Katika maisha bila shaka kuna siku ambazo uliwahi kuamka asubuhi na kuona siku yako inakwenda vizuri sana, una furaha, unafanikiwa, au unautulivu, au unapokea taarifa nzuri mahali Fulani, kazini kwako, kwenye familia n,k. Lakini kuna siku ambazo unaamka huoni uzuri wowote, aidha unaumwa, unaudhiwa na watu, unapata hasara kazini, unapokea taarifa za msiba, unaibiwa, unapigwa, unapata ajali Fulani, n.k.
Ukiwa kama mwanadamu, nyakati hizi za raha na masumbufu ni lazima ukumbane nazo, haijalishi utakuwa ni mkamilifu kiasi gani.. Na Mungu ameruhusu iwe hivyo, ili kutaka sisi tukue vema katika hali anayoitaka yeye..
Embu tafakari maandiko haya;
Mhubiri 7:14 “Siku ya kufanikiwa ufurahi, Na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote litakalofuata baada yake”.
Mungu ameyaweka hayo yaende sambamba, kwamba hili lisimuache Yule, wala Yule lisimwache huyu..Haiwezekani kila siku utakayoamka asubuhi tu iwe ya furaha,..au iwe ya huzuni tu..hapana,
Sasa kwanini afanye hivyo?
Sababu zipo tatu (3)
Mungu anapenda kutupa furaha, hivyo zipo nyakati utaburudishwa tu na Mungu, hata kama sio sasa wakati huo utafika tu katika maisha yako. Atakufajiri tu kwa njia zake mwenyewe anazozijua. Atakatiza furaha katika siku Fulani Fulani, au katika kipindi Fulani cha maisha, Hivyo Jifunze kumfurahia Mungu wako wakati unafanikiwa, kwa kumshukuru sana..(Yakobo 5:13)
Sikuzote mtu huwa anafikiri vizuri anapokuwa katika shida au mateso Fulani, anapopitia kuumwa kidogo, analazwa, hapo ndipo anapojitambua kuwa yeye sio kitu, hawezi kutenda jambo lolote kwa nguvu zake, au kwa mafanikio yake, hivyo hiyo inamfanya sikuzote tumaini lake alielekeze kwa Mungu. Kwahiyo basi ujifunze kufikiri sana unapokuwa katika matatizo au masumbufu fulani, kwasababu ndicho Mungu anachokitaka hapo, zidi kuwa mwombaji, jifunze Biblia, kaa uweponi, ukishindwa kulielewa hilo utakuwa ni mtu wa kulaumu laumu, kunung’unika nung’unika ovyo sikuzote uingiapo katika vipindi hivi.(Wakorintho 8:1-10 )
Mungu anataka uhai wetu wote, tuumimine mikononi mwake, anataka kila jambo tunalolifanya tuseme BWANA akipenda, (Yakobo 4:13-16 ), anataka tukiamka asubuhi tumwombe kibali cha siku mpya, tunapomaliza siku tumshukuru..Tunapoanza mwezi mpya tumwombe, tunapomaliza tumshukuru, tunapoongeza umri mwingine wa maisha tupeleke shukrani zetu kwake.
Ndivyo Mungu alivyokusudia tuishi. Ni vizuri tuyatambue haya mapema ili tusiwe watu wa kutokuzielewa njia za Mungu wakati mwingine. Tuendelee kumcha Mungu katika majira tuyapitiayo kwa wakati huo,
Anasema pale mema au mabaya yanapokuja tu ghafla, kwa kutokujua mwenyewe..Hiyo inakupa sababu ya kujinyenyekeza, mbele za Mungu, na kumkabidhi Mungu mambo yako yote. Kwasababu hujui kama kesho utakufa au utaendelea kuishi..Ndio maana pale anasema “ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote litakalofuata baada yake”
Kwa kumalizia tafakari tena maandiko haya;
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. 2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; 3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga; 4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza; 5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia; 6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa; 7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena; 8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani”.
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani”.
Bwana atusaidie.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.
Nyakati za kuburudishwa ni zipi? (Matendo 3:19).
NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?
Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)
Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.
Mego ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Mithali 17:1)
Rudi nyumbani
Print this post
Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima.
Nehemia ni mtu aliyekusudia kutoka katika moyo wake, kwenda kuukarabati ukuta wa Yerusalemu uliokuwa umebomoka, mtu huyu hakuwa nabii, wala kuhani, wala hakujulikana popote, lakini kwa kuguswa kwake moyoni kwa habari alizozisikia kuhusiana na uharibifu ule, aliumia sana, ndipo akajitia nguvu, kumwomba Mungu kibali na baadaye akapewa, na kuweza kwenda Yerusalemu kwa ajili ya kazi hiyo ya kuukarabati. Sasa hatuna muda wa kueleza historia yote, kwa muda wako waweza kusoma habari yake tangu mwanzo hadi mwisho katika kitabu hicho.
Hivyo naamini kwa kuyatazama mapito yake, utapata funzo, hata na wewe ambaye, anataka kuingia katika kazi ya kusimama “mahali palipobomoka” ili upakarabati.
Sasa wakati Nehemia anafika Yerusalemu, ili kuanza operasheni yake ya kuujenga tena ukuta ule, ilimbidi kwanza, atembee, katika malango yote, na sehemu zote za ukuta huo ili atathimini, uharibifu uliotokea, pamoja na nguvu na gharama zitakazotumika kuukarabati tena..
Biblia inatuambia, aliondoka, usiku wakati ambapo watu wamelala, akaanza kuuzunguka ukuta ule wa mji ambao ulikuwa ni mrefu sana, Kuonyesha kuwa mpango bora wa kukarabati kusudi la Mungu, huwa hashirikishwi kila mtu, bali watu wachache sana tena, waaminifu, ambao wanaweza kuchukua mzigo wako..Tusome
Nehemia 2:11 “Basi nikafika Yerusalemu, nikakaa huko muda wa siku tatu.12 Kisha nikaondoka usiku, mimi na watu wachache pamoja nami; wala sikumwambia mtu neno hili alilolitia Mungu wangu moyoni mwangu, nilitende kwa ajili ya Yerusalemu; wala hapakuwa na mnyama pamoja nami, ila mnyama yule niliyempanda mwenyewe”.
