Category Archive maswali na majibu

Ni sahihi kwa mkristo kupokea fedha kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu?

Je! ni sahihi kwa mkristo kupokea fedha kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu kama za uuzaji wa dawa ya kulevya, wizi au bangi?

Jibu: Kama wewe ni mtu uliyeokoka, aidha mchungaji, au mwalimu, au muimbaji au mshirika wa kawaida, sio sahihi kupokea fedha zozote kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu kama za ujambazi au wizi, au uuzaji wa madawa ya kulevya, kwasababu kwa kufanya vile ni sawa na kushiriki zile kazi.

Kwasababu huwezi kupenda fedha za mtu mwovu, halafu ukachukia na kazi zake.. Huwezi kupenda boga halafu ukachukia ua lake.. Mpaka umekikibali kitu maana yake tayari umekikubali na chanzo chake..

Hivyo kama utapokea fedha kutoka kwa mtu anayeuza madawa ya kulevya, au jambazi, tayari moja kwa moja umehakikia chanzo chake na kukikubali!, lakini kama umekikataa chanzo chake pia huwezi kukubali matunda ya chanzo hicho, Kama Bwana Yesu alivyosema katika…

Luka 6:43 “Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri;

44  kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu”

Kwahiyo kibiblia sio sahihi kwa mtu aliyeokoka kupokea fedha kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu, aidha kwa lengo la kuendeleza huduma, au kwa lengo la kujiendeleza yeye mwenyewe. Ni sharti kwanza mtu huyo ageuzwe njia zake kwa kumpokea Yesu kikamilifu na kubadili kazi yake hiyo kwa kufanya kazi halali, ndipo fedha zake ziwe safi. (Hapo atakuwa ameufanya mti wake kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri)

Na sio tu kupokea, vilevile watu hao wafanyao kazi haramu kibiblia hawaruhusiwi kuzipeleka fedha zao kama sadaka au zaka katika nyumba ya Mungu, kwani ni machukizo makubwa sana..

 Mithali 15:8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.

Soma pia Kumbukumbu 23:18 na Mithali 21:27.

Kwahiyo ni lazima kuvifanya vyanzo vyetu kuwa safi, ndipo na matunda ya vyanzo hivyo yawe safi, lakini kama vyanzo ni vichafu hata matunda yake yatakuwa machafu tu, kwa anayetoa na anayepokea. Ndio maana asilimia kubwa ya wanaopokea fedha kutoka kwa watu wanaofanya biashara haramu, zile fedha wanazozipokea ni lazima zitakuja kuwaletea madhara kwa namna moja au nyingine, kwasababu zinakuja na roho na maagizo ya ibilisi nyuma yake.

Bwana atusaidie.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mwana haramu ni nani kibiblia? (Kumbukumbu 23:2).

Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”

KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

Atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? Maana yake nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?

Swali: Katika Wagalatia 3:13 maandiko yanasema Bwana Yesu alisulubiwa juu ya mti, lakini tukirejea tena Yohana 19:19, tunaona biblia inasema Bwana alisulubishwa juu ya msalaba.. je maumbile ya huo msalaba au huo mti yalikuwaje?.. je ulikuwa ni mti uliosimama kama nguzo au miti miwili iliyokutana kama alama ya kujumlisha?

Jibu: Tuirejee mistari hiyo..

Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu AANGIKWAYE JUU YA MTI”.

Na tena..

Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI”.

Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba ambao ulikuwa ni wa malighafi ya mti, na si wa malighafi ya chuma, au ya shaba, hiyo ndio maana ya “kuangikwa juu ya mti”,

Lakini tukirudi katika umbile la msalaba wa Bwana kama ulikuwa ni wa wima mfano wa nguzo au wa kukutana mfano wa alama ya kujumlisha, ili tujue maumbile yake yalikuwaje ni lazima turejee historia kidogo, kwasababu biblia haijatoa maelezo juu ya umbile la msalaba, maelezo iliyotoa ni malighafi ya msalaba tu!.. kuwa ni malighafi ya mti kama tulivyosoma hapo katika Wagalatia 3:13.

Tukirudi katika Historia sote tunajua kuwa wakati Bwana yupo duniani, utawala uliokuwa unatawala dunia nzima ulikuwa ni utawala wa Rumi, na ndio uliomsulubisha Bwana Yesu.

Sasa kulingana na historia, warumi walikuwa na adhabu nyingi walizowahukumu nazo wahalifu. Na mojawapo wa adhabu walizozitoa kwa wahalifu wakuu ilikuwa ni kumtundika mtu juu ya msalaba, na msalaba huo haukuwa nguzo moja ndefu, hapana bali ulikuwa ni nguzo mbili zilizokutana! (kafuatilie historia).

Hivyo mtu alining’inizwa mikono ikielekezwa katika nguzo mlalo na miguu na kichwa vikielekezwa katika nguzo wima, na mwili huo ukishikiliwa na misumari, na watu walisulubiwa uchi wa mnyama pasipo hata kuwa na  kipande chochote cha kuzuia hata sehemu za siri.

Lengo la adhabu hiyo ilikuwa ni kumtesa mtu huyo kwa mateso na maumivu makali, na pia kumwua kwa kifo cha aibu, kutokana na kosa lake alilolifanya. Lakini si wahalifu wote waliokuwa wanahukumiwa adhabu hiyo, bali wale waliokutwa na kosa la kustahili kusulubiwa hivyo.

Kwahiyo Bwana Yesu aliangukia katika hukumu ya namna hii ya kusulubiwa  juu ya msalaba, ingawa hakufanya kosa la kustahili kuuawa!,  Lakini kwasababu ilikuwa ni kwa makusudi ya ukombozi wetu ilimbidi afe kifo cha aibu kama hicho ili sisi tupone!.

Lakini swali ni je! Wale wanaoamini kuwa Bwana Yesu alisulubiwa katika Nguzo ya wima, je hawataokolewa ikiwa wameshika na kuzitenda kanuni nyingine za imani?

Jibu ni la!.. Mtu akiamini kuwa Bwana Yesu alisulubiwa katika mti uliokuwa wima, au katika Miti miwili iliyokatana kwa mfano wa alama ya kujumlisha.. haimwongezei chochote wala haimpunguzii chochote katika vigezo vyake vya kuokolewa… Suala la msingi ni kuamini kuwa Yesu aliteswa na kusulubiwa kwaajili yetu, na akazikwa na kufufuka na akapaa mbinguni, na siku ya mwisho atarudi tena kutuchukua, hivyo tutubu na kuacha dhambi, lakini Mambo mengine hayana msingi sisi kuyajua…

Aina ya mti Bwana aliosulubiwa nao kama ni mshita, au mkoko hauna maana yoyote sisi kujua… vile vile na urefu wa mti au maumbile yake hivyo havitusaidii chochote wala havituongezei kitu katika vigezo vya kuokolewa, kama tu vile sura ya Bwana isivyoweza kutuongezea kitu kwa wakati huu (kwani hakuna anayeijua sura yake lakini bado wokovu tunapata) vivyo hivyo na maumbile ya msalaba hayatuongezei chochote, bali kuzaliwa mara ya pili.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

UTHAMINI WITO WA PILI WA YESU ZAIDI YA ULE WA KWANZA.

BASI MUNGU ALIMWADHIMISHA MNO.JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya kupwita-pwita? (Zaburi 38:10)

Jibu: Turejee,

Zaburi 38:10 “Moyo wangu unapwita-pwita, Nguvu zangu zimeniacha; Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka”.

Kupwita-pwita maana yake, ni “kudunda kwa haraka”, hivyo hapo biblia iliposema “kuwa moyo wangu unapwita pwita”, maana yake ni kuwa “moyo wa mwandishi unaenda mbio” kutokana na mateso aliyokuwa anayapitia.

Mtu anayepitia katika hali ya mateso, kutoka kwa watu wabaya.. ni kawaida kuumia moyo, Tuwapo katika hali kama hiyo, biblia imetufundisha kuwa waombaji na kujinyenyekeza kwa Mungu ili Bwana aiponye mioyo yetu na kutuokoa na mikono ya watesi.

Zaburi 17:14 “Ee Bwana, kwa mkono wako uniokoe na watu, Watu wa dunia hii ambao fungu lao li katika maisha haya”.

Zaburi 59:1 “Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu, Uniinue juu yao wanaoshindana nami. 

2 Uniponye nao wafanyao maovu, Uniokoe na watu wa damu. 

3 Kwa maana wanaiotea nafsi yangu; Wenye nguvu wamenikusanyikia; Ee Bwana, si kwa kosa langu, Wala si kwa hatia yangu.

 4 Bila kosa langu huenda mbio, hujiweka tayari; Uamke uonane nami, na kutazama”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Nitajuaje kuwa nimesamehewa dhambi zangu?

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.

Mtima ni nini kibiblia?.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini jiwe la kusagia Mungu alikataza lisiwekwe rehani? (Kumbukumbu 24:6).

Jibu: Turejee,

Kumbukumbu 24:6 “Mtu awaye yote asitwae jiwe la kusagia, la juu wala la chini, kuwa rehani; kwani hivi ni kutwaa maisha ya mtu kuwa rehani”.

Jiwe la kusagia lilikuwa ni jiwe lililotumika katika kusagia nafaka enzi za zamani, na hata sasa katika baadhi ya jamii.. Lilikuwa ni jiwe kubwa ambapo nafaka kama ngano inawekwa juu yake, na kisha jiwe lingine dogo linawekwa juu yake na kusaga nafaka hiyo.

Lilikuwa pia ni jiwe ambalo linapatikana karibia katika kila nyumba.. ni kama vile leo, jiko ilivyo zana ya msingi karibia katika kila nyumba, hata yule maskini kabisa hawezi kukosa jiko, vile vile na hili jiwe lilikuwa ni zana ya msingi sana.

Sasa Mungu alikatakaza Jiwe hilo (liwe la juu au la chini) lisiwekwe rehani kwa vyovyote vile, Maana yake kama mtu kamkopesha maskini, hapaswi kukubali rehani iwe jiwe la kusagia, kwasababu endapo Yule maskini kashindwa kulipa mkopo ule, basi jiwe lile la kusagia litachukuliwa na kwenda kuuzwa ili deni lile lilipwe, na hivyo Yule maskini atabaki hana hilo jiwe, na hivyo atashindwa kusaga nafaka zake kwaajili ya chakula chake cha kila siku, hata nafaka zile chache ambazo atazipata katika shamba lake, atashindwa kuzisaga kama riziki, na hivyo anaweza kufa kwa njaa.

Lakini rehani ya vitu vingine kama vyombo, au mashaba iliruhusiwa, kwasababu mtu angeweza kuishi bila hivyo vitu,  lakini si bila jiwe hilo la kusagia.

Jambo hilo linatufunza nini?

Tunajifunza kuwa na huruma kwa watu wa hali ya chini, Ni vizuri kutoa mkopo lakini si kila mkopo ni lazima tupate rehani, mikopo mingine tunaweza kuitoa tu bila kumweka mtu rehani, (hususani kwa wale watu ambao ni hali ya chini sana kiuchumi), hiyo itaonyesha upendo wetu na wema kwa watu na hata kuwafanya wavutiwe na imani yetu na kumfuata Mungu wetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JIWE LILILO HAI.

JIWE LA KUSAGIA

Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika..

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

LIONDOE JIWE.

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni kweli wanafunzi wa Yesu walikuwa hawanawi mikono?

Swali: Je ni kweli Bwana Yesu mwenyewe na wanafunzi wake walikuwa hanawi mikono kabla ya kula?..kulingana na Mathayo 15:2, na Luka 11:37

Jibu: Turejee,

Mathayo 15:1 “Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema

2 Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula”

Tusome tena, Luka 11:37..

Luka 11:37  “Alipokuwa akinena, Farisayo mmoja alimwita aje kwake ale chakula; akaingia, akaketi chakulani.

38  Farisayo huyo alipomwona, alistaajabu kwa sababu hakunawa kabla ya chakula”.

Je ni kweli Bwana Yesu na wanafunzi wake walikuwa hawanawi mikono kabla ya kula kulingana na mistari hiyo?

Jibu ni la! Bwana Yesu na wanafunzi wake walikuwa wananawa mikono kabla ya kula, huo ni usafi wa kawaida tu ambao kila mtu anao.

Hauwezi kutoka kushika mavumbi halafu uanze kula hivyo hivyo, labda uwe hauna akili timamu. Na Bwana pamoja na wanafunzi wake walikuwa ni watu wenye akili timamu, kama Bwana aliweza kuwaosha wanafunzi wake miguu kunawa mikono ni nini kwake? (Yohana 13:9-10).

Sasa swali kama Bwana na wanafunzi walikuwa wananawa mikono, kwanini Mafarisayo na Masadukayo waseme alikuwa hanawi?

Jibu ni kwamba Mafarisayo walikuwa wanafuata desturi za wazee, ambao kulingana na sheria ilikuwa kabla ya kula ni lazima mtu aoshe mikono mpaka kwenye kiwiko!.. Jambo ambalo halikufanywa na wanafunzi wa Yesu wala Bwana Yesu mwenyewe… kwani Bwana na wanafunzi wake walikuwa wananawa tu kawaida, bila kufikisha maji kwenye viwiko.

Marko 7:2  “wakaona wengine katika wanafunzi wake wakila vyakula kwa mikono najisi, yaani, isiyonawiwa.

3  Kwa maana Mafarisayo na Wayahudi wote wasiponawa mikono mpaka kiwiko, hawali, wakishika mapokeo ya wazee wao”

 Kama tu leo sisi tunavyonawa kabla ya kula, tukitaka kula huwa tunaosha tu viganja, lakini hatuoshi mkono mzima mpaka kwenye kiwiko, hivyo kulingana na desturi za wayahudi, mtu aliyeosha kiganja tu, bila kufika mpaka kwenye kiwiko, mtu huyo anahesabika kama bado hajanawa kabisa.

Hivyo kulingana na desturi hizo za kiyahudi, hata sisi tunaonawa sasa katika viganja tu, mbele zao tunahesabika kuwa  watu wanaokula bila kunawa!. Kwahiyo na Bwana pamoja na wanafunzi wake hawakuwa wananawa hadi kwenye viwiko, ndio maana wakashutumiwa vile, lakini walikuwa wananawa kama tu sisi tunavyonawa sasa.

Na ni kwasababu gani wanafunzi, hawakufuata desturi hizo za wazee za kunawa mpaka kwenye kiwiko?

Bwana Yesu alishatoa sababu kuwa kinachomwingia mtu hakiwezi kumtia unajisi bali kinachomtoka.

Mathayo 15:17  “Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?

18  Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.

19  Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano”

Hivyo na sisi tujihadhari sana na vitu tunavyovitoa katika vinywa vyetu kwasababu vinakuwa vinatoka mwilini, lakini zaidi sana tujitahidi kuwa wasafi kimwili, kwasababu hata Bwana Yesu alikuwa ananawa.

Bwana atubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Biblia inasemaje kuhusu Kazi?

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)

Jibu: Turejee..

Waefeso 5:25  “……kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;

26  ili makusudi alitakase na KULISAFISHA KWA MAJI KATIKA NENO;

27  apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa”..

Siri ya kanisa kutakaswa kwa “Maji” inaanzia pale Msalabani, wakati Yule Askari anamchoma Bwana mkuki ubavuni, biblia inaonyesha kuwa palitoka “Maji na Damu”. Ikifunua kuwa Maji ni lazima yahusike katika hatua za utakaso wetu, ndipo damu ya Yesu iweze kututakasa kabisa. Utauliza tunazidi kulithibitisha vipi hilo? Tusome Matendo 2:37-38

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”

Umeona hapo?.. Anasema tubuni mkabatizwe, mpate ondoleo la dhambi.. kwahiyo kumbe ubatizo unahusika sana katika kusafika utu wa ndani.. maana yake utakaso wa  Damu, unategemea ubatizo wa Maji, ili  Roho Mtakatifu aweze kukaa ndani ya mtu.  

Vitu hivi vitatu vinaenda pamoja (DAMU, MAJI na ROHO Mtakatifu). Huwezi kukichukua kimoja na kukiacha kingine!… Wala kusema kimoja kina umuhimu kuliko kingine… Vyote hivi vitatu vina umuhimu na maandiko yanasema vinapatana katika UMOJA!

1Yohana 5:9  “Kisha wako watatu washuhudiao duniani], ROHO, NA MAJI, NA DAMU; na watatu hawa hupatana kwa habari moja”.

Hiyo ndio sababu pia kwanini tunapaswa tubatizwe!.. Wengi leo wanaupuuzia ubatizo wa maji wanasema hauna umuhimu sana, ubatizo wa Roho Mtakatifu ndio wa muhimu.. Pasipo kujua kuwa Roho, na Maji na Damu vinapatana katika Umoja, ndio maana Bwana Yesu alimwambia Nikodemo kuwa kama hatazaliwa kwa MAJI (maana yake kwa ubatizo wa maji) na kwa ubatizo wa Roho Mtakatifu, hatauona ufalme wa mbinguni, na huko ndiko kuzaliwa mara ya pili.

Maana ya kuzaliwa mara ya pili ni kubatizwa katika maji na katika Roho Mtakatifu.

Yohana 3:4  “Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5  Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa MAJI NA KWA ROHO, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.

6  Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.

7  Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.

Na ubatizo ulio sahihi ni ule wa maji Tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Bwana Yesu (Matendo 2:38, Matendo 8:16, Matendo 10:48 na Matendo 19:5)

Bwana akubariki.

Ikiwa bado hujapata ubatizo sahihi, basi unaweza kuwasiliana nasi, tutakusaidia juu ya hilo, kwa Neema ya Bwana.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

NUNUA MAJI YA UZIMA.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni kweli Isaka alifarijika kwa kifo cha mamaye? (Mwanzo 24:67).

Jibu: Tusome,

Mwanzo 24:67 “Isaka akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake, Sara, akamtwaa Rebeka, akawa mkewe, akampenda; Isaka akafarijika kwa ajili ya kufa kwa mamake”.

Andiko hilo halimaanishi kuwa Isaya alipendezwa na kifo cha mamaye Sara, na hivyo akapata faraja kwa kufa kwake, bali linamaanisha kinyume chake.

Ikumbukwe kuwa Isaka alikuwa ni mwana pekee wa Sara, na Isaka alimpenda sana mama yake, na siku mama yake alipokufa ni wazi kuwa alihuzunika kwa kipindi kirefu,  lakini sasa kipindi anampata Rebeka kama mke wake, ile huzuni ikapungua kwa kiasi kikubwa na akajihisi faraja kama tu ile aliyokuwa anaipata kutoka kwa mama yake.

Ni nini tunajifunza kutoka katika habari hiyo?.

Hapa tunajifunza jinsi mwanamke wa kiMungu anavyopaswa awe!..

Rebeka alikuwa ni mwanamke wa mfano wa kuigwa, kwani aliweza kuwa faraja kwa mume wake kiasi kwamba mume wake akasahau uchungu wote wa kufiwa na mamaye (Maana yake Rebeka alikuwa ni mke kwa Isaka na hapo hapo mama kwa Isaka, kumlea na kumtia moyo). Lakini leo hii wanawake wengi wanafanyika mishale kwa waume zao, na si faraja.

 Mama, dada, binti, msichana kabla ya kwenda kujifunza kwa akina Musa, Eliya, na Danieli, hebu kwanza tenga muda wa kujifunza juu ya wanawake hawa.. Kwasababu tabia ya Musa haitakusaidia sana katika uanawake wako zaidi ya akina Rebeka, au Sara au Mariamu au Ruthu..

Ukitaka kuwa mke bora na mama bora kajifunze kwa akina Hana, Debora, na Tabitha..ukitaka kuwa binti bora nenda kajifunze kwa mashujaa wote wa kike katika biblia kabla ya kuwakimbilia wanaume.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

CHUKI ULIZO NAZO KWA MAADUI ZAKO, SIZO ALIZONAZO MUNGU JUU YAO.

KWANINI KRISTO AFE?

Nilikuwa naomba kujua utofauti kati ya DHAMBI, UOVU na KOSA kibiblia.asante!!

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya kukunguwazwa (Marko 14:27)

Jibu: Tusome,

Marko 14:27  “Yesu akawaambia, Mtakunguwazwa ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika”.

Kukunguwazwa maana yake ni “kuchukizwa”.. Mtu anapokufanya ukasirike au uchukie maana yake amekukunguwaza, biblia imetoa tafsiri ya neno hilo vizuri katika Mathayo 26:30.

Mathayo 26:30  “Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda mlima wa Mizeituni.

31  Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote MTACHUKIZWA kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika”.

Unabii huo alioutoa Bwana ulitimia masaa machache tu mbeleni, pale ambapo kikosi cha Askari wa kirumi kilitokea na kumkamata Bwana Yesu.

Na tunasoma Mitume hawakukifurahia kile kitendo, “WALICHUKIZWA SANA”, hata Petro kufikia hatua ya kutoa upanga na kumkata sikio mtumwa wa kuhani mkuu. Hicho ni kiwango kikubwa sana cha hasira.

Yohana 18:7  “Basi akawauliza tena, Mnamtafuta nani? Wakasema, Yesu Mnazareti.

8  Yesu akajibu, Nimekwisha kuwaambieni ya kwamba ni mimi; basi ikiwa mnanitafuta mimi, waacheni hawa waende zao.

9  Ili litimizwe lile neno alilolisema, Wale ulionipa sikumpoteza hata mmoja wao.

10  Basi Simoni Petro alikuwa na upanga, akaufuta, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio la kuume. Na yule mtumwa jina lake ni Malko”.

Vile vile na sisi tuliompokea Yesu ni lazima tutapitia tu vipindi vya kuchukizwa kwaajili ya Yesu.

Unapofika mahali na kukuta watu wanalikufuru jina la Yesu ni lazima utachukizwa tu!, unapofika mahali na kukuta watu kwa makusudi kabisa wanahubiri injili nyingine tofauti na ile ya kimaandiko ni lazima utachukizwa tu!.

Unapofika mahali na kukuta unatolewa unabii wa uongo, au kweli ya Mungu inapotoshwa kwa makusudi, ni lazima utachukizwa tu!, Unapofikia hatua ya kusumbuliwa kiimani na watu wengine kwasababu tu umeokoka, au umeamua kwenda katika njia sahihi ni lazima tu utakunguwazwa! hata wakati mwingine kufikia kiwango kama kile cha Petro cha kutamani kumdhuru mtu kabisa.

Lakini sisi hatujapewa ruhusa wala amri ya kumdhuru wengine, hata kama ni waovu au wanatutendea maovu, au hata kama wanamtukana Mungu mbele yetu, kazi tuliyopewa ni kuziokoa roho, na si kuziangamiza, kwasababu kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama bali juu ya majeshi ya mapepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

Lakini siku zote fahamu kuwa, ni lazima tu tutapitia vipindi vya kuchukizwa kwaajili ya Yesu, hilo haliepukiki kwa kila aliyezaliwa mara ya pili.

Yohana 15:20 “Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa WALINIUDHI MIMI, WATAWAUDHI NINYI; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kama kuua ni dhambi kwanini Mungu aruhusu mauaji katika Kumbukumbu 13:6-10?

Bwana alisema “Usiue” (Kutoka 20:6) lakini tunaona anawapa wana wa Israeli maagizo ya kuua wale wote wanaoabudu miungu? Je Hii inakaaje? (Kumbukumbu 13:6).

Jibu: Tusome,

Kumbukumbu 13:6 “Atakapokushawishi kwa siri ndugu yako, mwana wa mamaako, au mwana wako, au binti yako, au mke wa kifuani mwako, au rafiki yako aliye kama moyo wako, akikuambia, Twende tukaabudu miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako; 7 katika miungu ya mataifa yaliyo kando-kando yenu karibu nawe au mbali nawe, tokea ncha moja ya dunia hata ncha ya pili ya dunia;8 usimkubalie wala usimsikize; wala jicho lako lisimwonee huruma, wala usimwache, wala usimfiche;9 MWUE KWELI; mkono wako na uwe wa kwanza juu yake katika kumwua, na baadaye mikono ya watu wote.10 NAWE MTUPIE MAWE HATA AFE; kwa kuwa alitaka kukupotoa na Bwana, Mungu wako aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.11 Na Israeli wote watasikia na kuogopa, wasifanye tena uovu mfano wa huo katikati yako”

Ni kweli Mungu alikataza “Kuua” lakini pia kuna mahali pengine aliruhusu “kuua”, sasa ni rahisi kuhisi kuwa biblia inajichanganya, lakini kiuhalisia haijichaganyi.

Katika biblia zilikuwepo sheria za mtu binafsi lakini pia zilikuwepo sheria za Nchi/Taifa. Ikumbukwe kuwa Israeli lilikuwa ni Taifa la kidini, hivyo baadhi ya Amri na sheria zilikuwa ni za kitaifa. Kwahiyo mtu akiivunja sheria Fulani iliyoandikwa kwenye torati basi alikuwa amevunja sheria ya kitaifa.

Ili tuelewe vizuri tuchukue mfano wa mataifa ya sasa, katika mataifa mengi, (karibia yote) kuna sheria ya “kutoua” yaani raia haruhusiwi kumuua mwenzake kwa kosa lolote lile!!, lakini katika Taifa hilo hilo tunaona kuna sheria ya “kunyongwa” endapo mtu akikutwa na hatia iliyo kubwa sana..

Sasa Yule askari aliyetumwa kumweka kitanzi Yule mtuhumiwa, tayari kashafanya tendo la mauaji, lakini kwa kumnyonga Yule mhalifu, bado anakuwa hajavunja sheria ya “kuua”.. Kwasababu yeye kapewa amri ya kuua na mamlaka, lakini haja ua kwa matakwa yake yeye. Lakini kama ingekuwa kajichukulia sheria mkononi ya kuua basi angehesabika ni muuaji, na angekuwa amevunja sheria ya nchi. Na pia Nchi kuweka sheria ya Kuwaua wale waalifu sugu, haijamaanisha kuwa imeruhusu sheria ya watu kuuana huko uraiani.

Vivyo hivyo katika Israeli, Mungu alikataza mtu kujichukulia sheria mkononi za kuua, lakini pia aliruhusu mauaji kwa watu ambao watathibitika kisheria (yaani kitaifa) kuwa wamestahili kifo!.  Na mamlaka hayo aliwapa watu wote, tofauti na sasa ambapo wanapewa tu wale askari walioteuliwa kwa kazi hiyo.

Kwahiyo biblia haijichanganyi, lakini pia tunachoweza kujifunza ni kuwa Lile baya mtu analolifanya litamrudia hata kwa njia nyingine, mtu aliye muuaji naye pia atauawa, mtu anayefanya ubaya ule ubaya utampata na yeye siku za baadae.

Mathayo 26:51  “Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.

52  Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga”.

Soma pia Ufunuo 13:10.

Kwahiyo tujihadhari na dhambi tuwafanyiazo watu au tuzifanyazo mbele za Mungu, kwasababu yale tunayoyafanya tutapata malipo yake hapa hapa, kama ni mema au kama ni mabaya.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

MJUMBE WA AGANO.

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

IMANI NI KUWA NA UHAKIKA WA MAMBO YATARAJIWAYO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kupwelewa maana yake nini? (Matendo 27:26).

Tusome,

Matendo 27:25 “Basi, wanaume, changamkeni; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa.

26 Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja”.

Kupwelewa maana yake ni “kusafiri katika kina kifupi”. Meli au Mashua inaposafiri katika maji yenye kina kifupi, maana yake Meli hiyo au boti hiyo “inapwelewa”.

Katika safari ya Paulo kuelekea Rumi chini ya kikosi cha maaskari, maandiko yanatuonyesha safari ile ilikuwa ni ya misuko-suko mingi baharini, kwasababu wale mahabaria hawakulisikiliza shauri la Paulo ambalo aliwashauri wasing’oe nanga lakini wenyewe hawakusikia hivyo. Mwishowe wakakutana na misuko suko mikuu baharini, mpaka wakakata tamaa ya kuokoka.

Matendo 27:10 “akawaambia, Wanaume, naona kwamba safari hii itakuwa na madhara na hasara nyingi, si ya shehena na merikebu tu, ila na ya maisha yetu pia.
11 Lakini yule akida akawasikiliza nahodha na mwenye merikebu zaidi ya yale aliyoyasema Paulo”.

Wakiwa katika hiyo misukosuko, Paulo alitokewa na Malaika na kuambiwa kuwa hakuna atakayekufa katika safari hiyo, kwani ni lazima Paulo afike salama Rumi ili akalishuhudie Neno la Mungu na kule nako. Na jambo lingine aliloambiwa na Malaika yule ni kwamba Merikebu itapwelewa (yaani itasafiri katika kina kifupi) kando kando ya kisiwa kimoja, mpaka watakapofika kwenye hicho kisiwa.

Na kweli ufunuo huo mahabaria waliuhakiki kwani muda mfupi tu walipoanza kupima kina cha maji waliona kinaanza kupungua kwa jinsi walivyokuwa anaendelea mbele.

Matendo 27:27 “Hata usiku wa kumi na nne ulipofika, tulipokuwa tukichukuliwa huko na huko katika bahari ya Adria, kama usiku wa manane baharia wakadhani ya kuwa wanaikaribia nchi kavu.

28 Wakatupa bildi wakapata pima ishirini, wakaendelea kidogo wakatupa bildi tena, wakapata pima kumi na tano”.

Ni nini tunachoweza kujifunza katika safari hiyo ya Paulo?

1.Mungu atakuwepo na sisi hata katikati ya majaribu
Paulo, alikuwa amefungwa lakini katika kufungwa kwake, bado Mungu alikuwa naye, akimwongoza katika mapito yake, utaona pia wakati akiwa gerezani bado Bwana alikuwa naye, na kila mahali Bwana alikuwa naye, vile vile na sisi tunapokuwa katika majaribu, ambayo tunajua kabisa ni Mungu kayaruhusu basi hatupaswi kuwa na woga wala kukata tamaa, kwasababu Mungu atakuwa Pamoja nasi, na zaidi sana yeye alisema “hawezi kutuacha tujaribiwe kupita tuwezavyo”

2. Wokovu wa Mungu ni hata kwa maadui zetu.

Tunapokuwa katikati ya majaribu ni muhimu kujua kuwa Mungu katuweka pale kwa wokovu wa wengine, Utaona Paulo kafungwa lakini Mungu anamwokoa yeye Pamoja na wale Mabaharia, na wafungwa na watesi wake, anawaokoa na Mauti vile vile na sisi Mungu anapotuweka mahali ni ili tuokoke na wale tulio nao, haijalishi ni maadui zetu au watesi wetu.

Matendo 27:22 “Sasa nawapeni shauri, iweni na moyo mkuu, kwa maana hapana hata nafsi mmoja miongoni mwenu atakayepotea, ila merikebu tu.

23 Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,

24 akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.

25 Basi, wanaume, changamkeni; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa.

26 Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Kaanani ni nchi gani kwasasa?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

Rudi nyumbani

Print this post