Title November 2023

JUA HALITAKUPIGA MCHANA, WALA MWEZI WAKATI WA USIKU.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Nakukaribisha katika kuyatafakari maneno ya uzima.

Ulishawahi kuutafakari vema huu mstari?

Zaburi 121:5 Bwana ndiye mlinzi wako; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.  6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.  7 Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.  8 Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

Ni rahisi kumwelewa mtu anayekuambia, “leo jua limenipiga”, lakini si rahisi kumwelewa mtu anayesema “leo mwezi umenipiga” Ni wazi kuwa utamwona anakuchezea akili.  Si ni kweli?..Lakini hapa katika vifungu hivi ambavyo Mungu anaeleza ulinzi wake kwa watu wake jinsi ulivyo, anatumia mifano hiyo miwili  ya jua na mwezi. Na anaonyesha kuwa kama vile jua linavyompiga mtu, ndivyo na mwezi nao unavyompiga mtu.

Akiwa na maana gani?  

Tunajua kuwa mwezi hauna nguvu yoyote ya kumuunguza mtu au kumchosha, tofauti na jua. Lakini Mungu anaona hata mwangaza tu  huo wa mwezi ni pigo kwa mtu. Akiwa na maana  si katika mateso magumu, au dhiki kubwa zinazoonekana kwa macho ndio anazoshughulika nazo Mungu, lakini pia hata katika zile ndogo sana, ambazo unaweza kuona zikiendelea kuwepo hazina madhara yoyote kwako, Bwana anakulinda nazo.

Kwamfano wewe huwezi kuona umepata hasara pale nywele yako moja imepungua kichwani mwako, tena si rahisi kugundua,  lakini yeye anaithamini na ndio maana amezihesabu zote. Ikidondoka moja tu, anaona mapungufu, umekutana na mateso..

Mathayo 10:30  lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.,

Vivyo hivyo rohoni, unaweza kumwomba Mungu, niepushe na majaribu, kichwani kwako ukafikiri hili na hili labda magonjwa, umaskini, vita, vifungo,ajali,  kuteswa kwasababu ya imani, N.K. ndio Bwana anashughulika navyo hivyo kukulinda, au kukupa nguvu ya kuvishinda. Lakini anahakikisha hata zile honi za magari unazopishana nazo barabarani, haziyaharibu masikio yako, jani ulilokanyaga jana, halijaharibu mguu wako, bacteria walio katika mikono yako, hawaui seli za ngozi, idadi ya minyoo walio tumboni mwako, hawaendi kula maini na figo zako, kiwembe kinachopita kichwani mwako kila siku haking’oi mizizi ya nywele, n.k…Haya mambo unaweza kuona ni ya kawaida tu, lakini Bwana akitoa mkono wake umeisha.

Kwa ufupi ni kuwa zipo Nyanja nyingi sana za hatari, ambazo Bwana anatuepusha nazo, Ndio maana tunapaswa tuwe waombaji sikuzote, unapojiona upo salama, omba, unapojiona upo kwenye matatizo omba, muda wote dumu uweponi mwa Bwana. Hata kama utaona kama majaribu yamekulemea, Bwana ameahidi ushindi mwishoni, Ayubu alilemewa na mateso lakini mwishoni alirejeshewa mara dufu.

Ulinzi wa Mungu ni uhakika kwa watu wake, dumu katika katika maombi ili Bwana apate nafasi ya kutulinda vema, nyakati za jua na nyakati za mwezi. (Mathayo 26:41)

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?

MIEZI 13 YA KIYAHUDI.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Mwandamo wa mwezi/Mwezi mpya Ni nini kibiblia?

Kumaka ni nini katika biblia? (Mathayo 8:27)

Rudi nyumbani

Print this post

UFANYE MOYO WA MUNGU UWAELEKEE WATU WAKE.

Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu lililo Taa ya njia yetu na Mwanga wa Njia zetu (Zab 119:105).

Je sisi wanadamu tunaweza kuufanya Moyo wa Mungu uwaelekee watu wengine?. Jibu ni Ndio!. Katika biblia kuna watu baadhi  ambao kwa sehemu waliweza kuufanya Moyo wa Mungu uwaelekee watu wake, ijapokuwa watu hao hawakustahili kabisa kukaribiwa na Mungu.

Na watu hawa wi wengine Zaidi ya NABII MUSA NA NABII SAMWELI

Hebu tuweke msingi kwa kutafakari maandiko yafuatayo…

Yeremia 15:1 “Ndipo Bwana akaniambia, Hata wangesimama mbele zangu MUSA na SAMWELI, MOYO WANGU USINGEWAELEKEA WATU HAWA; watupe, watoke mbele za macho yangu, wakaende zao”.

Kumbe Musa na Samweli walikuwa wanatabia ya kuuelekeza Moyo wa Mungu kwa watu wake?.. Sasa kwa namna gani?…hebu tusome matukio yao baadhi, mmoja baada ya mwingine.

1. MUSA.

Kutoka 32:7 “Bwana akamwambia Musa, Haya! Shuka; kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao, 

8 wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu, wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.

9 Tena Bwana akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu

10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.

11 MUSA AKAMSIHI SANA BWANA, MUNGU WAKE, NA KUSEMA, BWANA, KWA NINI HASIRA ZAKO KUWAKA JUU YA WATU WAKO ULIOWALETA KUTOKA NCHI YA MISRI KWA UWEZA MKUU, NA KWA MKONO WENYE NGUVU? 

12 Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako. 

