Title August 2022

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia.

Je!, wewe ni Mwanamke?..kama ndio! basi fahamu kuwa upo katika hatari kubwa ya kuingiwa na roho za mapepo kuliko mwanaume!.

Hebu tutafakari mstari ufuatao, na kisha tujiulize maswali machache!.

1Timotheo 2.11 “Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.

12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.

13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye.

14 WALA ADAMU HAKUDANGANYWA, ILA MWANAMKE ALIDANGANYWA KABISA AKAINGIA KATIKA HALI YA KUKOSA”.

Hapo katika mstari wa 14, anasema “ADAMU HAKUDANGANYWA, ILA HAWA ALIDANGANYWA KABISA AKAINGIA KATIKA HALI YA KUKOSA”.

Maana yake pale Edeni, “Adamu hakudanganywa kabisa”…Adamu alikuwa anajua anachokifanya, alikubali kula lile tunda alilolipokea kutoka kwa mke wake, akiwa na akili timamu na..akijua kabisa lile ni kosa!..lakini Hawa alikuwa hajui chochote, yeye aliamini kile alichoambiwa na Nyoka ni ukweli mtupu!.hivyo alidanganywa na shetani..

Hiyo ikifunua kuwa kuna “KUNA UDHAIFU MKUBWA SANA KATIKA JINSIA YA KIKE”.

Utakumbuka tena, kipindi mfalme Sauli, alipoachwa na Mungu, kitu cha kwanza alichofikiria kukifanya ni kumtafuta mwanamke mwenye pepo la utambuzi katika nchi yake ile?

1Samweli 28:6 “Lakini Sauli alipouliza kwa Bwana, Bwana hakumjibu, wala kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa manabii.

7 Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, NITAFUTIENI MWANAMKE MWENYE PEPO WA UTAMBUZI, NIPATE KUMWENDEA NA KUULIZA KWAKE. Watumishi wake wakamwambia, Tazama, yuko mwanamke mwenye pepo wa utambuzi huko Endori.

8 Basi Sauli akajigeuza, na kuvaa mavazi mengine, kisha akaenda, yeye na watu wawili pamoja naye, wakamfikilia yule mwanamke usiku; akasema, Tafadhali unibashirie kwa utambuzi, ukanipandishie yeye nitakayemtaja kwako”.

Jiulize hapo ni kwanini aseme “NITAFUTIENI MWANAMKE MWENYE PEPO, NA SI MWANAUME mwenye pepo la utambuzi”?.. Si kwamba wanaume wachawi hawakuwepo, walikuwepo!… Lakini Sauli alijua kuna utofauti wa Mwanaume mwenye pepo, na Mwanamke mwenye pepo!… Alijua mwanamke mwenye pepo, anakuwa na pepo kweli kweli!..tofauti na mwanaume!.

Utaona tena kipindi akina Paulo wapo kule Filipi, walikutana na Mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, ambaye alikuwa anawatabiria watu na kuwapatia faida mabwana zake..

Matendo 16:16 “Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, KIJAKAZI MMOJA ALIYEKUWA NA PEPO WA UAGUZI AKATUKUTA, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua.

17 Akamfuata Paulo na sisi akipiga kelele, akisema, Watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye juu, wenye kuwahubiria njia ya wokovu.

18 Akafanya hayo siku nyingi. Lakini Paulo akasikitika, akageuka akamwambia yule pepo, Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu. Akamtoka saa ile ile.

19 Basi bwana zake walipoona ya kuwa tumaini la faida yao limewapotea, wakawakamata Paulo na Sila, wakawakokota mpaka sokoni mbele ya wakuu wa mji”.

Umeona?.. Ukizidi kujifunza biblia utakutana na maandiko yanayosema “Usimwache mwanamke mchawi kuishi (Kutoka 22:18)”… Jiulize ni kwanini inataja mwanamke na si mwanaume?…Sio kwamba haijawaona wanaume ambao ni wachawi!.. walikuwepo wanaume wachawi wengi, lakini kundi la wanawake ndilo lililokuwa limezama zaidi na ndilo lilikuwa hatari..

Sio ajabu kwanini unaona  hata leo hii,..Wanawake ndio wanaoongoza  kulipuka mapepo!. Hiyo ni kutokana na kwamba, ni rahisi kufungua milango ya roho zao zaidi ya wanaume!.

Maana yake ni kwamba…Kila kitu chochote kinachokuja mbele wanawake wengi ni rahisi kukiamini, pasipo kukifanyia uchunguzi wa kutosha, kila wazo linalokuja ni rahisi kulipokea bila kulifanyia uchunguzi wa kutosha, kila fundisho linalokuja ni rahisi kuliamini pasipo kulifanyia uchunguzi wa kutosha…mwisho wa siku wanajikuta wanaingiwa na roho nyingi zidanganyazo, na wanatumika na roho nyingi, pasipo wao wenyewe kujijua..

Mwanamke, si kila wazo linalotoka kwa Mume wako ni la kulipokea pasipo kulitafakari kwa kina, si kila fundisho ni la kuliamini pasipo kulichunguza mara mbili mbili.. Fahamu kuwa wewe ni lango kubwa na la kwanza dhaifu, ambalo shetani analitazama zaidi ya wanaume. Wanawake wengi wa siku hizi za mwisho ni wavivu wa kuyatafakari maandiko kwa kina.. ingawa sio wote!, lakini asilimia kubwa wapo hivyo, na pasipo kujijua kuwa wao ndio ndio windo kubwa na la kwanza la mapepo na roho zote za mashetani zaidi ya wanaume!..

Asilimia kubwa ya wanapenda kufuata mambo au kuamini mambo kwa kusikia tu!.. Kwa mfano kukizuka jambo Fulani ambalo linawafuasi wengi, wanawake wengi ni rahisi kuamini jambo hilo na kulifuata, pasipo kulichunguza kwa kina, au kulifuatilia..na huko huko ndiko wanakojikuta wameshafungua milango ya maroho ya mapepo ndani yao, bila wao wenyewe kujijua.

Baada ya kujijua kuwa wewe ni windo la roho za mapepo zaidi ya jinsia nyingine basi huna budi kuchukua tahadhari kubwa sana juu ya maisha yako, kwa kufanya jambo lifuatalo!.

JARIBU MAMBO YOTE.

Maandiko yanasema  katika kitabu cha 1Wathesalonike 5:21 “ jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema”.. Hapo anasema “jaribuni” pasipo kuonyesha jinsia,.. ikiwa na maana kuwa ni jukumu la jinsia zote “kujaribu mambo”.. Na sio kujaribu jambo moja tu bali “ kujaribu yote”.. Hata ushauri unaopewa na mtu wa kazini kwako, huna budi kuujaribu, hata habari unayoletewa na rafiki yako, huna budi kuijaribu!!..Hata habari unayoisikia katika redio au Tv, ijaribu..

1Yohana 4:1 “Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani”.

Kwanini tunajaribu kila kitu tunachokisikia?? Kwasababu “MANENO” ni “roho”..kila maneno tunayoyasikia yana roho ndani yake.. Hata Neno la Mungu ni Roho wa Mungu..tunaposikia maneno ya Mungu, maana yake tunampa nafasi Roho wa Mungu kusema ndani yetu. Sasa Utasema hilo tunalithibitisha vipi?..

Yohana 6:63 “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; MANENO HAYO NILIYOWAAMBIA NI ROHO, tena ni uzima”.

Umeona?.. Bwana Yesu anasema, maeneno ninayowaambia ni ROHO..  kadhalika tunaposikiliza mambo mengine nayo pia ni roho. Ndio maana hatuna budi kujaribu kila kitu tunachokisikia.. kama Bwana alivyosema katika..Luka 8:18 “Jiangalieni basi jinsi msikiavyo….”

Na tunayajaribu mambo kupitia nini?… Si kingine zaidi ya NENO LA MUNGU.

Biblia ndio Hadubini ya maisha yetu.. ndio kipimo cha mambo yote..Maana yake kama hupendi kujifunza biblia, kamwe hutaweza kuzipima roho, kama hujizoezi kujifunza biblia mwenyewe bila kusubiria kufundisha fundisha kila mara, kamwe hutaweza kuzijaribu roho kama zinatokana na Mungu au la!..Kama wewe ni wa kusubiria tu makala Fulani iachiwe usome, au mahubiri Fulani uyasikilize, ni wa kupenda kuletewa letewa tu!…wewe mwenyewe biblia unaiona ngumu fahamu kuwa wewe ni windo bora la mapepo!.

Mwanafunzi anayeona masomo ni magumu, siku zote ni Yule ambaye hapendi kusoma, bali yule anayependa kusoma anapoona mada ni ngumu, basi anafanya bidii kupambana mpaka aielewe…na kamwe hawezi kuona masomo ni magumu… vile vile na wewe kama unaona biblia ni NGUMU miaka nenda rudi!.. Basi huo ni uthibitisho kuwa wewe si mwanafunzi wa biblia, hujawa serious!!.. ndio maana inakuwa ni ngumu kwako!.. miaka na miaka.

Hivyo kama wewe ni mwanamke, kumbuka haya, na fahamu kuwa mapepo yanakutafuta wewe zaidi zaidi ya jinsia nyingine, hivyo huna budi kuongeza umakini katika kujilinda na hizo roho.. lakini kama hutaongeza umakini kwa kuamua kujifunza BIBLIA kwa kina!!, na kupima mambo yote!!! Basi jua kuwa roho za mapepo zitakusumbua daima..na mapepo mengine yatakuingia pasipo wewe kujua, lakini utakuja kuona madhara yake baadaye sana.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

MFANYE BWANA YESU MWENYEJI MAISHANI MWAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

USIOGOPE KUMWADHIBU MWANAO.

Tunaishi katika ulimwengu ambao, maadili yameporomoka sana, na bado yanaendelea kuporomoka kwa vijana na watoto..Na hiyo inatufanya tuelekeze lawama kwa watoto; tukisema watoto wa siku hizi wamebadilika sana, lakini ukweli ni kwamba wazazi ndio wamebadilika, watoto ni walewale.

Malezo ya mzazi kwa mtoto ni muhimu sana, mtoto si kama nyau, ambaye kitu pekee anachohitaji ni chakula tu na sehemu ya kulala, hata ukimwacha mwaka mzima bila kumjali kwa vingine, hakuna hasara yoyote, bado ataendelea kuwa paka..

Lakini kwa mwanadamu sivyo..yeye hafugwi, bali analelewa..na malezi ni zaidi ya chakula na nguo na mahali pa kulala.. Hapo ndipo wazazi wengi wanashindwa kuelewa.

Kwasababu mtoto atahitaji kuwa na maarifa, nidhamu, uadilifu, hekima, busara, upendo, utiifu, upambanuzi n.k. Ili aweze kuishi vema katika huu ulimwengu.

Hivi vyote hazaliwi navyo, bali anajifunza anapokuwa duniani..hivyo akikosa msaada sahihi, basi ibilisi atatumia fursa hiyo kumfundisha elimu yake na nidhamu yake hapa ulimwenguni.

Hivyo wewe kama mzazi au mlezi una jukumu kubwa sana zaidi ya lile la kumlisha na kumvisha na kumsomesha..hizo ni hatua 3 katika ya 1000, anazopaswa azijue.

Ikiwa hukupata masomo yaliyotangulia ya malezi ya watoto, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba hii, ili tuweze kukutumia chambuzi za nyuma. Au tembelea website yetu hii www.wingulamashahidi.org. au tutumie ujumbe kwa namba hizi +255693036618

Leo tutaona njia nyingine ya kumlea mtoto vema.

Na njia yenyewe si nyingine zaidi ya kutumia KIBOKO.

Lugha hii inaweza isiwe nzuri masikioni mwa wazazi lakini ni tiba nzuri kwa malezo yao. Hata ‘panadol’ haina ladha nzuri mdomoni, lakini pale inapotutibu tunaishukuru, ndio maana tunayo siku zote majumbani kwetu.

Lakini ni kwanini utumie kiboko kwa mtoto?

Sababu zipo mbili.

1) Ni kwasababu ujinga umefungwa moyoni mwake

2) Mungu naye huwa anatuadhibu sisi.

  1. Tukianzana na sababu ya kwanza biblia inatuambia..

Mithali 22:15

[15]Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.

Ni vizuri ukafahamu kuwa mtoto kama mtoto huwa ana ujinga mwingi ndani yake..yule si kama wewe, unapoona anang’ang’ania kitu fulani kisichopendeza halafu wewe kama mzazi unaamua tu kumwachia kisa anakililia, usidhani kuwa anaelewa matokeo ya kile anachokitaka..

Kumbuka yule hatafakari, wewe unatafakari, hivyo basi ukimsikia anatukana, usisubiri apumzike bali hapo hapo shika kiboko chapa. Ukiona unamwagiza kitu hatii, chapa..ukiona hawaheshimu watu wazima hata baada ya kuonywa mara nyingi..chapa..usiogope labda atakufa…biblia inasema kiboko cha adili hakiui..

Mithali 23:13

[13]Usimnyime mtoto wako mapigo; [14] Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

Hiyo itamsaidia sana kuundoa ujinga mwingi wa kipepo ambao mwingine kwa maneno tu, peke yake au kwa kufundishwa hauwezi kutoka..

  • 2) Mungu naye anatuadhibu.

Na sababu ya pili kwanini tuwaadhibu watoto wetu kwa kiboko pale wanapokosea..ni kwasababu Mungu naye anatuadhibu sisi watoto wake.

Biblia inasema hivyo..

Waebrania 12:6-7

[6]Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.

[7]Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?

Umeona..Sisi hatuna hekima ya kumzidi Mungu, tengeneza picha Bwana angekuwa anatuona tunatukana wengine halafu hachukui hatua yoyote anacheka tu..si tungaangamia..Mungu alipomuona Daudi anamchukua mke wa Huria halafu anaendelea kusema wewe ni mtumishi wangu unayeupendeza moyo wangu..Daudi leo angekuwa wapi kama sio kuzimu? Lakini Mungu alimuadhibu vikali…na baadaye akatubu akapona..

Nasi pia biblia inatuambia tutakuwa wakamilifu kama Baba yetu wa mbinguni alivyomkamilifu..(Mathayo 5:48)

Mzazi unayemtazama mwanao, anafanya ujinga, unaogopa kumchapa atalia..bado hujawa mkamilifu kama Mungu.

Hivyo anza sasa kutimiza huduma hii, ili kesho mtoto huyo afanyike baraka na neema kwa ulimwengu.

Lakini zingatia: Haimaanishi kuwa umpige pige mtoto ovyo kila saa anapokosea..hapana zipo sehemu zinastahili kiboko, zipo zinazostahili maonyo, zipo zinazostahili kuelimishwa..Zote zina umuhimu wake mkubwa bila kupuuzia hata moja.

Bwana akubariki

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

MALEZI YA MTOTO MCHANGA.

Rudi nyumbani

Print this post

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Wokovu na furaha ya wokovu ni vitu vinavyokwenda sambamba, palipo na wokovu ni lazima na furaha ya wokovu pia iwepo, vikipishana kidogo, basi ni tatizo kubwa sana ni sawa na chakula kilichokosa chumvi, utakula tu, ili kujaza tumbo lakini hutakifurahia hata kidogo,


Wakristo wengi sasa wameupokea wokovu, lakini , si wote wanayo furaha ya wokovu. Kuwepo katika wokovu ni suala ambalo unapaswa ufurahie, (U-enjoy), kama vile ufurahiavyo maisha ya utajiri. Lakini kama hilo jambo halipo ndani yako sasa, basi kuna tatizo kubwa.


