatupwa nje!
Unajua ni kwanini mpaka biblia inasema ndipo kutakuwa na kilio na kusaga meno, maana yake ni kuwa huyu mtu ambaye alikuwa ameshaweka mawazo yake katika kusheherekea, ghafla anajikuta yupo nje, ni wazi kuwa yeye ndio atakayeumia Zaidi kuliko wale ambao hawakuwahi kualikwa kabisa.
Hivyo kundi hili linafananishwa na watu wote, wanaoitwa wakristo walio kanisani, lakini hawana mavazi ya arusi. Na vazi la Arusi ni UTAKATIFU. Maandiko yanasema hivyo.
Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.
8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni MATENDO YA HAKI YA WATAKATIFU.
9 Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu.
Ndio maana malaika wa kanisani letu la Mwisho lijulikanalo kama Laodikia. Alipewa ujumbe, unaotuhusu sisi. Ambao hautaki tuwe vuguvugu. Kwasababu tukiwa vuguvugu tutatapikwa. Kumbuka kila kipindi cha Kanisa kilikuwa na malaika wake, mtoa ujumbe, na huyo malaika, alisema kigezo cha kila mmojawao kukubaliwa na Kristo. Tangu kanisa la kwanza, hadi sasa tupo kanisa la mwisho la saba, lijulikanalo kama Laodikia.
Huyo ndio malaika wetu mkuu, ambaye kaachiliwa kutushushia ujumbe huo, hatuna budi kuisikia sauti yake. Kwamba tuwe moto tusiwe vuguvugu, vilevile tununue mavazi meupe, kwa Kristo. Yaani tuishi maisha matakatifu wasiokuwa na madoa, ili tukidhi vigezo vya kunyakuliwa kwasababu tukikosa maisha hayo, kamwe tusijidanganye sisi ni wakristo.
Tuusome ujumbe wetu;
Ufunuo 3:14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.
15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, NA MAVAZI MEUPE UPATE KUVAA, AIBU YA UCHI WAKO ISIONEKANE, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.
22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”
Hivyo wewe kama mkristo, Epuka maisha ya uvuguvugu. Sababu ya wale wanawali watano wapumbavu kutoingia karamuni, ilikuwa ni hiyo hiyo ya uvuguvugu, hawana mafuta ya kutosha kuziwasha taa zao (Mathayo 25). Mungu anajua tabia ya kanisa la sasa, halipendi kukemewa dhambi linapenda mwonekano wa nje tu, lakini ndani ya uchafu. Bwana atusaidie roho hii isituvae.
Sasa ukishakidhi vigezo hivyo, maana yake unakuwa umepita kigezo cha “walioitwa” mpaka kuwa “mteule”. Unachongoja wewe ni unyakuo tu, parapanda itakapolia, utapaa mawinguni, na hata ukifa kabla Yesu hajarudi, utafufuliwa siku ile, kwasababu ulitii mwaliko na Sauti ya Malaika wako mkuu.
Lakini ukifa katika ukristo vuguvugu, kisha ukafa leo, siku ile ya unyakuo hutafufuliwa na watakatifu wengine, utaendelea kubaki makaburini mpaka siku ya hukumu. Ndugu, unasubiri nini, usiokoke? Na ikiwa umeokoka, maisha ya uvuguvugu utaendelea nayo mpaka lini? Leo upo kanisani, kesho disco, leo unamsifu Mungu, kesho unasikiliza nyimbo za kidunia, leo unatoa sadaka, kesho unakula rushwa, hayo maisha yatakufikisha wapi? Hujui kuwa tunaishi katika kizazi ambacho yamkini kinaweza shuhudia tukio la Unyakuo, kutokana na kutimia kwa dalili zote za siku za mwisho?
Embu tubu sasa umaanishe kumfuata Yesu, mambo aliyotuandalia Yesu ni mazuri yasiyoelekeza, mambo ambayo jicho haliwahi kuona wala sikio kusikia. Tusiyakose hayo. Kosa kila kitu, Usikose Unyakuo. Ikiwa upo tayari kutubu leo dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha.
Wasiliana nasi kwa namba hizi bure +255693036618/ +255789001312, tukupe mwongozo wa sala ya toba.. Fanya uamuzi wa haraka sasa, kwani kesho si yao.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)
Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza
Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu.
Warumi 6:8 “Lakini tukiwa TULIKUFA PAMOJA NA KRISTO, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye”
Kabla ya kujitathmini kama kweli tulikufa pamoja na Kristo hebu kwanza tukitafakari kifo cha Bwana Yesu.
Tunasoma kifo cha Mwokozi wetu hakikuwa cha ugonjwa, au cha uzee, au cha ajali… bali kilikuwa ni kifo cha mateso, Bwana Yesu alibeba msalaba wake mpaka Golgotha, na pale akatundikwa msalabani kwa dhihaka nyingi na maumivu makali na kwa masaa mengi.
Lakini pamoja na hayo alisema kuwa “mtu yeyote akitaka kumfuata, ajikane mwenyewe ajitwike msalaba wake ndipo amfuate..
Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate”.
Nataka tutafakari kwa undani mambo hayo matatu (3), kujikana, kubeba msalaba na kumfuata Yesu…
1. Ajikane mwenyewe.
Maana ya kujikana, ni kukataa mapenzi yako na kujiachilia kwa mapenzi ya mwingine, hivyo Kristo anataka mtu yeyote anayetaka kumfuata ni lazima ayaache yale anayoyapenda na kuyafuata yale yeye (Kristo) anayoyapenda.
2. Ajitwike Msalaba wake.
Kujitwika msalaba maana yake ni kubeba kitu ambacho utakwenda Kuteswa nacho. Kristo alibeba msalaba wake na akaenda kusulubiwa juu ya huo, na ndivyo sisi nasi tunapaswa tubebe misalaba yetu..
3. Anifuate
Amfuate wapi?…amfuate kila mahali atakapokwenda… na mwisho wa safari ya Yesu ni Golgotha, katika Kifo!….na kifo cha Bwana Yesu kilikuwa juu ya ule msalaba alioubeba, na si juu ya kitu kingine chochote, vile vile na sisi tunaposema tumekufa pamoja na Kristo ni lazima kifo chetu kiwe juu ya misalaba yetu tuliyoibeba na si juu ya kitu kingine chochote.
Je umeubeba msalaba wako?
Kama hukuubeba msalaba wako utasemaje basi ulikufa pamoja Kristo?.. Kama hujajikana nafsi utasemaje kuwa umekufa pamoja na Kristo?, Kama mapenzi ya baba yako yana nguvu kuliko mapenzi ya Mungu utasemaje ulikufa pamoja na Kristo?.. Kama unamwogopa mama yako kuliko kumwogopa Mungu utasemaje ulikufa pamoja na Kristo?… Kama kazi yako ina nguvu kuliko ibada za Kristo utasemaje ulikufa pamoja na Kristo?, kama kumkiri Kristo tu mbele ya watu ni ngumu utasemaje ulikufa pamoja naye?, kama maisha yako yamejaa uchafu wa kila aina utasemaje basi ulikkufa pamoja na Kristo?.. Wengi wamekufa pamoja na Yuda katika roho lakini si pamoja na Kristo, waliokufa pamoja na Kristo ni watu waliobeba misalaba yao..
Luka 14:25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,
26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
27 MTU YE YOTE ASIYEUCHUKUA MSALABA WAKE NA KUJA NYUMA YANGU, HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU”.
Na wote waliokufa pamoja na Kristo na kuzikwa pamoja naye ndio watakaoishi pamoja naye kama maandiko yanavyosema…
Warumi 6:8 “Lakini tukiwa TULIKUFA PAMOJA NA KRISTO, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye”
Je wewe umekufa pamoja na nani?.. na umekufa juu ya nini?….Ishara ya kufa pamoja na Kristo ni msalaba, je wewe unao huo msalaba katika maisha yako?
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?
BASI MUNGU ALIMWADHIMISHA MNO.
Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?
UTHAMINI WITO WA PILI WA YESU ZAIDI YA ULE WA KWANZA.
Abigaili.
Huu ni mwendelezo wa mafundisho maalumu yahusuyo wanawake.
Na Leo tutaisikia sauti ya Mungu iliyokuwa nyuma maisha ya huyu mama aliyeitwa Abigaili.
Abigaili ni mwanamke aliyeolewa na mwanaume ambaye halikuwa chaguo la Mungu kwake, ijapokuwa mwanaume huyo alikuwa tajiri, hatujui ni nini kilimsukuma Abigaili katika ujana wake kukubali kuolewa na mwanaume yule, labda pengine Nabali hakuanza vile, alikuja kubadilika baadaye, au pengine wazazi wake walimshurutisha aolewe naye kwasababu ya utajiri aliokuwa nao.
Lakini mwanaume huyo halikuwa chaguo sahihi la Abigaili Kutoka Kwa Mungu, kwani Nabali hakuwajali watu wa chini kabisa, Wala hakuwa mtu wa kurudisha fadhila. Utakumbuka wakati ambapo Daudi anakimbizwa na Sauli, akiwa kule maporini, alikutana na kundi kubwa la mifugo wa huyu Nabali, hivyo Daudi alichofanya ni kuwapa hifadhi watumwa wake, kuwahakikishia ulinzi, dhidi ya wavamizi wa mifugo ya wachungaji,kwasababu Nabali alikuwa na mifugo mingi sana na kipindi ambacho wanakwenda kuwakata manyoya kondoo wao, waporaji wenye silaha Huwa wanawavamia sana wafugaji..hivyo walidumu na Daudi Kwa muda wote huo mpaka walipomaliza shughuli zao.
Lakini siku moja Daudi alipungukiwa chakula yeye na jeshi lake hivyo wakaona mtu wa karibu atakayeweza kuwasaidia ni huyu Nabali. Ndipo Daudi akatuma wajumbe kwake kumuomba chochote alichonacho awasaidie.Lakini badala ya kupokea fadhili akapokea matusi. Ndipo Daudi akakasirika sana akataka kwenda kumuua Lakini mke wake alipopata habari akafanya kinyume chake akaaanda vyakula na kumpelekea Daudi, ndipo hasira yake ikageuka.
Embu tukisome kisa hichi Kwa ufupi;
1 Samweli 25:9-38
[9]Basi walipofika vijana wake Daudi, wakamwambia Nabali sawasawa na maneno hayo yote kwa jina la Daudi, kisha wakanyamaza.
[10]Naye Nabali akawajibu wale watumishi wa Daudi, akasema, Huyu Daudi ni nani? Na mwana wa Yese ni nani? Siku hizi kuna watumwa wengi wanaomtoroka kila mtu bwana wake!
[11]Basi mimi je! Nitwae mkate wangu, na maji yangu, na machinjo yangu niliyowachinjia hao watu wangu wakatao manyoya kondoo zangu, na kuwapa watu ambao siwajui wametoka wapi?
[12]Basi vijana wake Daudi wakageuka, wakaenda zao, wakarudi, nao wakaja wakamwambia sawasawa na maneno hayo yote.
[13]Kisha Daudi akawaambia watu wake, Haya! Jifungeni kila mtu upanga wake. Nao wakajifunga kila mtu upanga wake; Daudi naye akajifunga upanga wake; nao wakapanda nyuma yake Daudi, wapata kama watu mia nne; na watu mia mbili wakakaa na vyombo vyao.
[14]Lakini kijana mmojawapo alimpasha habari Abigaili, mkewe Nabali, kasema, Tazama, Daudi alituma wajumbe kutoka nyikani waje ili kumsalimu bwana wetu, naye akawatukana.
[15]Walakini watu hawa walitutendea mema sana, wala hatukupata dhara, wala sisi hatukupotewa na kitu cho chote, wakati wote tulipofuatana nao, tulipokuwako mavueni;
[16]watu hao walikuwa boma kwetu usiku na mchana, wakati wote tulipokuwa nao tukiwachunga kondoo.
[17]Basi sasa ujue na kufikiri utakayotenda; kwa sababu yamekusudiwa mabaya juu ya bwana wetu, na juu ya nyumba yake yote; kwa kuwa yeye ni mtu asiyefaa kabisa, hata mtu hawezi kusema naye.
[18]Ndipo Abigaili akafanya haraka, akatwaa mikate mia mbili, na viriba viwili vya divai, na kondoo watano waliofanyizwa tayari, na vipimo vitano vya bisi, na vishada mia vya zabibu, na mikate ya tini mia mbili; akavipakia vitu hivi juu ya punda.
[19]Akawaambia vijana wake, Haya! Tangulieni mbele yangu; angalieni, mimi nawafuata. Ila hakumwambia mumewe, Nabali.
[20]Ikawa, alipokuwa amepanda punda wake, na kutelemka penye sitara ya mlima, tazama, Daudi na watu wake walikuwa wakishuka kumkabili; naye akawakuta.
[21]Basi Daudi alikuwa amesema, Hakika ni bure nilivyokuwa nikilinda nyikani yote aliyo nayo mtu huyu, asipotewe na kitu cho chote cha mali yake yote; naye amenilipa mabaya badala ya mema.
[22]Mungu naye awafanyie hivyo adui za Daudi, na kuzidi, nikimwachia katika wote walio wake hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.
[23]Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.
[24]Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.
[25]Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.
[26]Basi sasa, bwana wangu, aishivyo BWANA, na iishivyo nafsi yako, kwa kuwa BWANA amekuzuia usimwage damu, tena usijilipize kisasi mkono wako mwenyewe, basi sasa adui zako, na hao wamtakiao bwana wangu mabaya, wawe kama Nabali.
[27]Na sasa zawadi hii, mjakazi wako aliyomletea bwana wangu, na wapewe vijana wamfuatao bwana wangu.
[28]Nakuomba ulisamehe kosa lake mjakazi wako, kwa kuwa hakika BWANA atamfanyia bwana wangu nyumba iliyo imara, kwa sababu bwana wangu anavipiga vita vya BWANA; tena uovu hautaonekana ndani yako siku zako zote.
[29]Na hata ijapokuwa binadamu angeinuka akuwinde, na kuitafuta nafsi yako, hiyo nafsi ya bwana wangu itafungwa katika furushi ya uhai pamoja na BWANA, Mungu wako; na nafsi za adui zako ndizo atakazozitupa nje, kama kutoka kati ya teo.
