Title October 2023

Je! waliokufa kabla ya Bwana Yesu wataokolewaje?

Swali: Je waliokufa kabla ya Bwana Yesu kuja (yaani watu wa agano la kale)wataokolewaje?.. kwamaana tunajua kupitia damu ya Yesu tu! ndio tunapata ukombozi wa hakika wa dhambi, sasa waliokuwa wanaishi katika agano la kale wataokolewaje na ilihali Kristo alikuwa hajafa bado, na damu iondoayo dhambi haijamwagika?.

Jibu: Ni kweli ukombozi unapatikana kupita damu ya Yesu tu!

Lakini ni vizuri kufahamu kuwa Agano jipya halikuja kulifanya agano la kale liwe uongo, badala yake limekuja kulikamilisha agano la kale, kama Bwana wetu Yesu alivyosema mwenyewe katika Mathayo 5:17..

Mathayo 5:17  “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza”

Sasa Ili tuelewe vizuri hebu tutafakari  mfano ufuatao.

Taasisi moja imedahili wanafunzi wake walioingia kupitia mfumo wa makaratasi, kwamba mwanafunzi ili akubalike kujiunga na chuo hana budi kuwasilisha fomu zake katika ofisi ya taasisi hiyo…. Lakini mwaka mmoja baadaye ikabadili mfumo na kuanza kudahili wanafunzi wapya kupitia mfumo wa kieletroniki kwamba ili mwanafunzi akubalike kujiunga na taasisi hiyo hana budi kutumia mfumo wa kielekroniki hata akiwa nyumbani kupitia internet. Na kwamba hakuna mwanafunzi yeyote atakayeweza kupokelewa bila kutumia mfumo huo, kwani ni mrahisi na mwepesi katika kutunza kumbukumbu.

Sasa swali ni je! mfumo huo mpya ulioanza utawafanya wale wanafunzi wa zamani ambao walitumia mfumo wa zamani kuwa si wanafunzi halali tena wa taasisi hiyo?.. au itawafanya wale waliokwisha kuhitimu zamani, waliotumia mfumo wa zamani vyeti vyao kuwa batili?.

Jibu ni la!.. Wataendelea kuwa wanafunzi, isipokuwa watakaojiunga upya hawana budi kutumia mfumo mpya..kwasababu mfumo wa zamani utakuwa umeshabatilika!.

Kadhalika na Agano la kale ni hivyo hivyo…Ulikuwa ni mfumo wa zamani wa kuwasogeza watu karibu na Mungu, lakini ulikuwa na mapungufu mengi!.. Lakini muda ulipofika, ulikuja mfumo bora Zaidi na mwepesi na wa haraka ambao utamwingiza mtu katika ufalme wa Mungu kirahisi na kihakika zaidi, na huo ndio mfumo wa Agano jipya kupitia agano la damu ya Yesu Kristo, na si tena damu ya mafahali na kondoo..kama maandiko yanavyosema katika Waebrania 10:4.

Waebrania 10:4 “Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.”

Na hivyo kulifanya Agano la kwanza liwe chakavu na agano la pili liwe jipya sawasawa na Waebrania 8:13.

Waebrani 8:13  “Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka”

Neno “kuukuu” maana yake ni “kuchakaa”… kwahiyo lilipokuja agano jipya, basi agano la kwanza likafanyika kuwa la kale, lisilotumika tena… hivyo kwasasa halifanyi kazi tena.

Kwahiyo waliokuwepo ndani ya Agano la kwanza kabla ya Bwana Yesu hao watahesabika kuwa watakatifu sawasawa tu waliopo sasa katika agano jipya leo, ndio maana akina Musa, Eliya, Henoko, Ibrahimu, Daudi, Danieli na wengineo wanatajwa kuwa miongoni mwa watakatifu, tena mashujaa wa Imani… ijapokuwa hawakubatizwa! Wala kumwona Masihi..

Lakini baada ya Bwana Yesu kuja na damu yake kumwagika basi wote watakaozaliwa baada ya hapo, hawana budi kulitumia agano jipya, na kuachana na lile la kale…na yeyote atakayejitumainisha kwa agano la kale basi hataweza kuokoka kabisa.

Hiyo ndio sababu kwanini tunapaswa tulijue sana Agano jipya na misingi yake, kwasababu tukianza kuwatanzama watu wa Agano la kale, pasipo kujua misingi ya agano jipya, tutajikuta tunachukua vitu visivyofaa kwa watati wa sasa….kwamfano tukimtazama Daudi na maisha yake na kanuni alizokuwa anatembelea si zote zitatufaa sisi watu wa agano jipya, kwamfano utasoma ijapokuwa Daudi aliupendeza Moyo wa Mungu sana lakini alikuwa na wake wengi na alikuwa na visasi na maadui zake.

