Category Archive Mafundisho

LIITE JINA LA BWANA KATIKA NYAKATI MBALIMBALI ZA MAISHA.

Upo umuhimu mkubwa wa kuliita Jina la Bwana

Warumi 10:12 “Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao;

13  kwa kuwa, KILA ATAKAYELIITIA JINA LA BWANA ATAOKOKA

Kuna umuhimu mkubwa wa kuliitia jina la Bwana kiusahihi, na kuna hatari kubwa ya kuliita au kulitaja jina la Mungu kimakosa.

Kutoka 20:7 “Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako, maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure”.

Kwahiyo kama kwa kulitaja jina la Mungu bure ni dhambi, vile vile kinyume chake ni kweli kwamba tukilitaja inavyopaswa na kwasababu muhimu basi ni Faida kubwa kwetu.

Kwanini?, ni kwasababu jina la Mungu lina nguvu kuliko mwonekano wake…amelitukuza jina lake kuliko umbile lake, ndio maana amependa kutujulisha jina lake Zaidi ya sura yake.

Mithali 18:10 “Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama”

Leo kwa neema zake tutatazama njia sahihi ya kulitaja jina la Bwana Mungu kulingana na mazingira tunayopitia ili tupate wokovu, tumaini, faraja, ushindi, Amani na Nguvu!.

  1.Katika kipindi cha mahitaji-Mwite YEHOVA-YIRE.

Yehova-Yire maana yake ni Mungu-Mpaji, (Mungu anayetoa kimiujiza)..Asili ya jina Yehova-Yire, ni kipindi Ibrahimu anakwenda kumtoa Isaka mwanae kama sadaka kwa Mungu, akiwa njiani mwanae Isaka alimwuliza Ibrahimu baba yake kuwa kuni zipo na moto pia upo lakini yupo wapi mwanakondoo?..Ndipo Ibrahimu kwa Imani alimjibu.. “Mungu atajipatia (Mwanzo 22:7-8)”.

Na walipofika katika mlima Moria ndipo wakamkuta kondoo ambaye tayari Bwana alikuwa amewaandalia. Ibrahimu akamwita Bwana YEHOVA-YIRE.

Vile vile na sisi tuwapo katika hali ya kuhitaji jambo Fulani (kama hitaji) tumwite Mungu kama YEHOVA-YIRE, itakuwa na mashiko Zaidi mbele zake kuliko kumwita au kumwomba tu kama MUNGU-MWENYEZI.

    2. Katika nyakati za Magonjwa- Mwite YEHOVA-RAFA

Yehova-Rafa maana yake ni “Mungu-atuponyaye”. Wakati wana wa Israeli wanaelekea Kaanani, Bwana Mungu aliwaahidi “kutowaletea magonjwa yale aliyowapiga nayo wamisri” endapo wakidumu katika sheria zake na amri zake.. Hivyo wana wa Israeli baada ya kusikia hivyo wakawa wanamwita Mungu YEHOVA-RAFA, kipindi walipopitia magonjwa na maradhi, na Mungu alikumbuka ahadi yake hiyo na aliwaponya na magonjwa yao.

Kutoka 15:26 “akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi Bwana nikuponyaye”.

Vile vile upitiapo magonjwa au maradhi, mwite Mungu kama YEHOVA-RAFA, na utauvuta uponyaji kirahisi Zaidi..ndivyo walivyofanya wana wa Israeli katika nyakati za magonjwa.

     3. Katika Nyakati za vita- Mwite YEHOVA-NISI

Yehova-Nisi maana yake ni “Bwana ni Mungu wa vita”. Kipindi wana wa Israeli wanashambuliwa na Waamaleki, Mungu alimwambi Musa anyanyue mikono yake miwili juu, na aliponyanyua Israeli walishinda na aliposhusha waamaleki walishinda, na mwisho wa vita vile Israeli walishinda kwasababu Haruni aliitegemeza mikono ya Musa kuanzia asubuhi mpaka jioni (Kutoka 17:8-16).

Ndipo wana wa Israeli wakamwita Bwana YEHOVA –NISI, maana yake “Mungu wa Vita” (bendera yao).. Kwahiyo Nyakati za Vita walimwimbia Bwana, na kumsifu kama YEHOVA NISI na si Yehova Yire, na Bwana aliwaonekania.

Na sisi tukutanapo na vita mbele yetu viwe vya kiroho, kiimani au kiuchumi.. basi ni vizuri tukamwita Mungu wetu kama Yehova Nisi, tukamsifu na kumwimbia kwa jina hilo,  na vita mbele yetu atavifanya maji!.. kwasababu yeye anaketi katika sifa.

   4. Katika vipindi vya Hatari- Mwite YEHOVA–ROHI.

Yehova-Rohi maana yake ni “Bwana ndiye mchungaji wangu”. Daudi alipopita vipindi vya hatari, alimwita Bwana kama mchungaji wake, Yehova-Rohi  na kumsifu kwa jina hilo (Zaburi 23). Na Bwana daima alionekana mbele yake alimwokoa na hatari za kifo na dhiki zilizopo mbele yake.

Vile vile na sisi tuonapo hatari, au tuhisipo hatari, jina jema la kumwita Bwana na kumtukuza nalo, na kumsifu nalo ni YEHOVA-ROHI.

  5.Katika kipindi cha mambo yasiyowezekanika –Mwite YEHOVA-EL – SHADAI.

Yehova-Elshadai maana yake “Bwana ni Mungu-Mwenyezi” (anayeweza kufanya mambo yote).

Kipindi ambacho Ibrahimu anaona uwezekano wa kupata mtoto haupo kutokana na umri wa mke wake Sara, Bwana alijidhihirisha kwake kama Mungu mwenye uwezo wote (Mungu mwenyezi), na Sara akapata mimba, Hivyo Ibrahimu na Israeli wote wakaendelea kumwomba BWANA kama YEHOVA-ELSHADAI Katika vipindi vya mahitaji yaliyo magumu, kama utasa, ukame n.k

   6. Katika nyakati za Upweke- Mwite YEHOVA-SHAMA.

Yehova-Shama maaana yake “Mungu yupo hapa” (Ezekieli 48:35). Nyakati ambazo unajiona upo peke yake, mwambie Bwana wewe upo hapa, YEHOVA-SHAMA, na uwepo wa kipekee utakufunika, ndivyo Israeli walivyomwita Bwana nyakati za upweke.

  7. Nyakati za kukosa Amani- Mwite YEHOVA-SHALOM.

Yehova-Shalom, maana yake ni “Mungu Amani yangu”. Gideoni alipotokewa na yule malaika alihisi atakufa, lakini malaika yule alimwambia “hutakufa” na Gideoni akapata “amani”akamwita Mungu Yehova-Shalom.. Mungu ni Amani yangu.

Waamuzi  6:22 “Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa Bwana; Gideoni akasema, Ole wangu, Ee Bwana MUNGU! Kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso.

23 Bwana akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa.

24 Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri”.

Na sisi vitokeapo vipindi vya Amani ya moyo kupotea na hofu kutawala, hususani hofu ya kifo, basi tumwite Mungu kama Yehova-Shalom, na amani yake itatufunika.

  8. Nyakati za kutamfakari Mungu kwa matendo yake- Mwite YEHOVA-ADONAI.

Yehova-Adonai maana yake ni “Mungu mwenye enzi yote(mfalme)” aliyeumba vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana. Sifa kwa ADONAI zina nguvu kama zikitajwa kwa maarifa hayo..

  9.Katika vipindi vya Kupotea na kuhitaji wokovu- Mwite YEHOVA-MWOKOZI (YESU KRISTO)

Maana ya YEHOVA-MWOKOVU ni YESU,… Tafsiri ya jina YESU ni Yehova-Mwokozi. Hili ndilo jina lenye nguvu katika vipindi karibia vyote. Na ndilo jina la ukombozi, na hakuna jina lingine litupasalo sisi kuokolewa kwalo isipokuwa jina hili la YESU, (Matendo 4:12).

Ikiwa umepotea dhambini, liite jina la YESU naye atakusaidia, ikiwa hutajabatizwa ili ukamilishe wokovu sawasawa na  andiko la Marko 16:16,  na ukabatizwe kwa jina la YESU, (Matendo 2:38, Matendo 19:5 na Matendo 10:48).

Yapo na majina mengine mengi yafaayo kumwita Bwana wetu katika nyakati hizo, lakini hayo yatoshe kusema tu, kuwa Mungu wetu anatupenda na anataka tupate faida, na faida moja wapo ni hiyo ya kulitumia jina lake wakati wa mahitaji.

Lakini katika hayo yote fahamu jambo moja kuwa unapoamua kuanza kulitaja jina la Bwana ili uvute msaada kutoka kwake, hakikisha unaacha UOVU..

2Timotheo 2:19  “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, KILA ALITAJAYE JINA LA BWANA NA AUACHE UOVU

Je umempokea Yesu Kristo, na kusafishwa dhambi zako kwa damu yake?

Kumbuka tunaishi majira ya kurudi kwa YESU mara ya pili, na shetani anafanya bidii nyingi kuhakikisha watu wanaenda katika lile ziwa la moto pamoja naye.

Bwana atusaidie.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ZIFAHAMU NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE SABA.

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?

UMEJIANDAAJE KWA NYAKATI ZA KUWA PEKE YAKO?

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUVURUGA MIPANGO YA MUNGU.

Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.

Kuna vitu ambavyo Mungu amepanga, vitokee kwa njia ya asili, na vingine amepanga vitokee ndani ya wakati wake alioukusudia.  Kwamfano ikiwa amekusudia baada ya miaka kumi ndio uone majibu ya lile hitaji ulilomwomba, yeye mwenyewe ataanza kukuandalia njia sasa, na hatimaye ule wakati ukifika basi atafungua njia ya kukipata.

Lakini vipi kama utakihitaji kwa majira haya ya sasa. Na wakati huo huo iwe ni mapenzi ya Mungu na sio yako. Je hilo linawezekana? Maana yake ni kuwa  uivuruge mipango yake ili afanye sasa hivi kile unachokihitaji. Je! Mungu anaruhusu tuwe watu wa namna hiyo?

Jibu ni ndio.

Na aliyetufundisha siri hiyo si mwingine zaidi ya Kiongozi wetu mkuu wa imani YESU KRISTO.

Embu tafakari haya maneno aliyoyasema.

Luka 18:1  Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa. 2  Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3  Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu. 4  Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5  lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima. 6  Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu. 7  Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8  Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?

Katika vifungu hivyo ni wazi kuwa Bwana anajifananisha na huyo kadhi, ambaye hakuwa tayari kumsaidia Yule mwanamke mjane haja yake kwa wakati ule.  Lakini kutokana na hatua alizozichukua Yule mwanamke ilimbidi tu ampe kama alivyotaka.

Na ndivyo ilivyo kwa Mungu wako. Upo wakati unaweza kupata kile unachokitaka kwa wakati wako, na si kwa wakati wa Mungu? Zipo kanuni ambazo ukizitumia, zitakusaidia kuuvuta msaada wa Mungu kwa haraka zaidi.

Kanuni ya kwanza: Ni kuomba bila kukata tamaa.

Maombi ya kung’ang’ana yanaugusa sana moyo wa Mungu, zaidi ya sisi tunavyoweza kufikiri. Kwa bahati mbaya ni pale tunapoona Mungu amekaa kimya tunadhani, hasikii. Yeye mwenyewe anasema aliyeumba sikio utasemaje hasikii?? Tangu lini?. Mungu huwa anasikia, lakini anasubiri umakini wako wa kile unachokililia kwake, Kama alivyofanya huyo mwanamke. Kiwango chako cha kutokata tamaa, hupelekea majibu ya haraka ya maombi yako. Ukiomba leo hujaona kitu, unaendelea hivyo hivyo kesho, ikiwa kesho haipo, unaendelea kesho kutwa..hivyo hivyo hata kama ni kwa miaka 5, hakuna kusema, Mungu hatendi, au amenisusa. Omba bila ukomo, tena huku ukiamini asilimia mia kuwa  Bwana analishughulikia ,Usibahatishe kuomba. Utapokea kinyume na wakati.

Kanuni ya pili: Kustahimili vipingamizi.

Vipingamizi vinaweza kutokea kwa wanadamu, na wakati mwingine hata katika Neno la Mungu. Kwa wanadamu ni kama vile kuvunjishwa tamaa. Na kuambiwa Mungu hayupo na wewe, au umemkosea Mungu. Hilo unaweza kukumbana nalo sana. Lakini vilevile, Mungu anaweza kukuuliza, unataka upokee hili kwa sifa ipi uliyonayo? Wewe utamjibuje? Hilo nalo utakumbana nalo moyoni mwako.

Embu fuatilia kisa hiki.

Mathayo 15:22  Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23  Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. 24  Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25  Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie. 26  Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. 27  Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28  Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.

