Title 2023

Je! Habari iliyo katika 1Nyakati 21:25, na 2Samweli 24:24, ya Daudi kununua kiwanja  inajichanganya?

SWALI:  Ni ipi gharama sahihi ambayo Daudi aliilipia, kununulia shamba la Arauna, kwa ajili ya kumjengea Mungu hekalu. Je! Ni shekeli 600, au shekeli 50?. Je! Biblia inajichanganya.

JIBU:  Tusome,

2Samweli 24: 24 Lakini mfalme akamwambia Arauna, La, sivyo; lakini kweli nitavinunua kwako kwa thamani yake; wala sitamtolea Bwana, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa nisizozigharimia. Hivyo Daudi akakinunua hicho kiwanja cha kupuria na wale ng’ombe kwa shekeli hamsini za fedha.  25 Naye Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Basi Bwana aliiridhia nchi, na tauni ikazuiliwa katika Israeli.

1Nyakati 21:25 “Basi Daudi akampimia Arauna thamani ya mahali pale shekeli mia sita za dhahabu kwa uzani  26 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akamlingana Bwana; naye akamwitikia kutoka mbinguni kwa moto juu ya madhabahu hiyo ya sadaka ya kuteketezwa”

Vifungu hivyo havijichanganyi,  vyote vipo sahihi. Mwandishi wa kitabu cha Samweli anaeleza lile eneo ambalo lilikuwa ni la kupuria tu, pamoja na wale ng’ombe gharama zake jumla ndio shekeli hamsini, lakini sio eneo lote la kiwanja. Tukirudi kwenye 1Nyakati mwandishi anaeleza sasa eneo lote, anatumia neno “mahali pale”. Kwamba jumla yake yote ni shekeli mia sita. Gharama zote za mahali pale zilikuwa ni shekeli 600

Kwamfano wewe unaweza ukawa umelenga kupanunua mahali Fulani kwa ajili ya shughuli zako za kimaendeleo. Lakini ikakugharimu ununue sehemu yote ili uweze kupamiliki vizuri na pale. Hivyo kama eneo lile tu moja gharama yake ilikuwa milioni 1, Lakini kwasababu ya kulipia fidia kwa watu kando kando kuwahamisha, na kodi, na ukarabati n.k. unajikuta unaenda mpaka milioni 20.

Ndicho kilichomkuta Daudi.

Kwahitimisho ni kuwa vifungu hivyo vipo sahihi havijichanganyi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

NI KWANINI WATU WENGI WANASHINDWA KUMWELEWA MUNGU?

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?

Novena ni nini? Na je ipo kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

VUNJA AGANO LA MAUTI.

Mtu anaingiaje agano na mauti?

“Agano” kwa jina lingine ni “Mkataba”

Mtu anapoingia mkataba na mtu mwingine ni sawa na kaingia agano na mtu huyo.

Sasa mwanadamu pia anaweza kuingia Agano na Mauti, Ndivyo biblia inavyotufundisha kuwa mtu anaweza kuingia agano na Mauti na kuingia katika mapatano na kuzimu.

Isaya 28:18 “Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo”.

Na kama mtu ameingia Agano na Mauti ni lazima mauti itakuwa na nguvu juu yake,itamwandama popote anapokwenda na itampata..hivyo ni lazima hilo agano livunjwe ili mtu huyo abaki huru, na uzima utawale ndani yake,

Sasa kinachomwingiza mtu katika agano la Mauti ni nini?..je ni ndoto anazoziota?, Au ni wachawi?, Au wanadamu?..

Jibu: Si wanadamu, wala wachawi, wala ndoto mtu anazoota bali ni “dhambi ndani ya mtu”…Biblia inasema “Mshahara wa dhambi ni Mauti”.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Sasa hapo hasemi “matokeo ya dhambi ni mauti” bali “mshahara wa dhambi ni mauti”.

Maana yake mtu anayefanya dhambi ni sawa na mtu anayefanya kazi za kumpatia mshahara..Kwamba ni lazima atakuwa na mkataba wa kazi (yaani agano la kazi) ili apokee mshahara.

Halikadhalika na mtu anayefanya dhambi, anakuwa kwanza ameingia agano na hiyo dhambi na ndipo anapokea mshahara wake baada ya kuitendea kazi, na mshahara wake ndio “Mauti”.

Kwahiyo kumbe Agano la Mauti ni “dhambi”..Ikiwa na maana kuwa mtu akiondoa dhambi katika maisha basi atakuwa amelivunja hilo agano la Mauti lililo ndani yake!.

Kumbe mtu anayeabudu sanamu tayari yupo katika agano na mauti, kumbe mtu anayezini tayari kashaingia agano/mkataba na mauti, Kumbe mtu anayeiba tayari yupo katika agano na mauti?, Na kwamba siku yeyote atakumbana na Mauti ya mwili na roho, na hatimaye kutupwa katika ziwa la moto ambako huko kuna mauti ya pili. (Ufunuo 20:14 na 21:8)

Sasa hili agano la Mauti tunalivunjaje?…je ni kwa kuwekewa mikono na watumishi?, Au kwa kunywa maji na mafuta yajulikanayo kuwa ya upako?, Au kwenda kukemea hayo maagano?

Jibu la swali hili hatulipati pengine popote isipokuwa kwenye biblia.

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Umeona kanuni ya Kuondoa dhambi?…si kwa kupakwa mafuta, au kuwekewa mikono kichwani…bali ni kwa KUTUBU NA KUBATIZWA.

Unapotubu kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi basi unapokea msamaha na papo hapo na lile agano la Mauti linavunjika!..sawasawa na maandiko hayo ya Isaya 28:18,

Isaya 28:18 “Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo”.

Lakini kama hakuna toba halisi na ubatizo basi agano la mauti bado lipo palepale..halijavunjika! Haijalishi mtu huyo atawekewa mikono na watumishi wangapi, au ataombewa na watu wangapi, au anaabudu dhehebu kubwa kiasi gani..kama bado hataki kuacha dhambi, zinazotajwa katika Wagalatia 5:19…basi Mauti bado ipo pale pale.

Tubu leo na Agano la Mauti litabatilika juu yako, kile kifo ambacho ulikuwa umekiona kimekukaribia kitapelekwa mbali nawe.. Na hakikisha toba yako inaendana na matendo, kama umetubia wizi, au uzinzi, au uchawi au jambo lingine lolote hakikisha kuanzia siku hiyo hurudii tena hayo..(Unafanyika kiumbe kipya).

Bwana atusaidie.
Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

DHAMBI YA MAUTI

MSHAHARA WA DHAMBI

Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?

Rudi nyumbani

Print this post

Novena ni nini? Na je ipo kibiblia?

Jibu: Neno “Novena” limetokana na neno la kilatini “Novem”… lenye maana ya “Tisa”(9). Madhehebu baadhi ikiwemo Katoliki na Orthodox yamelitoa neno hili na kulitumia katika aina Fulani ya mfululizo wa sala kwa kipindi cha siku 9.

Sala hizo zinahusisha kuomba kwaajili ya  jambo fulani au kushukuru, na zinahusisha ibada za kuomba Rozari kwa wakatoliki (jambo ambalo si sahihi kibiblia). Na kwanini kusali Rozari sio agizo la biblia?, fungua hapa kwa maelezo Zaidi >>>JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?

Sasa msukumo wa kuomba Novena, (yaani siku 9) mfululizo umetokana na matukio maalumu yanayotokea baada ya siku 9, au miezi 9 kumalizika. Kwamfano utaona kabla ya Pentekoste kutimia, walikusanyika Mitume na watu wengine baadhi mahali pamoja kuomba, na wakaomba kwa muda wa siku 9, baada ya Bwana Yesu kupaa na siku ya 10 ikawa ni Pentekoste.

Hivyo ushawishi huu wa kupokea Roho Mtakatifu baada ya maombi ya siku 9, ukaaminika na madhehebu hayo kubwa ni lazima uendelee ili kupokea kitu kingine mfano wa hicho kutoka kwa Mungu, vile vile mwanamke anajifungua mtoto baada ya miezi 9, hili nalo likawafanya viongozi wa madhehebu haya kuamini kuna kitu katika 9, (novena).

Sasa swali ni je! Biblia imetuagiza kutumia mfumo wa Novena, katika maombi ili kupokea jambo maalumu kutoka kwa Mungu? Kwamba tuwe na maombi maalumu ya kurudia rudia kwa muda wa siku 9 ili tupokee jambo kutoka kwa Mungu?.

Jibu ni la!.

Biblia haijaagiza mahali popote tusali “Novena” kwamba tuwe na kipindi Fulani maalumu cha siku 9 mara kwa mara ili Mungu aachilie kitu juu yetu. Utaratibu huu umetengenezwa na wanadamu, kufuatia ushawishi wa siku ya Pentekoste. Hivyo kama umetengenezwa na wanadamu, hauwezi kuwa Sharti, au Agizo la lazima kwa wakristo, kwamba usipofanya hivyo ni kosa kibiblia!.

Agizo hili linaweza kuwa la binafsi, kama tu vile mfungo usivyokuwa sharti, ni jinsi mtu atakavyosukumwa na kuongozwa kufunga!.

Lakini mbali na hilo hata kama Novena ingekuwa ni agizo la biblia, bado inavyofanyika na madhehebu baadhi ikiwemo Katoliki, bado haifanyiki sawasawa na maandiko.. Kwasababu katika biblia tunaona kabla ya Pentekoste walikuwa wamekusanyika mahali pamoja wakisali, wakimwomba Mungu na Mariamu mama yake Yesu alikuwemo miongoni mwao, naye pia akimwomba Mungu, na hawakuwa na sanamu ya mtakatifu Fulani aliyetangulia kufa!, bali walikuwa wakimwomba Mungu aliye juu, (Matendo 1:12-14)

Lakini leo hii katika sala hizo za Novena ni kinyume chake!, wanaoombwa ni watakatifu waliokufa ikiwemo Maria mwenyewe, jambo ambalo ni kinyume kabisa na maandiko!, hivyo badala ziwe sala za Baraka, zinageuka na kuwa ibada za sanamu! (Bwana Yesu atusaidie sana!!).

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Novena haipo kibiblia,..kama mtu atajiwekea utaratibu wake binafsi wa kusali Novena, na sala hiyo ikawa ni kulingana na Neno la Mungu, isiyohusisha sanamu wala desturi za kipagani basi hafanyi dhambi!, huenda ikawa bora kwake.

Lakini inapogeuka na kuwa sharti, na tena ikahusisha ibada za sanamu basi inakuwa ni machukizo makubwa mbele za Bwana kulingana na maandiko.

Bwana atusaidie!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

Kuna tofauti gani kati ya SALA na DUA?

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

Rudi nyumbani

Print this post

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

Waefeso 6:18  kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote

Yuda 1:20  Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu

Watu wengi wanaamini kuomba katika Roho ni kuomba kwa “kunena kwa lugha tu”. Nje ya hapo sio kuomba kwa Roho. Lakini tukiwa na mtazamo huo basi tutakuwa na uelewa finyu kuhusu Roho Mtakatifu.

Ukweli ni kwamba hiyo ni namna mojawapo kati ya nyingi ambazo Roho wa Mungu anamjalia mtu kuomba.

Maana ya ‘kuomba katika Roho’ Ni kuomba ‘ndani ya Roho ya Mtakatifu/ ndani ya utaratibu/ uwepo wa Roho Mtakatifu’. Na hiyo ni zaidi ya kunena kwa lugha, Hii ikiwa na maana Mtu anaweza kuomba lakini asiwe katika uwepo huo. Na matokeo ya hivyo ni maombi kuwa makavu sana, yasiyo na nguvu.

Sasa mstari mama unaotufundisha juu ya uombaji wa Roho Mtakatifu ni huu;

Warumi 8:26  “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA”

Hapo anasema “kuugua kusikoweza kutamkwa” . Maana ya kuugua hapo ni kuweka uzito, au presha, au shauku  ya kuomba ndani ya mtu isiyokuwa ya kawaida. Tofauti na angejitahidi kwa nguvu zake yeye mwenyewe. Sasa mtu akifikia hatua hiyo, basi tayari kuanzia huo wakati anaomba katika Roho hata kama maneno yake ni ya kawaida anayoyatumia. Maombi hayo yana nguvu na yanasikika sana mbele za Mungu.

Kwamfano, ndio hapo utakuta mtu anaomba, lakini mara anasikia kububujika machozi ndani yake, mwingine anazidi kuona kiu ya kuendelea kuombea jambo lile lile kwa muda mrefu tofauti na sikuzote. Mfano wakati ule Bwana Yesu alipokuwa Gethsamane anaomba.

mwingine anajisikia wepesi usio wa kawaida, uchovu wote umeondoka ijapokuwa alikuwa amechoka sana, anaanza furahia maombi, anafurahia kuendelea kubaki palepale muda mwingi kuendelea kuomba,

Sasa hali kama hizi ukizifikia, ujue tayari umeshazama katika Roho, umeshawezeshwa na Roho, maombi yako yanakuwa na nguvu sana,

Mwingine anasikia raha Fulani moyoni, akiwa anaomba, mwingine ndio anazama katika kunena kwa lugha (kwa kusukumwa na Roho), na sio kwa akili. Mwingine anasindikizwa na kuusikia uwepo wa Mungu umemfunika, nguvu za Mungu zinashuka mwilini mwake, n.k. na unajikuta unafurahia sana maombi..

Kusudi la sisi kuomba sio kwenda kujitesa au kujiumiza, hapana bali ni mahusiano, tena ya kama mtu anazungumza na Baba yake. Kiasi kwamba ukitoka kwenye maombi unaona umetoka kweli kuwasiliana na mtu, sio umetoka kuusemesha ukuta, usiokuwa na mrejesho wowote, umeomba hewani hewani tu

Sasa ni mapenzi ya Mungu kwamba sisi watoto wake kila tuombapo tuombe katika Roho Mtakatifu. Tuzame, tuyafurahie maombi yetu. Sasa tunawezaje kufikia hatua hiyo?

Kabla ya kuona namna ya kufikia hicho kilele. Tuone kwanza vikwazo vinavyomzuia mtu asiombe kwa Roho.

VIKWAVYO VINAVYOPINGANA NA MTU KUOMBA KATIKA ROHO.

  1. Mwili
  2. Shetani

Hawa ndio maadui wawili wakubwa wa mtu kuzama. Ndio maana wewe kama mwombaji ni lazima uwafahamu, na ujue kabisa huna budi kushindana nao na ni lazima ukutane nao. Vinginevyo usipowatilia  maanani kila siku maombi yako yatakuwa ni ya “kawaida sana” na kila utakapofikiria  kitu kinachoitwa maombi utaona kama vile unapelekwa gerezani.

Ndugu Mungu hajakusudia tujihisi hivyo sisi watoto wake tunapomkaribia yeye, tuwe kama tunaliomba sanamu lisilonena, amekusudia kutupa mrejesho, na ndio hiyo zawadi ya Roho kuugua ndani yetu. Lazima atupe mrejesho wake kwamba yupo nasi.

Sasa uanzapo, hakikisha unaunyima mwili wako, raha zote, zinazokinzana na wewe kuomba. Kwamfano, ukijiona mwili unasinzia au unapoa wakati wa kuomba usipende kukakaa kwenye kiti, ni heri upige magoti, ukishindwa tembea-tembea. Tena ni vizuri ukanyoosha na mikono yako juu, huku umefunika macho. Kisha anza kuomba.

Usiogope adhabu hizo za mwanzoni hazitadumu muda mrefu sana utaingia katika Roho, ni mwili tu unakuambia wacha, kunitesa, wewe ulazimishe tu, ukikuambia leo siku nzima umefanya kazi legea-legea, pinga hayo mawazo. Hivyo ukiwa Sasa katika hali hiyo. Anza kuomba lakini pia tumia ahadi za Mungu zilizopo kwenye biblia ni muhimu sana, kulingana na jambo unaloliombea, mkumbushe Bwana, ulisema hivi, na hivi kwenye Neno lako,, Ulisema ni nani aliye Baba, mtoto wake akimwomba mkate atampa jiwe, mkumbushe mwambie ulisema, kama ungetazama dhambi zetu ni nani angesimama,..mwambie ulisema niite nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa na magumu usiyoyajua n.k..Tumia njia hiyo, kujimimina kwa Bwana

Omba huku umetilia umakini(concentrate), mawazo yako ukiyalazimisha yasiende nje ya Mungu. Tengeneza picha halisi Mungu amesimama mbele yako kukusikia, fumba macho. Usiruhusu kufikia mambo ya nje, kwasababu akili yako itakuwa shapu kukutoa, ukitoka rudi, endelea kuomba. Ndio ni kipindi kifupi utataabika , lakini hatimaye utazama tu.. Sasa ukiendelea kudumu kwa kung’ang’ania huko  kwenye maombi hayo kwa kipindi fulani. Hayo mazingira rafiki ya Roho Mtakatifu kuyaingilia maombi yako. Utashangaa tu, wepesi usio wa kawaida umezuka ndani yako. Tangu huo wakati endelea kuomba kwa jinsi usikiavyo rohoni, kwani hayo maneno unayoyaomba mengine hutaelewa unayatolea wapi, huyo ni Roho Mtakatifu anaomba na wewe.

Ndio maana akasema msifikiri-fikiri, kwasababu Roho mwenyewe atawajalia.  Wengine kabla ya kuomba wanasema sijui nitaomba nini? Ndio hujui kwasababu bado hujazama, ukishazama utaweza tu kuomba kwasababu ni yeye ndio anayekujalia. Wengine wanasukumwa kunena kwa lugha n.k.

Adui wa pili ni shetani. Huyu anapaswa apingwe kwa kukemewa. Kabla ya kuanza maombi, hakikisha unayateka mazingira yako ya kimaombi. Ukimwomba Mungu, afukuze uwepo wote wa mapepo, hapo ulipo.  Dalili ya shetani, ni pale unashangaa ukiwa unataka kuomba kichwa kinauma au tumbo, au hali Fulani isiyo ya kawaida inakuvaa katika mwili wako. Huyo ni shetani, mpinge kwa kukemea kisha endelea na maombi. Au mwingine anaona mazingira ya kusumbuliwa, mara kelele Fulani za nje, au simu zinaingia, ambazo si kawaida sikuzote kuwepo. Ndio maana ni vizuri katika kuomba kwako uzime simu. Ukae mbali na mazingira yenye mwingiliano, hiyo itakufanya umpe adui wakati mgumu kukusumbua.

Zingatia tu: Shetani haogopi sana maombi ilimradi maombi, anaogopa sana maombi yaliyo katika Roho, Hata kama ni ya muda mfupi, hayapendi, na ndio atakayoyapiga vita sana. Hivyo usiwe mwepesi mwepesi kupenda kuomba juu juu.

Kwahiyo ukizingatia mambo hayo mawili kutakufanya uzame rohoni katika maombi yako yote. Na utayafurahia na utaona matokeo pia.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika sanduku la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

JE! TUNAPASWA TUOMBE MARA NGAPI KWA SIKU?

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

Rudi nyumbani

Print this post

Wakili ni nani kibiblia? Uwakili ni nini?

Wakili kibiblia ni mtu aliyepewa usimamizi wa nyumba (Au kaya) ya mtu mwingine. Na usimamizi huo unajumuisha kuanzia kwenye ngazi ya kifamilia, mpaka mali alizonazo bwana wake.

Uwakili tunaona tangu enzi za agano la kale, kwamfano, Eliezeri alikuwa ni wakili wa Ibrahimu. Na tunaona yeye ndio alikuwa mwangalizi wa mali zake, lakini pia ndiye aliyehusika kwenda kumtafutia Isaka, mke katika ukoo wa baba zake Ibrahimu (Mwanzo 15:2, Mwanzo 24).

Lakini pia tunamwona Yusufu, naye alikuwa ni wakili katika nyumba ya Potifa, aliachiwa vyote avisimamie, (Mwanzo 39:5-7).

Vilevile tukirudi kwenye agano jipya tunaona,  Bwana Yesu alitumia mifano ya mawakili, kuwawakilisha watumishi wake wanaofanya kazi ya kuhudumu/kulichunga kundi lake, kwamba kwa mifano ya wao na sisi tujifunze utumishi uliosahihi kwake.

Kwamfano Luka 12:40-48 Inasema;

“Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu.

41  Petro akamwambia, Bwana, mithali hiyo umetuambia sisi tu, au watu wote pia?

42  Bwana akasema, Ni nani, basi, aliye WAKILI mwaminifu, mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya utumishi wake wote, awape watu posho kwa wakati wake?

43  Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta anafanya hivyo.

44  Kweli nawaambia, atamweka juu ya vitu vyake vyote.

45  Lakini, mtumwa yule akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia kuja, akaanza kuwapiga wajoli wake, wanaume kwa wanawake, akila na kunywa na kulewa;

46  bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wasioamini.

47  Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.

48  Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi”

Ikiwa wewe umepewa dhamana ya kulichunga/kulisimamia kundi, basi tambua kuwa Bwana anataka aone uaminifu wako wa kuwahudumia na kuwalinda watu wake aliokupa. Yesu alipomuuliza Petro Je! Wanipenda akasema ndio nakupenda!, Hapo hapo akamwambia chunga kondoo zangu, lisha kondoo wangu. Kuonyesha kuwa ikiwa wewe ni mtumishi na unasema unampenda Bwana, basi ujue upendo wako ni kuwachunga na kuwalisha kondoo wa Bwana.