Sasa tutachukua na kujifunza Imani ya Daudi, unyenyekevu wa Daudi na mengine mazuri, lakini hilo la kuoa wake wengi, Agano jipya inalikataza, hilo la kulipiza kisasi agano jipya limetuzuia..…hatuna budi kumsikiliza aliye mkuu Zaidi ya Daudi, na Sulemani, na Musa, na Eliya ambaye ni Yesu, anayetajwa kama Mjume wa Agano jipya (katika Waebrania 9:15 na Waebrania 12:24), ambaye anasema kila amwachaye mkewe na kuoa mwingine azini, na ndoa ni mke mmoja, mume mmoja..si Zaidi ya hapo!(Mathayo 19:4), ambaye amesema “tusilipe kisasi” (Mathayo 5:38-39). n.k

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

MJUMBE WA AGANO.

LITURJIA NI NINI? NA JE IPO KIMAANDIKO?.

Biblia ilimaanisha nini iliposema “Mwanamke atamlinda mwanamume” Yeremia 31:22?

JE! ULEVI NI DHAMBI?.

Nini maana ya “Bwana Yesu ni mzaliwa wa kwanza wa waliokufa?”(Ufunuo 1:5)

NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Sukothi ni nini? (Mwanzo 33:17).

Jibu: Tusome,

Mwanzo 33:17 “Yakobo akaendelea mpaka Sukothi. Akajijengea nyumba, akawafanyia makundi yake vibanda. Kwa hiyo jina la mahali pale pakaitwa Sukothi”. 

Tafsiri ya neno “Sukothi” ni “Mahema”.. Hii ni lugha ya kiebrania.

Mahali hapa ni pale ambapo Yakobo alipiga kambi baada ya kutoka Padan-aramu, mji aliokuwepo Labani.(Mwanzo 28:1-2), na alikaa huko Padan-aramu kwa muda wa miaka 21, baada ya kulaghaiwa na Labani kwa muda wote huo.

Akiwa njiani baada ya kutoka kwa Labani alifika mahali ambapo ilimgharimu kutulia kidogo kisha andelee na safari, hivyo badala ya kujenga makazi ya kudumu, yeye akajenga mahema machache tu, kwasababu ya muda kwani bado alikuwa katika safari ya kuelekea Shekemu (Mwanzo 33:18). Hivyo Yakobo akaliita eneo hilo Sukothi kutokana na mahema hayo, na eneo hilo likaendelea kuitwa hivyo kwa vizazi vingi baadaye.

Na eneo la Sukothi kijeografia lipo maeneo ya nchi ya Yordani mpakani na Israeli.

Waamuzi 8:4 “Basi Gideoni akafika Yordani, akauvuka, yeye na hao watu mia tatu waliokuwa pamoja naye, walikuwa wamepungukiwa na nguvu, lakini wawafuatia vivyo.

 5 Naye akawaambia watu wa Sukothi, Tafadhali wapeni mikate hao watu waniandamao; kwa maana wanapungukiwa na nguvu, nami ni katika kuwafuatia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani”.

Kujua ni somo gani lingine tunalipata kuhusu Sukothi?…Fungua hapa >>TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

Kwanini Labani aseme Yakobo ni Mfupa wake na nyama yake?(Mwanzo 29:14)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?

Swali: Je sisi watu wa agano jipya ni lazima kuwa na vipindi vya kuombea mlimani?. Na je huko mlimani Mungu ndioko anakosikia Zaidi maombi kuliko chini?.. msaada!

Jibu: Hakuna agizo lolote katika biblia la mahali rasmi pa kuombea!, kama ni  mlimani au kama ni chini.. Lakini tunaweza kujifunza kupitia watu kadhaa katika biblia jinsi walivyoomba na kisha tunaweza kujifunga kitu.

BWANA YESU MWENYEWE.

Mathayo 14:22 “ Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.

23  Naye alipokwisha kuwaaga makutano, ALIPANDA MLIMANI FARAGHANI, KWENDA KUOMBA. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake”.

Na pia…

Luka 6:12  “Ikawa siku zile aliondoka AKAENDA MLIMANI ILI KUOMBA, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu”.

Soma pia Marko 6:46 na Yohana 6:15, utaona jambo hilo hilo la Bwana kupanda mlimani kuomba, na pia utaona sehemu nyingine alipanda na wanafunzi wake, soma Luka 9:28.

Umeona?.. Kama Bwana Yesu kuna nyakati alikuwa akienda mlimani kuomba, yeye pamoja na wanafunzi wake maana yake si bure!.. Kuna kitu cha ziada katika milima.

Na kitu hiko si kingine Zaidi ya UWEPO WA MUNGU. Milimani kunakuwa na Uwepo wa Mungu zaidi ya mabondeni?. Na kwanini milimani kunakuwa na Uwepo wa Mungu Zaidi ya sehemu nyingine nyingi?.

Ni kwasababu kule juu kunakuwa na utulivu,.. na siku zote utulivu unavuta uwepo wa Mungu, na milimani ni sehemu ambazo hazina usumbufu hivyo ni rahisi mtu kuzama katika roho kuliko akiwa chini penye masumbufu mengi na mwingiliano wa Sauti nyingi.

Umewahi kujiuliza ni kwanini minara ya simu huwa inapelekwa juu katika milima na haiwekwi mabondeni?.. Ni kwasababu kule juu network inapatikana vizuri Zaidi ya chini, kwasababu hakuna vizuizi vingi vya kuzuia mawimbi kusafiri. Sasa kama wanadamu wameiona hiyo siri iliyopo juu ya milima, vipi kwetu sisi wakristo?

Si kwamba Mungu hatakusikia ukiomba mabondeni, atakausikia lakini ule uwepo wa Mungu kwako unaweza usiupate vizuri kuliko kama ungeenda kuomba sehemu iliyoinuka (Milimani). Ndio maana utaona mtu anakuwa mzito kuomba, pasipo kujua chanzo ni nini?.. Wakati mwingine si mapepo!, bali ni mazingira tu!… Badili mazingira na utaona jinsi utakavyozama katika roho na maombi!.

Kwahiyo kama wakristo ambao pia ni mwanafunzi wa biblia, ni lazima tuwe na vipindi vya kupanda mlimani kuomba!. Kama mahali ulipo hapana milima, basi linaweza lisiwe jambo la lazima sana, lakini kama ipo basi tenga muda wa kufanya hivyo mara chache chache na utaona matokeo makubwa sana na vile vile utaona utofauti na utafungua mlango mpana sana wa kupokea mafunuo kutoka kwa Baba.

Bwana akubariki.

Marana tha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

UTAONA MAMBO MAKUBWA KULIKO HAYA.

AKIJUA YA KUWA ANA WAKATI MCHACHE TU”.

Fahamu Namna ya Kuomba.

KUNA AINA NGAPI ZA MAOMBI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu aikabidhi roho yake mikononi mwa Baba (Luka 23:46)?

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 43..

Luka 23:44  “Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda,

45  jua limepungua nuru yake; pazia la hekalu likapasuka katikati.

46  Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU.

47  Alipokwisha kusema hayo alikata roho. Yule akida alipoona yaliyotukia, alimtukuza Mungu, akisema, Hakika yake, mtu huyu alikuwa mwenye haki”.

“Mikononi mwako naiweka roho yangu”… haya yalikuwa ni maneno ya Mwisho ya Mwokozi wetu Yesu Kristo alipokuwa pale msalabani?.. lakini swali? Ni kwanini aseme hivyo? Je kulikuwa na ulazima wowote  wa yeye kusema vile, na sisi je tunafundishwa kusema maneno kama hayo tunapokaribia hatua za kumalizia safari zetu za maisha?

Kabla ya kujibu, ni muhimu kufahamu kuwa kabla ya Bwana Yesu kufa na kushuka kuzimu na kupewa zile funguo za Mauti, sehemu ya wafu haikuwa salama (maana yake roho za watatakatifu bado hazikuwa salama hata baada ya kufa).

Ndio maana utaona hata Nabii Samweli ambaye alikuwa ni mtu wa haki sana mbele za Mungu, lakini baada ya kufa kwake, yule mwanamke wa Endori aliyekuwa mganga aliweza kumtoa kuzimu na kumpandisha juu kichawi.

1Samweli 28:7 “Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, nipate kumwendea na kuuliza kwake. Watumishi wake wakamwambia, Tazama, yuko mwanamke mwenye pepo wa utambuzi huko Endori. 

8 Basi Sauli akajigeuza, na kuvaa mavazi mengine, kisha akaenda, yeye na watu wawili pamoja naye, wakamfikilia yule mwanamke usiku; akasema, Tafadhali unibashirie kwa utambuzi, ukanipandishie yeye nitakayemtaja kwako. 

9 Yule mwanamke akamwambia, Angalia, unajua alivyofanya Sauli, jinsi alivyowakatilia mbali hao wenye pepo wa utambuzi na wachawi katika nchi; mbona basi wanitegea tanzi uhai wangu, ili kuniua?

10 Naye Sauli akamwapia kwa Bwana, akasema, Aishivyo Bwana, haitakupata adhabu yo yote kwa jambo hili. 

11 Ndipo yule mwanamke aliposema, Je! Ni nani nitakayekupandishia? NAYE AKASEMA, NIPANDISHIE SAMWELI”.

Umeona hapa? roho ya nabii Samweli inataabishwa na wachawi hata baada ya kufa kwake.. Ndio maana utaona Samweli baada ya kupandishwa juu alimlalamikia Sauli kwanini anamtaabisha.

1Samweli 28:15 “Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Mbona umenitaabisha mimi, hata kunipandisha juu?….”

Kwasababu hiyo ndio maana Bwana Yesu akaikabidhi roho yake kwa Baba, kama tu alivyokuwa anazikabidhi kazi zake na safari zake kwa Baba kipindi akiwa hai, vivyo hivyo alifahamu kuwa kuna umuhimu wa kufanya hivyo pia kwaajili ya roho yake baada ya kufa.

Lakini tunaona alipokufa, Baba alimpa funguo za KUZIMU na MAUTI sawasawa na Ufunuo 1:17

Ufunuo 1:17 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18  na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU”

Maana yake kuwa kuanzia wakati wake mpaka mwisho wa dunia, shetani hatakuwa na uwezo tena wa kuzitaabisha roho za watakatifu waliokufa, hivyo Bwana Yesu sasa ndiye mwenye mamlaka hayo juu ya roho zote za waliokufa na walio hai.

Warumi 14:8 “Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana.