Huyu mwanamke, alihitaji wokovu ambao wakati wake ulikuwa bado kwa watu wa mataifa, kwasababu Yesu alikuwa bado hajasulibiwa. Hivyo alipojaribu tendo ambalo lilikuwa ni gumu masikioni mwa watu. Moja kwa moja alikutana na vipingamizi. Cha kwanza ni kutoka kwa mitume walipoona Bwana hamjibu lolote, wakaanza kutaka afukuzwe, kwasababu anasumbua watu. Anapiga-piga kelele ovyo, anawavunjia wayahudi heshima, mpagani huyu. Lakini yeye hakujali yale maneno.

Baada ya hapo  akakumbana na Bwana mwenyewe, ambaye hapo mwanzo alimtazama wala hakumjibu neno lolote. Kumbuka, tabia hiyo ya kutojibu watu hakuionyesha kwa huyu mwanamke tu, bali kwa watu wengine pia, lakini huyu tu habari yake ndio imerekodiwa kwasababu ya kitu alichokifanya. Na alipoambiwa habari za mbwa, hakusijikia vibaya, akawa na hoja hapo hapo za kutetea, kwamba hata mbwa wanapata yale masalio yaangukayo kutoka mezani mwa bwana zake. Na mwisho wa siku akapokea alichokihitaji kinyume na taratibu.

Vilevile na wewe unachomwomba Bwana, atakuuliza una vigezo gani vya kupokea hiki. Hezekia alikuwa na hoja za kumpa Bwana na hatimaye akaongezewa maisha kwa kuponywa ugonjwa wake. Na wewe pia jiandae kwa hoja nzito, na majibu yako kwa Bwana daima yawe ni haya “Bwana sistahili kupokea, lakini Kristo tayari alikufa kwa ajili yangu msalabani, kunistahilisha mbele zako  ndilo linalonipa ujasiri huu wa kupokea chochote mbele zako kwa imani sawasawa (Waebrania 4:16)”. Ukifanya hivyo jiandae kupokea unachokihitaji.

Kanuni ya tatu: Tenda jambo la ziada:

Tendo la ziada, huvuruga mipango mingi ya Mungu. Kwamfano usipende kumwendea Mungu vilevile kwa desturi na mazoea ya sikuzote. Onyesha uhodari Fulani kwa Mungu, onyesha imani Fulani kubwa kwa Mungu. Mara nyingi Yesu alikuwa anafuatwa na Jeshi kubwa la makutano na kila mmoja alikuwa anahitaji ahudumiwe. Lakini utagundua wapo waliowahi kuhudumiwa kwasababu ya imani yao, na matendo yao ya kipekee kwake.

Zakayo hakufuata mkumbo, alibuni njia yake akapanda juu ya mkuyu Bwana akamwona. Yule mwanamke aliyetokwa na damu, hakufuata mkumbo, aliamini nikigusa tu pindo la vazi la Yesu nitapona. Yesu akaghahiri mwendo wake ili amtafute. Wale vipofu wawili Yeriko, waliposikia Yesu anapita, walipaza sauti zao kwa nguvu, wakisema Yesu turehemu. Yesu akawaponya

Vivyo hivyo na wewe, fanya jambo la ziada kwa Mungu wako. Kama ni kumsifu basi msifu zaidi ya kawaida ya sikuzote, uone kama hatafanya jambo kwako la ajabu. Kama ni kumtolea Mungu Mtolee zaidi ya kile kipimo cha kawaida. Fanya jambo kuu. Jimalize kwa ajili ya Bwana kwa kitu Fulani,  Utaamsha moyo wa Mungu akuhudumie kwa haraka sana.

Kanuni ya nne: Pia kuwa mfungaji.

Esta, aliweza kuuvuruga utaratibu wa mfalme. Siku ambapo alipanga kumwendea bila kualikwa. Utaona kuwa alifuata kanuni ya kufunga pamoja na watu wake kwa siku tatu. Ndipo akamkabili mfalme. Na mfalme akatii jambo lile. Kwasababu ilikuwa ni kifo kumfuata mfalme kama hajakualika.

Vivyo hivyo na wewe umwombapo Mungu jambo fulani, hakikisha unaambatanisha mifungo. Kwasababu hiyo hukuongozea umakini wako mbele za Mungu.

Ikiwa utafuata utaratu huo, basi uwezekano wa kupokea mahitaji yako kinyume na njia za kawaida ni mkubwa sana. Uombapo katika eneo lolote liwe gumu au jepesi Bwana atakumulikia nuru zake.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU

KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.

IJUE KANUNI YA KUREJESHA NGUVU ZA KIROHO.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; 

SWALI: Nini maana ya Mithali 16:30

Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;  Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya. 

JIBU: Mstari huo haumaanishi mtu anayefumba macho yake, Huwa anaishia kuwaza mawazo mabaya, hapana kama ni hivyo basi,  tungekuwa tunafanya makosa kufumba macho tunapoomba.

Zaidi sana mtu mwenye hekima huwa anapoona jambo la kutisha ovu, au lenye aibu Ndio anayekuwa wa kwanza kufumba macho yake asiruhusu kuona kinachoendelea.. kama vile walivyofanya watoto wa Nuhu.(Mwanzo 9:23)

Hali kadhalika anaposema mtu aikazaye (aifumbaye), midomo yake. Haimaanishi mtu asiyezungumza-zungumza, Huwa anaishia kuyazungumza maneno yasiyofaa. Kama ni hivyo biblia isingesema;

Mithali 21:23

[23]Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu. 

Lakini je? Vifungu hivyo vilimaanisha Nini?

Hapo anaposema afumbaye macho yake ni kuwaza yaliyopotoka,..alimaanisha afumbaye macho asitazame kweli (ambayo ni Neno la Mungu), linapomfundisha au kumwonya. Mtu huyo lengo lake ni kuendelea katika mawazo yake mabaya ya dhambi. Mfano aambiwapo kuishi na mke ambaye si wako ni uzinzi, na wazinzi sehemu Yao ni Katika ziwa la moto, lakini hataki kuliona au kulisikia Hilo andiko, jibu lake ni kuwa anataka kuendelea katika matendo yake ya giza.

Ndicho kilichokuwa Kwa waliompinga Yesu., Ndio maana akasema  maneno haya; 

Mathayo 13:15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, 

Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Vilevile anaposema “Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya”

Anamaanisha, aizuiaye midomo yake kusema maneno ya uzima, ya staha, ya kujenga, ya adabu, ya maarifa, ya busara n.k.. Mwisho wake utakuwa ni kunena maneno mabaya tu.

Bwana alisema..

Luka 6:45

[45]Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake. 

