Title October 2024

Je YUDA alikuwa ni shetani kulingana na Yohana 6:70?

Swali: Je kwanini Bwana YESU aseme Yuda ni shetani, na kwanini amchague shetani kama mwanafunzi wake?


Jibu: Turejee..

Yohana 6:70 “Yesu akawajibu, Je! Mimi sikuwachagua ninyi Thenashara, NA MMOJA WENU NI SHETANI?

71  Alimnena Yuda, mwana wa Simoni Iskariote; maana huyo ndiye atakayemsaliti; naye ni mmojawapo wa wale Thenashara”.

Swali hili linafanana na lile la kwanini Bwana YESU amwite Herode “MBWEHA”.

Luka 13:31 “Saa ile ile Mafarisayo kadha wa kadha walimwendea, wakamwambia, Toka hapa, uende mahali pengine, kwa sababu Herode anataka kukuua.

32  Akawaambia, Nendeni, mkamwambie yule mbweha, Tazama, leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa, siku ya tatu nakamilika”.

Sasa kiuhalisia Herode sio “Mbweha”, wala Yuda siye “shetani”…Isipokuwa watu hao ndani yao wamebeba tabia za “Mbweha” na “shetani”.. Ni sawa na Bwana YESU anavyojulikana kama Mwanakondoo…haimaanishi Bwana YESU ni kondoo (mnyama), La!, isipokuwa ndani yake (katika roho) ipo tabia ifananayo na ya kondoo yaani ya “unyenyekevu”.

Hali kadhalika Yuda si “shetani” bali ndani yake kulikuwa na roho ya shetani ya usaliti na mauaji.

Luka 22:3 “SHETANI AKAMWINGIA YUDA, AITWAYE ISKARIOTE, naye ni mmoja wa wale Thenashara.

4  Akaondoka, akaenda akasema na wakuu wa makuhani na majemadari, jinsi atakavyoweza kumtia mikononi mwao”.

Hivyo Bwana YESU alikuwa anamaanisha roho iliyokuwemo ndani ya Yuda na si utambulisho wa YUDA, utaona pia kuna wakati alimwambia Petro kuwa ni shetani..

Mathayo 16:22 “Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata. 23  Akageuka, akamwambia Petro, NENDA NYUMA YANGU, SHETANI; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.

Hapa Bwana hakuwa anaongea na Petro, wala hakuwa anamkemea Petro, bali ile roho iliyokuwa ndani ya Petro (yaani ya ibilisi) ndio aliyokuwa anaikemea.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Bwana YESU hakumchagua shetani, wala Yuda hakuwa shetani bali alikuwa na roho ya shetani ndani yake.

Na hata leo kuna watu ambao ni “mashetani” katika muktadha huo, kwamba ndani yao kuna roho ya shetani.. Hivyo hatuna budi kila siku kujipambanua na kujipima na kujitakasa, ili tusiwe tusionekane kama mashetani.. na utakaso mkuu ni ule Bwana aliowaambia baadae wanafunzi wake, baada ya kumkemea Petro.

Mathayo 16:23 “Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.

24  Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.

25  Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona”.

Hapo baada ya maneno hayo kwa Petro, Bwana anaanza kusema “…Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake..”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je Yuda alienda wapi, ni mbinguni au jehanamu?

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

ZIFAHAMU KAZI KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

KUMJUA YESU SI KUPATA UZIMA WA MILELE.

Rudi Nyumbani

Print this post

LAANA NI NINI KIBIBLIA?

Kibiblia  Neno laana linatafsiri kwa namna mbili.

Namna ya kwanza, ni Kupoteza sifa ya kukubaliwa na Mungu kwa jambo lolote lile. Na hii chanzo chake ni lile anguko la mwanadamu tangu mwanzo.

Namna ya pili, ni apizo alitoalo mtu kwa mwenzake au alitoalo Mungu mwenyewe, kwa mwanadamu ili wafikiwe na ubaya fulani, au wakasifikiwe na Mema waliyokusudiwa.

 

LAANA YA KWANZA:

Sasa laana hii ya kwanza, inazalika kwasababu ya  asili yetu, ambayo ilionekana tangu Adamu, kuhasi maagizo ya Mungu, ambayo hata sisi sote tuliopo leo, asili hiyo ipo ndani yetu. Ni sawa na unavyomwona mdudu kama mende, ukimtazama tu tangu akiwa mtoto, utamchukia hata kabla hajaonyesha hali yake ya kupenda uchafu, kwasababu unajua asili hiyo ipo ndani yake. Atakuja kuwa mchafu tu.

 

Ndivyo ilivyo kwetu sisi, tayari Mungu alishaona tangu tunazaliwa tutamwasi tu yeye, mfano wa baba yetu Adamu.

Na ndio maana akaandaa mpango wa kuzaliwa upya mara ya pili, kupitia Yesu Kristo. Hivyo mtu yeyote anayezaliwa mara ya pili, anaondolewa katika laana hiyo ya kukataliwa na Mungu, na anakuwa mwana wa Baraka. Laana hii haiwezi kuondoka bila damu ya Yesu.

