Title October 2024

Simo ni mtu gani? (Ayubu 17:6).

Swali: Simo ni nini, au ni nani kama tunavyosoma katika Ayubu 17:6.

Jibu: Tusome mistari hiyo mpaka ule wa saba (7).

Ayubu 17:6 “Amenifanya niwe simo kwa watu; Nimekuwa mwenye kuchukiwa kwa wazi. 

7 Jicho langu nalo limekuwa giza kwa sababu ya majonzi, Na via vyangu vyote vimekuwa kama kivuli”

Neno hili “Simo” linasomeka tena katika Ayubu 30:9.

Ayubu 30:9 “Na sasa mimi nimekuwa wimbo wao, Naam, nimekuwa simo kwao

10 Wao hunichukia, na kujitenga nami, Hawaachi kunitemea mate usoni”.

Na maana ya neno hilo (simo) ni “MTU ANAYEDHARAULIKA”

Wakati Ayubu mtumishi wa MUNGU anapitia yale majaribu ya kufiwa na wanawe na kupoteza mali zake zote, na zaidi ya yote kupitia matatizo ya kiafya, ile fahari yake yote iliisha na kusababisha watu wengi kumdharau ikiwemo mke wake, mpaka hatimaye naye kuliona hilo na kusema hayo maneno.

Lakini pamoja na kuwa SIMO mbele ya watu, kwa MUNGU alikuwa LULU kubwa sana, kwani majaribu yale hayakuwa kwasababu ya yeye kumwacha MUNGU bali ni kwasababu ya yeye kumkaribia Mungu zaidi, na wakati ulipofika alipata mara mbili, ya alivyovipoteza na miaka mingi zaidi ya kuishi (Ayubu 42:12-16).

Na sisi tunajifunza mambo hayo hayo, kuwa tujaribiwapo kwaajili ya haki tuna heri…

Lakini tupitiapo majaribu mfano wa yale ya Ayubu tukiwa katika dhambi, tunapaswa tujifikiri mara mbili, kwani huenda ni mapigo na laana kutoka kwa Mungu ili tutubu na si kwa lengo la kuzijaribu imani zetu kama Ayubu.

Ndivyo Neno linavyoma katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 28.

Kumbukumbu la Torati 28:15-16,37-39 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. 

16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. 

37 Nawe utakuwa ushangao, na mithali, na dharau, kati ya mataifa yote huko atakakokuongoza BWANA. 

38 Mbegu nyingi utazichukua nje shambani, lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila. 

39 Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

Kwanini Mungu alimkataa Sauli? (1Samweli 15:23)

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

Rudi Nyumbani

Print this post

MMOJA APANDA, MWINGINE ATIA MAJI.

Huwezi kufanya kazi zote peke yako..

Aliyeunda injini ya gari, alihitaji mwingine mwenye ubobezi katika utengenezaji wa matairi, lakini pia alimhitaji mbobezi wa umeme wa magari, hivyo ili gari lisimame na kuanza kutembea limegharimu mikono na ujuzi wa wataalamu wengi.

Vile vile, mtumishi wa Mungu mmoja hawezi kufanya mambo yote peke yake, kuna wakati wengine watahusika tu.

Katika biblia kuna mahali Filipo alihubiri na kubatiza, lakini lakini Petro na Yohana waliwaombea hao waliobatizwa ili wajazwe Roho Mtakatifu.

Matendo 8:12 ”Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake.

13 Na yeye Simoni mwenyewe aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo; akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa inayotendeka.

14 Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;

15 ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;

16 kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.

17 Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu”

Umeona? mmoja Anabatiza wengine wanaombea ujazo wa Roho Mtakatifu..

Mambo yote yanakamilika namna hiyo katika ushirikiano na umoja wa Roho, na ndivyo kanisa la kwanza lilivyoenenda, hakukuwa na mashindano wala wivu katikati yao, tofauti na leo ambapo kila mtu anajiona bora kuliko mwingine.

Maandiko yanazidi kutuonyesha kuwa hata Paulo, hakupanda na kuwagia yeye, bali matunda yake yalipaliliwa na wengine.

1 Wakorintho 3:6-7 “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.

7 Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye”.

Kama mtumishi wa Mungu, Je unaweza kuruhusu watumishi wengine wawajenge wale uliowatafuta wewe?…

Kumbuka si kila mtumishi ni wa kweli!…wengi ni wa uongo, lakini je inapotokea umehakiki kuwa kweli yule ni mtumishi wa Mungu, je waweza kuruhusu yule uliyemvua wewe ajengwe na mtumishi mwingine kama wewe?.

Kama hilo jambo gumu basi msaada wa haraka kutoka kwa Bwana unahitajika kwasababu ndivyo Mitume walivyofanya na sisi tunapaswa tufuate hivyo vielelezo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAFUNUO YA ROHO.

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

Washami ni watu gani katika biblia?

