Guruguru na Goromoe ni wanyama gani? (Walawi 11:30)

Guruguru na Goromoe ni wanyama gani? (Walawi 11:30)

Jibu: Turejee.

Walawi 11:29 “Tena katika vitu vile vitambaavyo, vitambaavyo juu ya nchi, hivi ni najisi kwenu; kicheche, na panya, na mjombakaka, kwa aina zake, 

30 na GURUGURU na kenge, na mjusi na GOROMOE, na lumbwi. 

31 Wanyama hao ndio walio najisi kwenu katika hao watambaao; awaye yote atakayewagusa, wakiisha kufa, atakuwa ni najisi hata jioni”

Guruguru ni jamii ya mijusi wanaishi katika miti, tazama picha juu, na Goromoe ni mijusi wanaishi katika miamba au mchanga, tazama picha chini.

Kumjua Lumbwi ni mnyama gani fungua hapa >> Lumbwi ni nini katika biblia?

Viumbe hawa, Bwana Mungu aliagizwa wasiliwe katika Agano la kale, si kwasababu vilikuwa na sumu au madhara katika mwili, bali vilikuwa vimebeba tabia zinazowakilisha tabia za  jamii/ aina Fulani ambayo haikuwa inampendeza Bwana Mungu.

Na tulipoingia katika Agano jipya hakuna sheria tena ya kula au kutokula wanyama hao, maadamu hawana sumu kwenye mwili.

Kwahiyo Guruguru na Goromoe ni halali kuliwa kibiblia , ingawa si chakula kifaacho sana kwa jamii zote, ikiwa na maana kuwa kama ukiona havikufai vitu hivyo pia si dhambi kutovila, ingawa ni halali kuliwa.

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Lumbwi ni nini katika biblia?

Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Mafundisho maalumu Kwa ajili ya watumishi wa Mungu.

Huu ni mwendelezo wa mafundisho maalumu Kwa ajili watumishi wa Mungu, ikiwa wewe ni Mchungaji, mwalimu, mtume, askofu,Nabii, au mtu yoyote unayemtumikia Mungu katika nafasi yoyote kanisani au kwenye huduma basi mafundisho haya yatakufaa sana.

Wakati ule Yakobo alipodhamiria kwenda kukutana na ndugu yake Esau baada ya kutengana naye Kwa muda mrefu..maandiko yanasema walifurahi sana walipoonana kule nyikani. Na baada ya mazungumzo Yale kuisha,  sasa ikiwa ni wakati wao wa kuondoka pale nyikani walipokutana waelekee Kaanani.

Na kama tunavyosoma habari tunaona ndugu yake Esau alimshurutisha wasafiri pamoja naye. Ndipo Yakobo akamwambia Esau kuwa jambo hilo ni gumu kwake..kwasababu ya Hali ya makundi mbalimbali na watu na mifugo aliyokuwa nayo..Tusome..

Mwanzo 33:12-17

[12]Kisha Esau akamwambia, Twende zetu, tusafiri, nami nitakutangulia.

[13]Akamjibu, Bwana wangu anajua ya kuwa watoto ni wachanga, tena kondoo na ng’ombe nilio nao wanyonyesha. Hao wanyama wakiharakishwa siku moja, watakufa wote.

[14]Tafadhali bwana wangu na apite mbele ya mtumwa wake; nami nitawaongoza polepole kwa kadiri ya mwendo wa wanyama walio mbele yangu, na kwa kadiri ya mwendo wa watoto, hata nitakapofika kwa bwana wangu huko Seiri.

[15]Esau akasema, Nikuachie, basi, baadhi ya watu walio pamoja nami. Akasema, Pana haja gani? Na nione kibali tu machoni pa bwana wangu.

[16]Basi Esau akarudi siku ile ile akishika njia yake mpaka Seiri.

[17]Yakobo akaendelea mpaka Sukothi. Akajijengea nyumba, akawafanyia makundi yake vibanda. Kwa hiyo jina la mahali pale pakaitwa Sukothi.

Ni nini cha kujifunza hapo?

Yakobo alilitambua kundi analolichunga, alijua kuwa wapo watoto wachanga ndani yake, na mifugo pia michanga, Ambayo haijazoezwa kupelekwa mkiki mkiki, kwani ikilazimishwa kufanywa hivyo itakufa yote njiani. Hivyo akaomba muda wa kusafiri wake uongezwe, kusudi kwamba ayakokote taratibu taratibu mpaka yatakapofika kule Shekemu alipokuwa anapakusudia. Pengine mwendo wa siku moja tu ikamgharimu mwezi.

Tofauti na Esau yeye alikuwa na watu wa vita tu,watu walio hodari, Lakini Yakobo alikuwa na makundi yote. Na hivyo kwenda nayo taratibu taratibu ilimgharimu .

Hii ni kutufundisha asili ya msimamizi wa kweli, kwanza hulijali kundi lake, pia anakuwa tayari kuchukuliana na vile vyombo dhaifu. Kwasababu sio wote katika kanisa watakuwa na mwendo kama wa kwao, SI wote watakuwa wepesi kustahimili vishindo kama baadhi yao. Hivyo wewe kama kiongozi ni lazima ujifunze kuendana na makundi yote kama Musa kule jangwani, ili kisipotee chochote. Maana yake ni kuwa usiwe na haraka ya kufikisha kundi Mahali Fulani Kwa jinsi utakavyo, vinginevyo utawaua wengine.

Yakobo alipaita mahali pale Sukothi, kwasababu ndipo alipowajengea makundi yake vibanda. Na wewe pia jenga Sukothi yako.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

MAFUNDISHO YA NDOA.

MIGAWANYO MINNE (4), YA HUDUMA YA YESU.

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Rudi nyumbani

Print this post

Tatizo la kuvimba miguu kibiblia

Biblia inasema nini kuhusiana na kuvimba miguu na miguu kuuma?

Kama miguu imevimba na hujui chanzo, wala madaktari hawaoni tatizo…basi huenda ni Mungu anataka kusema na wewe jambo, ambalo ukilirekebisha basi tatizo hilo linaweza kukuisha moja kwa moja..

Hebu tusome maandiko yafuatayo katika biblia..

Nehemia 9:19  “hata hivyo wewe kwa wingi wa rehema zako hukuwaacha jangwani; NGUZO YA WINGU haikuwaondokea wakati wa mchana, ili kuwaongoza njiani; wala NGUZO YA MOTO haikuondoka wakati wa usiku, ili kuwapa mwanga na kuwaonyesha njia watakayoiendea. 

20 Ukawapa na roho yako mwema ili kuwaelimisha, wala hukuwanyima mana vinywani mwao, tena ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.

21 Naam, muda wa miaka arobaini uliwaruzuku jangwani, wasihitaji kitu; nguo zao hazikuchakaa, wala MIGUU YAO HAIKUVIMBA

Wana wa Israeli walipokuwa jangwani, Nguzo ya Wingu, Na nguzo ya Moto ambayo ni ufunuo wa ROHO MTAKATIFU juu yao, ambaye aliwaongoza kama ROHO MWEMA, katika njia yao..

Ikiwa na maana kuwa njia waliyokuwa wanaiendea ilikuwa ni njia sahihi waliyoongozwa na Roho wa Mungu ndio maana miguu yao HAIKUVIMBA!, lakini wangeenda njia nyingine tofauti na hiyo ya Roho Mwema, basi ni wazi kuwa miguu yao Ingevimba, hata kama wangekuwa hawatembei, wamekaa tu, bado ingevimba.

Kwahiyo na wewe kama unaona miguu yako imevimba, na hujui chanzo na wala huoni dalili ya kupona, huenda upendo wa Mungu unakukumbusha kuwa umtafute Roho Mtakatifu, kwani yeye ndiye atakayeyaongoza maisha yako ya kiroho, maumivu hayo ni ishara ya upendo wa Mungu kwako kutaka kukupa zawadi ya Roho wake Mtakatifu, akuongoze katika njia sahihi.

Sasa utampataje Roho Mtakatifu?

Utampata kwa kanuni ifuatayo..

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39  Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.

40  Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.

Tubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, kisha tafuta ubatizo sahihi na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TATIZO LA VISIGINO KUUMA KIBIBLIA

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

HUNA SHIRIKA NAMI.

Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?

Vihekalu vya fedha vya Artemi vilikuwaje? (Matendo 19:24).

MWANAMKE, BINTI, MAMA ( Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post

Vihekalu vya fedha vya Artemi vilikuwaje? (Matendo 19:24).

Jibu: Turejee

Matendo 19:24 “Kwa maana mtu mmoja, jina lake Demetrio, mfua fedha, aliyekuwa akifanya vihekalu vya fedha vya Artemi, alikuwa akiwapatia mafundi faida nyingi”.

Mahekalu yalikuwa ni majengo maalumu kwaajili ya ibada za miungu.. Lilikuwepo hekalu moja tu duniani la Mungu wa kweli, ambalo lilitengenezwa Yerusalemu, hilo pekee ndilo Mungu wa kweli wa mbingu na nchi alikuwa akiabudiwa ndani yake kipindi cha agano la kale. Lakini mahekalu mengine yote yaliyojenga tofauti na hilo yalikuwa yanamuabudu shetani kupitia sanamu.

Sasa kipindi Mtume Paulo na wanafunzi wengine wamefika mji wa Efeso, walikuta jamii ya watu wa pale wanamwabudu mungu mke waliyemwita Artemi.

Na katika huo mji wa Efeso walikuwa wamemtengenezea Hekalu kubwa, na ndani ya hilo hekalu kulikuwa na sanamu ya huyo mungu mke, Artemi ambayo wanaamini haikutengenezwa na mtu bali ilishushwa/ilianguka kutoka mbinguni (jambo ambalo halikuwa la kweli). Na watu kutoka pande zote za dunia walikuwa wanakuja hapo Efeso lilipo hekalu la huyo Artemi kumwabudu..

Matendo 19:35 “Na karani wa mji alipokwisha kuwatuliza watu, akasema, Enyi wanaume wa Efeso, ni mtu gani asiyejua ya kuwa mji wa Efeso ni mtunzaji wa HEKALU LA ARTEMI, aliye mkuu, NA WA KITU KILE KILICHOANGUKA KUTOKA MBINGUNI?”.