Kuna kipindi ulikuwa unajihisi furaha, na amani na wepesi ndani ya wokovu, haukujali ni magumu kiasi gani unapitia, lakini sasa unajiona kama hiyo raha haipo tena, wokovu unakuwa kama vile wa kujilazimisha, upo tu, unasogeza siku ilimradi, kesho ije.
Leo tutatazama, ni vitu gani vya kuzingatia kama mkristo, ili uweze kuirejesha ile furaha ya wokovu uliyoipoteza. Na kama hujawahi pia kuwa nayo basi zingatia kanuni hizi muhimu.


1) Jiepushe na dhambi: Hususani ya uzinzi


Daudi hakuwahi kupoteza furaha ya wokovu maisha yake yote, isipokuwa siku alipofanya dhambi ya makusudi, ya kuzini na mke wa askari wake(Huria), mwanzoni alidhani ni jambo jepesi tu, lakini aliponaswa katika huo mtego, alikaa muda mrefu sana, bila furaha ya wokovu, japokuwa alishasamehewa hiyo dhambi na Mungu..

Yeye ndio aliyeandika Zaburi ya 51, na katika dua zake alimwomba Mungu amrejezee furaha ya wokovu aliyoipoteza zamani.

Zaburi 51:12 “Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya wepesi”.

Nawe pia ikiwa umeokoka, halafu unaendelea kutenda dhambi, furaha hii itaondoka ndani yako, na ukristo wako utakuwa ni mzito na mgumu sana, pengine hata baada ya kutubu. Hivyo kaa mbali na dhambi.


2) Soma Neno:

Mahali pekee ambapo pana matumaini, faraja, nguvu ya kuendelea mbele, basi ni katika Neno la Mungu. Kama mkristo ukiwa mvivu wa kuchukua biblia yako na kusoma kila siku, huwezi kusonga mbele katika hii safari ya imani.

Kwamfano katika biblia utamsoma Ayubu, katika majaribu yake, utamsoma Ibrahimu na Sara katika kusubiri kwao, utamsoma Henoko na Eliya katika ukamilifu wao, utajifunza uvumilivu, saburi, upendo, amani, utasoma shuhuda mbalimbali za waliotendewa maajabu na Yesu n.k. Hivyo kwa maarifa hayo, ni ulinzi tosha kwako, wa kuufurahia wokovu wako.

Lakini ukiwa ni mkavu ndani, hapo ndipo ibilisi atakujaza biblia yake, ya hofu ya maisha, mashaka, wasiwasi, huzuni, wivu, chuki n.k.
Penda Neno la Mungu kama upendavyo chakula.

Mithali 3:1 “Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu.
2 Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani.
3 Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
4 Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu”.


3) Kuwa mwombaji:

Katika eneo ambalo hupaswi kuwa mvivu nalo basi ni hili, hapa shindana na mwili, ukikosa kuwa mwombaji, Kama Yesu alivyosema, Kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni (Mathayo 26:41).. Ni kweli kabisa majaribu yasiyokuwa na msingi yatakukuta, na hivyo utakuwa unaishi kila siku maisha ya kujikwaa kwaa..


4) Zingatia Ibada;

Ibada ni muhimu sana kwa mkristo, ikiwa umeokoka halafu huna desturi ya kuhudhuria ibadani, kujumuika na watakatifu wengine, utaikosa furaha ya wokovu wako..
Bwana alisema..

Waebrania 10:25 “wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia”.

Pia maandiko yanasema..

Mithali 27:17 “Chuma hunoa chuma; Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake”.

Vipo vitu ambavyo utavipata kwa juhudi zako mwenyewe, lakini vipo ambavyo utaongezewa na wengine, kuna mahali utaishiwa nguvu, mwingine atakushika mkono hata tu kwa karama yake. Binafsi nimeona nikitengenezwa ukristo wangu kwa sehemu kubwa sana nilipokuwa na wengine, zaidi ya nilivyokuwa mwenyewe.

Ibadani pia ni mahali ambapo, utapata fursa ya kumwimbia na kumwabudu Mungu, kwa nafasi na uhuru zaidi kuliko mahali ulipo mwenyewe. Na ukikosa ibada ya Sifa, pia furaha ya wokovu haiwezi kumiiminika ndani yako.Sifa huponya mioyo yetu. Huondoa uchungu na mizigo yetu,.Jaribu kudumu muda mrefu katika sifa, utaona badiliko kubwa sana moyoni mwako.


5) Hakikisha unapiga hatua kiroho.

Ukiridhika na hiyo hiyo hali ya kiroho muda mrefu, tatizo hili ni lazima likukute.. lilishawahi nikuta mimi, na likanisumbua sana.. Embu tengeneza picha mtoto ameshafikisha miaka 5, bado anategemea tu, maziwa ndio yawe chakula chake, Je! atafurahia chakula hicho kama alivyokuwa na miezi 5?, jibu ni la, kinyume chake ndio atadhoofika.


VIvyo hivyo na wewe ikiwa umeokoka, na kitambo sasa kimepita, hakikisha kila siku unapiga hatua mpya, katika kujifunza, kuacha dhambi, na zaidi sana, kushuhudia habari njema kwa walio nje.
Moja ya mambo ambayo yananipa furaha moyoni ya wokovu, ni pale napoona siku yangu haijapita bure bure bila kufanya kitu fulani kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Lakini nikipitisha muda fulani mrefu, nipo nahangaika hangaika tu na mambo ya kiulimwengu, huwa furaha hiyo inapotea kabisa, najiona kama Roho Mtakatifu ameniondoka.


Hivyo wewe kama mkristo hakikisha, kila siku unapiga hatua, anza kuwahubiria na wengine na bila shaka utaufurahia mwenyewe wokovu wako.


Hivyo katika mambo hayo matano (5), angalia ni wapi umezembea, kisha uchukue hatua nyingine ili usife kiroho, kwasababu ukiendelea nayo hiyo hali muda mrefu hatma yake itakuwa ni kurudi nyuma au kufa kiroho kabisa. Kubali kuanza upya na Bwana.
Kumbuka tatizo sio wokovu wetu, tatizo lipo katika mienendo yetu.
Bwana atusaidie.


Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Furaha ni nini?

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

Nini maana ya wokovu watoka kwa Wayahudi? (Yohana 4:22)

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

VIPINDI VINNE VYA MAISHA VILIVYO VIGUMU MTU KUMKUMBUKA MUUMBA WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

USINIONDOLEE ROHO WAKO MTAKATIFU.

Swali: Je! Roho Mtakatifu anaweza kuondoka juu ya Mtu?.Kulingana na Zaburi 51:11?

Tusome,

Zaburi 51:11 “Usinitenge na uso wako, Wala Roho yako mtakatifu usiniondolee“.

Jibu rahisi la swali hili ni ndio!, anaweza kuondoka juu ya mtu, na mtu akabaki kama alivyo…

Mfano wa mtu katika biblia ambaye aliondokewa na Roho Mtakatifu juu yake ni Mfalme Sauli.

1Samweli 16: 14 “Basi, roho ya Bwana ilikuwa imemwacha Sauli, na roho mbaya kutoka kwa Bwana ikamsumbua.

15 Nao watumishi wa Sauli wakamwambia, Angalia, sasa roho mbaya kutoka kwa Mungu inakusumbua”

Na sababu pekee iliyosababisha Roho wa Mungu kuondoka juu ya Sauli ni tabia ya Sauli ya kutokujali na vile vile kutoyatii maagizo ya Mungu, na kumdharau.

1Samweli 15:22 “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu”.

23 Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”.

Na madhara ya mtu aliyempoteza Roho Mtakatifu, ni KUONDOKEWA NA FADHILI ZA MUNGU JUU YA MAISHA YAKE.

Sauli aliondokewa na Fadhili za Mungu, baada tu ya Roho wa Mungu kuondoka juu yake..

2Samweli 7:14 “Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu; akitenda maovu nitamwadhibu kwa fimbo ya binadamu na kwa mapigo ya wanadamu;

15 LAKINI FADHILI ZANGU HAZITAMWONDOKA, KAMA VILE NILIVYOMWONDOLEA SAULI, niliyemwondoa mbele yako”.

Mtu aliyeondokewa na Fadhili za Mungu, anakuwa anaipoteza ile Amani ya KiMungu kipindi amempokea Roho, hali kadhalika ile furaha ambayo ilikuwa ndani yake inapotea!..ile raha aliyokuwa anaipata alipokuwa ndani ya wokovu, inapotea!…Ule utulivu aliokuwa anaupata kipindi Roho yupo juu yake, unapotea….kile kibali alichokuwa nacho kipindi cha mwanzo kinaondoka..anakuwa ni mtu wa kuhangaika, na kusumbuliwa na roho chafu za wivu, hasira, uchungu, na nyinginezo, kama ilivyokuwa kwa Sauli.

Maandiko yanasema Roho wa Mungu alipomwacha tu Sauli, pale pale roho mbaya ikaanza kumsumbua…akaanza kumwonea wivu Daudi, akaanza kuwa mkatili kwa kuwaua makuhani wa Mungu..

1Samweli 22:11 “Ndipo mfalme akatuma watu waende kumwita Ahimeleki, kuhani, mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, hao makuhani, waliokuwako huko Nobu; nao wakaenda kwa mfalme wote pia”.

Hizo ndizo hasara za kumpoteza Roho Mtakatifu.. Mfalme Sauli alipoasi, Fadhli za Mungu zilimwondoka, na akawa mtu wa kukosa amani, furaha, kujiamini, na wivu…

Lakini kumbuka pia, kuondokewa na Roho Mtakatifu si kuacha kunena kwa lugha, au kufanya miujiza, au kutoa pepo. Mtu aliyeondokewa na Roho Mtakatifu bado anaweza kutoa pepo, bado anaweza hata kunena au kwa lugha..

Kwasababu matunda ya Roho Mtakatifu ndani ya mtu sio Kunena kwa lugha, au kutabiri, au kuona maono, bali ni yale yanayotajwa katika kitabu cha Wagalatia 5:22 “ Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,”.. Mambo hayo ndio yanayopotea ndani ya mtu, pindi Roho Mtakatifu anapoondoka ndani yake.. Na si kunena kwa lugha, au kuona maono, au kutabiri.. Mtu anaweza kunena na kutabiri lakini Roho Mtakatifu akawa hayupo ndani yake..

Utauliza hilo tunalithibitisha vipi?.. Maandiko yanaonyesha Sauli hata baada ya Roho wa Mungu kuondoka ndani yake, bado aliendelea kutabiri..

1Samweli 18:10 “Ikawa siku ya pili yake, roho mbaya kutoka kwa Mungu ikamjilia Sauli kwa nguvu, NAYE AKATABIRI NDANI YA NYUMBA. Basi Daudi alikuwa akipiga kinubi kwa mkono wake kama siku zote; naye Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake”.

Umeona?.. Matunda ya Roho ni tofauti kabisa na kazi za Roho.. Kazi za Roho kama miujiza, unabii, ishara, zinaweza kufanyika kupitia yeyote yule. Bwana alimtumia Punda kuona maono ya malaika mbele ya Balaamu, atashindwaje kumpa maono mwenye dhambi?..

Kwahiyo maono au kunena kwa lugha, sio uthibitisho wa kwanza wa mtu aliye na Roho Mtakatifu, uthibitisho wa kwanza wa mtu mwenye Roho Mtakatifu ndani yake ni hayo matunda tunayoyasoma katika Wagalatia 5:22, ambayo ni Upendo, amani, furaha, Fadhili, kiasi..yaani kwaufupi ni utakatifu (Waebrania 12:24). Ndio maana Bwana Yesu alisema wengi watakuja siku ile na kusema Bwana Bwana hatukutoa pepo kwa jina lako, na kufanya unabii, lakini Bwana atawafukuza kutoka mbele zake.

Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Hata sasa Roho Mtakatifu anaweza kuondoka juu ya Maisha yetu!.. na tukazipoteza Fadhili za Mungu. Na ataondoka endapo TUTAMHUZUNISHA, au KUMZIMISHA.

TUNAMHUZUNISHAJE?

Maandiko yanasema katika Waefeso 4:30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi”.

Tabia za kutokujali Neno la Mungu, kama alivyokuwa Sauli ndizo za kwanza zitakazoweza kusababisha Roho Mtakatifu kuondoka juu yetu..Tunapolisikia Neno halafu hatulitii.. badala yake tunaendelea na mambo yale yale mabaya, hapo tunamhuzunisha Roho mtakatifu aliye ndani yetu…

Tunapoendelea kufanya mambo machafu, ambayo tunajua kabisa ni kinyume na Neno la Mungu, hapo tunamhuzunisha na hivyo ni rahisi kutuacha na tukaingiliwa na maroho mengine.

TUNAMZIMISHAJE?

Maandiko yanasema katika kitabu cha 1Wathesalonike 5:19 kuwa “Msimzimishe Roho”.. Maana yake Roho Mtakatifu anaweza kuzimika ndani yetu. 

Na tunamzimisha Roho kwa sisi kuacha kuomba, kuacha kufunga, kuacha kufanya ibada, kuacha kuifanya kazi ya Mungu, kuacha kumtolea, kuacha kumtukuza na kumsifu na kuifanya kazi yake na kuacha kuishi Maisha matakatifu. Mambo haya yanamfanya Roho Mtakatifu kuzimika ndani yetu, na hata kuondoka kabisa na kutuacha.

Bwana Yesu atusaidie tuzidi kudumu katika Neema yake na kuitunza zawadi nzuri ya Roho aliyotupatia (Matendo 2:39).

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

Mtakatifu ni Nani?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Rudi nyumbani

Print this post

Watu wenye kuvunja maagano ndio watu wa namna gani? (Warumi 1:31)

Napenda kujua watu wenye kuvunja maagano wanaozungumziwa katika Warumi 1:31, ndio watu wa namna gani?

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 28, ili tuweze kuelewa vizuri..

Warumi 1:28 “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.

29 Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,

30 wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao,

31 wasio na ufahamu, WENYE KUVUNJA MAAGANO, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;

32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao”.

Umeona? watu wenye kuvunja maagano sio watu WANAOOMBA NA KUVUNJAA MAAGANO YA UKOO!! LA!. Bali wanaovunja maagano wanaozungumziwa hapo, ni watu wote ambao hawadumu katika AHADI ZAO, au MANENO YAO WENYEWE. Na hawa wamegawanyika katika makundi matatu.

1.WANAOVUNJA MAAGANO YA IMANI.

Mtu anapoamua kumfuata Yesu, na kuokoka anakuwa ameingia KATIKA AGANO LA DAMU YA YESU. Kuanzia huo wakati damu ya Yesu inaanza kunena juu yake, mtu huyo anakuwa rafiki wa Mungu, na mrithi wa ahadi za Mungu, kwasababu tayari kashaingia katika Agano la Mungu, kupitia damu ya Yesu.

Lakini huyu mtu anapoamua kuacha Wokovu, na kuurudia ulimwengu, tafsiri yake ni kwamba KALIVUNJA LILE AGANO TAKATIFU LA DAMU YA YESU, Ambalo kupitia hilo alitakaswa dhambi zake na kuwekwa huru mbali na utumwa wa dhambi.. Mtu wa namna hii maandiko yanasema hali yake itakuwa mbaya sana baada ya kufanya hivyo.

