Category Archive Home

Watu wenye kuvunja maagano ndio watu wa namna gani? (Warumi 1:31)

Napenda kujua watu wenye kuvunja maagano wanaozungumziwa katika Warumi 1:31, ndio watu wa namna gani?

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 28, ili tuweze kuelewa vizuri..

Warumi 1:28 “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.

29 Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,

30 wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao,

31 wasio na ufahamu, WENYE KUVUNJA MAAGANO, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;

32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao”.

Umeona? watu wenye kuvunja maagano sio watu WANAOOMBA NA KUVUNJAA MAAGANO YA UKOO!! LA!. Bali wanaovunja maagano wanaozungumziwa hapo, ni watu wote ambao hawadumu katika AHADI ZAO, au MANENO YAO WENYEWE. Na hawa wamegawanyika katika makundi matatu.

1.WANAOVUNJA MAAGANO YA IMANI.

Mtu anapoamua kumfuata Yesu, na kuokoka anakuwa ameingia KATIKA AGANO LA DAMU YA YESU. Kuanzia huo wakati damu ya Yesu inaanza kunena juu yake, mtu huyo anakuwa rafiki wa Mungu, na mrithi wa ahadi za Mungu, kwasababu tayari kashaingia katika Agano la Mungu, kupitia damu ya Yesu.

Lakini huyu mtu anapoamua kuacha Wokovu, na kuurudia ulimwengu, tafsiri yake ni kwamba KALIVUNJA LILE AGANO TAKATIFU LA DAMU YA YESU, Ambalo kupitia hilo alitakaswa dhambi zake na kuwekwa huru mbali na utumwa wa dhambi.. Mtu wa namna hii maandiko yanasema hali yake itakuwa mbaya sana baada ya kufanya hivyo.

Waebrania 10:28 “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 Mwaonaje? HAIKUMPASA ADHABU ILIYO KUBWA ZAIDI MTU YULE ALIYEMKANYAGA MWANA WA MUNGU, NA KUIHESABU DAMU YA AGANO ALIYOTAKASWA KWAYO KUWA KITU OVYO, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”

Umeona?.. Ipo hatari kubwa sana ya KURUDI NYUMA baada ya kumpokea Yesu, kwasababu kwa kurudi nyuma kwako, ni sawa na UMELIVUNJA AGANO TAKATIFU.

2. AGANO LA NDOA.

Mtu aliyeoa au aliyeolewa katika Ndoa Takatifu, ambaye alisimama mbele ya kanisa la Kristo, na kuahidi mbele za Bwana kuwa ataishi na mwenzake katika hali yoyote ile atakayokutana nayo katika maisha, yaani katika hali ya shida na raha, na huzuni, na misiba na hata katika magonjwa na madhaifu..

Halafu ikatokea siku za mbeleni akamwacha Mwenzake, na kwenda kuoa au kuolewa na mwingine, Mtu wa namna hii ni MTU ANAYEVUNJA MAAGANO, ambaye adhabu yake ni kubwa sana.


Ndugu kama umeoa au umeolewa, fahamu kuwa hupaswi kumwacha mke wako au mume wako, unapaswa umvumilie katika kasoro zake, ukimwacha mke wako/mume wako kwasababu tu amekuwa mdhaifu katika mwili, au kwasababu anamepata ugonjwa fulani, au kwasababu amekuwa na hasira, au ameongezeka mwili au amezeeka..na ukaenda kuoa/kuolewa na mwingine, basi fahamu kuwa UMEVUNJA AGANO, na hatari ya kuvunja AGANO ni adhabu ya ziwa la Moto.

3.AGANO LAKO MWENYEWE.

Agano lako mwenyewe hilo linaweza kuwa NADHIRI uliyomwekea Mungu.. Kama umeweka Nadhiri Mbele za Mungu, basi hakikisha unaiondoa hiyo Nadhiri kwa kuitimiza..

Mhubiri 5:4 “Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; kwa kuwa yeye hawi radhi na wapumbavu; basi, uiondoe hiyo uliyoiweka nadhiri.

5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe”

Vile vile kama umepanga kufanya jambo fulani Jema basi litimize hilo, KWASABABU HILO NI AGANO LAKO LA HIARI uliloingia WEWE NA ROHO YAKO.

Kuna mhubiri fulani alitokewa na Bwana Yesu katika maono, na Bwana akamwambia “Kama hutakuwa mwaminifu katika maneno yako mwenyewe, basi huwezi kuwa mwaminifu katika maneno yangu”.

Akimaanisha kuwa kama umesema utafunga hii wiki, au utasali masaa mawili leo, au utafanya hiki au kile kwaajili ya ufalme wa mbingu, halafu kitu hicho ulichokipanga katika roho yako, hutakitekeleza basi wewe Sio mwaminifu katika maneno yako mwenyewe, sio mwaminifu katika maagano yako mwenyewe, hivyo wewe ni mtu kigeugeu, unayevunja maagano yako…na Mungu hawezi kukuamini pia..

Yakobo 1:7 “Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.

8 Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote”.

Kumbukumbu 23:23 “Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri Bwana, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako”.

Bwana atusaidie tusiwe watu wa kuvunja maagano, bali kutimiza maagano.
Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Paulo aungane na wale watu wanne wenye nadhiri?

Mtu mwenye “kitango” ni mtu wa namna gani kibiblia?

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?

Biblia inasema tusiwe kwazo kwa yeyote, je! inawezekanikaje kwa dunia hii ya sasa?(2Wakorintho 6:3).

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Rudi nyumbani

Print this post

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

Mafundisho maalumu kwa waongofu wapya: Sehemu ya tatu.

Ikiwa wewe ni mwongofu mpya, yaani umeokoka hivi karibuni, basi mafundisho haya yanakufaa sana katika hichi kipindi ulichopo.

Ikiwa ulipitwa na mafundisho ya nyuma, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba zetu hizi +255693036618 tukakutumia mafundisho hayo.

Ni muhimu kufahamu kuwa, unapookoka yupo adui atakayesimama kinyume chako kukupinga wakati wote, ili uiache imani. Na huyo si mwingine zaidi ya shetani. Hivyo katika hatua hizi za awali, huna budi kufahamu silaha madhubuti za kuweza kumwangusha, Kwasababu ukizikosa ujue kuwa utakufa tu kiroho. Na silaha yenyewe tunazisoma katika vifungu hivi;

Ufunuo 12:9 “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.
10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.
11 NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA- KONDOO, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.

Jiulize hapo kwanini haijasema wakamshinda kwa mafuta ya upako, au kwa kanisa zuri, au kwa maombi ya vita.. Bali kwa damu ya Mwana kondoo na kwa neno la ushuhuda wao.
Kuna nini katika damu ya Yesu? Na ushuhuda ulionao?
Ni lazima ufahamu umuhimu wa damu yake, katika maisha yako ya wokovu.
Damu ya Yesu ilifanya mambo makuu matatu

  1. Kuondoa dhambi
  2. Kunena juu yetu
  3. kukanyaga nguvu za ibilisi

1) Kuondoa dhambi.


Biblia inasema..

Waebrania 9:22 “Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo”.

