Jina la mwokozi wetu Yesu Kristo litukuzwe milele na milele. Nakualika Tena wakati huu tujifunze maneno ya uzima wa Roho zetu.
Wengi wetu tunavutiwa na maisha ya Yesu alipoanza huduma, tunafurahishwa na jinsi alivyokuwa anafanya miujiza mikubwa, alivyokuwa anahubiri kwenye miji na vijiji, alivyokuwa anaponya wagonjwa,kutoa Pepo na kufufua wafu n.k.
Lakini ni Wachache sana wanaweza kuyatafakari maisha ya Yesu kabla ya huduma. Na hayo ndio Yana umuhimu sana kwetu kuliko Yale aliyoyadhihirisha baadaye.
Maandiko yanasema Yesu alimpendeza Mungu kabla hata hajaanza huduma yoyote ya kuhubiri, kutoa Pepo, na kuokoa watu…alishampendeza Mungu kabla ya hayo yote, tunalithibitisha hilo katika kitabu Cha Mathayo 3 siku Ile anabatizwa na Yohana,
Mathayo 3:16-17
[16]Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake;
[17]na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.
Umeona alishampendeza Mungu kabla hata ya utumishi wowote, kuanza..tofauti na Leo tunavyodhani kwamba ili tumpendeze Mungu, ni sharti tuwe wahubiri wakubwa, au tuwe na upako, au tuwe wachungaji..hiyo sio kanuni ya Mungu.
Hivyo ni lazima tujue Mungu alipendezwa na Yesu kwa kipi? Ni kitu gani alikuwa anafanya mpaka kimfanye akubaliwe na Mungu namna Ile?
JIBU lipo katika Maisha aliyokuwa anaishi Kwa ile miaka 30 kabla ya huduma. Na hapa ndipo tunapaswa tupaangalie sana. Na tujifunze ili na sisi tufanane naye.
Watu wengi wanaona kama maisha yake ya awali yalifichwa sana, zaidi ya Yale aliyoyatenda katika huduma. Ni kweli ukitazama Kwa jicho la nje sehemu kubwa ya injili imeandika juu ya huduma ya Yesu, yaani ile miaka mitatu na nusu ya mwisho ya maisha yake. Lakini ukweli ni kwamba maisha ya Yesu kabla ya huduma ndio yameandikwa kwa wingi zaidi kuliko Yale aliyoyafanya katika huduma.
Hivyo Kwa neema za Bwana tutaona juu ya maisha yake yalikuwaje, tangu utotoni mpaka anakaribia kuanza huduma.
Sehemu ya kwanza tutaona Mahali ambapo maandiko yameeleza moja Kwa moja maisha yake yalivyokuwa. Na sehemu ya pili tutaona maandiko ambayo sio ya moja Kwa moja, lakini yalimwelezea Yesu maisha yake.
Tukianza na maandiko yanayoeleza moja Kwa moja juu ya maisha yake. Kama yafuatavyo;
Luka 2:52
[52]Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
Maisha yake yote alikuwa ni mtu mwenye bidii sana kuhakikisha hafanyi jambo lolote ambalo ni kinyume na mapenzi ya Mungu. Alikuwa yupo makini sana na hilo, lakini zaidi sana alihakikisha katika jamii hawi na harufu mbaya. Alizingatia kuwa na adabu na heshima Kwa Kila mtu aliyekutana naye.
Si ajabu watu walipomuona walimsifia sana, na kusema yule kijana anaheshima, yule kijana ni mtaratibu, natamani watoto wangu wangekuwa kama yule, hatumuoni kwenye kampani za wahuni, hatumuoni akiruka ruka na mabinti barabarani, hatumuoni akitembea Kwa majigambo barabarani, muda wote anatabasamu, hakasiriki haraka, anahekima kama za mtu mzima wakati bado ni kijana..
Yesu alipata sifa isiyo ya kawaida katika jamii, alipoishi duniani, hakuna mtu alimchukia Kwa Tabia zake, alijitoa kwelikweli kuishi kikamilifu katika jamii yake.
Na sisi pia hichi ndio kitu Mungu anataka kukiona katika maisha yetu tunapookoka kabla hata ya kufikiria kuwa wahubiri ,je mtaani kwako unaonekanaje, shuleni kwako Tabia zako zikoje? Mwonekano wako unawavutiaje watu, ofisini kwako kauli zako na wanyakazi wenzako Zina mvuto gani mpaka watu wakuone wewe ni mtu Bora kuliko wengine wote?
Luka 2:51
[51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
Aliwatii wazazi wake, hakukuwa na kiburi ndani yake, Neno utiifu kwa Yesu lilikuwa ni kama pumzi kwenye mapafu. Alipoagizwa alifanya, alipotumwa alikwenda, maisha yake yalikuwa ni ya namna hiyo, ili kutunza hadhi yake aliyokuwa nayo ya kuwapendeza watu wote..
Na sisi je tunaweza tukawa watiifu Kwa wazazi wetu wa kimwili na wa kiroho? Tuwatii viongozi wetu wa kiroho hata kama tutakuwa tunafahamu jambo Fulani zaidi ya wao, maadamu Bwana katuweka chini Yao.Hatuna budi kufanana na Yesu. Bwana atusaidie juu ya hilo.
Hii ni sifa nyingine inayomwelezea Yesu Tabia yake.
Luka 2:41-49
[41]Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka, wakati wa sikukuu ya Pasaka.
[42]Na alipopata umri wake miaka kumi na miwili, walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu;
[43]na walipokwisha kuzitimiza siku, wakati wa kurudi kwao, yule mtoto Yesu alibaki nyuma huko Yerusalemu, na wazee wake walikuwa hawana habari.
[44]Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao;
[45]na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta.
[46]Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
[47]Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.
[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
[49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?
Akiwa kijana mdogo wa miaka 12, hakujali atakula nini, atalala wapi, ataoga wapi..alinogewa na ibada na mafundisho hekaluni akaona hata ule muda wa sikukuu hautoshi yeye kukata kiu yake Kwa Mungu, akaendelea kubaki palepale siku tatu, akiwa amefunga, yeye ni kujifunza tu, na kuyatafakari maneno ya Baba yake..
Wazazi wake hawakujua kuwa angekuwa na kiu Kali namna ile, lakini baada ya pale walimzoea, ikawa ndiyo desturi ya maisha yake yote.
Yesu alikuwa ni mtu asiye mtoro wa ibada, alikuwa anatumia majira yake mengi, kwenda kwenye masinagogi na kutafakari Neno la Mungu pamoja na viongozi wake wa kidini. Hakuwa mtu wa kujitenga Tenga, kama watu wanavyodhani.
