Maandiko yanaonyesha kuwa kitu pekee cha asili kinachoweza kutenganisha watu wawili walio katika Ndoa ni KIFO.
Warumi 7:2 “Kwa maana mwanamke aliye na mume amefungwa na sheria kwa yule mume wakati anapokuwa yu hai; bali akifa yule mume, amefunguliwa ile sheria ya mume.
3 Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine.”
Lakini inapotokea Mtu anachukua nafasi ya KIFO, yaani anaivunja ndoa yake mwenyewe au ya Mtu mwingine iliyo ya Halali, basi mtu huyo kibiblia ni MFU, au jina lake lingine ni KIFO/MAUTI..Sasa utauliza KIFO kinaweza kuwa MTU jibu ni Ndio!.
Ufunuo 6:8 “Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda JINA LAKE NI MAUTI, na Kuzimu akafuatana naye…”
Kwahiyo Mtu anayechukua nafasi ya KIFO, katika ndoa yake mwenyewe au ya mwingine, huyo jina lake ni MAUTI kibiblia, awe mwanamke au mwanaume, huyo ni MAUTI, ni Mfu anayetembea.
Utauliza ni wapi tena katika maandiko, panaonyesha mtu aliyeharibu ndoa ya mwingine aliitwa MFU?
Mwanzo 20:2 “Ibrahimu akamnena Sara mkewe, Huyu ni ndugu yangu. Basi Abimeleki mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara.
3 Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, UMEKUWA MFU WEWE kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu”.
Umeona hapo?.. MUNGU anamwambia Abimeleki kuwa yeye ni MFU kwa kitendo tu cha kumchukua mke wa Ibrahimu.
Hebu jiulize hapo kwanini Mungu hajamwambia Mfalme Abimeliki kuwa umekuwa Najisi, au umekuwa Mjinga, au umekuwa Mpumbavu.. badala yake anamwambia amekuwa MFU!!!.. Maana yake pale alipo alikuwa ni Marehemu anayeishi.. Siku yoyote anashuka kaburini, na kila atakachojihusisha nacho kitakufa pia.
Hiyo pia ni hali ya Mtu anayeharibu ndoa yake mwenyewe au ya mwingine, kiroho jina lake ni MFU/MAUTI.
Na kumbuka maandiko yanasema Mauti anafuatana na Kuzimu.. Ufunuo 6:8 “Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda JINA LAKE NI MAUTI, na Kuzimu akafuatana naye…”
Maana yake huyu mtu anayeitwa MAUTI, anakwenda sambamba na kuzimu, na mwisho ni ZIWA LA MOTO.
Ufunuo 20:14 “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto”.
Je Mke au Mume uliye naye ni wako? Au wa mtu mwingine?… Unajua ni maumivu gani unayasababisha kwa mwingine unapomchukua Mke wake au Mume wake??..
Labda ulimchukua pasipo kujua maandiko au enzi bado hujaokoka, lakini sasa umejua …Mrudishe huyo mwanamke/mwanamume kwa aliyewake wake hata kama una watoto naye, (weka naye tu mipango ya namna ya kuwatunza watoto), lakini usiendelee kuishi naye kwani unafanya UZINZI, mrudishe kwa mume wake/mke wake, akikataa Mwache aishi mwenyewe, wewe utakuwa umejifungua katika kifungo cha Mauti….Vunja agano na Mauti kwa namna hiyo…
Isaya 28:18 “Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)
SWALI: Biblia inamaana gani kusema..maana Mungu wetu ni moto ulao?
Waebrania 12:29
[29]maana Mungu wetu ni moto ulao.
JIBU: Andiko hilo linaeleza sifa nyingine ya Mungu, kwamba si tu anajifananisha na maji, au nuru, au mafuta bali pia na “moto” tena ule “moto ulao”.
Kwanini aseme hivyo?
Ukianzia kusoma mistari ya juu utaona anaeleza madhara ya kuikataa sauti ya Kristo, kwamba ghadhabu yake inapokuja huwa ni mbaya mfano tu wa ile ghadhabu aliyoidhihirisha kwa wana wa Israeli kule jangwani walipoasi.
Waebrania 12:25
[25]Angalieni msimkatae yeye anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa yeye aliyewaonya juu ya nchi, zaidi sana hatutaokoka sisi tukijiepusha na yeye atuonyaye kutoka mbinguni;
Neno hili la moto ulao, mwandishi alilinukuu kwenye vifungu hivi vya agano la kale.
Kumbukumbu la Torati 4:23-24
[23]Jihadharini nafsi zenu, msije mkalisahau agano la BWANA, Mungu wenu, alilolifanya nanyi, mkajifanyia sanamu ya kuchonga, mfano wa umbo la kitu cho chote ulichokatazwa na BWANA, Mungu wenu,
[24]kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, ni moto ulao, Mungu mwenye wivu.
Mungu alijitambulisha kwa wana wa Israeli kwa sifa hii, ndio sababu hata mwanzoni kabisa alipomtokea Musa kule jangwani alijifunua kama kijiti kinachoungua lakini hakiteketei. Kufunua kuwa wakitembea katika njia zake moto wake hauwezi kuwala, hivyo wasiwe na hofu, bali utawalinda na kuwaimarisha,lakini wakiasi utawala hakika.
Moto huo ndio ule uliokuwa nguzo mbele yao kuwalinda. Na walipokosea waliadhibiwa kwa huo, wakaanguka watu wengi jangwani kwa yale mapigo tunayoyasoma.
Sasa tukirudi kwenye kitabu cha Waebrania. mwandishi anatoa angalizo pia kwamba tusiipuuzie sauti ya Mungu katika Kristo Yesu, kwasababu sasa hivi Mungu anazungumza na sisi moja kwa moja kutoka mbinguni, sio tena kwenye mahema au milimani,kama kule jangwani, hivyo tuongeze umakini
Tukikumbuka kuwa sifa zake ni zile zile…Yeye ni moto ulao hata sasa. Tunapofanya dhambi kwa makusudi tunapokengeuka na kudharau wokovu (Waebrania 6:4-8)…tuogope kwasababu moto wa wivu wake unaweza pita juu yetu, na kutuharibu kabisa, na kujikuta tupo katika ziwa la moto.
Lakini tunapotii, moto wake hautuharibu bali unatulinda na kutuimarisha..tunafananishwa na dhahabu, inayopitishwa kwenye moto kutakaswa.
Hivyo, maaana ya vifungu hivyo ni tunafahishwa kuwa Mungu ana sifa ya moto, tukilifahamu hilo tutautumiza wokovu wetu kwa kuogopa na kutetemeka. (Wafilipi 2:12). Wala hatutakwenda kutenda dhambi kwa makusudi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Biblia inamaana gani inaposema ‘tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao’?
Mwanzo 2:5-6
[5]hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana BWANA Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi;
[6]ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.
Tofauti na inavyodhaniwa, kwamba mvua ilinyesha juu ya nchi siku ile Mungu alipozichepusha mbegu ardhini. lakini haikuwa hivyo. Japokuwa hilo liliwezekana. Lakini Mungu hakutumia njia hiyo
kinyume chake alileta ukungu, ambao ni unyenyevu juu ya ardhi yote kutoka chini. Ukailowesha ardhi yote. Na hivyo mbegu zikapata uhai, zikamea.
Tunaona jambo kama hili alilifanya tena..wakati ule wa wafalme pindi walipotoka kwenda kupigana na wamoabu waliowaasi, biblia inatuambia walizunguka siku saba, bila maji, hatimaye wakamuuliza Bwana wafanyeje.
Ndipo Bwana akawaambia..chimbeni mahandaki, kisha nitayajaza maji bila mvua
2 Wafalme 3:16-18
[16]Akasema, BWANA asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki.
[17]Kwa kuwa BWANA asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu.
[18]Na jambo hili ni jepesi machoni pa BWANA; pia atawatia Wamoabi mikononi mwenu.
Bwana hushibisha kutoka juu, lakini pia hushibisha kutoka chini. Utakufunulia mambo yake ya rohoni moja kwa moja kutoka mbinguni, lakini pia atakufunulia kutoka hapa hapa duniani kupitia mambo yanayokuzungua yaani watu, vitu, n.k. na vyote vikaleta matokeo yale yale. Atakupa mahitaji yako kimiujiza, lakini pia kwa kupitia watu. Mungu wa vilivyo juu ndio Mungu yule yule wa vilivyo chini.
Ndivyo anavyotenda kazi, ili tusimzoelee uweza wake.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.
NUHU WA SASA.
Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?
Rudi Nyumbani
SWALI: Wanawake wenye cheo wanaotajwa kwenye biblia ni akina nani? (Matendo 17:12)
JIBU: Mitume walipoanza kulitekeleza agizo kuu la Bwana Yesu la kuenenda ulimwenguni kote kuhubiri injili, biblia inatuonyesha walikutana na makundi mbalimbali ya walioamini.
Sasa mojawapo ya kundi hilo ambalo liliipokea injili, walikuwa ni hawa wanawake wenye cheo.
Kwamfano tunaweza kuona jambo hilo katika ziara ya mtume Paulo kule Beroya.. alipofika kule alikutana wa wanawake wa namna hii, na akawahubiria wakaipokea injili.
Matendo ya Mitume 17:10-12
[10]Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi.
[11]Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.
[12]Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache.
Wanawake wenye cheo ni wanawake waliokuwa na sifa ya aidha nafasi za juu za kiutalawa, au ushawishi mkubwa kwenye jamii zao au wenye mali nyingi.
Wengi wao walipokutana na injili ya kweli ya Bwana Yesu Kristo waliipokea na kugeuka.
Lakini tunaona mahali pengine, mtume Paulo alipokwenda, wayahudi walimfanyia fitina kwa kuwatumia watu wa namna hii ili kuwataabisha..Kwamfano alipofika kule Antiokia mji wa Pisidia, na kuhubiri injili kwa ushujaa na wengi kuokoka. Wayahudi kwa sababu ya wivu wakawashawishi baadhi ya wanawake na wanaume wa namna hii..Ili wawapinge akina Paulo. Kwasababu walijua nguvu yao kijamii ni kubwa kiasi gani, hivyo itakuwa rahisi kutekeleza adhma yao.
Matendo ya Mitume 13:50
[50]Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao.
Hivyo hiyo ni kututhibitishia hata sasa, Watu wenye vyeo wana nafasi ya kuwa washirika wa injili. Hivyo tusibague wa kumuhubiria, kwasababu wote Kristo amewafia msalabani. awe ni mbunge, au waziri, awe ni tajiri, au maskini, msomi, au asiye na elimu,. wote ni wa Mungu na wanastahili wokovu, wasipotumiwa na Mungu wao, shetani atawatumia. Hivyo nguvu zetu za injili ziwe sawasawa kwa watu wote.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wale waliowekewa tayari ufalme ni akina nani?. (Mathayo 20:23).
Rudi Nyumbani
SWALI: Je ni halali kiongozi wa imani (Wachungaji), kugombea nafasi za kiserikali kama vile udiwani au kuwa wanasiasa au wafanya-biashara?
JIBU: Kabla ya kuangalia kiongozi wa imani. Embu tuangalie kwanza kwa mtu aliyeamini.
Je mtu aliyeamini kugombea nafasi za kiutawala ni dhambi?
Kugombea nafasi ya kiutawala, biblia haijaeleza moja kwa moja kuwa ni kosa au si kosa, Yategemea lengo/ nia ya huyo mtu, Ikiwa ataenda kule ili kutetea haki, huku akitembea katika misingi ya imani ni wazi kuwa hakuna kosa lolote yeye kufanya hivyo. Kwenye maandiko tunarekodi ya watu wa Mungu waliokuwa na vyeo katika nafasi ya kiserikali, lakini waliweza kuhifadhi misingi ya imani yao, mfano wa hao ni Yusufu na Danieli, ijapokuwa walikuwa katika falme za kipagani lakini waliweza kutembea na Mungu hatimaye wakapendwa sana.
Mfano mwingine katika historia kuna mkristo mmoja maarufu aliyeitwa William Wilberforce, yeye alizaliwa mwaka 1759, alipokuwa mtu mzima aligombea nafasi ya ubunge uko ulaya akaipata, lengo lake likuwa ni kuomba sheria ya biashara ya watumwa ifutwe ulaya, ijapokuwa shitaka lake lilipingwa na kupuuziwa kwa miaka mingi sana, lakini aliendelea kulipigania bila kuchoka mpaka mwisho wake lilikuja kupitishwa, hivyo kwa ajili yake yeye, biashara ya utumwa ilifutwa kule ulaya karne ya 18. Hivyo ikiwa mkristo atajiunga kwa madhumuni kama haya, si dhambi.
Lakini tukirudi katika eneo la “kiongozi wa kiroho”. Mpaka aitwe kiongozi maana yake wapo watu chini anaowachunga, ambao Bwana amempa awaangalie, na siku ya mwisho atatolea hesabu kwa ajili yao.
Sasa ikiwa ni hivyo. Mtu kama huyu kujihusisha na nafasi ya serikalini, au siasa, au kuwa mfanya-biashara ni makosa.
Ikumbukwe kuwa Bwana Yesu alitoa mipaka juu ya utumishi wake. Akasema mtu hawezi tumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja. Aidha atampenda huyu na kumchukia huyo
Mathayo 6:24 Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpendahuyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
Pengine utaliuza vipi kuhusu Paulo? maana alikuwa fundi wa kushona mahema?.
Ndio kiongozi au mchungaji anaweza akawa na shughuli yake ndogo ya pembeni kumsaidia kupata kipato, ili tu aweze kujitimizia mahitaji yake ya msingi,(ikiwa ni lazima) mfano alivyofanya mtume Paulo, alipokwenda kushona mahema (Matendo 18:3). Lakini sio kwa lengo la kuwa mfanya-biashara na wakati huo huo askofu. Paulo alifanya vile ili kumudu tu mahitaji yake ya msingi. Tofauti na inavyochukuliwa na watu leo kuwa “Alishikilia mambo yote” maana kama ni hivyo Paulo asingemwambia Timotheo maneno haya;
Timotheo 2:4 Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari.
Umeona? Mlango wa kujihusisha na mambo mengine, haupo.
Ndio maana kipindi kile baada ya Bwana Yesu kufufuka Petro alijaribu kurudia kazi yake ya uvuvi, alipohangaika usiku kucha na kukosa, asubuhi yake alipokutana na Yesu, swali la kwanza aliloulizwa Je! Petro unanipenda? Swali hilo aliulizwa mara tatu. Akajibu ndio…Yesu akamwambia basi lisha kondoo zangu.
Yaani toa akili zako huko kwenye uvuvi kafanye kazi ya utume uliyoitiwa. Baada ya hapo hatuona mahali popote Petro, akivua huku anafanya utume. (Yohana 21). Na hata kama ilitokea basi haikuwa kwa lengo la kuwa mfanya-biashara, bali kupata riziki ya siku.
Ukishakuwa kiongozi wa kiroho, tambua wewe hujatengenezwa kwa utumishi wa mambo mengine, bali kumtumikia Mungu tu, kazi uliyonayo ni kubwa zaidi ya zote ulimwenguni, na bado inawatenda kazi wachache, Bwana Yesu alisema. Hivyo hii ni kazi inayoweza kukufanya uwe bize wakati wote. Hupaswi kuwa mkuu wa mkoa wakati huo huo, ni mchungaji, kuwa mbunge au waziri, wakati huo huo ni askofu, utakwama tu mahali pamoja.
Na ni muhimu kufahamu kuwa huduma ya Kristo haipaswi kuhusishwa na utafutaji fedha ndani yake, bali ni kazi ya wito ambayo malipo yake hasa yapo mbinguni. Hivyo Bwana akikubariki, au asipokubariki, hilo halikufanya uache huduma na kuwekeza akili yako kwingineko, lakini fahamu kuwa aliahidi hatakuacha wala kukupungukia kabisa.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.
Rudi Nyumbani
Somo la nyuma tuliona msingi wa Ukristo ni nini.. kwamba Yesu Kristo Bwana wetu ndiye msingi wenyewe..Yeye huitwa jiwe kuu la pembeni, na mwamba ambao juu yake sisi sote tumewekwa, pasipo Yesu hakuna ukristo. Yeye ndio msingi wa imani yetu.
Lakini pia kikawaida msingi ukishakaa chini, huwa nguzo zinafuata juu yake, kazi ya nguzo ni kulifanya jengo liweze kushikamana na kusimama vema toka juu kwenye paa mpaka chini kwenye msingi wenyewe.
Hivyo wewe kama mkristo ukishaweka msingi chini wa nyumba yako ya kiroho, fahamu pia moja kwa moja utanyanyua na nguzo zake, ili kuliunda jengo. Je nguzo zenye ni zipi?
Hizi ndizo nguzo kuu saba (7), za ukristo .
Ni wajibu wa kila mwamini aliyekombolewa na Kristo, pindi tu alipookoka aanze kukua ki-upendo. Hii ndio nguzo mama, kwasababu Mungu mwenyewe ni upendo (1Yohana 4:8). Zaidi sana anapaswa afahamu kuwa, upendo wa ki-Mungu sio kama ule wa kibinadamu
wa kupenda wanaokupenda, hapana ..huu ni upendo unaozidi usio na sharti wa kujitoa, ambao unapenda mpaka maadui, zaidi na kuwaombea wanaokuudhi.
Mtu asiyejijenga katika huu, haijalishi atajitaabisha vipi kwa Kristo, kazi yake itakuwa ni ya hasara siku ile ya mwisho.
1 Wakorintho 13 : 1-13
1 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi
cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama
sina upendo, hainifaidii kitu.
4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha,
zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
Ili maisha ya mkristo yasimame vema, maombi ni nguzo nyingine inayomkamilisha. Biblia inasema maombi yanapaswa yawe ni jambo la daima.
Wakolosai 4:2 Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani;
Maombi ni sawa na maji mwilini, au mafuta kwenye gari, vikikosekana hivi vitu hakuna utendaji kazi wowote utakaoendelea, vivyo hivyo ukristo wako usipokuwa wa maombi, hautaendelea sana. Utakufa tu siku moja
Ili tujengeke vizuri kiwango cha chini Bwana alichotaka tuombe kwa siku ni saa moja (Mathayo 26:40). Bwana Yesu alikuwa mwombaji, mitume walikuwa waombaji, sisi yatupasaje?
Ukishaokoka, jambo linalofuata ni kuwa karibu na biblia yako. Katika hiyo utapata kuelewa mpango kamili wa Mungu katika maisha yako. Huku ukisaidiwa na waalimu na wakufunzi wako kwenye usomaji wako wa biblia, kama Bwana wetu Yesu alivyokuwa mdogo akifanya bidii kuwasikiliza waalimu wake.
Kujifunza na kusoma kunapaswa kuwe ni tendo la kila siku. Neno ni kama chakula na maombi ni maji. Hivi viwili ndivyo vinakukuza kiroho na kukujenga nafsi. Hupaswi kuacha kusoma.. Mkristo asiyeifungua biblia yake ni rahisi sana kuchukuliwa na upepo wa ibilisi kwa mafundisho potofu. Kwasababu hamjui Mungu.
Hekima, maarifa, imani, ufahamu,na mamkala vinatoka katika kulijua Neno na mafundisho. Hivyo soma hiyo kila siku, pia sikiliza mafundisho kutoka kwa waalimu wako sahihi wa kweli, kwasababu ni muhimu sana kuvipata.
Matendo 2:41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.
42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
1Timotheo 4:13 Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha
Ushirika ni kukutana pamoja na wenzako kujengana. Ushirika ni umoja wa Roho katikati yetu.
Waebrania 10:25 wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
Kama mtakatifu, hupaswi kujiaminisha utakuwa na utimilifu wote wa ki-Mungu ndani yako kivyako. Utahitaji kukamilishwa na wengine kwa sehemu baadhi, Ndio hapo suala la ushirika linakuja.
Ndio sababu Mungu ameweka karama tofauti tofauti ili tujengane. Katika ushirika mtaombeana, kushiriki meza ya Bwana pamoja, mtafarijiana, mtasaidiana n.k.
Na pia biblia inasema wawili walalapo watapata joto.
Mhubiri 4:9 Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.
10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!
11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona
moto?
12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatuhaikatiki upesi.
Muwapo pamoja kuna ulinzi wa kipekee unaongezeka juu yenu. Hivyo kamwe usijaribu ule ukristo wa kivyako-vyako. Ni lazima tuwe washirika wa kanisa. Kama kanisa la kwanza lilivyoweza kusimama kwa kanuni hiyo.
Utakatifu ni utambulisho wa ukristo. Huwezi kuwa mkristo, halafu ukawa mwovu, huwezi kupokea Roho Mtakatifu halafu sifa za utakatifu usizionyeshe ndani yako. Kwasababu maandiko yanasema Mungu tunayemtumikia ni Mtakatifu hivyo na sisi pia hatuna budi kuenenda katika utakatifu. Bwana Yesu pamoja na watakatifu wa kwanza walizingatia viwango vyote vya usafi na ukamilifu. Vivyo hivyo na sisi
1Petro 1:16 kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.
Ushuhudiaji unaanza pindi tu unapookoka. Kila mkristo ameitwa kuitenda kazi ya Bwana. Na ni lazima afanye hivyo kama sehemu ya maisha yake, ili safari yake ya wokovu hapa duniani iwe imara ni lazima azae matunda. Uwakili ni kazi yetu ya daima. Ukristo bila uinjilisti hauwezi kuwa imara. Kanisa la kwanza lilikuwa la kiinjilisti. Kila mmoja alitambua wajibu wake wa kuisambaza injili kila mahali walipokuwa wakilizingatia lile agizo la Bwana.
Matendo 8:4 Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.
.
Sifa ya Mungu ni utoaji, ndio maana mpaka leo tunanufanika na mengi katika ulimwengu wake. Hata tulipopotea katika dhambi alijitoa kwa ajili yetu kwa kumtoa mwanawe awe fidia.
Na sisi kujitoa kihali na kifedha kwa ajili ya injili na kanisa la Kristo, ni nguzo muhimu sana. Unawajibu wa kuisapoti huduma inayokukuza kiroho, kwa zaka na changizo zako, pamoja na kuwasaidia ndugu (maskini). Kwasababu, Bwana Yesu na kanisa la kwanza lilikuwa na desturi hiyo.
1 Wakorintho
16:1 Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo
Hivyo sisi sote tukizitendea kazi nguzo hizo muhimu, basi tuwe na uhakika jengo letu la Imani litakuwa imara sana, linaloweza kustahili tufani na majaribu yote, lililoundwa vyema, kwa utukufu wa Mungu, hata siku ile ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Yakobo 5:1-6
Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.
Biblia inatoa angalizo na tahadhari katika eneo la watu wanaoitwa matajiri. Kimsingi utajiri si dhambi, na ni mapenzi ya Mungu watu wake wafanikiwe, (lakini si katika hila).
Hivyo biblia inafunua siri za matajiri wengi wadhalimu, na kuwaonya mapema ili wajirekebishe kwasababu kuna adhabu kali wameandaliwa mbeleni kwa ajili yao.
Biblia inafunua vyanzo vikuu vya mafanikio yao, wala sio katika uchawi kama wengi wanavyodhani,.. bali vipo kwa “wale watu wawatumikiao”, walio chini yao, au wanaowatumia kufanya shughuli zao.
Matajiri wengi, huwatumia wao kama daraja la wao kufika juu, ndio hapo hutumia njia ya kuwatumikisha zaidi ya kawaida yao, na kuwalipa mishahara midogo, au hata wakati mwingine kuwadhulumu kabisa kutowapa kitu, na kuwanyanyasa, hawajali malalamiko yao, na changamoto zao na mahitaji yao. Wanachojali ni kiasi gani kimepatikana, au kazi ngapi zimekamilika. Ili wapate fedha wakazijaze hazina zao.
Lakini Hawajui kuwa Kilio chao kinamfikia Mungu mbinguni. Ijapokuwa wao wanaweza wasione chochote. Kumbe hawajui wanajikusanyia adhabu kali siku ile ya hukumu.
Biblia imetumia mfano wa “bwana na mkulima wake” aliyemwajiri kwenye shamba lake… akiwawakilisha watu wote wenye wafanya-kazi chini yao.
Anasema..
Yakobo 5:1-6
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.
[2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.
[3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.
[4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.
[5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.
[6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
Umeona? wamejilisha mioyo yao utajiri, wamejinenepesha tayari kwa machinjo yao wenyewe..
Hiyo ndio sababu pale mwanzo anatangulia kwa kusema “walie, na kupiga yowe”, kwa hiyo adhabu kali inayokuja juu yao…yaani akimaanisha watubu haraka sana, ili mabaya hayo yasiwakute.
Ujumbe huu ni hata sasa?
Yaweza kuwa bado hujafikia kiwango cha utajiri wowote lakini hata ukiwa na mtu/watu uliowaajiri chini yako, bado upo kwenye mkondo huo huo wa matajiri,
hivyo wajali sana watumwa wako wape maslahi yao,.sikiliza sana malalamiko yao, kuwa tajiri usiye na lawama, mfano wa Ayubu, ambaye aliwathamini sana watumishi wake mpaka akasema..
Ayubu 31:13-15
[13]Kama nimeidharau daawa(mashtaka) ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu, Waliposhindana nami;
[14]Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini? Naye atakapozuru, nitamjibuje?
[15]Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?
Kuwa tajiri kwa kutenda mema, hapo ndipo baraka zitakapokuja.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?
Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali.
Rudi Nyumbani
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya uzima. Leo napenda tujifunze tabia nyingine ya Bwana Yesu. Kwasababu yeye mwenyewe alituambia ‘tujifunze kwake’. Hivyo naamini tuna mengi ya kuyajua kuhusu yeye.
Habari hiyo tunaisoma katika vifungu hivi;
Luka 9:51 Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;
52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.
53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.
54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?
55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]
56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine.
Kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utakumbuka kuwa kuna wakati ulifika, ilikuwa wazi kwa watu wote, kuwa Yesu anatafutwa ili auawe, (hususani kule Yerusalemu). Na hilo lilimfanya mara kadha wa kadha asitembee kwa uwazi wote mbele ya makutano (Yohana 7:10), kwasababu, saa yake ya kuuawa ilikuwa bado haijafika.
Yohana 11:54 Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
Lakini mambo yalikuja kubadilika baadaye, hilo halikuendelea kwa wakati wote. Alipoona sasa kazi aliyopewa na Mungu ameimaliza, alionyesha tabia nyingine ambayo haikuwa ya kawaida. Biblia inatuambia, “aliukaza uso wake kuelekea Yerusalemu”, kule kule alipokuwa anatafutwa auawe.
Jambo ambalo lilileta mshtuko hata kwa mitume wake;
Yohana 11:7 Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.
8 Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?
9 Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.
Walishangaa, ujasiri huo ni wa namna gani? Ni sawa na wanajeshi waliokwenda vitani, halafu maadui wakawaua wanajeshi wote, akabakia mmoja tu, halafu huyo mmoja anasema nitakwenda kupambana na jeshi lote hilo peke yangu sitajificha. Ukweli ni kwamba inahitaji nguvu nyingine ya ziada ndani ya huyo mtu.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, aliukaza uso wake, kwenda kututetea sisi. Embu Fikiria kama angeulegeza, na kuendelea kuzunguka mahali pengine na sio kule uyahudi(Yerusalemu), wokovu wetu tungeupatia wapi?
Ilibidi, alazamishe mambo, japo mwili wake ulikuwa hautaki, ndio maana akiwa pale bustanini, anaomwomba Baba, akisema ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, ni kuonyesha kuwa hata mwili wake ulikuwa unagoma kuwepo kule Yerusalemu, na si mwili tu, bado mazingira pia hayakutaka, alipokuwa anakatiza kwa Wasamaria wenyeje wa pale hawakutaka kumruhusu akae kwao, kwasababu waliona kama anawaletea matatizo, ikumbukwe kuwa watu hao hao ndio waliokuwa wanataka kumfanya mfalme hapo mwanzo. Kuonyesha kuwa mazingira yalimgomea. Si mazingira peke yake, hata mitume wake nao, walifanya kama kumsindikiza tu, lakini mioyo yao walishajiandaa kuchukua hatua yoyote lolote litakapotokea, ndio maana pale bustanini, wale watu walipokuja kila mmoja akakimbia na njia yake.
Kwa ufupi kila kitu kilikataa, isipokuwa roho yake tu. Ndio sababu ya kwanini maandiko yanatuambia ‘aliukaza uso wake’ kwasababu haikuwa rahisi, si jambo tena la kuomba, au kubembeleza, au kushawishi, au kusubiri msimu mzuri. Bali ni kujitoa tu wote wote, katika hayo. Watu wengi tunadhani Yesu aliuchukua msalaba wake siku ile alipobebeshwa ule mti, hapana, aliuchukua msalaba wake Kwa kitendo hichi cha kuamua kuukaza uso wake, kuelekea kifoni. Hata aliposema tujitwike misalaba yetu, alilenga, eneo hilo.
Ni nini na sisi tunapaswa tukipokee kwa Bwana Yesu?
Kwa kuwa Roho wake naye yupo ndani yetu, hatuna budi kufahamu kuwa yapo majira katika safari yetu ya wokovu, hatutahitaji mazingira yawe mazuri, ndio tulitimize kusudi la Mungu, au ndugu kutukubalia, au marafiki kuafikiana na sisi, au miili kutuambia sasa ndio wakati, hapana..bali ni kujitwika misalaba yetu, “kwa kukaza nyuso zetu” na kumfuata Yesu.
Tukingoja vikwazo viondoke, au viondoshwe, tutajidanganya, na tutangoja sana, kwani vita vitaendelea kuwepo mpaka mwisho, mapambano hayaishi, tutashinda tu kwa kukaza tu nyuso zetu. Na Bwana atakuwa pamoja na sisi, ijapokuwa itaonekana ni kujipoteza lakini mwisho wake utakuwa ni uzima kama ulivyokuwa kwa Bwana Yesu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?
Rudi Nyumbani
Jiunge >>> WHATSAPP <<< kwa mafundisho.
Ikiwa ndoto hii inakujia mara kwa mara, Au imekujia kwa uzito fulani, basi hwenda Mungu anasema na wewe rohoni. Ndoto hii inaweza kuja katika maumbile mengi. Wengine wanaota wakivua samaki kwa mikono, wengine kwa ndoano, wengine kwa wavu, wengine wakivua samaki wadogo/wakubwa. n.k. Kwa vyovyote vile maadamu ni kuvua basi maudhui yake ni moja.
Kiroho, uvuvi humaanisha kuwavuta watu kwa Kristo kwa kazi ya injili.
Yesu alipokutana na wale thenashara, wengi wa hao walikuwa wakifanya kazi ya uvuvi. Hivyo hiyo ilikuwa ni njia rahisi ya Yesu kuwaeleza kusudi lake timilifu juu ya hicho wanachokifanya.
Ndio maana siku ile alipomfanyia Petro muujiza ule wa kupata samaki wengi, baada ya kutaabika usiku kucha bila kupata chochote, Yesu alimwambia usiogope tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.
Luka 5:10
[10]na kadhalika Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni.Yesu akamwambia Simoni, Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu.
Kuonyesha kuwa uvuvi wa nje, ni ufunuo wa uvuvi wa rohoni.
Utaona hata huduma ya malaika siku ile ya mwisho ya kuwatenga watu waovu na wema inafananishwa na huduma ya uvuvi wa samaki.
Mathayo 13:47-50
[47]Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;
[48]hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa.
[49]Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,
[50]na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Hivyo kwa namna moja au nyingine ikiwa umeokoka basi Bwana anakutaka uhihubiri injili, kwa wengine kwasababu wakati huo umefika kufanya hivyo. Usiangalie uzoefu wako, kwasababu kumshuhudia Kristo hakutegemei uzoefu bali nia ya upendo. Na Mungu mwenyewe ameahidi kukusaidia kunena uwashuhudiapo watu.
Lakini kama hujaokoka, basi Yesu anakuita na anaona wito wako kutokea mbali, kwamba ukawahubirie wengine. Hivyo ni wajibu wako kumtii na kuupokea wokovu ili kusudi hilo alilolipanga ndani yako alifanikishe juu yako, haijalishi ndoto hii umeota mtu wa dini gani au imani gani, iwe mwislamu, mhindu, mshirikina. Maana umeota msalaba. Ujue Kristo anakuita akuokoe.
Ikiwa upo tayari sasa kumpokea Yesu basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Jiunge >>> WHATSAPP <<< kwa mafundisho.
Ikiwa wewe bado hujamjua Kristo kabisa/ hujaokoka. Fahamu kuwa ndoto hii inakujuza kuwa Kristo anakuita akuokoe.
Msalaba hufunua wokovu wa Yesu Kristo, tulioupata kwa kifo chake juu ya mti huo.
Waefeso 2:16
[16]Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba.
Hivyo fungua moyo wako upokee wokovu huu bure, Kumbuka hakuna uzima wala tumaini, wala, amani,wala raha, wala faraja nje ya Kristo. Ndio maana umeota msalaba kwasababu Kristo anakupenda, hataki uangamie. Ikiwa upo tayari kumpokea leo basi fungua hapa kwa msaada…
Lakini ikiwa tayari umeokoka. Kristo anakutaka kumuangalia yeye zaidi… Kuongeza kiu yako, kwake, na mawazo yako kwake, na hiyo inaambatana na kujikana nafsi.
Luka 9:23-24
[23]Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.
[24]Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.
Hivyo kwa ujumla wake ndoto ya msalaba, aidha umeushika au umeubeba, au umeuona, ni ishara ya kumtazama Kristo.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani