Category Archive Uncategorized @sw-tz

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo aliye Bwana na mwokozi wetu. Utukufu na uweza ni vyake milele na milele. AMEN.

Leo tuone ni nini Bwana anasema nasi tena nyuma ya  tukio la Hajiri kijazi wa Sarai alipomtoroka bibi yake..

Kama tuonavyo katika maandiko mateso yalipozidi, alikimbilia jangwani..lakini akiwa kule jangwani, alilia sana  Bwana, amsaidie kwasababu kama tujuavyo jangwani ni mahali ambapo hakuna mahitaji yoyote ya kijamii..ukizingatia na yeye alikuwa mjamzito, hawezi kujihudumia kwa lolote.

Lakini upo uamuzi ambao hajiri aliuchukua ambao kama asingeuchukua kwa wakati ule, haijalishi angemlilia Mungu namna gani asingepata msaada wowote, wala asingeisikia sauti ya Mungu, ilipokuwa inamtafuta kusema naye kule jamgwani..

Na uamuzi wenyewe ulikuwa ni ule wa kukimbilia kwenye CHEMCHEMI YA MAJI. 

Mwanzo 16:6-12

[6]Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake.

[7]MALAIKA WA BWANA AKAMWONA KWENYE CHEMCHEMI YA MAJI katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri.

[8]Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai.

[9]Malaika wa BWANA akamwambia, Rudi kwa bibi yako, ukanyenyekee chini ya mikono yake.

[10]Malaika wa BWANA akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi.

[11]Malaika wa BWANA akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana BWANA amesikia kilio cha mateso yako.

[12]Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.

Ni vizuri tukaona kitu hapo…kumbe malaika alikuwa anamtafuta hamwoni…lakini alipofika katika ile chemchemi ya maji ndipo akamwona Hajiri kisha akazungumza naye na kumpa maagizo.

Hata sasa, watu wengi wanamlilia Mungu kweli awasaidie, wapo katika majangwa ya namna mbalimbali, na Mungu kweli anawasikia, lakini pale ambapo malaika wa Bwana wanatumwa kuwapa majibu yao hawawaoni, kwasababu hawapo katika chemchemi ya maji…wapo kwenginepo.

Na maandiko yanasema Yesu ndiye chemchemi ya maji ya uzima..

Yohana 4:13-14

[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

Ni mara ngapi tunakuwa wepesi wa kumlilia Mungu atusaidie, lakini kumuishi Kristo katika maisha yetu inakuwa ngumu.

Hatuna Muda wa kusoma Neno, hatuna muda wa kuomba, hatuna muda wa kufanya ibada, na kushuhudia habari njema, hatuna muda wa kudumu katika chemchemi ya maji ya uzima..lakini wakati huo huo tunalia Bwana tusaidie! Bwana tutetee! Bwana tubariki!, Bwana tuponye..tukiwa katika biashara zetu, katika kijiwe vyetu, katika mitandao ya kijamii tunachat, katika tv, tunaangalia movie, na tamthilia, katika party na starehe, tunakesha kila mwisho wa wiki, lakini kukesha kanisa mara moja kwa wiki hatuwezi. 

Tusahau kumwona malaika wa Bwana, akileta majibu ya maombi yetu..kwasababu macho yao hayaoni mahali pengine zaidi ya penye chemchemi ya maji ya uzima. Ndivyo walivyoumbwa, Kamwe malaika hawezi kukufuata kwenye kijiwe chako, au kwenye mihangaiko yako, kukupa majibu ya maombi yako. Atakuona tu, pindi uwapo uweponi mwa Kristo, hilo tu!…hawana shughuli na mambo ya ulimwengu huu.

Tumaanishe sasa kumrudia Bwana, kwa mioyo yetu yote..tujifunze kudumu uwepo mwa Kristo, Kuna faida nyingi. Ondoa uvivu wako katika masuala ya wokovu wa Roho yako. Ikiwa utaamka kila siku alafajiri kwenda kazini, kwanini uone uvivu kuhudhuria mikesha na ibada?

Bwana atusaidie…

Je umeokoka? Je! Unatambua ya kuwa tunaishi katika kizazi ambacho kinaweza kushuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa Kristo duniani? Kwasababu dalili zote zimeshatimia. Na kanisa tunaloishi ndio la mwisho lijulikanalo kama Laodikia?

Umejiwekaje tayari, ikiwa upo tayari kumkabidhi Kristo maisha yako. Na unahitaji mwongozo huo, au utapenda kupata ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi 

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

+255693036618/ +254789001312

Bwana akubariki shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WEWE U MUNGU UONAYE.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NUNUA MAJI YA UZIMA.

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Rudi nyumbani

Print this post

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

(1Samweli 23:1-14)

Keila ni moja ya miji midogo  iliyokuwa Israeli, lakini kuna wakati ulipitia taabu kubwa sana ya kuvamiwa na wafilisti, wakateswa wakaibiwa nafaka zao, hivyo wakiwa katika mahangaiko hayo, na mateso hakuna wa kuwasaidia, Maandiko yanatuonesha akatokea Daudi katika maficho yake, alipokuwa anamkimbia Sauli..Akapita katikati ya mji huo,akasikia, kuwa wafilisti wapo huko wanawatesa watu wa Keila.

Lakini Daudi aliguswa sana moyo, hakujali Maisha yake na kuendelea na safari yake ya mafichoni bali alichokifanya ni kukiita kikosi chake kidogo, na kukiambia adhima yake ya kuwasaidia, japokuwa watu wake walikuwa wachache, walijitia nguvu, ndipo Daudi akaenda kumuuliza Mungu, kama akiwapigania watu wa Keila atashinda au hatashinda, Mungu akamwambia, hakika atashinda, akauliza tena na mara nyingine Mungu akamjibu hivyo hivyo kuwa watashinda.