Lakini pia alikuwa ni jemedari wa maombi kweli kweli na Dua.
Alikuwa anaomba sana Kwa bidii, Kwa kulia na machozi sana, na kwa kujimimina sana. Maandiko yanasema hivyo;
Waebrania 5:7
[7]Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;
Na sisi je tunaweza tukaiga Tabia hii ya Bwana. Je! Furaha yetu ni kuwepo uweponi MWA Bwana muda mwingi au kuwepo katika anasa za Dunia? Au katika biashara zetu? Ni lazima Bwana apewe kipaumbele Cha kwanza.
Pamoja na kuwa alikuwa ni mtiwa mafuta wa Bwana ameandaliwa Kwa kusudi moja tu la kuwaokoa watu. Lakini kipindi anasubiri wakati wa Bwana, hakukaa hivi hivi tu, Mungu aliruhusu afanye kazi.
Marko 6:3
[3]Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake.
Yesu hakuwa kama Yohana mbatizaji, Kukaa majangwani mbali na watu muda wote, lakini alikuwa ni mtu ambaye yupo katikati ya jamii, anayejulikana, anafahamika, alifanya kazi pamoja na baba yake ya useremala.
Kwasasa tunaweza kusema alikuwa kariakoo akiuza vifaa vya majumbani na baba yake.
Lakini katika hayo yote aliishi maisha makamilifu ya kujichunga na kuwa na kiasi.
Hii ni kutuonyesha kuwa unapookoka, uwapo popote pale iwe ni kazini, au kwenye biashara Yako, bado unaweza kumpendeza tu Mungu. Hivyo tusiruhusu kazi ziwe kisingizio cha sisi kutoishi maisha makamilifu. Yesu alikuwa ni mtu wa kujichanganya, lakini hakuruhusu dhambi iwe juu yake. Alipouza kabati hakukwepa kulipa Kodi, hakumuuzia mtu meza Kwa bei isiyoendana na thamani yake. Hivyo ikampelekea Mungu ampende sana
Hayo ni maandiko ya moja Kwa moja yanayoeleza maisha ya Yesu yalivyokuwa.
Lakini maandiko mengine tunayapata wapi?
JIBU ni kuwa tunayapata katika kinywa Cha Yesu mwenyewe. Kwa kawaida mtu hawezi kusema maneno ambayo yeye hayaishi. Vinginevyo atakuwa ni mnafki, na Yesu yupo mbali sana na unafki, aliukemea sana, hata alipouona ndani ya mafarisayo na waandishi,walipowafundisha watu mambo ambayo wao hawayaishi.(Mathayo 23:1-5)
Hivyo ukitaka kufahamu Kwa kina maisha ya Yesu yalikuwaje sikikiza maagizo yote aliyokuwa anayatoa katika vitabu vyote vya injili.
Kwamfano. Mathayo soma sura yote ya 5-7 utaona maneno kadha wa kadha aliyokuwa anawafundisha makutano.
Anasema wapendeni adui zenu na kuwaombea(Mathayo 5:43-44): Yesu alikuwa anawaombea watu wote waliokuwa wanamchukia Kwa kumwonea wivu. Badala ya kuwatakia mapigo anawatakia maisha marefi, kuwaombea toba wageuzwe.
Anasema mtu akupigaye shavu la kuume mgeuzie la kushoto(Mathayo 5:38-40). Kuonyesha kuwa hakuwa mtu wa Shari, sikuzote alipotukanwa, au alipoaibishwa hakurudisha majibu, Bali alikubali kuaibishwa zaidi, ili aipushe malumbano zaidi.
Anasema amtazamaye mwanamke Kwa kumtamani amekwisha kuzini naye(Mathayo 5:28). Hakuwa na uvumilivu na macho yake, hakuwahi kuruhusu tamaa itawale maisha yake. Alijitenga na vichocheo vyote vya uzinzi, na mazungumzo yote yasiyofaa.
Alikuwa ni mtu wa kusamehe mara Saba sabini, hakuwa anawahukumu watu, au kuwalaumu(Mathayo 7:1-4)
Alikuwa si mtu wa kuruhusu hasira, aliona ukiwa hivyo adhabu Yako inakupasa ziwa la moto (Mathayo 5:21).
Bado alijishuhudia kuwa yeye ni mpole na mnyenyekevu (Mathayo 11:29), aliishi Kwa kujishusha, bila kumdharau yoyote, watu wote walikuwa na nafasi sawa kwake..
Na maandiko mengine mengi, aliyotuelekeza. Hivyo itoshe kusema maisha ya Yesu yaliyomfanya Mungu ampende kabla hata ya huduma ndiyo haya tunayoyasoma katika vitabu vya injili…
Hivyo ndugu Mimi na wewe yatupasa,. Tufikie hapo, acha kumuomba Mungu upako. Utakuja wenyewe tu endapo utampendeza Mungu kwanza kama Bwana Yesu, ukiwa unauhitaji. Penda mema chukia maasi..ndivyo Yesu alivyokuwa hapa duniani, hakuivumilia dhambi kwa namna yoyote, na matokeo yake Bwana akamtia nguvu kuliko mwanadamu yoyote aliyewahi kutokea hapa duniani.
Waebrania 1:9
[9]Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.
Bwana atusaidie sasa tuishi kama Kristo, ili baadaye tutende kama Kristo.
Bwana akubariki.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Mada Nyinginezo:
Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?
Kibiriti ni kitu gani? kama kinavyozungumziwa kwenye maandiko?
Nini maana ya Ukuta uliopakwa chokaa (Matendo23:3)?
FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.
Zaburi 144:1 “Na ahimidiwe Bwana, mwamba wangu, Anifundishaye mikono yangu vita, Vidole vyangu kupigana”
Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno yake ya uzima. Leo tutaona namna ya kuomba maombi ya vita. Tukisema maombi ya vita tunamaanisha maombi ya kushindana na nguvu zote za Yule mwovu katika ulimwengu wa Roho, maombi ya kulegeza vifungo na nira, na minyororo, na kuangusha ngome pamoja na kuta za Yule mwovu zinazokinzana na sisi katika ulimwengu wa Roho, kupitia majeshi yake ya mapepo wabaya.
Ndugu ni lazima ufahamu, Kuna aina nyingi za maombi, kuna maombi ya shukrani, maombi ya mahitaji, maombi ya upatanisho n.k.. Yote haya yana wakati wake wa kuyatumia. Lakini pia yapo maombi ya Vita, ambayo ni lazima sana na ni muhimu kwa Mkristo kuyatumia.
Hivyo siku ya leo tutaona ni jinsi gani tunaweza kutumia maombi haya ili tuziangushe ngome za adui yetu ibilisi kiwepesi.
