Category Archive Home

Mvinje ni mti gani? (Mwanzo 6:14)

Swali: Mti wa Mvinje uliotumika kutengenezea safina kulingana na Mwanzo 6:14 ndio mti gani kwasasa?.

Jibu: Tusome,

Mwanzo 6:13 “Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia. 

14 Ujifanyie safina ya MTI WA MVINJE; fanya na vyumba ndani ya safina, ukaifunike ndani na nje kwa lami”.

Mti wa Mvinje ni jamii ya miti inayoota karibia sehemu kubwa ya dunia, ikiwemo barani Afrika (Tazama picha juu).

Sifa ya miti hii ni migumu sana na Imara, lakini iliyo kuu kuliko zote ni uwezo iliyonayo ya kutoathiriwa na maji.

Tofauti na miti mingine, ambayo adui wake wa kwanza ni maji, (inapogusa maji basi inaoza), lakini Mti wa Mvinje wenyewe hauathiriwi na maji, hivyo kufanya mbao ya mti huo itumike kwa matumizi ya kutengeneza boti ndogo ndogo na hata kubwa (boti za wavivu na baadhi ya za abiria zinatengenezwa kwa kutumia miti hii), vile vile mbao ya mti wa Mvinje inatumika kutengenezea viti vya viwanja vya michezo na sehemu za Uma, na vile vile inatumika kutengenezea viungio vya barabara za treni (Reli), na matumizi mengine ya samani za ndani kama vile milango na makabati.

Kwa sifa miti hiyo iliyoibeba ndiyo ikawa sababu ya Mungu kumwambia Nuhu ajenge safina kwa kutumia miti hiyo, kwani ingetumika miti mingine huenda isingeweza kuvumilia kudumu juu ya maji kwa miezi yote ile mitano, kwani maandiko yanasema mvua ilinyesha siku 40 usiku na mchana, na maji yalidumu juu ya uso wa nchi siku 150 (Miezi 5) soma Mwanzo 7:4,24.

Maandiko mengine katika biblia yanayohusu mti wa mvinje ni pamoja na Isaya 6:13 na Isaya 44:14.

Lakini leo hii mvinje wetu ni nini?

Mti wa Mvinje leo hii si mwingine Zaidi ya msalaba utuokoao sisi na dhambi zetu, na safina yetu ni Bwana Yesu Kristo, tuwapo ndani ya Kristo basi gharika ya ghadhabu ya Mungu ambayo imekusudiwa kumwagwa katika siku hizi za mwisho haitatupata.

Je umeokoka? Kama bado unasubiri nini? Kumbuka dunia hii inaenda kuisha, tupo nyakati za majeruhi na unyakuo umekaribia.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mretemu ni mti gani?

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

Mwerezi ni nini?

FANYA BIDII ZOTE ULE MATUNDA YA UZIMA.

JE NI KUTII AU KUPATA KWANZA MAARIFA?

Rudi nyumbani

Print this post

Praitorio ni nini? Na Kwanini ilikuwa ni najisi kwa wayahudi kuingia humo? (Yohana 18:28)

Jibu: Turejee,

Yohana 18:28  “Kisha wakamchukua Yesu kutoka kwa Kayafa mpaka Praitorio, nayo ikawa alfajiri; lakini wao wenyewe hawakuingia ndani ya ile praitorio,wasije wakanajisika,bali wapate kuila Pasaka”.

Praitoria ni “ukumbi wa hukumu” ambao unakuwepo ndani ya majumba ya wafalme. Wahalifu ambao ilibidi kesi zao ziamuliwe na mfalme au liwaji wa mji, basi walipelekwa katika ukumbi huo na kukutana na mkuu huyo na kuhojiwa na moja kwa moja kutolewa hukumu.

Kipindi Wakuu wa makuhani wamemkamata Bwana Yesu, hawakuweza wao wenyewe kumhukumu kwasababu nchi ya Israeli yote ilikuwa chini ya utawala wa Warumi (kwaufupi ilikuwa ni koloni la Warumi), waliokuwa wanaiongoza serikali yote ni Warumi, na ndio waliokuwa wananatoa hukumu ya mwisho, ndio maana ikawabidi wakuu wa makuhani wampeleka Bwana Yesu kwa Pilato ambaye ndiye aliyekuwa liwali wa Uyahudi, na ndiye mwenye kutoa maamuzi ya mwisho (Mathayo 27:2).

Sasa kwasababu sheria za Wayahudi hazikuwawaruhusu wao kuchangamana na watu wa mataifa, wala kuingia katika nyumba zao tena hususani wakati wa sikukuu, hiyo ikawafanya wale wakuu wa makuhani wabaki nje wakati Kristo anaingizwa ndani ya Praitorio kuzungumza na Pilato.

Wayahudi hawakuingia katika nyumba za watu wa mataifa, kwasababu katika nyumba hizo kulikuwa na vitu najisi vilivyo kinyume na sheria za Musa, mfano wa vitu hivyo ni sanamu, utakuta hata kikombe tu cha kunywea maji kimetengenezwa kwa taswira ya miungu yao, na Zaidi sana vyakula vya watu wa mataifa vingi vilikuwa ni najisi kulingana na sheria za kiyahudi. Kwahiyo endapo Myahudi akiingia katika nyumba hizo na kushiriki vitu vyao hivyo hata kwa bahati mbaya au kwa kutokujua, basi tayari anakuwa amejitia unajisi, na mtu akiwa najisi anakuwa hastahili kushiriki sikukuu yoyote ya kiyahudi, (anatengwa kwa muda Fulani mpaka unajisi wake utakapoisha).

Ndio maana ikawepo sheria ya wao kutochangamana na watu wa mataifa wala kuingia katika nyumba zao..utazidi kulithibitisha hilo zaidi kipindi kile Mtume Petro ameenda nyumbani kwa Kornelio..

Matendo 10:26 “Lakini Petro akamwinua, akasema, Simama, mimi nami ni mwanadamu.

27  Na katika kusema naye akaingia ndani, akaona watu wengi wamekusanyika.

28  Akawaambia, NINYI MNAJUA YA KUWA SI HALALI MTU ALIYE MYAHUDI ASHIKAMANE NA MTU ALIYE WA TAIFA LINGINE WALA KUMWENDEA, lakini Mungu amenionya, nisimwite mtu awaye yote mchafu wala najisi.

29  Kwa sababu hiyo nalikuja nilipoitwa, nisikatae; basi nawauliza, ni neno gani mliloniitia?”

Lakini swali ni je! Hiyo sheria ya wayahudi kutochangamana na watu wa mataifa mpaka leo hii ni agizo la Mungu?..Kwamba watu wa mataifa ni najisi mpaka leo??

Jibu ni La!.. Kupitia msalaba wa Yesu Kristo umetufanya wote wawili kuwa mamoja.. Hakuna Myahudi wala Myunani, kwa kumwamini Yesu Kristo sote tunakuwa safi, na kitu kimoja mbele za Mungu, wala hakuna aliye bora kuliko mwingine..yeye Kristo ndiye aliyekibomoa hicho kiambaza cha kati kilichotutenganisha.

Waefeso 2:11  “Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwamba zamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili, mnaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, yaani, tohara ya mwilini iliyofanyika kwa mikono;

12  kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani.

13  Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo.

14  Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga.

15  Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani.

16  Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba.

17  Akaja akahubiri amani kwenu ninyi mliokuwa mbali, na amani kwao wale waliokuwa karibu.

18  Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kumkaribia Baba katika Roho mmoja”.

Tunakuwa Najisi tu tunapokuwa nje ya Yesu Kristo, na kinachotufanya kuwa najisi si kitu kingine Zaidi ya dhambi ndani ya maisha yetu, kama Bwana Yesu alivyosema katika Mathayo 15:17-20.

Je! umeokoka?, kama bado unasubiri nini?..Hizi ni siku za mwisho, na Bwana yupo mlangoni.

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

USIMPE NGUVU SHETANI.

Lumbwi ni nini katika biblia?

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Rudi nyumbani

Print this post

JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?

Shalom, nakusalimu katika jina la Yesu Kristo mwokozi wetu. Karibu tujifunze maneno ya uzima maadamu siku ile inakaribia.

Katika siku hizi za mwisho ni lazima uwe makini sana na mahali ulipo, kwasababu zama zimebadilika, si kila jambo la kuliamini, vilevile si kila jambo la kutoliamini. Unamuhitaji Roho Mtakatifu sana kukusaidia kuchagua kilicho sahihi.

Bwana anatufananisha sisi na kama kondoo, na yeye kama mchungaji. Na sikuzote, mchungaji mwema, huwa anawapeleka kondoo wake katika maji ya mito-salama. Na si kila mto ilimradi mto tu anawapeleka kondoo zake kunywea maji hapana, bali pale tu palipo na maji ya utulivu ndipo anapowapeleka kondoo zake.

Ndio maana katika Zaburi ya 23 Inasema;

Zaburi 23:1 ‘Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.  2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza’.

Ni kwanini maji ya utulivu, kwasababu maji yenye mvurugano, au yaliyotibuliwa yana hatari nyingi, huwenda ni makao ya viboko na mamba na hivyo kutembea kwao huko ndio kunafanya maji Yale yawe na mvuragano, kwahiyo kondoo akinywa maji pale yupo hatarini kuvutwa na mamba, akafanyika kitoweo.

Au huwenda maji hayo ni mkondo wa mafuriko, hivyo kitu chochote kitakachotelezea kule mtoni, si rahisi kupona kinyume chake ni kitasombwa na kupotelea mbali.

Hivyo maji yasiyotulia, si salama kwa mifugo. Na mchungaji apendaye kondoo huwa hawapeleki mifugo yake hapo.

Ndivyo ilivyo kwa Kristo, anapotuokoa, anatuongoza kwa Roho wake malipo na maji ya utulivu tukae hapo tunywe. Lakini tatizo linakuja ni sisi kuyakataa maji ya utulivu, tunayatafuta maji ya mivurugano.

Ndugu usiangalie ukubwa wa mto, au ukubwa wa Bwawa, haikuhitaji wewe kunywa mto mzima ndio ukate kiu yao. Naamanisha usiangalie wingi wa watu, au ukubwa wa jengo na madhabahu iliyopambwa, au utajiri wa kanisa ndio ufikiri kuwa hapo ni salama kwa roho yako. Bali tazama palipo na utulivu wa kiroho. Hapo ndipo utulize nafsi yako. Kwasababu unaweza kwenda mahali kwa lengo la kuikata kweli kiu yako kwa Bwana lakini kinyume chake ukakutana na mamba wakali wakakumaliza kabisa.

Palipo na maji salama ni wapi?

Kwanza ni pale Palipo na fundisho la Yesu: Yesu ndio maji yenyewe tulivu ya uzima, na sio nabii au mtume au askofu, au kanisa, au pesa, au umaarufu.. Hivyo angalia kiini cha fundisho unalofundishwa mahali ulipo, je yote yanalenga kukukuza kumjua Yesu au linakupeleka katika mambo mengine? Fikiri Tangu umekaa hapo, ni nini umeongeza katika kulijua Neno la Kristo katika kweli yote. Lakini Kama umejazwa maarifa ya ki-mwili tu zaidi yale ya Kristo, yaani  ya ki-ndoa, ki-uchumi, uchawi, biashara,pesa, hiyo ni injili nyingine, ni mafuriko ya adui, hakuna maji tulivu hapo, utazombwa na kuangamia kabisa.

Yohana 4:13  “Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; 14  walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele”

Palipo na Upendo: Hicho ni kigezo cha pili.

Yakobo 3:16  “Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya”.

Katika mkusanyiko wowote, fundisho la tendo la upendo wa ki-ndugu linapuuziwa, au halihimizwi, ndani  kuna vita visivyokoma kati ya washirika, pengine huwenda na viongozi kwa viongozi, hiyo ni ishara kuwa utulivu wa Roho haupo hapo, hivyo ni hatari pia kwa maisha yako ya kiroho.

Tujitahidi sana kuwa na vipimo hivi vya kiroho katika kuchagua mahali tukusanyakapo kupata maji ya uzima, vitakusaidia sana, kwasababu hizi ni siku za mwisho, na manabii wengi na makristo wa uongo na madhehebu na dini za uongo  zimezuka kila pembe ili kuwatoa watu kwenye mstari.

Yajali maisha yako ya kiroho. Mpende Kristo na Agizo lake.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

WALIKUWA WAMECHOKA NA KUTAWANYIKA KAMA KONDOO WASIO NA MCHUNGAJI.

JE! UNAMPENDA BWANA?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya neno ‘mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena’?

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema ‘mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena’ (Mithali 24:16)


JIBU: Ili kuielewa vema mstari huo  tuanzie vifungu vya juu yake kidogo.

Mithali 24:15 Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki; Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika; 

16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.

Hapo anazungumzia tabia za mtu mbaya anayejaribu kuharibu kazi za mtu mwema (mtakatifu). Kwamba anaweza kudhani kuwa kufanikiwa kwa mipango yake, kutamfanya Yule mtu akate tamaa ya kuendelea mbele, lakini kinyume chake, ni kuwa bado atanyanyuka tena na kuendelea mbele.

Kwamfano, watu Fulani wanaweza kuharibu umoja wa kanisa, kwa kupachika fitna na masengenyo ndani yake, na matokeo yake ikawa ni kanisa  kuvunjika au kugawanyika, lakini kiuhalisia watoto wa Mungu wa kweli, wenye mbegu ya Mungu ndani yao, watasimama tena na kuujenga ule umoja walioupoteza. Lakini wengine wasio wa Mungu, watakimbia, au watakata tamaa na kurudi nyuma, na kufurahia kuanguka kule.

Au jengo la kanisa linaweza likaharibiwa na wapagani au mazingira ya asili, lakini watu wenye mbegu ya Mungu hawakati tamaa watanyanyuka na kulijenga tena upya.

Ndivyo ilivyokuwa kipindi cha wafalme wakati ambapo hekalu la kwanza linabomolewa na Nebukadreza mfalme wa Babeli, Baadhi ya wayahudi hawakumwacha Mungu wao moja kwa moja, bali waliendelea kumtafuta na kumwomba sana (Akiwemo Danieli) hatimaye baada ya miaka 70 wakarudi kulijenga upya tena. Hata baadhi ya wafalme walipotoa tamko la kusitishwa kujengwa kwa hekalu hilo bado walisimamia kusudi lao lilelile mpaka kulimaliza ijapokuwa waliwekewa vikwazo vingi sana.

Halikadhalika Injili ya mitume ilizuiliwa mara nyingi, Kwamfano Paulo anasema shetani alimzuia mara tatu ili asiipeleke injili (1Wathesalonike 2:18). Wakati mwingine alifungwa Lakini hayo hayakumkwaza na kumfanya aache kuihubiri injili, kisa amezuiliwa, bali kila siku maisha yake yalikuwa ni ya utumishi kana kwamba hakuna kikwazo chochote mbele yake, hata alipokuwa gerezani alihubiri kwa nyaraka, ambazo baadhi ya hizo ndio hizi zinazofanyika Baraka kwetu hadi sasa.

Kama mitume wangehesabu vikwazo, vitisho, vifungo, kamwe wasingeweza kuieneza injili ile ulimwenguni kote kwa kasi ile. Hivyo na sisi, tufilisikapo, tupatapo hasara, tufiwapo, tusalitiwapo na baadhi ya ndugu, ikapelekea mpaka huduma kuvurugika, au maisha ya kiroho kudorora, tusife moyo wa kumtumikia Bwana au kuendelea mbele, bali tunaanza tena upya, kana kwamba ndio tumezaliwa tena mara ya pili leo.

Lakini mstari huo haumaanishi, kuanguka katika “dhambi”, kama wengi wanavyodhani. Mtakatifu hana tabia ya kuanguka anguka ovyo kwenye dhambi..Yaana leo adondoke kwenye uzinzi, halafu kesho tena aanguke kwenye uzinzi, kesho kutwa hivyo hivyo, halafu awe bado na nguvu ya kusimama kwa Bwana. Hilo jambo haliwezi kutokea kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili.

Kuanguka kwetu ni kuwekewa vikwazo na adui, vilivyo nje ya uwezo wetu, lakini sio vile vilivyo ndani ya uwezo wetu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako (Mithali 27:23)

Nini maana ya Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)

Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?

Rudi nyumbani

Print this post

Mierebi ni Nini kwenye biblia? (Isaya 15:7)

Mierebi ni aina ya miti inayostawi Mahali palipo na maji maji, Mahali pengine popote haistawi. Tazama mwonekano wake kwenye picha juu.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyolitaja Neno hili;

Mambo ya Walawi 23:40

[40]Nanyi siku ya kwanza mtajipatia matunda ya miti mizuri, na makuti ya mitende, na matawi ya miti minene, na mierebi ya vijitoni; nanyi mtafurahi mbele za BWANA, Mungu wenu, muda wa siku saba.

Isaya 44:2-5

[2]BWANA, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua.

[3]Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa;

[4]nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji.

[5]Mmoja atasema, Mimi ni wa BWANA; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa BWANA, na kujiita kwa jina la Israeli.

Soma pia Ayubu 40:22, na Isaya 15:7

Kama tunavyosoma hapo Bwana aliwaagiza Wana wa Israeli watumie matawi yake kama kitu Cha shangwe katika sikukuu ya vibanda..Pindi wanapokusanyika wayanyanyue juu wamwimbie Bwana nyimbo za furaha. Lakini bado tunaona sifa ya mti huu ni kuwa karibu na vijito vya maji.

Vivyo hivyo na watu wa Mungu Rohoni, Bwana anawaona kama mierebi yake, miti inayostahili kumsifu Bwana..Kwasababu ndani yao mito ya maji ya uzima inatiririka.. lakini wengine ambao hawana Kristo ni sawa na miti mikavu tu.

Na matokeo ya kukosa mito ya uzima ndani yako ni wewe kufanyika makao ya mapepo kwasababu mapepo ndio Yanakaa sehemu isiyo na maji.

Soma

Mathayo 12:43-45

[43]Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate. [44]Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa. [45]Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.

Umeona? Unasubiri nini usimpe Bwana Yesu maisha Yako? Huna Raha, Wala Tumaini, Wala faraja unapokuwa nje ya Kristo. Okoka Leo Bwana ayaponye maisha Yako.

Ikiwa upo tayari kuchukua uamuzi huo wa kuokoka na kufanyika Mwerebi mzuri wa Bwana basi fungua hapa Kwa ajili ya mwongozo huo>>

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mretemu ni mti gani?

Mti wa Mshita ni mti wa namna gani?

Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?

Mjusi hushika kwa mikono yake; Lakini yumo majumbani mwa wafalme.

Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?

NUNUA MAJI YA UZIMA.

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

Rudi nyumbani

Print this post

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Leo nataka tujifunze umuhimu wa kuchunguza mambo, kwani  tusipokuwa watu wa kuchunguza mambo basi tunaweza tusiuelewe uweza wa Mungu.

Asilimia kubwa ya watu wanaobarikiwa hawajui kuwa mafanikio yao ni kutokana na maombi ya watu wengine (ambao wanawaombea wao pasipo kujua), hivyo ni muhimu sana kufikiri wakati wa kufanikiwa.

Hebu tujifunze katika ile habari ya Kana ya Galilaya pale Bwana Yesu alipofanya muujiza wake wa kwanza wa kugeuza maji kuwa divai.

Maandiko yanasema baada ya Bwana Yesu kubadili yale maji kuwa divai, yule Mkuu wa meza, aliyeteuliwa kuandaa  vinywaji vya wageni wa kawaida na mgeni rasmi, hakujua kama ile divai mpya imetoka kwa Bwana, badala yake alidhani mwenye sherehe ndiye aliyeinunua, na ndipo akaenda kumfuata mwenye sherehe (Bwana harusi) na kumpongeza akidhani kuwa yeye ndiye kainunua ile divai mpya na kuwapa watu wote wanywe.

Na yule Bwana harusi naye akashangaa kupewa sifa ambazo si zake, huenda na yeye akadhani kuna mtu tu katikati ya sherehe kajitokeza na kujitolea kununua divai mpya ili kuimeza aibu.. kwamaana divai kuisha katikati ya sherehe na bado kuna watu wa muhimu hawajapata, ilikuwa ni aibu kubwa sana kwa wenye sherehe. Hivyo mpaka mwisho wa sherehe ni wachache sana ndio waliojua siri ya ile divai, kuwa na Bwana Yesu ndiye aliyeitoa.

Tusome,

Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.

2  Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.

3  Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.

4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.

5  Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.

6  Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.

7  Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.

8  Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.

9  Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,

10  akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa”.

 Sasa nataka tuone nyuma ya Baraka hizo alikuwa nani?, Nyuma ya muujiza huo alikuwa nani, na nyuma ya aliyetoa aibu alikuwa ni nani?.. kisha na sisi tutapata akili wakati wa kufanikiwa.

MWOMBAJI/ WAOMBAJI.

Kulipoonekana tatizo, Marimu alienda kumwomba Bwana na kumsihi sana. Huyu ndiye aliyekuwa mwanzo wa muujiza wa divai. Kama sio Mariamu watu wangeabika kwenye sherehe hata kama sherehe hiyo Kristo alikuwepo ndani.

Vile vile hata leo, ukiona jambo Fulani la heri limetokea mbele yako lililoziba aibu yako, hebu tafakari sana, usijivune wala usikimbilie kusema wewe ni mwenye bahati, huna bahati yoyote, hayo ni matokeo ya wengine kuomba kwaajili yako..haijalishi Kristo yupo na wewe.. Hata katika ile harusi Kristo alikuwepo ndani, alikuwa ni mwalikwa, lakini bado kama pasingekuwepo mwombaji, hakuna kitu kingefanyika.

Ukiona umebarikiwa kwa jambo Fulani au mambo yako fulani fulani yameenda sawa usikimbilie kujisifu, wala kujivuna, kwamba una bahati!!…fahamu kuwa hayo ni matokeo ya wengine kuomba kwaajili yako, na hao huenda unawajua au huwajui.

Mtoto ukifanikiwa jua wakati mwingine ni matokeo ya maombi ya wazazi wako na si kwasababu wewe una akili sana au una ujanja mwingi, kijana ukifanikiwa jua ni matokeo ya maombi ya ndugu zako, au wapendwa wenzako wanaokesha kwaajili yako pasipo wewe kujua.

Unapoona unapiga hatua kimaisha au kiroho, fahamu kuwa ni matokeo ya wanaokuongoza kiroho kukuombea, wala usidhani ni kwa nguvu zako au una bahati..

Waebrania 13:17  “Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi”

Ukilifahamu hili siku zote utakuwa mnyenyekevu na kumshukuru Mungu kwa kila jambo na pia kufikiri sana kuwaheshimu wanaokuombea na hata wewe kutenga muda kuwaombea!.. Laiti yule mkuu wa Meza na yule Bwana arusi wangejua kitu Mariamu alichowafanyia, kwenda kuwaombea kwa Bwana wangeshangaa sana, na kunyenyekea sana.

Laiti ungejua mambo watu wanayomwambia Bwana kuhusu wewe, usingebaki kama ulivyo..

Amani ya familia yako, Amani ya jamii yako, Amani ya nchi yako, ni matokeo ya maombi ya watu wengine wa Mungu wanaolia mbele zake usiku na mchana.. wala si kwasababu nyingine?, kama si hao ni kitambo sana mambo ya ulimwengu yangeshaharibika..(2Thesalonike 2:7).

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Rudi nyumbani

Print this post

SHUGHULIKA SANA NA DHAMBI YA KUSAHAU.

Nakusalimu katika jina kuu sana na lenye nguvu la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima ya Mungu wetu.

Sisi kama Wanadamu Kila mmoja wetu haijalishi ameokoka au hajaokoka, ndani yake ameumbiwa kiwango cha “kusahau”. Hii ni karama ya Mungu na ni vizuri kumshukuru Mungu Kwa jambo hili, kwasababu kama tungeikosa wanadamu wote tusingeishi hivi tulivyo Leo.

Lakini kusahau kukisimama Mahali pasipo-papasa, inageuka kuwa hatari kubwa sana, Tena dhambi yenye matokeo mabaya sana rohoni.

Kuna aina ngapi za kusahau?

Sasa kusahau kunaweza kuwa aidha kupoteza kumbukumbu ya lile jambo au tukio, Moja Kwa Moja akilini mwako, uwe kana kwamba hujawahi kulipitia. 

Au kunaweza kuwa kulipoteza tu Kwa muda katika kumbukumbu lakini utakapokumbushwa unalikumbuka Tena.

Kusahau kwenye madhara ni kupi?.

Kabla ya kutazama ‘kusahau’ kwenye hasara tuone kusahau kwenye faida kukoje.

Kusahau kwenye faida kunatimia katika mambo yasiyo na maana, au yenye maudhui hasi kwako. Kwa mfano pale mtu unapotukanwa, au unapopigwa kikumbo barabarani na mtu usiyemjua, unaposikia miziki isiyokufaidia huko nje, unapofiwa, unapodhulumiwa, unaposemwa, unapovunjiwa heshima, unapoaibishwa, unaposingiziwa n.k… Mazingira kama haya ambayo ni hasi…kusahau Kunahitajika sana na ni lazima ujifunze kuruhusu jambo hili liumbike ndani Yako ili uponyeke kwa haraka,.maana ndio sehemu yake hiyo inapopaswa itumike.

Lakini kusahau kusikokujenga ni pale unaposahau Matendo mema, au mambo chanya yakupasayo kutenda. Kwamfano Sheria inasema ” usitupe taka hapa” Halafu inapita wiki Moja umesahau agizo hilo, unarudia tena kutupa taka pale pale ulipokatazwa..Hapo utakuwa hujitafutii jambo lingine zaidi matatizo?

Vivyo hivyo katika Neno la Mungu pale unaposahau sahau Neno la Mungu hapo ndio pabaya sana. Wakristo wengi hatujui kuwa Mungu “anayorudia kutuambia ni mengi kuliko Yale mapya anayotaka kusema nasi”..Ni Kwanini? ni kwasababu tumekuwa wepesi wa kusahau Sheria zake.

Mambo yamekuwa kinyume chake, badala tusahau yaliyo mabaya tukumbuke yaliyo mema, tunasahau mema tunakumbuka mabaya sikuzote.

Ni shambuliko kubwa sana ambalo ibilisi amelipanda mioyoni mwa wanadamu. Ndio sababu uchungu haukomi, masengenyo hayaishi, vita vinazuka Kila siku, fitna, unafki, na uongo havina mwisho ni kwasababu Hali Ile Ile tuliyokuwa nayo nyuma mpaka sasa tunairuhusu ikae kwenye akili zetu.

Wakati nguvu hiyo tungepaswa tuitumie kulihifadhi Neno la Mungu mioyoni mwetu ili Matendo chanya yaendelea kutokea ndani yetu, hatufanyi hivyo.. maandiko yanasema..

Yakobo 1:22-25

[22]Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu.

[23]Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo.

[24]Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo.

[25]Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.

Tuweke mfano, tunaweza kusoma kwenye biblia kwamba Upendo hauhesabu mabaya, Wala haujivuni, Wala hauoni uchungu n.k(1Kor 13).. Sasa wakati uliposoma hili  neno, moyoni mwako unasema nitaliishi hili Neno, lakini inapita siku mbili unashangaa umerudia kule kule, unaanza ishi maisha ya namna Ile ya kwanza,. Tatizo lipo hapo kwenye kusahau. Laiti.hilo Neno lingekuwa limeganda viizuri kwenye moyo wako, ingekuwa breki pale tu mambo mabaya yanapojaribu kuvuka mipaka.

Sasa tunawezaje kuishinda Hali hii ya kusahau sahau?

Ni kama vile mwanafunzi darasani, mara nyingi anakuwa ni mtu wa.kurudia rudia kusoma na kufanyia sana mazoezi kile alichofundishwa..lengo la kufanya vile ni kulazimisha akili yake inakili Yale mafundisho kwa muda mrefu ili atakapoingia kwenye mtihani asisahau chochote…Lakini kama akisema Mimi ni ‘genius’ sina muda wa kurudia nilivyofundishwa..ni wazi kuwa mambo mengi yatamruka, na atafeli.

Hivyo na sisi sote ni wanafunzi wa Biblia. Soma biblia Kila siku ifanye kuwa rafiki Yako, usiwe mtu wa kusoma Leo, Tena wiki ijayo au mwezi ujao, ndio unakuja kusoma tena..SoMo tafakari mambo uliyoagizwa mule na Mungu Kila siku..Ndivyo itakavyokuwa rahisi kuliishi Neno la Mungu, kinyume na hapo usijidanganye Utasahau…kwasababu mwisho wa siku yatatoka moyoni mwako, na hivyo dhambi yoyote itakayokatisha mbele Yako, utashindwa kukabiliana nayo mapema. Mungu hapendi tuwe na tabia hii ya kusahau sahau Neno lake.

Kumbukumbu la Torati 6:6-9

[6]Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; [7]nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. [8]Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako. [9]Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako.

Piga vita kusahau Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu? Na je ni dhambi kuwa na Wivu?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

JE NI KUTII AU KUPATA KWANZA MAARIFA?

YESU ANA KIU NA WEWE.

DHAMBI YA MAUTI

PALE AHADI ZA MUNGU ZINAPOKUJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako (Mithali 27:23)

Haya ni Mafundisho maalumu Kwa ajili ya watumishi, ikiwa wewe ni kiongozi, askofu, mwalimu, mchungaji, mtume, mwinjilisti, unayesimama mahali fulani katika kulitazama kundi la Bwana, au jamii ya watu waliookoka, basi mafundisho haya ni maalumu kwako.

Biblia inasema;

Mithali 27:23

[23]Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako;  Na kuwaangalia sana ng’ombe zako.

Mchungaji Bora sikuzote anatambua ni wajibu wake kuwa karibu na mifugo yake wakati mwingi. Ili Kuhakikisha Mahali wanapolala ni salama, wanaogeshwa Kila wakati, wanapata chakula Bora, afya zao pia ni njema na wanachungwa Mahali salama.

 Kwamfano kama mchungaji akiwa Hana desturi ya kwenda zizini. Tunajua mifugo Kwa kawaida Huwa Haijui kujisafisha yenyewe, matokeo yake ni kwamba lile zizi litajaa vinyesi na mwisho wa siku watapata magonjwa na kufa, na hasara inaangukia kwa mchungaji?

Vilevile akiiachia mifugo yake ianze kujichunga yenyewe, inaenda popote iwezavyo kujitafutia chakula, bila shaka itapotea, kama sio kuibiwa, au kuliwa na wanyama wakali, au kula vitu visivyostahili.

Hivyo utaona ni sharti Mahali palipo na mifugo, hapapaswi kukosekana mchungaji hata kidogo. Hii inatufundisha sisi tulio watumishi, kuhakikisha tunafahamu Hali mbalimbali za watu wale tunaowaongoza.

Tunawajibu wa kuwapa chakula kizuri kitakachowakuza (yaani Neno la Mungu lisiloghoshiwa), tuna wajibu wa kuwalinda kiroho, dhidi ya mafundisho potofu na mitego ya ibilisi, Kwa kuwaonya na kuwakemea pale inapobidi wavukapo mipaka.

Tuna wajibu wa kuwaombea, tunawajibu wa kuwafariji na kuzijali Hali zao za mwilini katika maisha Yao ya kawaida.

Hivyo wewe kama kiongozi ikitokea upo mbali na kundi lako, usikawie sana, ukaliacha kundi lako ma-miezi na ma-miaka,bila kujua maendeleo yao, ukadhani kwamba litaweza kujichunga lenyewe, hiyo ni hatari..ni heri uwe mtu wa kwenda na kurudi, kwenda na kurudi… lakini pia ukiwa karibu nalo usiwe mlegevu kupeleka jicho lako Kila eneo la maisha Yao ya kiroho na ya kimwili, kuangalia ni wapi Pana mapungufu au  shida..ili kuondoa kasoro hizo, Ili kundi la Bwana listawi kama vile yeye atakavyo.

Ndio maana ya hili andiko Mithali 27:23 “Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako;  Na kuwaangalia sana ng’ombe zako”.

Ni wajibu wako kufanya hivyo, kwa hiari yako mwenyewe na sio kama unalazimishwa;

1 Petro 5:2

[2]lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

Kwanini Nuhu alimlaani Kaanani badala ya mtoto wake Hamu,

EPUKA MAKUNDI ILI UTAKATIFU WAKO UDUMU!.

FANYA KAMA UONAVYO VEMA.

ZIJUE TABIA ZA AHADI ZA MUNGU KWA MWAMINIO.

Rudi nyumbani

Print this post

Guruguru na Goromoe ni wanyama gani? (Walawi 11:30)

Jibu: Turejee.

Walawi 11:29 “Tena katika vitu vile vitambaavyo, vitambaavyo juu ya nchi, hivi ni najisi kwenu; kicheche, na panya, na mjombakaka, kwa aina zake, 

30 na GURUGURU na kenge, na mjusi na GOROMOE, na lumbwi. 

31 Wanyama hao ndio walio najisi kwenu katika hao watambaao; awaye yote atakayewagusa, wakiisha kufa, atakuwa ni najisi hata jioni”

Guruguru ni jamii ya mijusi wanaishi katika miti, tazama picha juu, na Goromoe ni mijusi wanaishi katika miamba au mchanga, tazama picha chini.

Kumjua Lumbwi ni mnyama gani fungua hapa >> Lumbwi ni nini katika biblia?

Viumbe hawa, Bwana Mungu aliagizwa wasiliwe katika Agano la kale, si kwasababu vilikuwa na sumu au madhara katika mwili, bali vilikuwa vimebeba tabia zinazowakilisha tabia za  jamii/ aina Fulani ambayo haikuwa inampendeza Bwana Mungu.

Na tulipoingia katika Agano jipya hakuna sheria tena ya kula au kutokula wanyama hao, maadamu hawana sumu kwenye mwili.

Kwahiyo Guruguru na Goromoe ni halali kuliwa kibiblia , ingawa si chakula kifaacho sana kwa jamii zote, ikiwa na maana kuwa kama ukiona havikufai vitu hivyo pia si dhambi kutovila, ingawa ni halali kuliwa.

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Lumbwi ni nini katika biblia?

Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Mafundisho maalumu Kwa ajili ya watumishi wa Mungu.

Huu ni mwendelezo wa mafundisho maalumu Kwa ajili watumishi wa Mungu, ikiwa wewe ni Mchungaji, mwalimu, mtume, askofu,Nabii, au mtu yoyote unayemtumikia Mungu katika nafasi yoyote kanisani au kwenye huduma basi mafundisho haya yatakufaa sana.

Wakati ule Yakobo alipodhamiria kwenda kukutana na ndugu yake Esau baada ya kutengana naye Kwa muda mrefu..maandiko yanasema walifurahi sana walipoonana kule nyikani. Na baada ya mazungumzo Yale kuisha,  sasa ikiwa ni wakati wao wa kuondoka pale nyikani walipokutana waelekee Kaanani.

Na kama tunavyosoma habari tunaona ndugu yake Esau alimshurutisha wasafiri pamoja naye. Ndipo Yakobo akamwambia Esau kuwa jambo hilo ni gumu kwake..kwasababu ya Hali ya makundi mbalimbali na watu na mifugo aliyokuwa nayo..Tusome..

Mwanzo 33:12-17

[12]Kisha Esau akamwambia, Twende zetu, tusafiri, nami nitakutangulia.

[13]Akamjibu, Bwana wangu anajua ya kuwa watoto ni wachanga, tena kondoo na ng’ombe nilio nao wanyonyesha. Hao wanyama wakiharakishwa siku moja, watakufa wote.

[14]Tafadhali bwana wangu na apite mbele ya mtumwa wake; nami nitawaongoza polepole kwa kadiri ya mwendo wa wanyama walio mbele yangu, na kwa kadiri ya mwendo wa watoto, hata nitakapofika kwa bwana wangu huko Seiri.

[15]Esau akasema, Nikuachie, basi, baadhi ya watu walio pamoja nami. Akasema, Pana haja gani? Na nione kibali tu machoni pa bwana wangu.

[16]Basi Esau akarudi siku ile ile akishika njia yake mpaka Seiri.

[17]Yakobo akaendelea mpaka Sukothi. Akajijengea nyumba, akawafanyia makundi yake vibanda. Kwa hiyo jina la mahali pale pakaitwa Sukothi.

Ni nini cha kujifunza hapo?

Yakobo alilitambua kundi analolichunga, alijua kuwa wapo watoto wachanga ndani yake, na mifugo pia michanga, Ambayo haijazoezwa kupelekwa mkiki mkiki, kwani ikilazimishwa kufanywa hivyo itakufa yote njiani. Hivyo akaomba muda wa kusafiri wake uongezwe, kusudi kwamba ayakokote taratibu taratibu mpaka yatakapofika kule Shekemu alipokuwa anapakusudia. Pengine mwendo wa siku moja tu ikamgharimu mwezi.

Tofauti na Esau yeye alikuwa na watu wa vita tu,watu walio hodari, Lakini Yakobo alikuwa na makundi yote. Na hivyo kwenda nayo taratibu taratibu ilimgharimu .

Hii ni kutufundisha asili ya msimamizi wa kweli, kwanza hulijali kundi lake, pia anakuwa tayari kuchukuliana na vile vyombo dhaifu. Kwasababu sio wote katika kanisa watakuwa na mwendo kama wa kwao, SI wote watakuwa wepesi kustahimili vishindo kama baadhi yao. Hivyo wewe kama kiongozi ni lazima ujifunze kuendana na makundi yote kama Musa kule jangwani, ili kisipotee chochote. Maana yake ni kuwa usiwe na haraka ya kufikisha kundi Mahali Fulani Kwa jinsi utakavyo, vinginevyo utawaua wengine.

Yakobo alipaita mahali pale Sukothi, kwasababu ndipo alipowajengea makundi yake vibanda. Na wewe pia jenga Sukothi yako.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

MAFUNDISHO YA NDOA.

MIGAWANYO MINNE (4), YA HUDUMA YA YESU.

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Rudi nyumbani

Print this post