Katika agano la kale Utakaso wa kila namna, ulitegemea damu za wanyama, kwasababu ndio kanuni ya Mungu ya kiroho ya kuondoa dhambi, hivyo tangu zamani zile haikupatikana damu yoyote kamilifu isiyo na hila wala mawaa itakayoweza kuondoa dhambi za mtu moja kwa moja, bila kuacha kimelea chochote. Na ndio maana kumbukumbu la dhambi lilikuwepo wakati baada ya wakati , hivyo ilimpasa kuhani mkuu kila mwaka aingie kule hemani akiwa na damu ya wanyama ili kuwapatanisha wana wa Israeli,
Lakini sasa Yesu alipokuja, damu yake ilikuwa ni kamilifu zaidi ya wanyama, yeye tu ndiye aliyeweza, kusafisha na kuondoa kabisa dhambi ya mwanadamu isikumbukwe na Mungu milele, bila kuhitaji tena kuhani kila mwaka kwenda kuomba rehema kwa dhambi zilizotangulia.


Hii ikiwa na maana gani?
Ukiukosa ufunuo huu, kuhusiana na nguvu iliyopo katika damu ya Yesu iliyomwagika msalabani, basi ni ngumu sana, kuamini kama dhambi zako za kale Mungu alishazifuta na kuzisahau kabisa kabisa.
Ni kawaida kwa waongofu wapya kuletewa mawazo haya na ibilisi kwamba, bado Mungu anawaona ni wachafu, bado Mungu anakumbuka zile dhambi walizozitenda nyuma, zile mimba walizotoa, ule uzinzi walioufanya nje ya ndoa, rushwa walizokuwa wanakula, mauaji waliyoyafanya, waganga waliokuwa wanawafuata.


Hii ndio silaha kubwa ya ibilisi kwa waongofu wapya. Wanajiona kama vile bado hawajasamehewa vizuri, bado laana zinawafuatilia, Ndugu, ujue hayo ni mawazo ya shetani, kwasababu umekosa kujua gharama Yesu aliyoingia kwa ajili ya dhambi zako. Ile damu yake kumwagika, ilikuwa ni kukomesha dhambi zako zote na laana zako kabisa kabisa..


Ndio maana hapo biblia inasema, wakamshinda kwa damu ya mwana-kondoo, na ushuhuda wao, yaani ushuhuda wa kukombolewa na Yesu. Ndio silaha kubwa sana ya kumshinda ibilisi.
Hivyo mawazo kama hayo yakikujia yakatae, sema mimi nimeshasamehewa, ya kale yamepita, tazama yamekuwa mapya. Mimi sina deni la dhambi, Ukifanya hivyo, shetani atajua umeshafahamu nafasi yako, hivyo atakukimbia, na utaishi maisha ya amani na kutojihukumu.


2) Kunena juu yetu.


Damu pia inafanya kazi ya kunena.

Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili”.

Kaini alipomuua ndugu yake Habili, Biblia inasema Mungu alimwambia Kaini sauti ya damu ya ndugu yake inamlilia kutoka ardhini (Mwanzo 4:10). Maana yake ni kuwa Mungu alikuwa anaisikia ili sauti ikinena, ikiomba, ikitaka haki itendeke, haikutulia tu.
Hata leo ukiona mtu anapitia majanga majanga fulani hivi, utasikia watu wakisema, ni kwasababu alimuua mama yake hivyo ile damu inamfuatilia..


Kuonyesha kwamba kuna uhalisia fulani katika damu ya mtu kupatiliza mema au mabaya.
Na ndivyo ilivyo kwa damu ya Yesu, inanena Mema, kuliko ile ya Habili, maana yake, hata sasa inazungumza, juu ya wale wote waliompokea yeye mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Inasema huyu anastahili kulindwa, huyu anastahili baraka, huyu anastahili furaha, huyu anastahili heshima, huyu anastahili kibali, afya n.k.


Hivyo wewe uliyeokoka ni wajibu wako kujua jambo hili, ili usiishi kama yatima hapa duniani. Ulipokuwa dhambini damu ya Yesu ilikuwa haineni juu yako, kwasababu haukuwa ndani ya agano lake. Lakini sasa upo, fahamu kuwa, Yesu anakuombea kila siku kwa Baba, hivyo kuwa na ujasiri ukijua kabisa nyuma yako ipo baraka, neema na habati wakati wote. Kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda utayathibitisha hayo yote.

Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea”.

Hivyo mishale yote ya hofu, wasiwasi, mashaka, ambayo shetani atajaribu kukutumia ili urudi nyuma, ikatae, mishale ya kesho nitaishije, nikipoteza kile kwasababu ya Yesu itakuwaje? ondoa hayo mawazo ya kuangamia, kwasababu ipo damu inayonena kwa ajili yako usiku na mchana, ili utembee katika njia salama ya uzima.

Zaburi 27:1 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?
2 Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka.
3 Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.
4 Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake”.
Lishike sana hili, ukilikosa, shetani atatumia upenyo huu kukurudisha nyuma, kama alivyofanikiwa kuwarudisha wengi.


3) Kukanyaga nguvu za ibilisi.

Utajiuliza ni kwanini Bwana Yesu, hakulisema hili neno “IMEKISHWA”, Mahali popote katika huduma yake, mpaka siku ile alipopelekwa pale msalabani? Ni kwamba alijua hakuna kuzimaliza nguvu na utawala wa ibilisi bila agano la damu timilifu.


Hivyo aliposema IMEKWISHWA, Ni kweli ilikwisha, na ndio maana aliwaambia mitume wake maneno haya;

Luka 10:18 “Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Ni lazima ujue kwa damu ya Yesu, shetani, hana nguvu yoyote juu yako. Kwamfano mwanajeshi dhaifu akitambua kuwa bomu alilonalo la nyuklia linaweza kuteketeza mji mzima, hataweza kuwa na hofu, na wanajeshi 1000 wenye nguvu, wanaomjia na bunduki zao. Kwasababu anafahamu akilituma tu kombora lake moja, kikosi chote kinakuwa jivu.


Ndivyo ilivyo kwako wewe uliyeokoka, fahamu kuwa hatua uliyopo, shetani hana nguvu zozote za kukushinda, kwasababu tayari nguvu zako ni nyingi kuliko zake, haijalishi hali yako ya uchanga kiroho. Hivyo, usiogope wachawi, usiogope mapepo, usiogope hata maadui zako. Lolote linalokuja mbele zako, uwe ni udhaifu, magonjwa, mashambulizi ya shetani, kemea kwa jina la Yesu, vitaondoka, usiwe mnyonge kwa shetani, kwasababu yule ni kama kinyago tu kinasimama hapo kukutisha, lakini hakina nguvu yoyote.
Hivyo zingatia sana kuyatafakari hayo.


Na Bwana akubariki.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

KAA MAJANGWANI.

USIMPE NGUVU SHETANI.

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

Rudi nyumbani

Print this post

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe karibu tuyatafakari maneno ya uzima.

Neno la Mungu linasema…

1Samweli 15:22 “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, KUTII ni bora kuliko dhabihu, Na KUSIKIA kuliko mafuta ya beberu.

23 Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; KWA KUWA UMELIKATAA NENO LA BWANA, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”.

Ni vizuri kumtolea Bwana, tena ni moja ya maagizo yake ambayo tukiyatenda kwa hiari yetu wenyewe basi tutapata thawabu nyingi. Lakini ni vizuri pia kujua jambo moja kuwa Mungu wa Mbingu na nchi si mkusanya mapato kutoka kwetu, na wala hahitaji kitu kutoka kwetu.

 Zaidi sana vyote tunavyomtolea yeye kama sadaka, vinaenda kutumika kwaajili ya watumishi wake na huduma alizowapa.. lakini yeye mwenyewe hakuna chochote anachokipokea.  Kwasababu yeye hahitaji kupokea chochote kutoka kwetu, kwamaana vitu vyote vinatoka kwake.

Kwahiyo kama fedha zetu haziendi mbinguni aliko yeye, wala matoleo yetu mengine hayapai mbinguni kumfikia, maana yake ni kwamba lipo jambo lingine ambalo ni muhimu sana kwake kupokea kutoka kwetu, Zaidi ya sadaka na matoleo tunayomtolea. Na jambo lenyewe si lingine Zaidi ya KULITII NENO LAKE.

Bwana anataka mioyo ya kutii tunapolisikia NENO LAKE.. Hiyo ndiyo dhabihu na sadaka anayoikubali kuliko zote..

Isaya 66:1 “Bwana asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?

2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, ATETEMEKAYE ASIKIAPO NENO LANGU”.

Unaona?..Unaposoma kwenye biblia kuwa “waasherati na wazinzi hawataurithi ufalme wa Mbinguni (Wagalatia 5:20)”.. na ukaacha kulitii hili NENO, na kinyume chake ukaendelea na uzinzi wako, huku ukijitumainisha kwa sadaka zako nyingi unazoendelea kuzitoa.. fahamu kuwa UNAFANYA MACHUKIZO MBELE ZA MUNGU!!..Kwasababu maandiko yanasema…

Mithali 15:8 “SADAKA YA MTU MBAYA NI CHUKIZO KWA BWANA…..”.

Unaposoma kuwa Wenye dhambi sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la Moto, kwasababu wamekataa kutubu dhambi zao, na wewe unajijua kabisa bado hujatubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, bado ukawa unaendelea na kulipa zaka zako, bado ukawa unaendelea na kuchangia kazi ya Mungu..nataka nikukumbushe kuwa UNAFANYA MACHUKIZO!!.. Mungu wetu si mkusanya mapato kutoka kwetu, na wala hahitaji fedha zetu… Yeye mwenyewe(Yesu Kristo) alisema maneno yafuatayo..

Mathayo 9:13 “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA”.

Bwana Yesu anachotaka kuona kutoka kwetu, MIOYO YA TOBA, iliyosikia Neno lake na kutetemeka na kuamua KUGEUKA!..Kumbuka kutii ni bora kuliko dhabihu. Kamwe usijitumainishe katika matoleo unayoyatoa na ukasahau kulitii NENO LA MUNGU. Bwana amelitukuza Neno lake kuliko kitu kingine chochote.

Kabla ya kufikiria kumtolea Mungu, fikiria kujitakasa kwanza, fikiria kuacha uzinzi na ukahaba kwanza, fikiria kuacha kuacha ulevi, fikiria kuacha wizi, fikiria kuacha Ugomvi na baada ya kuacha hayo yote, ndipo ufikirie kumtolea Bwana matoleo yako, lakini kamwe usitangulize dhambi zako mbele ndipo sadaka zako zifuate, kwasababu ukifanya hivyo utakuwa unajitafutia laana badala ya baraka..

Mithali 15:8 “SADAKA YA MTU MBAYA NI CHUKIZO KWA BWANA; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.

Kumbukumbu 23:7 “Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume.

18 Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”

Siku zote Litii Neno la Bwana, kwasababu hilo ndilo MWANGA WA NJIA YETU, YA KWENDA MBINGUNI.

Bwana akubariki,

Maran atha!!

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Dhabihu ni nini?

CHAMBO ILIYO BORA.

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

NINI MAANA YA KUTUBU

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

Rudi nyumbani

Print this post

KAA MAJANGWANI.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Sehemu ya pili: Kaa Majangwani:

Luka 1:80 “Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu rohoni, akakaa majangwani hata siku ya kutokea kwake kwa Israeli”.

Ni kawaida ya Mungu, kuwaandalia Watoto wake, mahali maalumu pa kukulia kiroho.. Ikiwa unatamani nguvu zako za rohoni ziongozeke kwa kasi wewe kama mwongofu mpya uliyezaliwa mara ya pili, huna budi kukaa majangwani.

Mungu alipowatoa wana wa Israeli Misri, hakuwavukisha moja kwa moja na kuwafikisha Kaanani ndani ya siku moja, bali aliwapitisha kwanza jangwani, kuwalisha huko na kuwakuza kiroho, kwa muda wa miaka 40, kwasababu walikuwa bado ni Watoto wachanga, na ndipo baadaye wakaingia Kaanani, wakiwa Hodari na nguvu nyingi rohoni.

Hosea 11:1 “Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misri”.

Biblia pia inatuambia Yohana mbatizaji alipozaliwa, alikimbilia majangwani huko kuishi, na matokeo yake akakua na kuongozeka nguvu nyingi sana rohoni kwa kasi, na ndio maana hatushangai kwanini Bwana Yesu anamshuhudia na kusema katika wazao wa wanawake hakuwahi kutokea mtu aliyekuwa mkuu kama Yohana Mbatizaji.(Mathayo 11:11).. Hiyo yote ni kwasababu gani? Ni kwasababu alitumia Muda mwingi majagwani.

Sasa Kiroho jangwani ni wapi?

Haimaanishi kuwa ni sisi tukimbilie majangwani tukaishi huko, ili tukue kiroho hapana… Kama tunavyojua jangwani ni mahali ambapo hapana uwepo wa wanadamu, ni mahali pa ukiwa, pasipokuwa na huduma zozote za kijamii.. Ndivyo inavyompasa mkristo aende rohoni.

Unapaswa katika hatua zako za awali za wokovu: Kwa bidii zote uwe tayari, kuukana huu ulimwengu. Kukaa mbali na mambo yote yanayousonga wokovu wako, bila kujali unapoteza nini, au unakosa nini..

Ukiokoka, kubali kuachana na wale marafiki zako wa kale uliokuwa unakwenda nao disco, uliokuwa unakunywa nao pombe, uliokuwa unatukana nao, kubali kuwa mpweke, kwa kipindi Fulani, kwani hivyo ndivyo unavyoiponya roho yako.

Ukiokoka, kubali wakati mwingine, kupoteza hiyo kazi isiyo halali kwa Mungu, kama unafanya biashara ya pombe acha, ..wala usidhani kuwa utaangamia, kwamba Mungu atakuacha ufe, hilo wazo ondoa, uwezo wa kukulisha Mungu anao, Kama alivyofanya kwa wana wa Israeli kule jangwani, atafanya na kwako pia..

Biblia inasema..

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, AENDE ZAKE NYIKANI HATA MAHALI PAKE, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo”.

Umeona, Mungu ameshaandaa mahali pako huko nyikani, pa kukulisha kwa wakati wako na majira yako. Hivyo usiogope wewe uliyemzaa Kristo maishani mwako.

Kama wewe ni binti kubali kukaa mbali na Fashion, kubali kujisitiri na kuchoma hivyo vimini na masuruali, kubali kuonekana umerukwa na akili kwa ajili ya Kristo, hata ulimwengu mzima ukikuona mjinga, kubali hiyo hali, weka kando kila mzigo wa dhambi, kwasababu ndivyo unavyoiponya roho yako.

Je! Faida yake ni ipi?

Faida yake ni kwamba Yesu anapata nafasi ya kukupitisha katika madarasa yake, na kwasababu husongwi na mambo mengine, hivyo kasi yako ya kukua kiroho itakuwa ni kubwa sana..

Maandiko yanasisitiza hilo katika;

Isaya 40:3 “Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, Itengenezeni nyikani njia ya Bwana; Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu”.

Kuonyesha kwamba mahali pekee ambapo utamtengenezea Mungu njia, katika maisha yako ni jangwani.

Leo hii utaona watu wengi wamedumu katika wokovu kwa miaka mingi, lakini huoni mabadiliko makubwa yoyote ndani yao, bado ni wachanga kila siku wanataka wanyweshwe tu maziwa, ni kwasababu gani?

Ni kwasababu hawakumpa Kristo, nafasi ya kuwafundisha majangwani..Walilikimbia jangwa, wakakaa ulimwenguni, na hivyo Bwana akawaacha.

Ndugu/Dada uliyeokoka hivi karibuni usiipuzie hiyo sauti inayokuambia, acha hiki, acha kile, mwache Rafiki yule, acha jambo lile..usiipuuzie kabisa, fanya hivyo, ni sharti upoteze, ili upate baadaye, majira haya ni kujikana nafsi yako, kuichukia nafsi yako, na kujitwika msalaba wako kumfuata Yesu, hilo haliwezi kuepukika ikiwa unataka ukue kiroho kwa kasi anayoihitaji Kristo ndani yako.

Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.

25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.

26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?

27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”.

Kabla ya kumzalia Mungu matunda ni lazima upitishwe jangwani, kutakaswa na Mungu, hivyo kuwa mwepesi kuacha udunia wako. Umfuate Yesu.

Bwana akubariki.

Shalom.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA: Sehemu ya 1

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNYAKUO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

Rudi nyumbani

Print this post

HATARI! HATARI! HATARI!

Unajua ni kwanini Bwana Yesu alisema  “Jiangalieni basi jinsi msikiavyo?” (Luka 8:18)

Alijua kuwa kuna hatari kubwa sana ya mtu aliyesimama kupotea kwa kile tu anachokisikia ikiwa hakitokani na yeye.. Hivyo si kila jambo ni la kulisikiliza na kuliweka moyoni, Zama hizi ni zama za uovu.

Mambo haya makuu matatu, kuwa nayo makini sana siku hizi za mwisho.

  1. Maono
  2. Ndoto
  3. Mafunuo

Ikiwa Maisha yako yote unayoishi ni kutegemea tu maono unayoonyeshwa, au ndoto, au mafunuo, na huku umeliweka Neno la Mungu nyuma basi ujue, hatari ya kupotea ni kubwa sana..tena sana. Haijalishi yatakuwa yanatoka kwa Mungu au kwa shetani, kama unaliweka Neno la Mungu nyuma..Bado hatari ya kupotea ni kubwa sana kuliko unavyodhani ndivyo ilivyo.. Najua inaweza ikawa ni ngumu kupokea lakini ukweli ndio huo.

Leo tupo wakati ambapo mtu atakuambia nimepelekwa kuzimu, nikaonyeshwa hiki, na kile, nimeonyeshwa watu wanaokula pipi za ivory, na soda za cocacola wapo kuzimu, nimeonyeshwa mabinti wote, walioingia katika ndoa bila ubikira, wanazini, waume zao ni wale wakwanza waliozini nao, kabla hawajaokoka hao ndio wanapaswa wakaolewe nao, hivyo wakiolewa na wengine wanazini..Nimeonyeshwa watu wote wanaosali siku ya jumapili wapo jehanamu, nimeambiwa na Yesu watu wote wanaoota ndoto wanapaa wajiandae na moto, nimeambiwa, kama umeokoka, unapaswa urudishe madeni yote uliyowahi kuwatapeli watu huko nyuma hata kama huna uwezo huo, usipofanya hivyo ni ziwa la moto, kama unakwenda beach kuogelea ni kuzimu, kama upo katika ndoa na unatumia uzazi wa mpango ujue ni motoni moja kwa moja…n.k n.k. Ni mengi mno..

Mambo kama haya embu tujaribu kudhania kuwa ni kweli yanatoka kwa Mungu..Lakini nikikuuliza swali ni nini kimekupa uhakika kuwa kinatoka kwa Mungu, utanipa jibu gani? Utasema ni kwasababu mpendwa yule kaonyeshwa au mimi nimeonyeshwa?? Au ninamwamini sana yule? Unadhani hilo tu linatosha?

Je! Ikitokea mwingine akakamwambia watu wote wenye Ngozi nyeusi, wanayo laana ya Hamu, hivyo wasipokombolewa kwa kupitishwa kwenye kemikali maalumu ya kuchubuliwa Ngozi zao, hawataingia mbinguni..Je! hilo nalo utalithibitisha vipi?

Ndugu ukiishi kwa Neno la Mungu, ni elimu tosha, ni ushuhuda tosha..hata kama mtu akikuambia nimeonyeshwa mashoga  wote wapo motoni, wewe uliye na Neno, hutashangaa kana kwamba ni jambo jipya, kwasababu Neno linakuambia hivyo..Hata kama asingekuletea maono hayo.

1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Hivyo hapo hujaishi kwa maono yako, bali kwa Neno la Mungu, basi upo salama.. Hatari inakuja ni pale mtu unapotegemea  tu shuhuda, na kuziamini moja kwa moja bila hata ya kuzipima..ndugu  utatoka nje ya mpango wa Mungu, utachanganywa, utaishi kwa hofu na wasiwasi, na presha kubwa, kwasababu huyu atakuambia hivi yule vile, yatachanganyikana ya ukweli na uongo..matokeo yake utashindwa kujua ni wapi umesimama..Na mtu wa namna hii ni rahisi sana kuanguka dhambini. Na ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kuijua biblia.. SOMA BIBLIA.

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Kuwa makini na shuhuda unazozisikiliza mitandaoni (youtube)..Kuwa makini na watu unaowafuatilia mitandaoni. Usipoijenga Imani yako katika Neno la Mungu, shetani atakusaidia kujenga Imani yako katika misingi yake mwenyewe.

Usiniamini mimi, wala usimuamini mtu yeyote, iamini biblia yako, hiyo inatosha..Utakuwa salama.

Mwingine atakuambia Bwana ameniambia leta nywele zako, na kucha zako, weka kwenye kitambaa chekundu, tuombe Pamoja, ukimuuliza misingi hiyo ameitolea wapi, atakuambia nimefunuliwa, na usipofanya hivyo huwezi kufunguliwa.. Hii ni Hatari kubwa sana! ..Kataa kusikiliza hayo mafunuo.

Mwingine atakuambia, pasipo kuniamini mimi, huwezi kwenda katika unyakuo, kataa

1Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;”

Usiwe mwepesi wa kuamini Neno lolote usilolithibitisha katika maandiko,

Bwana atusaidie..

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO YA MASHETANI

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

KUONGOZWA SALA YA TOBA

USIISHI KWA NDOTO!

MIHURI SABA

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?

Kama unadhani mazingira ni sababu ya wewe kutokuwa Mwanafunzi wa Yesu, basi tafakari mara mbili!.

Unaweza kusema labda Nimezaliwa katika dini inayompinga Kristo, nawezaje kuwa Mkristo tena yule wa kujikana nafsi?..nimeolewa na mtu ambaye anampinga Bwana Yesu? Na familia yangu yote haimwamini Yesu wala haiamini Ukristo..je inawezekana mimi kuwa mkristo na kuanza kwenda kanisani na hata kumtumikia yeye?

Jibu ni Ndio! Yote yanawezekana endapo utaamua kujikana nafsi kwa kumaanisha kumfuata Yesu..

Inawezekana kabisa kuwa mwanafunzi wa Yesu, na hata kuifanya kazi yake. Wewe sio wa kwanza kukutana na  mazingira kama hayo, hata katika biblia walikuwepo watu wa namna kama yako, ambao walikutana na mazingira magumu kuliko yako, lakini walishinda…lakini pia walikuwepo  walioshindwa..

Hebu tujifunze katika makundi yote mawili, ya walioshindwa na walioshinda.

1 . WALIOSHINDWA.

Tusome,

Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi”.

Hawa ni Wayahudi, ambao walimwamini Kweli Yesu lakini, walihofia kutengwa na ndugu zao na zaidi sana masinagogi yao, yaani watu wa dini yao!. Hivyo wakaishia tu kumwamini Yesu lakini hakuna chochote walichozalisha.

2 . WALIOSHINDA.

Lilikuwepo ambalo lilikuwepo katika mazingira magumu, lakini lilishinda.

Mfano wa hao ni YOANA MKEWE KUZA, wakili wa Herode. Na MANIELI ndugu wa Herode.

YOANA, MKEWE KUZA.

Huyu Yoana, alikuwa ni mke wa mtu aliyeitwa Kuza, ambaye alikuwa ni wakili wa mfalme Herode. Sasa ili kujua vizuri familia ya Herode ilikuwa ni ya watu wa namna gani, tusome mistari ifuatayo..

Mathayo 2:16 “Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi”.

Herode alimtafuta kumwua Bwana Yesu katika uchanga wake, na hata kipindi amekuwa mkubwa mwanae alimkata kichwa Yohana mbatizaji.(Mathayo 14:1-10), na Zaidi sana baadaye alikuja kumwua Yakobo, mtume wa Bwana Yesu (Matendo 12:1-2) na alitafuta kumwua na Petro pia, lakini Bwana alimwepusha na mauti yake hiyo..

Kwahiyo kwa ufupi ni kwamba Herode alikuwa ni mpinga Kristo kwa wakati huo, na endapo angesikia yeyote katika watu wake kajishikamanisha na Bwana Yesu, wazo lake ni lile lile la kuua.. lakini tunaona huyu mke wa Wakili wake, aliyajua hayo yote, na Pamoja na hayo, akaamua kumfuata Yesu na kuwa mwanafunzi wake, pasipo kujali atapitia nini mbeleni.

Na tena sio yule mwanafunzi wa siri siri, bali yule wa wazi kabisa..ambaye anaambatana na Bwana Yesu kila mahali, na tena anamhudumia..

Luka 8:1 “Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye,

2 na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3 NA YOANA MKEWE KUZA, WAKILI WAKE HERODE, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao”.

Umeona?..Yoana alijua kuna kifo kinamgoja wakati wowote, lakini alijikana nafsi na akawa moja ya wanawake wa mbele kabisa walioheshimiwa na Bwana Yesu.

MANAENI

Sio huyo tu! Kulikuwepo na mwanaume mwingine anayeitwa Manaeni..Huyu maandiko yanasema alikuwa ni NDUGU WA KUNYONYA wa Mfalme Herode…maana yake wametoka katika familia moja na Herode, wanajuana ndani na nje!.. lakini pamoja na kwamba anajua ndugu yake ni mfalme tena Mpinga-Kristo, yeye hakumwogopa.. bali aliacha vyote akachukua msalaba wake, akamfuata Yesu, na hatimaye Bwana akamfanya kuwa NABII wake.

Matendo 13:1” Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na MANABII NA WAALIMU, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na MANAENI ALIYEKUWA NDUGU WA KUNYONYA WA MFALME HERODE, na Sauli.

2 Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia”.

Kupitia watu hawa wawili YOANA Pamoja na MANAENI, itoshe kutupa kila sababu ya sisi kujikana nafsi!.

Watu hawa watasimama siku  ya hukumu Pamoja na sisi, ambao tunasema tupo katika mazingira magumu ya kumfuata Yesu, watatuhukumu.

Hivyo ndugu kama wewe umeolewa na mtu asiye mkristo, na sasa umemwamini Yesu, usione aibu wala usiogope, mkiri Kristo hadharani…kama wewe unaishi na wapagani ambao hawamwamini Yesu au wanampinga!.. bali usiwaogope.. wewe mfuate Yesu, kuwa mwanafunzi wake, jikane nafsi kama Yoana na Manaeni. Na Bwana Yesu atakuheshimu kuliko kawaida, atakutukuza kama alivyowatukuza Yoana na Manaeni.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.

Maherodi walikuwa ni akina nani, Na kazi yao ilikuwa ni ipi?

NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?

Wanafunzi wa Yesu, walimaanisha nini kusema kama “Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa”?

Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)

Rudi nyumbani

Print this post

NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA, WAENDE HEKALUNI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe karibu tujifunze biblia,

Luka 21:37 “Basi, kila mchana alikuwa akifundisha hekaluni, na usiku huenda kulala katika mlima uitwao wa Mizeituni

38 NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA WAENDE HEKALUNI ILI KUMSIKILIZA”.

Je unaijua sababu ya Bwana Yesu kulala juu ya mlima wa mizeituni?

Si kwasababu hakuwa na watu wa kumkaribisha kwake awe analala kwao? La! alikuwa nao tele!!, na wengine wenye uwezo mkubwa tu!.. mfano wa hao ni Yule Yusufu mwanafunzi wake ambaye alikwenda kumwomba Pilato auondoe mwili wake pale msalabani, maandiko yanasema alikuwa ni mtu tajiri.

Mathayo 27:57 “Hata ilipokuwa jioni akafika MTU TAJIRI wa Arimathaya, jina lake Yusufu, naye mwenyewe alikuwa mwanafunzi wa Yesu;

58 mtu huyu alimwendea Pilato akauomba mwili wa Yesu. Ndipo Pilato akaamuru apewe”.

Mwingine ni Yule aliyempa chumba Bwana Yesu wakati wa Pasaka, (maandiko yanasema mtu huyu alikuwa ni mtu anayemiliki ghorofa, na kuna chumba maalum, juu ya ghorofa ambacho alikuwa amempa Bwana Yesu na wanafunzi wake).

Marko 14:13 “Akatuma wawili katika wanafunzi wake, akawaambia, Nendeni zenu mjini; atakutana nanyi mwanamume amechukua mtungi wa maji; mfuateni;

14 na po pote atakapoingia, mwambieni mwenye nyumba, Mwalimu asema, Ki wapi chumba changu cha wageni, niile pasaka humo, pamoja na wanafunzi wangu?

15 Naye mwenyewe atawaonyesha orofa kubwa, imeandikwa tayari; humo tuandalieni”.

Umeona?..watu hawa wote walikuwa wanaishi pale pale Yerusalemu, ambao wangeweza kumhifadhi Bwana kipindi yupo Yerusalemu…na siyo hao tu, bali pia walikuwepo  na wengine wengi,

Lakini jiulize kwanini Bwana kipindi anakaribia kuteswa hakuwa anakwenda kulala katika nyumba zao?.. Sababu zipo mbili. 1) KUOMBA. na  2) KUWAHI IBADANI.

KUOMBA.

  Bwana Yesu alikuwa ni mtu wa kuomba sana..na alijua mazingira bora ya kuomba ni yapi?, si ghorofani wala nyumbani. Bali ni sehemu iliyo na utulivu. Alijua Nyumbani kunakuwa na usumbufu mwingi ambao ungeweza kumwondoa katika uwepo,(usumbufu wa watu na kimazingira), Ndiyo maana utaona mara kadhaa akipanda mlimani pamoja na wanafunzi wake kuomba.. Hiyo ikitufundisha na sisi tuwe watu wa kuchagua mazingira sahihi ya kuomba.

KUWAHI IBADANI.

Sababu ya pili ya Bwana Yesu kulala katika mlima wa Mizeituni, ni ili AWAHI IBADANI. Alijua mazingira ya nyumbani si mazingira ambayo si rafiki kwa yeye kuwahi hekaluni.. kwasababu ya maandalizi kuwa mengi..

 Utaona kipindi tu yupo kwa akina Miriamu na Martha, ni jinsi gani, Martha alivyokuwa anamhangaikia kumwandalia vyakula, mara  chai, mara maji ya kunawa na kadhalika…mahangaiko yale, yakachukua mpaka muda wa kuanza kujifunza, mwisho Bwana Yesu ikabidi aanze kufundisha kabla hata ya Martha kumaliza kupika.. na kilichofuata utaona Martha!, alikwazika!..

Sasa mambo kama hayo hayo Bwana Yesu aliyajua ndio maana akatafuta mlima ulio karibu na hekalu awe analala huko kipindi anaendesha semina ya Masomo pale Hekaluni.

Kwasababu kukisha pambazuka tu, kazi aliyo nayo ni yeye pengine ni kunawa tu uso na kuteremka hekaluni kufundisha, pengine ingemchukua tu robo saa, kufanya maandalizi, tofauti na angekuwa nyumbani kwa watu..kwasababu Mlima wa Mizeituni na hekaluni ni mita kadhaa tu, si mbali..!

Hivyo Bwana Yesu akawa anawahi hekaluni mapema sana, wa kwanza kabla ya wote!..na kuwafundisha wale waliowahi kama yeye (akawa kielelezo). Na wengine wote walipoona kuwa anawahi, na kumkuta akifundisha wachache waliowahi kama yeye, na wenyewe wakawa wanaamka asubuhi na mapema kwenda kumsikiliza, wasikose madarasa hayo ya asubuhi..

Luka 21:37 “Basi, kila mchana alikuwa akifundisha hekaluni, na usiku huenda kulala katika mlima uitwao wa Mizeituni. 38 NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA WAENDE HEKALUNI ILI KUMSIKILIZA”.

Kristo hata leo anawahi asubuhi na mapema Nyumbani kwake!.. na wote walio wake kweli kweli, wanawahi nyumbani kwake kumsikiliza! Na wanapokea Baraka!.

Katika siku hizi za mwisho, shetani anawaharibu wengi katika eneo la USINGIZI, na KUTOKUJALI. Asilimia kubwa ya watu wanaochelewa ibadani, au wasiofika kabisa ibadani ni kwasababu ya Usingizi!, au Kutokujali.

Kama kweli unamjali Bwana Yesu na maneno yake, huna sababu yoyote ya KUCHELEWA IBADANI, hata kama unakaa mbali na kanisa!, Amka mapema wahi kanisani!, KATISHA USINGIZI!!..Tabia ya kupenda usingizi kimwili, inafunua tabia ya kupenda usingizi katika roho, ambayo ni mbaya sana.

Na kama ukiona mahali ulipo ni mbali sana, basi siku moja kabla ya ibada, hamia karibu na maeneo ya kanisa, au kesha kanisani omba, asubuhi yake uamkie nyumbani kwa Bwana, utakuwa umejizolea Baraka nyingi zaidi.

Lakini kama utafika  nyumbani kwa Bwana kwa kuchelewa kwasababu ya usingizi!.. basi ni heri usingefika kabisa kanisani hiyo siku, kwasababu hakuna chochote unachokwenda kupokea hiyo siku!!, ni heri urudi nyumbani ukamalizie usingizi wako tu!!. Tabia ya KUPENDA USINGIZI na ya KUTOKUJALI ni tabia zinazomchukiza Bwana kuliko zote (soma Luka 22:46, Marko 13:35-37).

Na kumbuka hakuna maombi ya kuondoa KUONDOA USINGIZI!!..Dawa ya kuushinda usingizi ni kuamua kubadilisha tabia tu!, na wala si kuombewa!!.. Bwana Yesu alipowakuta akina Petro wamelala muda wa kuomba, hakwenda kukemea mapepo ndani yao!.. alichofanya aliwaambia WAAMKE WAOMBE!.. Roho zao zi radhi, lakini miili ndio midhaifu, hivyo wajilazimishe waamke!.

Na wewe leo hii, Amka mapema nenda Ibadani, amka mapema nenda kwenye maombi, amka mapema nenda shambani kwa Bwana, Ukatae usingizi, na pia Acha kuwa mtu wa KUTOKUJALI.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

 

:

NAWAAMBIA MAPEMA!

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Mlima wa Mizeituni  unaumuhimu gani kwetu?

Rudi nyumbani

Print this post

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Sehemu ya kwanza: LIA NA NYONYA.

Nakusalimu katika jina kuu lenye uweza la mwokozi wetu Yesu Kristo, sifa na heshima vina yeye milele na milele.

Haya ni Makala maalumu kwa waongofu wapya, ikiwa wewe umeokoka hivi karibuni, au una ndugu/mpendwa ambaye amempokea Bwana Yesu siku za karibuni basi Makala hizi ni muhimu sana kwako au kwa yule mwingine.

Tunaposema kuokoka, tunamaanisha Kuzaliwa mara ya pili. Na mtu anazaliwa mara ya pili, kwa kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu, na pia kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38), na kwa kupokea Roho Mtakatifu..Kwa kuzingatia hivyo vigezo, basi mtu huyo anakuwa ameshazaliwa mara ya pili.

Lakini sasa hilo peke yake halitoshi, wengi wanapotimiliza maagizo hayo wanajisahau na kudhani ndio tayari wameshatimilika, hakuna cha ziada.. Hawajui kuwa  mtu unaweza ukawa kweli umezaliwa mara ya pili lakini ni kiumbe kilicho kufa.. Utajiuliza ni kwa namna gani inakuwa hivyo?

Mtu anayezaliwa mara ya pili katika roho anafananishwa na mtoto, anayezaliwa mara ya kwanza katika dunia. Kwa kawaida mtoto huyo, ni lazima aonyeshe tabia kuu mbili. Kabla hajaweza hata kuona, au kuzungumza, au kujitambua..Ni lazima

  1. ALIE.
  2. Baadaye ANYONYE.

ALIE kwa sababu gani.. Mtoto anapotoka tumboni kwa mama yake, anakuwa kama kiumbe mfu, wanachofanya wakunga ni kumpiga kidogo, kumshutua ili atoe sauti, wakisikia analia basi wanatambua kuwa kiumbe kilichozaliwa ni hai, hivyo baada ya muda kidogo wanamsogeza katika hatua nyingine,

Ambayo ni kunyonyeshwa.

Cha kushangaza ni kwamba mtoto yule anaposogezwa katika nyonyo la mama yake, hakuna mtu yeyote anayemfundisha kunyonya, utaona ni yeye mwenyewe anajua wajibu wake, wa kula, ndio hapo utaona saa hiyo hiyo ataanza kufyonza maziwa kana kwamba alishawahi kufundishwa huko tumboni jukumu lake kabla hajafika duniani.

Sasa kiroho pia ndio ipo hivyo. Ikiwa wewe umezaliwa kweli mara ya pili, hizi ni hatua za awali kabisa ambazo utazionyesha. Na kupitia hizo sisi wengine tutathibitisha kweli wewe ni kiumbe kipya hai. Kwani  ni lazima utoe kelele fulani rohoni.. Huwezi kutulia, ambao sisi tuliokomaa kiroho tutazitambua, japo wewe hutoweza kuzielewa katika hatua yako ya uchanga rohoni..

Sisi tutaona kuhangaika kwako kutaka msaada wa kumjua Mungu, Na sisi tukishalitambua hilo, basi tunakuwa na wajibu mkubwa sana wa kukusaidia, kukosegezea matiti (Neno la Mungu) unyonye..

