Blog Archive

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

kalamu yenye uongo
Wingu la Mashahidi
KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.
Loading
/

SWALI: Mstari huu una maana gani? Je, ni kweli waandishi waliweza kubadilisha baadhi ya maneno ya torati, Na hivyo inaifanya biblia isiamike hadi sasa?

Yeremia 8:8 “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.

JIBU: Hii ni hoja inayotumiwa sana na wapinga-biblia, au wapinga-ukristo. Wakisimamia mstari huu, na kusema, unaona? Biblia ilichakachuliwa, zamani na waandishi wa kiyahudi kwa kuongeza baadhi ya maneno katika torati  iliyoandikwa na mwenyezi Mungu,.. Kwahiyo hiyo inathibitisha kuwa  biblia ni kitabu chenye kasoro..

Lakini je tukisoma vifungu hivyo, vinatuambia waliibadilisha torati?

Kabla ya kuendelea kusoma zaidi, embu tuitafakari tena hiyo kauli hapo mwishoni, anasema  “kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo”. Ahaa Kumbe waandishi ndio wameifanya kuwa uongo..Lakini yenyewe kama yenyewe sio uongo.. Mfano nikikuambia, unanifanya kuwa mwongo mbele za ndugu zangu, haimaanishi kuwa mimi ni mwongo..maana yake ni kuwa, pengine ni kwasababu uliyawakilisha  maneno yangu isivyopaswa, aidha kwa kuongeza chumvi au kupunguza, na kwasababu hiyo basi, mimi nikaonekana nimeongopa, lakini sivyo, mimi nilisema ukweli mwanzo, isipokuwa wewe ndio umeniwakilisha vibaya.

Ndivyo ilivyokuwa hapo, waandishi, ambao kazi yao kubwa ilikuwa ni kufundisha na kuwaelezea watu, walianza, kutoa tafsiri zisizo sawa za torati, na kuwafundisha watu na kuwaandikia, mfano Bwana Yesu alisema, waliipindua amri ya tano;  inayosema waheshimu baba yako na mama yako, na kuwaambia watu, ikiwa kuna chochote umekiweka wakfu hupaswi kumsaidia mzazi wako, hata kama akiangamia kwa njaa ni sawa tu..Jambo ambalo Mungu hakuliagiza hata kidogo, ilikuwa ni wajibu wa kila mtu kumsaidia mzazi wake, awapo katika uhitaji (Soma Marko 7:7-13)

Umeona, sasa tukirudi kwenye ile habari ya mwanzo ili kuthibitisha hilo vizuri, ukiendelea kusoma vifungu vinavyofuata utaona Yeremia, anaeleza kwa undani jinsi kalamu za hao waandishi zilivyoweza kuipa torati tafsiri zisizo sahihi..

Yeremia 8:8 “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.

9 Wenye hekima wametahayari, wamefadhaika na kushikwa; tazama, wamelikataa neno la Bwana, wana akili gani ndani yao?

10 Basi, kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao na mashamba yao nitawapa wale watakaowamiliki; MAANA KILA MMOJA WAO, TANGU ALIYE MDOGO HATA ALIYE MKUBWA, NI MTAMANIFU; TANGU NABII HATA KUHANI, KILA MMOJA HUTENDA MAMBO YA UDANGANYIFU.

11 KWA MAANA WAMEIPONYA JERAHA YA BINTI YA WATU WANGU KWA JUU-JUU TU, WAKISEMA, AMANI, AMANI, WALA HAPANA AMANI.

12 Je! Walitahayarika, walipokuwa wametenda machukizo? La! Hawakutahayarika, wala hawakuweza kuona haya usoni; basi wataanguka miongoni mwao waangukao; wakati wa kujiliwa kwao wataangushwa chini, asema Bwana..

Umeona hapo? Anasema, hao waandishi na makuhani, wanawatabiria watu amani, amani, na kuwaambia mnaishi sawasawa na torati ya Mungu inavyosema, hivyo hamwezi kupatwa na madhara, ili hali ndani yao wanatamani, ni waovu, waabudu masanamu, wanakula rushwa n.k.. 

Wakati torati inakataza vikali vitu hivyo, wenyewe wanawatumainisha watu, Mungu anawapenda, ndio hapo anasema,  wanawaponya jeraha zao kwa juu juu tu, mwisho wa siku  wanaadhibiwa, halafu wanasema Mungu ni mwongo.. Mbona anatupiga bila sababu!.

Je! Waandishi wa namna hii wapo hadi sasa?

Jambo hili lipo hadi sasa katika kanisa la Mungu, Siku hizi za mwisho makristo na manabii wengi sana wa uongo wametokea, nao wanawaponya watu wa Mungu juu juu tu, hawawaelezi ukweli, mpaka inafikia hatua Mungu anaonekana mwongo, hasikii wala hajibu.

Wanawaambia,  utafanikiwa, utabarikiwa, kesho yako ni ya kung’ara kama jua, wanawaambia watoe sadaka nyingi, watumie maji ya upako, mafuta na chumvi, wakati mwingine wafunge mwaka mzima, Mungu atawabariki.. Lakini wanasahau kuwa hao watu wana mizigo ya dhambi, ndiyo inayowafanya wasijibiwe maombi yao.. Kama vile maandiko yanavyosema..

Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.

3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya”.

Hivyo hao watu wanataabika, januari mpaka disemba, lakini hawaona nuru yoyote, hawaona uzima wowote, ndio kwanza hali inakuwa mbaya, mwishoni wanakataa tamaa wanasema Mungu hajibu maombi, wanawageukia waganga wa kienyeji.

Ndugu, Neno la Mungu ni kweli kabisa, akisema atakuponya, atakuponya kweli, akisema atakubariki atakubariki kweli, lakini ni sharti ujue, anataka nini kwanza kwako ili hivyo vyote vikujie.. Anachotaka ni wewe uache dhambi, uache, rushwa, uache uzinzi, uache uongo, uache vimini, uache fashion za kidunia, anasa, uache ulevi, uwe mtakatifu. Ndipo hayo yote yatakapokujia..

Epuka injili zizisogusia dhambi katika maisha yako, ziepuke kama ukoma, hizo huwa zinakuja na maneno mazuri sana ya kushawishi na kufariji, lakini hazitakusaidia chochote, Mungu ni mtakatifu, kamwe hajibu maombi ya mwenye dhambi.