Sasa kwasababu walikuwa wanamwamini huyo mungu waliyemwita Artemi kuwa ni mkuu na aliye na wafuasi wengi, wale wageni walikuja kutoka mataifa ya mbali walipata changamoto ya kumwabudu wakiwa makwao (huko katika mataifa yao ya mbali),

Hivyo ili kutatua hiyo changamoto..baadhi ya mafundi waliokuwepo pale Efeso wakaanza biashara ya kutengeneza vijihekalu vidogo vidogo vinavyobebeka vinavyofanana kabisa na lile hakalu lenye sanamu ya huyo Artemi, ili watu wanaotoka mbali wakiisha kumwabudu wakiwa Efeso waweze kuondoka na vijihekalu hivyo na kwenda navyo huko walikotokea na kuendeleza ibada zao, ambapo wengine waliviweka kwenye vyumba vyao, wengine katika vimilima na sehemu mbali mbali.

Vihekalu hivyo vilitengenezwa kwa madini ya “fedha”, ambapo mafundi wakiongozwa na fundi mkuu aliyeitwa Demetrio waliyeyusha madini hayo ya fedha na kuyatengeneza kwa muundo wa hilo hekalu.

Lakini Paulo pamoja na wanafunzi wengine wa Bwana walijua uongo huo wa shetani, na hivyo walipoingia huo mji wa Efeso waliupindua kwa injili ya kweli, na wengi wakamwamini Mungu wa kweli na kumpokea Yesu na kuacha ibada hizo za miungu, ambayo nyuma yake ni shetani anaabudiwa.

Ukisoma mistari ya juu utaona matokeo ya injili ile iliwafanya maelfu ya watu waache uchawi waliokuwa wanaufanya, na kumgeukia Mungu.

Matendo 19:18  “Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao.

19  Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu.

20  Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu”.

Na hata sasa uweza wa Mungu upo,  Injili ya Kristo ina nguvu nguvu kuliko uchawi!. Sawasawa na Warumi 1:16 “Kwa maana siionei haya Injili kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia”.

1Wakorintho10:4-5 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;

6  tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”

Usiionee haya (aibu) injili.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

Rudi nyumbani

Print this post

TAA YA MWILI NI JICHO,

Karibu tujifunze biblia,

Mathayo 6:22  “Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.

23  Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa na giza. Basi ile nuru iliyomo ndani yako ikiwa giza; si giza hilo”

Umewahi kujiuliza ni kwa namna gani “Jicho” limefananishwa na “Taa ya mwili”?

Siku zote taa ikiwa inaangaza basi nyumba yote inakuwa na Nuru na ndipo vitu vyote vilivyomo ndani vinaweza kuonekana, lakini ikizima nyumba yote inakuwa giza na hakuna kitakachoonekana.

Hali kadhalika na jicho likiwa halioni, au likiwa limefumbwa basi kinachoonekana ni giza, huwezi kuona chochote, huwezi kuona mikono yako, wala miguu yako, wala kiungo kingine chochote, huwezi kuona mbele wala nyuma wala kitu kingine chochote. Kwa ufupi unakuwa ni kipofu!. Hayo ni matokeo ya jicho kuharibika!.

Sasa Bwana Yesu analinganisha Nuru iliyopo ndani yetu na jicho.. Kwamba Nuru iliyopo ndani yetu, kazi yake ni kutuongoza njia, kama vile Jicho linaloona linavyoongoza njia na kuusaidia mwili wote kusonga mbele,  vile vile Nuru iliyopo ndani yetu kazi yake ni kuongoza maisha yetu katika njia sahihi.

Sasa Nuru iliyopo ndani yetu au inayopaswa iwe ndani yetu ni nini?.

Mathayo 5:16 “Vivyo hivyo NURU YENU NA IANGAZE mbele ya watu, wapate kuyaona MATENDO YENU MEMA, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.

Umeona hapo?.. kumbe Nuru ni “Matendo yetu mema” .. kwamba matendo yetu yanapokuwa mema, basi ni sawa na macho yanayoona!.. Kumbe matendo yetu yakiwa mabaya sisi ni sawa na vipofu!, wala hatujui tunapokwenda!…kama Bwana Yesu alivyosema katika…

Mathayo 15:14  “Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili”.

Je unataka kuona mambo yaliyopo mbele yako? na njia unayoielekea? kama ni salama?.. je! Unataka kuona hatari inayokuja na kuepukana nayo?.. Basi fanya matendo mema!!…usiende kwa waganga wala wasoma nyota wala manabii, wewe yasafishe matendo yako tu!, na utaona mambo yajayo!..

Hiyo ndio siri nyingine iliyopo nyuma ya “Matendo yetu mazuri”.. sio tu yanaupendeza moyo wa Mungu na kutupa baraka.. bali pia yanatuongoza na kutufanya tuone mambo yajayo (yaliyopo mbele yetu).

Na unayasafishaje matendo yako?.. Si kwa nguvu zako bali kwa Neema iliyopo ndani ya damu ya Yesu, ambayo hiyo inakuja kwa njia ya kutubu dhambi na kumaanisha kuziacha pamoja na kupata ubatizo sahihi..

Hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukupa uwezo wa wewe kufanya matendo yampendezayo Mungu, na hivyo macho yako ya kiroho yatakuwa angavu… Utakuwa na uwezo wa kuona hatari zilizopo mbele yako na kuepukana nazo, utakuwa na uwezo mkubwa wa kuona hasara zilizopo mbele yako na kuzikwepa, utakuwa unauwezo wa kuona mema yaliyopo mbele yako na kuyafuata na vile vile utakuwa na uwezo wa kuona hatari inayokufuata nyuma yako n.k

Lakini kanuni ni hiyo moja tu!..Ifanye Nuru yako (matendo yako) yaangaze!

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TWAENENDA KWA IMANI NA SI KWA KUONA.

Kama ulimwengu ujao utakuwa na watakatifu tu, sasa hao watakaotawaliwa watatoka wapi?

RUHUSU TOHARA IPITE JUU YA KARAMA YAKO.

ITII SAUTI ILIYOPO NYUMA YA KILA ISHARA YA MUNGU!

LAKINI MAKINDA WAWEZA KUYATWAA UWE NAYO.

Rudi nyumbani

Print this post

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

Wivu ni nini kibiblia na kuna aina ngapi za Wivu unaowapata watu? Na je ni dhambi kuwa na Wivu?

Katika kitabu cha Wagalatia biblia imetaja “Wivu” kuwa ni mojawapo ya tunda la mwili. Sasa swali ninapopata wivu wa kimaendeleo nafanya dhambi? Au ninapopata wivu wa mwanandoa mwenzangu kukosa uaminifu je nayo ni dhambi?


Jibu: Tusome,

Wagalatia 5:19-21
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi..

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira……….. ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”

Ni kweli Wivu ni mojawapo wa matendo ya mwili ambayo ni dhambi mtu kuwa nayo, lakini kama ya kuingia ndani zaidi katika andiko hili..ni vizuri kuzijua kwanza aina za wivu..

Upo “Wivu wa kiMungu” na vile vile upo “wivu wa kidunia”, ni kama tu “hasira” au “hofu”. Ipo hasira ya kiMungu na vile vile ipo hasira ya kidunia au ya kiulimwengu.

Hasira ya kidunia ni ile inayoyoishia au inayompelekea mtu kutenda dhambi, kama kutukana, kuua, kuonea, kuiba n.k.. kwaufupi matunda yake ni mabaya daima… Lakini hasira ya kiMungu ni ile inaiyoishia katika kumjenga mtu na kumtengeneza zaidi, na kumrudisha kwa Mungu au katika njia sahihi kwa upendo.

Mfano wa hasira ya kiMungu ni ile Bwana Yesu aliyokuwa nayo juu ya Mafarisayo na Masadukayo.
Utaona Mafarisayo na Masadukayo walikuwa wanamwudhi sana Bwana lakini hasira ya Bwana haikuishia katika kuwatukana, au kuwashushia moto na kuwaangamiza ingawa alikuwa na uwezo huo, au kuwaharibu kwa njia yoyote ile… bali katika kuwahurumia..

Marko 3:1-5 “Akaingia tena katika sinagogi; na palikuwako huko mtu mwenye mkono uliopooza;

2 wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato; wapate kumshitaki.

3 Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, Simama katikati.

4 Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza.

5 AKAWAKAZIA MACHO PANDE ZOTE KWA HASIRA, AKIONA HUZUNI kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena”.

Hasira ya namna hii biblia imesema tuwe nayo ila tusitende dhambi, jua lisizame tukiwa nayo bado mioyoni..(Waefeso 4:26).

Sasa tukirudi katika Mantiki ya hofu na wivu ni hivyo hivyo, ipo hofu ya kiMungu na ya ipo hofu ya kidunia, vile vile upo wivu wa kiMungu na upo wivu wa kidunia.
Wivu wa kidunia ni ule unaoishia kutenda dhambi.. Mfano mtu atamwonea mwingine wivu kwasababu kapata kitu fulani ambacho yeye hajakipata, hivyo atatamani au atatafuta njia yule mtu akipoteze kile kitu ndipo atulie.

Mfano wa wivu huu ni ule aliokuwa nao Kaini, alipoona sadaka ya ndugu yake imekubaliwa na kwake imekataliwa. Badala atafute njia ya kuboresha sadaka yake ikubalike mbele za Mungu kama ya ndugu yake, yeye akatafuta kumwua ndugu yake, (wivu unaoish kuleta chuki, masengenyo, vinyongo, visasi ni wa kishetani)..ambao ni dhambi mtu kuwa nao sawasawa na hiyo Wagalatia 5:20.

Wivu wa kiMungu ni ule unaomfanya mtu atamani kuwa mwema kama mwingine alivyo mwema, unaomfanya mtu atamani kufanya vizuri kama mwingine anavyofanya vizuri pasipo kumtakia madhara yule mwingine, (kwa ufupi haufurahii kuanguka wala kupunguka kwa mwingine)..zaidi sana mafanikio ya mwingine yanakuwa siku zote ni darasa kwake….