Lakini pia uwakili sio tu kwa waliowatumishi wa Mungu, bali pia kwa kila mwaminio, aliyeokoka, amepewa uwakili wa kuifanyia kazi  kwa ile talanta aliyopewa.

Bwana Yesu alitumia mfano wa Yule mtu aliyesafiri, akawaita watumwa wake, akawawekea mali yake yote wafanyie biashara, Hivyo mmoja akapewa talanta 5, mwingine 2, mwingine 1. Kama tunavyoijua habari wale wawili wa kwanza wakafanikiwa kuzalisha, lakini Yule mmoja wa mwisho hakuifanyia chochote talanta yake, akaiacha mpaka aliporudi bwana wake. Matokeo yake ikawa ni kunyang’anywa na kutupwa katika giza la nje (Mathayo 25:14-30).

Hiyo ni kutufundisha kuwa hakuna hata mmoja wetu, ambaye hajapewa karama na Mungu, hivyo unapaswa ujiulize, je! Talanta yangu ninaitumiaje, Uwakili wangu ninautumiaje Je! Ni katika kuujenga ufalme wa Mungu, au katika mambo yangu mwenyewe.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa waliokoka wote ni mawakili wa Kristo. Na hivyo Bwana anataka aone wakihudumu katika nyumba yake kwa uaminifu wote. Na ndivyo mitume wa Bwana walivyojiona mbele za Mungu.

1Wakorintho 4:1  Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.

2  Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.

Vifungu vingine ambavyo utakutana na neno hili ni hivi; Luka 16:1-13, 1Wakorintho 9:17, Waefeso 3:2, Wakolosai 1:25.

Bwana akubariki.

Swali ni je! Umeokoka? Kama sio unasubiri nini? Mpokee sasa Bwana Yesu ili akupe uzima wa milele bure. Kumbuka hizi ni siku za mwisho, Yesu yu mlangoni kurudi , akikukuta hujaitendea kazi talanta yako utamjibu nini, Na umeshaisikia injili?

Ikiwa upo tayari leo kumpokea Bwana, akusamehe dhambi zako, basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

ANGALIA JINSI USIKIAVYO:

Mtakatifu ni Nani?

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)

Beelzebuli ni nani? (Mathayo 12:24).

Mierebi ni Nini kwenye biblia? (Isaya 15:7)

Rudi nyumbani

Print this post

Hadaa ni nini kibiblia? (2Petro 2:14)

Kuhadaa ni kudanganya, au kulaghai, kutumia njia isiyosahihi/ ya mkato kufanikisha au kupata jambo.

Neno hilo utalipata katika vifungu hivi baadhi;

Mwanzo 31:20 “Yakobo akamhadaa Labani, Mshami, kwa kuwa hakumwambia ya kwamba anakimbia”

Mithali 12:5 “Mawazo ya mwenye haki ni adili; Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa”

Warumi 1:28  Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. 1.29  Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na HADAA; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya

2Petro 2:14  wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, wenye kuhadaa roho zisizo imara, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana;

2Petro 2:18  Maana wakinena maneno makuu mno ya kiburi, kwa tamaa za mwili na kwa ufisadi huwahadaa watu walioanza kuwakimbia wale wanaoenenda katika udanganyifu;

Mifano halisi ya kuhadaa ni hii;

> Kama mume, unapotoka na kwenda kwenye kumbi za starehe kucheza miziki na kuzini na kulala huko na makahaba, kisha unamwambia mke wako umesafiri, huko ni kuhadaa.

>Kama mfanyabiashara, unapopunguza uzito jiwe la mizani, ili umpimie mteja kipimo kidogo kwa bei ileile, au unapozidisha bei ya bidhaa juu zaidi ya ile iliyo elekezi, huko ni kuhadaa.

> Kutumia ujuzi wako, au utumishi wako, kusema uongo, ili kupata maslahi Fulani kutoka kwa huyo mtu. Kwamfano wewe ni mchungaji, halafu unasema Bwana ameniagiza mtoe kiwango Fulani cha fedha kila mmoja ili kupokea uponyaji kutoka kwangu, . Hapo umewahadaa watu wa Mungu, kwasababu unajua kabisa tumeambiwa tutoe bure, kwasababu tulipokea bure.

Tabia ya kuhadaa ni tabia ya shetani, kwani ndio silaha ya kwanza aliyoitumia kumwangusha mwanadamu pale Edeni, alipokwenda kumuhadaa Hawa, kwa kumwaminisha kuwa akila matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya hatokufa. Lakini ilikuwa kinyume chake.

Bwana Yesu anasema, shetani ni baba wa uongo. Hivyo na sisi tunapodhihirisha tabia hii ya kutumia udanganyifu na hila, ni wazi kuwa tunadhihirisha tabia za wazi na za asili za shetani.  Kumbuka Hadaa ni zao la wivu na kutokupenda maendeleo kwa wengine.

Tukiwa na upendo. Tabia hii itakufa ndani yetu. Tuutafute upendo wa Mungu

Je! Unasumbuliwa na dhambi hii au dhambi nyingine yoyote? Yesu pekee ndio tiba, atakusaidia kuishinda. Ikiwa upo tayari leo kumfanya kuwa Bwana na kuupokea msamaha wake bure. Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

WENYE KUHADAA ROHO ZISIZO IMARA.

Sukothi ni nini? (Mwanzo 33:17).

Kuba ni nini (Ayubu 22:14)?

Ipi tofauti kati ya matoleo na sadaka?

Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;

Fahamu Maana ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! waliokufa kabla ya Bwana Yesu wataokolewaje?

Swali: Je waliokufa kabla ya Bwana Yesu kuja (yaani watu wa agano la kale)wataokolewaje?.. kwamaana tunajua kupitia damu ya Yesu tu! ndio tunapata ukombozi wa hakika wa dhambi, sasa waliokuwa wanaishi katika agano la kale wataokolewaje na ilihali Kristo alikuwa hajafa bado, na damu iondoayo dhambi haijamwagika?.

Jibu: Ni kweli ukombozi unapatikana kupita damu ya Yesu tu!

Lakini ni vizuri kufahamu kuwa Agano jipya halikuja kulifanya agano la kale liwe uongo, badala yake limekuja kulikamilisha agano la kale, kama Bwana wetu Yesu alivyosema mwenyewe katika Mathayo 5:17..

Mathayo 5:17  “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza”

Sasa Ili tuelewe vizuri hebu tutafakari  mfano ufuatao.

Taasisi moja imedahili wanafunzi wake walioingia kupitia mfumo wa makaratasi, kwamba mwanafunzi ili akubalike kujiunga na chuo hana budi kuwasilisha fomu zake katika ofisi ya taasisi hiyo…. Lakini mwaka mmoja baadaye ikabadili mfumo na kuanza kudahili wanafunzi wapya kupitia mfumo wa kieletroniki kwamba ili mwanafunzi akubalike kujiunga na taasisi hiyo hana budi kutumia mfumo wa kielekroniki hata akiwa nyumbani kupitia internet. Na kwamba hakuna mwanafunzi yeyote atakayeweza kupokelewa bila kutumia mfumo huo, kwani ni mrahisi na mwepesi katika kutunza kumbukumbu.

Sasa swali ni je! mfumo huo mpya ulioanza utawafanya wale wanafunzi wa zamani ambao walitumia mfumo wa zamani kuwa si wanafunzi halali tena wa taasisi hiyo?.. au itawafanya wale waliokwisha kuhitimu zamani, waliotumia mfumo wa zamani vyeti vyao kuwa batili?.

Jibu ni la!.. Wataendelea kuwa wanafunzi, isipokuwa watakaojiunga upya hawana budi kutumia mfumo mpya..kwasababu mfumo wa zamani utakuwa umeshabatilika!.

Kadhalika na Agano la kale ni hivyo hivyo…Ulikuwa ni mfumo wa zamani wa kuwasogeza watu karibu na Mungu, lakini ulikuwa na mapungufu mengi!.. Lakini muda ulipofika, ulikuja mfumo bora Zaidi na mwepesi na wa haraka ambao utamwingiza mtu katika ufalme wa Mungu kirahisi na kihakika zaidi, na huo ndio mfumo wa Agano jipya kupitia agano la damu ya Yesu Kristo, na si tena damu ya mafahali na kondoo..kama maandiko yanavyosema katika Waebrania 10:4.

Waebrania 10:4 “Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.”

Na hivyo kulifanya Agano la kwanza liwe chakavu na agano la pili liwe jipya sawasawa na Waebrania 8:13.

Waebrani 8:13  “Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka”

Neno “kuukuu” maana yake ni “kuchakaa”… kwahiyo lilipokuja agano jipya, basi agano la kwanza likafanyika kuwa la kale, lisilotumika tena… hivyo kwasasa halifanyi kazi tena.

Kwahiyo waliokuwepo ndani ya Agano la kwanza kabla ya Bwana Yesu hao watahesabika kuwa watakatifu sawasawa tu waliopo sasa katika agano jipya leo, ndio maana akina Musa, Eliya, Henoko, Ibrahimu, Daudi, Danieli na wengineo wanatajwa kuwa miongoni mwa watakatifu, tena mashujaa wa Imani… ijapokuwa hawakubatizwa! Wala kumwona Masihi..

Lakini baada ya Bwana Yesu kuja na damu yake kumwagika basi wote watakaozaliwa baada ya hapo, hawana budi kulitumia agano jipya, na kuachana na lile la kale…na yeyote atakayejitumainisha kwa agano la kale basi hataweza kuokoka kabisa.

Hiyo ndio sababu kwanini tunapaswa tulijue sana Agano jipya na misingi yake, kwasababu tukianza kuwatanzama watu wa Agano la kale, pasipo kujua misingi ya agano jipya, tutajikuta tunachukua vitu visivyofaa kwa watati wa sasa….kwamfano tukimtazama Daudi na maisha yake na kanuni alizokuwa anatembelea si zote zitatufaa sisi watu wa agano jipya, kwamfano utasoma ijapokuwa Daudi aliupendeza Moyo wa Mungu sana lakini alikuwa na wake wengi na alikuwa na visasi na maadui zake.

Sasa tutachukua na kujifunza Imani ya Daudi, unyenyekevu wa Daudi na mengine mazuri, lakini hilo la kuoa wake wengi, Agano jipya inalikataza, hilo la kulipiza kisasi agano jipya limetuzuia..…hatuna budi kumsikiliza aliye mkuu Zaidi ya Daudi, na Sulemani, na Musa, na Eliya ambaye ni Yesu, anayetajwa kama Mjume wa Agano jipya (katika Waebrania 9:15 na Waebrania 12:24), ambaye anasema kila amwachaye mkewe na kuoa mwingine azini, na ndoa ni mke mmoja, mume mmoja..si Zaidi ya hapo!(Mathayo 19:4), ambaye amesema “tusilipe kisasi” (Mathayo 5:38-39). n.k

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

MJUMBE WA AGANO.

LITURJIA NI NINI? NA JE IPO KIMAANDIKO?.

Biblia ilimaanisha nini iliposema “Mwanamke atamlinda mwanamume” Yeremia 31:22?

JE! ULEVI NI DHAMBI?.

Nini maana ya “Bwana Yesu ni mzaliwa wa kwanza wa waliokufa?”(Ufunuo 1:5)

NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Sukothi ni nini? (Mwanzo 33:17).

Jibu: Tusome,

Mwanzo 33:17 “Yakobo akaendelea mpaka Sukothi. Akajijengea nyumba, akawafanyia makundi yake vibanda. Kwa hiyo jina la mahali pale pakaitwa Sukothi”. 

Tafsiri ya neno “Sukothi” ni “Mahema”.. Hii ni lugha ya kiebrania.

Mahali hapa ni pale ambapo Yakobo alipiga kambi baada ya kutoka Padan-aramu, mji aliokuwepo Labani.(Mwanzo 28:1-2), na alikaa huko Padan-aramu kwa muda wa miaka 21, baada ya kulaghaiwa na Labani kwa muda wote huo.

Akiwa njiani baada ya kutoka kwa Labani alifika mahali ambapo ilimgharimu kutulia kidogo kisha andelee na safari, hivyo badala ya kujenga makazi ya kudumu, yeye akajenga mahema machache tu, kwasababu ya muda kwani bado alikuwa katika safari ya kuelekea Shekemu (Mwanzo 33:18). Hivyo Yakobo akaliita eneo hilo Sukothi kutokana na mahema hayo, na eneo hilo likaendelea kuitwa hivyo kwa vizazi vingi baadaye.

Na eneo la Sukothi kijeografia lipo maeneo ya nchi ya Yordani mpakani na Israeli.

Waamuzi 8:4 “Basi Gideoni akafika Yordani, akauvuka, yeye na hao watu mia tatu waliokuwa pamoja naye, walikuwa wamepungukiwa na nguvu, lakini wawafuatia vivyo.

 5 Naye akawaambia watu wa Sukothi, Tafadhali wapeni mikate hao watu waniandamao; kwa maana wanapungukiwa na nguvu, nami ni katika kuwafuatia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani”.

Kujua ni somo gani lingine tunalipata kuhusu Sukothi?…Fungua hapa >>TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

Kwanini Labani aseme Yakobo ni Mfupa wake na nyama yake?(Mwanzo 29:14)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?

Swali: Je sisi watu wa agano jipya ni lazima kuwa na vipindi vya kuombea mlimani?. Na je huko mlimani Mungu ndioko anakosikia Zaidi maombi kuliko chini?.. msaada!

Jibu: Hakuna agizo lolote katika biblia la mahali rasmi pa kuombea!, kama ni  mlimani au kama ni chini.. Lakini tunaweza kujifunza kupitia watu kadhaa katika biblia jinsi walivyoomba na kisha tunaweza kujifunga kitu.

BWANA YESU MWENYEWE.

Mathayo 14:22 “ Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.

23  Naye alipokwisha kuwaaga makutano, ALIPANDA MLIMANI FARAGHANI, KWENDA KUOMBA. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake”.

Na pia…

Luka 6:12  “Ikawa siku zile aliondoka AKAENDA MLIMANI ILI KUOMBA, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu”.

Soma pia Marko 6:46 na Yohana 6:15, utaona jambo hilo hilo la Bwana kupanda mlimani kuomba, na pia utaona sehemu nyingine alipanda na wanafunzi wake, soma Luka 9:28.

Umeona?.. Kama Bwana Yesu kuna nyakati alikuwa akienda mlimani kuomba, yeye pamoja na wanafunzi wake maana yake si bure!.. Kuna kitu cha ziada katika milima.

Na kitu hiko si kingine Zaidi ya UWEPO WA MUNGU. Milimani kunakuwa na Uwepo wa Mungu zaidi ya mabondeni?. Na kwanini milimani kunakuwa na Uwepo wa Mungu Zaidi ya sehemu nyingine nyingi?.

Ni kwasababu kule juu kunakuwa na utulivu,.. na siku zote utulivu unavuta uwepo wa Mungu, na milimani ni sehemu ambazo hazina usumbufu hivyo ni rahisi mtu kuzama katika roho kuliko akiwa chini penye masumbufu mengi na mwingiliano wa Sauti nyingi.

Umewahi kujiuliza ni kwanini minara ya simu huwa inapelekwa juu katika milima na haiwekwi mabondeni?.. Ni kwasababu kule juu network inapatikana vizuri Zaidi ya chini, kwasababu hakuna vizuizi vingi vya kuzuia mawimbi kusafiri. Sasa kama wanadamu wameiona hiyo siri iliyopo juu ya milima, vipi kwetu sisi wakristo?

Si kwamba Mungu hatakusikia ukiomba mabondeni, atakausikia lakini ule uwepo wa Mungu kwako unaweza usiupate vizuri kuliko kama ungeenda kuomba sehemu iliyoinuka (Milimani). Ndio maana utaona mtu anakuwa mzito kuomba, pasipo kujua chanzo ni nini?.. Wakati mwingine si mapepo!, bali ni mazingira tu!… Badili mazingira na utaona jinsi utakavyozama katika roho na maombi!.

Kwahiyo kama wakristo ambao pia ni mwanafunzi wa biblia, ni lazima tuwe na vipindi vya kupanda mlimani kuomba!. Kama mahali ulipo hapana milima, basi linaweza lisiwe jambo la lazima sana, lakini kama ipo basi tenga muda wa kufanya hivyo mara chache chache na utaona matokeo makubwa sana na vile vile utaona utofauti na utafungua mlango mpana sana wa kupokea mafunuo kutoka kwa Baba.

Bwana akubariki.

Marana tha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

UTAONA MAMBO MAKUBWA KULIKO HAYA.

AKIJUA YA KUWA ANA WAKATI MCHACHE TU”.

Fahamu Namna ya Kuomba.

KUNA AINA NGAPI ZA MAOMBI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu aikabidhi roho yake mikononi mwa Baba (Luka 23:46)?

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 43..

Luka 23:44  “Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda,

45  jua limepungua nuru yake; pazia la hekalu likapasuka katikati.

46  Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU.

47  Alipokwisha kusema hayo alikata roho. Yule akida alipoona yaliyotukia, alimtukuza Mungu, akisema, Hakika yake, mtu huyu alikuwa mwenye haki”.

“Mikononi mwako naiweka roho yangu”… haya yalikuwa ni maneno ya Mwisho ya Mwokozi wetu Yesu Kristo alipokuwa pale msalabani?.. lakini swali? Ni kwanini aseme hivyo? Je kulikuwa na ulazima wowote  wa yeye kusema vile, na sisi je tunafundishwa kusema maneno kama hayo tunapokaribia hatua za kumalizia safari zetu za maisha?

Kabla ya kujibu, ni muhimu kufahamu kuwa kabla ya Bwana Yesu kufa na kushuka kuzimu na kupewa zile funguo za Mauti, sehemu ya wafu haikuwa salama (maana yake roho za watatakatifu bado hazikuwa salama hata baada ya kufa).

Ndio maana utaona hata Nabii Samweli ambaye alikuwa ni mtu wa haki sana mbele za Mungu, lakini baada ya kufa kwake, yule mwanamke wa Endori aliyekuwa mganga aliweza kumtoa kuzimu na kumpandisha juu kichawi.

1Samweli 28:7 “Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, nipate kumwendea na kuuliza kwake. Watumishi wake wakamwambia, Tazama, yuko mwanamke mwenye pepo wa utambuzi huko Endori. 

8 Basi Sauli akajigeuza, na kuvaa mavazi mengine, kisha akaenda, yeye na watu wawili pamoja naye, wakamfikilia yule mwanamke usiku; akasema, Tafadhali unibashirie kwa utambuzi, ukanipandishie yeye nitakayemtaja kwako. 

9 Yule mwanamke akamwambia, Angalia, unajua alivyofanya Sauli, jinsi alivyowakatilia mbali hao wenye pepo wa utambuzi na wachawi katika nchi; mbona basi wanitegea tanzi uhai wangu, ili kuniua?

10 Naye Sauli akamwapia kwa Bwana, akasema, Aishivyo Bwana, haitakupata adhabu yo yote kwa jambo hili. 

11 Ndipo yule mwanamke aliposema, Je! Ni nani nitakayekupandishia? NAYE AKASEMA, NIPANDISHIE SAMWELI”.

Umeona hapa? roho ya nabii Samweli inataabishwa na wachawi hata baada ya kufa kwake.. Ndio maana utaona Samweli baada ya kupandishwa juu alimlalamikia Sauli kwanini anamtaabisha.

1Samweli 28:15 “Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Mbona umenitaabisha mimi, hata kunipandisha juu?….”

Kwasababu hiyo ndio maana Bwana Yesu akaikabidhi roho yake kwa Baba, kama tu alivyokuwa anazikabidhi kazi zake na safari zake kwa Baba kipindi akiwa hai, vivyo hivyo alifahamu kuwa kuna umuhimu wa kufanya hivyo pia kwaajili ya roho yake baada ya kufa.

Lakini tunaona alipokufa, Baba alimpa funguo za KUZIMU na MAUTI sawasawa na Ufunuo 1:17

Ufunuo 1:17 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18  na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU”

Maana yake kuwa kuanzia wakati wake mpaka mwisho wa dunia, shetani hatakuwa na uwezo tena wa kuzitaabisha roho za watakatifu waliokufa, hivyo Bwana Yesu sasa ndiye mwenye mamlaka hayo juu ya roho zote za waliokufa na walio hai.

Warumi 14:8 “Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana.

9 Maana Kristo alikufa akawa hai tena KWA SABABU HII, AWAMILIKI WALIOKUFA NA WALIO HAI PIA”.

Kwahiyo kwasasa hatuna hofu tena ya kwamba baada ya kifo roho zetu zitataabishwa, bali tukifa basi uhai wetu (roho zetu) zinafichwa mbali na adui. Na sehemu hiyo ya maficho ambayo shetani hawezi kuifikia ni Paradiso, mahali pa mangojeo na raha, huku tukiingoja ile siku ya ahadi, ya unyakuo wa kwenda mbinguni. Haleluya!.

Kwahiyo kwasasa hatuna maombi ya kuzikabidhi roho zetu kwa baba wakati wa kufa, kwasababu tayari Kristo anazo funguo za mauti na kuzimu, bali tunapaswa wakati huu sasa tulio hai tuyakabidhi maisha yetu kwake, na kuishi maisha ya kumpendeza,  ili tutakapomaliza safari ya maisha yetu basi tujikute tupo sehemu salama, kwasababu hatujui ni saa ipi tutaimaliza safari yetu ya maisha hapa duniani.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

JIWE LILILO HAI.

ORODHA YA IMANI POTOFU- Sehemu ya 1.

Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?

Kwanini Bwana Yesu alisema pale msalabani naona kiu?

Rudi nyumbani

Print this post