Rehani ni nini kibiblia?, na je sisi wakristo tunaruhusiwa kuweka kitu rehani?
Rehani ni mali iliyowekwa kama dhamana kwa mkopo uliochukuliwa, maana yake mkopo usipolipwa basi mali ile inachukuliwa ili kufidia ule mkopo.
Katika biblia (Agano la kale), Rehani iliruhusiwa lakini kwa kuiangalia hali ya mtu. Kama mtu alikuwa ni tajiri mwenye uwezo basi alipokopa alipaswa aweke rehani mali itakayosimama badala ya ule mkopo endapo atashindwa kuulipa.
Lakini kama mtu alikuwa ni maskini sana, na hana kitu isipokuwa jiwe la kusagia tu na mavazi, basi hakupaswa kutozwa rehani katika hivyo alivyo navyo, ilikuwa ni dhambi kubwa kutwaa jiwe la kusagia la maskini au mavazi yake kama Rehani.
Kumbukumbu 28: 6 “Mtu awaye yote asitwae jiwe la kusagia, la juu wala la chini, kuwa rehani; kwani hivi ni kutwaa maisha ya mtu kuwa rehani”.
Kumbukumbu 24:17 “Usipotoshe hukumu ya mgeni, wala ya yatima; wala usitwae mavazi ya mjane, yawe rehani;
18 bali kumbuka ya kuwa ulikuwa mtumwa katika Misri, Bwana, Mungu wako, akakukomboa huko; kwa hiyo nakuamuru kutenda neno hili”.
Kwa urefu kwanini si sawa kutwaa jiwe la kusagia la maskini kama rehani waweza kufungua hapa >>>Kwanini jiwe la kusagia Mungu alikataza lisiwekwe rehani? (Kumbukumbu 24:6).
Sasa swali je na sisi wakristo ni sahihi kuweka kitu rehani au kupokea rehani kutoka kwa mtu tuliyemkopesha?
Jibu: Rehani haijakatazwa katika biblia, kama umemkopesha mtu kitu cha thamani, na mtu huyo si ndugu yako katika Imani (yaani mpendwa mwenzako) au si ndugu yako katika mwili (yaani mwanafamilia) waweza kupokea Rehani, ili kumhamasisha kurejesha lile deni, (ikiwa lengo lako si kumkandamiza bali kumhamasisha na kama mtu huyo uwezo huo anao).
Lakini kama ni maskini na kaja kukopa kwako, si vizuri kuchukua rehani. Waweza kumkopa bila rehani yoyote, ni itakuwa baraka kwako.
Lakini kama ni ndugu yako katika Imani na katika damu, si vyema kumtoza rehani, wala riba, katika mazingira yoyote yale, awe tajiri au maskini, waweza kumkopa ukitumai kuwa atakulipa tu pasipo kutaka dhamana.
Lakini pia kama wewe ni mkopaji, (maana yake unakopa kutoka kwa mtu/taasisi kwaajili ya shughuli fulani) si dhambi kusimamisha kitu kama rehani itakayosimama kwaajili ya mkopo wako (kama mtu huyo au taasisi hiyo inahitaji hayo yote).
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
“Humfukuza punda wake asiye baba”, nini maana ya mstari huu? (Ayubu 24:3)
Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)
TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.
Rudi nyumbani
Rahabu ni nani?
Jina “Rahabu” limeonekana mara kadhaa katika biblia likiwa na maana Zaidi ya moja. Maana ya kwanza ni linamwakilisha Mwanamke wa kikanaani aliyekuwa kahaba, aliyewahifadhi wapelelezi wa kiisraeli walioingia kuipeleleza Yeriko, na maana ya pili Taifa la Misri.
Kama tu vile neno “Mharabu” katika biblia linamaanisha Jamii ya watu wa Arabia, lakini pia linamaanisha “Mtu au Malaika anayeharibu Vivyo hivyo na jina Rahabu lina maana Zaidi ya moja.
1.RAHABU (Kahaba).
Habari ya Rahabu aliywakuwa kahaba tunaipata katika kitabu cha Yoshua mlango wa 2 na wa 6. Mwanamke huyu aliwahifadhi wapelelezi wa kiisraeli walioingia Yeriko kuipeleleza nchi ile.
Yoshua 2:1 “Yoshua, mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kutoka Shitimu kwa siri, ili kupeleleza, akawaambia, Enendeni mkaitazame nchi hii, na Yeriko. Wakaenda wakafika nyumbani kwa kahaba mmoja jina lake aliitwa Rahabu, wakalala huko.
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, kusema, Tazama, watu wawili wa wana wa Israeli wameingia humu leo usiku, ili kuipeleleza nchi.
3 Mfalme wa Yeriko akatuma watu kwa Rahabu, akasema, Watoe watu wale waliokuja kwako, walioingia ndani ya nyumba yako, maana wamekuja ili kuipeleleza nchi.
4 Yule mwanamke akawatwaa wale watu wawili, akawaficha, akasema, Naam, wale watu walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka”
2.TAIFA LA MISRI.
Jina Rahabu pia katika biblia limetumika kuwakilisha Joka kubwa la baharini ambalo ufunuo wake ni Taifa la Misri.
Isaya 30:7 “Kwa maana Misri huwasaidia bure, bila faida; Kwa hiyo nimemwita, Rahabu aketiye kimya”
Isaya 51:10 “Si wewe uliyemkata-kata Rahabu? Uliyemchoma yule joka? Si wewe uliyeikausha bahari, Na maji ya vilindi vikuu; Uliyevifanya vilindi kuwa njia, Ili wapite watu waliokombolewa?”
Zaburi 87: 4 “Nitataja Rahabu na Babeli Miongoni mwao wanaonijua. Tazama Filisti, na Tiro, na Kushi; Huyu alizaliwa humo”
Soma pia Ayubu 26:12, na Zaburi 89:10..
Jambo kubwa na kuu tunaloweza kujifunza kwa RAHABU (Aliyekuwa Kahaba) ni IMANI.
Alikuwa na Imani juu ya mambo yatarajiwayo sawasawa na Waebrani 11:1. Aliziamini nguvu za MUNGU wa Israeli, hivyo akajua yatakayofuata baadaye kuwa ni anguko la Yeriko, hivyo akatafuta njia ya kujinusuru yeye na familia yake kwa kujiungamanisha na jamii ya Israeli.
Waebrania 11:31 “Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani”.
Yakobo 2:25 “Vivyo hivyo na Rahabu, yule kahaba naye, je! Hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipowakaribisha wajumbe, akawatoa nje kwa njia nyingine?
26 Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa”.
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.
Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)
Machukizo au Chukizo ni nini? kama tunavyosoma katika biblia?
Machukizo linatokana na neno “chukizo” na chukizo ni kitu kinachosababisha chuki/hasira. Kwa Mungu kitu chochote kinachoipandisha ghadhabu yake kinaitwa “chukizo”.
Na vitu vifuatavyo ndivyo vilivyokuwa machukizo kwa MUNGU.
1. Ibada ya Sanamu.
Sanamu ya aina yoyote ile ilikuwa ni machukizo kwa Mungu na hicho ndicho kitu cha kwanza kilichokuwa kinaletea wivu kwa Mungu.
Kumbukumbu 27:15 “Na alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. Na watu wote wajibu, waseme, Amina”.
Kumbukumbu 32:16 “Wakamtia wivu kwa miungu migeni, Wakamkasirisha kwa machukizo.
17 Walitoa sadaka kwa pepo, si Mungu, Kwa miungu wasiyoijua, Kwa miungu mipya iliyotokea siku zilizo karibu, Ambayo baba zenu hawakuiogopa”.
Soma pia Kumbukumbu 27:15, na 2Wafalme 23:24
2. Uasherati na ulawiti.
Walawi 18: 22 “Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo”.
Soma tena Mambo ya Walawi 20:13
3. Mavazi yasiyopasa.
Kumbukumbu 22:5 “Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”
Mfano wa mavazi yasiyopasa, ni suruali kwa mwanamke, na nguo mfano wa magauni kwa wanaume.
4. Sadaka yenye kasoro.
Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.
Kumbukumbu 17:1 “Usimchinjie Bwana, Mungu wako, ng’ombe wala kondoo aliye na kilema, wala neno ovu lo lote; kwa kuwa hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”.
Na yapo machukizo mengine mengi!.
Lakini pia lipo chukizo moja KUU na KUBWA ambalo litatokea kule YERUSALEMU, ambalo ni CHUKIZO LA UHARIBIFU, linalomhusu Mpinga-kristo.
Kwa upana juu ya CHUKIZO LA UHARIBIFU, basi fungua hapa >>CHUKIZO LA UHARIBIFU
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.
Kemoshi ni nani? (Yeremia 48:46)
Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?
Swali: Huyu Kemoshi alikuwa nani, na nini tunajifunza kutoka kwake?
Jibu: Turejee,
Yeremia 48:46 “Ole wako! Ee Moabu, Watu wa Kemoshi wamepotea; Maana wana wako wamechukuliwa mateka, Na binti zako wamekwenda utumwani”.
“kemoshi” hakuwa mtu bali alikuwa ni “mungu” wa watu wa Moabu. Kumbuka kila taifa lilikuwa na mungu wake; Israeli walikuwa na MUNGU wao ambaye ni YEHOVA, Muumba wa mbingu na nchi, Tiro walikuwa na mungu wao anayeitwa “baali”, Sidoni walikuwa na mungu wao anayeitwa “ashtoreti”, wana wa Amoni walikuwa na mungu wao anayeitwa “milkomu”. N.k na hawa wana wa Moabu mungu wao ndio anayekuwa anaitwa “kemoshi” ambaye kiuhalisia ni “pepo”.