Je! Umeokoka?  Kweli kweli kwa kumaanisha kumfuata Kristo? Kama la! Basi huu ndio wakati wako sasa kuanza upya na Kristo. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi, waweza tupigia kwa namba uzionaza hapo chini.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAJIBU YA MASWALI YANAYOULIZWA NA WASIO WAKRISTO (Sehemu ya kwanza).

Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?

Yesu ni Mungu?, Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?

Nini maana ya “Torati na manabii”?

Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Rudi nyumbani

Print this post

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

unawaza nini juu ya ufalme wa mbinguni?
Wingu la Mashahidi
UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?
Loading
/

Unawaza nini juu ya kuipeleka injili mbele?..Je unafikiri nini juu ya hali ya kiroho ya  wanao miaka kadhaa mbele?, endapo parapanda itakuwa haijalia miaka 20 ijayo, je hali ya kiroho ya wanao itakuwaje, ukilinganisha na kasi ya maadili kuporomoka?.. Je umewahi kufikiri kufanya chochote leo hii, ili miaka ya mbeleni watoto wako au Watoto wa wengine, wasikose chakula cha uzima?…

Kizazi tulichopo ni kizazi kinachoharibika kila siku, umewahi kufikiri hali itakuwaje miaka 10 mbeleni?..kama umewahi kufikiri kwamba hali utakuwa mbaya Zaidi kuliko sasa, basi pia jiulize leo hii unafanya nini ili wakati huo utakapofika, shetani asipate nafasi inayoiona mbeleni.

Kumbuka wewe usipotumia muda wako leo, au akili zako leo, au nguvu zako leo, kufikiri na kufanya jambo lolote juu ya ufalme wa Mbinguni, Bwana atafanya kupitia wengine, (kwasababu kazi yake ni lazima iende mbele) lakini wewe wewe utakuwa umejipunguzia thawabu zako mbele zake.

Hebu Leo tujifunze juu ya watu wawili katika biblia, ambao kupitia hao, tutapata hamasa na hekima katika kufikiri kuujenga ufalme wa mbinguni.

Mtu wa kwanza ni DANIELI, na wa pili ni YUSUFU. Watu hawa wawili wote walijaliwa uwezo wa kutafsiri ndoto, lakini kila mmoja kwa namna yake.

DANIELI:

Kuna wakati Mfalme Nebkadneza, (Mfalme wa Babeli) aliota Ndoto, lakini akawa ameisahau ile ndoto, na Danieli alipomwomba Bwana, aliweza kufunuliwa ndoto ile Pamoja na Tafsiri yake..na akaenda kumwambia mfalme, na ndoto ile na tafsiri yake vikathibitika..Na Mfalme akamtukuza sana Danieli, lakini si kama Yusufu.

YUSUFU:

Farao Mfalme wa Misri, naye aliota ndoto kama Nebukadneza…na ndoto ile alipoamka aliikumbuka…lakini cha ajabu ni kwamba hakuwaficha watafsiri wake ndoto ile, bali aliwahadithia alichokiota..yeye alichokuwa anahitaji tu ni maana ya ile ndoto..

Na alikuwa anajua kuwa watatokea waongo wengi, ambao watamwambia uongo..na kweli walitokea wengi wakampa tafsiri ya ndoto yake..lakini tafsiri zote hizo alizikataa..

Sasa ni Siri gani iliyofanya Tafsiri ya Yusufu ikubalike Zaidi ya zile nyingine zote??

Siri yenyewe ni mikakati baada ya kuielezea ile tafsiri..

Yusufu baada ya kusema kuna miaka 7 ya neema inakuja na 7 ya Njaa.. hakuishia hapo tu!.. lakini alitoa mikakati ni NINI CHA KUFANYA KATIKA HIYO MIAKA 7 YA NEEMA NA MIAKA 7 YA NJAA. Ndio utaona akamshauri Farao atafute mtu mwenye akili amweke juu ya kazi zake zote akusanye chakula cha kutosha katika miaka ya neema, ili itakapokuja miaka ya njaa basi hazina iwepo kubwa. (Hilo ndio wazo lililompandisha hadhi Yusufu, na wala si tu tafsiri)!..

Farao aliona hata kama tafsiri itakuwa ni ya UONGO, lakini wazo alilotoa YUSUFU NI LA HEKIMA NA AKILI…, hata kama Njaa haitakuja kama alivyotafsiri, lakini wazo tu la kuweka chakula akiba ni wazo kubwa sana na la akili sana, ambalo pengine katika utawala wake wote Farao hajawahi kushauriwa hivyo…

Tusome..

Mwanzo 41:28 “ Ndivyo nilivyomwambia Farao, ya kwamba Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya hivi karibu.

29 Tazama, miaka saba ya shibe inakuja, katika nchi yote ya Misri.

30 Kisha kutakuja miaka saba ya njaa baada yake; na shibe ile yote itasahauliwa katika nchi ya Misri, na njaa itaiharibu nchi.

31 Wala shibe ile haitajulikana katika nchi kwa sababu ya njaa inayokuja baadaye, maana itakuwa nzito sana.

32 Na ndoto ya Farao kwa vile ilivyokuja mara mbili, ni kwa sababu neno hilo Mungu amelithibitisha, na Mungu atalitimiza upesi.

33 BASI, FARAO NA AJITAFUTIE MTU WA AKILI NA HEKIMA AMWEKE JUU YA NCHI YA MISRI.

34 FARAO NA AFANYE HIVI, TENA AKAWEKE WASIMAMIZI JUU YA NCHI, NA KUTWAA SEHEMU YA TANO KATIKA NCHI YA MISRI, KATIKA MIAKA HII SABA YA KUSHIBA.

35 NA WAKUSANYE CHAKULA CHOTE CHA MIAKA HII MYEMA IJAYO, WAKAWEKE AKIBA YA NAFAKA MKONONI MWA FARAO WAKAKILINDE KUWA CHAKULA KATIKA MIJI.

36 NA HICHO CHAKULA KITAKUWA AKIBA YA NCHI KWA AJILI YA MIAKA HIYO SABA YA NJAA, ITAKAYOKUWA KATIKA NCHI YA MISRI, NCHI ISIHARIBIKE KWA NJAA.