Vivyo na hivyo na sisi, hatuna budi tujipime na kujichunguza…macho yetu hutazama Nini, vinywa vyetu vimejawa na maneno gani.? Lakini fahamu kuwa huwezi kushinda jicho lako, au ulimi wako ikiwa Kristo hajaumbika ndani yako.

Je! Unataka msaada Kwa Yesu Kristo? Kama jibu ni Ndio, basi unachopaswa kufanya cha kwanza ni kuyaachilia maisha yako kwake. Ili akusamehe dhambi zako. Ndipo akupe nguvu ya kushinda dhambi.

Hivyo bofya hapa Kwa ajili ya Mwongozo wa Sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

NI WAKATI UPI UTAUONA USO WA KRISTO?

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

Rudi nyumbani

Print this post

BWANA ANASAMEHE.

Jina la Bwana na Mwokozi Mkuu YESU KRISTO lihimidiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu lililo hai, ambalo ndilo taa na mwanga wa njia yetu ya kwenda mbinguni (Zab.119:105).

Moja ya hubiri kubwa na kongwe la shetani, ni kuwahubiria watu kuwa “MUNGU HASAMEHI na ANACHUKIA WATU”.

Fundisho hili ni silaha kubwa sana ya kumfanya mtu asijaribu kumtafuta Mungu, au hata kama alikuwa ameshaanza hatua za kuutafuta uso wa Mungu, basi akate tamaa njiani. Anajua mtu akifahamu kuwa anaweza kusamehewa na Mungu basi hatampata tena, na yeye anataka watu waendelee kudumu katika dhambi ili hatimaye waukose uzima wa milele kama yeye alivyoukosa.

Sasa sifa moja kuu ya MUNGU aliyeumba mbingu na nchi, ni MSAMAHA. Maana yake “anatoa msamaha hata kwa mtu asiyestahili kusamehewa”.. Na hii ndio sifa ya kwanza inayomfanya yeye (MUNGU) kutisha!..na wala si tu yale matendo ya miujiza aliyoyafanya kule Misri, au anayoendelea kuifanya hata sasa, ambayo kimsingi tunadhani hayo ndiyo yanayomfanya Mungu atishe.

Muujiza Mkuu na wa kwanza unaomfanya Mungu kutisha, ni KUSAMEHE NDAMBI, na KUZIONDOA KABISA NDANI YA MTU.

Zaburi 130:3 “Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha, ILI WEWE UOGOPWE”.

Je! Unajihisi wewe ni mwenye dhambi, na unahisi dhambi yako haifutiki??…fahamu kuwa MUNGU kuna msamaha, na sio tu msamaha bali pia na ondoleo la dhambi, kiasi kwamba baada ya kusamehewa Mungu anaondoa mpaka msingi wa hiyo dhambi, kiasi kwamba wakati mwingine haitakuwa na nguvu juu yako.

Je unahisi mauaji uliyoyafanya hayawezi kusameheka?, je unahisi mawazo uliyowaza au unayowaza hayana msamaha?, je unahisi tendo ulilolifanya na tena umelirudia mara nyingi nyingi halina msamaha?..kama hayo mawazo yapo ndani yako basi fahamu kuwa ni adui ndiye anayekuambia hivyo.

Yote uliyoyafanya yanasameheka ikiwa utataka Bwana akusamehe!. Unachopaswa kufanya ni kutubu tu kwa kumaanisha kuacha hayo unayoyafanya, Ikiwa utatubu kweli kwa kumaanisha, basi kwa IMANI amini kuwa Mungu kashakusamehe, hauhitaji kutokewa na Malaika na akamwambie kwamba umesamehewa, wewe Amini tu, kwasababu ndivyo biblia inavyotufundisha kwamba “tuenende kwa Imani na si kwa kuona” (2Wakorintho 5:7).

Na ukishaamini namna hiyo, basi Mungu kashakusamehe lile kosa au yale makosa uliyoyafanya hata kama uliyafanya kwa kurudia rudia mara 100, tayari atakusamehe deni yako yote. Lakini kumbuka msamaha si ondoleo!.. Mtu anaweza kukusamehe tusi ulilomtukana, lakini kama ile roho ya kutukana haijaondoka ndani yako basi unaweza kurudia tena kesho na kesho kutwa kumtukana matusi yale yale.

Kwahiyo ili lile kosa lisijirudie rudie tena katika maisha yako, linahitaji kuondolewa kwa mizizi yake ndani yako. Sasa kanuni ya kuondoa mzizi wa dhambi ndio shetani amewafumba watu macho wasiione.

Lakini ashukuriwe Mungu kwasababu ipo wazi katika maandiko.

Tusome,

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Hapa Petro anawaonyesha hawa Makutano, kanuni ya KUONDOA MZIZI wa dhambi ndani yao, baada ya wao KUTUBU dhambi,  kwamba WAKABATIZWE KWA JINA LAKE YESU KRISTO. Kama ishara ya kuuvua utu wa kale na kuuvaa utu upya, na kwa ishara hiyo ya maji basi ule mzizi wa dhambi utaondoka ndani yao, zile dhambi za kujirudia rudia zitakoma, kwahiyo mtu wa Mungu anabaki huru mbali na dhambi.

Na tena Mungu wetu kwa upendo wake anatuongezea na zawadi ya Roho Mtakatifu, ndani yetu kama Muhuri wa Mungu kwa kile tulichokitubia.

Je bado umezishikilia dhambi zako? Kwanini usiungame leo kwa kutubu na kubatizwa?. Na kumbuka ungamo sahihi ni lile la kutubu kwa kumaanisha, na ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO, Kutubu kusikotoka moyoni, na ubatizo usio sahihi haviwezi kuleta matokeo yoyote kwa mtu.

Bwana akubariki.

Ikiwa utahitaji msaada katika kuongozwa sala ya Toba, au ubatizo basi waweza wasiliana nasi na tutakusaidia katika hilo.

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA KUTUBU

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

BABA UWASAMEHE

UMEONDOLEWA DHAMBI?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Rudi nyumbani

Print this post

IJUE KANUNI YA KUREJESHA NGUVU ZA KIROHO.

Je Imani yako imefifia?, je upendo wako umepoa?, je Amani yako imepungua?, na haki yako imepoa?.. Na hujui cha kufanya na ndani bado una haja sana ya kuwa na mambo hayo?.. Basi suluhisho lipo ndani ya biblia.

Ifuatayo ni kanuni moja nyepesi ya kurejesha joto la ROHO MTAKATIFU ndani yako. Kumbuka mtu aliyejaa Roho Mtakatifu ataonyesha matunda yafuatayo…

Wagalatia 5:22  “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23  upole, kiasi;…”.

Ikiwa mambo haya yalikuwa ndani yako lakini sasa huyaoni tena, au ikiwa hauna kabisa, basi tumia kanuni ifuatayo kuyarejesha/kuyajenga ndani yako.

KAA KARIBU NA WATU WATU WANAOMWITA BWANA.

Watu wanaomwita Bwana, kwa lugha nyingine ni watu waliookoka kikweli kweli,…Utauliza kwa namna gani?…Tusome maandiko yafuatayo..

2Timotheo 2:22  “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, PAMOJA NA WALE WAMWITAO BWANA KWA MOYO SAFI”.

Hapo mwisho anasema, ukatafute haki, Imani na upendo na amani “pamoja na wale wote wamwitao Bwana kwa moyo safi”.

Kumbe! Haki inapatikana kwa watu wanaomwita Bwana kwa dhamiri safi, kumbe tukikaa na watu waliomaanisha kumwita Bwana na kumtafuta basi Amani tutaipata, na upendo na Imani.

Kama maandiko yasemavyo kwamba “chuma hunoa chuma, Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake” (Mithali 27:17). Vivyo hivyo na sisi tunapokaa na watu wenye kumaanisha kumtafuta Mungu basi ule moto ulio ndani yao atahamia na kwetu pia.

Lakini tukijitenga na kubaki wenyewe, au tukijumuika na watu wengine wasio na nia ya dhati kumtafuta Bwana, ni ngumu kuuwasha ule moto wa Roho ndani yetu!, tutabaki kama tulivyo!.. Kanuni ni kukaa pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi!…Vile vile tunapojitenga na kuamua kukaa peke yetu kwa muda mrefu ni pia ni hatari!!.. Imani, amani, upendo na haki yako vinaweza kuathirika pakubwa.

Sasa tunawapatia wapi watu wamwitao Bwana kwa moyo safi?.

1.Katika kanisa lililo hai.

Hii ni sehemu pekee ambayo utawapata watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, jiunge na kanisa la kiroho lililo karibu nawe, au hata lililo mbali ikiwa lililo karibu nawe halina utakatifu. Jumuika na watu hao, katika utii na unyenyekevu, na katika ibada zote, na hapo Roho Mtakatifu atakujenga ndani yako na kukujaza nguvu zake, utaona Imani yako inapata nguvu, upendo wako uliopoa unawaka tena, haki yako iliyopotea inarudi na Amani yako pia inahuika upya, na ifanye hiyo iwe desturi yako daima.

Waebrania 10:25 “wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine;..”.

Na utajuaje kanisa hilo, ni la kiroho?.

Kigezo cha kwanza ni mwonekano wa nje wa waabuduo wa mahali hapo!, ukiona mwonekano na mazungumzo ya waabuduo si ya kiMungu, kwamba wanazungumza kidunia na wanavaa kidunia, kiasi kwamba hauoni tofauti na mtu anayeenda disko na anayeshiriki mahali hapo, basi tuchukua tahadhari hapo si sehemu salama!.

Vile vile mafundisho yanayofundishwa mahali pale kama hayalengi TOBA, na UJIO wa PILI wa BWANA YESU, na UTAKATIFU wa MWILINI na ROHONI, pia hapo si sehemu salama, lakini kama kanisa lina vigezo hivyo vya Utakatifu wa kimafundisho na kimwonekano, basi ndani yake watakuwepo watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, kaa hapo na utaona mabadiliko makubwa ya kiroho ndani yako.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA WEWE NI KIJANA, BASI FAHAMU YAFUATAYO NA UCHUKUE TAHADHARI!

Ikiwa wewe ni kijana basi fahamu basi fahamu mambo yafuatayo.

1.MAWAZO MABAYA YANAANZIA UJANANI.

Mwanzo 8:21 “Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, MAANA MAWAZO YA MOYO WA MWANADAMU NI MABAYA TANGU UJANA WAKE; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya”.

Mawazo ya kuidharau injili, mawazo ya ukaidi wa moyo na kiburi cha uzima yanaanzia ujanani.

Yeremia 22: 21 “Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako TANGU UJANA WAKO, KUTOKUITII SAUTI YANGU”.

   2. MUNGU ANATAFUTWA UJANANI NA SI UZEENI!.

Mhubiri 12: 1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Maana yake katika uzee “haitawezekana kabisa” kumtafuta Mungu kama utapuuzia wito wa Mungu katika ujana wako!!!. Wakati wa Ujana ndio wakati wa kujifunga NIRA YA MUNGU iliyotajwa na BWANA YESU katika Mathayo 11:29.

Maombolezo 3:27 “Ni vema mwanadamu aichukue NIRA WAKATI WA UJANA WAKE.

28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake”.

   3. KAMA UTACHAGUA ANASA, BASI FAHAMU KUWA SIKU YA MWISHO UTASIMAMA HUKUMUNI.

Mhubiri 11:9 “Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya KWAMBA KWA AJILI YA HAYO YOTE MUNGU ATAKULETA HUKUMUNI”

Maana yake kama utachagua uzinzi katika ujana wako, au ulevi, au anasa nyingine yeyote basi pia jiweke tayari kusimama mbele ya kiti cha hukumu siku ile ya mwisho, ambapo maandiko yanasema kila mtu atatoa habari zake mwenyewe (Warumi 14:12), na tena kila neno la upuuzi litatolewa hesabu yake siku ile ya hukumu (Mathayo 12:36).

  4. NEEMA YA WOKOVU HAIKUBEMBELEZI.

Ufunuo 22:10 “ Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11  MWENYE KUDHULUMU NA AZIDI KUDHULUMU; NA MWENYE UCHAFU NA AZIDI KUWA MCHAFU; NA MWENYE HAKI NA AZIDI KUFANYA HAKI; NA MTAKATIFU NA AZIDI KUTAKASWA”.

Ikiwa umechagua uchafu!, basi usiufanye kidogo!..ufanya sana, lakini kama umechagua USAFI, basi JITAKASE SANA, usiwe hapo katikati (vuguvugu!)..

   5. UTAKAPOKUWA MZEE UTAPELEKWA USIKOTAKA.

Yohana 21:18  “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka”.

Uhuru ulionao si wa Daima, ipo siku utaisha, na wengine watakuwa na mamlaka juu yako…….

Je wewe kama kijana sasa umejipangaje?..je unawaza nini katika ujana wako huu? au unafikiri nini?…Kwanini usiamua kumgeukia Muumba wako leo!, na kuachana na udunia, na tamaa za ujanani, ambazo hazina faida yoyote Zaidi sana zina hasara nyingi?

2Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”.

Bwana Yesu akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Ikiwa unahitaji msaada wa kuokoka na ubatizo basi wasiliana nasi kwa namba zetu tajwa hapo chini.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Je! Mke wa ujana wako ni yupi kibiblia?

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

SWALI: Nini maana ya  Mithali 21:1

“Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo”.


JIBU: Kuna mithali inayosema “maji hufuata mkondo”. Ikiwa na maana, palipo na mfereji kule kule unapoelekea ndipo maji nayo huelekea. Mfano ukielekeza mrefeji shambani mwako, basi maji yale yataelekea huko si kwingineko, ukielekezea mfereji nyumbani mwako, basi maji yatakuja ndani mwako. Kamwe maji  hayajiamulii  pa kuririkia.

Vivyo hivyo na Mungu, ndivyo anavyofananisha mamlaka yake juu ya wafalme na wakuu wa dunia hii. Kwamba mashauri yao, hawajiamulii tu peke yao kwa kujitakia. Kwamfano utakumbuka kuna wakati  Mungu alimnyanyua Moyo Koreshi mtawala wa Uajemi ili awape ruhusu wayahudi warudi katika nchi yao wakamjengee nyumba.

Ezra 1:1 Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema,  2 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi;  3 Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya Bwana, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu.  4 Na mtu awaye yote aliyesalia mahali po pote akaapo hali ya ugeni, na asaidiwe na watu wa mahali pake, kwa fedha, na dhahabu, na mali, na wanyama, zaidi ya vitu vitolewavyo kwa hiari ya mtu, kwa ajili ya nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu

Mungu huyo  huyo ndiye aliyemfanya mfalme Nebukadreza kuwa na moyo mkatili ili awachukue watu wake utumwani kwasababu ya makosa yao.(Yeremia 27:6, 43:10)

Mungu anaweza kuwatumia watawala kuadhibu taifa, au kuwabariki watu wake. Hii ni kuonyesha kuwa hakuna tawala yoyote katika hii dunia inamilikiwa na fikra za mwanadamu asilimia 100, bali mengi ya mashauri ya wakuu hutoka juu mbinguni, au yameruhusiwa na Mungu. Wao ni kama maji tu yanayofuata mkondo wa kusudi la Mungu.

Ndio jambo ambalo Mungu alimwambia Mfalme Nebukadreza kwamba “aliye juu ndiye anayetawala”(Danieli 5:21) lakini yeye alidhani ni uongo, mpaka siku alipoondolewa kwenye ufalme wake kwa miaka 7, na kurudishwa baadaye.

Hivyo, jambo hili, sio tu la viongozi wa kidunia, lakini pia hata wa kanisani. Ikiwa kanisa ulilopo linasimamia kweli na utakatifu na Kristo Yesu ndio kiini cha fundisho lao, basi waheshimu sana viongozi wako, kwasababu si kila shauri linalotoka kwenye vinywa vyao, ni wao wamefikiria. Wao ni kama maji tu yaliyomwagwa kwenye mfereji, ili kukuongoza wewe. ukishandana nao, au ukipuuzia kuongozwa nao, wakati mwingine unapingana na maamuzi ya Mungu wako bila kujijua.

Waheshimu viongozi wako wanaokulea kiroho, kama vile unavyowaheshimu watawala ya kidunia.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

TENGENEZA MAMBO YA NYUMBA YAKO.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu katika mafundisho ya Neno la Mungu.

Ni vema tukafahamu tarajio la Mungu kwa kila mwanadamu ni lipi kabla ya kumaliza mwendo wake hapa duniani. Utaona kipindi kile kabla mfalme Hezekia hajafa, Neno la Mungu lilimjia kwa kinywa cha Nabii Isaya na kumwambia, atengeneze mambo yake, kwasababu kifo chake kimekaribia.

Isaya 38:1 Siku hizo Hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na Isaya nabii, mwana wa Amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona

Kwanini Mungu hakumwambia, “pumzika sasa usihangaike-hangaike” kwasababu kipindi si kirefu utaenda kufa? Lakini anamwambia “TENGENEZA”, mambo yako.

Mungu alijua kabisa  nyenzo pekee ya kuwa salama kule ng’ambo ya pili ni kutengeneza sasa mambo yako angali unaishi.

Inasikitisha kuona, watu wengi, wanaishi tu hohe-hahe, wakihubiriwa habari za wokovu, wanakuwa wepesi kusema, ‘siku moja nitaokoka!’ . Wakidhani kuwa mbinguni ni kuingia kama vile mtu aingiavyo kwenye basi/daladala, ambapo siku hiyo hiyo atakata tiketi, na siku hiyo hiyo utasafiri.

Mbingu ina maandalizi. Na maandalizi yake ni hapa duniani, ukiyakamilisha hayo utaonekana umestahili kuingia mule. Bwana anatazamia si tu Uokoke, halafu basi.  anatazamia pia Uache Urithi wa rohoni kwa vizazi vingine, huko ndiko kutengeneza mambo ya nyumbani mwako.  Kama vile tu mtu mwenye busara ambaye anajua anapokaribia kufa ni sharti aache urithi kwa watoto wake. Lakini kama hana urithi atawaachia nini?.

Lazima ujue umewekwa na Mungu pia umzalie matunda. Kwahiyo usiwe na amani kuondoka duniani, kienyeji-enyeji tu, anza kutengeneza wokovu wako leo, uwe na faida kwenye ufalme wa mbinguni. Hata utakapofika kule Bwana aone, ile talanta aliyokupa walau imeongeza jambo Fulani katika ufalme wa Mungu duniani.

Mathayo 25:20  Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida. 21  Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. 22  Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida. 23  Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. 24  Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya; 25  basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako. 26  Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; 27  basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake. 28  Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. 29  Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa. 30  Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno

Je! Mali zako, vitu ulivyo navyo, elimu yako, ujuzi wako, karama yako, vina sehemu gani katika kuundeleza ufalme wa Mungu?.  Kama mtu uliyeokoka Je! Moyo wako kimaombi upo wapi?, Usomaji wako wa Neno umeufichia wapi?. Ukuaji wako wa kiroho umekwama wapi. Tusijione salama katika hayo mazingira na angali muda unakwenda. Ipo hatari, tusipoyatengeneza maisha yetu ya kiroho. Upo wa kusimama mbele ya kiti cha enzi cha hukumu, ambapo kila mmoja atatoa hesabu ya mambo yake mwenyewe.

Hivyo huu ni wakati wetu kila mmoja kujitathimini ndani, kwasababu hapa duniani ni wapitaji tu, hatuna maisha marefu, hujui ni lini utaondoka, au Bwana atarudi lini. Tufahamu tu huko tuendako kama hatujajitengeneza vema sasa, kuingia haiwezekani.

Bwana atupigishe hatua.

Shalom.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

ANGALIA JINSI USIKIAVYO:

TENGENEZA  NYAVU ZAKO, OSHA NYAVU ZAKO.

BASI NIKAOGOPA, NIKAENDA NIKAIFICHA TALANTA YAKO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 14 (Yoeli, na Obadia).

Rudi nyumbani

Print this post

SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.

(Jihadhari na Marashi)

Si mambo yote yanayokubalika katika jamii basi yanafaa kwa mkristo.. Si mambo yote yanayokubaliwa na wengi basi yanafaa..ni muhimu kuchuja kila tunaloambiwa au tunayokutana nalo, kabla ya kulikubali, ndivyo biblia inavyotufundisha.

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.

Mojawapo ya jambo ambalo ni muhimu kuchukua nalo tahadhari ni “Matumizi makali ya marashi”. Unapojipulizia marashi ambayo mtu aliye mita 10 mbali nawe anayasikia, basi fahamu kuwa upo katika hatari kubwa sana.

Utauliza kivipi au kwa namna gani? Hebu turejee katika maandiko kidogo..

Utakumbuka ile habari ya yule mwanamke aliyemmiminia Bwana marhamu ya thamani nyingi mwilini mwake, na maneno Bwana Yesu aliyoyasema kuhusu kazi ya ile marhamu aliyomiminiwa?. Biblia inasema marhamu ile ilikuwa ni ya thamani kubwa, maana yake yenye kunukia sana na kwa eneo kubwa, kiasi kwamba mtu aliye mbali anaweza kuisikia harufu ya marhamu ile.

Tusome

Marko 14:3 “Naye alipokuwapo Bethania, nyumbani mwa Simoni mkoma, ameketi chakulani, alikuja mwanamke mwenye KIBWETA CHA MARHAMU YA NARDO SAFI YA THAMANI NYINGI; akakivunja kibweta akaimimina kichwani pake.

4  Palikuwa na watu waliochukizwa katika nafsi zao wakisema, Kwani kupoteza marhamu namna hii?

5  Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa dinari mia tatu na kuzidi, wakapewa maskini. Wakamnung’unikia sana yule mwanamke.

6  Yesu akasema, Mwacheni; mbona mnamtaabisha? Amenitendea kazi njema;

7  maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamnami sikuzote.

8  Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu MARHAMU KWA AJILI YA MAZIKO”.

Umeona hapo?.. wakati huyu mwanamke anadhani Marhamu ile ingeweza kumfanya Bwana anukie vizuri mbele za watu na aonekane mtanashati.. lakini Bwana aliyaona yale manukato tofauti na mwanamke alivyoyaona, Bwana Yesu aliona hayafai kwa utanashati, bali kwa MAZIKO!.

Lakini kwasababu mwanamke alikuwa na nia njema ya kutubu na kumthaminisha Bwana ndio maana akapata kibali kwa muda ule, lakini Ujumbe tayari tumeachiwa, “kuwa marhamu kama hizo ni kwaajili ya maziko” so kwaajili ya utanashati.

Hiyo ikimaanisha kuwa kumbe kuna vitu tunaweza kuvipaka mwilini, au kuvivaa, na kumbe ni malighafi za MAUTI, Na KIFO!!. Ijapokuwa kwa nje tunaweza kuonekana watanashati na tunaovutia, lakini kumbe tumejipaka au tumekivaa kifo!.

Bwana Yesu angeweza kuwaambia wale watu kuwa marhamu ile amepakwa kwa kuwekwa tayari kukutana na mkutano ili kwamba wasikie harufu nzuri itokayo mwilini mwake, kwani bado alikuwa na siku kadhaa za kuhubiri mbele za watu kabla ya kufa, lakini wala yeye hakuziona hizo siku bali aliona marhamu ile inafaa kwa matumizi ya MAZIKO! Na si utanashati kama wengine wote walivyotazamia.

Mama/dada jiulize hayo marashi unayojipulizia mwilini mwako je unajiweka tayari kwa nini?..je kwaajili ya maziko yako??..

Na asilimia kubwa ya watu wanaotumia marashi makali ni lazima wanakuwa wanasumbuliwa na roho za mauti au uasherati… hivyo ni muhimu kuchukua tahadhari ya kiroho! Na si kila kitu kuiga kwasababu tu, tumeona ni kitu chenye kukubalika kila mahali.

Mama/dada Kama unatamani kujipamba basi jipambe kwa mapambo ya kibiblia, ambayo ndiyo yale yanayotajwa katika 1Timotheo 2:9 na 1Petro 3:3.

1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; YAANI, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.

6  Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada zinazoendana:

Mafundisho mengine:

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

Mawaa ni nini? Kama tunavyosoma katika biblia?

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUISHINDA HALI YA MSONGO WA MAWAZO.

Msongo wa mawazo ni nini? Ni shinikizo au mfadhaiko wa kiakili, unaomkumba mwanadamu, pale anapokutana  na  matatizo, au taabu, au dhiki au shida Fulani. Hivyo inapotokea mtu huyu anashindwa kuzitatua changamoto hizo, ndipo msongo huo huja.

Kwamfano labda mtu amegundulika, ana ugonjwa usiotubika, na kaambiwa na daktari hawezi kupona, mtu kama huyu ni rahisi kukumbwa na msongo wa mawazo,

Au labda mwingine  hana kazi na akiangalia familia inamtegemea, na bado hajafikia malengo yake kulinganisha na umri alionao, moja kwa moja mtu kama huyu ni rahisi kukumbwa pia na msongo wa mawazo. N.k.

Na kama tiba isipopatikana matokeo yake yanaweza kuwa mtu huyo, kupata matatizo ya kiafya, wengine kuchanganyikiwa, wengine kujitenga na watu, wengine kujifungia ndani kulia tu usiku kucha, wengine kutenda vitendo viovu,hata kujiua.

Je! Mkristo anaweza kuwa na msongo wa kimawazo? Jibu ni ndio anaweza kuwa nao. Lakini tiba imeshatolewa. Tutaona katika somo hili kwa namna gani, kwasababu yawezekana wewe ni mmoja wapo ambaye unakutana na hali hii na hujui cha kufanya.

Embu tuone kwanza baadhi ya watu katika maandiko ambao walipitia misongo ya mawazo

1) Eliya:

Eliya wakati amemaliza kuwaua manabii wa Baali, akatazama huku na huku na kujiona kama ni yeye peke yake ndiye nabii wa Mungu aliyebaki, hivyo ikampelekea ajitenge, na kukimbilia jangwani, akae huko mpaka afe.  Lakini Mungu alikuja kumtokea baada ya siku 40, akampa majibu ya faraja, kwamba asidhani yupo peke yake kuna wengine 7,000 amejisazia, rudi Israeli, kanitumikie.(1Wafalme 18-19)

2) Mfalme Daudi.

Alikumbwa mara nyingi na msongo wa mawazo katika maficho yake alipokuwa anawindwa na mfalme Sauli. Mara nyingi alifikia hatua ya kukata tamaa ya maisha. Embu tafakari haya maneno aliyoyasema Daudi.

Zaburi 69:1 Ee Mungu, uniokoe, Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu.  2 Ninazama katika matope mengi, Pasipowezekana kusimama. Nimefika penye maji ya vilindi, Mkondo wa maji unanigharikisha.  3 Nimechoka kwa kulia kwangu, Koo yangu imekauka. Macho yangu yamedhoofu Kwa kumngoja Mungu wangu.  4 Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua.  5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu, Wala hukufichwa dhambi yangu

3) Ayubu

Baada ya kupotelewa na mali zake, na watoto wake, hadi mwili wake kubaki mifupa tu. Mkandamizo ulimjia. Ayubu anasema;

Ayubu6:2 Laiti uchungu wangu ungepimwa, Na msiba wangu kutiwa katika mizani pamoja!  3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa bahari; Kwa hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka

 Mpaka akanza kusema maneno magumu, ya kulaana siku aliyozaliwa. Mtu kama huyu alikuwa katika hali mbaya sana kifikra na kiakili.

4) Petro

Petro na Yuda walipitia jambo moja, kukana na kusaliti, ni dhambi pacha. Isipokuwa Yuda alikwenda kujinyonga kwasababu msongo wa mawazo ulimshinda, lakini Petro hakujinyonga. Yeye alikwenda kujificha na kulia sana kwa “majonzi”.  Tengeneza picha ni wewe unamkana Mungu wako, tena kwa maneno ya dhihaka mbele za watu. Hali hiyo unadhani itakufanya ujionaje kama sio mateso ya kiakili baada ya hapo?. Wengine wanapitia hali kama hizi, wanapojiona wamemtenda Mungu dhambi kubwa sana, isiyosameheka, wakidhani kuwa Mungu hawajali tena, hawathamini.(Mathayo 26:75)

5) Mitume 11.

Baada ya Bwana Yesu kufa, hofu ya wayahudi ikawavaa mitume, wakiona kuwa wao ndio wanaofuata kuuliwa baada ya kiongozi wao kufa.. Hivyo hiyo ikawapelekea kujifungia ndani, wasitoke. Msongo mkubwa sana wa mawazo uliwavaa, kutoka kwa wayahudi.(Yohana 20:19-29)

Itoshe tu kutumia mifano hiyo michache, kwani wapo wengine wengi sana katika biblia waliopitia hali kama hizi, mfano ni Musa, Yusufu, Yeremia, Nebukadreza, Hana(mamaye Samweli),  Danieli, Mtume Paulo wote hawa ukisoma habari zao katika biblia utayathibitisha hayo.

Lakini Je! Waliwezaje kuzishinda hizo hali.

Utagundua, walipopotia taabu zao, walilikumbuka TUMANI la Mungu. Ndilo lililowapa nguvu ya kuweza kuvuka nyakati hizo mbaya walizozipitia.  Waliyazingatia haya maneno;

1Petro 5:6  Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; 7  HUKU MKIMTWIKA YEYE FADHAA ZENU ZOTE, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

Na lile alolilisema Yesu..

Mathayo 11:28  Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha

Pale akili zilipogoma, fikra kuzima, moyo kuwa baridi, walijifunza kumtwika Mungu, huzuni zao, mateso yao, shida zao. Hata pale ambapo hazikutatulika kwa wakati walioutarajia, lakini waliendelea na mwisho wa siku Bwana alikuja kuyaweka yote sawa. Kwasababu yeye mwenyewe alisema.

Yeremia 29:11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi TUMAINI siku zenu za mwisho

Hivyo ndugu, ikiwa na wewe upo katika hali hii ya msongo wa kimawazo, katika eneo lolote lile, iwe la kiroho, kihuduma, kifamilia, kikazi, kiafya, kimaendeleo. Umeshindwa kuendelea mbele, Usiogope. Kwa Mungu lipo TUMAINI, zaidi ya Matumaini yote ya kibinadamu.

Haijalishi msongo huo, umekupata kutokana na dhambi zako, au kutokana na hali zilizo nje ya uwezo wako. Usiogope. Mponyaji, mfajiri, mtatuaji wa matatizo yupo. Huyu si mwingine zaidi ya YESU KRISTO mwokozi.

Mungu akikupa tumaini, ujue ni lazima litokee, lakini mwanadamu akikupa tumaini, ni kusudi tu kukufariji, lakini tatizo linaweza kubaki palepale.  Yesu hayupo hivyo. Mtazame tu yeye. Wakati wa shida, ndio wakati wa kukimbilia chini ya mbawa zake, sio kuwakimbilia wanadamu.

JE! UFANYEJE?

  1. Katika hali hiyo, Usiache kuomba sana  & Kumsifu Mungu & Kushukuru, siku zote za maisha yako. Ongeza kiwango chako katika eneo hili.
  2. Soma sana Biblia: Utapata faraja ya Roho katika uwezo wa Mungu aliowatendea wengine.
  3. Usiwe mtu wa kutanga-tanga sana. Tuliza akili zako, si lazima utafute ushauri kwa kila mtu, jiachie kama vile huna tatizo lolote, ukimkabidhi Bwana yote, ukijua yeye yupo kazini.
  4. Kila wakati Jiambie, “Mungu wangu atayaweka yote sawa mwisho wa siku”.
  5. Mawazo ya kushindwa/kujihukumu yanapokuja yapinge.  Sema “Bwana ndiye boma langu na ngome yangu, na mwamba wangu sitatikisika”.

Na hakika, katika muda fulani, utaona Mungu anakuvusha, anakuponya, anakufariji, anakuondolea huo mzigo. Huo ni uhakika sio makisio. Usiache tu kuendelea na Bwana..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Mafundisho Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

TUMAINI NI NINI?

UKIOKOKA,HIZI FIKRA ZIKIJA NDANI YAKO, ZIKATAE.

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post