Sasa utaona Mungu aliwakataza wana wa Israeli wasiabudu miungu mingine tofauti na yeye…lakini wapo waliotii na wapo waliokaidi na kuamua kuifuata miungu hiyo ya mataifa mengine na kuiabudu na kuisujudia. Na Mfalme Sulemani alikuwa miongoni mwa waliokengeuka dakika za mwisho kwa kuifuata miungu hiyo ya mataifa, ingawa baadaye alikuja kutubu.
2Wafalme 23:13 “Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, MFALME WA ISRAELI, KWA ASHTORETHI, CHUKIZO LA WASIDONI, NA KEMOSHI, CHUKIZO LA MOABU, NA MILKOMU, CHUKIZO LA WANA WA AMONI, mfalme akapanajisi”.
Hii miungu hata leo inaabudiwa katika sehemu mbalimbali ikiwemo Africa, isipokuwa katika majina mengine tofauti na hayo.
Mila nyingi za kiafrica asili yake ni miungu hii, kwamfano mungu wa wasidoni aliyeitwa Ashtorethi alikuwa ni mtu wenye kuchongwa maumbile ya mtu, na kusujudiwa, na kufanyiwa matambiko..na sasa jamii nyingi na makabila mengi (ikiwemo na wakristo) wanafanya hayo hayo wanapokutanika katika vijiji vyao, pasipo kujua kuwa ni ibada za sanamu kama zile zile tu ambazo mataifa wasiomjua Mungu walikuwa wanazifanya.
Bwana atusaidie tuepukane na ibada hizo za sanamu.
Mistari mingine inayomtaja huyo mungu “kemoshi” ni pamoja na Hesabu 21:9, Waamuzi 11:24, 1Wafalme 11:7, 1Wafalme 11:33, Yeremia 48:7, na Yeremia 48:13.
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Antiokia ipo nchi gani kwa sasa? Na nini tunaweza kujifunza kupitia mji huo?
Jibu: Antiokia ni mji uliopo kusini mwa Taifa la UTURUKI na Kaskazini mwa Taifa la SIRIA.
Mji huu una historia kubwa sana ya kanisa, kwani ndicho kitovu cha jina “Ukristo”. Maandiko yanasema Wanafunzi (yaani watu waliomwamini YESU na kumfuata) waliitwa “wakristo” kwanza hapo Antiokia na si Yerusalemu kanisa lilipoanzia.
Matendo 11:26 “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. NA WANAFUNZI WALIITWA WAKRISTO KWANZA HAPO ANTIOKIA.
27 Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia”.
Antiokia ni mji uliomiminiwa uliokuwa na Neema ya Ukristo kuliko miji mingi, lililojaa Mitume, manabii na waalimu.. kwani hata Mtume Paulo safari yake ya kuanza kuhubiri injili ilianzia pale.
Matendo 13:1 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli.
2 Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.
3 Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.
4 Basi watu hao, wakiisha kupelekwa na Roho Mtakatifu wakatelemkia Seleukia, na kutoka huko wakasafiri baharini hata Kipro”.
Matendo 14:26 “Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza”.
Mji wa Antiokia kwasasa umejaa wa Islamu kutokana na Taifa hilo la Uturuki kuwa la kiislamu, ingawa kuna asilimia ndogo ya wakristo wanaoishi humo. Mahali ambapo uamsho mkubwa wa injili ulianzia sasa adui kapateka na kupafanya kuwa mji wa kipagani… Na miji mingine imenyanyuka yenye uamsho kuliko huo, sawasawa na Neno lile..
Marko 10:31 “Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho; na wa mwisho watakuwa wa kwanza”
Hivyo hiyo ni tahadhari hata kwetu, “Tushike tulicho nacho, mpaka mwisho adui asije akatupokonya taji yetu”.
Mji wa Antiokia mwaka 2023, Februari 6 kulitokea tetemeko kubwa sana lililoua watu elfu 55, na kuharibu makazi mengi sana.
Bwana atusaidie tuwe na mwisho mwema.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Masomo maalumu yahusuyo (Wanawake na mabinti).
Alamothi ni nini? Na nini ufunuo wake? (1Nyakati 15:20)
Jibu: Tusome,
1Nyakati 15:19 “Hivyo hao waimbaji, Hemani, Asafu, na Ethani, wakaagizwa kupiga matoazi yao ya shaba kwa sauti kuu;
20 na Zekaria, na Yaasieli na Shemiramothi, na Yehieli, na Uni, na Eliabu, na Maaseya, na Benaya, wenye vinanda vya SAUTI YA ALAMOTHI”
“Alamothi” maana yake ni “wanawake vijana”… Hivyo hapo anaposema vinanda vya sauti ya Alamothi, maana yake ni vinanda vya sauti za “wanawake vijana”.