[30]Tena itakuwa, hapo BWANA atakapokuwa amemtendea bwana wangu sawasawa na mema yote aliyoyanena juu yako, na kukutawaza juu ya Israeli;
[31]hili halitakuwa kwazo, wala chukizo la moyoni kwa bwana wangu, ama ya kuwa umemwaga damu bure, ama ya kuwa bwana wangu amejilipiza kisasi mwenyewe; tena hapo BWANA atakapokuwa amemtendea bwana wangu mema, ndipo umkumbuke mjakazi wako.
[32]Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe BWANA, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;
[33]na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.
[34]Kwa kuwa ni kweli, aishivyo BWANA, Mungu wa Israeli, aliyenizuia nisikudhuru, kwamba hungefanya haraka kuja kunilaki, hakika huyu Nabali asingaliachiwa hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.
[35]Basi Daudi akapokea mkononi mwake vitu vile alivyomletea; akamwambia, Haya! Kwea kwa amani kwenda nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako, nami nimeukubali uso wako.
[36]Kisha Abigaili alimjia Nabali; na tazama, alikuwa amefanya karamu nyumbani mwake, kama karamu ya kifalme; na moyo wake huyo Nabali ukafurahiwa ndani yake, kwa maana amelewa kabisa. Kwa sababu hiyo hakumwambia neno, dogo wala kubwa, hata kulipopambazuka.
[37]Ikawa asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, mkewe alimwambia mambo hayo, na moyo wake ukafa ndani yake, akawa kama jiwe.
[38]Tena ikawa, yapata siku kumi baadaye, BWANA alimpiga huyo Nabali, hata akafa.
Kundi kubwa la wanawake wengi wa sasa wanaotaka kuolewa kigezo wanachokitazama Kwa wanaume ni Mali, wanasahau kuwa hata shetani hutoa Mali. Nabali alimsumbua sana Abigaili katika maisha yake ya ukamilifu, na kama asingekuwa na bidii katika busara yake angeshauliwa mbali na Daudi pamoja na Mali zao. Kufunua kuwa Kristo kama mfalme wetu, Huwa anaziadhibu familia Kwa makosa ya wanandoa wasiowajibika kiroho. Haijalishi wingi wa Mali walizonazo. Wewe kama mwanamke unayekaribia kuolewa kumbuka mwanaume anayemcha Mungu ndio chaguo sahihi kwako, na si vinginevyo.
Wanawake wengi wapo kwenye ndoa, lakini baadaye sana ndio wanakuja kugundua kuwa waume walionao hawakuwa Kutoka Kwa Bwana. Wengine ni wazinzi, wengine ni walevi kama Nabali, wengine hawajali kazi za Mungu Wala Roho zao wenyewe, wengine majambazi, wengine wanawatesa n.k.
Lakini utaona busara ya Abigaili haikuwa kwenda kutafuta mwanaume mwingine aolewe naye, kisa mume wake ni mpumbavu, ila aliendelea kudumu katika haki na ukamilifu, aliendelea kumwombea rehema mume wake hata Kwa maadui zake. Ijapokuwa alikuwa mjinga, lakini hakujaribu kujitenga na mumewe, alimwachia Mungu amfanyie wepesi. Na tunaona Mungu mwenyewe ndio alikuja kushughulika na Nabali akamuua, Kisha Abigaili akawa mke wa Mfalme Daudi. Pumziko la ndoa yake likaja.
Hata sasa wewe kama mwanamke ambaye upo katika ndoa chungu. Huitaji kuizira ndoa hiyo, badala yake omba rehema, na wokovu Kwa mume wako kwa Yesu. Naye ataugeuza moyo wake. Bwana hatatumia njia ya kumuua, lakini ataua uovu na ubaya ulio ndani yake. Na atakuwa tu mume Bora, lakini usichoke kuomba ukasema nimeomba sana sijaona mabadiliko.yoyote… wewe endelea kuomba hata kama itapita miaka 20, ujue Mungu anaona na kusikia maombi Yako tu, atatenda jambo. Huyo atakuwa mume Bora zaidi ya unavyodhani, usipozimia moyo.Hivyo iga busara ya Abigaili.
Anza sasa kuijenga ndoa Yako. Bwana akubariki.
Shalom.
Je! Umeokoka? Je unafahamu kuwa hizi ni nyakati za mwisho na Mlango wa neema unakaribia kufungwa? Unasubiri nini usiokoke? Itakufaidia nini uupate ulimwengu wote halafu upate hasara ya nafsi Yako? Ikiwa upo tayari kumkabidhi Leo Bwana Yesu maisha Yako. Basi wasiliana nasi Kwa namba zetu hizi Kwa ajili ya mwongozo huo Bure.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
NI KITU GANI TUNAJIFUNZA KWA RISPA, BINTI AYA?
Je! kuna mwanamke mwingine aliyempaka Bwana marhamu (manukato) zaidi ya Mariamu ndugu yake Lazaro?
Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo
Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)
SWALI: Kwanini wayahudi walimwambia Yesu kuwa hawajawahi kuwa watumwa wa mtu yeyote angali tunajua kuwa walishawahi kuwa watumwa kule Misri kwa miaka 400?
JIBU: Tusome;
Yohana 8:31 “Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; 32 tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru. 33 Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru? 34 Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi. 35 Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote. 36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”.
Kauli ya hawa wayahudi haikuwa kauli ya kweli bali ya uongo uliowazi, Na lengo la majibu yao halikuwa kutafakari Yesu anayoyasema bali kumpinga tu, Na ndio maana hawakuona shida kuzungumza uongo wa wazi, kwani vitabu vyao vinaeleza walishawahi kuwa watumwa Misri,Babeli, Ashuru na sehemu kadha wa kadha walishawahi kutumikishwa na mataifa hata wakiwa katika taifa lao wenyewe.
Lakini Yesu hakulenga utumwa wa mwilini kama wao walivyodhani, bali ule wa rohoni, wa dhambi, yaani tamaa, wivu, uongo, mawazo mabaya, hasira n.k. Mambo ambayo walikuwa hawana.Lakini kwasababu lengo lao lilikuwa ni kumpinga waliendelea bado kusema uongo hata juu yake..Kwamfano ukisoma vifungu vinavyofuata katika mazungumzo yao, ule mstari wa 48 utaona wanasema kwamba yeye ni msamaria tena ana pepo. Jambo ambalo ni uongo mwingine wa makusudi. Kwani Walijua kabisa Yesu ni myahudi, na wazazi wake Yusufu, na ndugu zake wote wapo nao, mpaka kazi yao ya useremala waliyoifanya waliijua, tena wakamwita Rabi sehemu nyingine, lakini kwasababu wapo kibishi wakazusha uongo na kusema yeye ni msamaria, tena mwenye pepo.
Na ndio maana Bwana Yesu katika mazungumzo hayo hayo (Mstari wa 44) akawaeleza wazi kuwa wao ni wa Baba yao ibilisi kwasababu “hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo ”. kwasababu ya uongo wao.
Hii ni kutufundisha nini?
Tuipende kweli, Kwasababu tusipolipenda Neno la Mungu, shetani atatutumia kulipinga Neno hilo hilo kwa kushuhudia habari za uongo uliowazi na wala hututaona shida, kama ilivyokuwa kwa wayahudi hawa.
Je! Umeokoka, je! Unahakika wa maisha yako ya milele baada ya kifo? Je! Unatambua kuwa hizi ni siku za mwisho, na roho ya mpinga-Kristo inatenda kazi ndani ya watu ambao hawajaokolewa leo? Unasubiri nini usimgeukie muumba wako, tamaa za dunia zitakufikisha wapi?umefungwa Rohoni upo chini ya Utumwa wa dhambi, anayeweza kukuweka huru ni Yesu tu peke yake. Ikiwa upo tayari kuokoka leo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618 / +255789001312, kwa ajili ya mwongozo huo bure.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.(
JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.
Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)
Tunaona kuna baadhi ya watu ambao majina yao yameongezwa vionjo kwa mbele, kwa mfano Simoni Petro, Yuda Iskariote, Tomaso pacha, Simoni mkananayo, Yohana Mbatizaji n.k
Watu hawa ambao majina yao yanaonekana kuongezewa vionjo mbele yake ni kwa lengo la kuwatofautisha na watu wengine wenye majina kama ya kwao. Na vionjo hivyo vilivyokuwa vinawekwa ni aidha kulingana na mahali (miji) wanayotokea, au majina ya wazazi wao, au matendo/huduma wanazozifanya.
Wafuatao ni baadhi ya majina ya watu yaliyoongezewa vionjo kulingana na Matendo waliyokuwa wanayafanya;
Kulingana na Mahali walipotokea;
Kwahiyo ili kumtofautisha na Simoni Petro au Simoni mwingine yeyote, ndipo huyu akaitwa Simoni Mkananayo au Simoni Zelote.
Kulingana na majina ya Wazazi/ Ndugu
1 .Yakobo wa Alfayo: Yakobo alikuwa ni mtoto wa Mtu aliyeitwa Alfayo, Aliitwa hivyo ili kumtofautisha na akina Yakobo wana wa Zebdayo na wengine waliokuwepo kwa wakati huo.(Marko 3:18).
2. Yuda mwana wa Yakobo: Huyu alikuwa ni mwanafunzi wa Bwana Yesu ambaye pia aliitwa kwa jina lingine “Thadayo”(Marko 3:18). Ili kumtofautisha na Yuda aliyemsaliti Bwana Yesu, ndipo kwa jina lingine akajulikana hivyo kama Yuda wa Yakobo au Thadayo.
3. Tomaso aitwaye Pacha (Yohana 20:2)– Ni kuonyesha Tomaso kuwa alikuwa na Pacha lakini hakutajwa katika maandiko huyo pacha wake alikuwa ni nani, ila aliitwa hivyo ili kumtofautisha na wakina Tomaso wengine waliokuwepo pale.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Je jina lako ni nani? Na linabeba ujumbe gani?… >>JINA LAKO NI LA NANI?