Baadhi ya watakatifu hawajui namna ya kuomba, wanafikiri pale unaposema shindwa shetani! Shindwa shetani! Kwa Saa tatu, au usiku kucha ndivyo wanavyomwangusha ibilisi. Uhalisia ni kwamba, hatumshindi ibilisi kwa maneno yetu kuwa mengi, Bali tunamshinda ibilisi kwa Neno la Mungu kukaa ndani yetu kwa wingi. Ambalo hilo litakusaidia kujua SILAHA unazopaswa uzitumie kumpiga nazo shetani. Bila kufahamu Silaha zako za kiroho, ni ngumu sana kumshinda shetani kimaombi. Kwasababu maombi yako yatakuwa ni ya juu juu, yasiyokuwa na nguvu za kiroho.
Bwana asipokufundisha kupigana vita, haijalishi maombi yako yatakuwa na maneno mengi kiasi gani, huwezi angusha ngome za adui. Hivyo penda sana kulisoma Neno la Mungu kwa kulitafakari kwasababu huko ndiko utakapojifunza kupigana vita vyako.
Kibiblia zipo silaha nyingi ambazo Mungu alizitumia kuwapigania watu wake, na Leo tutaziorodhesha chache, na tutaona jinsi tunavyoweza pia kuzitumia rohoni. Kwasababu kumbuka Neno la Mungu halijaandikwa kutupa stori Fulani tu, tuifurahie halafu basi hapana, bali kila tendo, kila Neno linatafsiri kubwa sana rohoni.
Hivyo hizi ni baadhi ya silaha ambazo Mungu alizitumia kuwasaidia watu wake kupigana vita;
Mungu aliangusha mvua ya mawe kubwa sana, kwa wale watu wa Yerusalemu na wenzake walioungana kupigana na Yoshua kipindi kile wanaenda kuimiliki nchi yao, Utaona baadhi yao waliuliwa na Israeli, lakini wengi wa hao Mungu alimalizia kutoa hazina yake ya mvua kubwa ya mawe ikawaangamiza wengi sana kuliko hata wale waliouliwa na Yoshua.
Yoshua 10:11 “Kisha ikawa, hapo walipokuwa wakimbia mbele ya Israeli, hapo walipokuwa katika kutelemkia Bethhoroni, ndipo Bwana alipowatupia mawe makubwa kutoka mbinguni juu yao hata kufikilia Azeka, nao wakafa; hao waliokufa kwa kuuawa na hayo mawe ya barafu walikuwa ni wengi kuliko hao waliouawa na wana wa Israeli kwa upanga”
Jinsi ya kuomba: Bwana peleka, mawe yako ya barafu, katika madhabahu Zote za ibilisi, peleka mvua yako ya barafu katika vilinge vya kichawi, vinavyosimama kinyume na imani yangu. Haribu, bomoa, kila mbinu iliyoundwa dhidi yangu mimi (Taja maeneo yote ya maisha yako). Kama ulivyomshindia Yoshua nishindanie na mimi. [Hivyo Endelea kuita mvua hiyo na katika ulimwengu wa Roho, kwa jinsi unavyoiita kwa imani ndivyo inavyokuwa].
Yesu alipoingia hekaluni, alikutana na watu walioigeuza nyumba ya Mungu kuwa pango la wanyang’anyi. Ndipo akaunda kikoto kile, akapindua meza zote na kuwachapa wote waliofanya biashara pale, akawafukuza hekaluni kwa mamlaka yote, hekalu likawa safi kwa muda mfupi.
Yohana 2:15 “ Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng’ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao; 16 akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara”
Namna ya kuomba: Bwana naunda kikoto chako, napindua madhahabu zote za kipepo zilizoundwa moyoni mwangu na Yule adui, ninatawanyisha, ninasambaratisha, kila uovu, kila sanamu iliyopachikwa na Ibilisi (taja maeneo yote yanayohitaji maombi), kinyume na mapenzi ya Mungu. Ninavuruga kazi zote za ibilisi, kikoto cha Bwana kisafishe mwili wangu, kisafishe ibada yangu, kisafishe maisha yangu ya rohoni, kisafishe nyumba yangu, Naondosha uovu wa kila namna hata katika kazi yangu. [Sasa kwa jinsi unavyoomba kwa bidii na kurejea tukio hilo, ndivyo katika Roho Bwana anamnyuka shetani kwa namna ile ile. Ng’ang’ania hapo omba kwa imani kwa muda mrefu, kwasababu ndivyo ibilisi anavyodondoshwa].
Bwana hutumia vitisho pia, kuwaondoa maadui, utakumbuka wakati Fulani wana wa Israeli, walizungukwa na maadui kwa muda mrefu. Hadi nchi ikaingiwa na njaa, watu wakaanza kulana ili waishi. Lakini jinsi Mungu alivyowaondoa maadui zao inashangaza. Kwasababu alifanya tu, kuwasikilizisha sauti za vita. Hivyo wale maadui waliposikia waliogopa sana wakawa wanakimbia kwa hofu kubwa sana huku wanaacha nyara zao nyuma. Baadaye Wayahudi kwenda wanashangaa hawawaoni maadui zao, wakijuliza ni nini kimetokea, mpaka waache na nyara, wakagundua kuwa ni Bwana ndiye aliyewatetea. Ndipo wakazichukua nyara kiwepesi na vita vikawa vimeisha kwa namna ile.
2Wafalme 7:6 “Kwa maana Bwana alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari, na kishindo cha farasi, kama kishindo cha jeshi kubwa; wakaambiana, Tazama, mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti, na wafalme wa Wamisri, waje wapigane nasi. 7 Kwa hiyo wakaondoka, wakakimbia kungali giza bado, wakaziacha hema zao, na farasi zao, na punda zao, na kimo chao vile vile kama kilivyokuwa, wakakimbia wapate kujiponya nafsi zao”
Namna ya kuomba: Bwana peleka sauti zako za vita, katika ngome ya ibilisi, wafukuze waende mbali nami, hazina zote na vipawa vyote walivyoniibia katika roho na mwili ninavirejeza kwa Sauti yako ya vita. Watawanyike kwa njia saba. Vyote walivyoviiba navirejesha, fungua mipaka yangu, safisha hema yangu, adui atoweke kwa sauti za vita vya Bwana. [ Omba kwa kutaja maeneo yote ambayo unataka Bwana akutetee katika hayo].
Wale malaika wa Bwana walioshuka Sodoma ili kuipeleleza, walikutana na wenyewe wa mji ule, ambao walitaka kulala nao. Hivyo malaika wale wakiwa nyumbani kwa Lutu. Maandiko yanaema waliwapiga upofu watu wale wasiweze kuiona nyumba mpaka asubuhi. Utakumbuka pia Paulo alipofika katika kile kisiwa kilichoitwa. Alishindana sana na Yule mchawi mpaka akamwomba Mungu ampige kwa upofu akawa kipofu kwa muda.
