Category Archive maswali na majibu

Nini maana ya kukunguwazwa (Marko 14:27)

Jibu: Tusome,

Marko 14:27  “Yesu akawaambia, Mtakunguwazwa ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika”.

Kukunguwazwa maana yake ni “kuchukizwa”.. Mtu anapokufanya ukasirike au uchukie maana yake amekukunguwaza, biblia imetoa tafsiri ya neno hilo vizuri katika Mathayo 26:30.

Mathayo 26:30  “Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda mlima wa Mizeituni.

31  Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote MTACHUKIZWA kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika”.

Unabii huo alioutoa Bwana ulitimia masaa machache tu mbeleni, pale ambapo kikosi cha Askari wa kirumi kilitokea na kumkamata Bwana Yesu.

Na tunasoma Mitume hawakukifurahia kile kitendo, “WALICHUKIZWA SANA”, hata Petro kufikia hatua ya kutoa upanga na kumkata sikio mtumwa wa kuhani mkuu. Hicho ni kiwango kikubwa sana cha hasira.

Yohana 18:7  “Basi akawauliza tena, Mnamtafuta nani? Wakasema, Yesu Mnazareti.

8  Yesu akajibu, Nimekwisha kuwaambieni ya kwamba ni mimi; basi ikiwa mnanitafuta mimi, waacheni hawa waende zao.

9  Ili litimizwe lile neno alilolisema, Wale ulionipa sikumpoteza hata mmoja wao.

10  Basi Simoni Petro alikuwa na upanga, akaufuta, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio la kuume. Na yule mtumwa jina lake ni Malko”.

Vile vile na sisi tuliompokea Yesu ni lazima tutapitia tu vipindi vya kuchukizwa kwaajili ya Yesu.

Unapofika mahali na kukuta watu wanalikufuru jina la Yesu ni lazima utachukizwa tu!, unapofika mahali na kukuta watu kwa makusudi kabisa wanahubiri injili nyingine tofauti na ile ya kimaandiko ni lazima utachukizwa tu!.

Unapofika mahali na kukuta unatolewa unabii wa uongo, au kweli ya Mungu inapotoshwa kwa makusudi, ni lazima utachukizwa tu!, Unapofikia hatua ya kusumbuliwa kiimani na watu wengine kwasababu tu umeokoka, au umeamua kwenda katika njia sahihi ni lazima tu utakunguwazwa! hata wakati mwingine kufikia kiwango kama kile cha Petro cha kutamani kumdhuru mtu kabisa.

Lakini sisi hatujapewa ruhusa wala amri ya kumdhuru wengine, hata kama ni waovu au wanatutendea maovu, au hata kama wanamtukana Mungu mbele yetu, kazi tuliyopewa ni kuziokoa roho, na si kuziangamiza, kwasababu kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama bali juu ya majeshi ya mapepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

Lakini siku zote fahamu kuwa, ni lazima tu tutapitia vipindi vya kuchukizwa kwaajili ya Yesu, hilo haliepukiki kwa kila aliyezaliwa mara ya pili.

Yohana 15:20 “Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa WALINIUDHI MIMI, WATAWAUDHI NINYI; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kama kuua ni dhambi kwanini Mungu aruhusu mauaji katika Kumbukumbu 13:6-10?

Bwana alisema “Usiue” (Kutoka 20:6) lakini tunaona anawapa wana wa Israeli maagizo ya kuua wale wote wanaoabudu miungu? Je Hii inakaaje? (Kumbukumbu 13:6).

Jibu: Tusome,

Kumbukumbu 13:6 “Atakapokushawishi kwa siri ndugu yako, mwana wa mamaako, au mwana wako, au binti yako, au mke wa kifuani mwako, au rafiki yako aliye kama moyo wako, akikuambia, Twende tukaabudu miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako; 7 katika miungu ya mataifa yaliyo kando-kando yenu karibu nawe au mbali nawe, tokea ncha moja ya dunia hata ncha ya pili ya dunia;8 usimkubalie wala usimsikize; wala jicho lako lisimwonee huruma, wala usimwache, wala usimfiche;9 MWUE KWELI; mkono wako na uwe wa kwanza juu yake katika kumwua, na baadaye mikono ya watu wote.10 NAWE MTUPIE MAWE HATA AFE; kwa kuwa alitaka kukupotoa na Bwana, Mungu wako aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.11 Na Israeli wote watasikia na kuogopa, wasifanye tena uovu mfano wa huo katikati yako”

Ni kweli Mungu alikataza “Kuua” lakini pia kuna mahali pengine aliruhusu “kuua”, sasa ni rahisi kuhisi kuwa biblia inajichanganya, lakini kiuhalisia haijichaganyi.

Katika biblia zilikuwepo sheria za mtu binafsi lakini pia zilikuwepo sheria za Nchi/Taifa. Ikumbukwe kuwa Israeli lilikuwa ni Taifa la kidini, hivyo baadhi ya Amri na sheria zilikuwa ni za kitaifa. Kwahiyo mtu akiivunja sheria Fulani iliyoandikwa kwenye torati basi alikuwa amevunja sheria ya kitaifa.

Ili tuelewe vizuri tuchukue mfano wa mataifa ya sasa, katika mataifa mengi, (karibia yote) kuna sheria ya “kutoua” yaani raia haruhusiwi kumuua mwenzake kwa kosa lolote lile!!, lakini katika Taifa hilo hilo tunaona kuna sheria ya “kunyongwa” endapo mtu akikutwa na hatia iliyo kubwa sana..

Sasa Yule askari aliyetumwa kumweka kitanzi Yule mtuhumiwa, tayari kashafanya tendo la mauaji, lakini kwa kumnyonga Yule mhalifu, bado anakuwa hajavunja sheria ya “kuua”.. Kwasababu yeye kapewa amri ya kuua na mamlaka, lakini haja ua kwa matakwa yake yeye. Lakini kama ingekuwa kajichukulia sheria mkononi ya kuua basi angehesabika ni muuaji, na angekuwa amevunja sheria ya nchi. Na pia Nchi kuweka sheria ya Kuwaua wale waalifu sugu, haijamaanisha kuwa imeruhusu sheria ya watu kuuana huko uraiani.

Vivyo hivyo katika Israeli, Mungu alikataza mtu kujichukulia sheria mkononi za kuua, lakini pia aliruhusu mauaji kwa watu ambao watathibitika kisheria (yaani kitaifa) kuwa wamestahili kifo!.  Na mamlaka hayo aliwapa watu wote, tofauti na sasa ambapo wanapewa tu wale askari walioteuliwa kwa kazi hiyo.

Kwahiyo biblia haijichanganyi, lakini pia tunachoweza kujifunza ni kuwa Lile baya mtu analolifanya litamrudia hata kwa njia nyingine, mtu aliye muuaji naye pia atauawa, mtu anayefanya ubaya ule ubaya utampata na yeye siku za baadae.

Mathayo 26:51  “Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.

52  Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga”.

Soma pia Ufunuo 13:10.

Kwahiyo tujihadhari na dhambi tuwafanyiazo watu au tuzifanyazo mbele za Mungu, kwasababu yale tunayoyafanya tutapata malipo yake hapa hapa, kama ni mema au kama ni mabaya.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

MJUMBE WA AGANO.

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

IMANI NI KUWA NA UHAKIKA WA MAMBO YATARAJIWAYO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kupwelewa maana yake nini? (Matendo 27:26).

Tusome,

Matendo 27:25 “Basi, wanaume, changamkeni; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa.

26 Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja”.

Kupwelewa maana yake ni “kusafiri katika kina kifupi”. Meli au Mashua inaposafiri katika maji yenye kina kifupi, maana yake Meli hiyo au boti hiyo “inapwelewa”.

Katika safari ya Paulo kuelekea Rumi chini ya kikosi cha maaskari, maandiko yanatuonyesha safari ile ilikuwa ni ya misuko-suko mingi baharini, kwasababu wale mahabaria hawakulisikiliza shauri la Paulo ambalo aliwashauri wasing’oe nanga lakini wenyewe hawakusikia hivyo. Mwishowe wakakutana na misuko suko mikuu baharini, mpaka wakakata tamaa ya kuokoka.

Matendo 27:10 “akawaambia, Wanaume, naona kwamba safari hii itakuwa na madhara na hasara nyingi, si ya shehena na merikebu tu, ila na ya maisha yetu pia.
11 Lakini yule akida akawasikiliza nahodha na mwenye merikebu zaidi ya yale aliyoyasema Paulo”.

Wakiwa katika hiyo misukosuko, Paulo alitokewa na Malaika na kuambiwa kuwa hakuna atakayekufa katika safari hiyo, kwani ni lazima Paulo afike salama Rumi ili akalishuhudie Neno la Mungu na kule nako. Na jambo lingine aliloambiwa na Malaika yule ni kwamba Merikebu itapwelewa (yaani itasafiri katika kina kifupi) kando kando ya kisiwa kimoja, mpaka watakapofika kwenye hicho kisiwa.

Na kweli ufunuo huo mahabaria waliuhakiki kwani muda mfupi tu walipoanza kupima kina cha maji waliona kinaanza kupungua kwa jinsi walivyokuwa anaendelea mbele.

Matendo 27:27 “Hata usiku wa kumi na nne ulipofika, tulipokuwa tukichukuliwa huko na huko katika bahari ya Adria, kama usiku wa manane baharia wakadhani ya kuwa wanaikaribia nchi kavu.

28 Wakatupa bildi wakapata pima ishirini, wakaendelea kidogo wakatupa bildi tena, wakapata pima kumi na tano”.

Ni nini tunachoweza kujifunza katika safari hiyo ya Paulo?

1.Mungu atakuwepo na sisi hata katikati ya majaribu
Paulo, alikuwa amefungwa lakini katika kufungwa kwake, bado Mungu alikuwa naye, akimwongoza katika mapito yake, utaona pia wakati akiwa gerezani bado Bwana alikuwa naye, na kila mahali Bwana alikuwa naye, vile vile na sisi tunapokuwa katika majaribu, ambayo tunajua kabisa ni Mungu kayaruhusu basi hatupaswi kuwa na woga wala kukata tamaa, kwasababu Mungu atakuwa Pamoja nasi, na zaidi sana yeye alisema “hawezi kutuacha tujaribiwe kupita tuwezavyo”

2. Wokovu wa Mungu ni hata kwa maadui zetu.

Tunapokuwa katikati ya majaribu ni muhimu kujua kuwa Mungu katuweka pale kwa wokovu wa wengine, Utaona Paulo kafungwa lakini Mungu anamwokoa yeye Pamoja na wale Mabaharia, na wafungwa na watesi wake, anawaokoa na Mauti vile vile na sisi Mungu anapotuweka mahali ni ili tuokoke na wale tulio nao, haijalishi ni maadui zetu au watesi wetu.

Matendo 27:22 “Sasa nawapeni shauri, iweni na moyo mkuu, kwa maana hapana hata nafsi mmoja miongoni mwenu atakayepotea, ila merikebu tu.

23 Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,

24 akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.

25 Basi, wanaume, changamkeni; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa.

26 Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Kaanani ni nchi gani kwasasa?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

Rudi nyumbani

Print this post

Dia ni nini katika biblia? (Mithali 13:8)

Jibu: Tusome,

Mithali 13:8 “Dia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake; Bali mtu maskini hasikii ogofyo lo lote”.

Dia ni Kiswahili kingine cha neno “Fidia”, Kwahiyo hapo biblia inaposema “Dia” ya nafsi ya mtu ni utajiri wake, na maskini hasikii ogofyo lolote, maana yake ni kwamba “Fidia ya mtu anapokutana na matatizo ni itatoka katika vitu alivyonavyo” ikiwa na maana kuwa mtu anapokutwa na tatizo labda kasababisha hasara Fulani au kafanya kosa Fulani katika jamii, lililomsababishia apigwe faini, au kakutana na watu na kaingiliwa na wahalifu katika nyumba yake, basi Mali alizo nazo zinaweza kuwa fidia kwaajili ya uhai wake, maana yake anaweza kuwapa wale watu sehemu ya mali zake na akaisalimisha roho yake.

Lakini mtu asiye na kitu kabisa (yaani Yule maskini kikweli kweli), huwa hawezi kupokea vitisho vyovyote, hakuna jambazi yeyote anayefikiria kwenda kuvunja nyumba ya maskini akiwa na mtutu ili amwibie mali zake.. Ikiwa na maana kuwa, maskini siku zote yupo huru!.. hafuatiliwi na mtu, wala hakuna mtu ana habari na maisha yake (hapokei ogofyo lolote).

Ni hekima gani tunaipata hapo? Au ni nini tunajifunza hapo?

Ili tuelewe ni nini tunajifunza hapo, hebu tuanzie kusoma kuanzia mstari wa 7

Mithali 13:7 “Kuna mtu mwenye kujitajirisha, lakini hana kitu; Kuna ajifanyaye kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.

8 Dia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake; Bali mtu maskini hasikii ogofyo lo lote”

Hii ni hekima ambayo inaweza kutusaidia kuwa salama..sio lazima tuwapo na mali, tujionyeshe kuwa na mali kwa watu!, ndio maana hapo biblia inasema “kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.”.. Unapokuwa mtu wa kujionyesha mbele za watu mali ulizo nazo, unajiweka katika hatari ya kutoa DIA (Fidia) kwaajili ya uhai wako, kwasababu kila mtu atatamani hizo mali ulizo nazo, utavutia watu waovu na wasio waovu, utavutia majambazi, utavutia wenye mamlaka na watu  wapendao rushwa n.k

Hivyo hekima ni kujiweka katika maisha ya wastani, hata kama unazo mali nyingi, si lazima ujulikane wewe ni tajiri kuliko wote.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Azidishaye mali yake kwa riba, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.