 

Hiyo ndio sababu kwanini maandiko yanasema Yesu alifanyika laana kwa ajili yetu. Maana yake, tunapokombolewa na yeye tunafanywa kuwa watu wengine kabisa wenye asili nyingine wasio na laana, wenye kukubaliwa na kupendwa na Mungu.

 

Wagalatia 3:13  Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;

14  ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.

 

Hivyo wewe uliyeokoka, na kupokea Roho Mtakatifu unaitwa, mbarikiwa, unaitwa mungu duniani, mtoto wa Mungu kwelikweli.

LAANA YA PILI

Lakini laana ya pili, kama tulivyoona ipo katika maapizo ambayo huyatoa Mungu au mwanadamu mwenyewe.

a) Tukianzana na zile zinazonenwa na Mungu

Mungu anaweza kukutamkia laana, hata kama utakuwa umekombolewa na yeye. Unaweza kushiriki mabaya. Laana hizi zinaweza kukufanya usipoteze wokovu wako, lakini zikakukosesha mambo mengi sana duniani.

 

Mfano wa hizi ndio zile alizowaambia wana wa Israeli, kwamba watakapoacha sheria zake, basi watatawanywa katika mataifa yote, watakuwa mikia na sio vichwa, nchi itazuliwa Baraka zake, wataondokeshewa adui zao N.k. (Kumbukumbu 28)

 

Mfano pia wa hizi, ndio kama ile aliyoilaani nchi, na nyoka pale Edeni. Akasema itatoa miiba, na nyoka atakwenda kwa tumbo (Mwanzo 3:17). Vilevile ndio ile aliyomwambia Kaini kuwa atakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani (Mwanzo 4:12).

 

Hata sasa wapo wengi wanaokutana na maapizo hayo ya Mungu kwa kufanya dhambi au makosa ya makusudi. Namna ya kueupuka laana hizi ni kutii agizo la Mungu.

Kwasababu unapozizoelea zitakufanya uangukie kabisa kwenye kundi lile la kwanza la kukataliwa kabisa..la watu ambao hawajaokoka.

 

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

7  Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; 8  bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.

 

Kinyume cha laana ni Baraka, unapotii amri za Mungu, umejiwekea mazingira mazuri ya kupokea Baraka.

 

b) Lakini pia zipo laana  zinazonenwa na  mwanadamu.

Hizi nazo zimegawanyika katika makundi mawili.

 

i) Kundi la kwanza ni la watu wa Mungu/wenye haki.

Kwamfano Utakumbuka Hamu alipoona uchi wa baba yake. Nuhu aliulaani uzao wake, Hivyo watu wa Mungu wamepewa mamlaka hiyo, hata sasa, ndio maana Bwana Yesu alisema mtakalolifunga duniani, limefungwa mbinguni, na akatusihi pia tuwe watu wa kubariki kuliko  kulaani. (1Petro 3:9)

Unapokosewa na mwenye dhambi epuka kutoa neno la madhara kwake, kwasababu hakika jambo hilo litampata na kumwangamiza kabisa. Ndicho alichokifanya Elisha kwa wale vijana arobaini na wawili waliomdhihaki.

 

ii) Kundi la pili ni laana zitokazo kwa watu waovu.

 

Husasani wachawi, nao pia huweza kusema jambo likatokea, Utakumbuka kisa cha Balaamu mchawi, alipoajiriwa na Balaki kwenda kuwalaani Israeli wa Mungu, lakini alishindwa akajikuta anawabariki badala ya kuwalaani.

Akasema hakuna uchawi (Hesabu 23:23).

Ikiwa wewe umeokoka, huna haja ya kuogopa laana za hawa, kwasababu haziwezi kukupata, kwasababu unalindwa na nguvu za Mungu, hizi huwa zinawapata watu ambao wapo nje ya Kristo YESU.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NUHU WA SASA.

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

KUVUNJA MAAGANO YA UKOO.

Rudi Nyumbani

Print this post

FAIDA NYINGINE MUHIMU YA KUMTOLEA MUNGU.

(Masomo maalumu yahusuyo Sadaka na Matoleo)

Angalizo: Masomo haya hayana lengo ya kuhimiza matoleo, (Au kuwaweka watu katika mitego ya kutoa) bali yana lengo la kutoa elimu sahihi ya kiMungu juu ya faida za kumtolea Mungu kwa njia yeyote ile.

Na wajibu wa kumtolea Mungu si wa waumini (au washirika tu peke yao) bali wa kila mtu ikiwemo wainjilisti, wachungaji, maaskofu, wazee wa kanisa, mitume, waimba kwaya na wengine wote. Hivyo ni muhimu pia kujifunza mambo haya, ili tupate faida (Isaya 48:17)

2Wakorintho 9:11 “mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, UMPATIAO MUNGU SHUKRANI KWA KAZI YETU.

12 Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali HUZIDI SANA KUWA NA FAIDA KWA SHUKRANI NYINGI APEWAZO MUNGU;”

Nataka uone hilo neno.. “HUZIDI SANA KUWA NA FAIDA”… Maana yake ni kwamba pamoja na faida hiyo iliyotajwa hapo ya “kuwatimizia watakatifu riziki zao”..lakini pia Faida iliyo kubwa kupita yote ni hiyo kwamba “MUNGU ATAPEWA SHUKRANI NYINGI”.

Unawasaidia mayatima, wale mayatima watamshukuru MUNGU SANA KWA KILE WALICHOKIPOKEA… Na ndicho Mungu anachokihitaji sana.. SHUKRANI… shukrani.

Unaweza kuona kama shukrani ni jambo dogo!.. lakini kwa MUNGU ni jambo kubwa…

Mungu anapendezwa na shukrani kuliko maombi mengi tuyapelekayo mbele zake… Unaweza kutumia lisaa limoja kumshukuru tu MUNGU kwa mema yake na ukapata faida kubwa kuliko kupeleka mahitaji orodha ya mahitaji kwa muda huo.. (Shukrani ni darasa pana sana na lenye faida kubwa sana kiroho).

Na hapa Neno la Mungu linasema kuwa “shukrani atakazopewa MUNGU kutoka kwa wale waliopokea, basi hizo ni faida kubwa”.

Mtu akimshukuru Mungu kwaajili ya kile ulichotoa, hiyo ni faida kubwa kwako, Maskini akimshukuru Mungu kwaajili ya kile ulichotoa hiyo ni faida kubwa kwako, Mtumishi wa Mungu akimshukuru Mungu kwaajili kile ulichotoa hiyo ni faida kubwa kwako, Yatima akimshukuru Mungu kwaajili kile ulichotoa hiyo ni faida kubwa kwako, Mnyonge akimshukuru Mungu kwaajili ya kile ulichotoa hiyo ni faida kubwa kwako.

2Wakorintho 9:11 “mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, UMPATIAO MUNGU SHUKRANI KWA KAZI YETU.

12  Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Shukrani ni nini kibiblia?

Mistari ya biblia kuhusu shukrani.

HUNA SHIRIKA NAMI.

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Rudi Nyumbani

Print this post

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

Wakorintho 2:10  Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.

11  Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu

Sifa mojawapo ya Roho Mtakatifu, ni kuchunguza, na tunajua mpaka kitu kichunguzwe ni lazima tu kitakuwa kimesitirika, kwa lugha nyingine tunaweza kusema kipo katika mafumbo. Hivyo Roho Mtakatifu anafanya kazi ya  kuyachunguza “YOTE”. Akiwa na maana Mafumbo yote, si tu yale yaliyo chini bali pia hata yaliyo kule juu Mungu mwenyewe alipo.

Na leo tutanyambua aina hizo za mafumbo kwa upana, ili tuelewe ni kwa jinsi gani Roho Mtakatifu alivyomsaada mkubwa sana kwetu.

Mafumbo yamegawanyika katika sehemu kuu tatu (3)

  1. Mafumbo ya wanadamu
  2. Mafumbo ya shetani
  3. Mafumbo ya Mungu

Mafumbo ya Wanadamu:

Ukipokea Roho Mtakatifu,  moja kwa moja unaongezewa hekima, ya kuweza kupambanua, na kuhukumu, akili zote za kibinadamu. Wala hakuna litakalokushinda, kwamfano Bwana Yesu alipowekewa mitego mingi na wayahudi ili watafute kosa ndani yake, wapate kumshitaki, hawakuweza kumshinda kwasababu saa ile ile, alielewa vema mawazo yao kwa Roho Mtakatifu aliyekuwa ndani yake.

Kwamfano katika ile habari ya kulipa kodi walipomjaribu, walishindwa kabisa kabisa.

Mathayo 22:15  Ndipo Mafarisayo wakaenda zao, wakafanya shauri, jinsi ya kumtega kwa maneno.

16  Wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na Maherodi, wakasema, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yote, kwa maana hutazami sura za watu.

17  Basi utuambie, Waonaje? Ni halali kumpa Kaisari kodi, ama sivyo? 18  Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema, Mbona mnanijaribu, enyi wanafiki?

19  Nionyesheni fedha ya kodi. Nao wakamletea dinari. 20  Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii, na anwani hii?

21  Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu. 22  Waliposikia, walistaajabu, wakamwacha, wakaenda zao

Wakati mwingine walimletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, ili wamnase wakashindwa pia, kwasababu Yesu alikuwa na Roho wa Mungu ndani yake(Yohana 8:1-11). Ndio maana Yesu naye akatupa hakikisho hilo kwamba katika kuenenda kuhubiri kwetu,  tusihofu watakapotaka kutushitaki, na kutupeleka mabarazani, au mahakamani, kutuhukumu, kwani yeye mwenywe atatupa kinywa cha hekima ambacho watesi wetu hawatatuweza.

Yohana 21:12  Lakini, kabla hayo yote hayajatokea, watawakamata na kuwaudhi; watawapeleka mbele ya masinagogi, na kuwaua magerezani, mkipelekwa mbele ya wafalme na maliwali kwa ajili ya jina langu.

13  Na hayo yatakuwa ushuhuda kwenu.

14  Basi, kusudieni mioyoni mwenu, kutofikiri-fikiri kwanza mtakavyojibu;

15  kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga.

Lakini pia Roho achunguzaye mafumbo hutupa hekima sio tu ya kutambua lakini pia ya kufanya hukumu sahihi.

Utakumbuka kisa kile cha Sulemani na wale wanawake wawili makahaba, ambao kila mmoja alikuwa ana mng’ang’ania mtoto Yule mmoja wakisema ni wake. Lakini Sulemani alipewa hekima ya kutoa hukumu vema, kwa kuwaambia nileteeni upanga, nimgawanye, ili kila mtu achukue nusu yake. Yule ambaye mtoto si wake akasema na iwe hivyo, lakini Yule mwingine akamwonea huruma. Ndipo Sulemani akatambua kuwa mtoto ni wa Yule mama aliyemwonea huruma (1Wafalme 3:16-28)

Sasa hiyo yote ni kazi ya Roho Mtakatifu ya kuchunguza mafumbo ya wanadamu, na kutupasha habari.

Lakini pia hutumia  njia ya maono au  ndoto kutufahamisha. Mafumbo yaliyositirika mioyoni mwa watu. Mfano wa Yusufu kwa Farao, na Danieli kwa ile ndoto ya Nebukadreza, Mambo ambayo hata walioziota ndoto zenyewe hawakuzikumbuka wala kujua maana zao, lakini Roho Mtakatifu aliwafunulia.

Hivyo ndivyo Roho Mtakatifu anavyotusaidia kuchunguza mafumbo ya wanadamu.

Mafumbo ya shetani:

Si kawaida ya shetani kujidhihirisha kwa wazi kama wengi wanavyodhani, bali huja kama malaika wa nuru, hivyo kama hujajazwa Roho Mtakatifu vema kamwe huwezi yajua mafumbo yake. Ndicho walichokikosa baadhi ya watakatifu wa kanisa la Thiatira.

Ufunuo 2:24  Lakini nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, wo wote wasio na mafundisho hayo, wasiozijua fumbo za Shetani, kama vile wasemavyo, Sitaweka juu yenu mzigo mwingine.

25  Ila mlicho nacho kishikeni sana, hata nitakapokuja.

Swali ni je haya Mafumbo ya shetani yanakujaje?

Yapo Manabii wa Uongo:

Manabii hawa wa uongo wamegawanyika katika makundi mawili.

Kundi la watumishi wa Mungu: Hawa ni ambao hawajasimama vema, hivyo wakati mwingine shetani hutumia vivywa vyao au mafundisho yao kupotosha wengine, bila hata ya wao kukusudia wakati mwingine. Mfano wa hawa alikuwa ni Petro, wakati ule aliposimama mbele ya Yesu na kuanza  kumkemea kwamba hatakwenda msalabani. Lakini Yesu palepale alitambua si Petro anayezungumza bali ni shetani, akamkea na kumwambia nenda nyuma yangu shetani (Mathayo 16:23).

Mfano wa hawa pia ni wale manabii 400 wa Ahabu. Ambao walimtabiria mfalme kuwa akienda vitani atashinda, kumbe ni pepo la uongo liliwaingia vinywani mwao likawaonyesha maono feki. Matokeo yake yakawa ni mfalme kufa (1Wafalme 22).

Mfano wa watumishi wa namna hii wanaompa shetani nafasi kuwatumia ni wengi sana. Hivyo si kila neno ambalo utaambiwa na kila anayeitwa mtumishi ulipokee tu au uliamini, ukijawa Roho vema utaweza yapambanua vizuri mafumbo haya ya shetani katikati ya vinywa vyao. Atakupa upambanuzi, kwa mafuta aliyoyaweka ndani yako.

Kundi la watumishi wa shetani: Hawa wanajijua kabisa kuwa ni watumishi wa ibilisi, ni wachawi wanaovaa suti na majoho, na kusimama madhabahuni, hawana hata ushirika na Kristo. Kuwatambua hawa Roho alitufundisha, ni kutazama matunda yao. (Mathayo 7:15-20), asilimia kubwa ya hawa wanajigamba kwa vitu, ukubwa. Na mafundisho yao ni ya mwilini. lakini pia kwasababu wana mapepo ya utambuzi hupendelea sana kujitii manabii. Ni wengi leo wanawafuata kwasababu ya kazi hiyo, wakidhani wanatabiriwa na Roho Mtakatifu kumbe ni mizimu. Ukijawa Roho vema utaweza kuzitambua hizo Roho. Kwasababu hazina ushirika hata kidogo na jina la Yesu, au mambo ya rohoni.

Mafumbo ya Mungu.

Mungu pia ana mafumbo yake, ambayo kama huna Roho Mtakatifu huwezi yatambua. Kwamfano Kristo anatembea leo duniani, akiwa na kiu, na njaa na uchi, na anagonga kwenye milango ya watu..Sasa kwasababu wewe hujui unadhani akija kwako atakutokea amevaa mavazi meupe na uso unaong’aa kama jua,  hujui kuwa amekuja kama watumishi wa Mungu wa kweli wanaojitaabisha kwa ajili ya roho yako, kukulea na kukulisha neno la Mungu. Lakini wewe unasema hawa ni matapeli, omba omba.

Mathayo 25:31  Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;

32  na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;

33  atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.

34  Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;

35  kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

36  nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.

37  Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?

38  Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?

