Sukothi ni nini? (Mwanzo 33:17).

Sukothi ni nini? (Mwanzo 33:17).

Jibu: Tusome,

Mwanzo 33:17 “Yakobo akaendelea mpaka Sukothi. Akajijengea nyumba, akawafanyia makundi yake vibanda. Kwa hiyo jina la mahali pale pakaitwa Sukothi”. 

Tafsiri ya neno “Sukothi” ni “Mahema”.. Hii ni lugha ya kiebrania.

Mahali hapa ni pale ambapo Yakobo alipiga kambi baada ya kutoka Padan-aramu, mji aliokuwepo Labani.(Mwanzo 28:1-2), na alikaa huko Padan-aramu kwa muda wa miaka 21, baada ya kulaghaiwa na Labani kwa muda wote huo.

Akiwa njiani baada ya kutoka kwa Labani alifika mahali ambapo ilimgharimu kutulia kidogo kisha andelee na safari, hivyo badala ya kujenga makazi ya kudumu, yeye akajenga mahema machache tu, kwasababu ya muda kwani bado alikuwa katika safari ya kuelekea Shekemu (Mwanzo 33:18). Hivyo Yakobo akaliita eneo hilo Sukothi kutokana na mahema hayo, na eneo hilo likaendelea kuitwa hivyo kwa vizazi vingi baadaye.

Na eneo la Sukothi kijeografia lipo maeneo ya nchi ya Yordani mpakani na Israeli.

Waamuzi 8:4 “Basi Gideoni akafika Yordani, akauvuka, yeye na hao watu mia tatu waliokuwa pamoja naye, walikuwa wamepungukiwa na nguvu, lakini wawafuatia vivyo.

 5 Naye akawaambia watu wa Sukothi, Tafadhali wapeni mikate hao watu waniandamao; kwa maana wanapungukiwa na nguvu, nami ni katika kuwafuatia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani”.

Kujua ni somo gani lingine tunalipata kuhusu Sukothi?…Fungua hapa >>TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

Kwanini Labani aseme Yakobo ni Mfupa wake na nyama yake?(Mwanzo 29:14)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments