yubile ni nini kwenye maandiko?

yubile ni nini kwenye maandiko?

Yubile, wengine huiita yubilei, au yubilii.

Ni mwaka wa hamsini (50), katika kalenda ya miaka ya kiyahudi. Mungu aliwaagiza wana wa Israeli, wahesabu miaka saba, kisha waizidishe mara saba,  7×7=49.

Na ule  unaofuata wa 50, uliitwa mwaka wa yubile.

Ni mwaka ambao Mungu aliwaagiza wapumzike kabisa, hawakuruhusiwa kupanda wala kuvuna. Kwa miaka miwili mfululizo(yaani mwaka wa 49 na ule wa 50), kwasababu ule wa 49 ni sabato ya kila mwaka wa 7, ndio maana miaka miwili inatokea hapo. Sasa swali la kujiuliza wangewezaje kuishi miaka yote miwili bila kufanya kazi? Jibu ni kwamba Mungu aliwabariki mara dufu katika mwaka wa 48, hivyo wakafanikiwa kukusanya vingi vya kuwatosha miaka yote hiyo miwili ijayo bila kazi.

Lakini pia ulikuwa ni mwaka wa kusamehe madeni sambamba na hilo ulikuwa mwaka pia wa kuwaachilia huru watumwa.

Walawi 25:8 Nawe utajihesabia Sabato saba za miaka, maana, miaka saba mara saba; zitakuwa ni siku za Sabato saba za miaka kwenu, maana miaka arobaini na kenda.

9 Ndipo utakapoipeleka pande zote hiyo baragumu yenye sauti kuu, siku ya kumi ya mwezi wa saba; katika siku hiyo ya upatanisho mtaipeleka baragumu katika nchi yenu yote.

10 Na mwaka wa hamsini mtautakasa, na kupiga mbiu ya kuachwa mahuru katika nchi yote kwa watu wote wanayokaa; itakuwa ni yubile kwenu, nanyi kila mtu atairudia milki yake mwenyewe, nanyi mtarejea kila mtu kwa jamaa yake.

11 Mwaka huo wa hamsini utakuwa ni yubile kwenu; msipande mbegu, wala msivune kitu hicho kimeacho chenyewe, wala msizitunde zabibu za mizabibu isiyopelewa.

12 Kwa kuwa ni yubile; utakuwa mwaka mtakatifu kwenu; mtakula maongeo yake yatokayo shambani.  13 Mwaka huo wa yubile mtairudia kila mtu milki yake.

14 Tena kama ukimwuzia jirani yako cho chote, au kununua cho chote mkononi mwa jirani yako, msidanganyane wenyewe kwa wenyewe;

15 kwa hesabu ya miaka iliyo baada ya yubile, ndivyo utakavyonunua kwa jirani yako, na kama hesabu ya miaka ya mavuno ndivyo atakavyokuuzia wewe

Yubile, ilifunua  kazi ya msalaba baadaye. Kwani Bwana wetu Yesu ndiye aliyekuja kutimiza kazi  hii rohoni.

Kwanza ndani yake tunapokea pumziko kamili la utumwa wa dhambi. Pili tunasamehewa deni zetu (dhambi zetu), Na Tatu tunafanywa huru, katika vifungo vya shetani. Yaani Magonjwa na mapepo.

Huo ndio mwaka wa Bwana uliokubaliwa, ndio Yubile yetu halisi.

lakini pia sisi kama waamini katika mwenendo wetu, tuna mambo ya kujifunza tuipatazampo Yubile?.

Kwanza ni umuhimu wa kupumzika, kuahirisha mambo yetu kupata muda na Mungu. Si tupate tu siku moja kwa wiki kuwa karibu na Mungu. Wakati mwingine Mungu anataka kipindi kirefu. Wewe kama mfanyakazi, au umejiajiri, jiwekee utaratibu baada ya kipindi fulani uwe na likizo ndefu ambayo unaitenga kwa Mungu wako,kuutafuta uso wake, ni muhimu sana.

pili tunajifunza kusamehe watu madeni yao. Si kila tunayemdai lazima atulipe, fikiria juu ya hilo. Yesu alisema achilieni nanyi mtaachiliwa. Hujui ni wapi na wewe sikumoja utakwama, na utatamani.uachiliwe.

na mwisho kuwapa uhuru watumwa wetu ikiwa wewe ni mwajiri, fikiria kuwa mfanyakazi wako anahitaji pumziko refua, mpatie, bila kumpunguzia mshahara wake. Bwana ataona umeitunza yubilee yake pia kimwili. Na sio kufanya kumbukizi ya ndoa, au kuzaliwa, hiyo sio yubilei.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Sikukuu ya kutabaruku ni ipi?

SIKUKUU YA VIBANDA.

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.

Kitabu cha Matendo ya mitume hakimtaji moja kwa moja mwandishi wake, lakini tunaweza kumtambua, kutokana na utambulisho wake mwanzoni mwa waraka huo, kwamba ni LUKA. Kwasababu waraka huu aliulekeza kwa mtu mmoja aliyeitwa Theofilo, ambaye anamtaja pia alimtumia waraka wa kwanza uliozungumzia habari za Yesu tangu mwanzo hadi siku alipochukuliwa juu, na huu si mwingine zaidi ya waraka wa Luka. Soma  Luka. (1:1-3)

Ndio maana inaaminika aliyeandika waraka huu ni Luka.

Matendo 1:1  Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, Theofilo, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha,

2  hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua;

3  wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.

Kitabu hichi cha matendo ya mitume, kama jina lake linavyojieleza kinaeleza hasaa jinsi mitume wa Bwana walivyoanza kulitekeleza lile agizo kuu la Yesu alilowaambia wakahubiri injili kwa kila kiumbe. Tangu Yerusalemu, uyahudi, samaria na dunia nzima.

Kinatufundisha jinsi Roho Mtakatifu alivyowaongoza hadi kukamilisha jukumu hilo la injili ulimwenguni mwote kwa mafanikio makubwa.

Na mambo ambayo tunajifunza kwao ni haya:

Umoja: Hawakuwa na nia tofauti tofauti, bali moja ya Kristo, walikubali kudumu katika fundisho la mitume bila shuku yoyote. Walifanya yote kwa ushirikiano kwasababu vitu vyote waligawana kama kila mtu alivyokuwa na hitaji lake.

Matendo 4:32  Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika.

Mashauri ya pamoja:  Hata mahali ambapo hakukueleweka vema, au kutokea kwa mikanganyiko waliweza kukaa katika Baraza la wazee na mitume, kutafakari kwa pamoja ndipo hekima ya Roho ikaamua yawapasayo kutenda.(Matendo 15: 1-21).Ndio maana hawakuwa na madhehebu.

Furaha ya Roho: Kanisa lilifurahia ibada, na imani ndani ya Kristo. Sio la watu ambao walisukumwa kufanya majukumu yao, bali wote waliona ni raha kumfuata Kristo kwa moyo mweupe.

Matendo 2:46  Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe

Maombi: Mara nyingi walidumu katika maombi,  hekaluni, na manyumbani mwao (Watendo 1:14)

Upendo: Walipendana, Waliweza kuwa na vitu vyote shirika, hawakubaguana, wala kuwa na ubinafsi kiasi kwamba hakukuwa na yoyote aliyekuwa na mahitaji ndani ya kanisa.

Matendo 2:44  Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika, 45  wakiuza mali zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja

Uvumilivu: Walipitia dhiki, wengine wapigwa mawe, waliburutwa, lakini hawakuitupilia mbali imani, kinyume chake ndio injili walizidi kuihubiri.

Matendo 8:1,4

 1  Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume…..4  Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.Hivyo hayo ni baadhi ya mambo ambayo na sisi tunaweza kujifunza katika kanisa la mwanzo.

Je! Umeokoka?

Kama bado unasubiri nini? Kumbuka hizi ni siku za mwisho. Tubu dhambi zao leo, mwamini Yesu, ukabatizwe akusamehe dhambi zako, Ikiwa utapenda kupata msaada huo wa kumpokea Kristo, basi fungua hapa kwa mwongozo huo >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUJIFUNUA KWA YESU KWA PILI.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

Mwandishi wa kitabu cha Mithali ni nani?

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Wafalme

Rudi Nyumbani

Print this post

UKWELI KUHUSU UISLAMU, Sehemu ya Tatu: Kisima cha Zamzam.

Kisima cha Zamzam ni nini, na ukweli wake ni upi?


Angalizo: Makala hii haina lengo la kushambulia Imani Fulani, wala kushabikia Imani Fulani, pia haina lengo la kumchafua mtu yoyote, wala kumdhalilisha, bali kutoa elimu sahihi kuhusiana na tunayoamini na yanayoaminiwa.


Kisima cha “Zamzam”, ni kisima kilichopo katika msikiti wa Al Haram uliopo Makka, katika nchi ya Saudi Arabia. Kisima hiki kipo umbali mfupi kutoka katika jiwe/jabali jeusi la Kaaba. (umbali wa mita 20 mashariki mwa jiwe hilo).

Kulingana na Uislamu, kisima hiko kilijitokeza hapo kimiujiza kipindi kile Hajiri kijakazi wa Sara alipoachwa na Abramu katika lile jangwa (katika vilima vya Safa na Marwah) na akakosa maji ya kunywa yeye na mwanae Ismaili.

Na Hajiri alipoona mwanae anakaribia kufa, akaanza kuzunguka vilima hivyo vya Safa na Marwah mara saba, na alipokuwa katika mzunguko wa saba, ndipo Malaika Jibra’il (Gabrieli) akatokea na kukitokeza kisima hiko kimiujiza na kilipotokea, Hajiri akaanza kusema zamzam, maana yake “acha kutiririka”

Hadithi za kiislamu zinazidi kusema kuwa kisima hiko kilikauka, lakini kikaja kuvumbuliwa tena na babu yake Muhamad aliyeitwa Muttalib katika karne ya sita(6).

Lakini pia binamu yake Muhamad aliyeitwa “Ibn Abbas” alisema “Maji ya zamzam yanafaa kwa nia yoyote ile, mtu akinywa kwa lengo la kupona ugonjwa basi mungu atamponyesha kupita maji hayo, kama mtu atakunywa kwa lengo la kuondoa njaa, basi mungu ataiondoa njaa yake, kama mtu atayanywa kwa lengo la kukata kiu basi mungu ataikata kiu yake kwasababu hata Ismail alikunywa maji hayo na kukata kiu yake kali”.

Na kwasababu hiyo maelfu ya watu wanayatumia maji hayo wakiamini yamebeba uponyaji wa kimungu ndani yake??. (Je ukweli wa mambo haya ni upi)?

Awali ya yote tufahamu kuwa Ishamaeli, mwana wa Hajiri hakuwa mwana wa Ahadi kulingana na biblia, hali ISAKA, mwana wa Sara ndiye aliyekuwa mwana wa Ahadi.  Hadithi zote zilizopo na zinazotungwa zinazoshinikiza kuwa Ishamaeli ndiye mwana wa Ahadi, si za kweli.

Ishmaeli aliahidiwa Baraka nyingine za Mungu lakini si za Mzaliwa wa kwanza. Baraka za mzaliwa wa kwanza zilikuwa kwa Isaka aliyekuwa mwana wa Sara.

Sasa ukweli wa kisima hiko kibiblia ni upi na je kuna muujiza wowote katika kisima hiko?

Habari ya kisima hiko, ambako biblia haisemi kwamba kinaitwa “Zamzam” inapatikana katika kitabu kile cha Mwanzo 21, Hebu tuianzie ile habari mbali kidogo katika ule mstari wa 9 ili tuielewe habari..

Mwanzo 21:9 “Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka.

10 Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.

11 Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe.

12 Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.

13 Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako.

14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.

15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.

16 akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia.

17 MUNGU AKASIKIA SAUTI YA KIJANA. MALAIKA WA MUNGU AKAMWITA HAJIRI KUTOKA MBINGUNI, AKAMWAMBIA, UNA NINI, HAJIRI? USIOGOPE, MAANA MUNGU AMESIKIA SAUTI YA KIJANA HUKO ALIKO.

18 ONDOKA, UKAMWINUE KIJANA, UKAMSHIKE MKONONI MWAKO, KWA KUWA NITAMFANYA KUWA TAIFA KUBWA. 

19 mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.

20 mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.

21 akakaa katika jangwa la parani; mama yake akamtwalia mke katika nchi ya misri”.

Sasa kulingana na maandiko hayo matakatifu, ni Dhahiri kuwa Ishmaeli (au Ismail), hakuwa mwana wa ahadi ndio maana aliondolewa katika hema ya Sara, na Mungu alikuwa upande wa Sara. Lakini kwasababu Mungu ni wa rehema asingeweza kumwacha kabisa Hajiri na Ishamaeli kwani nao pia ni uzao wa Ibrahimu, ndio maana akawaokoa na mauti katika jangwa lile lisilo na maji.

Na utaona Malaika wa Mungu alimfumbua macho Hajiri ili akione kisima, na si kwa “alikitokeza kisima kile kimiujiza”.. Maana yake ni kwamba kisima kile tayari kilikuwepo pale, isipokuwa macho ya Hajiri hayakukiona, na yalipofumbuliwa ndipo akakiona na kumshukuru Mungu.

Sasa swali la Msingi ni hili, je kisima hiko kiliendelea kuwepo?, na je Mungu aliagiza chochote juu ya kisima hiko, kwamba watu waende huko kuchota maji yake?

Jibu ni kwamba kisima hiko kiliendelea kuwepo, kwasababu kilikuwepo kabla ya hapo pia!..na ulipofika wakati kilipotea kama tu visima vingine vilivyopotea… Na wala maji yake hayakuwa na muujiza wowote kwa Ishmaeli Zaidi ya maji mengine yoyote.

Yale yalikuwa ni maji ya kawaida tu, ambayo mtu akinywa anakata kiu, na ndilo lililokuwa lengo la Mungu, kwa Hajiri na Ishmaeli, kwamba wanywe wakate kiu basi, waweze kuokoka na mauti ya kukosa maji, na si kwamba wakifanye kuwa kisima kitakatifu cha kufanyia ibada.

Sasa kulingana na hadithi za kiislamu, wanakiri kuwa kilipotea hiko kisima, lakini ajabu ni kwamba kimekuja kugunduliwa na kufukuliwa karne ya 6, (Jambo hilo si kweli, ni uongo wa adui).

Huenda hiko kisima kilichopo sasahivi ni kisima tu kilichoibuliwa na watu, na zaidi hata kama kingekuwa ni chenyewe (halisi) kile alichoonyeshwa Hajiri na Malaika, kisingekuwa na Uungu wowote ndani yake kwani Mungu hajawahi kuweka agano lake katika visima! Au mito au bahari.

Ingekuwa ndivyo basi ule mto Yordani ambao Naamani-Mkoma aliokwenda kuoga mara saba na ukoma wake kuondoka basi hata leo wakoma na wagonjwa wangetiririka pale kuoga ili kupona magonjwa yao…

2Wafalme 5:9 “Basi Naamani akaja na farasi wake na magari yake, akasimama mlangoni pa nyumba ya Elisha.

10 Naye Elisha akampelekea mjumbe, akisema, Enenda ukaoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itakurudia, nawe utakuwa safi………………

14 Ndipo akashuka, akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; nayo nyama ya mwili wake ikarudi ikawa kama nyama ya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi”.

Sasa huo ni mto Yordani ambao mpaka leo upo! Na ndio mto Bwana YESU aliobatizwa na Mbingu zikafunuka juu yake kumshuhudia.. Lakini maji yake leo hayawezi kutumika kama maji ya kiungu.. Vipi hayo mengine?.

Na pia kisima hiko cha Hajiri hakikuwepo Saudi Arabia, bali kilikuwepo Parani katika jangwa la Sinai.

Kwahiyo maji hayo ya zamzam, yanayotoka huko Saudi Arabia, (Makka), si maji ya kiungu na  mkristo/asiye mkristo hapaswi kuyatumia kwa matumizi yoyote, matokeo ya kutumia maji hayo kwa lengo la kupata uponyaji, au utatuzi wa tatizo lingine lolote ni KUONGEZA TATIZO HILO!.

Inasadikika pia maji haya yanatumika katika baadhi ya misiba, (yanatiwa katika vyakula vya misibani), na katika baadhi ya vyakula vya biashara, na matumizi mengine,

Ikiwa unahudhuria mazishi yoyote yale (yawe ya kikristo au sio ya kikristo), hakikisha unatakasa vyakula vyote kwa Imani kwa damu ya YESU kabla ya kula!.. Usile tu!..Vile vile kila ununuacho kama bidhaa ya chakula, pasipo kujua asili ya utengenezaji wake, kabla ya matumizi, takasa kwa Imani kwa damu ya YESU.

Lakini si maji ya zamzam tu yenye shida kiroho, bali pia na maji yajulikanayo kama “ya upako yauzwayo katika baadhi ya makanisa”..yote yanabeba sifa moja na haya ya ZAMZAM.

Ukiona maji yanauzwa kwa kivuli cha upako, kwamba uyatumiapo utapata uponyaji au ufunguzi!, kuwa makini sana!.

Watumishi wa kweli wa Mungu, wanatumia maji kwa uongozo maalumu wa Roho Mtakatifu, na si kama utaratibu au mwenendo wa mara zote, kwamba kila tatizo ni maji na tena yanauzwa!, na tena yanaaminishwa kuwa ndio kitu kiponyacho!, hayo ni mafundisho ya ibilisi, ambayo ni muhimu kuwa nayo makini!.

Ukikuta maji yanauzwa usinunue!, ukikuta mafuta yanauzwa usinunue!..Ibilisi ni yule yule, anayefanya kazi kwenye kila kitu kilicho kinyume na Neno la Mungu.

Usikose Makala zijazo…

Je umempokea YESU kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako?..kumbuka yeye pekee ndiye Njia ya kufika mbinguni, na si mwanadamu yoyote aliye hai au aliyekufa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya kwanza: (Msikiti wa AL-Aqsa).

HAJIRI NI KAMA MLIMA SINAI ULIOKO ARABUNI.

JE! NI CHEMCHEMI IPI INATOKA NDANI YAKO, YA MITO AU YA KISIMA?

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.

SWALI: Naomba kufahamu maana ya 1Wakorintho 15:24-25 , hususani hapo anaposema ‘hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake. 26  Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti’.

1Wakorintho 15:24  Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.

25  Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.

26  Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.


JIBU: Bwana Yesu alikuja duniani kwa kazi maalumu ya kumkomboa mwanadamu pamoja na kumkamilisha. Na ukombozi huu, aliukamilisha wote siku ile pale msalabani kwa kifo chake. Hivyo tangu wakati ule mwanadamu ambaye atampokea, tayari maadui zake wote wamewekwa chini yake, ikiwemo na mauti yenyewe.

Lakini pia ni muhimu kufahamu, ukamilifu wa ukombozi wetu, sio sasa, kwasababu ijapokuwa tumeokolewa na ndani yetu tuna uzima wa milele, bado tutakufa (ki-mwili), bado tutaugua, bado tutazeeka, bado tutakula kwa taabu, bado tutapitia dhiki na masumbufu, bado tutakutana na uovu kila mahali tuendapo.

Hivyo ‘ukamilifu’ wetu kabisa kabisa bado. Lakini ‘ukombozi’ wetu tayari, tunaokoka tukiwa hapa hapa duniani, tukifa tunakuwa tunaishi. Sasa Ndio maana Yesu alikuja mara ya kwanza kama MWANAKONDOO achukuaye dhambi za ulimwengu, lakini pia atarudi mara ya pili, ambapo safari hii atakuja kama MFALME, Atawalaye kwa mamlaka na nguvu nyingi.

Safari hii atakuja sasa kwa ajili ya huo ukamilifu, kwanza atayahukumu  mataifa na falme zao,(Mathayo 25:31-46) vilevile mapepo (Ufunuo 19:20), kisha ataurekebisha huu ulimwengu ulioharibika,(Ufunuo 6:12-17) na kuufanya kuwa zaidi hata ya edeni. Kisha atatawala na watakatifu wake, kwa kipindi cha miaka elfu moja (Ndio ule utawala wa amani wa Kristo wa miaka 1000), Ufunuo 20, hapa hapa duniani, kwa wakati huo dhiki nyingi sana zitaondoka, watu wataishi muda mrefu sana, biblia inasema mtu atakayekufa na miaka mia ataitwa mtoto mchanga,(Isaya 65:20) wanyama hawatakuwa wakali tena, , hakutakuwa na laana ya nchi kutoa miiba, wala kuzaa kwa uchungu. Hichi ni kipindi ambacho dunia itakuwa salama na tulivu sana. Ni wakati wa Raha ambao Yesu amewaandalia watumishi wake.

Lakini wapo baaadhi watakufa (lakini sio sisi tutakaonyakuliwa), kwasababu shetani alikuwa bado hajahukumiwa amefungwa tu, hicho ndio kipindi ambacho Kristo atakwenda kutokomoza mauti ya mwili, hivyo shetani atafunguliwa kwa muda, ajaribu kuwaangusha watakatifu, atashindwa na kutupwa kwenye ziwa la moto pamoja na watu wote waovu (Ufunuo 20:7-10). Hapo ndipo mwisho wa yote, hakuna tena mauti, wala kifo, wala uchungu, wala huzuni,. Yesu atayakamilisha yote, ambapo adui wa mwisho ndio huyo mauti ya mwili.