Tengeneza picha, wenyeji wa mtu huyo wanasikia, Shujaa Daudi amekuja kuwasaidia, walifurahi kiasi gani, Na ndivyo ilivyokuwa Daudi akaenda kuwapigania watu hao, akashinda na kurejesha mateka yote, tena  na Zaidi akawarejeshea. 

Wanawake, wazee, vijana wa Keila wakahuika mioyo yao, wakafurahia kuona ng’ombe zao, ngano zao, watumwa wao, mali zao zimerudi.. Waliruka ruka na kucheza, na kumpenda sana Daudi.

Lakini habari mbaya ziliwafikia kwa ghafla watu wa Keila, biblia inasema, Sauli aliyekuwa anamwinda Daudi alipata taarifa kuwa adui yake amefika Keila, kuwasaidia watu wale. Hivyo, akatuma vikosi vyake, kwenda kumkamata. Lakini safari hii sio tena kumtafuta, bali kwenda kuwafuata wakuu wa mji huo, na kuwaambia wamkamate Daudi wamfikishe kwa Sauli ili amuue.

Lakini kabla Sauli hajatuma vikosi vyake, Daudi naye akapata taarifa kuwa Sauli amejua yupo kule, hivyo alichokifanya ni kwenda kumuuliza Mungu kama ilivyokawaida yake, kuhusiana na jambo hilo kama kweli watu wa Keila watamtoa na kumpa Sauli au La..

Matarajio ya Daudi yalikuwa ni hapana, akiamini kuwa wale watu aliowaokoa kwa mkono mkuu, watampa hifadhi watamficha, hawawezi kumsaliti, Lakini Bwana akamwambia Daudi kuwa, hao watu watakutoa kwa Sauli. Hapo Daudi akawa hana jinsi Zaidi ya kuingia tena maporini kwenda kutafuta mahali pa kujificha.

1Samweli 23:7 “Kisha Sauli aliambiwa ya kwamba Daudi amefika Keila. Sauli akasema, Mungu amemtia mkononi mwangu; kwa maana amefungwa ndani, kwa vile alivyoingia katika mji wenye malango na makomeo. 

8 Basi Sauli akawaita watu wote waende vitani, ili waishukie Keila, na kumhusuru Daudi na watu wake.  9 Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera. 

10 Ndipo Daudi akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mimi mtumwa wako nimesikia hakika ya kuwa Sauli anataka kuja huku Keila, ili kuuharibu mji kwa ajili yangu. 

11 Je! Watu wa Keila watanitoa, nitiwe mkononi mwake? Je! Sauli atashuka, kama mtumwa wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, nakusihi, umwambie mtumwa wako. Naye Bwana akamjibu, Atashuka. 

12 Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? Bwana akasema, Watakutia. 

13 Basi Daudi na watu wake, ambao wapata kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda po pote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akaacha kutoka nje. 

14 Basi Daudi alikuwa akikaa nyikani ngomeni, akakaa katika nchi ya milima milima kwenye nyika ya Zifu. Naye Sauli alikuwa akimtafuta kila siku, lakini Mungu hakumtia mikononi mwake.”

Maana yake ni nini habari hii?

Wenyeji waliona ni heri mmoja wao aangamie lakini mji wote upone mikononi mwa jeshi la Sauli. Hawakujali msaada mkubwa aliowapatia, wakamwogopa mtu ambaye hakuwajali hata kidogo walipokuwa katika mateso yao. Mfano Dhahiri wa watu wa kipindi kile cha Bwana Yesu.. 

Hawakujali miujiza waliyotendewa, hawakujali wafu waliofufuliwa, pepo waliotolewa, vipofu walioona, habari njema za faraja zilizohubiriwa na Yesu, Watoto wao walioponywa. Lakini Waliposikia tu kuna hatari ya Herode kuja kuwaangamiza.. Wakasema ni heri Mmoja afe ili taifa zima lisiangamie.

Yohana 11:47  “Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi.

48  Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu.

49  Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;

50  wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima”

Wakamsulibisha mwokozi wao.. Hata Sasa hatushangai kuona, watu wakimfurahia Kristo anapowasaidia tu nyakati za mateso yao, anapowabariki, anapowalinda, anapowaponya.. Lakini ikija tu tufani ndogo ya ibilisi kwa ajili ya Kristo, tayari wanamsaliti, wanautupilia mbali wokovu, akiambiwa anafukuzwa kazi kisa Yesu wake, anasahau, mema yote aliyofanyiwa na Bwana siku zote za Maisha yake. Anamwacha. Akiona umri umeenda haolewi, anasema huku kuvaa magauni ya nini tena, ngoja nivae vimini nitembee nusu uchi, ili nipate mchumba.

Tusiwe kama watu Keila, ambao walimsaliti shujaa wao kisa mtu asiyewajali, tusimwache Yesu kisa vitisho vya shetani vidogo vinavyopita mbeleni yetu. Kisa wazazi hawapendezwi na Imani yetu. Tukumbuke yeye ndio jemedari wetu, kama alitupigania vipindi vya nyuma atatupigania hata sasa.

Tumpende Bwana Mungu wetu kwa mioyo yetu yote, kwa nguvu zetu zote, kwa roho zetu zote, na kwa akili zetu zote.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Naivera ni nini? Kwanini Daudi aliihitaji alipomtafuta Mungu?

Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

Haya ni Mafundisho maalumu kwa ajili ya wanawake..

JIBU: Ni vema kujua mfungo ni nini na madhumuni yake ni yapi.

Mfungo ni kitendo cha kujizuia kufanya jambo fulani la lazima kwa kipindi fulani kwa lengo la kumkaribia Mungu zaidi..

Kwamfano mfungo hasaa hulenga kujizuia kula au kunywa , wengine huzuia usingizi, wengine kazi, wengine mawasiliano n.k. inategemea unalenga nini.

Hivyo pale unapojizuia kula au kunywa lengo lako ni upate utulivu wa kuwa karibu zaidi na Mungu katika maombi na kumtafakari.

Kwahiyo kwa jinsi unavyojiweka mbali zaidi na masuala ya mwili ndivyo unavyoupa zaidi mfungo wako nguvu.

Hivyo tukirudi katika swali je tunaruhisiwa kushiriki tendo la ndoa tuwapo katika mfungo? 

Jibu ni kuwa hakuna katazo lolote..kwasababu shabaha ya mfungo wako lilikuwa katika kujizuia kula au kunywa..

Lakini ikiwa utapenda kuzuia pia tendo la ndoa, ni vizuri lakini hapo ni jambo la makubaliano na mwenzi wako, ikiwa ataliridhia kwa wakati huo msifanye tendo la ndoa, ili mwelekeze fikra zenu zote kwa Bwana…hapana shida. Ni vema.

Lakini ikiwa mmoja wenu hajaridhia, hapo hupaswi kuzuia, kwasababu uolewapo au uoapo, huna amri juu ya mwili wako, isipokuwa mwenzako, kwahiyo akikataa hupaswi kupinga.Ni lazima ufanye.

Biblia inasema..

1 Wakorintho 7:3-5

[3]Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

[4]Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

[5]Msinyimane isipokuwa MMEPATANA kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.

Vilevile ikiwa nyote hamjaridhia…pia bado hakuharibu mfungo wenu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kushiriki tendo la ndoa, ndani ya mfungo, hakubatilishi mfungo wa mtu. Isipokuwa tu maandiko yanatuelekeza  iwe ni kwa kiasi ili mpate na muda wa kusali 

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

Mwanazuoni ni mtu aliyejikita katika utafiti au usomi wa ndani katika tasnia Fulani, lengo lake likiwa ni kupata uvumbuzi wa yale magumu yenye utata au yaliyojificha.. Hivyo mwanazuoni wa biblia ni mtu anayeingia ndani kujifunza Biblia, ili kuieleza katika urahisi zaidi au katika ufasaha zaidi  kwa jamii au kutoa majibu ya mambo magumu yaliyo ndani ya biblia.

Mwanazuoni anajitofautisha na mwana-theolojia, kwa namna ya kwamba mwanatheolojia yeye yupo kisomi zaidi, kusoma kanuni na taratibu za kidini, hivyo anapohitimu, anakuwa amepata maarifa yale yale yaliyokwisha kuandaliwa. Lakini mwanazuoni, ni mtu ambaye hafungwi na taratibu, anaweza jitenga, kuchunguza, kusoma kwa ndani na kujua maana ya mambo.

Si kila mwanazuoni lazima apitie vyuo vya biblia.. Mtu akijikita katika kusoma biblia kwa undani na kujua siri nyingi zilizo ndani yake, huyo huitwa pia mwanazuoni.

Vilevile si kila mchungaji ni mwanazuoni. Mchungaji kazi yake ni kulichunga kundi la kulilisha, lakini ni vizuri pia mchungaji yeyote awe mwana-zuoni wa biblia. Kwasababu katika siku hizi za hatari zenye mafundisho mengi potofu, na udanganyifu mwingi wa dini za uongo, kila mmoja wetu hana budi kuwa mwanazuoni(mwanafunzi) wa biblia, ili awasaidie na wale ambao, hawajui kweli ya Neno la Mungu.

Lakini..

Kuna aina mbili za wanazuoni;

  1. Wanazuoni ambao hawana msukumo wa Roho Mtakatifu.
  2. Wanazuoni ambao huvuviwa na Roho Mtakatifu.

Mfano wa hilo kundi la kwanza, ndio wale waandishi na mafarisayo, waliokuwa kipindi cha Bwana Yesu, hawa waliipokea torati kama vitabu vya kidini tu, na kuvikariri, na kutunga hata na taratibu zao nyingine ambazo Mungu hakuwaagiza kabisa.

Walikuwa wanayachunguza maandiko, lakini wanamweka Mungu nyuma, Matokeo yake wakashindwa hata  kumwona Kristo katika kila kipengele cha torati walichosoma, badala ya kumpokea wakampinga..Ndipo hapo Yesu akawaambia..

Yohana 5:39  “Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. 40  Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima”

Lakini kundi la pili la wanazuoni ni lile ambalo lina nia ya kuujua ukweli, na kiu yao ni wokovu na sio mashindano au usomi, mfano wa hawa ni wale watakatifu wa Beroya, ambao tunawasoma katika..

Matendo 17:10  “Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi. 11  Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. 12  Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache”.

Mfano tena wa hawa, ni Nabii Danieli.. ambaye pia biblia inatuonyesha alikuwa ni mtafiti (mwanazuoni) aliyekuwa anasoma sana vitabu, na matokeo yake akagundua hesabu ya miaka ambayo wangekaa Babeli, hivyo akajinyenyekeza mbele za Mungu akaomba dua na rehema, na Mungu akamsikia, na kumfunulia zaidi..

Danieli 9:1 “Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo;  2 katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini”.

Mwingine ni mtume Paulo ambaye mpaka uzee wake alikuwa anasoma vitabu, soma (2Timotheo 4:13), na ndio maana hatushangai  ni kwanini Mungu alimjalia mafunuo mengi namna ile.. mpaka akamuasa na Timotheo naye awe vilevile..

1Timotheo 4:13  “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha”.

Zipo faida nyingi za kila mmoja wetu kuwa mwanazuoni, Kama Apolo asingekuwa mwanafunzi mzuri wa maandiko, asingeweza kuwashinda wayahudi ambao walilisumbua sana kanisa la kwanza kwa imani zao potofu..(Soma Matendo 28:24-28).

Hivyo kuwa mwanazuoni huchangiwa na;  kwanza kwa kuwa na bidii ya kusoma biblia binafsi,  pili kuhudhuria mafundisho ya biblia kanisani, tatu kusoma vitabu mbalimbali vya Kikristo, Nne kusikiliza mafundisho yenye maudhui ya biblia kwenye radio, televisheni na bila shaka, kwenye tovuti kama yetu hii www.wingulamashahidi.org.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyotuhimiza kuwa wasomi/wanafunzi wa biblia..wenye lengo la kujifunza  kumjua Mungu, (lakini sio mfano wa waandishi na mafarisayo, ambao lengo lao lilikuwa ni vyeo na ukubwa, na heshima waonekane wanayajua maandiko mengi, wasomi, wakubwa waogopwe). Lakini tukiwa na kiu ya kujua mapenzi ya Mungu katika maandiko, ni bora kwetu na kwa wengine..

Wakolosai 4:6  “Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.

Mathayo 4: 4  “Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu”.

Yoshua 1:8 “Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Biblia ni nini?USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU

Gombo ni nini?

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Wakati ambapo Israeli inapitia manyanyaso makali kutoka kwa wakaanani kwa miaka 20, mpaka yakawafanya wamlilie Mungu kwa nguvu ili awaokoe..Tunasoma kwenye biblia Mungu alisikia kilio chao akawanyanyulia mwamuzi Debora pamoja na baraka..

Hivyo Mungu akawaagiza wana wa Israeli wapange majeshi, ili wakapigane na adui zao, na hakika Bwana atawashindia..makabila mengi yalikubali kupeleka majeshi yao, lakini yapo makabila mengine hayakutaka kujishughulisha na jambo hilo..na hayo si mengine zaidi ya  Dani, Asheri, na nusu ya kabila la Manase na Gadi. Haya yote yalikuwa mbali kidogo na eneo la vita, Yaliona kama vile vita haviwahusu wao, hivyo yakawa bize kuendelea na mambo yao..

Waamuzi 5:17

[17]Gileadi alikaa ng’ambo ya Yordani, 

Na Dani, mbona alikaa katika merikebu? 

Asheri alikaa kimya penye bandari ya bahari, 

Alikaa katika hori zake.

Kwamfano kama hapo maandiko yanasema Dani alikaa katika merikebu, maana yake ni kuwa alikuwa ni mfanya biashara, aliona kuacha biashara zake za melini, za uchukuzi, na kwenda kujishughulisha na vita, ni upotezaji wa muda, kupigania taifa la Mungu ni kazi kichaa, wacha niendelee na biashara zangu..Na ndivyo hata hayo mataifa mengine yalivyokuwa, yalichowaza ni biashara, na mahangaiko ya hii dunia mpaka Agizo la Mungu likawa halina maana tena kwao, hata utumwa wa taifa lao hawakuuona, mateso na dhihaka taifa lao lilipokuwa linapitia hawakuona kama ni kitu zaidi ya biashara.

Ndipo Debora akaongozwa na Roho kutunga wimbo huo wa kuwashutumu ambao mpaka sasa tunausoma..

Hata sasa, tabia za makabila haya kama Dani zipo miongoni mwa wakristo wengi, ni mara ngapi utamwambia mkristo twende tukashuhudie, kwasababu tumeamuriwa kufanya hivyo na Kristo..lakini atakuambia sina muda, nipo buzy, sina mtu wa kumuacha kwenye biashara yangu…

Anaona biashara yake ni bora kuliko kuokoa roho za watu wanaopotea, huyu ni Dani anayekaa merikebuni..kipaumbele chake ni shughuli za huu ulimwengu, kazi, pesa, ndizo anazozitaabikia kutoka Januari mpaka Disemba, mwaka kwa mwaka, hana rekodi ya kufanya chochote kizuri  kwa ajili ya ufalme wa Mungu, lakini yupo tayari kujenga majumba, na mahoteli, na ma-meli ili kutanua wigo wake wa kibiashara..

Ni kweli Mungu anaweza kuokoa watu wake pasipo wewe, lakini vilevile kumbuka Mungu anaweza kubaki na mbingu yake pasipo wewe..usipokwenda mbinguni hakumpunguzii yeye kitu.

Hatushangai hata ni kwanini hili kabila la Dani halionekani miongoni mwa makabila ya Israeli yatakayookolewa siku za mwisho (Ufunuo 7:1-8). Sababu mojawapo ni hii..Na sisi tujichunguze tutambue kipaumbele chetu kwa kwanza ni kipi. Je siku ile tutakuwa na ujasiri wa kusimama mbele ya Kristo?

Bwana atupe kuliona hili.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?.

NYOTA ZIPOTEAZO.

Kuna tofauti gani kati ya ‘Mungu’ na ‘Mola’?

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?

Rudi nyumbani

Print this post

AKAKIVUNJA KIBWETA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE.

Yesu alipokuwa nyumbani kwa Yule Simoni mkoma, alitokea mwanamke mmoja na kufanya jambo ambalo lilizua malalamika mengi sana kwa wale waliokuwa pale, kama tunavyoifahamu habari, mwanamke Yule alikuwa na kibweta (kijagi), kilichojaa marhamu(pafyumu), na thamani yake ilikuwa ni kubwa sana, ni sawa na pesa za kitanzania, milioni 6, Mshahara wa mwaka wa mtu anayelipwa vizuri.

Lakini maandiko yanatuambia, mwanamke Yule hakufungua tu kile kifuniko cha kibweta ili aimimine pafyumu  kichwani pa Yesu hapana, bali “ alikivunja kabisa”, kwa namna nyingine aliharibifu kijagi hicho, kuonyesha kuwa hii pafyumu haitatumiwa tena sehemu nyingine yoyote, itaishia yote hapa, na hilo ndio lililowafanya wale watu waliokuwa pale walalamike, na kusema upotevu wote huu wa nini?..

Anaimwaga pafyumu yote kama maji, lakini Yule mwanamke hakujali, aliimaliza yote, mpaka nyumba yote ikiwa inanuka pafyumu.

Tusome kidogo..

Marko 14:3  “Naye alipokuwapo Bethania, nyumbani mwa Simoni mkoma, ameketi chakulani, alikuja mwanamke mwenye kibweta cha marhamu ya nardo safi ya thamani nyingi; akakivunja kibweta akaimimina kichwani pake.

4  Palikuwa na watu waliochukizwa katika nafsi zao wakisema, Kwani kupoteza marhamu namna hii? 5  Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa dinari mia tatu na kuzidi, wakapewa maskini. Wakamnung’unikia sana yule mwanamke.

6  Yesu akasema, Mwacheni; mbona mnamtaabisha? Amenitendea kazi njema;7  maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamnami sikuzote.

8  Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu marhamu kwa ajili ya maziko. 9  Amin, nawaambia, Kila ihubiriwapo Injili katika ulimwengu wote, na hili alilotenda huyu litatajwa kwa kumbukumbu lake”

Nachotaka tuone juu ya habari hii, ni kwamba tunaweza kudhani kuwa ni huyu mwanamke tu, ndiye aliyekuwa na kibweta kile cha thamani,..Ukweli ni kwamba wale wote walikuwa na vibweta vyao, isipokuwa tu katika maumbile tofuati.. kuna mahali walivivunja au watavivunja, na kutumia kwa ajili ya vitu watakavyoviona vya thamani..

Hata sasa, kila mmoja wetu anachokibweta chake, ni suala tu la muda.. Utajiuliza, unamtazama msanii Fulani kwenye tv, anamwaga pesa, na kuwapa makahaba, au ananunua gari la kifahari, halafu wewe unaanza kulalamika na kusema upotevu wote huo wa nini, si ni heri angewasaidia maskini, kuliko kutumia kwa anasa.. Usimlaumu kibweta chake ndio amekivunjia hapo.

Leo hii, utaona, mtu kumtolea Mungu, au kusapoti huduma ambazo zinamsaidia kiroho ni ngumu, hata halifikirii.. Lakini mwanawe akitaka kwenda shule, atahangaika kila mahali kumtafutia ada, au akiumwa, anahitaji kwenda kutibiwa India, atauza, gari mpaka shamba, kusudi kwamba aokoe maisha ya mwanawe..Hicho ni kibweta chake amekivunja.

Kuonyesha kuwa kumbe anaweza kupoteza chochote cha thamani kwa ajili ya kitu cha muhimu. Tujiulize, Utasema mimi sina kibweta cha thamani..Ukweli ni kwamba unacho, bado hujaona mahali pa muhimu pa kukimwaga. Wakati utafika tu,.

Tujiulize, vipi kuhusu Mungu wetu..Yesu wetu aliyetuokoa, twaweza kudhubutu kuwa kama huyu mwanamke? Ambaye alikivunjia kwa Bwana?..Hakujua kwa kufanya vile, injili yake itahubiriwa kizazi baada ya kizazi.. Na Yesu ni yeye Yule jana na leo na hata milele.. Kama alimfanyia huyu, anaweza pia akakufanyia na wewe, kwa namna yako..Lakini ni lazima ukivunje kibweta chako kwake..Kumbuka Bwana anasema maskini manao siku zote,..Unafurahi vipi, Bwana akuhudumie, halafu wewe umuhudumii?

Tafakari.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Rudi nyumbani

Print this post

MIGAWANYO MINNE (4), YA HUDUMA YA YESU.

1.) DUNIANI (miaka 33 na nusu)

2) KUZIMU (Siku tatu)

3) MBINGUNI (Miaka elfu mbili na …)

4) DUNIANI TENA (Miaka 1000)

Ni vema tukaifahamu hii migawanyo kwa kina ili tujue huduma ya Bwana wetu Yesu sasa ni ipi kwa watu wake.

1.DUNIANI (miaka 33 na nusu):

 Bwana aliposhuka duniani, aliishi miaka thelathini na tatu na nusu, ndani ya miaka hii alikuwa na lengo la kuwafundisha na  kuwakomboa wanadamu wote kutoka katika laana ya dhambi na mauti. Na siku ile alipokwenda msalabani, ndipo akakamilisha kusudi hili. Ndio pale aliposema IMEKWISHA. Akiwa na maana  kuwa kuanzia huo wakati na kuendekea kila mwanadamu atakayemwamini yeye ni lazima aokolewe.

Kusudi lake la kwanza likawa limekwisha.

2) KUZIMU (Siku tatu):

Kusudi la pili lilikuwa ni kuzimu.  

Pindi tu alipokufa hakwenda mbinguni moja kwa moja bali alishuka kuzimu. Kuzimu ni mahali pa wafu. Hivyo zamani wafu wote waliokuwa wema na waovu, wote walikuwa wapo makaburini, isipokuwa waovu walitengwa mahali pao mbali na wema. Waovu walikuwa katika vifungo vya hukumu. Lakini wema walikuwa sehema salama. 

Sasa Bwana Yesu aliposhuka kuzimu, alifanya huduma kwa makundi yote mawili. Kwamfano lile Kundi la waovu alikwenda kulihubiria makosa yao, ni kwanini wamestahili hukumu, Soma..

1Petro 3:19 “ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;

20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji”.

Maana yake ni kuwa hata sasa, ikiwa utakufa katika dhambi, ni moja kwa moja utakwenda huku wafu hawa walipo ambapo hapana raha, ndio Jehanamu yenyewe iliyopo chini ya dunia.

 Lakini  walio wema Bwana Yesu aliwachukua na kuwafungua kutoka katika vifungo vya kaburi, na kuwahamishia mahali pazuri sana  pajulikanapo kama peponi.

Mathayo 27:50 “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.

51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;

52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;”

Hivyo ikiwa wewe ni mtakatifu ukifa sasa, hutajiona ukishuka makaburini, bali utajiona ukichukuliwa juu, mbinguni. Lakini sio kule Kristo alipokwenda,(huko tutafika baadaye) bali katika mbingu ya katikati, ambayo hiyo utakaa huku ukisubiria ule ukombozi wa miili yetu, Siku ile ya Unyakuo. Ambapo kwa pamoja utaungana na watakatifu walio hai, na moja kwa moja kwenda mbinguni kule Kristo alipo kwenye karama ya mwana-kondoo. Hivyo hudumu hii ya Yesu iliishia pale siku ile alipofufuka.(1Wakorintho 15:51-55)

  1. 3) MBINGUNI (Miaka elfu mbili na …)

Hii ndio huduma ambayo mpaka sasa inaendelea ya mwokozi wetu. Alisema mwenyewe maneno haya..

Yohana 14:1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.

2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.

3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo”.

Mpaka anasema ninakwenda kuwaandalia makao, maana yake ni kuwa hapo kabla sisi hatukuwa na makao yoyote mbinguni. Hivyo makao haya ndio ile Yerusalemu mpya, ambayo itashuka kutoka kwa Mungu mbinguni, baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha.

Haya ni makao ya milele, hivyo hatushangai ni kwanini hadi sasa Bwana anatuandalia. Bwana atusaidie tusiikose ile mbingu mpya na nchi mpya ambayo Yerusalemu mpya ipo ndani yake. Ni makao ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia. Huko tutamashangaa Mungu sana, kwa kipindi kisichokuwa na mwisho.

  • 4) DUNIANI tena (Miaka 1000):

Huu ndio wakati wa ule utawala wa miaka elfu moja, ambao Kristo atakuja kutawala na watakatifu wake, hapa duniani, ndio kule kurudi kwa pili kwa Yesu Duniani, akiwa kama Mfalme wa wafalme, na Bwana wa Mabwana.  Ni wakati wa sabato ya watakatifu wote. Utajiuliza kulikuwa na umuhimu gani Mungu kuipitisha kwanza hii miaka 1000, na sio tuingie moja kwa moja kwenye Yerusalemu yake iliyo ndani ya mbingu mpya na nchi mpya?

Ni kwasababu Bwana anataka kuwahakikishia watu wake kuwa hakuna chochote walichokipoteza pindi walipokuwa wanataabika kwa ajili yake hapa duniani, pindi walipojikana, kwa kuacha kila kitu, na kudharauliwa,.hivyo ili kuwaonyesha hakuna walichokipoteza, atawarudishia hiyo miaka ya raha, na wenyewe watakuwa wafalme na Mabwana duniani. Wakati huo dunia haitakuwa kama hii tena, bali itarejezwa hata zaidi ya Edeni, na amani itakuwepo duniani.(Soma Ufunuo 20:1-4). Watatawala pamojanna Kristo kwa amani na furaha isiyoelezeka.

Ndugu, tukiyaona haya, tunatambua sasa wakati tuliobakiwa nao ni mchache sana. Siku yoyote unyakuo utapitia, mlango wa neema utafungwa, dalili zote zimeshatimia Jiulize Je, umejiandaaje? Au umejiwekaje tayari kumpokea Bwana Yesu. Na hata kama hatarudi wakati wako. Ukifa leo hii, huko uendako utakuwa ni mgeni wa nani?

Yesu yupo mlangoni kurudi, tubu dhambi zako ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako. Hizi ni siku za mwisho. Tunachokisubiri sasa ni unyakuo tu, dalili zote zimeshatimia.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

Je mbinguni itakuwa ni kuimba tu wakati wote?.

KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

Mungu kamwe hajatuweka hapa duniani tutafute “dunia njema”, Dunia ambayo tutaishi mbali na hatari, mbali na majanga, mbali ni watu wabaya au waovu, hapana, hili ni jambo ambalo kila mtu aliyempokea Kristo au aliyeokoka anapaswa alijue, hata tujitahidi vipi kutafuta mahali ambapo patakuwa pazuri kwetu bado hatutapaona…

Kwasababu duniani hii ilishaharibika tangu Adamu alipoasi, na iliendelea kuwa hivyo hivyo, na hata sasa itakuwa hivyo hivyo ya hatari hadi mwisho wake, hakuna  mahali utaenda au utakaa na kusema hapa hakuna ukinzani, hakuna masumbufu.., ni kitendo cha muda tu, ukiyashazoelea hayo mazingira mapya utavumbua shida nyingine nyingi na hatari zilizopo hapo,ambazo kule hukuziona, nenda kote ulimwenguni ndio uhalisia ulivyo..

Kitu Mungu anachokifanya ni kutufanya tuwe salama katika mazingira haya mabaya, lakini sio kubadili mazingira yawe mbingu kwetu. Anachofanya ni kutuandalia meza, tule tunywe, katikati ya watu waovu, katikati ya wachawi, katikati ya waganga, katikati ya wauaji, katikati ya wapagani.. Lakini tusidhuriwe na wao..Na anafanya hivyo ili tumaini letu liwe kwake tu.

Daudi alilijua hilo akasema maneno haya katika Zaburi..

ZABURI 23

1 Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji

5 WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.

Umeona, anasema waandaa meza mbele yangu machoni pa watesi wangu.. Machoni pa wafanyakazi wenzangu wanaonionea wivu, machoni pa wafanya-biashara wenzangu wanaoniendea kwa waganga, machoni pa majirani zangu wanaoniundia visa kila kukicha..Hapo ndipo Mungu anapokuletea chakula chako, anapokuchunga, anapokupa faraja..Kamwe usitazamie atakupeleka mbinguni, kukupa rizki, au Baraka zako.

Usihangaike kumwomba Mungu akubadilishie mazingira akupe mengine, au akubadilishie watu akupe wengine, au akubadilishie majirani, au wafanyakazi, au akuhamishe mahali ulipo akusogeze kwingine kwasababu hapo ulipo ni pabaya sana.. Mungu atakusogeza wakati wake ukifika, lakini fahamu kuwa hata huko uendako, hata hao watu wengine uwakutao, matatizo yanaweza kuzuka hata makubwa kuliko ya kwanza.. Lakini mwombe Bwana katika mazingira yoyote akusaidie,, Hilo linatosha yeye awe mchungaji wako, awe mwamba wako, awe jemedari wako wa vita, ndio maombi anayotaka kuyasikia, na huwa anayajibu upesi, maombi ya namna hii. Mwombe akufanikishe hapo hapo ulipo, akupe amani na faraja hapo hapo ulipo..

Bwana Yesu alimwomba Mungu maneno haya..

Yohana 17:15 “Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu”.

Si mapenzi ya Bwana, wewe ukae mbali na walimwengu, bali katikati yao, mpaka wakati wa Bwana utakapofika ndio akuondoe na kukupeleka pengine.  Wakristo wengi wameathiriwa na mazingira yanayowazunguka, wanapoona hatari nyingi mbele yao au  nyuma yao. Badala waweke tegemeo lao kwa Bwana awasaidie watimize mapenzi ya Mungu, wanabakia kuyalaumu mazingira, wakisema, ni kwasababu ya hiki, ni kwasababu ya kile..Yule ananipiga vita ndio maana sina muda na Mungu..Laiti ningeondoka hapa na kwenda kule ningetumika vizuri zaidi  n.k…

Ndugu, Dunia hii iliyoanguka haina mahali utakuta pana unafuu, zaidi ya pengine, hapatakuwa na wachawi lakini patakuwa na magonjwa, hapatakuwa na magonjwa lakini patakuwa na uzito kiroho, au mwitikio wa watu kwa Mungu ni mdogo, hapatakuwa na maskini lakini patakuwa na majanga,..Hivyo hatari zipo na zitaendelea kuwepo kwasababu mkuu wa ulimwengu huu yupo kote.

Lakini tukiegemea kwa Bwana, na kumlilia yeye atembee nasi, atulinde, atuokoe, atupe amani, atupe faraja,atupiganie, na sio kuyalaumu mazingira, tutakuwa salama.

Wakati Fulani Mungu alinionyesha usiku katika ndoto, nilijikuta nimeingia katika jumba Fulani, lakini sikufahamu kama ni milki ya adui..Hivyo nikiwa kule nikawa kuzungumza na mama mmoja ambayr alikuwa kama kafungwa, lakini ghafla, mahali pale palibadilika,nikaanza kuwaona watu wanaotumiwa na ibilisi ndani ya mazingira yale, nikagundua uwepo wa pale sio wa ki-Mungu, bali ni milki ya ibilisi, basi nikawa natafuta mlango wa kutoka niondoke, lakini milango yote ilikuwa imepotea, basi nikawa nazunguka zunguka kwenye lile jumba lenye mazingira ya kutisha, kutafuta mlango wa kutokea sioni, kila nikiingia kwenye mlango mmoja, nakutana na chumba kingine, nikifungua kile huku nikitazamia ndio mlango wa kutoka nje, ndio kwanza nazama katika vyumba vya ndani zaidi..

Lakini nikiwa huko ndotoni, nikajikuta Napata hisia nyingine, nikasema Bwana ndiye ngome yangu ninahofu ya nini..Nikasema sitahangaika tena kutafuta mlango wa kutokea, nitatulia tuli, niendelee kumwangalia Bwana wangu, nikasema hapa nitatoka tu nisiwe na hofu..Na muda huo huo ghafla , nikawaona wenzangu wakiwa katika chumba kimoja wapo ndani ya hilo jumba, tukakutana wote tukiwa na amani sana kana kwamba pale sio ndani ya jumba la shetani, tukawa tunakula na kunywa, halafu tukaanza kuimba nyimbo nzuri za kumsifu Mungu, nakumbuka mahali pale niliona uwepo mzuri wa Bwana kana kwamba tulikuwa kanisani,

Na ghafla nikashutuka, ndipo Mungu akanifundisha neno hili..

Zaburi 23:5 Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.

6 Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.

Hivyo tuondoe hofu ya watu, tumtazame Bwana. Na yeye atatuokoa.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

Ni miaka mingapi ya njaa Daudi aliyoambiwa achague? Ni miaka 7 au miaka 3?

Rudi nyumbani

Print this post

Karismatiki ni nini?

karismatiki maana yake nini?

Karismatiki ni neno la kiyunani lenye maana ya “Zawadi za neema”.. Au kwa lugha nyepesi zaidi, tunaweza kusema, “vipawa vya neema”. Ambavyo hivyo hutolewa na Roho Mtakatifu mwenyewe na sio mwanadamu. Neno hili utalisikia sana vinywani vya madhahebu mbalimbali ya kikristo.

Ni mkondo ambao ulianza, mwanzoni mwa karne ya ishirini, (1906), kule Azusa Marekani, wakati ambapo dhehebu la Pentekoste lilipoanza. Lililoamini kuwa uthibitisho wa Mungu kuwepo katikati ya watu basi ni kuonekana kwa zile karama za Roho Mtakatifu, ambazo zinazungumziwa katika kitabu cha 1Wakorintho 12.

Kwamba kanisa ili liwe hai, ni sharti vipawa vya Roho kama vile Kunena kwa lugha, kutoa unabii, uponyaji na miujiza, vidhihirike ndani yake. Ikumbukwe kuwa tangu kanisa la kwanza la mitume kupita, vipawa hivi vilionekana kama vimekufa, havipo tena, lakini, viliibuliwa tena na Roho Mtakatifu mwanzoni mwa hiyo karne ya ishirini, ambapo baadhi ya wakristo walikaa chini na kufunga na kumwomba Mungu ajifunue kwa namna hiyo kama ilivyokuwa katika kanisa la kwanza la mitume. Na kweli wakiwa katika maombi hayo, Roho Mtakatifu alishuka, watu wengi wakaanza kunena kwa lugha, na karama mbalimbali kuonekana.

Ni jambo ambalo lilikuwa  gheni, kwa madhehebu mengi makongwe, ambayo yalikuwa tayari yameshajikita katika mifumo ya kidini kwa muda mrefu. Kama vile Katoliki, Lutheran, Angalican, Moravian n.k.

Hivyo basi mvuto  wa vipawa hivi, ulivyoendelea kuwa mkubwa, mpaka kufikia miaka ya 1980, madhehebu mengine mengi yakaanza kurithi mfumo huu wa karismatiki, ikiwemo dhehebu kama Katoliki, ( wakaitwa Karismatiki Katoliki), mengine ni Lutheran, na Anglikana, n.k. ijapokuwa yamekuwa na upishano kati ya wao kwa wao katika mifumo ya imani hii .

Hivyo kwa ufupi tunaweza kusema kanisa lolote linalosisitiza udhihirisho wa vipawa/karama za Roho, kama vile uponyaji, unabii, kunena kwa lugha, huitwa Kanisa la Karismatiki.

Ni nini tunapaswa tufahamu kuhusu vipawa vya Roho(Karismatiki).

Ni kweli kanisa linalokosa vipawa hivi, ni kanisa lililo nusu-mfu, au mfu kabisa. Kwasababu Mungu sio sanamu, ambaye anapokea tu ibada, lakini hatoi vipawa/zawadi kwa watu wake. Hayupo hivyo. Lakini pia ukengeufu mkubwa umeingia na kuvichafua vipawa vya Mungu, ikiwa na maana, kuwa mkristo usipokuwa makini utajikuta unapokea Roho nyingine na sio Yule wa Mungu.

Ni kuwa makini katika siku hizi za mwisho, wimbi kubwa la manabii wa uongo, linazukia huku, mafunuo yasiyo ya ki-Mungu yanaibuka na kuwapoteza watu kutoka huku, matumizi ya visaidizi kama maji, na chumvi za upako, vimewapoteza wengi,..Hivyo kumetokea mvurugano mkubwa sana. Mtu atanena kwa lugha leo, kesho atakwenda kuzini, jiulize ni roho gani ameipokea huyo?

Ni nini tunapaswa tufanye?

Nyakati hizi za mwisho, Tujitahidi sana kuitegemea  BIBLIA kwa kila kitu tunachokitenda, au tunachoongozwa kukifanya, Ikiwa ni karama hakikisha haikinzani na kanuni za msingi za Neno la Mungu, hiyo ndio njia pekee ya kuthibitisha kuwa kipawa hicho ni cha ki-Mungu. Lakini nje ya hapo utapotea. Ikiwa utapokea ufunuo, au unabii, usiupokee tu, ilimradi ni fulani kasema, kisa kaona maono, hakikisha kwanza katika biblia, Je! Ndivyo ilivyo? Au La!. Kwasababu  shetani ameingilia sana mikusanyiko mingi, ajaribu kuiangusha kwa namna hii.

Haiwezekani,  useme mimi nimepokea Roho Mtakatifu, ninanena kwa lugha, ninaimba kwa Roho,  Halafu  anakuacha uendelee kuabudu sanamu la mtakatifu Fulani,sanamu la Mariamu au uombe sala za wafu. Huyu sio Roho Mtakatifu, haijalishi atajiita ni Karismatiki namna gani.

Hivyo ni kuwa makini, tusije pokea roho nyingine isiyokuwa ya Mungu. Hizi ni zama za uovu.

1Yohana 4:1  “Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani”

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti kati ya Kipawa na Karama?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

HATA ILIPOTIMIA SIKU YA PENTEKOSTE.

SEMA KWA LUGHA NYINGINE.

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

Rudi nyumbani

Print this post

Makanda ni nini?

Makanda ni neno lingine la KAPU.

Ambalo hutumika kuhifadhi au kubebea vitu mbalimbali hususani vyakula au nafaka.

Katika biblia Neno hilo utakutana nalo katika vifungu kadha wa kadha, mfano wapo ni hivyo ni hivi; 

Mathayo 15:37

[37]Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa.

Marko 8:8

[8]Wakala, wakashiba, wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba.

Luka 16:6-7

[6]Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.

[7]Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.

Luka 16:5-7

[5]Akawaita wadeni wa bwana wake, kila mmoja; akamwambia wa kwanza, Wawiwani na bwana wangu?

[6]Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.

[7]Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.

Ni nini twapaswa kujua nyuma ya makanda ya mikate waliyoyakusanya wanafunzi wa Yesu ambayo baadaye waliyasahau mpaka wakaanza kulalamikiana na kulaumiana..Hadi Yesu akawakemea..(Marko 8:14-21)

Ni kwamba waliweka mioyo yao katika makapu yao, katika hazina zao, hata waliposahau wakapaniki.

Ni hali iliyopo sasa miongoni mwetu sisi, tuliookolewa. Tunafikiri sana makapu yetu yana nini, kwa miezi 10 mbele, kwa miaka 3 ijayo..na pale tunapopungukiwa hata uhusiano wetu na Mungu unakufa..Lakini Bwana Yesu anatuambia tusiwe wasiwasi, wala tusiyasumbukie hayo..bali tuutafuta kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine atatuzidishia..kwasababu maisha ni zaidi ya chakula.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ila atapewa mara mia sasa,Ndugu wake(Marko 10:30)

JE! UNAMPENDA BWANA?

Mtu akizaa watoto mia, lakini nafsi yake haikushiba mema;

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Rudi nyumbani

Print this post