Title 2023

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Mathayo 9:14  “Wakati ule wanafunzi wake Yohana wakamwendea, wakasema, Kwa nini sisi na Mafarisayo twafunga, BALI WANAFUNZI WAKO HAWAFUNGI?

15  Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja WATAKAPOONDOLEWA BWANA ARUSI; NDIPO WATAKAPOFUNGA”.

Wanafunzi walipokuwa na Bwana Yesu katika mwili, chochote walichokihitaji walikipata kirahisi kwasababu Neema walikuwa naye katika mwili, walipohitaji uponyaji Kristo alikuwepo kuwaponya, walipohitaji kuona ishara na miujiza kama ile ya mikate mitano kulisha elfu tano, waliiona kirahisi.

Kila walichokihitaji walikipata, kwasababu Mtenda miujiza walikuwa wanamwona dhahiri na kumshika. Lakini ulipofika wakati wa Kristo kuchukuliwa juu, mambo yalibadilika!!, ile hali ya kusubiria kufanyiwa mambo na Bwana ikapotea, ikawabidi waanze kutafuta wenyewe namna ya kufanya mambo!. Ni kama tu kifaranga cha kuku kilichoachwa na mama yake, kikawaida kinaanza kujitafutia chenyewe, kitatembea huku na kule kama mama yake kutafuta chakula.

Ndicho kilichowatokea Mitume Bwa Yesu, ulipofika wakati wanakutana na wagonjwa na yule Bwana Yesu wa kukimbiziwa  wagonjwa hayupo!!!.. ndipo ufahamu wa kutafuta nguvu alizokuwa nazo Bwana Yesu ukawajia!.

Ndipo wakaanza kutafiti ni vitu gani vilivyokuwa vinampa nguvu Bwana Yesu, kufanya miujiza ile na kuishi maisha yale!, ndipo wakaanza kutafakari maisha yake na kugundua kuwa muda mwingi Bwana aliutumia KUFUNGA na KUKESHA MILIMANI KUOMBA.

Na wao ikawabidi wabadilike na kuanza kuwa WAFUNGAJI NA WAOMBAJI kama Bwana Yesu ili baadhi ya mambo yawezekanike kama yalivyowezekanika kwa Bwana, vinginevyo baadhi ya mambo yasingeenda sawa, Ndio maana utaona akina Petro walipokuwa na Bwana ni kama walikuwa wanavutwa vutwa katika suala la uombaji (Utaona kuna mahali Bwana Yesu alikuja kuwaamsha Zaidi ya mara 2 waombe lakini wakarudi kulala).

Marko 14:34  “Akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa mkeshe.

35  Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akiomba ya kuwa, ikiwezekana, saa hiyo imwepuke. 36  Akasema, Aba, Baba, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki; walakini, si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.

37  AKAJA AKAWAKUTA WAMELALA USINGIZI, AKAMWAMBIA PETRO, JE! SIMONI, UMELALA? Hukuweza kukesha saa moja? 14.38  Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu.

39  Akaenda zake tena, akaomba, akisema neno lilo hilo.

40  AKAJA TENA AKAWAKUTA WAMELALA, maana macho yao yamekuwa mazito, wala hawakujua la kumjibu.

41  Akaja mara ya tatu, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike; yatosha, saa imekuja; tazama, Mwana wa Adamu anatiwa mikononi mwao wenye dhambi”.

Hapa tunaona akina Petro wakiwa wanavutwa vutwa katika suala la uombaji, lakini tunaona mambo yanabadilika baada ya Bwana Yesu kuondoka, walianza kufunga na kukesha katika maombi mengi,.. Kuna mahali Petro anaonekana kufunga kwa kuomba mpaka anazimia kwa njaa.

Matendo 10:9  “Hata siku ya pili, walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda kuomba, yapata saa sita ya mchana;

10  AKAUMWA NA NJAA SANA, AKATAKA KULA; LAKINI WALIPOKUWA WAKIANDAA, ROHO YAKE IKAZIMIA,

11  akaona mbingu zimefunuka, na chombo kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi”

Hii ikifunua nini?

Kristo mpaka sasa hayupo nasi katika Mwili, hivyo na sisi pia tupo katika Nyakati za KUFUNGA na KUOMBA.

Ndugu Hizi ni nyakati za “Kufunga na kuomba”. Bwana Yesu alisema mambo mengine hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kuomba/kusali.

Mathayo 17:21 “[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga]”

Je Unataka kumwona Mungu katika maisha yako?..Funga na kuomba!..je  unataka kuongezeka viwango vya kumjua Mungu?..Funga na kuomba!…Je Unataka Neema iongezeke juu yako! Na mambo mengine mengi yaliyo mazuri uyaone??, basi funguo ni Mifungo na Maombi. (Na kumbuka hapa biblia inazungumzia Maombi na sio maombezi). Usifunge na kwenda kutafuta kuombewa na mtumishi!.. Bali funga na omba mwenyewe!.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Kwanini maombi kwa Marehemu si sahihi kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?

Kwa utamaduni wa sasa mtu anapokufa, huwa anafukiwa chini ardhini, na juu huwekewa  kiashirio Fulani cha kawaida kuonesha eneo hilo lipo kaburi. Lakini  watu wengine hupenda kuyapa thamani makaburi ya watu wao, hivyo kwa juu hujengea, kichumba Fulani kinachopambwa kwa vito au mawe ya thamani , wengine wanaweka mnara Fulani n.k. Sasa vitu hivi vyote vinavyojengewa juu ndio huitwa Maziara.

Kwamfano katika picha hii, ni mfano wa Ziara ambalo lilijengwa na wenyeji wa Marekani kama kumuenzi raisi wao wa kwanza wa taifa hilo aliyeitwa George Washington.