Rudi Nyumbani

Print this post

Hii ni maana ya Mathayo 6:29 hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya vifungu hivi; 

Mathayo 6:29

[29]nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.


JIBU: Katika habari hiyo Mungu anaeleza jinsi anavyoweza kutujali na kututunza sisi kipekee kwa uweza wake wa ki-Mungu, akifananisha na jinsi anavyoyatunza maua yake ya kondeni ambayo leo yapo kesho yananyauka na kutupa tanuruni.

ndio hapo anasema tusiwe na shaka ya leo tuvae nini,  kama Mungu anayavika vizuri maua hayo ambayo ni kwa muda mfupi tu huchanua baadaye hunyauka, si zaidi sisi tulio na thamani nyingi zaidi ya hivyo vyote?

Tena anasisitizia hata Sulemani katika fahari yake yote, hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya maua hayo.

Kumbuka Sulemani alikuwa ni mtu tajiri sana, mavazi yake yalikuwa ni ya thamani sana, lakini yalitegemea kuchovywa na kurembwa kwa rangi mbalimbali, ambazo hizo baada ya kipindi fulani hupauka au kuchuja.

Lakini maua hayapakwi rangi bali uzuri ule ni rangi yao kwa asili itokayo ndani. hayafifi rangi. Sulemani hakuwahi kuwa na vazi la namna hiyo.

Isitoshe maua nayo licha ya kuwa na mwonekano mzuri lakini pia hutoa harufu yao nzuri ya asili, kitu ambacho hawezi kukiona kwenye vazi la aina yoyote zuri duniani kutoa harufu yake yenyewe, yanategemea kupuliziwa marashi.

Hivyo hiyo ni kutufundisha kuwa Mungu anaweza kutunawirisha na kutupendezesha zaidi ya matarajio yetu, lakini hiyo hutimia kwanza pale tunapojishughulisha  na mambo ya ufalme wake, ndio hayo mengine sasa ya chakula na mavazi atuzidishie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ONA FAHARI JUU YA BWANA.

Nyinyoro ni nini?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi Nyumbani

Print this post

UCHAWI UNA GHARAMA, JIFUNZE KUMTOLEA MUNGU.

(Masomo maalumu yahusuyo faida za matoleo).

Jifunze kutoa sadaka!!, jizoeze kutoa sadaka, jitaabishe kutoa sadaka!!.

Utoaji si agizo la washirika bali hata viongozi (wachungaji, waalimu, wainjilisti na watu wote wanaoujenga mwili wa Kristo), pasipo kujali Umri wala kipato. Hili ni agizo la Bwana YESU lenye baraka na laana nyuma yake (soma Mathayo 25:31-46).

 Sadaka inayotolewa katika misingi ya Neno la Mungu, inafanya mambo makubwa zaidi ya yale tuyajuayo.

Sadaka inayotolewa katika msingi wa Neno la Mungu, inameza sadaka nyingine zilizotolewa na upande wa ibilisi.

Ile fimbo ya Musa ilibidi aitoe na kuitupa, ndipo ilipoweza kumeza zile fimbo nyingine za wachawi wa Farao.

Sasa zile fimbo zilizomezwa, laiti zingeendelea kuwepo zingeleta madhara mengine kwani zilikuwa ni za kichawi, na zilitumika na wachawi kwa shughuli za kichawi.

Sasa ilimgharimu Musa kuitoa fimbo yake kwanza ili imeze zile nyingine. Vile vile iliwagharimu wachawi kutoa fimbo zao za gharama ili wahindane na Musa.

Vile vile kuna mambo mengine yanahitaji tu matoleo yatatuke..(Kasome Waamuzi 20:20-40).

Sasa wale waganga wa Misri walizigharimia zile fimbo zao, hazikutokea tu… huenda walizinunua kwa fedha na kuzifanyia matambiko mengi.

Kitabu cha Matendo ya Mitume kinatuonyesha jinsi waganga wanavyougharimia uganga wao.

Matendo 19:17 “Habari hii ikajulikana na Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawaingia wote, na jina la Bwana Yesu likatukuzwa.

18 Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao.

19 Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu

Hapo anasema gharama ya vile vitabu vya uganga vilivyochomwa ilikuwa ni elfu 50.

Sasa tukisema elfu 50, kwenye vichwa vya wengi inadhaniwa ni shilingi za kitanzania, zinazotosha tu gharama ya nauli kutola mkoa mmoja hadi mwingine..La!.

Kujua thamani halisi ya vipande vya fedha elfu 50…rejea kile kiasi Yuda alichoongwa ili amsaliti Bwana YESU, maandiko yanasema alipewa kiasi cha vipande 30 tu vya fedha na vipande hivyo vilitosha kununulia shamba (ambalo hatujui ni hekari ngapi) lakini tunajua ni hekari nyingi maana zilitumika kama eneo la makaburi..soma Mathayo 27: 3-7.

Sasa piga hesabu kama vipande 30 vya fedha ya Yuda vimenunua shamba, na hapo vitabu vya waganga gharama yake ni vipande vya fedha elfu 50..gawanya hapo uone waganga waliugharimia uganga wao kiasi gani…

Utaona hapo ni zaidi ya mashamba 1,600 na kama shamba moja litauzwa tu kwa gharama ya shilingi za kitanzania milioni moja…basi jumla yake vile vitabu vyote ni zaidi ya BILIONI MOJA.

Kwahiyo wale waganga waligharimia mabilioni kuusimamisha uganga wao!!!…..

Halafu wewe na mimi kuigharimia injili  kidogo tu tunaona tabu!!!!…..Fikiri mara mbili…fikiri mara mbili!!!.

Jenga ufalme wa Mungu, kwani shetani anajenga ufalme wake kwa kasi na gharama.

Bwana atusaidie.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

UCHAWI WA BALAAMU.

Kupiga ramli ni nini katika biblia?

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

UJIO WA BWANA YESU.

Rudi Nyumbani

Print this post

IHUBIRI INJILI, KILA MAHALI KWASABABU AKUZAYE NI MUNGU.

Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe.

Upo umuhimu wa kuhubiri injili mahali popote na katika mazingira yoyote kwasababu ni agizo la Bwana mwenyewe (Mathayo 28:18-20).

Wapo wanaoamini kuwa injili ya mitaani na masokoni hazina faida yoyote kwasababu watu wanakuwa hawapo katika utulivu.

Na pia wapo wanaoamini kuwa injili  za kwenye mikutano au makanisani ndizo zilizo bora kwasababu watu wanakuwa katika utulivu.

Lakini nataka nikuambie Injili zote zina umuhimu, (Za watu walio katika utulivu na utayari wa kusikiliza na za ambao hawako katika utayari)... na Mitume wa Bwana YESU walihubiri zote (katika masinagogi na masokoni).

Matendo 17:17 “Basi katika sinagogi akahojiana na Wayahudi na waliomcha Mungu, na wale waliokutana naye sokoni kila siku”.

Na hata Bwana wetu YESU alifanya hivyo pia..

Luka 8:1 “Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye”

Lakini leo nataka nikupe umuhimu wa injili za mitaani (za watu wasio na utayari wa kusikia).

Kikawaida ni ngumu kumsimamisha mtu barabarani na kumwambia asimame asikilize… Wengi wanakuwa hawana utayari huo.

Lakini anapopita au anapokuwa ameketi na wewe kukaa mbali naye kidogo na kulazimisha asikie kile anachokisema pasipo hata ridhaa yake, kuna vitu vitaingia ndani yake hata kama hataki.

Kwani lile Neno atakalolisikia hata kama ni moja, litakuwa mbegu njema ndani yake ambayo itachupuka kwa wakati wake.

Kwahiyo ni heri kusikia hata hilo moja kuliko kutokusikia kabisa, kwasababu wengine hata kanisani hawaendi kabisa, wengine ni wa imani nyingine, hawajawahi na wala hawana mpango wa kwenda kanisani wala kusogea mahali penye mahubiri….na wengine wanaamini wapo sahihi katika njia zao, hivyo hawahitaji kusikia kingine chochote, wameridhika na kutosheka na wanavyovijua au walivyo navyo.

Hivyo ukisema uwasubiri, au uombe ridhaa ya kuzungumza nao, hawafungui huo mlango!…sasa kundi hili linasaidikaje?…je kwa kuliacha tu?…au kusubiri au kuliombea tu!…

Jibu: Linasaidika kwa kusikia kwa lazima!.

Ezekieli 2:7 “Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana”

Umeona?..ni lazima wasikie kwa lazima…Kwani atakapolisikia lile neno, pengine alishakwisha kusikia mengine kama hayo 99 na hivyo hilo moja lilikuwa limesalia kufikia hatua yake ya kutafakari zaidi na kutubu…na kupitia hilo neno moja basi ataenda kukata shauri la kumpokea Bwana YESU au kuachana na mwenendo anaouendea.

Vile vile huenda hilo la kwako ndilo Neno lake la kwanza kati ya maneno 99 yanayomngojea mbele ili aokoke. Kwahiyo unaposema na kuhubiri, unakuwa umeianza safari nyingine ndani ya maisha yake, ambayo inaweza kukamilika pengine baada ya miezi au miaka baadae…

Tatizo kubwa linalotukumba wahubiri ni kuona mtu hakati shauri pale pale tunapohubiri, pasipo kujua kuwa kazi za Roho Mtakatifu ndani ya mtu hatuwezi kuzitafsiri kwa akili.

Wapo ambao wanaosikia Neno kwa mara ya kwanza, wengine ndio mara ya pili na wengine ni mara yao ya mia na ya kuokoka.

Ni wachache sana, ambao wamepewa Neema wanaweza kukata shauri la uhakika siku ile ile wanapolisikia Neno, huwa wengi wanakuwa ni mashamba yenye magugu mengi, ambao inawachukua muda kutengenezeka, wanahitaji kusikia mara nyingi, ndio maana Bwana Mungu alikuwa anawatuma manabii wake kupiga kelele katika miji na vijiji, mara nyingi sana, kwasababu ya ugumu wa mioyo.

Isaya 58:1 “Piga kelele, usiache, Paza sauti yako kama tarumbeta; Uwahubiri watu wangu kosa lao, Na nyumba ya Yakobo dhambi zao”.

Kazi ya kuhubiri si nyepesi, ni mapambano mengi na uvumilivu mwingi, na endelevu mpaka mmoja atubu, ndio maana maandiko yanasema mmoja anapopatikana basi malaika wanashangilia.

Luka 15:10 “Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye”

Swali ni je! UMEOKOKA???.

Pengine ni wewe ndiye unayeisikia injili muda mrefu na hutaki kubadilika, hutaki kuacha udunia, hutaki kuacha kuvaa suruali mwanamke, hutaki kuacha kuvaa vimini, hutaki kuacha ukahaba na ulevi, na kiburi na usengenyaji na wivu… nataka nikutahadharishe jambo moja kuwa Injili ya kurudia rudia kwako si mfano wa yale matangazo yanayojirudia kwenye redio au Tv, bali ni ushuhuda!.

Mathayo 24:14 “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja”.

Kama umeisikia mara kwa mara na unaendelea kuidharau, utakutana nayo mbele ya kile kiti cha hukumu, na hiyo itakuhukumu, hiyo ni kulingana na biblia.

Warumi 2:16 “katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu”.

Sasa endelea kusitasita na kuwa hivyo ulivyo mpaka ile siku…haya yote unayoyasoma na kuyasikia, utayathibitisha siku ile.

Bwana atusaidie..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

IMANI NI NINI?

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

TUSIWE WAVIVU WA KUSIKIA.

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

Rudi Nyumbani

Print this post

VIGEZO VYA NEEMA YA MUNGU.

Tangu mwanzo mwanadamu alikuwa akijaribu kujiokoa kwa njia yake mwenyewe ikiwemo kuonyesha matendo yake mazuri, na mwenendo wake mkamilifu lakini hakuweza. Pengine aliweza kushinda wizi kikamilifu lakini uongo ukamshinda, aliweza kushinda uzinzi wote, lakini tamaa zikamtawala, aliweza kushinda ibada za sanamu na vinyago, lakini kusamehe kukamshinda. Alipoweza kushinda kimoja, nyuma yake kulikuwa na elfu vinavyo mhukumu.

 

Na hiyo ilimfanya asikidhi vigezo vya kuingia mbinguni, kwasababu watakaoiona mbingu na Mungu ni watakatifu asilimia mia wasio na doa lolote. Ndio maana maandiko yanasema wote wameoza,wamepotoka hakuna amtafutaye Mungu. Bali tunahesabiwa haki bure kwa neema ya Bwana Yesu Kristo.

 

Warumi 3:11  Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu. 12  Wote wamepotoka, wameoza wote pia; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja.

 

Ndio sababu ya Yesu kuja duniani, ili kwa kupitia kumwamini yeye tuipokee hiyo neema ya kuitwa watakatifu, bila kuonyesha kwanza kipimo chochote kwa Mungu. 

Maana yake ni kuwa mimi na wewe tunapomwamini Yesu Kristo, ni moja kwa moja tunaitwa watakatifu, tuliosamehewa dhambi zetu, na kuondolewa pia. 

 

Ikiwa umemwamini leo Yesu Kristo, moja kwa moja Mungu hakuhesabii tena dhambi yoyote kama mkosaji. Ijapokuwa utakuwa hujakamilika bado.  Hii ndio maana ya neema, yaani kukubaliwa kusikostahili. Ilikupasa kwanza uwe na matendo makamilifu asilimia 100 kama Bwana Yesu, ndio uitwe mtakatifu uliyestahili kumwona Mungu. Lakini sasa kwa kuupokea ukombozi wa Yesu Kristo, dhambi zako, zimefuta unaitwa mtakatifu, kabla hata ya ukamilifu wa utakatifu wenyewe kukufikia. Ndio maana sisi tulio ndani ya Kristo hatuna budi kuwa na amani, na furaha wakati wote. Kwasababu ule mzigo mzito wa kujitahidi sisi wenyewe kuingia mbinguni umeondolewa na Yesu Kristo Bwana wetu, kwa kifo chake pale msalabani.