Ufunuo 21:1  Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2  Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.

3  Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.

4  Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.

5  Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.

6  Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure

Wakati huo ndio Kristo atakuwa ameikamilisha kazi yake yote, na kumrudishia Baba ufalme wote, kama ilivyokuwa kule mwanzo, ili tumwabudu Mungu, sio  katika kukombolewa, au kuchungwa, au katika kuongozwa tena, katika ile mbingu mpya na nchi mpya, Huduma ya Kristo itakuwa imeisha.

Yatakuwa makao yetu milele. Mambo ambayo tumeandaliwa huko ndugu, jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia. Unasubiri nini leo usimpe Bwana maisha yako? Kumbuka tunaishi katika nyakati ambazo Kristo amekaribia sana kurudi. Moja ya hizi siku parapanda italia, tutakwenda mbinguni. Tubu dhambi zako, mwamini Yesu, upokee uzima wa milele.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000

SIFA SITA (6), ZINAZOIKAMILISHA ILE SIKU YA BWANA ITISHAYO.

ILI TUONEKANE WAKAMILIFU MBELE ZA MUNGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

KILINDI CHAPIGIA KELELE KILINDI.

Zaburi 42:7

[7]Kilindi chapigia kelele kilindi kwa sauti ya maboromoko ya maji yako, Gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tutafakari pamoja Neno la Mungu.

Biblia inatuambia kila jambo tunalolifanya lina matokeo sawa rohoni. Ikiwa wewe ni mwizi malipo ya wizi utayapata rohoni, ikiwa wewe ni muuaji, malipo ya uuwaji utayapokea vilevile rohoni, mito ya maji inapoelekea huko huko ndipo inaporudia.

Ufunuo 13:10

Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.

Sasa hapo tumeona katika eneo la ubaya, je vipi katika upande wa Mema?

Maandiko hayo hayo yanatuambia kwamba Kilindi hupigia kelele kilindi.

maana yake ni nini?

kilindi ni mahali pa katikati kabisa mwa bahari. Sasa mwandishi wa zaburi  anatumia mifano ya kitu halisi kana kwamba kinaongea… anasema Kinaita chapigia kelele kilindi. Na cha kushangaza ni kwamba hakiiti eneo lingine lolote la maji labda ufukweni.. au kwenye rasi, au ghuba.. hapana bali kinapigia kelele kilindi chenzake.

Kilindi chapigia kelele kilindi

Maana yake ni nini?

Tukitaka mambo ya ndani ya Mungu, mambo ya vilindini, lazima na sisi tuwe vilindini. Ni muunganiko wa ki-Mungu. kila kiwango kina sauti yake. kamwe hizo sauti haziingiliani, ni sawa na mbwa amwite tai kwa sauti yake ya kubweka, haiwezekani kuja inahitaji, ajifunze sauti yake ili yule tai aelewe, vinginevyo atakuwa anapiga kelele tu.

Na sisi vivyo hivyo kwa Mungu, wengi tunatamani tumwone Mungu kwa undani katika maisha yetu, lakini hatutaki tuzame ndani yake.

Mwandishi wa Zaburi mwanzoni kabisa kabla hajasema maneno hayo kwenye hiyo sura 42 anasema

Zaburi 42:2-3

[2]Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai, Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?

[3]Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako.

Kuonyesha ni mtu ambaye alimtamani sana Mungu wake.

Sehemu nyingine Daudi anasema..

Zaburi 63:1-8

[1]Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,

Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.

[2]Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu, Nizione nguvu zako na utukufu wako.

[3]Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.

[4]Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.

[5]Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono; Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.

[6]Ninapokukumbuka kitandani mwangu, Nakutafakari Wewe makesha yote ya usiku.

[7]Maana Wewe umekuwa msaada wangu, Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.

[8]Nafsi yangu inakuandama sana; Mkono wako wa kuume unanitegemeza.

Umeona, usiku kucha, anamtafakari Mungu, kuonyesha ni mtu ambaye moyo wake upo kwa Mungu asilimia mia..unategemea vipi mtu kama huyo Mungu asijifunue kwake kwa viwango vile?

Nafasi hii pia mimi na wewe tunayo. Tumfuate Mungu wetu vilindini, ili ajifunue kwetu katika viwango vingine..

Na hiyo inakuja kwa kile Bwana Yesu alichosema..Tujitwike misalaba yetu tumfuate, tuwe tayari kuacha vyote visivyompendeza yeye na kumtii. Na kwa kufanya hivyo rohoni tunatafsirika kuwa tunamwita Mungu wa vilindini.

Anza sasa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

Ni kelele gani zinazozungumziwa hapo katika Waefeso 4:31.

NIONDOLEENI KELELE ZA NYIMBO ZENU (Amosi 5:23)

Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?

Rudi Nyumbani

Print this post

UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya Pili: (Jiwe/Jabali la Kaaba).

Je “Kaaba” ni nini na ipo kwenye biblia?, Na wanyama wanaochinjwa kuelekea Kaaba je tunaruhusiwa kuwala?.

Angalizo: Makala hii haina lengo la kushambulia Imani Fulani, wala kushabikia Imani Fulani, pia haina lengo la kumchafua mtu yoyote, wala kumdhalilisha, bali kutoa elimu sahihi kuhusiana na tunayoamini na yanayoaminiwa.


Kama hujapitia sehemu ya kwanza ya Makala hii, inayohusu msikiti wa Al-Aqsa uliopo Yerusalemu pamoja na unabii wake basi waweza fungua hapa >>> UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya kwanza: (Msikiti wa AL-Aqsa).

Leo tunaendelea na sehemu ya pili, na tutalitazama “Jiwe la Kaaba” na uhusiano wake na Imani ya kikristo.

“Kaaba” au kwa jina lingine al-Ka’ba al-Musharrafa ni jengo la “Jiwe Jeusi” lililopo katikati ya msikiti uitwao “Masjid al-Haram” uliopo mahali pajulikanapo kama “Makka”, huko nchini Saudi Arabia.

Jiwe hili linaaminika na dini ya kiislamu kuwa “nyumba ya mungu”. Na pia linaaminika kuwa ni ufunuo Mungu aliompa Abramu (Ibrahimu) pamoja na Ishaeli mwanae kama mahali pekee na sahihi alipopachagua Mungu pa kuabudia, kulingana na Quran, Al Imran 3:96 (Sasa kujua ukweli wa jambo hili kibiblia soma Makala hii mpaka mwisho).

Zaidi inaaminika kuwa mahali hapo “Kaaba (hapo Makka)” ndipo mahali ambapo Malaika walikuwa wakimwabudu Mungu kabla ya mwanadamu kuubwa, na baadaye mwanadamu alipoumbwa ndipo Adamu akapajenga tena mahali hapo kama sehemu ya kumwabudu Mungu, na baadaye baada ya mafuriko ya Nuhu mahali hapo pakapotea, pakawa hapajulikani, na alipotokea Ibrahimu ndio akapata ufunuo wa mahali hapo (kujua usahihi na ukweli wa jambo hili kibiblia soma Makala hii mpaka mwisho).

Baadaye kulingana na imani ya kiislamu, Abramu (Ibrahimu), aliambiwa awaambie wageni wote kutoka uarabuni na kila mahali wasafiri na kufika hapo kuhiji, na hiyo ndio sababu ya watu wa Imani ya kiislamu kuwasili huko Makka kuhiji kila mwaka.

Na si tu watu kuwasili pale, bali pia wanyama wachinjwapo wanaelekezwa (kibla) huko Maaka palipo na Kaaba.

Swali?.. Je ukweli wa mambo huu ni upi?

Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa Mwana wa Ahadi alikuwa ni Isaka mzao wa Sara, na si Ishmaeli aliyekuwa mzao wa kijakazi Hajiri.. Ingawa Mungu alimbariki pia Ishmaeli mwana wa Hajiri, lakini hakuwa amekusudiwa kubeba ahadi yoyote ya urithi wa mzaliwa wa kwanza, kwanini?.. kwasababu hakuwa mwana wa mke halali wa kwanza wa Abramu, na hiyo ndio sababu ya Sara kumfukuza Hajiri, na Mungu akawa upande wa Sara.

Mwanzo 21:9 “Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka.

10 Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.

11 Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe.

12 Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.

13 Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako.

14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba”.

Sasa Imani ya kiislamu inaamini kuwa Ishmaeli(au Ismail) ndiye mwana wa ahadi halali wa Abramu, na biblia haisemi hivyo, na hapa ndipo MAKOSA YALIPOANZIA!!!!...Ndipo adui alipoanza kutengeneza MTI WAKE!!.

Na kwasababu hiyo, ya kuamini kuwa Ishmaeli ndiye mwana wa ahadi na si Isaka, basi ndipo zikazuka habari nyingine zisizo za kweli kwamba Abramu alishuka mpaka Makka na kupewa ufunuo uliopotea zamani kuwa mahali pa kuabudia ni hapo Makka, na pia zikatengenezwa habari nyingine kuhusiana na kisima maarufu kijulikanacho kama ZAMZAM, ambacho tutakuja kukiangalia katika Makala inayofuata na hatari yake kiroho.

Ukweli ni kwamba Abramu baada ya kumruhusu Hajiri aondoke na Ishmaeli, hakuendelea kufuatilia habari zake kwani Mungu alishamwambia amsikilize Sara, na ajihusishe na Isaka Zaidi ya Ishmaeli, hivyo si kweli kwamba Abramu aliwahi kushuka Saudi Arabia akiwa na Ishmaeli na kupewa ufunuo wa mahali hapo Makka, na hata biblia haionyeshi mahali popote jambo hilo.

Zaidi biblia inaeleza wazi kuwa baada ya Isaka kumzaa Yakobo, na Yakobo kulizaa Taifa la Israeli, kupitia Taifa hilo la Israeli alitokea Mfalme Daudi, ambaye baada ya kumpendeza sana Mungu, ndipo Mungu akauchagua mji wake Daudi (yaani Yerusalemu) uwe mahali pa kuweka nyumba yake na jina lake, na mahali pa kuabudia mpaka nyakati zake Masihi (yaani YESU).

2Nyakati 6:5 ”Tangu siku ile nilipowatoa watu wangu katika nchi ya Misri, sikuchagua mji wo wote wa kabila zote za Israeli ili kujenga nyumba, jina langu liwe humo; wala sikumchagua mtu ye yote awe mkuu juu ya watu wangu Israeli;

6 LAKINI NIMEUCHAGUA YERUSALEMU, JINA LANGU LIWE HUMO; NA DAUDI NIMEMCHAGUA AWE JUU YA WATU WANGU ISRAELI”.

Na tangu wakati ambapo Hekalu la Mungu lijengwe na Sulemani, mwana wa Daudi pale Yerusalemu, wenye Imani ya kiyahudi ndio walikuwa wanatoka Mataifa mbali mbali kwenda kuabudu pale, kwamaana ndio mahali alipopachagua Mungu aliweke jina lake.

Na hata watu wakiwa mbali walikuwa wanaabudu kuelekea Yerusalemu mahali hekalu lile lilipojengwa, mfano wake ni nabii Danieli katika Danieli 6:10, soma pia 1Wafalme 8:29-30.

Hivyo watu waliendelea kuwasili Yerusalemu mahali pale ambapo Mungu alipachagua, kwa miaka mingi ndio maana hata kibla ya kwanza ya uislamu ilikuwa ni hapo hapo Yerusalemu, walipokuja kujenga msikiti,  mahali hekalu lilipojengwa, ingawa walikuja kugeuza na kusema si hapo tena bali ni Makka, penye “Kaaba”.

Na Masihi alipokuja (YAANI YESU KRISTO) ndipo atakapoonyesha sehemu sahihi ya kuabudia, alipopachagua MUNGU kabla ya kuwekwa misingi ya Ulimwengu, na kwamba watu wote wakusanyike hapo ili wamwabudu MUNGU sawasawa na mapenzi yake.

Kwani watu wote walijua kuwa siku Masihi atakapokuja atasahihisha mambo yote, na kuonyesha njia sahihi, sasa njia hiyo ni ipi?? Tusome maandiko yafuatayo..

Yohana 4:19 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

20  Baba zetu waliabudu katika mlima huu, NANYI HUSEMA YA KWAMBA HUKO YERUSALEMU NI MAHALI PATUPASAPO KUABUDIA.

21  Yesu akamwambia, MAMA, UNISADIKI, SAA INAKUJA AMBAYO HAMTAMWABUDU BABA KATIKA MLIMA HUU, WALA KULE YERUSALEMU.

22  Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23  Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo WAABUDUO HALISI WATAMWABUDU BABA KATIKA ROHO NA KWELI. KWA MAANA BABA AWATAFUTA WATU KAMA HAO WAMWABUDU

24  Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

25  Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.

26  Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye”.

Umeona mahali sahihi alipopachagua Mungu pa Ibada?.. Si Yerusalemu tena, wala mahali pengine popote bali ni katika Roho Mtakatifu, na katika kweli ya MUNGU.

Maana yake kama mtu hana Roho Mtakatifu ndani yake basi hawezi kuwa na ibada halisi, kama hawezi kuutunza mwili wake na roho yake, basi hakuna mahali pengine popote duniani atakapoweza kumfanyia Mungu ibada akaikubali, kwasababu maandiko yanasema miili yetu ni HEKALU la ROHO MTAKATIFU (Soma 1Wakorintho 3:16 na 1Wakorintho 6:19).

Na Hekalu tafsiri yake ni sehemu ya nyumba ya ibada, hivyo ibada ya kwanza inaanza ndani ya mtu, hiyo ikiharibiwa mtu huyo hata aende wapi hawezi kumwona MUNGU wala kukutana na MUNGU, hata apae juu ya sayari zote, bado atakuwa mbali na Mungu na maombi yake hayasikilizwi.

Lakini kama akitakasika katika utu wake wa ndani na wa nje, basi mahali popote pale alipo ibada itakuwa inabubujika ndani yake, na hiyo ndio siri ya agano jipya.

Sasa swali ni je!, Wanaoenda Yerusalemu au Makka wanafanya makosa?

Kama mtu ataenda Yerusalemu kwa lengo la utalii, au kujifunza mambo, na pengine kumshukuru Mungu kwa atakayojifunza…hafanyi makosa lakini kama ni kwa lengo la Ibada, akiamini kuwa ile ni ardhi takatifu, hivyo atakokea kitu cha ziada, anakosea sana kwasababu Bwana Yesu alishasema.. saa yaja, nayo ipo, kwamba waabuduo halisi hawataenda tena Yerusalemu, bali watamwabudu katika roho na kweli.

Vile vile wanaoenda kuhiji Makka, wapo nje ya Imani kabisa, kwasababu hata huko Makka hapajaagizwa kabisa na Mungu, ni ufunuo wa ibilisi uliosambaa ili kuwafanya watu wasimwabudu MUNGU WA KWELI katika roho na kweli, badala yake katika makosa makubwa. Hivyo wanaokwenda kuhiji Makka wanahitaji msaada wa kumjua YESU, na NEEMA yake, ili watoke katika hayo makosa.

Hali kadhalika hakuna agizo lolote la mnyama achinjwapo basi aelekezwe Yerusalemu wala Makka, hayo pia ni maagizo ya ibilisi, ambayo yanalengo la kuingiza roho katika vile tuvilavyo.

Ikiwa nyama inauzwa buchani, Mkristo anaweza kuinunua akiongozwa na Amani ya Roho mtakatifu, na baada ya kuinunua anaweza kuitakasa kwa maombi, kisha akaitumia, lakini kama katika bucha hilo, wauzaji wamekiri waziwazi kuwa nyama hiyo imechinjwa kwa kuelekezwa kibla yoyote ile iwe ya Yerusalemu au Makka au penginepo popote nyama hiyo usinunue wala usile, kwasababu ya Dhamiri, ndivyo maandiko yasemavyo..

1Wakorintho 10:25 “Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri;

26  maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo

27  Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.

28  Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri.

29  Nasema, dhamiri, lakini si yako, bali ya yule mwingine. Maana kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?”

Usikose mwendelezo wa sehemu inayofuata wa Kisima cha Zamzam, na mengineyo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

MJUE SANA YESU KRISTO.

DANIELI: Mlango wa 9

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Tafsiri ya Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.

14 Nami nitaonekana kwenu, asema Bwana, nami nitawarudisha watu wenu waliofungwa, nami nitawakusanya ninyi, nikiwatoa katika mataifa yote, na katika mahali pote, nilikowafukuza, asema Bwana; nami nitawaleta tena, hata mahali ambapo kutoka hapo naliwafanya mchukuliwe mateka

Huu ni utabiri ambao Mungu aliwaambia Israeli, pindi tu walipochukuliwa utumwani Babeli, akiwaahidia atawarudisha tena kwenye nchi yao baada ya miaka sabini. Na zaidi ya hayo akawapa pia na Neno la ahadi kwamba wakati huo wakimtafuta kwa mioyo yao yote, watamwona, watamwomba atawasikia, na wote watarejeshwa nyumbani ijapokuwa walichukuliwa mbali sana.

Na kweli utabiri huo ulikuja kutumia, kwani mwishoni mwa hiyo miaka sabini, mbiu ilipigwa waisraeli wote warudishwe kwao. Na aliwaonekania sana pindi waliporejea.

Ni neno la ahadi hata kwetu,

Kwamba tukimtafuta yeye kwa mioyo yetu yote, tutamwona. Kumbuka anasema “MIOYO YETU YOTE”. Kosa linatokea pale tunapompenda Mungu kwa sehemu, leo kwake kesho kwa shetani. Ndio Inayopelekea tusimwone Mungu katika ukamilifu wake wote. Mungu anahitaji vyako vyote vielekee kwake, ndipo tumwombe na kumwita ili atuitikie..

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

Nini Maana ya Adamu?

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

Rudi Nyumbani

Print this post

MAFUNZO YA BIBLIA KWA WATOTO

Darasa la Kwanza:

KUIFUNGUA BIBLIA.

DARASA LA TANO -Fanyeni yote kwa jina la Yesu Kristo

 

DARASA LA SITA: TABIA YA YUSUFU

DARASA LA SABA: KUANGAZA NURU YA KRISTO

Mwendelezo unakuja…..

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAOMBI YA KUOMBEA WATOTO.

NINYI AKINA BABA MSIWACHOKOZE WATOTO WENU

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Utatu mtakatifu upo kibiblia?

Katika mapokeo ya kikristo, moja ya eneo ambalo limezuia mikanganyiko mingi, ni eneo hili linalohusiana na “Uungu wa Mungu” . Migawanyiko ya madhehebu mengi unayoyaona sasa chimbuko kubwa hasaa ni hapa.

Wapo wanaoamini Mungu ni mmoja amegawanyika katika nafsi tatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu), lakini wapo wanaoamini Mungu ni mmoja mwenye nafsi moja (Hajagawanyika), yaani Yesu ni Yule Yule Yehova aliyekuwa zamani zile, wengine hawaamini kabisa kama Yesu anastahili kuwekwa katika nafasi ya uungu, wengine hawaamini kuwa Roho Mtakatifu ni halisi, bali ni nguvu tu ya Mungu, ni Yesu na Mungu tu basi.  Je! Ukweli ni upi? Na Je tunapaswa tusimamie wapi?

Jambo la kwanza kufahamu, ni kuangalia kiini, cha kumjua Mungu? Kama kiini kimeharibika hapo ndipo penye shida kubwa. Tunaposema kiini, tunamaanisha idadi ya miungu. Cha ajabu ni kwamba makundi yote haya yanaamini “Mungu ni mmoja”, sawasawa na maandiko yanavyosema..

Marko 12:29  Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, BWANA MUNGU WETU NI BWANA MMOJA;

30  nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.

Tena kizuri zaidi ni kwamba wote wanaamini kazi ya Kristo ya ukombozi, wanaamini pia kazi za Roho Mtakatifu mioyoni mwetu.

Kinachotofautisha ni kutambua tu, nafasi zao za kiungu. Hilo tu, ambalo kimsingi halina nguvu sana, zaidi ya kuzitambua kazi zao mioyoni mwetu. Ni sawa na watu wawili wanaoshindania kama MUWA, ni jamii gani ya mmea, mmoja anasema ni tunda, mwingine anasema ni aina ya jani. Embu jiweke wewe katika hiyo nafasi, ukiulizwa swali hilo utasema ni nini?. Ni rahisi kusema “muwa” ni tunda, lakini kibaolojia muwa ni jamii ya “jani”, isipokuwa limerefu tu zaidi ya mengine na lina maji matamu, .

Sasa je! Kufahamu kama ni jani, au ni tunda? Maarifa hayo yanaweza kubadili asili yake? Kwamba ukifahamu sukari yake itaongezeka, au itawabadilikia maumbo. Wewe na yeye hamna tofauti, kiladha, isipokuwa kiufahamu tu.

