TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

Tuwaonapo nzige wa jangwani ni nini tunajifunza?


Shalom.. Karibu tuongeze jambo lingine kuhusu ufalme wa mbinguni..

Bwana Yesu alipotuambia utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake…Alimaanisha kweli ufalme huo ili kuupata inahitaji kuutafuta…Lakini jambo ambalo hatujui pia ni kuwa ufalme huo haujafichwa katika mambo magumu sana, kiasi kwamba itatuhitaji tuwe na shahada kubwa za elimu, au maarifa makubwa kuzijua, badala yake siri hizo zimefichwa katika mambo madogo sana, na hayo ndiyo yanayofanya ufalme huo usionekane kirahisi..Mambo mepesi sana ambayo huwezi kutazamia kama kweli hapo ndipo siri za Mungu zilipo.

Kwa mfano embu tafakari Bwana Yesu alivyosema..Watafakarini Kunguru (Luka 12:24),..hawapandi, wala hawavuni, wala hawana maghala lakini baba yenu wa mbinguni anawalisha hao wote, je ninyi si Zaidi kuliko hao wote?. Ikiwa wewe unaishi Dar es alaam au sehemu za pwani utakuwa umeshakutana na kunguru wengi sana, lakini kama Bwana Yesu asingelizunguza hili neno, ungekuwa unaona kama ni viumbe vyenye kero Fulani, vinaishi mjini tu kuuchafua mji, lakini kumbe siri moja ya ufalme wa mbinguni ipo hapo, kiasi kwamba mtoto wa Mungu akiitumia basi, atafanikiwa sana,

Kama hujui ni mmoja wa ndege wachache sana wanaoishi miaka mingi, kunguru anaishi mpaka miaka 80, anaishi mjini mahali wanaposema Maisha magumu(vyuma vimekaza), na kila siku anakula, anakunywa! Sasa ni rahisi kusema kunguru ndivyo walivyoumbwa staili hiyo ya maisha..Lakini Bwana Yesu anasema..Je! wale wanachokipi cha kuwapita nyie mpaka waishi Maisha ya kutokujisumbukia kama yale?..

Ndugu kama wewe umekosa Imani ya maneno kama hayo ya Kristo, nataka nikuambie wapo wenzako wanaishi kwa Neno hilo na Bwana anawahudumia kwa kila kitu Zaidi hata ya kunguru, mmojawapo ni mimi, hakuna siku inayopita bila kuwa na ushuhuda mpya maishani mwangu…mpaka nimeshazizolea naziona ni kawaida tu..Lakini zamani nalipoanza tu kuliamini hili Neno, nilijaribu kumweleza mchungaji mmoja kulitokea utata mkubwa.. Haijalishi Tutajaribu kuleta tafsiri nyingine tuzijuazo lakini Maneno ya Yesu ni imara, yatathibitika milele na milele..Hayo ndio mambo marahisi ambayo Mungu anajifunua ndani yake, lakini yanadharauliwa na wengi.

Leo hii tunasikia tena kuna jambo limezuka la wadudu wanaojulikana kama NZIGE WA JANGWANI, sana sana katika ukanda wa Afrika Mashariki. Tupaswa pia tujiulize maswali Je! Tupowatazama hawa wadudu tunaona tu maafa na majanga au tunaona pia kitu kingine ndani yake?..

Lakini biblia inawataja nzige kama moja ya kiumbe vinne vyenye AKILI nyingi sana..

Soma..

Mithali 30:24 “Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo; Lakini vina akili nyingi sana.

25 Chungu ni watu wasio na nguvu; Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.

26 Wibari ni watu dhaifu; Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.

27 NZIGE HAWANA MFALME; LAKINI HUENDA WOTE PAMOJA VIKOSI VIKOSI.

28 Mjusi hushika kwa mikono yake; Lakini yumo majumbani mwa wafalme”.

Kama hujawahi kufuatilia tabia ya nzige hawa, basi fahamu kuwa hawana tofuati sana na nzige hawa wa kawaida tunaowaona ambao kila mmoja anajitegemea kivyake, tofauti ipo tu pale ambapo wameshakuwa wengi huwa wote wanabadilika tabia, wanajikusanya pamoja..kisha wakishajikusanya wanaanza kuruka katika wingi wao, kama kimbunga, ukitazama kwa mbali unaweza ukaona kama ni vumbi tu linakuja jinsi walivyo wengi, unaambiwa katika kilometa moja ya mraba, wapo nzige Zaidi ya milioni 150, na katika kimbunga hicho wapo Zaidi ya nzige bilioni 100, na wote hawa wanaruka pamoja.

kwa siku wanaweza kusafiri zaidi ya kilimeta 150, sasa licha ya wao kuwa wengi hivyo unaambiwa katika kuruka kwao na kupishana kwao wakiwa bado hivyo mabilioni kwa mabilioni huko juu, hawagongani wakiwa angani, wala hawagusani, japokuwa wanaruka karibu karibu sana..Hawana kiongozi wa kuwaweza katika mstari, na kuwasimamia na kuwaambia wewe pita hapa, au wewe pita kule, lakini wanayo akili ya hali ya juu, ya kuwafanya waruke kwa ustaarabu, wakiwa na anza moja, ya kuelekea upande mmoja..

Na ndio hiyo inayowafanya wafanikiwe kufika mbali wote wakiwa pamoja, wahame kutoka taifa moja hadi lingine wakiwa na idadi hiyo hiyo ya majeshi..Na kusababisha maafa makubwa sana ya mazao isiyoelezeka..

Embu fikiria kikundi kimoja kinachojaza eneo la kilometa moja ya mraba, kwa siku moja kinauwezo wa kutafuna mazao, yanayoweza kuliwa na watu elfu thelathini na tano (35,000) ..Na wenyewe wakivamia basi wanamaliza mamilioni ya Hektari za mraba.. Na ndio maana wanakuwa tishio sana kwa mataifa..Hawa ndio mfano wa wale walitumwa kuitafuna nchi yote ya Misri.

Sasa, kwanini Biblia inatuambia wanaakili nyingi..Ni kwasababu Mungu anataka ni sisi tupate hekima ndani yake ili tufanikiwe katika kumshinda adui..

Si mpango wa Mungu tangu zamani tuwe na viongozi juu yetu sisi wa kutuongoza..Wana wa Israeli walimwomba Mungu awape mfalme juu yao..Mungu alikasirishwa sana na mawazo yao, kwasababu Mungu alitamani wamtumikie yeye wakiwa na nia moja kila mmoja bila kushurutishwa na mtu Fulani wa pembeni..(Soma 1Samweli 8:1-22)

Leo hii na sisi, tukitaka ulimwengu huu, tumshinde Shetani, hatuhitaji mpaka tuambiwe na watu Fulani majukumu ya kufanya..Bali sote kwa pamoja kila mmoja kwa nafasi yake, na kwa karama Mungu aliyopewa anyanyuke kwa nguvu zake aishambulie kambi ya Adui shetani kwa kuihubiri injili, tusisibirie mpaka Mchungaji wetu atuambie hivi au vile, tusisubiri mpaka viongozi watushurutishe tutoke tukaifanye kazi ya Mungu…Kwa jinsi shetani anavyoaharibu hakuna mtu asiyejua kuwa huu ni wakati wa mapambano..

Sisi ikiwa kila mmoja atasimama kwa nafasi yake, kama vile HAWA NZIGE WA JANGWANI.. Tukatoka tukiwa na lengo moja la kumuharibu ibilisi na kazi zake zote..Basi tujie kuwa kuzimu itabakia kuwa gofu..shetani atapata hasara isiyokuwa ya kawaida..Watu watamkimbilia Kristo kwa namna isiyoelezeka…Na tukitoka wote kama Jeshi kiongozi wetu akiwa ni Roho Mtakatifu na si mtu, kamwe hatutapishana kauli, kamwe hatutagongana katika njia zetu kama jinsi hawa nzige kwa wingi wao wasivyogongana wakiwa angani..

Lakini hiyo yote ni mpaka mimi na wewe, kutokuongejea mpaka tupangiwe majukumu ya kufanya na mtu Fulani, au mhubiri Fulani, au mpaka kanisa litupangie majukumu..

Naamini katika wakati huu wa kumalizia, tutalitafakari na hilo, katika kazi ya ujenzi wa ufalme wa mbinguni..Bwana azidi kutupa neema yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

UHURU WA ROHO.

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

SAA YA KUHARIBIWA IIJIAYO ULIMWENGU WOTE.

SIKU ILE NA SAA ILE.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments