Title April 2022

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

Swali: Katika Kumbukumbu 28:53, tunaona Mungu anasema watu watakula nyama za wana wao, na uzao wa tumbo lao, je alikuwa anamaanisha nini kusema hivyo?.

Jibu: Tusome,

Kumbukumbu 28:53 “Nawe utakula uzao wa tumbo lako mwenyewe, nyama ya wana wako na binti zako aliokupa BWANA, Mungu wako; katika mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako”.

Ukisoma kuanzia juu mstari wa kwanza wa sura hiyo ya 28, utaona baraka ambazo Mungu aliwaahidia wana wa Israeli endapo wataenda katika sheria zake na amri zake..kwamba watabarikiwa mjini na vijijini, hali kadhalika watabarikiwa waingiapo na watokapo..na zaidi sana uzao wa matumbo yao utabarikiwa.

Kumbukumbu 28:1 “Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako.

3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.

4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako”.

Lakini ukizidi kusogea mbele katika mstari wa 15, Utaona Mungu anatoa tahadhari na ole kwa hao hao Israeli kama endapo watamwacha na kwenda kuabudu miungu mingine, na kuzivunja amri zake, basi watakumbana na laana nzito.

Na mojawapo ya laana hizo waliambiwa kuwa watakula nyama za watoto wao kutokana na njaa Bwana atakayowapiga nayo.

Kumbukumbu 28:15 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.

16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani………….

49 BWANA atakuletea taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usiloufahamu ulimi wake;

50 taifa lenye uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana;

51 naye atakula uzao wa ng’ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa; wala hatakuachia nafaka, wala divai, wala mafuta, wala maongeo ya ng’ombe wako, wala wana-kondoo wako, hata atakapokwisha kukuangamiza.

52 Naye atakuhusuru katika malango yako yote, hata kuta zako ndefu, zenye maboma, ulizokuwa ukiziamini, zishuke, katika nchi yako yote kila upande; naye atakuhusuru katika malango yako yote kila upande, katika nchi yako yote aliyokupa BWANA, Mungu wako.

53 NAWE UTAKULA UZAO WA TUMBO LAKO MWENYEWE, NYAMA YA WANA WAKO NA BINTI ZAKO aliokupa BWANA, Mungu wako; katika mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako”.

Sasa unaweza kuuliza jambo hilo lilitimia lini?..kwamba wana wa Israeli walifikia hatua ya kula nyama za watoto wao.

Kama wewe ni msomaji wa biblia, utakumbuka kuna wakati Israeli ilimwacha Mungu, na matokeo ya kumwacha Mungu..Bwana akaruhusu jeshi la Shamu liwazunguke…na kwa hofu ya jeshi hilo kubwa, wana wa Israeli walijifungia ndani ya mji..(kumbuka miji ya zamani ilikuwa inazungushiwa ukuta pande zote). Hivyo mlango wa mji ukifungwa hakuna mtu anayeweza kuingia wala kutoka.

Kwahiyo Israeli walijifungia mjini kwa kipindi kirefu kwa hofu ya jeshi la washami lililopo nje.

Na matokeo ya kujifungia ndani kwa muda mrefu ni chakula kuisha ndani, na kuanza kufikiria kula mavi ya njiwa na kula wanyama wasiolika, ilifikia hatua kichwa cha punda kinaauzwa kwa fedha nyingi sana.

Na njaa ilipozidi watu wakaanza kula watoto wao, mpaka taarifa zikamfikia mfalme za wanawake wawili waliokuwa wanagombania kula nyama za watoto wao.

Tusome,

2 Wafalme 6:24 “Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria.

25 Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha.

26 Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme.

27 Akasema, BWANA asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni?

28 Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, MTOE MTOTO WAKO, TUMLE LEO, NA MTOTO WANGU TUTAMLA KESHO.

29 Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake.

30 Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake”.

Umeona?..Mungu kamwe hasemi uongo!..alisema siku watakayomwacha watakula watoto wao, na kweli ikatokea hivyo hivyo kama alivyosema siku walipomwacha na kuzivunja amri zake…walikula nyama za watoto wao waliowazaa wenyewe. (Unaweza kusoma pia Yeremia 19:9, Maombolezo 4:10, na Ezekieli 5:10).. utaona jambo hilo hilo.

Hiyo inatufundisha nini?

Inatufundisha kuwa maneno ya Mungu kamwe hayapiti..aliposema watu watakula nyama za watoto wao ni kweli ilitokea…hali kadhalika anaposema kuwa wazinzi na waasherati na waabudu sanamu hawataurithi uzima wa milele kwasababu wamemkataa yeye…basi neno hilo litatimia kama lilivyo na wala hasemi uongo..

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.

Na sio tu hasara ya kuukosa ufalme wa mbinguni, bali hata maisha ya mtu aliyemkataa Mungu akiwa hapa duniani, yatakuwa ni ya tabu tu siku zote, hatakuwa na furaha wala amani, hatafanikiwa wala kuwa na tumaini, na atakufa na kumbukumbu lake litasahauliwa.

Je umempokea Yesu?.

Kama bado ni nini unachosubiri? Kumbuka unyakuo wa kanisa upo karibu wakati wowote parapanda ya mwisho inalia na watakatifu watanyakuliwa, wewe ambaye hujaokoka.lwo hii utakuwa wapi siku hiyo??..au wewe uliye vuguvugu leo, siku ile utakuwa mgeni wa nani?.

Bwana akubariki.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?

Zile Rangi saba za Upinde wa Mvua zinawakilisha nini?

Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Mtu ni kiumbe cha kwanza kilichoumbwa na Mungu duniani, chenye mfano wake na sura yake, kilichoumbiwa utashi na ujuzi ndani yake, kilichotofautishwa  na wanyama wote na viumbe vyote vilivyoumbwa na  Mungu duniani Ndicho kinachoitwa mtu.

Tunasoma hilo katika,

Mwanzo 1:26

[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

Lakini jina Binadamu/mwanadamu, ni neno lililozuka kufuatana na jina la mtu wa kwanza aliyeitwa Adamu.

Jina hilo alipewa na Mungu..Hivyo watu wote waliozaliwa na yeye waliita “wana wa Adamu”kwa kifupi “wanadamu” ambapo jina hilo kwa kiharabu linatamkwa “bin-Adam” ambapo sisi tunatamka “Binadamu”

Lakini ni mtu yule yule..isipokuwa asingeweza kuitwa binadamu siku ile ya kwanza alipoumbwa kwasababu alikuwa bado hajapewa jina, na pia halikuwa hana baba wa mwilini.

Ni sawa na Neno mwebrania na mwisraeli… kabla ya Yakobo kubadilishwa jina lake wana wote wa Ibrahimu hata Ibrahimu mwenyewe aliitwa Mwebrania..(Mwanzo 14:13)

Lakini Yakobo alipobadilishwa jina na kuitwa Israeli, utaona uzao wake wote baada ya pale ulizoeleka na kuitwa waisraeli mpaka leo. Lakini bado mahali pengine waliendelea pia kuitwa waebrania kwa asili yao.

Ndivyo ilivyo kwa mtu na mwanadamu. Ni yule yule kulingana na majira.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

Uru wa Ukaldayo ni nini?

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).

Mjoli ni nini/ ni nani katika biblia?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Easter ni nini?..Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?

Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?

Jibu: Pasaka ni sikukuu ya kiyahudi, ambayo ilianza kuadhimishwa kipindi wana wa Israeli wanatoka nchi ya Misri, wakati ambao Mungu aliwaambia wapake damu ya mwanakondoo katika miimo ya nyumba zao ili Yule Malaika atakapopita asiweze kuwadhuru wazaliwa wao wa kwanza, Hivyo Yule malaika alipopita na kuikuta ile damu ya mwanakondoo katika miimo ya nyumba zao, alipita juu, (maana yake hakuingia katika hiyo nyumba kuua wazawaliwa wa kwanza).

Sasa kitendo hicho cha Malaika kupita juu, ndicho kinachoitwa Pasaka, (kwa lugha kiingereza “passover”). Kwa maelezo marefu kuhusu pasaka na umuhimu wake, na kama inaruhusiwa kusheherekewa mpaka sasa na sisi wakristo, fungua hapa >>PASAKA IPO KIBIBLIA?

Lakini swali lingine ni kuhusu Easter? Je Easter ni nini?, je ipo kwenye biblia? na je sisi wakristo tunaruhusiwa kuiadhimisha easter?.

Jibu: Neno Easter, halipatikani mahali popote katika biblia, kama jinsi pasaka linavyopatikana katika sehemu nyingi, katika biblia (Easter lenyewe halipo kabisa).

Sasa Easter kama haipo imetoka wapi katika Ukristo?

Asili ya Easter, ni mungu wa kipagani (wa kike), aliyeaminika kuleta “uzao” kama vile “baali”  alivyokuwa.. mungu huyu aliabudiwa na jamii za watu wa Saxons, ambao kwasasa ni maeneo ya Ujerumani, na aliitwa “easter” kutokana na “mawio ya jua”. Upande jua linapochomoza, uliaminika kuwa ni upande wa neema na ndio unaomstahili huyu mungu mke, hivyo upande wa mashariki ni “East” kwa lugha ya kiingereza, kwahiyo kwa heshima ya mungu huyo wa uzao ndio wakamwita “easter”..yaani “wa mashariki”.

Na mungu huyu “easter” alikuwa anatolewa sadaka za kafara kipindi kile kile cha sikukuu za pasaka za kiyahudi, tarehe hizo zilikuwa zinagongana, kipindi ambacho Wayahudi wanasheherekea pasaka, ndio kipindi ambacho watu hao wa-Saxons na wengine wengi walikwenda kumtolea mungu wao huyo easter sadaka.

Kwasababu ni kawaida ya shetani kutafuta kuchanganya ukristo na upagani, alinyanyua watu kadhaa na kuoanisha siku ya kufufuka kwa Bwana Yesu, na siku ya sadaka za mungu huyo “easter”. Hivyo ili desturi na kumbukumbu la mungu wao huyo “easter” lisife kabisa kabisa, ndipo wakaiita ile jumapili ya kufufuka kwa Bwana kama “jumapili ya easter”.

Sasa swali ni je! Na sisi wakristo tunaruhusiwa kuadhimisha easter kama sherehe ya kufufuka kwa Bwana Yesu?

Siku ya kufufuka Bwana Yesu, itabaki pale pale, na ni vizuri kuiadhimisha, kwasababu ni siku ya ushindi wetu, siku ya matumaini, na siku ya Shangwe, Mitume na watakatifu wote, kipindi wamejifungia ndani kwa hofu ya wayahudi, siku walipomwona Bwana kafufuka walifurahi furaha kuu.

Luka 24:34 “wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni.

35 Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate.

36 Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu.

37 Wakashituka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho.

38 Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu?

39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo.

40 Na baada ya kusema hayo aliwaonyesha mikono yake na miguu yake.

41 BASI WALIPOKUWA HAWAJAAMINI KWA FURAHA, huku wakistaajabu, aliwaambia, Mna chakula cho chote hapa?”.

Hivyo na sisi hatuna budi kuiadhimisha siku hiyo  kwa furaha nyingi, katika siku ile ile Bwana aliyofufuka, (yaani Jumapili ya pasaka), haijalishi watu wanaiitaje hiyo siku, watu wameipa jina gani, hata kama wangekuwa wameipa jina la “siku kumwabudu shetani” sisi hatutazami majina watu walioyapa siku, (tunaitazama siku yenyewe).. hata siku tulizozaliwa tukizifuatilia katika historia tutakuta zimepewa majina ya ajabu ajabu, lakini wau hawaachi kuziazimisha kisa tu zimepewa majina ya ajabu, au zimeangukia katika tarehe za kuadhimisha mambo mabaya..

Leo ukifuatilia katika historia au kumbukumbu, utakuta kila tarehe imengukia katika maandimisho fulani ya sikukuu za kipagani, hivyo hatuwezi kuacha kufanya mambo ya msingi katika hizo siku, na kuzifuata kalenda za kipagani.

Kwahiyo sisi wakristo tunasheherekea siku ya kufufuka kwa Bwana kama “jumapili ya ushindi” na si kama “easter”. Na hatusheherekei kipagani.

Siku ya kufufuka kwa Bwana Yesu, tunapoiadhimisha kwa kwenda Bar, kulewa hapo tumeisheherekea easter, na si siku ya kufufuka kwa Bwana, siku ya jumapili ya kufufuka kwa Bwana tunapoisheherekea kwa kwenda disko, au kwenye kumbi za anasa, hapo tutakuwa tunamwadhimisha mungu “easter” na si “ufufuo wa Bwana”. Kwasababu waliokuwa wanamwadhimisha huyo mungu mke easter, katika siku hiyo walikuwa wanalewa na kucheza kipagani na kumtolea sadaka.

Lakini sisi wakristo hatuadhimishi/kusheherekea siku hiyo kipagani hivyo, bali siku ya kufufuka kwa Bwana ni siku ya kufanya ibada, ni siku ya kutafakari maisha yetu ya ukristo, tangu tumempokea Yesu mpaka sasa tumeshapiga hatua kiasi gani?..na kama tumerudi nyuma basi tutengeneze mambo yetu, ni wakati wa kutafakari ni mambo yako mangapi mazuri ya kiroho, yaliyokuwa yamekufa, na je yamefufuka!.. Kama bado ni wakati wa kutafuta kuyafufua.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

Sharoni ni nini au ni wapi kibiblia?(1Nyakati 5:16)

SHUSHANI NGOMENI NI WAPI KWA SASA?

Rudi nyumbani

Print this post

Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,

SWALI: Naomba kufahamu Zaburi 102:6 inamaana gani? Mwandishi anaposema..

Zaburi 102:6

[6]Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,

Na kufanana na bundi wa mahameni.


Mwari ni aina ya ndege ambao, wana midomo mirefu, na kifuko kikubwa shingoni ambacho wanatumia kuhifadhia chakula kabla hawajakimeza. Ni ndege ambao wanapendelea sehemu za maji maji ambapo inakuwa ni rahisi wao kupata samaki..(Tazama picha juu)

Lakini mwari anayezungumziwa hapa ni jamii nyingine ya jangwani tofauti na yule wa majini..Kwa kawaida ndege hawa(jamii zote) ni ndege wanaopenda sana kujitenga, huwezi wakuta wanatembea pamoja..na mara nyingine utawakuta wapo katika hali ya kupooza wakitumia masaa mengi hata siku wakiwa wameficha vichwa vyao chini ya mbawa zao. Kwa ufupi ni ndege wa upweke sana.

Ndivyo mwandishi wa zaburi alivyojifananisha na ndege hawa kwa upweke aliokuwa anaupitia

Lakini zaidi anajilinganisha pia na bundi wa mahameni.. Bundi ni ndege ambao wanajitenga pia..wanapendelea sehemu za majangwa au mapango au kwenye majumba yaliyoachwa zamani, au makaburini.

Katika hali hizo za unyonge huwa wanatoa milio ya ajabu ajabu hususani wakati wa usiku.

bundi wa mahameni

Wakati fulani niliwahi kwenda mlimani kusali, mlima huo ulikuwa mbali na makazi ya watu, na ulikuwa na mwamba mkubwa kwa nyuma..lakini kwa juu sikuona ndege yoyote isipokuwa bundi mmoja ambaye kila usiku unamsikia analia tu peke yake kwa kule juu…ni ndege wa upweke sana.

Ndivyo mtunzi wa Zaburi alivyokuwa anajifananisha na ndege hawa, kwa hali aliyokuwa nayo wakati huo.

Anasema tena nimekuwa kama shomoro  Aliye peke yake juu ya nyumba.

shomoro aliye peke yakeShomoro ni hawa ndege wadogo wanaotengeneza viota vyao kwenye pembe au mabati ya nyumba. Ni ndege ambao huwezi kuwakuta wanatembea mmoja mmoja.ikitokea hivyo ni aidha mmojawapo amekufa au mgonjwa.

Hivyo mtunzi wa Zaburi anaaeleza kimifano jinsi apitiavyo taabu kutoka kwa maadui wake, hali yake inavyofanana na hao ndege..jinsi aliavyo mbele za Mungu akimwomba amsikie.

Tusome tokea mistari ya juu kidogo;

Zaburi 102:1-8

1 Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, Kilio changu kikufikie.

2 Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi.

3 Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, Na mifupa yangu inateketea kama kinga.

4 Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka, Naam, ninasahau kula chakula changu.

5 Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu.

6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni.

7 Nakesha, tena nimekuwa kama shomoro Aliye peke yake juu ya nyumba.

8 Adui zangu wananilaumu mchana kutwa; Wanaonichukia kana kwamba wana wazimu Huapa kwa kunitaja mimi.

Umeona, lakini katika kuugua kwake kote, Bado, Mungu alikuwa tegemeo lake, na mwisho wa siku, ukiendelea kusoma utaona Mungu anasema..

Zaburi 102:16-21

16 Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni, Atakapoonekana katika utukufu wake,

17 Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao.

18 Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo, Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana.

19 Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu, Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi,

20 Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa, Na kuwafungua walioandikiwa kufa.

21 Watu walitangaze jina la Bwana katika Sayuni, Na sifa zake katika Yerusalemu,

Hii ni kuonesha kuwa maombi na dua za wacha Mungu si bure..Bwana anasikia na atawatoa katika taabu zao endapo hawataacha kumlilia.

Ikiwa unasumbuliwa na magonjwa au hali ambazo wewe mwenyewe umeshindwa kuziondoa..Fahamu kuwa ukimtumaini Bwana katika hali hiyo hiyo ya kuwa mwari na bundi atakuponya..kabisa kabisa, au kukupa haja yako.

Maombolezo 3:31-33

31 Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele.

32 Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.

33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.

Bwana akubariki.Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Lumbwi ni nini katika biblia?

Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

Neno ‘Kima’ linamaanisha nini Katika biblia? (Mathayo 27:9 )

Tofauti na “Kima” mnyama ambaye anajulikana (jamii ya nyani), ukirudi katika biblia Neno hili lina maana nyingine pia.

Kima maana yake ni “thamani ya kitu katika pesa”.

Kwa mfano tukisema kima cha nazi ni Tsh. 1000. Maana yake ni kuwa thamani ya nazi ni sh. 1000.

Kwamfano Neno hilo utalipata katika vifungu hivi;

Mithali 31:10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani”.

Yaani thamani mke mwema, inazidi thamani ya madini ghali ya Marijani (Ruby).

Mathayo 27:9 “Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima;”

Walawi 27: 11 “Na kama ni mnyama ye yote asiye safi, wa namna ambayo hawamsongezi kwa Bwana, basi atamweka huyo mnyama mbele ya kuhani;

12 na kuhani atamtia kima, akiwa mwema akiwa mbaya; kama wewe kuhani utakavyomtia kima, ndivyo itakavyokuwa.

13 Lakini kwamba ataka kumkomboa kweli, ndipo atakapoongeza sehemu ya tano juu ya hesabu yako.

14 Na mtu atakapoiweka nyumba yake iwe wakfu kwa Bwana ndipo kuhani ataihesabu kima chake hiyo nyumba, ikiwa njema ikiwa mbaya; kama kuhani atakavyoihesabu kima chake ndivyo itakavyokuwa”.

Soma pia Walawi 27:23, Ayub 18:28, Matendo 7:16

Je, kipo kima kinachozidi thamani ya Bwana Yesu?

Yuda alijaribu, kumsaliti Bwana kwa kima cha fedha, lakini Pamoja na kupokea mapesa yote, bado mwisho wa siku aliona, thamani yake hailinganishwi na utajiri wowote wa ulimwengu, ijapokuwa alikuwa ni mwizi lakini utaona alirudisha fedha zao zote, na kwenda kujinyonga.

Sasa Ikiwa watu waovu wanauona uthamani wa Bwana, hadi kwenda kujiua, iweje wewe uone kazi ni bora kuliko Bwana Yesu, anasa ni bora kuliko ibada?.

Je! thamani ya Bwana wako inazidi thamani ya huu ulimwengu? Bwana Yesu alisema Itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima halafu upate hasara ya nafsi yako? Itakufaidia nini?

Tubu mgeukie Bwana..

Ikiwa hujampa Bwana Yesu Maisha yako, na upo tayari kufanya hivyo leo, kwa kumaanisha kabisa, basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa Sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Konde la Soani ni nini? (Zaburi 78:12,43)

Deraya ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 59:17

Bushuti ni nini?

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Tunguja ni nini katika biblia? (Mwanzo 30:14).

Hisopu/ Hisopo ni nini katika biblia?(Zaburi 51:7)

Kuhusuru ni nini kibiblia? (Luka 19:43)

Kujuzu ni nini kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 12:4?

Rudi nyumbani

Print this post

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

Ni eneo la pango ambalo lilikuwa karibu na mji wa Israeli unaoitwa Hebroni, ambalo Ibrahimu alilinunua kwa mtu mmoja aliyeitwa Efroni, kwa ajili ya maziko ya mke wake Sara.

Mwanzo 23:13 “Akamwambia Efroni, na watu wa nchi wanasikiliza, akisema, Tafadhali unisikilize; nitatoa kima cha shamba, nawe ukipokee kwangu, nami nitamzika humo maiti wangu.

14 Efroni akamjibu Ibrahimu, akamwambia,

15 Bwana wangu, unisikilize. Sehemu ya nchi, ambayo thamani yake ni shekeli za fedha mia nne, n’nini hii baina yako na yangu? Basi uzike maiti wako.

16 Ibrahimu akakubali maneno ya Efroni. Ibrahimu akampimia Efroni ile fedha aliyotaja masikioni mwa wazawa wa Hethi, shekeli za fedha mia nne za namna inayotumika na wenye biashara”.

Eneo hilo baadaye lilikuja kugeuka kuwa kaburi la kifamilia, kwani hapo hapo ndipo Ibrahimu alipokuja kuzikwa na watoto wake, halikadhalika, ndipo Yakobo na Esau walipomzikia baba yako Isaka,

Na wakati wakiwa kule Misri, Yakobo aliwaagiza Watoto wake,pia  wakamzike katika kaburi hilo la familia, la Makpela.

Mwanzo 49:29 “Akawaamuru, akasema, Mimi ninakwenda kukusanywa pamoja na watu wangu; mnizike pamoja na baba zangu, katika pango iliyomo shambani mwa Efroni, Mhiti;

30 katika ile pango iliyomo shambani mwa Makpela, iliyo mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake ya kuzikia.

31 Humo walimzika Ibrahimu, na Sara mkewe; humo wakamzika Isaka, na Rebeka mkewe; nami humo nikamzika Lea;

32 shamba na pango iliyomo lililonunuliwa kwa wazawa wa Hethi”.

Eneo hilo kwasasa, pale Israeli limejengwa msikiti, ujulikanao kama “msikiti wa Ibrahimi”, japo wote wayahudi na waislamu, hakuna hata mmoja anaweza kusema anao umiliki wa moja kwa moja wa hapo.

Lakini Je pango la makpela lina umuhimu kwetu hadi sasa au kwa Wayahudi?

Pango hili, au lolote lile ambalo lilizikiwa watakatifu, halina umuhimu wowote katika Imani yetu, Zaidi ya mambo ya kihistoria tu. Myahudi au mkristo yoyote ukizikwa karibu na eneo hilo, hakutakufanya uende mbinguni, Wapo wengine wanafikiri, wakienda Yerusalemu na kuomba kwenye ule ukuta wa Nehemia wa maombolezo, ndio maombi yao yatasikiwa. Au wakienda kubatizwa katika mto Yordani kama Bwana Yesu ndio ubatizo wao utapokelewa, jambo ambalo sio kweli.

Halikadhalika na Pango hilo la makpela halina umuhimu wowote, kwa mtu yeyote, kuzikiwa pale.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?

Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango,ikiwamo mipira?

Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

Uru wa Ukaldayo ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

MAPENZI YA MUNGU NI YAPI?

Bwana Yesu alisema maneno haya katika Mathayo 7:21-23.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; BALI NI YEYE AFANYAYE MAPENZI YA BABA YANGU ALIYE MBINGUNI”

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Sasa unaweza kujiuliza hayo “Mapenzi ya Mungu ndio yapi” Kwasababu hapo tunaona kumbe hata unaweza kutoa pepo lakini ukawa bado huyafanyi mapenzi ya Mungu…vile vile unaweza ukawa unatabiri na kutoa unabii na unabii huo ukatimia lakini, bado ukawa mbali na mapenzi ya Mungu.

Sasa Mapenzi ya Mungu ni yapi?..ambayo tukiyafanya hayo hata kama tutakuwa hatutoi pepo wala kutoa unabii wala kutabiri bado tuta urithi ufalme wa mbunguni?.

Tusome,

1 Wathesalonike 4:2 “Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu.

3 Maana HAYA NDIYO MAPENZI YA MUNGU, KUTAKASWA KWENU MWEPUKANE NA UASHERATI;

4 KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE KATIKA UTAKATIFU NA HESHIMA;

5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.

Umeyaona Mapenzi ya Mungu?
Kumbe Mapenzi ya Mungu si miujiza wala upako, bali UTAKATIFU..

Kumbe hata tukiwa na Imani kubwa ya kuweza kugeuza maji kuwa asali bado upo uwezekano mkubwa wa kupotea katika ziwa la moto, kama HATUNA UTAKATIFU.

Hii ni tahadhari kubwa sana kwetu..Lakini biblia inazidi kulithibitisha hilo kwetu katika..

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, AMBAO HAPANA MTU ATAKAYEMWONA MUNGU ASIPOKUWA NAO” .

Ndugu yale maono unayoyaona katika ndoto, ni kweli ni ya kiMungu lakini hayo sio tiketi ya kukufikisha mbinguni, tiketi ya kukufikisha mbinguni ni utakatifu wa mwili na roho.

Ile imani iliyo nayo kiasi kwamba chochote utakachokisema kwa jina la Bwana kinatokea, sio tiketi ya kufika mbinguni kama hutaacha uasherati wako, au ulevi wako, au wizi wako au utukanaji wako.

Ile ahadi Mungu aliyokuonyesha kwa njia ya unabii au ndoto, sio tiketi ya wewe kuurithi uzima wa milele, kama hutadumu katika kuyafanya mapenzi ya Mungu (Yaani Utakatifu).

Uuimbaji unaoimba, unabii unaoutoa, lugha unazonena hazitakufikisha popote kama hutaamua kujitakasa kwa kuacha kuvaa vimini, kuacha kuvaa suruali (kama ni mwanamke), kuacha kujipaka uso rangi, kuacha kuvaa kope na kucha za bandia, kama hutaacha kuvaa hereni, wigi na kupaka lipstiki na kunyoa kiulimwengu..

Utauliza inamaana wanawake kuvaa suruali  na vimini sio mapenzi ya Mungu?..Jibu ni NDIO!. Rejea vizuri hiyo mistari…

“KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE KATIKA UTAKATIFU NA HESHIMA”.

Sasa jiulize vimini ni nguo za heshima?, Suruali ni nguo za heshima?..Je unaweza kwenda kumtambulisha mchumba wako kwa wazazi wako akiwa amevaa Suruali?? Au vimini??..Kama huwezi basi jua hayo sio mavazi ya heshima na hayafai..na mapenzi ya Mungu ni “kila mtu kuuweza mwili wake kwa utakatifu na Heshima

Kama hutaacha hayo yote, na umesikia kama hivi, basi siku ile utatimiza huu unabii unaosema.. “wengi watasema siku ile wakisema, hatukufanya hichi au kile” na Bwana atawakataa dhahiri.

Mimi na wewe na ndugu zetu tusiwe watu hao watakaotimiza huo unabii.

Bali tujiepushe na dhambi na kujitakasa, ndivyo tutakavyofanya mapenzi ya Mungu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je suruali ni vazi la kiume tu?

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?.

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Watu wenye ulemavu wa akili, wataenda mbinguni?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Jibu: Uwezo na Uweza ni kitu kimoja.. tofauti ni kwamba kimoja kinatumika kwa Mungu na kingine kwa wanadamu.

Wanadamu na wanyama na shetani na malaika na viumbe vingine vyote vinao UWEZO wa kufanya mambo. Lakini havina UWEZA wa kufanya jambo.

Mwenye UWEZA wa kufanya jambo ni Mungu tu peke yake.

Mwanadamu ana UWEZO wa kuua lakini wa kuurudisha Uhai hana…kwasababu kuurudisha uhai ndani ya mtu kunahitaji UWEZA, na UWEZA huo anao Mungu tu.

1 Wakorintho 6:14 “Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa UWEZA wake”.

Vile vile mwanadamu na shetani wanao UWEZO wa kuipotosha roho, lakini Kuiokoa hawawezi!..Kwasababu kuiokoa roho ya Mwanadamu inahitajika UWEZA na sio UWEZO. NA Uweza huo ni Mungu tu! Ndio anao.

Warumi 1:16 “Kwa maana siionei haya Injili; KWASABABA NI UWEZA WA MUNGU UULETAO WOKOVU, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia”.

Swali ni je!..Unawatumainia wenye UWEZO au mwenye UWEZA?.

Shetani anao uwezo wa kukupa mali lakini si Uzima wa milele!, Wanadamu wana uwezo wa kukupotosha lakini wa kukuokoa hawawezi.

Mwanadamu anao uwezo wa kutibu, lakini kuponya hawezi, Mwenye Uwezo wa kuponya nk Mungu tu peke yake.

Unaweza kusoma pia juu ya Uweza wa Mungu katika Nehemia 1:10, Nehema 9:32, Marko 12:24, na Matendo 8:10.

Kwanini usimtumainie huyo mwenye uweza wa kufanya mambo yote, huyo ndio wa kumtumainia na vile vile wa kumwogopa..

Luka 12:5 “Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumwua mtu ana UWEZA wa kumtupa katika Jehanum; naam, nawaambia, Mwogopeni huyo”.

Na sasa UWEZA huo wa kiungu upo juu ya Bwana Yesu Kristo pekee, ambaye mamlaka yote ya mbinguni na duniani, amekabidhiwa yeye.

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,Tumepewa mtoto mwanamume; Na UWEZA wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani”.

Je umempokea Yesu?..kama bado unasubiri nini?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Tofauti ya deni na dhambi ni nini?

Roho Mtakatifu ni nani?.

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

MFANYE BWANA YESU MWENYEJI MAISHANI MWAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Kuna njia kuu sita(6)

Ni vema ukazifahamu hizi njia Mungu anazozungumza na watu, ili usitegemee tu njia moja uifahamuyo wewe, matokeo yake ukakosa shabaha ya kuzisikia sauti za Mungu kila siku maishani mwako zinapozungumza na wewe.

1. Ya kwanza ni Njia ya moja kwa moja:

Hii ni Aidha kwa Sauti, ndoto, au maono,

Ni mojawapo ya njia ambayo Mungu anazungumza na watu. Na ndio inayojulikana na kutegemewa na wengi.

Ayubu 33:14-15

[14]Kwa kuwa Mungu hunena mara moja,  Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. [15]Katika ndoto, katika maono ya usiku,  Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

Katika maisha yetu kwa namna moja au nyingine Mungu alishazungumza nasi kwa njia hii. Unaweza usione, maono au usisikie sauti lakini kila mtu huwa anaota. Na kwa njia hiyo Mungu huzungumza.

  1. Kwa njia ya Neno lake:

Hii ndio sauti ya Mungu namba moja ambayo inazungumza na mtu moja kwa moja na kwa wakati wote..ni sauti ambayo hailinganishwi na sauti nyingine zozote.

Ukiwa ni msomaji mzuri wa Neno, utamsikia Mungu katika nyanja zote za Maisha akikufariji, akikuonya, akikushauri, akikuongoza n.k. Ni pakeji iliyojitosheleza., ambayo hailinganishwi na njia nyingine yoyote.

2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;”

    3. Njia nyingine ni Amani.

Ikiwa wewe umeokoka, na umejazwa Roho Mtakatifu, basi ujue mara nyingi sana Mungu atatumia amani yake moyoni mwako kuamua mambo mengi..

Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 10:11-13

[11]Na mji wo wote au kijiji cho chote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; mkae kwake hata mtakapotoka. [12]Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni.

[13]Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.

Wakolosai 3:15a “Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu;..”

Kuonyesha kuwa amani itokayo kwa Roho ni sauti ya Mungu kutuongoza, ikiwa umepoteza amani ghafla katika mazingira fulani kuwa makini sana hapo. Wakati mwingine ni Mungu anazungumza.

   4. Kwa kupitia watu.

Hapa anaweza akachagua aidha apitie mtu mwovu au mtu mwema. Mara nyingi sana Mungu anazungumza na watu kupitia watumishi wake, yaani wahubiri, waalimu, wainjilisti n.k.

Yeremia 25:4

[4]Naye BWANA ametuma kwenu watumishi wake wote, hao manabii, akiamka mapema na kuwatuma, lakini ninyi hamkusikiliza, wala hamkutega masikio yenu, msikilize.

Na mara nyingine tena anaweza kutumia watu wa kidunia kukuonya..kama vile maaskari, wakuu wa hii dunia n.k.

Hivyo ni kuzingatia sana unachokisikia au kufundishwa au kuonywa na watu, hususani watumishi wa Mungu..Mara nyingine sauti ya Mungu ipo nyuma yao.

     5. Kwa kupitia mazingira.

Mazingira yanaweza yakawa ya kimaisha, au ya kihali…kwa mfano Mungu akitaka uelewe jambo fulani, wakati mwingine hatumii sauti ya moja kwa moja, kwasababu pengine unaweza kulichukulia juu juu tu au usimwelewe, hivyo atakupitisha katika maisha fulani au mazingira fulani, na kwa kupitia hayo utajua kabisa hapo ni Mungu alikuwa akisema na wewe.

Mfano wa watu kama hawa alikuwa ni Nebukadreza, yeye alionywa na Mungu, awe mnyenyekevu na amche Mungu, lakini hakusikia, kinyume chake akapuuzia ule unabii aliopewa na Danieli. Matokeo yake baada ya miezi 12, akageuzwa kuwa kama mnyama, akawa anaishi huko misituni akila majani kama ng’ombe..mpaka siku alipoelewa somo kuwa aliye juu ndiye anayetawala falme zote za duniani. Ndipo akajinyenyekeza ,hivyo Mungu akamrudishia ufalme wote wa dunia. (Danieli 4)

   6. Kwa kupitia vitu vya asili na viumbe.

Sauti ya Mungu imejificha sana katika vitu vinavyotuzunguka na asili, kiasi kwamba tungefahamu vema basi tusingekuwa na ugumu wa kumwelewa Mungu.

Embu fikiri Bwana Yesu alivyotuambia..tafakarini Kunguru?..hawapandi hawavuni wala hawana maghala ya chakula lakini wanakula..Je sisi si mara nyingi zaidi ya hao? (Luka 12:24)

Hili ni neno ambalo lilikwepo tangu enzi na enzi kiasi kwamba watu wangekuwa wanalitafakari kabla hata ya Yesu, wasingekuwa na hofu ya maisha pale wanapotaka msaada kutoka kwa Mungu.

Vivyo hivyo utazamapo, bahari, milima, miti,  zipo sauti nyingi sana za Mungu nyuma yake .. Chukua muda mwingi kutafakari, utaisikia sauti ya Mungu waziwazi.

Mungu alimwambia Ibrahimu angalia juu tazama nyota za mbinguni na mchanga wa baharini upate imani kwangu.

Hivyo ni vizuri ukapata maarifa haya usije ukaangamia kwa kutomwelewa Mungu. Leo hii watu wanategemea njia moja tu..ile ya moja kwa moja..yaani kusikia sauti, au kuona maono au kuota ndoto. Na kusahau hizi nyingine.. Ndio hapo utasikia wakisema nimeomba sana, nimelia sana Mungu aseme na nini, lakini sijawahi kumsikia.

Ni kwanini? Nikwasababu wanalazimishia njia hiyo hiyo moja Mungu aseme nao..

Hawajui kuwa Mungu hapangiwi fomula ya kuzungumza.Hivyo wewe uombapo..kuwa mtulivu, soma sana Neno mtafakari Mungu..subiri azungumze kwa jinsi apendavyo yeye. Atakujibu tu aidha kwa Neno lake, au mtumishi wake, au amani moyoni mwako, au kwa kutazama mambo ya asili, ukiona hivyo basi ujue ni Mungu huyo.

Hivyo kaa katika utulivu wa Roho, zingatia kusoma Neno..kwasababu maarifa kama haya utayapata katika biblia na sio kwa kuota au kuona maono.

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

Unyenyekevu ni nini?

ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.

Rudi nyumbani

Print this post

ENZI NA MAMLAKA AMEZIFANYA KUWA MKOGO

Jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Wakolosai 2:14 “akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

15 AKIISHA KUZIVUA ENZI NA MAMLAKA, NA KUZIFANYA KUWA MKOGO KWA UJASIRI, akizishangilia katika msalaba huo”.

Je unajua maana ya Mkogo? (mkogo ni nini?)

Mkogo ni neno lenye maana ya “tamasha”.. kwamfano watu wanaofanya tamasha la sarakasi, ni sawa na kusema wanafanya “mkogo wa sarakasi”

Hivyo hapo maandiko yaliposema “Bwana Yesu amezivua enzi na Mamlaka na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri”..Maana yake “amezivua enzi na mamlaka na kuzifanya kuwa tamasha kwa ujasiri”.

Sasa swali, ni Enzi gani na Mamlaka gani, Bwana Yesu aliyavua?.. ni yake mwenyewe au mengine?

Jibu: Enzi na mamlaka yaliyovuliwa hapo na Bwana sio yake yeye mwenyewe.. bali ni yale ya NGUVU ZA GIZA. Bwana amemvua shetani juu ya huu ulimwengu na wanadamu kwa kifo chake pale msalabani.. Na baada ya kumvua, akayavaa yeye mamlaka hayo.. (kumbuka mamlaka hayo ya shetani alimvua Adamu, pale Edeni).

Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, NIMEPEWA MAMLAKA YOTE MBINGUNI NA DUNIANI”.

Huu ulimwengu sasahivi upo chini ya mamlaka ya Bwana Yesu, shetani ni kama mpangaji tu!..nyakati na majira yatakapotimia ataondolewa moja kwa moja. Hivyo shetani sasahivi si kitu kwa Bwana Yesu..

Yohana 14:30 “Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, WALA HANA KITU KWANGU”.

Sasa ni wakati gani ambapo Enzi na mamlaka yalifanyika mkogo (yaani tamasha)?

Ni wakati Bwana Yesu akiwa msalabani, wakati dunia inaona ni kifo cha aibu, lakini Bwana yeye aliona ushindi, wakati wachache wanamhuzunikia na kumlilia pale msalabani.. yeye (Bwana) alikuwa anashangilia ushindi, na kuonyesha tamasha la wazi kwa ujasiri, jinsi shetani na majeshi yake yalivyokuwa yanavuliwa mamlaka pale msalabani.

Wakolosai 2:15 “akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo”.

Bwana leo hii anatawala mbinguni na duniani, shetani hana lolote mbele zake.

Je kwanini tusimtumainie leo huyo?.. Kwanini tusimfanye kuwa nguzo ya Maisha yetu?..yeye ambaye amemvua shetani mamlaka na enzi. Hata sasa tunapozungumza Bwana Yesu anamiliki vitu vyote vya mbinguni na duniani, na vilivyopo chini ya dunia, na vitu vyote vinapiga goti, na vitapiga goti mbele zake.

Tukimwelewa Yesu kwa namna hii, kamwe hatutamtamani shetani na Fahari zake, na pia hatutamwogopa shetani, wala hatutawaogopa wachawi.. Ukiona unahofu ya shetani, au wachawi na umesema umeokoka au umempokea Yesu, basi jua bado hujamjua Bwana Yesu vizuri.

Siku ukimjua na kumwelewa, hutabaki kama ulivyo.

Mpokee Yesu, mtumainie Bwana.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

TUMEKUWA TAMASHA KWA DUNIA; KWA MALAIKA NA WANADAMU.

ZUMARIDI NI MADINI GANI?

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?

Hapo ndipo, atakapompa Mungu Baba ufalme wake.

Rudi nyumbani

Print this post