Nehemia 2:11 “Basi nikafika Yerusalemu, nikakaa huko muda wa siku tatu.
12 Kisha nikaondoka usiku, mimi na watu wachache pamoja nami; wala sikumwambia mtu neno hili alilolitia Mungu wangu moyoni mwangu, nilitende kwa ajili ya Yerusalemu; wala hapakuwa na mnyama pamoja nami, ila mnyama yule niliyempanda mwenyewe”.
Anaendelea kusema…
13 Nikatoka nje usiku, kwa njia ya lango la bondeni, nikashika njia iendayo kisima cha joka, na lango la jaa; nikazitazama kuta za Yerusalemu, zilizokuwa zimebomoka; na malango yake yameteketezwa kwa moto. 14 Kisha nikaendelea mpaka lango la chemchemi, na ziwa la mfalme; LAKINI HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.15 Kisha nikapanda usiku kando ya kijito, nikautazama ukuta; kisha nikarudi nyuma, nikaingia kwa lango la bondeni, nikarejea hivyo.16 Wala mashehe hawakujua nilikokwenda, wala nilivyotenda; wala sijawaambia Wayahudi, wala makuhani, wala wakuu, wala mashehe, wala watu wengine waliokuwa wakiifanya kazi hiyo. 17 Kisha nikawaambia, Mnaona hali hii dhaifu tuliyo nayo, jinsi Yerusalemu ulivyo hali ya ukiwa, na malango yake yalivyoteketezwa kwa moto; haya! Na tuujenge tena ukuta wa Yerusalemu, ili tusiwe shutumu tena.
13 Nikatoka nje usiku, kwa njia ya lango la bondeni, nikashika njia iendayo kisima cha joka, na lango la jaa; nikazitazama kuta za Yerusalemu, zilizokuwa zimebomoka; na malango yake yameteketezwa kwa moto. 14 Kisha nikaendelea mpaka lango la chemchemi, na ziwa la mfalme; LAKINI HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.
15 Kisha nikapanda usiku kando ya kijito, nikautazama ukuta; kisha nikarudi nyuma, nikaingia kwa lango la bondeni, nikarejea hivyo.
16 Wala mashehe hawakujua nilikokwenda, wala nilivyotenda; wala sijawaambia Wayahudi, wala makuhani, wala wakuu, wala mashehe, wala watu wengine waliokuwa wakiifanya kazi hiyo. 17 Kisha nikawaambia, Mnaona hali hii dhaifu tuliyo nayo, jinsi Yerusalemu ulivyo hali ya ukiwa, na malango yake yalivyoteketezwa kwa moto; haya! Na tuujenge tena ukuta wa Yerusalemu, ili tusiwe shutumu tena.
Hapo mwanzo alipoanza safari,alikuwa na mnyama wake, Ambaye ni farasi/punda.. Mnyama Yule alimsaidia sehemu baadhi tu kufika,na kuona uharibifu uliotokea katika kuta, lakini alifika mahali, ambapo mnyama asingeweza kupita katika penyo zile, bali ni mtu tu! Hapo ndipo ikabidi amwache mnyama Yule, atembee yeye kama yeye, mguu kwa mguu, kutazama sehemu za ukuta, ndogo ndogo, za mafichoni, zilizokuwa zimeharibiwa vibaya sana na maadui zao. Asingefanya hivyo, ukarabati wake ungeishia pale pale punda alipoishia, asingekarabati kote.
Ndipo alipomaliza ziara hiyo, akarejea mjini, na kuwaambia makuhani na wahusika wote, hali ilivyokuwa.
Bwana anasema..
Ezekieli 22:30 “Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu”.
Sikuzote kusimama mahali palipomoboka si rahisi, Mungu anatafuta watu hao mfano wa Nehemia hawaoni,,ni lazima tufahamu kuwa zipo gharama kubwa sana, za kukarabati, waweza kudhani, utakwenda na taasisi, au utakwenda na ushirika, au utakwenda na kiwango Fulani cha pesa kwenye akaunti yako.. Hapana vyote hivyo vinaweza kukusaidia kwa muda tu, bali utafika wakati hivyo vyote havitakusaidia, bali itakubidi usimame wewe kama wewe, kama ni kuomba, kama ni kuhubiri, kama ni kukemea dhambi, kama ni kuanzisha jambo..
Mnyama aliye chini yako, hataweza kuvuka nawe, ndugu zako hawataweza kutembea na wewe,katika maono hayo Mungu aliyokupa juu ya kusudi lake, .. Bali ni wewe kama wewe.
Ilimpasa Nehemia afanye hivi, japokuwa alipitia changamoto nyingi, mpaka mbeleni wakawa wanamdhihaki na kumwambia, ukuta unaoujenga jinsi ulivyo dhaifu, hata mbweha wakipita juu yake utaanguka.(Nehemia 4:3), Lakini hakuvunjika moyo, yeye aliendelea kusimama mpaka mwisho ..
Walipokuwa wanaujenga, mkono mmoja ulishika silaha, na mwingine tofali, waliujenga katika hofu, usiku kucha, Lakini mwishoni ulikamilika, katika utukufu mwingi. Na faida yake ni kwamba hadi sasa tunaisoma habari ya Mtu huyu Nehemia, na kumbukumbu lake lipo hadi leo.(Nehemia 4: 17-23)
Ndugu zipo kuta nyingi sana zilizobomolewa na ibilisi, hadi sasa Bwana anatafuta watu watakaosimama, makanisani kujenga nyumba yake, watakaosimama kwa vijana, kuwaweka kwenye misingi ya imani, watakaosimama kwa familia na watoto kuwafundisha kumcha Bwana. Watakaosimama katika Neno la Mungu, kufundisha injili ya kweli isiyoghoshiwa, na kukemea mafundisho potofu..
Swali ni Je! Sisi tutaweza kusimama na kujenga upya?
Kama ni hivyo basi tuwe tayari hata wakati mwingine kusimama peke yetu, kama Nehemia, pale ambapo hatuona sapoti, uwe ndio wakati wa kusonga mbele, na kuitenda kazi ya Mungu, pale ambapo tunaona vita, na dhihaka, tusife moyo bali uwe ndio tuifanye kazi, usivunjike moyo wala usikate tamaa..Kwasababu Kujenga kuna gharama. Lakini faida zake ni kubwa sana mwishoni.
Shalom.
Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)
Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?
Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?
TIMAZI NI NINI
UFUNUO: Mlango wa 17
Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?
Neno Buruji lina maana gani katika biblia?
SWALI: Naomba kufahamu mstari huu unamaana gani?
Mhubiri 4:4 “Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.
JIBU: Sulemani ni mtu ambaye alipewa na Mungu uwezo wa kutambua hekima ya mambo yote yanayotendeka huku duniani.. Na moja ya jambo ambalo aliliona na kutolea habari zake ni kuhusiana na chanzo cha mafanikio mengi ya watu ni nini?.. Na ndio hapo anasema..
“Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake”.
Kwamba kila utajiri, au kazi za ustadi, yaani nyumba nzuri, magari mazuri, mavazi mazuri, hatua zote za mafanikio, asilimia kubwa hutokana na mtu kupingana na mwenzake, kwa tafsiri iliyo nzuri ni kwamba hutokea mtu kushindana na mwingine..ambacho chanzo chake ni wivu.
Kwamfano, mtu atasema mbona Fulani amenunua gari, mimi sijanunua, ngoja nikakope pesa nifanye kazi juu chini na mimi mwaka huu ninunue la kwangu zuri kuliko lile.. Sasa mtu kama huyu atapata gari kweli, lakini chanzo cha gari lake sio malengo yake, bali ni kwasababu wenzake wanayo magari yeye hana.
Hata mashirika makubwa, kufanikiwa kwao ni kwa mashindano, utaona kampuni moja la simu limetoa ofa hii, kesho lingine linaiga ofa ile ile na zaidi, ili lisipoteze wateja.. Hivyo yamefanikiwa kwa njia hizo hizo, za mashindano.
Tajiri mmoja atashindana na tajiri mwenzake ili awe namba moja, hivyo atafanya kazi kwa bidii usiku kucha, ili asishindwe na mwenzake, watashindana kibidhaa n.k.. Mchungaji mmoja atashindana na mchungaji mwingine kwa wingi wa washirika, au kwa ukubwa wa kanisa,
Sasa hayo yote Sulemani ameyaona na kusema ni ubatili, ni sawa na kujilisha(kuufuata) Upepo. Maana yake ni kuwa mafanikio yanayokuja kutoka katika wivu, au mashindano, hayana afya yoyote kiroho.
Hii inatufundisha nini?
Wafilipi 2:14-15 inasema..
“14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,
15 mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu”
Kama watakatifu, hatupaswi kutafuta kitu chochote kwa kushindana, utasema mwenzangu ana neema kubwa kama ile, ngoja na mimi nikafunge na kuomba nimpite,. Hapana, bali tunapaswa tuishi kwa kumtazama Mungu,kila mmoja katika nafasi yake aliyopewa na Mungu, na kuitendea bidii hiyo, kwasababu kwa kupitia hiyo ndio Mungu atatufanikisha, na sio kwa neema za wengine..
Bwana atubariki.
mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali share na wengine ujumbe huu;
Nini maana ya “Amali” na “Ijara” katika biblia?
Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.
Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?
Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)
Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo Bwana wetu, Karibu tuzidi kuyachambua maandiko;
Mwanadamu anasongwa na mambo mawili pale linapokuja suala la kuamua hatma ya maisha yake ya milele. Je! Atii au apate maarifa kwanza?. Pale Mungu anapomwambia Usizini? Je, asifanye hivyo? Au achunguze kwanza ni nini kipo nyuma ya tendo hilo, ndipo awe huru sasa kuchagua kuzini au kutokuzini?
Ukweli ni kwamba asili ya mwanadamu ni kutaka maarifa kwanza, ya kitu ndipo baadaye atii, Lakini Je! Biblia inatufundisha nini kuhusiana na maamuzi sahihi na Salama ambayo Mungu aliyaweka kwa mwanadamu.
Tukisoma ile habari ya pale bustanini biblia inatuambia,.. Mungu alipanda miti yake, kisha alipomaliza akatoa maagizo kuhusiana nayo akasema..
Mwanzo 2:16 “Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, 17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika”.
Lakini mwanadamu akaona, hayo maelezo ya Bwana Mungu hayajitoshelezi, kwanini atuzuie tusile, hajui kuwa sisi tunataka tupate sababu kwanza, (tupate maarifa), kujua ni nini kwanza kipo nyuma ya mti huo, ndipo tuwe sasa huru kuchagua kuula, au kutoula. Ndipo wao wakauendea na kuula.
Mwanzo 3:4 “Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, 5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya. 6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni MTI WA KUTAMANIKA KWA MAARIFA, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala”.
Lakini walipofanya vile, hawakuvuna chochote, matokeo yake wakajikuta tayari wameshaingia kwenye matatizo ambayo mpaka sasa tunayashiriki, yale maarifa waliyoyategemea kuwafanya wawe bora, yakawa mauti kwao.
Asili yetu sisi wanadamu hatukuumbwa kwenye kupata maarifa kwanza, ndio tuishi, bali kwenye kutii kwanza.. Ndivyo tulivyotengenezwa na Mungu.. Kwamba tukitembea katika kutii tutakuwa salama sikuzote,..hayo mengine yatakuja baadaye. Ndicho alichokifanya Ibrahimu alipoambiwa akamtoe mwanawe sadaka ya kuteketezwa alitii kwanza, hakudadisi na kusema kwanini huyu Mungu atoe maagizo ya kishetani kama haya ya kuua watu, yeye alitii, ndipo akaja kujua sababu baadaye.
Hii ikiwa na maana kuwa,..Kama Yesu katuambia wazinzi wote, na waongo wote, hawataurithi uzima wa milele, bali sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Tunahitaji nini tena, kutafuta uzuri uliopo nyuma ya uzinzi, mpaka tukaujaribu.au kutafuta eneo la kijeografia la jehanamu, tulione ndio tuamini?
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Bwana Yesu anasema.. Yeye ndio njia, na kweli na uzima, mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye (Yohana 14:6), FULL STOP!..Sasa kwanini tutafiti njia zetu wenyewe za kutupa wokovu? Kwanini uishi kwa mitazamo yako, au ya wanadamu, wanaokuambia hakuna mwisho wa dunia, au hakuna maisha baada ya kifo
Katika nyakati hizi za hatari ambazo biblia inazitaja (2Timotheo 3:1), ni lazima “tuongeze maarifa ya kulijua Neno la Mungu, na sio maarifa ya kuyadadisi maneno ya Mungu, kama Adamu na Hawa”..Tutapotea haraka sana, tukiwa watu wa namna hii, kutilia mashaka maneno ya Mungu, kila andiko tunalolisoma, tunasema kwanini iwe hivi, au iwe vile?, kwani kuna shida gani, nikinywa bia yangu na simdhuru mtu? Acha kabisa hayo mawazo ya ibilisi..Utapotea…Wewe tii sasa, sababu utakuja kuzijua mbeleni. Sayansi itakuambia haipo hivyo, ukweli ni huu, mwanadamu wa kwanza alikuwa ni sokwe, uthibitisho umepatikana, hakuna Mungu..Ndugu hapo ndio umepotea kabisa, Kumbatia Neno la Mungu.
Tunapohubiriwa tuache anasa, jambo la kwanza ni kutii, hilo Neno, haijalishi itatugharimu kiasi gani..Tunapohubiriwa tuvae mavazi ya kujisitiri, tuache vimini, tuache rushwa. Tusiulize ulize kwanini..Ni kuweka kando kwanza..Sababu tutakuja kujua huko mbeleni.
Tunusuru roho zetu…Tulipokee Neno la Mungu kama lilivyo.
Bwana atusaidie sana.
Maran Atha.
Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?
Maana ya watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.
AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.
Bilauri ni nini kibiblia?(Ufunuo 21:11,22:1)
TUYATENDE MAMBO YOTE KWA UZURI NA UTARATIBU.
Je mke wa Musa alikuwa ni Mweusi?
SWALI: Naomba kufahamu maana ya huu mstari;
Mithali 17:17 “Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu”.
JIBU: Huu mstari unaeleza rafiki wa kweli anapaswa aweje, pia rafiki ambaye atazidi kuwa kama ndugu anapaswa aweje?
Anasema ‘Rafiki hupenda sikuzote’, Ndio.. hii ni tabia ya rafiki wa kweli, hupenda nyakati zote, ziwe ni nzuri , au ni mbaya, kwamfano, rafiki ambaye siku umemfurahisha anakupenda, lakini siku pia umemuudhi anakupenda, siku umempa anakupenda, lakini siku umemnyima bado anakupenda zaidi. Rafiki ambaye wakati mnawasiliana anakupenda, lakini wakati mlipopotezana kimawasiliano kwa muda mrefu bado anakupenda.
Huyo ndio rafiki wa kweli..
Lakini hapo anaposema “Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu” ..Maana yake ni kuwa Yule ambaye anakuwa na wewe bega kwa bega, katika wakati wa shida zako, na taabu zako, na misiba yako huyo si rafiki tena bali ni ndugu..
Unamwona anakujali, wakati unaugonjwa wa hali ya juu, unamwona, anakushika mkono wakati umefilisika, unamwona unakufariji sana wakati wa msiba wako, unamwona anatafuta kila mbinu, kukusogeza mahali wakati upo katikati ya mateso. Huyo ni rafiki aliyefanyika ndugu.
Kwasababu kama hapo inavyosema ‘ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu’..Maana yake ili mtu aitwe ndugu, ni lazima awe amezaliwa mahususi kwa ajili ya siku za shida zako.
Je! Na sisi tunapoitana ‘ndugu’ na ‘rafiki’ tunatambua wito wetu katika hayo?
Lakini tunamwona mmoja ambaye, ni zaidi ya rafiki, ni pia ni zaidi ya ndugu, ambaye sio tu amekuwa karibu na sisi katika shida zetu, na mateso yetu na hukumu zetu.. Lakini pia aliyatoa maisha yake yote, pamoja na uhai wake, ili kufa kwa ajili yetu.
Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”
Hivyo basi, hatuna budi na sisi kuuthamini upendo mkuu namna hii, kwa kukubali kukombolewa na yeye, ili tuoshwe dhambi zetu. Kumbuka hakuna ukombozi nje ya Yesu Kristo, vilevile hakuna uwezekano wowote wa sisi kumpendeza Mungu kwa matendo yetu wenyewe. Na ndio maana ilimpasa aje, ili atukomboe, kutoka dhambini.
Waebrania 2:3 “sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”;
Ikiwa upo tayari kumkabidhi Bwana Yesu maisha yako, basi waweza wasiliana nasi kwa namba zetu hizi, +255693036618/ +255789001312 kwa ajili ya mwongozo huo, bure, na hakika Bwana atayaokoa maisha yako, na kukufanya kuwa mpya tena.
Bwana akubariki.
RAFIKI MWEMA.
JIRANI YANGU NI NANI?
KAMA VILE UMEME UTOKAVYO MASHARIKI UKAONEKANA HATA MAGHARIBI.
Mretemu ni mti gani?
Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?
Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?
Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Nakukaribisha tena tuzidi kuyatafakari maandiko.
Moja ya mambo ambayo, yalimuhuzunisha sana Bwana Yesu ni pale alipowatazama watu wake na kuwaona wanafanana na kundi la kondoo wafugwao waliopoteza tumaini kabisa na kutawanyika, kila mmoja mahali pake anapopajua yeye..Ina huzunisha sana..
Embu Tusome; kwa utulivu habari hiyo;
Mathayo 9:35-36
[35]Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. [36]Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa WAMECHOKA na KUTAWANYIKA kama kondoo wasio na mchungaji.
[35]Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.
[36]Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa WAMECHOKA na KUTAWANYIKA kama kondoo wasio na mchungaji.
Hapo biblia inasema walikuwa WAMECHOKA..na KUTAWANYIKA.
Kuchoka kunakozumgumziwa hapo, sio tu kule kwa kutembea umbali mrefu, katika kutafuta chakula / maji…hiyo ni sehemu ya kwanza..Bali kuchoka kunakolengwa hapo hasaa kunakuja kutokana na kukandamizwa, kujeruhiwa, na kufukuzwa, kutishwa..pamoja na hofu na wasiwasi wa mashaka ya kuraruliwa na mbwa mwitu wakali.
Hii ndio hali halisi yasasa.. Watu wa Mungu WAMECHOKA. Sio kidogo bali wamechoka kwelikweli, Kutokana na kudanyanywa, kuumizwa na watumishi wa uongo, wameharibiwa, wametawanywa.., manabii wa uongo wamechukuliwa fedha zao wakiwaahidia kubarikiwa na kufunguliwa, lakini mwisho wa siku wanajikuta wapo katika matatizo zaidi, wanahangaika huku na kule kutafuta msaada wa kumkaribia Mungu, lakini hawauoni,
badala wapewe tiba ya Neno la Mungu wanapewa maji ya upako, wanafika makanisani badala wahubiriwe Yesu, wanahubiriwa bikira Mariamu na watakatifu wa kale, na sala za wafu, badala wahubiriwe neema iliyo katika Kristo Yesu, wanahubiriwa siri zilizo ndani ya wachawi.
Imefikia hatua watu wamekata tamaa kabisa, kila mmoja anaona ni heri, asiamini kanisa lolote, ajisalie tu peke yake nyumbani..kuliko kwenda na kusikiliza madanganyo. Ni ni mbaya sana..
Ndio jambo ambalo Bwana Yesu analiona sasa hivi ulimwenguni..na kulihurumia kundi lake jinsi lilivyotawanyika…na kuonewa sana..
Ikiwa wewe ni mhubiri, halafu hutimizi wajibu wako wa kuwaongoza watu katika njia sahihi..ujue kuwa utawajibishwa siku ile mbele za Bwana.
Kama tunaigeuza kazi ya Mungu biashara, hatujali maisha ya kiroho ya watu wa Mungu, hata wakija watakavyo kanisani tunaona ni sawa, …tufahamu kuwa tutawajibishwa na Bwana siku ile.
Yeremia 23:1-4
[1]Ole wao wachungaji, wanaoharibu kondoo za malisho yangu na kuwatawanya! Asema BWANA. [2]Kwa sababu hiyo BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, juu ya wachungaji wanaowalisha watu wangu, Mmetawanya kundi langu, na kuwafukuza, wala hamkwenda kuwatazama; angalieni, nitawapatiliza uovu wa matendo yenu, asema BWANA. [3]Nami nitakusanya mabaki ya kundi langu, katika nchi zile zote nilizowafukuza, nami nitawaleta tena mazizini mwao; nao watazaa na kuongezeka. [4]Nami nitaweka juu yao wachungaji watakaowalisha; wala hawataona hofu tena, wala kufadhaika, wala hatapotea hata mmoja wao, asema BWANA.
[1]Ole wao wachungaji, wanaoharibu kondoo za malisho yangu na kuwatawanya! Asema BWANA.
[2]Kwa sababu hiyo BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, juu ya wachungaji wanaowalisha watu wangu, Mmetawanya kundi langu, na kuwafukuza, wala hamkwenda kuwatazama; angalieni, nitawapatiliza uovu wa matendo yenu, asema BWANA.
[3]Nami nitakusanya mabaki ya kundi langu, katika nchi zile zote nilizowafukuza, nami nitawaleta tena mazizini mwao; nao watazaa na kuongezeka.
[4]Nami nitaweka juu yao wachungaji watakaowalisha; wala hawataona hofu tena, wala kufadhaika, wala hatapotea hata mmoja wao, asema BWANA.
Tujiulize, sisi tunaosema tumeitwa kumtumikia Bwana.. Ni utumishi gani tunaoufanya? Tunadhani watu wa Mungu watapotezwa sikuzote?
Mungu anajua kuwakusanya watu wake. Na atawanyanyulia watumishi waaminifu. Sawasawa na Neno lake. Lakini sisi wengine tutawajibishwa.
Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).
JE! UNAMPENDA BWANA?
USIYADHARAU MARUDIA YA BWANA.
“Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika”,Maana yake nini?
NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?
HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.
Kwa tafsiri za kidunia mtu asiye na akili ni mtu ambaye hawezi kufiriki, kuelewa, kuwasiliana, kupanga au kutatua matatizo. Hivyo, mwanadamu mwenye mtindio wa ubongo, anajulikana kama hana akili, mtu anayefeli darasani, anajulikana kama hana akili, mtu anayeshindwa na wenzake katika maisha anajulikana pia kama asiye na akili.
Lakini je! Biblia nayo inasemaje kuhusiana na mtu asiye na akili. Sifa zake ni zipi.
Zifuatazo ndizo sifa za mtu asiye na akili mbele za Mungu, ikiwa wewe unayo mojawapo au zote, basi fahamu huna akili, haijalishi utakuwa ni wa kwanza, kimaisha, au kielimu, au kicheo. Mungu anakuona unao mtindio wa ubongo, hujakamilika. Na matokeo yake utashindwa kutumia akili zako zote kumpenda yeye kama alivyotupa maagizo katika ‘Mathayo 22:37’
Zaburi 14:2 “Toka mbinguni Bwana aliwachungulia wanadamu, Aone kama yuko mtu mwenye akili, Amtafutaye Mungu. 3 Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja, Hakuna atendaye mema, La! Hata mmoja”.
Ukishaona Mungu hana umuhimu kwako, ni uthibitisho tosha,akili zako zimepunguka kwa kiasi kikubwa mno. Ni sawa, na mbwa asiyemjua bwana wake anayemfuga siku zote. Au mtoto asiyemtambua mama yake amnyonyeshaye kila siku. Fanya bidii kumtafuta Muumba wako, kwasababu hilo ndio jaribio la kwanza alilotuumbia Mungu, ili kuthibitisha kwamba kweli sisi ni wanadamu tuliokamilika, tunaweza kumtafuta aliyetubuni.?
Mithali 11:12 “Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza”.
Ukishajiona wewe ni bora kuliko mtu mwingine, au unamwona mwenzako hana lolote jipya la kukufaa wewe, tambua kuwa tayari akili yako imeathirika, fanya haraka sana, kujirekebisha katika eneo hilo, ili usipoteze upeo wako wa kufikiri vema, na wa kupambanua mambo. Kamwe usimdharau mtu yeyote duniani. Hata kama ni mpumbavu wa mwisho.. Kwasababu Mungu naye hamdharau mtu aliyemuumba japokuwa ni mnyonge (Ayubu 36:5)
Mithali 28:16 “Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana; Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake”.
