Jina la Bwana YESU KRISTO, Mkuu wa uzima, libarikiwe.
Karibu tujifunze biblia, neno la Mungu wetu lililo taa na mwanga wa njia yetu (Zab.119:105)
Biblia inatufundisha kuwa TUMTAKE BWANA na NGUVU ZAKE.
Zaburi 105: 4 “MTAKENI BWANA NA NGUVU ZAKE, Utafuteni uso wake sikuzote”.
Wengi tunaishia “Kuzitaka tu nguvu za Bwana” …. lakini biblia hapa inatufundisha tumtake Bwana pamoja na nguvu zake, maana yake mambo hayo mawili yanaenda sambamba…
Unaweza kuwa na nguvu za Bwana, lakini usiwe na Bwana kabisa!, utauliza kwa namna gani?.
Bwana Yesu alisema, wengi watakuja siku ile na kusema Bwana hatukufanya miujiza mingi kwa jina lako?, lakini yeye atasema “sikuwajua kamwe”.
Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?.
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, SIKUWAJUA NINYI KAMWE; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Nataka uone hapo anaposema “sikuwajua kamwe”.. Neno “kamwe” maana yake ni kwamba hajawahi kabisa kuwa na mahusiano nao, katika kipindi chote na maisha yao..maana yake tangu wakiwa duniani Bwana hakuwajua watu hao, ingawa walikuwa wanazo nguvu za Mungu zikitembea nao, walikuwa na nguvu za Mungu za kutoa pepo, za kufanya miujiza mingi, lakini hawakuwa na Mungu katika maisha yao.
Sasa biblia inatufundisha tumtake “Bwana na Nguvu zake”, cha kwanza tumatake yeye Bwana, halafu cha pili ndio kiwe nguvu zake!.
Sasa tunamtakaje Bwana na tunampataje Bwana?..Tunampata Bwana kwa kuyafanya mapenzi yake.
Na mapenzi ya Mungu ni yapi?
1Wathesalonike 4:3 “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;
4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;
5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.
Na tunatakaswa kwa kumwamini Bwana Yesu Kristo, ambapo Imani hiyo inazaa toba na ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU KRISTO kwaajili utakaso wa dhambi (Matendo 2:38) . Kwa kufanya hayo basi utakuwa umemtaka Bwana, na yeye ataingia katika maisha yako, na atadhihirisha neema yake kwako pamoja na nguvu zake.
Lakini usitangulize kuzitafuta nguvu za Mungu na huku yeye hayupo nawe!.
Bwana atusaidie.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
JINSI YA KUSIMAMA NA KUFUNDISHA/ KUHUBIRI
NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?
SWALI: Bwana Yesu asifiwe naomba kufahamu maana ya hili andiko;
1Wakorintho 14:20 “Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima”
JIBU: Kwa kawaida mtoto mchanga anakuwa kama mjinga, haelewi mambo mengi, anachofahamu ni kile tu kilichopo nyumbani, mambo mengine ya nje, hayajui, na ndicho kinachomfanya asijisumbue na hayo mengine, ambayo watu wazima wanayasumbukia,. Vivyo hivyo na Mungu anataka katika suala la uovu, tuwe hivyo. Kama wajinga, hatujui kinachoendelea, hatuna maarifa nayo, hatuwezi kuyaelewa. Na hiyo itatufanya tuwe salama.
Kwamfano ukiulizwa habari za nyimbo Fulani mpya za kidunia zilizotoka, huna taarifa nazo, Ukiulizwa habari za ligi za mipira, ni kama taarifa usizozielewa, ukisemeshwa na mambo ya kubeti, ni kama mtu anazungumza na wewe kwa lugha za mafumbo.
Ndio maana andiko hili linasema hivyo;
1Wakorintho 16:19b “…lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya”
Kutokujua kila kitu katika huu ulimwengu sio dhambi, na wala hilo halitakuzuia uishi vema. Hivyo tunapaswa tuchuje, ni nini kinatufaa na kipi kisichotufaa, Vile visivyotufaa tuviweke kando, tuwe watoto katika hivyo, lakini vile vitujengavyo, ambalo ni NENO LA MUNGU, basi tuwe watu wazima. Tulijue sana hilo kwasababu ndio uzima wetu ulipo.
Bwana akubariki
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?