37 NENO HILO LIKAWA JEMA MACHONI PA FARAO, NA MACHONI PA WATUMWA WAKE WOTE.

38 Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?

39 Farao akamwambia Yusufu, Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe.

40 Basi wewe utakuwa juu ya nyumba yangu, na kwa neno lako watu wangu watatawaliwa. Katika kiti cha enzi tu nitakuwa mkuu kuliko wewe”.

Umeona?.. watafsiri wengine walikuwa wanakuja na tafsiri zao lakini mwisho wa siku wanamshauri Farao mambo yasiyo na hekima, wala yasiyojenga, wala yasiyo na manufaa..ndio maana hata tafsiri zao Mfalme alizikataa.. Lakini  Yusufu alipotoa tafsiri na mikakati bora baada ya ile tafsiri ndipo hata tafsiri yake ikathibitika.

Na utaona Yusufu alipokea kibali sana mbele ya Farao, Zaidi hata ya Danieli alivyotukuzwa na Nebukadreza.

Je na wewe unataka kibali leo mbele za Mungu? Kama Yusufu alivyopata mbele ya Farao??..kama ndio! basi anza kufikiri kuhusu Injili ya Kristo, katika siku za mbeleni, na anza kufanya kitu kuanzia sasa. Kama ni mhubiri basi weka hazina kwa vizazi vinavyokuja… Kama ni mtu wa kukirimu, basi changia injili kwa mali zako kwa kadiri uwezavyo, ili kusudi Watoto wanaochipukia wasikue na kukuta idadi ya disco na bar zimezidi makanisa, wasije wakakuta idada ya vikundi vya wahuni vimezidi vya watu wema, wasije  wakakutana na ugumu wa kuitafuta injili ya kweli, Zaidi ya huu tulionao sisi katika kizazi chetu..

 shetani anayo mikakati sasahivi ya kuharibu kizazi hata cha tano kijacho..na hata sasa kashaanza kufanya juhudi hizo, inatupasaje sisi, tunaosema tumeokoka sasa? Kama wewe umeipata injili ya kweli, kiurahisi, basi rahisisha pia kwa wanaokuja, ambao kwa ambao hawajasikia..ndivyo Mungu atakavyokupa kibali.

Mithali 13:22 “Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi”

Tujifunze kwa Yusufu, ili na sisi tupate kibali mbele za Mungu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Kwanini  vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.

Rudi nyumbani

Print this post

Mti wa Mshita ni mti wa namna gani?

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
Mti wa Mshita ni mti wa namna gani?
Loading
/

Swali: Mti wa Mshita uliotengenezea sanduku la Agano ndio upi kwasasa?(Kutoka 25:10)

Jibu: Tusome

Kutoka 25:10 “Nao na wafanye sanduku la MTI WA MSHITA; urefu wake na uwe dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu, na kwenda juu kwake dhiraa moja na nusu.

11 Nawe ulifunike kwa dhahabu safi, ulifunike ndani na nje, nawe tia na ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote”.

Mshita ni jamii ya miti ambayo hata sasa ipo, na inapatikana katika sehemu nyingi za dunia, ikiwemo katika bara letu la Afrika, na hata katika Afrika mashariki.  (Tazama picha juu). Mti wa Mshita ni mti unaostahimili ukame zaidi ya miti mingi.

Tabia za mti wa mshita, ni kwamba ni moja ya miti migumu, na vile vile ni mti ambao hauharibiwi  na wadudu wala maji, wala hauingiaa fangasi kirahisi, jambo linaloifanya mbao ya mti huo iweze kutumika kutengenezea baadhi ya vyombo vya kuhifadhia vyakula, na sifa nyingine ya mbao ya mti wa Mshita ni rahisi kupakika rangi, kwasababu uso wake ni mwororo.

Sasa Kwanini Sanduku la Agano lilitengenezwa kwa mti wa Mshita?

Jibu, ni kwasababu ya tabia au sifa za mti huo.

Ndani ya Sanduku la Agano kulihifadhiwa chakula (yaani ile pishi ya mana) kwaajili ya ukumbusho wa vizazi vijavyo vya wana wa Israeli..Hivyo ni lazima chakula hicho kihifadhiwe ndani ya sanduku lililo imara lisiloingia fangasi wala wadudu waharibifu. Mbao nyingine zaidi ya Mshita, hazina sifa hizo!

Vile vile ndani ya Sanduku kulikuwa na zile mbao mbili, ambazo Musa aliambiwa azitengeneze, zilizoandikwa Amri kumi na chanda cha Mungu mwenywe, Mbao hizo ziliwekwa ndani ya Sanduku kuwa ukumbusho wa daima, hivyo ni lazima zihifadhiwe katika Sanduku lililo gumu ambalo haliharibiki haraka..

Na vile vile kulikuwa na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka, ambayo ilihifadhiwa nayo pia kama ukumbusho wa utumishi wa kikuhani wa nyumba ya Lawi.. Fimbo hiyo nayo ilipaswa ihifadhiwe ndani ya sanduku imara lisiloruhusu unyevunyevu au maji kuingia.

Na sanduku la Agano linafananishwa na mioyo yetu..  Katika kitabu cha Yeremia 31:31, Biblia ilitabiri kuwa katika Agano jipya tulilopo sisi, sheria za Mungu zimeandikwa mioyoni mwetu.. Mioyo yetu kwa Bwana ni kama mti wa Mshita, Hivyo hatuna budi kuzidi kuiimarisha mioyo yetu, kwa kukaa mbali na dhambi ili tuzidi kuzidumisha sheria za Mungu katika mioyo yetu.

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

Mwerezi ni nini?

FANYA BIDII ZOTE ULE MATUNDA YA UZIMA.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

wana wa manabii
Wingu la Mashahidi
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
Loading
/

Swali: Katika biblia tunasoma sehemu kadha wa kadha zikiwataja “wana wa manabii”.. Je! Hawa wana wa manabii walikuwa ni watu gani?, na kazi yao ilikuwa ni ipi? Na kwanini waliitwa hivyo?.. Na je hata leo kuna wana wa manabii?

Jibu: Ni kweli Katika Agano la kale lilikuwepo kundi la watu waliojulikana kama Wana wa Manabii. (Soma 1Wafalme 20:35, 2Wafalme 6:1, 2Wafalme 4:1, na 2Wafalme 2:5).

Watu hawa walikuwa ni “manabii wa Mungu”, ambao walijitia katika kifungo cha kujifunza juu ya Nabii zilizotangulia kabla yao..

Kumbuka sio kujifunza jinsi manabii wanavyoishi au wanavyokula au wanavyoona maono!… La! Hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kumfundisha mtu mwingine namna ya kuona maono!…hivyo ni vipawa vya Mungu ambayo ni Mungu mwenyewe anaviweka ndani ya mtu, na hatujifunzi wala hatufundishwi.. Ni sawa na ndoto…

Hakuna mtu anayeweza kumfundisha mwenzake jinsi ya kuota!.. Ndoto zinakuja zenyewe, kwasababu ni vipawa  vya asili ambavyo Mungu kaviweka kwetu sote.. Na nabii za Mungu, zinawajia watu maalumu ambao Bwana kawachagua, na si kupitia kujifunza!.

Kwahiyo hawa wana wa manabii, au kwa lugha nyingine “Wanafunzi wa manabii” walikuwa ni watu waliojikita kujifunza Nyakati na Majira, Pamoja na Nabii zilizotangulia kutolewa na manabii wengine waliowatangulia..(kumbuka walikuwa wanajulikana kama wana wa manabii, na sio wana wa NABII!)..

Na lengo la kufanya hivyo (yaani kupokea maarifa hayo) ni ili wawe salama, na wawe na uhakika wa Nabii watakazozitoa isije wakapotoka na kutoa unabii wa uongo.

Kwa mfano Nabii anaweza kuona maono au kupata ujumbe kuhusu Taifa la Israeli, sasa ili authibitishe ujumbe ule au ono lile kama kweli ni kutoka kwa Bwana, ni sharti awe na Nabii nyingine za kutosha, za waliomtangulia zinazosapoti ono lake hilo jipya!..  Na akija kugundua kuwa Nabii mwingine, mkuu aliyetangulia alishatabiri jambo kama hilo au linalokaribiana na hilo… basi ndipo Ono lake hilo linathibitika… lakini akija kukuta ono lake linakinzana na maono ambayo manabii wakuu waliyatoa, ndipo analiacha, kwasababu sio kutoka kwa Bwana… (kwasababu kamwe Bwana hawezi kujipinga katika maneno yake).

Hivyo ndio maana ilihitajika shule ya manabii, ambayo lengo lake ni kujifunza kujua Nabii zilizotangulia juu ya watu, na mataifa…

Ili tuzidi kuelewa vizuri, utakumbuka kipindi cha Nabii Yeremia wakati anatabiri kwamba Israeli watachukuliwa utumwani kwenda Babeli.. utaona Yeremia alikuwa ni mtu mwenye elimu ya kutosha kuhusu Nabii zilizotangulia, alihakiki jumbe anazozipokea katika maono, kwa nabii za waliomtangulia kama wakina Isaya, na wengineo..

Na jambo moja utaona alilojifunza ni kuwa “Manabii karibia wote, hawakuwahi kutabiri juu ya amani kwa mataifa, manabii wengi walikuwa wanatabiri juu ya Vita na Mabaya na Tauni”.. Na Yeremia alijua Mungu hawezi kujipinga.. Hivyo maono yake aliyahakiki kwa namna hiyo..

Lakini utaona alitokea mtu anaitwa Hanania, ambaye alijitokeza na kuanza kutabiri juu ya Amani kwa Israeli kwamba hawataenda utumwani, watakuwa salama, ni ilihali Taifa zima limemwacha Mungu..jambo ambalo linakinzana na Nabii Mungu alizozitoa kupitia manabii wakuu waliotangulia… Na Yeremia kuliona hilo akamwambia Hanania maneno yafuatayo…

Yeremia 28:7 “Lakini lisikilize sasa neno hili nilisemalo, masikioni mwako, na masikioni mwa watu wote,

8 MANABII WALIOKUWAKO KABLA YA ZAMANI ZANGU, NA ZAMANI ZAKO, WALITABIRI JUU YA NCHI NYINGI, NA JUU YA FALME KUBWA, HABARI YA VITA, NA YA MABAYA, NA YA TAUNI”.

Umeona jambo Yeremia alilomwambia huyu Hanania?…

Yeremia alikuwa ni Mwana wa manabii, lakini Hanania alikuwa ni mtu tu aliyejizukia na kujiita Nabii, hana elimu yoyote ya Nabii za Mungu.. na akaanza kuwafariji watu kwa maneno ya uongo!..Jambo ambalo lilimchukiza sana Mungu, na hata kumwua Hanania.

Yeremia 28:15 “Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, Sikia sasa, Ee Hanania; Bwana hakukutuma; lakini unawatumainisha watu hawa maneno ya uongo.

 16 BASI BWANA ASEMA HIVI, TAZAMA, NAKUTUMA UENDE ZAKO TOKA JUU YA USO WA NCHI; MWAKA HUU UTAKUFA, KWA SABABU UMENENA MANENO YA UASI JUU YA BWANA.

17 BASI NABII HANANIA AKAFA, MWAKA UO HUO, MWEZI WA SABA”.

Lakini leo hii shetani kaligeuza hili Neno “Wana wa Manabii”. Leo hii kuna watu wamefungua vyuo vyao, wakiwa wenyewe wanajiita Manabii wakuu, na vijana wao wanawaita “wana wao (yaani wana wa manabii)”.. Lakini ukiingia katika madara yao na kusikia wanachofundishwa, ni huzuni tupu!.

Utasikia wanachofundishwa ni jinsi ya kuona maono, jinsi ya kutumia na kutengeneza mafuta na chumvi na mengineyo, utaona wanafundishwa mtindo wa maisha na mtindo wa kuongea, na kuvaa kama nabii mkuu wao, na jinsi ya kumwogopa na kumtukuza baba yao, nabii mkuu..

Na watasomea hata miaka 5 na wakitoka hapo wanapewa na vyeti, tayari wakufunzi!!!..

