Title February 2023

Kwanini Tomaso atake kwenda kufa pamoja na Lazaro? (Yohana 11:14-16).

Jibu: Tusome,

Yohana 11:14  “Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15  Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake.

16  Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, Twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye”

Kwa haraka ni rahisi kutafsiri kuwa Tomaso alitaka na yeye kwenda kufa pamoja na Lazaro, lakini kiuhalisia sio hivyo!.

Tomaso hakutaka kwenda kufa pamoja na Lazaro, bali hapo alimaanisha “kwenda kufa pamoja na Bwana Yesu”.

Ili tuelewe vizuri tuanze kusoma kisa hicho kuanzia juu mstari ule wa tano..(Zingatia vipengele vilivyoainishwa kwa herufi kubwa).

Yohana 11:5  “ Naye Yesu alimpenda Martha na umbu lake na Lazaro.

6  Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo.

7  Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, TWENDENI UYAHUDI TENA.

8  Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, JUZIJUZI TU WAYAHUDI WALIKUWA WAKITAFUTA KUKUPIGA KWA MAWE, NAWE UNAKWENDA HUKO TENA?

9  Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10  Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake.

11  Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.

12  Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.

13  Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.

14  Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15  Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake. 16  Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, TWENDENI NA SISI, ILI TUFE PAMOJA NAYE”

Katika kisa hiki tunaona Bwana Yesu anawapa taarifa wanafunzi wake ya kurejea tena kule Uyahudi ambapo walitaka kumpiga mawe mpaka afe!.. na taarifa hiyo ikawashitusha wanafunzi inakuwaje anataka kurudi tena huko kwenye hatari! (Maana yake si ndo anaenda kufa sasa!)

Lakini  Tomaso aliposikia wanafunzi wenzake wakimhoji hivyo, ndipo na yeye akawashauri kwamba wasimwache aende pake yake huko uyahudi, bali nao pia waende pamoja naye, ili kama ikitokea kauawa basi na wao wafe pamoja naye!.

Ni moyo mzuri aliokuwa nao Tomaso, lakini hakujua kuwa kufa kwaajili ya Kristo ni Neema na si jambo la kujiamulia tu au kujivunia kwamba linaweza kutendeka kwa uwezo wa mtu.

Mtume Petro alijaribu hilo zoezi kama la Tomaso likamshinda, kwasababu alidhani anaweza kufa ajili ya Kristo kwa nguvu zake..

Luka 22:31 “Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;

32  lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.

33  Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani AU HATA KIFONI.

34  Akasema, Nakuambia, Petro, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui”.

Zaidi sana huyu Tomaso ambaye alitaka kwenda kufa pamoja na Bwana, siku Bwana anakamatwa alimkimbia, hakuonekana!..(huenda ndo alikuwa Yule kijana aliyekimbia uchi, Marko 14:52)…na zaidi sana hata baada ya kufufuka kwake bado ilikuwa ni ngumu kuamini mpaka alipotokewa na Bwana Yesu..(huyo ndio mtu aliyetaka kwenda kufa na Yesu Yerusalemu)

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Tomaso hakutaka kwenda kufa na Lazaro, vinginevyo ingekuwa haina maana… lakini kinyume chake alitamani kwenda kufa pamoja na Bwana kwasababu aliamini huo ni ushujaa mkuu wa Imani.

Jambo tunaloweza kujifunza ni kuwa, hatupaswi kuzitumainia nguvu zetu, hatuwezi kusema tutamtumikia Mungu kwa nguvu zetu, hatuwezi kujivuna kuwa tutafanya hiki au kile kwa nguvu zetu, bali siku zote hatuna budi kuwa katika hali ya unyenyekevu, na kujishusha mbele za Bwana, kama tunatamani kufa kwaajili ya Bwana kifo cha kishujaa, basi tumalizie kwa kusema, BWANA TUSAIDIE

Na chochote kile tukifanyacho au tukikusudiacho ni lazima kumalizia kwa kusema “KWA MSAADA WA BWANA KITAFANIKIWA”.. Lakini tukijivuna kuwa tunaweza hiki au kile, tutaishia kumkana na hata kumsaliti.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti kulingana na (Zaburi 89:48)?

Nini maana ya “mtakayoyafunga duniani, yatakuwa yamefungwa mbinguni”?

Rudi nyumbani

Print this post

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

Swali: Je mapepo yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai kama mawe, milima, bahari, maji au nyumba, na hata kubadilisha maumbile ya hivyo vitu?

Jibu ni LA! Mapepo hayawezi kuviingia vitu visivyo na uhai bali yanaweza kuvitumia vitu visivyo na uhai.. mapepo hayawezi kuyaingia mawe au maji au mchanga au maji kama vile yanavyoingia ndani ya mtu, na kuviendesha vitu hivyo kama yanavyowaendesha wanadamu… Sehemu pekee ambayo mapepo yanaweza kuingia ni ndani ya viumbe hai kama wanadamu na wanyama, basi!

Biblia imerekodi mara kadhaa mapepo kuingia ndani ya watu (Luka 8:27) na pia ndani ya wanyama soma Marko 5:12-13. Lakini hakuna mahali popote panapoonyesha mapepo yamewahi kuingia ndani ya mawe au katika maji au katika mchanga, au katika matofali au katika gari la farasi au katika chakula..

Mapepo yanachoweza kufanya ni kuvitumia tu vitu vya asili, kwamfano yanaweza kuvumisha upepo lakini si kuingia ndani ya upepo, vile vile yanaweza kutetemesha ardhi lakini si kuiingia ardhi, yanaweza kuitikisa bahari lakini si kuiingia bahari… uwezo ambao hata sisi wanadamu tunao, sisi tunaweza kuvumisha upepo tukiwa na kifaa kinachoitwa feni, lakini si kuuingia upepo, vile vile tunaweza kutengeneza mawimbi ya bahari kwa vyombo maalumu n.k, lakini hiyo haimaanishi kuwa tumeiingia bahari na kuiendesha bahari kama vile tunavyoiendesha mikono yetu au miguu yetu.

Na mapepo ni hivyo hivyo, hayana uwezo wa kuviingia vitu visivyo na uhai.

Kwahiyo tunachopaswa kufanya ili roho za mapepo zisiweze kutumia vitu vya asili kutuletea matatizo ni sisi kudumu katika usafi na utakatifu pamoja na kuomba… tukifanya hivyo shetani na mapepo yake hawawezi kutumia vitu vinavyotuzunguka kutuletea madhara, hawawezi kuzitumia nyumba zetu kama vituo vyao vya mikutano.

Lakini tusipojisogeza karibu na Mungu, basi shetani atatumia vitu vyote kutudhuru, atatumia ardhi, bahari, mabonde, na magari na hata nyumba kutuletea matatizo…

Isaya 13:21 “Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini watacheza huko”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

MAJINI WAZURI WAPO?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

Rudi nyumbani

Print this post

Je! kuna mambo ambayo Mungu hawezi kuyafanya kulingana na Waamuzi 1:19?

Jibu: Tusome,

Waamuzi 1:19 “Bwana alikuwa pamoja na Yuda; naye akawafukuza watu waliokaa katika nchi ya milimani; ASIWEZE KUWAFUKUZA HAO WALIOKAA KATIKA HILO BONDE, kwa kuwa wao walikuwa na magari ya chuma”.

Ni kweli Bwana hakuweza kuwafukuza hao watu waliokaa mabondeni… Lakini si kwamba alikuwa hana uwezo wa kuwafukuza, bali kulikuwa na kusudi kwanini hakuweza kuwafukuza..

Ili tuelewe vizuri tuanzie kuisoma habari hiyo kuanzia mstari wa 17..(zingatia maneno yaliyoanishwa kwa herufu kubwa).

Waamuzi 1:17 “Kisha Yuda akaenda pamoja na nduguye Simeoni, na WAKAWAPIGA WAKANAANI waliokaa katika Sefathi, na kuuharibu mji kabisa. Na jina la mji huo ulikuwa ukiitwa Horma. 

18 Pamoja na haya Yuda aliutwaa Gaza pamoja na mipaka yake, na Ashkeloni na mipaka yake, na Ekroni na mipaka yake.

 19 BWANA ALIKUWA PAMOJA NA YUDA; naye akawafukuza watu waliokaa katika nchi ya milimani; asiweze kuwafukuza hao waliokaa katika hilo bonde, kwa kuwa wao walikuwa na magari ya chuma”.

Mstari wa 19, unaanza kwa kusema “Bwana alikuwa pamoja na Yuda” maana yake ni kwamba, katika vita Yuda alivyokwenda kupigana, Bwana alikuwa pamoja naye..(kumbuka Yuda anayezungumziwa hapa sio Yule mwana wa Yakobo, wala sio Yule Yuda aliyemsaliti Bwana Yesu), bali ni kabila la Yuda kwa ujumla, ambalo wakati wa kuingia katika nchi ya Ahadi lilipaswa liupiganie urithi wake kwa kuwatoa wenyeji wa Kanaani ili kusudi wapate ardhi ya kukaa wao, kama urithi wa kabila zima.

Hivyo katika harakati za kupambania urithi wao huo walikutana na makabila mengi mbalimbali, ambayo mengine yalikuwa na nguvu sana na mengine manyonge, yale yaliyokuwa manyonge Yuda walikwenda kwa ujasiri na kuyapiga na kuyapokonya ardhi, kwasababu hayakuwa na silaha zenye nguvu za kuwazidi,

Lakini yale yaliyokuwa na Nguvu nyingi za kivita, Yuda waliyaogopa, hivyo hawakudhubutu kwenda kupigana nayo, na kwasababu hiyo Mungu asingeweza kuyaondoa kwasababu Mungu kamwe hatembei na watu wasio na Imani, hivyo akawaacha,

Lakini kama wangechukua hatua ya kwenda kupambana na hao maadui zao, pasipo kutazama ni silaha za aina gani wanazomiliki, ni wazi kuwa Mungu angewasaidia katika vita hiyo, na hatimaye wangewaondoa hao watu na kuutwaa urithi wao.

Sasa baadhi ya makabila ambayo Yuda waliyaogopa ndio hao waliokuwa wanakaa mabondeni, na sababu ya kuyaogopa biblia imeitaja pale kuwa “makabila hayo yalikuwa na magari ya chuma kwaajili ya vita”..Yuda wakaogopa wasiende kupigana nayo, jambo ambalo Yoshua mtumishi wa Mungu alishawaonya kuwa wasiyaogope makabila hayo..

Yoshua 17:17 “Kisha Yoshua alinena na nyumba ya Yusufu, maana, ni Efraimu na Manase, akawaambia, Wewe u taifa kubwa la watu, nawe una uwezo mwingi; hutapata kura moja tu; 

18 lakini hiyo nchi ya vilima itakuwa ni yako; maana, ijapokuwa ni mwitu, wewe utaukata, na matokeo yake yatakuwa ni yako; kwa kuwa wewe utawafukuza hao Wakanaani, WAJAPOKUWA WANA MAGARI YA CHUMA, WAJAPOKUWA NI WENYE UWEZO”

Utaona pia hiyo sio mara ya kwanza wana wa Israeli kuyaogopa mataifa yenye nguvu kupita wao, soma pia Hesabu 13:33 na Waamuzi 4:3

Hiyo inatufundisha nini?

Tunachojifunza ni kuwa “Mungu hawezi kufanya jambo lolote kwetu pale tunapomkosea Imani” Hilo ndilo jambo ambalo Mungu hawezi kufanya!!! Na lingine ambalo hawezi kufanya ni DHAMBI!

Yakobo 1:6 “Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.

7  Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.

8  Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote”.

Ukiamini kuwa Mungu hawezi kukuponya, basi fahamu kuwa KWELI HATAWEZA KUKUPONYA!, Ukiamini kuwa Mungu hawezi kukutendea jambo Fulani au kukupigania, basi fahamu kuwa ni KWELI MUNGU HATAWEZA KUKUTENDEA HILO JAMBO, wala KUKUPIGANIA katika hiyo vita iliyo mbele zako.

Siku zote fahamu kuwa PASIPO IMANI HAIWEZEKANI KUMPENDEZA MUNGU (Waebrania 11:6).

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu?

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao;

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

Jibu: Tusome,


Waefeso 2:20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”

Hapo maandiko yanasema tumejengwa juu ya “Msingi wa Mitume na Manabii “na si juu ya “Mitume na Manabii” .. Na pia inasema tumejengwa juu ya “Msingi” na si juu ya Misingi ya mitume na manabii. Ikiwa na maana kuwa Msingi ni mmoja tu, ambao tumejegwa juu yake, (mbele kidogo tutakuja kuuona huo msingi ni nini).


Sasa yapo maswali mawili hapo ya kujiuliza; 1) Hawa Mitume na Manabii ni akina nani na 2) Huo msingi ni nini?


1) Mitume na Manabii:


Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapa katika Waefeso 2:20 sio hawa waliopo sasa, Bali ni wale walioandika biblia, kama Musa, Yeremia, Hosea, Ezekieli na Malaki vile vile mitume wale 12 wa Bwana pamoja na wengine kama akina Paulo, ambao waliandika biblia.


