Ramli ni elimu ya ufalme wa giza, wanayotumia waganga na wenye mapepo ya utambuzi katika kutabiri mambo yajayo, hivyo mtu yeyote anayetumia elimu hiyo kutabiri mambo yajayo, mtu huyo anapiga ramli.
Na watu walipiga ramli aidha kwa njia ya kutumia viganja vya mikono, au kwa kutumia viungo vya Wanyama.
Katika agano la kale, Bwana Mungu aliwakataza wana wa Israeli wasipige ramli ya aina yoyote ile, baadhi walitii na wengi hawakutii, bali waliendelea kupiga ramli na kufanya mambo mengine mabaya…jambo lililowafanya watolewe kutoka katika nchi yao na kupelekwa Babeli na Ashuru utumwani.
2Wafalme 17:16 “Wakaziacha amri zote za Bwana, Mungu wao, wakajifanyizia sanamu za kusubu, yaani, ndama mbili, wakafanya na Ashera, wakaliabudu jeshi lote la mbinguni, wakamtumikia Baali. 17 Wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, WAKAPIGA RAMLI, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, hata kumkasirisha. 18 Kwa hiyo Bwana akawaghadhibikia Israeli sana, akawahamisha mbali na uso wake; wala hapana aliyesalia ila kabila ya Yuda peke yake 19 Hata na watu wa Yuda hawakuyashika maagizo ya Bwana, Mungu wao, lakini walikwenda katika amri za Israeli walizokuwa wamezifanya wenyewe. 20 BASI BWANA AKAKIKATAA KIZAZI CHOTE CHA ISRAELI, AKAWATESA, NA KUWATIA KATIKA MIKONO YA WATU WENYE KUWATEKA NYARA, HATA ALIPOKWISHA KUWATUPA, WATOKE MACHONI PAKE”.
2Wafalme 17:16 “Wakaziacha amri zote za Bwana, Mungu wao, wakajifanyizia sanamu za kusubu, yaani, ndama mbili, wakafanya na Ashera, wakaliabudu jeshi lote la mbinguni, wakamtumikia Baali.
17 Wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, WAKAPIGA RAMLI, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, hata kumkasirisha.
18 Kwa hiyo Bwana akawaghadhibikia Israeli sana, akawahamisha mbali na uso wake; wala hapana aliyesalia ila kabila ya Yuda peke yake
19 Hata na watu wa Yuda hawakuyashika maagizo ya Bwana, Mungu wao, lakini walikwenda katika amri za Israeli walizokuwa wamezifanya wenyewe.
20 BASI BWANA AKAKIKATAA KIZAZI CHOTE CHA ISRAELI, AKAWATESA, NA KUWATIA KATIKA MIKONO YA WATU WENYE KUWATEKA NYARA, HATA ALIPOKWISHA KUWATUPA, WATOKE MACHONI PAKE”.
Lakini swali la kujiuliza, je ni kweli Ramli ina matokeo yoyote??..Kwamba mtu akienda kwa mganga na kupiga ramli ili ajue kesho yake itakuwaje, ni kweli atatabiriwa sahihi mambo yajayo?.
Jibu ni la!.. Shetani kamwe hajui kesho kutatokea nini, kama vile mwanadamu asivyojua kesho ni nini kitatokea. Mwenye uwezo wa kujua kesho ni Mungu peke yake!, kwasababu yeye ndio MWANZO na MWISHO, fahamu zake hazina mipaka.
Lakini shetani anachoweza kufanya ni kupanga jambo leo ambalo anatumaini kuwa kesho litatokea. Kwahiyo mtu anayekwenda kwa mganga, akitaka kujua kesho yake itakuwaje..shetani atakachokifanya ni kumpangia huyo mtu kesho yake, jinsi itakavyokuwa.
Kwamfano mtu anakwenda kwa mganga kutaka kujua kama kesho atatembelewa na wageni au la!.. na yule mganga akamtabiria na kumwambia kwamba kesho atatembelewa na wageni, na tena akawataja na majina, na muda watakaokuja.. Na kweli kufikia hiyo kesho, hao wageni wakaja kama alivyotabiriwa jana.
Sasa hapo sio kwamba huyo mganga, kimiujiza kapelekwa kesho na kuona matukio yake. Bali anachokifanya ni kutuma mapepo, ambayo yatakwenda kuwaingia hao watu aliowataja na kuwashawishi wamtembelee huyo mtu katika huo muda aliopanga yeye siku ya kesho.
Kwahiyo hao wageni na wenyewe kama hali zao za kiroho zipo chini, basi wataingiliwa na hayo mapepo na kesho kwa kujua au kutokujua wanajikuta wanakwenda safari ambayo hawajaitegemea, ili kutimiza ubashiri wa huyo mganga!.
Kwahiyo wote wanaopiga ramli, ndio kitu wanachofanyiwa na shetani (wanatengenezewa matukio) pasipo wao kujua, wakidhani wanaambia mambo yajayo. Hiyo ndio sababu Bwana aliwakataza na anatukataza Watoto wake hata leo, tujiepushe na Ramli na aina yoyote ile pamoja na ushirikina, kwasababu zinaasisiwa na shetani, baba wa Uongo. (Yohana 8:44).
Shetani angekuwa anajua mambo yajayo (future), basi angejua hata siku ya unyakuo ni lini, lakini hajui chochote!. Anachojua kiufasaha ni mambo yaliyopita tu!, kwasababu tayari ni matukio ambayo yameshatokea, jambo ambalo pia lipo ndani ya uwezo wetu sisi wanadamu kujua mambo yaliyopita, lakini si kujua mambo yajayo.
Kwahiyo unapokwenda kwa mganga kupiga ramli kutaka kujua kesho yako, fahamu kuwa ni umeenda kwa shetani kutengenezewa kesho yako na si kuambiwa kesho yako, Utatengenezewa vifo na shetani, utatengenezewa mikosi, na shida, na vile vile utatengenezewa baraka bandia ambazo mwisho wake ni laana.
Ukitaka kuijua kesho yako itakuwaje soma Neno la Mungu..Hilo ndio litakupa unabii kamili na wa uhakika wa kesho yako jinsi itakavyokuwa.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wasikisaze chakula?
Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?
Nini maana ya kupiga Kite! Katika biblia.
Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?
Rudi nyumbani
Print this post
Jibu: Tusome..
1 Timotheo 3:8 “Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, SI WATU WA KUTUMIA MVINYO SANA, si watu wanaotamani fedha ya aibu”.
Kufuatia mstari huu wengi wamejikuta wamezama katika ulevi. Pasipo kujua msingi wa andiko hili kwa undani.
Tukisoma maandiko pasipo msaada wa Roho Mtakatifu tutajikuta tunaangamia badala ya kuponyeka..
