Category Archive maswali na majibu

Je! Sulemani alienda mbinguni?

JIBU: Jibu ni ndio.

Kosa alilolifanya Sulemani la kushawishiwa na wake zake kuwajengea madhabahu miungu, (1Wafalme 11:3:13) maandiko hayatuthibitishii kuwa lilikuwa ni endelevu, kana kwamba alimwacha Mungu moja kwa moja, hapana, au alitenda dhambi isiyosameheka kabisa hapana. Ni wazi kuwa Sulemani alitubu, kwa kosa lile, tunaposoma kitabu cha Mhubiri ambacho alikiandika katika uzee wake, kinatupa picha ya mambo mengi ambayo aliyatenda au aliyadhania kuwa ni sawa lakini mwisho wake akagundua ni ubatili ni sawa na kuufuata upepo. Na ndio maana mwisho kabisa akahitimisha, kuwa jumla ya yote yampasayo mtu ni kumcha Bwana na kuepukana na uovu. Kuonyesha kuwa Sulemani aligundua usahihi upo wapi, kabla hajafa.

Lakini pia asingetajwa katika vizazi vya ukoo wa  Bwana Yesu kama angekuwa ni mmojawapo wa waliopotea. Hivyo hatuwezi kusema kuwa Sulemani alikwenda kuzimu, hata kama hakuna maandiko ya moja kwa moja yanayoonyesha mahali alipotubu.

Kikubwa tujifunze katika kosa alilolifanya. Maandiko yanasema kutii ni bora kuliko dhabihu. Kama Sulemani angetii agizo la Bwana la kutokuoa wanawake wa-kimataifa, hayo yote yasingemkuta. Lakini alidhani kwa hekima zake kuwa nyingi asingeweza kudanganyika. Ndio alikuwa mjanja mwanzoni katika ujana wake, lakini sekunde za mwisho za uzee wake shetani alimpiga mweleka. Zipo dhambi ambazo shetani anakuandalia uzitende baadaye, lakini maandalizi yake anayatengeneza sasa.  Tii kila agizo la Mungu, hata kama ni dogo kiasi gani, hata kama litaonekana ni jepesi kulishinda kiasi gani sasa, wewe tii, kwasababu Mungu anaona mbele wewe unaona hapa. Simama katika Neno, sio katika mitazamo yako, ndipo utakapoweza kumshinda shetani, ikiwa wenye hekima kama hawa walinaswa katika tundu bovu wewe ni nani usinasike pindi unapolipuuzia Neno la Mungu linalokusemesha moyoni mwako uache hiyo tabia au hiyo dhambi?.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

SHAMBA HUWA HALIMTAMBUI WALA KUMSUBIRIA MKULIMA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?

Nchi ya Nodi ambayo Kaini alikimbilia ndio nchi gani kwasasa?(Mwanzo 4:16).

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inamaana gani inaposema ‘tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao’?

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema ‘tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao’? Mhubiri 3:11


JIBU:

Mhubiri 3:11 “Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho”

Mwanadamu alivyoumbwa ni tofauti na wanyama au viumbe hai vingine.  Kwani vyenyewe tangu vilipoumbwa mpaka sasa havibadiliki, wala haviendelei, kimaarifa, kiuelewa, au kiujuzi.. Lakini sisi wanadamu kila siku ndani yetu kuna kiu  ya kujua zaidi na zaidi, kufahamu zaidi na zaidi, kutafuta zaidi na zaidi, kutokuridhika hata kama tumepata.. Na hiyo ndiyo inayotupelekea kupiga hatua mpya kila leo. Sasa hiyo hali isiyokoma ndani yetu ndio inayoitwa UMILELE.

Na Mungu ameiruhusu iwepo ndani ya mwanadamu, kuvumbua, mambo mapya, tangu zamani hata sasa, na anafanya bidii kutafuta akidhani labda atafikia ukomo anaoutazamia, lakini kila kunapokucha ndipo anapogundua kuwa bado sana kuyaelewa mambo ya Mungu. Wanadhani pengine kwa kugundua ndege, ndio itawafikisha mbinguni, lakini kumbe, ndio wanaona anga halina mwisho.

Maana yake ni kuwa, hata milele yote ya maisha, au ya maarifa, au ya uvumbuzi kamwe hatutakaa tummalize Mungu. Yatosha sisi kukaa katika pendo lake, kuyatenda mapenzi yake katika Kristo Yesu,. Lakini tusipoteze nguvu zetu kumtafiti Mungu, ni heri tutumie hizo kuutafiti utukufu wake ili tumwabudu kuliko kuzitafiti njia zake, au kanuni zake alizojibunia, tutapoteza muda.

Sulemani alisema..

Mhubiri 8:17 basi, niliiona kazi yote ya Mungu, ya kuwa haitafutikani na mwanadamu kazi inayofanyika chini ya jua; kwa sababu mwanadamu na akijisumbua kadiri awezavyo kuitafuta, hata hivyo hataiona; naam, zaidi ya hayo, mwenye hekima ajapodhania ya kuwa ataijua, lakini yeye hataweza kuiona.

Dumu katika mapenzi yake Mungu, tunayojifunza kupitia biblia, kwani hilo ndio FUNGU letu tulilowekewa.

Ndio maana ya hilo Neno; Mhubiri 3:11 “Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho”

Je! Umeokoka? Je! Unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho, na Kristo yupo mlangoni kurudi? Umejiandaaje? Tubu mgeukie Bwana akuponye.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

SWALI: Biblia ilimaanisha nini iliposema Kaini ‘Akatoka mbele ya uso wa Bwana’. Kutoka kule kulimaanisha nini?


JIBU: Tunaona baada ya Kaini kumuua ndugu yake Habili kwa wivu, ambao ulizuka baada ya sadaka yake kukataliwa na ya ndugu yake kukubaliwa. Mungu alimsemesha, na kumweleza laana yake itakayompata baada ya pale. Lakini mwisho wa maneno yale, Tunaona Kaini anaonekana akitoka mbele ya uso wa Bwana. Maana yake ni nini?

Tusome.

Mwanzo 4:9 “Bwana akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu? 

10 Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.  11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;  12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. 

13 Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.  14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua. 

15 Bwana akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. Bwana akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga.  16 Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni”

Alitokaje?

Kutoka mbele ya uso wa Bwana hapo, sio Kuahirisha mazungumzo yaliyokuwa yanaendelea baina yake yeye na Mungu hapana. Bali ni kumwacha Mungu moja kwa moja. Yaani kwa ufupi mkataba wake na Mungu aliumalizia pale. Hakuna cha dhabihu tena wala sadaka, wala kumwomba Mungu, wala kujihusisha na tendo lolote la kiibada. Akaanza kujishughulisha na mambo ya kidunia tu, na sayansi, na utafiti na uvumbuzi, na akafanikiwa sana katika bidii yake hiyo, yeye na uzao wake wote, wakawa watu hodari duniani, lakini waovu sana (Soma Mwanzo 4:20-22). Na hawa ndio waliopelekea gharika kuletwa duniani.

Tofauti na uzao wa Adamu kwa Sethi, wao waliendelea kuwepo mbele ya uso wa Bwana, wakitaka fadhili na rehema kwa Mungu daima,wakiliitia jina lake.

Mwanzo 4:25 “Adamu akamjua mke wake tena; akazaa mwana mwanamume, akamwita jina lake Sethi; maana alisema, Mungu ameniwekea uzao mwingine mahali pa Habili; kwa sababu Kaini alimwua.  26 Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kuliitia Jina la Bwana”.

Mpaka sasa makundi haya mawili yapo duniani. Lipo ambalo halina habari na Mungu,(Ambao ndio uzao wa Kaini rohoni) bali mambo ya kidunia tu, na limefanikiwa sana katika hayo, ni jepesi katika uvumbuzi na utafiti, lakini  Mungu kwao ni kama historia za mababu wa kale, ni kama vile mashariki na magharibi zilivyo mbali. Lakini sisi hatupaswi kufanana wa watu hao. Bali kama Watoto wa Adamu kwa Sethi. Furaha yetu ipo katika Bwana. Tegemeo letu ni yeye, na nguvu zetu ni yeye, haijalishi tutakosa vyote au tutapata vyote. Yeye ndiye atakayekuwa urithi wetu milele.

Je! Wewe upo kundi lipi?   Uthibitisho ni maisha yako ulipoyaelekeza.

Hizi ni nyakati za mwisho. Kristo anarudi. Tubu mgeukie Bwana, mtafute yeye.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Bustani ya Edeni ipo nchi gani?

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

Rudi nyumbani

Print this post

Petro na Adrea waliitwa na Bwana wakati gani?

Swali: Katika kitabu cha Luka 5:1-7 tunaona kuwa Bwana Yesu aliwakuta Petro na Andrea ufukweni na akawaita, lakini tukirejea kwenye Yohana 1:35-42 tunasoma kuwa aliwaita wakati wapo kwa Yohana Mbatizaji?.. Je biblia inajichanganya?

Jibu: La! Biblia haijichanganyi hata kidogo, vinginevyo kitabu chote kitakuwa cha uongo!.. Lakini kwasababu ni kitabu cha kweli,  basi kamwe hakiwezi kujichanganya!.

Kabla ya kuichambua mistari hiyo hebu tuisome kwanza..

Luka 5:1 “Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,

2  akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, lakini wavuvi wametoka, wanaosha nyavu zao.

3  Akaingia katika chombo kimoja, NDICHO CHAKE SIMONI, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni.

4  Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.

5  Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, TUMEFANYA KAZI YA KUCHOSHA USIKU KUCHA, TUSIPATE KITU; LAKINI KWA NENO LAKO NITAZISHUSHA NYAVU.

6  Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika”

Hapa ni kweli Bwana aliwakuta Andrea na Petro baharini wakivua samaki.. Lakini katika kitabu cha Yohana tunasoma habari nyingine tofauti kidogo..

Yohana 1:35 “Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake.

36  Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!

37  Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.

38  Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?

39  Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi.

40  ANDREA, NDUGUYE SIMONI PETRO, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.

41  HUYO AKAMWONA KWANZA SIMONI, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo).

42  Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe)”.

Uhalisia ni kwamba Bwana Yesu alikutana na Adrea na Petro kwa mara ya kwanza kipindi wanatoka kwa Yohana Mbatizaji, lakini Bwana Yesu hakuwaambia wamfuate, (yaani wawe wanafunzi wake)!.. Lakini kwa tukio lile tayari walikuwa wameshafahamiana na Bwana.

Sasa tunapokuja katika tukio la kule baharini, ndipo Kristo anawaambia waache Nyavu zao wamfuate na yeye atawafanya kuwa wavuvi wa watu badala ya kuwa wavuvi wa samaki.

Kwahiyo  katika tukio hili la pili ni wazi kuwa tayari Petro na Andrea walikuwa wanamjua Bwana, Ndio maana tunaona hata haikuwa ngumu kwa Petro kumkubalia Bwana akitumie chombo chake katika kuwafundisha makutano (Na Bwana anaonyesha kama kuwa na ujasiri wote katika kutumia chombo cha Petro na kumpa maagizo kana kwamba tayari wanajuana).. na ndio maana pia tunaona haikuwa ngumu kwa Petro kumwamini Bwana na kwenda kushusha nyavu kwa neon la Bwana.. kwasababu tayari alikuwa anamjua, walishakutana huko nyuma..

Kwahiyo hakuna mkanganyiko katika habari hizo, isipokuwa ni waandishi wawili wamenukuu matukio mawili tofauti.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Yakobo na Yohana waliitwa “Wana wa Ngurumo”?

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?

Je Bwana Yesu aliruhusu wanafunzi wake kubeba Fimbo au hakuwaruhusu? (Marko 6:8 na Mathayo 10:10).

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.

SWALI: Mstari huu unamaana gani? Mithali 19:21 Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.


JIBU: Kila moyo wa mwanadamu, unamatamainio mengi, lakini uhalisia ni kwamba sio matamanio yote ni ya ukweli au yanania nzuri baadaye, kwamfano mtu atataka mali nyingi, lakini moyo wake unasema atakapopata nyumba kubwa na gari atawakomoa waliomdharau, atalipiza kisasi, atafanya anasa ,atatembea kwa majigambo, ataongeza Masuria.

Na  ndio maana mengi ya malengo kama haya yawezi kusimama kwa watoto wa Mungu, kwasababu yana hila nyingi nyuma yake. Mtume Yakobo aliliweka wazi jambo hili, ni kwanini wakati mwingine hatupokei majibu ya maombi yetu alisema..

Yakobo 4:2  “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! 3  Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”

Lakini kinyume chake anasema Shauri la Bwana ndilo litakalosimama. Maana yake ni kuwa Hekima ya Bwana inayopima  haya yote imaamua cha kutoa na kutokutoa. Hivyo si matamainio yako yote unayoyaona ni mema, basi yatakuwa mema pia mbele za Mungu, mengine yana udaganyifu mwingi. Ndio maana Yeremia 17: 9 inasema “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua”?

Hivyo tuombapo jambo ni busara kumalizia na kusema “Bwana mapenzi yako yatimizwe”.

Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala Mwangalie sana

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)

JIFUNZE KUDUMU UWEPONI MWA MUNGU.

Je ni kweli Yuda hakuwa na dhambi kwa kumsaliti Bwana, kwasababu tayari ilikuwa imeshatabiriwa?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Abramu aliondoka Harani kabla au baada ya kifo cha baba yake?.

Swali: Maandiko yanatuonyesha Tera, baba yake Abramu aliishi jumla ya miaka 205 (Mwanzo 11:32) na tena yanaonyesha kuwa Tera alimzaa Abramu akiwa na miaka 70 (Mwanzo 11:26), na ukirudi kwenye Mwanzo 12:4 biblia inatuonyesha tena Abramu alitoka nchi ya Harani alipofikisha miaka 75.

Sasa ukipiga mahesabu vizuri utaona miaka aliyoishi Tera baba yake Abramu isingepaswa iwe 205, bali iwe miaka 145 yaani (70+75=145) kama Abramu aliondoka kwelii Harani baada ya kifo cha babaye! , Lakini tunaona biblia inatuambia umri wa Tera ulikuwa ni miaka 205. (Je biblia inajichanganya!)

Jibu: Jibu ni kwamba Biblia haijichanganyi na wala haijawahi kujichanganya, vinginevyo ingekuwa ni kitabu cha uongo!. Lakini tunaona maneno yaliyomo ndani ya biblia ni ya uzima tena yenye Nguvu.

Sasa tukirudi kwenye swali letu, je! Abramu alitoka Nchi ya Harani kabla au baada ya kufa baba yake? Jibu ni kwamba alitoka BAADA YA BABA YAKE KUFA!, Na si kabla!. Tunalithibitisho hilo Zaidi katika kitabu cha Matendo ya Mitume..

Matendo 7:2 “Naye akasema, Ndugu zangu na baba zangu, sikilizeni: Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Ibrahimu, alipokuwa katika Mesopotamia, kabla hajakaa Harani,

3  akamwambia, Toka katika nchi yako na katika jamaa zako, ukaende hata nchi nitakayokuonyesha.

4  Ndipo alipotoka katika nchi ya Wakaldayo, AKAKAA HARANI, AKATOKA HUKO BAADA YA KUFA BABAYE, Mungu akamhamisha mpaka nchi hii mnayokaa ninyi sasa.

Sasa kama ni hivyo kwanini hesabu ya miaka haikai sawa..badala ya  miaka 145 anaonekana kufa akiwa na miaka 205?.

Jibu ni kwamba Tera hakumzaa Abramu akiwa na miaka 70, bali maandiko yanasema alipofikisha umri wa miaka 70 akamzaa Abramu, Nahori na Harani. (watoto watatu).

Mwanzo 11:26 “Tera akaishi miaka sabini, akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani”. 

Maana yake ni kwamba watoto hawa watatu walianza kuzaliwa  baada ya Tera kufikisha miaka 70, na si kwamba wote watatu walizaliwa ndani ya mwaka mmoja, bali walizaliwa katika vipindi tofauti tofauti pengine walipishana miaka mitano mitano au hata kumi kumi au hata Zaidi ya hapo, lakini Tera alipofikisha miaka 70 ndipo alipoanza kuzaa!

Sasa swali la msingi hapa ni mtoto yupi aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa na yupi aliyekuwa wa mwisho kati ya hao watatu..

Katika hiyo Mwanzo 11:26 tunaona Abramu akitajwa wa kwanza, sasa hiyo haimaanishi kuwa yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa!!.. Orodha hiyo imetajwa kufuatia heshima ya watu hao na si ukubwa!.. Abramu ndiye aliyetukuka mbele za Mungu Zaidi ya hao ndugu zake wawili ndio maana kawekwa hapo wa kwanza..kwasababu habari inayoendelea itamhusu yeye yeye na uzao wake.. hiyo ndio sababu ya yeye kutajwa wa kwanza na si nyingine.. Lakini kuhalisia aliyekuwa mkubwa kuliko wote pale ni Harani.

Tunajuaje Harani ndiye aliyekuwa mkubwa kuliko Abramu na Nahori?…

Kwanza Abramu alisafiri na Lutu, ambaye alikuwa ni mtoto wa Harani kaka yake.. Na wakati huo tayari Lutu alikuwa mtu mzima kipindi anasafiri na Abramu (Mwanzo 12:5)… Pili Abramu na Nahori aliyetajwa wa pili kwenye orodha alimwoa mtoto wa Harani kaka yake.

Mwanzo 11:29 “Abramu na Nahori wakajitwalia wake. Jina la mkewe Abramu aliitwa Sarai, na jina la mkewe Nahori ALIITWA MILKA, BINTI HARANI, ambaye alikuwa baba wa Milka na wa Iska”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Abramu hakuwa mtoto wa kwanza wa Tera bali huenda alikuwa wa pili au wa tatu, Harani ndiye aliyekuwa wa kwanza ingawa kwenye orodha ameonekana wa mwisho…na Tera hakumzaa Abramu akiwa na miaka 70 bali akiwa na miaka 130. Na Abramu aliondoka Harani alipofikisha miaka 75 baada ya kifo cha baba yake, ambaye alikufa akiwa na miaka 205.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! biblia inajichanganya katika 1Petro 2:13 na Matendo 5:29.

Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)

WEWE U MUNGU UONAYE.

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

Je Ni kweli haturuhusiwi kula nyama kulingana na Isaya 66:3?

Rudi nyumbani

Print this post

Waliouawa Shitimu kwa pigo walikuwa ni watu Elfu 23 au elfu 24?.

Swali: Napenda kujua je!, idadi ya Wana wa Israeli waliouawa kwa pigo kule Shitimu ilikuwa ni Elfu 23 au elfu 24?..maana sehemu moja tunaona biblia inataja watu elfu 23 (1Wakorintho 10:8) na sehemu nyingine Elfu 24, (Hesabu 25:9) je biblia inajichanganya?.

Jibu: Biblia haijichanganyi sehemu yoyote kwasababu sio kitabu cha Uongo, bali ni kitabu kilichojaa maneno ya uzima wa Mungu, na ya kweli.

Sasa ili tuielewe vizuri tuisome habari yenyewe kuanzia ule mstari wa kwanza wa kitabu hicho cha Hesabu 25

Hesabu 25:1 “Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu; 2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.

3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.

4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.

5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal peori.

6 Na tazama, mtu mmoja miongoni mwa wana wa Israeli akaja na kuwaletea nduguze mwanamke Mmidiani mbele ya macho ya Musa, na mbele ya macho ya mkutano wote wa wana wa Israeli, hapo walipokuwa walia mbele ya mlango wa hema ya kukutania.

7 Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake;

8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli.

9 Nao waliokufa kwa hilo pigo walikuwa WATU ELFU ISHIRINI NA NNE HESABU YAO

Hapa tunaona ni watu elfu 24 waliokufa kwa pigo hilo… lakini tunaona idadi nyingine tofauti ikitajwa katika kitabu cha Waraka kwa wakorintho.

1Wakorintho 10:8  “Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, WAKAANGUKA SIKU MOJA WATU ISHIRINI NA TATU ELFU”.

Sasa je! Biblia inajichanganya? Jibu ni La!

Ukweli ni kwamba idadi ya waliokufa kwa pigo ni watu elfu 24 na si elfu 23 lakini kwanini Paulo katika hiyo 1Wakorintho 10:8 aseme ni elfu 23?

Ni lazima uangalie ni nini Paulo alichokuwa anajaribu kukupitisha kwa watu wa wakorintho, Lengo na Nia ya Paulo ilikuwa ni kuwaonyesha madhara ya Uasherati, jinsi unavyoweza kuleta madhara makubwa ndani ya kipindi kifupi!.

Sasa hapa Paulo anasema walianguka watu elfu 23 “KATIKA  SIKU MOJA”. Ikiwa na maana kuwa huwenda lile pigo lilienda Zaidi ya “siku moja” . Huwenda lilidumu siku mbili au Zaidi ya hapo! Ndipo likakoma!.. lakini katika ile siku moja tu ya kwanza walianguka watu elfu 23 (hiyo ni idadi kubwa sana)…na idadi ya wote waliokufa mpaka siku ya mwisho pigo lilipokoma ilikuwa ni watu elfu 24.

Sasa Paulo anajaribu kuwaonya Wakorintho jinsi uasherati unavyoweza kuleta madhara makubwa ndani ya kipindi kifupi kuliko wanavyodhania, kama ilivyokuwa kwa hawa wana wa Israeli walivyozini na wanawake wa Moabu..

Ndio maana tukirudi nyuma kidogo kwenye kitabu hicho hicho, mlango ule wa 6 utaona jinsi Paulo anavyoelezea ubaya wa dhambi ya uasherati..kwamba ni mbaya  Zaidi ya dhambi zote mtu anazoweza kuzifanya katika mwili…

1Wakorintho 6:15 “Je! Hamjui ya kuwa MIILI YENU NI VIUNGO VYA KRISTO? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!

16  Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.

17  Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye.

18  Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ILA YEYE AFANYAYE ZINAA HUTENDA DHAMBI JUU YA MWILI WAKE MWENYEWE.

19  Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

20  maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.

Ni nini tunajifunza?

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni madhara ya Uasherati, wengi wanasema nikishafanya uasherati nitatubu tu!..pasipo kujua kuwa uasherati wa mara moja unaweza kuleta madhara makubwa ndani ya muda mfupi!ll…Wana wa Israeli walipomaliza kufanya dhambi hiyo ndani ya siku moja walikufa watu elfu23, nafasi ya kutubu hawakuiona..

Vile vile dhambi ya uasherati inaweza kukuharibia mambo yako mengi ndani ya siku moja. Inaweza kukuharibia maisha yako moja kwa moja ndani ya siku moja, inaweza kukupeleka kuzimu ndani ya siku moja, na inaweza kukuletea majuto makubwa ndani ya siku moja, Zaidi sana biblia inasema mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa.

Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.

Itaishindaje dhambi ya Uasherati?.. Je kwa kuomba tu? Jibu ni La!..bali kwa kuikimbia kama Yusufu alivyoikimbia..

1Wakorintho 6:18  “Ikimbieni zinaa..”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)

Kipaku ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Mhubiri 10:16 “Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana, Na wakuu wako hula asubuhi!”


Mstari huu umegawanyika katika sehemu mbili;

  1. Sehemu ya kwanza ya huu mstari inasema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana.
  2. Na ya pili ni hiyo, ikiwa wakuu wako hula asubuhi.

Tuitazame sehemu ya kwanza: mfalme kijana.

Hapo mhubiri anajaribu kueleza uhusiano uliopo kati ya uongozi na ukomavu wa mtu. Akatumia mfano wa kijana, kwasababu mara nyingi ni ngumu sana kuipata busara kwa vijana,  kutokana na kuwa hawana uzoefu mwingi wa maisha na pia hawajaandaliwa vya kutosha, kumudu nafasi za uongozi, kinyume chake kitakachowaongoza ni hisia tu za ujana na si vinginevyo. Na ndio maana mtu kama Sulemani alilitambua hilo alipotawadhwa tu mfalme akiwa bado kijana mdogo, alimwomba Mungu ampe hekima ya namna ya kuwaongoza watu wake. Na Bwana akamjalia.

1Wafalme 3:7 “Na sasa, Ee Bwana, Mungu wangu, umenitawaza niwe mfalme mimi mtumwa wako badala ya Daudi baba yangu; nami ni mtoto mdogo tu; sijui jinsi inipasavyo kutoka wala kuingia. 

8 Na mtumwa wako yu katikati ya watu wako uliowachagua, watu wengi wasioweza kuhesabiwa, wala kufahamiwa idadi yao, kwa kuwa ni wengi. 

9 Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?  10 Neno hili likawa jema machoni pa Bwana, ya kuwa Sulemani ameomba neno hili”

Walikuwepo pia wafalme wengine waliotawadhwa wakiwa wadogo kama Yoashi, lakini akasaidiwa na kuhani Yehoyada katika ufalme wake, na ukawa bora (2Wafalme 11-12)

 Lakini tunakuja kuona kwa mwanawe Sulemani aliyeitwa Rehoboamu. Yeye naye alikuwa ni kijana lakini hakutaka mashauri kwa wazee waliomtangulia, kinyume chake, akasikiliza mashauri ya vijana wenzake Hivyo ikapelekea ufalme wake kugawanyika, na kupoteza makabila kumi kati ya kumi na mbili ya Israeli.(Soma 1Wafalme 12:1-16)

Lakini sehemu ya pili ya mstari huu inasema Ole wako nchi ikiwa wakuu wako hula asubuhi.

Maana yake kwamba kuwa na viongozi ambao wanatanguliza maslahi yao kabla ya kazi, nchi hiyo sikuzote huishia pabaya. Sikuzote watu wanakwenda kufanya kazi asubuhi, wakitarajia kile walichokihangaikia kutwa nzima ndio wakifaidi jioni, lakini hapa tunaona ni kinyume chake. Na jambo hili ni kweli, Tunaona katika baadhi ya mataifa yanayoendelea, wananchi wao wanapitia katika taabu, na umaskini wa hali ya juu, kutokana na kuwa viongozi wao, wanatazama maslahi yao binafsi wanapoingia madarakani na sio maslahi ya taifa.. Uchu wa madaraka na ukuu, ndio wanachokitazama lakini sio kujenga mataifa yao.

Hii inafunua nini rohoni?

Neno hili linawahusu, watumishi wote wa Mungu wanaosimama katika ngazi za uongozi. Ikiwa wewe bado ni kijana au mchanga katika huduma(hata kama una-mvi) na umepewa kundi ulichunge, Omba sana hekima kwa Mungu, pia kuwa tayari kujifunza kwa waliokutangulia, Sikuzote viongozi-wachanga, katika hatua za awali wanajiamini kuwa wanajua kila kitu, lakini kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda ndivyo wanavyotambua kasoro zao nyingi. Hivyo ili kuepuka, kufanya makosa ya kiutumishi, tafuta sana msaada kwa Mungu katika hekima na mashauri.

Lakini pia, ikiwa wewe ni mchungaji, askofu, mtume, mwalimu, au unatumika katika huduma yoyote, epuka tamaa hususani ya mali. Si kila shilingi unayoipata uipeleke tumboni, au kujijengea majumba na biashara. Ni heri ukatazama kwanza hali ya kanisa la Kristo. Kama mchungaji mwema yakupasa kuipendezesha kwanza nyumba ya Bwana, kisha Baadaye Bwana mwenyewe ndio akupendezeshe wewe. Unatembelea gari ya Tsh milioni 40, halafu kanisa ni la makuti, Hapo ni nini unategemea kama sio ufukara wa kiroho hadi kimwili baadaye.

Kwahiyo hekima hizi zinatuonya, ili uongozi wetu usianguke mbeleni, hivyo tuzingatie sana maneno haya ya hekima. Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

VIJANA NA MAHUSIANO.

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.

NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Bwana Yesu aliruhusu wanafunzi wake kubeba Fimbo au hakuwaruhusu? (Marko 6:8 na Mathayo 10:10).

Swali: Tukisoma Marko 6:8, tunaona Bwana Yesu anawaruhusu wanafunzi wake “wabebe fimbo”, lakini tukirejea katika Mathayo 10:10 tunasoma habari tofauti, Bwana Yesu anawakataza wasibebe chochote hata fimbo..sasa mwandishi yupi yupo sahihi na yupi hayupo sahihi? Je biblia inajichanganya yenyewe?.

Jibu: Biblia kamwe haijichanganya mahali popote, vinginevyo kitabu kizima kitakuwa ni cha uongo!. Lakini kama ni kitabu cha kweli kilichojaa maneno ya kweli ya uzima, na Roho Mtakatifu basi hakiwezi kuwa kitabu cha ushuhuda wa uongo!, au unaochanganya!..kinachochanganyikiwa ni fahamu zetu katika kukielewa kitabu hicho, lakini chenyewe kama chenyewe hakina kasoro yoyote.

Awali ya yote tuisome mistari hiyo…

Marko 6:7 “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu;

8  akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;

9  lakini wajifungie viatu; akasema, Msivae kanzu mbili”.

Hapa ni kweli tunaona Bwana anawaambia wasibebe chochote ila Fimbo tu!… Tusome tena habari hiyo katika kitabu cha Mathayo..

Mathayo 10:7 “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.

8  Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.

9  Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;

10  wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, WALA FIMBO; maana mtenda kazi astahili posho lake”.

Hapa tunaona Bwana anawakataza hata Fimbo wasibebe, na ilihali kule kwenye kitabu cha Marko tunaona anawaambia wasibebe kitu kingine chochote isipokuwa Fimbo tu!.. Sasa mwandishi yupi ni wa kweli na yupi ni wa uongo?.

Jibu ni kwamba waandishi wote ni wa kweli hakuna aliye mwongo!,

Katika Marko Bwana anawaambia wasibebe vitu vya njiani isipikuwa FIMBO TU!.. Sasa fimbo hakikuwa chakula bali ni kifaa kinachomwezesha mtu kutembea katika milima na mabonde! Ni kama tu kiatu kilivyo msaada kwa miguu katika safari ndefu za miiba na mavumbi.. Fimbo na yenyewe ilikuwa ni hivyo hivyo..

Kwahiyo fimbo ilikuwa ni sehemu ya kitu cha msingi mtu anachoweza kuwa nacho kwa safari kama tu vile mtu alivyo na kanzu au kiatu au nguo.

Lakini sasa Bwana alichowakataza ni wao kubeba fimbo ya pili au ya tatu, kana Kamba moja ikivunjika basi kutakuwepo na akiba. Hicho ndicho kitu Bwana alichowakataza akawaambia wabebe fimbo moja tu!. Wasihofie endapo hiyo waliyonayo itapata itilafu, kwani huko wanakokwenda Mungu wa mbinguni atawafungulia mlango watapata nyingine.

