JIBU: Neno jinsia kwa mara ya kwanza limeonekana kwa wanadamu, Pale Mungu alipomtoa Hawa ubavuni mwa Adamu na kumwita jina lake mwanamke, hapo ndipo jinsia mbili zilipozaliwa yani ya kike na ya kiume, Hapo kabla Adamu alikuwa ni mwanadamu mwenye maumbile yote ndani yake, yaani ya kike na ya kiume,sasa siku alipotolewa ubavu wake, ile sehemu ya uzuri iliondolewa na kuumbwa mwanamke yeye akawabakiwa na ile sehemu ya misuli tu.
Hivyo tukirudi kwa upande wa malaika,ni kwamba suala la malaika wa kike, au wa kiume hilo halipo, japo biblia inawatambulisha kwa vyeo vya kiume, hata majina yao Mikaeli, Gabrieli, n.k yote hayo ni majina yenye asili ya kiume, hata Mungu wetu naye anachukua cheo cha kiume, tunamwita Baba japo yeye sio mwanaume, wala mwanamke.Ni kwanini basi wanatambulika kama wanaume na si wanawake, Ni kwasababu jinsia ya kiume ni jinsia inayoonyasha ukuu, na uweza, na mamlaka, na kutawala kuliko ile ya kike, na hivyo ili kuonyesha kuwa mbingu ndio inayotawala dunia hivyo kulikuwa hakuna budi, viumbe vyote vya kimbinguni vitambulike kwa jinsia ya kiume, ikiwemo Mungu wetu mwenyewe.Mkuu ya vyote.
Laiti kama pale mwanzo Adamu ndiye angetoka kwa Hawa, Na mwanamke angekuwa ni kichwa cha vyote dunia basi mbingu nayo ingejitambulisha kwetu kwa vyeo na majina ya KIKE..Kuna watu wanaosema, wapo malaika wa kike na wa kiume, na ndio maana kipindi kile cha Nuhu walishuka baadhi wakajitwalia wake na wanadamu na hivyo kuzaa yale majitu/wanefili (Mwanzo 6).
Lakini huo mtazamo sio wa kimaandiko, kwani Bwana Yesu anatuambia tutakapokwenda mbinguni tutafanana na malaika hakuna kuoa wala kuolewa. (Marko 12:25). Kuonesha kuwa malaika hawana jinsia, tulizonazo sisi, viungo vya uzazi viliwekwa kwa lengo la kuzaliana kujiaza nchi, na si kwa jambo lingine.Vile vile na sisi je! tutakapokwenda mbinguni tutafanana wote?. Jibu ni hapana, Mungu alishamaliza kumuumba mwanaume na mwanamke, hivyo kama wewe ni mwanaume utakuwa na asili ya uanaume milele katika huo mwili wa utukutu utakaopewa, na kama wewe ni mwanamke vilevile utakuwa na asili ya uanawake milele katika huo mwili wa utukufu utakaopewa, isipokuwa tu katika masuala ya uzazi ndio tutafanana na malaika..hakuna kuzaa wala kuzaliana,wala kuoa au kuolewa.
Lakini maumbile yetu, yatakuwa kama yetu wenyewe, na malaika kama yao wenyewe kwa jinsi walivyoumbwa na Mungu.
Ubarikiwe sana.
Mada Nyinginezo:
KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.
JE! BAADA YA ULIMWENGU HUU KUISHA MALAIKA WATAKUWA NA KAZI GANI TENA?
KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.
NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?
USIWE SABABU YA WATU KUMKUFURU MUNGU.
SWALI: Mstari huu una maana gani? “yuko mwenye haki apoteaye katika haki yake, yuko na mtu mwovu azidishaye maisha yake katika udhalimu wake.(Mhu 7:15)”
JIBU: Shalom,Tukianza na mstari wa 15 anasema:
“Mambo hayo yote nimeyaona mimi katika siku za ubatili wangu, yuko mwenye haki apoteaye katika haki yake, yuko na mtu mwovu azidishaye maisha yake katika udhalimu wake.
Huyu ni Sulemani akizungumza maneno hayo, anasema akiwa katika siku za UBATILI wake, yaani akiwa katika siku za masumbuko yake ya kutafuata jumla ya mambo yote, alikutana na Fumbo moja ambalo lilimtatiza sana, na Fumbo lenyewe ndio hili “yuko mwenye haki apoteaye katika haki yake, yuko na mtu mwovu azidishaye maisha yake katika udhalimu wake”. Au kwa lugha nyingine iliyorahisi ni kusema wenye haki wengi hawaishi muda mrefu, lakini wale waovu ndio wanakuwa na maisha marefu. Aligundua Kumbe haki haipimwi kwa kipimo cha umri mrefu mtu anaoishi. Fumbo hili linafanana na lile lingine alilolisema katika:
Mhubiri 9: 11 “Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.”
Hata wewe mambo haya yatagonga kwenye kichwa chako lakini huo ndio uhalisi, Ni mara ngapi unasikia na kutazama wale watu ambao hawana elimu,wala hawana ujuzi tena kama wamefika mbali sana, wengine labda ni darasa la 7 lakini hao ndio wanaokuwa matajiri sana? . Hili ni funzo kwako ikiwa utatafuta ujuzi au elimu kwa kigezo cha kuwa bilionea, utavunjika moyo , vilevile ikiwa unautafuta ufalme wa mbinguni ili uje upate utajiri kwa sadaka, kadhalika utavunjika moyo sana! Au leo hii unaokoka ili mambo yako ya kiuchumi yakae vizuri, yaani hiyo ndio sababu ya wewe kuokoka.. unajeweka katika hatari kubwa ya kuvunjika moyo huko mbeleni…Hekima na wokovu havina ushirika na pesa kabisa.. Tukiendelea na mistari unaofuata anasema ..
Mhubiri 7: 16 “Usiwe na haki kupita kiasi; Wala usijiongezee hekima mno; Kwani kujiangamiza mwenyewe?
17 Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwani ufe kabla ya wakati wako?
18 Ni vizuri kwamba ulishike neno hilo; naam, hata kwa neno hilo tena usiuondoe mkono wako; kwa kuwa mtu yule amchaye Mungu atatoka katika hayo yote.”
Kuna mambo mawili hapo la kwanza usiwe na haki kupita kiasi na pili usiwe mwovu kupita kiasi, yote haya yanaweza kukusababishia kifo ambacho hakijafikia umri wake. Lakini nataka upigie mstari jambo moja hapo la msingi hasemi usiwe na haki au usiwe na hekima, hapana bali anasema usiwe na haki KUPITA KIASI wala usiwe na HEKIMA KUPITA KIASI, hii inafunua tabia ya kujikweza, kujionyesha kuwa wewe ni kitu Fulani, wewe ni mtakatifu kuliko wengine, mifano dhahiri ya matukio kama haya tunayo, tunaweza kuyaona si kwa wengine zaidi ya waandishi na mafarisayo.. Ukisoma Luka 18:10-14 utaona Bwana Yesu alitoa mfano huu….
“Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.
11 Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.
12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.
13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.
14 Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.
Unaona, walijihesabia haki kupita kiasi, kufunga kwao, kutoa kwao zaka,kutokuzini kwako, ndio kulikowapa kiburi wajione wao ni kundi fulani maalumu mbele za Mungu na hiyo iligeuka kuwa hasara kwao kwa kuupoteza wokovu ambao wao ndio wangetakiwa waupate wakwanza.. Hivyo kama tukiangalia maudhui ya huyu mhubiri hasaa yalikuwa ni kutaka kuonyesha kuwa, sio mwenye haki, sio mwovu, sio mwenye hekima kupita kiasi sio mpumbavu anaweza kujiongeza maisha kwasababu ya mwenendo wake. Na ndio maana anahitimisha kwa maneno haya “18 Ni vizuri kwamba ulishike neno hilo; naam, hata kwa neno hilo tena usiuondoe mkono wako; KWA KUWA MTU YULE AMCHAYE MUNGU ATATOKA KATIKA HAYO YOTE.”” Unaona, ukimcha Bwana utaepukana na hayo yote, Kumcha Bwana ni kujinyenyekeza mbele za Mungu kwa kuitii injili yake na maagizo yake yote anayokupa kwa kufanya hivyo basi utapata hekima iliyo sahihi ya kumwendea mbele zake..Ndio mhubiri maana huyo huyo anasema kumcha Bwana ndio chanzo cha hekima na maarifa, Na sio hekima ndio chanzo cha kumcha Bwana.
Hivyo leo hii mtu Yule atakayekubali kumtii Kristo na kuyaishi maneno yote aliyoyasema atakuwa na uhakika kuwa amesimama upande ulio salama. Lakini ukiwa mtu wa dini(kama mafarisayo na waandishi, ambao wao wanajiona wao tu ndio wanao Mungu wengine wote ni waovu, Na hiyo inawafanya hata hatawaki kusikia jambo lingine lolote, mfano tu leo, hata mtu umwelezeje kwamba biblia inasema hivi, maadamu tu dhehebu lake au dini yake halifundishi hivyo au haliamini hivyo basi hakusikilizi,..huko ni kujihesabia haki kupita kiasi biblia inakokukataza), Na ukiwa pia mwovu, mambo hayo mawili basi jua utakumbana na mauti (rohoni na mwilini).
Ubarikiwe.
Mada Nyinginezo:
MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.
USIMFANYIE JEURI ROHO WA NEEMA.
KWANINI BWANA YESU ALISEMA PALE MSALABANI NAONA KIU?
KUCHEZA KARATA NI SAHIHI KWA MTU ALIYE MKRITO?
Swali: Je hizi lugha ni zipi, na je! ni lazima kila mkristo aliyepokea Roho Mtakatifu anene kwa lugha mpya
JIBU: Hili ni moja ya jambo linalowachanganya wengi sana, Na nilinichanganya hata mimi pia kwa muda mrefu, na lingine linalofanana na hili ni juu ya uthibitisho halisi wa mtu kuwa amepokea Roho Mtakatifu ni upi?..
Lakini napenda ufahamu kuwa tukiweza kutofautisha kati ya hivi vitu viwili yaani “vipawa vya Roho Mtakatifu” na “Roho Mtakatifu” mwenyewe tutaweza kuondoa huu utata kwa sehemu kubwa sana.. Biblia inasema Kunena kwa lugha ni moja ya karama ya Roho Mtakatifu kama zilivyokarama nyingine, mfano Unabii, miujiza, uponyaji, ualimu, uinjilisti n.k. Lakini hatutaenda sana huko turudi kwenye msingi wa swali letu linalouliza juu ya Kunena kwa Lugha. Tukirudi nyuma kidogo kabla siku ile Bwana Yesu kupaa, aliorodhesha baadhi ya ishara ambazo zitaambata na wale wote waliomwamini na mojawapo ya ishara hizo alisema watanena kwa lugha mpya.
Marko 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.
Sasa Neno “Lugha mpya”, ni Neno lisilo na mipaka (Halifungiki), yaani kwa ufupi Lugha yoyote usiyoijua wewe ukiinena kwako ni Lugha mpya, iwe ni ile iliyopo katika nchi yako, au nje ya nchi yako, au iwe ya ulimwengu huu au sio ya ulimwengu huu maadamu hauitambui bado kwako ni Lugha mpya. Hivyo ukisoma maandiko utaona ulikuwa ni mpango wa Roho Mtakatifu tangu zamani, kuwa utafika wakati atazungumza na watu wote wa ulimwenguni kwa lugha tofauti, unabii huo unaweza kuusoma katikaIsaya 28: 11 “La, bali kwa midomo ya watu wageni, na kwa lugha nyingine atasema na watu hawa;”Sasa utagundua kumbe lengo la kwanza Roho Mtakatifu kusema kwa lugha gheni katikati ya watu ni ili kuwavuta kwake wamwamini.
Hapa ni lazima atumie lugha za kibinadamu, Mfano dhahiri ni kile kilichotokea Siku ile ya Pentekoste, Walijikuta wote wanazungumza Lugha za mataifa mengine ya mbali na wale waliokuwa wanasikia wote walishikwa na butwaa na kusema hakika haya matendo makuu ya Mungu..Na kwa kitendo kile tu maelfu ya watu walivutwa Kwa Kristo.Na jambo hili liliendelea kwa muda mrefu sana.
Na pia kusudi la pili la lugha hizi Roho Mtakatifu kuziachia duniani ni ili kudhihirisha uwepo wake katikati ya waaminio, Hapa ndipo mtu anajikuta ananena lugha asiyoifahamu kwa uweza wa Roho wa Mungu..kuna Lugha za kimbinguni pia, ambazo hizo hazina matunda yoyote kwa watu wasioamini, na ndio maana Mtume Paulo alionya akasema ikiwa mtu atajikuta katika hali kama hii basi na anyamaze na anene na nafsi yake mwenyewe na Mungu wake kwa jinsi anavyojaliwa, vinginevyo ataonekana kama mwendawazimu kama akifanya hivyo katikati ya watu wasioamini, na Mungu sikuzote ni Mungu wa utaratibu. (1Wakorintho 14:28).
Fikiri mtu asiyeujua kabisa Ukristo, anaingia kanisani ghafla anashangaa watu wanaanza kuzungumza lugha zisizoeleweka…moja kwa moja atahisi amekutana na watu pengine ni wendawazimu au wanaabudu miungu..lakini akiingia na kusikia lugha yake pale inaongelewa katika ufasaha wote na anayeiongea sio hata wa jamii ya watu wake..Na maneno anayoongea ni ya kumtukuza Mungu..atashangaa sana na kuogopa kusema huu ni muujiza?..na hivyo atajua mahali pale kuna uwepo Fulani wa kiMungu na hivyo atatubu na kumgeukia Mungu. Na kusema kuwa kila mwaminio ni lazima anene kwa lugha mpya, kauli hiyo inapingana kabisa na maandiko.
Kumbuka kuwa mtu haneni lugha kama apendavyo yeye, au ajisikiavyo yeye bali ni kama vile Roho ANAVYOMJALIA MTU KUTAMKA (Soma Matendo 2:4), kama tu vile mtu asivyoamua kuona maono mpaka Mungu amwonyeshe na lugha ndio ziko hivyo hivyo..Vinginevyo mtu utakuwa ananena tu kwa akili zake, na ndivyo watu wengi walivyofanya leo hii, ambayo yanafanya tunaonekana kama watu waliorukwa na akili..
Kunena kwa lugha ni kipawa cha Mungu na Mungu anakigawa kwa jinsi apendavyo yeye mwenyewe, mmoja atampa lugha mpya, mwingine unabii, mwingine tena uponyaji, mwingine uongozi, wingine matendo ya miujiza, mwingine kufundisha n.k..lakini wote hatuwezi kuwa manabii, au wote waalimu au wote wenye kufanya matendo ya miujiza au wote wenye kunena kwa lugha au wote wachungaji.
1Wakorintho 12.27 “Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
28 Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.
29 Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza?
30 Wote wana karama za kuponya wagonjwa? WOTE WANENA KWA LUGHA? Wote wafasiri?.”
Na jambo lingine la muhimu la kufahamu ni kuwa mtu anaweza kuwa na ananena kwa lugha mpya lakini bado asiwe na Roho Mtakatifu ndani yake, kama tu vile mtu anaweza akawa ni nabii, akaona maono yote duniani, na asiwe nabii wa kweli, kama tu vile mtu anaweza akaponya magonjwa kwa karama Mungu aliyompa na kufanya miujiza mingi isiyokuwa ya kawaida na bado Kristo asimtambue.(Mathayo 7:21).
Hivyo usijisifie karama, kwasababu Roho Mtakatifu sio karama yeye ni zaidi ya hicho, ikiwa utapenda kupata maelezo marefu juu ya uthibitisho fasaa unaomtambulisha mtu kuwa amepokea Roho Mtakatifu atanitumia ujumbe inbox, nikutumie somo lake.
Hivyo kwa kumalizia ikiwa wewe ni mmojawapo wa waliokirimiwa kipawa hichi Unaponena kwa lugha mwombe pia Mungu akupe kutafsiri, Sehemu hii inaonekana kwa wachache katika kanisa lakini ndio inayofaa zaidi, kuliko kunena tu maneno yasiyojulikana kanisani mbele ya watu, kwasababu hilo linaweza kuwa na manufaa tu kwako mwenyewe lakini lisiwe na msaada wowote kwa wengine.
Lakini kama litaambatana na tafsiri hilo linafaa sana na lina nguvu kwasababu linalijenga kanisa la Kristo kwa ujumla.
1Wakorintho 14:27 “Kama mtu akinena kwa lugha, wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na mmoja na afasiri.
28 Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na anyamaze katika kanisa; aseme na nafsi yake tena na Mungu.”
Jivunie karama yako ikiwa inalijenga kanisa la Kristo, na sio kwa kujionyeshea kuwa ni hodari wa kunena, Mtume Paulo alijisifia zaidi ya mtu yoyote, lakini alisema ni heri anene maneno matano lakini yanalifaa kanisa kuliko kunena maneno Elfu kwa lugha.
Bwana akubariki.
[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=-v8ToQZwJho[/embedyt]
Mada zinazoendana:
JE! NI LAZIMA WATU WOTE WANENE KWA LUGHA?
JE! KARAMA NI UTHIBITISHO WA KUWA NA MUNGU?
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
JIBU: Kulikuwa na sababu kuu mbili kwanini Bwana Yesu kuzungumza maneno yale, Sababu ya kwanza ilikuwa ni ili kutimiza maandiko kama Yohana alivyoandika katika Injili yake.
Yohana 19:28 “Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu.”
Unaona hapo?. Ikumbukwe kuwa sehemu kuwa ya unabii aliomuhusu Yesu katika agano la kale ulitimia ndani ya wakati huu wa Mateso ya Bwana Yesu. Yaani matukio mengi sana yaliyokuwa yanatendeka na kutokea ndani ya kile kipindi kifupi cha wiki moja ya mwisho yalikuwa ni mfulilizo wa matukio ya kinabii..Jaribu kifikiria kitendo kama kile cha Yesu tu kupigwa kofi (Yohana 18:22), tayari kilishatabiriwa kitafanyika (soma Ayubu 16:18),kutemewa mate(Ayubu 30:10),kusalitiwa,vazi lake kupigwa kura, kudhihakiwa. (Zab 22)n.k…
Vivyo hivyo na kusema hili nina KIU tayari lilishatabiriwa kama tu vile yale maneno mengine kama“Eloi Eloi Lama sabakthani” yalivyotabiriwa kwahiyo alisema maneno yale ili kutimiza maandiko. Pia Ikumbukwe kuwa Bwana Yesu alikaa msalabani muda wa saa 6, licha ya mahangaisho yale ya huku na kule kubebeshwa misalaba na jana yake na pamoja usiku uliopita alikuwa akikesha katika majonzi mengi na kupigwa bila kula wala kuonja chochote, ni wazi kuwa Kiu kilimshika sana Tunasoma katika…hakuna mwanadamu wa kawaida ahangaishe hivyo halafu asisikie kiu..haiwezekani…Na unabii wa kuchoka kwake ulitabiriwa pia katika Biblia kitabu cha zaburi.
Zab 22:15 ‘Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti”
Unaona hii ni kuonyesha kuwa mwili wake alikaukiwa na maji mpaka mdomo wake ukawa mkavu kiasi cha ulimi wake kuganda kwenye taya zake.. Na ndio maana akasema nasikia kiu. Lakini pia sababu nyingine ya pili ambayo ni ya rohoni, ilikuwa ni kuonyesha kuwa sasa shughuli yote imekwisha, ni wakati sasa wa kunywa, maadui wamekwisha shindwa. Sikuzote kiu huwa kinakuja baada ya kufanya kazi Fulani ngumu ya kuchosha,au mazoezi n.k.. na ndio maana tunamwona Samsoni Siku ile wayahudi walipomfunga kamba na kumpeleka kwa wafilisti kwa usalama wa nchi yao,waliona ni heri wampoteze mtu mmoja ili taifa letu zima lisiangamie mikononi mwa wafilisti, kama tu vile wayahudi walivyomfunga Bwana Yesu na kumpeleka kwa watu wa mataifa wamsulibishe,walisema ni heri mmoja afe ili taifa zima lisiangamie mikononi mwa Warumi. Lakini tunajua ni kitu gani kilitokea pale mara baada ya vita kuisha pale Samsoni alipowapiga wale wafilisti 1000 kwa taya ile moja ya Punda, Tunasoma Samsoni aliona KIU sana.
Waamuzi 15:15 “Naye akaona mfupa mbichi wa taya ya punda, akautwaa, akapiga watu elfu kwa mfupa huo;16 Samsoni akasema, Kwa taya ya punda chungu juu ya chungu, Kwa taya ya punda nimepiga watu elfu.17 Ikawa, alipokuwa amekwisha kunena akautupa ule mfupa wa taya mkononi mwake; na mahali pale pakaitwa Ramath-lehi.18 Kisha akaona kiu sana, akamwita Bwana akasema, Wewe umetupa wokovu huu kwa mkono wa mtumishi wako; na sasa nitakufa kwa kiu, na kuanguka katika mikono ya watu wasiotahiriwa.19 Lakini Mungu akapasua mahali penye shimo palipo katika Lehi, pakatoka maji; naye alipokwisha kunywa, roho yake ikamrudia, akaburudika; kwa hiyo jina la mahali pale likaitwa Enhakore, napo pa katika Lehi hata hivi leo.20 Naye akawa mwamuzi wa Israeli: katika siku za Wafilisti muda wa miaka ishirini.”
Hivyo kitendo cha Yesu kutoa kauli ile ilikuwa ni ishara ya rohoni kuonyesha kuwa tayari shetani kashashindwa vita..Na ndio maana maneno yaliyofuata baada ya pale yalikuwa ni haya IMEKWISHA!.(Yohana 19:30).
Ubarikiwe.
Mada Nyinginezo:
KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?
BASI MUNGU AKAMUADHIMISHA SANA.
MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI:
MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.
AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA
JIBU: Tusome:
Yakobo 5:17 “Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.
18 Akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake.”
Kwakuwa habari hii inamzungumzia Eliya hivyo ili kuelewa vizuri hiyo bidii aliyokuwa nayo ni vizuri tukarejea kwenye tukio halisi lenyewe ili tuone ni jinsi gani aliomba. Sasa ukiangalia vizuri utaona biblia haijatoa maelezo mengi juu ya maombi aliyoyaomba siku ile alipozuia mvua. Inaonyesha tu Eliya akitokea kwenye tukio na kuzungumza maneno yale na kuondoka,
1Wafalme 17:1 “Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.
2 Neno la Bwana likamjia, kusema,
3 Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani.”
Lakini siku ile anarudi, ili kuifungua tena mbingu kwa Neno la Mungu, tunaona halikuwa ni jambo la kutamka na kuondoka tu kuna vitu viliendelea pale embu Tusome:
1Wafalme 18:41 “Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka, ule, unywe; kwani pana sauti ya mvua tele.
42 Basi Ahabu akainuka ili ale na kunywa. Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi, akainama uso mpaka magotini.
43 Akamwambia mtumishi wake, Kwea sasa, utazame upande wa bahari. Akakwea, akatazama, na kusema, Hakuna kitu. Naye akanena, Enenda tena mara saba.
44 Ikawa mara ya saba akasema, Tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. Akanena, Enenda, umwambie Ahabu, Tandika, ushuke, mvua isikuzuie.
45 Ikawa, muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikanyesha mvua nyingi. Ahabu akapanda garini, akaenda zake Yezreeli.”
Hapo unaweza ukajifunza mambo kadhaa, cha kwanza Eliya kabla hata hajamwomba Mungu, alishaamini kuwa mvua inakwenda kunyesha siku hiyo katika nchi, na ndio maana alikuwa na ujasiri wa kumwambia Mfalme Ahabu inuka unywe kwani pana sauti ya mvua tele.
Pili alipoonenda magotini sasa ili kumwomba Mungu jibu lake halikuja ndani ya wakati alioutazamia pengine aliomba lisaa la kwanza, akitazamia kabla hata hajamaliza juu kutakuwa kumeshafunga, lakini Yule mtumishi wake alipoenda alirudisha repoti kuwa juu hakuna dalili yoyote ya mvua kunyesha, lakini aliendelea kukaa uweponi mwa Bwana akimshukuru kwa matendo yake makuu, lisaa lingine likapita akamwambia mtumishi wake haya nenda katazame tena, akarudi akasema hakuna kitu, ikaendelea hivyo hivyo lisaa la tatu, la nne, mpaka lisaa la 7 pengine, akamwambia nenda katazame usichoke, ndipo Yule mtumishi wake akarudi akasema ninaona kawingu kadogo kama cha mkono wa mtoto mchanga, Ndipo Eliya alipoacha kuomba akijua kuwa tayari imekwisha kuwa..
Na kama ingetokea hakuna kitu chochote kilichotokea ni wazi kuwa angeendelea hivyo hivyo hata mara 20 au 50, au 100 kwa nguvu ile ile akijua kuwa Mungu ameshamsikia..Huko ndiko kuomba kwa BIDII ambapo hata sisi tunapashwa tuwe nako, Ni rahisi kumwamini Mungu tunapompelekea mahitaji yetu lakini kudumu uweponi Mwake hatuwezi pale tunapoona majibu yanachelewa kidogo, hayajaja ndani ya wakati tuliotuzamia..Tunaanza kumtilia Mungu mashaka pengine hajatusikia. Lakini tukiendelea kushikilia na kumwamini Mungu kuwa ameshatenda, hata kama itapita siku, wiki, mwezi, miaka, ukizidi kushikilia nakwambia milango yote itafunguka mbele yetu. Hivyo kwa ufupi kuomba kwa bidii kunakozungumziwa hapo ni Kukaza kumwamini Mungu mpaka majibu yanapotokea.
Ubarikiwe sana.
Mada Nyinginezo:
ROHO YA ELIYA KATIKA AGANO JIPYA INATENDAJE KAZI?
KUNA TOFAUTI GANI KATI YA SALA NA DUA?
“WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI”
TUMEPEWA, SI KUMWAMINI TU KRISTO, ILA NA KUTESWA KWA AJILI YAKE;
JIBU: Kauli hiyo ilitoka kwa Mungu mara baada ya Petro kupewa maono yale ya lile shuka kubwa lililoshuka kutoka mbinguni likiwa limebeba viumbe vya kila aina najisi na safi akaambiwa avichinje ale,.Lakini Petro saa hiyo hiyo akamjibu Mungu akamwambia Mungu sijawahi kula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi katika maisha yangu yote..Ndipo Mungu akamwambia “Vilivyotakaswa na Mungu, usiviite wewe najisi”. Ufunuo huo japo Petro alipewa kumaanisha sisi watu wa mataifa ambao hapo kwanza tulikuwa tunaonekana najisi mbele ya waisraeli, lakini Bwana alipokuja alitutakasa wote kwa damu yake hivyo sisi watu wa mataifa sio najisi tena….na hivyo Mungu hawezi kuwatakasa wanadamu walio chanzo cha uovu wote asiwatakase Wanyama ambao sio wao waliofanya makosa, kwahivyo Wanyama nao wametakaswa hakuna kilicho najisi tena….
Kwahiyo ono lile Petro aliloonyeshwa ni Ufunuo mkubwa sana unaoonyesha wazi wazi kuwa mbele za Mungu hakuna kiumbe chochote kilichonajisi msalaba umefumbua hilo fumbo….Ikimaanisha kuwa viumbe vile ambavyo hapo mwanzo vilikuwa haviliwi sasa vyote vinaweza kuliwa, na sisi watu wa mataifa ambapo hapo kwanza tulikuwa hatustahili kumjua Mungu wa Israeli(tulikuwa najisi) sasa ni Taifa teule la Mungu. Utaona jambo hilo hilo Mtume Paulo akilirudia sehemu fulani na kusema amehakikishiwa na Mungu kabisa hakuna kitu chochote kilichonajisi kwa asili yake Ukisoma
Warumi 14:14 “Najua, tena nimehakikishwa sana katika Bwana Yesu, ya kuwa hakuna kitu kilicho najisi kwa asili yake, lakini kwake yeye akionaye kitu kuwa najisi, kwake huyo kitu kile ni najisi.”
Lakini kumbuka pia kauli hiyo haijatupa ruhusa ya sisi kuwa walafi, biblia hiyo hiyo inasema japo vitu vyote ni halali lakini si vyote vifaavyo kwa mtu,(1Wakoritho 6:12), Kumbuka hata wanyama wale au vyakula vile vinavyokubalika na wengi na vinavyoonekana kuwa ni safi, bado vinaweza visimfae mtu mmoja mahali Fulani, Sio wote wanapenda nyama ya samaki, si wote nyama ya ng’ombe inawakubali, si wote nyama ya kuku inawakubali, si wote maziwa yanamanufaa mwilini mwao, sasa mtu kama huyo akila na kusema kuku imekubaliwa kwenye maandiko ngoja niishambulie, baadaye ikishamsumbua anaanza kulalamika, lakini ameshindwa tu kutumia hekima kufahamu neno hili “vyote ni halali lakini si vyote vifaavyo”..
Vilevile ukila nyoka, au panya, au mjusi, au mende, kama hicho ni chakula kinachokubalika na jamii yenu na wewe pia unakipenda na hakikuletei madhara yoyote mwilini mwako, Hakuna shida yoyote kula tu hata vipepeo, na kinyonga ilimradi uvipokee kwa shukrani [yaani kwa kumaanisha](1Timotheo 4:3), Na sio kwa ulafi, kisa tu vimehalalisha vyote.
Bwana akubariki.
Mada Nyinginezo:
BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “ENENDENI ULIMWENGUNI MWOTE,MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE”?
WAPUNGA PEPO WANAOZUNGUMZIWA KWENYE BIBLIA NI WATU WA NAMNA GANI?
JE! BAADA YA ULIMWENGU HUU KUISHA MALAIKA WATAKUWA NA KAZI GANI TENA?
ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.
HISTORIA YA ISRAELI.
JIBU: Neno kujikana linamaana kuwa, ‘kukataa matamanio yako binafsi au malengo yako kwa sababu fulani’. Hivyo kujikana kunakozungumziwa katika biblia ni kujikana kwa Kristo. Hii ikiwa na maana kuwa unapoamua kumfuata Kristo unakuwa tayari kuyakataa matamainio yako hata kama ni mazuri kiasi gani, hata kama yanatia maanani kiasi gani, unayaweka chini na kukubali kuyafuata yale ya Bwana Yesu tu. Na ndio maana mtume Paulo aliweka wazi na kusema hivi:
“7..Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.
8 Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo; (Wafilipi 3:7-8)”.
Unaona hii ni nguzo kuu na ya muhimu sana, inayomtambulisha mtu kama amemfuata Kristo. Wanaotubu dhambi zao ni wengi lakini wanaodhamiria kumfuata Kristo ni wachache sana. Unapoamua kuwa binti wa kikristo, uwe tayari kuukana uzui wako, na kuacha kuvaa vimini na suruali, nguo za kikahaba, na mapambo ya kiulimwengu…ili ufanyike mwanafunzi wa Yesu vinginevyo bado hujawa mkristo hata kama utasema umeokoka. Vile vile kijana unapokuja kwa Kristo uwe tayari kukataa tamaa zote za ujanani, disco, miziki ya kidunina, pombe na sigara, uasherati, unavipiga vita unaamua kumwangalia Kristo kuanzia huo wakati na kuendelea. Ni mambo ambayo ungeweza kuyafanya kama vijana wengine katika ujana wako lakini unajikana kwa ajili ya kuujua uzuri ulio katika Kristo. Na Bwana Yesu akishaona huo moyo wako hapo ndipo na yeye anapochukua nafasi ya kukufanya kuwa mtu mwingine wa tofauti kabisa katika viwango vya rohoni. Unafanyika kuwa mwanafunzi wake kweli kweli kama mitume wake.
Na hili ni tendo endelevu ambalo linapaswa liwe kila siku, hata katika kuifanya kazi ya Mungu unapaswa ujikane mwenyewe, muda ambao ungetakiwa kufanyabiashara kama watu wengine wewe unaifanya kazi ya Mungu, Vilevile tumeagizwa tudumu katika sala, wakati ambao ungepaswa ulale usiku kama watu wengine wewe unaamka kuomba, huko ni kujikana nafsi. Bwana anakokuzungumzia. Lakini pamoja na hayo katika kujikana huko, na kupoteza matamanio yako au vitu vyako kwa ajili ya Kristo yeye mwenyewe anatuambia, kwa kufanya hivyo ndivyo tunavyozipata. Kwa Mungu hakuna matujo kwani sikuzote mawazo anayotuwazia sisi na ya amani wala sio mabaya ili kutupa sisi tumaini zuri katika siku zetu za mwisho (Yeremia 29:11).
Na ndio maana hatuoni shida hata anapotuambia tuache kila kitu kwa ajili yake. Faida yake tutaiona kama sio katika ulimwengu huu basi katika ulimwengu unaokuja. Kwasababu anatuwazia kusudi jema siku zote. Hivyo, Ni heri uonekane unapoteza kila kitu sasa kwasababu tu umeamua kumfuata Kristo, kuliko kupata kila kitu cha ulimwengu huu na mwisho wa siku unaishi katika ziwa la moto, itakufaidia nini?.
Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na AJIKANE MWENYEWE, ajitwike msalaba wake, anifuate.
25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.
26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?”.
Ubarikiwe.
Mada Nyinginezo:
HUYU AZAZELI NI NANI TUNAYEMSOMA KATIKA(WALAWI 16:8)
SWALI: Nina swali kuhusu alama ya mnyama, kulingana na baadhi ya injili zinazohubiriwa ni kuwa ..alama ya mnyama itapimwa kwa siku ya kuabudu, yani wale watakaokubali kusali jumapili wote watakuwa wamepokea 666, ikimaanisha kuwa Papa atatangaza siku moja tu ya kuabudu iwe jumapili dunia nzima, lengo likiwa kuvunja amri ya nne itunze siku ya saba, kwahyo amri ya papa itakapopita itapiga 666 kwa wote watakaokubaliana nayo, wana refer maandiko ya Danieli 7:25 KUWA ATABADILI MAJIRA NA SHERIA.
JIBU: Shalom ndugu, Ni kweli kabisa wapo wanaoamini kuwa Papa atageuza MAJIRA NA SHERIA kulingana na Danieli 7:25….Lakini ukijifunza biblia utagundua kuwa majira yanayozungumziwa hapo sio siku moja maalum itabadilika…hapana! Kwasababu majira ni Neno pana na la wingi ambalo linaweza kuwa kipindi Fulani cha muda…labda cha siku kadhaa, wiki, miezi au miaka kadhaa…kinachoambatana na tukio Fulani. Ili tuelewe vizuri hebu tuchukue mifano kadhaa ya kwenye biblia..
Luka 21: 7 ‘’Wakamwuliza wakisema, Mwalimu, mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini ishara ya kuwa mambo hayo ya karibu kutukia? 8 Akasema, Angalieni, msije mkadanganyika, kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ndiye; tena, MAJIRA YAMEKARIBIA. Basi msiwafuate hao’’.
Katika mstari huo unaona neno MAJIRA lilivyotumika hapo, sio kipindi cha SIKU MOJA MAALUM ambacho kitafika watu watakuja kwa jina lake na kusema wao ndio…Utaona sio tafsiri yake hiyo, bali majira ilivyotumika hapo ni kwamba ‘itafika kipindi Fulani cha muda’ ambacho hakijulikani kitadumu kwa muda gani ambapo watatokea manabii wa uongo wakija kwa jina la Yesu…Na hicho kipindi ndio hichi tunachoishi sasa, Pia tunaweza kujifunza katika huu mfano mwingine Bwana alioutoa..
Luka 12:54 ‘’Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo. 55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua MAJIRA haya?’’
Unaona hapo tena?…Majira yanayozungumziwa hapo ni kipindi Bwana Yesu alichokuwepo duniani akihubiri na kufundisha njia za haki…ni majira ambayo makutano walishindwa kufahamu kuwa Masihi yupo ulimwenguni…Na majira hayo ni kipindi cha miaka mitatu na nusu Bwana aliyokuwa anahubiri..na sio siku Fulani moja maalum. Pia mfano mwingine ni huu..
Kutoka 21:18 ‘’Watu wakigombana, na mmoja akimpiga mwenziwe kwa jiwe, au kwa konde, asife, lakini yualazwa kitandani mwake;atakapoinuka tena na kuenenda nje kwa kutegemea fimbo, ndipo hapo yule aliyempiga ataachwa; ila atamlipa kwa ajili ya hayo majira yake yaliyompotea, naye atamwuguza hata apone kabisa..’’..
Hapo pia utaona ‘majira’ sio siku moja maalumu bali kipindi cha muda. Kadhalika pia tunaweza kujifunza mfano huu wa mwisho maana ya majira..
Luka 21: 29 ‘’Akawaambia mfano; Utazameni mtini na miti mingine yote. 30 Wakati iishapo kuchipuka, mwaona na kutambua wenyewe ya kwamba MAJIRA YA MAVUNO yamekwisha kuwa karibu. 31 Nanyi kadhalika, mwonapo mambo hayo yanaanza kutokea, tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu u karibu.’’
Unaona majira ya mavuno yanayozungumziwa katika maandiko sio siku moja MAALUMU, kama wasabato wanavyodhania, bali ni kipindi Fulani cha mavuno ambacho kinaweza kuwa ni siku kadhaa, au wiki kadhaa…Ipo mifano mingi unaweza ukapitia Pia (pitia Luka 21:54-55, Luka 21:23-25, Luka 19:41-44 utaelewa zaidi juu ya jambo hilo).
Kwahiyo tukirudi pale kwenye Danieli 7:25…Kwamba Mpinga kristo atabadili ‘’majira na sheria’’ biblia haikumaanisha kuwa mpinga kristo atakuja kubadilisha siku moja ya kuabudu Jumamosi na kuwa jumapili…Hapana bali MAJIRA yatakayobadilika hapo ni MAJIRA YA mfumo mzima wa maisha, kutoka kuwa ya amani na kuwa ya dhiki, huwezi kununua wala kuuza bila ile chapa…wakati huo Majira ya Neema yatakuwa yameisha na sasa ni majira ya dhiki kuu….yatakuwa ni majira ya mavuno..na hayo hayatakuwa siku moja hapana ni kipindi fulani cha muda ambacho kitadumu miaka mitatu na nusu…Kwahiyo mfumo wake mpya wa umoja wa dini na madhehebu yote ndio utakaobadili majira ya ulimwengu mzima..
Kama vile ujio wa Kristo ulivyobadili majira kutoka majira ya utumwa wa dhambi na sheria na kutuingiza katika majira ya Neema na uhuru wa roho, kadhalika baada ya unyakuo wa kanisa kupita Mpinga Kristo ataiingiza dunia katika majira mapya ya dhiki kuu na ghadhabu ya Mungu. Kumbuka sasahivi tunaishi kipindi cha majira ya Neema ya Kristo, ambacho kinajulikana kama kipindi cha MAJIRA YA MATAIFA.(ukisoma Luka 21:24 utaona jambo hilo) Na kipindi hichi kitaishia na unyakuo. Hivyo fundisho la wasabato linalosema kutotunza sabato, ndio kupokea alama ya mnyama, ni fundisho potofu na linapaswa liepukwe kwasababu halina msingi wowote wa kimaandiko.
Bwana akubariki sana.
Mada Nyinginezo:
SABATO HALISI NI LINI, JE! NI JUMAPILI AU JUMAMOSI?, NI SIKU GANI ITUPASAYO KUABUDU?
LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.
NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.
KWANINI MUNGU ANAMPA NABII HOSEA MAAGIZO YA KUMUOA MWANAMKE KAHABA?
SWALI: Biblia inaposema “Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao. (Mathayo 5:3)”je hatuna ruhusa ya kuwa matajiri katika roho?.
JIBU: Maskini ni mtu ambaye yupo katika hali ya kutojitosheleza, Sasa Bwana aliposema “heri walio maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni ni wao”, hakumaanisha kuwa HERI wale wasio na maarifa yoyote au ufahamu wa mambo ya rohoni (yaani watu wasiomjua Mungu), hapana bali alimaanisha heri wale ambao kila siku wapo katika hali ya uhitaji wa kufahamu mambo ya ufalme wa mbinguni, watu ambao hawajajikinai, watu ambao kila siku wanatamani kuongeza kitu kipya katika maisha yao ya rohoni, watu wenye kiu na njaa ya kumjua Mungu kila siku…
Hao ndio Mungu anawaona ni maskini wa roho ambao kila siku wanamlilia yeye BABA, tupe! Tupe! Chakula cha rohoni..Lakini kuna wengine hawana haja tena ya kujua zaidi mambo ya rohoni, tayari wameshahitimu, pengine labda kwa kuwa walipitia vyuo vya biblia, au wameshasoma sana maandiko, hivyo wanajiona sasa wanajua kila kitu, hawana haja tena ya kujifunza, hata wakiletewa habari ya mpya wanadharau moyoni mwao wanaona kwamba hakuna chochote huyu mtu anaweza kuniongezea? Ndivyo ilivyokuwa kwa wale waandishi na mafarisayo.
Hawakutaka kukaa chini kuyasikiliza maneno ya YESU walimdharau na kumwona si kitu tofauti na yale makutano walimsikiliza kwasababu ndani yao kulikuwa na kiu na njaa na shauku ya kumjua Mungu zaidi na zaidi, na ndio maana Bwana Yesu akazungumza maneno yale.Ikiwa wewe unajiona hapo katika dhehebu lako ndio umefika, na hivyo huna haja ya kuambiwa chochote hata kama kinatoka kwenye maandiko basi fahamu kabisa kuwa upo mbali sana na ufalme wa mbinguni.
Ufunuo 3:17 “Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.”
Mtume Paulo mpaka anafikia uzee wake, anakaribia kufa pamoja na kwamba Mungu alimfanya kuwa askofu wa mataifa yote, mwenye heshima duniani kote katikati ya waaminio, mtu ambaye Mungu alimpa mafunuo makubwa ambaye hata sasa nyaraka zake tunazitumia kama mwongozo lakini mpaka dakika ya mwisho anamwagiza Timotheo kwamba siku akimfuata vifungoni mwake asiache kumpelekea vile vitabu vya ngozi ili azidi kujifunze zaidi,(2Timotheo 4:13) inatupasaje sisi?…
Huo ni mfano mzuri wa mtu aliye maskini wa roho, haridhiki sehemu alipo, haridhiki na kile alichonacho au alichopewa katika dhehebu lake au dini yake, kila siku anataka zaidi na zaidi amjue Mungu…Sio ajabu mtume Paulo aliandika hivi:1Wakorintho 8:2 “Mtu akidhani ya kuwa anajua neno, hajui neno lo lote bado, kama impasavyo kujua.”Hivyo tupende kila siku kutamani kupiga hatua moja zaidi rohoni, na hiyo inakuja kwa kutokukinai kujifunza Neno la Mungu kila siku.
Ubarikiwe sana.
Mada Nyinginezo:
UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.
NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?
SWALI: Ninafahamu kwamba, watu waliokua wanakusanya vitabu/maandiko matakatifu kwa lengo la kuandaa BIBLIA, walikua wakiongozwa na ROHO MTAKATIFU Mwenyewe. Ili kitabu au maandishi yachaguliwe, waliangalia vigezo gani?-sababu na sikia, kuna baadhi ya vitabu havikuchukuliwa -Mfano Injili ya petro , na ya Tomaso.
JIBU: Hiyo ipo wazi kabisa kila kitabu cha biblia cha mwandishi yoyote tunayemsoma kimevuviwa na Roho Mtakatifu, hali kadhalika pia kuwepo kwa idadi ya vitabu 66 katika biblia hilo nalo ni tendo lililovuviwa na Roho Mtakatifu na wala sio wazo la kibinadamu kama wale ambao sio-wakristo wanavyofikiri. Ni mpango ambao Mungu alishaupanga kabla hata ya kuwekwa misingi ya dunia. Lakini siku zote Mungu huwa anamtumia “mtu” kutenda kazi japo sio kwamba hawezi kutenda pasipo hao hapana bali huo ni utaratibu wake tu aliojiwekea yeye(ndivyo ilivyompedeza).
Sasa tukirudi katika agano la kale, kukusanywa vitabu vile vyote 39, Mungu alitia hekima kwa wayahudi washindania Imani wakati ule,waliomcha Mungu, waliokuwa wasomi na wafuatiliaji wazuri wa unabii na historia ya taifa la Israeli kwa ujumla, hivyo kwao haikuwa kazi kubwa, kuvihakiki vitabu vya manabii waliowatangulia, Hivyo wale waliokubalika na habari zao zilithibitika kuja kutokea kweli,.Kwamfano vitabu vya torati ya Musa, ni vitabu ambavyo havikuwa na tashwishwi yoyote kwa wayahudi kwani ni vitabu vinavyoeleza chimbuko lao na vimepita kizazi hadi kizazi havijapotea tangu siku vilipoandikwa.. Vile vile Ukiangalia vitabu kama Esta,Ruthu,Wafalme, n.k. ni vitabu vya historia ambavyo vinaeleza habari zilizohalisi kabisa, vile vile vitabu vya manabii kama Isaya, Yeremia,Danieli vyote hivyo ni vitabu vilivyothibitika kuwa ni Vitabu vya wakati wote, na unabii wake ni thabiti ambao watu walikuwa wanawaona. Na kwa kuzingatia hayo ndio vikapatikana vile vitabu 39 vya Agano la kale. Lakini katika agano jipya, utaona kulikuwa pia kuna vitabu ambavyo vilishakubalika tangu kanisa la kwanza.
Kwamfano nyaraka za mtume Paulo zilikuwa zinatumiwa tayari na watakatifu wa makanisa yote yaliyokuwa Asia wakati ule kabla hata yeye hajaondoka, nyaraka zake zilikuwa zinazungushwa toka kanisa hadi kanisa..tunasoma hilo katika
Wakolosai 4:16 “Waraka huu ukiisha kusomwa kwenu fanyeni kwamba usomwe katika kanisa la Walaodikia pia; na ule wa Laodikia usomwe na ninyi”…
Kwahiyo haikuwa ngumu kuendeleza utaratibu huo mpaka kwa makanisa ya mbeleni. Vile vile utaona mtume Paulo, pia akirejea baadhi ya vifungo ambavyo vilikuwa katika vitabu vya Injili mfano Injili ile ya Luka, soma (1Timotheo 5:18b,linganisha na Luka 10:7) utalibitisha hilo kuwa kumbe hata Paulo alishapokea vitabu vya Injili kama sehemu ya maandiko matakatifu ya kurejea hiyo ni kuonyesha kuwa vitabu vya Injili vilikuwa tayari vimeshapokewa kama sehemu ya maandiko matakatifu ya wakati wote tangu kanisa la kwanza. Sasa baadaye watu kama wakina Klementi wa Rumi , Ignatusi wa Antiokia na Polikapi na wengine wakaja kutaja vitabu vingine. Na baadaye tena mabaraza kadhaa yaliitishwa ili kuthibitisha Uvuvio wa vitabu hivyo Na vigezo walivyokuwa wanatumia, ni kama vifuatavyo..
1) cha kwanza je! Mwandishi wa kitabu husika alikuwa ni mtume au alikuwa na uhusiano wa karibu na mitume.
2) Je! Kitabu husika kinakubalika na kanisa kwa ujumla.
3) Je! Kitabu kinabeba mafundisho halisi na ya msingi (kumtambua Yesu Kristo kama kiini cha Imani)?
4) Je! Kitabu hakivunji miiko na kanuni za rohoni ambazo zinathibitishwa na kazi ya Roho Mtakatifu mwenyewe?.
5) Kitabu lazima kiwe kwa sehemu Fulani kimenukuu vitabu vingine vya agano la kale..Kwamfano unaona nyaraka za Paulo nyingi zilinukuu vitabu vya Zaburi,Ayubu na Mwanzo.. Hivyo baraza la mwisho ambalo lilihitimisha kuwepo kwa vitabu 66 vya Biblia vilivyovuviwa, lilifanyika mwaka 397WK. Na ndio vitabu tulivyonavyo sasa. Lakini kumbuka kama tulivyosema kazi ya vitabu vya biblia kuwa 66 sio mwanadamu alipanga, hata ingekuwaje, kwa namna yoyote ile, kwa kupitia hatua hizo au nyingine zozote biblia ingetufikia tu kwa ukamilifu wake wote.
Ubarikiwe.
Mada Nyinginezo:
KITABU CHA YASHARI KINACHOZUNGUMZIWA KATIKA 2SAMWELI 1:17-18, NI KITABU GANI?
VITABU VYA BIBLIA: SEHEMU YA 1
NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?
NJIA MUNGU ALIYOIWEKA KWA KILA JAMBO:
UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?