Title August 2022

KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MAENEO YA IBADA: Sehemu ya 1


KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

Kuna mambo ambayo yanaonekana madogo, lakini yana madhara makubwa sana rohoni. Watu hawafahamu kuwa wanaweza kufa kabisa kiroho kwa tabia ya kuendekeza USINGIZI ibadani..

Embu tusome habari ya Eutiko, tuone ni jambo gani Bwana anataka tufahamu nyuma ya matukio yaliyokuwa yanaendelea pale..

Tusome.

Matendo ya Mitume 20:7-10

[7]Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.

[8]Palikuwa na taa nyingi katika orofa ile tulipokuwa tumekusanyika.

[9]Kijana mmoja, jina lake Eutiko, alikuwa ameketi dirishani, akalemewa na usingizi sana; hata Paulo alipoendelea sana kuhubiri, akazidiwa na usingizi wake akaanguka toka orofa ya tatu; akainuliwa amekwisha kufa.

[10]Paulo akashuka, akamwangukia, akamkumbatia, akasema, Msifanye ghasia, maana uzima wake ungalimo ndani yake.

Nataka tuyatathimini hayo mazingira..kwanza walipokuwa wanasilizia injili ni katika gorofa, na gorofa yenyewe si ya kwanza bali ni ya tatu.. 

Pili japokuwa mahali pale ilikuwa ni usiku lakini biblia inatuambia kulikuwa na taa nyingi sana..maana yake ni kuwa mazingira yote yalikuwa yanaonekana, yapo wazi hivyo mahali pa hatari palionekana, na mahali salama pia palionekana.

Lakini tunaona huyu Eutiko alichagua kwenda kukaa katika dirisha la gorofa, akijua kabisa mahali pale si salama kukaa endapo akiteleza kidogo na kuanguka..

Lakini hakujali hilo, baada ya muda kidogo akasinzia.. Na matokeo yake akaanguka kutoka katika ile gorofa ya tatu. Na alipofika chini alikuwa tayari ameshakufa..

Ni kwanini habari hii iandikwe hapa? Kumbuka kila hadhithi inayoandikwa katika biblia inafundisho kubwa sana nyuma yake.

Sasa kitendo cha kuwepo katika gorofa ya tatu.

Inamaanisha kuwa mahali popote Neno la Mungu, linahubiriwa, au ibada inaendelea, iwe ya jumapili, au fupi ya maombi au mikesha, Rohoni mnakuwa mmechukuliwa mpaka mbingu ya Tatu (ndio ile gorofa ya tatu), juu sana mahali ambapo Mungu yupo na kiti chake cha enzi kilipo.

Na huko kuna Nuru nyingi, kama tulivyoona jinsi taa nyingi zilivyokuwa pale gorofani. Ikiwa na màana kuwa wakati unajaribu kuchagua kusogea mbali na uwepo wa Mungu utatambua kabisa mahali ulipo si salama..

Tabia ya kusinzia inakutuma ukae dirishani mwa uwepo wa Bwana na sio ukumbini. Ni kuonyesha jinsi gani usivyo “siriazi” na Mungu.

Na hatimaye unaanguka kutoka uweponi mwa Bwana..na kufa moja kwa moja kiroho.

Leo imekuwa ni desturi na mtu/watu wengi kila wafikapo nyumbani kwa Mungu ni lazima wasinzie, na wenyewe wanaona ni kawaida, wanadhani pale ni sawa na ofisini kwao, au shuleni kwao, ambapo hakuna jambo lolote la rohoni linalokuwa linaendelea.

Wanasahau kuwa wamepewa neema ya kupandishwa hadi kwenye kiti cha enzi cha Mungu, lakini wanakaa madirishani.

Ndugu ikiwa wewe ni mmojawapo wacha hii tabia, ukiindekeza utaanguka na kufa kabisa kiroho. Nimeona watu wengi wenye tabii hii, wakirudi nyuma ulimwenguni, wengine wakichuliwa na mawimbi ya ibilisi.

Kuwa siriazi na Mungu wako, tambua kilichokupeleka pale, unapoona wengine hawasinzii, haimaanishi kuwa hawahisi usingizi kama wewe, wanahisi lakini watalalaje mbele ya kiongozi wao mkuu? Wanaogopa kumvunjia heshima yake. Vilevile wanataka wapokee kikamilifu kile kilichowapeleka pale,

Hivyo kataa usingizi na wenyewe utakukimbia, na hiyo inakuja kwa kuzingatia kwa makini kile  kinachoendelea pale, mawazo yako yote yakiwa pale, ukijua kabisa kila siku ni mpya nyumbani kwa Bwana, na Mungu anatembea.

Lakini kama utaenda kwa desturi na mazoea, au kukamilisha ratiba, utakuwa ni mtu wa kulala lala na siku moja utakufa kabisa kiroho kwasababu uwepo wa Mungu umekwisha kukuacha. Mheshimu Mungu.

Bwana atasaidie sana.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MIMI NI ALFA NA OMEGA.

DHAMBI YA MAUTI

YESU ANA KIU NA WEWE.

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

Sikio lisikialo, na jicho lionalo, BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

Rudi nyumbani

Print this post

Tufanyaje ili tuonekane tunampenda Mungu?

SWALI: Naomba kufahamu kumpenda Mungu kukoje, Je tufanyeje ili tuonekane tunampenda?


JIBU: Tofauti na sisi tunavyotafsiri upendo, kwamba ni kuonyesha hisia zilizo nzuri kwa mwingine, Kwamfano kuhurumia, kujali, kuthamini, kuhudumia, kusifia, kujitoa n.k.

Lakini kwa Mungu ili tuonekane tunampenda yeye, ni zaidi ya kuonyesha hisia.. Kwani waweza kuwa na hisia nzuri kwa Mungu, mpaka ukatoa machozi, unapotafakari matendo yake makuu, Unapotazama wema wake na fadhili zake, na uumbaji wake wote, vikakufanya ujihisi kumpenda sana Mungu.

Lakini hili mbele za Mungu linaweza lisihesabike, kwasababu si kile Mungu anachotaka kukiona kwetu..

Hivyo ni vizuri kufahamu mambo haya makuu matatu (3), ambayo  ukifanya bidii kuyatenda, bila hata kuonyesha hisia Fulani kubwa,  Mungu atakuona unampenda sana, na matokeo yake atajidhihirisha kwako. Mambo yenyewe ni haya;

1). Zishike amri zake:

Amri zake ni pamoja na kukaa mbali na dhambi, halikadhalika, kupendana sisi kwa sisi.

Biblia inasema..

1Yohana 5:3 “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.

4 Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu”.

Umeona, Bado Bwana Yesu analirudia tena hilo hilo neno katika

Yohana 14:15 Mkinipenda, mtazishika amri zangu.

16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;

Na amri yake iliyo kuu aliyotupa, ni kupendana sisi kwa sisi, kama nafsi zetu (Yohana 13:34), na zaidi kuwapenda mpaka wale wanaotuchukia. Tukizingatia hayo mambo mawili, huku tukijilinda na dhambi, kwa maisha ya utakatifu, hiyo ni dalili ya kwanza inayofunua upendo wetu wa kweli kwa Mungu.