9 Maana Kristo alikufa akawa hai tena KWA SABABU HII, AWAMILIKI WALIOKUFA NA WALIO HAI PIA”.

Kwahiyo kwasasa hatuna hofu tena ya kwamba baada ya kifo roho zetu zitataabishwa, bali tukifa basi uhai wetu (roho zetu) zinafichwa mbali na adui. Na sehemu hiyo ya maficho ambayo shetani hawezi kuifikia ni Paradiso, mahali pa mangojeo na raha, huku tukiingoja ile siku ya ahadi, ya unyakuo wa kwenda mbinguni. Haleluya!.

Kwahiyo kwasasa hatuna maombi ya kuzikabidhi roho zetu kwa baba wakati wa kufa, kwasababu tayari Kristo anazo funguo za mauti na kuzimu, bali tunapaswa wakati huu sasa tulio hai tuyakabidhi maisha yetu kwake, na kuishi maisha ya kumpendeza,  ili tutakapomaliza safari ya maisha yetu basi tujikute tupo sehemu salama, kwasababu hatujui ni saa ipi tutaimaliza safari yetu ya maisha hapa duniani.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

JIWE LILILO HAI.

ORODHA YA IMANI POTOFU- Sehemu ya 1.

Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?

Kwanini Bwana Yesu alisema pale msalabani naona kiu?

Rudi nyumbani

Print this post

MTAKENI BWANA NA NGUVU ZAKE.

Jina la Bwana YESU KRISTO, Mkuu wa uzima, libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia, neno la Mungu wetu lililo taa na mwanga wa njia yetu (Zab.119:105)

Biblia inatufundisha kuwa TUMTAKE BWANA na NGUVU ZAKE.

Zaburi 105: 4 “MTAKENI BWANA NA NGUVU ZAKE, Utafuteni uso wake sikuzote”. 

Wengi tunaishia “Kuzitaka tu nguvu za Bwana” …. lakini biblia hapa inatufundisha tumtake Bwana pamoja na nguvu zake, maana yake mambo hayo mawili yanaenda sambamba…

Unaweza kuwa na nguvu za Bwana, lakini usiwe na Bwana kabisa!, utauliza kwa namna gani?.

Bwana Yesu alisema, wengi watakuja siku ile na kusema Bwana hatukufanya miujiza mingi kwa jina lako?, lakini yeye atasema “sikuwajua kamwe”.

Mathayo 7:22  “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?.

23  Ndipo nitawaambia dhahiri, SIKUWAJUA NINYI KAMWE; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Nataka uone hapo anaposema “sikuwajua kamwe”.. Neno “kamwe” maana yake ni kwamba hajawahi kabisa kuwa na mahusiano nao, katika kipindi chote na maisha yao..maana yake tangu wakiwa duniani Bwana hakuwajua watu hao, ingawa walikuwa wanazo nguvu za Mungu zikitembea nao,  walikuwa na nguvu za Mungu za kutoa pepo, za kufanya miujiza mingi, lakini hawakuwa na Mungu katika maisha yao.

Sasa biblia inatufundisha tumtake “Bwana na Nguvu zake”, cha kwanza tumatake yeye Bwana, halafu cha pili ndio kiwe nguvu zake!.

Sasa tunamtakaje Bwana na tunampataje Bwana?..Tunampata Bwana kwa kuyafanya mapenzi yake.

Na mapenzi ya Mungu ni yapi?

1Wathesalonike 4:3 “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;

4  kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

5  si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.

Na tunatakaswa kwa kumwamini Bwana Yesu Kristo, ambapo Imani hiyo inazaa toba na ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU KRISTO kwaajili utakaso wa dhambi (Matendo 2:38) . Kwa kufanya hayo basi utakuwa umemtaka Bwana, na yeye ataingia katika maisha yako, na atadhihirisha neema yake kwako pamoja na nguvu zake.

Lakini usitangulize kuzitafuta nguvu za Mungu na huku yeye hayupo nawe!.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSIMAMA NA KUFUNDISHA/ KUHUBIRI

USIMPE NGUVU SHETANI.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

KUOTA UPO KANISANI.

Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana 1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;

SWALI: Bwana Yesu asifiwe naomba kufahamu maana ya hili andiko;

1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima”

JIBU: Kwa kawaida mtoto mchanga anakuwa kama mjinga, haelewi mambo mengi, anachofahamu ni kile tu kilichopo nyumbani, mambo mengine ya nje, hayajui, na ndicho kinachomfanya asijisumbue na hayo mengine, ambayo watu wazima wanayasumbukia,. Vivyo hivyo na Mungu anataka katika suala la uovu, tuwe hivyo. Kama wajinga, hatujui kinachoendelea, hatuna maarifa nayo, hatuwezi kuyaelewa. Na hiyo itatufanya tuwe salama.

Kwamfano ukiulizwa habari za nyimbo Fulani mpya za kidunia zilizotoka, huna taarifa nazo, Ukiulizwa habari za ligi za mipira, ni kama taarifa usizozielewa, ukisemeshwa na mambo ya kubeti, ni kama mtu anazungumza na wewe  kwa lugha za mafumbo.