Wivu huu sio mbaya na si dhambi mtu kuwa nao, kwasababu matunda yake ni mazuri..
Mfano wa huu ni ule Mtume Paulo, aliojaribu kuutia kwa ndugu zake Waisraeli ili wamgeukie Mungu zaidi.

Warumi 11:14 “nipate kuwatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao”.

Lakini pia upo Wivu mwingine wa KiMungu ambao unaishia kuharibu vitu vya kishetani lakini si kimharibu mtu..

Mfano wa wivu huu ni alikuwa nao Bwana Yesu juu ya Hekalu la Mungu, alipoingia na kukuta watu wanafanya biashara ndani ya hekalu, maandiko yanasema Bwana alizipindua meza zao, na kuharibu biashara zao lakini si kuwaharibu wao.. Na wanafunzi wake wakakumbuka andiko la wivu wa nyumba ya Mungu utamla (Yohana 2:17).

Wivu huu pia na sisi tunapaswa tuwe nao tunapoona kazi ya Mungu inachafuka, ni lazima tusimame kuziharibu hizo kazi za shetani kwa maombi na kwa mafundisho sahihi, lakini si kwa kuwadhuru watu au kuwatukana, au kuwaletea madhara yoyote ya kimwili.

Wivu wa namna hii pia upo katikati ya wanandoa na wanafamilia, kama kuna kiashiria chochote cha mwanandoa au mwanafamilia kutoka kwenye mstari wa uaminifu, au nidhamu, au maadili au heshima…Wivu wa namna hii huwa unanyanyuka!, sasa vibaya yule aliyemwaminifu, au aliye imara katika ndoa au familia kusimama na kuharibu au kuziba upenyo wowote ambao shetani anataka kuchukua nafasi ndani ya hiyo familia au ndoa…lakini kwa hekima pasipo kumdhuru mtu.

Lakini wivu wa wanandoa au wanafamilia unaoishia kuua huo hautokani na Mungu!.

Je na wewe unasumbuliwa na dhambi ya Wivu wa kidunia ambao unaishia kusengenya, kuona hasira, kuua, kutukana n.k Na hujui utatokaje katika hilo shimo?.

Bwana Yesu amekuja kwaajili ya kututoa katika hayo mashimo, kwa nguvu zetu hatuwezi kutoka huko wala kujitoa.
Nguvu pekee ya kututoa huko ni kwa njia kwa ya Roho Mtakatifu, kwa somo kamili kuhusiana na Roho Mtakatifu, jinsi ya kumpomea na jinsi.atakavyokuwezesha kushinda yale usiyoweza kuyashinda basi tutumie ujumbe inbox ili uweze kupata somo hilo.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JIHADHARI NA DHAMBI YA WIVU/HUSUDA.

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

MWE NA HASIRA, ILA MSITENDE DHAMBI.

USHUJAA WA ROHONI HAUANGALII UZOEFU WAKO.

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?

Mambo ya Walawi 11:9-12

[9]Katika hao wote walio ndani ya maji mtakula hawa; kila aliye na mapezi na magamba, ndani ya hayo maji, na ndani ya bahari, na ndani ya mito, mtakula hao.

[10]Na hao wote wasio na mapezi na magamba, ndani ya bahari, na ndani ya mito, katika hao waendao majini, na katika wote wenye uhai, waliomo majini, hao ni machukizo kwenu,

[11]watakuwa machukizo kwenu; msiile nyama yao, na mizoga yao itakuwa machukizo kwenu.

[12]Kila asiye na mapezi wala magamba aliye ndani ya maji ni machukizo kwenu.

Mapezi ya samaki, ni vile vitu kama mbawa ngumu zenye mfano wa miiba  zinazokaa Kwa juu, au pembeni au nyuma mwa mwili wa samaki.Ukitazama samaki kama perege, sato au sangara utaona mapezi Yao.Na faida za mapezi hayo ni kuwa yanasaidia kuogelea, kuelea vema kwenye maji, kukunja Kona, kuongeza kasi na kusimama au kugeuka Kwa haraka.

Halikadhalika samaki waliokuwa na magamba ndio tu walioruhusiwa kuliwa. Na magamba yaliwasaidia kujilinda na maadui au wadudu wavamiaji kwenye mwili. Kwani ngozi ya samaki ni laini hivyo isipofunikwa na magamba magumu kama yale, meno makali ya maadui yanapopita ni rahisi kujeruhiwa, Yanakaa kama dirii kifuani mwa askari.

Lakini si samaki wote walikuwa na haya mapezi na magamba, Bali wengine hawakuwa nayo mfano wa Hawa ni kama kambale, papa, pomboo, pwezi.

Sasa Kwanini viumbe hivyo vikatazwe kuliwa na ufunuo wake ni upi Rohoni?

Kama tunavyofahamu agano la kale ni kivuli Cha agano jipya, sio kwamba viumbe hivyo vikiliwa vitamkosesha mtu mbingu, au vitamnajisi roho , hapana. Bali vilifanywa vile kwa makusudi ili kutupitishia sisi ujumbe wa Rohoni katika agano letu jipya. Kwamba na sisi kama tutafanana na mojawapo wa viumbe hivyo Rohoni basi tunakuwa najisi mbele za Mungu.

Samaki mwenye magamba ni mwenye ulinzi wa kutosha dhidi ya mashambulizi ya maadui. Na sisi tunapokosa ulinzi wa Rohoni mfano wa yule askari anayezungumziwa katika Waefeso 6, mwenye dirii ya haki kifuani, ngao ya Imani mkononi na chepeo ya wokovu kichwani. Tunakuwa ni wadhaifu, kiasi Cha kutoweza simama mbele ya adui yetu shetani. Hivyo ni kuhakikisha kuwa umesimama imara katika wokovu wako, lakini pia utambue haki uliyopewa katika  msalaba wa Yesu Kristo na Imani Yako timilifu ndani ya wokovu wako. Hapo utakuwa umejidhatiti vya kutosha mfano wa samaki mwenye gamba gumu, au mamba aliyefunikiwa na ngozi yenye gamba.

Ayubu 41:13 “Ni nani awezaye kumbambua magamba yake? Ni nani atakayepenya dirii yake maradufu?  14 Ni nani awezaye kuifungua milango ya uso wake? Meno yake yatisha kandokando yake.  15 Magamba yake yenye nguvu ndiyo fahari yake, Yamefungamana pamoja kama kwa kufungwa kwa muhuri.  16 Jinsi yalivyoshikamana Hata upepo hauwezi kupita kati.  17 Yamefungamana pamoja; Yameshikamana, hata hayawezekani kutengwa”

Vilevile samaki aliyekuwa na mapezi alikuwa ni mwepesi kukatiza katika maji. Ni sawa na mabawa Kwa ndege, au miguu na kwa mtu. Hivyo na sisi katika ulimwengu huu wa dhambi ili tusionekane kuwa najisi tuvae mapezi yetu ambayo maandiko yanasema .Ndio ule utayari wa kuihubiri injili.

Waefeso 6:15

[15]na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

Tusienende Kama watu wasio na kusudi maalumu la kufanya duniani, tuvae utayari, ndio mapezi yetu tutembee ulimwengu kote kiuhubiri/ kushuhudia habari njema.Kwasababu tukikosa haya, siku ile ya mwisho, tutatengwa samaki wema na waovu..Kisha wale waovu watatupwa nje.

Mathayo 13:47  ‘Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;

48  hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa. 49  Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki’

Tusiwe samaki najisi.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)

Lumbwi ni nini katika biblia?

Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.

Je! Ni dhambi kumpiga au kumuua mnyama bila sababu yoyote?

Manyoyota ni nini (Ayubu 37:6)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini Maana ya Adamu?

Nini tafsiri ya jina Adamu,

Adamu ni neno la kiebrania lenye maana ya “wa udongo” yaani aliyetokana na udongo/ardhi. Mtu wa kwanza kuumbwa alipewa jina hilo Adamu na Mungu mwenyewe kufuatia asili yake alipotolewa.

Mwanzo 2:7 “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai”.

Na jina “Adamu” hakupewa mtu mmoja tu bali wote wawili (yaani mwanamume na mwanamke)

Mwanzo 5:1” Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya;

 2 mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki AKAWAITA JINA LAO ADAMU, siku ile walipoumbwa”.

Kwa urefu na kina Zaidi, kwanini Mungu awape wote wawili jina moja fungua hapa >>> Kwanini Mungu aliwaita Adamu na Hawa jina moja?

Watoto wote waliozaliwa baada ya Adamu, wakaitwa Wana-damu. (wana wa aliyekuwa wa udongo). Hivyo na sisi wote asili ya miili yetu ni ardhini, ndio maana tunakufa na miili yetu inaoza ardhini.

Lakini baada ya maisha haya, kama tukishinda vita vya kiimani vya ulimwenguni,  maandiko yanasema tutavikwa miili mipya ya kimbinguni, hivyo hatutaitwa tena wanadamu, wala hatutaishi kwa kula na kunywa kama wanyama, wala tamaa za mwili hazitakuwepo tena bali tutakuwa kama Malaika kwasababu tutapewa miili mingine isiyo ya udongo.

Marko 12:25 “Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni”.

Je una tumaini la kuvikwa mwili mpya wa kimbinguni?..

Kumbuka tumaini hilo na uhakika huo tunaupata tu endapo tupo ndani ya Kristo, na tunaishi maisha yanayompendeza yeye.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?.

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Kwanini Kristo aitwe Mwana-kondoo. (Yohana 1:29)

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

Rudi nyumbani

Print this post

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo Bwana wetu. Karibu katika kujifunza maneno ya uzima ya mwokozi wetu.

Leo tutaona jinsi “moyo wa toba ya kweli” unavyopokelewa kitofauti sana na Mungu. Kama tunavyoifahamu ile habari ya mwana mpotevu, jinsi alivyoingiwa na tamaa, ya kwenda kuanzisha maisha yake ya anasa mbali na baba yake. Na siku zilipozidi kwenda, mali zilipoisha, njaa kali ikamkuta Akaanza kula vyakula vya majalalani ambavyo viliwastahili tu nguruwe.  Lakini Biblia inasema, hakung’ang’ania tu  kuendelea kutaabika katika hali ile ile milele mpaka kufa kwake. Bali alijinyenyekeza akazingatia kurudi kwa baba yake akiwa na moyo wa toba, ili baba yake amfanye tu mtumwa. Na alipofanya vile, akiwa njiani anarudi, biblia inatumbia kuna tukio lilitokea.

Na tukio lenyewe ni “kuonekana kwake tokea mbali” . Tusome;

Luka 15:17  “Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. 18  Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; 19  sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako. 20  Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. 21  Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. 22  Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; 23  mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi; 24  kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia”

Embu tafakari, iweje, Baba yake ndio awe wa kwanza kumwona tokea mbali na sio watumwa ambao sikuzote wao ndio wanaosimama mlangoni mwa nyumba au kuzunguka zunguka huku na huko, au kwanini isiwe hata ndugu zake wengine, badala yake baba yake ndio anayekuwa wa kwanza kumwona?

Sio kana kwamba hao wengine walikuwa hawali mboga za majani, hawaoni mbali kwa macho yao kuwa hafifu, hapana, bali Baba yake alikuwa na jicho lingine la rohoni kama DARUBINI. Hilo lilikuwa linaona mahangaiko, na manyanyaso ya mwanaye tokea mbali, kiasi kwamba alipofanya geuko moyoni mwake, tayari baba yake alishahisi, na akiwa njiani anakuja tayari baba yake alishajua kuwa mwanawe yupo njiani. Hivyo kabla hata mtoto hajamwona Baba, kabla hata hajaifikia nyumba yao akiwa kilomita kadhaa mbali, tayari baba alikwenda kukutana naye na kumkumbatia na kumbusu sana.

Ndivyo ilivyo kwa Mungu wetu. Pale mtu anapokuwa na moyo wa toba ya kweli rohoni, haihitaji wewe kwenda kusema maneno mengi sana mbele za Mungu, kana kwamba ndio utasikiwa. Yeye anayo darubini yake, Lakini kule kuzingatia tu kurudi kwa Baba yako wa mbinguni, ukaanza kuchukua hatua. Hiyo ni toba kubwa sana ambayo itamfanya Mungu, kabla ya wewe kumfikia tayari ameshakufikia, haraka sana na kukupa tiba ya moyo wako, na raha nafsini mwako.

Hii ni kuonyesha kuwa toba ya kweli, ni ule moyo uliogeuka. Sio tu kuongozwa sala maalumu. Ndio tunajua sala ikiambatana na geuko ni vema sana, lakini ikiwa utasalishwa sala hizo elfu 10 halafu ndani yako, ni vilevile tu, hapo unapoteza muda wako ndugu.

Alikuwepo Yule mwanamke mwenye dhambi nyingi sana, alipokwenda kwa Bwana Yesu saa ile ile akaanza kulia akitubia dhambi zake, akidondosha machozi yake miguu pa Yesu, huku akiyapangusa kwa nywele zake. Lakini Yesu alipomwona akasema ‘Umesamehewa dhambi zako nyingi’, mwanamke Yule hakusalishwa sala yoyote.(Luka 7:36-50).

Ili Mungu afike kwako upesi, kuwa na toba ya kweli, ili upate kibali cha haraka kwa Mungu, sio wingi wa maombi yako, bali geuko la dhati. Na Bwana mwenyewe atakufikia kabla hujamfikia yeye.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

Kwanini Nuhu alimlaani Kaanani badala ya mtoto wake Hamu,

UMUHIMU WA KUISHI MAISHA YAMPENDEZAYO MUNGU SASA.

MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

Forodhani ni mahali gani?

Rudi nyumbani

Print this post

TAFUTA HEKIMA, MAARIFA, UFAHAMU NA BUSARA.

Jina la Mwokozi Mkuu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;

 11 Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi. 

Haya ni mambo manne ambayo ni muhimu sana kuwa ndani yetu.

  1. Hekima – Ni uwezo wa kupanga na kupambanua mambo
  2. Maarifa- Ni elimu au taarifa kuhusiana na jambo fulani
  3. Ufahamu- Ni hali  ya kuweza kufahamu jambo Fulani kwa kina
  4. Busara- Ni hali ya kuona mbele (yaani mambo yajayo) na kuamua lililo sahihi. Mithali 27:12

Mambo haya manne ni Bwana pekee anayeweza kuyatoa.. Mithali 2:6 “Kwa kuwa Bwana huwapa watu hekima; Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu” .

Zifuatazo ni faida kuu tatu (3) za kupata Hekima, Maarifa, ufahamu na busara.

  1. KUOKOKA NA NJIA YA UOVU.

Hii ni faida ya kwanza ya kupata Hekima, Ufahamu, busara na Maarifa; “Kumwokoa mtu na njia ya uovu”

Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;

11 Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi. 

12 ILI KUKUOKOA NA NJIA YA UOVU, Na watu wanenao yaliyopotoka; 

13 Watu waziachao njia za unyofu, Ili kuziendea njia za giza; 

14 Wafurahio kutenda mabaya; Wapendezwao na upotoe wa waovu; 

15 Waliopotoka katika njia zao; Walio wakaidi katika mapito yao”

Njia ya Uovu ni njia yoyote ile ambayo itampelekea mtu kufanya maovu, mfano wa hayo ni yale yanayotajwa katika Wagalatia 5:19-21 “uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo”.

2. KUKUOKOA NA MALAYA:

Mithali 2:16 “…Ili kuokoka na malaya, Naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake..”

Mtu aliye Malaya ni yule anayefanya uasherati aidha kwa lengo la kutafuta pesa au kujifurahisha, na hili ni neno linalotumika kuwakilisha jinsia zote mbili za watu wenye tabia hizo. Na Malaya anaweza kuwa ni mtu aliye ndani ya ndoa au nje ya ndoa.

Mtu mwenye busara (Maana yake anayeona mbele), hawezi kunaswa na mtego wa Malaya.. Mfano wa mtu aliyekuwa na busara katika biblia ambaye aliokoka na mtego wa Malaya ni Yusufu, ambaye alitegewa mtego na mke wa Potifa, lakini aliushinda mtego ule wa ibilisi.

Lakini kama Yusufu hangekuwa na Busara akilini mwake, basi angenaswa katika mtego ule wa  uasherati alipobembelezwa na mke wa Potifa, na hivyo angekuwa amejiingiza katika matatizo makubwa sana, ambayo yangehatarisha hata maisha yake ya kimwili na kiroho.. kama biblia inavyosema hapa..

Mithali 2:16 “Ili kuokoka na malaya, Naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake;

17 Amwachaye rafiki wa ujana wake, Na kulisahau agano la Mungu wake. 

18 Maana nyumba yake inaelekea mauti, Na mapito yake yanakwenda kwenye wafu. 

19 Katika hao wamwendeao harudi hata mmoja, Wala hawazifikilii njia za uzima”

Soma tena maandiko mengine yanayohusu tabia za Malaya, jinsi anavyobembeleza katika Mithali 7:7-23, Mithali 22:14 na Mithali 23:27.

Ukiona mtu kanaswa na mtego basi ni matokeo ya kupungukiwa Hekima, busara, maarifa na ufahamu.. kama biblia inavyosema katika Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake” .Kwasababu mtu aliyejaa mambo hayo hawezi kunaswa na mitego hiyo.

3. KUKUPELEKA KATIKA NJIA YA WATU WEMA

Faida ya kwanza tuliona ni “kumwokoa mtu katika njia ya uovu” lakini Hii ya tatu na ya mwisho, ambayo ni “Kukupeleka mtu katika njia ya watu wema”.. Hekima, busara, Maarifa na ufahamu haviishii tu kumwokoa mtu na njia mbaya na kumwacha hapo katikati bali pia kumpeleka/kumwongoza katika njia nzuri.

Mithali 2:20 “Ili upate kwenda katika njia ya watu wema, Na kuyashika mapito ya wenye haki.

21 Maana wanyofu watakaa katika nchi, Na wakamilifu watadumu ndani yake. 

22 Bali waovu watatengwa na nchi, Nao wafanyao hila watang’olewa”.

Watu wema wana Njia yao, wapo katika mkondo wao, si kila mahali wanapita, na hao ndio wanaodumu katika nchi, … Sasa ili kuiona hiyo njia waliyopo basi Hekima, Busara, Maarifa na ufahamu vinahitajika. Na vyote hivyo vinatoka kwa Mungu.

Sasa swali? Mtu anapataje Hekima, Ufahamu, Busara na Maarifa ili kuepukana na hayo yote, na kupata faida hizo.

Tukitaka Hekima, Maarifa, Ufahamu na Busara biblia imetupa kanuni rahisi katika kitabu cha Ayubu.

Ayubu 28:20 “Basi hekima yatoka wapi? Na mahali pa ufahamu ni wapi? 

21 Kwa kuwa imefichwa mbali na macho ya wote walio hai, Na kusitirika na ndege wa angani. 

22 Uharibifu na Mauti husema, Tumesikia habari zake kwa masikio yetu. 

23 Mungu ndiye aijuaye njia yake, Naye anajua mahali pake. 

24 Maana anatazama hata miisho ya nchi, Na kuona chini ya mbingu nzima. 

25 Apate kuufanyia upepo uzito wake; Naam, anayapima maji kwa kipimo. 

26 Hapo alipoiwekea mvua amri, Na njia kwa umeme wa radi. 

27 Ndipo alipoiona na kuitangaza; Aliithibitisha, naam, na kuichunguza. 

28 Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, KUMCHA BWANA NDIYO HEKIMA, NA KUJITENGA NA UOVU NDIO UFAHAMU”.

Kumcha Bwana na kuepukana na Uovu ndio chanzo cha Hekima, maarifa, busara na ufahamu.

Maana yake Jishughulishe sana na masuala ya kiMungu sana, Jifunze Neno la Mungu, kusanyika na wengine katika maombi, ibada na kufanya uinjilisti na mambo mengine yote yanayofanana na hayo, kwa kufanya hivyo ndivyo Hekima, na hayo mambo mengine yatakapoingia ndani yako na kujaa.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.

Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)

Nini maana ya “Mwenye hekima huvuta roho za watu”

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?

Rudi nyumbani

Print this post