Maran atha
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?
MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.
Kwanini mtu afanye miujiza na bado asiende mbinguni?
Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuyatafakari maneno ya uzima.
Tukimtafakari Yesu, jinsi alivyopendwa na Mungu kiasi cha kukabidhiwa vyote na Baba, jinsi alivyojaliwa kutenda miujiza mikubwa ambayo hata vitabu vyote duniani vingeandika habari zake visingetosha kueleza biblia inasema hivyo, tunatamani sana kuwa kama yeye. Yesu ni mtu pekee ambaye alikuwa akimwomba Mungu kitu chochote anapewa saa hiyo hiyo, Lakini mwisho wa siku anakuja kutoa siri ya kukubaliwa kwake..Siri ambazo anasema manabii wengi na wafalme walitamani kuyafahamu hayo wasiyafahamu(Luka 24:10). Lakini mimi na wewe tunazifahamu.
Na siri mojawapo ni hii inayohusiana na namna ya kudili na maadui zetu na wale wanaotuudhi. Alisema hivi,
Mathayo 5:44 “lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi”,
Mwanzoni nilipokuwa nasoma huu mstari nilidhani nimeulewa vizuri, lakini baadaye nilikuja kujua kimatendo kuwa nipo mbali sana nao, nilipotafakari matukio ambayo niliudhiwa na watu, Na muda niliotenga kuwaombea hao watu walioniudhi na kunichukia.. Nikagundua kuwa sijawahi kufanya hivyo.
Ni kweli nilisamehe, lakini kusamehe kwangu kuliishia tu katika ‘kusamehe’ na baada ya hapo ikawa ni kujiepusha naye ili asiniudhi tena. Lakini kwa Mungu huo bado sio ukamilifu, Ukamilifu ni kumwombea huyo anayekuudhi.. Na Zaidi sana kumpenda yule ambaye unahisi ni adui kwako.
Bwana wetu Yesu Kristo ni mtu aliweza kuishi kile alichokisema, Vinginevyo angekuwa ni mnafki.. Yeye ni mtu ambaye aliweza kuishi na mmoja wa maadui zake hatari sana. Adui aliyemuuza mbele ya macho yake. Na huyo si mwingine Zaidi ya Yuda. Yesu alimjua tangu mwanzo kuwa ndiye atakayemsaliti, Lakini hakuwahi kumfukuza, hakuwahi kumnenea mabaya, Zaidi sana alimwita RAFIKI, na pale alipokula chakula kizuri alimchagua Yuda kula naye(Yohana 13:18).. Na tunajua Yesu si mnafki, alipomwita Yuda rafiki(Mathayo 26:50), alimaanisha kweli, kwamba yule alikuwa ni rafiki yake tena hata Zaidi ya mitume wengine.
Tengeneza picha Japo Yesu alijua unafiki wake, lakini ndani yake hakukuwa na sababu ya kutomwona kama yeye ni rafiki tu. Aliweza kuishi naye miaka yake yote ya kiutumishi, akamwongezea na neema juu ya kutoa Pepo na kufanya miujiza. Alipopanda kuwaombea wanafunzi wake, alimwombea na Yuda pia, japokuwa alijua kuwa huyo ndiye msaliti wake. Yuda hakuwahi kumrudishia fadhili Yesu wakati wowote, hata kipindi kile yule mwanamke anamwagia marahamu, yeye bado alipinga. Lakini Yesu alimpenda.
Tujiulize na sisi tuliookoka tunaweza kuwa kama mwana wa Mungu Yesu Kristo. Kuishi na maadui zetu tunaojua wanakwenda kutuchinja na Zaidi sana tunawaombea na kuwabariki? Huo ndio ukamilifu ambao Mungu anataka kuuona kwetu.
Hii ndio sababu kwanini Yesu anasema tuwe watu wa namna hiyo na si vinginevyo anasema..
Mathayo 5:45 “ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki”.
Umeona? Kwasababu tabia ya Mungu ndio hiyo, anawarehemu watu wote, wanaomshukuru na wasiomshukuru, hata maadui zake, anawapa chakula. Kwasababu anajua huwenda siku moja watatubu. Hata sisi pia kabla ya kuokolewa, tulikuwa katika dhambi, tulimkosea sana yeye, lakini hakututendea jambo lolote baya, akatusamehe,. Vivyo hivyo anataka na sisi tufanye kwa maadui zetu, na kwa wale wanaotuchukia.
Ikiwa ni mfanyakazi wako anakuudhi, chukuliana naye tu..Hamna namna, mwombee, mbariki, usiwe mwepesi kumfukuza kazi. Ikiwa ni mpendwa mwenzako anakukwaza mara kwa mara, hupaswi kumsamehe tu na kujiepusha naye mbali, bali umwombee, na Zaidi umwite rafiki yako.