Nini maana ya ampokeaye Nabii atapata thawabu ya Nabii? (Mathayo 10:41).

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya andiko hili  “Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.(Yohana 5:37)”

Jibu: Tusome,

Yohana 5:37  “Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. SAUTI YAKE HAMKUISIKIA WAKATI WO WOTE, WALA SURA YAKE HAMKUIONA.

38  Wala neno lake hamnalo likikaa ndani yenu, kwa kuwa ninyi hammwamini yule aliyetumwa na yeye.”

Hapa Bwana Yesu hamaanishi kwa Wayahudi hawajawahi kuisikia sauti ya Mungu, wala kuliona umbile lake!. Hapana bali andiko hilo linamaansha kuwa Mungu alijidhihirisha kwao kimaumbile lakini hawakumwona na vile vile alijidhihirisha kwao kisauti lakini hawakumsikia.

Sawasawa kabisa na alivyosema katika Kitabu cha Isaya

Isaya 50:2 “Basi, NILIPOKUJA, MBONA HAPAKUWA NA MTU? NILIPOITA, MBONA HAPAKUWA NA MTU ALIYENIJIBU? Je! Mkono wangu ni mfupi, hata nisiweze kukomboa? Au je! Mimi sina nguvu za kuponya? Tazama, kwa kukemea kwangu naikausha bahari, mito ya maji naifanya kuwa jangwa; samaki wao wanuka kwa sababu hapana maji, nao wafa kwa kiu”.

Umeona hapo?.. kumbe kuna wakati Bwana anatujia kimaumbile lakini hatumwoni?… Sasa utauliza ni wakati gani anatujia hatumwoni, na ni wakati gani anapaza sauti yake hatuisikii??

Kupitia watumishi wake wa kweli, wanapotujia kama wageni na kutuletea habari njema, ujio wao unafananishwa kabisa na ujio wa Kristo kwetu kimaumbile, haihitaji yeye Mungu atutokee ndio ihesabike kuwa tumeliona umbile lake, bali watumishi wake tu kutujia tayari hao ni umbile lake…… utasema hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko??

Mathayo 25:41 “Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42  kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43  nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45  Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, KADIRI MSIVYOMTENDEA MMOJAWAPO WA HAO WALIO WADOGO, HAMKUNITENDEA MIMI.

46  Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele”.

Umeona?.. Vile vile tusiposikiliza sauti za watumishi wake, ni sawa na hatujaisikiliza sauti yake!.. Ndio maana hapo katika Isaya 52:2 anasema “nilipoita mbona hamkuitika?”.. maana yake ni kwamba wenyewe walidhani sauti wanayoisikia ni ya mwanadamu kumbe ni ya Mungu.. vile vile walidhani umbile walionalo mbele yao ni la mwanadamu kumbe ndio umbile la Mungu, kwahiyo wakayadharau maneno ya Mungu aliyoyazungumza kupitia watumishi wake..

Na hapa Kristo anarudia tena maneno hayo hayo ya Isaya na kusema… “Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. SAUTI YAKE HAMKUISIKIA WAKATI WO WOTE, WALA SURA YAKE HAMKUIONA.”.. Maana yake Mungu alizungumza nao mara nyingi, na kuonekana kwao mara nyingi lakini hawakuwahi kumsikia wala kumwelewa wala kumfahamu hata mara moja, kwasababu mioyo yao ilikuwa mbali naye.

Na sisi tunajifunza kuwa sauti ya Mungu haiji kwetu kama sisi tunavyotaka au tunavyopanga, wala Mungu hatujii kimaumbile kama sisi tunavyotaka!..

Ni wengi sana wanafunga na kukesha ili kwamba Mungu awatokee, na waisikie sauti ya Mungu kama vile redio,..kama unafanya hivyo nataka nikuambie kuwa “unapoteza muda wako”.. kwasababu hiyo sio Njia ya MUNGU kuzungumza na sisi, hizo ni njia zetu sisi wanadamu za kuwasiliana..Mungu yeye anazo njia zake, ni lazima tuzijue hizo, tusilazimishe atumie zetu… “atafanya hivyo akipenda”, lakini si kanuni yake!.

Ukitaka kuisikia sauti ya Mungu vizuri, soma Neno na kulitafakari, Sikiliza mahubiri ya watumishi wa Mungu wa kweli, na ishi maisha matakatifu. Hapo utamwona Mungu sana katika maisha yako na utamsikia sana.

Bwana atusaidie na kutubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana?

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Swali: Kwanini Mungu aliwapeleka wana wa Israeli Misri kwa miaka 400, Ni kosa gani kubwa walilolifanya mpaka Mungu kuwauza kwa Farao miaka yote hiyo?

Jibu: Hakuna kosa lolote walilolifanya mpaka kufikia hatua hiyo ya kupelekwa Misri katika nyumba ya utumwa. Bali Mungu aliruhusu iwe hivyo, kwa makusudi maalumu. Ni kama tu Yusufu alivyoenda kuuzwa kwa Misri kwa Potifa, maandiko hayaonyeshi kuwa Yusufu alifanya kosa lolote lililompelekea kwenda kuuzwa kama mtumwa kwa Potifa, lakini maandiko yanaonyesha kuwa Mungu alimpeleka Misri kwa lengo la kuwaokoa watu wengi siku za mbeleni, tunalisoma hilo katika Mwanzo 45:4-8

Mwanzo 45:4 “Yusufu akawaambia ndugu zake, Karibuni kwangu; basi, wakakaribia. Akasema, Mimi ni Yusufu, ndugu yenu, ambaye mliniuza kwenda Misri. 

5 Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike nafsi zenu, kwa kuniuza huku; MAANA MUNGU ALINIPELEKA MBELE YENU KUHIFADHI MAISHA YA WATU.

 6 MAANA MIAKA HII MIWILI NJAA IMEKUWA KATIKA NCHI, NA IKO TENA MIAKA MITANO ISIYO NA KULIMA WALA KUVUNA. 

7 MUNGU ALINIPELEKA MBELE YENU KUWAHIFADHIA MASAZO KATIKA NCHI, NA KUWAOKOA NINYI KWA WOKOVU MKUU

8 Basi si ninyi mlionipeleka huku, ila Mungu; naye ameniweka kama baba kwa Farao, na bwana katika nyumba yake yote, na mtawala katika nchi yote ya Misri”.

Hali kadhalika Mungu aliwapeleka wana wa Israeli Misri na kuwafanya kuwa watumwa, kwa malengo makuu mawili.. ambayo yanafanana na yale ya Yusufu.

1.MUNGU KUTANGAZA UKUU WAKE.

Kupitia wokovu wa Israeli kutoka Misri kwa mapigo yale 10 aliyompiga nayo Farao, na kwa kupitia ishara za ajabu alizozofanya jangwani kama kushusha Mana, kuleta Kware, kudhihirisha Nguzo ya Wingu na Moto n.k, ulimwengu umeweza kumjua Mungu wa Ibrahimu kuwa ni Mungu mkuu na wa haki na mwenye nguvu nyingi na maajabu mengi.

Kwahiyo ijapokuwa Israeli waliteswa Misri lakini maisha yao baadaye yalikuja kuwa mahubiri makubwa sana kwa ulimwengu kumjua Mungu wa kweli, pengine wasingepitia hiyo njia ya mateso tusingemjua Mungu kwa kiwango hicho.

2. KUTANGAZA NJIA YA WOKOVU

Lengo la pili la wana wa Israeli kupitia yale maisha ni kutangaza njia ya Wokovu. Maisha yao kuanzia Misri mpaka Kaanani, ni ufunuo kamili wa maisha ya Wokovu kutoka Dhambini(Misri), kueleka mbinguni (Kaanani) mji wa raha.

Tunapomwamini Bwana Yesu na kutubu dhambi zetu, katika roho ni kama tumetoka Misri..na hivyo Kristo anatuweka huru mbali na vifungo vyote vya dhambi, kwasababu maandiko yanasema “atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi (Yohana 8:34)”.

Hii inatufundisha nini?.. Si kila mateso tunayoyapitia yanatokana na makosa tuliyoyafanya?.. Yusufu hakuna kosa alilolifanya mpaka kufikia kuuzwa Misri kwa Potifa na hata kufungwa gerezani, vile vile wana wa Israeli hakuna kosa walilolifanya mpaka kufikia kuwa watumwa kwa muda ule, bali Mungu aliruhusu hayo yatokee ili mwisho wake aonyeshe utukufu wake!..

Kwahiyo hatutakiwi kukata tamaa tunapopitia shida, maadamu tuna uhakika tupo sawa na Mungu (yaani tunaishi maisha yanayompendeza yeye), vile vile tunapopitia magonjwa ya muda mrefu hatupaswi kukata tamaa wala kulaumu, bali tunapaswa kushukuru na kuendelea kuomba na kuishi maisha yanayompendeza, kwasababu Mungu anataka kufanya maisha yetu kuwa ushuhuda..

Hata Kristo maisha yake yalikuwa ni ya ushuhuda, alikuwa kama namna ya mtumwa (Wafilipi 2:7-8), lakini alijua mwisho wake utakavyokuja kuwa, na sisi hatuna budi kuwa watu wa namna hiyo hiyo, kwasababu mwisho wetu utakuwa mzuri hata kama mwanzo wetu umekuwa mbaya na wa kukatisha tamaa, maadamu tupo katika Neno lake na amri zake, basi hatuna haja ya kuwa na hofu, ni suala la muda tu.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

MAJARIBU 10 WANA WA ISRAELI WALIYOMJARIBU MUNGU.

JIHADHARI NA MKUTANO WA WATU WALIOCHANGANYIKANA.

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

Rudi nyumbani

Print this post

Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?

Jibu: Tuanzie kusoma ule mstari wa 3

Wagalatia 2:3 “Lakini Tito aliyekuwa pamoja nami, naye ni Myunani, hakulazimishwa kutahiriwa.

4  BALI KWA AJILI YA NDUGU ZA UONGO WALIOINGIZWA KWA SIRI; AMBAO WALIINGIA KWA SIRI ILI KUUPELELEZA UHURU WETU TULIO NAO KATIKA KRISTO YESU, ILI WATUTIE UTUMWANI;

5  ambao hata saa moja hatukujitia chini yao, ili kwamba kweli ya Injili ikae pamoja nanyi.”

Hapo kuna mambo matatu (3).. NDUGU WA UONGO, 2) WALIINGIA KWA SIRI, na 3) KUUPELELEZA UHURU.

1.NDUGU WA UONGO.

Watu waliookoka waliitwa NDUGU, na hata leo wanaitwa hivyo hivyo “Ndugu”, lakini wapo Ndugu wa Kweli na pia wapo wa “Uongo”. Ndugu wa kweli ni wale waliookoka kikweli kweli, ambao wapo katika kundi au kusanyiko katika Nia ya KRISTO na si kwaajili ya kutafuta mambo yao wenyewe (1Wakorintho 16:20 na Wagalatia 1:2).

Lakini “Ndugu wa Uongo” Hao ni watu ambao wanajiingiza katika kanisa, ikiwa Nia yao si kumtafuta Kristo wala kumtumikia bali kutafuta mambo yao mengine kama Fedha, au Fursa Fulani, na wengine kuupeleleza uhuru wa wakristo na wengine ni mawakala kabisa wa Ibilisi, wanajiunga kwa lengo la kuliharibu kundi na kulisambaratisha. Mfano wa hao ndio wale Paulo aliwaozungumzia katika waraka kwa Wafilipi..

Wafilipi 3:17 “Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi.

18  Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;

19  mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.

20  Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo”.

Makundi haya ya Ndugu wa Uongo, yamesambaa katika nafasi zote, kuanzia Wachungaji, Mitume, manabii, waimbaji, mpaka washirika/waumini.

2. WANAJIINGIZA KWA SIRI

Kundi hili la Ndugu wa Uongo, huwa hawajiingizi kwa wazi bali kwa siri, maana yake ni kwamba wanajigeuza na kufanana na Ndugu wa kweli.. lakini ndani yao wanajua ni nini wanatafuta sawasawa na maandiko yanavyosema..

2Wakorintho 11:13  “Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.

14  Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.

15  Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”

3. KUUPELELEZA UHURU.

Sasa ni Uhuru gani ambao Wakristo wanao?.. Jibu: Ni uhuru unaotuweka mbali na utumwa wa Sheria… Katika Ukristo hatuna sheria za kutahiriwa, kwamba ni lazima mtu atahiriwe au asitahiriwe ndipo akubaliwe na Mungu, vile vile na sheria nyingine zote kama kushika sabato na kushika miezi na sikukuu, kuna aina fulani tu ya chakula n.k hizo zote maandiko yanasema tumewekwa huru nazo..

Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

17  mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo……………………..

20 Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani,

21  Msishike, msionje, msiguse;

22  (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu?

23  Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili”.

Sasa walikuwepo wayahudi ambao wanajiingiza katika kanisa la Kweli la Kristo, si kwa lengo la kumtumikia Bwana, bali kwa lengo la kuwatwika watu mzigo wa kushika sabato, na mwandamo wa mwezi na sikukuu za kiyahudi.

Hata sasa wapo watu baadhi ambao wengine wanatenda mfano wa hayo kwa kujua au kwa kutokujua, mfano mapokeo ya kushika sabato yanauua uhuru wetu katika Kristo, mapokeo ya kutahiriwa yanaua uhuru wetu katika Kristo n.k

Hivyo hatuna budi kuzipima roho, si kila pokeo ni la kupokea.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx

Mada Nyinginezo:

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).

Rudi nyumbani

Print this post

Kama Kristo alizichukua dhambi zetu na kutusamehe kwanini kila siku tunatubu?.

Jibu: Ni kweli Kristo alizichukua dhambi zetu kama biblia inavyosema katika kitabu cha Petro..

1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.

Lakini hiyo haimaanishi kuwa tumeshakamilika asilimia mia kwamba hatutakuwa na kasoro zozote kuanzia hapo na kuendelea…Kasoro chache chache na madhaifu machache chache bado tutaendelea kuwa nayo mpaka siku tutakapopata ukombozi wa miili yetu (Waefeso 4:30).

Wakati parapanda ya mwisho itakapolia hapo ndipo tutapata ukombozi wa miili yetu, na tutakuwa wakamilifu asilimia zote kwasababu tutapewa miili mingine isiyo na kasoro wala madhaifu.. lakini sasa ulimwenguni bado tupo katika mapambano, bado tupo vitani, bado ibilisi yupo, bado tutapitia vipindi vya kukosea vidogo vidogo, lakini si vya kutuangusha kabisa!!.. Kama kile Petro alichopitia wakati anakutana na Paulo kule Antiokia (Soma Wagalatia 2:11-14).

Vile vile tutapitia vipindi vya kuudhiwa, na kupata hasira, tutapitia vipindi vya kukosea kuongea, kukosea kutenda, tutapitia vipindi pia vya kuwakosa wengine pasipo kujua au kwa kujua, tutapitia vipindi vya kumkosa Mungu kwa kujua au kwa kutokujua n.k.. sasa kwa kasoro hizo zote tunazozibeba ni lazima tuwe watu wa kuomba rehema na toba mara kwa mara ili muda wote tudumu katika usafi na pia Bwana anyooshe mapito yetu..

Hiyo ndiyo sababu pia Bwana Yesu akatufundisha kuomba toba na rehema kila mara..

Luka 11:1 “Ikawa alipokuwa mahali fulani akiomba, alipokwisha, mmoja katika wanafunzi wake alimwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.

2  Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]……………….

4 UTUSAMEHE DHAMBI ZETU, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu]”.

Kwahiyo ni lazima kuomba rehema na toba kila siku, kwasababu bado tupo katika mwili, na pia ni ishara ya unyenyekevu kwa Mungu.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Fahamu Namna ya Kuomba.

JIRANI YANGU NI NANI?

Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8).

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Ni kweli haturuhusiwi kula nyama kulingana na Isaya 66:3?


Jibu: Tusome,


Isaya 66:3 “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao”.


Mstari huo tukiusoma kama ulivyo ni rahisi kutafsiri kuwa “Biblia imekataza kuchinja wanyama na kula nyama”…lakini kiuhalisia hiyo sio maana yake kabisa…kwasababu kama hiyo ingekuwa ndio maana yake basi pia hapo imekataza matoleo… na tunajua matoleo ni jambo linalokubalika mbele za Mungu (Warumi 25:26).


Sasa tukisoma kuanzia ule mstari wa kwanza utaona Mungu anawakemea au kuwaonya wale watu ambao wanakusanya vingi na vikubwa na kwenda kumtolea Mungu, wakidhani kuwa Mungu anapendezwa na sadaka zao hizo kubwa na nyingi na huku mioyoni wapo mbali na Mungu.


Na utaona Bwana anazidi kusema.. “Mbingu na dunia ni mali yake, hakuna chochote tutakachoweza kumpa yeye ambacho kitakuwa cha kipekee”…ikifunua kuwa Mungu hana haja na vitu bali mioyo yetu, kwasababu kila kitu ni chake.


Isaya 66:1 “BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?


2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu”.


Umeona?..Mtu mnyonge ndiye atakayemwangalia Bwana, mtu mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno lake…Maana yake mtu wa namna hii atakapoleta sadaka yake ndio Mungu atakayoikubali, lakini mtu mwovu na mwenye kiburi Mungu haitaki sadaka yake.


Sasa endapo mtu mwovu anayemkataa Mungu analeta sadaka yake mbele za Mungu, sadaka yake hiyo inaonekana kama ni sadaka ya hatia.


Kama akileta Ng’ombe na kumpeleka kwa Kuhani kama sadaka ya kuteketezwa, Bwana ataiona sadaka hiyo kama ni kafara ya Mtu sio ya ng’ombe, hivyo atajitafutia laana badala ya baraka.


Utaona maandiko yanazidi kulisisitiza hilo katika Mithali 15:8

.
Mithali 15:8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA…”

Ndio maana katika Isaya 66, Bwana anasema..


Isaya 66:3 “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao”.


Kwahiyo tunachoweza kujifunza ni kuwa, Bwana hapendezwi na matoleo mabaya, yeye alisema kulitii Neno lake ni bora kuliko dhabihu Soma (1Samweli 15:22).


Hivyo usipeleke madhabahuni fedha haramu, fedha iliyopatikana kwa rushwa, kwa wizi, kwa uuuzaji wa vitu haramu kama bangi, pombe, sigara au hata kwa uuzaji wa mwili.


Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya BWANA, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa BWANA, Mungu wako, yote mawili”


Vile vile hatupaswi kumtolea Mungu dhabihu huku hatuna mapatano sisi kwa sisi..


Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,
24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”


Bwana Yesu atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi?

HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Tomaso atake kwenda kufa pamoja na Lazaro? (Yohana 11:14-16).

Jibu: Tusome,

Yohana 11:14  “Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15  Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake.

16  Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, Twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye”

Kwa haraka ni rahisi kutafsiri kuwa Tomaso alitaka na yeye kwenda kufa pamoja na Lazaro, lakini kiuhalisia sio hivyo!.

Tomaso hakutaka kwenda kufa pamoja na Lazaro, bali hapo alimaanisha “kwenda kufa pamoja na Bwana Yesu”.

Ili tuelewe vizuri tuanze kusoma kisa hicho kuanzia juu mstari ule wa tano..(Zingatia vipengele vilivyoainishwa kwa herufi kubwa).

Yohana 11:5  “ Naye Yesu alimpenda Martha na umbu lake na Lazaro.

6  Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo.

7  Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, TWENDENI UYAHUDI TENA.

8  Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, JUZIJUZI TU WAYAHUDI WALIKUWA WAKITAFUTA KUKUPIGA KWA MAWE, NAWE UNAKWENDA HUKO TENA?

9  Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10  Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake.

11  Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.

12  Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.

13  Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.

14  Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15  Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake. 16  Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, TWENDENI NA SISI, ILI TUFE PAMOJA NAYE”

Katika kisa hiki tunaona Bwana Yesu anawapa taarifa wanafunzi wake ya kurejea tena kule Uyahudi ambapo walitaka kumpiga mawe mpaka afe!.. na taarifa hiyo ikawashitusha wanafunzi inakuwaje anataka kurudi tena huko kwenye hatari! (Maana yake si ndo anaenda kufa sasa!)

Lakini  Tomaso aliposikia wanafunzi wenzake wakimhoji hivyo, ndipo na yeye akawashauri kwamba wasimwache aende pake yake huko uyahudi, bali nao pia waende pamoja naye, ili kama ikitokea kauawa basi na wao wafe pamoja naye!.

Ni moyo mzuri aliokuwa nao Tomaso, lakini hakujua kuwa kufa kwaajili ya Kristo ni Neema na si jambo la kujiamulia tu au kujivunia kwamba linaweza kutendeka kwa uwezo wa mtu.

Mtume Petro alijaribu hilo zoezi kama la Tomaso likamshinda, kwasababu alidhani anaweza kufa ajili ya Kristo kwa nguvu zake..

Luka 22:31 “Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;

32  lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.

33  Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani AU HATA KIFONI.

34  Akasema, Nakuambia, Petro, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui”.

Zaidi sana huyu Tomaso ambaye alitaka kwenda kufa pamoja na Bwana, siku Bwana anakamatwa alimkimbia, hakuonekana!..(huenda ndo alikuwa Yule kijana aliyekimbia uchi, Marko 14:52)…na zaidi sana hata baada ya kufufuka kwake bado ilikuwa ni ngumu kuamini mpaka alipotokewa na Bwana Yesu..(huyo ndio mtu aliyetaka kwenda kufa na Yesu Yerusalemu)

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Tomaso hakutaka kwenda kufa na Lazaro, vinginevyo ingekuwa haina maana… lakini kinyume chake alitamani kwenda kufa pamoja na Bwana kwasababu aliamini huo ni ushujaa mkuu wa Imani.

Jambo tunaloweza kujifunza ni kuwa, hatupaswi kuzitumainia nguvu zetu, hatuwezi kusema tutamtumikia Mungu kwa nguvu zetu, hatuwezi kujivuna kuwa tutafanya hiki au kile kwa nguvu zetu, bali siku zote hatuna budi kuwa katika hali ya unyenyekevu, na kujishusha mbele za Bwana, kama tunatamani kufa kwaajili ya Bwana kifo cha kishujaa, basi tumalizie kwa kusema, BWANA TUSAIDIE

Na chochote kile tukifanyacho au tukikusudiacho ni lazima kumalizia kwa kusema “KWA MSAADA WA BWANA KITAFANIKIWA”.. Lakini tukijivuna kuwa tunaweza hiki au kile, tutaishia kumkana na hata kumsaliti.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti kulingana na (Zaburi 89:48)?

Nini maana ya “mtakayoyafunga duniani, yatakuwa yamefungwa mbinguni”?

Rudi nyumbani

Print this post