 

 

Lakini sasa, katika nyakati hizi za mwisho suala hili la neema limetafsirika vibaya, kama tu nyakati zile za zamani, na hapo yatupasa  tuwe makini sana. Ni sawa na taifa litangaze neema kwa nchi yake na kusema, sasa huduma zote za maji ni bure, hakuna kulipia bili,matumizi ni kama unavyotaka. halafu uone watu wanatumia fursa hiyo kwenda kufungulia  mabomba yatiririshe maji kwenye mitaro na mabarabarani, kila mahali kuwe ni maji tu,  Bila shaka utasema hawa watu wamerukwa na akili, hawana sifa ya kupewa huduma hiyo tena.

 

Ndivyo ilivyo kwa jambo linaloitwa neema, tusijipojua kanuni zake, tutajikuta badala ya kupokea wokovu, tunapokea maangamizi. Badala ya kukazana kumpendeza Mungu, tunastarehe katika dhambi,  Na ndicho kinachoendelea sasa kwa sehemu kubwa miongoni watu na madhehebu.

 

Yafuatayo ni mambo ambayo ujiepushe nayo kwa nguvu zote, wewe uliyeipokea neema ya Mungu.

 

  1. Kuipokea neema bure,

2 Wakorintho 6:1

[1]Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.

Ukisoma vifungu vichache vya nyuma anasema mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya, ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya.

 

Mtu ambaye hataki geuko, baada ya kusamehewa dhambi zake, huyo ni mtu ambaye ameipokea neema bure, haithamini, ameitwa mtakatifu, halafu hataki kuishi maisha matakatifu, anaendelea na maisha yake yale yale ya kale.. Mtu kama huyo asijidanganye neema hiyo ni batili. Mtu yeyote aliyeokoka  wakati huo huo una wajibu wa kuanza kupiga hatua za mabadiliko, na unapaswa uithamini sana hiyo zaidi ya vyote, kwasababu ni Mungu ndiye akutakasaye baada ya hapo.

 

Lakini pia mtu ambaye amekaa muda mrefu hamzalii Mungu matunda, anahesabika kama aliyeipokea neema ya Mungu bure, na hivyo mwisho wake unakuwa ni kukatwa.

 

Tito 2:11  Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa;12  nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; 

 

Je! Umeitii neema hii inayokufundisha kukataa machafu ya duniani?. Leo yapo madhehebu yanayosema, ukiokoka umekoka milele, kazi yako imeisha, hata usipoonyesha  bidii nyingine yoyote kwa Mungu,huwezi potea. Ndugu yangu kuwa makini sana na imani hizi. Neema haipokelewi bure.

 

  1. Kuipungukia Neema

Epuke pia  kuipungukia neema.

 

Waebrania 12:15-17

[15]mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo. 

[16]Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kimoja. 

[17]Maana mwajua ya kuwa hata alipotaka baadaye kuirithi baraka, alikataliwa (maana hakuona nafasi ya kutubu), ijapokuwa aliitafuta sana kwa machozi.

Kuipungukie neema Ni tabia ya kuishusha thamani neema, na kuilazimisha  itende kazi hata katika kiwango ambacho si chake.

 

Hii hasa huja kwa watu ambao wanazoelea kufanya dhambi mara kwa mara wakiamini kuwa kwasababu Mungu hawahesabii makosa basi hata wakifanya kosa lolote hawawezi kupotea.

Ndugu, neema si kuhalalisha maisha ya dhambi. 

Biblia inasema..

Warumi 6:1  Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? 2  Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi?

3  Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

4  Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

Usitende dhambi za mazoelea, ukadhani neema itakuwa sikuzote kukufunika. Ukiifanyia jeuri neema, itaondoka kwako.

 

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, 6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

 

  1. Kuibadili neema ya Mungu.

 

Yuda 1:4  Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.

 

Neema ya Mungu inaweza badilishwa ikamaanishwa kivingine kabisa. Kwamfano utaona leo hata mashoga, wanavyama vyao wakisema sisi tupo chini ya neema. Walevi nao, wenye dhambi nao wanasema neema ya Yesu ipo duniani sasa, kumwokoa kila mtu.

 

Hivyo watakuambia maneno kama usihukumu usije ukahukumiwa. Na wana amani na ujasiri katika hayo wanayoyafanya na wengine wanajiita maaskofu na wachungaji, wakihalalisha kila kitu kiovu kufanyika kwa kivuli cha neema.

 

Hao ndio waibadilishao neema ya Bwana Yesu kuwa ufisadi, hilo Neno ufisadi ni zaidi ya uasherati, Ni pamoja na matendo yote maovu kupita kiasi. Lakini neema ya Yesu,.haikuja kufunuki dhambi, bali ilikuja kuondoa dhambi ndani ya mtu. Usiwe mmojawapo aibadilishaye neema ya Mungu.

 

Hivyo kwa vifungu hivyo itoshe kusema kuwa NEEMA tunaipokea bure, lakini ili iweze kufanya kazi lazima tujue sifa zake,  kisha tuzikubali, vinginevyo tutajidanganya na kuangamia.  Ni sawa na mtu akupe gari bure, lakini usipoliweka mafuta, na kujua kuliendesha linakuwa halina tofauti na mdoli wa gari.

Lakini ukiithamini neema, itakutunza, itakuhifadhi na kuyaficha makosa yako yote, Hivyo utaendelea kuonekana mkamilifu asilimia mia mbele za Mungu, na hata ukifa, ni moja kwa moja mbinguni.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

Print this post

Neno Siuze linamaanisha nini kwenye biblia?

Siuze ni ‘Sembuse’, kwa uandishi mwingine.

Kwamfano mtu anaposema kauli hii

 “Kama Bwana Yesu alikuwa mwombaji siuze mimi, kuzidi hapo?


.Ni sawa tu  na kusema “Kama Bwana Yesu alikuwa mwombaji sembuse mimi, kuzidi hapo?

Maana ya Neno hilo ni. “Si zaidi

‘Kama Bwana alikuwa mwombaji si zaidi mimi kuzidi hapo’.

Vifuatavyo ni baadhi ya vifungu ambavyo utalisoma neno hili kwenye biblia;

 

2 Mambo ya Nyakati 6:18

[18]Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga! 

 

2 Wakorintho 3:9

[9]Kwa maana ikiwa huduma ya adhabu ina utukufu, siuze huduma ya haki ina utukufu unaozidi. 

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Neno vuruvuru linamaanisha nini katika biblia?

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Kuna Mbingu ngapi?

Rudi Nyumbani

Print this post

IFUATE KANUNI SAHIHI YA MUNGU

Zipo kanuni za ki-Mungu tunaweza kuzifuata na zikaleta matokeo kabisa halisi, lakini zisiwe na manufaa kwetu katika suala la wokovu.  Sasa kabla ya kuangalia ni kwa namna gani? 

chukulia mfano wa kawaida.

Mwanamke yeyote anaweza kubeba ujauzito katika mazingira mbalimbali, kwamfano anaweza akatwezwa nguvu (akabakwa), na akapata ujauzito, lakini pia anaweza kwenda kujiuza kama kahaba na bado akapata ujauzito, vilevile anaweza akasubiri aolewe kwanza katika ndoa halali ndipo apokee ujauzito na likafanikiwa vilevile tu, kuleta kiumbe duniani, kama angefanya hayo kabla ya ndoa, au atokapo nje ya ndoa yake.

Sasa unaweza jiuliza, katika njia zote hizo ambazo angepata ujauzito ni ipi iliyo halali inayokubalika mbele za Mungu na wanadamu. Bila shaka ni hiyo njia ya mwisho ambayo ni ya kuolewa kwanza, ndipo apokee ujauzito kutoka kwa mume wake mmoja wa halali. Na ndio mtoto huyo hujulikana kama halali sio haramu.

Lakini cha ajabu ni kuwa ijapokuwa njia halali ipo lakini feki pia huleta matokeo yaleyale mfano wa halali. Kwasababu gani? Kwasababu kanuni ya kupata mtoto, si kanuni ya uhalali. Hivyo ni vitu viwili tofauti, 

Hata Ibrahimu, alikuwa na watoto wengi, alitangulia Ishmaeli, kisha baadaye wakazaliwa na watoto wengine sita kwa suria mwingine, mbali na Isaka. Wote walikuwa wanadamu, viumbe wa Mungu, wenye akili na nguvu na baraka, wasio na hatia. Lakini lilipokuja suala la urithi, ndipo kubaguliwa  kulipokuja, Watoto wote wa masuria walifukuzwa wakapewa zawadi tu bali Isaka alipewa vyote.

Mwanzo 25:5-6

[5]Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo. 

[6]Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu. 

Hii ni kutufundisha nini hasaa katika maisha yetu ya wokovu.

Zipo kanuni nyingi sana za kiroho ambazo mtu yeyote, hata ambaye  hajamwamini Yesu anaweza zitumia na zikatoa matokeo yaleyale sawa tu na mtu ambaye ameokoka.

Kwamfano, kufanya miujuza na ishara kwa jina la Yesu. Watu hawajui kuwa jambo hili huhitaji imani tu, katika jina lake. Hivyo wale wafikiao kiwango hicho haijalishi ni mwizi, ni mpagani, anaweza pokea muujiza na akafanya pia muujiza sawa tu na yule aliyeokoka.

Kwasababu gani? kwasababu amefanikiwa kufuata kanuni ambayo ni Imani.

Akijua lile neno linalosema  ‘yote yawezekana kwake yeye aaminiye’’ (Marko 9:23). Ndio maana walikuwepo watu wengi wasiokuwa wayahudi kipindi kile cha Yesu walipokea miujiza mikubwa, zaidi ya wayahudi kwasababu tu ya ukubwa wa imani zao. Na sio haki zao.

Vivyo hivyo hata katika kuomba. Mtu yeyote aombaye hupokea. Ni kanuni ya asili ya rohoni, haijalishi ni nani.

Mathayo 7:8

[8]kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. 