39  Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

40  Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

Umeona hao wanaozungumziwa hapo, sio wale maskini unaowaona barabarani, au omba-omba, bali ni watendakazi wa Mungu. Hivyo watu wanaoonyosha mikono yao, kuwatengemeza watumishi na madhabahu za kweli za Mungu, wamejaliwa kuyajua mafumbo haya ya Mungu.

Mafumbo ya Mungu yapo mengi sana, ndio siri za ufalme wa mbinguni ambazo zipo ndani ya Yesu Kristo. Ambazo Yesu mwenyewe alizizungumza pia katika Mathayo 13.

Vilevile ukitaka umwone Mungu fumbo lake ni upendo, Ukitaka upewe na Mungu, fumbo lake ni utoe, ukitaka ukwezwe na Mungu fumbo lake ni unyenyekevu.

Kwanini leo utaona mtu anasema sijawahi kumsikia Mungu, na angali Mungu anasema nasi kila siku? Sijawahi kukutana na Mungu, na angali Mungu anakutana nasi kila siku? Sijawahi kuziona nguvu za Mungu, na wakati zipo nasi kila kitu? Ni kwasababu hajajawa vema Roho Mtakatifu, ambaye atamjalia kuujua moyo wa Mungu upo wapi.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, tunahitaji  kujazwa Roho na hiyo inakuja tutengapo muda wetu mwingi kila siku kutafakari sana Neno, pamoja na kuomba kila siku kwa muda usiopungua saa moja , hiyo itakupelekea kujazwa vema Roho, na hatimaye tutaweza kuyachunguza yote, na kuyatambua yote. Na wala hatutashindwa aidha na mwanadamu au shetani.

Ubarikiwe.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Roho Mtakatifu ni nani?.

ZIFAHAMU KAZI KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

Rudi Nyumbani

Print this post

ALIWAANGAMIZA BAADAYE WALE WASIOAMINI.

Karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu lililo Mwanga wa Njia zetu,  na Taa iongozayo miguu yetu (Zaburi 119:105).

Neno hili lililo Taa linasema..

Yuda 1:5 “Tena napenda kuwakumbusha, ijapokuwa mmekwisha kujua haya yote, ya kwamba Bwana, akiisha kuwaokoa watu katika nchi ya Misri, ALIWAANGAMIZA BAADAYE WALE WASIOAMINI”

Maandiko hayo yanatufundisha kuwa KUOKOLEWA sio Mwisho wa safari. Kwani ni kweli wana wa Israeli waliokolewa kutoka Misri jeshi lote.. lakini si wote walioingia nchi ya Ahadi, bali watu wawili tu  ambao ni Yoshua na Kalebu, na watoto wao ambao walizaliwa jangwani, lakini wengine wote MUNGU aliwaangamiza jangwani ijapokuwa aliwatoa Misri.

Leo wanaookolewa ni WENGI, wanaomkiri YESU ni wengi!, lakini pia ni wengi wanaoangamizwa na Bwana, kwasababu ya kutotembea na Mungu katika wokovu wao.

Wengi wa wana wa Israeli walijaa viburi (Mfano wa Dathani na Kora, soma Hesabu 16:1-50) na wengine walijaa mioyoni mwao manung’uniko na ibada za sanamu, na wengine walikuwa ni watu wa kumjaribu Mungu kila wakati..ingawa wote walikuwa wameokoka na utumwa wa Farao, lakini kwa bahati mbaya hawakuiona ile nchi ya Ahadi.

WALIOKOLEWA lakini baadaye WALIANGAMIZWA!…. WALIFUNGULIWA lakini baadaye WALIANGAMIZWA…. WALIPONYWA lakini baadaye WALIANGAMIZWA… Na jambo linalohuzinisha Zaidi ni kwamba waliangamizwa jangwani wakiwa bado wanakula Mana (Baraka za mbinguni), Vile vile waliangamizwa wakiwa chini ya WINGU NA NGUZO YA MOTO (Upako na Utumishi) na Zaidi ya yote walikuwa wameshabatizwa katika roho katika bahari ya Shamu.

Mambo haya yanabaki kuwa funzo na onyo kwetu ili tusifanya makosa kama hayo, kama maandiko yasemavyo..

1Wakorintho 10:1  “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;

2  wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;

3  wote wakala chakula kile kile cha roho;

4  wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.

5  Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.

6  Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani.

7  Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.

8  Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.

9  Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

10  Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.

11  Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

12  Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.

Je unajivunia ubatizo?… Unajivunia dhehebu?…unajivunia Karama uliyo nayo?… unajivunia upako?.. Vyote hivyo wana wa Israeli walikuwa navyo, lakini wengi wao waliangamizwa.

Utakase ukristo wako, kaa mbali na dhambi!, usimjaribu Mungu, usiabudu sanamu baada ya kuokoka, jitenge na mambo ya ulimwengu, tembea na Mungu kama Yoshua na Kalebu, na Bwana atusaidie sote katika hayo.

Amen.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SHIKA SANA ULICHO NACHO, ASIJE MTU AKAITWAA TAJI YAKO.

Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)

MNGOJEE BWANA

ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.

NIFANYALO WEWE HUJUI SASA; LAKINI UTALIFAHAMU BAADAYE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kututa ni nini? (Mhubiri 2:26).

Swali: Neno “Kututa” lina maana gani kama tusomavyo katika Mhubiri 2:26?