Kumuonea mtu kwasababu ya unyonge wake, au udhaifu wake, ni jambo la hatari sana. Ukimdhulumu mwenzako, au kumnyima haki yake, au kutumia hila kumwibia kisa tu hana maarifa ya jambo hilo, kumpiga mkeo, au watoto bila sababu, basi fahamu kuwa wewe ni sawa ni mjinga mbele za Mungu.. Tukae mbali na uonevu wa aina yoyote.
Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.
Uzinzi, ni kipingamizi sio tu cha kiroho, bali pia cha kiakili. Watu wazinzi, wanajiharibia sana uwezo wao wa kupambanua mambo ya kiroho kwa sehemu kubwa sana. Kwasababu Roho Mtakatifu huwa anategemea miili yetu kutenda kazi, hivyo mwili wako unapochafuliwa, hawezi kupata nafasi ya kuwa mwalimu wako. Ndio hapo Unabaki tu kuwa wewe kama wewe, kama mnyama tu. Epuka uzinzi kwa gharama zote, ni hatari..
Mithali 15:24 “Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini”.
Hapo biblia inatueleza wazi, mtu mwenye akili, huwaza ni jinsi gani atakavyoepukana na kuzimu iliyo chini, huwaza kwenda mbinguni, huwaza kuepukana na ziwa la moto. Lakini kinyume chake ni kweli, mtu asiyewaza hatma ya maisha yake baada ya kufa itakuwaje, badala yake yupo tu, anachowaza ni ajengeje magorofa hapa duniani, ukimweleza habari za kuzimu hata hashtuki, huyo kwa Bwana hana akili.
Mithali 10:8 “Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka”
Ukiwa ni mtu wa kupinga maagizo mema, unayopewa, bali unajiona upo sawa machoni pako mwenyewe, ukielezwa, uvaaji vimini ni dhambi, unasema hatupo agano la kale, unapoelezwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ni lazima, unasema sisi hatuamini hilo. Ujue kuwa unajiangamiza mwenyewe. Kila agizo lililo kwenye Neno la Mungu linapaswa lipokelewe na kukubaliwa kama lilivyo pasipo kuuliza uliza.
Mithali 10:14 “Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa; Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu”.
Ukiwa mtu wa kutozingatia, au kutotendea kazi kile unachoambiwa au kukisikia, kuhusiana na mafundisho ya adili, yaani unasahau sahau, amri au fadhili za Mungu, unakuwa mwepesi kuanguka ovyo katika dhambi, ni uthibitisho kuwa huna akili kwa mujibu wa kibiblia. Tunapaswa tuwe watu wa kuzitafakari sheria za Mungu wakati wote, kama vile mwanafunzi akaririvyo kila siku masomo yake, ili yamsaidie kufaulu mitihani yake ya mwisho.
Mithali 3:3 “Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako. 4 Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu”.
Mithali 3:3 “Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
4 Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu”.
Mithali 24:30 “Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili. 31 Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake”.
Mithali 24:30 “Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.
31 Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake”.
Ukiwa mvivu, wa kufanya kazi ya Mungu. Bwana anasema huna akili, yaani Ikiwa hujishughulishi na chochote, unajitafutia matitizo yako mwenyewe. Tumeumbwa, tujishughulishe, kama Mungu alivyojishughulisha..Kama huwezi mtumikia Bwana kwa kujitoa kwa asilimia zote kwenye kazi yake, ni lazima ufanye kazi ya mikono, ili ufanikiwe. Lakini tukishindwa kujishughulisha, ni kwa hasara yetu wenyewe.
Hivyo tukiwa tuna mojawapo ya tabia hizo ni busara tukazidhibiti ndani yetu. Ili tuweze kuishi kwa akili Bwana anazotaka tuwe nazo.
Zingatia: Mungu anazungumza na mtu mwenye akili timamu, rohoni. Ni lazima tufikie hapo ili Bwana aseme na sisi.
Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)
Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?
Watu wenye ulemavu wa akili, wataenda mbinguni?
Nini maana ya ‘Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma’?
HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.
NI NINI BWANA ANATAZAMIA KILA TUNAPOSHIRIKI MEZA YAKE.
Mume: Kumpenda mke wake Kama mwili wake mwenyewe, ( Waefeso 5:25): Ikiwemo kumuhudumia kiafya, kimavazi, kimalazi, na kiroho.
Mke: Kumtii Mume wake: Kumsikiliza, kumuheshimu, kukubali kuongozwa. (Waefeso 5:22).
Wote: Haki ya ndoa. (1Wakorintho 7:5)
Lakini ikitokea mmoja, ameshindwa kusimama katika nafasi yake, labda tuseme, mume hamjali mkewe, anampiga, anatoka nje ya ndoa, anamtukana, hamtimizii majukumu yake ya kimwili na watoto wake. Afanyaje?
Au mke hamweshimu mume wake, anamdharau, anafanya ukahaba, anamzungumzia vibaya kwa watu wa nje, anajiamulia mambo yake mwenyewe pasipo kumshirikisha mumewe..afanyaje?
Je! na yeye aache kutimiza wajibu wake?
Jibu ni hapana: Embu wazia hili jambo; Ulishawahi kuishi katika nyumba ya kupanga, ambapo mnajikuta wapangaji mpo 10 mnashea umeme au maji, na kila mwisho wa mwezi bili inakuja, na mnapaswa muigawanye sawa sawa kwa kila mmoja wenu. Kwa kawaida hapo panakuwa na ukinzani mkubwa, kwasababu wapo wengine watasema, mimi sina matumizi mengi kama ya Yule.. Na hiyo inapelekea mwingine kujiongezea matumizi yake kwa makusudi ilimradi tu afanane na wale wengine, labda atufungulia bomba la maji ili yamwagike, ili mwisho wa mwezi utakapofika alipe sawasawa na matumizi ya wale wengine.
Lakini hajui kuwa anajiumiza yeye mwenyewe na wale wenzake, kwasababu anapoongeza matumizi ndipo gharama inapokuja juu zaidi, atalipa zaidi ya mwanzo. Ni heri angebakia vilevile akubali kuumia yeye, ili wote wapone.
Ndivyo ilivyo katika ndoa ikiwa mmoja hatimizi wajibu wake wa kindoa, suluhisho sio mwingine kujibu mapigo, bali ni kuendelea hivyo hivyo katika nafasi yake. Ili kuinusuru ndoa. Kama mwanaume hakupendi, wewe mtii, mweshimu, msikilize, kama mwanamke hakutii, wewe mpende, mpe haki yake, ..
Biblia inasema; .. 1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu”.
Inaendelea kusema;
1Wakorintho 7:16 “Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?
Haijalishi itachukua miaka mingapi. Kuwa mvumilivu, timizia wajibu kwao. Hayo mengine mwachie Mungu.
Mithali 25:21 “Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa; 22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na Bwana atakupa thawabu.
Hili andiko linaingia pia kwa wanandoa. Wakati unaona kama wewe unaonewa, hujui kuwa Yule mwingine anateswa rohoni anapoona hurudishi mapigo, hilo jambo linakuwa ni moto mkubwa ndani yake, na sikumoja tu, atakuja kwa machozi, na kutubu mbele zako. Ni kitendo cha muda.
Unapoumizwa, usidhani kuwa Mungu haoni, lakini unapomwachia Mungu yote, basi yeye peke yake ndiye atakayeshughulika kutafuta njia ya kutatua hilo tatizo. Kiboko cha Mungu kitapita, kitamnyoosha. Hivyo unapaswa uwe mtulivu, simama katika nafasi yako. Bwana atamtengeneza yeye mweyewe.. au atatengeneza njia kwa namna nyingine. Hivyo dumu katika utakatifu.
Warumi 12:17 “Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.18 Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana”.
Warumi 12:17 “Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.
18 Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.
19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana”.
Zingatia hayo, usirejeshe ubaya kwa mwanandoa mwanzako.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?
MJUE SANA YESU KRISTO.
REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.
NDOA NA HARUSI TAKATIFU.
VIJANA NA MAHUSIANO.
Kwanini Bwana Yesu alie machozi, na ilihali yeye ni Mungu?
MAFUNDISHO MAALUMU KWA WANA-NDOA; FAMILIA TAKATIFU: Marimu na Yusufu.
Karibu katika mwendelezo ya Masomo ya wanandoa . Ikiwa wewe ni mwanandoa au unajiandaa kuingia katika ndoa, basi masomo haya ni muhimu sana kwako kuyajua.
Tulishatazama, huko nyuma jinsi ndoa ya kwanza ya wazazi wetu Adamu na Hawa ilivyokuwa, na changamoto walizokutana nazo, na jinsi walivyoweza kukabiliana nazo. Ikiwa hukupata masomo hayo, basi utatumia ujumbe inbox tukutumie.
Leo tutatazama familia nyingine takatifu. Ambayo ni ya Yusufu na Mariamu. Yapo mambo mengi sana ya kujifunza, juu ya wanandoa hawa, Na ndio maana kwanini Mungu alikusudia mwokozi wa ulimwengu aje kwa kupitia watu hawa, Ni Kwasababu kuna mengi ya kujifunza kwao. Tutaona pia utaratibu Mungu aliowawekea katika kutimiza kusudi lake hapa duniani.
Alikuwa ni mtu aliyeepuka madhara kwa wengine: Yusufu hakuwa kama Samsoni, ambaye alipoona mwanamke aliyemchumbia amepewa rafiki yake, akakasirika, na kwenda kuchukua mbweha mia tatu, na kuwapeleka kwenye shamba la ngano la wafilisti, kuyateketeza ili ajilipizie kisasi (Waamuzi 15:1-20).
Lakini Yusufu hakuwa hivyo, yeye alipoona binti aliyemchumbua ana mimba, alitafuta njia ya kuepusha madhara kwa dada huyo, hivyo akakusudia ‘’kutomuabisha’’. Akapanga mipango yake ya kumuacha kwa siri,..huenda alipoulizwa vipi mbona humwoi msichana huyu, akawa anasema bado sijafikia muafaka, nitawapa majibu.
Mathayo 1:18 “Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.19 Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri”.
Mathayo 1:18 “Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
19 Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri”.
Sasa Ikiwa alikuwa na hofu ya kumwaibisha asipigwe mawe, unatazamia vipi mtu kama huyu, angeweza kumpiga mke wake hata baada ya ndoa , au awe anatoa siri za madhaifu ya mke wake kwa watu wa nje?
Mwanamke anapoteleza, sio lazima wakati wote upeleke taarifa kwa jamii, aaibike au umpige, au umfukuze, bali ni kumvumilia, kwasababu mengine yanatokea kwa sababu ambazo utakuja kuzijua mbeleni. Tabia hii alikuwa nayo Baba-wa-Yesu (kimwili)
Alikuwa ni bikira: Ni binti ambaye alijitunza tangu anazaliwa mpaka anakuwa mwanamke, Na hiyo ikapelekea kupata neema ya kuchumbiwa na mzao wa Daudi (Yusufu). Kumbuka ahadi ya kuzaliwa Kristo haikuwa kwa Mariamu, bali ilikuwa kwa uzao wa Daudi. Hivyo Mungu alipomuona Mariamu, na ukamilifu wake katika mwili ndipo akasema huyu anafaa kupata neema ya kukutana na Yusufu atimize kusudi la Mungu.
Maana yake ni nini, upo umuhimu sana, wa msichana kujitunza sana mwili wake, kwani hiyo itakupelekea kupata mwanaume bora, na uzao bora. Ni kweli si wote wataingia katika ndoa wakiwa bikira, lakini ikiwa umetambua sasa, wajibu wako, na umeokoka, huna budi kujitunza sana, na hata baada ya ndoa, ili hicho kitakachotoka tumboni mwako kiwe kitakatifu.
SASA BAADA YA KUONA SIFA HIZI KUU (2), WALIZOKUWA NAZO HAWA WANANDOA, TUONE UTARATIBU WA KIMAJUKUMU JINSI MUNGU ALIVYOUGAWANYA KWAO.
Malaika Gabrieli alitumwa kwa Mariamu, ili kumpa taarifa ya kupata mimba kwa uweza wa Roho na kwamba mtoto huyo ataitwa Yesu.
Lakini baada ya hapo, Mungu hakuendelea tena kusema na Mariamu moja kwa moja. Bali alimgeukia mumewe Yusufu, na kumwagiza kuwa atakapozaliwa amwite jina lake YESU.
Mathayo 1:20 “Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao”.
Mathayo 1:20 “Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao”.
Na utaona baada hapo, wakiwa kule Bethelehemu, bado Malaika anamtokea Yusufu tu, na kumwambia, mchukue mtoto na mama yake, wapeleke Misri, kwasababu Herode anataka kumuua mtoto.(Mathayo 2:13-14)
Tengeneza picha Mariamu angekuwa ni mwanamke kiburi, angesema, mbona Mungu hajasema na mimi kuhusiana na hilo?, Kwanza si wewe uliyembeba masihi, mateso huyajui, huko Misri ni nani unayemjua, nangojea Mungu anithibitishie kwanza mimi..lakini hakuwa hivyo alikubali kutii, bila kujadili jadili.
Bado utaona, akiwa kule Misri, malaika anamtokea tena Yusufu peke yake na kumwambia, mchukue mke na mtoto urudi nao Israeli kwasababu Herode amekufa. Safari tena ya mihangaiko ikaanza, huku Mariamu akisikiliza maagizo ya mumewe na kutii (Mathayo 2:19-20).. Lakini wakiwa pale Bethelehemu, wametulia ili sasa waanze maisha, saa hiyo hiyo, Yusufu anamwambia mke wake, tuondoke hapa tuende tena Nazareti, Mungu ameniagiza hivyo (Mathayo 2:22-23).
Mariamu hakuwa na kigugumizi kumsikiliza mume wake, hakuwa na kazi nyingine yoyote zaidi ya kupokea maagizo ya uongozi kuhusu familia au mtoto kutoka kwa mumewe.
Kwa mwanamke: Tambua kuwa mume ndio kichwa cha familia, Mungu atamtumia yeye, kuyalinda na kuyatamia maono yako, huwezi kufanikiwa bila yeye. Haijalishi Mungu kakuonyesha mambo makubwa kiasi gani hapo mwanzoni. Ikiwa humtii mume wako, ujue kuwa unajiharibia wewe mwenyewe. Utiifu ni muhimu sana, hata wakati ambapo unaona sehemu unapopelekwa sio pa kuvutia.
Ndio maana unawajibu sana wa kumwombea mume wako, ikiwa ni mwenye dhambi, Mungu ambadilishe. Kwasababu yeye ndio usalama wa maono yako.
Kwa mwanaume: Umewekwa kama kichwa, ni lazima utambue kulinda maono mema ya mkeo, Si kila taarifa nzuri itakufikia wewe wa kwanza, Wakati mwingine inaanzia kwa mwanamke, kama ilivyokuwa kwa Mariamu, kisha wewe baadaye, hivyo uonapo hivyo, usipige vita, bali, sikiliza, tafakari, pia tendea kazi, Hapo ndipo Mungu atakapokutumia, kuijenga familia bora. Wewe kama mlinzi huna budi, kutimiza wajibu wako,wa kumtunza mkeo na kumpenda kama maandiko yanavyosema. Jambo lolote linaloihatarisha familia yako, shughulika nalo kwelikweli usimwachie mwanamke alitende.
Hivyo kwa kuzingatia mambo hayo, Ndoa zetu zitakuwa bora, mfano wa ile ya Yusufu na Marimu. Na Bwana atatupa zawadi ya kuzaa vitakatifu kama Ilivyokuwa kwa Yesu na wadogo zake wote. Tambua wajibu wako, simama katika nafasi yako.
WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.
ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.
KUWA RAFIKI WA DUNIA NI KUWA ADUI WA MUNGU.
USIOGOPE KUMWADHIBU MWANAO.
SWALI: Biblia inaposema “Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake”, ina maana gani?
Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
JIBU: Ili kuelewa neno hilo, wazia mfano huu; Mtu mmoja ameshitakiwa na mahakama kwa kosa la uchafuzi wa mazingira, hivyo, akapewa adhabu ya kulipa faini ya sh. Milioni 5 ndani ya wiki 3, au jela miaka 3. Sasa ikatokea mtu huyu akawa hana cha kulipa,.. Unadhani atakuwa katika hali gani? Ni wazi kuwa atapoteza amani yote, hawezi kuwa katika furaha, hawezi kuwa katika raha wakati wote huo kwasababu anajua hukumu ya kifungo ipo mbele.. Ili amani yake irudi, hana budi apate kiwango hicho alipe. Lakini akatokea mtu, akasema mimi nitakuchukua adhabu hiyo nitamlipia deni lake. Bila shaka furaha na amani ya yule mdaiwa itarejea tena.
Hivyo tunaweza kusema, ili kuirejesha ile amani yake ya mwanzo, alikuwa hana budi kutumikia adhabu kwanza..
Sasa tukirudi katika huo mstari ..biblia inaposema;
Huyo ni Bwana Yesu anayezungumziwa hapo, sasa anaposema, Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”. Ni kwamba ili sisi kuipokea Amani yetu, tuliyoipoteza tangu kule edeni, ilitupasa kwanza tutumikie adhabu ya makosa.. Lakini ashukuruwe Kristo kwasababu alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, akapigwa na kuteswa ili sisi tupone. Adhabu ya amani yetu aliichukua yeye.
Na ndio maana Warumi 8:1 inasema; “Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu”.
Ukiwa ndani yake, amani yako inarejeshwa bila kulipa gharama yoyote. Lakini inastaajabisha kuona bado wapo watu hawataki kulipiwa deni zao. Wakidhani kuwa wataweza kustahimili hukumu ya Mungu siku ile. Ndugu ikiwa upo nje ya Kristo huna tumaini lolote. Ukifa ni moja kwa moja jehanamu kwenye ziwa la moto. Adhabu yako ni Mauti katika lile ziwa la moto milele.
Hiyo ndio sababu kwanini unamuhitaji Yesu Kristo leo, kwasababu ukishakufa leo hakuna tumaini, wala huna matendo yoyote ya kumshawishi Mungu, afute dhambi zako. Wasubiri nini, usimgeukie Bwana Yesu akusafishe Maisha yako angali ukiwa hai? Tubu sasa mpokee yeye. Muda ni mchache.
KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.
BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?
Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?
Sadaka ya Amani ilikuwaje?
Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?
Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.