Nini maana ya vifungeni viuno vya Nia zenu? (1Petro 1:13)
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)
Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)
SWALI: Nimesikia hili neni Rhema, likitajwa sana Kwa watumishi na sehemu mbalimbali, naomba nifahamishwe maana yake Nini, mbona silioni kwenye biblia?
JIBU: Ni vema kutambua kuwa Biblia, katika eneo la agano jipya sehemu kubwa imeandikwa kwa lugha ya kiyunani. Hivyo Kuna baadhi ya maandishi ambayo tukiyasoma katika lugha nyingine mfano kwenye yetu hii ya kiswahili, tunaweza kuona yalimaanisha jambo lile lile moja lakini tukirudi kwenye lugha ya asili ya kiyunani yalimaanisha maana zaidi ya Moja.
Kwamfano, tunapokutana na hili Neno “NENO”. kwenye tafsiri yetu ya kiswahili, Mahali pote limeandikwa hivyo hivyo tu “Neno” likimaanisha Neno la Mungu.
Lakini tukirudi kwenye lugha ya asili ya kiyunani zipo sehemu limelitajwa kama “Logos”na sehemu nyingine kama “Rhema”
Logos ikiwa na maana Neno la Mungu la Daima/ wazo la Mungu/mpango wa Mungu ulioandikwa na pia kama Yesu Kristo mwenyewe, ambaye ndio Neno lililofanyika mwili.
Lakini ‘Rhema’: maana yake ni “Neno lililosemwa na Mungu” . Ni neno la wakati husika, sio la daima.
Mfano wa maandiko yanayolitaja Neno kama Logos ni haya: Yohana 1:1-18, Yakobo 1:22, Waebrania 4:12. N.k
Na mfano wa maandiko yanayolitaja Neno la Mungu kama Rhema ni haya;
Mathayo 4:3-4
[3]Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. [4]Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
Hapo Bwana aliposema, “ila Kwa Kila Neno litokalo katika kinywa Cha Bwana”..alimaanisha Neno lisemwalo na Bwana.. mfano wa Eliya alipomwambia yule mwanamke mjane, Bwana asema hivi; “lile pipa la unga halitapinguka, Wala Ile chupa ya mafuta haitaisha”. (1Wafalme 17:14). Halikuwa Neno ambalo lilitumika Kwa wakati wote, ambalo hata sasa tunaweza litumia sisi, Bali la wakati ule ule tu, amefunuliwa, akalisema na ikiwa hivyo.
Lakini ‘Rhema’ ni yaliyonenwa Kwa wakati huo tu..tofauti ya Yale yaliyokuwa Daima.
Neno lingine ambalo linasomeka kama Rhema katika biblia,. Ni wakati ule mitume wamehangaika usiku kucha kutafuta samaki, lakini kulipokucha Yesu akawaambia watweke.mpaka vilindini wakavue. Petro akasema maneno haya;
Luka 5:5
[5]Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.
Aliliamini Neno lililosemwa na Bwana (na ikiwa vile).
Ili kuelewa vizuri tunaweza kusema “logos” ni BIBLIA TAKATIFU, na Rhema’ ni Neno mtu analofunuliwa Kwa kipindi Fulani.
JE! MUNGU ANASEMA NA SISI HATA SASA KAMA RHEMA?
Ni kweli Mungu ameshatupa njia yake kuu ya kusema na sisi, ambayo ni Kwa kupitia Biblia. Lakini pia bado Mungu anasema nasi, na kutushushia Neno lake Kwa wakati husikia litufae.
Tuwapo katika kanisa. Mungu hutumia karama mbalimbali, kusema nasi, au kutupa ujumbe wake. Anasema kutumia unabii au fundisho, au Neno la hekima, au maono, au ndoto, kutuwasilishia Neno lake.
Lakini pia ni lazima tujue kuwa Neno hilo lililofunuliwa ni sharti lisikinzane na Neno lake lililoandikwa. Vyote viwili vikichanganyikana huleta matokeo makamilifu na kutufanya tumwone Mungu katika uhalisia wake zaidi katika maisha yetu, kwasababu yeye Yu hai.
Lakini ipo hatari kubwa sana. Kwani katika siku hizi za mwisho wapo baadhi ya watu wanalichukua Neno liliokuwa kama Rhema, na kulifanya logos yao. Ndio hapo wanaposoma Bwana Yesu alitema mate chini akachanganya na udongo, akampaka mtu machoni akaona, hivyo na wenyewe wanafanya hivyo Kwa kisingizio kuwa andiko limeruhusu. Au wanapomsoma mtume Paulo anatoa leso yake, Kisha watu wanapona kupitia Ile, na wenyewe wanafanya hivyo hivyo, wakisema andiko limeruhusu. Hawajui kuwa ulikuwa ni ufunuo wa wakati ule ambao si agizo kuu, ni Rhema’.