Hiki ni kipindi ambacho Mfalme Daudi alikuwa analitoa sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumbani kwa Ben-edomu na kulipandisha Yerusalemu.
Na wakati wanalipandisha Daudi aliwaandaa wana wa Asafu (watu walio hodari wa kuimba) wenye matoazi pamoja na kundi lingine la watu nane (8) viongozi wa sifa, wenye vinanda vitakavyotoa sauti kuwafuatiliza wanawake vijana waimbaji (Alamothi).
Ni nini tunajifunza?
Kikubwa tunachoweza kujifunza ni jinsi “wanawake walivyo na nafasi kubwa katika kumwimbia Mungu”. Daudi aliona, wana wa Asafu pekee haitoshi (ambao ni wanaume) …..zinahitajika pia sauti za wanawake vijana, katika kumwimbia Mungu. Na utaona jambo hilo Mungu alilikubali sana na likawa Baraka sana kwa Mfalme Daudi.
Na Mungu ni yule yule hajabadilika, kama alizikubali sifa za Daudi na kundi lake, atafanya hivyo hata leo, ikiwa tutasimama vyema katika nafasi zetu.
Ikiwa wewe ni mwanamke au binti.. fahamu kuwa sauti yako ni ya thamani sana katika kumwimbia Mungu, (ndio maana si nzito kama ya mwanaume). Hivyo chukua nafasi hiyo katika kulitimiza kusudi la Mungu ndani yako. Tafuta namna yoyote umwimbie Mungu na Bwana atakubariki.
Zaburi ya 46 ambayo iliandikwa na wana wa Kora, ni Zaburi maalumu kwa ALAMOTHI. Ni nyimbo iliyokusudiwa iimbwe na Maalamothi, yenye kumtukuza Mungu kuhubiri uweza wake.
Zaburi 46:1 “Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.
3 Maji yake yajapovuma na kuumuka, Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.
4 Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu, Patakatifu pa maskani zake Aliye juu.
5 Mungu yu katikati yake hautatetemeshwa; Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 Mataifa yalighadhibika, falme zikataharuki; Alitoa sauti yake, nchi ikayeyuka.
7 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Njoni myatazame matendo ya Bwana, Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.
10 Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.
11 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu”
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?
Ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda.
TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.
Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza Naam, wanne walio na mwendo mzuri.
AGANO LA KALE
Vitabu vya Agano la Kale vimegawanyika katika makundi makuu manne (4)
1. VITABU VYA SHERIA. (Tazama jedwali chini).
JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA MILANGO/SURA | MAJIRA YA UANDISHI | |
---|---|---|---|---|
1. | MWANZO | MUSA | 50 | Jangwani |
2. | KUTOKA | MUSA | 40 | Jangwani |
3. | MAMBO YA WALAWI | MUSA | 27 | Jangwani |
4. | HESABU | MUSA | 36 | Jangwani |
5. | KUMBUKUMBU LA TORATI | MUSA | 34 | Jangwani |
2. VITABU VYA HISTORIA (Tazama Jedwali chini).
N/A | JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA MILANGO | MAHALI KILIPOANDIKIWA |
---|---|---|---|---|
1. | YOSHUA | Yoshua | 24 | Kaanani |
2. | WAAMUZI | Nabii Samweli | 21 | Israeli |
3. | RUTHU | Nabii Samweli | 4 | Israeli |
4. | 1SAMWELI | Nabii Samweli | 31 | Israeli |
5. | 2SAMWELI | Ezra (Mwandishi) | 24 | Israeli |
6. | 1WAFALME | Yeremia (Nabii) | 22 | Israeli |
7. | 2WAFALME | Yeremia (Nabii) | 25 | Israeli |
8. | 1NYAKATI | Ezra (Mwandishi) | 29 | Uajemi |
9. | 2NYAKATI | Ezra (Mwandishi) | 36 | Uajemi |
10. | EZRA | Ezra (Mwandishi) | 10 | Israeli |
11. | NEHEMIA | Nehemia | 13 | Israeli |
12. | ESTA | Mordekari | 10 | Shushani Ngomeni(Uajemi) |
3. VITABU VYA MASHAIRI (Tazama Jedwali chini).
N/A | JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA MILANGO | MAHALI KILIPOANDIKIWA |
---|---|---|---|---|
1. | AYUBU | Musa | 42 | Jangawani |
2. | ZABURI | Daudi, Sulemani, Wana wa Asafu,Ethani, Hemani, Musa, wana wa Kora na wengine wasiotambulika. | 150 | Israeli |
3. | MITHALI | Sulemani | 31 | Yerusalemu (Israeli) |
4. | MHUBIRI | Sulemani | 12 | Yerusalemu (Israeli) |
5. | WIMBO ULIO BORA | Sulemani | 8 | Yerusalemu (Israeli) |
4. VITABU VYA MANABII WAKUBWA (Tazama Jedwali chini).
N/A | JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA MILANGO | MAHALI KILIPOANDIKIWA |
---|---|---|---|---|
1. | ISAYA | Isaya (Nabii) | 66 | Israeli |
2. | YEREMIA | Yeremia (Nabii) | 52 | Israelil (Yerusalemu) |
3. | MAOMBOLEZO | Yeremia (Nabii) | 5 | Misri |
4. | EZEKIELI | Ezekieli (Nabii) | 48 | Babeli |
5. | DANIELI | Danieli (Nabii) | 12 | Babeli |
5. VITABU VYA MANABII WADOGO (Tazama jedwali chini).
N/A | JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA MILANGO | MAHALI KILIPOANDIKIWA |
---|---|---|---|---|
1. | HOSEA | Hosea (Nabii) | 14 | israeli |
2. | YOELI | Yoeli (Nabii) | 3 | israeli |
3. | AMOSI | Amosi (Nabii) | 9 | israeli |
4. | OBADIA | Obadia (Nabii) | 1 | israeli |
5. | YONA | Yona (Nabii) | 4 | israeli |
6. | MIKA | Mika (Nabii) | 7 | israeli |
7. | NAHUMU | Nahumu (Nabii) | 3 | israeli |
8. | HABAKUKI | Habakuki (Nabii) | 3 | israeli |
9. | SEFANIA | Sefania (Nabii) | 3 | israeli |
10. | HAGAI | Hagai (Nabii) | 2 | israeli |
11. | ZEKARIA | Zekaria (Nabii) | 14 | israeli |
12. | MALAKI | Malaki (Nabii) | 4 | israeli |
AGANO JIPYA
Vitabu vya Agano jipya vimegawanyika katika makundi makuu matano (5)
1. VITABU VYA INJILI (Tazama jedwali chini)
N/A | JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA MILANGO | MAHALI KILIPOANDIKIWA |
---|---|---|---|---|
1. | MATHAYO | Mathayo (Mtume) | 28 | Antiokia (Siria) |
2. | MARKO | Marko (Mwanafunzi) | 16 | Rumi au Siria |
3. | LUKA | Luka (Mwanafunzi na, Tabibu) | 24 | Antiokia (Siria) |
4. | YOHANA | Yohana(Mtume, mwana wa Zebedayo) | 21 | Efeso (Uturuki) |
2. KITABU CHA HISTORIA (Tazama jedwali chini)
N/A | JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA MILANGO | MAHALI KILIPOANDIKIWA |
---|---|---|---|---|
1. | Matendo ya Mitume | Luka (Mwanafunzi na Tabibu) | 28 | Rumi |
3. VITABU VYA NYARAKA ZA PAULO MTUME (Tazama jedwali chini)
N/A | JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA SURA | MAHALI KILIPOANDIKWA |
---|---|---|---|---|
1. | WARUMI | Paulo (Mtume) | 16 | Korintho (Ugiriki) |
2. | 1WAKORINTHO | Paulo (Mtume) | 16 | Efeso (Uturuki) |
3. | 2WAKORINTHO | Paulo (Mtume) | 13 | Makedonia (Ugiriki) |
4. | WAGALATIA | Paulo (Mtume) | 6 | Efeso (Uturuki) |
5. | WAEFESO | Paulo (Mtume) | 6 | Gereza |
6. | WAFILIPI | Paulo (Mtume) | 4 | Gereza |
7. | WAKOLOSAI | Paulo (Mtume) | 4 | Gereza |
8. | 1WATHESALONIKE | Paulo (Mtume) | 5 | Korintho (Ugiriki) |
9. | 2WATHESALONIKE | Paulo (Mtume) | 3 | Korintho (Ugiriki) |
10. | 1TIMOTHEO | Paulo (Mtume) | 6 | Makedonia (Ugiriki) |
11. | 2TIMOTHEO | Paulo (Mtume) | 4 | Rumi (Kifungoni) |
12. | TITO | Paulo (Mtume) | 3 | Ugiriki |
13. | FILEMONI | Paulo (Mtume) | 1 | Rumi (kufungoni) |
14. | WAEBRANIA | inaaminika kuwa ni Paulo (Mtume) | 13 | Rumi |
4. VITABU VYA NYARAKA KWA WATU WOTE (Tazama jedwali chini)
N/A | JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA MILANGO | MAHALI KILIPOANDIKWA |
---|---|---|---|---|
1. | YAKOBO | Yakobo (Ndugu yake Bwana YESU) | 5 | Haijulikani |
2. | 1PETRO | Petro (Mtume) | 5 | Babeli |
3. | 2PETRO | Petro (Mtume) | 3 | Haijulikani |
4. | 1YOHANA | Yohana (Mtume) | 5 | Inaaminika Efeso |
5. | 2YOHANA | Yohana (Mtume) | 1 | Efeso |
6. | 3YOHANA | Yohana (Mtume) | 1 | Haijulikani lakini inasadikika Efeso |
7. | YUDA | Yuda (Ndugu yake Bwana YESU) | 1 | Haijulikani |
5. KITABU CHA UNABII (Tazama jedwali chini)
N/A | JINA LA KITABU | MWANDISHI | IDADI YA MILANGO | MAHALI KILIPOANDIKIWA |
---|---|---|---|---|
1. | UFUNUO WA YOHANA | Yohana (Mtume, mwana wa Zebedayo) | 22 | Patmo (kisiwani) |
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).