Hebu tujifunze kisa cha Musa, pindi anazaliwa..Biblia inatuambia, alipozaliwa, mama yake alimficha ili Farao asimuue, lakini alipoona hali imekuwa  mbaya, alimtengenezea kisafina kidogo, kisha, akamtupa mtoni.. Lakini mtoto yule alipokuwa katika kila kisafina, hakukaa kimya tu, bali alikuwa anapiga kilele, analia,sana na binti Farao aliposikia alikwenda kutazama na kufungua aone ni nini kipo ndani, akakaona katoto, wakakahurumia..Embu tusome kwa ufupi kisa hicho;

Kutoa 2:6 “Akakifungua, akamwona mtoto, na tazama, MTOTO YULE ANALIA. BASI AKAMHURUMIA, akasema, Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania.

7 Basi umbu lake mtoto akamwambia binti Farao, Je! Niende nikamwite mlezi katika wanawake wa Kiebrania, aje kwako, akunyonyeshee mtoto huyu?

8 Binti Farao akamwambia, Haya! Enenda. Yule kijana akaenda akamwita mama yake yule mtoto.

9 Binti Farao akamwambia, Mchukue mtoto huyu, ukaninyonyeshee, nami nitakupa mshahara wako. Yule mwanamke akamtwaa mtoto, akamnyonyesha.

10 Mtoto akakua, naye akamleta kwa binti Farao, akawa mwanawe. Akamwita jina lake Musa, akasema, Ni kwa sababu nalimtoa majini”.

Umeona? Mtoto yule angeangamia kama asingelia, lakini alipolia, akahurumiwa akatafutiwa msaada mapema wa kunyonyeshwa, na hatimaye akakua akaja kuwa Mkombozi wa Israeli, ndiye Musa tunayemsoma.

Ndugu/Dada uliyeokoka hivi karibuni, kutojishughulisha kwako na mambo ya Mungu, kunathibitisha kuwa wewe ni kiumbe mfu, kutoulizia kwako Habari ya ibada, kunatuambia kuwa wewe si kiumbe hai..Hupaswi kujificha, hupaswi kujiepusha na kiongozi wako wa kiimani..hupaswi kukaa mbali na wapendwa, hupaswi kupitisha siku nyingi hujulikani upo wapi, au maendeleo yako ya kiroho hayatambuliki.. kataa hiyo hali kwa nguvu zote..

Wewe tayari ni kiumbe kipya, yatamani sana maziwa ya roho.. Usisubiri kukumbushwa kumbushwa kuhudhuria mafundisho ya kuukulia wokovu, kama mtoto mchanga ambaye hafundishwi na mtu kunyonya ni wajibu wako kutafuta kufundishwa Neno la Mungu, kwa bidi zote..Sio wewe utafutwe.

1Petro 2:2 “Kama watoto wachanga wazaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili k hayo mpate kuukulia wokovu.

Hivyo anza sasa kubadilisha mwenendo wa Maisha yako.. Jifunze kuomba na wapendwa, jifunze, kusoma biblia mwenyewe kuanzia sasa, jifunze kuuliza maswali, jifunze kumshirikisha na kukuonyesha njia sahihi.

Wagalatia 6:6 “Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake up

Hivyo zingatia mambo hayo makuu mawili. Na Bwana akutie nguvu.

Shalom.

Sehemu ya pili itafuata…

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

UMEITIMIZA HAKI YOTE?

ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya wokovu watoka kwa Wayahudi? (Yohana 4:22)

Swali: Bwana alimaanisha nini kusema wokovu watoka kwa Wayahudi?, kwani si tunajua Wokovu unatoka kwa Mungu, iweje hapo aseme unatoka kwa Wayahudi?

Jibu: Tusome,

Yohana 4:22 “Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.”

Wokovu unaozungumziwa hapo, ni “Wokovu wa Roho”..na si wokovu wa vita au kitu kingine!, na aliposema kuwa “unatoka kwa Wayahudi” hakumaanisha kuwa Wayahudi ndio wanaoutoa wokovu na kuwapatia wengine la!, hakuna mtu wala Taifa linaloweza kuiokoa roho ya mtu!!, bali alimaanisha kuwa “wokovu unaanzia kwa wayahudi”, na ndipo unaenda kwa wengine…(yaani kwa watu wa mataifa ikiwemo na wasamaria ndani yake).

Ndio maana utaona ni kwanini Bwana wetu Yesu hakuzaliwa nje na jamii ya Israeli, wala hakuzaliwa katika Samaria, au katika Taifa lingine lolote tofauti na Israeli, badala yake alizaliwa Israeli, sawasawa na unabii Mungu alioutoa kupitia manabii wake wa zamani kama Musa, Daudi, na wengineo.

Na baada ya kuzaliwa katika jamii ya Wayahudi (yaani waisraeli), hakuanza kuhubiri injili yake kwa jamii ya watu watu wa mataifa, halafu ndio afuate kwa watu wa jamii ya Israeli(wayahudi) bali badala yake alianza kwanza kwa Wayahudi, na walipokataa ndipo akaruhusu injili ihubiriwe pia kwa watu wa mataifa ambao ndani yake pia wapo wasamaria.

Mathayo 10:5 “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, AKAWAAGIZA, AKISEMA, KATIKA NJIA YA MATAIFA MSIENDE, WALA KATIKA MJI WO WOTE WA WASAMARIA MSIINGIE.

6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

7 Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Umeona?..Wanafunzi walikatazwa na Bwana kuhubiri kwa watu wa Mataifa katika mwanzo wa Injili, lakini baadaye, baada ya Wayahudi kushiba, na kukinai….Bwana Yesu aliwaruhusu pia wanafunzi wake waende kwa watu wa mataifa duniani kote wakahubiri injili kwa kila kiumbe.

Marko 16:14 “Baadaye akaonekana na wale kumi na mmoja walipokuwa wakila, akawakemea kwa kutokuamini kwao na ugumu wa mioyo yao, kwa kuwa hawakuwasadiki wale waliomwona alipofufuka katika wafu.

15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Tunazidi kulithibitisha hili pia, kipindi Mtume Paulo anawahubiria wayahudi wa Antioko..

Matendo 13:45 “Bali Wayahudi, walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana.

46 Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa LAZIMA NENO LA MUNGU LINENWE KWENU KWANZA; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa milele, angalieni, twawageukia Mataifa.

47 Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, Upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.

48 Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini”.

Umeona?.. Wokovu umeanzia kwa Wahayudi, na ukaenda kwa watu wa Mataifa. Hiyo ndio sababu ya Bwana Yesu kusema.. “Yohana 4: 22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.”

Je umeupokea Wokovu wa Bwana Yesu ambao tumeletewa sisi watu wa mataifa, ambao hapo kwanza hatukustahili?. Kama bado unasubiri nini?.. Pengine kweli umeupata Wokovu, lakini je! Unaujali kwa kuutunza?.. Au ni kama tu utambulisho katika Maisha yako, lakini hauna thamani nyingine yoyote ya ziada katika Maisha yako?.

Kumbuka kama unavaa nusu uchi, au nguo ambazo si za kujisitiri, kama vile suruali(kwako wewe mwanamke) au vimini tambua kuwa unaudharau wokovu wa Bwana, kama unalewa, au unacheza kamari, au unazini, au unafanya uchawi, au unaiba baada ya kuisikia injili mara nyingi, au baada ya kubatizwa..tambua kuwa unaudharau wokovu wa Bwana.

Hatari ya kutouthamini Wokovu wa Bwana ni hii tunayoisoma katika Waebrania 2:1.

Waebrania 2:1 “Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa.

2 Kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki,

3 SISI JE! TUTAPATAJE KUPONA, TUSIPOJALI WOKOVU MKUU NAMNA HII? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”

Utapataje kupona, wewe ambaye huujali Msalaba?..siku ile utakuwa mgeni wan ani?..ni heri ukatengeneza mambo yako leo ili uwe na uhakika wa maisha yako ya umilele.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

USIMPE NGUVU SHETANI.

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Mataifa ni nini katika Biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

Nakusalimu tena katika jina la Bwana Yesu mwokozi  wetu, karibu katika kutafakari Maneno ya uzima..huu ni mwendelezo wa Makala  zinazohusu malezo ya Watoto kwa mzazi.

 Ikiwa wewe ni mzazi au mlezi na unao Watoto wadogo chini yako wa kuwalea, au unatarajia kuwa na Watoto.. Basi Makala hii ni muhimu sana kwako,

Zipo Makala nyingine tulishazitazama huko nyuma ikiwa hukuzipitia, basi waweza waweza wasiliana nasi inbox kwa namba hizi +255693036618 tuweze kukutumia.

Leo tutaona umuhimu wa kuwafundisha, Watoto nyimbo za kumsifu Mungu au kumwimbia..Awali ya yote ni lazima ufahamu kuwa, kila mtoto amewekewa ibada ya sifa ndani yake, haijalishi utalipenda hilo au hautalipenda..Na ibada hiyo huwa inakamilika pale anapokutana na Watoto wenzake kwenye michezo sehemu za wazi..Hapo ndipo utajua hicho kitu kipo ndani yake.

Kaa chunguza kwa makini, mahali palipo na Watoto wengi wamekusanyika, utasikia wakiimba vi-nyimbo Fulani mbalimbali, kulingana na kile ambacho walifundishwa, au wanachokisikia watu wengine wakiimba..

Na ndio maana Bwana Yesu alitumia mfano wa Watoto wanaocheza, masokoni, kwa kuimba, kukifananisha kizazi hiki jinsi mienendo yao ilivyokuwa na mwitikio mdogo wa injili..

Luka 7:31 “Bwana akasema, Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Nao wamefanana na nini?

32 Wamefanana na watoto walioketi sokoni na kuitana, wakisema, Tuliwapigia filimbi wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia”.

Sasa wewe ukiwaona wanaimba unaweza kuchukulia kirahisi rahisi sana ukasema wanacheza tu, wanajifurahisha..lakini rohoni wanaonekana wanasifu katika ukamilifu wote, na hivyo wanasababisha madhara makubwa sana, hata kwa upande wa pili.

Ili tuelewe vizuri embu tujifunze kisa kimoja, kilichotokea Yerusalemu kipindi kile Bwana Yesu, anaingia akiwa amepanda punda na mwanapunda..Biblia inasema, watu walimtandikia nguo zao chini, na wengine majani ya mitende, wakaanza kumsifu kwa nguvu, wakisema Hosana hosana, Mwana wa Daudi..

Lakini wakati huo huo kulikuwa na kundi la Watoto linaongozana nao pembeni likiwasikiliza.. linajifunza hizo nyimbo..ndipo tunaona mwishoni kabisa wale watu walipomaliza sifa zao, Bwana Yesu aliingia Hekaluni, Lakini kule hekaluni, Watoto, hawakukaa kimya, wakaanza kutoa walivyovisikia,..wakawa wanakiimba kile wachokisikia kule nje! Hosana hosana, mwana wa Daudi..

Tendo lile likawa bughza kwa maadui wa Kristo, walipokuwa wanawasikia Watoto wakipiga kelele kama nyuki hekaluni, wakiimba walichokuwa wanakisikia, ndipo wakamfuata Kristo, kumuonya.. Lakini tunaona, Bwana hakuwaambia sawa nitawanyamazisha kinyume chake akawapa siri nyingine ambayo walikuwa hawaijui..akawaambia maneno haya.. “HAMKUPATA KUSOMA, KWA VINYWA VYA WATOTO WACHANGA NA WANYONYAO UMEKAMILISHA SIFA”

Mathayo 21:9-10,15-16

 “9 Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.

10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?

11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya…..

15 Lakini wakuu wa makuhani na waandishi walipoyaona maajabu aliyoyafanya, na watoto waliopaza sauti zao hekaluni, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi! Walikasirika,

16 wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umekamilisha sifa?”

Umeona? Kumbe sifa za kweli zimekamilika katika vinywa vya Watoto wachanga, sio ajabu kuona mapepo yale yakilipuka ndani ya wale waandishi na wakuu wa makuhani, na kutaka kumshambulia Yesu kwasababu yao..

Mapepo yaliyokuwa yameigeuza nyumba ya Mungu kuwa pango la wanyang’anyi, sasa yanakutana na waaabuduo halisi wanaomwabudu Mungu katika Roho na kweli wamefika..(watoto)..Ni lazima yataabikie tu..

Lakini Habari hii inatufundisha nini sisi wazazi na walezi?

Kama sifa za kweli zimekamilika katika vinywa vya Watoto wachanga, basi tunapaswa tutumie nguvu nyingi sana kuwafundisha Watoto kumwimbia na kumsifu Mungu,  Ni muhimu sana, kwasababu hizo tu zinatosha kumtikisa shetani na ufalme wake..

Lakini kinyume chake ni kweli, kama mtoto hatoimba nyimbo za Mungu, badala yake amekaririshwa, bongofleva, na manyimbo ya kidunia, tufahamu kuwa sifa hizo pia zinakuwa zimekamilika kwa shetani. Hivyo, shetani anatukuzwa, na ufalme wa Mungu unadidimia.

Inasikitisha leo hii, kuona makundi ya Watoto wengi barabarani wanaimba nyimbo za wasanii wa kidunia, ambazo hata wewe mtu mzima kusikiliza unaziba masikio, mpaka unajiuliza hivi wazazi au walezi wao wapo wapi?

Wazazi wapo buzy na kazi, wapo buzy na biashara, wanachozingatia kwao tu ni elimu za duniani basi..Hayo mengine hawahangahiki nayo, hawajui kuwa mapepo yanapata nafasi katika mahekalu yao( yaani Nyumba zao), kwasababu ya sifa za Watoto wao za kipepo, zinamtukuza Ibilisi mwenyewe..

Ndugu, ukitaka furaha katika nyumba yako, embu wafundishe Watoto wako kuimba mapambio, vichwa vyao vijae sifa na nyimbo, waimbe hizo wakati wote, wachezecheze wakiimba hizo sio bongofleva.. kataa mtoto wako kujifunza, hizo nyimbo, wala usimvumilie unapomwona anaziimba bali mkemee.. sio kila mahali umpeleke mtoto au uende naye, huko atajifunza manyimbo ya ibilisi..

Wakati huu ambao bado ni wachanga, vichwa vyao huwa vinakamata sana upesi, hivyo tumia fursa hiyo, kuwapeleka Watoto, Sunday school, na kwenye mafundisho yao, ili wafunze huko kuimba na kumtukuza Mungu..Amani ije nyumbani kwako.

Bwana atusaidie sana, kuliona hilo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

MALEZI YA MTOTO MCHANGA.

KAMA “MAMA” UMEBEBA HATIMA YA MTOTO WAKO WA KIUME.

Je! Siku ya unyakuo watoto wachanga watanyakuliwa?

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

UMEITIMIZA HAKI YOTE?

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

Rudi nyumbani

Print this post