Tabia kama hii, haitokani na sisi wanadamu bali na Mungu, kwa nguvu zetu hatutaweza, lakini tukiwa na Neno la Mungu sana mioyoni mwetu, atatusaidia kuidhihirisha tabii yake hii ya kiMungu. Na kama tukifaulu kushinda, Basi tujue ndivyo Baba atakavyotukaribia, na kujifunua kwetu. Kwasababu tunafanya yanayompendeza.
Hivyo, tumwombe Bwana atusaidie, na sisi tuonyeshi bidii katika kudhihirisha jambo hilo, ili tuwe wakamilifu kama yeye alivyomkamilifu.
Tahadhari:
Epuka mahubiri, unayoambiwa walete maadui zako hapa tuwapige kwa moto wa Roho Mtakatifu wafe. Epuka sana, hayo hayakusaidii kitu Zaidi sana yanakuongezea chuki na visasi moyoni mwako. Ambayo ni zao la shetani na sio Roho Mtakatifu. Bali penda ushauri wa Bwana Yesu, kisha uutende hata kama ni mgumu, lakini ndio njia yenyewe ya kumfikia Mungu, hakuna nyingine.. Wapende maadui zako, kisha waombee
Bwana akubariki.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
USIMPELEKEE BWANA MASHITAKA, YA MAADUI ZAKO.
YAFAHAMU MAPENZI KAMILI YA MUNGU KWA MAADUI ZAKO.
BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.
FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.
Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?
Jibu: Iskariote sio jina la mtu fulani, au la mzazi wa Yuda, bali ni jina lenye maana ya “Mtu wa Keriothi/ Kariote”…
Neno Iskariote ni neno la kigiriki lililoungwa na maneno mawili: “Is” ambalo maana yake ni “mwana wa” na la pili ni “Kariote”..likimaanisha mji wa Kariote au Keriothi
Kwahiyo ukiunganisha maneno hayo mawili maana yake ni “Mwana wa Keriothi”
Na Keriothi ni mji uliokuwepo katika Nchi la Moabu, ambayo kwasasa ni maeneo ya nchi ya Jordani.
Na Wamaobu walikuwa ni watu wa mataifa, hawakuwa waIsraeli, kwa urefu kuhusu Taifa hili unaweza kufungua hapa >>> MOABU NI WAPI
Sasa swali ni je! Kwanini Yuda aitwe hivyo, na asiitwe tu Yuda! Kwanini atambulike kama Mwana wa Keriothi(Iskariote)?… kulikuwa na umuhimu gani yeye kutajwa kwa jina hilo?.
Jibu rahisi ni kwamba, alitajwa vile ili kumtofautisha na wakina Yuda wengine, kwasababu kulikuwa na watu wengi wanaoitwa Yuda ambao pia walikuwa wanafuatana na Yesu. Na Kuna mwingine alikuwa mdogo wake Yesu.
Kwa mfano utaona kuna wanafunzi wawili wa Bwana Yesu waliokuwa na majina yanayofanana..wote walikuwa wanaitwa Simoni, sasa ili kuwatofautisha ndio mmoja akajulikana kama Simoni Petro na mwingine Simoni Mkananayo. (Mathayo 10:2-4).
Vile vile kulikuwa na wanawake wengi waliomfuata Bwana walioitwa Mariamu, sasa ili kuwatofautisha hao akina Mariamu, ndipo hapo wengine wakatajwa kulingana na miji waliyotokea mfano Mariamu aliyetolewa pepo saba alijulikana kama Mariamu Magdalene, kufuatia mji aliotokea ujulikanao kama Magdalene. (Luka 8:2).
Na Yuda Iskariote aliitwa hivyo kufiatia mji ambao Baba yake alitokea (Keriothi).
Yohana 6:71 “Alimnena Yuda, mwana wa Simoni Iskariote; maana huyo ndiye atakayemsaliti; naye ni mmojawapo wa wale Thenashara”.
Soma pia Yohana 13:2, na Yohana 13:26, huenda baba yake Yuda alikuwa ni myahudi lakini mwenyeji wa Kerioth pamoja na Yuda mwanae.
Kuhusiana na mji wa Keriothi au Kariote, pitia mistari ifuatayo; Amosi 2:2, Yeremia 48:24, na Yoshua 15:25.
Na sisi Bwana anatujua majina yetu kulingana na tabia zetu.
Kutoka 33:17 “BWANA akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, nami nakujua jina lako”
Mbele za Mungu kila mtu anajulikana kwa tabia yake…fulani mcha Mungu, fulani mwombaji, fulani mkaribishaji, fulani mwizi, fulani mzinzi, fulani msengenyaji.
Bwana atujalie tujulikane kwa majina mazuri na mema mbele zake ili tupate neema.
Kutoka 33:17 “BWANA akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, nami nakujua jina lako”
Maran atha
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.
ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.
Jibu: Kulikuwa na tukio zaidi ya moja la Bwana Yesu kupakwa mafuta…Tukio la kwanza ni hilo tunalolisoma katika injili tatu, (Mathayo 26:6-13 na Marko 14:3-8 na Yohana 12:1-3), ambapo biblia inaonyesha moja kwa moja kuwa ni Mariamu ndugu yake Lazaro, ndiye aliyempaka Bwana Marhamu siku sita kabla ya pasaka.
