Swali: Katika biblia Beelzebuli alikuwa ni nani?, na kwanini Mafarisayo wamwite Bwana Yesu Belzebuli/.
Jibu: Jina Beelzebuli ni mwunganiko wa maneno matatu (3), Beel-ze-buli.. “Beel” maana yake ni“bwana au mkuu”… “Ze” ni kiunganishi chenye maana ya “wa” na “Buli” ni pepo wachafu mfano wa inzi.
Kwahiyo ukiunganisha maneno hayo matatu linakuja neno “Mkuu/bwana wa pepo”.. sawasawa na biblia ilivyotafsiri katika Mathayo 12:24.
Mathayo 12:22 “Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona. 23 Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa Daudi? 24 Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa BEELZEBULI MKUU WA PEPO”.
Mathayo 12:22 “Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona.
23 Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa Daudi?
24 Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa BEELZEBULI MKUU WA PEPO”.
Sasa huyu Beelzebuli mkuu wa pepo ni nani?
Si mwingine Zaidi ya “shetani mwenyewe”. Biblia inamtaja shetani kuwa ndiye mkuu wa ufalme wa giza, na ndiye mkuu wa pepo wote walioasi (Ufunuo 12:9).
Kwahiyo Mafarisayo walipoona Bwana anatoa mapepo kwa uweza wa Mungu na wenyewe hawawezi, wakaingiwa na wivu, na kuamua kuzusha kuwa anatoa pepo kwa uwezo wa shetani (beelzebuli) na si kwa uwezo wa kiMungu. Lakini jibu la Bwana lilikuwa “shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake, vinginevyo ufalme wake hautasimama”.
Mathayo 12:26 “NA SHETANI AKIMTOA SHETANI, AMEFITINIKA JUU YA NAFSI YAKE; BASI UFALME WAKE UTASIMAMAJE? 27 Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu. 28 Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajili”
Mathayo 12:26 “NA SHETANI AKIMTOA SHETANI, AMEFITINIKA JUU YA NAFSI YAKE; BASI UFALME WAKE UTASIMAMAJE?
27 Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu.
28 Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajili”
Hii ikifundisha kuwa uweza wa Mungu pekee ndio unaoweza kutoa pepo!. Shetani kwamwe hawezi kutoa pepo kwani mapepo yake yote yanafanya kazi yake..anachokifanya ni kubadilisha tu tatizo ndani ya mtu, au kuongeza tatizo ndani ya mtu.
Watu wanaoenda kwa waganga na kusema wameaguliwa na kupona, kiuhalisia hawajapona bali wamebadilishiwa tatizo au wameongezewa pepo lingine juu ya lile lililokuwepo ili kutuliza tu maumivu, lakini baada ya muda lile tatizo litajirudia na lingine kubwa Zaidi ya hilo (kwasababu kamwe shetani hawezi kulitoa pepo lake ndani ya mtu, kwasababu yeye ndiye kaliweka humo, sasa akilitoa si atakuwa anafanya kazi ya Mungu, na yeye kamwe hawezi kufanya hivyo, kwasababu hana mapenzi na wanadamu, yeye anachokitafuta ni kuwaangamiza wadamu na si kuwaweka huru).
Kwahiyo wanaoenda kwa waganga ili kupata tiba, hakuna tiba yoyote wanayoipata Zaidi ya kuongeza matatizo..Suluhisho la tabu na matatizo yote ni Yesu tu!, huyo ndiye maandiko yanasema kuwa akikuweka huru unakuwa huru kweli kweli (Yohana 8:36), na si waganga wala wachawi wala watabiri.
Kama umewaza kwenda kwa waganga kwasababu ya tatizo ulilokuwa nalo, leo hii badilisha fikra zako, kule unaenda kuongeza matatizo na si kupunguza. Mkimbilie Yesu, huyo peke yake ndiye Suluhisho na ndiye mwenye upendo wa kweli.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.
MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.
Je ni kweli hakuna aliyepaa mbinguni zaidi ya Mwana wa Adamu? (Yohana 3:13)
Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?
Rudi nyumbani
Print this post
Swali: Mti wa Mvinje uliotumika kutengenezea safina kulingana na Mwanzo 6:14 ndio mti gani kwasasa?.
Jibu: Tusome,
Mwanzo 6:13 “Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia. 14 Ujifanyie safina ya MTI WA MVINJE; fanya na vyumba ndani ya safina, ukaifunike ndani na nje kwa lami”.
Mwanzo 6:13 “Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia.
14 Ujifanyie safina ya MTI WA MVINJE; fanya na vyumba ndani ya safina, ukaifunike ndani na nje kwa lami”.
Mti wa Mvinje ni jamii ya miti inayoota karibia sehemu kubwa ya dunia, ikiwemo barani Afrika (Tazama picha juu).
Sifa ya miti hii ni migumu sana na Imara, lakini iliyo kuu kuliko zote ni uwezo iliyonayo ya kutoathiriwa na maji.