Ndugu! Huo ni uongo wa shetani…

Wana wa manabii katika Agano la kale, hawakufundishwa wala hawakuwa wanajifunza mitindo ya kuongea ya manabii waliowatangulia…wala walikuwa hawajifunzi jinsi ya kuona maono! (kwasababu tayari walikuwa na hiyo karama, ndio maana wakaitwa manabii)..Walichokuwa wanajifunza ni Nabii zilizotangulia zinazohusu wakati waliopo wao, na za mataifa mengine, kuanzia zilizoandikwa katika Torati ya Nabii Musa, mpaka wakati waliopo wao, ili kusudi wasije wakapotoka na maono waliyokuwa wanayapokea.

Na sisi leo hii wote ni wana wa Manabii.. ambao manabii wetu si baba zetu wa kiroho!!! Wala si maaskofu wetu, bali ni MITUME WA KWENYE BIBLIA, na MANABII WA KWENYE BIBLIA!!!...Tunatembea katika Nabii walizozitoa hao, wakina Musa, Isaya, Yeremia, Habakuki, na mitume wakina Petro, Yohana, Paulo n.k.. (Na nabii zao hazijawahi kukinzana),Kwasababu walikuwa na Roho mmoja.

Kwamfano Nabii Isaya alitoa unabii ufuatao..

Isaya 13:6 “Pigeni kelele za hofu; maana siku ya Bwana i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu”.

Nabii Yoeli naye alitoa unabii kama huo huo katika Yoeli 3:14, na manabii wengine wote walitabiri hayo hayo…

Kwahiyo ili sisi tuhesabike kuwa “Wana wa manabii” ni lazima maono yetu tunayoyaona katika ndoto, au kwa wazi, ni lazima yapatane na huo unabii wa Isaya, na Yoeli na wengineo katika biblia!… usipopatana na huo unabii wa Isaya basi hilo Ono au huo Unabii ni wa UONGO!!! Ni kutoka Kuzimu!!!...

Tukiota au tukiona maono ambayo yanatuonyesha au kutuambia kuwa “Tufurahi, tupige kelele za shangwe, kwasababu siku ya Bwana bado sana”..basi hilo ni Ono kutoka kuzimu!!!..

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba wana wa manabii, ni manabii ambao walikuwa wamejikita katika kusoma Nabii za manabii wa Mungu waliowatangulia, ili wasifanye makosa katika kutoa nabii zao.

Na sisi ni lazima tuwe wanafunzi wa biblia, turejee biblia katika kuhakiki kila kitu, na hatupaswi kuamini tu kila jambo ambalo tunalipokea katika ndoto au maono.

Bwana Yesu na atusaidie sana.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

Nini maana ya “Torati na manabii”?

Nini maana ya “Roho za manabii huwatii manabii?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI
Wingu la Mashahidi
JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.



Loading





/

Jina kuu la Bwana na Mwokozi wa Ulimwengu, Simba wa kabila la Yuda, na Mkuu wa wafalme wa dunia, Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, neno la Mungu wetu, lililo mwanga wa njia yetu, na taa iongozayo miguu yetu.

Upo wakati wakati ambao tutahitaji Bwana atuguse mara ya pili, lakini ni vizuri kujua kanuni ya kupokea Uponyaji pindi tunapomsihi Bwana atuguse tena…

Hebu tusome kisa kimoja katika biblia na kisha tutafakari na tujifunze, kanuni ya kupokea uponyaji mkamilifu.

Tusome Marko 8:22-26, (Zingatia maneno yaliyoanishwa kwa herufi kubwa).

Marko 8:22 “Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.

23 Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, AKAMTEMEA MATE YA MACHO, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu?

24 AKATAZAMA JUU, AKASEMA, NAONA WATU KAMA MITI, INAKWENDA.

25 Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, NAYE AKATAZAMA SANA; akawa mzima, akaona vyote waziwazi.

26 Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie”.

Katika kisa hichi hebu tujiulize swali lifuatalo, kisha tuendelee mbele..

Je inawezekana mtu atazame juu halafu aone watu?, tena watu wenyewe wanatembea? Na tena wanatembea kwa kasi kama miti?… Nilitegemea hata angesema anaona “ndege wanaruka, wanakimbia kama miti”!! Lakini yeye anasema anaona watu!!……Bila shaka ulishawahi kusafiri na basi linalokwenda kasi, na njiani ukaona namna miti inavyoonekana kama inarudi nyuma kwa kasi sana…Ndivyo alivyoona huyu mtu alipotazama juu..aliona watu!..

Kwa kawaida, huu sio uponyaji!!.. Huyu mtu hakuwa amepata uponyaji wowote, bali alikuwa katika hatua za mwanzo za kupokea uponyaji..ni kama tu TV iliyowashwa ambayo bado haijakamata mawimbi!!..inakuwa inaonyesha tu chenga chenga…

Lakini tunaona tabia ya kipekee ya huyu kipofu baada ya kuguswa na Bwana mara ya pili.

Utaona huyu kipofu mara ya kwanza alipoguswa, alitazama juu hakutumia muda mrefu kutazama, badala yake, kwa haraka haraka akakimbilia kumjibu Bwana kwa kusema “anaona watu kama miti”….. lakini baada ya kuguswa na Bwana mara ya pili, ni kama alijifunza kitu kuwa hana budi kutokuwa na haraka ya mambo…utaona alitulia na KUTAZAMA SANA!! (pengine alitumia dakika kadhaa kutazama juu), akawa bado anaona ile ile miti, lakini hakuacha kutazama…..

Na alipozidi KUTAZAMA SANA, pengine akaanza kuona  ile miti inafutika kidogo kidogo, akaanza kuona anga linakuwa jeupe na kidogo kidogo akaanza kuona mawingu, na pengine akaanza kuona ndege wanaruka, na alipotazama mbele akamwona Bwana Yesu, ndipo akasema sasa ninaona!!! Haleluya.

Na sisi hatuna budi KUTAZAMA SANA!!..Tusiishie kutazama kidogo tu! tusiishie kuzungumza, wala kunung’unika, wala kukosoa, wala kutoa hitimisho, pale tunapoona uponyaji haujakamilika….bali turuhusu uponyaji wa Bwana ufanye kazi!… Tuwe na Subira huku tukiliamini Neno lake.

Kutazama sana, ni kudumu katika kumwamini Mungu, hata kama unaona lile tatizo bado halijatatuka… wewe endelea kumwamini Bwana na kusubiri, bila kutoa uso wako juu mpaka muujiza wako utakapokamilika..

Pengine ulimwomba Bwana kuhusu hali unayopitia ya kiroho au kimwili,  lakini uliishia kuona chenga chenga katika huo ugonjwa, au hilo tatizo..lakini sasa umeijua kanuni..Msii Bwana akuguse tena kwa mara nyingine, lakini safari hii USIRUHUSU IMANI YAKO IPUNGUE, WALA USIUKIRI UGONJWA.…Utaona muujiza wa ajabu, ukitendeka!!.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

Mwerezi ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?

Wana wa Asafu
Wingu la Mashahidi
Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?



Loading





/

Kabla ya kuwafahamu wana wa Asafu, ni vizuri kumfahamu Asafu mwenyewe alikuwa ni nani.

Asafu alikuwa ni mmoja wa walawi ambao, mfalme Daudi alimuweka  kama kiongozi wa mbele wa sifa, atakayesimama mbele ya sanduku la Mungu daima kumsifu Mungu. (Soma 1Nyakati 6:31-32, 39).

1 NYAKATI: MLANGO 16

1 Wakaliingiza sanduku la Mungu, na kuliweka katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake; wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.

2 Na Daudi alipokwisha kuitoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Bwana.

3 Kisha akawagawia kila mtu wa Israeli, waume kwa wake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu.

4 Akawaagiza baadhi ya Walawi kwamba watumike mbele ya sanduku la Bwana, wamfanyie ukumbusho, na shukrani, na sifa, Bwana, Mungu wa Israeli;

5 Asafu mkuu wao, na wa pili wake Zekaria, na Yeieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Matithiya, na Eliabu, na Benaya, na Obed-edomu, na Yeieli, wenye vinanda na vinubi; naye Asafu mwenye kupiga matoazi;

Kulingana na maandiko, biblia inasema huyu Asafu hakuwa tu mwimbaji, bali Mwonaji pia,

2Nyakati 29:30 “Tena Hezekia mfalme na wakuu wakawaamuru Walawi, wamwimbie Bwana sifa kwa maneno ya Daudi, na ya Asafu mwonaji. Wakaimba sifa kwa furaha, wakainama vichwa, wakaabudu”.

Baadaye, uzao wake uliendeleza  nyayo zake, na wote wakawa waimbaji katika hekalu la Mungu lililokuja kujengwa baadaye, na hata baada ya ule uhamisho wa Babeli, waliporudi bado waliweza kuwekwa katika kazi hiyo hiyo ya Sifa..

Soma, Ezra 2:41 “Waimbaji; wana wa Asafu, mia moja ishirini na wanane”.,

Pia Nehemia 7:44

Halikadhalika kuna baadhi ya Zaburi zilijulikana kama Zaburi za Asafu,Ambazo ni Zaburi 50 na ya 73-83. (Baadhi ya tafsiri zinaonyesha hivyo). Hiyo ni kuonyesha kuwa Mungu alimtumia yeye na uzao wake kwa njia ya uimbaji, kutoa nabii ambazo zinatusaidia hadi sasa.

Lakini kwasasa wana wa Asafu ni akina nani? Na tunapata funzo gani?

Wana wa Asafu ni watu wote wanaotumikia madhabahuni pa Bwana katika huduma ya kumsifu na kumwimbia Mungu. Watu hawa wanatenda kazi kubwa inayompendeza Mungu na kwa kupitia wao, Mungu huwa anapitisha, jumbe zake nyingi, na nabii nyingi zinazookoa na kuponya watu kama ilivyokuwa kwa wana  wa Asafu, hii ikiwa na maana, kwamba wakitumika vema katika kazi yao, basi ni utumishi mkubwa sana, hata Zaidi ya huduma nyingine zote.

Lakini, watu hawa walijua kanuni ya kumwimbia Mungu, walimwimbia Mungu katika “uzuri wa utakatifu”, sawasawa 1Nyakati 16:29. Tofauti na sasa, waimbaji wengi, wamekuwa wasanii, wanageuza uimbaji wa injili kuwa Sanaa na sio wito na huduma ya Kristo Yesu.

Wanasahau kuwa huduma yao ndio ya kwanza kabisa inayomkaribia Mungu Zaidi ya nyingine zote,..Huduma ya Maserafi na Makerubi malaika watakatifu wasimamao mbele ya Mungu daima

Lakini kinyuma chake, Mwimbaji wa injili, utamkuta anakata mauno, anavaa vimini, anapamba uso kama Yezebeli, anaimba kwa staili za wasanii wa kidunia.. Twategemea vipi Mungu atasema au atawaponya, au atawafungua na watu wake kupitia uimbaji huo?, Haiwezekani..Inasikitisha kuona, kanisa la sasa, kundi kubwa la watu walioharibikiwa linatoka kwa wanakwaya na waimbaji.

Kumbuka Sababu  iliyowafanya wana wa Israeli,wapelekwe utumwani haikuwa tu kuabudu maashera hapana, ilikuwa pia ni hiyo ya unafki katika kumwimbia.

Amosi 6:5 “ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi;”

Bwana anatuonya vikali, na sisi pia atatuadhibu vikali kama tutakuwa na tabia kama za wao,  anataka anapoimbiwa aimbiwe katika “uzuri wa utakatifu” (1Nyakati 16:29)..Maana yake ni kwamba wewe mwongoza sifa, wewe mwimbaji, wewe mpiga kinanda,wewe mpiga gitaa, uwe kielelezo kuanzia mavazi yako, usemi, hadi tabia, mbele za watu. Utakatifu ndio uwe leseni yako, ya kumwimbia Mungu.

Kama utashindwa utakatifu, ni heri uache tu, ukafanye kazi nyingine, kwasababu utakuwa unajizombea laana badala ya baraka.

Mahali Mungu anasifiwa na kuabudiwa ni kuwa makini sana.. wengine walipoteza Maisha walipojaribu kuvuruga utaratibu pindi Mungu anapokuwa anasifiwa (Soma 2Samweli 6:1-11 ), Vivyo hivyo na wewe mwimbishaji kanisani, usipokuwa siriazi na huduma yako, uwezekano wa kukutwa na hayo upo mkubwa sana.

Bwana anataka sote tuwe wana wa Asafu, ili atutumie kumtukuza yeye, Pamoja na kuzungumza na watu wake, ili aziponye roho za watu..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAOMBI YA YABESI.

