Biblia inatuambia kuwa ilikuwa ni desturi ya Bwana Yesu kuingia hekaluni siku za sabato..Je! hiyo haimaanishi kuwa ni lazima na sisi tuishike sabato? (Luka 4:16)?.
Jibu: Tusome
Luka 4:16 “Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; NA SIKU YA SABATO AKAINGIA KATIKA SINAGOGI KAMA ILIVYOKUWA DESTURI YAKE, AKASIMAMA ILI ASOME”.
Bwana Yesu kuingia siku ya sabato katika masinagogi haimaanishi kuwa na yeye alikuwa anaiadhimisha au kuiabudu siku hiyo, kama walivyokuwa wanafanya wayahudi..La!.. yeye ndiye aliyekuwa Bwana wa Sabato (Luka 6:5).. hivyo kamwe hakuwahi kuitumikia au kuiadhimisha sabato kama walivyokuwa wanafanya wayahudi.
Sasa kama ni hivyo, ni kwanini biblia iseme ilikuwa ni DESTURI YAKE kwenda hekaluni kila sabato?
Ni kwasababu siku ya sabato ndio siku ambayo wayahudi wengi walikuwa wanakusanyika hekaluni kusikiliza maneno ya Mungu, siku nyingine walikuwa wanafanya kazi…hivyo ili Bwana awapate ilikuwa hana budi awafuate hekaluni katika siku hiyo hiyo ambayo wao wanaiheshimu, lakini endapo wangekuwa wana siku nyingine ya kukusanyika hekaluni tofauti na hiyo sabato, basi ingekuwa ni desturi ya Bwana kuwafuata katika hiyo siku.
Ni sawa na mtu atenge siku moja ya jumamosi au jumapili, na kuifanya kuwa desturi yake kwenda kufanya UINJILISTI WA NYUMBA KWA NYUMBA!!.. Sasa kwa kuitenga hiyo siku haimaanishi kuwa anaiadhimisha hiyo siku.. bali anaitumia hiyo siku kufanya uinjilisti wa nyumba kwa nyumba kwasababu katika siku hizo watu wengi wanakuwa manyumbani, hivyo ni siku nzuri za kufanya uinjilisti, tofauti na siku nyingine za katikati ya wiki ambazo watu wengi wanakuwa katika shughuli zao, na si manyumbani.
Na Bwana Yesu, na mitume wengine wote walizitumia siku za Sabato kuingia katika masinagogi kuhubiri, si kwasababu wanaziadhimisha siku hizo, bali kwasababu katika siku hizo ndizo watu wengi wanakuwa wanapatikana katika majengo ya ibada.
Sasa swali lingine hili; Sabato halisi ni ipi? na ni siku gani tupasayo kuabudu? Ili kufahamu kwa urefu fungua hapa >> Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.
Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.
Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!
BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?
Rudi nyumbani
Print this post
Swali: Katika Mathayo 5:14 biblia inasema kuwa “Nuru yetu na iangaze mbele za Watu”, halafu tukienda kwenye Mathayo 6:1 maandiko yanasema “tusifanye wema wetu machoni pa watu”, hapa nahitaji ufafanuzi.
Mathayo 5:14 “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. 15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. 16 VIVYO HIVYO NURU YENU NA IANGAZE MBELE YA WATU, WAPATE KUYAONA MATENDO YENU MEMA, WAMTUKUZE BABA YENU ALIYE MBINGUNI”.
Mathayo 5:14 “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.
15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.
16 VIVYO HIVYO NURU YENU NA IANGAZE MBELE YA WATU, WAPATE KUYAONA MATENDO YENU MEMA, WAMTUKUZE BABA YENU ALIYE MBINGUNI”.
Tusome pia Mathayo 6:1-2..
Mathayo 6:1 “Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, KUSUDI MTAZAMWE NA WAO; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni. 2 Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ILI WATUKUZWE NA WATU”
Mathayo 6:1 “Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, KUSUDI MTAZAMWE NA WAO; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.
2 Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ILI WATUKUZWE NA WATU”
Mistari hiyo miwili haijichanganyi, isipokuwa fahamu zetu ndizo zinazojichanganya.
Bwana Yesu aliposema Nuru yetu na iangaze mbele za watu.. ni ili Mungu atukuzwe kupitia matendo yetu mema tunayoyafanya!… Lakini tukifanya jambo lolote ambalo halitamrudishia Mungu utukufu bali litatupa sisi utukufu, huo sio wema Bwana Yesu alioumaanisha kuwa tuungaze..Ndio maana hapo kwenye Mathayo 5:16 anamalizia kwa kusema.. “wapate kuyaona matendo yenu mema, WAMTUKUZE BABA YENU ALIYE MBINGUNI.”..Na sio watutukuze sisi!!!.
Lakini tunapofanya Wema huku lengo letu ni watu watupe sisi utukufu, au watusifu, au watuone ni mashuhuri, huo sio wema bali ni Ubaya uliovaa vazi la wema ndani yake.. ndio maana katika huo mstari wa 2, Bwana anaweka msisitizo kwa kusema…
Mathayo 6:2 “Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ILI WATUKUZWE NA WATU”.
Umeona hapo lengo la wao kufanya mema yote hayo ni ili watukuzwe na watu, na si Mungu atukuzwe kupitia wao!..Hivyo hiyo ni dhambi!..
Jambo lolote tulifanyalo lisilomrudishia Mungu utukufu hata kama liwe jema kiasi gani, mbele za Mungu ni dhambi!.
Wakati Fulani Mfalme Herode aliwafanyia Wema watu wa Tiro kwa kuwasamehe na kuwapatia riziki, na akaandaa hotuba ambayo iliwafurahisha sana watu wa Tiro, hata kufikia hatua watu hao kumtukuza kwa kusema “Sauti yake ni sauti ya Mungu na si mwanadamu!”..
Na utaona baada ya pale, Mungu alimpiga Herode kwa Chango, kwasababu hakumpa Mungu utukufu, bali alijitukuza yeye!..(Habari hiyo unaweza kuisoma katika kitabu cha Matendo 12:20-24).
Kwahiyo na sisi hatuna budi kuzipima dhamira zetu katika wema wote tunaoufanya.. Je! Lengo letu ni kumpa Mungu utukufu, au kujitukuza sisi. Kama wema tunaoufanya ni kwa lengo la Mungu kutukuzwa basi huo tuufanye kwa bidii sana kwasababu mwisho wake ni Mungu kutukuzwa, lakini kama lengo ni sisi kutukuzwa, basi tujihadhari na huo.
NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.
LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.
NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.
Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?
IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.
Jibu: Tusome,
Luka 12:49 “Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi? 50 LAKINI NINA UBATIZO UNIPASAO KUBATIZIWA, nami nina dhiki kama nini hata utimizwe!”
Luka 12:49 “Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi?
50 LAKINI NINA UBATIZO UNIPASAO KUBATIZIWA, nami nina dhiki kama nini hata utimizwe!”
Ubatizo Bwana Yesu aliokuwa anaumaanisha hapo, ni kile kitendo cha KUZIKWA na KUFUFUKA kwake. Kwasababu maana yenyewe ya Neno ubatizo ni KUZIKWA.
Hivyo kwa kupitia mauti ya Bwana Yesu, Deni la dhambi zetu limefutwa/LIMEZIKWA. Na kama vile alivyofufuka katika upya na utukufu, pasipo mzigo wa dhambi zetu, vile vile na sisi tunapomwamini yeye na kubatizwa kwa njia ya maji, kama ishara ya kuakisi ubatizo wake yeye (wa kuzikwa na kufufuka kwake) tunakuwa tunakufa kwa habari ya dhambi na tunafufuka katika upya.
Wakolosai 2:12 “MKAZIKWA PAMOJA NAYE KATIKA UBATIZO; NA KATIKA HUO MKAFUFULIWA PAMOJA NAYE, KWA KUZIAMINI NGUVU ZA MUNGU ALIYEMFUFUA KATIKA WAFU. 13 Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote”.
Wakolosai 2:12 “MKAZIKWA PAMOJA NAYE KATIKA UBATIZO; NA KATIKA HUO MKAFUFULIWA PAMOJA NAYE, KWA KUZIAMINI NGUVU ZA MUNGU ALIYEMFUFUA KATIKA WAFU.
13 Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote”.
Kwahiyo ubatizo wa Maji ni kivuli cha Ubatizo wa Bwana Yesu, (wa kuzikwa kwake na kufufuka kwake). Kama vile Bwana alivyozikwa katika makosa yetu na kufufuka pasipo makosa yetu, na sisi tunapozama katika maji na kuibuka juu… katika ulimwengu wa roho, tunakuwa tumekufa katika utu wa kale na tumefufuka katika utu upya. (Dhambi zetu zinakuwa zimeondolewa, Matendo 2:38).
Tunakuwa tunatembea katika utukufu ule ule ambao Bwana Yesu alitembea nao baada ya kufufuka kwake.. Na katika ulimwengu wa roho tunakuwa tumeketi naye..
Waefeso 2:5 “hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema. 6 AKATUFUFUA PAMOJA NAYE, AKATUKETISHA PAMOJA NAYE KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, katika Kristo Yesu”
Waefeso 2:5 “hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.
6 AKATUFUFUA PAMOJA NAYE, AKATUKETISHA PAMOJA NAYE KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, katika Kristo Yesu”
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Ubatizo Bwana alioumaanisha katika Luka 12:50 ni KUZIKWA na KUFUFUKA KWAKE. Na kabla ya huo kutimizwa ilipasa Bwana apitie mateso mengi (dhiki), kwa kukataliawa na kuteswa Kalvari, ndio maana anamalizia kwa kusema “nami nina dhiki kama nini hata utimizwe!”
Luka 9:22 “akisema, Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi, na kukataliwa na wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa NA SIKU YA TATU KUFUFUKA”.
Kufuatia maandiko hayo utaona ni jinsi gani ubatizo wa maji ulivyokuwa wa muhimu, na wala si wa kuupuuzia hata kidogo, Na maandiko yanasema mtu asipozaliwa kwa Maji na kwa Roho, (Yohana 3:5) hawezi kuurithi uzima wa milele. (na Kuzaliwa kwa maji ni ubatizo wa Maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo).
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?
Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?
Jina la Bwana Yesu libarikiwe, karibu tujifunze tena maneno ya Uzima ya Bwana wetu, Yesu Kristo. Neno la Mungu ni taa inayoongoza miguu yetu, na Mwanga wa njia zetu! (Zab. 119:105).
Ipo hali Fulani ambayo, Watoto wa kiume wengi wanakuwa na mapenzi mengi kwa mama zao, na kinyume chake asilimia kubwa ya Watoto wa kike wanakuwa na mapenzi Zaidi kwa baba zao kuliko mama zao. Ingawa si wakati wote au kwa Watoto wote inakuwa hivi, lakini asilimia kubwa inatokea kuwa hivyo.
Na biblia pia utaona imetaja au kuonyesha kuwepo kwa aina hii ya mahusiano kati ya wazazi na Watoto wa jinsia tofauti.
Hebu tusome visa kadhaa vya baadhi ya wafalme wa kwenye biblia, kisha kisha tuendelee mbele.
Yeremia 52:1 “SEDEKIA alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja hapo alipoanza kumiliki; naye akamiliki miaka kumi na mmoja huko Yerusalemu; NA JINA LA MAMA YAKE ALIITWA HAMUTALI, BINTI YEREMIA WA LIBNA. 2 NAYE ALITENDA YALIYO MABAYA MACHONI PA BWANA, sawasawa na yote aliyoyatenda Yehoyakimu. 3 Maana, kwa sababu ya hasira ya Bwana, mambo haya yalitokea katika Yerusalemu na katika Yuda, hata akawaondosha wasiwe mbele za uso wake, naye Sedekia akamwasi mfalme wa Babeli.
Yeremia 52:1 “SEDEKIA alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja hapo alipoanza kumiliki; naye akamiliki miaka kumi na mmoja huko Yerusalemu; NA JINA LA MAMA YAKE ALIITWA HAMUTALI, BINTI YEREMIA WA LIBNA.
2 NAYE ALITENDA YALIYO MABAYA MACHONI PA BWANA, sawasawa na yote aliyoyatenda Yehoyakimu.
3 Maana, kwa sababu ya hasira ya Bwana, mambo haya yalitokea katika Yerusalemu na katika Yuda, hata akawaondosha wasiwe mbele za uso wake, naye Sedekia akamwasi mfalme wa Babeli.
Hapa tunaona Mama wa Sedekia anatajwa kama sababu ya Ubaya wa Mfalme Sedekia… Sasa sio huyo tu!
1Wafalme 14:21 “Rehoboamu akaanza kutawala alipokuwa mwenye miaka arobaini na mmoja, akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji aliouchagua Bwana miongoni mwa kabila zote za Israeli, ili aliweke jina lake huko. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA NAAMA, MWAMONI. 22 BASI YUDA WAKAFANYA MAOVU MACHONI PA BWANA; WAKAMTIA WIVU, KWA MAKOSA YAO WALIYOYAKOSA, KULIKO YOTE WALIYOYAFANYA BABA ZAO.
1Wafalme 14:21 “Rehoboamu akaanza kutawala alipokuwa mwenye miaka arobaini na mmoja, akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji aliouchagua Bwana miongoni mwa kabila zote za Israeli, ili aliweke jina lake huko. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA NAAMA, MWAMONI.
22 BASI YUDA WAKAFANYA MAOVU MACHONI PA BWANA; WAKAMTIA WIVU, KWA MAKOSA YAO WALIYOYAKOSA, KULIKO YOTE WALIYOYAFANYA BABA ZAO.
Ijapokuwa Rehoboamu alikuwa ni mwana wa Sulemani, na mjukuu wa Daudi, lakini mama yake anatajwa kumfanya awe mbaya…(sasa sio huyo peke yake..)
1Wafalme 15:1 “Mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya alianza kutawala juu ya Yuda. 2 Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; NA JINA LA MAMAYE ALIITWA MAAKA, BINTI ABSALOMU. 3 AKAZIENDEA DHAMBI ZOTE ZA BABAYE, ALIZOZIFANYA KABLA YAKE; wala moyo wake haukuwa mkamilifu na Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi babaye”.
1Wafalme 15:1 “Mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya alianza kutawala juu ya Yuda.
2 Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; NA JINA LA MAMAYE ALIITWA MAAKA, BINTI ABSALOMU.
3 AKAZIENDEA DHAMBI ZOTE ZA BABAYE, ALIZOZIFANYA KABLA YAKE; wala moyo wake haukuwa mkamilifu na Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi babaye”.
Si huyu peke yake…
1Wafalme 8:26 “Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala; akatawala mwaka mmoja huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA ATHALIA BINTI OMRI MFALME WA ISRAELI. 27 Akaiendea njia ya nyumba ya Ahabu, AKAFANYA YALIYO MABAYA MACHONI PA BWANA, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa alikuwa mkwe wa jamaa ya Ahabu”.
1Wafalme 8:26 “Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala; akatawala mwaka mmoja huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA ATHALIA BINTI OMRI MFALME WA ISRAELI.
27 Akaiendea njia ya nyumba ya Ahabu, AKAFANYA YALIYO MABAYA MACHONI PA BWANA, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa alikuwa mkwe wa jamaa ya Ahabu”.
Sio hawa tu…Unaweza kusoma pia habari za Mfalme Yothamu (2Wafalme 15:33), na Mfalme Manase (2Wafalme 21:1-2) na wengine wengi katika biblia, ambao utaona Uovu wao umesababishwa na mama zao.
Vile vile walikuwepo watu wa kawaida ambao hawakuwa wafalme, ambao pia tabia zao ziliathiriwa na mama zao, mfano wa hao ni yule kijana wa mwanamke wa kiisraeli, ambaye Habari zake tunazisoma katika Walawi 24:10-14, kijana huyu alimtukana Mungu, na akapigwa mawe mpaka kufa, na wengine wengi.
Lakini pia walikuwepo wafalme ambao walifanya mazuri, na Uzuri wao huo, Pamoja na sifa zao mbele za Bwana zilisababishwa na Mama zao..
1Wafalme 22:42 “Yehoshafati alikuwa mwenye miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na mitano huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA AZUBA BINTI SHILHI. 43 AKAIENDEA NJIA YOTE YA ASA BABAYE; WALA HAKUGEUKA, AKIFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA…..”.
1Wafalme 22:42 “Yehoshafati alikuwa mwenye miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na mitano huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA AZUBA BINTI SHILHI.
43 AKAIENDEA NJIA YOTE YA ASA BABAYE; WALA HAKUGEUKA, AKIFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA…..”.
1Wafalme 14:2 “Naye alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; NA JINA LA MAMAYE ALIITWA YEHOADANI WA YERUSALEMU. 3 AKAFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA, ila si kama babaye Daudi; akafanya kama yote aliyoyafanya baba yake Yoashi”.
1Wafalme 14:2 “Naye alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; NA JINA LA MAMAYE ALIITWA YEHOADANI WA YERUSALEMU.
3 AKAFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA, ila si kama babaye Daudi; akafanya kama yote aliyoyafanya baba yake Yoashi”.
1Wafalme 15:2 “Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala miaka hamsini na miwili huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA YEKOLIA WA YERUSALEMU. 3 AKAFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA, kama yote aliyoyafanya babaye Amazia”.
1Wafalme 15:2 “Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala miaka hamsini na miwili huko Yerusalemu. NA JINA LA MAMAYE ALIITWA YEKOLIA WA YERUSALEMU.
3 AKAFANYA YALIYO MEMA MACHONI PA BWANA, kama yote aliyoyafanya babaye Amazia”.
Sasa katika maandiko hayo yote, unaweza kujiuliza ni kwanini ni waMama, wanahusishwa na si waBaba?.. Ni kwasababu kuna muunganiko wa kipekee kati ya Mama na mtoto wake wa kiume, ambapo Mama asipoutumia vizuri huo muunganiko, anaweza kujikuta anaharibu hatima ya mtoto wake wa kiume moja kwa moja. (Ni vizuri kulijua hili mapema, ili mambo yatakapoharibika huko mbeleni, usije ukasema ulikuwa hujui!!)
Mama unapokuwa mtu wa kidunia, unakuwa mtu wa kumkataa Mungu, fahamu kuwa na mtoto wako wa kiume ni rahisi sana, kuamini hiyo njia yako kuwa ni njia sahihi, kuliko hata mtoto wako wa kike.
Lakini mtoto wako wa kiume anapokuona wewe ni mtu unayemcha Mungu, ni mtu unayeutafuta sana uso wa Mungu, na kuukataa ubaya, ni rahisi sana, mwanao wa kiume, na yeye kuwa kama wewe, hiyo ni (Siku zote weka hilo akilini).
Wafalme wote waliofanya machukizo kwa Bwana, waliharibiwa na Mama zao. Vile vile wafalme wote waliofanya Mema mbele za Bwana, na hata kusifiwa ni kutokana na Mama zao. Hakuna mahali popote wababa wametajwa, katika kutenengeneza hatima za Watoto wao wa kiume.
Hivyo kama Mama, Jifunze kuwapeleka Watoto wako Kanisani, ukiwapeleka wewe Zaidi ya baba hawawezi kuiacha hiyo njia, hata kama watakuja kuyumba kidogo, lakini watairudia tu njia hiyo siku moja!..
Vile vile wafundishe kusoma Neno, na kushika vifungu vya biblia, na kuomba.. Ukifanya hayo kwa Watoto wako wewe kama Mama, ni rahisi mambo hayo kuwaingia Zaidi kuliko kama angefanya Baba.
Halikadhalika msifie mwanao katika mambo ya ki-Mungu na mema, zaidi ya mambo ya ulimwengu huu tu…sauti yako ina thamani kubwa zaidi kwake kuliko baba yake, angefanya hivyo.
Na vile vile wewe Mtoto wa kiume, jifunze kumsikiliza Mama yako, anayekufundisha njia za Mungu, na kukuelekeza njia sahihi.. Kwasababu usipomsikiliza huyo, hakuna mwingine utakayekuja kumsikiliza tena katika Maisha yako.
Ipo methali ya watu wa ulimwengu isemayo “ASIYEFUNZWA NA MAMAYE, HUFUNZWA NA ULIMWENGU”. Ni watu wa kidunia wameitunga methali hii kufuatia uhalisia waliouona, kuwa kwa Mama kunayo mafunzo makuu, Zaidi ya kwa baba.
Hivyo Wewe kama Mama mtengeneze mwanao katika njia ya haki Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”., ..na wewe kama mtoto wa kiume, msikilize Mama yako.
MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)
MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 2)
Je suruali ni vazi la kiume tu?
Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?
VIJANA NA MAHUSIANO.
TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!
SWALI: Biblia inamaana gani kusema “ maana vitu vyote ni watumishi wako”?. Je wanaotumia vifaa vya upako kama vile chumvi, maji, udongo, kuombea watu, wanatimiza kusudi lile lile la Mungu kwasababu na vyenyewe vinafanya kazi ya Mungu kwa nafasi hiyo? Je kwa mujibu wa andiko hilo ni sawa?
Zaburi 119:90 “Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa. 91 Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, MAANA VITU VYOTE NI WATUMISHI WAKO”.
Zaburi 119:90 “Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa.
91 Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, MAANA VITU VYOTE NI WATUMISHI WAKO”.
JIBU: Ni kweli kama andiko hilo linavyosema, vitu vyote tunavyoviona katika mbingu na katika nchi ni watumishi wa Mungu, yaani, jua, mwezi, nyota, mawingu, milima, moto, maji, upepo, mafuta, udongo, mende, mbu, nzi, konokono, kipepeo vyote vinamtumikia Mungu.
Lakini swali ambalo tunapaswa tujiulize je vinamtumkia Mungu katika utumishi gani?
Ulishawahi kwenda kumuomba mjusi akusaidie kuomba rehema mbele za Mungu? Ulishawahi kuliomba jua likupe ridhki, ulishawahi kuamka asubuhi na kuuambia mwezi ukuponye magonjwa yako, na ukuepushe na ajali?
Kwanini usifanye hivyo, ilihali vyote vinamtumikia Mungu?.. Lazima ufahamu utumishi wao ni upi mbele za Mungu, kwa mfano, biblia inasema..
Zaburi 19:1 “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake”.
Ikiwa na maana kuwa tutazamapo mbingu na anga, basi tunahubiriwa utukufu wa Mungu kwa kupitia hivyo, hapo tayari vimeshamtumikia Mungu, lakini hatuwezi kwenda kutumia mawingu ili Bwana atujibu maombi yetu.
Mungu kaweka njia kwa kila jambo, Na njia pekee ambayo alituchagulia sisi ili tumfikie Mungu, na kupokea wokovu wetu, na baraka zetu ni kwa kupitia YESU KRISTO tu na JINA LAKE Hapo ndipo tunapoweza kusaidiwa mahitaji yetu, na dua zetu. Kwasababu hatuna jina lingine au kitu kingine chochote kiwezacho kutuokoa sisi isipokuwa Jina lake tu. . (Matendo 4:12)
Sasa wapo watu wanasema, mbona, Yesu alitumia udongo, mbona manabii walitumia chumvi,..Wanashindwa kuelewa yapo MAINGILIO YA MUNGU. Ambapo Mungu mwenyewe upo wakati anashuka mahali Fulani kwa muda , kulitimiza kusudi lake Fulani, ndipo anapotumia chochote apendacho, kisha baada ya hapo hakuna kitu kingine cha ziada katika hicho kitu.
Ndio maana utaona wakati ule alipomtumia punda kuzungumza na Balaamu, hatuona tena, punda wakitumika kuzungumza na watu, kana kwamba ndio kanuni, hali kadhalika, Elisha alipoambiwa alale juu ya yule kijana kisha atakuwa mzima, hatuona tena, tendo hilo likifanyika hadi leo hii, tukilala juu ya wagonjwa ili wapate afya.
Ipo hatari kubwa sana ya kutumia vitu vya Mungu na kuvigeuza kuwa ndio kanuni za uponyaji, kosa mojawapo lililowafanya wana wa Israeli Mungu achukizwe nao, hadi kupelekwa tena utumwani Babeli, lilikuwa ni kuitumia ile sanamu ya shaba, Musa aliyoagizwa na Mungu aitengeneze kule nyikani, watu waiangaliapo wapone.
Hivyo watu wasiomjua Mungu, na MAINGILIO YAKE YA MUDA, wakaigeuza kuwa ndio sehemu ya ibada, walipofika nchi ya ahadi wakaiundia madhabahu kisha wakaanza kumwomba Mungu kupitia ile, mwisho wa siku wakawa wanaabudu mapepo pasipo wao kujijua na matokeo yake wakapelekwa Babeli utumwani.
Hivyo nawe pia ukiona mahali popote uendapo, vitu kama hivyo vimefanywa kama kanuni, kila wiki ni maji ya upako, mafuta, chumvi, au kingine chochote, ujue kuwa huna tofauti na wale waabudu sanamu, na jua na mwezi, na unayemwabudu hapo sio Mungu bali ni shetani mwenyewe. Na Unamkasirisha Bwana sana.
Jina ambalo tumepewa sisi, tulitegemee kwa kila kitu, na kila saa ni jina la YESU KRISTO TU.. Hilo ndio uligeuze kuwa sanamu yako, na si kitu kingine chochote. Kama ulikuwa unafanya hivyo basi acha mara moja.
Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.
Hivyo, kwa hitimisho ni kuwa, mstari huo haumaanishi maji, au chumvi, au udongo, au kitu kingine chochote kinaweza kufanya shughuli ya upatanisho wa mwanadamu. Hapana ni uongo. Vinamtumikia Mungu, lakini sio katika mambo ya wokovu wetu.
Bwana atuepushe na sanamu.
Shalom
NEHUSHTANI (NYOKA WA SHABA).
USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.
KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.
Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”
Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,
Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?
Unyenyekevu ni nini?
Jina la mwokozi wetu Yesu Kristo lihimidiwe milele. Karibu tuyatafakari maandiko. Na leo tutaona ofisi kuu tatu za shetani, ambazo, zinafanya kazi humu duniani.
Biblia inasema..
Ufunuo 16:13 “Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. 14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi”.
Ufunuo 16:13 “Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.
14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi”.
Hapa, tunaona watatu wanatajwa, ambao ni;
Haya ni mapepo makuu matatu ya juu sana na yanayofanya kazi kwa kushirikiana, na kichwa chao akiwa ni ibilisi mwenyewe. Muunganiko huu ndio unaoukamilisha utawala mchafu wa mashetani unaofanya kazi duniani.
Sasa Ofisi ambayo, inafanya kazi sasa kwa nguvu ni hiyo ya JOKA, lakini hizo nyingine mbili zilizosalia yaani ya Mnyama na Nabii wa Uongo, kwasasa zinafanya kazi katika siri, lakini zitakuja kufanya kazi vema, katika kipindi cha dhiki, baada ya unyakuo kupita. Kipindi hicho ndio zitawepa mamlaka kamili ya kujidhihirisha duniani.
Sasa tuone kazi za hizi roho tatu ni zipi;
Kama tunavyofahamu kazi kuu ya JOKA ni kumeza: Biblia inapomtaja joka (shetani), inalenga moja kwa moja katika kummeza Kristo mahali popote anapozaliwa,
soma Ufunuo 12:3-5
“3 Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba. 4 Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake. 5 Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi”.
“3 Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.
4 Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.
5 Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi”.
Na ndio maana utaona pindi Kristo anazaliwa duniani, Joka hili lilisimama ndani ya Herode, kutaka kumuua, lakini lilishindwa..Hivyo mahali popote Kristo anapozaliwa, ni lazima joka ajitokeze kuleta vita, hata sasa mtu anapotaka kuokoka kwa kumaanisha kweli kumfuata Kristo, ajue kuwa ni lazima atakutana na vita vya hili joka, kwasababu sikuzote halitaki kumwona Kristo katika mioyo ya watu.
Na ndio mwishoni biblia inasema, likaenda kusimama katika mchanga wa bahari, yaani mahali ambapo, nchi kavu na Habari vinakutana, fukwe (beach), Yaani ikifunua kuwa lipo mpakani, kuwazuia watu wanataoka kutoka katika giza kuja katika nuru, hapo ndipo vita ilipo.. Kwa maelezo marefu juu ya hili fungua link hii usome >>>> NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.
Ufunuo 12:17 “Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”.
Hivyo, fahamu kuwa ukitaka kuwa mtakatifu, basi ujue pia joka litasimama kukupinga vikali. Lakini halitaweza kukushinda, ikiwa umedhamiria kweli kumfuata Kristo. Lakini ukiwa nusu nusu, yaani unataka hutaki, litammeza Kristo wako, na hutazalisha chochote katika wokovu wako.
Biblia inapotaja mnyama, inazungumzia utawala wa ibilisi kupitia falme kubwa za dunia. Alishatumia falme za dunia kadha wa kadha huko nyuma, kama vile Babeli, Umedi, Uyunani na Rumi, kuangusha watakatifu wa Mungu. Na utaunyanyua tena ufalme mwingine ambao utakuwa na nguvu sana, ufalme huu kichwa chake kitakuwa ni RUMI, na utafanya kazi kwa kipindi kifupi sana yaani miaka pungufu ya saba (7), lakini utaleta, mabadiliko makubwa sana duniani, kiasi kwamba kila mtu atalazimishwa aufuate huo utawala.
Usipoufuata, hutaweza kuuza wala kununua, wala kuajiriwa. Biblia inasema utawala huo wa kishetani ambao utakuwa na chapa ya 666 nyuma yake, utafurahiwa na watu wote watatakaokuwa wamesalia, ambao majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha mwana-kondoo kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu. Lakini wale wote watakaoonyesha dalili ya kuukataa au kuupinga, mwisho wao utakuwa ni kifo cha mateso makali sana ya dhiki.
Ufunuo 13:8 “Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia”.
Jambo ambalo wengi wetu hatulijui ni kuwa, utawala huu tayari ulishafanya kazi huko nyuma,ambao ni Rumi, na ulishawaua watakatifu wengi sana Zaidi ya milioni 80, Lakini sasa Mungu ameuzuia kwa muda, lakini ndiyo utakaokuja kuzuka tena na kuyaongoza mataifa yote, katika utawala mpya, moyo wa utawala huo ni Vatican, Rumi, utakuwa na nguvu nyingi Zaidi ya ule wa kwanza, kwasababu utakuwa na sapoti ya mataifa yote makubwa unayoyajua leo hii duniani.
Ufunuo 17:8 “Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako”.
Kama jina lake lilivyo, ni nabii, kazi yake ni kuwapotosha watu, kwa kuwapa maagizo ya uongo, wadhani kuwa wanapokea maagizo kutoka kwa Mungu kumbe ni kwa ibilisi. Biblia inasema hata sasa wapo manabii wa uongo, ambao wanaiga kazi ya mkuu wao, atakayekuja. Nabii huyu ndiye mpinga-kristo mwenyewe.
1Yohana 2:18 “Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho”.
Mpinga-Kristo huyu ambaye atakuja rasmi mara baada ya unyakuo wa kanisa kupita, atapewa uwezo wa kufanya ishara za uongo na shetani mwenyewe,atapewa uwezo wa kutenda miujiza feki kama ile ya Yane na Yambre kipindi cha Musa.
2Wathesalonike 2:6 “Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake. 7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa. 8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake; 9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo”;
2Wathesalonike 2:6 “Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.
8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;
9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo”;
Na kazi yake kubwa itakuwa ni kuwashurutisha watu, waipokee ile chapa ya mnyama, na wengi watamuamini sana na kuipokea kwasababu ya zile ishara atakazokuwa anazifanya duniani.
Ufunuo 13:12 “Naye atumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake. Naye aifanya dunia na wote wakaao ndani yake wamsujudie mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona. 13 Naye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu. 14 Naye awakosesha wale wakaao juu ya nchi, kwa ishara zile alizopewa kuzifanya mbele ya huyo mnyama, akiwaambia wakaao juu ya nchi kumfanyia sanamu yule mnyama, aliyekuwa na jeraha la upanga naye akaishi. 15 Akapewa kutia pumzi katika ile sanamu ya mnyama, hata ile sanamu ya mnyama inene, na kuwafanya hao wote wasioisujudu sanamu ya mnyama wauawe. 16 Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao; 17 tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake. 18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.
Ufunuo 13:12 “Naye atumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake. Naye aifanya dunia na wote wakaao ndani yake wamsujudie mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
13 Naye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu.
14 Naye awakosesha wale wakaao juu ya nchi, kwa ishara zile alizopewa kuzifanya mbele ya huyo mnyama, akiwaambia wakaao juu ya nchi kumfanyia sanamu yule mnyama, aliyekuwa na jeraha la upanga naye akaishi.
15 Akapewa kutia pumzi katika ile sanamu ya mnyama, hata ile sanamu ya mnyama inene, na kuwafanya hao wote wasioisujudu sanamu ya mnyama wauawe.
16 Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao;
17 tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.
18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.
Na mwisho kabisa, roho hizi zote tatu, yaani ya joka, mnyama na nabii wa uongo, zitaungana, na kuwaendelea wafalme wote wa duniani, ikiwemo wa hilo taifa lako unaloishi, ili wapatane kwa kitu kimoja, kupigana na Mungu mwenyezi, pale Israeli, katika vita ile ya Harmagedoni, kipindi hicho ndicho Kristo atahitimisha vyote kwa kuwaua wanadamu wengi sana, na kuanzisha utawala wake mpya wa amani wa miaka elfu moja hapa duniani, naye atatawala kama MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA. Haleluya.
Hivyo ndugu, fahamu kuwa hizi ni nyakati za mwisho, kipindi kifupi sana tumebakiwa nacho, Unyakuo ni siku yoyote, dalili zote zimeshatimia, mfumo wa yule mnyama upo tayari, unatenda kazi tu kwa siri kwa dini ya uongo ya rumi, ni wakati wowote kunyanyuka, Tubu dhambi zako mgeukie Bwana Yesu kwa kumaanisha. Kubali kujitwika msalaba wako umfuate, kwasababu parapanda italia siku yoyote.
Bwana akubariki.
UNYAKUO.
UFUNUO: Mlango wa 12
UFUNUO: Mlango wa 13
UFUNUO: Mlango wa 17
USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.
DANIELI: Mlango wa 1
NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.
WhatsApp
Moja ya maagizo ambayo Bwana Yesu aliwapa wanafunzi wake alipowatuma kwenda kuhubiri injili mbali, lilikuwa ni kutokulipisha fedha katika huduma yoyote watakayoitoa, hali kadhalika kutokubeba chochote katika safari yao. Yaani wasiwe na maandalizi yoyote ya njiani, Lakini mwishoni kabisa mwa maagizo yake aliyasema maneno haya “maana mtenda kazi astahili posho lake”.. Sasa swali linakuja Je hili posho ni lipi alilostahili huyu mtandakazi ili hali ameitwa atoe bure?
Mathayo 10:8 “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure. 9 Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu; 10 wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi astahili posho lake”.
Mathayo 10:8 “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.
9 Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;
10 wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi astahili posho lake”.
JIBU: Posho aliyostahili ni ile ambayo Bwana Yesu mwenyewe atampa katika kazi ya injili anayoipeleka, kwa kupitia watu wakarimu ambao Bwana Yesu mwenyewe atawagusa moyo huko waendako aidha kwa kuwapa maji, au chakula, au nguo, na wakati mwingine hata fedha.
Hiyo yote ni kuonyesha kuwa Bwana Yesu anaweza kumtunza mtumwa wake, katika mazingira yoyote atakayomtuma. Na ndiyo maana mwishoni kabisa akawaambia maneno haya;
Luka 22:35 “Akawauliza, Je! Hapo nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu? Wakasema, La!
Ni kufunua kuwa hatupaswi kuwa na wasiwasi wa maandilizi yoyote ya huduma ya Kristo, pale ambapo hatuna chochote, Bwana anataka tuwe wepesi (SIMPLE), tusijali sana tutakula nini, tutavaa nini huko tuendako, kesho tutatolea wapi nauli ya kurudi, hilo jambo Bwana hataki sisi kama watumwa wake tulifikirie, kwasababu ameahidi kabisa ikiwa tunatenda kazi yake kiuaminifu, basi tumestahili posho yake, hivyo anza kutumika.
Lakini haimaanishi kuwa, wakati wote, hata kama unacho, ndio ujifanye hauna, hapana, bali, upo wakati wewe kama mtumishi wa Mungu utabarikiwa na utakuwa navyo vya kuendea huko katika ziara, hivyo vitumie hivyo, Na ndio maana wakati mwingine Bwana aliwaambia wajibebe fimbo ya njiani, na kujifungia viatu, wakati sehemu nyingine kama tuliyosoma hapo juu aliwakataza.(Marko 6:8-9)
Kwahiyo, kwa vyovyote vile, Bwana atatutunza, ilimradi tunamtumkia yeye kwa uaminifu. Tusiwe na wasiwasi na huduma yake, Haleluya..
Shalom.
ANGALIENI MWITO WENU.
WITO WA MUNGU HAUVUKI NENO LAKE.
MAAGIZO AMBAYO HAYAJAAGIZWA!
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.
BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.
HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU
Kuna makundi mawili ya WACHAWI!.
1. Wachawi wa kawaida wanaojulikana; wanaopaa na Nyungo, na kuloga na kuwanga!. Hawa wanamharibia mtu Maisha yake ya kimwili tu, kufanya mtu awe na kasoro fulani fulani za kimwili, au kimaisha.
2. Manabii wa Uongo: Hili ni kundi la Pili la wachawi!, ambalo ni hatari sana kuliko hilo la kwanza!.. kundi hili haliwalogi watu kimwili bali kiroho.. yaani kazi yake ni kumsababisha mtu aukose uzima wa milele kwa kuiacha Imani au kwa kutoijua imani.
Hili kundi la Pili, ndiyo lile Mtume Paulo alilolizungumzia katika kitabu cha Wagalatia na lile Bwana alilotuambia tujihadhari nalo.
Wagalatia 3:1 “Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa? 2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? 3 Je! Mmekuwa wajinga namna hii? BAADA YA KUANZA KATIKA ROHO, MNATAKA KUKAMILISHWA SASA KATIKA MWILI?”
Wagalatia 3:1 “Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?
2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?
3 Je! Mmekuwa wajinga namna hii? BAADA YA KUANZA KATIKA ROHO, MNATAKA KUKAMILISHWA SASA KATIKA MWILI?”
Na Bwana Yesu alituonya tujihadhari na kundi hilo la Pili, Zaidi ya lile la kwanza.
Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali”.
Manabii wa uongo ni wachawi wanaologa roho, ambao wamevaa mavazi ya karama za Mungu, wanajiita wachungaji, waalimu, wainjilisti, waimbaji, wahubiri n.k lakini katika utu wao wa ndani ni waharibifu wa roho za watu!.
Hawa hawatakuonea wivu wewe kwa Maisha mazuri hapa duniani, tena watakuhubiria hayo!, watakupaka na mafuta, na kukulisha chumvi, na udongo ilimradi tu, upate mafanikio, wala hawataona wivu wewe kuzaa Watoto, wala hawatakuonea wivu wewe kufurahi duniani, kama lile kundi la kwanza, ambalo halitaki ufanikiwe hapa duniani.
Manabii wa uongo!, wenyewe hawana shida na wewe kufanikiwa.. wenyewe wanashida moja tu kwako!.. kwamba USIURITHI UZIMA WA MILELE!!!!. Hilo tu!!
Hebu tujifunze kwa nabii mmoja wa uongo katika biblia, (aliyekuwa mchawi wa roho za watu), na kisha tutapata kujifunza zaidi…
Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, MCHAWI, NABII WA UONGO, Myahudi jina lake BAR-YESU; 7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, MTU MWENYE AKILI. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu. 8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), AKASHINDANA NAO, AKITAKA KUMTIA YULE LIWALI MOYO WA KUIACHA ILE IMANI”.
Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, MCHAWI, NABII WA UONGO, Myahudi jina lake BAR-YESU;
7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, MTU MWENYE AKILI. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu.
8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), AKASHINDANA NAO, AKITAKA KUMTIA YULE LIWALI MOYO WA KUIACHA ILE IMANI”.
Umeona hapo kazi ya huyo mchawi (aliye nabii wa uongo) ni ipi?.. Haikuwa kumwangia na kumloga Sergio asiwe Tajiri, au asiwe na akili, au asiwe na Watoto, bali ilikuwa ni KUMTIA MOYO WA KUIACHA IMANI YA BWANA YESU!!!.
Ndugu, Manabii wa uongo hata leo wanafanya kazi hiyo hiyo!.. wanashikiria biblia, wanahubiri, na wana majina ya kikristo (kama huyu Bar-Yesu) na mbaya zaidi wanatoa mpaka pepo, lakini ndani yako ni wauaji wa roho!!..
Kaka/Dada usifurahie kufarijiwa na mhubiri anayekuambia kuwa mambo yote ni sawa na huku hayaoni maisha yako yaliyojaa uzinzi, usifarijiwe na mchungaji yeyote, au nabii, au mwalimu, au padri, anayekuambia kuwa wewe ni mtoto wa Mungu, unayependwa na ilihali wewe ni mwizi, ni mlevi, ni muabudu sanamu, ni mgomvi, ni mtu wa hasira, ni mtu wa kutosamehe, ni mtu wa vinyongo na mtazamaji pornography, ni mtu wa kujichua ni mtu wa kuvaa na kutembea nusu uchi.. Tambua kuwa wewe bado hujawa mtoto wa Mungu katika hiyo hali ya dhambi uliyopo.
Jua huyo mchungaji au mwalimu anayekufundisha hivyo, hakupeleki kwenye Imani, bali anakutoa kwenye Imani..
Hiyo ndio kazi kubwa ya manabii wa Uongo!. KUKUFANYA UKAE MBALI NA ILE KWELI, AU USIIELEWE KABISA!!. Na ubaya ni kwamba hawa manabii wa uongo, WENGI WAO wanaujua ukweli! Lakini kwasababu wapo kwaajili ya kazi waliotumwa na baba yao (ibilisi), basi ndio wanaendelea kuwapotosha watu makusudi..
Neno la Mungu linasema..
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU”.
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU”.
Itafute kweli yote ya Neno la Mungu..na JIHADHARI NA MANABII WA UONGO!..
Bwana Yesu anarudi na hizi ni siku za Mwisho.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10 WHATSAPP-Group
Usimwache mwanamke mchawi kuishi! Biblia ilimaanisha nini?
Nini maana ya “Torati na manabii”?
JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?
ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO
Jibu: Biblia haitupi andiko la moja kwa moja kuwa uchongaji wa ndevu au nywele ni dhambi. Hilo hasaa linategemea na nia, au kiwango , au mtindo. Hapo ndipo yaweza kuwa rahisi kuhukumu kama ni dhambi au la!. Kwamfano mwingine amenyoa kawaida, kisha kwa kumalizia akapenda kuzichonga kwa lengo la kuzifanya ziwe katika mpangilio wake bora lakini hana nia nyingine yoyote, hiyo sio dhambi.
Lakini mwingine anaweka ndevu au nywele zake katika mitindo, fulani mfano tu watu wa kiulimwengu, mfano anachonga pembeni, kisha katikati anaacha kimchirizi kidogo cha nywele (kiduku), utajiuliza huyu mtu nia yake ni nini? Sisi tumeambiwa, Nuru yetu iangaze mbele za watu, ili watakapoona matendo yetu wamtukuze Baba yetu wa mbinguni.. Lakini wewe kama mkristo, unayechonga nywele kwa mitindo hiyo, ni nuru gani unaangaza?
Hali kadhalika tumeambiwa tusiifuatishe namna ya dunia hii (Warumi 12:1).
Hatuna budi kufahamu kuwa miili yetu ni makao ya Mungu, mwenyewe, hivyo lolote tunalolifanya ni lazima tujiulize kwanza mwenye hekalu anapendezwa na huu mtindo ninaomwekea, ikiwa amani ya Kristo ipo ndani yako na una ujasiri wote kumuhubiri Kristo katika hali hiyo fanya, lakini ikiwa hakuna amani, acha mara moja.
1Wakorintho 3:16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi
Je kwa mkristo aliyeokoka, ni dhambi kunyoa ndevu zake?
NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.
Kwanini ndugu wanaokaa pamoja wawe kama mafuta ya Haruni?
Panda/ Sauti ya panda ni nini kibiblia?(Danieli 3:5)
KUJIPAMBA NI DHAMBI?
Kupoza ni nini?
Jibu: “Kupoza” ni Kiswahili kingine cha neno “kuponya”. Hivyo badala ya kutumia neno kuponya, linaweza kutumika neno “kupoza” likawa na maana ile ile. (kama vile neno mtu na mwanadamu inavyoweza kuwa na maana moja).
Bwana Yesu aliwapa Mitume wake uwezo wa kupoza wagonjwa kupitia jina lake.
Marko 6:12 “Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu. 13 Wakatoa pepo wengi, wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, WAKAWAPOZA”.
Marko 6:12 “Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu.
13 Wakatoa pepo wengi, wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, WAKAWAPOZA”.
Na uwezo huo haukuishia tu kwa wale mitume 12, bali aliendelea hata watumishi wengine wengi waliomwamini Bwana Yesu kama akina Stefano na akina Barnaba, na Paulo.
Matendo 28:8 “Ikawa babaake Publio alikuwa hawezi homa na kuhara damu. Paulo akaingia kwake, akaomba, akaweka mikono yake juu yake, na KUMPOZA. 9 Yalipokwisha kutendeka hayo wengine waliokuwa na magonjwa katika kisiwa wakaja WAKAPOZWA”.
Matendo 28:8 “Ikawa babaake Publio alikuwa hawezi homa na kuhara damu. Paulo akaingia kwake, akaomba, akaweka mikono yake juu yake, na KUMPOZA.
9 Yalipokwisha kutendeka hayo wengine waliokuwa na magonjwa katika kisiwa wakaja WAKAPOZWA”.
Na uwezo huo haukuishia tu kwa wakristo wa kanisa la Kwanza, bali hata leo uwezo huo Bwana katupa, wote tumwaminio pale tunapokwenda kuhubiri injili..
Mathayo 10:7 “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. 8 POZENI WAGONJWA, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure”.
Mathayo 10:7 “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.
8 POZENI WAGONJWA, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure”.
Na si katika kuhubiri tu!.. bali hata popote pale tutakapokuwepo, uwezo huo utakuwa nasi..
Marko 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; 18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.
Marko 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.
Yesu, anafanya miujiza hata leo!.
LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.
SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.
Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?