 Ndio maana andiko hili linasema hivyo;

1Wakorintho 16:19b  “…lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya”

Kutokujua kila kitu katika huu ulimwengu sio dhambi, na wala hilo halitakuzuia uishi vema. Hivyo tunapaswa tuchuje, ni nini kinatufaa na kipi kisichotufaa, Vile visivyotufaa tuviweke kando, tuwe watoto katika hivyo, lakini vile vitujengavyo, ambalo ni NENO LA MUNGU, basi tuwe watu wazima. Tulijue sana hilo kwasababu ndio uzima wetu ulipo.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

Nini maana ya vifungeni viuno vya Nia zenu? (1Petro 1:13)

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)

Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)

Nitajuaje kuwa nimesamehewa dhambi zangu?

Rudi nyumbani

Print this post

Rhema ni nini, katika biblia?

SWALI: Nimesikia hili neni Rhema, likitajwa sana Kwa watumishi na sehemu mbalimbali, naomba nifahamishwe maana yake Nini, mbona silioni kwenye biblia?


JIBU: Ni vema kutambua kuwa Biblia, katika eneo la agano jipya sehemu kubwa imeandikwa kwa lugha ya kiyunani. Hivyo Kuna baadhi ya maandishi ambayo tukiyasoma katika lugha nyingine mfano kwenye yetu hii ya kiswahili, tunaweza kuona yalimaanisha jambo lile lile moja lakini tukirudi kwenye lugha ya asili ya kiyunani yalimaanisha maana zaidi ya Moja.

Kwamfano, tunapokutana na hili Neno “NENO”. kwenye tafsiri yetu ya kiswahili, Mahali pote limeandikwa hivyo hivyo tu “Neno” likimaanisha Neno la Mungu.

Lakini tukirudi  kwenye lugha ya asili ya kiyunani zipo sehemu limelitajwa kama “Logos”na sehemu nyingine kama “Rhema”

Logos ikiwa na maana Neno la Mungu la Daima/ wazo la Mungu/mpango wa Mungu ulioandikwa  na pia kama Yesu Kristo mwenyewe, ambaye ndio Neno lililofanyika mwili.

Lakini ‘Rhema’: maana yake ni “Neno lililosemwa na Mungu” . Ni neno la wakati husika, sio la daima.

Mfano wa maandiko yanayolitaja Neno kama Logos ni haya: Yohana 1:1-18, Yakobo 1:22, Waebrania 4:12. N.k

Na mfano wa maandiko yanayolitaja Neno la Mungu kama Rhema ni haya;

Mathayo 4:3-4

[3]Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. [4]Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

Hapo Bwana aliposema, “ila Kwa Kila Neno litokalo katika kinywa Cha Bwana”..alimaanisha Neno lisemwalo na Bwana.. mfano wa Eliya alipomwambia yule mwanamke mjane, Bwana asema hivi; “lile pipa la unga halitapinguka, Wala Ile chupa ya mafuta haitaisha”. (1Wafalme 17:14). Halikuwa Neno ambalo lilitumika Kwa wakati wote, ambalo hata sasa tunaweza litumia sisi, Bali la wakati ule ule tu, amefunuliwa, akalisema na ikiwa hivyo.

Lakini ‘Rhema’ ni yaliyonenwa Kwa wakati huo tu..tofauti ya Yale yaliyokuwa Daima.

Neno lingine ambalo linasomeka kama Rhema katika biblia,. Ni wakati ule mitume wamehangaika usiku kucha kutafuta samaki, lakini kulipokucha Yesu akawaambia watweke.mpaka vilindini wakavue. Petro akasema maneno haya;

Luka 5:5

[5]Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.

Aliliamini Neno lililosemwa na Bwana (na ikiwa vile).

Ili kuelewa vizuri tunaweza kusema  “logos” ni BIBLIA TAKATIFU, na Rhema’ ni Neno mtu analofunuliwa Kwa kipindi Fulani.

JE! MUNGU ANASEMA NA SISI HATA SASA KAMA RHEMA?

Ni kweli Mungu ameshatupa njia yake kuu ya kusema na sisi, ambayo ni Kwa kupitia Biblia. Lakini pia bado Mungu anasema nasi, na kutushushia Neno lake Kwa wakati husikia litufae.

Tuwapo katika kanisa. Mungu hutumia karama mbalimbali, kusema nasi, au kutupa ujumbe wake. Anasema kutumia unabii au fundisho, au Neno la hekima, au maono, au ndoto, kutuwasilishia Neno lake.

Lakini pia ni lazima tujue kuwa Neno hilo lililofunuliwa ni sharti lisikinzane na Neno lake lililoandikwa. Vyote viwili vikichanganyikana huleta matokeo makamilifu na kutufanya tumwone Mungu katika uhalisia wake zaidi katika maisha yetu, kwasababu yeye Yu hai.

Lakini ipo hatari kubwa sana. Kwani katika siku hizi za mwisho wapo baadhi ya watu wanalichukua Neno liliokuwa kama Rhema, na kulifanya logos yao. Ndio hapo wanaposoma Bwana Yesu alitema mate chini akachanganya na udongo, akampaka mtu machoni akaona, hivyo na wenyewe wanafanya hivyo Kwa kisingizio kuwa andiko limeruhusu. Au wanapomsoma mtume Paulo anatoa leso yake, Kisha watu wanapona kupitia Ile, na wenyewe wanafanya hivyo hivyo, wakisema andiko limeruhusu. Hawajui kuwa ulikuwa ni ufunuo wa wakati ule ambao si agizo kuu, ni Rhema’. 

Na madhara ya jambo hili ndio linageuka kuwa ibada ya sanamu. Tunayo mifano kadhaa katika biblia ya watu ambao waligeuza Rhema kuwa Logos, ikawapelekea kuingia katika laana. Kipindi Wana wa Israeli wakiwa jangwani, walipomkosea  Mungu alimwagiza Musa aunde nyoka wa shaba, ili Kila amtazamaye apone. Na kweli ilikuwa vile. Lakini baada ya pale haikuwa sheria mama kama vile torati, kana kwamba waendelee kufanya vile.  lakini tunaona baadhi ya watu walikuja kuifanya kama ndio sehemu Yao ya ibada ya uponyaji Kwa Mungu,.mpaka Mungu akachukizwa ikawapelekea kupelekwa tena utumwani Babeli, ikiwa kama mojawapo ya sababu.(2Wafalme 18:4)

Agizo letu la wakati wote ni JINA LA YESU TU! ndio logos yetu Bwana aliyotuagiza tutumie, wakati wote. Ikiwa hujafunuliwa kutumia kisaidizi/kiambatanishi kingine basi usifanye kwani huyo sio Mungu nyuma yake. Tegemea Biblia zaidi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

Miimo ni nini na kizingiti ni nini?

Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post

Kujikinai/kukinai ni nini?

Neno hilo kama linavyotumika kwenye biblia..linamaanisha aidha mojawapo ya mambo haya matatu:

  1. Kushiba Hadi kufikia hatua ya kutokipenda Tena kile ulichokipokea Mwanzo.
  2. Kuwadharau wengine Kwa kufanya mambo ambayo huruhusiwi kuyafanya
  3. Kujigamba/kujiona wewe unajitosheleza Kwa HAKI yako.

1. Kwamfano katika vifungu hivi limetumika kwa tafsiri ya kushiba,..

Mithali 27:7

[7]Nafsi iliyoshiba hukinai sega la asali;  Bali nafsi yenye njaa huona kila kitu kichungu kuwa kitamu.

Mithali 25:17

[17]Mguu wako usiingie katika nyumba ya jirani yako ila kwa kiasi;  Asije akakukinai na kukuchukia.

Mhubiri 1:8

[8]Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.

2). Lakini pia vifungu hivi, vinaeleza kukinai kama kuonyesha kudharau wengine, kwa kukaidi maagizo kwa makusudi.

Kumbukumbu la Torati 17:12

[12]Na mtu afanyaye kwa kujikinai, kwa kutomsikiza kuhani asimamaye hapo kwa kumtumikia BWANA, Mungu wako, au mwamuzi, na afe mtu huyo; nawe utauondoa uovu katika Israeli.

Soma pia.. Kutoka 21:14

3) Halikadhalika mahali ambapo kunaonesha kujikinai kama kujihesabia haki mwenyewe ni hapa

Luka 18:9-14

[9]Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.

[10]Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.

[11]Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.

[12]Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.

[13]Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.

[14]Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

Soma pia 2Petro 2:11, 

Hivyo na sisi hatupaswi kuwa na sifa hizo mioyoni mwetu. Uendapo mbele za Bwana, Acha kujihesabia haki, Bali jinyenyekeze penda kuomba rehema Kwa Bwana, zaidi ya kueleza sifa zako..na hatimaye Mungu atakuridhia, kwasababu Mungu anawapinga wenye kiburi na kuwapa neema.wanyenyekevu.

Amen

Je! Umeokoka? Ikiwa bado na unapenda Kristo akusamehe dhambi zako zote, na akupe uzima wa milele. Basi fungua hapa ili uweze kupata mwongozo sala ya toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

Mawaa ni nini? Kama tunavyosoma katika biblia?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

Tofauti ya deni na dhambi ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

“Romans road to salvation”

Njia ya wokovu ndani ya kitabu Cha Warumi ni Nini? 

Ni mpango wa wokovu wa mwanadamu, ambao umeainishwa vyema kutoka katika kitabu Cha Warumi.

Kitabu hichi kinaeleza jinsi mtu anavyoweza kuupokea wokovu kutoka Kwa Mungu.

Hivyo ikiwa wewe bado hujaufahamu mpango wa Mungu kwako, wa namna ya kuupokea wokovu basi kitabu hichi kimeanisha vifungu ambavyo vinakuonesha ni jinsi gani utaweza kuupokea.

Lakini pia ikiwa wewe hujui ni wapi pa kuanzia unapokwenda kuwashuhudia watu habari za wokovu, basi kitabu hichi kinakupa mwongozo wa namna ya kuwahubiria wengine habari njema. Na vifungu muhimu vya kusimamia..

Hivi ni vifungu “mama”

Cha kwanza: Warumi 3:23

Warumi 3:23

[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;

Tuendapo Kwa Mungu, lazima tujue hakuna mwenye haki hata mmoja sote Tumepungukiwa na utukufu wa Mungu. Tumetenda dhambi, Vilevile ikiwa wewe ni mhubiri/mshuhudiaji, huna budi kumuhubiria mtu jambo hilo, kwamba hakujawahi kutokea mwema hapa duniani. Hivyo wote tunauhitaji mpango wa Mungu wa wokovu katika maisha yetu.

Kifungu Cha pili: Warumi 6:23

[23]Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.

Hapa, Mungu anatuonesha, matokeo ya kudumu katika dhambi zetu, ambazo wote tulikuwa nazo, kuwa ikiwa tutaendelea kubaki katika Hali hiyo hiyo basi tutakutana na mauti ya milele, lakini tukipokea zawadi ya Mungu basi tutapata uzima wa milele.

Kifungu Cha Tatu:  Warumi 5:8

[8]Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.

Kwamba sasa hiyo zawadi ya Mungu ambayo itapelekea uzima wa milele ni Yesu Kristo, yeye ndiye aliyetolewa na Mungu kuzichukua dhambi zetu zote, kwa kifo cha pale msalabani. Pale tuliposhindwa sisi wenyewe basi Yesu alikuja kutusaidia kuchukua makosa yetu.

Kifungu Cha nne: Warumi 10:9-10.

Hiki sasa kinaeleza Namna ya kuupokea wokovu;

Warumi 10:9-10

[9]Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

[10]Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.

Kwa kuamini kwetu kuwa Yesu Yu hai, na kwamba anakomboa wanadamu, na vilevile kumkiri Kwa kinywa kuwa ndiye Bwana na mwokozi wetu. Basi tunaupokea msamaha huo wa dhambi Bure, bila gharama yoyote. Na deni letu la dhambi linakuwa limefutwa tangu huo wakati

Hivyo ni sharti ujue kuwa msamaha wa dhambi hauji Kwa matendo Yako mema, Bali unakuja Kwa kuikubali kazi ya Yesu msalabani iliyofanyika Kwa ajili ya ukombozi wako.

Halikadhalika Wewe kama mshuhudiaji vifungu hivi viwepo kichwani mwako.

Kifungu Cha tano cha mwisho: Warumi 5:1

[1]Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,

Maana yake ni kuwa baada ya mtu kumkiri Kristo, na kumkubali kama Bwana na mwokozi wake. Basi anapaswa awe na AMANI na Mungu kwasababu hakuna mashtaka yoyote ya adhabu juu yako. Hakuna hukumu yoyote ya mauti ipo juu yake.

Huo ndipo mpango wa awali wa wokovu wa Mungu Kwa mwanadamu. Ambapo tunapaswa kufahamu kama ulivyoanishwa katika  kitabu hichi Cha Warumi.

Kisha baada ya hapo tunawafundisha watu kuitimiza haki yote au kusudi lote la Mungu juu yetu, Ikiwemo ubatizo wa maji, na ule wa Roho Mtakatifu.

Ikiwa bado hujaokoka, na utapenda kuupokea msamaha wa Yesu Bure maishani mwako, basi Unaweza kuwasiliana na sisi Kwa namba uzionazo chini ya chapisho hili kwa ajili ya mwongozo huo Bure. Vilevile na Ule wa ubatizo.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?

Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?

USIISHIE TU KUPATA HAKI, BALI PATA NA WOKOVU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je! ile habari ya Herode kutaka kumwua Yohana mbatizaji inajichanganya?(Mathayo 14:5 na Marko 6:20).

Swali: Katika Mathayo 14:5 tunasoma kuwa Herode alitaka kumwua Yohana mbatizaji, lakini tukirudi katika  Marko 6:20 tunasoma habari nyingine tofauti kuwa Herode hakutaka kumwua Yohana mbatizaji, badala yake alimweshimu na kumwogopa na kumwona kama Nabii..je ni habari ipi iliyo sahihi kati ya hizo mbili?

Jibu: Awali ya yote tusome mistari hiyo..

Mathayo 14:3 “Maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga, akamtia gerezani, kwa ajili ya Herodia, mke wa Filipo nduguye.

4 Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye.

5 NAYE ALIPOTAKA KUMWUA, ALIWAOGOPA WATU, MAANA WALIMWONA YOHANA KUWA NABII.

Hapa ni kweli tunasoma kuwa Herode alikusudia kumwua Yohana.. Lakini tusome tena Marko 6:17-20

Marko 6:17 “Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu, akamkamata Yohana, akamfunga gerezani, kwa ajili ya Herodia, mkewe Filipo ndugu yake, kwa kuwa amemwoa;

18  kwa sababu Yohana alimwambia Herode, Si halali kwako kuwa na mke wa nduguyo.

19  Naye yule Herodia akawa akimvizia, akataka kumwua, asipate.

20  MAANA HERODE ALIMWOGOPA YOHANA; AKIMJUA KUWA NI MTU WA HAKI, MTAKATIFU, AKAMLINDA; NA ALIPOKWISHA KUMSIKILIZA ALIFADHAIKA SANA; NAYE ALIKUWA AKIMSIKILIZA KWA FURAHA.”