Tofauti na miti mingine, ambayo adui wake wa kwanza ni maji, (inapogusa maji basi inaoza), lakini Mti wa Mvinje wenyewe hauathiriwi na maji, hivyo kufanya mbao ya mti huo itumike kwa matumizi ya kutengeneza boti ndogo ndogo na hata kubwa (boti za wavivu na baadhi ya za abiria zinatengenezwa kwa kutumia miti hii), vile vile mbao ya mti wa Mvinje inatumika kutengenezea viti vya viwanja vya michezo na sehemu za Uma, na vile vile inatumika kutengenezea viungio vya barabara za treni (Reli), na matumizi mengine ya samani za ndani kama vile milango na makabati.
Kwa sifa miti hiyo iliyoibeba ndiyo ikawa sababu ya Mungu kumwambia Nuhu ajenge safina kwa kutumia miti hiyo, kwani ingetumika miti mingine huenda isingeweza kuvumilia kudumu juu ya maji kwa miezi yote ile mitano, kwani maandiko yanasema mvua ilinyesha siku 40 usiku na mchana, na maji yalidumu juu ya uso wa nchi siku 150 (Miezi 5) soma Mwanzo 7:4,24.
Maandiko mengine katika biblia yanayohusu mti wa mvinje ni pamoja na Isaya 6:13 na Isaya 44:14.
Lakini leo hii mvinje wetu ni nini?
Mti wa Mvinje leo hii si mwingine Zaidi ya msalaba utuokoao sisi na dhambi zetu, na safina yetu ni Bwana Yesu Kristo, tuwapo ndani ya Kristo basi gharika ya ghadhabu ya Mungu ambayo imekusudiwa kumwagwa katika siku hizi za mwisho haitatupata.
Je umeokoka? Kama bado unasubiri nini? Kumbuka dunia hii inaenda kuisha, tupo nyakati za majeruhi na unyakuo umekaribia.
Bwana akubariki.
Mretemu ni mti gani?
Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?
Mwerezi ni nini?
FANYA BIDII ZOTE ULE MATUNDA YA UZIMA.
JE NI KUTII AU KUPATA KWANZA MAARIFA?
Jibu: Turejee,
Yohana 18:28 “Kisha wakamchukua Yesu kutoka kwa Kayafa mpaka Praitorio, nayo ikawa alfajiri; lakini wao wenyewe hawakuingia ndani ya ile praitorio,wasije wakanajisika,bali wapate kuila Pasaka”.
Praitoria ni “ukumbi wa hukumu” ambao unakuwepo ndani ya majumba ya wafalme. Wahalifu ambao ilibidi kesi zao ziamuliwe na mfalme au liwaji wa mji, basi walipelekwa katika ukumbi huo na kukutana na mkuu huyo na kuhojiwa na moja kwa moja kutolewa hukumu.
Kipindi Wakuu wa makuhani wamemkamata Bwana Yesu, hawakuweza wao wenyewe kumhukumu kwasababu nchi ya Israeli yote ilikuwa chini ya utawala wa Warumi (kwaufupi ilikuwa ni koloni la Warumi), waliokuwa wanaiongoza serikali yote ni Warumi, na ndio waliokuwa wananatoa hukumu ya mwisho, ndio maana ikawabidi wakuu wa makuhani wampeleka Bwana Yesu kwa Pilato ambaye ndiye aliyekuwa liwali wa Uyahudi, na ndiye mwenye kutoa maamuzi ya mwisho (Mathayo 27:2).
Sasa kwasababu sheria za Wayahudi hazikuwawaruhusu wao kuchangamana na watu wa mataifa, wala kuingia katika nyumba zao tena hususani wakati wa sikukuu, hiyo ikawafanya wale wakuu wa makuhani wabaki nje wakati Kristo anaingizwa ndani ya Praitorio kuzungumza na Pilato.
Wayahudi hawakuingia katika nyumba za watu wa mataifa, kwasababu katika nyumba hizo kulikuwa na vitu najisi vilivyo kinyume na sheria za Musa, mfano wa vitu hivyo ni sanamu, utakuta hata kikombe tu cha kunywea maji kimetengenezwa kwa taswira ya miungu yao, na Zaidi sana vyakula vya watu wa mataifa vingi vilikuwa ni najisi kulingana na sheria za kiyahudi. Kwahiyo endapo Myahudi akiingia katika nyumba hizo na kushiriki vitu vyao hivyo hata kwa bahati mbaya au kwa kutokujua, basi tayari anakuwa amejitia unajisi, na mtu akiwa najisi anakuwa hastahili kushiriki sikukuu yoyote ya kiyahudi, (anatengwa kwa muda Fulani mpaka unajisi wake utakapoisha).
Ndio maana ikawepo sheria ya wao kutochangamana na watu wa mataifa wala kuingia katika nyumba zao..utazidi kulithibitisha hilo zaidi kipindi kile Mtume Petro ameenda nyumbani kwa Kornelio..