13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.

14 NA BWANA AKAUGHAIRI ULE UOVU ALIOSEMA YA KWAMBA ATAWATENDA WATU WAKE”.

Hapo Mstari wa 14 unasema, Bwana akaghairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake. Na hiyo yote ni baada ya Musa kuwaombea wana wa Israeli, na hivyo Mungu akaghairi yale mabaya nakuendelea kutembea na watu wake.

Huenda Musa asingewaombea basi wote wangefutiliwa mbali na kweli Mungu angeenda kumfanya Musa kuwa Taifa kuu.

Lakini si huyo tu peke yake, tumwangwalie na Samweli pia.

2. SAMWELI

1Samweli 12:16 “Na sasa simameni, mkalione jambo hili kubwa, Bwana atakalolitenda mbele ya macho yenu.

17 Leo je! Si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana, kwamba apeleke ngurumo na mvua; NANYI MTAJUA NA KUONA YA KUWA UOVU WENU NI MWINGI SANA, MLIOUFANYA MACHONI PA BWANA, KWA KUJITAKIA MFALME.

18 Basi Samweli akamwomba Bwana, naye Bwana akapeleka ngurumo na mvua siku ile; nao watu wote wakamwogopa Bwana sana, na Samweli pia.

19 Watu wote wakamwambia Samweli, Utuombee sisi watumwa wako kwa Bwana, Mungu wako, tusije tukafa; maana tumeongeza dhambi zetu zote kwa uovu huu, wa kujitakia mfalme.

20 Samweli akawaambia, Msiogope; ni kweli mmeutenda uovu huu wote; lakini msigeuke na kuacha kumfuata Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa mioyo yenu yote. 

21 Wala msigeuke upande, maana, kufuata vitu vya ubatili, 

22 visivyoweza kusaidia wala kuokoa, kwa kuwa havifai kitu. Maana Bwana hatawaacha watu wake kwa ajili ya jina lake kuu; kwa kuwa imempendeza Bwana kuwafanya ninyi kuwa watu wake mwenyewe. 

23 WALAKINI MIMI, HASHA! NISIMTENDE BWANA DHAMBI KWA KUACHA KUWAOMBEA NINYI; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka”

Hapo mstari wa 23, Nabii Samweli anawaombea wana wa Israeli kwa Bwana, ambao kimsingi walikuwa wanaenda kuangamizwa kutokana na dhambi yao ya kujitakia mfalme, lakini Samweli anasimama kuwaombea na kuwaambia maneno ya faraja.

Je na sisi tunawaombea wengine na kuwapatanisha na Mungu wao kama alivyofanya Musa na Samweli?

Huenda hasira ya Mungu imewaka juu ya kanisa la Mungu, je! Unasimama kuliombea?, huenda hasira ya Mungu imewaka juu ya familia yako, je unasimama kuiombea toba?..huenda hasira ya Mungu imewaka juu ya ndugu zako, juu ya jamii yako, juu ya nchi yako, juu ya watu wengine.. Je unasimama kuwombea? Au unawahukumu na kuwalaumu?.

Bwana atusaidie tuwe watu wa kuwaombea wengine na kuwapatanisha na Mungu wao, na hata ifikie hatua ya kuona kuwa “KUTOWAOMBEA WENGINE NI DHAMBI”, na hapo tutafananishwa kama wana wa Mungu. Kumbuka siku zote kuwa Mungu anatumia watu, na hivyo katika wokovu wa wengine anatafuta mtu atakayeweza kusimama mahali palipoboka ili asimwage hasira yake, na mtu huyo ni mimi na wewe, ikiwa tutakuwa tayari kutumiwa na yeye.

Mathayo 5:9 “Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

TAA YA MWILI NI JICHO,

NIFANYE NINI NIWEZE KUDHIBITI HASIRA?

TAFUTA HEKIMA, MAARIFA, UFAHAMU NA BUSARA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuota unakata kucha.

Nini tafsiri ya kuota “unakata kucha”

Swali: Niliota nipo kanisani na mimi ndio bibi-arusi, na mchungaji akaniambia nitoke nikakate kucha ndio nirudi kufunga ndoa, nini tafsiri yake?

Jibu: Tusome mistari ifuatayo.

Kumbukumbu 21:10 “Utakapokwenda vitani kupigana juu ya adui zako, na Bwana, Mungu wako, awatiapo mikononi mwako, nawe uwachukuapo mateka,

11 ukaona kati ya mateka mwanamke mzuri, ukafanya tamaa kwake, ukawaza kumtwaa kuwa mkeo;

12 ndipo umchukue kwenu nyumbani kwako, naye atanyoa kichwa, AKATE NA KUCHA

13 avue na mavazi ya uteka wake akae nyumbani mwako, awakalie matanga babaye na mamaye mwezi mzima, kisha uingie kwake uwe mumewe, naye awe mkeo.”

Kucha ndefu za mkononi ni ishara ya “uteka”. Mwanamke aliyetekwa katika vita zamani, kabla ya kuolewa na wale waliomteka ilikuwa ni sharti wamnyoe nywele na kumkata kucha!. Lengo la kufanya vile ni kuondoa ufahamu wa maisha ya kwanza, na kumweka katika ufahamu wa maisha mapya.. ambapo kiroho ni kama anaondolewa roho ya uteka ndani yake, na kuingizwa roho ya uhuru katika jamii mpya anayoenda kuianza.

Kwahiyo kama wewe ni mwanamke, na umeota mchungaji amekwambia ukakate kucha ndipo urudi ufunge ndoa ,tafsiri yake ni kwamba kuna vifungo umefungwa ambavyo ni lazima vifunguliwe kwanza ndipo uweze kuingia katika ndoa!.

Ni kifungo kikubwa na cha kwanza ndani ya maisha ya mtu ni “dhambi”. Biblia inasema “atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi” (Yohana 8:34).

Kwahiyo ni lazima ujiangalie maisha yako na ufikiri kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, na pia kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu Kristo ili upate ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38) na pia kupokea Roho Mtakatifu. Kwa kufanya hivyo utakuwa umewekwa huru mbali na kifungo cha dhambi na vifungo vingine vya roho na mwili.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba kucha ndefu ni ishara ya utumwa wa dhambi, hivyo zingatia kuokoka kikweli kweli, kabla ya kufanya mambo mengine yoyote, usijivunie dini wala dhehebu, bali okoka na simama.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Kuota unasubiriwa mahali fulani uhutubie, halafu unachelewa.

Kuota upo nchi nyingine.

KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

KUOTA UNATOKA DAMU YA HEDHI.

KUOTA UNAKOJOA KITANDANI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kumaka ni nini katika biblia? (Mathayo 8:27)

Jibu: Neno “kumaka” limeonekana mara mbili katika biblia na maana yake ni “kushangaa/ mshangao”. Mtu anapokutana na jambo au anapoona kitu au tukio la ajabu ambalo hajawahi kuliona au kukutana nalo hapo kabla huwa anapatwa na mshangao! Sasa huo mshangao ndio unaoitwa “kumaka”.

Mathayo 8:27  “Wale watu WAKAMAKA wakisema, Huyu ni mtu wa namna gani hata pepo na bahari zamtii?”

Hapa wanafunzi walipomwona Bwana Yesu anazikemea pepo za bahari na kumtii, waliingiwa na mshangao wa ajabu kujiuliza yule ni mtu wa namna gani?

Utalisoma tena tukio hilo katika Luka 8:27, Lakini pia utaona Bwana Yesu alifanya mambo mengi makubwa ambayo yaliwashangaza watu wengi, (soma Marko 5:42, na Luka 4:36).

Hiyo ni kuonesha uweza wa Bwana Yesu Kristo wa kutenda miujiza ulivyokuwa Mkuu. Lakini uweza Mkuu na Muujiza Mkuu Bwana Yesu alioufanya na anaondelea kufanya leo, ambao hakuna mwingine yeyote awezaye kuufanya ni Muujiza wa KUFUTA DHAMBI!.

Miujiza mingine yote Bwana Yesu alisema nasi pia tunaweza kuifanya, lakini ule wa kusamehe dhambi ni yeye tu ndiye anayeweza kuufanya.

Marko 2:9 “Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?

10  Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza)”

Kwahiyo na sisi tunapaswa kuutafuta na kuupokea huu muujiza mkuu anaotoa Bwana Yesu wa kusamehewa dhambi, kwasababu kama hatutasamehewa dhambi na tukaponywa magonjwa peke yake bado haitatufaidia chochote, lakini tukipata msamaha wa dhambi hata kama tusipopokea uponyaji wowote katika mwili bado ni faida kubwa kwetu, kwasababu tutaurithi uzima wa milele.

Je! Umepokea msamaha wa dhambi zako?.. na je unaijua kanuni ya kupokea msamaha mkamilifu kutoka kwa Bwana?

Kanuni ya kupokea msamaha wa dhambi ni rahisi, nayo ni Kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu. Hatua hizo tatu ukizifuata, utapokea muujiza ambao hujawahi kuupokea katika maisha yako yote.

Matendo 2:36  “Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

37  Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39  Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

NI NINI BWANA ANATAKA KUTOKA KATIKA MUUJIZA ALIOKUFANYIA?

BABA UWASAMEHE

NINI MAANA YA KUTUBU

UMEONDOLEWA DHAMBI?

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana jijaribuni wenyewe na ‘isipokuwa mmekataliwa’?

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema jithibitisheni wenyewe kama mmekuwa katika imani, na pale pia inaposema “isipokuwa mmekataliwa”? Maana yake ni nini?

2 Wakorintho 13:5

[5]Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa.

JIBU: Kama wakristo biblia inatuasa tuwe watu wa kufanyia mazoezi Imani yetu, ili tujithibitishe kama kweli tupo katika mstari sahihi wa Imani au la.

Ili kuelewa tuchukue mfano wa  kijana mdogo ambaye anajifunza kuendesha baiskeli. Kwa hatua za mwanzo ni dhahiri kuwa atatumia baiskeli yenye miguu mitatu, ili iweze kumsaidia kumpa uwiano asianguke, na hivyo akiwa katika baiskeli Ile anaweza kuiendesha Kwa jinsi awezavyo kwasababu akikosa ule uwiano( balance), basi Ile miguu ya pembeni itamsaidia..na hivyo ataendesha bila changamoto yoyote, kama tu yule mtu anayejua kuendesha.

Lakini ijapokuwa atakuwa  anaiendesha Kwa kasi au maringo kiasi gani bado hajaweza kuwa mwendeshaji kamili, Mpaka siku yatakapotolewa Yale matairi ya pembeni, na kumwacha aimudu  mwenyewe ile baiskeli kama waendeshaji wengine. Pale ndipo utakapojua kweli huyu alikuwa ameshaweza au la!. 

Hivyo tunaweza kusema, kama hajaweza kujisimamia mwenyewe tayari amekataliwa (yaani, hajakubalika kama mwendesha baiskeli kamili)

Ndivyo ilivyo katika ukristo. Kuna wakati utakuwa unashikwa mkono, lakini upo wakati utahitaji kusimama mwenyewe kujithibitisha, kwamfano labda ilikuwa ikifika muda wa maombi unapigiwa simu/ au unahimizwa na kiongozi wako kufanya hivyo, na kweli unaamka na unasali sana. Lakini huna budi kujijengea ufahamu huu ikiwa siku moja kiongozi wako hayupo, au amesahau kukupigia simu au amepoa  je utaamka mwenyewe uombe?. Ukiona Unaweza kufanya hivyo basi tayari wewe umethibitika katika Imani. Lakini ikiwa ni kinyume chake basi bado kiroho hujakubalika.

Jiulize unapokuwa Mazingira yasiyo ya kikanisa, mazungumzo unayozungumza ni ya namna gani. Ikiwa sio ya maana, hata kama utakuwa unahubiri na kuzungumza habari za Mungu, uwapo na wapendwa muda mrefu kiasi gani..bado kiroho hujakubalika (umekataliwa)..unapaswa ujitengeneze .

Hivyo yatupasa tujijaribu Kwa namna hiyo. Ukristo ni sisi kuwa Nuru katika Giza, sio Nuru katika Nuru tu. Hatuvai vizuri tunapokwenda kanisani tu, Bali hata tunapokuwa katika Mazingira yasiyo ya ibadani. Huko ndiko kujithibitisha. Mungu anavutiwa na mkristo anayethibitisha Imani yake miongoni mwa wenye dhambi zaidi ya yule anayefanya Kwa waaminio. Jitathimini unapokuwa mwenyewe, ni Nini unatazama mitandaoni, muda wako mwingi unautumiaje,ni nani unayechati naye?. Wajibu wako Kwa Bwana unautimizaje? Huko ndiko kujithibitisha.

Lakini ikiwa tuwapo nje tunashindwa kuwa kama tuwapo ndani basi hilo Neno “isipokuwa mmekataliwa”, ndio linakuja..maana yake bado hatujakidhi vigezo vya kiroho, Mungu anavyovitazamia kwetu. Ukiwa ni kundi la kusukumwa  kutenda jambo Fulani la kiroho lililo wajibu wako, bado hujakubalika.

ukiona hivyo basi yakupasa ufanye juhudi, kumaanisha wokovu wako Kwa Mungu. Kama mkristo usijisifu kwenye juhudi za kusimamiwa, jisifu kwenye juhudi za kujisimamia.

Hiyo ndio tafsiri yake, lakini Neno hilo halimaanishi kama watu wengine wanavyodhani kuwa wapo watu ambao “Mungu amewakataa” ambao hata iweje hawawezi kuupokea wokovu hapana, watu wote wanapokelewa na Mungu wanapotii sauti ya Mungu. Hakuna mtu ambaye akimfuata Mungu hata akionyesha juhudi kiasi gani  atakataliwa, hapana.

Bwana akubariki.

Je! Na wewe upo kundi gani? Una habari kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Neema ya Kristo inakuita hata Leo, ujue kuwa haitafanya hivyo milele. Ni heri utubu dhambi zako ufanye badiliko, upate ondoleo la dhambi, Yesu Akupe uzima wa milele. 

Ikiwa upo tayari Kwa jambo hilo basi..fungua hapa Kwa mwongozo huo >>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mathayo 23:15 inaposema namfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Nini maana ya “wanawake saba watamshika mtu mume mmoja”

NI NANI ATAKAYEWAPA ILIYO YENU WENYEWE?

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

UNAVYOZIDI KUWA MWENYE HAKI, NDIVYO KUJITAMBUA KWAKO KUNAVYOPUNGUA.

Rudi nyumbani

Print this post

Jina Lusifa (lucifer), tunalisoma wapi kwenye biblia? 

JIBU: Hakuna Mahali popote katika biblia ya Toleo letu la Swahili Union version (SUV) au matoleo mengine kadha wa kadha ya kiswahili, utapishana na hili Neno Lusifa. Lakini swali, kama ni hivyo Kwanini tunalitumia kumwakilisha shetani. Je! Limetokea wapi?

Neno hili ni la kilatini, ambalo linamaanisha NYOTA YA ALFAJIRI. Hivyo tukirudi katika maandiko upo unabii katika kitabu Cha Isaya unaomwelezea shetani, na unamtaja yeye kama ndio  Ile “Nyota ya alfajiri”

Isaya 14:12

[12]Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi!  Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!

Hivyo watakatifu wa zamani, walipokuwa wanatafsiri biblia kutoka katika lugha ya kiyahudi kwenda kilatini (vulgate), kwenye Karne ya 4  Ndipo Neno hili nyota ya alfajiri ambalo linalosomeka kama “Helel” Kwa lugha ya kiebrania likaandikwa kama “lusifa” Kwa kilatini.

Na baadaye Neno hili lilikuja kupata umaarufu, zaidi katika biblia ya Toleo la kiingereza inayojulikana  kama King James version (KJV), kwani waliendelea kuliacha Neno hili la kilatini, Mahali palepale  panaposema nyota ya alfajiri. 

Hivyo umaarufu wa Neno hilo ukasambaa sio tu Kwa waongeaji wa lugha ya kilatini, Bali mpaka Kwa wale wa kiingereza. Na ndio maana mpaka sasa wewe unalifahamu.

Lakini matoleo mengine mengi, Ikiwemo letu hili la kiswahili (SUV), haikutoa katika hiyo lugha ya kilatino, Bali imeacha vilevile kama nyota ya alfajiri.

Hivyo Kwa kuhitimisha ni kuwa shetani ndio huyo huyo Lusifa. Ikiwa utapenda kufahamu majina yake mengine kama yanavyotajwa kwenye biblia basi fungua hapa >>> APOLIONI.

Je! Unahabari kuwa hizi ni siku za mwisho na Yesu anakaribia kurudi? Umejiandaaje? Kumbuka shetani anatambua kuwa muda wake umeisha(Ufunuo 12:12), iweje wewe usitambue. Ni nini unachokisubiria usimkaribishe Yesu katika maisha Yako?  Huu ulimwengu hauna muda mrefu unaisha, itakufaidia nini upate kila kitu, kisha upate hasara ya nafsi yako? Jifikirie  usisubiri kukumbushwa kumbushwa, ni wewe mwenyewe kuona hali halisi, kisha uchukue hatua

, ikiwa upo tayari Kumpa Bwana Yesu maisha yako, basi fungua hapa Kwa mwongozo wa Sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

 Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Shetani ni nani?

YUKO WAPI MFALME WA WAYAHUDI?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

Rudi nyumbani

Print this post

KUWA NA  MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.

Moja ya maeneo ambayo yamekuwa na uelewa mchanga katika ukristo, ni pamoja na eneo la Roho Mtakatifu. Wengi tunachofahamu kuhusiana na huduma ya Roho Mtakatifu ni kunena kwa lugha tu! Basi. Lakini hilo ni tone moja kati ya bahari kubwa, tunahitaji kumwelewa kwa mapana na marefu ili tujue utendaji kazi wake ulivyo kwa wanadamu na ulimwengu.

Kipo kitabu cha Roho Mtakatifu, ikiwa utapenda kukipata wasiliana nasi kwa namba zilizo chini ya chapisho hili/ au tutumie ujumbe whatsapp.

Leo  tutaona sehemu mojawapo ambayo inahusiana na mafuta ya Roho Mtakatifu.  Unaweza ukajiuliza, kwanini kila mara watu waliposhukiwa na Roho Mtakatifu, maandiko yanatumia neno “wakajazwa”, na sio neno kama ‘wakavikwa’  au labda ‘wakalishwa’. Kwasababu tukisema wakavishwa maana yake tunamfanya yeye kuwa kama nguo, au tukisema wakalishwa tunamfanya yeye kuwa kama chakula. Lakini tukisema wakajazwa tunamfanya yeye kuwa kama kimiminika, na hicho si kingine zaidi ya MAFUTA. Roho Mtakatifu anakuja kwetu kama MAFUTA. Ni vema kulitambua hilo!

Sasa si watu wote wanayo mafuta yote ya Roho Mtakatifu kama Bwana Yesu alivyokuwa,. Leo tutaona aina mbalimbali za mafuta hayo, kisha tujitahidi tuyapokee yote kwa msaada wa Roho.

1.Mafuta ya nguvu

Haya yanapatikana katika UMOJA.

Zaburi 133:1 Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa umoja.  2 Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake.

Maana yake ni kuwa jinsi watakatifu wanavyoshirikiana  pamoja kwa umoja, rohoni, yanaonekana ni mafuta mengi yanashuka katikati yao, mengi kiasi cha kufika hata katika upindo wa mavazi. Wanatiwa mafuta, na hayo ni ya nguvu. Kwasababu palipo na umoja ndipo penye nguvu.

Na ndio maana siku ile ya pentekoste, Mungu aliwakutanisha kwanza mahali pamoja wakawa wapo orofani pale sio katika kupiga zoga, hapana, bali katika kusali na kuomba, na kutafakari maneno ya Bwana(Matendo 1:12-14). Na ghafla, wakashangaa, katika siku ya kumi, Roho Mtakatifu amewashukia wote wakajazwa nguvu. Wakawa mashahidi wa Bwana tangu siku ile  na kuendelea (Matendo 2).

Jambo kama hilo utalithibitisha tena katika Matendo 12:14, walipokuwa wamekaa pamoja kumwomba Mungu, mahali pale pakatikiswa, wajazwa Roho Mtakatifu wakanena Neno la Mungu kwa ujasiri. Hivyo hivyo na sisi  tupenda ushirika na wengine, hususani katika kuomba na kufunga. Tukiwa watu wa namna hii tutajazwa mafuta haya na tutapokea ujasiri mwingi sana katika wokovu wetu.

Soma (Mhubiri 4:12)

2. Mafuta ya shangwe

Haya yanapatikana katika usafi na utakatifu.

Waebrania 1:8  Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9  Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio

Shangwe ni ile furaha iliyopitiliza, inayodhihirika hata mpaka kwa nje. Halikadhalika Roho Mtakatifu naye anayo shangwe yake, ambayo hiyo inazidi hata hii ya kidunia, kwasababu ya kwake inakufanya ufurahi sio tu katika raha bali mpaka katika majaribu. (Luka 10:21)

Kwamfano utaona Bwana Yesu alikuwa nayo hata pale msalabani.

Wakolosai 2:15  akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.

Tukiwa watu wa kupenda haki(utakatifu), mafuta haya Roho anayaminina, mioyoni mwetu. Maisha yetu yanakuwa ni ya furaha tu, daima, vipindi vyote. Haijalishi mauvimu, kero, udhia, yataonekana kwa nje, lakini rohoni ni shangwe nyingi za Roho Mtakatifu, ndivyo Mungu alichokiweka ndani ya Kristo na kwa wakatifu wa kale ( Matendo 13:52, Waebrania 11:13, , Mathayo 5:12).

Hivyo Tuchague kupenda maisha ya haki ili tuyapate mafuta haya. Ni muhimu sana, ukipoteza furaha ya wokovu, huwezi kusonga mbele.

3. Mafuta ya upambanuzi

Haya yanaachiliwa katika kulitunza Neno la Mungu ndani yako.

1Yohana 2:26  Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza. 27  Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake.

Kumbuka biblia ni sauti ya Mungu katika maandishi, hivyo unavyoiweka moyoni mwako, ndivyo inavyoumbika  na kuwa sauti kamili ya Mungu. Na hiyo ndio itakayokufudisha, na kukusaidia kupambanua, ikiwa wewe ni mkristo na una miaka  mingi katika wokovu halafu hujawahi kuisoma BIBLIA yote, bado kuna viwango Bwana hawezi kusema na wewe.  Lakini Unavyozidi kujifunza Neno ndivyo mafuta haya yanavyoachiliwa ndani yako kukufundisha. “Huna Neno, huna sauti ya Mungu”

4. Mafuta ya kuhudumu

Haya huachiliwa katika kuwekewa mikono na wakufunzi wako, au kuombewa na kanisa (wazee wa kanisa).

Huu ni utaratibu mwingine Mungu ameuachilia, katika kanisa, vipo vitu ambavyo huwezi kuvipokea wewe tu mwenyewe. Bali kutoka kwa waliokutangulia kiimani.

Elisha alitiwa mafuta na Eliya, akasimama mahali pake kihuduma (1Wafalme 19:15-16)

Musa aliwatia mafuta wale wazee 70, sehemu ya roho yake ikawaingia (Hesabu 11:16-25)

Daudi na Sauli wote walitiwa mafuta ya Samweli, ndipo wakapokea nguvu kutoka kwa Mungu, kutumika. (1Samweli 15:1, 16:12,)

Vilevile Timotheo, aliwekewa mikono na mtume Paulo  (2Timotheo 1:6), akapokea neema ya kuyasimamia makanisa ya Kristo, mahali pa Paulo.

Vivyo hivyo na wewe usikwepe, wala usimdharau kiongozi wako wa kiroho, hata kama atakuwa ana madhaifu. Anayo sehemu yake aliyopewa na Mungu kwa ajili yako. Jinyenyekeze omba akuwekee mikono neema ya Mungu ijae ndani yako ya kuhudumu, ili Bwana akunyanyue katika viwango vya juu zaidi.

Hivyo kwa kuzingatia aina hizo 4, tukazipokea basi tutamsogelea Bwana katika mafuta mengi sana ya juu. Mfano wa Bwana wetu Yesu Kristo. Roho Mtakatifu atajifunua zaidi ndani yetu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Nini maana ya’Shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo’Ayubu 20:4

Wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza

Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?

Masihi ni nani?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Wapalestina ni watu gani, na sehemu yao katika biblia ni ipi?

Jina Palestina limetoka na Neno la kiyunani Filistia,  lenye maana ya ardhi ya wafilisti. Kwahiyo ile Filisti inayotajwa kwenye biblia ndio Palestina unayoisikia sasa.

Lakini Jambo ambalo wengi wanachanganya ni kudhani kuwa wafilisti walikuwa ni waarabu. Si kweli, kwani waarabu walikuwa ni watoto wa Ishmaeli kutoka kwa Ibrahimu, lakini wafilisti walikuwepo kabla hata ya Ibrahimu, na walitokea katika uzao wa Hamu.

Mwanzo10:14 na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti na Wakaftori.

Watu hawa walikuwa ni wapagani moja kwa moja, na waliabudu miungu yao mikuu mitatu iliyoitwa Ashtorethi, Baal-zebubu, na Dagoni.(Waamuzi 16:23, 2Wafalme 1:2, 1Samweli 31:10,)

Wafilisti walikwenda kuweka makazi yao, katika nchi ya Kaanani. Upande wa kusini, kutoka mto Yordani mpaka ule wa ile habari kubwa (Bahari ya Mediterenia). Na baadaye kipindi cha akina Samweli wakawa na miji yao mitano imara iliyoitwa Gaza, Ashdodi, Gathi, Ashkeloni, Ekroni (1Samweli 6:17, Yoshua 13:3)

Hivyo Ibrahimu alipoitwa na Mungu na kuambiwa aindee nchi ile aliwakuta tayari wapo, na wameshajiwekea ngome zao (Mwanzo 21:32, 34, 26:1).

Na wana wa Israeli walipokuwa wanavuka kuingia nchi yao ya ahadi Waliambiwa wawaangamize wakaanani wote, kwasababu wamepewa nchi yote. Lakini tunaona walipuuzia, na kule kukawia kawia kwao na kuridhika, Mungu akawaambia watu hawa watakuwa “mwiba” kwao .  

Waamuzi 2:1 Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi;  2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani?  3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.

Na ndivyo ilivyokuwa Yoshua hakuweza kuwatoa wenyeji wote wa Filisti(Yoshua 11:20-23). Na ndio hao wakaja kuwasumbua baadaye.

Ni wazi kuwa Israeli walipigana vita vingi, lakini moja wa maadui zao waliokuwa wanawasumbua sana basi ni hawa wafilisti, kwasababu walikuja kupata nguvu, sio tu ya wingi wa watu, bali pia ya kiteknolojia katika silaha, kiasi kwamba Israeli ilitegemea kunolewa silaha zao kutoka Filisti.(1Samweli 13:19-23). Na zaidi sana waliwazidi Israeli hata kimaendeleo, kwa kipindi kirefu hawakuweza kuwashinda

Na wana wa Israeli walipomkosea Mungu aliwaweka kwenye mikono yao, wakataabishwa kwa muda mrefu, kisha walipomlilia Bwana, walinyanyuliwa mkombozi. Ndio hapo tunawaona waamuzi kama wakina Samsoni, Shamgari, Samweli, Sauli, Daudi.Wakipigana vita vingi sana na watu hawa.Ambavyo tunavyosoma katika biblia (Waamuzi, Samweli 1&2, Wafalme 1&2,)

Kuanguka kwa wafilisti.

Lakini wakati Israeli inachukuliwa utumwani taifa hili nalo halikupona lilianguka, katika mkono wa mfalme Nebukreza wa Babeli, na kupotea kabisa. (Yeremia 47:47, Ezekieli 25:15-17, Sefania 2:4-7).

Tangu huo wakati hakukuwa na taifa rasmi la wafilisti, wala haikuwa rahisi kuwatambua kwa miaka zaidi ya 2500.  Mpaka ilipofikia mwaka 1948, Taifa la Israeli kuundwa tena kwa mara ya kwanza, eneo hilo la wafilisti, kusini mwa Israeli, lilikuwa tayari linajulikana kama “Palestina”

Palestina ya leo ni mahali palipo na mchanganyiko wa jamii mbalimbali za watu, walio wa asili ya kifilisti wakiwa ni wachache sana, lakini wengi wao sasa ni waislamu waliohamishiwa hapo na waturuki, kutoka katika mataifa mbalimbali kati ya karne ya 16-19, pamoja waarabu katika karne ya 20 ambao nao waliletwa na waingereza.

Hivyo mpaka sasa tunavyoona, ni kwamba Palestina imemezwa zaidi na dini ya kiislamu na jamii kubwa ya waharabu. Na cha kushangaza ni kwamba ijapokuwa  jamii ya sasa ni tofauti kabisa,na wafilisti wa zamani, bado migororo ile ile ya zamani inanyunyuka tena. Kuonyesha kuwa Neno la Mungu halipiti milele.

Ule mwiba bado utawasumbua wayahudi.

Nini kinaendelea rohoni?

Lakini ipo sababu nyingine ya Rohoni. Kumbuka kuwa hatma ya huu ulimwengu, itakuwa ni Dunia nzima kusimama kinyume na taifa teule la Mungu Israeli. Ili Yesu Kristo atokee mawinguni na kuwapigania watu (Matendo 1:6, Ufunuo 19) .  Na tayari Mungu alishaahidi kuwa atafanya mataifa yote kuwa kama kikombe cha kulemea,. Ili tu ayachonganishe, kisha mwisho wake uwe ni yeye kulitetea taifa lake, ndipo huo mwisho ufike.

Wewe huoni mvuragano huu, unayagusa mataifa yote duniani.

Zekaria 12:3 Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake

Unaweza kuona ni jinsi gani tupo mwishoni kabisa mwa dunia. Hii neema tuliyonayo huku katika mataifa, ndio inafikia ukomo wake, na kurejea Israeli. Maana Mungu anasema atawarudia watu wake (Warumi 10&11), na kuwaokoa, wakati huo yatakapokuwa yanatendeka unyakuo utakuwa umeshapita huku kwetu.

Zekaria 12:9 Hata itakuwa siku hiyo, ya kwamba nitatafuta kuwaangamiza mataifa yote watakaokuja kupigana na Yerusalemu.  10 Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.  11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido

Je! Unaishije sasa hivi, Umehubiriwa injili mara ngapi, bado unashupaza shingo yango? Huko uendako unatarajia ukawe mgeni wa nani. Na ukweli umeshaujua kuwa tunaishi katika siku za kumalizia, Unyukuo wa kanisa ni wakati wowote. Huu ni wakati sasa ya kuyathimini maisha yako ya rohoni, angalia dunia inapoelekea, kufumba na kufumbua mambo yanabadilika. Uamuzi ni wako. Lakini ikiwa utapenda Yesu akuokoe, akufanye kiumbe kipya basi fungua hapa upate mwongozo wa sala ya toba. >>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

USIMPE NGUVU SHETANI.

Mataifa ni nini katika Biblia?

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Washami ni watu gani katika biblia?

Jibu: Washami wametajwa mara nyingi katika biblia, baadhi ya mistari iliyowataja na kama ifuatayo.. 2Samweli 8:6, 1Wafalme 20:21, 2Wafalme 5:2, Yeremia 35:11, Amosi 9:7 na sehemu nyingine nyingi utaona jamii hii ya watu ikitajwa.

Tukio mojawapo maarufu lililozungumziwa katika biblia liwahusulo Washami, ni lile la Nabii Elisha kulipiga upofu Jeshi lao na kuliongoza mpaka katikati ya Samaria. (soma 2Wafalme 6:10-20).

Sasa swali hawa Washami walikuwa ni watu gani?

Washami walikuwa ni watu walioishi katika Nchi ijulikanayo kama Siria/Syria kwasasa,

Kiswahili cha Siria ni  “Shamu” hivyo wenyeji wa nchi ya Shamu ndio walioitwa Washami.

Jamii ya watu hawa Washami, kwasasa haipo!, wala haijulikani, kutokana na Falme nyingi kupita zilizotawala dunia na hivyo kuchanganya jamii za watu katika maeneo husika, hivyo hakuna jamii ya washami ijulikanayo leo duniani, lakini nchi hiyo bado ipo, na sasa wanaishi waarabu (Uzao wa Ishmaeli), ndio inayoitwa Siria, na makao makuu yake ni Dameski. (Kumbuka hawa waarabu sio washami  waliozungumziwa katika biblia, bali wapo tu kama wahamiaji waliohamia katika hiyo nchi)

Kiroho Washami wanawakilisha jeshi la Adui, kwani ukisoma katika biblia  utaona ni karibia mara zote jeshi hili lilikinzana na Israeli. Na utaona wakati ule Elisha alipokuwa na mtumish wake, walipoona jeshi la Washami limewazunguka, Elisha alimwambia mtumishi wake asiogope kwani walio upande wao ni wengi kuliko jeshi wanaloliona mbele yao.

2Wafalme 6:15 “Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?

16 Akamjibu, USIOGOPE; MAANA WALIO PAMOJA NASI NI WENGI KULIKO WALE WALIO PAMOJA NAO.

17 Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.”

Hali kadhalika na sisi ni lazima siku zote tuone, na kufahamu kuwa jeshi la Mungu linalotuzunguka ni kubwa kuliko lile la Adui, ikiwa tupo ndani ya Neema ya damu yake!, lakini kama tupo nje ya Neema ya damu yake (yaani wokovu), basi tufahamu kuwa adui atakuwa na nguvu juu yetu, na wala hakuna tutakachoweza kumfanya, Nguvu yetu na ujasiri wetu upo katika Yesu tu?

Je umeokoka? Kama bado ni afadhali ukaokoka leo, maana hujui kesho itakuwaje, na kama unahitaji msaada huo basi wasiliana nasi kwa namba zetu tajwa hapa chini.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Wasamaria walikuwa ni watu gani?

Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Je Yuda alienda wapi, ni mbinguni au jehanamu?

Rudi nyumbani

Print this post

Nchi iligawanyikaje kama tunavyosoma katika Mwanzo 10:25?

Swali: Je katika Mwanzo 10:25 tunasoma kuwa nchi/dunia iligawanyika? Swali ni Je! Iliwaganyikaje? Na je ule ndio ulikuwa mwanzo wa mabara saba (7) tuliyonayo leo?.

Jibu: Tusome,

Mwanzo 10:25 “ Eberi akazaliwa wana wawili wa kiume; jina la wa kwanza ni Pelegi maana KATIKA SIKU ZAKE NCHI ILIGAWANYIKA; na jina la nduguye ni Yoktani”.

Kama ukiendelea mbele kidogo kusoma Mlango wa 11 wa kitabu hiko cha Mwanzo utaona kuna tukio lilitokea ambalo ndio lile la kujengwa kwa Mnara wa Babeli, ambapo watu wale walipokuwa katika hatua za awali za kuujenga Mungu alishuka na kuchafua lugha zao na Semi zao, ili wasisikilizane. Na hiyo ikawafanya waache kuujenga ule mnara na kila mmoja kutawanyika na njia yake.

Mwanzo 11:1 “Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja. 

2 Ikawa watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari; wakakaa huko. 

3 Wakaambiana, Haya, na tufanye matofali tukayachome moto. Walikuwa na matofali badala ya mawe, na lami badala ya chokaa.

4 Wakasema, Haya, na tujijengee mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote.

5 Bwana akashuka ili auone mji na mnara waliokuwa wakiujenga wanadamu.

6 Bwana akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. 

7 Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao.

 8 BASI BWANA AKAWATAWANYA KUTOKA HUKO WAENDE USONI PA NCHI YOTE; wakaacha kuujenga ule mji.

 9 Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote”.

Hapo Mstari wa 8  unasema “BWANA AKAWATAWANYA KUTOKA HUKO WAENDE USONI PA NCHI YOTE”.

Sasa huo Mtawanyiko waliotawanywa wanadamu ndio “mgawanyiko wa nchi” unaozungumziwa katika Mwanzo 10:25 na unarudiwa tena katika 1Nyakati 1:19, Na ulitokea katika nyakati za mtu mashuhuri aliyeitwa “Pelegi” aliyekuwa mwana wa Eberi.

Hivyo mgawanyiko wa nchi haukuwa wa kiografia bali wa watu!.. na wala mabara 7 hayakuzaliwa hapo!, na Zaidi sana biblia haijataja mahali  popote kuwa dunia iligawanyika na kuwa mabara 7, huenda yalikuwa hivi hivi saba tangu uumbaji, au huenda yalizalika kipindi Fulani baada ya uumbaji, tusichokijua sisi lakini  si hiko kilichotajwa katika Mwanzo 10:25. Mgawanyiko huo wa Mwanzo 10:25 unahusu watu na si mabara.

Kujua ufunuo uliopo nyuma ya mnara wa Babeli basi fungua hapa >>TUUTAFUTE USEMI MMOJA. TUUJENGE MNARA WA MUNGU

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

MNARA WA BABELI

Babeli ni nchi gani kwasasa?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)

Shokoa ni nini katika biblia?

YESU KATIKA USINGIZI WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post