Hata katika agano la kale, enzi za biblia, yapo makaburi yaliyokuwa ya kawaida, lakini pia yapo yaliyokuwa yamejengewa maziara. Na hayo yalikuwa hususani ya wafalme na manabii wakubwa waliotokea Israeli, ambao waliuliwa kikatili mfano wa hao  ni Zekaria, Hagai na Malaki.  Na waliohusika sana kutengeneza maziara haya walikuwa ni hawa waandishi na mafarisayo(Watu wa kidini). Wakidai kuwa wanawa-enzi manabii wao, lakini tunaona Yesu akiwakemea kwa dhambi ya unafki waliyokuwa wanaifanya kwa tendo hilo.

Tusome.

Mathayo 23:29  Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki, 30  na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii. 31  Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii. 32  Kijazeni basi kipimo cha baba zenu. 33  Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum? 34  Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji; 35  hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu. 36  Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.

Soma pia (Luka 11:47-48).

Swali ni je! Walikuwa wanafanya makosa kutenda jambo lile?

Jibu ni hapana, Bali walichokuwa wanakifanya nje, hakikuendana na kile kilichokuwa mioyoni mwao na ndio maana akawaita wanafiki. Kwasababu walikuwepo pia manabii wa Mungu na watu wenye haki wakati wao, mfano wa Yohana, pamoja na yeye mwenyewe lakini walikuwa wanataka kuwaua. Na ndivyo walivyokuja kufanya kwa Bwana, pamoja na mitume wako na watakatifu wa kanisa la kwanza kama vile wakina Stefano.

Je! Sisi tujengapo maziara kama heshima  kwa wafu wetu tunatenda dhambi?

Jibu ni la, Endapo tu hatutashirikisha ibada yoyote ya wafu mahali pale. Lakini kama ni kwa kumbukumbu, au kumu-enzi marehemu wako, hakuna shida kuweka ziara (kupamba kaburi lako kwa jinsi upendavyo). Lakini fahamu tu hilo halitakuongezea jambo lolote rohoni. Wala halimfaidii kwa lolote Yule marehemu kule alipo.

Je! Ni sawa kwa Mkristo kusafisha kaburi la mfiwa wako, na kufanya ibada mahali pale?

Kutunza kaburi lolote, yaani kulisafisha, kulirepea, kulipandia bustani, kulilinda.. Si kosa kibiblia, kwasababu tunaona katika biblia makaburi yalitunzwa kwa bustani, soma (Yohana 20:15), pia yalilindwa, Na zaidi yalihifadhiwa yasiharibiwe. Soma

2Wafalme 23:16 Naye Yosia alipogeuka, aliyaona makaburi yale yaliyokuwako huko, juu ya mlima; akatuma watu, akaitoa ile mifupa katika yale makaburi, akaiteketeza juu ya madhabahu, akainajisi, sawasawa na lile neno la Bwana, alilolinena yule mtu wa Mungu, aliyetamka mambo hayo.  17 Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli.  18 Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria.

Hivyo, upendapo kutunza kaburi la mpendwa wako, aliyefariki hufanyi kosa.

Vipi katika kufanya ibada?

Zipo ibada za wafu, ambazo ndizo zinazofanyika mara nyingi katika makaburi ya marehemu, ibadani hizo, zinahusianisha kuwaombea wafu hao, n.k. Ibada hizi ni za kipagani, na mkristo hapaswi kuzifanya ni  ibada za miungu. Au wengine wanakwenda kuzungumza na kaburi wakiamini Yule mtu yupo pale makaburini anawasikia. Huo ni uchawi.

Hivyo hakuna mahusiano yoyote ya kiibada katika makaburi. Endapo imetokea unakwenda kufanya maziara (yaani kukarabati au kupamba), basi unachofanya ni kufungua kwa maombi na kufunga kwa maombi, kisha mnaendelea na kazi yenu, ili kutimiza hili andiko

Wakolosai 3:17  “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Na kama mmeguswa kutafakari maneno ya Mungu mahali pale, kama mfanyapo sehemu nyingine zozote, mfano kazini, shuleni, chini ya mwembe n.k..  Basi iwe ni kwa Mungu na sio kwasababu ya makaburi. Epuka Ibada za wafu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

MAKABURI YAKAFUNUKA; IKAINUKA MIILI MINGI YA WATAKATIFU WALIOLALA;

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Nini maana ya kuabudu?

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

Praitorio ni nini? Na Kwanini ilikuwa ni najisi kwa wayahudi kuingia humo? (Yohana 18:28)

Nini maana ya Ukuta uliopakwa chokaa (Matendo23:3)?

Makanda ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.

Je unajua kuwa roho ya mpinga-kristo imeshaanza kutenda kazi na inaendelea kutenda kazi hata sasa?

1 Yohana 4:3 “Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; NA SASA IMEKWISHA KUWAKO DUNIANI”.

Andalizi la mwisho la Mpinga Kristo kabla ya chapa yake kuanza kufanya kazi ni hili “MUNGU HAANGALII MWILI BALI ROHO”.

Roho ya Mpinga-kristo inawaandaa sasa watu na hiyo saikolojia, kwamba waamini Mungu haangalii mwili bali roho tu.

Na kwanini anafanya hivyo?.. ni ili iwe vyepesi kwake siku ile  kuwatia watu CHAPA mwilini (Usoni na mikononi)

Kwasababu asipowaandaa na hiyo saikolojia itakuwa kwake ni ngumu sana kuwashinikiza waipokee chapa katika vipaji vya nyuso na katika mwili siku zile baada ya unyakuo wa kanisa kupita.

Kwahiyo anaanza na saikolojia ndogo tu kwamba kuvaa hereni sio kosa, kutoboa pua sio kosa, kujichora tattoo na hina sio kosa na kupaka lipstick midomoni na wanja machoni sio dhambi.. ( kwamba Mungu hawezi kumhukumu mtu kwa vitu vinavyowekwa mwilini)

Ndugu usidanganyike,  je! Umewahi kujiuliza kwanini Mungu atawahukumu watu wote watakaoipokea  ile chapa ya mnyama  katika VIPAJI vya nyuso zao na katika MIKONO yao siku ile?..

Kama Mungu haangalii mwili kwanini chapa ya 666 itiwe katika mwili na Mungu awahukumu wale wote watakaoipokea chapa hiyo?, maana maandiko yanasema watu wote watakaoipokea chapa hiyo katika vipaji vya nyuso zao au katika mikono basi watahukumiwa katika lile ziwa la moto (Ufunuo 14:9-10).

Sasa kama tu alama ya kishetani katika kipaji cha uso au katika sehemu ya mkono, inaweza kuwa sababu ya mtu kukataliwa na Mungu milele!, vipi hizo tattoo unazochora mwilini, vipi hizo hina unazozipaka na  wanja unaoupaka machoni?, vipi hizo lipstick unazopaka mdomoni na rangi unazopaka kwenye kucha?… Vipi hizo hereni unazozining’iniza masikioni?.

Kama tu leo ni ngumu kuelewa kuwa kupaka wanja ni kosa kibiblia, utashawishikaje siku ile kuamini kuwa kuandikwa alama ya 666 kwenye kipaji cha uso wako ni kosa?..nataka nikuambie kuwa siku ile utaipokea tu chapa kama kawaida.  Kama tu leo kutoboa masikio na kuweka hereni na kutoboa pua na kuweka pini huoni shida, utaonaje shida siku ile utakapotobolewa  katika mkono wako na chipu kuwekwa mwilini mwako?.

Tafakari sana dada!!… tafakari sana kaka!! Tafakari sana Mama, tafakari sana Baba…Usiwe mwepesi kuiga mambo yanayoendelea na kuonekana ulimwenguni, hususani yanayofanywa na watu wengi!…(Mengi ya hayo yanaongozwa na roho ya mpinga kristo)…Ni kweli unajipenda, na ni vizuri kufanya hivyo, ni kweli unapenda uonekane vizuri na maridadi mbele za watu, ni vizuri pia kufanya hivyo lakini vipi na roho yako? Je itaendelea kubaki salama?.

Shetani amewafunga wengi macho siku hizi za mwisho wasiyaelewe maandiko! Na kuwaaminisha kuwa Mungu haangalii mwili bali anaangalia roho.

Dada usidanganyike! Kwasababu udanganyifu upo leo.. na utaendelea kuwepo mpaka wakati wa chapa ya mnyama.

Tupa hereni zote, kachome mawigi, ondoa pistick, na wanja machoni.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

JE CHANJO YA KORONA NI ALAMA YA MNYAMA?

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”

Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”.

Kutundua ni kujali mtu kupita kiasi, au kuonyesha wema uliopitiliza.

Hivyo hapo anaposema amtunduiaye mtumwa wake tangu utotoni, mwisho wake atakuwa ni mwanawe. Anamaanisha amjalie mtumwa wake, kupita kiasi, yaani kuishi naye kama sio mtumwa kwake, (kumdekeza), na kama mfano ikiendelea hivyo kwa kipindi kirefu, mwisho wake utakuwa ni kumfanya mwanawe, yaani mrithi.

Zamani enzi za biblia, watu walikuwa aidha wananunua watumwa, au wanawazalisha majumbani kwao, ikiwa na maana kama mtu huyo alikuwa na mtumwa, kisha mtumwa Yule akazaa, sasa wale watoto wanakuwa pia ni watumwa wa Yule bwana.

Na kulikuwa na sheria kwamba kila baada ya miaka 7, mbiu ilipigwa ya kuwafanya watumwa wote huru, hivyo waliotaka kuondoka waliondoka, lakini waliotaka kuendelea, basi waliendelea kwa mkataba mwingine wa miaka saba. Na hivyo mtumwa huyo aliwajibika kutumika ipasavyo muda wote huo wa mkataba wake (Kumbukumbu 15:1-18).

Sasa hapa, biblia inaeleza tabia ya bwana ambaye moyo wake ni wa kitofauti. Bwana ambaye, anatabia ya kumjali sana mtumwa wake kuliko uhalisia, huwenda anamuhurumia, kumwona anafanya kazi nyingi, hivyo anampa kidogo tu, au anapokwenda kwenye sherehe hamwachi nyumbani anakwenda naye pia, hata akiwa nyumbani majukumu anapewa machache sana, anakaa naye mezani pamoja wanacheka n.k… Sasa katika hali kama hiyo, ikiwa mtumwa huyo, atadumu kubaki kwa bwana wake, kwa kipindi kirefu, Yule bwana, atamfanya tu kuwa kama mmojawapo wa mwanawe, maana yake siku atakapotoa urithi, na huyu lazima apewe, kwasababu ameishi kama mtoto wake kwa kipindi kirefu.

Na hii ni kweli, hata katika kipindi hichi, labda mfanyakazi kaajiriwa kwenye nyumba fulani, kisha mwenye nyumba akampenda, akawa naye kwa kipindi cha miaka mingi, mwishowe, atamfanya tu kama mwanafamilia, na hatimaye atapata kitu kama mmojawapo wa watoto wake.

Ni kufunua nini rohoni?

Hii ni Tabia aliyokuwa nayo Mungu kwetu sisi watu wa mataifa.

Tulipokwenda kwake, hatukuwa wana wake, au warithi, bali warithi walikuwa ni wayahudi tu, lakini kwa ukarimu wake, akatutoa katika utumwa na kutufanya WANA, jambo ambalo si kawaida kwa bwana yoyote, kutenda kwa kijakazi aliyezaliwa kusikojulikana. Ndicho alichokuja kukifanya Yesu;

Yohana 15:15  Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.

Yohana 8:35  “Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote. 36  Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”.

Hivyo mimi na wewe tunafanyika, WANA na WARITHI, wa Mungu kwa njia ya Bwana Yesu. Haleluya. Utukufu na heshima ni kwa Bwana wetu Yesu!! milele na milele.

Lakini ni nini tunapaswa kukifanya?

Ni kukubali tu kudumu katika nyumba yake. Kama vile mtumwa Yule ambaye aliamua kudumu tangu UTOTONI. Hivyo na wewe umepewa neema, dumu katika neema, dumu katika wokovu, acha kutanga tanga huku na kule. Mungu akaghahiri mema kwako. Ulimwengu hauwezi kukupa unafuu wowote, ni kwa Kristo tu ndio utapata raha nafsini, Hakuna mateso kwa Kristo, Utumwa wake ni mwepesi sana alisema hivyo. Soma (Mathayo 11:28-30).

Ikiwa hujaokoka unasubiri nini sasa? Embu fanya uamuzi wa haraka sana umgeukie Kristo akuokoe. Hizi ni siku za mwisho, anakaribia kurudi kuwanyakua wateule wake. Kama upo tayari kutubu leo dhambi zako, basi fungua hapa kwa  ajili ya mwongozo wa sala ya toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

Maana ya Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Ni kwa namna gani haki huinua taifa? (Mithali 14:34)

AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE

Nini maana ya Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;

Nini maana ya kukunguwazwa (Marko 14:27)

Rudi nyumbani

Print this post

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu lililo hai (Zab.119:105)

Je unaijua nguvu ya kinywa chako? Biblia inasema kuwa MAUTI na UZIMA huwa katika uwezo wa ULIMI. Na mtu awezaye kuutumia vizuri ulimi wake atakula matunda yake.

Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”.

Sasa ULIMI una matunda mawili tu!, ambayo ni “Uzima na Mauti”. Maana yake mtu anaweza kuutumia ulimi wake ukamletea UZIMA, lakini pia anaweza kuutumia na ukamletea MAUTI.

Yule kijana aliyempelekea Daudi habari za kifo cha Sauli, kinywa chake mwenyewe kilimletea “Mauti” (2Samweli 1:16) hali kadhalika Mfalme Yehoshafati alipokuwa katika hatari ya kufa, kwa kinywa chake mwenyewe alijiokoa. (2Nyakati 18:31).

Lakini leo nataka tuangalie faida za kutumia ULIMI katika eneo la  MAOMBI.

Wengi tumezoea kuomba kimoyomoyo, jambo ambalo ni zuri lakini si wakati wote linafaa!!.. kuna mazingira ni lazima utumie kinywa chako kutoa maneno dhahiri yanayosikika!..Kuna ngome zinahitaji kusikia sauti ndipo zitii!, Kuna ngome zinahitaji kuamrishwa na kukemewa ndipo zitii (Kuta za Yeriko zilihitaji kelele nyingi ili zianguke)….Hali kadhalika katika imani inahitajika sauti ya kinywa ili kuthibitisha wokovu mtu alioupata…

Warumi 10:9  “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

10  Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.

Kwa hiyo si kila wakati maombi ya ukimya yanafaa… Ni lazima ujifunze kubadili gear unapoingia katika maombi ya vita, hata motokaa haisafiri kwa gear moja tu, ikienda hivyo itakwamaa mahali Fulani.

Sasa biblia inatufundisha kuwa “Mauti na Uzima” huwa katika uwezo wa kinywa. Maana yake ni kwamba tukitumia vizuri ndimi zetu wakati wa kuomba tunauwezo wa kuvihuisha vitu vingi vilivyokufa, na pia kuviua baadhi ya vitu visivyofaa maishani mwetu.

Tunaviuaje vitu visivyofaa?.. Tunaviua kwa “kuvitamkia kifo” kwa mfano ule ule wa Bwana Yesu alivyoutamkia ule Mtini, na ukafa wakati ule ule.

Mathayo 21:18  “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.

19  Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; AKAUAMBIA, YASIPATIKANE MATUNDA KWAKO TANGU LEO HATA MILELE. MTINI UKANYAUKA MARA.

20  Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara?

21  Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng’oka, ukatupwe baharini, litatendeka.

22  Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea”.

Mstari wa 19 unasema “..akauambia, yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele, mtini ukanyauka mara.” Hapo Bwana Yesu aliuua huo mtini kwa kutumia kinywa chake. (Aliutumia ulimi wake na akala matunda yake), na anatuambia tukiwa na Imani tunaweza kufanya kama hayo na hata Zaidi ya hayo.

Hivyo na sisi ni lazima tujifunze kutumia Ndimi zetu kuua baadhi ya vitu ambavyo shetani kavipanda katika maisha yetu.

Unapoamka kusali Ua kazi za giza katika siku yako, unapotembea zihukumu kazi za giza kwa kutumia kinywa chako.. kwasababu unapotamka na kuamini moyoni mwako basi fahamu kuwa ni lazima yatokee hayo uliyoyasema.

Zitamkie mauti kazi za shetani katika utumishi wako, katika familia yako, katika watoto wako, katika shughuli zako, katika vitu vyako unavyomiliki, Usiishie tu kuomba kimya kimya pasipo kutoa maneno yoyote.. Paza sauti kwasababu kuna nguvu Mungu kaiweka katika ulimi wa mwanadamu.

Wachawi na mawakala wote washetani wanajua nguvu iliyopo katika ulimi, ndio maana wanautumia kuleta madhara makubwa katika maisha ya watu.. sasa na watu waliookoka ni lazima kutumia ulimi kutangua maneno yote yaliyonenwa au yanayonenwa kinyume na maisha yetu ya kiroho na kimwili.

Vile vile ni lazima tutumie Ndimi zetu kutamka UZIMA wa vitu vilivyokufa katika maisha yetu. Nabii Ezekieli aliambiwa aitabirie mifupa mikavu ili iweze kuwa na uhai tena, na katika maono yale aliitabiria mifupa ile kwa kinywa chake na ikarudia uzima na likaamka jeshi kubwa sana (soma Ezekieli 37:1-8).

Sehemu zote Bwana Yesu alipoenda kuponya wagonjwa alitumia kinywa chake kutamka, na sisi ni lazima tutumie vinywa vyetu kutamka uzima juu ya vitu viliyokufa ndani yetu. Ikiwa ni huduma, ikiwa ni karama, ikiwa ni shughuli unayoifanya, ikiwa ni watoto, au kitu kingine chochote kilicho chema ni sharti kipate uzima kupitia kinywa chako!. Fanya hivyo daima, usiache hata siku moja hata kama unaona kwa nje ni pakavu, endelea kwasababu vita vya kiroho si vita vya kimwili, na ukiwa na bidii kufanya hivyo mwisho utakula matunda ya ulimi wako.

Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

Rudi nyumbani

Print this post

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na Mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Ni muhimu kujua kanuni kadhaa za kuomba ili maombi yetu yawe na majibu.

Tumewahi kujifunza kanuni kadhaa huko nyuma na leo imempendeza Bwana tujifunze kanuni nyingine.

Neno la Mungu linasema yafuatayo katika kitabu cha Yakobo 4:2-3.

Yakobo 4:2 “ Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!

3  Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.

Kumbe sababu ya kutopata yale tunayoyaomba ni jinsi tunavyoomba!.. (kwamba tunaomba vibaya!).

Na kuomba vibaya kunakozungumziwa hapo si kukosea kupangilia maneno wakati wa kuomba, bali ni kuomba kusikompendeza Bwana, ambako ni nje na mapenzi ya Mungu, mfano wa maombi hayo ni yale mtu anaomba Bwana ampatie fedha ili awe nazo awakomeshe wanaomdharau. (Maombi ya namna hii ni maombi mabaya, na mara nyingi hayana majibu)

Hivyo unapoomba zingatia mambo yafuatayo.

1.Kuwa na Nia Njema:

Nia njema, maana yake ni kusudi jema… Kama unahitaji Bwana akupe mafanikio Fulani ya kiroho au ya kimwili, hakikisha Nia yako ni njema, kwamba utokane tu na ugumu unaoupitia, na pia upate kitu cha kuwasaidia wengine, na si kwa lengo la kuwakomesha wanaokudharau. Ukiwa na Nia ya kupata vitu ili wengine waone, maombi hayo yanaweza yasijibiwe kabisa.

2. Mwombe Mungu mahitaji na si Fedha.

Wengi wetu tunapenda kupeleka maombi ya kupata fedha kutoka kwa Mungu.. Lakini kiuhalisia hayo si maombi bora. Tunasahau kuwa tunachokihitaji sana ni mahitaji yetu kama chakula, mavazi, makazi, afya na mengineyo, ambayo hayo Mungu anaweza kukutimizia pasipo fedha.

Ukiwa na haja ya chakula, mwambie Bwana naomba chakula na yeye anajua namna ya kukupatia hicho chakula kama kwa njia ya kukupatia fedha ukanunue, au kwa kukuletea mtu atakayekupa hicho chakula, (usikimbilie moja kwa moja kumwambia Bwana akupe fedha ya chakula), kwani yeye anazo njia nyingi za kukulisha wewe, si lazima kwa kutumia fedha.

Vile vile ukitaka mavazi, makazi, biashara, afya n.k  Mwambie Bwana akupe vitu hivyo, na wala usiombe fedha za kupata mavazi, au za kupata makazi, au za kufanya biashara.. wewe mwambie naomba mavazi, yeye anajua jinsi ya kukupatia kama kupitia mlango huo wa fedha au kupitia watu yeye anajua, vile vile usiombe mtaji kwa Mungu, badala yake iombe ile kazi kwasababu wakati wewe unawaza kupata mtaji kwanza kumbe pengine Mungu amekuandalia mahali utakapoanza kufanya kazi pasipo mtaji.

Ukihataji Bwana akupe kifaa cha kazi au chombo za kukurahisishia usafiri, usimwambie Bwana akupe Pesa za kununua chombo hicho, badala yake mwombe Bwana akupe hicho chombo, kwa njia anayoijua yeye.

Ukitaka kusafiri usimwombe Bwana fedha za kusafiri, wewe mwombe akusafirishe, yeye atajua njia atakayotumia kukufikisha kule unakotaka kwenda, kama atanyanyua mtu na kukusafirisha kwa gharama zake au bure, au atafungua mlango wa wewe kupata fedha hizo, ila usijifunge kwa kanuni ya fedha.

Vile vile unapoumwa usimwombe Mungu pesa za matibabu, mwombe afya, yeye anajua njia atakayotumia kukupa hiyo afya, na mambo mengine yote, epuka Kutaja “Pesa” mbele za Mungu!!.. bali taja lile hitaji!.

Kwanini maombi mengi ya kuomba Pesa hayajibiwi?

Kwasababu kuna roho nyuma ya pesa, inayowasukuma watu katika tamaa mbaya za kidunia, na kuwatoa wengi kwenye Imani, ndivyo maandiko yanavyosema.

1Timotheo 6:10  “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”

Ndio maana utaona asilimia kubwa ya watu waliopata pesa wanakuwa na kiburi!. Lakini waliopewa na Bwana ni wanyenyekevu. Mtu aliyezawadiwa baiskeli na yule aliyenunua baiskeli kwa fedha, utaona yule aliyenunua anakuwa na kiburi Zaidi ya yule aliyepewa. Ingawa wote wana baiskeli!.

Yule aliyezawadiwa nyumba na yule aliyejenga kwa fedha yake, utaona yule aliyejenga anakuwa na kiburi Zaidi ya yule aliyezawadiwa. Na mapenzi ya Mungu ni sisi tuwe wanyenyekevu na si watu wenye viburi, hivyo kamwe hawezi kukupa kitu ambacho baadaye kitakuja kukupa kiburi.

Ni wachache sana ambao Mungu anawabariki kwa fedha, kwasababu anajua tayari ameshawatengeneza mioyo yao, hawawezi kuwa na kiburi hata wawe na kiasi gani cha fedha, na hiyo naweza kusema ni asilimia 1% lakini wengi Mungu hawapi hizo fedha wanazozihitaji kwasababu anajua tamaa tulizo nazo. Na ukiona mtu ana fedha nyingi na ana kiburi (hizo fedha hajapewa na Mungu!!).

Kama mkristo biblia inatufundisha tusiwe watu wa kupenda fedha, wala kuzisifia wala kuzitukuza, badala yake tumtukuze Mungu na tumfanye Mungu siku zote kuwa MPAJI WETU (YEHOVA YIRE)!!. Kwamba fedha ziwepo au zisiwepo bado tutaishi, bado tutavaa, bado tutakula, bado tutamiliki vitu.. Tuliookoka tuna uwezo wa kuishi bila fedha wala vitu vilivyotukuzwa na wanadamu na bado tukawa na maisha bora kuliko watu wenye mambo hayo.

Mhubiri 5:10 “Apendaye fedha hatashiba fedha, Wala apendaye wingi hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili”.

Bwana atusaidie.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?

Ni kwa namna gani haki huinua taifa? (Mithali 14:34)

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?

Rudi nyumbani

Print this post

Alani ni nini?(1Samweli 17:51)

Alani ni kifuko cha kuhifadhia upanga ambacho huvaliwa kiunoni na askari hususani wakati wa vita. Tazama picha juu.

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

1Samweli 17: 51 “Ndipo Daudi akapiga mbio, akasimama juu ya Mfilisti, akautwaa upanga wake, akaufuta alani mwake, akamwua, akamkata kichwa kwa upanga huo. Nao Wafilisti walipoona ya kuwa shujaa wao amekufa, wakakimbia”

1Nyakati 21:27 “Bwana naye akamwamuru malaika; naye akaurudisha upanga wake alani mwake tena”.

Yohana 18:11  “Basi Yesu akamwambia Petro, Rudisha upanga alani mwake; je! Kikombe alichonipa Baba, mimi nisikinywee?”

Soma pia,  Ezekieli 21:3, 5

Je! Chombo hichi kinafunua nini rohoni?

Kama tujuavyo upanga na alani, ni kama pochi na pesa, havitengani. Na upanga, kibiblia ni Neno la Mungu (Waefeso 6:17, Waebrania 4:12). Hivyo Neno la Mungu halihifadhiwi penginepo zaidi ya kwenye moyo. Pale linapohitajika kutumika hutolewa moyoni na sio penginepo. Kwahiyo chombo hichi kijulikanacho kama Alani, kinauwakilisha moyo wa Mtu.

Na kama tunavyojua upanga hutumiwa na mtu yoyote, unaweza hata kumwangamiza  mwenye nao, ukitumiwa na adui. Ndivyo alivyojaribu kufanya shetani alipomjaribu Bwana na kumwambia ‘imeandikwa’, Lakini kwasababu Yesu alikuwa amejaa ‘Kweli yote’. Aliweza kumpokonya upanga huo huo na kummaliza nao.

Hivyo ni muhimu pia kujaa ‘Kweli yote’ sio Neno tu peke yake, yaani kuufahamu ukweli wa Neno la Mungu. Kwasababu ibilisi anaweza kulitumia kukuangusha ikiwa hutakamilishwa katika hilo, kwamfano anaweza kuja kukwambia kuoa wake wengi si dhambi, kwani Yakobo, alioa wake wengi, Daudi alioa wake wengi, Sulemani alioa wake wengi, na wote hawa walikubaliwa vizuri na Mungu, vivyo hivyo na wewe ukifanya hivyo utakubaliwa tu, hamna shida,. Lakini je! Hiyo ni kweli yote? Kweli yote inasema Mungu alimuumba mtu mke na mume, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.(Mathayo 19:4-9), hakuumba Adamu mmoja, Hawa wengi. Hivyo usipojua kuligawanya vema Neno la Mungu kwa msaada wa Roho ni rahisi shetani kukupiga.

Na ndio maana maandiko yanatusihi tuivae ‘kweli’ kiunoni.

Waefeso 6:13  “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. 14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?

Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi

Kwanini Bwana Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wakanunue upanga?

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

Kwanini Mungu aseme “Alaaniwe azuiaye upanga wake usimwage damu” (Yeremia 48:10).

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kutoka 21:10 ina maana gani?.

Jibu: Tuanze kusoma  kuanzia mstari wa 7..

Kutoka 21:7 “Mtu akimwuza binti yake awe kijakazi, hatatoka yeye kama watumwa wa kiume watokavyo. 

8 Kwamba bwana wake hakupendezewa naye, akiwa amemposa, ndipo atakubali akombolewe; hana amri yeye kumwuza aende kwa watu wageni maana amemtenda kwa udanganyifu. 

9 Kwamba amposa mwanawe, atamtendea kama desturi zipasazo binti zake. 

10 Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia.  11 Kwamba hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali”.

Jibu: Kwa desturi za kiyahudi mtumwa wa kiume au wa kike anapaswa amtumikie bwana wake kwa muda wa miaka 6 tu, ukifika mwaka wa 7 anakuwa yupo huru kuondoka.,

Kumbukumbu 15:12 “Ikiwa nduguyo, mume wa Kiebrania, au mwanamke wa Kiebrania, akiuzwa kwako, naye amekutumikia miaka sita; basi mwaka wa saba mwache huru aondoke kwako.

 13 Nawe utakapomwacha huru aondoke kwako, usimwache aende zake mikono mitupu”

Ikiwa mtumwa wa kiume aliingia na mke wake basi utakapofika mwaka wa 7 ataondoka na mke wake huyo, (Kutoka 21:1-3) lakini kama aliingia bila mke na akaozwa mke kutoka katika familia ya bwana wake, basi utakapofika mwaka wa 7 atatoka yeye kama yeye, lakini mke na watoto watabaki kwa baba wa mke wake, hana amri ya kuondoka nao, lakini kama hataki kumwacha mke wake na watoto wake basi atamtumikie bwana wake huyo daima kwa agano la kutobolewa sikio kwa uma.

Kutoka 21:5 “Lakini huyo mtumwa akisema waziwazi, Mimi nampenda bwana wangu, na mke wangu na watoto wangu; sitaki mimi kutoka niwe huru; 

6 ndipo hapo huyo bwana wake atamleta mbele ya Mungu na kumleta mlangoni, au penye mwimo wa mlango; na bwana wake ATALITOBOA SIKIO LAKE KWA UMA; ndipo atamtumikia sikuzote”.

Hivyo ishara ya kutobolewa sikio ilikuwa ni ishara ya mtumwa kukataa uhuru wake.

Lakini kwa upande wa mtumwa wa kike (yaani kijakazi) ilikuwa ni tofauti kidogo. Kama kijakazi aliingia bila kuolewa na baadaye kijana wa bwana wake akampenda na kumwoa, kama mke wa kwanza basi famila ya kijana inapaswa kumfanya kama binti yao.

Lakini kama ameolewa kama mke wa pili, na bado ni kijakazi, na bwana wake hamtaki tena awe mke wake au suria wake, basi utakapofika mwaka wa 7, wakati wa maachilio, yeye hatamwachilia kama mabinti wengine wajakazi wanaoachiwa huru, bali kinyume chake ataachiliwa kwa gharama (maana yake atakombolewa).

Hivyo yule baba wa mtoto wa kiume aliyemwoa huyo binti, atamwuza kwa mojawapo wa ndugu aliye karibu, na si kwa mgeni (yaani mtu kutoka taifa lingine tofauti na Israeli), na asipopatikana wa kumnunua ndipo yule kijana ataendelea kuishi naye huku akimtimizia haki yote ya ndoa, ikiwemo CHAKULA, MAVAZI NA HAKI YA NDOA (Ngono).

Vitu hivyo vitatu ni sheria avitimize, si kwasababu hamtaki tena na kakosa mtu wa kumnunua basi aanze kumnyanyasa kwa kumnyima chakula chake na mavazi pamoja na haki ya ndoa ambayo imenenenwa na mtume Paulo kwa uongozo wa Roho katika 1Wakorintho 7:5. Na ikitokea kashindwa kumtimizia hayo mambo matatu basi atamwacha aende zake huru, bila gharama zozote za kumkomboa.

Kutoka 21: 10 “Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia. 

11 Kwamba hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali”.

Mambo gani tunajifunza?

1.Kutoboa masikio si ishara nzuri.

Asili ya kutoboa sikio na kuweka hereni haikuwa nzuri, watu waliotobolewa masikio enzi za zamani ni watu waliokataa uhuru wao, hali kadhalika roho hiyo hiyo inatembea mpaka leo, kibiblia mwanamke au mwanaume hapaswi kutoboa masiko yake. Huenda ulitobolewa enzi hujaokoka, sasa umeshaokoka usiweke hereni baki katika uhalisia wako.

Wengi wanaosumbuliwa na nguvu za giza ni kutokana na vitu wanavyoviweka katika miili yao, na hawajui kuwa hivyo ndio vyanzo vya roho zinazowasumbua.

2. Ni lazima kutimiza haki ya Ndoa

Mtu aliyeoa au aliyeolewa ni sharti amtimizie mwenzie haki zote za ndoa ikiwemo upendo, na ukaribu wakati wowote unapohitajika. Maandiko yanasema mume hana amri juu ya mwili wake kadhalika mke.

1Wakorintho 7:2  “Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.

3  Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

4  Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

5  Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

EPUKA MUHURI WA SHETANI

USIMPE NGUVU SHETANI.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu?

JIBU: Picha nyingi zinazochorwa kumweleza Yesu, takribani nyingi ya hizo  zinamwonyesha ni mtu mwenye nywele ndefu. Lakini Je uhalisia wake ni upi, ni kweli alikuwa na nywele ndefu au fupi?

Maandiko yanaeleza utamaduni wa wayahudi, kwa wanaume ilikuwa kuacha nywele zirefuke kama zile za mwanamke ni aibu kwa mtu huyo. Anajivunjia heshima kubwa.

1Wakorintho 11:14  “Je! Hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu ni aibu kwake? 15  Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi”

Hivyo hakukuwa na mtu aliyekuwa na nywele ndefu isipokuwa tu mtu aliyeitwa mnadhiri wa Mungu.

Lakini Je! Yesu alikuwa ni Mnadhiri ?

Kabla ya kufahamu kama Yesu alikuwa mnadhiri au la! Tufahamu kwanza mnadhiri alikuwa ni nani, na sheria ya mnadhiri ilikuwaje

Mnadhiri ni mtu aliyetengwa au aliyejitenga mwenyewe/ aliyejitoa wakfu kwa Mungu, kufuata na sababu binafsi, aidha kwa sababu ya shukrani yake ya kutendewa jambo Fulani kama vile kuponywa ugonjwa, au  kupatiwa mtoto, au kupata kitu Fulani kwa Mungu alichokuwa anamwomba. Hivyo katika agano la kale, kulikuwa na sheria ya mnadhiri. Na mnadhiri alikuwa yoyote Yule aidha mwanamke au mwanaume.

Sheria za mnadhiri ni zipi?

Kulingana na Hesabu 6:1-8

  1. Hakuruhusiwa kunywa divai, wala zabibu, wala juisi ya zabibu,  wala mbegu zake. Yaani kwa ufupi kitu chochote kilichomzao wa zabibu hakuruhusiwa kunywa
  2. Hakuruhusiwa kukata nywele zake, tangu siku hiyo aliyomwekea Mungu nadhiri mpaka atakapoitoa
  3. Hakuruhusiwa kugusa maiti. Hata kama ni ndugu yake wa karibu amekufa, baba yake au dada yake. Hakuruhisiwa  kufanya hivyo
  4. Ni lazima awe mtakatifu kwa Bwana; Maana yake ajitenge na mambo yote yaliyo najisi kipindi chote awapo katika kiapo chake.

Katika biblia, kulikuwa na makundi mawili ya wanadhiri

  1. Wanadhiri wa daima: Hawa ni waliotengwa tangu tumboni mwa mama zao: Mfano wao alikuwa  ni Samsoni, Samweli, Yohana Mbatizaji.. Hawakukatwa nywele zao, lakini pia hawakunywa divai maisha yao yote.
  2. Wanadhiri wa muda: Hawa ni aidha waliamua wenyewe katika kipindi Fulani katika maisha yao waingie kwenye viapo hivyo kwa Mungu, yaani wamtumikie yeye daima mpaka kufa kwao, au waliokuwa na nadhiri za muda, ambapo pengine baada ya miezi miwili, au mwaka mmoja wanaiondoa na kwenda kunyoa nywele zao, na kuendelea kutumia mizabibu nk. Mfano wa Hawa alikuwa ni mtume Paulo, ambaye kipindi Fulani anashuhudia naye alikuwa na nadhiri hiyo.

Matendo 18:18  “Baada ya hayo Paulo akazidi kukaa huko siku nyingi, kisha akaagana na ndugu akaabiri kwenda Shamu; na Prisila na Akila wakaenda pamoja naye, alipokwisha kunyoa kichwa chake huko Kenkrea; maana alikuwa ana nadhiri”

Sasa tukirudi kwa Bwana Yesu.

Je! Na Yeye alikuwa ni mnadhiri?

Jibu ni hapana, kwasababu Bwana alikunywa mzao wa mzabibu.

Mathayo 26:29  Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.

Kuonyesha kuwa hapo kabla alikuwa anakunywa.

Soma pia  Mathayo 11:19, Na Yohana 2:1-12, inatupa picha alitumia mzao wa mzabibu. Halikadhalika aligusa maiti, (Marko 5:41), na zaidi ya yote Bwana hakufungwa na sheria za torati.

Hivyo kwa kifupisho ni kwamba Bwana Yesu hakuwa na nywele ndefu, yawezekana alikuwa na nywele nyingi lakini hazikuwa ndefu kama za mwanamke, mfano wa aonekanavyo kwenye baadhi ya picha zinazochorwa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Nini maana ya Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza (Yakobo 4:9)

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?

Kati ya nyaraka kumi na tatu (13) alizoziandika mtume Paulo, Nne (4) kati ya hizo, aliziandika akiwa gerezani. Alipokuwa Rumi, ambapo maandiko yanatuonyesha  alipelekwa na kuwekwa chini ya kifungo maalumu ambacho aliruhusiwa watu kumtembelea lakini pia kuwahubiria injili akiwa katika kifungo hicho cha nyumba.

Matendo 28:16  “Tulipoingia Rumi Paulo alipewa ruhusa kukaa kwake mwenyewe pamoja na askari aliyemlinda…. 30  Akakaa muda wa miaka miwili mizima katika nyumba yake aliyokuwa ameipanga, akawakaribisha watu wote waliokuwa wakimwendea, 28.31  akihubiri habari za ufalme wa Mungu, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri mwingi, asikatazwe na mtu”.

Hivyo huko ndipo panaaminika aliandika nyaraka hizi nne. Ambazo ni

  1. Waefeso,
  2. Wafilipi,
  3. Wakolosai,
  4. Filemoni.

Sasa ni kwanini Nyaraka hizi na si nyingine?

Ni kwasababu ya habari za kufungwa kwake, alizozitaja katika nyaraka hizo; Ambazo zinaonyesha mazingira hayo alikuwa kifungoni.

Kwamfano ukisoma vifungu hivi, utaona,

Waefeso 3:1,4:1, Wafilipi 1:13, Wakolosai 4:3, Filemoni 1:10.

Je Ni nini cha kujifunza, katika vifungo vya mtume Paulo?

Yamkini Paulo alitamani awe huru kwa wakati ule ili aendelee kuihubiri injili kwa mataifa yote. Lakini hakujua mpango wa Mungu kwa nyaraka zake. Hakujua kuwa  Mungu atazihifadhi kwa mamia ya miaka, ili ziwe injili kwa vizazi vijavyo. Na matokeo yake ni kuwa nyaraka hizo zimehubiri injili kuliko hata wakati alipokuwa anazunguka mwenyewe kwenye mataifa akiwa huru.

Kwamfano mafunzo yaliyo katika kitabu cha Waefeso, yanatoa mwongozo mzuri kuanzia Viongozi wa kanisa, watakatifu hadi ngazi za kifamilia. Na jinsi gani mtakatifu anavyopaswa avae silaha za haki ili aweze kumpinga adui yake shetani (Waefeso 6:11-18)

Hii ni kuthibitisha maneno yale ya maandiko yanayosema kwamba injili  haifungiki.

2Timotheo 2:9  “Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi

Na wewe pia ujionapo upo katika mazingira yanayokubana kuitangaza injili ya Bwana, usiwe na mawazo ya kukata tamaa, hapo hapo tazama upenyo wowote uutumie, kwasababu wewe umefungwa lakini sauti ya Mungu iliyo ndani yako, inauwezo wa kufika duniani kote, kwa vizazi vyote, hata kama umefungiwa kwenye chumba cha giza, namna gani, injili ya Kristo, inaangusha ngome popote.

Nyanyuka sasa, fanya jambo kwa Bwana, iamini nguvu ya msalaba.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?

Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).

Tarishi au Matarishi ni akina nani  kwenye biblia?

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”

Rudi nyumbani

Print this post