Na madhara ya jambo hili ndio linageuka kuwa ibada ya sanamu. Tunayo mifano kadhaa katika biblia ya watu ambao waligeuza Rhema kuwa Logos, ikawapelekea kuingia katika laana. Kipindi Wana wa Israeli wakiwa jangwani, walipomkosea Mungu alimwagiza Musa aunde nyoka wa shaba, ili Kila amtazamaye apone. Na kweli ilikuwa vile. Lakini baada ya pale haikuwa sheria mama kama vile torati, kana kwamba waendelee kufanya vile. lakini tunaona baadhi ya watu walikuja kuifanya kama ndio sehemu Yao ya ibada ya uponyaji Kwa Mungu,.mpaka Mungu akachukizwa ikawapelekea kupelekwa tena utumwani Babeli, ikiwa kama mojawapo ya sababu.(2Wafalme 18:4)
Agizo letu la wakati wote ni JINA LA YESU TU! ndio logos yetu Bwana aliyotuagiza tutumie, wakati wote. Ikiwa hujafunuliwa kutumia kisaidizi/kiambatanishi kingine basi usifanye kwani huyo sio Mungu nyuma yake. Tegemea Biblia zaidi.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?
NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.
Miimo ni nini na kizingiti ni nini?
Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?
Neno hilo kama linavyotumika kwenye biblia..linamaanisha aidha mojawapo ya mambo haya matatu:
Mithali 27:7
[7]Nafsi iliyoshiba hukinai sega la asali; Bali nafsi yenye njaa huona kila kitu kichungu kuwa kitamu.
Mithali 25:17
[17]Mguu wako usiingie katika nyumba ya jirani yako ila kwa kiasi; Asije akakukinai na kukuchukia.
Mhubiri 1:8
[8]Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.
Kumbukumbu la Torati 17:12
[12]Na mtu afanyaye kwa kujikinai, kwa kutomsikiza kuhani asimamaye hapo kwa kumtumikia BWANA, Mungu wako, au mwamuzi, na afe mtu huyo; nawe utauondoa uovu katika Israeli.
Soma pia.. Kutoka 21:14
Luka 18:9-14
[9]Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.
[10]Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.
[11]Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.
[12]Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.
[13]Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.
[14]Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.
Soma pia 2Petro 2:11,
Hivyo na sisi hatupaswi kuwa na sifa hizo mioyoni mwetu. Uendapo mbele za Bwana, Acha kujihesabia haki, Bali jinyenyekeze penda kuomba rehema Kwa Bwana, zaidi ya kueleza sifa zako..na hatimaye Mungu atakuridhia, kwasababu Mungu anawapinga wenye kiburi na kuwapa neema.wanyenyekevu.
Amen
Je! Umeokoka? Ikiwa bado na unapenda Kristo akusamehe dhambi zako zote, na akupe uzima wa milele. Basi fungua hapa ili uweze kupata mwongozo sala ya toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?
Mawaa ni nini? Kama tunavyosoma katika biblia?
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
“Romans road to salvation”
Njia ya wokovu ndani ya kitabu Cha Warumi ni Nini?
Ni mpango wa wokovu wa mwanadamu, ambao umeainishwa vyema kutoka katika kitabu Cha Warumi.
Kitabu hichi kinaeleza jinsi mtu anavyoweza kuupokea wokovu kutoka Kwa Mungu.
Hivyo ikiwa wewe bado hujaufahamu mpango wa Mungu kwako, wa namna ya kuupokea wokovu basi kitabu hichi kimeanisha vifungu ambavyo vinakuonesha ni jinsi gani utaweza kuupokea.
Lakini pia ikiwa wewe hujui ni wapi pa kuanzia unapokwenda kuwashuhudia watu habari za wokovu, basi kitabu hichi kinakupa mwongozo wa namna ya kuwahubiria wengine habari njema. Na vifungu muhimu vya kusimamia..