NI KITU GANI TUNAJIFUNZA KWA RISPA, BINTI AYA?

SOMO no.02 (BINTI WA YEFTHA).

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri.

Rudi nyumbani

Print this post

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

kuota mafuriko
Wingu la Mashahidi
KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.
Loading
/

Naomba kufahamu Je! Kuota mafuriko ni kiashiria cha nini?

Mafuriko kazi yake si nyingine Zaidi ya kugharikisha, tofauti na mvua ambayo kazi yake ni kustawisha na kuleta mazao.. Hivyo ikiwa unaota ndoto ya namna hii mara kwa mara, au imekujia mara moja lakini kwa uzito sana, ambao sio wa kawaida basi ujue bila shaka kuwa kuna mafuriko makubwa (rohoni) yapo mbele yako, wengine utakuta wanaota mto umefurika na unataka kuwachukua, na kwa chini maji yake yanakwenda kwa kasi sana, au wengine wanaota wapo baharini na mawimbi makubwa yanakipiga chombo chao kidogo, kisha kinaanza kuyumba yumba na kuanza kuzama, wangine wanaogelewa lakini maji yanawazidia wanashindwa kuendelea mbele..n.k. Hivyo Ukikutana na ndoto yoyote inayohusiana na maji mengi(mafuriko) ujumbe wake ni mmoja, kwamba HATARI IPO MBELE YAKO..Na mafuriko hayo hayaletwi na mwingine zaidi ya shetani.

Sasa ndoto hii inalenga makundi yote mawili.

Kundi la Kwanza:Ni la watu ambao hawajamjua bado Kristo. 

Watu ambao wapo mbali na wokovu, ambao Yesu Kristo hajawabadilisha Maisha yao. Ikiwa wewe ni mmojawapo na umeota ndoto ya namna hiyo, basi ujue kuwa ni Mungu anakuonyesha, ni jinsi gani, mwisho wako utakavyokuwa,..Nataka nikuambie Sikuzote ukiwa nje ya Yesu Kristo hakuna wimbi ambalo halitakuchukua, liwe kubwa au dogo..kwasababu nyumba yako hujaijengwa juu ya mwamba ulio imara..

Sikia Yesu anachokisema…

Mathayo 7:24  “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25  mvua ikanyesha, MAFURIKO YAKAJA, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.

26  Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27  mvua ikanyesha, MAFURIKO YAKAJA, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa”.

Hivyo inategemea na maisha yako yalivyo, kama wewe ni mlevi basi ujue lipo furiko la mauti ibilisi amekuandalia kukuletea katika huo huo ulevi wako.., kama wewe ni mzinzi basi jiandae na furiko lihusianalo na uzinzi wako ambalo litakuchukua na kukupeleka moja kwa moja mpaka kuzimu..Kama wewe ni mlaji rushwa, ni mwizi, ni tapeli, ni muuaji, ni mshirikina, ni mwabudu sanamu, basi jiandae na furiko la mauti mbele yako..ambalo halitakuachia kichwa wala mkia..Utakwenda moja kwa moja, na ghafla utajikuta kuzimu..kwasababu hiyo ndio nia ya shetani sikuzote..Soma Ufunuo 12:14-17

Kundi la Pili: Watu ambao wameokoka.

Ikiwa wewe upo ndani ya Kristo(Umeokoka).. na unaota ndoto zihusianazo  na mafuriko, basi ujue ni aidha Mungu anakuonyesha hatari iliyopo mbele yako, hila ulizopangiwa na ibilisi hivyo Bwana anataka akuepushe nazo..

Hivyo hapo unapaswa uongeze viwango vyako vya maombi, usiwe mvivu omba kwa bidii, na kudumu katika utakatifu..Kiasi kwamba hata wimbi lolote(mafuriko) la ibilisi likikuta katika mazingira yoyote yale basi huwezi kupepesuka kwasababu umejengwa juu ya mwamba imara Yesu Kristo..

Au namna nyingine ni Mungu anakutahadharisha, utazame vizuri hali yako ya kiroho sasa…Pengine umerudi nyuma na hiyo itakuwa kwako rahisi kuchukuliwa na mawimbi ya mafuriko hivyo unapaswa uimarishe wokovu wako usimame imara..

ZABURI 124

“1 Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Israeli na aseme sasa, 

2 Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Wanadamu walipotushambulia. 

3 Papo hapo wangalitumeza hai, Hasira yao ilipowaka juu yetu 

4 Papo hapo maji yangalitugharikisha, Mto ungalipita juu ya roho zetu; 

5 Papo hapo yangalipita juu ya nafsi zetu Maji yafurikayo. 

6 Na ahimidiwe Bwana; Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao. 

7 Nafsi yetu imeokoka kama ndege Katika mtego wa wawindaji, Mtego umevunjika, nasi tumeokoka. 

8 Msaada wetu u katika jina la Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi”.

Amen.

Je! Ungependa kuokoka leo?

Ni vizuri ukafanya maamuzi hayo haraka..Usijiangalie labda wewe ni muislamu, au ni mkristo..ikiwa Kristo yupo mbali na wewe, haijalishi ulizaliwa katika dini au la, maisha yako sikuzote yatakuwa hatarini..Leo hii sikuambii umpe YESU Maisha yako, ili kusudi kwamba hatari hizo zisikukute mbeleni..Hapana pamoja na hayo ndani ya Kristo zipo faida nyingi utazipata..Kwanza kabisa atakupa uzima wa milele, Na Pili anakupenda na anakuhitaji wewe mwana wake uliyepotea.. aliyekuumba ukae katika uwepo wake..Umfurahie yeye na yeye akufurahie wewe.

Hivyo Ikiwa upo tayari leo hii Yesu aingie ndani yako..Na umemaanisha kweli kutaka kubadilika na akuokoe Maisha yako na dhambi zako zote basi..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

   Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

KUOTA UPO UCHI.

BONDE LA KUKATA MANENO.

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

UVUMILIVU WA MUNGU ULIPOKUWA UKINGOJA.

TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

SAA YA KIAMA.

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
SAA YA KIAMA.



