Kwanini Yuda aliitwa Iskariote?..nini maana ya Iskariote?

Kwanini Yuda aliitwa Iskariote?..nini maana ya Iskariote?


Jibu: Iskariote sio jina la mtu fulani, au la mzazi wa Yuda, bali ni jina lenye maana ya “Mtu wa Keriothi/ Kariote”…

Neno Iskariote ni neno la kigiriki lililoungwa na maneno mawili: “Is” ambalo maana yake ni “mwana wa” na la pili ni “Kariote”..likimaanisha mji wa Kariote au Keriothi
Kwahiyo ukiunganisha maneno hayo mawili maana yake ni “Mwana wa Keriothi”

Na Keriothi ni mji uliokuwepo katika Nchi la Moabu, ambayo kwasasa ni maeneo ya nchi ya Jordani.
Na Wamaobu walikuwa ni watu wa mataifa, hawakuwa waIsraeli, kwa urefu kuhusu Taifa hili unaweza kufungua hapa >>> MOABU NI WAPI

Sasa swali ni je! Kwanini Yuda aitwe hivyo, na asiitwe tu Yuda! Kwanini atambulike kama Mwana wa Keriothi(Iskariote)?… kulikuwa na umuhimu gani yeye kutajwa kwa jina hilo?.

Jibu rahisi ni kwamba, alitajwa vile ili kumtofautisha na wakina Yuda wengine, kwasababu kulikuwa na watu wengi wanaoitwa Yuda ambao pia walikuwa wanafuatana na Yesu. Na Kuna mwingine alikuwa mdogo wake Yesu.

Kwa mfano utaona kuna wanafunzi wawili wa Bwana Yesu waliokuwa na majina yanayofanana..wote walikuwa wanaitwa Simoni, sasa ili kuwatofautisha ndio mmoja akajulikana kama Simoni Petro na mwingine Simoni Mkananayo. (Mathayo 10:2-4).

Vile vile kulikuwa na wanawake wengi waliomfuata Bwana walioitwa Mariamu, sasa ili kuwatofautisha hao akina Mariamu, ndipo hapo wengine wakatajwa kulingana na miji waliyotokea mfano Mariamu aliyetolewa pepo saba alijulikana kama Mariamu Magdalene, kufuatia mji aliotokea ujulikanao kama Magdalene. (Luka 8:2).

Na Yuda Iskariote aliitwa hivyo kufiatia mji ambao Baba yake alitokea (Keriothi).

Yohana 6:71 “Alimnena Yuda, mwana wa Simoni Iskariote; maana huyo ndiye atakayemsaliti; naye ni mmojawapo wa wale Thenashara”.

Soma pia Yohana 13:2, na Yohana 13:26, huenda baba yake Yuda alikuwa ni myahudi lakini mwenyeji wa Kerioth pamoja na Yuda mwanae.

Kuhusiana na mji wa Keriothi au Kariote, pitia mistari ifuatayo; Amosi 2:2, Yeremia 48:24, na Yoshua 15:25.

Na sisi Bwana anatujua majina yetu kulingana na tabia zetu.

Kutoka 33:17 “BWANA akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, nami nakujua jina lako”

Mbele za Mungu kila mtu anajulikana kwa tabia yake…fulani mcha Mungu, fulani mwombaji, fulani mkaribishaji, fulani mwizi, fulani mzinzi, fulani msengenyaji.

Bwana atujalie tujulikane kwa majina mazuri na mema mbele zake ili tupate neema.

Kutoka 33:17 “BWANA akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, nami nakujua jina lako”

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

TUUTAFUTE USEMI MMOJA. TUUJENGE MNARA WA MUNGU

Rudi nyumbani

Print this post

Je! kuna mwanamke mwingine aliyempaka Bwana marhamu (manukato) zaidi ya Mariamu ndugu yake Lazaro?

Jibu: Kulikuwa na tukio zaidi ya moja la Bwana Yesu kupakwa mafuta…Tukio la kwanza ni hilo tunalolisoma katika injili tatu,  (Mathayo 26:6-13 na Marko 14:3-8  na Yohana 12:1-3), ambapo  biblia inaonyesha moja kwa moja kuwa ni Mariamu ndugu yake Lazaro, ndiye aliyempaka Bwana Marhamu siku sita kabla ya pasaka.

Tusome,

Yohana 12:1 “Basi, siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alifika Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye Yesu alimfufua katika wafu.

2  Basi wakamwandalia karamu huko; naye Martha akatumikia; na Lazaro alikuwa mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye.

3  Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu”.

Lakini tukirudi katika Injili ya Luka, tunasoma tukio lingine ambalo linakaribia sana kufanana na hili la Bethania, ambapo biblia inasema alitokea mwanamke mmoja mwenye dhambi na kuanguka miguuni pake na kulia huku akimpaka mafuta.

Jibu: Turejee..

Luka 7:36 “Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani.

37  Na tazama, mwanamke MMOJA WA MJI ULE, ALIYEKUWA MWENYE DHAMBI, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu.

38  Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.”

Sasa ni viashiria gani vinatuthibitishia kuwa yale yalikuwa ni matukio mawili tofauti?

  1. Katika Mlango wa 7 wa kitabu cha Luka tunaona Bwana Yesu alikuwa akihubiri Miji ya Galilaya (Naini na Kapernaumu), ambayo ipo kaskazini mwa Israeli, mbali kabisa na mji wa Bethania ambao upo kusini mwa Israeli, Na Mariamu dada yake Lazaro alikuwa anaishi huko Bethania mbali kabisa na Galilaya na Biblia inaonyesha tukio hili lilitokea huko katika mojawapo wa miji ya Galilaya.. ikimaanisha kuwa lilikuwa ni tukio lingine tofauti na lile lililotokea la Mariamu wa Bethania, na lilikuwa ni tukio lililowahi kutoka kabla ya hili la mwisho la Bethania.
  • Tunaona Mariamu wa Bethania, alipompaka Bwana Marhamu huko Bethania hakumpaka kwa machozi na toba, lakini huyu aliyempaka Marhamu akiwa Huko Galilaya, maandiko yanaonyesha kuwa alienda mbele zake akalia kwa machozi na toba, na hakuna aliyelalamika kwa upotevu wa ile Marhamu zaidi sana Yule Farisayo alimnung’unikia Bwana kwanini anakubali kuguswa na mtu mwenye dhambi.
  • Tukio la Bethania la Marimu ndugu yake Lazaro halikuhusishwa Bwana kupanguswa miguu yake na nywele za Mariamu.. lakini hili la Galilaya linataja kuwa mwanamke huyu alilia huku akimbusubusu miguu Bwana na kuipangusa kwa nywele zake.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa haya ni matukio mawili tofauti, yaliyotokea kukaribiana na biblia haikumtaja Yule mwanamke wa Galilaya alikuwa ni nani?.. labda huenda alikuwa ni Yule Yule Mariamu alimpaka mara mbili, au ni mwanamke mwingine ambaye biblia haijamtaja jina lake.

Lakini hayo yote si ya muhimu sana kuyajua, (kwamba ni nani, au ni matukio mangapi) lililo la muhimu kulijua ni tendo hilo la kiimani wanawake hawa waliloyoyafanya.. sasa kujua kwa undani Siri iliyokuwepo katika kumpaka Bwana mafuta fungua hapa >>> AKAKIVUNJA KIBWETA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE.

Bwana atubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?

SWALI: Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani? Ni mpangalio wake upoje kulingana na mwandishi?


JIBU: Kitabu Cha Zaburi hakikuandikwa na mtu mmoja, Bali ni mjumuisho wa waandishi mbalimbali. Kitabu hiki ndio kilichoandikwa na waandishi wengi kuliko vyote kwenye biblia.

Kiliandikwa katika nyakati mbalimbali Kwa kipindi Cha miaka elfu moja na zaidi..kitabu hiki kimebeba mashahiri, maombolezo, nyimbo na maombi.

WAANDISHI:

  1. DAUDI

Mfalme Daudi ndiye aliyeandika Kwa sehemu kubwa  kitabu hichi; 

Jumla Zaburi zilizojuliakana kuwa zimeandikwa na Daudi ni 73. Lakini pia zipo nyingine 2 ambazo hazikutajwa moja Kwa moja lakini waandishi wengine katika nyaraka zao walinukuu baadhi ya maneno kwenye Zaburi, na kusema ni ya Daudi.

Ambazo ni Zaburi 2 ambayo sehemu ya maandishi hayo yanatajwa katika Matendo 4:25, 

Na Zaburi 95 Waebrania 4:7

Hivyo kudhaniwa kuwa Daudi aliandika Zaburi 75;

Hizi ndio orodha ya hizo Zaburi 73 alizoziandika yeye;

3-9

11-32

34-41

51-65

68-70

86

101

103,

 108-110

122

124

131

133

138-145

2. SULEMANI

Mwandishi mwingine ni Sulemani yeye aliandika Zaburi mbili tu..ambazo ni  Zaburi 72 na Zaburi 127″

3. ETHANI na HEMANI

Nyingine zimeandikwa na Ethani na Hemani, Hawa ni watu ambao waliokuwa na hekima nyingi mfano wa Mfalme Sulemani, wanatajwa katika vifungu hivi;

1 Wafalme 4:30-31

30 Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri.31 Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka.

Ethani aliandika Zaburi moja tu nayo ni Zaburi 89

Hemani pia aliandika Zaburi moja ambayo ni Zaburi 88

4. MUSA

Mwandishi mwingine alikuwa ni  Musa yeye pia aliandika Zaburi 1 ambayo ni ya 90.

5. ASAFU

Zaburi nyingine 12 ziliandikwa na Asafu na familia yake.

Ambazo ni 

50, 73-83

6. WANA WA KORA

Wana wa Kora, waliandika Zaburi 11

  42, 44-49,84-85, 87-88 

7. WASIOTAMBULIKA

Na Zaburi nyingine 48, zilizobakia hazijulikani waandishi wake.

Hivyo Kwa ufupisho ni kwamba Daudi aliandika Zaburi 73, Sulemani 2, Musa 1, Ethani 1, Hemani 1, Asafu 12, Wana wa Kora 11, wasiotambulika ni 48.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata uchauzi zaidi ya kitabu Cha Zaburi pitia link hii >> https://wingulamashahidi.org/2020/11/27/vitabu-vya-biblia-sehemu-ya-9-kitabu-cha-zaburi/

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.

Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)

Rudi nyumbani

Print this post

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

(Masomo maalumu kwa Wakristo, Je! Unajijua nafasi yako?.. je unajijua kuwa wewe ni manukato yanayokubalika na pia yasiyokubalika kwa upande mwingine?).

Manukato ni neno lingine la “Marashi”.. Na kazi ya manukato/Marashi ni kukifanya kitu kivutie, hakuna mtu anayejipaka marashi ili mtu amkimbie. Lakini changamoto ni kwamba haijalishi marashi yatakuwa ni mazuri kiasi gani, ni lazima kwa upande mwingine kuna mtu yatamtia kichefuchefu tu. (Si kila marashi yaliyo mazuri kwa mtu, yatakuwa mazuri kwa watu wote).. ni lazima upande mmoja utayakosoa tu.

Na siku zote, marashi yaliyokosolewa huwa yanatia kichefuchefu na hata wakati mwingine kumuumiza Yule anayeyasikia..

Kadhalika biblia inasema kuwa sisi ni Manukato ya Kristo. Na kama ni manukato ni lazima upande mmoja yatakubalika na upande mwingine yatakatalika.. Na siri ya manukato ya Kristo ni kwamba wengi wanayachukia zaidi ya wale wanayoyapenda..

2Wakorintho 2:14 “Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu.

15  KWA MAANA SISI TU MANUKATO YA KRISTO, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea;

16  katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima. Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo?

17  Kwa maana sisi si kama walio wengi, walighoshio neno la Mungu; bali kama kwa weupe wa moyo, kama kutoka kwa Mungu, mbele za Mungu, twanena katika Kristo”.

Wakristo wengi wanadhani kuwa wanapookoka bali wataanza kupendwa, na kukubalika na kupokea kibali kila mahali. Ni kweli hayo yanaweza kutokea kwasababu kwa Mungu yote yanawezekana.. Lakini fahamu kuwa wewe ni marashi mazuri lakini yenye kuleta harufu mbaya kwa wanaopotea..

Maisha ya usafi na ukamilifu unayoishi ni harufu nzuri kwa wanaookolewa, (Maana yake ni mfano mzuri wa kuigwa, kwa waongofu wapya na waaliookoka), kuomba kwako na kufunga kwako na kuhubiri kwako ni harufu nzuri kwa waliookoka kama wewe.

Lakini kwa wale ambao hawamtaki Yesu, fahamu kuwa maisha yako ni kichefuchefu kwao….ni lazima watakupinga tu, ni lazima watakuletea vita tu, ni lazima watakukosa tu, ni lazima watakurushia mishale tu..Kwasababu kwao wewe ni manukato yenye harufu mbaya, tena harufu inayoleta mauti kabisa…yaani maisha yako yanawahukumu..

Hili ni jambo la kufahamu wewe uliyempokea Kristo na kuokoka!.. Kamwe usifikiri kuwa utaendelea furaha yako ndani ya Kristo ni jambo linalovutia machoni pa wengine… Ukristo ni vita, unapoamua kuwa mkristo ni kama mtu aliyevaa kombati na kuingia vitani.. Kwahiyo tegemea kukumbana na maadui wa imani, watakaokukosoa na kukutatisha tamaa..

Yohana 15:18  “Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.

19  Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.

20  Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Neno hili limetajwa mara moja katika biblia, kwenye kitabu cha;

Matendo 1:12 “Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato”.

Ni mwendo ambao ulitengwa maalumu wa mtu kusafiri siku ya sabato, ambao urefu wake ulikuwa ni dhiraa elfu mbili (2000), ambao ni sawa na Kilometa moja kwa makadirio.

Kutoka mlima wa mizetuni mpaka mjini Yerusalemu, ni umbali uliokuwa  ndani ya hiyo kilometa moja, ndio huo walisafiri mitume wa Bwana siku hiyo.

Lakini Je! Agizo hilo tunalipata wapi katika agano la kale?

Hakuna andiko la moja kwa moja katika torati ya Musa linaloeleza kuwa mwendo wa sabato, ulipaswa uwe ndani ya hizo dhiraa elfu mbili. Bali Marabi wa kiyahudi baadaye walidhani hivyo kulingana na uhalisia wa maandiko haya.

Kutoka 16:29 “Angalieni, kwa kuwa Bwana amewapa ninyi hiyo Sabato, kwa sababu hii huwapa siku ya sita chakula cha siku mbili; kaeni kila mtu mahali pake, mtu awaye yote asiondoke mahali pake kwa siku ya saba

Kwamba anaposema Usiondoke mahali pako, anamaanisha ndani ya mipaka ya mji wako, hii ikiwa na maana ukiwa ndani ya mipaka uliruhusiwa kutembea, utakavyo. Na kama ikitokea unatoka, basi hupaswi kusafiri Zaidi ya hizo dhiraa elfu 2000.

Na hiyo waliirithi kufuatana na sheria ya malisho ya nje ya mji ambayo walipewa walawi katika..

Hesabu 35:4 “Na yale malisho ya miji mtakayowapa Walawi, ukubwa wake utakuwa tangu ukuta wa mji kupima kiasi cha dhiraa elfu pande zote.  5 Nanyi mtapima hapo nje ya mji upande wa mashariki dhiraa elfu mbili, na upande wa kusini dhiraa elfu mbili, na upande wa magharibi dhiraa elfu mbili, na upande wa kaskazini dhiraa elfu mbili, huo mji ulio katikati. Hayo ndiyo yatakayokuwa kwao malisho ya miji”.

Hivyo kwa kurejea sheria hizo, wakahitimisha kuwa mwendo wa mtu kusafiri nje ya mji siku ya sabato ni hizo dhiraa elfu mbili(2000) au kilometa moja . Ndio Wakauita mwendo wa Sabato. Lakini hakukuwa na sheria ya moja kwa moja inayoeleza mwendo huo ulipaswa uwe katika vipimo hivyo.

Lengo la kufanya vile ni kuwafanya watu wasitawanyike mbali na eneo la kuabudia, ndani ya mji, siku hiyo ya Bwana.

Hata sasa. Ni lazima Kila mmoja wetu awe na mwendo wake wa sabato katika siku ya Bwana..kumbuka jumapili ni siku ya Bwana, hupaswi kwenda mbali na uwepo wa Mungu, siku hiyo sio siku ya kufanya biashara, sio siku ya kwenda kwenye mihangaiko isiyokuwa na lazima, Bali ni siku maalumu Kwa ajili ya ibada..penda kuwepo kanisani, mikutanoni, kwenye semina, kwenye mafundisho redioni,mitandaoni, kwenye vitabu vya kiroho.n.k.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni kweli hakuna aliyepaa mbinguni zaidi ya Mwana wa Adamu? (Yohana 3:13)

Je ni kweli Yesu peke yake ndiye aliyepaa mbinguni, na Eliya hakupaa wala Henoko? Kulingana na Yohana 3:13?

Jibu: Tusome,

Yohana 3:13 “Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”

Mstari huu lengo lake si kutoa taarifa za waliopaa mbinguni au ambao hawajapaa!, tukiusoma kwa lengo hilo basi ni rahisi kuchanganyikiwa, na kuona biblia inajichanganya…

Mfano mtu anaweza kusikika akitoa kauli hii “hakuna mtu aliyewahi kuja kwangu kunitazama, isipokuwa mtoto wangu tu”.. Kauli hiyo mtu asipojua kwanini imezungumzwa vile, anaweza kutafsiri kuwa “hakuna mtu yeyote aliyewahi kufika nyumbani kwake huyo ndugu, iwe mgeni au mwenyeji, isipokuwa mtoto wake tu…..maana yake anaishi tu peke yake peke yake, au nyumba yake ipo mafichoni mahali ambapo watu hawawezi kufika, au pengine amefunga mlango kwa wageni hivyo hakuna mtu yeyote anayeweza kumtembelea”…

Lakini kumbe hakumaanisha hivyo, yule aliyemsikia hakuanza kusikiliza mwanzo wa maneno yake bali alichukua kipande cha mwisho cha maneno yake… lakini kumbe maneno yake hasa yalianza hivi….. “Tangu nilipoanza kuugua, mpaka nilipopona hakuna mtu aliyewahi kuja kwangu kunitazama isipokuwa mtoto wangu tu “

Na kauli ya Bwana Yesu, aliposema hakuna aliyepaa juu ila aliyeshuka, ina mantiki hiyo hiyo…

Sasa Ili tuelewe vizuri, tuanzie kusoma mstari ule wa 12.

Yohana 3:12 “Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni?

13  Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”

Hapa tunaona ni Bwana Yesu anampa Nikodemu taarifa kuwa “yeye pekee ndio mwenye taarifa za mbinguni, yaani siri za ufalme wa mbinguni”  asizozijua mtu mwingine yeyote.

Na kwanini siri hizo anazo yeye tu peke yake?, na si mwingine yeyote?..Kwasababu ni yeye tu pekee ndiye aliyetokea mbinguni, wengine wote asili yao ni hapa duniani, hivyo hawawezi kujua mambo ya mbinguni wala siri za ndani za mbinguni, kwasababu hawakutokea huko. Lakini Yesu asili yake sio duniani..yeye alikuwepo mbinguni kabla hajazaliwa na Mariamu.

Nabii Eliya alipaa mbinguni lakini hakutokea mbinguni, hivyo hawezi kuyajua ya mbinguni, kwasababu asili yake ni duniani,  yeye  alizaliwa hapa  duniani kama wanadamu wengine wote, mbinguni alienda kama tu sehemu ya mwaliko.. Kama sisi tutakavyoalikwa siku ile ya mwisho ya parapanda.. Tutaenda kama wageni waalikwa, lakini Kristo si mgeni mwalikwa bali Mwalikaji/naye ni mwenyeji.

Ni sawa na Mtoto wa mfalme wa Taifa fulani, aje aishi Tanzania na baada ya muda arejee nchini mwake, halafu kuna kijana mwingine raia wa Tanzania, mzaliwa wa Tanzania apewe mwaliko wa kwenda kuishi Huko kwenye huo ufalme, kipindi chote cha maisha yake.. Je huyu kijana aliyealikwa anaweza kuwa sawa na yule kijana aliye mwana wa Mfalme?.. Au watakuwa na uelewa sawa kuhusiana na mambo ya huo ufalme?.

Jibu ni la! Ni wazi kuwa Huyu kijana wa Mfalme atakuwa  anajua siri nyingi za Taifa lake, kuliko huyu kijana aliyealikwa, kwasababu ni mzaliwa wa kule, na zaidi sana ni mwana wa mfalme, lakini huyu aliyealikwa hatajua sana mambo ya ufalme ule, kwasababu yeye ni kama mwalikwa tu.

Ni hivyo hivyo kwa Eliya na Henoko.. Hao ni waalikwa tu mbinguni, lakini hawakuwa wenyeji wa kule,

Lakini Yesu ni Mwalika, na tena ni mfalme.. hivyo Kristo pekee ndiye ajuaye mambo yote ya  mbinguni, siri zote za Ufalme wa mbinguni, kwasababu yeye ni mwana wa Mfalme na pia asili yake ni kwenye huo ufalme.

Ndio maana sasa biblia inasema hapo… “Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni? Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”.

Maana yake hakuna mtu aliepaa mbinguni kwenda kuzichukua siri na kutujuza sisi, isipokuwa Yule aliyeshuka kutoka kule, ambaye ni Yesu Kristo mwenyewe, Mwana wa Adamu.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

MJUE SANA YESU KRISTO.

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mikononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?


Mithali 17:16 “Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mkononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?”..

Hili andiko lina maana gani?

Jibu: Awali ni vizuri kufahamu hekima inayozungumziwa hapo ni hekima gani?

Hekima inayozungumziwa hapo si hekima ya ki Mungu, kwasababu hekima ya Mungu haipatikani kwa fedha…bali hekima inayozungumziwa hapo ni ile ya kiulimwengu, ambayo hiyo inaweza kupatikana kutoka kwa watu,na kwa njia ya kununuliwa (kwa njia ya kwenda katika shule za wenye hekima)…ambapo mtu atalipa kiasi fulani cha Ada na kisha kufundishwa hiyo hekima.

Mfano wa shule za hekima, ni hizi tulizonazo sasa, ambapo mtu atajiunga na shule fulani na kwenda kupewa Maarifa katika eneo fulani la maisha, ambayo yatamfanya aishi vizuri na kupata mafanikio katika maisha.

Kwahiyo hapo biblia iliposema… “Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mkononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?”

Tafsiri yake kwa lugha nyepesi ni hii………. “ina maana gani mpumbavu kuwa na fedha ya kulipia elimu yake na ikiwa hana Moyo wala Nia ya kuipata hiyo hekima?”

Ni jambo ambalo kweli halina Maana,…kwasababu hata akienda kutafuta kuinunua hiyo hekima hataipata kwasababu moyo wake haupo huko, hivyo ataenda kupoteza fedha tu…

Andiko hili linatufundisha umuhimu wa kufanya kitu kwa moyo (iwe cha kimwili Au cha kiroho)… Kama hujanuia kufanya kitu kwa moyo basi ni heri usikifanye kabisa kwasababu ni sawa na kupoteza muda au fedha.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini maombi kwa Marehemu si sahihi kibiblia?

Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama

TAFUTA HEKIMA, MAARIFA, UFAHAMU NA BUSARA.

Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

Rudi nyumbani

Print this post

Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?

SWALI: Kwanini vitabu vya biblia vipo katika mtiririko ule, na sio kinyume chake?

Ni vema kufahamu kuwa mtiririko wa kibiblia wa agano la kale na agano jipya, haukuwekwa na Mungu, kwamba kianze kitabu hiki kifuate hiki, kianze cha Mwanzo kisha kifuate cha Kutoka. Hapana bali ni utaratibu uliowekwa na wanadamu, ambao kimsingi unamaudhui mazuri, na uligawanya hivyo ili kumsaidia msomaji kufahamu vizuri, kuliko vingeorodheshwa  tu kila kimoja eneo lake, ingewia ngumu kwa msomaji anayependa kujifunza Biblia kuelewa kiwepesi.

Mtiririko ambao sisi tunaoutumia ni tofauti na mtiririko ambao Wayahudi wanautumia kwa vitabu vya agano la kale.

Kwa mfano mtiririko wetu (Ambao unajulikana kama mtiririko wa kiprotestanti), una vitabu 39 vya Agano la kale. Lakini mtitiriko wa Kiyahudi, una vitabu 24 kwa agano hilo hilo la kale,.

Vitabu vyetu ni kama vifuatavyo

Vitabu vya Sheria

  1. Mwanzo
  2. Kutoka
  3. Mambo ya Walawi
  4. Hesabu
  5. Kumbukumbu la Torati

Vitabu vya Historia

  • Yoshua
  • Waamuzi
  • Ruthu
  • 1Samweli
  • 2Samweli
  • 1Wafalme
  • 2Wafalme
  • 1Mambo ya Nyakati
  • 2Mambo ya Nyakati
  • Ezra
  • Nehemia
  • Esta

Vitabu vya Mashairi

  1. Ayubu
  2. Zaburi
  3. Mithali
  4. Mhubiri
  5. Wimbo ulio bora

Vitabu vya Manabii (Wakubwa)

  • Isaya
  • Yeremia
  • Maombolezi
  • Ezekieli
  • Danieli

Vitabu vya manabii (Wadogo)

  • Hosea
  • Yoeli
  • Amosi
  • Obadia
  • Yona
  • Mika
  • Nahumu
  • Habakuki
  • Sefania
  • Hagai
  • Zekaria
  • Malaki                                                     

Lakini utajiuliza kwanini biblia ya kiyahudi iwe na vitabu 24 na sio 39? Je vingine vimeondolewa? Jibu ni hapana, bali baadhi yao vilijumuishwa kama ni kitabu kimoja kwamfano.

> Vitabu viwili vya wafalme kwao ni kitabu kimoja.

> Vitabu viwili vya Mambo ya Nyakati kwao ni kitabu kimoja.

> Vitabu viwili vya Samweli kwao ni kitabu kimoja.

> Ezra na Nehemia vimeweka kama kitabu kimoja.

> Vitabu 12 vya Manabii wadogo kwao ni  kitabu kimoja.

Jumla yake ni vitabu 24 Badala ya 39.

Hivyo tukirudi katika biblia yetu, yenye vitabu 39 kwa agano la kale, Orodha ile haijawekwa kulingana na vipindi vilipoandikwa, bali kulingana na ‘asili ya vitabu’. Ndio hapo utaona hiyo migawanyo mikuu mitano (Yaani vitabu vya Sheria, vya historia, vya mashairi, vya Manabii wakubwa na wale wadogo).

Kutaja manabii wakubwa haimaanishi kuwa walikuwa na vyeo vya juu au walikuwa na nguvu zaidi ya wale wengine hapana, bali ni kutokana na wingi wa uandishi wao, yaani waliokuwa na uandishi mwingi waliwekwa katika kundi hilo la manabii wakubwa.

Tukirudi katika agano jipya.

Vipo vitabu 27, na vyenyewe pia havijaandikwa kulingana na wakati wa uandishi, japo havipishani sana na wakati wa uandishi.

Huu ndio mgawanyo wake.

Vitabu vya Injili

  1. Mathayo
  2. Marko
  3. Luka
  4. Yohana

Kitabu cha Historia

  • Matendo

Nyaraka za Paulo

  • Warumi
  • 1Wakorintho
  • 2Wakorintho
  • Wagalatia
  • Waefeso
  • Wafilipi
  • Wakolosai
  • 1Wathesalonike
  • 2Wathesalonike
  • 1Timotheo
  • 2Timotheo
  • Tito
  • Filemoni

Nyaraka kwa wote

  1. Waebrania
  2. Yakobo
  3. 1Petro
  4. 2Petro
  5. 1Yohana
  6. 2Yohana
  7. 3Yohana
  8. Yuda

Unabii

  • Ufunuo

Halikadhalika Nyaraka za Mtume Paulo ziliorodheshwa katika mpangilio ule kutoka na  urefu wa uandishi na sio umuhimu wa nyaraka Fulani zaidi ya nyingine, kwamfano utaona kitabu cha kwanza kwa urefu cha Mtume Paulo ni Warumi na ndio kilichowekwa cha kwanza. Vilevile kirefu zaidi ya vyote alivyoviandika kwa Watu, ni cha Timotheo ndicho kilichopangiliwa cha kwanza.

Lakini pamoja na kwamba havikuweka katika mpangalio wa nyakati za uandishi bado zinamtiririko mzuri unaelekeana na historia, kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka ufunuo.  Japo pia katika usomaji haimaanishi ufuate mtiririko huo, bali unaweza kuanza vyovyote upendavyo kwa jinsi Roho Mtakatifu atakavyokuongoza.Kwasababu hakuna sehemu yoyote katika maandiko tumewekewa mtiririko huo.

Pia zipo biblia nyingine mfano ile ya Kikatoliki yenye vitabu 73, ambayo kimsingi haijavuviwa na Roho wa Mungu kwani kuna baadhi ya vitabu vimeongezwa ambavyo hukinzana na mafundisho ya msingi ya imani, na hivyo hatupaswi kuifuata. Biblia yetu ina vitabu 66 tu. Kama vilivyoorodheshwa hapo juu. Zaidi ya hivyo hutoka kwa Yule mwovu.

Bwana akubariki sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

HISTORIA YA BIBLIA YA KING JAMES, INA FUNZO GANI KWETU?

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya kiMungu?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

JE BWANA YESU ALIMTOKEA YUDA BAADA YA KUFUFUKA KWAKE?.

Je Bwana Yesu alimtokea Yuda baada ya kufufuka kwake?.. maana tunasoma katika 1Wakorintho 15:5 kuwa aliwatokea wale Thenashara ambao mmojawao alikuwa ni Yuda.

Jibu: Kwanza ni muhimu kujua maana ya Neno “Thenashara”.. Tafsiri ya Thenashara ni “kumi na mbili”. Maana yake popote biblia inapotaja neno hilo, iliwalenga wale Mitume 12 wa Bwana Yesu.

Na katika kipindi cha huduma ya Bwana Yesu, Yule Yuda aliyemsaliti alikuwa miongoni mwa hao Thenashara. Lakini tunaona baada ya kufa walibaki Mitume 11 tu..na kipindi Bwana Yesu anafufuka Yuda tayari alikuwa ni Marehemu kwani alijinyonga kabla hata ya Bwana kufufuka, hivyo hakuuona ufufuo wa Bwana,  Lakini tukienda mbele katika kitabu cha 1Wakorintho 15:3 tunasoma kuwa Bwana aliwatokea wote 12.. Je ni kwamba biblia inajichanganya au la?

Tusome..

1Wakorintho 15:3  “Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyoyapokea mimi mwenyewe, ya kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko;

4  na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;

5 na ya kuwa alimtokea Kefa; TENA NA WALE THENASHARA;

6  baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala”

Ni kweli Bwana aliwatokea wale Thenashara (yaani Mitume 12), lakini Yule wa 12 hakuwa Yuda kwasababu biblia inasema nafasi yake ilichukuliwa na mtu mwingine aliyeitwa Mathiya.

Tusome.

Matendo 1:23  “Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya. 24  Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

25  ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. 26  Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye AKAHESABIWA KUWA PAMOJA NA MITUME KUMI NA MMOJA”

Hapo anasema Mathiya akahesabiwa kuwa pamoja na Mitume 11, maana yake yeye alikuwa wa 12. Kwahiyo Mathiya alihesabika miongoni mwa Thenashara, na ndio maana hapo katika 1Wakorintho 15:5 Mtume Paulo kataja kumi na Mbili, lakini Yule wa 12 hakumlenga Yuda bali Mathiya.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Thenashara ni nini? (Marko3:16)

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?

Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?

Rudi nyumbani

Print this post

Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?

SWALI: Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?


Mimbari ni eneo lililoinuka ambalo limetengwa rasmi katika kanisa kwa ajili ya Neno la Mungu kuhubiriwa, au taarifa za kikanisa kuwasilishwa, au huduma nyingine za kiibada kutendeka kama vile uimbaji wa kwaya.

Lakini Madhabahu ni eneo la kanisa ambalo watu huenda kuomba, kutoa sadaka, kupeleka shukrani na sifa, na kushiriki meza ya Bwana (yaani mahali pa kukutana na Mungu). Madhabahuni pa Mungu sio tu pale mbele ya kanisa, bali ni lile eneo lote la kanisa. Isipokuwa tu lile la mbele ndio linasimama kama kitovu cha madhabahu yote.

Mara nyingi mimbari pia huwa palepale madhabahuni. Hivyo unaweza kusikia mtu anasema nakwenda kusimama madhabahuni kuhubiri, mwingine utamsikia anasema nakwenda kusimama mimbarani. Wote wawili hawajabadili maana.

Hivyo ikiwa unakwenda kwa kuhubiri, au kuhutubu, au kuimba kwaya kiuhalisia hapo ni sawa na unasimama mimbarani, lakini ikiwa unakwenda kwa ajili ya kuomba, kutoa sadaka, kufanya ibada kama kusifu na kuabudu, hapo huisogelei mimbari bali madhahabu ya Mungu.

Mimbarani ni mahali pa kusikilizwa, lakini madhabahuni, ni mahali pa kushiriki

Mambo ambayo hupaswi kufanya mimbarani kama mhubiri.

  • Kutoka toka sana nje ya mimbari pindi uhubiripo
  • Kufundisha maudhui ambayo yapo nje ya Neno la Mungu. Mfano, siasa, michezo
  • Kujigamba/ Kujisifu zaidi ya kumtukuza Kristo
  • Kupuuzia kujiandaa, kimaombi na kiroho, kabla ya kusimama mimbarani

Mambo ambayo hupaswi kufanya uwapo madhahabuni kama mshirika.

  • Usitoe sadaka yako kama una neno na ndugu yako.(Mathayo 5:23-24)
  • Usivae mavazi yasiyo na utukufu machoni pa Bwana
  • Usizunguke zunguke, au kuzungumza ovyo uwapo kanisani (kuwa mtulivu). Kumbuka eneo lote la kanisa ni madhabahu ya Mungu, na sio pale mbele tu.
  • Hakikisha huchelewi kufika madhabahuni pa Mungu, wala huikatishi ibada na kuondoka

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?

Biblia inasema tujihadhari na “Mbwa” hawa mbwa ni akina nani? (Wafilipi 3:2)

UPAKO NI NINI?

Rudi nyumbani

Print this post