Jibu: Turejee..

Mhubiri 2:26 “Kwa sababu Mungu humpa yeye aliyemridhia hekima na maarifa na furaha; bali mkosaji humpa taabu, ili kukusanya na KUTUTA, apate kumpa huyo ambaye Mungu amridhia. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.

“Kututa” maana yake ni “KULIMBIKIZA”..

Kwahiyo maneno hayo tunaweza kuyaweka katika Kiswahili hiki.. “Kwa sababu Mungu humpa yeye aliyemridhia hekima na maarifa na furaha; bali mkosaji humpa taabu, ili kukusanya na KULIMBIKIZA, apate kumpa huyo ambaye Mungu amridhia. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.

Andiko hili linatufundisha hatari ya kukusanya mali na kulimbikiza, ikiwa tupo nje ya KRISTO. Kwa maana hapo maandiko yanasema, mali za mtu huyo (mkosaji), alizojikusanyia na kujilimbikizia, atanyang’anywa na kupewa yule Mungu aliyemridhia.

Lakini pia mstari huo unatuonyesha thawabu kuu ambazo Mungu humpa yule aliyemridhia. Na hizo si nyingine Zaidi ya HEKIMA, MAARIFA na FURAHA.

Kabla ya kumpa mtu Mali humpa Hekima, Maarifa na Furaha na hivi vitatu ndivyo vitu vya kuvitafuta kwa MUNGU kabla ya kuomba vitu vingine kama Mali. Kama Sulemani aliomba Hekima kwanza na Mungu akampa Hekima na Mali ikawa ni nyongeza.

Hali kadhalika na sisi hatuna budi kutafuta hekima, Maarifa, Ufahamu na Furaha kwa bidii kwani tukiyapata hayo basi hayo mengine tutazidishiwa, na hata tusipoyapokea, bado hekima na maarifa vitabaki kuwa utajiri mkuu.

Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu.

14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.

15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye.

16 Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.

17 Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani.

18 Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashikamanaye naye”

Tafuta Hekima, tafuta Maarifa, tafuta Ufahamu, Busara na Furaha..

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?

NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

Rudi Nyumbani

Print this post

Ono la kile kijiti kuwaka moto pasipo kuteketea lilibeba ufunuo gani? (Kutoka 3:2 )

Swali: Katika Kutoka 3:2 tunasoma kuwa Mungu alisema na Nabii Musa kupitia kile kijiti ambacho kilikuwa kinawaka moto lakini hakikuteketea, je kulikuwa kuna sababu gani au ufunuo gani katika ishara ile?


Jibu: Tuanze kusoma mstari ule wa kwanza mpaka ule wa tatu, ili tupate kuielewa vizuri habari..

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu. 

2 Malaika wa Bwana akamtokea, KATIKA MWALI WA MOTO ULIOTOKA KATIKATI YA KIJITI; AKATAZAMA, NA KUMBE! KILE KIJITI KILIWAKA MOTO, NACHO KIJITI HAKIKUTEKETEA. 

3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei”

Lengo la Mungu kumwonyesha Musa Ono hilo kubwa, halikuwa kumburudisha au kumsisimua, bali ulikuwa ni ujumbe wa MUNGU kwa Musa na kwa Israeli wote ambao watasumiliwa baadae.

Na ujumbe huo si mwingine Zaidi ya ule tuusomao katika Isaya 43:1-4..

Isaya 43:1 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.

2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; UENDAPO KATIKA MOTO, HUTATEKETEA; WALA MWALI WA MOTO HAUTAKUUNGUZA. 

3 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako. 

4 Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako”

Hapo katika mstari wa Pili (2) anasema… “UENDAPO KATIKA MOTO, HUTATEKETEA; WALA MWALI WA MOTO HAUTAKUUNGUZA”.

Na hiyo ndio sababu ya Mungu kumwonesha Musa ono lile, kwamba watakapopita (wana wa Israeli) katika Moto (yaani majaribu mbalimbali) hawataungua..mfano wa kile kijiti kilichowaka moto lakini hakikuteketea.

Hivyo kwa ufunuo huo Israeli walielewa kuwa Mungu anasema nao, kwamba atakuwa pamoja nao katika mapito yote, hivyo wasiogope majaribu wala moto watakaokutana nao, kwani hautawateketeza, kinyume chake utawateketeza maadui zao…mfano wa akina Shadraka, Meshaki na Abednego, ambao walitupwa katika tanuru la moto, na badala ya moto ule kuwala wao, uligeuka na kuwala maadui zao wale walioshika na kuwatupa motoni.

Danieli 3:20 “Kisha akawaamuru baadhi ya watu mashujaa wa jeshi lake kuwafunga Shadraka, na Meshaki, na Abednego, na kuwatupa katika ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto. 

21 Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa suruali zao, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.

22 Basi kwa sababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto ukawaua wale watu waliowashika Shadraka, na Meshaki, na Abednego. 

23 Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, katikati ya ile tanuru iliyokuwa inawaka moto. 

24 Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme. 

25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu”

Ni hivyo hivyo hata sasa, Mungu anawalinda wale wote wamwaminio na kumtumainia yeye,  wanakuwa kama kijiti kilichopo motoni lakini hakiteketei.. Wengine wakipitia majaribu wanapotea kabisa, lakini watu wa Mungu wanapita katikati ya moto na wanatoka salama.

Je umempokea Bwana YESU?. Je yeye ni tumaini lako na ngao yako?..Kama upo nje ya Kristo fahamu kuwa Moto utakuunguza, na ibilisi atakumaliza. Lakini ukiwa ndani ya YESU utakuwa salama.

Mpokee YESU kama bado hujampokea, hizi ni siku za mwisho naye amekaribia kurudi sana.

Waebrani 10:37  “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia.

38  Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

DUNIANI MNAYO DHIKI.

UJIO WA BWANA YESU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani?

Kitabu cha Waebrania ni moja ya nyaraka ambazo waandishi wake hawajajitambulisha aidha ndani au mwanzoni  au mwishoni mwa nyaraka hizo. Lakini kwa kutathimini baadhi ya nukuu za mwandishi, huwenda alikuwa ni mtume Paulo aliyeuandika. Kufuata na kumtaja Timotheo kwenye waraka huo, na tunajua Timotheo alikuwa chini ya utume wa Paulo, kwani  ndiye aliyeongozana naye na kumtaja sana katika nyaraka zake nyingi.

Waebrania 13:23  Jueni ya kuwa ndugu yetu Timotheo amekwisha kufunguliwa; ambaye, akija upesi, nitaonana nanyi pamoja naye.

Na pia jinsi mwandishi alivyomalizia waraka wake,  kwa kusema “neema na iwe nanyi nyote”.  Ni salamu inafanana na nyaraka zote za mtume Paulo, kila alipomaliza alihitimisha na  baraka hizo.

Japo wengine wanasema namna ya uandishi haifanani na mtume Paulo, yawezekana alikuwa ni Apolo, au Barnaba, au sila au mtu mwingine tofauti na Paulo.

Lakini kwa vyovyote vile kumtambua mwandishi, si lengo la uandishi, lengo ni kufahamu kilichoandikwa ndani humo.

Maelezo mafupi ya kitabu hichi.

Kwa ufupi, kama kitabu hichi kinavyoanza kujitambulisha,  kinasema

WARAKA KWA WAEBRANIA.

Maana yake ni kitabu kilichoelekezwa kwa wayahudi-wakristo waliokuwa katika kanisa wakati ule. Ndio maana kwa jinsi ulivyoandikwa waraka huu, mwandishi anazungumza na mtu ambaye mwenye uelewa wa dini ya kiyahudi na taratibu zake za kiibada.

Dhumuni kuu ni kueleza UKUU WA YESU JUU YA WATU WOTE, NA MAMBO YOTE YA AGANO LA KALE.

Kwamfano anaeleza Yesu alikuwa mkuu juu ya;

  1. Manabii wa agano la kale

Waebrania 1:1  Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2  mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. 3  Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu

  1. Alikuwa mkuu zaidi ya malaika: Soma Waebrania 1:13-2:18

Waebrania 1:13  Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14  Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

  1. Alikuwa mkuu zaidi ya Musa, Yoshua na Haruni. (Soma, Waebrania 3:1-19, 4:1-13, 4:14-10:18)
  2. Alikuwa mkuu zaidi ya kafara za agano la kale. (Soma, Waebrania 10:11-14).

Waebrania 10:11  Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi.

12  Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu;

13  tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake. 14  Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.

Hivyo kitabu hichi kinamfafanua Kristo kwa undani, jinsi alivyo na ukuu zaidi ya mambo yote ya agano la kale. Na kwamba watu wote tangu Adamu mpaka Ibrahimu wasingeweza kukamilishwa bila Kristo. Waliishi wa ahadi hiyo ya kuja mkombozi, wakiingojea kwa shauku na hamu (Waebrania 11).

Lakini pia kitabu hichi  kinatoa angalizo kwa wayahudi wasirudi nyuma kwasababu ya dhiki na mateso yanayowapata kwa ajili ya imani ya Yesu Kristo. (Waebrania 12:1-13, 10:26-31), Bali wamtazame Kristo kama kielelezo chao, jinsi alivyostahimili mashutumu makuu namna ile.  Hii ni kutuhamasisha na sisi kuwa tunapopitia dhiki leo basi nasi tumtazame Kristo aliyestahili, mapingamizi yale, wala hakuutupa ujasiri wake.

Waebrania 12:1  Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

2  tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.

Ielewe kwa kina Waebrania 13:5 maana yake.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Je ni Mungu au Malaika?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kupenda fedha kutaibomoa ndoa yako.

Mafundisho maalumu kwa wanandoa – Wanawake.

Ikiwa utapenda kupata mafundisho mengine ya namna hii, basi fungua link hii uweze kuyasoma. >>.

https://wingulamashahidi.org/category/mafundisho-ya-wanandoa/

Habari ya Samsoni na Delila inafundisho kubwa nyuma yake kwa wanandoa. Wengi wanafikiri Delila alikuwa mwanamke kahaba ambaye Samsoni alimuokota tu na kukutana naye. Lakini uhalisia ni kwamba Delila alikuwa ni mke wa Samsoni.