Loading





/

Cha kushangaza ni kwamba wakristo tu peke yetu ndio hatujui saa tunayoishi na muda gani mchache tuliobakiwa nao, na hata kama tunajua basi wengi bado hatujachukulia kwa uzito jambo hili ukilinganisha na jinsi wanasayansi na shetani wanavyolichukulia kwa upande wao..Wanasayansi leo hii wameunda saa yao maalumu ijulikanyo kama “Doomsday clock” (saa ya kiama), ambayo hiyo inawakaumbusha ni wakati gani wanaoishi sasa, wameifananisha na saa  yetu hii ya kawaida, kwamba mshale ukifika tu saa 6 kamili usiku basi usiku wa manane umeanza, vilevile na siku mpya imeanza, Hivyo hiyo saa yao sasa ipo katika muundo huo huo kwamba zimebaki dakika chache sana kabla ya kuingia usiku wa manane wao(yaani kiama), wanakadiria kuwa  miaka yote ya nyuma saa hiyo ilikuwa haijafikia usiku wa manane lakini  kuanzia  mwaka 1947 ilifikia dakika 7 kabla ya kuingia usiku wa manane, na hiyo ni kwa jinsi walivyokuwa wanaona hali ya dunia inavyokwenda kwa matetesi ya vita vya mabomu ya Atomiki, kwamba muda wowote vita vinaweza kuanza na vikianza tu basi itachukua muda mfupi sana dunia kuwa sio sehemu tana ya kuishi mwanadamu.

Na kila siku mshale wao unapanda, mwaka 2015 walikadiria ni dakika 3 tu zimebaki , mwaka 2017 walikadiria dakika 2.5, mwaka jana walikadiria dakika 2 kabla ya kufikia saa 6 ya usiku wao…Yaani tafsiri yake ni kuwa hatari ya kukifikia kiama cha dunia ni kikubwa kuliko inavyodhaniwa katika miaka iliyopita…

Kama ulikuwa hujui sikuzote Mungu kabla hajaleta uharibifu wa hii dunia ni sharti kwanza wanadamu wajiharibu wenyewe, Ndivyo ilivyokuwa hata katika kipindi cha Nuhu, watu walijiharibu wenyewe kupindukia kukawa hakuna tena sababu ya maisha na ndipo Mungu akamaliza kila kitu (Mwanzo 6:12), ndugu  usione ukadhani kuwa duniani kuna amani, usidanganyike na siasa za dunia, ni jambo la kawaida kuficha ukweli ili watu wasiwe na wasiwasi lakini  nyuma yake ipo hofu kubwa ambayo wao wenyewe wanaitambua, pamoja na wanasayansi wao, kwa huu ugunduzi wa mabomu ya Atomiki ambayo hata leo kwenye vyombo vya habari unaona mataifa mengi yanagombana kila siku kuhusu hayo, kwasababu wanajua vita vikishaanza basi ndio mwisho wa kila kitu,..

muda mfupi chini nitakuonyesha video fupi, ya jaribio la kwanza la bomu la Atomiki lilidondoshwa huko Urusi tarehe 30 Octoba 1961, ukubwa wake ukiachilia mbali yale ya Nagasaki na Heroshima yaliyomaliza vita ya pili ya dunia kwa kuuwa  zaidi ya watu laki 2 kule Japan. Hili ni mara 1000 zaidi ya yale kwa uharibifu wake, tazama video fupi chini uone lilivyodondoshwa.

Lakini kabla hayo hayajatokea Unyakuo utakuwa umeshapita, katika ule mfufulizo wa maono 7 aliyoonyeshwa mtumishi wa Mungu maarufu William Branham  na kuambiwa hayo yatatokea kabla ya kuja kwa pili kwa Kristo, kama wengi tunafahamu na tunavyosoma katika historia, matano kati ya yale yalitimia kama yalivyo mawili bado, William Branham alionyeshwa kabla ya kutokea vita ya pili ya dunia jinsi hitler atakavyonyanyuka na kuiongoza dunia yote katika vita na jinsi  kifo chake kitakavyoishia na kuwa cha kiajabu ajabu, habari hiyo aliihubiri na ikajulikana na watu wote kabla hata ya kutokea kwa vita ya pili ya dunia, hilo lilikuwa ni ono la pili kati ya yale saba, sasa ono la saba ambalo lilikuwa ndio la  mwisho alionyeshwa kuangamizwa kwa taifa la Marekani, anasema alisikia mlipuko mkubwa usio wa kawaida nyuma yake na alipogeuka hakuona kitu chochote zaidi ya vipande vya mabaki na moshi tu,…Na hicho si kingine zaidi ya bomu la nyuklia.

Sasa hiyo alioneshwa kwa taifa lake, jambo hilo litakuja kuwa ulimwenguni kote, lakini mpaka hayo yote yatokee unyakuo utakuwa umeshapita, Mpaka sasa unaweza kuona ni saa gani hii tunaishi, Kama wanasayansi watu wa kidunia hawaishi kama vile wanayo wiki moja mbeleni, iweje mimi na wewe leo tuishi kama vile tuna maelfu ya miaka mbeleni,..Bwana anakuja, dalili zote zinaonesha, sijui tanataka tuoneshwe dalili zipi tena ndio tuamini na sisi kuwa tunaishi ukingoni mwa wakati..laiti kama na sisi tungekuwa na saa yetu basi saa yetu ingesoma tupo  visekunde vichache kabla ya kwenda katika unyakuo kwa Baba na kuanza kwa utawala mpya wa miaka 1000 wa Bwana wetu YESU KRISTO..

Tazama video fupi chini ya bomu lijulikanalo kama TSAR BOMBA, jinsi lilivyoachiwa ili ufahamu yatakayowakuta wale wote watakaokosa unyakuo.

Bwana Yesu akubariki sana Mtu wa Mungu, Tafadhali share na wengine


Mada Nyinginezo:

KATI YA UNYAKUO WA KANISA, DHIKI KUU, VITA VYA HAR-MAGEDONI, UTAWALA WA MIAKA 1000, VITA YA GOGU NA MAGOGU, HUKUMU YA KITI CHA ENZI CHEUPE. JE, NI KIPI KINAANZA NA KINGINE KUFUATA?

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

KITABU CHA UZIMA NI KIPI?

KUZIMU NI MAHALI PA NAMNA GANI ,JE! HUKO WANAISHI WATU WAKIFA NA KWENDA KUPATA MATESO AU NI VINGINEVYO?


Rudi Nyumbani:

Print this post