Swali: Je biblia inajichanganya katika Zaburi 8:4-5 na Waebrania 2:6-7. Maana sehemu moja inataja ‘Mungu’, na sehemu nyingine ‘Malaika’.
Jibu: Turejee.
Zaburi 8:4 “Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie?
5 Umemfanya mdogo punde KULIKO MUNGU; Umemvika taji ya utukufu na heshima”.
Tusome tena Waebrania 2:6-7..
Waebrania 2:6 “Mwanadamu ni nini hata umkumbuke, Ama mwana wa binadamu, hata umwangalie?
7 Umemfanya mdogo punde kuliko MALAIKA, Umemvika taji ya utukufu na heshima, Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako”.
Katika Waebrania mwandishi ana nukuu maneno kutoka katika Zaburi, lakini ni kama ana nukuu kitu tofauti na kilichoandikwa kule, kwamaana yeye anataja Malaika na wakati mwandishi wa Zaburi alitaja Mungu.. Sasa swali biblia inajichanganya?.
Jibu ni La! Biblia haijichanganyi wala haijakosewa.. Isipokuwa fahamu zetu na pambanuzi zetu ndizo zinazojichanganya.
Sasa ili tuelewe ni vizuri kuzielewa kwanza lugha za kibiblia..
Si kila mahali panapotajwa Mungu, panamaanisha Mungu-muumba, La! Sehemu nyingine panamaanisha Ufalme wa Mungu (yaani jeshi la Mbinguni yaani Malaika na vyote vilivyopo kule)…Na sehemu mojawapo ambayo iliyotajwa Mungu ikimaanisha Jeshi la Mbinguni ni hii Zaburi 8:5 “…Umemfanya mdogo punde KULIKO MUNGU”.
Mungu inayotajwa hapo inamaanisha Ufalme wa Mungu (yaani jeshi la Malaika) na si MUNGU aliye Muumbaji, ambaye ni MMOJA.
Ni sawa na jina ISRAELI katika biblia,…kuna mahali linamaanisha mtu mmoja (ambaye ni Yakobo mwana wa Isaka, Mwanzo 35:10).. Lakini pia jina hili kuna mahali linamaanisha TAIFA (Ufalme, Kutoka 5:2).
Au “Yuda”, kuna mahali anatajwa kama Mtu (Mwana wa Yakobo), lakini pia kama Taifa.
Vivyo hivyo na Mungu, cheo hicho kinaweza kufunua “Ufalme” au nafasi ya MUNGU MWENYEWE kama Muumba.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba mwandishi wa kitabu cha Waebrania hajapishana na mwandishi wa Zaburi.
Kujua kwa mapana ni ufunuo uliopo nyuma ya andiko hili.. “Amefanyika bora kuliko Malaika” basi fungua hapa >>>AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Ielewe kwa kina Waebrania 13:5 maana yake.
UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.
Mbaruti ni nini?.(Mibaruti ni mimea ya aina gani) na umebeba ujumbe gani kiroho?.
Jibu: Turejee,
Mathayo 7:16 “Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?”
Soma pia 2Wafalme 14:9, 2Nyakati 25:18 na Hosea 10:4.
Mbaruti/Mibaruti ni jamii ya mimea yenye maua, ambayo mara nyingi inajiotea maporini. (Mimea hii inatoa matunda ambayo ina miiba inayoizunguka pande zote, kuifanya kutolika na wanyama walao nyasi). Tazama picha juu..
Katika biblia Bwana YESU alinukuu mimea huu wa mbaruti katika swali lililowahusu manabii wa uongo.. Aliuliza je watu huchuma tini katika mibaruti?,.. Maana yake ni jambo lisilowezekana kupata matunda ya “Tini“ kutoka katika jamii ya mimea hiyo ya maua ya mibaruti.
Vile vile akasema haiwezekani kuchuma zabibu kutoka kwenye miti ya miiba…
Kuonyesha kuwa Manabii wa uongo wanatoa matunda yenye MIIBA MIIBA!!.yasiyofaa kwa kuliwa bali yanaumiza na kuchoma!.
Moja ya matunda wanayotoa ni tamaa za fedha, (wakizitamani na kuwafundisha watu hizo)..ambazo biblia inasema wanaozama huko wanajichoma kwa maumivu mengi..
1Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”.
Manabii wa uongo kamwe hawahubiri wala kufundisha Toba na Utakatifu, wala safari ya kwenda mbinguni hawaihubiri kwasababu huko hawaendi!.na wao si wasafiri wa kwenda huko, hivyo mioyo yao ipo hapa hapa duniani na wanahubiri vitu vya duniani, pasipo kuweka mambo katika uwiano.
Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?
17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni. 7.20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua”
Bwana atusaidie.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
NI SAHIHI KABISA, HUU SI WAKATI WA TINI!
SHAMBA HUWA HALIMTAMBUI WALA KUMSUBIRIA MKULIMA.
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?
Kwanini Bwana Yesu alivikwa taji ya miiba?
Mungu amejifunua katika Ofisi kuu 3, (Baba, Mwana na Roho Mtakatifu).
Lakini katika dhihirisho zote hizi tatu (3) Mungu anabaki kuwa mmoja na si watatu.
Sasa swali ni je kama ni mmoja kwanini ajifunua hivyo katika utatu?
Jibu rahisi ni kwamba, Mungu kajidhihirisha hivyo kwa lengo la kumkamilisha Mwanadamu na si kujitambulisha yeye. Na kwanini mwanadamu akamilishwe kupitia dhihirisho hizo tatu?..Ni kwasababu alikuwa amepotea na kujitenga mbali naye kwasababu ya dhambi.
(Dhambi zinatutenganisha sisi na Mungu) Kama maandiko yanavyosema…katika Isaya 59:2.
Mwanzo katika Edeni Mungu alikuwa karibu sana na MTU, aliweza kumwona, kumsikia, na hata kuzungumza naye (Mwanzo 3:8). Lakini baada ya dhambi kuingia ule ukaribu na Mungu ukapotea, Adamua akawa hawezi kumwona tena Mungu wala kumsikia kama alivyokuwa anamsikia mwanzo…Ile dhambi ikamtenga mbali na Mungu. (Isaya 59:2).
Na Mungu kwa upendo wake kwetu, akaanza mpango wa kuturejesha karibu naye tena. Tumwone tena, tuseme naye, tutembee naye na tumhisi ndani yetu kama mwanzo. Lakini matengenezo hayo si ya mara moja kama maharibifu. (kuharibu mahusiano ni mara moja, lakini kujenga inagharimu muda mrefu).
Na neno la ahadi ni kwamba siku moja MASKANI ya MUNGU itakuwa pamoja na wanadamu kuliko hata ilivyokuwa EDENI.
Ufunuo 21:3 “Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, NAYE ATAFANYA MASKANI YAKE PAMOJA NAO, NAO WATAKUWA WATU WAKE. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao”.
Sasa mahusiano hayo yaliyoharibika Mungu alianza kuyatengeneza hatua kwa hatua..na sasa tupo katika hatua ya mwisho wa matengenezo hayo.. Hebu tuzitazame hizo hatua moja baada ya nyingine.
1.MUNGU JUU YETU. (Kama Baba)
Hii ni hatua ambayo Mungu alianza kuongea na watu kwa njia ya Maono na Ndoto, lakini akawa haonekani. Na alisema na watu wachache tu walioitwa manabii. Huu ni wakati ambao MUNGU alijidhihirisha kama NENO tu!.. (Maana yake MANENO YAKE ndiyo yaliyokuwa yanafahamika tu lakini yeye mwenyewe haonekani kwa macho).
Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu”.
2. MUNGU PAMOJA NASI (Kama Mwana).
Huu ni wakati ambao Mungu aliuvaa mwili, ili yale MANENO aliyokuwa anasema na watu kwa njia ya maono na ndoto basi ayaseme kwa mdomo wa damu na Nyama na kuyafafanua na kuyafundisha ili watu wamwone na kumwelewa.. Na mwili ambao aliuvaa ndio ukaitwa YESU.
Yohana 1:14 “Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.
Umeona?..Mungu anaanza kumsogelea tena mwanadamu kwa karibu.. Kwahiyo YESU ni Mungu aliyeuvaa mwili kwa lengo hilo la kuyasema yale maneno ya Mungu yaliyokuwa yanayosikika kwa ndoto na maono kupitia manabii..
Kuzidi kuuthibitisha uungu wa YESU basi soma mistari ifuatayo (Yohana 20:28, 1Yohana 1:1-2, Tito 2:13, Isaya 9:6 na 1Timotheo 3:16).
Lakini isingetosha tu Mungu aonekane katika mwili na kuyahubiri maneno yake kwa mdomo kama alivyokuwa anaongea na Adamu pale Edeni na huku bado mwanadamu hajui kanuni ya kuishi katika mapenzi ya Mungu…Hivyo akaongeza mpango wa pili juu yake wa kumfundisha mwanadamu njia na kanuni za kuishi kimatendo, kwahiyo ikambidi aishi kama mwanadamu ambaye anamcha Mungu.
Lengo si kutafuta ukamilifu yeye, bali ni kutufundisha sisi ukamilifu, ndio maana akaishi chini ya wazazi ili awafundishe watoto namna ya kuishi maisha ya kumcha Mungu, na tena akawa mtu mzima ili awafundishe watu wazima kanuni za kumcha Mungu, ndio maana akawa anaomba, akawa anafunga, akawa anamwambudu Mungu kana kwamba kuna Mungu juu n.k.
Hivyo maisha yake yakawa njia ili sisi tufahamu njia (soma Yohana 14:6). Lakini yeye hakuwa mtu, bali ni Mungu ndani ya mwili wa Mtu kwa lengo la kutufundisha njia..
Wafilipi 2:5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu”
Lakini pia isingetosha yeye ahubiri maneno yale kwa kinywa chake, na awe mwalimu wa kutufundisha sisi na ili hali bado tuna laana ya dhambi tuliyoirithi toka kwa wazazi wetu wa kwanza Adamu na Hawa
Hivyo akaongeza mpango mwingine wa tatu (2) juu ya hiyo miwili, kwamba autoe mwili wake huo kuwa sadaka ya dhambi baada ya kumaliza huduma kazi hizo mbili.. Hiyo ndio sababu kwanini Kristo afe msalabani..Ni ili sisi tupate ondoleo la dhambi.
3. MUNGU NDANI YETU (Kama Roho Mtakatifu).
Baada ya kurejesha uhusiano namna hiyo, kwamba sasa tunamwona MUNGU na tumeondolewa dhambi na kile kizuizi kulichokuwa kinatutenga sisi na Mungu, na ile laana ya Adamu tuliyokuwa tunaibeba. Mungu aliongeza mpango mwingine wa Mwisho ambao kupitia huo tutakuwa karibu na Mungu moja kwa moja, kwamba tutamsikia na kumwona na kumwelewa sana.
Na mpango huo si mwingine Zaidi ya yeye kuingia ndani yetu, kama ROHO, ili atusaidie madhaifu yetu..Ni sawa na mchezaji aliye katika michezo anayepewa kinywaji cha kuongeza nguvu na kusisimua misuli ili ashinde katika mchezo ule.
Na Roho Mtakatifu ni MUNGU katika ROHO, ambaye anaingia ndani yetu na KUSISIMUA uwezo wetu wa kumwelewa MUNGU, UWEZO wetu wa KUSHINDA DHAMBI, uwezo wetu wa KUMCHA MUNGU, Uwezo wetu wa kukumbuka n.k (Yohana 14:26 na Yohana 16:12-13).
Sasa kuthibitisha kuwa Roho Matakatifu ndiye yule yule Mungu soma 2Wakorintho 3:17.
Hii ni zawadi kubwa na kipekee sana, na ya mwisho inayomsogeza Mtu karibu na Mungu kuliko zote.
Sasa swali la ziada ni hili; Kwanini KRISTO aondoke!
Sababu ya KRISTO kuondoka na kwenda juu mbinguni ni kwenda kutuandalia sisi makao (Yaani ile YERUSALEMU MPYA), Makao ya watakatifu. (soma Yohana 14:2, Ufunuo 3:12 na Ufunuo 21:2).
Na makao hayo anayokwenda kutuandalia ni ili wakati utakapofika tukae naye milele, katika mbingu mpya na nchi mpya. (Maskani yake iwe pamoja nasi)…Hapo yale yaliyoharibika Edeni yatakuwa yametengenezwa upya tena katika utukufu Mkuu kuliko ule wa kwanza.
Ufunuo 21:3 “Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.
5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli”.
Je umeuona mpango wa Mungu??…na je umeyaona pia madhara ya dhambi??… Dhambi ilitutenga mbali na Mungu na mpaka sasa inatutenga mbali na Mungu..
Na kanuni pekee ya kumkaribia MUNGU ni kwa kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha (Mithali 28:13). Unapotubu kwa kumaanisha kuziacha unamkaribisha YESU maishani mwako ambaye humwoni kwa macho sasa, lakini siku moja utamwona… Lakini zawadi kubwa atakayokupa ambayo itakufanya ujihisi upo naye hata kama humwoni ni ROHO MTAKATIFU (ambaye kiuhalisia ni yeye mwenyewe katika mfumo wa Roho).
Na huyo Roho Mtakatifu atakulinda na ulimwengu, mpaka siku ya mwisho, ambayo BWANA YESU ATAKUJA na kutupa TAJI ZA UZIMA, na kukaa naye milele katika maisha ya furaha, yasiyo na mwisho, wala dhiki wala mateso, wala uchungu, wala vilio..kwasababu mambo ya kwanza yatakuwa yameshapita.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?
KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000
Kwa namna gani tumefanyika Makuhani na Ufalme?.(Ufunuo 1:6)
REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.