Matendo 10:26 “Lakini Petro akamwinua, akasema, Simama, mimi nami ni mwanadamu. 27 Na katika kusema naye akaingia ndani, akaona watu wengi wamekusanyika. 28 Akawaambia, NINYI MNAJUA YA KUWA SI HALALI MTU ALIYE MYAHUDI ASHIKAMANE NA MTU ALIYE WA TAIFA LINGINE WALA KUMWENDEA, lakini Mungu amenionya, nisimwite mtu awaye yote mchafu wala najisi. 29 Kwa sababu hiyo nalikuja nilipoitwa, nisikatae; basi nawauliza, ni neno gani mliloniitia?”
Matendo 10:26 “Lakini Petro akamwinua, akasema, Simama, mimi nami ni mwanadamu.
27 Na katika kusema naye akaingia ndani, akaona watu wengi wamekusanyika.
28 Akawaambia, NINYI MNAJUA YA KUWA SI HALALI MTU ALIYE MYAHUDI ASHIKAMANE NA MTU ALIYE WA TAIFA LINGINE WALA KUMWENDEA, lakini Mungu amenionya, nisimwite mtu awaye yote mchafu wala najisi.
29 Kwa sababu hiyo nalikuja nilipoitwa, nisikatae; basi nawauliza, ni neno gani mliloniitia?”
Lakini swali ni je! Hiyo sheria ya wayahudi kutochangamana na watu wa mataifa mpaka leo hii ni agizo la Mungu?..Kwamba watu wa mataifa ni najisi mpaka leo??
Jibu ni La!.. Kupitia msalaba wa Yesu Kristo umetufanya wote wawili kuwa mamoja.. Hakuna Myahudi wala Myunani, kwa kumwamini Yesu Kristo sote tunakuwa safi, na kitu kimoja mbele za Mungu, wala hakuna aliye bora kuliko mwingine..yeye Kristo ndiye aliyekibomoa hicho kiambaza cha kati kilichotutenganisha.
Waefeso 2:11 “Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwamba zamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili, mnaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, yaani, tohara ya mwilini iliyofanyika kwa mikono; 12 kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani. 13 Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo. 14 Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga. 15 Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani. 16 Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba. 17 Akaja akahubiri amani kwenu ninyi mliokuwa mbali, na amani kwao wale waliokuwa karibu. 18 Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kumkaribia Baba katika Roho mmoja”.
Waefeso 2:11 “Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwamba zamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili, mnaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, yaani, tohara ya mwilini iliyofanyika kwa mikono;
12 kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani.
13 Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo.
14 Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga.
15 Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani.
16 Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba.
17 Akaja akahubiri amani kwenu ninyi mliokuwa mbali, na amani kwao wale waliokuwa karibu.
18 Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kumkaribia Baba katika Roho mmoja”.
Tunakuwa Najisi tu tunapokuwa nje ya Yesu Kristo, na kinachotufanya kuwa najisi si kitu kingine Zaidi ya dhambi ndani ya maisha yetu, kama Bwana Yesu alivyosema katika Mathayo 15:17-20.
Je! umeokoka?, kama bado unasubiri nini?..Hizi ni siku za mwisho, na Bwana yupo mlangoni.
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.
USIMPE NGUVU SHETANI.
Lumbwi ni nini katika biblia?
NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?
Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)
Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?
SWALI: Biblia inamaana gani inaposema ‘mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena’ (Mithali 24:16)
JIBU: Ili kuielewa vema mstari huo tuanzie vifungu vya juu yake kidogo.
Mithali 24:15 Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki; Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika; 16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
Mithali 24:15 Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki; Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika;
16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
Hapo anazungumzia tabia za mtu mbaya anayejaribu kuharibu kazi za mtu mwema (mtakatifu). Kwamba anaweza kudhani kuwa kufanikiwa kwa mipango yake, kutamfanya Yule mtu akate tamaa ya kuendelea mbele, lakini kinyume chake, ni kuwa bado atanyanyuka tena na kuendelea mbele.
Kwamfano, watu Fulani wanaweza kuharibu umoja wa kanisa, kwa kupachika fitna na masengenyo ndani yake, na matokeo yake ikawa ni kanisa kuvunjika au kugawanyika, lakini kiuhalisia watoto wa Mungu wa kweli, wenye mbegu ya Mungu ndani yao, watasimama tena na kuujenga ule umoja walioupoteza. Lakini wengine wasio wa Mungu, watakimbia, au watakata tamaa na kurudi nyuma, na kufurahia kuanguka kule.
Au jengo la kanisa linaweza likaharibiwa na wapagani au mazingira ya asili, lakini watu wenye mbegu ya Mungu hawakati tamaa watanyanyuka na kulijenga tena upya.