Lakini mwanamke huyu, aliweza kubadilishwa akili kwa tamaa tu ya fedha. Ni mwanamke ambaye alipendwa sana na Samsoni, chochote ambacho angetaka kwa Samsoni angepatiwa. Lakini Wafilisti walipoona mwenendo wa Samsoni jinsi alivyompenda sana mwanamke huyu. Wakatumia fursa ile, kumshawishi Delila, kwa kumuahidia donge kubwa la fedha. Ili tu atoe siri ya asili ya nguvu zake.

Delila, akakubali, akaanza kumshawishi Samsoni, kwa kipindi kirefu, na hatimaye akafunuliwa siri ya nguvu zake. Akaenda akaziuza kwa wafilisti, kwa vipande vya fedha.

Waamuzi 16:4 Ikawa baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki, jina lake akiitwa Delila.

5 Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja.

6 Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe.

Kama mke, upendo wako unapohamia kwenye fedha, ni dalili madhubuti kuwa unaua  nguvu ya ndoa yako (ambayo ipo kwa mume). Usitangulize mali mbele ya ndoa yako, wala usishawishiwe na fedha kwa chochote ukadharau thamani ya mumeo. Samsoni hakuwa mfanya biashara au mwajiriwa wa kampuni Fulani, hakuwa hata na akaunti benki. Lakini alikuwa mwamuzi wa Taifa teule la Mungu. Mtetezi wa wanyonge, na mkombozi wa walioonewa, hakujitajirisha yeye, alilitajirisha taifa,. Jambo ambalo Delila hakulithamini. Akawa tayari kuoelewa na fedha(wafilisti) na sio nguvu zake(Samsoni).

Leo wapo wamama, ambao wanachotafuta kwa waume zao ni fedha tu,fedha tu, fedha tu.. wakikosa hiyo wapo tayari kufanya chochote. Wengine hata kuanzisha mahusiano na watu wengine wenye uwezo wa juu,  hawajua kuwa mwanaume anaweza asiwe tajiri kifedha, lakini ana nguvu za kuiendesha na kuilinda familia yako, jamii yako, ndugu zako, kipawa alichonacho kikaweza kukufanya wewe ukae vizuri au kuistaajabisha jamii au taifa, Lakini endapo tu utakiona hicho na kukithamini ndani yake.

Hivyo, kama mwanamke, toa moyo wako hapo kabisa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

https://wingulamashahidi.org/category/mafundisho-ya-wanandoa/

Mtande ni nini? Ni funzo gani lipo nyuma yake?

KITENDAWILI CHA SAMSONI

Je! mtu anapofunga kwa muda wa SAA 24,anapaswa kunywa maji au kitu chochote?

Rudi Nyumbani

Print this post

VAA MAVAZI, USIVALIE MAVAZI.

Je hayo mavazi uvaayo ni kwa lengo gani?.. ili uonekane na nani?.. 

1 Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi”.

Sasa kuvaa mavazi si vibaya, hata hivyo tunapaswa tuvae mavazi, (hilo ni agizo la Bwana tangia Edeni, Bwana Mungu alipowafanyia mavazi ya ngozi wazazi wetu wa kwanza).

Lakini hapo katika 1Petro 3:3 hasemi “kuvaa mavazi”..bali na anasema “kuvalia mavazi”.

Kuna tofauti ya “kuvaa” na “kuvalia”.

Kuvalia maana yake “hayo mavazi yamelengwa kwa kusudi maalumu la kutazamwa na watu”

Kwamfano makahaba (wanawavalia mavazi ya kikahaba wateja wao ili miili yao iuzike vizuri). vile vile wahuni wanawavalia mavazi wahuni wenzao ili watazamwe na wao.

Kijana wa kiume anayevaa suruali ya kubana huyo hajavaa mavazi bali “amevalia mavazi”…. amewavalia mavazi aina fulani ya watu (wahuni wa kike), ili wamtazamapo wamtamani.

Dada anayevaa suruali ya aina yoyote ile, anakuwa hajavaa mavazi bali kavalia mavazi (kamvalia mtu),

Na lengo lake si lingine zaidi ya kutaka kutamaniwa, na Neno la Mungu linasema “yeyote amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye nafsini mwake”

Kwahiyo mwanamke anayetazamwa na kutamaniwa kwa uvaaji wake, naye pia kazini na yule aliyemtamani (hiyo ni kulingana na Neno la Mungu).

Kama unavyokuwa makini na kile kinachoingia ndani yako (yaani chakula)...vile vile ongeza umakini kwa kila unachojivika nje.

Usiwe mwepesi wa kwenda na kila fasheni inayoingia…kiasi kwamba kila mtindo unaoingia unaupokea, ni lazima uchague kama unavyochagua chakula.

Ni lazima uwe na uchaguzi unaokufaa kama vile ulivyo na uchaguzi wa baadhi ya vyakula vikufaavyo.

Jiulize je hilo vazi la mgongo wazi kama umevaa au umevalia,?…

Hilo vazi linaloonyesha kitovu na mapaja je umevaa au umevalia?

Hiyo kaptura kijana uliyoivaa na kutembea nayo barabarani umevaa kwa lengo gani?..je unamvalia nani?

Jisitiri, na pia jiheshimu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post