Vivyo hivyo na kwenye uungu wa Mungu, Tunatafuta  “UJUZI”. Na ujuzi ni mzuri, lakini mara nyingi tunapoung’ang’ania sana haujengi, bali huleta matengano, Ni upendo tu  ndio unaojengwa.

1Wakorintho 8:1b…Twajua ya kuwa sisi sote tuna ujuzi. Ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga

Ndio maana kwanini hatushangai kuona kanisa la kwanza, liliweza kutembea katika utimilifu wote wa ki-Mungu ijapokuwa hawakuwa na maarifa ya kutosha ya kutambua uungu wa Yesu, vema, isipokuwa baadaye sana katika nyaraka za mitume, ambayo hata hivyo waliita ‘Siri ya Mungu’. Lakini hao hao waliweza kumwabudu Kristo, lakini pia wakamwabudu Baba, bila shida yoyote, wapo waliotambua siri hii, lakini wapo ambao hawakutambua vema.

Kuonyesha kuwa hilo sio jambo la kung’ang’ania sana kana kwamba usipojua utakwenda kuzimu, kama inavyochukuliwa leo, mpaka kutupelekea matengano.

Ukweli ni kwamba Mungu wetu ni Yule Yule mmoja, isipokuwa ametenda kazi kwenye nafasi tatu tofauti kwa lengo la kumkamilisha mwanadamu, na sio yeye. Na sio kana kwamba ni watu watatu wamepatana katika jambo moja. Ni sawa na maji, mvuke na barafu. Vyote vitatu vikiwekwa pamoja vinaweza kuonekana na vitu tofauti tofauti kabisa, lakini ni kitu kile kile kimoja, ambacho ni maji. Ndivyo alivyo Mungu wetu.

Kutembea katika ofisi ya ubaba, na wakati huo huo mwana, na wakati huo huo Roho Mtakatifu, sio shida kwake, amefanya hivyo ili sisi tukamilishwe. Kama mwanadamu asingeanguka hakukuwa na haja ya Mungu kujifunua katika ofisi zote, angebakia katika ubaba wake ule ule mmoja,

Ni sawa na mtu aliyebuni simu, kama kusingekuwa na changamoto ya umbali ya nini mtu kuzungumza kupitia kifaa hicho?. Vivyo hivyo Mungu kuuvaa mwili, ni ili kutuunganisha sisi na yeye, katika mahusiano ambayo tuliyapoteza pale Edeni. Baadaye akaingia kabisa ndani yetu, kwa Roho wake Mtakatifu, kiasi kwamba sasa tunamwabudu Mungu wetu moja kwa moja ndani ya mioyo yetu.

Kwahiyo, Mungu wetu hajagawanyika. Ni Yule Yule mmoja, wala hana nafsi tatu, bali moja. Wala hakuna mahali kwenye maandiko yanathibitisha kuwa Mungu anazo nafsi tatu. Lakini hilo si jambo la kuzozana nalo, kwa wanaoamini Mungu anazo nafsi tatu, maadamu hawaamini miungu mingi. Akimwabudu Baba, ni Yule Yule, akimwambudu Yesu ni yuleyule Mungu, akimwabudu Roho bado haabudu Mungu mwingine zaidi yake yuleyule mmoja. Hilo ni suala tu la kiufahamu ambalo halimwondolei mtu wokovu.

Hivyo ikiwa wewe ni mkristo, umemwamini Kristo kama ni mwokozi wako, na mwenzako pia kampokea kama wewe tu ulivyopokea,  lakini haamini kama ni Mungu bali ni mwana wa Mungu. Lakutosha, usishindanie mambo ambayo ni ya ujuzi.  Mwombee tu, Mungu ampe ufahamu kamilifu, kwasababu kujua kama utatu mtakatifu ni sahihi au sio sahihi hilo haliwezi kumtenga na Mungu wake, maadamu haubudu nje ya hao.  Tukue kiufahamu, tusimpe adui nafasi ya kuleta mtengano yasiyo na maana.

Kwa maarifa ya ndani zaidi kuhusu, mafundisho ya uungu wa Mungu pitia haya masomo >>>

JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?

Je Yesu ni Mungu au Nabii?

MADHIHIRISHO MATATU YA MUNGU.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Roho Mtakatifu ni nani?.

Rudi Nyumbani

Print this post

UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya kwanza: (Msikiti wa AL-Aqsa).

Je msikiti wa Al-Aqsa ni nini, na unahusikaje katika unabii wa biblia?

Angalizo: Makala hii haina lengo la kushambulia Imani Fulani, wala kushabikia Imani Fulani, pia haina lengo la kumchafua mtu yoyote, wala kumdhalilisha, bali kutoa elimu sahihi kuhusiana na tunayoamini na yanayoaminiwa.

MSIKITI WA Al-Aqsa

Msikiti wa Al-Aqsa ni msikiti uliopo katika mji wa YERUSALEMU, ndani ya Nchi ya Israeli, Msikiti huu unaaminika kuwa ni sehemu ya tatu ya utakatifu kulingana na dini ya kiislamu, Sehemu ya kwanza ikiwa ni Makka (au Mecca), ya pili ni Al-masjid an Nabawi iliyopo Medina (nchini Saudi Arabia), na ya tatu ndio hii Al-Asqa.

Msikiti wa Al-Aqsa umejengwa pembezoni mwa jengo maarufu kama “Kuba ya Mwamba” (au Dome of Rock), tazama picha chini.

kuba ya mwamba

Msikiti huu wa Al-Aqsa unaaminika ulijengwa na mtu aliyeitwa Umayyad caliph Abd al-Malik kati ya Karne ya saba (7) na ya nane (8), baada ya KRISTO. Na kulingana na dini  ya kiislamu, inaaminika kuwa Muhamad ndipo alipopaa mbinguni na kwenda kupewa ufunuo wa kitabu cha Quran (Sasa kujua kama ni kweli au si kweli soma Makala hii mpaka mwisho)..

Mbali na kwamba katika msikiti huu ndio panaaminika kuwa mahali Muhamad alipopaa lakini pia zamani paliaminika na waislamu wa kwanza kuwa ndio maahali pa kutazama wakati wa sala, maarufu kama “kibla”. Hebu tuielezee hii Kibla kidogo..

Kibla ni neno la kiaramu lenye maana ya “Uelekeo”, Waislamu wanaposali kulingana na Imani yao, wanapaswa waelekee upande Fulani, sasa zamani Kibla ilikuwa ni katika huu msikiti wa Al-Aqsa uliopo Yerusalemu Israeli, lakini baadae walikuja kubadilisha kulingana na kuwa mahali pajulikanapo kama Makka (Mecca) huko Saudi Arabia, ambapo ndipo Muhamad alipozaliwa.

Hivyo sasa waslamu wote wanaposali wanaelekea kibla huko Makka Saudi Arabia na si tena Yerusalemu, na pia mtu anapozikwa anaelekezewa huko Makka, na vile vile mnyama anapochinjwa anaelekezewa huko huko Makka (kujua usahihi wa jambo hili na kama wakristo wanaruhusiwa kushiriki vyakula hivyo endelea kufuatilia Makala hizi)..