Watu hawajui hata kufanikiwa kwa shetani hutegemea maombi, na yeye pia huenda mbele za Mungu kuomba na hupewa..hajiamulii tu mambo yake ovyo ovyo bila idhini ya Mungu, kwasababu hii dunia si yake… utauliza kwa namna gani, ? unamkumbuka shetani kipindi cha Ayubu, yeye naye alikwenda kujihudhurisha mbele za Mungu, ndipo akaleta uharibifu. Akapeka haja zake akasikiwa, dua zake na magoti yake.

Ayubu 1:6

[6]Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao. 

Watu wengi wanapoona wanamwomba Mungu wanajibiwa wanadhani, ndio wamekubaliwa na Mungu. Kumbe unaweza kuomba kama mwana-haramu usiyekuwa na urithi wa uzima wa milele, bali haki ya kupokea tu unachokiomba.

Unaweza ukafanya miujiza kama mwana-haramu. Lakini usiende mbinguni.

Mathayo 7:22-23

[22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 

[23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu. 

 Unaweza ukamwamini Yesu, na kumuhofu,  lakini ukaamini kama mashetani.

Yakobo 2:19

[19]Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka. 

unaweza ukawavuta watu kwa Kristo na wakaokoka, lakini ukawa mtu wa kukataliwa kama tu Paulo alivyosema katika; 

1 Wakorintho 9:27

[27]bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa. 

Sasa kanuni sahihi ya Mungu ni ipi ili tuonekane kamili na halali?

Kanuni Mungu anayoitazama kwetu ni Wokovu uliokamilishwa kwa matendo yake.

Angalia mwishoni pale kwenye Mathayo 7:23 Bwana Yesu alichokisema;

“ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Umeona je unaishi maisha gani?. hicho ndio kipimo cha ki-Mungu, 

Alisema pia.

Yakobo 2:24

[24]Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake. 

Hakikisha maisha yako yanaendana na ukiri wako, wa imani yako, usiishi tu kama mtu ambaye hajaamini ukijitumainisha, kuona maombi yako yanajibiwa, karama yako inafanya kazi, imani yako inatenda kazi..hizo ni kanuni za kupokea lakini sio kanuni za uhalali wa kuurithi uzima wa milele. Ishi kama mtu ampendezaye Bwana wake kimwenendo, ndipo hayo mengine yakifuata huna hasara.

Nyakati hizi za mwisho, adui anaweka uzito kwenye mioyo ya watu wasipende kutafuta maisha matakatifu, kinyume chake wabakie tu kwenye miujiza, uponyaji, utabiri…Siku ile hivyo vitu havitafuata na wewe ndugu, bali matendo yako.

Ufunuo wa Yohana 14:13

[13]Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao. 

Tuanze sasa kujipima mienendo yetu. Kisha tutumie nguvu nyingi hapo kujirekebisha, sawasawa na imani tuliyoipokea, ili tuwe wana halali waliozaliwa kweli ndani ya Kristo, watakaorithi uzima wa milele.

Wokovu wa kweli hufunuliwa kwa mwenendo mzuri. Tuitazame sana kanuni hii.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KANUNI JUU YA KANUNI.

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI AU KUTOA TALAKA?

Print this post

Biblia inasema nini kuhusu mtu ‘Mwenye kujipendekeza (Mithali 29:5)

SWALI: Naomba kufahamu ujumbe ulio katika Mithali 29:5

‘Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake’.

JIBU: Mithali hii inazungumzia madhara yanayoibuka katika tabia ya kujipendekeza.

Kujipendekeza ni kitendo cha mtu kumthaminisha mtu, hata kama alikuwa hastahili sifa hizo, ili tu upate kitu Fulani kutoka kwake. Kumthaminisha kunaweza kuwa kumsifia, au kumpongeza, au kumzungumzia mema yake kupita kiasi, au kueleza mabaya ya wengine kwa huyo mtu, n.k.

 Na yote hayo hayawi kwa lengo la kuuthamini kweli uzuri wa Yule mtu, hapana bali  ni aidha upate kupendwa wewe zaidi ya wengine, au usaidiwe, au upewe cheo,  au kipaumbele Fulani. Hata kama utaona mabaya yake huwezi kumwambia kwasababu, huna lengo la kusaidia bali upate matakwa yako tu.

Sasa  hilo ni kosa, matokeo ya hilo biblia inatuambia “unamtandikia wavu ili kuitega miguu yake”. Yaana unampeleka kwenye mtego au aungamivu wake kabisa.  Hii ni kweli, tunaona hata viongozi wengi wa nchi wameponzwa na wasaidizi wao wa karibu,na matokeo yake wakaiharibu  nchi, kwasababu tu ya kupokea sifa za uongo kutoka kwao, kwamba wanafanya vema, wanawajibiki vizuri n.k..  Kama ilivyokuwa kipindi kile cha Mfalme Sedekia na wale manabii wa uongo wajipendekezao, walimtabiria uongo, lakini Yeremia alimweleza mfalme ukweli  hawakutaka kumsikiliza. Matokeo yake Mfalme Sedekia akaingia katika matatizo makubwa ya kutobolewa macho na kupelekwa utumwani, hiyo yote ni kwasababu alikaa na manabii wajipendekezao (Yeremia 34-41), kama tu ilivyokuwa Kwa Mfalme Ahabu naye na manabii wake mia nne wa uongo.

Hii ni kutufundisha nini?

Hasaa biblia hailengi, tuwe makini na watu wajipendekezao. Hapana, kwasababu wakati mwingine si rahisi kuwatambua, inahitaji neema ya Mungu. Lakini inalenga hasaa katika upande wetu , kwamba sisi tujiepushe na ‘tabia ya kujipendekeza”. Kwasababu tunaweza kudhani tunatafuta faidi yetu tu wenyewe, lakini kumbe tunamsababishia madhara Yule mtu ambaye tunajipendekeza kwake. Tunategea wavu mbaya sana, aanguke na kupotea kabisa, na huo si upendo.

Itakusaidia nini akutendee mema, halafu yeye aangamie?

Hivyo, pastahilipo kweli kusifia tusifie, lakini si kwa lengo la kujipendekeza, kwasababu tukienda huko, tunatenda dhambi kubwa zaidi. Hiyo ndio maana ya hivyo vifungu, tufikiriapo kujipendekeza, tuone kwamba ni watu wasio na hatia tunawategea wavu waangamie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kama ni Mungu ndiye kaumba zao la Bangi kwanini tena iwe dhambi kuitumia??

Swali: Biblia inasema tumepewa mboga za majani kuwa chakula chetu, na Bangi pia ipo miongoni mwa zao la mboga za majani…sasa kwanini iwe dhambi kulitumia kama mboga au kiburudisho cha kusisimua (kuvuta) na ilihali ni Mungu mwenyewe ndio kaumba?


Jibu: Turejee..

Mwanzo 9:3 “Kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa MBOGA ZA MAJANI, kadhalika nawapeni hivi vyote”.

Ni kweli maandiko hayo yanathibitisha ulaji wa mboga, lakini si mboga zote!.. Tukisema kila mboga iliyopo kondeni tumepewa tule, tutakuwa hatujayaelewa vizuri maandiko kwasababu  kuna mboga nyingi sana ambazo sumu!, ambazo zinamwonekano mzuri lakini hazifai kwa chakula… na Mungu hawezi kumpa ruhusa Mtu wake aliyemuumba, ale SUMU!..

Zipo mboga kwaajili ya chakula cha wanadamu, nyingine kwaajili ya wanyama na hazifai kwa wanadamu… vile vile zipo mboga zisizofaa kwa chakula cha wanadamu na wanyama… Mboga hizo zinabaki tu kwa utukufu wa Mungu, au kwaajili ya urembo, mfano wa mboga hizo ni MAUA.

Kuna Maua ambayo yana mwonekano mzuri sana lakini ni SUMU kali sana, mfano wa hayo ni kama haya yanavyoonekana hapa chini.

maua sumu

Hayo ni mfano wa Mboga, lakini si kwaajili ya kula bali kwaajili ya urembo tu.. yameumbwa na Mungu kwa lengo hilo, hivyo mtu akila hayo anaweza kupata madhara makubwa ya kiafya au hata kifo.

Vile vile na Bangi, inaweza kuwepo katika kundi hilo la MAUA, kama itatumika kwa urembo si vibaya, lakini kwa matumizi mengine ya ndani ya mwili wa binadamu ni hatari.

Kwahiyo si kila kilicho halalishwa basi kinafaa kwa matumizi yote.. hapana!.. Mboga zimehalalishwa lakini si kwa matumizi ya chakula tu, ndivyo maandiko yanavyotufundisha..

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.

Kwahiyo ulaji, au uvutaji wa Bangi ni dhambi kibiblia, vile vile matumizi ya tumbaku kula au kuvuta ni dhambi, kwani miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na tena maandiko yanasema mtu akiliharibu hekalu hilo Mungu naye atamharibu mtu huyo (Soma 1Wakoritho 3:16-17 na 1Wakorintho 6:19).

Na Bangi inaharibu ufahamu wa mtu, ambao ndani yake kunazalika hasira, kutokujali, vurugu, matukano, mauaji, uasherati na mambo yote mabaya..

Hivyo Bangi ni haramu, vile vile tumbaku na mazao mengine yaletayo matokeo kama hayo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nyungu ni nini kibiblia?(Ayubu 41:20,31, Waamuzi 6:19)

MTINI, WENYE MAJANI.

JE UNAZAA MATUNDA NA KUWAPONYA MATAIFA?

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Nini maana ya mmoja alikufa kwaajili ya wote hivyo walikufa wote? (2Wakorintho 5:14)?

Rudi Nyumbani

Print this post