2 Wakorintho 3:6 “Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; KWA MAANA ANDIKO HUUA, BALI ROHO HUHUISHA”.
Umeona?..andiko linaweza KUUA!!, shetani alijaribu kulitumia Andiko kumwangamiza Bwana Yesu kule jangwani wakati anajaribiwa.. “Alimwambia, jitupe chini kwakuwa imeandikwa (Mathayo 4:6-7)”..Lakini kwasababu Bwana alikuwa amejaa Roho Mtakatifu aliweza kutambua hila za shetani, na kumshinda.
Kwahiyo tukirudi katika hilo andiko linalosema kuwa Mashemasi wasiwe watu wa kutumia mvinyo sana, ni vizuri kujua muktadha wa andiko hilo, ili tusije tukafanya makosa katika kupambanua maandiko.
Sasa ili tuelewe vizuri andiko hilo maana yake ni nini, hebu twende mbele kidogo mpaka mlango wa 5, wa kitabu hicho hicho cha 1Timotheo. (Tafadhali zingatia maneno yaliyoainishwa kwa herufi kubwa).
1 Timotheo 5:23 “Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia mvinyo KIDOGO, kwa ajili ya TUMBO lako, na MAGONJWA yakupatayo mara kwa mara”.
Hapa tunaona Mtume Paulo kwa kuongozwa na Roho anamwambia Timotheo asitumie maji tu, bali na Mvinyo, (Na mvinyo wenyewe si mwingi bali KIDOGO).
Na ni kwasababu gani atumie mvinyo?..je! ni kwasababu ya burudani, au kujisisimua?? au kujiliwaza??, au kupunguza mawazo???…jibu ni la!..Bali ni kwasababu ya TUMBO na MAGONJWA, yampatayo mara mwa mara.
Maana yake mvinyo huo ulitumika kwa ajili la Matibabu ya magonjwa..na si kwaajili ya ulevi au kujisisimua..ndio maana hapo Paulo anamalizia kwa kusema KIDOGO..kiasi ambacho hakiwesi kumlewesha mtu, kwasababu ukitumika mwingi, utavuka lengo la matibabu, na kumfanya mtu alewe.
Na mvinyo uliokuwa unatumika, kwa matumizi ya matibabu, haukuwa kila aina ya mvinyo tu!..bali uliokuwa unatumika ni DIVAI tu!. Zamani Divai ilitumika kwa matumizi mengi, ikiwemo matibabu ya tumbo na sio tumbo tu bali hata majeraha.. Tunaweza kulithibitisha hilo katika ile Habari ya msamaria mwema.
Luka 10:33 “Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia, 34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia MAFUTA NA DIVAI; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza”.
Luka 10:33 “Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,
34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia MAFUTA NA DIVAI; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza”.
Sasa Paulo kama alivyomuasa hapo Timotheo (ambaye ni askofu wa makanisa )kwamba ATUMIE MVINYO KIDOGO (Zingatia hili neno KIDOGO!!) kwa ajili ya tumbo na magonjwa ya mara kwa mara, na si burudani, ndio hivyo hivyo anawaasa mashemasi na maaskofu wengine kwamba na wao wasiwe watu wa kutumia mvinyo nyingi (maana yake watumie kidogo)..kwaajili ya magonjwa ambayo yatakuwa yanawapata mara kwa mara.
Kwasababu madhara ya kutumia mvinyo nyingi ni kulewa. Na maandiko yanasema ulevi ni dhambi.
Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho”.
Sasa swali la kujiuliza ni je, hata leo tunapopatwa na magonjwa ya tumbo, au majeraha ya mwili tutumie Divai kujitibu?.
Jibu ni la!.. Sasahivi tunayo madawa mengi, yanayotibu tumbo na majeraha kwa ukamilifu wote. Ni sehemu chache sana za dunia zilizosalia zinazotumia njia hiyo ya matumizi ya divai kidogo kwaajili ya tiba ya tumbo au vidonda.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba ULEVI NI DHAMBI, na walevi wote hawataurithi uzima wa milele.
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21 husuda, ULEVI, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ULEVI, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
Kama bado hujampokea Yesu, kumbuka hizi ni siku za Mwisho, kama bado ni mzinzi, au MLEVI, au mtukanaji, au mwizi, au muuaji, tambua kuwa upo hatarini!..hivyo suluhisho ni kumpokea Yesu ili akuoshe dhambi zako na kukusafisha.
Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango,ikiwamo mipira?
Je tunaruhusiwa kutumia vidonge wakati wa kufunga?
Nini maana ya “Andiko huua, bali Roho huhuisha (2Wakorintho 3:6)
Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)
Je! mabalasi Bwana Yesu aliyoyatumia kugeuzia maji kuwa divai, yalitumika tu kwa kazi hiyo?
SWALI: Biblia ina maana gani kusema maneno haya kwa habari ya mitume?
Matendo 5:13 “hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha;”
JIBU: Tusome habari hiyo tena;
Matendo ya Mitume 5:12-16 [12]Na kwa mikono ya mitume zikafanyika ishara na maajabu mengi katika watu; nao wote walikuwako kwa nia moja katika ukumbi wa Sulemani; [13]na katika wote wengine hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha; [14]walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake; [15]hata ikawa katika njia kuu hutoa nje wagonjwa, na kuwaweka juu ya majamvi na magodoro, ili Petro akija, ngawa kivuli chake kimwangukie mmojawapo wao. [16]Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao walioudhiwa na pepo wachafu; nao wote wakaponywa.
Matendo ya Mitume 5:12-16
[12]Na kwa mikono ya mitume zikafanyika ishara na maajabu mengi katika watu; nao wote walikuwako kwa nia moja katika ukumbi wa Sulemani;
[13]na katika wote wengine hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha;
[14]walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake;
[15]hata ikawa katika njia kuu hutoa nje wagonjwa, na kuwaweka juu ya majamvi na magodoro, ili Petro akija, ngawa kivuli chake kimwangukie mmojawapo wao.
[16]Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao walioudhiwa na pepo wachafu; nao wote wakaponywa.
Japokuwa Mungu alidhihirisha uweza mwingi na maajabu kwa mikono ya mitume, lakini kulikuwa na aina maisha/ mwenendo ambao haukuwa mwepesi kwa watu wengine kuufuata kama wao.
Na ndio maana maandiko yanasema hapo “hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao, japokuwa walikuwa wanawaadhimisha, yaani wanawaonea fahari kama maaskari wa Bwana, waaminifu.
Na mwenendo wenyewe ambao uliwafanya watu wasiweze kufuatana nao, ndio huo wa kutokuogopa vifo, mapigo, mabaraza ya makuhani, mashutumu, na sura za watu.
Ikumbukwe kuwa mitume walipoitwa hawakutumwa kwanza nchi za mbali bali waliagizwa waanzie kwanza pale pale Yerusalemu ambapo palikuwa na ukinzani mkubwa sana kutoka kwa wafalme na viongozi wa kidini,
na cha hatari zaidi mitume walikuwa wanaongozwa kwenda kuhubiri katika hekalu lile lile ambalo, Kristo alipindua meza zao, hata baadaye tena Petro na Yohana walipofungwa, kwasababu ya kuhubiria watu, mule hekaluni..utaona malaika aliwatoa na kuwaaagiza warudi kule kule hekaluni kuhubiri.