Hapa tunasoma Herode hakutaka kumwua Yohana, kwasababu alimwogopa na kuamini kuwa ni mtu wa haki. Sasa swali je! Habari hizi mbili zinajichanganya?

Jibu ni La! Hazijichanganyi!!, kwasababu waandishi wa vitabu hivyo walivuviwa na Roho Mtakatifu na pia biblia kamwe haijawahi kujichanganya, vinginevyo ingekuwa ni kitabu cha uongo!, lakini tunaona ni kitabu chenye nguvu na kilichojaa mafunuo yaliyo halisi, hivyo kinachojichanganya ni fahamu zetu na tafakari zetu katika kuyaelewa maandiko na si biblia.

Sasa tukirudi katika hiyo habari ya Herode,  tukianzia mistari ya juu katika vitabu vyote viwili, tunasoma Mfalme Herode (Antipa) alisikia habari za Yohana Mbatizaji na mahubiri yake, na Yohana katika kuhubiri kwake alimtaja Herode na kumwambia si halali yeye kuwa na mke wa ndugu yake (Mathayo 14:3-4).

Lakini kwasababu Herode ni mtu wa heshima, na asingetaka masuala yake ya kindoa yachafuliwe hadharani tena na mtu aliye myahudi, alitafuta njia ya kumwua Yohana Mbatizaji, lakini alikosa kwasababu muda wote Yohana alikuwa akizungukwa na watu, (Mathayo 14:5) na wayahudi wote walimwamini Yohana kama nabii wa Mungu, hivyo laiti kama Herode angechukua maamuzi ya haraka ya kumwua Yohana mbele ya umma ingekuwa ni hatari kwa ufalme wake, kama tu jinsi mafarisayo walivyoogopa kumkosoa Yohana mbele ya umati, kwa hofu ya kupigwa mawe (Luka 20:6), au kama jinsi wakuu wa makuhani walivyoogopa kumkamata Bwana Yesu wamwue, kwaajili ya makutano (Luka 22:2).

Hivyo njia aliyotumia Herode ni kumkata Yohana na kumfunga gerezani, ikiwa nia yake ni kumtenga na makutano na mwisho aweze kufanikisha nia yake ya kumwua. Na wakati huo huo mkewe Herodia, alikuwa akimsapoti Herode katika mpango huo.

Lakini tunavyozidi kuisoma habari hiyo tunaona Herode alikuja kubadilisha mawazo baadaye.. kwani baada ya kumtia Yohana mbatizaji gerezani, kuna vipindi ambavyo havijatajwa huenda Herode alikuwa anaenda gerezani kumsikiliza Yohana, au alikuwa analetewa mahubiri ya Yohana kutoka gerezani (kwasababu hata Yohana alivyokuwa gerezani bado wanafunzi wake walikuwa wanaweza kwenda kumtembelea na kumpelekea habari au yeye mwenyewe kuwatuma wapeleke habari, soma Luka 7:18-20).

Na hayo yakamfanya  Herode abadili mtazamo na maamuzi, na kumwamini kuwa ni mtu wa Mungu, ijapokuwa anamweleza maneno ya kumchoma na kumkera (Soma Marko 6:20), hivyo akaamua kubadili mawazo na kufikiri kutomuua!.

Lakini mkewe Herodia akawa na wazo lile lile la kumuua, na Herode akawa anatafuta njia ya kumlinda Yohana asiuawe na Herodia (Marko 6:19). Wakiwa katika hayo mazingira, Herodia akapata nafasi siku ile ya sikuku ya kuzaliwa kwa Herode ambapo alimtumia binti yake kukitaka kichwa cha Yohana Mbatizaji, na kutokana na nadhiri Herode alizoziweka mbele ya binti yake na mbele ya umati wote wa watu, alishindwa kukataa..kwani ingeudhoofisha ufalme wake, hivyo akaruhusu Yohana akakatwe kichwa ingawa si kwa mapenzi yake!.

Mathayo 14:6 “Hata ilipofika sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti Herodia alicheza mbele ya watu, akampendeza Herode.

7  Hata akaahidi kwa kiapo ya kwamba atampa lo lote atakaloliomba.

8  Naye, huku akichochewa na mamaye, akasema, Nipe hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.

9  Naye mfalme akasikitika; lakini kwa ajili ya viapo vyake, na kwa ajili ya wale walioketi chakulani pamoja naye, akaamuru apewe;

10  akatuma mtu, akamkata kichwa Yohana mle gerezani”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba… Herode alibadili mawazo yake juu ya Yohana, hivyo biblia haijichanganyi.

Lakini pia ni funzo gani tunalipata katika habari hii ya Herode na Herodia mke wa ndugu yake?

Funzo kuu tunalolipata ni kuwa si halali mtu kumwacha mke wake au mume wake na kwenda kuoa au kuolewa na mwingine.

Luka 16:18 “Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Je! habari ya muda aliotawala Mfalme Yekonia inajichanganya? (2Wafalme 24:8 na 2Nyakati 36:9).

Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Yohana mbatizaji alibatizwa na nani?

Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?

MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post