Hivi ni vifungu “mama”
Warumi 3:23
[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
Tuendapo Kwa Mungu, lazima tujue hakuna mwenye haki hata mmoja sote Tumepungukiwa na utukufu wa Mungu. Tumetenda dhambi, Vilevile ikiwa wewe ni mhubiri/mshuhudiaji, huna budi kumuhubiria mtu jambo hilo, kwamba hakujawahi kutokea mwema hapa duniani. Hivyo wote tunauhitaji mpango wa Mungu wa wokovu katika maisha yetu.
[23]Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Hapa, Mungu anatuonesha, matokeo ya kudumu katika dhambi zetu, ambazo wote tulikuwa nazo, kuwa ikiwa tutaendelea kubaki katika Hali hiyo hiyo basi tutakutana na mauti ya milele, lakini tukipokea zawadi ya Mungu basi tutapata uzima wa milele.
[8]Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.
Kwamba sasa hiyo zawadi ya Mungu ambayo itapelekea uzima wa milele ni Yesu Kristo, yeye ndiye aliyetolewa na Mungu kuzichukua dhambi zetu zote, kwa kifo cha pale msalabani. Pale tuliposhindwa sisi wenyewe basi Yesu alikuja kutusaidia kuchukua makosa yetu.
Hiki sasa kinaeleza Namna ya kuupokea wokovu;
Warumi 10:9-10
[9]Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.
[10]Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
Kwa kuamini kwetu kuwa Yesu Yu hai, na kwamba anakomboa wanadamu, na vilevile kumkiri Kwa kinywa kuwa ndiye Bwana na mwokozi wetu. Basi tunaupokea msamaha huo wa dhambi Bure, bila gharama yoyote. Na deni letu la dhambi linakuwa limefutwa tangu huo wakati
Hivyo ni sharti ujue kuwa msamaha wa dhambi hauji Kwa matendo Yako mema, Bali unakuja Kwa kuikubali kazi ya Yesu msalabani iliyofanyika Kwa ajili ya ukombozi wako.
Halikadhalika Wewe kama mshuhudiaji vifungu hivi viwepo kichwani mwako.
[1]Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Maana yake ni kuwa baada ya mtu kumkiri Kristo, na kumkubali kama Bwana na mwokozi wake. Basi anapaswa awe na AMANI na Mungu kwasababu hakuna mashtaka yoyote ya adhabu juu yako. Hakuna hukumu yoyote ya mauti ipo juu yake.
Huo ndipo mpango wa awali wa wokovu wa Mungu Kwa mwanadamu. Ambapo tunapaswa kufahamu kama ulivyoanishwa katika kitabu hichi Cha Warumi.
Kisha baada ya hapo tunawafundisha watu kuitimiza haki yote au kusudi lote la Mungu juu yetu, Ikiwemo ubatizo wa maji, na ule wa Roho Mtakatifu.
Ikiwa bado hujaokoka, na utapenda kuupokea msamaha wa Yesu Bure maishani mwako, basi Unaweza kuwasiliana na sisi Kwa namba uzionazo chini ya chapisho hili kwa ajili ya mwongozo huo Bure. Vilevile na Ule wa ubatizo.
Bwana akubariki.
Shalom
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)
TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!
Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.
Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?
Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?
Swali: Katika Mathayo 14:5 tunasoma kuwa Herode alitaka kumwua Yohana mbatizaji, lakini tukirudi katika Marko 6:20 tunasoma habari nyingine tofauti kuwa Herode hakutaka kumwua Yohana mbatizaji, badala yake alimweshimu na kumwogopa na kumwona kama Nabii..je ni habari ipi iliyo sahihi kati ya hizo mbili?
Jibu: Awali ya yote tusome mistari hiyo..
Mathayo 14:3 “Maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga, akamtia gerezani, kwa ajili ya Herodia, mke wa Filipo nduguye.
4 Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye.
5 NAYE ALIPOTAKA KUMWUA, ALIWAOGOPA WATU, MAANA WALIMWONA YOHANA KUWA NABII.”
Hapa ni kweli tunasoma kuwa Herode alikusudia kumwua Yohana.. Lakini tusome tena Marko 6:17-20
Marko 6:17 “Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu, akamkamata Yohana, akamfunga gerezani, kwa ajili ya Herodia, mkewe Filipo ndugu yake, kwa kuwa amemwoa;
18 kwa sababu Yohana alimwambia Herode, Si halali kwako kuwa na mke wa nduguyo.
19 Naye yule Herodia akawa akimvizia, akataka kumwua, asipate.
20 MAANA HERODE ALIMWOGOPA YOHANA; AKIMJUA KUWA NI MTU WA HAKI, MTAKATIFU, AKAMLINDA; NA ALIPOKWISHA KUMSIKILIZA ALIFADHAIKA SANA; NAYE ALIKUWA AKIMSIKILIZA KWA FURAHA.”
Hapa tunasoma Herode hakutaka kumwua Yohana, kwasababu alimwogopa na kuamini kuwa ni mtu wa haki. Sasa swali je! Habari hizi mbili zinajichanganya?
Jibu ni La! Hazijichanganyi!!, kwasababu waandishi wa vitabu hivyo walivuviwa na Roho Mtakatifu na pia biblia kamwe haijawahi kujichanganya, vinginevyo ingekuwa ni kitabu cha uongo!, lakini tunaona ni kitabu chenye nguvu na kilichojaa mafunuo yaliyo halisi, hivyo kinachojichanganya ni fahamu zetu na tafakari zetu katika kuyaelewa maandiko na si biblia.
Sasa tukirudi katika hiyo habari ya Herode, tukianzia mistari ya juu katika vitabu vyote viwili, tunasoma Mfalme Herode (Antipa) alisikia habari za Yohana Mbatizaji na mahubiri yake, na Yohana katika kuhubiri kwake alimtaja Herode na kumwambia si halali yeye kuwa na mke wa ndugu yake (Mathayo 14:3-4).
Lakini kwasababu Herode ni mtu wa heshima, na asingetaka masuala yake ya kindoa yachafuliwe hadharani tena na mtu aliye myahudi, alitafuta njia ya kumwua Yohana Mbatizaji, lakini alikosa kwasababu muda wote Yohana alikuwa akizungukwa na watu, (Mathayo 14:5) na wayahudi wote walimwamini Yohana kama nabii wa Mungu, hivyo laiti kama Herode angechukua maamuzi ya haraka ya kumwua Yohana mbele ya umma ingekuwa ni hatari kwa ufalme wake, kama tu jinsi mafarisayo walivyoogopa kumkosoa Yohana mbele ya umati, kwa hofu ya kupigwa mawe (Luka 20:6), au kama jinsi wakuu wa makuhani walivyoogopa kumkamata Bwana Yesu wamwue, kwaajili ya makutano (Luka 22:2).
Hivyo njia aliyotumia Herode ni kumkata Yohana na kumfunga gerezani, ikiwa nia yake ni kumtenga na makutano na mwisho aweze kufanikisha nia yake ya kumwua. Na wakati huo huo mkewe Herodia, alikuwa akimsapoti Herode katika mpango huo.
Lakini tunavyozidi kuisoma habari hiyo tunaona Herode alikuja kubadilisha mawazo baadaye.. kwani baada ya kumtia Yohana mbatizaji gerezani, kuna vipindi ambavyo havijatajwa huenda Herode alikuwa anaenda gerezani kumsikiliza Yohana, au alikuwa analetewa mahubiri ya Yohana kutoka gerezani (kwasababu hata Yohana alivyokuwa gerezani bado wanafunzi wake walikuwa wanaweza kwenda kumtembelea na kumpelekea habari au yeye mwenyewe kuwatuma wapeleke habari, soma Luka 7:18-20).
Na hayo yakamfanya Herode abadili mtazamo na maamuzi, na kumwamini kuwa ni mtu wa Mungu, ijapokuwa anamweleza maneno ya kumchoma na kumkera (Soma Marko 6:20), hivyo akaamua kubadili mawazo na kufikiri kutomuua!.
Lakini mkewe Herodia akawa na wazo lile lile la kumuua, na Herode akawa anatafuta njia ya kumlinda Yohana asiuawe na Herodia (Marko 6:19). Wakiwa katika hayo mazingira, Herodia akapata nafasi siku ile ya sikuku ya kuzaliwa kwa Herode ambapo alimtumia binti yake kukitaka kichwa cha Yohana Mbatizaji, na kutokana na nadhiri Herode alizoziweka mbele ya binti yake na mbele ya umati wote wa watu, alishindwa kukataa..kwani ingeudhoofisha ufalme wake, hivyo akaruhusu Yohana akakatwe kichwa ingawa si kwa mapenzi yake!.
Mathayo 14:6 “Hata ilipofika sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti Herodia alicheza mbele ya watu, akampendeza Herode.
7 Hata akaahidi kwa kiapo ya kwamba atampa lo lote atakaloliomba.
8 Naye, huku akichochewa na mamaye, akasema, Nipe hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.
9 Naye mfalme akasikitika; lakini kwa ajili ya viapo vyake, na kwa ajili ya wale walioketi chakulani pamoja naye, akaamuru apewe;
10 akatuma mtu, akamkata kichwa Yohana mle gerezani”.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba… Herode alibadili mawazo yake juu ya Yohana, hivyo biblia haijichanganyi.
Lakini pia ni funzo gani tunalipata katika habari hii ya Herode na Herodia mke wa ndugu yake?
Funzo kuu tunalolipata ni kuwa si halali mtu kumwacha mke wake au mume wake na kwenda kuoa au kuolewa na mwingine.
Luka 16:18 “Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini”.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Je! habari ya muda aliotawala Mfalme Yekonia inajichanganya? (2Wafalme 24:8 na 2Nyakati 36:9).
Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.
Yohana mbatizaji alibatizwa na nani?
Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?
Biblia inatufundisha kuwa Mazungumzo mabaya ndiyo yanayoharibu tabia njema ya mtu.
1Wakorintho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema”.
Maandalizi ya dhambi karibia zote yanaanzia katika “mazungumzo”.. wanaopanga kuua wanaanzia na mazungumzo, wanaopanga kuiba wanaanzia katika mazungumzo, hali kadhalika wanaopanga kufanya zinaa na uasherati wanaanza na mazungumzo.
Kwahiyo kama mtu wa Mungu jiangalie sana aina ya mazungumzo yako hali kadhalika na mtu unayezungumza naye.
Yusufu alijua siri ya mazungumzo na hiyo ikamsaidia kushinda dhambi ya “zinaa”. Kwani maandiko yanasema Yusufu hakukubali kulala na mke wa Potifa na hata KUZUNGUMZA NAYE!
Mwanzo 39:7 “Ikawa baada ya mambo hayo, mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia, Lala nami.
8 Lakini akakataa, akamwambia mke wa bwana wake, Tazama, bwana wangu hajui kitu kilichowekwa kwangu nyumbani, na vyote alivyo navyo amevitia mkononi mwangu.
9 Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?
10 Akawa akizidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, WALA AONGEE NAYE”.
Wengi tunaishia hapo kuwa Yusufu alikataa kulala naye.. lakini biblia inatuonyesha kuwa alikataa pia KUONGEA NAYE..
Huu ni mtego ambao shetani anawanasa wengi katika siku hizi za mwisho, utakuta mtu anajisifia hawezi kuanguka, lakini ni mtu aliejaa mazungumzo na jinsia nyingine kwa kiwango kikubwa!, ni mtu wa mizaha na utani na wa maneno maneno…hawezi kukaa bila angalau kuanzisha mazungumzo yasiyo na maana na mwingine, hawezi kutulia asipochati na mtu mwingine..
Hapo ni ngumu kushinda dhambi ya zinaa, au dhambi nyingine yeyote… Kwasababu biblia imeshasema kuwa, mazungumzo mabaya ndiyo yanayoharibu tabia ya mtu! (1Wakorintho 15:33), haihitaji maelezo mengi!
Ni lazima tu utaharibikiwa tabia ukiwa ni mtu wa mazungumzo mazungumzo yasiyo na maana… hususani na watu ambao bado hawajamjua Mungu.. na watu wa jinsia nyingine.
Chunga mdomo wako, kama unaipenda tabia yako!
Maran atha
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
MAZUNGUMZO MABAYA HUHARIBU TABIA NJEMA.
JIHUDHURISHE, ILI AANZISHE MAZUNGUMZO NA WEWE
ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.
AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE
Amri za kwanza Mungu aliziandika juu ya mawe aliyoyachonga yeye mwenyewe, lakini mawe yale ambayo juu yake amri 10 yalivunjwa vunjwa na Musa wakati ule ule aliposhuka kutoka mlimani…
Kutoka 31: 18 “Hapo Bwana alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa chanda cha Mungu”
Baadaye Mungu akamwambia Musa achonge, mbao nyingine mbili za mawe mfano wa zile za kwanza zilizochongwa na Mungu mwenyewe..Na Musa alipochonga aliwapa wana wa Israeli…
Kutoka 34:1 “Kisha Bwana akamwambia Musa, Chonga mbao mbili za mawe mfano wa zile za kwanza; nami nitaandika juu ya mbao hizo maneno hayo yaliyokuwa juu ya mbao za kwanza, hizo ulizozivunja”.
Mbao hizi za pili nazo hazikudumu muda mrefu, kwamaana alipokuja Mfalme Nebukadreza alivunja sanduku na kuzipoteza kabisa,.na kukawa hakuna tena sanduku la ushuhuda ambalo ndani yake mna mbao hizo za mawe zilizobeba Amri za Mungu.
Lakini baada ya miaka Mingi kupita Bwana Mungu akarudia tena kuziandika amri hizo kwa mara nyingine ya mwisho, lakini safari hii si katika mwamba aliouchonga yeye kwa vidole vyake, wala si katika mwamba uliochongwa na Musa, BALI KATIKA MOYO WA MTU.
Yeremia 31:31 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; NITATIA SHERIA YANGU NDANI YAO, NA KATIKA MIOYO YAO NITAIANDIKA; NAMI NITAKUWA MUNGU WAO, NAO WATAKUWA WATU WANGU.
34 Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena”.
Umeona? Kumbe agano jipya linahusu Moyo!.. Maana yake hatuhitaji tena kwenda Yerusalemu kuzisikia amri, wala sharia wala maagizo ya Mungu, bali tunapomwamini Yesu zile sharia zinaandikwa ndani yetu na kidole cha Mungu mwenyewe.
Na matokeo ya sharia, na amri za Mungu kuandikwa ndani ya mioyo yetu, maana yake muda wote zitakuwa zinabubujika na hivyo hakuna haja ya mtu kukufundisha kuzishika amri, zenyewe tu zitakuwa zinabubujika ndani yako.. kama maandiko yanavyosema hapo katika mstari wa 34…. “Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana”.
Hiyo ndio sababu kwanini watu waliompokea Yesu kikweli kweli na kujazwa na Roho wake Mtakatifu, haihitaji kuwaambia wala kuwakazania kuwa ulevi ni dhambi, au uvaaji mbaya ni dhambi.. Tayari sheria ipo ndani yao, hata pasipo kuambiwa na mchungaji,… ndani ya mioyo tayari kuna mahubiri yaliyoandikwa na kidole cha Mungu mwenyewe yanayowaambia kuwa si sawa kufanya baadhi ya mambo. Hayo mahubiri haihitaji wasafiri mbali kwenda kuyatafuta, tayari yanakuwa yameandikwa ndani yao, haihitaji kuwakumbusha kusali, tayari hayo mahubiri yapo ndani yao, haihitaji kuwakumbusha kwenda ibadani, tayari hayo maagizo Bwana kayaandika ndani yao, hivyo daima yanabubujika.
Kumbukumbu 30:11 “Kwa maana maagizo haya nikuagizayo leo, si mazito mno kwako, wala si mbali.
12 Si mbinguni, hata useme, Ni nani atakayetupandia mbinguni akatuletee, aje atuambie tusikie, tupate kuyafanya?
13 Wala si ng’ambo ya pili ya bahari, hata useme, Ni nani atakayetuvukia bahari, akatuletee, aje atuambie, tusikie, tupate kuyafanya?
14 Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na MOYO WAKO, upate kulifanya”
Lakini maandiko hayo hayawezi kuandikwa ndani ya moyo wa mtu, kama mtu huyo hajafungua moyo wake kwa kumwamini Yesu na kumkiri kwa kinywa, vile vile kwa kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, pamoja na kubatizwa, kwa maana maandiko yanasema hivyo..
Warumi 10:6 “Bali ile haki ipatikanayo kwa imani yanena hivi, Usiseme moyoni mwako, Ni nani atakayepanda kwenda mbinguni? (Yaani, ni kumleta Kristo chini),
7 au, Ni nani atakayeshuka kwenda kuzimuni? (Yaani, ni kumleta Kristo juu, kutoka kwa wafu.)
8 Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo.
9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.
10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.
Je sheria za Mungu zimeandikwa ndani yako??
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?
Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?
TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.
Mawaa ni nini? Mawaa ni dosari au kasoro iliyo katika kitu, ambayo inapelekea kukifanya kitu hicho kisifae tena, au kikose vigezo.
Kwamfano mtu ambaye ana sifa ya kuwa na uso mzuri halafu, kukatokea jipu shavuni. hapo ni sawa na kusema ana-mawaa. Jipu lile limeuharibu uzuri wake.