Lakini pia sio Fimbo tu!, bali hata kanzu!.. wasibebe na kujifungasha mizigo ya kanzu nyingi, waende na hiyo moja tu iliyopo mwilini kwasababu huko waendako Baba yao wa mbinguni anajua kuwa wana haja na nazo, hivyo wasitie wasiwasi kwasababu mtenda kazi amestahili posho yake (watapata huko waendako). Ndio maana akawakataza wasibebe kanzu mbili…

Marko 6:8 “akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;

9  lakini wajifungie viatu; akasema, MSIVAE KANZU MBILI”.

Hapo mwisho anasema “msivae kanzu mbili” maana yake ile moja waliyonayo mwilini inatosha.. vile vile wasibebe fimbo nyingine ya pili, hiyo moja watakayokuwa nayo inatosha!..sawasawa na hiyo Mathayo 10:10..

Kwahiyo biblia haijichanganyi, bali shetani ndiye anayetuchanganya….

Sasa kufahamu ni somo gani tunaloweza kujifunza nyuma ya hii habari fungua hapa>>> Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?

Je suruali ni vazi la kiume tu?

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

Je! habari ya muda aliotawala Mfalme Yekonia inajichanganya? (2Wafalme 24:8 na 2Nyakati 36:9).

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?

Jibu: Biblia haijichanganyi mahali popote na haijawahi kujichanganya isipokuwa viwango vyetu vya kutafakari ndivyo vinavyotufanya  tuone kuna utata mwingi kwenye biblia (na kumbuka tunapozungumzia biblia tunamaanisha ile yenye vitabu 66) na si zaidi ya hivyo!.

Vitabu 66 vya biblia ndivyo vilivyohakikiwa na Roho Mtakatifu kwa vizazi vyote kama Neno la Mungu lililo hai.

Sasa kabla ya kwenda kuitafakari mistari hiyo hebu tuisome kwanza..

Mwanzo 15:13 “Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa MIAKA MIA NNE

14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi”

Tusome tena,..

Kutoka 12:40 “Basi wana wa Israeli kukaa kwao, maana, muda waliokaa ndani ya Misri, ulikuwa NI MIAKA MIA NNE NA THELATHINI. 

41 Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo MIA NNE NA THELATHINI, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya Bwana yalitoka nchi ya Misri”.

Sasa swali ni hili, Mungu alimdanganya Abramu kuwa uzao wake utakaa miaka 400 na kumbe ni miaka 430?, je Mungu ni mwongo?

Jibu ni la! Hakudanganywa, kwasababu hiyo miaka 430 bado ipo katika namba mia nne, Mungu hakumwambia kuwa atakaa miaka mia nne kamili, bali alimwambia tu miaka mia nne, ikiwa na maana kuwa inaweza kuwa ni miaka mia nne kamili au miaka 410 au 430 au 470 au hata 490 lakini haitazidi hiyo miaka 400 na kuwa 500.

Ni sawa na mtu akuulize wewe una miaka mingapi na umwambie una miaka 30 au 40, unaweza kumpa namba ya ujumla lakini kiuhalisia huenda unayo miaka 30 na miezi 6 au na miezi 7,au una miaka 40 na miezi 8 au 9.. Kwahiyo wewe kumwambia kuwa una miaka 30 au 40 unakuwa hujamdanganya.. Ni kweli ndio miaka yako, isipokuwa hujapenda kumwambia na miezi iliyo mbele ya hiyo miaka..Ungekuwa umemdaganya endapo kama ungemwambia unayo miaka 30 kamili au 40 kamili, hapo utakuwa umemdanganya!..

Vile vile Bwana Mungu hakumwambia Abramu kuwa Uzao wake utakaa utumwani miaka 400 kamili, bali alimwambia tu utakaa miaka 400.. Na ndivyo ilivyokuwa.

Kwahiyo biblia haijichanganyi.. Tazama pia miezi aliyotawala Yekonia je inajichanganya? >>> YEKONIA ALITAWALA MUDA GANI?

Je umeokoka?..kumbuka kuwa hizi ni siku za mwisho, na unyakuo wa kanisa ni muda wowote kuanzia sasa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Je! kuna mambo ambayo Mungu hawezi kuyafanya kulingana na Waamuzi 1:19?

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Je! habari ya muda aliyotawala Mfalme Yekonia inajichanganya? (2Wafalme 24:8 na 2Nyakati 36:9).

Je! biblia inajichanganya katika 1Petro 2:13 na Matendo 5:29.

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

Rudi nyumbani

Print this post