Mwanzo 19:10”Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu kwao nyumbani, wakaufunga mlango. 11 Kisha wakawapiga hao watu walioko mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa, hata wakachoka kwa kuutafuta mlango”.
Namna ya kuomba: Bwana piga upofu majeshi ya mapepo yote mabaya yaliyokuja kufanya vita kinyume changu mimi, wasione roho yangu, uufiche uhai wangu ndani yako, shusha kiwi na giza mbele yao. Wapapase, wasione huduma yangu, (taja mambo yako yote ambayo unatamani ibilisi asiyaone), waangamie na kuishia shimoni, watafute lakini wasione. [Hivyo Kwa jinsi unavyosimamia vifungu hivyo ndivyo unavyoshinda vita rohoni kiwepesi kwasababu mambo hayo yanatendeka kwelikweli].
Jiwe la Mungu ni Yesu. Yeye mwenyewe alijifananisha na jiwe hilo lililo zito sana na gumu. Akasema. Likimwangukia mtu linamsaga tikitiki, na yoyote atakayeliangukia atavunjika vunjika Kuonyesha ni jinsi gani lilivyo bora, ndio lile lililopiga sanamu ya Nebukadreza, na kuisaga kama unga, na kupotea kabisa(Danieli 2:34).
Mathayo 21:44 “Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika; naye ye yote ambaye litamwangukia, litamsaga tikitiki”.
Namna ya Kuomba: Yesu simama mwenyewe unitetee, kama jiwe lililo hai lenye nguvu na imara. Piga kila aina ya kuta nzito za ibilisi zinazozuia upenyo wangu. Nazibomoa kwa jiwe hili, ninalirusha katika kila Nyanja, impige ibilisi katika kipaji cha uso wake, aanguke kama Goliathi mbele ya Daudi. Wewe uliye jiwe piga kila ngome, ya mwovu lisage na kuharibu na kusagasaga, kazi zote za mwovu mbele yangu ziwe kama makapi mbele ya Upepo.[Lielekeze jiwe hili, liangushe kwelikweli kwa imani ndivyo itakavyokuwa katika ulimwengu wa roho]
Natumai mpaka hapo umeshapata mwangaza wa namna ya kulitumia Neno kuomba maombi haya ya vita, Kwasababu ya muda, hatuwezi toa maelezo ya silaha zote zilizo katika biblia, Hivyo hizi ni silaha nyingine ambazo zitumie, zikusaidie.
6) UPEPO WA KUSULISULI NA RADI: Andiko la kusimamia (Zaburi 77:18). Omba Bwana avuruge, na kuichosha mikakati yote ya adui dhidi yako mfano wa kisulisuli kizungushacho makapi.
7) GHARIKA YA BWANA: Andiko la kusimamia (Mwanzo 6:17). Kama Bwana alivyoangamiza waovu wakati ule wa Nuhu kwa gharika Omba Bwana akafungue madirisha yake ya mbinguni, agharikishe majeshi ya kipepo yanayokufuatilia yakuangamize, yaangamie kama majeshi ya Farao katika bahari ya Shamu.
8) UPANGA WA BWANA: Andiko la kusimamia (Ufunuo 19:15). Omba ule upanga wa Bwana ukatao kuwili, ukate, na kuua mambo yote maovu ya adui yanayosimama mbele yako
9) KUTAWANYWA USEMI: Andiko la kusimamia (Mwanzo 11:7-9). Kama alivyouvuruga usemi wa wajenzi wa Babeli wasielewane, vivyo hivyo akaruge hila za ibilisi na mapepo yake zisipatane juu yako.
10) MOTO WA BWANA: Andiko la kusimamia (2Wafalme 1:10). Moto ukaunguze mapando yote, ya ibilisi, aliyoyapanda moyoni mwako,
11) NZIGE, PARARE, MADUMADU, TUNUTU: Andiko la kusimamia (Yoeli 2:25). Bwana akatume jeshi lake la waharibuo, wakatafune kazi zote za mwovu, wakalete hasara, warudishe nyuma, na kudhoofisha ufalme wote wa giza.
12) MAJIPU YA BWANA: Andiko la kusimamia (Kutoka 9:9). Bwana alete hali mbaya ya mateso, kwa wakuu wote wa giza wafanyao vita kinyume na wewe.
13) TETEMEKO: Andiko la kusimamia (1Samweli 14:15) . Bwana alete utisho na mashaka, na tetemeko kwa wakuu wa giza na mapepo yasimamo kinyume cha kazi ya Mungu.
14) UKAME (kiu na njaa): Andiko la kusimamia (Amosi 8:11). Bwana alete ukame wa kiroho, kwa majoka yote yanayosimama kutaka kumeza watu wa Mungu, yafe na kuteketea kwa kukosa mawindo ya watu.
15) RUNGU LA BWANA: Andiko la kusimamia (Yeremia 51:20). Lipige na kuleta majeraha katika ufalme wa giza, liziraishe mapepo yote na vikaragosi vyake vyote vifanyavyo vita na wewe.
Zipo na silaha nyingine nyingi katika maandiko Hatuwezi kuziorodhesha zote, Hivyo kwa jinsi Neno la Mungu linavyokaa ndani yako, ndivyo utakavyoweza kuzivumbua na kuzitumia. Na zote hizo ni sharti tuziombe katika jina la Yesu na uweza wa damu yake.Maombi ya namna hii yana nguvu sana, na yatakufanya udumu kwa muda mrefu katika kuomba. Na kufungua vifungo vingi sana katika ulimwengu wa Roho.
Kumbuka pia, vita hivi hatuvielekezi kwa wanadamu, bali kwa Shetani na majeshi yake ya mapepo na kazi zake zote. Kwasababu maandiko yanasema vita vyetu sio juu ya damu na nyama, maana yake ni kwamba sio juu ya wanadamu wenzetu. Bali ni juu ya falme za giza, zikawaachilie mateka, waje kwa Bwana, na sio tuwaue wao pamoja na mateka wao.
Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 6.13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama”
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Mada Nyinginezo:
FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.
NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?
JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.
Nini maana ya “Andiko huua, bali Roho huhuisha (2Wakorintho 3:6)
Karibu tujifunze biblia.
Matendo 3:22 “ Kwa maana Musa kweli alisema ya kwamba, Bwana Mungu wenu atawainulieni nabii, katika ndugu zenu, kama mimi; msikieni yeye katika mambo yote atakayonena nanyi.