Au ukinunua bati la kuwekeza kwenye nyumba yako, halafu ukaona tobo katikati ya bati hilo, tayari lina mawaa, halifai kwa ujenzi. Au shati jeupe halafu likawa na doa dogo jeusi, huo ni mfano wa mawaa, halifai kwa kuvalika.
Vilevile rohoni na sisi pia hatupaswi kuonekana na mawaa ya aina yoyote, Kwamfano katika vifungu hivi; Mungu anatarajia kanisa lake alilolikomboa kutoka katika dhambi lisionekane na mawaa (dosari yoyote) ndani yake
Wakolosai 1:21 “Na ninyi, mliokuwa hapo kwanza mmefarikishwa, tena adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha sasa; 22 katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele zake, watakatifu, wasio na mawaa wala lawama”
Hivyo wewe kama mkristo uliyeokoka, ni lazima ujue kuwa una wajibu wa kuishi maisha ya utakatifu na ukamilifu, usiseme nimeokolewa kwa neema Yesu alishayamaliza yote, Hivyo unaenda kama utakakavyo, anaitenda kazi ya Mungu huku unaishi na mke/mume ambaye si wako. Wewe una mawaa, na hivyo mbingu huwezi kuiona.
Au unatoa zaka, unaimba kwaya, ni kiongozi wa vijana, na huku unatazama picha za ngono mtandaoni, hapo una-mawaa, Unafunga na kusali, unadumu hekaluni usiku na mchana na huku unakula rushwa kazini kwako. Hapo ndugu una-mawaa.
Hivyo hatuna budi kuwa kanisa la Kristo kwelikweli Bwana analolitazamia lisilo na mawaa wala lawama, wala kunyanzi. Ndivyo tutakavyopokewa kuingia katika uzima wa milele.
Neno hilo utalipata katika vifungu hivi
1Timotheo 6:13 “Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato, 14 kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo”.
Yohana 1:27 “Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa”.
Soma pia
Waebrania 9:14, 2Petro 2:13
Bwana akubariki.
Je! Umeokoka, kama la! Ni nini unachosubiria mpaka sasa, una habari kuwa parapanda inakaribia kulia, Yesu anarudi? Dalili zote zimeshatimia? Fikiri akikukuta katika hali hiyo utamweleza nini? Angali ukweli umeshaujua? Embu tubu leo dhambi zako, mgeukie Kristo, azioshe, akupe uzima wa milele bure.
Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo akupe uzima wa milele bure, basi fungua hapa ili uweze kupata mwongozo wa sala hiyo. >>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).
TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.
FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
Katika maandiko hakuna vifungu vya Moja Kwa Moja vinavyorekodi tukio la Bwana Yesu kunena Kwa lugha.
Lakini Kwa ufahamu wa Rohoni tuliopewa twajua kuwa ni wazi Yesu alinena Kwa lugha. Kutokurekodiwa Kwa tukio hilo hakumaanishi kuwa hakuwahi kunena Kwa lugha, kwasababu maandiko yanasema yapo mambo mengi aliyoyafanya Yesu kama yangeandikwa hata vitabu vyote duniani visingeweza kutosha, Kwa wingi wa habari zake.(Yohana 21:25)
Hivyo si Kila tukio la Bwana Yesu limeandikwa kwenye biblia.
Halikadhalika Ifahamike kuwa taaarifa za kunena Kwa lugha aliyezieleza kwa mara ya kwanza Kwa mitume ni Bwana Yesu.(Hawakufunuliwa baadaye) Hivyo hawezi kuwaambia watu jambo ambalo yeye mwenyewe halipo ndani yake, au hajawahi kulifanya.
Marko 16:17-18
[17]Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
[18]watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
Vilevile Yesu ndiye mwanadamu pekee aliyetiwa mafuta mengi na Roho kuliko mtu yeyote aliyewahi kutokea duniani, (Waebrania 1:9). Zile karama zote za Roho zilikuwepo ndani yake, alikuwa ni nabii, mwalimu, mwinjilisti, mchungaji, mtume, n.k. na karama za uponyaji, miujiza, upambanuzi alikuwa nazo, hivyo hatuwezi kushangaa pia na hii kunena Kwa lugha kuwemo ndani yake.
Kwa kuhitimisha ni wazi kuwa Bwana Yesu alinena Kwa lugha. Hivyo akampendeza kukimwaga kipawa hicho na kwetu pia.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
IJUE FAIDA YA KUNENA KWA LUGHA MPYA!
YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.