Mtu yeyote aliyepo sasa, au atakayekuja kutokea na kujiita mtume au nabii, basi afahamu kuwa andiko hilo la Waefeso 2:20 halimhusu hata kidogo. Na shetani amewapandikiza watu wengi kiburi (watu wanaojulikana kama mitume na manabii wa leo), na kuanza kujivuna kuwa wao ndio Msingi wa kanisa.. Jambo ambalo si la kweli hata kidogo.


2) Msingi


Msingi ambao sisi tumejengwa juu yake ni ule waliokuwa nao Mitume, ikiwa na maana kuwa kile Mitume walichokifanya msingi, ndicho hicho hicho sisi (kanisa la Mungu) tunajengwa juu yake. Sasa ni kitu gani Mitume na Manabii wa kwenye biblia walikifanya msingi?… Hicho si kingine zaidi ya YESU KRISTO MWENYEWE!!!. Huyu ndiye Msingi wa kanisa na ndiye aliyekuwa msingi wa mitume, na ndio msingi wetu sisi na bado ataendelea kuwa msingi siku zote.


1Wakorintho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, YESU KRISTO”.


YESU KRISTO ndio Mwamba ule ambao yeye mwenyewe alisema kuwa kanisa lake litajengwa juu yake.


Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.


Umeona? Mwamba unaonenewa hapo sio Petro bali ni yeye YESU MWENYEWE!.. yaani huo Ufunuo Petro alioupata wa YESU KUWA MWANA WA MUNGU Ndio MSINGI, na NDIO MWAMBA ambao kanisa litajengwa juu yake.


Kanisa lolote leo ambao YESU sio kiini cha Imani hiyo, hilo sio kanisa la kweli, vile vile imani yoyote ile isiyomweka YESU kama msingi badala yake inawemweka mwanadamu mwingine au mnyama au sanamu basi imani hiyo ni imani ya Uongo n.k


Mahubiri yoyote yasiyomweka YESU msingi, hayo ni mahubiri kutoka kwa Yule adui.
Mtumishi yoyote Yule, awe mchungaji, mwalimu, mtume, nabii au mwinjilisti asiyemweka YESU kama kiini na kitovu cha Mafundisho huyo si wa kweli, kwa mujibu wa maandiko.
Vile vile mtu yeyote ajiitaye Mkristo na Yesu si msingi wa maisha yake, huyo ni mkristo jina tu wa uongo.
Bwana atusaidie tumweke Yesu msingi wa maisha yetu.


Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

Rudi nyumbani

Print this post

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Neno la Mungu linasema..

Warumi 5:1 “Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo”.

Je! ni haki gani hiyo tunayohesabiwa, ambayo tukiisha ipata basi tutapata amani?

Jibu ni kwamba si haki moja!, bali ni haki ZOTE Njema!… Mfano wa hizo ni kama zifuatazo…

1.HAKI YA KUISHI MILELE.

Tunapomwamini Bwana Yesu tunapata haki ya kupata UZIMA WA MILELE.. ambayo tuliupoteza pale Wazazi wetu wa kwanza walipoasi.

Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;

26  naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?”

Pia Yohana 3:36, Bwana Yesu anasema maneno kama hayo hayo…

2. HAKI YA KUWA NA UZIMA, NA AFYA.

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”

Hivyo magonjwa hayatatutawala, bali uzima na afya, kama tukiwa ndani ya Yesu, maana yake  AFYA ni haki yetu!.. tunapopitia maradhi ya muda mrefu maana yake hapo ni shetani katudhulumu haki yetu, hivyo hatuna budi kuishindania haki yetu mpaka tuipate katika mahakama ya kimbinguni, huku tukitumia katiba yetu biblia. Na tunapong’ang’ania kwa bidii bila kuchoka, wala kukata tamaa basi tunaipata haki yetu ya kuwa wazima siku zote.

3. HAKI YA KUMWONA MUNGU.

Unapomwamini Yesu ni haki yako kumwona Mungu katika maisha haya na katika yale yajayo.. Kumwona Mungu si lazima tumwone kwa macho, bali utamwona  katika maisha.. Maana yake utapitia vipindi vingi vya maisha ambavyo vitakujulisha kuwa Mungu yupo nawe, pia utaona miujiza mingi ya kiMungu ambayo itakujulisha kuwa Mungu yupo nawe, na zaidi sana kila utakapomwita Mungu utamwona..

Mathayo 28:20 “……….na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”.

4. HAKI YA KUPOKEA ROHO MTAKATIFU.

Zamani Roho Mtakatifu alikuwa anashuka juu ya baadhi ya watu tu (ambao ni manabii) tena kwa kitambo kidogo, lengo ni kuwapa ujumbe kutoka kwa Mungu, na baada ya hapo anaondoka.. Kwasababu ROHO TAKATIFU ya Mungu haiwezi kukaa ndani ya Mwanadamu aliye mchafu.

Lakini baada ya Bwana YESU kuja, kaja kutuletea Haki ya sisi kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu, jambo ambalo si la kawaida..

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39  Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”

Hivyo yale matunda ya Roho tunayoyasoma katika Wagalatia 5:22, ambayo ni upendo, amani, furaha n.k Hayo yote ni haki yetu sisi kuyapata.. Kuwa amani ni haki yako wewe uliye ndani ya Kristo, kuwa na furaha ni haki yako.

5. HAKI YA KUFANIKIWA KIMWILI NA KIROHO.

Tunapomwamini Bwana Yesu na kukaa ndani yake, hatupati tu haki ya vitu vya kiroho, bali pia tunapata haki ya vitu vingine vya kimwili ikiwemo mafanikio.

3 Yohana 1:2  “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”

Pia Neno la Mungu linasema..

2Wakorintho 8:9  “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake”.

Na haki nyingine zote zilizosalia, ni Ahadi yetu. Ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana kuingia ndani ya Kristo.. Ukiwa nje ya Kristo, shetani atakudhulumu haki zako zote hizo na hakuna popote utakapokwenda kushitaki.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

UMEITIMIZA HAKI YOTE?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Nitajuaje kuwa nimesamehewa dhambi zangu?

Pale unapotubu, kwa kumaanisha kabisa kuacha maovu, na maisha ya kale ya dhambi, wakati huo huo Mungu anakusamehe dhambi zako kabisa kabisa. Lakini hutasikia, hisia Fulani, au badiliko Fulani la wakati huo huo, kwani fikra zako za dhambi za zale bado zitaendelea kuzunguka kwenye akili yako. Hivyo wengi wakishaona hivi wanadhani kuwa Mungu hawajawasamehe, na hivyo wanaendelea kubaki katika mashaka, au kurudia rudia kumlilia Mungu awasamehe.

Na hapa hapa shetani ndipo anapata nafasi ya kuwatesa, na kuwakandamiza, wengine wanajikuta kila siku wanaomba Toba Mungu nisikie unisamehe!, Mungu nisikie unisamehe!, kumbe tayari Mungu alishawasamehe tangu siku ile ya kwanza walipomaanisha kweli kweli kugeuka na kukataa kurudia dhambi zao.

Ndugu, fahamu hata kama wewe utakuwa na kumbukumbu la nyuma la dhambi zako, lakini kwa Mungu ni tofauti, yeye akisamehe anasahau kabisa.

Waebrania 8:12  “Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena”.

Unapokwenda mbele za Mungu, lazima uamini kwa moyo wako wote umeshasamehewa, vita vya kimawazo vinavyoanza kuja tangu huo wakati, huna budi kuvishinda, kwa kuvipinga, ukisikia moyoni mwako unaambiwa, aah! Wewe dhambi zako ni nyingi, ile dhambi ulishamkufuru Roho Mtakatifu, pinga, kataa sema mimi nimeshasamehewa kwa damu ya Yesu Kristo.

Kisha unavyozidi kufanya hivyo baada ya kipindi Fulani utaona amani ya Mungu imekuvaa.

Lakini pia ni lazima ukumbuke kuwa yapo mambo yanayochangia pia kusamehewa dhambi zetu, na yenyewe ni sisi kuwasamehe waliotukosea kama wapo.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 6:14  “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. 15  Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu”.Hivyo uombapo msamaha zingatia kuwa moyo wako ni mweupe kwa wengine.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NINI MAANA YA KUTUBU

Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

KIFAHAMU KIGEZO  CHA KUSAMEHEWA NA MUNGU.

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inasema tujihadhari na “Mbwa” hawa mbwa ni akina nani? (Wafilipi 3:2)

Jibu: Tusome..

Wafilipi 3:2  “Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao”

Hapa kuna makundi matatu yaliyotajwa ambayo tunapaswa tujihadhari nayo, kundi la Kwanza ni “MBWA” kundi la Pili ni “WATU WAJIKATAO” na kundi la tatu ni “WATU WATENDAO MABAYA”.

Sasa kabla ya kwenda kuangalia Mbwa ni watu wa namna gani, kwanza tuyatazame haya makundi mawili ya mwisho, ambayo ni watu wajikatao na watenda mabaya..

Watu “watendao mabaya” wanaozungumziwa hapo, ni watu walio ndani ya imani lakini wanatenda mabaya.. watu hawa biblia imetuonya tujihadhari nao, yaani tusichangamane.. Mtume Paulo alizidi kuliweka hili vizuri katika kitabu cha 1Wakorintho 5:9-11.

1Wakorintho 5:9  “Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.

10  Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.

11  Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye”.

Lengo la kutochangamana na makundi haya ya watu walio ndani ya kanisa lakini ni watenda mabaya, ni ili wajisikie aibu kwa wanayoyafanya na hatimaye wageuke na kutubu.

Kundi la Pili: Ni “Watu Wajikatao”.. kumbuka hapa anasema “watu wajikatao” na sio “watu wajikataao” kuna tofauti ya kujikata na kujikataa.. hapa wanazungumziwa watu wanaojikata!.. Sasa ni watu gani hao wanaojikata?.. si wengine bali walikuwa ni wayahudi ambao walikuwa wanashinikiza tohara, kuwa ndio dalili ya kukubaliwa na Mungu..

Lilikuwepo kundi la walioamini, ambao hata sasa lipo lililokuwa linasisitiza tohara kuwa ni jambo la lazima, na kwamba mtu asipotahiriwa hawezi kukubaliwa na Mungu. Watu hawa walikuwa kweli wamemwamini Yesu lakini sheria za torati bado zilikuwa zinawaendesha, ambazo kimsingi hizo haziwezi kumkamilisha mtu, bali Neema ya Yesu pekee… kushika mwezi, mwaka, siku, sabato haya yote hayafai katika kumkamilisha mtu.

1Wakorintho 7:19  “Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu bali kuzihifadhi amri za Mungu.

20  Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa”

Kwa maelezo mengine marefu kuhusiana na watu wajikatao unaweza kufungua hapa >>> WATU WAJIKATAO

Na kundi la Tatu na la Mwisho, ambalo biblia imetaja tujihadhari nalo ni kundi la “MBWA”.

 Sasa utajiuliza hawa “Mbwa” ni akina nani?

Bwana Yesu aliwataja wazi kabisa hawa Mbwa ni wakina nani.. Tusome..

Mathayo 7:15  “Jihadharini na MANABII WA UONGO, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni MBWA-MWITU WAKALI.

16  Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti”

Umeona?… Kumbe Mbwa wanaozungumziwa hapo ni “Manabii wa Uongo” na tena hawajatwi kama Mbwa tu!, bali kama “Mbwa-Mwitu” tena wakali!.. maana yake wasiohurumia kundi.. Na hatutawatambua kwa mionekano yao, kwasababu kwa nje wamevaa mavazi ya kondoo, (wanafanana na watumishi wa kweli wa Mungu) lakini tutawatambua kwa matunda yao, maana yake kwa yale wanayoyafundisha na wanayoyaishi.

Na manabii wa uongo ni mjumuisho wa Mitume wa Uongo, wachungaji wa uongo, waalimu wa Uongo, pamoja na waimbaji wa Uongo. Kwaufupi watu wote wanaosimama kutangaza injili kwa wengine! Lakini maisha yao ya ndani si wakristo, ila kwa nje wanasifika kama watumishi wa Mungu.

Ikiwa mtu atasimama na kuhubiri injili nyingine tofauti na ile iliyoandikwa katika biblia, basi huyo kibiblia ni “Mbwa”, ikiwa mtu atahubiri injili isiyo ya wokovu, badala yake ya kumpoteza mtu au kumfanya afurahie dhambi..mtu huyo kibiblia ni Mbwa, na tumetahadharishwa kukaa mbali naye.

Nabii wa Kweli wa Mungu atakuwa kama Musa!, Mpole kuliko wote, na mwenye kuwaelekeza watu kwa Mungu na si kwake wala kwa shetani.

Kumbukumbu 13: 1 “Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu,

 2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo;

 3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote.

4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye”

Je! Unaongozwa na nani?.. Manabii wa Uongo, Miujiza na Ishara au NENO LA MUNGU?.

Kumbukumbu 6:4 “Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja. 

5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Watu wajikatao ni watu wa namna gani? (Wafilipi3:1).

Mstari huu una maana gani? “Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi”. (Mhubiri 11:1)Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?.

HAKUONA MAHALI PA KUTUA KWA WAYO WA MGUU WAKE.

VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI

Rudi nyumbani

Print this post

Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 8 ili tuweze kuelewa vizuri..


Mathayo 22:8 “Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.
9 Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.
10 Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.
11 Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.
12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? NAYE AKATEKEWA”.


“Kutekewa” kunakozungumziwa hapo si Kutekewa maji au kinywaji fulani, hapana!…Bali maana yake Ni “KUKOSA MANENO”


Mtu anayekosa Neno la kujibu pale anapoulizwa, mtu huyo Ndio katekewa..
Katika habari hiyo Bwana Yesu anatoa mfano wa mtu aliyeishiwa maneno baada ya kukutwa hana vazi la harusi.


Hali itakayokuwa kwa wengi katika Ile siku ya mwisho. Maandiko yanaonyesha kuwa katika siku ya mwisho, Bwana atawakataa watu wengi, ambao hawakuwa na vazi la Harusi walipokuwa duniani.
Na vazi la harusi maandiko yameweka wazi kuwa Ni “Matendo ya haki ya watakatifu”.


Ufunuo 19:8 “Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu”


Katika siku ile wengi watadhani Ni dini zao zintakazowapa kibali Cha kuingia uzimani, wengine watadhani Ni Imani zao n.k. pasipo kujua kuwa bila utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu.


Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”


Na Utakatifu hatuupati kwa nguvu zetu, Bali kwa msaada wa Bwana.


Tunapotubu kwa kudhamiria kabisa kuacha dhambi zetu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi Kama bado hatujabatizwa Basi Bwana anatupa Roho wake mtakatifu ambaye huyo ndiye atakayetusaidia sisi kuweza kuwa wakamilifu na watakatifu.


Hivyo tukiupata utakatifu katika maisha yetu, Basi katika Roho tutaonekana mbele zake tumevaa vazi la harusi na hivyo siku Ile hatutatekewa mbele zake, hatutaishiwa maneno.


Lakini tukiyakosa hayo, huku tukitumainia dini zetu, na madhehebu yetu, na theologia zetu… basi tujue kuwa tutakosa cha kujibu mbele zake siku Ile..


Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

BALI WANA WA UFALME WATATUPWA NJE!.

TAFUTA KWA BIDII KUWA MTAKATIFU.

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Rudi nyumbani

Print this post

Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?

JIBU: Wapo wanaofikiri kwamba shetani amefungwa, atakuja kufunguliwa kipindi Fulani huko mbele, lakini pia wapo wanaodhani, shetani anaishi mahali Fulani kuzimu( aidha chini ya bahari, au kwenye sayari fulani), ambapo huko kuna amesimika utawala wake unaofanana na huu wa duniani.

Lakini ukweli ni kwamba shetani hajafungwa, wala hayupo katika eneo Fulani rasmi la mwilini, ambalo unaweza kwenda ukakutana naye.

Ikumbukwe kuwa ibilisi anafanya kazi katika ulimwengu wa roho, alipoasi mbinguni, alitupwa chini duniani, akaanza kazi yake ya kuudanganya ulimwengu mpaka akafanikiwa kuuteka ukawa chini ya milki yake, Tunalithibitisha hilo katika maneno aliyomwambia Bwana Yesu.

  Luka 4:5 Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja.

6  Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo.

7  Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako. 8  Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke

Hivyo shetani yupo anazunguka zunguka duniani hana makao rasmi, Alimwambia hivyo Mungu.

Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.  7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo”.

Atakuja kufungwa kipindi ambacho utawala wa miaka 1000 wa amani wa Yesu Kristo kuanza, na baadaye atafunguliwa kidogo, lakini kwasasa hajafungwa yupo duniani ndio chanzo cha maovu yote, wala hana eneo Fulani rasmi kwamba amejijengea  anaishi huko na mapepo yake, hapana bali wanafanya kazi katika ulimwengu wa roho, wakijigawanya tu katika vitengo mbalimbali, wengine katika anga, wengine, katika mataifa, wengine katika familia moja moja, na wengine katika kila huduma/au kanisa la Kristo lilipo, wengine katika uchawi n.k.

Hivyo, sisi tutamshinda na kumpinga tu kwa kulishika Neno la Mungu, na kudumu katika maombi daima.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

POPOBAWA NI KWELI YUPO?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

MATESO YA KUZIMU.

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

Rudi nyumbani

Print this post

MAGONJWA YAKUPATAYO MARA KWA MARA.

1Timotheo 5:23  “Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara”

Haya ni maneno ya mtume Paulo kwa mtoto wake wa kiroho Timotheo, Ni rahisi kuyachukulia juu juu, lakini ukitazama kwa undani utaona jinsi watu wa kale walivyojitoa kwa Bwana,bila kuruhusu hali zao za mwilini kuwakwamisha.

Kama tunavyosoma, Timotheo alikuwa ni kijana mwenye bidii sana, aliyetumika na Mtume Paulo katika kuineza injili sehemu kubwa ya dunia, lakini kijana huyu hakuwa vizuri sana kiafya kama tunavyodhani, alikuwa anasumbuliwa na tumbo, lakini kama hilo halitoshi, alikuwa pia anapatwa na magonjwa ya MARA KWA MARA, tena katika ujana na sio uzee. Ni heri magonjwa hayo yangekuwa ni ya siku moja, bali ya mara kwa mara. Paulo aliishi naye kwa muda mrefu hivyo alikuwa anamwelewa sana, anashangaa leo yupo sawa, kesho, ni mgonjwa, wiki hii yupo sawa, wiki ijayo tumbo linamsumbua sana.

Lakini katika yote hayo, hakuwa kama Dema ambaye alimwacha Paulo, akaurudia ulimwengu, yeye aliendelea kuitenda kazi ya Bwana katika madhaifu yake ya mwili,  Ni mtu tu pekee ambaye Paulo alijiona amani kumwachia hata huduma yake aiendeleza duniani. Alikuwa kama Elisha kwa Eliya.

Hivyo mwishoni kabisa mwa huduma, tunaona hapa Paulo anamwandikia waraka huu na kumsisitiza, asinywe maji tu peke yake, bali na mvinyo kidogo kwa ajili ya magonjwa hayo ya mara kwa mara, Paulo hapa anampa ushauri wa kitabibu, zaidi ya ule wa kiroho, kwani zamani mvinyo , ulitumika kwa ajili ya baadhi ya magonjwa, lakini sasa kwa wakati wetu tunazo dawa za hospitalini. Unaweza kujiuliza Paulo ambaye Mungu alimtumia kwa ishara na miujiza ya kupita kawaida, angepaswa amweke, mikono, na kukemea magonjwa hayo ya mara kwa mara yamwachie, lakini alitambua kuwa si kila wakati hali itakuwa hivyo, mambo mengine Mungu anayaruhusu yatokee kwa sababu zake.

Ni kama Elisha, ambaye, alisumbuliwa na ugonjwa ambao ulikuja kumuua, lakini hakumwacha Bwana, na kusema Mungu gani huyu hanioni, aliendelea kuwa nabii wa Mungu,

2Wafalme 13:14 “Basi Elisha alikuwa ameshikwa na ugonjwa wake uliomwua; naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatelemka amtazame, akamlilia mbele yake, akasema, Baba yangu! Baba yangu! Gari la Israeli na wapanda farasi wake!”

Ni nini Bwana anataka tujifunze?

Katika madhaifu yetu, kamwe tusipunguze spidi ya kumtumikia Mungu, kwasababu mambo tunayoyapitia sisi walishayapitia watakatifu wengine waliotutangulia. Kijana Timotheo, alikuwa ni mdhaifu sana kimwili, lakini aliichapa injili ya Kristo, bila kujali yamsibuyo. Alisafiri huko na huko.

Yawezekana na wewe, ni mhubiri au mtumishi wa Bwana, lakini vidonda vya tumbo, haviishi ndani yako ijapokuwa umemwomba sana Bwana aviondoe lakini bado huoni matokeo yoyote, endelea hivyo hivyo kutumika usisubiri upone, una magonjwa Fulani ya kichwa ambayo yanakuja na kuondoka, yanakuja na kuondoka, yasikukwamishe, mkumbuke Timotheo, kunywa dawa za hospitalini, songa mbele, unasumbuliwa na saratani, unasumbuliwa na sukari, inapanda, inashuka, kila siku ni kuchoma sindani, Usingoje kwanza Bwana akuponye, endelea, kwani huzijui njia za Bwana, hujui ni kwanini leo upo hivyo, huwenda amekusudia, uishi maisha marefu kuliko zaidi ya wengine katika hali hiyo hiyo ili jina lake litukuzwe, na uwaponye wengi wanaosumbuliwa na maradhi kama hayo, Elisha baada ya kufa katika ule ugonjwa wake, tunaona bado mifupa yake ilifufua wafu, Hivyo kuugua si kikwazo cha Mungu kutokututumia sisi.

Tujipe moyo tusonge mbele, Bwana anatupenda, kwani yeye mwenyewe alisema, pale tuwapo dhaifu ndipo tulipo na nguvu.

2Wakorintho12:9  “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. 12.10  Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Nini maana ya..“wakiwazuia watu wasioe” (1Timotheo 4:1)

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

KANSA/SARATANI INATIBIKA.

Rudi nyumbani

Print this post