USIISHI KWA NDOTO!

USIISHI KWA NDOTO!

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, nakukaribisha katika kuyatafakari maandiko. Leo tutajifunza mbinu nyingine ambayo adui shetani anaitumia kuwapunguzia watu kasi ya kumtafuta Mungu.

Ni wazi kuwa kila mtu ana kiu ya kusikia sauti ya Mungu katika maisha yake, na ana kiu ya kujua ni nini kinamzunguka, ni hatari gani iliyopo sasa na iliyopo mbele yake. Na kutokana na wengi kukosa kufahamu ni namna gani wanaweza kuisikia sauti ya Mungu, wameishia kujikita kuishi kwa ndoto wanazoota, wakiamini  kuwa kila ndoto wanayoota ni Mungu anazungumza nao.

Leo nataka nikuambie ndugu, ambaye pengine una kiu ya kutafuta kuisikia sauti ya Mungu katika maisha yako, nataka nikuambie sauti ya Mungu haipo katika ndoto unazoota kila siku, njia pekee ya kuisikia sauti ya Mungu si ndoto unazoota bali ni NENO LA MUNGU linalokaa ndani yako. Sauti ya Mungu ni Neno lake katika biblia na si ndoto!.

Si kila ndoto ni sauti ya Mungu kwako. Nyingi zinakuja kutokana na shughuli zako za kila siku na mambo yaliyoujaza moyo wako.

Kwa mfano kama maisha yako yamejaa kutazama filamu za kidunia, na kusikiliza miziki, basi ndoto zako zitajaa hayo mambo, kama moyo wako umeujaza kutukana na maisha ya anasa, na ndoto zako pia zitakuwa hivyo hivyo, kama maisha yako yamejaa kufanya shughuli nyingi kutwa kuchwa, basi na ndoto zako zitakuwa zinahusiana na hizo hizo shughuli unazozifanya..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;….”.

Sasa inapotokea mtu anaacha kulisoma Neno, na kuishi kwa ndoto zake, na kwamba kila anachoota anatafsiri kwamba ni ujumbe kutoka kwa Mungu, mtu namna hiyo ni rahisi sana kupotezwa na uongo wa shetani. Kwasababu ameacha kujua njia sahihi ya kuisikia sauti ya Mungu, na amekijita kwenye ndoto anazoota kila siku.

Sauti ya Mungu, ni Neno lake ndani ya biblia takatifu. Ukitaka kujua Mungu anataka kuzungumza nawe nini kwa wakati huu, au kwa wakati ujao, nenda kasome biblia, na utaisikia sauti ya Mungu kwa wakati huo..inakuambia nini, (Ni kweli Mungu anaweza kuzungumza na mtu kwa ndoto, lakini hiyo ni mara chache sana..ukilinganisha na jinsi anavyoweza kuzungumza na sisi kwa kupitia Neno lake).

Yusufu japokuwa alikuwa na kipawa hicho cha Mungu kuzungumza naye kwa ndoto, lakini biblia inarekodi mara tatu tu, katika maisha yake yote. Lakini leo utaona mtu kila ndoto anayoota kwake ni ujumbe kutoka kwa Mungu!!. Na huku kaisahau kabisa biblia, hafahamu chochote kuhusu maneno ya Mungu.

Ndugu, Kama unaishi kwa ndoto, (Na kwamba kila asubuhi unapoamka wewe ni kutafuta tafsiri ya ndoto yako kwa watumishi), fahamu kuwa upo mbali sana na sauti ya Mungu, na ndoto unazoota umepofushwa macho ukidhani kuwa Mungu anazungumza na wewe kila siku huko kwenye ndoto zako. Mifano wa sauti ya Mungu kwako na kwangu ni hii >>

Mathayo 5:21 “Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu.

22 Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto”.

Mathayo 5:38 “Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino;

Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili”.

Na..

Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki”.

Hiyo ndio mifano ya sauti na maonyo ya Mungu kwetu, ambayo ipo moja kwa moja isiyo na mafumbo yoyote. Lakini tukizutumainia ndoto tunazoota kila siku, na kufikiri huo ndio mlango wa kwanza wa Mungu kuzungumza na sisi, tutakuwa tumepotea njia pakubwa sana.

Hivyo tusiishi kwa ndoto, bali kwa Neno la Mungu!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

Akawaambia Enendeni ulimwenguni mwote,MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE.(Marko16:15.) Yesu Anamaanisha nini kusema MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
M
M
2 years ago

Be blessed

William lasway
William lasway
2 years ago

Barikiwa sana mtumishi wa Mungu