Sasa swali ni je! Huu msikiti ambao sasahivi upo pale Yerusalemu, unaoaminika na watu Zaidi ya Bilioni 1.9, kuwa ndio sehemu ya Tatu kwa utakatifu, je msikiti huu utaendelewa kuwepo pale milele au utakuja kuondolewa?.

Jibu: Kujua kama utaondolewa au la! Turejee Biblia..

Maandiko yanasema lile Hekalu la Kwanza lililojengwa na Sulemani, lilitengenezwa juu ya Mlima Moria, ambapo ni eneo lile lile Abrahamu alipotaka kwenda kumtoa mwanae Isaka kama sadaka ya kuteketezwa, na sasa ndio eneo hili hili ambalo msikiti wa Al-Aqsa umejengwa.

Na ilikuwaje Hekalu kuondolewa na msikiti kujengwa?..

Sababu iliyofanya Msikiti huo kujengwa mahali pale pale Hekalu lilipokuwepo… ni kuvunjwa kwa hekalu hilo mara ya kwanza na ya pili…na wayahudi (yaani waisraeli), kuondolewa katika nchi yao na kutapanywa katika mataifa yote mwaka ule wa 70 Baada ya Kristo.

Wayahudi walipoondolewa katika nchi yao kutokana na makosa yao kwa Mungu, ndipo Ngome ya kiarabu ikateka na kujenga msikiti huo.

Adhabu ya Mungu kwa Israeli, haikuwa ya milele, kwani aliahidi atawarudia tena, na kuwarudisha katika nchi yao, na tena watalijenga Hekalu. (soma Ezekieli 40-48), na kufikia mwaka 1948, Israeli walirejea nchini kwao na mpaka sasa wapo pale.

Na hatua ya kwanza ya matengenezo ni wao kuirudia torati waliyopewa na Musa, hivyo watalijenga Hekalu kama lile la kwanza na baadaye, watamwagiwa Neema na macho yao kufumbuliwa Zaidi kwa kumwamini Masihi YESU, aliye hekalu halisi, sawasawa na Warumi 11 (kwani kwasasa wengi wao hawaamini hivyo).

Warumi 11:1 “Basi, nauliza, Je! Mungu aliwasukumia mbali watu wake? Hasha! Kwa kuwa mimi nami ni Mwisraeli, mmoja wa wazao wa Ibrahimu, mtu wa kabila ya Benyamini.

2  Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu………………………

25  Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26  Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”.

Sasa kabla ya huo wakati wa Israeli kufumbuliwa macho,na kumjua Kristo kama Hekalu halisi, watasimamisha kwanza Hekalu la damu na nyama, na mahali litakapojengwa ni palepale lilipojengwa hekalu la kwanza. Na hapo si pengine bali ni eneo lile lile Msikiti wa Al-aqsa ulipo.

Maswali yafuatayo yananyanyuka:

Je! Ni ni kitatokea?..na je huo msikiti utaondolewa kupisha ujenzi wa Hekalu, na kama utaondolewa je utaondolewaje?..na ni lini?.

Jibu ni  kwamba Msikiti ule ni lazima utaondolewa pamoja na ile Kuba ya Mwamba (Dome of Rock)!!, kwasababu Neno la Mungu limeshasema hivyo kwamba Hekalu litajengwa…na Neno la Mungu halijawahi kupita (kilichotabiriwa katika Ezekieli 40-47  kitatimia kama kilivyo), hakuna shaka juu ya hilo, haijalishi ni muda gani utapita!!.. Wakati utakapofika wa unabii huo kutimia msikiti wa Al-Aqsa utaondoka.

Ni kwa njia gani utaondolewa?.. hakuna anayejua kama ni kwa njia ya Amani, au kwa njia nyingine, lakini dunia nzima itatii tu kwasababu ni Bwana ndiye aliyeyasema hayo, na kuyapanga si MTU, wala WATU wala Taifa la Israeli, bali ni MUNGU mwenyewe!!, hivyo hata wakati wa kuondolewa hakuna atakayejisifu kuwa ni nguvu zake, bali Mungu mwenyewe ndiye atakayehusika hapo.

Na dalili zote zinaonyesha kuwa tumekaribia sana hicho kipindi, kwani waisraeli wameshakusanya utajiri mkubwa na utaalamu mwingi, kiasi kwamba endapo ikitokea ukaanza leo, basi hakuna kizuizi chochote cha kifedha wala kiutalaamu.

Na ujenzi huo unauhusiano mkubwa sana na mpinga-Kristo ajaye, ambapo biblia inasema atatafuta kuingia katika hekalu hilo, ili atafute kuabudiwa yeye kama Mungu (2Wathesalonike 2:4), na maandalizi ya mpinga-kristo yapo ukingoni..nafasi yake ipo tayari, kinachongojewa ni parapanda.

HOJA NYINGINE ZISIZO SAHIHI.

  1. Je Muhamad alipaa??..

Je ni kweli Muhamad alipaa, na je ni kweli Qurani ni kitabu cha Mwenyezi Mungu?

Jibu ni la! Hakupaa!!..Kwasababu Biblia inatuambia manabii waliopaa ni wawili tu, Henoko na Eliya.. na BWANA YESU ambaye ndiye Mkuu wa Uzima. Hao ndio waliopaa, na wengine watakaopaa ni watu watakaofufuliwa na kwenda mbinguni siku ya unyakuo, na watakatifu watakaokuwa hai siku ya kurudi kwa Bwana, pamoja na wale manabii wawili waliotajwa katika Ufunuo 11, basi!

Na pia Quran sio kitabu cha mwenyezi Mungu chenye kumfikisha mtu mbinguni. Kinaweza kuwa kitabu chenye baadhi ya maonyo yaliyo sahihi ambayo mtu akiyafuata anaweza kuwa mzuri katika jamii, lakini si kuurithi uzima wa milele…Kwa ujumla kitabu hiko hakina mafundisho ya Uzima wa milele, kwasababu kinamkataa YESU kama NJIA PEKEE ya WOKOVU wa mwadamu.

Na kitabu chochote kisichoelekeza moja kwa moja Uzima wa milele uliopo ndani ya YESU, au  mtu yeyote yule asiyeamini kuwa YESU ndiye BWANA, na Mwokozi, na ndiye njia pekee ya UZIMA, huyo mtu hana uzima wa milele haijalishi atakuwa anafanya mambo mengine yanayoonekana mazuri machoni pa watu, lakini kama hatamwamini Bwana YESU baada ya kumsikia, matendo yake hayo hayatamsaidia chochote, kwasababu hakuna mwanadamu atakayeweza kusimama kwa matendo yake peke yake.

Yohana 3:18 “ Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu”.

Usikose mwendelezo kuhusiana na Kibla ya wanyama na “Kaaba”, na kama wakristo tunaruhusiwa kushiriki vyakula hivyo.. Pia usikose kufuatilia Makala hizi pamoja na nyingine nyingi, juu ya ukweli kuhusiana na Uislamu na Imani nyingine.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

UFUNUO: Mlango wa 11

Je! Wapalestina ni watu gani, na sehemu yao katika biblia ni ipi?

Rudi Nyumbani

Print this post