23 Na itakuwa ya kwamba kila mtu asiyemsikiliza nabii huyo ataangamizwa na kutengwa na watu wake”
Unabii huo unamhusu Bwana Yesu Kristo, lakini swali la Msingi hapa, je! Ni wakati gani ambao “watu wataangamizwa na kutengwa” kwa kutomsikiliza huyu Masihi…Kwasababu ni wengi leo hawamsikilizi wala kumtii lakini hawaangamizwi wala kutengwa na watu wao.
Hapo kuna mambo mawili ambayo yatatimia kwa pamoja.. 1) KUANGAMIZWA, na 2) KUTENGWA.
Haya ni mambo mawili ambayo yatatimia kwa wakati mmoja kwa wote ambao hawatamsikiliza Masihi.
Sasa swali, ni hili unabii huo utatimia lini wa watu kuangamizwa na kutengwa?
Tusome,
2Wathesalonike 1:7 “na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; WAKATI WA KUFUNULIWA KWAKE BWANA YESU kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake
8 katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu;
9 watakaoadhibiwa kwa MAANGAMIZI ya milele, KUTENGWA na uso wa Bwana na UTUKUFU WA NGUVU ZAKE;”
Umeona hapo?. Kumbe wote wasioitii injili, leo siku ya mwisho (ya kufunuliwa Bwana Yesu) wataangamizwa!, na sio tu kuangamizwa, bali pia “watatengwa na uso wa Mungu” na “kutengwa na utukufu wa nguvu zake”…Maana yake wataanza kwa kutengwa kutoka kwa ndugu zao (wakati wa kutenganishwa kondoo na mbuzi Mathayo 25:31-35) na pia watatengwa na vitu vyote Mungu alivyoviumba ikiwemo dunia na kila kitu…sawasawa na Mithali 2:21-22.
Mithali 2:21 “Maana wanyofu watakaa katika nchi, Na wakamilifu watadumu ndani yake.
22 Bali waovu watatengwa na nchi, Nao wafanyao hila watang’olewa”
Ni jambo baya sana kutengwa na uso wa Mungu na kuangamizwa!..
Wengi leo wanamkataa Yesu na kuikataa Injili wakidhani ipo njia nyingine ya kufika mbinguni.. Bwana Yesu yeye mwenyewe alisema kwa kinywa chake kuwa..
Yohana 14:6 “..Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.
Hakuna njia nyingine ya kumfikisha mtu mbinguni isipokuwa njia ya Msalaba!.. Usidanganyike kwa vyovyote vile.
Mwisho wa dunia unakuja, Mpokee Yesu leo, Itii injili yake inayosema… usizini, usiibe, usivae mavazi ya nusu tupu, usivae mavazi yapasayo jinsia nyingine, usijichore mwili, usitukane n.k
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Mada Nyinginezo:
Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?
Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)
Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
SWALI: Naomba kufahamu ni hekima gani tunaipata nyuma ya vifungu hivi, vinavyosema “Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri”.
JIBU: Mithali 30:29 “Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri. 30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hajiepushi na aliye yote; 31 Jimbi aendaye tambo; na beberu; Na mfalme ambaye haasiki”.
Swali la kujiuliza ni kwanini wameonekana wana mwendo mzuri na wa kupendeza, jibu ni kwasababu ya tabia yao ya ujasiri na kuamini kuwa wao ni wamiliki.
kwamfano Simba ni mfalme wa pori, kila kitu kilicho mbele yake anakiona ni chakula, hivyo hana uoga na lolote. Anamiliki wanyama wote , hata wale wanaoonekana ni wakubwa na wenye nguvu kuliko yeye. Wote wanamkimbia.
Anamtaja pia jimbi/jogoo, ambaye na yeye ni mfalme wa shamba, usemi wa “kutanua mbawa” umeanzia kwake. Yeye anaamini anaweza kumiliki mitetea yote na kundi lote la kuku. Watafiti wanasema kule kuwika kwa jogoo, sio bila sababu tu. Hapana, bali ni anatuma ujumbe kwa majogoo wengine wasimsogelee kwenye miliki yake na kutafiti kama yupo ambaye anamkaribia, ajiandae kwa mapambano. Tofauti na ndege wengine walio madume, hawana tabia za kujimilikisha kama Jogoo, au kupigana ili kumiliki shamba.
Anamtaja pia Beberu,(Mfalme wa zizi) katika kundi, beberu utamtambua tu kwa tabia zake, hujiaminisha sana, muda wote hatulii, analimiliki kundi lote kana kwamba yeye ndio mchungaji-msaidizi (Zekaria 10:3). Katika Historia unabii wa Aleksanda mkuu aliyetawala Ugiriki ya kale, ambaye aliteka ngome nyingi sana, kila alipopatamani alikwenda na akashinda alifananishwa na beberu katika maandiko Kutokana na Tabia zake hizo (Danieli 8:5). Hata sasa mataifa yanayotaka kumiliki mataifa mengine kwasababu ya nguvu zao za kijeshi, au kiuchumi au kisiasi, hujulikana kama mataifa ya kibeberu.
hiyo ni kufuatana na Tabia ya beberu ya kupenda kumiliki zizi.
Lakini wa mwisho anamtaja pia, Mfalme asiyeasika. Ambaye ni mtawala wa Nchi. Kama tunavyojua wafalme ndio viongozi wa taifa, humiliki vyote, na yoyote atakayekatiza mbele yake kujaribu kuuangusha ufalme wake, humuua. Mfalme ni zaidi ya raisi, Wafalme wengi waliteka ngome kwa vita, sio kwa kuchaguliwa, Ujasiri na misimamo yao huwamilikisha.
Ni hekima gani tunaipata?
Hivyo mwandishi wa mithali anajaribu kuonyesha , ujasiri na ushujaa ambao na sisi tunaweza kuupata endapo tutakuwa ndani ya Kristo. Bwana atatufanya tuwe na roho kama za wanyama hawa, mienendo yetu itakuwa bila WOGA sikuzote. Tutaishi kama watu wasio na mashaka kwa lolote. Hatutaogopa wanadamu, wala matatizo, wala wachawi, wala magonjwa, wala shida yoyote. Kwasababu tunajua uwezo wa kuyashinda hayo na kuyamiliki tunao mfano wa Simba na mfalme.
Bwana Yesu aliye mfalme wetu, anayemiliki sasa mbinguni na duniani, Simba wa Yuda, aliyashinda na sisi pia tutayashinda endapo tutakuwa ndani yake alisema hivyo.
Yohana 16:33 “…jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.
Je! Utapenda kumpa leo Yesu maisha yako? Ili aanze upya na wewe, akupe tumaini jipya la uzima wa milele? Na ujasiri wa kuishi hapa duniani bila woga?
Kama jibu ni ndio basi fuatiliza mwongozo huu, na Leo Leo utaupokea wokovu >> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Mada Nyinginezo:
NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?
Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?
Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?
Je ni kweli Isaka alifarijika kwa kifo cha mamaye? (Mwanzo 24:67)
Kupwelewa maana yake nini? (Matendo 27:26).
YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.
Jibu: Turejee,
Kumbukumbu 24:6 “Mtu awaye yote asitwae jiwe la kusagia, la juu wala la chini, kuwa rehani; kwani hivi ni kutwaa maisha ya mtu kuwa rehani”.
Jiwe la kusagia lilikuwa ni jiwe lililotumika katika kusagia nafaka enzi za zamani, na hata sasa katika baadhi ya jamii.. Lilikuwa ni jiwe kubwa ambapo nafaka kama ngano inawekwa juu yake, na kisha jiwe lingine dogo linawekwa juu yake na kusaga nafaka hiyo.
Lilikuwa pia ni jiwe ambalo linapatikana karibia katika kila nyumba.. ni kama vile leo, jiko ilivyo zana ya msingi karibia katika kila nyumba, hata yule maskini kabisa hawezi kukosa jiko, vile vile na hili jiwe lilikuwa ni zana ya msingi sana.
Sasa Mungu alikatakaza Jiwe hilo (liwe la juu au la chini) lisiwekwe rehani kwa vyovyote vile, Maana yake kama mtu kamkopesha maskini, hapaswi kukubali rehani iwe jiwe la kusagia, kwasababu endapo Yule maskini kashindwa kulipa mkopo ule, basi jiwe lile la kusagia litachukuliwa na kwenda kuuzwa ili deni lile lilipwe, na hivyo Yule maskini atabaki hana hilo jiwe, na hivyo atashindwa kusaga nafaka zake kwaajili ya chakula chake cha kila siku, hata nafaka zile chache ambazo atazipata katika shamba lake, atashindwa kuzisaga kama riziki, na hivyo anaweza kufa kwa njaa.
Lakini rehani ya vitu vingine kama vyombo, au mashaba iliruhusiwa, kwasababu mtu angeweza kuishi bila hivyo vitu, lakini si bila jiwe hilo la kusagia.
Jambo hilo linatufunza nini?
Tunajifunza kuwa na huruma kwa watu wa hali ya chini, Ni vizuri kutoa mkopo lakini si kila mkopo ni lazima tupate rehani, mikopo mingine tunaweza kuitoa tu bila kumweka mtu rehani, (hususani kwa wale watu ambao ni hali ya chini sana kiuchumi), hiyo itaonyesha upendo wetu na wema kwa watu na hata kuwafanya wavutiwe na imani yetu na kumfuata Mungu wetu.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika..
Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?
Swali: Je ni kweli Bwana Yesu mwenyewe na wanafunzi wake walikuwa hanawi mikono kabla ya kula?..kulingana na Mathayo 15:2, na Luka 11:37
Jibu: Turejee,
Mathayo 15:1 “Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema
2 Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula”
Tusome tena, Luka 11:37..
Luka 11:37 “Alipokuwa akinena, Farisayo mmoja alimwita aje kwake ale chakula; akaingia, akaketi chakulani.
38 Farisayo huyo alipomwona, alistaajabu kwa sababu hakunawa kabla ya chakula”.
Je ni kweli Bwana Yesu na wanafunzi wake walikuwa hawanawi mikono kabla ya kula kulingana na mistari hiyo?
Jibu ni la! Bwana Yesu na wanafunzi wake walikuwa wananawa mikono kabla ya kula, huo ni usafi wa kawaida tu ambao kila mtu anao.
Hauwezi kutoka kushika mavumbi halafu uanze kula hivyo hivyo, labda uwe hauna akili timamu. Na Bwana pamoja na wanafunzi wake walikuwa ni watu wenye akili timamu, kama Bwana aliweza kuwaosha wanafunzi wake miguu kunawa mikono ni nini kwake? (Yohana 13:9-10).
Sasa swali kama Bwana na wanafunzi walikuwa wananawa mikono, kwanini Mafarisayo na Masadukayo waseme alikuwa hanawi?
Jibu ni kwamba Mafarisayo walikuwa wanafuata desturi za wazee, ambao kulingana na sheria ilikuwa kabla ya kula ni lazima mtu aoshe mikono mpaka kwenye kiwiko!.. Jambo ambalo halikufanywa na wanafunzi wa Yesu wala Bwana Yesu mwenyewe… kwani Bwana na wanafunzi wake walikuwa wananawa tu kawaida, bila kufikisha maji kwenye viwiko.
Marko 7:2 “wakaona wengine katika wanafunzi wake wakila vyakula kwa mikono najisi, yaani, isiyonawiwa.
3 Kwa maana Mafarisayo na Wayahudi wote wasiponawa mikono mpaka kiwiko, hawali, wakishika mapokeo ya wazee wao”
Kama tu leo sisi tunavyonawa kabla ya kula, tukitaka kula huwa tunaosha tu viganja, lakini hatuoshi mkono mzima mpaka kwenye kiwiko, hivyo kulingana na desturi za wayahudi, mtu aliyeosha kiganja tu, bila kufika mpaka kwenye kiwiko, mtu huyo anahesabika kama bado hajanawa kabisa.
Hivyo kulingana na desturi hizo za kiyahudi, hata sisi tunaonawa sasa katika viganja tu, mbele zao tunahesabika kuwa watu wanaokula bila kunawa!. Kwahiyo na Bwana pamoja na wanafunzi wake hawakuwa wananawa hadi kwenye viwiko, ndio maana wakashutumiwa vile, lakini walikuwa wananawa kama tu sisi tunavyonawa sasa.
Na ni kwasababu gani wanafunzi, hawakufuata desturi hizo za wazee za kunawa mpaka kwenye kiwiko?
Bwana Yesu alishatoa sababu kuwa kinachomwingia mtu hakiwezi kumtia unajisi bali kinachomtoka.
Mathayo 15:17 “Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?
18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.
19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano”
Hivyo na sisi tujihadhari sana na vitu tunavyovitoa katika vinywa vyetu kwasababu vinakuwa vinatoka mwilini, lakini zaidi sana tujitahidi kuwa wasafi kimwili, kwasababu hata Bwana Yesu alikuwa ananawa.
Bwana atubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Mada Nyinginezo:
Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?
Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).
Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?
SWALI: Naomba kufahamu kwanini mafuta yaliendelea kutumika wakati Yesu tayari alikuwa ameshakuja duniani?
Marko 6:12 “ Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu. 13 Wakatoa pepo wengi, wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza”
JIBU: Ndio, Bwana Yesu alikuwa na kanuni nyingi za kuwaponya watu, kuna wakati alitamka tu na mtu akapokea uponyaje wake, utakumbuka habari ya Yule mtu aliyepooza alimwambia jitwike kitanda chako uende nyumbani(Marko 2:1-9), vilevile kuna wakati alimgusa kwanza mgonjwa, kisha akaponywa, utamkumbuka Yule mkoma, aliyemfuata na kumpigia magoti kumwomba amponye, maandiko yanasema akamgusa na kusema nataka takasika,(Marko 1:40-42). Vilevile Kuna wakati alitoa tu agizo la kutekelezwa na katikati ya agizo hilo, mtu anapokea uponyaji wake, ile habari ya wale wakoma 10, inatuthibitishia hilo,(Luka 11:17-19) na kuna wakati alitumia visaidizi, kama udongo, mate, kama ishara ya nje, ya mtu Yule kupokea uponyaji wake. Ukisoma habari ya Yule mtu ambaye alikuwa kipofu tangu kuzaliwa utali hakiki hilo nalo (Yohana 9:6).
Na hapa ndivyo ilivyokuwa aliwapa maagizo wanafunzi wake, Pale alipowaita na kuwatuma kwenda kuhubiri injili Ukisoma kuanzia mstari wa 7, Utaona aliwapa maagizo hayo ya kutoa pepo, na bila shaka na ya kuwapaka mafuta wote waliokuwa wagonjwa kwa jina lake.
Lakini hiyo haikuwa staili, kwamba kila mahali watakapokwenda wawe na chupa za mafuta, au maji, au udongo au chochote.
Hata sasa, hatupaswi kudhani Bwana hawezi kutuagiza tutumie kitu chochote cha asili kama ishara ya nje ya kuachilia uponyaji wake. La! Tusifikiri hivyo, Lakini hilo halipaswi lifanyike mara zote, au kama staili, kama inavyofanywa sasa, watu hawahubiri tena Neno la Mungu, kinachopigiwa kampeni ni mafuta na maji ya upako. Lakini mitume hawakufanya hivyo, ukisoma mstari wa 12, hapo anasema “Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu”. Umeona, Walijua jukumu lao kubwa ni kuwahubiria kwanza watu habari za dhambi zao. Na katika huduma hayo mengine yanafuata tena kwa uongozo wa Roho Mtakatifu.
Ni jambo linalosikitisha sasa, Jina la Yesu halitumiwi tena, shetani ameingilia eneo hili na kulivuruga, watu wakidhani hiyo ndio kanuni ya Mungu iliyobora ya watu kupokea uponyaji, wamemgeuza kama mganga wa kienyeji ambaye yeye kazi yake ni kutoa tu miti-shamba lakini hajali hali ya mtu ya kiroho.
Wengine wanakimbilia lile andiko la Yakobo ambalo linasema,
Yakobo 5:14 “Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
15 Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa”
Wanasahau kuwa kilichotangulia ni kuombewa kwanza..kuungamanishwa dhambi zake, kupatanishwa na Mungu, kisha ndio mafuta yafuate, kwa jina(agizo) la Bwana.
Tukikariri kwamba wakati wote tunapaswa tutumie chumvi kisa Elisha aliagizwa atupe chumvi kwenye chemchemi ya maji ili aondoe mapooza(2Wafalme 2:19-22), basi tukariri pia kitendo cha kulala juu ya maiti, kila tunapowaombea wafu ili wafufuke, kwasababu Elisha naye alifanya kitendo kama hicho(2Wafalme 4:32-34). Unaona, tutaonekana ni wachawi.
Ndugu, kuwa makini na staili za kisasa za uponyaji, ni makundi machache sana yanayoongozwa na Bwana kutumia vitu hivi vya asili katika kufanya huduma, na utaona havitumiki mara kwa mara au kila siku bali kwa mwongozo Fulani. Lakini ukiona mahali hapo ndio imekuwa staili, kimbia hapo Mungu hayupo hiyo ni ibada ya sanamu. Wana wa Israeli walimkosea Mungu hivyo hivyo, baada ya kuona Mungu amewaponya kwa kuitazama ile nyoka ya shaba, Musa aliyoagizwa aiunde kule jangwani, wao wakadhani Mungu sikuzote yupo katika sanamu ile, matokeo yake ikawa walipofika katika nchi ya ahadi wengine waliendelea kuiunda, wakiitazama ili kutatuliwa matatizo yao, ikawa ni chukizo kubwa sana kwao. Mpaka baadaye sana mfalme Yosia alipokuja kuivunja vunja, ndipo hasira ya Mungu ikaisha.(2Wafalme 18:1-5)
Hivyo usigeuze kitu chochote kuwa sanamu yako, kukitegemea hicho angali maisha yako yapo mbali na dhambi utakumbana na laana badala ya baraka. Tumepewa jina la YESU hilo ndio mwanzo na mwisho. Vinginevyo vyote tusubiri kwanza uongozo wa Roho Mtakatifu, kama haupo, tuache.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Mada Nyinginezo:
Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)
NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?
MAOMBI YA KUFUNGULIWA KIUCHUMI.
Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?
SWALI: Katika Mithali 30:24, tunaona wanatajwa wanyama wanne, wenye akili sana, lakini naomba kufahamu juu ya Yule wanne ambaye ni mjusi, Anaposema “Mjusi hushika kwa mikono yake; Lakini yumo majumbani mwa wafalme” Maana yake ni nini?
JIBU: Tusome,
Mithali 30:24 “Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo; Lakini vina akili nyingi sana. 25 Chungu ni watu wasio na nguvu; Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari. 26 Wibari ni watu dhaifu; Lakini hujifanyia nyumba katika miamba. 27 Nzige hawana mfalme; Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi. 28 Mjusi hushika kwa mikono yake; Lakini yumo majumbani mwa wafalme”
Mjusi ni kiumbe ambaye ameumbiwa wepesi wa kupanda na kupita karibia sehemu zote zenye upenyo hata ule mdogo sana, uwezo wa mikono yake unamfanya aweze kusimama katika pembe yoyote ile ya ukuta, iwe ni ukuta wa juu, au wa pembeni, au wa chini, kwake vyote ni sawasawa, tofauti na wanyama wengine, ambapo pengine hutegemea kucha zao, ambazo hizo zinawasidia kupanda baadhi ya maeneo tu kama miti.
Na ndio maana utawakuta katika kila nyumba, hawazuiliki, hadi katika majumba ya wafalme biblia inasema hivyo utawakuta, mahali ambapo pana ulinzi, pana uangalizi, lakini wao wanaingia huko bila shida yoyote na kufanya makazi.
Ni kutufundisha nini katika hekima yake?
Ni kwamba, na sisi tunapokuwa ndani ya Kristo tunapewa mikono kama ya mjusi katika roho. Uwezo wa hali ya juu kupanda kila kuta ngumu, Hatuzuiliki kwa kitu chochote, popote tutakapotaka kupafikia tutapafikia, hata katika malango mazito ya ibilisi tutayamiliki.
Mwanzo 22:17 “katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; NA UZAO WAKO UTAMILIKI MLANGO WA ADUI ZAO; 18 na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu”
Je! Unataka uupokee uwezo huo? Kanuni ni moja tu, nayo ni kumpa Kristo maisha yako, jikane nafsi yako, simama kikamilifu na Bwana, kisha utaona jinsi Mungu anavyokupigania kuangusha kuta na kumshinda ibilisi kiwepesi, ziwe za kimaisha au za kiroho. Kwako hakuna kikwazo kitakachokuwa kigumu kukishinda.
Bwana akubariki.
Je! Utapenda kufahamu hekima iliyo nyuma ya wale watatu waliosalia?
Fungua link hizi>>>
Wibara > Wibari ni nani?(Mithali 30:26)
Nzige >TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Mada Nyinginezo:
Nzige, Parare, madumadu na tunutu ni wadudu gani? (Yoeli 2:25)?
Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 5
Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8)
Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?
Jibu: Turejee..
Waefeso 5:25 “……kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
26 ili makusudi alitakase na KULISAFISHA KWA MAJI KATIKA NENO;
27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa”..
Siri ya kanisa kutakaswa kwa “Maji” inaanzia pale Msalabani, wakati Yule Askari anamchoma Bwana mkuki ubavuni, biblia inaonyesha kuwa palitoka “Maji na Damu”. Ikifunua kuwa Maji ni lazima yahusike katika hatua za utakaso wetu, ndipo damu ya Yesu iweze kututakasa kabisa. Utauliza tunazidi kulithibitisha vipi hilo? Tusome Matendo 2:37-38
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”
Umeona hapo?.. Anasema tubuni mkabatizwe, mpate ondoleo la dhambi.. kwahiyo kumbe ubatizo unahusika sana katika kusafika utu wa ndani.. maana yake utakaso wa Damu, unategemea ubatizo wa Maji, ili Roho Mtakatifu aweze kukaa ndani ya mtu.
Vitu hivi vitatu vinaenda pamoja (DAMU, MAJI na ROHO Mtakatifu). Huwezi kukichukua kimoja na kukiacha kingine!… Wala kusema kimoja kina umuhimu kuliko kingine… Vyote hivi vitatu vina umuhimu na maandiko yanasema vinapatana katika UMOJA!
1Yohana 5:9 “Kisha wako watatu washuhudiao duniani], ROHO, NA MAJI, NA DAMU; na watatu hawa hupatana kwa habari moja”.
Hiyo ndio sababu pia kwanini tunapaswa tubatizwe!.. Wengi leo wanaupuuzia ubatizo wa maji wanasema hauna umuhimu sana, ubatizo wa Roho Mtakatifu ndio wa muhimu.. Pasipo kujua kuwa Roho, na Maji na Damu vinapatana katika Umoja, ndio maana Bwana Yesu alimwambia Nikodemo kuwa kama hatazaliwa kwa MAJI (maana yake kwa ubatizo wa maji) na kwa ubatizo wa Roho Mtakatifu, hatauona ufalme wa mbinguni, na huko ndiko kuzaliwa mara ya pili.
Maana ya kuzaliwa mara ya pili ni kubatizwa katika maji na katika Roho Mtakatifu.
Yohana 3:4 “Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa MAJI NA KWA ROHO, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.
Na ubatizo ulio sahihi ni ule wa maji Tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Bwana Yesu (Matendo 2:38, Matendo 8:16, Matendo 10:48 na Matendo 19:5)
Bwana akubariki.
Ikiwa bado hujapata ubatizo sahihi, basi unaweza kuwasiliana nasi, tutakusaidia juu ya hilo, kwa Neema ya Bwana.
Shalom
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Mada Nyinginezo:
MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.
TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
SWALI: Naomba kufahamu maana ya huu mstari..Kwanini biblia imtaje Mungu kama mtu, angali maandiko yanasema yeye sio mtu.
Kutoka 15:3
[3]BWANA ni mtu wa vita, BWANA ndilo jina lake.
JIBU: Neno hilo halimaanishi kuwa Mungu ni mtu, Bali biblia hutumia mifano halisi ya kibinadamu kuwasilisha picha Fulani Rohoni..
Kwamfano ukisoma andiko lingine linalopatikana katika Mithali 30:26, utaona mnyama anayeitwa Wibari anatajwa kama mtu..
Mithali 30:26
[26]Wibari ni watu dhaifu; Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.
Tunafahamu kabisa wanyama hawa wibari(Pimbi) sio watu, isipokuwa kwa wingi wa akili zao, mwandishi anawafananisha na watu, Ni kwasababu gani? Ni Kwasababu ijapokuwa ni waoga, wadhaifu, wanawindwa na kila mnyama mkali..lakini hawajengi nyumba zao katika sehemu dhaifu kama kwenye viota, au kwenye mashimo, au vichaka, ambapo ni rahisi kuvamiwa au kuharibiwa na majanga, Bali wanaweka makazi Yao katika miamba mikubwa iliyojificha sana Mahali ambapo ni ngumu adui kuwashambulia.. wanafananishwa na watu waliojenga maisha yao juu ya MWAMBA, pekee yaani Yesu Kristo
Mathayo 7:24 “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba; 25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba”
Hivyo tukirudi katika andiko hilo, anaposema “BWANA ni mtu wa vita”. Anajaribu kumfananisha Bwana na shujaa wa kivita, jemedari mwenye uzoefu mkubwa sana katika vita vikali, mfano wa Sauli, au Daudi, ambao walikuwa wanasimama mstari wa mbele katika vita, ili sisi tupate picha jinsi gani Mungu wetu alivyo mkuu sana, pale anapoitwa Bwana wa Majeshi, tumwelewe uweza wake wa kutupigania na kutusaidia kuangusha ngome za ibilisi jinsi ulivyomkubwa haijalishi zimekita mizizi kiasi gani.
Zaburi 24:8 “Ni nani Mfalme wa utukufu? Bwana mwenye nguvu, hodari, Bwana hodari wa vita”
Hivyo mstari huo hakumaanisha kuwa yeye ni mtu.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP
Mada Nyinginezo:
Ufunuo 12 inaelezea vita vya wakati upi?
Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza
NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU
Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?
Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?
NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA, WAENDE HEKALUNI.