Ndivyo ilivyokuwa kipindi cha wafalme wakati ambapo hekalu la kwanza linabomolewa na Nebukadreza mfalme wa Babeli, Baadhi ya wayahudi hawakumwacha Mungu wao moja kwa moja, bali waliendelea kumtafuta na kumwomba sana (Akiwemo Danieli) hatimaye baada ya miaka 70 wakarudi kulijenga upya tena. Hata baadhi ya wafalme walipotoa tamko la kusitishwa kujengwa kwa hekalu hilo bado walisimamia kusudi lao lilelile mpaka kulimaliza ijapokuwa waliwekewa vikwazo vingi sana.
Halikadhalika Injili ya mitume ilizuiliwa mara nyingi, Kwamfano Paulo anasema shetani alimzuia mara tatu ili asiipeleke injili (1Wathesalonike 2:18). Wakati mwingine alifungwa Lakini hayo hayakumkwaza na kumfanya aache kuihubiri injili, kisa amezuiliwa, bali kila siku maisha yake yalikuwa ni ya utumishi kana kwamba hakuna kikwazo chochote mbele yake, hata alipokuwa gerezani alihubiri kwa nyaraka, ambazo baadhi ya hizo ndio hizi zinazofanyika Baraka kwetu hadi sasa.
Kama mitume wangehesabu vikwazo, vitisho, vifungo, kamwe wasingeweza kuieneza injili ile ulimwenguni kote kwa kasi ile. Hivyo na sisi, tufilisikapo, tupatapo hasara, tufiwapo, tusalitiwapo na baadhi ya ndugu, ikapelekea mpaka huduma kuvurugika, au maisha ya kiroho kudorora, tusife moyo wa kumtumikia Bwana au kuendelea mbele, bali tunaanza tena upya, kana kwamba ndio tumezaliwa tena mara ya pili leo.
Lakini mstari huo haumaanishi, kuanguka katika “dhambi”, kama wengi wanavyodhani. Mtakatifu hana tabia ya kuanguka anguka ovyo kwenye dhambi..Yaana leo adondoke kwenye uzinzi, halafu kesho tena aanguke kwenye uzinzi, kesho kutwa hivyo hivyo, halafu awe bado na nguvu ya kusimama kwa Bwana. Hilo jambo haliwezi kutokea kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili.
Kuanguka kwetu ni kuwekewa vikwazo na adui, vilivyo nje ya uwezo wetu, lakini sio vile vilivyo ndani ya uwezo wetu.
Shalom.
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako (Mithali 27:23)
Nini maana ya Mithali 27:6 “Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;
Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?
Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)
Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?
Mierebi ni aina ya miti inayostawi Mahali palipo na maji maji, Mahali pengine popote haistawi. Tazama mwonekano wake kwenye picha juu.
Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyolitaja Neno hili;
Mambo ya Walawi 23:40
[40]Nanyi siku ya kwanza mtajipatia matunda ya miti mizuri, na makuti ya mitende, na matawi ya miti minene, na mierebi ya vijitoni; nanyi mtafurahi mbele za BWANA, Mungu wenu, muda wa siku saba.
Isaya 44:2-5
[2]BWANA, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua. [3]Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa; [4]nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji. [5]Mmoja atasema, Mimi ni wa BWANA; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa BWANA, na kujiita kwa jina la Israeli.
[2]BWANA, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua.
[3]Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa;
[4]nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji.
[5]Mmoja atasema, Mimi ni wa BWANA; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa BWANA, na kujiita kwa jina la Israeli.
Soma pia Ayubu 40:22, na Isaya 15:7
Kama tunavyosoma hapo Bwana aliwaagiza Wana wa Israeli watumie matawi yake kama kitu Cha shangwe katika sikukuu ya vibanda..Pindi wanapokusanyika wayanyanyue juu wamwimbie Bwana nyimbo za furaha. Lakini bado tunaona sifa ya mti huu ni kuwa karibu na vijito vya maji.
Vivyo hivyo na watu wa Mungu Rohoni, Bwana anawaona kama mierebi yake, miti inayostahili kumsifu Bwana..Kwasababu ndani yao mito ya maji ya uzima inatiririka.. lakini wengine ambao hawana Kristo ni sawa na miti mikavu tu.
Na matokeo ya kukosa mito ya uzima ndani yako ni wewe kufanyika makao ya mapepo kwasababu mapepo ndio Yanakaa sehemu isiyo na maji.
Soma
Mathayo 12:43-45
[43]Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate. [44]Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa. [45]Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.
Umeona? Unasubiri nini usimpe Bwana Yesu maisha Yako? Huna Raha, Wala Tumaini, Wala faraja unapokuwa nje ya Kristo. Okoka Leo Bwana ayaponye maisha Yako.
Ikiwa upo tayari kuchukua uamuzi huo wa kuokoka na kufanyika Mwerebi mzuri wa Bwana basi fungua hapa Kwa ajili ya mwongozo huo>>
Mti wa Mshita ni mti wa namna gani?
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
Mjusi hushika kwa mikono yake; Lakini yumo majumbani mwa wafalme.
Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?
NUNUA MAJI YA UZIMA.
Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).
Jibu: Turejee
Matendo 19:24 “Kwa maana mtu mmoja, jina lake Demetrio, mfua fedha, aliyekuwa akifanya vihekalu vya fedha vya Artemi, alikuwa akiwapatia mafundi faida nyingi”.
Mahekalu yalikuwa ni majengo maalumu kwaajili ya ibada za miungu.. Lilikuwepo hekalu moja tu duniani la Mungu wa kweli, ambalo lilitengenezwa Yerusalemu, hilo pekee ndilo Mungu wa kweli wa mbingu na nchi alikuwa akiabudiwa ndani yake kipindi cha agano la kale. Lakini mahekalu mengine yote yaliyojenga tofauti na hilo yalikuwa yanamuabudu shetani kupitia sanamu.
Sasa kipindi Mtume Paulo na wanafunzi wengine wamefika mji wa Efeso, walikuta jamii ya watu wa pale wanamwabudu mungu mke waliyemwita Artemi.
Na katika huo mji wa Efeso walikuwa wamemtengenezea Hekalu kubwa, na ndani ya hilo hekalu kulikuwa na sanamu ya huyo mungu mke, Artemi ambayo wanaamini haikutengenezwa na mtu bali ilishushwa/ilianguka kutoka mbinguni (jambo ambalo halikuwa la kweli). Na watu kutoka pande zote za dunia walikuwa wanakuja hapo Efeso lilipo hekalu la huyo Artemi kumwabudu..
Matendo 19:35 “Na karani wa mji alipokwisha kuwatuliza watu, akasema, Enyi wanaume wa Efeso, ni mtu gani asiyejua ya kuwa mji wa Efeso ni mtunzaji wa HEKALU LA ARTEMI, aliye mkuu, NA WA KITU KILE KILICHOANGUKA KUTOKA MBINGUNI?”.
Sasa kwasababu walikuwa wanamwamini huyo mungu waliyemwita Artemi kuwa ni mkuu na aliye na wafuasi wengi, wale wageni walikuja kutoka mataifa ya mbali walipata changamoto ya kumwabudu wakiwa makwao (huko katika mataifa yao ya mbali),
Hivyo ili kutatua hiyo changamoto..baadhi ya mafundi waliokuwepo pale Efeso wakaanza biashara ya kutengeneza vijihekalu vidogo vidogo vinavyobebeka vinavyofanana kabisa na lile hakalu lenye sanamu ya huyo Artemi, ili watu wanaotoka mbali wakiisha kumwabudu wakiwa Efeso waweze kuondoka na vijihekalu hivyo na kwenda navyo huko walikotokea na kuendeleza ibada zao, ambapo wengine waliviweka kwenye vyumba vyao, wengine katika vimilima na sehemu mbali mbali.
Vihekalu hivyo vilitengenezwa kwa madini ya “fedha”, ambapo mafundi wakiongozwa na fundi mkuu aliyeitwa Demetrio waliyeyusha madini hayo ya fedha na kuyatengeneza kwa muundo wa hilo hekalu.
Lakini Paulo pamoja na wanafunzi wengine wa Bwana walijua uongo huo wa shetani, na hivyo walipoingia huo mji wa Efeso waliupindua kwa injili ya kweli, na wengi wakamwamini Mungu wa kweli na kumpokea Yesu na kuacha ibada hizo za miungu, ambayo nyuma yake ni shetani anaabudiwa.
Ukisoma mistari ya juu utaona matokeo ya injili ile iliwafanya maelfu ya watu waache uchawi waliokuwa wanaufanya, na kumgeukia Mungu.
Matendo 19:18 “Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao. 19 Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu. 20 Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu”.
Matendo 19:18 “Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao.
19 Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu.
20 Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu”.
Na hata sasa uweza wa Mungu upo, Injili ya Kristo ina nguvu nguvu kuliko uchawi!. Sawasawa na Warumi 1:16 “Kwa maana siionei haya Injili kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia”.
1Wakorintho10:4-5 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) 5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; 6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”
1Wakorintho10:4-5 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”
Usiionee haya (aibu) injili.
Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)
Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?
NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?
ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.
Wivu ni nini kibiblia na kuna aina ngapi za Wivu unaowapata watu? Na je ni dhambi kuwa na Wivu?
Katika kitabu cha Wagalatia biblia imetaja “Wivu” kuwa ni mojawapo ya tunda la mwili. Sasa swali ninapopata wivu wa kimaendeleo nafanya dhambi? Au ninapopata wivu wa mwanandoa mwenzangu kukosa uaminifu je nayo ni dhambi?
Wagalatia 5:19-2119 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi.. 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira……….. ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”
Wagalatia 5:19-2119 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi..
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira……….. ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”
Ni kweli Wivu ni mojawapo wa matendo ya mwili ambayo ni dhambi mtu kuwa nayo, lakini kama ya kuingia ndani zaidi katika andiko hili..ni vizuri kuzijua kwanza aina za wivu..
Upo “Wivu wa kiMungu” na vile vile upo “wivu wa kidunia”, ni kama tu “hasira” au “hofu”. Ipo hasira ya kiMungu na vile vile ipo hasira ya kidunia au ya kiulimwengu.
Hasira ya kidunia ni ile inayoyoishia au inayompelekea mtu kutenda dhambi, kama kutukana, kuua, kuonea, kuiba n.k.. kwaufupi matunda yake ni mabaya daima… Lakini hasira ya kiMungu ni ile inaiyoishia katika kumjenga mtu na kumtengeneza zaidi, na kumrudisha kwa Mungu au katika njia sahihi kwa upendo.
Mfano wa hasira ya kiMungu ni ile Bwana Yesu aliyokuwa nayo juu ya Mafarisayo na Masadukayo.Utaona Mafarisayo na Masadukayo walikuwa wanamwudhi sana Bwana lakini hasira ya Bwana haikuishia katika kuwatukana, au kuwashushia moto na kuwaangamiza ingawa alikuwa na uwezo huo, au kuwaharibu kwa njia yoyote ile… bali katika kuwahurumia..
Marko 3:1-5 “Akaingia tena katika sinagogi; na palikuwako huko mtu mwenye mkono uliopooza; 2 wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato; wapate kumshitaki. 3 Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, Simama katikati. 4 Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza. 5 AKAWAKAZIA MACHO PANDE ZOTE KWA HASIRA, AKIONA HUZUNI kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena”.
Marko 3:1-5 “Akaingia tena katika sinagogi; na palikuwako huko mtu mwenye mkono uliopooza;
2 wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato; wapate kumshitaki.
3 Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, Simama katikati.
4 Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza.
5 AKAWAKAZIA MACHO PANDE ZOTE KWA HASIRA, AKIONA HUZUNI kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena”.
Hasira ya namna hii biblia imesema tuwe nayo ila tusitende dhambi, jua lisizame tukiwa nayo bado mioyoni..(Waefeso 4:26).
Sasa tukirudi katika Mantiki ya hofu na wivu ni hivyo hivyo, ipo hofu ya kiMungu na ya ipo hofu ya kidunia, vile vile upo wivu wa kiMungu na upo wivu wa kidunia.Wivu wa kidunia ni ule unaoishia kutenda dhambi.. Mfano mtu atamwonea mwingine wivu kwasababu kapata kitu fulani ambacho yeye hajakipata, hivyo atatamani au atatafuta njia yule mtu akipoteze kile kitu ndipo atulie.
Mfano wa wivu huu ni ule aliokuwa nao Kaini, alipoona sadaka ya ndugu yake imekubaliwa na kwake imekataliwa. Badala atafute njia ya kuboresha sadaka yake ikubalike mbele za Mungu kama ya ndugu yake, yeye akatafuta kumwua ndugu yake, (wivu unaoish kuleta chuki, masengenyo, vinyongo, visasi ni wa kishetani)..ambao ni dhambi mtu kuwa nao sawasawa na hiyo Wagalatia 5:20.
Wivu wa kiMungu ni ule unaomfanya mtu atamani kuwa mwema kama mwingine alivyo mwema, unaomfanya mtu atamani kufanya vizuri kama mwingine anavyofanya vizuri pasipo kumtakia madhara yule mwingine, (kwa ufupi haufurahii kuanguka wala kupunguka kwa mwingine)..zaidi sana mafanikio ya mwingine yanakuwa siku zote ni darasa kwake….
Wivu huu sio mbaya na si dhambi mtu kuwa nao, kwasababu matunda yake ni mazuri..Mfano wa huu ni ule Mtume Paulo, aliojaribu kuutia kwa ndugu zake Waisraeli ili wamgeukie Mungu zaidi.
Warumi 11:14 “nipate kuwatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao”.
Lakini pia upo Wivu mwingine wa KiMungu ambao unaishia kuharibu vitu vya kishetani lakini si kimharibu mtu..
Mfano wa wivu huu ni alikuwa nao Bwana Yesu juu ya Hekalu la Mungu, alipoingia na kukuta watu wanafanya biashara ndani ya hekalu, maandiko yanasema Bwana alizipindua meza zao, na kuharibu biashara zao lakini si kuwaharibu wao.. Na wanafunzi wake wakakumbuka andiko la wivu wa nyumba ya Mungu utamla (Yohana 2:17).
Wivu huu pia na sisi tunapaswa tuwe nao tunapoona kazi ya Mungu inachafuka, ni lazima tusimame kuziharibu hizo kazi za shetani kwa maombi na kwa mafundisho sahihi, lakini si kwa kuwadhuru watu au kuwatukana, au kuwaletea madhara yoyote ya kimwili.
Wivu wa namna hii pia upo katikati ya wanandoa na wanafamilia, kama kuna kiashiria chochote cha mwanandoa au mwanafamilia kutoka kwenye mstari wa uaminifu, au nidhamu, au maadili au heshima…Wivu wa namna hii huwa unanyanyuka!, sasa vibaya yule aliyemwaminifu, au aliye imara katika ndoa au familia kusimama na kuharibu au kuziba upenyo wowote ambao shetani anataka kuchukua nafasi ndani ya hiyo familia au ndoa…lakini kwa hekima pasipo kumdhuru mtu.
Lakini wivu wa wanandoa au wanafamilia unaoishia kuua huo hautokani na Mungu!.
Je na wewe unasumbuliwa na dhambi ya Wivu wa kidunia ambao unaishia kusengenya, kuona hasira, kuua, kutukana n.k Na hujui utatokaje katika hilo shimo?.
Bwana Yesu amekuja kwaajili ya kututoa katika hayo mashimo, kwa nguvu zetu hatuwezi kutoka huko wala kujitoa.Nguvu pekee ya kututoa huko ni kwa njia kwa ya Roho Mtakatifu, kwa somo kamili kuhusiana na Roho Mtakatifu, jinsi ya kumpomea na jinsi.atakavyokuwezesha kushinda yale usiyoweza kuyashinda basi tutumie ujumbe inbox ili uweze kupata somo hilo.
JIHADHARI NA DHAMBI YA WIVU/HUSUDA.
Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?
MWE NA HASIRA, ILA MSITENDE DHAMBI.
USHUJAA WA ROHONI HAUANGALII UZOEFU WAKO.
USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.
Nini tafsiri ya jina Adamu,
Adamu ni neno la kiebrania lenye maana ya “wa udongo” yaani aliyetokana na udongo/ardhi. Mtu wa kwanza kuumbwa alipewa jina hilo Adamu na Mungu mwenyewe kufuatia asili yake alipotolewa.
Mwanzo 2:7 “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai”.
Na jina “Adamu” hakupewa mtu mmoja tu bali wote wawili (yaani mwanamume na mwanamke)
Mwanzo 5:1” Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya; 2 mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki AKAWAITA JINA LAO ADAMU, siku ile walipoumbwa”.
Mwanzo 5:1” Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya;
2 mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki AKAWAITA JINA LAO ADAMU, siku ile walipoumbwa”.
Kwa urefu na kina Zaidi, kwanini Mungu awape wote wawili jina moja fungua hapa >>> Kwanini Mungu aliwaita Adamu na Hawa jina moja?
Watoto wote waliozaliwa baada ya Adamu, wakaitwa Wana-damu. (wana wa aliyekuwa wa udongo). Hivyo na sisi wote asili ya miili yetu ni ardhini, ndio maana tunakufa na miili yetu inaoza ardhini.
Lakini baada ya maisha haya, kama tukishinda vita vya kiimani vya ulimwenguni, maandiko yanasema tutavikwa miili mipya ya kimbinguni, hivyo hatutaitwa tena wanadamu, wala hatutaishi kwa kula na kunywa kama wanyama, wala tamaa za mwili hazitakuwepo tena bali tutakuwa kama Malaika kwasababu tutapewa miili mingine isiyo ya udongo.
Marko 12:25 “Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni”.
Je una tumaini la kuvikwa mwili mpya wa kimbinguni?..
Kumbuka tumaini hilo na uhakika huo tunaupata tu endapo tupo ndani ya Kristo, na tunaishi maisha yanayompendeza yeye.
Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?.
Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?
KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?
Kwanini Kristo aitwe Mwana-kondoo. (Yohana 1:29)
JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?
JIBU: Kibiblia ni neno linalomaanisha “mvurugano” au “mvurugiko”
Neno hilo utalisoma katika kifungu hiki;
Isaya 17:13 “Mataifa wananguruma kama ngurumo ya maji mengi; Lakini atawakemea, nao watakimbia mbali sana, Watafukuzwa kama makapi milimani mbele ya upepo, Na kama mavumbi vuruvuru mbele ya tufani. 14 Wakati wa jioni, tazama, kuna hofu; Na kabla ya mapambazuko hawako; Hilo ndilo fungu lao watutekao, Na ajali yao wanaotunyang’anya mali zetu”.
Hapo ni Bwana anawahakikishia watu wake ulinzi madhubuti dhidi ya adui zao. Anasema mambo matatu yatawakumba hao wanaojaribu kuwaangamiza watu wa Mungu.
La kwanza,watakemewa na kukimbia mbali sana: Ni kama wakati wa washami kipindi cha nabii Elisha, Bwana alipowasikilizisha kelele za majeshi wakakimbia wakashindwa hata kuchukua na nyara zao nyuma(2Wafalme 7).
La pili ni “ watafanana na makapi mbele ya upepo: Kwa kawaida ngano inapopepetwa yale makapi huwa yanarushwa na upepo mbali sana, ndivyo watakavyofanywa waadui wa watoto wa Mungu wanapokaribiwa, watatoweka ghafla.
Na la tatu anasema watakuwa kama mavumbi ‘vuruvuru’ mbele ya tufani: Kwa kawaida upepo mkali wa kisulisuli au tufani inapopita juu ya ardhi iliyokuwa kavu, ule upepo wake mkali unatabia ya kuvuruga mavumbi, na kuyafanya yaruke hewani yasambae tu ovyo vyo, na hiyo husababishia hali ya hewa kuchafuka sana. Hivyo, Bwana anasema, ndivyo itakavyokuwa kwa watu hao, watavurugwa, kiasi cha kutokuelewana, kila mmoja atakuwa na lake, ni kuchanganyikiwa tu, Ndio maana ya hilo andiko.
Lakini ni nini Bwana anataka tujifunze?
Ni kwamba tuwapo ndani Kristo, hatuna haja ya kuwa na hofu, kwasababu shetani na majeshi yake, yatakutana kwanza na jeshi la Bwana kabla ya kutufikia sisi. Ndicho Elisha alichomwambia Gehazi, kwamba jeshi letu ni kubwa kuliko la kwao.
Hivyo mtakatifu yoyote unayedumu katika wokovu (usio wa mdomo bali wa roho), ulinzi huu unao. Lakini kinyume chake ni kweli ikiwa upo nje ya Kristo, huna ulinzi wowote kwa Bwana, na matokeo yake shetani anaweza kufanya lolote atakalo juu yako, hata kukuua.
Swali ni Je! Umeokoka?
Kama bado na upo tayari kufanya hivyo sasa basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo was ala hiyo. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;
Je! Sulemani alienda mbinguni?
Nini maana ya uvuvio?
MZUNGUKO WAKO NI UPI?
Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?
Ila atapewa mara mia sasa,Ndugu wake(Marko 10:30)
Manyoyota ni nini (Ayubu 37:6)
SWALI: Kwanini Nuhu alimlaani Kanaani badala ya mtoto wake Hamu, ambaye ndiye aliyekuwa na makosa?
JIBU: Ni kweli kama tunavyosoma katika maandiko, pindi ambapo Nuhu amelima shamba lake la mizazibu akaaanda divai nyingi akanywa akalewa mpaka akalala uchi hadharani, tunaona mtoto wake mmoja aliyeitwa Hamu alipomuona hakuchukua hatua stahiki kumsitiri Baba yake
Lakini wale watoto wake wawili (yaani Yafethi na Shemu) walipomwona baada ya kuambiwa na Hamu, hawakutaka kutazama bali walichukua mavazi yao mabegani Kisha wakaenda kinyume nyume wakamfunika Baba Yao.
Nuhu alipopata taaarifa, aliyoyafanya mwanawe wa mwisho alimlaani, lakini laana yake haikuwa Kwa Hamu Moja Kwa Moja Bali Kwa mtoto wake aliyeitwa Kaanani..Sasa swali ni je Kwanini afanye hivyo Kwa Kaanani mjukuu wake, angali kitendo kimetendwa na Hamu.
Mwanzo 9:20-25
[20]Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu; [21]akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake. [22]Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. [23]Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao. [24]Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea. [25]Akasema, Na alaaniwe Kanaani; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.
Ipo mitazamo mingi katika jambo hilo, wapo wengine wanaomini kuwa Shemu alikuwepo na mwanaye huyo mkubwa Kaanani, na huwenda yeye naye alipuuzia kumsitiri Babu yake, au alifanya jambo baya kwake, wengine wanasema Hamu tayari alikuwa amebarikiwa na Mungu hivyo Baba yake asingeweza Tena kumlaani mtu ambaye amebarikiwa (Mwanzo 9:1),ndio maana laana akaisogeza kwa mjukuu wake.
Wengine wanaaanimi aliposema alaaniwe Kaanani, ni lugha tu iliyomaanisha pia “Baba wa kaanani”
Lakini ni vema tukaona muktadha wa uandishi wote, ikumbukwe kuwa aliyekiandika kitabu hicho ni Musa, na tunafahamu hatma ya taifa la Israeli, ilikuwa si katika mataifa yote duniani, bali pale Kaanani. Hivyo, ulikuwa ni unabii, wa Nuhu, kuonyesha moja wa uzao Shemu uitwao kaanani utalaaniwa. Hivyo tunapokuja kusoma juu ya anguko la wenyewe wa taifa lile, walivyoangamizwa na kuteketezwa na taifa la Israeli, ni kutukumbusha kuwa tayari Kaanani ilikuwa imeshalaaniwa tangu zamani, kuangamizwa kwao na maovu yao ni matokeo ya laana iliyotajwa zamani.
Shalom
Kanaani ni nchi gani kwasasa?
Nchi ya Nodi ambayo Kaini alikimbilia ndio nchi gani kwasasa?(Mwanzo 4:16).
Wakaanani walikuwa ni watu gani?
saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada
KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?
KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?