Waebrania 10:28 “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 Mwaonaje? HAIKUMPASA ADHABU ILIYO KUBWA ZAIDI MTU YULE ALIYEMKANYAGA MWANA WA MUNGU, NA KUIHESABU DAMU YA AGANO ALIYOTAKASWA KWAYO KUWA KITU OVYO, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”

Umeona?.. Ipo hatari kubwa sana ya KURUDI NYUMA baada ya kumpokea Yesu, kwasababu kwa kurudi nyuma kwako, ni sawa na UMELIVUNJA AGANO TAKATIFU.

2. AGANO LA NDOA.

Mtu aliyeoa au aliyeolewa katika Ndoa Takatifu, ambaye alisimama mbele ya kanisa la Kristo, na kuahidi mbele za Bwana kuwa ataishi na mwenzake katika hali yoyote ile atakayokutana nayo katika maisha, yaani katika hali ya shida na raha, na huzuni, na misiba na hata katika magonjwa na madhaifu..

Halafu ikatokea siku za mbeleni akamwacha Mwenzake, na kwenda kuoa au kuolewa na mwingine, Mtu wa namna hii ni MTU ANAYEVUNJA MAAGANO, ambaye adhabu yake ni kubwa sana.


Ndugu kama umeoa au umeolewa, fahamu kuwa hupaswi kumwacha mke wako au mume wako, unapaswa umvumilie katika kasoro zake, ukimwacha mke wako/mume wako kwasababu tu amekuwa mdhaifu katika mwili, au kwasababu anamepata ugonjwa fulani, au kwasababu amekuwa na hasira, au ameongezeka mwili au amezeeka..na ukaenda kuoa/kuolewa na mwingine, basi fahamu kuwa UMEVUNJA AGANO, na hatari ya kuvunja AGANO ni adhabu ya ziwa la Moto.

3.AGANO LAKO MWENYEWE.

Agano lako mwenyewe hilo linaweza kuwa NADHIRI uliyomwekea Mungu.. Kama umeweka Nadhiri Mbele za Mungu, basi hakikisha unaiondoa hiyo Nadhiri kwa kuitimiza..

Mhubiri 5:4 “Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; kwa kuwa yeye hawi radhi na wapumbavu; basi, uiondoe hiyo uliyoiweka nadhiri.

5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe”

Vile vile kama umepanga kufanya jambo fulani Jema basi litimize hilo, KWASABABU HILO NI AGANO LAKO LA HIARI uliloingia WEWE NA ROHO YAKO.

Kuna mhubiri fulani alitokewa na Bwana Yesu katika maono, na Bwana akamwambia “Kama hutakuwa mwaminifu katika maneno yako mwenyewe, basi huwezi kuwa mwaminifu katika maneno yangu”.

Akimaanisha kuwa kama umesema utafunga hii wiki, au utasali masaa mawili leo, au utafanya hiki au kile kwaajili ya ufalme wa mbingu, halafu kitu hicho ulichokipanga katika roho yako, hutakitekeleza basi wewe Sio mwaminifu katika maneno yako mwenyewe, sio mwaminifu katika maagano yako mwenyewe, hivyo wewe ni mtu kigeugeu, unayevunja maagano yako…na Mungu hawezi kukuamini pia..

Yakobo 1:7 “Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.

8 Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote”.

Kumbukumbu 23:23 “Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri Bwana, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako”.

Bwana atusaidie tusiwe watu wa kuvunja maagano, bali kutimiza maagano.
Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Paulo aungane na wale watu wanne wenye nadhiri?

Mtu mwenye “kitango” ni mtu wa namna gani kibiblia?

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?

Biblia inasema tusiwe kwazo kwa yeyote, je! inawezekanikaje kwa dunia hii ya sasa?(2Wakorintho 6:3).

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Rudi nyumbani

Print this post

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

Mafundisho maalumu kwa waongofu wapya: Sehemu ya tatu.

Ikiwa wewe ni mwongofu mpya, yaani umeokoka hivi karibuni, basi mafundisho haya yanakufaa sana katika hichi kipindi ulichopo.

Ikiwa ulipitwa na mafundisho ya nyuma, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba zetu hizi +255693036618 tukakutumia mafundisho hayo.

Ni muhimu kufahamu kuwa, unapookoka yupo adui atakayesimama kinyume chako kukupinga wakati wote, ili uiache imani. Na huyo si mwingine zaidi ya shetani. Hivyo katika hatua hizi za awali, huna budi kufahamu silaha madhubuti za kuweza kumwangusha, Kwasababu ukizikosa ujue kuwa utakufa tu kiroho. Na silaha yenyewe tunazisoma katika vifungu hivi;

Ufunuo 12:9 “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.
10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.
11 NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA- KONDOO, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.

Jiulize hapo kwanini haijasema wakamshinda kwa mafuta ya upako, au kwa kanisa zuri, au kwa maombi ya vita.. Bali kwa damu ya Mwana kondoo na kwa neno la ushuhuda wao.
Kuna nini katika damu ya Yesu? Na ushuhuda ulionao?
Ni lazima ufahamu umuhimu wa damu yake, katika maisha yako ya wokovu.
Damu ya Yesu ilifanya mambo makuu matatu

  1. Kuondoa dhambi
  2. Kunena juu yetu
  3. kukanyaga nguvu za ibilisi

1) Kuondoa dhambi.


Biblia inasema..

Waebrania 9:22 “Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo”.

Katika agano la kale Utakaso wa kila namna, ulitegemea damu za wanyama, kwasababu ndio kanuni ya Mungu ya kiroho ya kuondoa dhambi, hivyo tangu zamani zile haikupatikana damu yoyote kamilifu isiyo na hila wala mawaa itakayoweza kuondoa dhambi za mtu moja kwa moja, bila kuacha kimelea chochote. Na ndio maana kumbukumbu la dhambi lilikuwepo wakati baada ya wakati , hivyo ilimpasa kuhani mkuu kila mwaka aingie kule hemani akiwa na damu ya wanyama ili kuwapatanisha wana wa Israeli,
Lakini sasa Yesu alipokuja, damu yake ilikuwa ni kamilifu zaidi ya wanyama, yeye tu ndiye aliyeweza, kusafisha na kuondoa kabisa dhambi ya mwanadamu isikumbukwe na Mungu milele, bila kuhitaji tena kuhani kila mwaka kwenda kuomba rehema kwa dhambi zilizotangulia.


Hii ikiwa na maana gani?
Ukiukosa ufunuo huu, kuhusiana na nguvu iliyopo katika damu ya Yesu iliyomwagika msalabani, basi ni ngumu sana, kuamini kama dhambi zako za kale Mungu alishazifuta na kuzisahau kabisa kabisa.
Ni kawaida kwa waongofu wapya kuletewa mawazo haya na ibilisi kwamba, bado Mungu anawaona ni wachafu, bado Mungu anakumbuka zile dhambi walizozitenda nyuma, zile mimba walizotoa, ule uzinzi walioufanya nje ya ndoa, rushwa walizokuwa wanakula, mauaji waliyoyafanya, waganga waliokuwa wanawafuata.


Hii ndio silaha kubwa ya ibilisi kwa waongofu wapya. Wanajiona kama vile bado hawajasamehewa vizuri, bado laana zinawafuatilia, Ndugu, ujue hayo ni mawazo ya shetani, kwasababu umekosa kujua gharama Yesu aliyoingia kwa ajili ya dhambi zako. Ile damu yake kumwagika, ilikuwa ni kukomesha dhambi zako zote na laana zako kabisa kabisa..


Ndio maana hapo biblia inasema, wakamshinda kwa damu ya mwana-kondoo, na ushuhuda wao, yaani ushuhuda wa kukombolewa na Yesu. Ndio silaha kubwa sana ya kumshinda ibilisi.
Hivyo mawazo kama hayo yakikujia yakatae, sema mimi nimeshasamehewa, ya kale yamepita, tazama yamekuwa mapya. Mimi sina deni la dhambi, Ukifanya hivyo, shetani atajua umeshafahamu nafasi yako, hivyo atakukimbia, na utaishi maisha ya amani na kutojihukumu.


2) Kunena juu yetu.


Damu pia inafanya kazi ya kunena.

Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili”.

Kaini alipomuua ndugu yake Habili, Biblia inasema Mungu alimwambia Kaini sauti ya damu ya ndugu yake inamlilia kutoka ardhini (Mwanzo 4:10). Maana yake ni kuwa Mungu alikuwa anaisikia ili sauti ikinena, ikiomba, ikitaka haki itendeke, haikutulia tu.
Hata leo ukiona mtu anapitia majanga majanga fulani hivi, utasikia watu wakisema, ni kwasababu alimuua mama yake hivyo ile damu inamfuatilia..


Kuonyesha kwamba kuna uhalisia fulani katika damu ya mtu kupatiliza mema au mabaya.
Na ndivyo ilivyo kwa damu ya Yesu, inanena Mema, kuliko ile ya Habili, maana yake, hata sasa inazungumza, juu ya wale wote waliompokea yeye mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Inasema huyu anastahili kulindwa, huyu anastahili baraka, huyu anastahili furaha, huyu anastahili heshima, huyu anastahili kibali, afya n.k.


Hivyo wewe uliyeokoka ni wajibu wako kujua jambo hili, ili usiishi kama yatima hapa duniani. Ulipokuwa dhambini damu ya Yesu ilikuwa haineni juu yako, kwasababu haukuwa ndani ya agano lake. Lakini sasa upo, fahamu kuwa, Yesu anakuombea kila siku kwa Baba, hivyo kuwa na ujasiri ukijua kabisa nyuma yako ipo baraka, neema na habati wakati wote. Kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda utayathibitisha hayo yote.

Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea”.

Hivyo mishale yote ya hofu, wasiwasi, mashaka, ambayo shetani atajaribu kukutumia ili urudi nyuma, ikatae, mishale ya kesho nitaishije, nikipoteza kile kwasababu ya Yesu itakuwaje? ondoa hayo mawazo ya kuangamia, kwasababu ipo damu inayonena kwa ajili yako usiku na mchana, ili utembee katika njia salama ya uzima.

Zaburi 27:1 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?
2 Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka.
3 Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.
4 Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake”.
Lishike sana hili, ukilikosa, shetani atatumia upenyo huu kukurudisha nyuma, kama alivyofanikiwa kuwarudisha wengi.


3) Kukanyaga nguvu za ibilisi.

Utajiuliza ni kwanini Bwana Yesu, hakulisema hili neno “IMEKISHWA”, Mahali popote katika huduma yake, mpaka siku ile alipopelekwa pale msalabani? Ni kwamba alijua hakuna kuzimaliza nguvu na utawala wa ibilisi bila agano la damu timilifu.


Hivyo aliposema IMEKWISHWA, Ni kweli ilikwisha, na ndio maana aliwaambia mitume wake maneno haya;

Luka 10:18 “Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Ni lazima ujue kwa damu ya Yesu, shetani, hana nguvu yoyote juu yako. Kwamfano mwanajeshi dhaifu akitambua kuwa bomu alilonalo la nyuklia linaweza kuteketeza mji mzima, hataweza kuwa na hofu, na wanajeshi 1000 wenye nguvu, wanaomjia na bunduki zao. Kwasababu anafahamu akilituma tu kombora lake moja, kikosi chote kinakuwa jivu.


Ndivyo ilivyo kwako wewe uliyeokoka, fahamu kuwa hatua uliyopo, shetani hana nguvu zozote za kukushinda, kwasababu tayari nguvu zako ni nyingi kuliko zake, haijalishi hali yako ya uchanga kiroho. Hivyo, usiogope wachawi, usiogope mapepo, usiogope hata maadui zako. Lolote linalokuja mbele zako, uwe ni udhaifu, magonjwa, mashambulizi ya shetani, kemea kwa jina la Yesu, vitaondoka, usiwe mnyonge kwa shetani, kwasababu yule ni kama kinyago tu kinasimama hapo kukutisha, lakini hakina nguvu yoyote.
Hivyo zingatia sana kuyatafakari hayo.


Na Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

KAA MAJANGWANI.

USIMPE NGUVU SHETANI.

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

Rudi nyumbani

Print this post

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe karibu tuyatafakari maneno ya uzima.

Neno la Mungu linasema…

1Samweli 15:22 “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, KUTII ni bora kuliko dhabihu, Na KUSIKIA kuliko mafuta ya beberu.

23 Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; KWA KUWA UMELIKATAA NENO LA BWANA, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”.

Ni vizuri kumtolea Bwana, tena ni moja ya maagizo yake ambayo tukiyatenda kwa hiari yetu wenyewe basi tutapata thawabu nyingi. Lakini ni vizuri pia kujua jambo moja kuwa Mungu wa Mbingu na nchi si mkusanya mapato kutoka kwetu, na wala hahitaji kitu kutoka kwetu.

 Zaidi sana vyote tunavyomtolea yeye kama sadaka, vinaenda kutumika kwaajili ya watumishi wake na huduma alizowapa.. lakini yeye mwenyewe hakuna chochote anachokipokea.  Kwasababu yeye hahitaji kupokea chochote kutoka kwetu, kwamaana vitu vyote vinatoka kwake.

Kwahiyo kama fedha zetu haziendi mbinguni aliko yeye, wala matoleo yetu mengine hayapai mbinguni kumfikia, maana yake ni kwamba lipo jambo lingine ambalo ni muhimu sana kwake kupokea kutoka kwetu, Zaidi ya sadaka na matoleo tunayomtolea. Na jambo lenyewe si lingine Zaidi ya KULITII NENO LAKE.

Bwana anataka mioyo ya kutii tunapolisikia NENO LAKE.. Hiyo ndiyo dhabihu na sadaka anayoikubali kuliko zote..

Isaya 66:1 “Bwana asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?

2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, ATETEMEKAYE ASIKIAPO NENO LANGU”.

Unaona?..Unaposoma kwenye biblia kuwa “waasherati na wazinzi hawataurithi ufalme wa Mbinguni (Wagalatia 5:20)”.. na ukaacha kulitii hili NENO, na kinyume chake ukaendelea na uzinzi wako, huku ukijitumainisha kwa sadaka zako nyingi unazoendelea kuzitoa.. fahamu kuwa UNAFANYA MACHUKIZO MBELE ZA MUNGU!!..Kwasababu maandiko yanasema…

Mithali 15:8 “SADAKA YA MTU MBAYA NI CHUKIZO KWA BWANA…..”.

Unaposoma kuwa Wenye dhambi sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la Moto, kwasababu wamekataa kutubu dhambi zao, na wewe unajijua kabisa bado hujatubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, bado ukawa unaendelea na kulipa zaka zako, bado ukawa unaendelea na kuchangia kazi ya Mungu..nataka nikukumbushe kuwa UNAFANYA MACHUKIZO!!.. Mungu wetu si mkusanya mapato kutoka kwetu, na wala hahitaji fedha zetu… Yeye mwenyewe(Yesu Kristo) alisema maneno yafuatayo..

Mathayo 9:13 “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA”.

Bwana Yesu anachotaka kuona kutoka kwetu, MIOYO YA TOBA, iliyosikia Neno lake na kutetemeka na kuamua KUGEUKA!..Kumbuka kutii ni bora kuliko dhabihu. Kamwe usijitumainishe katika matoleo unayoyatoa na ukasahau kulitii NENO LA MUNGU. Bwana amelitukuza Neno lake kuliko kitu kingine chochote.

Kabla ya kufikiria kumtolea Mungu, fikiria kujitakasa kwanza, fikiria kuacha uzinzi na ukahaba kwanza, fikiria kuacha kuacha ulevi, fikiria kuacha wizi, fikiria kuacha Ugomvi na baada ya kuacha hayo yote, ndipo ufikirie kumtolea Bwana matoleo yako, lakini kamwe usitangulize dhambi zako mbele ndipo sadaka zako zifuate, kwasababu ukifanya hivyo utakuwa unajitafutia laana badala ya baraka..

Mithali 15:8 “SADAKA YA MTU MBAYA NI CHUKIZO KWA BWANA; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.

Kumbukumbu 23:7 “Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume.

18 Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”

Siku zote Litii Neno la Bwana, kwasababu hilo ndilo MWANGA WA NJIA YETU, YA KWENDA MBINGUNI.

Bwana akubariki,

Maran atha!!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Dhabihu ni nini?

CHAMBO ILIYO BORA.

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

NINI MAANA YA KUTUBU

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

Rudi nyumbani

Print this post

NITAJUAJE KUWA NIMEITWA ILI KUMTUMIKIA MUNGU?

SWALI: Bwana Yesu asifiwe, naomba kufahamu nitajuaje kama nimeitwa ili kumtumikia Mungu, ni viashiria gani vitanitambulisha?


JIBU: Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe milele na milele.
Ni vizuri kufahamu kama vile ilivyokuwa ni mapenzi ya Mungu, watu wote waokolewe na kufikiwa na injili, sawasawa na;

1Timotheo 2:3 “Hili ni zuri, nalo lakubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu;
4 ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli”.

Vivyo hivyo ni mapenzi ya Mungu watu wote wawe watumishi wake,wasimame kwa ajili ya kazi yake hapa duniani, tunalithibitisha hilo katika maneno ya Bwana Yesu mwenyewe alisema..

Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, MTU YEYOTE, akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate”.

Anasema mtu yeyote, akitaka kumfuata,…Kumfuata kuwa nani? Ni kumfuata kuwa mwanafunzi wake..Ni sharti ajikane mwenyewe maisha yake na kujitwika msalaba wake kila siku na kumfuata yeye.
Kumbuka si kila mtu anaweza kuwa mwanafunzi wa Yesu, Kipindi kile kulikuwa na makutano yaliyohitaji wokovu tu, na pia kulikuwa na wanafunzi wake, ambao ndio wale mitume wake, na wale wengine sabini, pamoja na lile kundi la wanawake wacha Mungu lililokuwa linaongozana naye..


Sasa hao wanafunzi wake ndio waliokuja kuwa watumishi wake, katika nyanja mbalimbali..
Hivyo, kilichoweza kuwatofautisha wanafunzi(watumishi) wa Yesu na wale wengine, ni kwamba wale wanafunzi walikubali kuingia gharama zote, alizoziorodhesha Yesu, za kiutumishi, wale wengine hawakuweza, ndio ilipotokea hapo.

Luka 14:25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,
26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?
29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,
30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.
31 Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?
32 Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali.
33 Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Hizo ndio gharama za utumishi.. Ikiwa wewe (Au mtu yeyote) utaweza kuzifuata, basi, tayari wewe ni mtumishi wa Yesu hapa duniani, kama utakuwa tayari kuacha kila kitu kwa ajili yake, wewe ni mtumishi wake, kuacha mambo yote ya kiulimwengu, kupoteza hata kazi yako, au elimu yako, Kukubali kutengwa na ndugu na wazazi pale inapobidi lakini usimwache Yesu, wewe ni mtumishi wake.


Tofauti na wengi wanavyodhani, kwamba ili ujue wewe ni mtumishi wa Yesu, ni lazima uoteshwe kwanza ndoto, au utokewe na Yesu kama mtume Paulo, au uwekewe mikono na askofu kanisani.. Ndugu hapo bado hujafanyika mwanafunzi wa Yesu, ikiwa ndani yako bado hakuna kujikana nafsi na kupoteza kila kitu kwa ajili yake. Yuda alikuwa ni mtume wa Yesu ambaye si kutokewa naye, bali aliishi naye akala naye kwa miaka mitatu, lakini mwisho wa siku akaishia kumsaliti Bwana wake..Hiyo yote ni kwasababu hakuwa tayari kuuacha ulimwengu kwa ajili ya Kristo.


Kwa kawaida ili mtu apewe dhamana ya kuwa askari wa kulinda raia, ni lazima mafunzo yake yawe tofauti kabisa na ya raia wengine, na ndivyo ilivyo kwa Bwana Yesu..Vigezo ndio hivyo ameshavitoa.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba, kila mmoja ameitwa kuwa mtumishi wa Mungu, isipokuwa ni wachache ndio wanaoweza kuingia gharama zake, Lakini ingetokea dunia nzima au wakristo wote wameingia hizo gharama basi wote ni watumishi bila kujali, jinsia, rangi, umri, au vyeo vyao.
Fanyika sasa mwanafunzi wa Yesu, naye atakuweka katika utumishi wake.


Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana alimaanisha nini kusema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake”?

INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.

SIKU YA MAONYESHO MAKUU YA BWANA YESU, IPO KARIBU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MIHURI SABA

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)

Rudi nyumbani

Print this post

KAA MAJANGWANI.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Sehemu ya pili: Kaa Majangwani:

Luka 1:80 “Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu rohoni, akakaa majangwani hata siku ya kutokea kwake kwa Israeli”.

Ni kawaida ya Mungu, kuwaandalia Watoto wake, mahali maalumu pa kukulia kiroho.. Ikiwa unatamani nguvu zako za rohoni ziongozeke kwa kasi wewe kama mwongofu mpya uliyezaliwa mara ya pili, huna budi kukaa majangwani.

Mungu alipowatoa wana wa Israeli Misri, hakuwavukisha moja kwa moja na kuwafikisha Kaanani ndani ya siku moja, bali aliwapitisha kwanza jangwani, kuwalisha huko na kuwakuza kiroho, kwa muda wa miaka 40, kwasababu walikuwa bado ni Watoto wachanga, na ndipo baadaye wakaingia Kaanani, wakiwa Hodari na nguvu nyingi rohoni.

Hosea 11:1 “Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misri”.

Biblia pia inatuambia Yohana mbatizaji alipozaliwa, alikimbilia majangwani huko kuishi, na matokeo yake akakua na kuongozeka nguvu nyingi sana rohoni kwa kasi, na ndio maana hatushangai kwanini Bwana Yesu anamshuhudia na kusema katika wazao wa wanawake hakuwahi kutokea mtu aliyekuwa mkuu kama Yohana Mbatizaji.(Mathayo 11:11).. Hiyo yote ni kwasababu gani? Ni kwasababu alitumia Muda mwingi majagwani.

Sasa Kiroho jangwani ni wapi?

Haimaanishi kuwa ni sisi tukimbilie majangwani tukaishi huko, ili tukue kiroho hapana… Kama tunavyojua jangwani ni mahali ambapo hapana uwepo wa wanadamu, ni mahali pa ukiwa, pasipokuwa na huduma zozote za kijamii.. Ndivyo inavyompasa mkristo aende rohoni.

Unapaswa katika hatua zako za awali za wokovu: Kwa bidii zote uwe tayari, kuukana huu ulimwengu. Kukaa mbali na mambo yote yanayousonga wokovu wako, bila kujali unapoteza nini, au unakosa nini..

Ukiokoka, kubali kuachana na wale marafiki zako wa kale uliokuwa unakwenda nao disco, uliokuwa unakunywa nao pombe, uliokuwa unatukana nao, kubali kuwa mpweke, kwa kipindi Fulani, kwani hivyo ndivyo unavyoiponya roho yako.

Ukiokoka, kubali wakati mwingine, kupoteza hiyo kazi isiyo halali kwa Mungu, kama unafanya biashara ya pombe acha, ..wala usidhani kuwa utaangamia, kwamba Mungu atakuacha ufe, hilo wazo ondoa, uwezo wa kukulisha Mungu anao, Kama alivyofanya kwa wana wa Israeli kule jangwani, atafanya na kwako pia..

Biblia inasema..

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, AENDE ZAKE NYIKANI HATA MAHALI PAKE, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo”.

Umeona, Mungu ameshaandaa mahali pako huko nyikani, pa kukulisha kwa wakati wako na majira yako. Hivyo usiogope wewe uliyemzaa Kristo maishani mwako.

Kama wewe ni binti kubali kukaa mbali na Fashion, kubali kujisitiri na kuchoma hivyo vimini na masuruali, kubali kuonekana umerukwa na akili kwa ajili ya Kristo, hata ulimwengu mzima ukikuona mjinga, kubali hiyo hali, weka kando kila mzigo wa dhambi, kwasababu ndivyo unavyoiponya roho yako.

Je! Faida yake ni ipi?

Faida yake ni kwamba Yesu anapata nafasi ya kukupitisha katika madarasa yake, na kwasababu husongwi na mambo mengine, hivyo kasi yako ya kukua kiroho itakuwa ni kubwa sana..

Maandiko yanasisitiza hilo katika;

Isaya 40:3 “Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, Itengenezeni nyikani njia ya Bwana; Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu”.

Kuonyesha kwamba mahali pekee ambapo utamtengenezea Mungu njia, katika maisha yako ni jangwani.

Leo hii utaona watu wengi wamedumu katika wokovu kwa miaka mingi, lakini huoni mabadiliko makubwa yoyote ndani yao, bado ni wachanga kila siku wanataka wanyweshwe tu maziwa, ni kwasababu gani?

Ni kwasababu hawakumpa Kristo, nafasi ya kuwafundisha majangwani..Walilikimbia jangwa, wakakaa ulimwenguni, na hivyo Bwana akawaacha.

Ndugu/Dada uliyeokoka hivi karibuni usiipuzie hiyo sauti inayokuambia, acha hiki, acha kile, mwache Rafiki yule, acha jambo lile..usiipuuzie kabisa, fanya hivyo, ni sharti upoteze, ili upate baadaye, majira haya ni kujikana nafsi yako, kuichukia nafsi yako, na kujitwika msalaba wako kumfuata Yesu, hilo haliwezi kuepukika ikiwa unataka ukue kiroho kwa kasi anayoihitaji Kristo ndani yako.

Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.

25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.

26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?

27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”.

Kabla ya kumzalia Mungu matunda ni lazima upitishwe jangwani, kutakaswa na Mungu, hivyo kuwa mwepesi kuacha udunia wako. Umfuate Yesu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA: Sehemu ya 1

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNYAKUO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

Rudi nyumbani

Print this post

HATARI! HATARI! HATARI!

Unajua ni kwanini Bwana Yesu alisema  “Jiangalieni basi jinsi msikiavyo?” (Luka 8:18)

Alijua kuwa kuna hatari kubwa sana ya mtu aliyesimama kupotea kwa kile tu anachokisikia ikiwa hakitokani na yeye.. Hivyo si kila jambo ni la kulisikiliza na kuliweka moyoni, Zama hizi ni zama za uovu.

Mambo haya makuu matatu, kuwa nayo makini sana siku hizi za mwisho.

  1. Maono
  2. Ndoto
  3. Mafunuo

Ikiwa Maisha yako yote unayoishi ni kutegemea tu maono unayoonyeshwa, au ndoto, au mafunuo, na huku umeliweka Neno la Mungu nyuma basi ujue, hatari ya kupotea ni kubwa sana..tena sana. Haijalishi yatakuwa yanatoka kwa Mungu au kwa shetani, kama unaliweka Neno la Mungu nyuma..Bado hatari ya kupotea ni kubwa sana kuliko unavyodhani ndivyo ilivyo.. Najua inaweza ikawa ni ngumu kupokea lakini ukweli ndio huo.

Leo tupo wakati ambapo mtu atakuambia nimepelekwa kuzimu, nikaonyeshwa hiki, na kile, nimeonyeshwa watu wanaokula pipi za ivory, na soda za cocacola wapo kuzimu, nimeonyeshwa mabinti wote, walioingia katika ndoa bila ubikira, wanazini, waume zao ni wale wakwanza waliozini nao, kabla hawajaokoka hao ndio wanapaswa wakaolewe nao, hivyo wakiolewa na wengine wanazini..Nimeonyeshwa watu wote wanaosali siku ya jumapili wapo jehanamu, nimeambiwa na Yesu watu wote wanaoota ndoto wanapaa wajiandae na moto, nimeambiwa, kama umeokoka, unapaswa urudishe madeni yote uliyowahi kuwatapeli watu huko nyuma hata kama huna uwezo huo, usipofanya hivyo ni ziwa la moto, kama unakwenda beach kuogelea ni kuzimu, kama upo katika ndoa na unatumia uzazi wa mpango ujue ni motoni moja kwa moja…n.k n.k. Ni mengi mno..

Mambo kama haya embu tujaribu kudhania kuwa ni kweli yanatoka kwa Mungu..Lakini nikikuuliza swali ni nini kimekupa uhakika kuwa kinatoka kwa Mungu, utanipa jibu gani? Utasema ni kwasababu mpendwa yule kaonyeshwa au mimi nimeonyeshwa?? Au ninamwamini sana yule? Unadhani hilo tu linatosha?

Je! Ikitokea mwingine akakamwambia watu wote wenye Ngozi nyeusi, wanayo laana ya Hamu, hivyo wasipokombolewa kwa kupitishwa kwenye kemikali maalumu ya kuchubuliwa Ngozi zao, hawataingia mbinguni..Je! hilo nalo utalithibitisha vipi?

Ndugu ukiishi kwa Neno la Mungu, ni elimu tosha, ni ushuhuda tosha..hata kama mtu akikuambia nimeonyeshwa mashoga  wote wapo motoni, wewe uliye na Neno, hutashangaa kana kwamba ni jambo jipya, kwasababu Neno linakuambia hivyo..Hata kama asingekuletea maono hayo.

1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Hivyo hapo hujaishi kwa maono yako, bali kwa Neno la Mungu, basi upo salama.. Hatari inakuja ni pale mtu unapotegemea  tu shuhuda, na kuziamini moja kwa moja bila hata ya kuzipima..ndugu  utatoka nje ya mpango wa Mungu, utachanganywa, utaishi kwa hofu na wasiwasi, na presha kubwa, kwasababu huyu atakuambia hivi yule vile, yatachanganyikana ya ukweli na uongo..matokeo yake utashindwa kujua ni wapi umesimama..Na mtu wa namna hii ni rahisi sana kuanguka dhambini. Na ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kuijua biblia.. SOMA BIBLIA.

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Kuwa makini na shuhuda unazozisikiliza mitandaoni (youtube)..Kuwa makini na watu unaowafuatilia mitandaoni. Usipoijenga Imani yako katika Neno la Mungu, shetani atakusaidia kujenga Imani yako katika misingi yake mwenyewe.

Usiniamini mimi, wala usimuamini mtu yeyote, iamini biblia yako, hiyo inatosha..Utakuwa salama.

Mwingine atakuambia Bwana ameniambia leta nywele zako, na kucha zako, weka kwenye kitambaa chekundu, tuombe Pamoja, ukimuuliza misingi hiyo ameitolea wapi, atakuambia nimefunuliwa, na usipofanya hivyo huwezi kufunguliwa.. Hii ni Hatari kubwa sana! ..Kataa kusikiliza hayo mafunuo.

Mwingine atakuambia, pasipo kuniamini mimi, huwezi kwenda katika unyakuo, kataa

1Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;”

Usiwe mwepesi wa kuamini Neno lolote usilolithibitisha katika maandiko,

Bwana atusaidie..

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO YA MASHETANI

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

KUONGOZWA SALA YA TOBA

USIISHI KWA NDOTO!

MIHURI SABA

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

Rudi nyumbani

Print this post