Matendo ya Mitume 5:18-21
[18]wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza; [19]lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema, [20]Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu. [21]Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha. Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete.
[18]wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;
[19]lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema,
[20]Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu.
[21]Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha.
Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete.
Unaona, Hata wakati kanisa linapitia dhiki Yerusalemu, na kuwafanya watakatifu wote watawanyike, ni mitume peke yao waliendelea kubaki Yerusalemu.
Matendo ya Mitume 8:1
[1]Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume.
Hivyo kwa utumishi wa namna hiyo wa kuhatarisha maisha, haikuwa vyepesi kwa watu wengi, kuufuata..japokuwa watu walikuwa pamoja nao bega bega, wakifurahia ushujaa wao, wakitamani waendelee kumtumikia Mungu kwa ujasiri, injili ienee.
Jambo kama hilo tunaliona pia katika huduma ya Bwana Yesu..
Biblia inasema wengi wa wakuu wa kidini walimuamini lakini hawakuweza kumkiri kwasababu ya hofu wa watu..
Yohana 12:42
[42]Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.
Watu wengi hawakuweza kuambata na Yesu katika mapito yake lakini aliaminiwa na wengi.
Hii ni kufunua nini kwa watumishi wa Mungu?
Ikiwa umeitwa kama mtumishi wa Mungu..Ni lazima maisha yako yajikite katika utumishi wa Mungu kwelikweli, yaani viwango vyako vya kujikana lazima viwe juu zaidi ya watu wengine..
Ndivyo Mungu atakavyokutumia na ndivyo watu watakavyokuadhimisha kama ilivyokuwa kwa mitume.
Chachu yetu ni lazima izidi ya watu wengine. Bwana atusaidie sana.
Shalom.
THAWABU ZA SIRI, ZA WATAKATIFU MBINGUNI.
SIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, BALI MAFARAKANO.
KWANINI MITUME WAMUULIZE BWANA FARAGHANI?
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?
Ulafi ni nini kibiblia?
Kupatiliza ni neno lenye maana ya “kupiga/kuadhibu ”..mfano badala ya kusema “fulani, kapigwa na Mungu, unaweza kusema fulani kapatilizwa na Mungu”
Lakini swali la kujiuliza ni je!..Mungu huwa anapiga watu (anapatiliza)?
Jibu ni ndio!. Huwa anatoa adhabu, anawapatiliza waovu vile vile na wema endapo wakitoka nje ya mstari.
Lakini siku zote adhabu za Mungu lengo lake ni ili sisi tutubu na si kutukomoa au kutukomesha, kama sisi wanadamu tunavyokomeshana.
Tunapopatwa na majanga tofauti tofauti, ni ili tutubu tuache njia zetu mbaya na tulitafute kusudi la Mungu juu ya maisha yetu. Na pale tunapopata ufahamu na kugeuka kuiacha ile njia mbaya tuliyokuwa tunaiendea basi moja kwa moja, Bwana anaondoa yale mapatilizo na kutupatia mema.
Mfano wa mtu aliyepigwa baada ya kuliacha kusudi la Mungu ni nabii Yona.Yeye alidhani kuacha kuitii sauti ya Mungu ataendelea kuwa salama!…kumbe kinyume chake ndio anazidi kuielekea ile hatari.
Akajikuta amekaa tumboni mwa samaki siku 3, bila kula wala kunywa.
Vile vile Bwana anawapatiliza Waovu hata kizazi cha tatu na cha nne..
Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; NAWAPATILIZA wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao”.
Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; NAWAPATILIZA wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao”.
Umeona?..ukiabudu sanamu, kama babu yako au kama baba yako au bibi yako au mama yako…Bwana atakupatiliza wewe mzao wake kama na wewe utaendelea na kuabudu sanamu kama wao.
Vile vile na wakristo wote waliomwamini Yesu wamepewa mamlaka na nguvu za kuvamia kambi za adui katika ulimwengu wa roho na kupatiliza (kupiga) kila kazi zote za giza, na kuyaacha huru mateka..
Tunaweza kuyasoma hayo katika…
2 Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; 4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) 5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; 6 tena TUKIWA TAYARI KUPATILIZA maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.
2 Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;
4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
6 tena TUKIWA TAYARI KUPATILIZA maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.
Na tunazipiga/patiliza Ngome za Adui kwa KUOMBA, KUHUBIRI na KUSOMA NENO.
Maran atha!.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp group:Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
KWANINI UPIGE MISHALE CHINI?
NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.
Ngome ni nini? Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?
Yapo maombi ya namna tofauti tofauti, lakini yote ni lazima yaangukie katika mojawapo ya makundi haya Matano (5).
Wengi hawafahamu kama sifa zetu ni maombi yanayojitegemea kwa Mungu, haya ni maombi yanayomwasilia Mungu katika mfumo wa nyimbo, halikadhalika pia kwa kumwadhimisha kwa matendo yake makuu aliyoyafanya kwa kuzungumza kwa vinywa vyetu.. ndio maombi ya kwanza yenye nguvu. Tunapomsifu Mungu katika Roho na kweli, ni Zaidi ya maombi mengine yote tunayoweza kuyapeleka kwake.,
Biblia inasema Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu;(1Nyakati 16:29), Na pia Mataifa yote yamsifu yeye. Mambo mengi, na vifungo vingi huwa vinafunguka, pale tu tunapomsifu Mungu kwa kumaanisha katika Roho na kweli, Kwasababu ni maombi yanayouvuta uwepo wa Mungu kwa haraka sana juu ya mtu, Na ndio maana ibada zote lazima zitanguliwe na maombi haya.
Ni maombi ya kuwaombea wengine, Zaidi ya kwako mwenyewe. Kuwaombea watakatifu, kuwaombea, wanyonge, kuliombea taifa, viongozi, hata maadui zako n.k. Haya ni maombi ambayo yanampendeza Mungu sana. Danieli alifunga na kuomba kwa ajili ya taifa lake Israeli, na dhambi zao, Na Mungu akamsikia akamrehemu (Danieli 9:1-27).
Bwana Yesu alipokuwa duniani, sehemu kubwa ya maombi yake ilikuwa ni kutuombea sisi (Yohana 17) hivyo akasema pia, tuombeane sisi kwa sisi ili tupate kuponywa (Yakobo 5:16). Ikiwa na maana wengi hawawezi kuokoka/kufunguliwa wenyewe, ikiwa sisi hatutawaombea, Na pale maombi haya yanapokuwa ya muda mrefu (ya dua), basi huwa yana nguvu Zaidi, kupelekea kutupa kibali cha kupendwa na Mungu, kama ilikuwa kwa Danieli.
Ni maombi ya kupeleka haja zetu kwa Mungu, ikiwemo, kumwomba Roho wake, rizki, amani, furaha, uponyaji, kibali, fursa, gari n.k. Bwana Yesu alisema pia, tuombapo tuombe Bwana atupe rizki zetu,(Mathayo 6:11). Na pia alisema tuombe nasi tutapewa. Haya ndio maombi yanayojulikana na kuombwa na watu wengi sana.
Luka 11:11 “Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka? 12 Au akimwomba yai, atampa nge? 13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”
Luka 11:11 “Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka?
12 Au akimwomba yai, atampa nge?
13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”
Ni maombi muhimu kwa kila mwanadamu, ni maombi ya wakati wote, ya asubuhi, ya mchana, na jioni, tunamshukuru Mungu, kwa uhai, afya, chakula, makazi, Malazi, familia,
Wakolosai 3:15 inasema “….tena iweni watu wa shukrani.”. Ulishawahi kushukuriwa kwa wema Fulani uliomtendea mtu, ukaona hali unayojisikia ndani ya moyo wako kwa shukrani ile..Ndivyo ilivyo kwa Mungu anapoona Sio kila majira tunaenda kumpelekea tu mahitaji yetu..Bali wakati mwingine tunamkaribia kumshukuru kwa vile anavyotufanyia. Inampendeza sana moyo. Na wakati mwingine kupelekea hata kupewa vile vilivyosalia, kwasababu tunaonyesha kuthamini neema yake.
Ni maombi ya kushindana, na nguvu za giza, kwa mamlaka ya rohoni tuliyopewa katika damu ya Yesu, Hapa tunatangaza ushindi, na pia kutamka kwa Imani katika Neno la Mungu. Yapo mambo mengine ibilisi hawezi kuyaachia kirahisi rahisi. Hivyo inahitaji kukemea, kuamuru, kuvunja, na kubomoa, kwa Imani.
Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. 11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.
Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.
11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.
Hivyo kama watakatifu tukijifunza kutumia aina hizi tano za maombi, bila kupuuzia hata moja, basi, tutakuwa ni askari wazuri sana katika roho.
Shalom
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.
Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?
YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.
WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA
LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA.
Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1)
Warumi 5:20 “Lakini sheria iliingia ili kosa lile liwe kubwa sana; NA DHAMBI ILIPOZIDI, NEEMA ILIKUWA NYINGI ZAIDI”.
Ili tuweze kuelewa vizuri labda tujifunze katika mfano mmoja au miwili ya kimaisha.
Umewahi kujiuliza ni kwanini gharama za usafiri wa Umma zipo chini, kuliko zile za usafiri binafsi?. Leo hii ukisafiri kutoka mkoa mmoja hadi mwingine, kwa kutumia basi la umma, utaona gharama zipo chini, kuliko ukitumia usafiri wako binafsi.
Sasa ni kwasababu gani iko hivyo?..Ni kwasababu mnapokuwa wengi mnachangia zile gharama, na hivyo kusababisha nauli kuwa ndogo kwa kila mmoja, lakini ukiwa peke yako itakubidi ubebe wewe gharama zote za usafiri, Maana yake badala ya kutoka Dar es salaam mpaka Dodoma kwa Tsh. Elfu 20, utajikuta unatumia laki 2 kwa safara hiyo hiyo, endapo utatumia usafiri binafsi.
Kwahiyo kwa ufupi tunaweza kusema “wenye uhitaji wa kusafiri wanapokuwa wengi, basi kunakuwa na neema ya punguzo la bei)”.
Au umewahi kujiuliza ni kwanini baadhi ya dawa au chanjo za magonjwa sugu ambayo yanaathiri watu wengi kwa wakati mmoja, kama Kifua kikuu, Ukimwi, au CORONA yanatolewa bure bila malipo?..si kwasababu madawa hayo ni ya gharama za chini, la! Ni ya gharama kubwa sana, lakini kwasababu yana waathiri watu wengi kwa wakati mmoja, nchi inafanya juhudi dawa hizo zipatikane bila malipo, ili hasara isiwe kubwa kwa taifa!..
Hivyo itaingia gharama ya kuyanunua madawa hayo kwa bei ya juu, na kuyagawa bure kwa wananchi!.
lakini laiti kama magonjwa hayo yangekuwa yanawaathiri watu wachache tu!, basi yangepatikana kwa gharama zile zile za juu tu!
Vivyo hivyo katika Imani, dhambi ya mtu mmoja pekee isingetosha kumleta Kristo ulimwenguni.. Kwasababu gharama ya kumwokoa mwanadamu ni kubwa sana si ndogo!. (Mungu kumtoa mwana wake wa pekee si gharama ndogo!). 1Wakorintho 7:23 “Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu”. Soma pia 1Petro 1:18.
Hivyo ilibidi wakosaji tuwe wengi, ili Neema nayo iwe nyingi!!…iweze kupatikana bure!! Hiyo ndiyo sababu kwanini Kristo hakuja ulimwenguni siku ile ile Adamu alipoasi.. Bali alikuja miaka mingi baadaye..
Warumi 5:16 “…….kwa maana hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja ikaleta adhabu; BALI KARAMA YA NEEMA ILIKUJA KWA AJILI YA MAKOSA MENGI, IKALETA KUHESABIWA HAKI”.
Hiyo ndio sababu pia kwanini kanuni ya kuupokea wokovu imerahisishwa namna hii!.. Ni kitendo tu cha KUMWAMINI Bwana YESU, na KUTUBU!, kwa kudhamiria kuacha dhambi, na KUBATIZWA katika ubatizo sahihi, na KUPOKEA ROHO MTAKATIFU. Basi!.. Ukiifuata hiyo kanuni, utakuwa umeupokea Wokovu kamili, na umeipokea Neema ya Mungu katika Maisha yako.
Itii injili leo, inapokuonya juu ya uvaaji wako mbaya, juu ya vimini unavyovaa na wigi unazovaa, juu ya wanja unaoupaka, juu ya lipstick unazotumia, juu ya suruali unazozivaa, juu ya mitindo yote ya kidunia uliyo nayo.. juu ya ulevi wako, na anasa na utukanaji ulionao!. Tubu leo na kuitii injili, kabla ya ule mwisho kufika..
Ukiyadharau maneno ya Mungu ya Uzima yanayokuonya leo, utafika wakati utatamani wokovu utaukosa.. na wakati huo, upo karibu kufika, wakati mlango wa neema utakuwa umefungwa!.. kitakachokuwa kimesalia ni hukumu ya ziwa la Moto!.
Waebrania 10:28 “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu. 29 MWAONAJE? HAIKUMPASA ADHABU ILIYO KUBWA ZAIDI MTU YULE ALIYEMKANYAGA MWANA WA MUNGU, NA KUIHESABU DAMU YA AGANO ALIYOTAKASWA KWAYO KUWA NI KITU OVYO, NA KUMFANYIA JEURI ROHO WA NEEMA?.
Waebrania 10:28 “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.
29 MWAONAJE? HAIKUMPASA ADHABU ILIYO KUBWA ZAIDI MTU YULE ALIYEMKANYAGA MWANA WA MUNGU, NA KUIHESABU DAMU YA AGANO ALIYOTAKASWA KWAYO KUWA NI KITU OVYO, NA KUMFANYIA JEURI ROHO WA NEEMA?.
Kama hujampokea Yesu na kubatizwa na ungehitaji kumpokea leo na kubatizwa, basi tumia namba hizo hapo chini, kuwasiliana nasi ili tukusaidie juu ya hilo, pale mahali ulipo. Au tafuta kwa bidi mahali popote ambapo utaweza kupata msaada huo mapema sana kabla mambo hayajaharibika Zaidi.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
GHARAMA YA UFALME WA MBINGUNI.
BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?
KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
TUNALINDWA NA NGUVU ZA MUNGU.
Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele.AMEN. Nakukaribisha katika kuyatafakari maneno ya Mungu, na leo tutaona vile uaminifu unavyomshawishi Mungu, kukupa neema Zaidi ya unachokiomba.
Tumekuwa na maombi mengi sana mbele za Mungu, wakati mwingine tunatamani Mungu atutumie kama Fulani katika biblia, Lakini tusipojua kanuni za Ki-Mungu, kamwe hatutakaa tuvipate, haijalishi tutakuwa ni waombaji au wafungaji wazuri namna gani mbele za Mungu.
Mungu kumfanya Musa, kuwa Mchungaji wa taifa la Israeli, haikuwa ni kwasababu ni mwisraeli tu au anaomba sana. Hapana, ni kwasababu ya maamuzi aliyoyafanya zamani, ambayo yalimponza hata kuwa vile kama alivyokuwa kwa miaka 40. Musa aliona kustarehe katika jumba la kifalme, si kitu, moyo wake ukaanza kuugua juu ya ndugu zake waebrania aliokuwa anaona wanateswa, hivyo siku moja alipoona mmojawapo anaonewa na Mmisri, alikuwa radhi kumtetea ndugu yake, mpaka kumuua yule mmisri, kuonyesha kuwa aliwapenda waebrania kwelikweli, Hata siku ya pili yake, alipoona hao hao waebrania wanagombana, hakuwaacha hivi hivi tu, bali alikwenda kutafuta namna ya kuwapatanisha ili wawe na umoja. Lakini yule aliyemtapeli mwenzake, akamwambia unataka kuniua kama ulivyomuua yule mmisri jana.
Musa angeweza kukana hayo mashtaka hata kwa rushwa kwasababu alikuwa na uwezo huo.. Lakini kinyume chake, akawa tayari, kukubali mashutumu, kwamba yeye ndiye aliyefanya vile, akakimbia akaenda zake jangwani, huku moyo wake ukiugua tu kwa ajili ya ndugu zake. Utaona japokuwa hakujua njia sahihi ya kuwaokoa ndugu zake, lakini alijitahidi kwa kadiri ya uwezo wake, kufanya awezacho.(Matendo 7:22-40)
Huyo ndio mtu ambaye baada ya miaka 40, Mungu anamtokea katika kijiti cha moto, akimwambia, nakutuma uenda Misri ukawaokoe watu wangu kwa mkono mkuu. Ndipo Mungu akamtumia kwa uwezo mkubwa namna ile, kwasababu aliona uaminifu wake, katika kile alichokitamani.
Matendo 7:35 “Musa huyo waliyemkataa, wakisema, Ni nani aliyekuweka kuwa mkuu na mwamuzi? Ndiye aliyetumwa na Mungu kuwa mkuu na mkombozi, kwa mkono wa yule malaika aliyemtokea katika kile kijiti. 36 Huyo ndiye aliyewatoa, akifanya ajabu na ishara katika nchi ya Misri, na katika bahari ya Shamu, na katika jangwa muda wa miaka arobaini”.
Matendo 7:35 “Musa huyo waliyemkataa, wakisema, Ni nani aliyekuweka kuwa mkuu na mwamuzi? Ndiye aliyetumwa na Mungu kuwa mkuu na mkombozi, kwa mkono wa yule malaika aliyemtokea katika kile kijiti.
36 Huyo ndiye aliyewatoa, akifanya ajabu na ishara katika nchi ya Misri, na katika bahari ya Shamu, na katika jangwa muda wa miaka arobaini”.
Ukitamani kuwa mchungaji, onyesha tabia hizo tangu sasa kabla hujawa mchungaji wa kanisa la Kristo, ili Bwana ashawishwe, kukupa huduma hiyo, je, unalipenda kundi la Mungu, je unalithamini? , je upo tayari kuwalisha watu chakula cha kiroho, na kusimama nao katika shida zao, bila kuruhusu ibilisi awameze?
Hilo ni jambo la muhimu sana, kulifanya sasa ndugu..
Daudi kabla hajafanywa na Mungu kuwa mchungaji wa Israeli, aliwahi kuwa mchungaji wa kondoo na mbuzi, lakini alipoona adui wanataka kuja kulishambulia kundi, hakuliacha na kukimbia, bali aliweza kupambana na simba, Pamoja na dubu na kuwashinda, akiwa na fimbo tu. Mungu akamuona kuwa huyu anafaa hata kwa watu wangu Israeli kwasababu anathamini, kundi analoliongoza, hata kuwa tayari kuyahatarisha Maisha yake, kwa ajili ya hili..(1Samweli 17:34-36)
Umeona, Bwana Yesu alisema..
Luka 16:10 “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia”.
Je ni sisi tuitwao wachungaji/Waalimu, wainjilisti, tunazo tabia hizi?
Wapo watu wengine wanasema, Bwana naomba unipe mali nyingi kama Sulemani, ili nizitumie kuisogeza injili yako mbele. Kumbuka, kabla Mungu hajakupa, atahitaji kwanza, aone ulichonacho unakitoaje? Umebarikiwa laki moja, Je!, ulishawahi kuwa radhi kutoa vyote, au sehemu kubwa ya mali zako kwa Mungu mara nyingi, hata kuwa tayari kulala njaa, au kukosa mahitaji yako, kwa Mungu?
Ikiwa hivyo hufanyi, unaishia tu kuomba, jua kuwa utajiri huo unaouhitaji, kamwe hutaweza kuupata.
Mtume Paulo, alilijua hilo, ndio maana akawa mwaminifu sana katika kumtumikia Mungu, katika udogo, ndipo Mungu akamfanya kuwa mtume na Mwalimu wa mataifa.
1Timotheo 1:12 “Nami namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu kwa sababu aliniona kuwa mwaminifu, akaniweka katika utumishi wake;”
Hivyo ndugu, chochote, ukitamanicho kwa Mungu, waweza kukupata, lakini, anza sasa, kujitoa kwa hicho, kuwa tayari kuiponza roho yako, hata wakati mwingine kupoteza kila kitu, kwa ajili ya utumishi huo, na hakika yake utakipata kwa Mungu.
Uaminifu wako sasa ni mtaji wa ukitakacho kesho.
JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?
THAWABU YA UAMINIFU.
Gongo na Fimbo ni nini?
Unyenyekevu ni nini?
NIFANYE NINI ILI NIPENDWE NA MUNGU?
Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?
Jibu: Tusome,
Isaya 45:3 “nami nitakupa hazina za gizani, na mali zilizofichwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA, nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli”.
Hazina za gizani ni baraka zote zilizoshikiliwa na adui shetani ambazo zingepaswa ziwe zetu.
Hazina hizi zinakuwa zinashikiliwa na adui kwa kitambo tu, na pale tunapotia bidii basi tunaweza kuzitwaa na kuzirejesha kwetu.
Mfano wa hazina za gizani ni zile wana wa Israeli walizozipata kutoka katika jeshi la Washami.
Wakati ule ambao Israeli walikuwa wana njaa kali, hata kufikia hatua watu kula mavi ya njiwa, na kichwa cha punda…na wakati huo huo mji wote ulikuwa umezungukwa na jeshi la Washami pande zote.
na Mungu akayasikilizisha majeshi ya washami mishindo ya farasi, na kwa hofu kubwa wakaacha vyakula vyao vyote na kukimbia kutoka katika zile kambi zao walizokuwepo, na wana wa Israeli wakaenda kuzitwaa zile Nyara na vile vyakula.. Hivyo wakawa wamepewa na Bwana hazina zilizikuwepo gizani.
2 Wafalme 7:5 “Basi wakaondoka kabla ya mapambazuko, ili waende mpaka kituo cha Washami; na walipofika mwanzo wa kimo cha Washami, kumbe! Hapana mtu. 6 Kwa maana Bwana alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari, na kishindo cha farasi, kama kishindo cha jeshi kubwa; wakaambiana, Tazama, mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti, na wafalme wa Wamisri, waje wapigane nasi. 7 Kwa hiyo wakaondoka, wakakimbia kungali giza bado, wakaziacha hema zao, na farasi zao, na punda zao, na kimo chao vile vile kama kilivyokuwa, wakakimbia wapate kujiponya nafsi zao. 8 Basi wale wenye ukoma walipofika mwisho wa kituo, waliingia katika hema moja, wakala, na kunywa, wakachukua fedha, na dhahabu, na mavazi, wakaenda wakavificha; wakarudi, wakaingia katika hema ya pili, vile vile wakachukua vitu, wakaenda, wakavificha. 9 Ndipo wakaambiana, Mambo haya tufanyayo si mema; leo ni siku ya habari njema, na sisi tunanyamaza; mkingoja hata kutakapopambazuka, madhara yatatupata; basi twende tukawaambie watu wa nyumba ya mfalme. 10 Basi wakaenda, wakawaita mabawabu wa mji; wakawaambia, Tulifika kituo cha Washami, na tazama, hapana mtu ye yote huko, wala sauti ya mtu, ila farasi wamefungwa, na punda wamefungwa, na hema zao kama walivyoziacha. 11 Na mabawabu wakaita wakawaambia watu wa nyumba ya mfalme. 12 Mfalme akaondoka usiku, akawaambia watumishi wake, Sasa nitawaonyesha ninyi walivyotutendea Washami. Wanajua ya kuwa tuna njaa; basi wametoka kituoni, ili kujificha kondeni, wakisema Watakapotoka mjini, tutawakamata hai; tena tutapata kuingia mjini. 13 Na mmojawapo wa watumishi wake akajibu, akasema, Kunradhi; baadhi ya watu na watwae farasi watano katika hao waliosalia, waliobaki ndani ya mji (tazama wamekuwa kama mkutano wote wa Israeli waliobaki ndani yake; tazama, wamekuwa kama mkutano wote wa Israeli walioangamia), tukawapeleke tukaone. 14 Basi wakatwaa magari mawili na farasi zake; mfalme akawatuma kuwafuata Washami, akasema, Enendeni, mkaangalie. 15 Wakawafuata mpaka Yordani; na kumbe! Njia yote ilikuwa imejaa mavazi na vyombo, walivyovitupa Washami, wapate kukimbia upesi. Watu wale waliotumwa wakarudi, wakamwambia mfalme. 16 Basi watu wakatoka, wakaziteka nyara hema za Washami. Ikawa kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, sawasawa na neno la BWANA”.
2 Wafalme 7:5 “Basi wakaondoka kabla ya mapambazuko, ili waende mpaka kituo cha Washami; na walipofika mwanzo wa kimo cha Washami, kumbe! Hapana mtu.
6 Kwa maana Bwana alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari, na kishindo cha farasi, kama kishindo cha jeshi kubwa; wakaambiana, Tazama, mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti, na wafalme wa Wamisri, waje wapigane nasi.
7 Kwa hiyo wakaondoka, wakakimbia kungali giza bado, wakaziacha hema zao, na farasi zao, na punda zao, na kimo chao vile vile kama kilivyokuwa, wakakimbia wapate kujiponya nafsi zao.
8 Basi wale wenye ukoma walipofika mwisho wa kituo, waliingia katika hema moja, wakala, na kunywa, wakachukua fedha, na dhahabu, na mavazi, wakaenda wakavificha; wakarudi, wakaingia katika hema ya pili, vile vile wakachukua vitu, wakaenda, wakavificha.
9 Ndipo wakaambiana, Mambo haya tufanyayo si mema; leo ni siku ya habari njema, na sisi tunanyamaza; mkingoja hata kutakapopambazuka, madhara yatatupata; basi twende tukawaambie watu wa nyumba ya mfalme.
10 Basi wakaenda, wakawaita mabawabu wa mji; wakawaambia, Tulifika kituo cha Washami, na tazama, hapana mtu ye yote huko, wala sauti ya mtu, ila farasi wamefungwa, na punda wamefungwa, na hema zao kama walivyoziacha.
11 Na mabawabu wakaita wakawaambia watu wa nyumba ya mfalme.
12 Mfalme akaondoka usiku, akawaambia watumishi wake, Sasa nitawaonyesha ninyi walivyotutendea Washami. Wanajua ya kuwa tuna njaa; basi wametoka kituoni, ili kujificha kondeni, wakisema Watakapotoka mjini, tutawakamata hai; tena tutapata kuingia mjini.
13 Na mmojawapo wa watumishi wake akajibu, akasema, Kunradhi; baadhi ya watu na watwae farasi watano katika hao waliosalia, waliobaki ndani ya mji (tazama wamekuwa kama mkutano wote wa Israeli waliobaki ndani yake; tazama, wamekuwa kama mkutano wote wa Israeli walioangamia), tukawapeleke tukaone.
14 Basi wakatwaa magari mawili na farasi zake; mfalme akawatuma kuwafuata Washami, akasema, Enendeni, mkaangalie.
15 Wakawafuata mpaka Yordani; na kumbe! Njia yote ilikuwa imejaa mavazi na vyombo, walivyovitupa Washami, wapate kukimbia upesi. Watu wale waliotumwa wakarudi, wakamwambia mfalme.
16 Basi watu wakatoka, wakaziteka nyara hema za Washami. Ikawa kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, sawasawa na neno la BWANA”.
Sasa huo ni mfano wa hazina ambazo zilikuwa gizani (yaani zimeshikiliwa na adui), lakini baadaye zikaondolewa kutoka kwa adui na kupewa watu wa Mungu. Na hata sasa zipo hazina nyingi ambazo zipo gizani, ambazo zinapaswa ziwe za kwetu..Adui kazishikilia, na sisi tusipopiga hatua kwenye kuteka nyara basi adui ataendelelea kuzimiliki na sisi tutaendelea kuteseka.
Na hazina zenyewe zinaweza kuwa ni WATU au VITU. Kuna watu wetu wengi leo ambao wameshikwa na adui vile vile kuna vitu vyetu vingi ambavyo vimeshikwa na adui, ambavyo tukiwa imara katika Imani tunaweza kuvitwaa na kuviteka. Maandiko yanasema..
2 Wakorintho 10:4 “maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) 5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKRA IPATE KUMTII KRISTO”.
2 Wakorintho 10:4 “maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKRA IPATE KUMTII KRISTO”.
Maana yake tukivaa silaha hizo za Mungu, basi tutakuwa na uwezo wa kuziteka hazina zote za gizani…kama ni watu wetu wapo gizani, basi tunaweza kuwatoa huko, kama ni vitu vyetu vipo gizani, basi tunaweza kuvirejesha endapo tukivaa silaha hizo na kuingia vitani.
Sasa swali ni je!. Hizo silaha za kwenda kuteka nyara hazina za gizani ni zipi? Si nyingine zaidi ya zile silaha 7 tunazozisoma katika kitabu cha Waefeso 6:10-18, ambazo ni WOKOVU, KWELI, HAKI, IMANI, UTAYARI,NENO, na MAOMBI.
Ni kupitia silaha hizo tu, ndio tunaweza kuzipata hazina za gizani na mali zilizofichwa sawasawa na hiyo Isaya 45:3.
Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi
TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.
Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards),ni sawa?
Kwanini Mungu aseme, Alaaniwe azuiaye upanga wake usimwage damu (Yeremia 48:10).
Deraya ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 59:17
WhatsApp
Kikawaida ulafi ni tabia ya kupenda kula kuliko pitiliza, Sio vibaya kula, na pia sio dhambi kula na kushiba..
Lakini tabia hii inapovuka mipaka kiasi kwamba kila kitu kinachokuja mbele ya macho yetu ni kutamani kukila kama vile wanyama..(huo ni ulafi).
Biblia imetaja tabia hii kuwa haitokani na Roho Mtakatifu Kwasaababu matunda ya tabia hiyo ni mabaya.
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21 husuda, ulevi, ULAFI, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
21 husuda, ulevi, ULAFI, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
Mtu mlafi atatoa chochote ili ale au anywe, hata kama ameshiba, atatafuta kila njia ili aliridhishe tumbo lake kwa chochote atakachokitamani, anaweza hata kuiba, au kudhulumu, au kufanya jambo lolote lisilo la kiMungu ilimradi tu, apate chakula anachokihitaji.
Anaweza kuhudhuria karamu yoyote atakayoalikwa hata kama hiyo karamu ni ya mashetani..lengo lake ni ili ale na kunywa tu!.
Mtu mlafi ni rahisi kuingia katika mtego wowote wa ibilisi, Esau aliuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa chakula,
Waebrania 12:16 “Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya CHAKUKA KIMOJA”.
Hebu tuangalie hekima moja ya Sulemani aliyoiandika kuhusiana na ulafi na madhara yake.
Mithali 23:1 “Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala, Mwangalie sana yeye aliye mbele yako. 2 Tena ujitie kisu kooni, KAMA UKIWA MLAFI. 3 Usivitamani vyakula vyake vya anasa; Kwa maana ni vyakula vya hila…… 6 Usile mkate wa mtu mwenye husuda; Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa; 7 Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. ATAKUAMBIA HAYA, KULA, KUNYWA; LAKINI MOYO WAKE HAUWI PAMOJA NAWE. 8 Tonge lile ulilokula utalitapika, Na maneno yako matamu yatakupotea.”
Mithali 23:1 “Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala, Mwangalie sana yeye aliye mbele yako.
2 Tena ujitie kisu kooni, KAMA UKIWA MLAFI.
3 Usivitamani vyakula vyake vya anasa; Kwa maana ni vyakula vya hila……
6 Usile mkate wa mtu mwenye husuda; Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;
7 Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. ATAKUAMBIA HAYA, KULA, KUNYWA; LAKINI MOYO WAKE HAUWI PAMOJA NAWE.
8 Tonge lile ulilokula utalitapika, Na maneno yako matamu yatakupotea.”
Umeona?..wanawake wengi na mabinti wanaingia katika mtego wa dhambi ya uasherati kutokana na ulafi (wanatamani kila aina ya chakula wanachokiona), na shetani anakitumia hicho kuwakamata.
Wengine wanaingia katika mitego ya kula rushwa kwasababu ya Ulafi, wengine wanaingia katika mitego ya kuua, au kudhulumu kwasababu ya Ulafi.
Na hata wengine wanaingia katika umaskini kwasababu ya ulafi (biblia inasema hivyo katika Mithali 23:20-21), Kwasababu muda wote mtu huyo anakuwa anafikiria kula tu, na hafikiri vitu vingine.
Na mojawapo ya dalili za siku za mwisho, biblia imetabiri ni watu kuwa WALAFI (watu watakuwa wakila na kunywa).
Luka 17:26 “Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu. 27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote”.
Luka 17:26 “Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.
27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote”.
Hivyo hatuna budi kuwa na kiasi na kujihadhari na ulafi.
Luka 21:34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ULAFI, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo; 35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima.
Luka 21:34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ULAFI, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;
35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima.
Na pia tabia ya ULAFI, siku zote inaenda kinyume na MFUNGO.
Mtu aliye mlafi, huwa hapendi wala hawezi kufunga na hivyo anakuwa pia anakosa baraka nyingi za kiroho kwasababu maandiko yanasema “mambo mengine hayatoki isipokuwa kwa kufunga na kuomba(Mathayo 17:21)”.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba tunapookoka hatuna budi kuacha na ULAFI pia!, Kwasababu tabia hiyo haitokani na Roho Mtakatifu.
1 Petro 4:3 “Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na KARAMU ZA ULAFI, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali.
Bwana atubariki.
Je! Mbinguni Kutakuwa na kula na kunywa?.
Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?
Katika Mathayo 15:21-28, Yesu alikuwa na maana gani alipomwambia huyu Mama kwamba chakula cha watoto hawapewi mbwa?
CHAKULA CHA ROHONI.
SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya huu mstari,
Mithali 16:2 “Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe; Bali Bwana huzipima roho za watu”.
JIBU: Kama vile Biblia inavyosema moyo huwa mdanganyifu kuliko kitu kingine chochote, (Yeremia 17:9), ikiwa na maana ni kawaida ya mwanadamu, kuziona njia zake zote alizozichagua ni sawa mbele zake, ni mara chache sana, kusikia mtu anakiri kuwa uamuzi anaoufanya ni wa kishetani,
Nimekutana na waganga wa kienyeji wanasema kitu tunachokifanya ni sawa, hakina madhara yoyote, ukienda kwa waabudu sanamu, watakuambia vivyo hivyo hizi ni ishara tu, tunaabudu Mungu yuleyule, Ukienda kwa wauza pombe watakuambia nao maneno hayo hayo n.k… Kwasababu biblia inasema njia “ZOTE” (sio moja) za mtu ni safi machoni pake mwenyewe.
Lakini Bwana huzipima roho za watu. Ikiwa na maana, Mungu anazichunguza nia zetu. Yeye hashawishwi na kile tunachokiona ni sawa, kwa macho yetu, au kwa mitazamo yetu, bali anatazama ndani Zaidi ya mwanadamu, anaweka kwenye mizani, anatazama nia, ya mtu ilikuwa ni nini, na matokeo yake yatakuwa ni nini mwishoni..
Kwamfano Mafarisayo na Masadukayo, walijihesabia haki, kwa mapokeo yao, wakijiona kuwa ni watakatifu, na bora kuliko wengine, lakini Bwana Yesu aliwaita wanafki. Kwasababu, kazi yao ilikuwa ni kusafisha kikombe kwa nje tu, lakini ndani ni kuchafu, wanafunga ili waonekane na watu, wanaomba ili waonekane ni wazuri katika mambo hayo. Walikuwa wanajifanya kumwita Yesu Rabi, lakini ndani wamejaa wivu. (Mathayo 23:1-39)
Hivyo nasi twapasa tulijue hilo, ili tusidanganyike.
Kitabu cha 1Wakorintho 13, inasema nijaposema kwa lugha za wanadamu na Malaika, nijapoutoa mwili wangu uungue moto, nijapotoa mali zangu zote niwape maskini, nijapokuwa na unabii, na Imani timilifu ya kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo mimi si kitu, ni sawa na bure tu.
Waweza kuwa mhubiri mzuri, mkubwa, unaokoa roho za watu, nawe ukaona njia hiyo ndiyo inayompendeza Mungu zaidi, lakini ndani yako unahubiri kwasababu ya fitina, kama inavyosema Wafilipi 1:15, au upate umaarufu, au upate fedha,.ujue unachokifanya ni bure.
Hivyo, katika lolote tulifanyalo, ili liwe na faida njema nyuma yake, lazima tujue nia yetu ya dhati kufanya hivyo ni nini, Ndicho Bwana anachokitazama sana, kuliko, hichi cha nje tukionyeshacho.
Kulikuwapo na wale watu, waliokataa, kwenda harusini walipoalikwa, na ukitazama kibinadamu sababu za wao kutokwenda zina mashiko kabisa, mwingine anasema ninaoa, hivyo ni sharti niwe na mke wangu kwa kipindi hiki, lakini Bwana Yesu aliona kama ni UDHURU wanatoa wote, kwasababu yeye ndio anayechunguza mioyo, akaona kutoa kwao udhuru ni kwasababu hawakuthamini wito wake tangu mwanzo.
Luka 14:16 “Akamwambia, Mtu mmoja alifanya karamu kubwa akaalika watu wengi, 17 akamtuma mtumwa wake saa ya chakula awaambie wale walioalikwa, Njoni, kwa kuwa vitu vyote vimekwisha kuwekwa tayari. 18 Wakaanza wote kutoa udhuru kwa nia moja. Wa kwanza alimwambia, Nimenunua shamba, sharti niende nikalitazame; tafadhali unisamehe. 19 Mwingine akasema, Nimenunua ng’ombe jozi tano, ninakwenda kuwajaribu; tafadhali unisamehe. 20 Mwingine akasema, Nimeoa mke, na kwa sababu hiyo siwezi kuja. 21 Yule mtumwa akaenda, akampa bwana wake habari ya mambo hayo. Basi, yule mwenye nyumba akakasirika, akamwambia mtumwa wake, Toka upesi, uende katika njia kuu na vichochoro vya mji, ukawalete hapa maskini, na vilema, na vipofu, na viwete. 22 Mtumwa akasema, Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa ingaliko nafasi. 23 Bwana akamwambia mtumwa, Toka nje uende barabarani na mipakani, ukawashurutishe kuingia ndani, nyumba yangu ipate kujaa. 24 Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.
Luka 14:16 “Akamwambia, Mtu mmoja alifanya karamu kubwa akaalika watu wengi,
17 akamtuma mtumwa wake saa ya chakula awaambie wale walioalikwa, Njoni, kwa kuwa vitu vyote vimekwisha kuwekwa tayari.
18 Wakaanza wote kutoa udhuru kwa nia moja. Wa kwanza alimwambia, Nimenunua shamba, sharti niende nikalitazame; tafadhali unisamehe.
19 Mwingine akasema, Nimenunua ng’ombe jozi tano, ninakwenda kuwajaribu; tafadhali unisamehe.
20 Mwingine akasema, Nimeoa mke, na kwa sababu hiyo siwezi kuja.
21 Yule mtumwa akaenda, akampa bwana wake habari ya mambo hayo. Basi, yule mwenye nyumba akakasirika, akamwambia mtumwa wake, Toka upesi, uende katika njia kuu na vichochoro vya mji, ukawalete hapa maskini, na vilema, na vipofu, na viwete.
22 Mtumwa akasema, Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa ingaliko nafasi.
23 Bwana akamwambia mtumwa, Toka nje uende barabarani na mipakani, ukawashurutishe kuingia ndani, nyumba yangu ipate kujaa.
24 Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.
Hivyo na sisi tusitoe udhuru katika mambo ya ki-Mungu, unapoitwa uokoke, hata kama unazo sababu elfu za kutokuacha hicho unachokifanya ikiwa Mungu anataka ukiache, tii tu. Kwasababu hatuwezi kumshawishi Mungu kwa mitazamo yetu tu, kwa vile tuonavyo sisi kuwa ni bora, au vafaa Zaidi kwasasa, naye akashawishika, bali anaelewa kila kitu, na matokeo ya vyote mwishoni utakuwaje..
Hatuna budi, kumtii Mungu.
Bwana akubariki.
UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?
Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?
KUWA MWAMINIFU KWA MANENO YAKO MWENYEWE,
AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE ALIYE JUU.
NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.
VIACHENI VYOTE VIKUE HATA WAKATI WA MAVUNO.
MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?