Tusome,
Yohana 12:1 “Basi, siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alifika Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye Yesu alimfufua katika wafu.
2 Basi wakamwandalia karamu huko; naye Martha akatumikia; na Lazaro alikuwa mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye.
3 Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu”.
Lakini tukirudi katika Injili ya Luka, tunasoma tukio lingine ambalo linakaribia sana kufanana na hili la Bethania, ambapo biblia inasema alitokea mwanamke mmoja mwenye dhambi na kuanguka miguuni pake na kulia huku akimpaka mafuta.
Jibu: Turejee..
Luka 7:36 “Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani.
37 Na tazama, mwanamke MMOJA WA MJI ULE, ALIYEKUWA MWENYE DHAMBI, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu.
38 Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.”
Sasa ni viashiria gani vinatuthibitishia kuwa yale yalikuwa ni matukio mawili tofauti?
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa haya ni matukio mawili tofauti, yaliyotokea kukaribiana na biblia haikumtaja Yule mwanamke wa Galilaya alikuwa ni nani?.. labda huenda alikuwa ni Yule Yule Mariamu alimpaka mara mbili, au ni mwanamke mwingine ambaye biblia haijamtaja jina lake.
Lakini hayo yote si ya muhimu sana kuyajua, (kwamba ni nani, au ni matukio mangapi) lililo la muhimu kulijua ni tendo hilo la kiimani wanawake hawa waliloyoyafanya.. sasa kujua kwa undani Siri iliyokuwepo katika kumpaka Bwana mafuta fungua hapa >>> AKAKIVUNJA KIBWETA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE.
Bwana atubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
SWALI: Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani? Ni mpangalio wake upoje kulingana na mwandishi?
JIBU: Kitabu Cha Zaburi hakikuandikwa na mtu mmoja, Bali ni mjumuisho wa waandishi mbalimbali. Kitabu hiki ndio kilichoandikwa na waandishi wengi kuliko vyote kwenye biblia.
Kiliandikwa katika nyakati mbalimbali Kwa kipindi Cha miaka elfu moja na zaidi..kitabu hiki kimebeba mashahiri, maombolezo, nyimbo na maombi.
Mfalme Daudi ndiye aliyeandika Kwa sehemu kubwa kitabu hichi;
Jumla Zaburi zilizojuliakana kuwa zimeandikwa na Daudi ni 73. Lakini pia zipo nyingine 2 ambazo hazikutajwa moja Kwa moja lakini waandishi wengine katika nyaraka zao walinukuu baadhi ya maneno kwenye Zaburi, na kusema ni ya Daudi.
Ambazo ni Zaburi 2 ambayo sehemu ya maandishi hayo yanatajwa katika Matendo 4:25,
Na Zaburi 95 Waebrania 4:7
Hivyo kudhaniwa kuwa Daudi aliandika Zaburi 75;
Hizi ndio orodha ya hizo Zaburi 73 alizoziandika yeye;
3-9
11-32
34-41
51-65
68-70
86
101
103,
108-110
122
124
131
133
138-145
2. SULEMANI
Mwandishi mwingine ni Sulemani yeye aliandika Zaburi mbili tu..ambazo ni Zaburi 72 na Zaburi 127″
3. ETHANI na HEMANI
Nyingine zimeandikwa na Ethani na Hemani, Hawa ni watu ambao waliokuwa na hekima nyingi mfano wa Mfalme Sulemani, wanatajwa katika vifungu hivi;
1 Wafalme 4:30-31
30 Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri.31 Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka.
Ethani aliandika Zaburi moja tu nayo ni Zaburi 89
Hemani pia aliandika Zaburi moja ambayo ni Zaburi 88
4. MUSA
Mwandishi mwingine alikuwa ni Musa yeye pia aliandika Zaburi 1 ambayo ni ya 90.
5. ASAFU
Zaburi nyingine 12 ziliandikwa na Asafu na familia yake.
Ambazo ni
50, 73-83
6. WANA WA KORA
Wana wa Kora, waliandika Zaburi 11
42, 44-49,84-85, 87-88
7. WASIOTAMBULIKA
Na Zaburi nyingine 48, zilizobakia hazijulikani waandishi wake.
Hivyo Kwa ufupisho ni kwamba Daudi aliandika Zaburi 73, Sulemani 2, Musa 1, Ethani 1, Hemani 1, Asafu 12, Wana wa Kora 11, wasiotambulika ni 48.
Bwana akubariki.
Ikiwa utapenda kupata uchauzi zaidi ya kitabu Cha Zaburi pitia link hii >> https://wingulamashahidi.org/2020/11/27/vitabu-vya-biblia-sehemu-ya-9-kitabu-cha-zaburi/
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.
Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?
NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA
JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.