2) Uchukie ulimwengu:

Kuupenda ulimwengu kunakwenda kinyume na kumpenda Mungu, biblia inasema hivyo katika;

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

Ukisema unampenda Mungu, halafu, bado unapenda fashion, unapenda anasa, unapenda party party, na tafrija tafrija, mipira, muvi muvi kila wakati, miziki ya kidunia, kampani za wenye dhambi, vijiwe vijiwe visivyo na maana.

Basi ufahamu upendo kwa Mungu hautakaa uwepo ndani yako, Biblia inasema hivyo. Jitenge na mambo ya kiulimwengu kwa jinsi uwezavyo, tafuta ndugu katika Bwana ndio wawe watu wako wa karibu, biblia ndio iwe novel yako, nyimbo za sifa ndio ziwe mziki wako, kanisani ndio pawe kijiweni pako. Ukizingatia hayo kwa bidii, basi kidogo kidogo, upendo kwa Mungu usio wa kinafki utaingia ndani yako. Na Mungu atauona.

3) Husisha kila kitu chako chote kwa ajili ya Mungu:

Biblia inasema..

Marko 12:29 “Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;

30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote”.

Hapo hajasema, “mpende tu Bwana Mungu wako”, halafu basi, bali anasema utampenda kwa mambo yote manne, yaani roho, moyo, mwili na akili.

Mungu hataki kupendwa kwenye roho tu, bali hata kwenye akili zako, na nguvu zako. Ikiwa unafikiria Mungu anataka umtafute tu siku za ibada, umwabudu halafu basi, bado hujakamilisha kumpenda, bali anataka nguvu zako unazokwenda kuzisumbukia huko katika kutanga tanga kwako ziishie kwake, Mali zako, kujitoa kwako katika kuujenga ufalme wa Mungu, na kusambaza habari zake.

Vilevile akili yako yote uitumie kwake, ubuni utafiti ni kwa jinsi gani, unaweza kuifanya kazi ya Mungu iwe bora zaidi, kama vile unavyofikiri kila siku ni jinsi gani unavyoweza kuyafanya maisha yako kuwa bora kwake, sio tu kumwachia mtumishi Fulani,au mchungaji Fulani afanye yeye kila kitu, angali vingine vipo ndani ya uwezo wako wewe.

Kwa kuzingatia mambo hayo matatu, basi utakuwa umempenda Mungu, na yeye atalijua hilo, na matokeo yake ni kujidhihirisha kwako, na kukuhudumia. Huko ndio kumpenda Mungu.

Zaburi 91:14 “Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.

15 Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;

16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?

Rudi nyumbani

Print this post

Ila atapewa mara mia sasa,Ndugu wake(Marko 10:30)

SWALI: Mbona katika Marko 10:30 Bwana Yesu anasema tutapata mara mia ‘wake’? Hii si inatupa uthibitisho kuwa ndoa za mitara ni sawa?


JIBU: Tusome kwa ukaribu vifungu vyenyewe;

Marko 10:28 “ Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.
29 Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au
ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, NA NDUGU WAKE, na mama,
na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho; na wa mwisho watakuwa wa kwanza”.

Hapo hakuna mahali popote Bwana Yesu amesema tutapata mara mia ‘wake’, isipokuwa anasema tutapata mara mia  “ndugu wake”.  Akimaanisha ndugu wa KIKE, kama tu alivyosema ndugu WAUME, tutapata mara mia.

Maana yake ni kwamba mtu yeyote anayeingia gharama ya kumfuata Yesu kwa moyo wake wote, na kwa ajili ya injili yake, Bwana ameahidi kumrudishia kila kitu alichokipoteza mara100 zaidi.

Ikiwa aliwaacha dada  zake kumi(10), basi Bwana atamrudishia ndugu wadada mara mia zaidi.. yaani ndugu wadada elfu moja (1000), watakuja kuwa karibu naye.. wenye upendo kama tu ule wa wale wa kwanza   kwake.

Lakini tuseme, labda tuliacha wake zetu kwa ajili ya injili, Je! Mungu hataturudishia thawabu mara mia kwa kuwaacha wao?

Jibu ni kwamba ataturudishia pia mara mia, lakini haimaanishi kuwa tutapewa ‘wake’ tuwaoe, hapana, bali tutapewa ndugu, wenye Usaidizi kama tu wa wake.. Kumbuka, mwanamke aliumbwa kuwa msaidizi wa Adamu, hakuumbwa kuwa chombo cha starehe..

Hivyo hudumu aliyoitiwa mke duniani ni kuwa msaidizi.. Vivyo hivyo Mungu atakunyanyulia ndugu ambao watasimama kama wasaidizi kwako katika huduma, mara mia, kama wake.

Lakini haimaanishi utawaoa, hapana, kama itakavyokuwa kwa ndugu mara mia atakaokupa, hawataingia kwenye tumbo la mama yako na kuzaliwa ili wawe ndugu yako, bali watatoka nje, na kusimama kama ndugu.. Vivyo hivyo na kwa watoto na mambo mengine yote.

Lakini kwanini iwe hivyo? Ni ili kulitimiza lile neno la Bwana Yesu alilosema..

 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake
kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha”.(Luka 9.24)

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TWEKA MPAKA VILINDINI.

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000

MADHARA YA KUTOIJUA KWELI YOTE!

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

IJUE HEKIMA YA MUNGU KATIKA KUKUINUA KIMAISHA.

Ipo hekima ambayo Mungu anaitumia, pindi anapotaka kututoa katika hatua moja ya kimaisha kwenda nyingine.

Kiasili, nafsi zetu sisi wanadamu zinapenda kupokea majibu ya maombi pale tu tunapoomba… Lakini hekima ya Mungu wakati mwingine si kutupa kile tunachokiomba wakati ule ule tunapoomba… Wakati mwingine inaweza kuchukua muda mrefu kupokea majibu, na bado ikawa ni mapenzi ya Mungu.

Yapo mambo ambayo tukimwomba Mungu, ni rahisi kupokea majibu papo kwa hapo, lakini yapo ambayo yatachukua muda kujibiwa!..Sasa si kwasababu Mungu hawezi kujibu papo hapo! La!, anaweza kwasababu hakuna kinachomshinda yeye, lakini anapoyachelewesha wakati mwingine kwa faida yetu.

Hebu tengeneza picha, mtoto wa miaka 6 ambaye hajui hata kusoma, anamwomba Baba yake ambaye ni tajiri sana, ampe gari!.. Ni kweli Baba yake anao uwezo wa kumpa gari pale pale alipoomba, lakini hawezi kumpa kwasababu bado hajajua hata kusoma, atawezaje kuendesha hilo gari?..kwasababu aendapo akipewa gari katika akili hiyo aliyonayo, kitakachofuata ni Ajali!.. na mzazi atakuwa amemwua mtoto wake, badala ya kumpa uzima!..

Kwahivyo Ni sharti kwanza aende darasani akafundishwe kusoma na kuandika, na hesabu.. halafu akishajua hayo yote, ndipo aende kwenye shule ya udereva, akajifunze kanuni za uendeshaji magari, na baada ya kuhitimu na kupata leseni, ndipo baba yake ampe gari!..

Hivyo zoezi zima hilo la kusoma mpaka kupata leseni mpaka siku ya kukabidhiwa gari, linaweza kuchukua miaka hata 10. Kwahiyo ni sawa na kusema kwamba, mtoto kajibiwa ombi lake la kupewa gari baada ya miaka 10.

Lakini endapo mtoto Yule angeomba “peremende” kwa Baba yake, ni dhahiri kuwa “angepatiwa muda ule ule alioomba”.

Na kwa Mungu wetu ni hivyo hivyo, yapo mambo ambayo tukiomba tutajibiwa wakati huo huo, lakini yapo mambo mengine yatachukua muda mrefu sana, hata miaka kadhaa kujibiwa!!…

Hivyo kama umezoea kumwomba Mungu jambo na kupokea majibu yake saa hiyo hiyo, na ukamwomba jambo lingine ukaona hujajibiwa muda huo huo kama unavyotaka wewe!!.. Fahamu kuwa sio kwamba Mungu kakunyima hilo jambo, au kwamba hajasikia maombi yako!.. Amesikia maombi yako, na tayari majibu kashayaachia, lakini yatakuja kudhihirika siku nyingi za mbeleni endapo ukidumu katika kuishikilia ahadi hiyo.

Hebu tujifunze mfano mmoja juu ya wana wa Israeli, kipindi wanatoka Misri..

Tunasoma katika maandiko kuwa, kipindi wanaingia Kaanani, Mungu hakuwatoa wakaanani katika ile nchi ndani ya siku moja, au ndani ya mwaka mmoja, biblia inasema ilichukua miaka kadhaa, Mungu kuwaondoa Wakaanani na wengineo waliokuwa wanaikalia ile nchi ya Ahadi.

Sasa ni kwasababu gani Mungu hakuwaondoa Wakaanani wote na wahivi wote ndani ya siku moja??..Jibu: Si kwasababu hakuwa na uwezo huo, alikuwa nao tele, lakini kwafaida ya watoto wake Israeli, ilikuwa hana budi kuwapa urithi huo kidogo kidogo!…kwasababu angewapa siku ile ile, basi yangezuka matatizo mengine, ambayo tunayasoma katika mistari ifuatayo…

Tusome,

Kutoka 23: 27 “Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao. 

28 Nami nitapeleka mavu mbele yako, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako. 

29 SITAWAFUKUZA MBELE YAKO KATIKA MWAKA MMOJA; NCHI ISIWE UKIWA, NA WANYAMA WA BARA WAKAONGEZEKA KUKUSUMBUA. 

30 NITAWAFUKUZA KIDOGO KIDOGO MBELE YAKO, HATA UTAKAPOONGEZEKA WEWE, NA KUIRITHI HIYO NCHI” 

Umeona hapo?..Sababu ya wao kutopewa Nchi yote ndani ya siku moja, ni lli wanyama wasiongezeke juu ya nchi, na kuwaletea madhara.. Kwasababu kipindi wanatoka Misri, walikuwa wachache.. halafu wanakwenda kupewa nchi kubwa!.. ni lazima sehemu kubwa ya nchi hiyo itakuwa MAPORI!.. Kwasababu hakuna watu wa kuijenga wala kukaa juu yake..na hivyo Nyoka wataongezeka, chatu na fisi wataongezeka, watakaokula mifugo yao..hali kadhalika samba na mbu!, watakuwa wengi kwasababu ya wingi wa mapori, na hivyo itanyanyuka shida nyingine..

Kwahiyo hekima ya Mungu, ikaamua maadui wa Israeli wasifukuzwe wote, bali waachwe kwanza kwa kitambo kifupi, waendelee kufyeka mapori, mpaka idadi ya Israeli itakapoongezeka, kufikia kiwango cha kuweza kuitawala nchi nzima, ndipo maadui wote waondolewe!.

Na sisi ni nini tunajifunza hapo?…tunajifunza kuwa wavumilivu, na kuwa na Subira katika ahadi za Mungu na kwamba si kila ombi litajibiwa siku tunayoitaka sisi.

Ikiwa wewe ni binti au kijana, na umemwomba Mungu akupe mwenza wa maisha, na unaona hujibiwi kwa wakati unaotaka wewe, huenda ni kwasababu wakati wake haujafika! Aidha Umri wako ni mdogo, au pengine akili yako bado haijakuwa vya kutosha, bado haijafundishwa vya kutosha maisha ya ndoa,.. Na ili Mungu asikupoteze ndio maana hakupi unachotaka kwa wakati huo huo.

Vile vile Ukimwomba Mungu mali na huku akili yako inawaza kwenda kujionyesha mbele za watu, fahamu kuwa Mungu ameshasikia maombi yako, lakini hutapokea saa hiyo hiyo, ulipopmba…badala yake utakwenda kwanza kwenye madarasa yake ambayo atakufundisha maisha ukiwa na mali, (huenda yakachukua hata miaka 20), inategemea na akili yako, na ukifaulu madarasa yake! basi atakupatia!..kwasababu utakuwa umeshajengeka vya kutosha, kiasi kwamba mali haziwezi kukuangusha wala kukurudisha nyuma kiroho, wala kuwaharibu wengine.

Na maombi mengine yote ni hivyo hivyo..yanayo hatua mpaka tuone matokeo, hivyo tuwe wavumilivu na watu wa subira..

Bwana Yesu atubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

IJUE SIRI YA UTAUWA.

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

Tofauti kati ya lijamu na hatamu ni ipi kibiblia?

Kigao ni nini? Na Je kinafunua nini kwa agano jipya?

Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Kaanani ni nchi gani kwasasa?

Kaanani ni jina la zamani la nchi za Mashariki ya kati!..Eneo la Kaanani liliundwa na sehemu ya nchi zifuatazo, Nchi ya Israeli yote, pande za Magharibi mwa nchi ya Yordani, Kusini mwa nchi ya Lebanoni na nchi ya Palestina yote.

Nchi ya Kaanani, hapo kwanza ilikuwa inakaliwa na watu waliojulikana kama Wakaanani, ambao biblia inawataja kama watu waliokuwa wenye sifa na wenye maumbile makubwa. Ndio maana tunasoma kipindi wale wapelelezi wa Kiisraeli walipotumwa kuipeleleza nchi hiyo ya Kaanani, walirudi na ripoti ya kuogopesha, wakasema wamekutana na Wanefili ndani ya hiyo nchi.

Hesabu 13:31 “Bali wale watu waliopanda pamoja naye wakasema, HATUWEZI KUPANDA TUPIGANE NA WATU HAWA; KWA MAANA WANA NGUVU KULIKO SISI.

 32 Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; NA WATU WOTE TULIOWAONA NDANI YAKE NI WATU WAREFU MNO. 

33 KISHA, HUKO TULIWAONA WANEFILI, WANA WA ANAKI, WALIOTOKA KWA HAO WANEFILI; TUKAJIONA NAFSI ZETU KUWA KAMA MAPANZI; nao ndivyo walivyotuona sisi”.

Nchi ya Kaanani Mungu alimpa Ibrahimu na uzao wake wote, Ndio maana Wakaanani waliokuwa wanaishi katika nchi hiyo (Hao wanefili) Mungu alikuja kuwaondoa kwa mkono hodari..

Mwanzo 17:7 “Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako. 

8 Nami nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao”

Baada ya Israeli kuitwaa Sehemu ya nchi ya Kaanani, waliibadilisha jina na kuiita Nchi ya Israeli. Na tangu wakati huo mpaka leo, inajulikana kama nchi ya Israeli, Ingawa si sehemu yote, sehemu nyingine ya Kaanani, Mungu hakumalizia kuwapa wana wa Israeli, kwasababu walikengeuka na kuanza kuingia maagano na wakaanani.

Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi; 

2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani? 

3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu

4 Ikawa, hapo huyo malaika wa Bwana alipoyanena maneno haya, kuwaambia wana wa Israeli wote, ndipo hao watu wakainua sauti zao na kulia” 

Kiroho, safari ya wana wa Israeli, kutoka Misri kwenda Kaanani, inafananishwa na safari yetu sisi ya kwenda Mbinguni (kwenye nchi yetu ya Ahadi) kutoka katika Ulimwengu wa dhambi.

Na kama jinsi safari ile ilivyokuwa na Majaribu mengi njiani, kiasi kwamba walioanza Safari kuanzia mwanzo hadi mwisho walikuwa ni wachache sana, yaani watu wawili tu (Yoshua na Kalebu). Vivyo hivyo safari ya kwenda mbinguni ni mapambano, kwasababu watakuwa wachache sana watakaoshinda…

Luka 13:22 “Naye alikuwa akipita katika miji na vijiji, akifundisha, katika safari yake kwenda Yerusalemu. 23  Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia,

24  Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze”

Hapo anasema TUJITAHITI!!..maana yake ni kwamba “JITIHADA BINAFSI PIA ZINAHITAJIKA” .. Si suala la kukaa tu na kuomba na kusubiri!…bali ni suala la kutia bidii pia!!…Wengi watakaoikosa mbingu ni kwasababu ya kutotia bidii kuutafuta ufalme wa Mungu!..(maana yake ni watu wasio na jitihada katika mambo ya kiMungu).

Sasa swali ni je!, mimi na wewe tunazo hizo jitihada za kuingia katika Kaanani yetu?.

Kama bado upo nje ya Wokovu, (yaani hujampokea Yesu) basi fahamu kuwa upo katika hatari ya kuikosa mbingu na kama tayari umeshampokea Bwana Yesu lakini unaishi maisha ya uvuguvugu, ya kutokujali, ya kusukumwa sukumwa, au kumbembelezwa bembelezwa…basi fahamu kuwa upo mbali na ufalme wa mbinguni, na siku ya kurudi kwa Bwana itakukuta kama mwivi.. kwasababu maandiko yanasema “tutie jitihada”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Biblia ilimaanisha nini watu wasitoe vizazi vyao kwa Moleki?

Kwanini iwe ni nchi ibubujikayo maziwa na asali?

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

Rudi nyumbani

Print this post

MIMI NI ALFA NA OMEGA.

Mara nyingi Bwana Yesu amekuwa akijitambulisha kwa majina mbalimbali, kwa mfano ukisoma Ufunuo 19:13 inasema jina lake anaitwa Neno la Mungu.. Hii ikiwa na maana popote palipo na Neno la Mungu, basi Kristo yupo hapo, na mtu anayeliishi hilo, basi anamuishi Kristo maishani mwake.

Ukisoma pia Isaya 9:6 inasema

“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani”

Hapo mwishoni inasema, jina lake ataiwa mfalme wa Amani, ikiwa na maana kuwa mahali popote amani ya kweli ile idumuyo ilipo, basi Kristo naye yupo hapo pia,kwasababu yeye ndio mfalme wa hiyo.

Lakini tukirudi katika kitabu cha Ufunuo1:8, Yesu anasema maneno haya;

“Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi”.

Anayarudia tena maneno hayo hayo katika.. Ufunuo 21:6,22:13.

Maana yake ni nini?

Alfa ni herufi ya kwanza katika lugha ya kigiriki, na omega ni herufi ya mwisho ya lugha hiyo.  Kwa lugha yetu ni sawa na tuseme Yesu ni “A” na Yesu ni “Z”, Maana yake ni kuwa yeye ni Neno la Kwanza na pia ni Neno la mwisho.

Lakini hajaishia hapo, anasisitizia kabisa kwa kusema yeye ni ‘Mwanzo na Yeye ni mwisho’. Jiulize kwanini hajasema yeye ni ‘juu na yeye ni chini’, au ‘yeye ni mashariki na yeye ni magharibi’ au ‘yeye ni mbele na yeye ni nyuma’, bali anasema yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho?.. Ni muhimu sana kutafakari hili!!

Akiwa na maana kuwa, popote palipo na mwanzo, yeye anapaswa awepo hapo, na popote palipo na mwisho yeye ndio muhitimishaji. Jambo ambalo watu wengi hawalitambui, Na ndio maana inakuwa ngumu kumwona Yesu katika maisha yetu.

Kwasababu hatumtangulizi yeye, katika mwanzo wa mambo yetu, na vilevile hatuhitimishi na yeye katika mwisho wote wa mambo yetu. Tunachukulia kiwepesi wepesi tu, tunamweka Kristo katikati ya mambo yetu, tukidhani kuwa tutamwona akitembea na sisi. Hana kanuni hiyo!

Watu wote wanaonza na Yesu na kuhitimisha na Yesu, katika mambo yao yote, angalia maisha yao, utaona ni ya ushuhuda tu kila siku.

Hivyo haya ni maeneo muhimu sana ya kuzingatia kuanza naye, ukiyachezea haya, umeshamkosa Yesu.

  1. Siku: Unapoanza siku mpya, kabla hujafanya jambo lolote, kabla hujaangalia msg ulizotumiwa na boss wako, kabla hujawasha data kwenye simu yako. Amka piga magoti, mshukuru Mungu, chukua muda mwambie Mungu asante kwa kunipa neema ya siku mpya. Msifu, mtangulize katika mambo yako yote. Ndipo baadaye mengine yafuate. Halikadhalika unapomaliza siku, mshukuru Mungu, kwa kukushindania siku nzima, tenga muda wa kutosha kufanya hivyo, soma biblia kidogo, omba. Usikimbilie tu kitandani, na kusema nimechoka, wacha nilale, nilishashukuru asubuhi. Kumbuka yeye anasema ni Alfa na Omega, ili akamilike kwako vyote viwili vinapaswa viende sambamba.
  2. Wiki: Unapoanza wiki, anza na Bwana, siku ya kwanza ya wiki ni Jumapili, hivyo hakikisha siku hii hukosi ibadani, vilevile hakikisha jumamosi yako, unakuwepo nyumbani kwa Mungu kumshukuru. Na ndio maana kanisa kunakuwa na mikesha ya ijumaa kuamkia jumamosi, au jumamosi kuamkia jumapili. Hakikisha unakwenda kumshukuru Mungu, kwa wiki nzima. Kwa kufanya hivyo, utamwona Kristo akitembea katika wiki yako nzima kukupigania.
  3. Mwezi: Vivyo hivyo katika mwanzo wa mwezi mpya, na mwisho wa mwezi wako. Huna budi kuwepo ibada kumshukuru Mungu, na ni vema kabisa kumshukuru Mungu ukiwa na matoleo yako.  Wana wa Israeli waliagizwa kila mwezi mpya wawe na kusanyiko, hivyo na wewe usianze mwezi kama mnyama, bali tenga muda wa kumshukuru muumba wako.(Ezra 3:5)
  4. Mwaka: Ufungapo mwaka, na ufunguapo mwaka, ni sharti uwe uweponi mwa Bwana. Umealikwa kwenye sherehe,usiende, unalazimishwa uwepo kazini, omba ruhusa, ni heri ukatwe mshahara wa mwezi huo, kuliko kuliko kumkosa Yesu mwaka mzima. Yeye ni Alfa na Omega.
  5. Kazi: Biblia inasema malimbuko yote ni ya Bwana, ikiwa unaanza kazi mpya, hakikisha mshahara wako wa kwanza unampa Bwana, na pale unapoacha, na kupata nyingine, vivyo hivyo fanya kwa Bwana.(Zaburi 3:9), hata katika bishara yako, au popote panapokuingizia kipato.
  6. Uzao: Wazaliwa wote wa kwanza, ni wa Bwana, pia na wa mwisho. Ukitaka ubarikiwe uzao wa tumbo lako, embu usimzuilie Bwana watoto wako. Ana mama yake Samweli alifanya vile kwa mwanaye, Samweli, matokeo yake mpaka leo tunamsoma habari zake, lakini kama angemzuilia, tungemjulia wapi?.

Hakikisha unapompa Bwana mwanao, sio unampa kwa mdomo tu, unamwacha aje kupenda mwenyewe kanisa akiwa mkubwa, bali unamgharimikia kwa Bwana mahitaji yote yanayompasa, utampa elimu, lakini zaidi elimu ya biblia kwa bidii, unamtafutia madarasa ya biblia spesheli kutoka kwa watumishi wa Mungu, unamtoa wakfu kwa Bwana, maana yake hata akikwambia mimi sitakuja kuajiriwa bali nitakuwa mchungaji, hakuna kipingamizi chochote juu yake, unamsapoti kwa furaha yote.

Ukifanya hivyo, utakuja kuvuna ulichokipanda mbeleni. Kwake huyo mtoto na kwa wazao wako wote waliosalia. Kwasababu umemfanya Yesu Alfa na Omega kwenye uzao wako.

Hivyo popote pale, hakikisha unaanza na Kristo, na unamaliza na Kristo. Na hakika tutamwona katika mambo yetu yote.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

Nini maana ya K.K, na B.K?  (B.C na A.D).

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?

Agano ni makubaliano kati ya pande mbili; Na kuna aina saba (7) za maagano kibiblia.

1)Agano kati ya “MTU NA MTU”, 2) kati ya “MTU NA KITU”, 3) kati ya “MTU NA shetani” 4) kati  ya “MTU  NA MUNGU” 5) kati ya  “MUNGU NA MTU”, 6) kati ya “MUNGU NA VIUMBE Vyake” 7) kati ya “MUNGU, NA MWANAE”.

Kwa taratibu tuvitazame vipengele vyote hivyo vya maagano. Na kisha tutajifunza ni Agano lipi lenye nguvu kuliko yote!

  1. Agano kati ya “MTU NA MTU”.

Mfano wa Agano kati ya Mtu na mtu, ni lile Yakobo aliloingia na Labani..Kwamba Yakobo asiwatese wana wake huko aendako.. na wala asije akaongeza mke wake wengine zaidi ya hao wanawe aliompa..

Mwanzo 31:43 “Labani akajibu, akamwambia Yakobo, Hao binti ni binti zangu, na wana ni wanangu, na wanyama ni wanyama wangu, na yote uyaonayo ni yangu; nami naweza kuwatendea nini leo binti zangu na wana wao waliowalea

44 Haya! Na tufanye agano, mimi na wewe, liwe kwa ushahidi kati ya mimi na wewe.

45 Yakobo akatwaa jiwe akalisimamisha kama nguzo…………

50 Ukiwatesa binti zangu, na ukitwaa wake zaidi ya binti zangu, wala hapana mtu pamoja nasi, tazama, Mungu ni shahidi kati ya mimi na wewe?”

Mfano wa mwingine wa Agano la “Mtu na mtu”..ni lile “agano la Ndoa”.. Watu wawili wanafunga ndoa, wanakuwa wameingia Agano la kuishi pamoja, mpaka kifo kitakapowatenganisha..Agano hilo linakuwa ni la mtu na mtu, mbele ya Mungu wa mbinguni. Na ikitokea mmojawapo kavunja agano hilo, basi laana itakuwa kuu yake.

2. Agano kati ya “MTU NA KITU”.

Mtu pia anaweza kuingia agano na kitu.. Kwamfano utaona Ayubu ambaye alikuwa ni mtu mkamilifu sana, aliweza kuingia agano na Macho yake, kwamba asimtazame mwanamke na kumtamani..

Ayubu 31:1 “Nilifanya agano na macho yangu; Basi nawezaje kumwangalia msichana?”

Hii ikiwa na maana kuwa hata sisi tunaweza kuweka Agano na macho yetu yasitazame ubaya, na midomo yetu isizungumze mabaya na miguu yetu isikimbilie mabaya n.k

3. Agano kati ya “MTU NA SHETANI”

Mtu anaweza kuingia Agano na shetani (miungu), na agano hili ndio baya kuliko maagano yote, kwasababu kamwe shetani hawezi kumpa mtu uzima, bali mauti!. Na maagano haya watu wanaingia aidha kwa kujua au kutokujua.. Mara nyingi Mila na Desturi!, na Kuhudhuria kwa waganga wa kienyeji na maisha ya dhambi ndiyo yanawaingiza watu kwenye maagano na mashetani bila kujua..

Kutoka 23:31 “Nami nitakuwekea mpaka wako tangu Bahari ya Shamu hata bahari ya Wafilisti, tena tangu jangwani hata huo Mto; kwa kuwa nitawatia wenyeji wa nchi mkononi mwako; nawe utawafukuza mbele yako.

 32 Usifanye maagano pamoja nao, wala pamoja na miungu yao

33 Wasikae katika nchi yako, wasije wakakufanya kunitendea mimi dhambi; kwa sababu ukiitumikia miungu yao, jambo hili halikosi litakuwa ni tanzi kwako”

4. Agano kati ya “MTU NA MUNGU”.

Watu pia wanaweza kuingia maagano na Mungu wa mbingu na nchi…Mfano katika biblia utaona kipindi Israeli wamerudi nchini kwao baada ya kukaa utumwani miaka mingi, waliporudi waliweka agano na Mungu kuwa watawaacha wanawake wa kimataifa waliowaona na vile vile wataifuata torati ya Musa.

Ezra 10:3 “Haya basi! NA TUFANYE AGANO NA MUNGU WETU, kuachana na wake zetu, na wale waliozaliwa nao, tukilifuata shauri la bwana wangu, na shauri la hao wanaoitetemekea amri ya Mungu wetu; mambo haya na yatendeke kwa kuifuata torati”

5. Agano kati ya “MUNGU NA MTU”

Agano hili linakuwa thabiti, tofauti na lile ambalo mtu anaingia na Mungu, kwasababu Mungu kamwe havunjagi maagano, lakini sisi wanadamu tunavunja maagano, tunayoyaingia.. Mfano wa Agano ambalo Mungu aliingia na mtu au watu, ni lile aliloliingia na Ibrahimu, kuwa atakuwa Baba wa mataifa mengi..

Mwanzo 17: 1 “Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. 

2 Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana. 

3 Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema,

 4 Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi,

 5 wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi.

 6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako. 

7 Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako.

 8 Nami nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao.

 9 Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada yako”.

Agano hili ambalo Mungu aliingia na Ibrahimu, mpaka leo lina nguvu.. Ndio maana unaona ni kwanini Taifa la Israeli bado ni Taifa teule la Mungu. Na ambarikiye Israeli amebarikiwa, na amlaaniye amelaaniwa (Hesabu 24:9).

6. Agano kati ya “MUNGU NA VIUMBE”

Mungu pia anaweza kuingia agano na viumbe vyake alivyoviumba.. vilivyo na uhai na visivyo na uhai.. kama kama wanyama na mawe na miti na mabonde… Mfano wa Agano kama hili ni lile alilolifanya wakati anaigharikisha dunia, nyakati za NUHU.

Mwanzo 9:9 “Mimi, tazama, nalithibitisha agano langu nanyi; tena na uzao wenu baada yenu;

 10 tena na kila kiumbe hai kilichoko pamoja nanyi, ndege, na mnyama wa kufugwa, na kila mnyama wa mwitu katika nchi pamoja nanyi; wote wanaotoka katika safina, hata kila kilicho hai katika nchi.

11 Na agano langu nitalithibitisha nanyi; wala kila chenye mwili hakitafutwa tena kwa maji ya gharika; wala hakutakuwa tena gharika, baada ya hayo, kuiharibu nchi. 

12 Mungu akasema, Hii ndiyo ishara ya agano nifanyalo kati yangu na ninyi, na kila kiumbe hai kilichoko pamoja nanyi, kwa vizazi vyote hata milele; 

13 Mimi nauweka upinde wangu winguni, nao utakuwa ni ishara ya agano kati yangu na nchi.

14 Hata itakuwa nikitanda mawingu juu ya nchi, upinde utaonekana winguni,

 15 nami nitalikumbuka agano langu, lililoko kati yangu na ninyi, na kila kiumbe hai katika wote wenye mwili, wala maji hayatakuwa gharika tena kuwaharibu wote wenye mwili.

 16 Basi huo upinde utakuwa winguni; nami nitauangalia nipate kulikumbuka agano la milele lililoko kati ya Mungu na kila kiumbe hai katika wote wenye mwili kilichoko katika nchi”.

Agano hili Mungu aliloingia na ardhi na wanyama kwamba hatawagharikisha tena kwa maji, lina nguvu mpaka leo, ndio maana utaona tangu wakati wa Nuhu mpaka leo hakuna gharika tena, na ule upinde tunaouna ni ishara ya agano lake hilo aliloingia nasi pamoja na viumbe vyote..

7. Agano kati ya “MUNGU, NA Mwanawe”.

Hili ndio Agano kuu, na lenye Nguvu kuliko maagano yote!.. Agano hili ndio lile aliloingia na Mwanawe mpendwa Yesu Kristo, kupitia Damu ya mwanawe. Na kwanini Agano hili lina nguvu?.. ni kwasababu Yesu Kristo ni Mungu katika mwili, hivyo Agano hili, ni Mungu kaingia na NAFSI YAKE MWENYEWE. Hivyo haliwezi kuvunjika wala haliwezi kupungua nguvu..

Agano la Mungu aliloingia na viumbe vyake kwamba havitagharikishwa kwa maji, ni kweli mpaka leo lina nguvu, lakini itakuja gharika nyingine ya moto na si ya maji, hivyo Agano la kwanza limetupa uzima lakini si wa milele, kwasababu itakuja gharika nyingine ya moto..

2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.

7  Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.

Lakini Agano la Damu ya Yesu ni Agano jipya, na la Mwisho, hakuna agano lingine litakalokuja katika haya maisha litakalokuwa timilifu zaidi ya hili. Kwamba kila amwaminiye Mwana wa Mungu (YESU KRISTO), anao uzima wa Milele, na anakuwa mrithi wa Baraka na ahadi za Mungu.

Kwahiyo ni muhimu sana kumpokea Yesu kila mmoja, ili tuweze kushiriki Baraka hizi za Agano jipya la Mungu.

Na damu ya Agano jipya, (yaani Damu ya Yesu), ina nguvu kuu ya kuvunja maagano yote, mtu aliyoingia na miungu, au shetani.. na kumwacha mtu kuwa huru kabisa kabisa.

Je umeingia ndani ya Agano la Damu ya Yesu?..

Kama bado, Mlango wa Neema bado upo wazi, lakini hautakuwa wazi hivyo siku zote, siku moja utafungwa na hakuna atakayeweza kuinga.. Kama unataka uzima, na kheri, basi mpokee Yesu, lakini kama hupendi uzima wala kheri basi baki kama ulivyo…

Waebrania 12:24  “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.

25  Angalieni msimkatae yeye anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa yeye aliyewaonya juu ya nchi, zaidi sana hatutaokoka sisi tukijiepusha na yeye atuonyaye kutoka mbinguni”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Watu wenye kuvunja maagano ndio watu wa namna gani? (Warumi 1:31)

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

MJUMBE WA AGANO.

KUVUNJA MAAGANO YA UKOO.

SHUSHANI NGOMENI NI WAPI KWA SASA?

Rudi nyumbani

Print this post

ITII SAUTI ILIYOPO NYUMA YA KILA ISHARA YA MUNGU!

Shalom, karibu tujifunze maandiko.

Kila ishara inayo sauti nyuma yake..Kwa mfano “tunapoona ishara ya mawingu kuwa meusi”..ujumbe au sauti uliopo nyuma ya hiyo ishara ni kwamba “muda si mrefu mvua inashuka”..Sasa sio kwamba mawingu yametoa sauti na kusema “mvua inakuja”..la! mawingu hayawezi kuongea.. lakini yametoa tu ishara, ambayo ndani ya hiyo ishara ipo sauti.

Hali kadhalika pia na kwa upande wa Mungu wetu,  Sauti yake pia wakati mwingine ipo katika Ishara.. Mungu anaweza kuzungumza moja kwa moja tukaisikia sauti yake, lakini pia sauti yake anaweza kuiweka ndani ya ishara fulani, kwamba tutakapoona ishara hiyo, basi ni wajibu wetu kutambua sauti gani ipo nyuma ya hiyo ishara.

Na siku zote sauti ya Mungu ipo  kwa lengo la kutufundisha, kutufariji na kutuonya!. Wengi Mungu kashazungumza nasi kwa njia ya Ishara..lakini hatujamsikia Mungu… Wengi tumeshaonywa sana kwa njia ya Ishara lakini hatujasikia..na huku tukidhani Mungu hajawahi kuzungumza nasi…

Neno la Mungu linasema..

Isaya 50:2 “Basi, nilipokuja, mbona hapakuwa na mtu? Nilipoita, mbona hapakuwa na mtu aliyenijibu?…”

Umeona?..Kumbe Mungu huwa anatujia lakini hatujui kama ametujia, na huwa anatuita lakini hatusikii!..Ni kwanini?..ni kwasababu hatuijui Sauti ya Mungu.. Tukidhani kuwa ana njia moja tu ya kusema na sisi.

Hebu tumwangalie mtu mmoja katika biblia ambaye Mungu alizungumza naye kwa njia ya Ishara lakini aliipuuzia sauti ya Mungu, iliyokuwepo nyuma ya hiyo ishara.. Na mtu huyo si mwingine zaidi ya Mtume Petro.

Kuna wakati Bwana Yesu alimwambia Petro kuwa “kabla jogoo hajawika mara mbili atamkana mara tatu”..

Hebu tusome,

Marko 14:29 “Petro akamwambia, Hata wajapokunguwazwa wote, lakini siyo mimi

30  Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, Leo, usiku huu, kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu”.

Hapo Bwana Yesu alimpa Petro “ishara ya jogoo” na akampa na “Sauti” moja kwa moja nyuma ya hiyo ishara, kwamba atamkana!. ..Angeweza kumwambia tu “leo utanikana” asimpe na ishara yoyote…lakini hapa utaona  hapa Bwana Yesu anampa Petro “Ishara” na “sauti ya hiyo ishara”.

Na kweli wakati ulipofika,  Petro akaanza kumkana Bwana Yesu, na pengine wakati anaanza tu kumkana kwa mara ya kwanza..papo hapo “Jogoo akawika”.. na Petro akamsikia Yule jogoo akiwika lakini hakutilia maanani…hakukumbuka kwamba Bwana alimwambia kabla ya jogoo kuwika atamkana!…

Hivyo kwa kuwika tu jogoo mara ya kwanza, ilitosha kumkumbusha Petro dhambi yake na kumfanya “atubu”..

Lakini Petro hakuizingatia hiyo sauti ya Mungu, iliyomwamsha roho yake atubu… badala yake akaendelea na dhambi yake!.. akaendelea kumkana Bwana tena kwa mara nyingine ya pili na ya tatu!.. Lakini kwasababu Bwana ni wa rehema, akairudia tena ishara ile ile, ya jogoo kuwika mara nyingine ya pili..

Na jogoo alipowika  mara ya pili, ndipo akili zikamrudia Petro, na kutafakari..na kugundua dhambi yake ambayo tayari ameshairudia mara tatu..Na ndipo akaenda kutubu!..lakini kama asingeisikia sauti ile nyuma ya ile ishara, huenda angeendelea kumkana Bwana zaidi na zaidi na madhara yake yangekuwa makubwa mbeleni.

Umeona hapo!.. tafsiri rahisi ya kisa hicho ni kwamba.. kipindi Petro anaanza kumkana Bwana,  Mungu alimtumia jogoo kumwambia Petro, “Acha Hicho unachokifanya”…usimkane Bwana!.. lakini hakusikia, “Yeye alidhani ni mlio wa jogoo tu”…Bwana akarudia tena kwa mara nyingine..Acha!..Sauti iliyotoka ni ya jogoo, lakini katika ulimwengu wa roho ni Mungu anasema acha!, ndipo Petro akapata akili.

Sasa kama Mungu alimtumia jogoo kumwonya Petro, unadhani ni mara ngani katumia watu au wanyama na viumbe kuzungumza nasi?..kutuonya tubadili njia zetu?, tutubu dhambi zetu? Tufanye hiki au kile?..

Je unadhani tukikataa leo kutubu na kulitii Neno lake siku ile tutakuwa na udhuru wowote!..je unadhani siku ile tutakuwa na cha kujitetea kwamba Bwana hajawahi kusema nasi?..Siku ya hukumu utaona ile miti uliyokuwa unadhani ni miti tu, kumbe ilikuwa ni sauti ya Mungu kwako, siku ile utaona ule ugonjwa uliokuwa unakurudia mara mbili mbili ulikuwa ni sauti ya Mungu kwako…

Siku ile utaona wale wanyama waliokuwa wanashambulia mazao yako ni sauti ya Mungu kwako,..siku ile utaona kumbe hata wale wezi waliokuibia na wale matapeli waliokudhulumu, ni Mungu alikuwa anazungumza na wewe,…. na utajuta na kusema laiti ningeisikia ile sauti na kutii!!, na wakati huo utakuwa umeshachelewa.

Na tabia ya Mungu ni kuwa “sauti yake imejificha katika vitu vinyonge tunavyovidharau sisi”… Sauti yake aliificha nyuma ya mlio wa jogoo, kwa Petro, vile vile utasoma pia kuna wakati punda aliweza kusema maneno ya Mungu mbele ya Balaamu.. Vivyo hivyo kamwe tusitegemee kuisikia sauti ya Mungu katika mambo makubwa, yeye anatumia hata vitu vinyonge kusema na sisi..

Bwana Yesu atusaidie tuitii sauti ya Mungu, iliyopo nyuma ya kila ishara yake.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TEGEMEA MUNGU KUZUNGUMZA NAWE KATIKA MAMBO MADOGO

SAUTI NYUMA YA ISHARA.

ISHARA ITAKAYONENEWA

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Rudi nyumbani

Print this post

“Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika”,Maana yake nini?

Nini maana ya “Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika”. Kwanini Bwana Yesu apigwe? Na kwanini kondoo wake watawanyike!… Na je! Anayempiga ni nani?.

Tusome,

Mathayo 26:31 “Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika”

Bwana Yesu alipigwa na Mungu, lakini si kwasababu ya makosa yake, (yeye hakufanya dhambi hata moja, hakufanya kosa hata moja)…Lakini lakini ni kwasababu gani alipigwa??.. ni kwaajili yetu sisi..

Kumbuka Bwana Yesu hakuja kuiondoa adhabu, ambayo tayari ilikuwa imeshatolewa juu yetu..bali alikuja kuichukua adhabu.. Kwasababu kama ingekuwa kaja kuiondoa adhabu, basi hata yeye asingepanda msalabani(asingeadhibiwa)...Adhabu juu yetu tayari ilikuwa imeshatolewa, na ilikuwa ni lazima itekelezeke(Imfikie mlengwa).. Ni sawa na mtu akutupie jiwe kutoka mbali, na jiwe lile likiwa hewani, ghafla anatokea mtu anakaa mbele yako ili lile jiwe lisikupate wewe bali limpate yeye!..

Sasa kiuhalisia mtu huyo kakuokoa wewe na madhara ya jiwe lile, lakini hajaondoa madhara ya lile jiwe..au hajazuia jiwe lile lisirushwe kutoka kwa aliyerusha!!..Ni lazima limpate tu!..yeye kachukua tu maumivu yako, maana yake atachubuka yeye badala yako wewe, ataumia yeye badala yako wewe, atapigwa yeye badala yako wewe.. Mlengwa ulikuwa ni wewe, lakini yeye kajitokeza katikati ya safari ili yeye aumie wewe upone.

Ndicho Bwana YESU alichokuja kukifanya.. si kuondoa Adhabu iliyokwisha kutamkwa juu yetu na Mungu, si kuondoa laana iliyokwisha kutamkwa juu yetu, si kuondoa dhiki na mateso na masikitiko yaliyokwisha kukusudiwa juu yetu tangu siku ile pale Edeni, bali ni kuyachukua yeye hayo masikitiko, kuyachukua yeye hayo maumivu, kuyabeba yeye hayo mapigo..

Ndio maana maandiko yanasema…

Isaya 53: 4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; LAKINI TULIMDHANIA YA KUWA AMEPIGWA, AMEPIGWA NA MUNGU, NA KUTESWA.

 5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, NA KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA”.

Umeona hapo?.. Tulipomwona kaangikwa msalabani, tulidhania kuwa Mungu kamwadhibu kwa makosa yake..Kumbe sio!.. Mungu shabaha yake ilikuwa ni kwetu sisi wala si kwake..lakini yeye akajitokeza kuyapokea yale mapigo!..Hivyo ni sawa na kusema KAPIGWA NA MUNGU KWA MAPIGO AMBAYO SI YAKE!!

Kwahiyo alipopigwa namna hiyo na MUNGU kwa mapigo ambayo si yake.. Kwa kitambo kidogo,  dunia ilikaa kimya!.. Wanafunzi wake (na wafuasi wake), walitawanyika kwasababu Mchungaji hayupo, walibaki bila mchungaji kwa kipindi cha siku tatu!..walikaa kwa huzuni na maombolezo wakati dunia inafurahia…Lakini baada ya kitambo kifupi, Bwana Yesu alipofufuka, ndipo wakakusanywa tena..

Yohana 16:19  “Yesu alifahamu ya kwamba wanataka kumwuliza, akawaambia, Ndilo hilo mnaloulizana, ya kuwa nalisema, BADO KITAMBO KIDOGO NANYI HAMNIONI, NA TENA BADO KITAMBO KIDOGO NANYI MTANIONA?

20  Amin, amin, nawaambia, Ninyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utafurahi; ninyi mtahuzunishwa, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha”.

Hiyo ndio sababu ya Bwana Yesu kusema haya maneno…

Mathayo 26:31 “Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, NITAMPIGA MCHUNGAJI, NA KONDOO WA KUNDI WATATAWANYIKA”

Mungu alimpiga Bwana Yesu kwa kosa lisilo lake pale Kalvari, na kondoo wakatawanyika kwa kitambo..

Hivyo mimi na wewe baada ya kujua haya, na Mhanga, Bwana wetu Yesu Kristo aliouingia kwaajili yetu, basi tutazidi kuuheshimu  wokovu wetu kuliko kawaida..

Tunapotafakari kuwa tulipaswa tufe katika huzuni, katika tabu na baada ya hapo tutupwe katika ziwa la moto milele, lakini Bwana Yesu kaja kutuzuilia hilo, kwa kuchukua yeye laana zetu..basi tunajikuta tunakuwa wanyenyekevu mbele zake, na kuzidi kumheshimu Mungu katika maisha yetu, na kudumu katika Imani na utakatifu, na usafi.

Bwana Yesu atusaidie tuzidi kuuthamini msalaba!.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! UNAMPENDA BWANA?

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUISHINDA DHAMBI INAYONITESA.

SWALI: Shalom. Naomba kufahamu nifanye nini ili niweze kuishinda ile dhambi inayonitesa.?


JIBU: Dhambi inayomtesa mtu kwa jina lingine inaitwa “dhambi izingayo kwa upesi”, ambayo tunaisoma katika;

Waebrania 12:1

[1]Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

Si kila dhambi, huwa inaondoka kirahisi ndani ya mtu pindi anapookoka..

Ni kweli asilimia kubwa ya dhambi mtu anajaliwa na Roho Mtakatifu kuziacha wakati ule anapotubu, na na kudhamiria kumfuata Yesu kwa moyo wake wote, kwamfano mwingine alikuwa ni mwizi, mwongo, mshirikina, mzinzi n.k.

Lakini alipookoka hivi vyote akaviacha kiwepesi kabisa..Lakini ndani yake kukawa na shinikizo kubwa la kuendelea kufanya punyeto, au mawazo machafu kumtawala..hivyo hiyo hali ikawa inamtesa  kwa kipindi kirefu na kumfanya akose raha, wakati mwingine amejaribu kuomba sana lakini hali ipo vilevile.

Mwingine hayo yote ameweza  kuyashinda lakini dhambi ya usengenyaji imekuwa ni mzigo mzito sana kwake kuutua, mwingine ulevi, mwingine kutazama picha za ngono n.k.

Ndugu ikiwa umeokoka na unaona hiyo dhambi ni kikwazo kikubwa  kwako, nataka nikuambie huna budi kushindana nayo hadi uishinde..kwasababu usipoishinda itakupeleka jehanamu.

Kaini alikuwa na dhambi ya hasira na wivu, akaipuuzia, lakini  Mungu akamwambia, unapaswa uishinde

Mwanzo 4:6-7

[6]BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?

[7]Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

Dhambi kama hizi huwa zilishatia mizizi mrefu ndani ya mtu tofauti na nyingine, hivyo kuziondoa inahitaji nguvu ya zaida..

Na njia pekee ya kuzishinda hizi ni moja tu nayo ni “kwa Kuua vichocheo vyote vinavyokupelea kuitenda dhambi hiyo”..

Mithali 26:20 Inasema;

“Moto hufa kwa kukosa kuni;..”

Moto hauwezi kuendelea muda mrefu mahali ambapo hapana kichocheo chake kama kuni au mafuta..haijalishi utakuwa na nguvu kiasi gani, mwishowe utazima tu.

Hakuna dhambi yoyote iliyo ngumu kuishinda hapa duniani endapo vichocheo vyake vitauliwa kikamilifu.

Kwa mfano kufahamu ni jinsi gani utaweza kuishinda dhambi ya uzinzi fungua hapa..>>> MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

Kwa siku za mwanzo, utaona ni shida lakini kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda Mungu anakutia nguvu na hatimaye inakuwa ni dhambi nyepesi sana kuishinda kuliko hata zote…

Ni kawaida hata hata gari lililo katika mwendo kasi likichuna breki kwa ghafla, haliwezi kusimama hapo hapo…litasogea mbele kidogo, ndipo litulie japokuwa tairi tayari zilishaacha kuzunguka, kitambo kidogo.

Vivyo hivyo na wewe katika hiyo dhambi inayokuzinga kwa upesi, inayokufanya usipige mbio kwa wepesi, katika safari yako ya ukristo, kwa siku za mwanzoni itaonyesha  kama kuleta ukinzani lakini kwa jinsi unavyokaa mbali na vichocheo vyake hatimaye itakufa tu ndani ndani yako…ni kitendo cha muda.

Kwamfano kama wewe ni mvuta sigara, kiu ya kuvuta ikija, ondoka mazingira ya upatikanaji wake, vilevile wale marafiki uliokuwa unavuta nao jitenge nao waone kama kaburi, hicho kiu kitakutesa tu kwa muda mfupi, lakini uking’ang’ana utakuja kushangaa kimetoweka tu ghafla..hapo ndio tayari kimekufa..

Shindana, hadi ushinde…usikubali kusema mimi nimeshindwa kuacha hiki au kile, usikubali hiyo hali, usiwe mnyonge wa dhambi, kwasababu wanyonge wote hawataurithi uzima wa milele biblia inasema hivyo katika Ufunuo 21:27

Ikiwa ni fashion, wewe kama mwanamke ni lazima uishinde, ikiwa ni kamari, ikiwa ni miziki ya kidunia kanuni ni hiyo hiyo…Ua vichocheo vyote. Kaa mbali nayo, ulizoea kutazama picha za ngono mitandaoni, na ulipookoka mawazo yale yanajirudia rudia kwenye fahamu zako, endelea kukaa mbali na vichocheo hivyo, acha mazungumzo mabaya, left magroup masiyokuwa na msingi kwako, epuke kutazama au kusikiliza kitu chochote chenye maudhui ya uzinzi, marafiki wazinzi waepuke, marafiki wasiokuwa na maana wa jinsi tofauti wapeuke, utafika wakati hayo mawazo machafu yatakukimbia..

Zingatia hayo, na matokeo utayaona.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

CHUKIZO LA UHARIBIFU.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi nyumbani

Print this post