Category Archive Uncategorized @sw-tz

Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?

SWALI: Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”. Kwanini isingesema tu mara moja saba, mpaka ianze sita,halafu tena saba?


JIBU: Ni lugha ya zamani, iliyotumika kuwekea msisitizo kitu hususani kile cha mwisho, yaani, kama inadhaniwa ni sita, basi kipo na cha saba ambacho ndio zaidi.

Kwa mfano ukisoma ile Mithali 6:16  inayozungumzia mambo sita ambayo Mungu anayachukia utaona anaongezea na kingine cha saba, ambacho  ni “kupanda mbegu ya fitina katika ya ndugu” ikiwa na maana hicho ndio kibaya zaidi..

Mithali 6:16 “Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.

17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;

18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;

19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu”.

Ukisoma pia  Mithali 30:18 “utaona Sulemani anasema tena kati ya mambo ambayo yanamshangaza mienendo yao, yapo matatu lakini lile la nne ndio zaidi, ambalo ni mwendo wa kijana pamoja na msichana.

Mithali 30:18 “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.

19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana”.

Vivyo hivyo, ukisoma Mithali 30:29, Sulemani anasema pia vipo vitu vitatu vyenye mwendo wa kupendeza lakini akakiongezea na cha nne chenye mwendo wa kupendeza zaidi nacho ni mfalme asiyehasika.

Mithali 30:29 “Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hajiepushi na aliye yote;

31 Jimbi aendaye tambo; na beberu; Na mfalme ambaye haasiki”.

Soma, pia vifungu hivi;

Mithali 30:15 “Mruba anao binti wawili, Waliao, Nipe! Nipe! Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe, Naam, vinne visivyosema, Basi!

16 Kuzimu; na tumbo lisilozaa; Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!”

Ayubu 5:19 “Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.

Amosi 1:3 “Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Dameski, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya kupuria vya chuma”;

Soma pia Amosi 1:4.

Na hata sasa, katika mambo saba(7) ambayo  biblia inasema yanamkamilisha mwanadamu, lipo la nane(8) ambalo ndio kuu zaidi linaloitwa UPENDO.

Tusome.

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa,

6 na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa,

7 na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, UPENDO.

8 Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.

Ni vizuri tukawa na hayo mengine yote, lakini tukikosa upendo wa Ki-Mungu, basi bado hatujakamilishwa.

Je! Upendo wa AGAPE upo ndani yako?

Ili kufahamu tunaupate upendo wa namna hii, fungua link hii>>

https://wingulamashahidi.org/2020/12/21/nitaupataje-upendo-wa-ki-mungu-ndani-yangu/ 

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

UFUNUO: Mlango wa 1

Je! kuna madhara kuchukiwa na kila mtu kwasababu huna mali?. Kama biblia inavyosema katika Mithali 14:20?.

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Rudi nyumbani

Print this post

Ni yupi aliyekuwa mkwe wa Musa kati ya Reueli na Yethro?

JIBU: Ukisoma katika kitabu cha Kutoka, utaona kuna habari kama inajichanganya kuhusiana na baba-mkwe halisi wa Musa, Kwamfano Kutoka 2:18 Inasema aliitwa Reueli, lakini sehemu nyingine zote zilizosalia kama vile Kutoka 3:1,4:18, inamtaja kama ni Yethro. Je  kuna makosa ya kiuandishi?

Embu tusome baadhi ya vifungu hivyo;

Kutoka 2:15 “Basi Farao alipopata habari, akataka kumwua Musa; lakini Musa akakimbia mbele ya Farao, akakaa katika nchi ya Midiani; akaketi karibu na kisima.

16 Basi kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja wakateka maji, wakazijaza birika maji, wapate kunywesha kundi la baba yao.

17 Wachungaji wakaja wakawafukuza; lakini Musa akasimama, akawasaidia, akalinywesha kundi lao.

18 Walipofika kwa Reueli baba yao, akasema, Imekuwaje hata mkarejea mapema leo?

19 Wakasema, Mmisri mmoja alituokoa katika mikono ya wachungaji, tena zaidi ya hayo, akatutekea maji, akalinywesha kundi.

20 Akawaambia binti zake, Yuko wapi basi? Mbona mmemwacha mtu huyo? Mwiteni, ale chakula.

21 Musa akawa radhi kukaa kwake mtu yule, naye akampa Musa binti yake, Sipora.

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu”.

Jibu ni kuwa hakuna hitilafu, yoyote ya kiuandishi isipokuwa zamani ilikuwa ni jambo la kawaida mtu mmoja kuwa na jina zaidi ya moja, Kwamfano tukimtazama Yakobo, Mungu alimwambia utaitwa Israeli, Hivyo majina yake yote mawili utayakuta yakiandikwa sehemu mbalimbali katika biblia Lakini mtu ni Yule Yule mmoja.

Vivyo hivyo na Yethro mkwewe Musa, aliitwa pia Reueli, na kwasababu alikuwa ni kuhani, hatushangai kuona akiwa na majina mawili, moja la kwake la asili na lingine la kikuhani.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Rudi nyumbani

Print this post

TABIA ZA WATAKAOMKARIBIA SANA MUNGU SIKU ILE.

Kwa mara ya kwanza Yohana alionyeshwa maono ya jinsi mbinguni kulivyo, na mfumo wake mzima wa utawala ulivyojiunda.

Tukisoma mambo yale tusidhani, Mungu alikuwa anamuonyesha Yohana sinema tu ya mbinguni jinsi kulivyo, Hapana zipo siri kubwa sana zinazotuhusu sisi, endapo tutazitambua.

Leo kwa ufupi tutazama ngazi hizo, na ni jinsi gani zilivyoficha siri za sisi kumkaribia Mungu..

Ukisoma kile kitabu cha Ufunuo, sura ya 4 yote, utaona Yohana alionyeshwa mbingu zikifunga. Na moja kwa moja macho yake yakakiona kile kiti cha Enzi cha Mungu kilichojaa utukufu mwingi.

Lakini kiti hichi hakikusimama peke yake, bali alionyeshwa pia viti 24 ambavyo vimekizunguka kile kiti cha enzi ambavyo vimekaliwa na wale wazee 24, na katikati ya vile viti 24 aliona pia wenye uhai 4 ambao wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi. Na nyuma ya wale wazee 24 kulikuwa maelfu kwa maelfu ya malaika mbinguni  wamemzunguka Mungu, wakimsifu na kumtukuza. Soma Ufunuo sura ya 4 yote.

Embu tusome baadhi ya vifungu kidogo; Tafadhali soma kwa utulivu,usiviruke.

Ufunuo 4:1 “Baada ya hayo naliona, na tazama, mlango ukafunguka mbinguni, na sauti ile ya kwanza niliyoisikia kama sauti ya baragumu ikinena nami, ikisema, Panda hata huku, nami nitakuonyesha mambo ambayo hayana budi kuwako baada ya hayo.

2 Na mara nalikuwa katika Roho; na tazama, kiti cha enzi kimewekwa mbinguni na mmoja ameketi juu ya kile kiti;

3 na yeye aliyeketi alionekana mithili ya jiwe la yaspi na akiki, na upinde wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi, ukionekana mithili ya zumaridi.

4 Na viti ishirini na vinne vilikizunguka kile kiti cha enzi, na juu ya vile viti naliona wazee ishirini na wanne, wameketi, wamevikwa mavazi meupe; na juu ya vichwa vyao walikuwa na taji za dhahabu.

5 Na katika kile kiti cha enzi kunatoka umeme na sauti na ngurumo. Na taa saba za moto zilikiwaka mbele ya kile kiti cha enzi, ndizo Roho saba za Mungu.

6 Na mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na mfano wa bahari ya kioo, kama bilauri; na katikati ya kile kiti cha enzi, na pande zote za kile kiti, walikuwako wenye uhai wanne, wamejaa macho mbele na nyuma”.

Ufunuo 5:11 “Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,

12 wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.

13 Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele.

14 Na wale wenye uhai wanne wakasema, Amina. Na wale wazee wakaanguka, wakasujudu.

Sasa ni vizuri ukajiuliza kwanini walivyozidi kumkaribia Mungu, walionekana na maumbile tofauti tofauti. Ikumbukwe kuwa hao wote wanaozungumziwa hapo ni malaika, hakuna mwanadamu hata mmoja. Jiulize ni kwanini wawe ni wazee, na si vijana, na vilevile kwanini wale wenye Uhai wanne wawe na maumbile kama yale na si vinginevyo.?

Hiyo ni kufunua kuwa rohoni, na sisi tukitaka kumkaribia sana Mungu, basi hatuna budi kupitia hatua kama za wale wanaoonekana wapo karibu sana na Mungu.

Kwamfano tukiwatazama wale wazee 24, wanafunua kuwa ili mtu aweze kumkaribia Mungu sana, ni lazima awe ni mzee rohoni, awe amekomaa siku za wokovu ndani yake. Awe kama Ibrahimu, awe kama Henoko aliyetembea na Mungu kwa miaka 300 bila kumwacha, awe kama Eliya aliyemtumikia Mungu mpaka uzee wake, awe kama Ayubu, Hana, na Simoni, Zekaria na Elizabeti. Ambao hao walitembea katika haki yote na Mungu wao bila kumwacha. Watu wa namna hiyo, wanapomaliza siku zao hapa duniani, na wametembea na Mungu tangu ujana wao, mpaka kufa kwao, basi ni wazee rohoni. Na hivyo watakapovuka kule ng’ambo watakuwa karibu sana na Mungu.

Kwasababu Mungu naye, anajitambulisha kama mzee wa siku (Danieli 7:9). Hivyo na wale watakaomkaribia ni lazima wawe wameshiba siku za wokovu, Lakini ikiwa wewe unataka kuwa mkristo tu wa kufa ili uende mbinguni, hutaki kutenda mapenzi ya Mungu angali ukiwa hapa duniani, hutaki kukua kiroho, ujue kuwa ukifa leo hii, kamwe hutakaa umkaribie Mungu kule mbinguni, utakuwa mtu baki tu, haijalishi umeikwepa hukumu

Kwa urefu wa somo hilo fungua link hii>>

https://wingulamashahidi.org/2021/02/22/tutamkaribia-mungu-kwa-idadi-ya-mvi-zetu-rohoni/

Sasa tupige hatua mbele kidogo, kumbuka hawa malaika 24 ambao walifanana sana na wanadamu wazee 24 ni kweli walikuwa karibu na sana na Mungu, lakini wapo waliokuwa karibu zaidi ya Mungu kuliko wao. Na hao si wengine zaidi ya wale wenye uhai 4.

Wenye Uhai 4 walisimama moja kwa moja mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, mbele ya wale wazee 24, Ndio makerubi wa Mungu. Hawa walikuwa na nyuso 4 kila mmoja. Uso wa kwanza upande wa kulia ulikuwa ni wa simba, upande wa kushoto ulikuwa ni wa ndama, upande wa nyuma ulikuwa ni wa Tai, na upande wa  mbele ulikuwa ni kama wa binadamu. Ndivyo Ezekieli alivyoonyesha kwa uwazi wote viumbe hai hao  jinsi walivyo (Ezekieli 1:1-26)

Japokuwa Yohana alionyeshwa upande mmoja mmoja wa kila kiumbe hai huyo kwasababu kulikuwa na sababu ya yeye kuonyeshwa vile, Lakini wote hao walikuwa na sura 4 kila mmoja wao (Soma Ufunuo 4).

Sasa kama tulivyotangulia kusema, haikuwa sinema tu, kwamba Mungu anataka kutuonyesha viumbe hao jinsi walivyo wa ajabu hapana. Bali alikuwa anatuonyesha kuwa na sisi tukitaka kumkaribia zaidi yeye. Ni lazima tuwe kama wao Rohoni, kwamba ni lazima uwe na sura hizo nne, ili ukidhi vigezo vya kuwa karibu sana na Mungu. hivyo tu.

Na leo kwa ufupi tutatazama kila uso wa hao makerubi, unawakilisha nini kwa leo. Tukianzana na ule..

USO WA SIMBA:

Kama tunavyojua simba ni mnyama jasiri asiye na woga,

Mithali 30:29 “Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hajiepushi na aliye yote;”

Kuonyesha kuwa kama mkristo, ni lazima uvae sura ya ujasiri kwa ajili ya imani yako na injili, kama Yesu Kristo alivyokuwa, na ndio maana anaitwa Simba wa Yuda (Ufunuo 5:6). Yeye hakuogopa mwanadamu yoyote, ilipofika suala la wokovu hata Herode alipotaka kumkamata, aliwaambiwa wale watu akisema “mwambieni Yule MBWEHA”!.. kuonyesha kuwa yeye hababaishwi na mwanadamu yoyote kuhubiri injili.

Vilevile na sisi ni lazima tuwe kama simba tukiwa hapa duniani kwasababu shetani naye hatufuati kama kondoo, bali kama Simba, biblia inasema hivyo katika 1Petro 5:8, Unategemea vipi na sisi tumwendee kwa upole katika kuuharibu ufalme wake?

USO WA NDAMA:

Upande wa kushoto wa vile viumbe walikuwa na uso wa ndama. Kama tunavyojua ndama ni wanyama wa kafara, wa kuchinjwa, wa kuchukua  dhambi za watu n.k. Hivyo hiyo ni kuonyesha kuwa unapokuwa mkristo ni lazima uso wa ndama/mwana kondoo, uwe nao pia. Yaani ukubali kuteseka kila siku kwa ajili ya manufaa ya wengine, na si yako tu peke yako. Ukubali hata kujinyima kwa ajili ya injili,

Paulo alisema..”Ninakufa kila siku”.. 1Wakor 15:31. Hata Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa tayari kuutoa uhai wake kwa ajili yetu, ili sisi tupate ondoleo la dhambi. Vivyo hivyo na sisi kama wakristo, tunapaswa tuwe na uso huu wa ndama ndani yetu. Tuwe tayari kufa kila siku kwa ajili ya injili ya Kristo. Kujitoa ikiwemo na mali zetu  na nguvu zetu kwa ajili ya injili., kama alivyofanya Kristo na mitume wake.

USO WA TAI:

Wenye uhai 4 walikuwa na uso wa Tai kwa nyuma. Tai ni ndege anayeiona mbali sana, Jicho lake linaweza kuona chakula kutokea mbali sana, mahali ambapo wewe huwezi hata kumuona juu. Na sio tu chakula, bali pia maadui.

Na ndio maana Bwana Yesu alisema katika siku za mwisho, ni Tai tu ndio watakaoweza kuona chakula cha kweli cha roho kilipo. Wengine wote watakuwa kama kuku, wakisikia Kristo yupo huku wanakimbilia, yupo kule wanakimbilia, manabii wa uongo na imani potofu zikiwachanganya, wanabahatisha kwasababu macho yao hayawezi kuona mbali.

Luka 17:37 “Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai”.

USO WA MWANADAMU:

Wenye uhai 4 hawa walikuwa pia na nyuso wa binadamu kwa mbele.

Kumbuka mwanadamu, ndiye aliyejuu ya zaidi ya wanyama wote ambao Mungu alishawahi kuwaumba. Mwanadamu anao ujuzi, hekima, utashi, fikra, elimu, ujuzi, maarifa. Kwa kutumia tu utashi aliopewa na Mungu anaweza kubuni na kuvumbua mambo makubwa sana, ambayo yanaweza kumletea matokeo chanya au matokeo hasi. Inategemea na dhima yake ni nini.

Hivyo, Na sisi pia ni lazima tutumie utashi wetu tuliopewa na Mungu, kumpendeza Mungu. Sio kila mahali, tutatumia maombi tu peke yake hapana. Wakati ule Mungu anampa Musa maagizo ya kutengeneza vitu vya hemani, alimwambia akamtafute mtu aliyeitwa Bazaleli, ambaye Mungu atampa  ujuzi na utashi wa uchongaji wa vitu hivyo.

Kutoka 31:1 “Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda;

3 nami nimemjaza roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina,

4 ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba”,

Tujiulize je! Sisi tulishawahi kumbunia nini Mungu?  Watu wa ulimwengu wanatushinda, wao kila siku wanambunia mungu wao shetani, mambo mapya kila siku, mengi ya kuwavutia wao, wanamtungia kila aina ya nyimbo za miundo tofauti tofauti, lakini sisi kama wakristo, ujuzi wetu tuliopewa na Mungu tumeuweka kapuni, tukimwimbia Mungu badala tufikirie ni jinsi gani nyimbo zetu zitakuwa zimejaa Roho, sisi tunawaiga wale wa kidunia staili zao.

Bwana atusaidie sana.

Hivyo Bwana atusaidie sana. Nyuso zote hizo 4 tuwe nazo. Yaani tuwe jasiri kama Simba, tuwe wa kujitoa kama ndama, tuwe na jicho la kuona mbali chakula chetu kilipo kama Tai, na pia tuwe na hekima na ujuzi kama mwanadamu.

Tukiweza hayo, basi tujue kuwa tutakuwa karibu sana Mungu, kuliko tunavyodhani, kwasababu shetani anakuwa hana upenyo wa kutuingilia. Kwasababu kila upande kuna uso tunamwona.

Mwisho, kabisa, upako wa wenye uhai hawa wanne ulitembea pia katika nyakati saba za kanisa. Hivyo kama utapenda kufahamu kwa urefu juu ya nyakati hizo na jinsi mihuri ile ilivyofunguliwa basi fungua link hii utakutana na mfufulilizo wa maelezo hayo.

https://wingulamashahidi.org/2018/07/19/mihuri-saba/

Bwana akubariki sana.

Je! Umeokoka ndugu? Je! Una habari kuwa tunaishi katika kipindi ambacho tutashuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa Kristo duniani?  Unalifahamu hilo? Kwasababu hakuna dalili hata moja Kristo aliyoizungumzia haijatimia. Ni heri ukayasalimisha maisha yako leo kwake, ili siku ile isikukute pabaya.

Tubu kwa kumaanisha kabisa, kisha kabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo upate ondoleo la dhambi zako.

Jina la Bwana libarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

UFUNUO: Mlango wa 4

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

WALIYATWAA MAVAZI YAKE, WAKAFANYA MAFUNGU MANNE,

Yohana 19:23 “Nao askari walipomsulibisha Yesu, waliyatwaa mavazi yake, wakafanya mafungu manne, kwa kila askari fungu lake; na kanzu nayo. Basi kanzu ile haikushonwa, ilikuwa imefumwa yote pia tangu juu.

24 Basi wakaambiana, Tusiipasue, lakini tuipigie kura, iwe ya nani. Ili litimie andiko lile linenalo, Waligawanya nguo zangu, Na vazi langu wakalipigia kura. Basi ndivyo walivyofanya wale askari”.

Ulishawahi kujiuliza ni kwanini biblia haijakaa kimya kuhusiana na mavazi ya Yesu pale Goligotha, na jinsi yalivyopigiwa kura? Mpaka kufikia hatua ya kugawanywa katika mafungu manne (4) kwa wale askari wanne waliokuwa pale msalabani.? Na lile moja la 5 ambalo ni kanzu yake kupigiwa kura?. Haikuandikwa kutengeneza stori tu, kwamba Yesu alikuwa na mavazi matano, bali kulikuwa na maana nzito nyuma yake.

Hiyo ni kuonyesha kuwa hakubakiwa na nguo hata moja muda ule alipotundikwa  pale msalabani. Alisulibiwa akiwa uchi kabisa wa mnyama. Ni jambo ambalo haliwezekani kwamba nguo nyingine zipigiwe kura, na kugawanya, halafu nyingine abakiwe nazo kutundikiwa msalabani, Maandiko hayatuonyeshi hivyo. Kile tunachokiona kwenye misalaba ya kuchonga au kwenye muvi  kwamba Bwana Yesu alisulibiwa akiwa na kipande cha nguo cha kumsitiri, si kweli. Ukweli ni kwamba alisulibiwa akiwa uchi kabisa wa mnyama. Hata hivyo wakati ule wa Rumi wahalifu wote waliouliwa kwa kusulibiwa ilikuwa ni lazima wasulibiwe uchi, ili kwamba sio tu wafe kwa mateso bali pia wafe kwa aibu.

Je! ulishawahi kutafakari kwa utulivu kwanini Kristo aruhusu hayo yote yampitie, wakati alikuwa na uwezo kabisa wa kuyaepuka? Unadhani hakikuwa kitendo cha aibu kile? Kilikuwa ni kitendo kikubwa sana cha aibu, ambacho ninauhakika hata wewe ungekuwepo wakati ule usingedhubutu hata kumwangalia pale msalabani akiwa katika hali ile. Lakini yeye hakuona aibu, kuwekwa uchi, ilimradi tu mimi na wewe tu tuokoke. Huko ni kujitoa kulikopitiliza.

Hakunionea haya mimi, vilevile hakukuonea haya wewe, kinyume chake biblia inatuambia aliidharau aibu,

Waebrania 12:2 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba NA KUIDHARAU AIBU, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu”.

Unaona, ukitafakari hilo vizuri, ndugu yangu, hutaona sababu ya wewe kumwonea aibu Bwana wako, katika dunia hii mbovu. Hutaona aibu kuitwa mshamba, kwa ajili yake, hutaona sababu  kuogopa kuitangaza injili yake.

Paulo alisema..

Warumi 1:16 “Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia”.

Alimwambia pia Timotheo maneno hayo hayo;

2Timotheo 1:8a “Basi usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, ..;”

Huu si wakati wa kufikiria Fulani atanionaje, au marafiki watanichukuliaje, au majirani watanizungumziaje ikiwa nitampa Kristo Maisha yangu. Kumbuka Yesu hakukuonea haya wewe, aliposulibiwa uchi mbele ya kadamnasi, mbele ya maelfu ya watu waliokuwa pale Goligota, kwanini wewe umwonee haya yeye wakati hujafikia hata hatua ya kutembezwa uchi barabarani kwa ajili yake?.

Ukimkataa leo wakati utafika atakukataa na wewe.

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Tengeneza picha unasimama mbele ya mamilioni kwa mamilioni ya malaika, halafu Kristo anakuonea aibu mbele yao, utajisikiaje? Hali Fulani mbaya,

Hivyo chukua msalaba wako ujitwike umfate Kristo. Hizi ni siku za mwisho, yupo mlangoni kurudi. Kama bado hujatubu basi huu ndio wakati wako, mwamini yeye ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako na yeye mwenyewe atakupa Roho wake Mtakatifu atakayekuongoza katika kweli yote.

Ikiwa utahitaji kuokoka, basi wasiliana nasi kwa namba hizi hapo chini, Nasi tutakusaidia katika hilo.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

VAZI KUU AMBALO MUNGU AMETUANDALIA KILA MMOJA WETU.

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

Kutahayari ni nini katika biblia?(2Timotheo 2:15)

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

Nguo za magunia katika biblia ni zipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

SWALI: Je! kuna mchango wowote sisi tunaweza kuuweka ili tupate wokovu wetu? Na  kama sio kwanini basi maandiko yanasema, ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu nao wenye nguvu ndio wanaouteka (Mathayo 11:12)?


JIBU: Kuhusu mchango wetu katika Neema ya wokovu, maandiko yapo wazi ni kuwa HAUPO.

Waefeso 2:8 “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;

9 wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu”.

Lakini swali linakuja kama ni hivyo basi kwanini, maandiko yanasema..

Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”.

Jibu ni kuwa adui yetu tupo naye ni shetani, huyo ndiye anayeifanya njia ya wokovu ionekane ni ya jitahada kidogo. Hivyo inahitaji nguvu ya ziada kuiona na vilevile kuiendea kwasababu ni nyembamba sana na imesonga.

Mathayo 7:13 “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

14 Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache”.

Kwamfano leo hii, shetani anaweza kukuzuia usimfanyie Kristo ibada, kisa tu wazazi wako wamekataa, au kazi yako imekusonga, au mazingira si rafiki hakuna mtu atakayekuelewa, unadhani ukiiruhusu hiyo hali, ataurithi uzima wa milele?. Haiwezekani, inahitaji kulazimisha mambo, kutumia nguvu, kukubali kuchukiwa, au wakati mwingine kupoteza hata kile ulichonacho, ili mradi tu usiopoteze wokovu wako.

Hapo ndipo neno ufalme wa mbinguni unapatikana  kwa nguvu, nao wenye nguvu ndio wanauteka.

Kwamfano, Kristo alituambia tukeshe tuombe, lengo la kusema vile lilikuwa ni kusudi tusiingie majaribuni(Mathayo 26:41), kwasababu adui yetu shetani anaishi kutuwinda. Sasa kama wewe husali, ili kuulinda wokovu wako uliopewa bure na Kristo bila kuusumbukia, unaona uvivu, ufahamu kuwa shetani atakesha kwa ajili yako, na siku ya siku ikifika atakuletea majaribu mazito, kama alivyowaletea wakina Petro usiku ule mpaka kufikia hatua ya kumkana Bwana na wengine kumtoroka uchi, unadhani walipenda? Hapana hiyo yote ni kutokana na kupuuzia kwao maagizo ambayo Yesu aliwapa muda mchache kabla kwamba wakeshe waombe, wao wakalala.

Vivyo hivyo, na wewe usipokuwa mwombaji, usipojitesa kufunga wakati mwingine, hata kutumika kwa ajili ya Kristo, ni ngumu  sana kuutunza wokovu wako kama sio kuupoteza kabisa.

Hivyo, hatumwamini Yesu na kubakia hivyo hivyo tu, hapana hiyo ni hatua moja, hatua ya pili ni lazima tushindane na tupambane, tupigane vita, na tuumie ili kuulinda wokovu wetu kwasababu adui yetu shetani yupo kuuwinda wokovu wetu usiku na mchana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

Neema ni nini?

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.

Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

SWALI: Je! Mungu anashindwa na mwanadamu? Kama sio Kwanini siku ile aliposhindana na Yakobo alikiri kushindwa?

Mwanzo 32:25 “Naye alipoona ya kuwa hamshindi, alimgusa panapo uvungu wa paja lake; ukateguka uvungu wa paja la Yakobo alipokuwa akishindana naye.

26 Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki.

27 Akamwuliza, Jina lako n’nani? Akasema, Yakobo.

28 Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda”.

JIBU: Jibu ni ndio Mungu anakubali kushindwa, Pengine utauliza unakubalije kushindwa wakati yeye ni Mungu asiyeshindwa na chochote.

Tabia za Mungu sio kama  zetu, Mungu huwa anathamini sana, NIA, BIDII na MATAMANIO ya mtu, kiasi kwamba hata kama matamanio hayo yatakuwa  kinyume na mpango wake, au mapenzi yake, ikiwa tu mtu huyo ataendelea kuking’ang’ania basi mwisho wa siku atamwachia, akipate anachokitafuta haijalishi kitakuwa ni kibaya au chema. Huko ndiko kushindwa kwa Mungu.

Na ndicho kilichotokea kwa Yakobo, aliposhindana na Mungu usiku kucha, akiomba apewe jambo ambalo halikuwa mpango wa Mungu kumpa wakati ule, lakini alipong’ang’ania bila kukata tamaa, kwa kupigana mieleka, ikambidi Mungu ampe tu kulingana na haja yake.

Jambo hili hili utaliona pia wakati ule Bwana Yesu akiwa duniani, utakumbuka kuwa mwanzoni kabisa alitumwa kwa Wayahudi na sio kwetu sisi mataifa, lakini siku moja alikutana na mwanamke mmoja king’ang’anizi wa kimataifa aliyeishi nchi moja iliyoitwa Tiro. Mwanamke huyo alikuwa na binti yake aliyesumbuliwa na mapepo. Na alipokutana na Yesu alitaka aponywe, lakini Yesu hakuongea naye chochote, kwasababu sio hakutumwa kwao, lakini mama huyo hakukata tamaa, baada ya kumlilia sana,  ndipo Yesu akafungua kinywa chake akamwambia, maneno haya;

Mathayo 15:24 “Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli

25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Unaona, hapo, neema ya wokovu ilikuwa haijatufikia bado watu wa mataifa, kwasababu Kristo alikuwa hajasulibiwa bado, lakini mwanamke huyu, aliiwahi kabla hata ya wakati wenyewe kujika, jambo ambalo lilikuwa kinyume kabisa na mpango wa Mungu. Na ndio maana Kristo alitumia maneno magumu kama yale ili mradi tu adhoofishe mataminio yake, akawa hajibiwi, akawa anaitwa mbwa. Lakini mwisho wa siku Yesu kuona bado ni king’ang’anizi basi akakubali kushindwa. Akampa haja ya moyo wake, kama alivyofanya kwa Yakobo.

Hata wewe leo hii, unaweza shindana na Mungu nawe ukamshinda, hilo linawezekana kabisa, pengine hukustahili kupokea  uponyaji wa ugonjwa wako sasa, kutokana na mambo uliyomkosea Mungu, pengine,hustahili kupewa hilo hitaji lako kwa sasa hivi, labda pengine  limekusudiwa ulipokee baadaye sana, baada ya miaka 15, pengine hustahili kuwa na hiyo karama sasa hivi, lakini uking’ang’ana na Mungu, anaweza kukusogezea karibu hilo hitaji lako haijalishi alitaka litimie baada ya miaka 20.

Na ndio maana Bwana Yesu alituambia mfano huu, naomba nawe pia uutafakari vizuri;

Luka 18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”.

Usichoke kung’ang’ana na Mungu wako..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

BWANA HUWAJUA HAO WAMKIMBILIAO.

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Bwana Yesu alitupa dalili za kurudi kwake, akatuambia mkiona dalili Fulani Fulani kama vile matetemeko, mlipuko wa magonjwa, manabii wa uongo, vita n.k. Basi tujue yupo mlangoni kurudi. Lakini kamwe hakutupa dalili ya SIKU yenyewe atakayorudi itakuwaje.. Na hiyo ndio hatari Zaidi kwasababu watu wengi leo hii japokuwa wanajua Yesu atarudi siku yoyote kutokana na kuwa dalili hizo zimeshatimia zote, Lakini bado wanachunguza chunguza siku yenyewe, wakidhani  labda watashtukia lolote.

Bwana Yesu alisema siku ya kuja kwake, inafanana na siku zile za Nuhu, Siku zile mpaka Nuhu anaingia kwenye Safina hakuna mtu yeyote alitambua kuwa tayari Mungu ameshaihukumu dunia.. mpaka zikapita siku saba, nyingine ndipo mvua ya gharika ikashuka kwenye dunia.

Mathayo 24:38 “Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina,

39 WASITAMBUE, HATA GHARIKA IKAJA, IKAWACHUKUA WOTE, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.

40 Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;

41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.

42 Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu”.

Unaona? Leo hii, kama wewe sio “bibi-arusi” wa kweli wa Kristo, nikimaanisha, kama sio mkisto aliyesimama katika wokovu kweli kweli, usitazamie utatambua lolote siku  Kristo anarudi kuwanyakua watakatifu wake. Kwasababu hata Bibi-arusi wake mwenyewe hatojua siku hiyo itakavyokuwa sembuse wewe?..

Na ndio maana aliwaambia mpaka na wateule wake, kwamba wajiweke tayari, waifanye kazi yake, watimize wajibu wao walioitwa hapa duniani wa kuitangaza injili yake, kwasababu saa wasiodhani ndio atakayokuja..

Mathayo 24:43 “Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.

44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika SAA MSIYODHANI MWANA WA ADAMU YUAJA.

45 Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47 Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.”

Hakuna mtu atakayeitambua siku hiyo, itakuja ghafla tu bila hodi, hakuna dalili yoyote itakayotutambulisha, itakuwa kama tu ilivyo leo, au jana,  wakati ambapo watu wanapanga mipango yao ya kimaisha, wanalijenga taifa lao, wanauza pombe, na kufanya biashara hapo hapo, Unyakuo unapita , mmoja anatwaliwa mmoja anaachwa..

Watu wengi sana wataingiwa na butwaa, wakisema mbona Bwana hakutupa taarifa au kiashirio fulani, mbona, angani hakukuonekana chochote, mbona tulitazamia jambo Fulani kwanza tulione, ndio unyakuo upite, imekuwaje, amesharudi, wakati watu wengine hawajahubiriwa bado injili. Lakini ndio hivyo tayari watakatifu wameshaondolewa.

Wakati huo upo karibu sana ndugu yangu, ridhika na dalili tunazoziona, kwasababu hakutakuwa na nyingine Zaidi ya hizo zilizoandikwa kwenye biblia.  Usidhani malaika atatokea hapo mawinguni kutuhubiria injili kwamba kesho Yesu ndio anarudi.

Kama utakosa unyakuo, basi ujue, utakuwa katika majuto na vilio na kusaga meno kusikokuwa kwa kawaida. Majuto hayo, unaweza ukayaona sio kitu leo kwasababu bado hayajakukuta, lakini  subiri siku hiyo ikufikie, hutatamani uishi. Hicho kiburi cha uzima ulichonacho leo, siku hiyo kitayeyuka chote, utamtafuta Mungu hutamwona. Utalia hakuna atakayekusikia, makanisa yatakuwa hayana faida yoyote kwako. Hakuna chochote kitakuwa na maana kwao, kwasababu hata pesa hazitafanya kazi wakati huo.

Ndugu, ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho bado unayo nafasi ndogo sana ya kutubu, Tubu leo kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako, na Kristo atakupokea.

Shalom.

Kumbuka katika saa usiyodhani Kristo anakuja!

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengi

Mada Nyinginezo:

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

MATESO YA KUZIMU.

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA VILE UMEME UTOKAVYO MASHARIKI UKAONEKANA HATA MAGHARIBI.

Ni kipi kinakupa ujasiri wa kuishi ukristo ya juu juu tu ndugu ?

Bwana atusaidie tujue majira tunayoishi..

Ulishawahi kutafakari kwa makini kwanini Bwana alifananisha kuja kwake na umeme? Kama tunavyosoma katika kitabu cha  Mathayo 24:27-28

“Kwa maana kama vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.

28 Kwa kuwa po pote ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai”.

Umeme unaozungumziwa hapo sio huu wa transforma unaowaka majumbani, hapana, ni ule wa radi tunaouona sana sana wakati wa mvua, ule mwanga, unaomulika kwa ghafla sana bila hodi, ambapo kwa kawaida ukimulika mara moja usiku, mahali hapo panabadilika unaweza ukadhani ni mchana, kwa jinsi unavyoangaza sana ..

Ndivyo Bwana Yesu alivyoifananisha na siku ya kurudi kwake kuja kulichukua kanisa, Nuru yake itamulika ulimwenguni kote kwa muda mfupi sana, ambao hakuna mwanadamu yoyote anaweza kuutazamia, na Nuru hiyo itamulika, kwa wakati mmoja ulimwenguni kote, kama vile mwanga wa radi unavyoonekana mashariki mpaka magharibi kwa wakati mmoja.

Kipindi hicho, ambacho kipo karibuni kutokea, Yesu atafunua siri ambazo, zitatuandaa moja kwa moja kwa ajili ya kwenda katika unyakuo. Na siri zenyewe hazijaandikwa hata kwenye biblia, kwasababu hakukuwa na umuhimu wa kuandikwa kwasababu, si za wakati wote, bali za wakati maalumu. Ambao ndio huo wa kurudi kwake kulinyakua kanisa lake.

Utauliza maneno hayo tumeyajulia wapi.?

Kumbuka, sikuzote, mwanga wa radi unapowaka angani, kinachofuata huwa ni Ngurumo. Hivi vitu viwili huwa vinakwenda pamoja. Sasa wakati huo ambao Kristo atakapoangaza Nuru yake ulimwenguni kote kwa kipindi kifupi sana.. Kutaambata na NGURUMO za rohoni,. Ndio zile ngurumo SABA zinazozungumziwa katika kitabu cha Ufunuo sura ya 10.

Ngurumo hizo Yohana alizisikia zikitoa sauti zao, lakini alipotaka kuziandika kwa ajili yetu sisi, alisikia sauti ikimwambia asiziandike bali azitie muhuri..Tusome.

Ufunuo 10:3 “Naye akalia kwa sauti kuu, kama simba angurumavyo. Na alipolia, zile ngurumo saba zikatoa sauti zao.

4 Hata ngurumo saba zilipotoa sauti zao, nalikuwa tayari kuandika. Nami nalisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Yatie muhuri maneno hayo yaliyonenwa na hizo ngurumo saba, usiyaandike”.

Umeona? Hizo ni jumbe, maalumu ambazo Kristo atazifunua kwa kanisa lake safi, kwa watu maalumu siku hizi za mwisho, wakati huo ambao MWANGA huo utamulika duniani kote. Hatujui ni nini Yesu kakiandaa kwa watu wake, lakini mpaka hakijafunuliwa sasa, ni kuonyesha kuwa ni mambo ya ndani sana ya siri, ambayo hayo ndio yatampa bibi-arusi wa Kristo Imani ya kwenda katika unyakuo.

Sasa mwanga  huo wa rohoni ukishamulika ulimwenguni kote, kama upo nje ya Kristo, basi ujue unyakuo utakupita tu, kwasababu hutaweza kuelewa hata Sauti ya hizo ngurumo saba zitakazonenwa ulimwenguni baada ya hapo.

Utauliza tena hilo tumelijuaje?

Ni kama tu kipindi kile cha Bwana Yesu sauti ilitoka juu mbinguni kuzungumza na makutano yaliyokuwa yanamfuata, lakini kwasababu NURU ilikuwa imeshawapita walichobakia kusikia tu ni ngurumo badala ya Sauti , ndivyo itakavyokuwa siku hiyo..

Yohana 12:28 “Baba, ulitukuze jina lako. Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.

29 Basi mkutano uliosimama karibu wakasikia, walisema ya kwamba kumekuwa ngurumo; wengine walisema, Malaika amesema naye.

30 Yesu akajibu, akasema, Sauti hiyo haikuwako kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu”.

Na ndio maana leo hii unaposisitizwa umtafute Kristo, maadamu muda mchache umebakia, wewe unachukulia mambo rahisi rahisi tu unadhani siku hiyo utaweza kuelewa kitu. Yesu alilijua hilo na ndio maana akatuambia, tujitahidi sasa kwa sababu upo wakati watu wengi watatamani waingie lakini wasiweze..wakati wenyewe ndio huo wakati wa NURU ya mwisho. Kwasababu itamulika kwa haraka sana kama vile radi, hatujui matukio hayo yatachukua muda gani pengine siku kadhaa tu, au wiki kadhaa tu, na kila kimekwisha.

Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako”;

Mimi sijui unasubiria nini, usiokoke, Wewe unadhani mambo yataendelea kuwa hivi milele? Hujui kuwa hii injili hadi sasa ingepaswa iwe imesharudi Israeli, maandalizi yao yapo tayari, usiku na mchana wanamlilia YEHOVA pale Yerusalemu kwenye ukuta ule wa maombolezo,  kuomba warudishiwe ufalme, lakini sisi tumekaa tu tukidhani, neema hii tutakuwa nayo milele.

Ni vizuri tukajua agenda ya Mungu kwetu ni ipi sisi watu wa mataifa, inashangaza kuona mkristo anachojua ni kutabiriwa tu, na injili za kupokea, na mafanikio ya mwilini basi hana habari na mambo ya ufalme wa mbinguni. Inahuzunisha sana.

Biblia inatuambia “utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.

Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu”, (Wafilipi 2:12-13)

Kumbuka: UMEME na NGURUMO vipo mbioni.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

[07/11, 09:47] Justina Raphael: https://wingulamashahidi.org/2024/03/14/usiwe-mkristo-wa-kukaa-tu-ghalani/

*USIWE MKRISTO WA KUKAA TU GHALANI,*

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima ya mwokozi.

Watu waliomwamini Yesu Kristo, yaani waliopokea ondoleo la dhambi zao. Hutambulika kama NGANO, lakini watu ambao bado wapo kwenye dhambi, hujulikana kama MAKAPI.

Sasa kazi ya kwanza ambayo Yesu anaifanya kwa mwamini, ni kumtenganisha yeye na makapi, kisha humweka katika ghala lake.

Mathayo 3:12 Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.

Ghalani ni uweponi mwa Mungu, yaani kutengwa na udunia.

Soma pia..Mathayo 13:29-30.

Sasa kama wewe unafahamu ukulima, unajua kabisa si mbegu zote zinawekwa ghalani kwa matumizi ya chakula, zipo nyingine, zinachukuliwa na kurudishwa shambani ili kwenda kuzalisha nyingine. Na baadaye huongeza ghala la mkulima.

Tofauti kabisa na ile inayobakia pale ghalani, itaendelea kubakia vilevile hata miaka 10, lakini ile inayokwenda shambani, ndani ya hicho kipindi cha miaka 10, yaweza kuongeza magunia mengi sana ya ngano nyingine.

Ndio maana Bwana Yesu alisema maneno haya;

Yohana 12:24 Amin, amin, nawaambia, CHEMBE YA NGANO ISIPOANGUKA KATIKA NCHI, IKAFA, HUKAA HALI IYO HIYO PEKE YAKE; BALI IKIFA, HUTOA MAZAO MENGI. 25 Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele. 26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.

Umeona hapo? Kumbe isipoanguka na kuoza basi itaendelea kubakia katika hali ile ile. Lakini ikikubali kuanguka na kuoza, ardhini, basi itachipuka kama shina, na mwisho wa siku itazaa sana.

Na hapa ndipo waamini wengi, hawataki kuingia gharama. Wanatamani wamzalie Mungu matunda, lakini hawawezi, kwasababu hawajakubali “kufa na kuoza” kwa habari ya huu ulimwengu.

Hawajakubali kuziangamiza nafsi zao kwa ajili ya Kristo. Sasa hiyo ndio inayopelekea wabakie tu kama wakristo wa ghalani,wasioweza kuzalisha chochote.

Yesu alitoa sifa za mbegu yenye kuzaa katika ule mfano wa mpanzi, akasema nyingine ziliangukia njiani, nyingine kwenye miamba, nyingine kwenye miiba, na nyingine kwenye udongo mzuri. Akasema vilizoangukia kwenye udongo mzuri ziliweza kuzaa kwa tendo moja tu la “kuvumilia”

Kuvumilia nini?

Kuvumilia dhiki, na udhia kwasababu ya Kristo, kuvumilia vishawishi vya anasa, udanganyifu wa mali, na shughuli za ulimwengu huu zilizopitiliza, lakini pia kwa unyofu wa moyo walikuwa wanalitendea kazi Neno ili walilolisikia lisiwe bure adui akaliiba ndani yao. (Luka 8:11-15). Hao ndio wakristo wasio wa ghalani, ni wakristo waliokubali kutoka nje, kumletea Bwana matunda.

Je! Na sisi tunaweza kupiga hatua nyingine? Umeokoka ndio, lakini ni lazima wokovu wako uwe na matokeo kwa wengine, uwavute na wengine kwa Kristo, kama wewe ulivyovutwa. Hivyo kubali kumaanisha kumfuata Yesu na kukaa mbali na udunia kwa kadiri uwezavyo.

Jitoe pia kwa Bwana, mali zako, zitumike kuhubiri injili, tenga fungu lako kwa Bwana, penda kusapoti kazi za Mungu, usiwe msomaji tu na kusema Amen!. Onyesha kuwa na wewe ni mtendaji kazi ili thawabu yenu iwe ni moja, na yule mtendaji kazi mwingine.

Bwana atusaidie, tutoke ghalani.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho 

Mada Nyinginezo:

SIKU ILE NA SAA ILE.

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

UFUNUO: Mlango wa 14

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Mego ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Mithali 17:1)

Mithali 17: 1 Afadhali mego kavu pamoja na utulivu, Kuliko nyumba yenye karamu nyingi pamoja na magomvi.


JIBU: Mego ni neno linalotokana na  kitenzi “mega”,(kumega) kitu kilichomegwa, ni kama kimenyofolewa sehemu Fulani kwa  sana. Kwa lugha rahisi tunaweza kusema ni kitu kidogo sana.

Sasa hapo anaposema Afadhali mego kavu, anamaanisha afadhali chakula kidogo sana (Mfano wa mkate mkavu), pamoja na utulivu, au amani, au furaha, kuliko nyumba yenye karamu nyingi pamoja na magomvi, hasira, wivu, fitna, yaani, nyumba ambayo, utapata kila kitu, utakula chakula chenye mboga saba mezani, utakunywa kila aina ya kinywaji, lakini nyuma yake kuna vikwazo, na mafarakano.

Hiyo inatufundisha pia katika mambo ya Maisha, ni heri ufanye kazi mahali utalipwa mshahara mdogo lakini, utapata nafasi ya kutulia na Mungu wako, au utafanya kazi halali itakayokupa amani, kuliko kukimbilia kazi zenye mishara mikubwa, lakini nyuma yake inakukosesha, au haikupi muda wa kutosha kumtafakari Mungu wako.

Na ndio maana sehemu nyingine biblia  inatumia neno “konzi” ikiwa na maana kipimo cha mkono tu, uridhike nacho kuliko vipimo vingi lakini unataabika rohoni na mwilini.

Mhubiri 4:6 “Heri konzi moja pamoja na utulivu, Kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kujilisha upepo”.

Kabla hatujaamua jambo lolote tunapaswa tujihakikishie kwanza usalama wa roho zetu, si kila aina ya fursa inayokuja mbele yetu ni ya kuikimbilia kisa tu inatupa donge nono, au inatupa Maisha mazuri. Wengi wamerudi nyuma kiimani, kama sio kuupoteza wokovu wao kabisa kisa tu tamaa ya “VINGI” au Tamaa ya mali.

Yupo mtu mmoja aliacha kazi ya uchungaji alioitiwa na Mungu, kisa tu haimlipi vizuri, akaingia katika biashara, akaanza kufanikiwa na kuzidi, mpaka akawa anaenda China kuleta mzigo, sikumoja akiwa njiani anaelekea katika miradi yake Daresalaam, akapata ajali mbaya sana, akafa.

Jiulize huko anatapokwenda atakuwa mgeni wa nani?

Hivyo na wewe ridhika na kile unachokipata hata kama ni mego kavu, maadamu  kinakupa amani, na Muda kwa Mungu wako. Ridhika tu na hicho, hapa duniani tunapita.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho 

Mada Nyinginezo:

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Je ni wanyang’anyi wawili waliomtukana Bwana Yesu au mmoja?

Rudi nyumbani

Print this post

MUNGU HAONI SHIDA KUMUHAKIKISHIA MWOVU ULINZI.

Baada ya Kaini kumuua ndugu yake, na Mungu, kumlaani kwa laana ile ya kwamba atakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani, utaona alimwomba Bwana ampunguzie adhabu yake, na baada ya kupunguziwa kwa kutiwa alama, haikuishia hapo,  bado Mungu alimuhakikishia usalama mwingine wa juu Zaidi.  Tusome;

Mwanzo 4:14 “Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.

15 Bwana akamwambia, KWA SABABU HIYO YE YOTE ATAKAYEMWUA KAINI ATALIPIZWA KISASI MARA SABA. Bwana akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga”.

Unaona hapo kwenye mstari  wa 15, Bwana akimuhakikishia ulinzi wa kipekee sana. Jambo ambalo si rahisi mtu mwovu kufanyiwa na mtu yeyote, kwasababu hakuna tendo lolote la kishujaa alilotenda Kaini mpaka alipiziwe kisasi mara saba, kwa yeyote atakayemuua, ni heri ingekuwa ni mara moja, lakini mara saba, hiyo angepaswa afanyiwe mtu mwenye haki.

Tengeneza picha diktekta, ambaye ameshutumiwa kwa mauaji ya maelfu ya watu, kama vile HITLER wa ujerumani, leo hii, unasikia Mungu anasema mtu yeyote atakayemuua Hitler atalipizwa kisasi mara saba, unaweza kudhani Mungu anafurahishwa na maovu. Ndivyo ilivyokuwa kwa Kaini, Mungu haoni shida kumuhakikishia mwovu ulinzi na mafanikio. Hilo tunapaswa tulijue.

Lakini afadhali ingeishia kwa Kaini tu, Tabia yake ya uuaji iliendelea mpaka kwa uzao wake. Utaona yupo mmoja aliitwa, Lameki, yeye alikuwa muuaji kuliko hata baba yake, anasema alimuua mtu kwa kumtia jeraha tu, alimuua mtu kwa kumchubua tu, akiwa na maana mtu aliyemkosea  kwa jambo dogo sana alikuwa  radhi kumuua, bila kujali chochote.

Huku akitumia kivuli kile kile cha baba yake, cha usalama aliohakikishiwa na Mungu, tena na Zaidi, anasema kama ikitokea mtu atataka kumlipizia kisasi kwa uuaji wake, basi akumbuke kuwa Mungu atamlipizia sio tu mara saba, bali mara saba sabini.

Mwanzo 4:23 “Lameki akawaambia wake zake, Sikieni sauti yangu, Ada na Sila; Enyi wake za Lameki, sikilizeni usemi wangu; Maana nimemwua mtu kwa kunitia jeraha; Kijana kwa kunichubua;

24 Kama Kaini akilipiwa kisasi mara saba, Hakika Lameki atalipiwa mara sabini na saba”.

Unaona? Walikuwa wanajiamulia kufanya mauaji tu kama vile kuchinja kuku, kwasababu walijua hakuna laana yoyote itakayowapata,. Hiyo ndio sababu ulimwengu wa kipindi kile ulizidi kuwa mwovu kupitiliza, mpaka ikafikia hatua ya Mungu kusema, mwisho wa kila mwanadamu umefika.

Mwanzo 6:5 “Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.

6 Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.

7 Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya…….

11 Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia ikajaa dhuluma.

12 Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.

13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia.

Lakini siku moja ilipofika Gharika kubwa ilishuka ikauangamiza ulimwengu wote, wakapona tu watu 8, yaani Nuhu pamoja na familia yake. Na adhabu yao haikuishia tu, pale, bado huko kuzimu walipo sasa hivi, wanaendelea na mateso makali yasiyokuwa ya kawaida.

Ndugu yangu, fahamu kuwa Mungu anaweza kukuahidia ulinzi, na usalama, na afya na amani, na furaha, angali bado upo katika dhambi zako, hilo sio jambo gumu  kwake kukupa, liweke tu akilini, angali ukiwa unafanya uchawi wako bado Mungu anaweza kukuhakikishia Maisha ya heri hapa duniani, angali unaua watu, unauza madawa ya kulevya unauza pombe, unazini nje ya ndoa.. Bado Mungu atakuhakikishia ustawi wa mambo yako.

Hivyo usishangae kwanini waovu hawakumbwi na madhara yoyote, tena Zaidi ndio wanafanikiwa na kustarehe kama ulivyokuwa uzao wa Kaini, jinsi ulivyokuwa na mafanikio makubwa duniani, kuliko hata ule uzao wa Sethi lakini mwisho wao ulikuwa ni gharika.

Huu si wakati wa kustarehe katika dhambi, kisa tu hatuoni dhara lolote mbele yetu, tujue kuwa sisi watu wa kizazi hichi ndio tupo katika hatari kubwa ya kukumbana na ghadhabu kali ya Mungu, inayokaribia kuja duniani hivi karibuni, kuliko hata vizazi vingine vya nyuma vilivyotangulia.

Kwasababu maovu tunayoyafanya sasa hivi, yamezidi hata yale ya wakati wa Nuhu, licha ya kwamba sisi tumeshaufahamu ukweli wote na kuiona njia..

Bwana Yesu alisema.

Mathayo 11:23 “Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.

24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Ndugu, Tubu dhambi zako, usipumbazwe na ulinzi wa Mungu, angali upo bado katika dhambi, hizi ni  siku za mwisho, mwisho wa dunia upo karibu sana, dalili zote zimeshatimia, Jiulize UNYAKUO ukipita leo, utakuwa wapi ndugu yangu? Utamweleza nini Kristo siku ile ya hukumu, utamwambia mimi sikusikia injili? Na wale wa Sodoma na Gomora ambao sasahivi wapo kuzimu waseme  nini?

Tafakari Maisha yako, duniani hapa tunapita, na vitu vyote vinapita,. Mgeukia Kristo ayabadilishe Maisha yako leo ili akufanye kuwa kiumbe kipya, kisha uishi  Maisha ya kama mtu anayemsubiria Kristo kweli kweli, na sio kama mtu wa kidunia, acha kudhani kuwa Mungu hayaoni maovu unayotenda.

Bwana atusaidie sote.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho

Mada Nyinginezo:

UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI.

USIOMBE MAOMBI YASIYOKUWA NA MAJIBU NA WALA USIMTUKANE MUNGU.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 2

https://wingulamashahidi.org/2018/07/17/uzao-wa-nyoka/

UFUNUO: Mlango wa 1

Rudi nyumbani

Print this post