Title 2023

Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?

Jibu: Tuanzie kusoma ule mstari wa 3

Wagalatia 2:3 “Lakini Tito aliyekuwa pamoja nami, naye ni Myunani, hakulazimishwa kutahiriwa.

4  BALI KWA AJILI YA NDUGU ZA UONGO WALIOINGIZWA KWA SIRI; AMBAO WALIINGIA KWA SIRI ILI KUUPELELEZA UHURU WETU TULIO NAO KATIKA KRISTO YESU, ILI WATUTIE UTUMWANI;

5  ambao hata saa moja hatukujitia chini yao, ili kwamba kweli ya Injili ikae pamoja nanyi.”

Hapo kuna mambo matatu (3).. NDUGU WA UONGO, 2) WALIINGIA KWA SIRI, na 3) KUUPELELEZA UHURU.

1.NDUGU WA UONGO.

Watu waliookoka waliitwa NDUGU, na hata leo wanaitwa hivyo hivyo “Ndugu”, lakini wapo Ndugu wa Kweli na pia wapo wa “Uongo”. Ndugu wa kweli ni wale waliookoka kikweli kweli, ambao wapo katika kundi au kusanyiko katika Nia ya KRISTO na si kwaajili ya kutafuta mambo yao wenyewe (1Wakorintho 16:20 na Wagalatia 1:2).

Lakini “Ndugu wa Uongo” Hao ni watu ambao wanajiingiza katika kanisa, ikiwa Nia yao si kumtafuta Kristo wala kumtumikia bali kutafuta mambo yao mengine kama Fedha, au Fursa Fulani, na wengine kuupeleleza uhuru wa wakristo na wengine ni mawakala kabisa wa Ibilisi, wanajiunga kwa lengo la kuliharibu kundi na kulisambaratisha. Mfano wa hao ndio wale Paulo aliwaozungumzia katika waraka kwa Wafilipi..

Wafilipi 3:17 “Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi.

18  Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;

19  mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.

20  Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo”.

Makundi haya ya Ndugu wa Uongo, yamesambaa katika nafasi zote, kuanzia Wachungaji, Mitume, manabii, waimbaji, mpaka washirika/waumini.

2. WANAJIINGIZA KWA SIRI

Kundi hili la Ndugu wa Uongo, huwa hawajiingizi kwa wazi bali kwa siri, maana yake ni kwamba wanajigeuza na kufanana na Ndugu wa kweli.. lakini ndani yao wanajua ni nini wanatafuta sawasawa na maandiko yanavyosema..

2Wakorintho 11:13  “Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.

14  Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.

15  Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”

3. KUUPELELEZA UHURU.

Sasa ni Uhuru gani ambao Wakristo wanao?.. Jibu: Ni uhuru unaotuweka mbali na utumwa wa Sheria… Katika Ukristo hatuna sheria za kutahiriwa, kwamba ni lazima mtu atahiriwe au asitahiriwe ndipo akubaliwe na Mungu, vile vile na sheria nyingine zote kama kushika sabato na kushika miezi na sikukuu, kuna aina fulani tu ya chakula n.k hizo zote maandiko yanasema tumewekwa huru nazo..

Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

17  mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo……………………..

20 Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani,

21  Msishike, msionje, msiguse;

22  (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu?

23  Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili”.

Sasa walikuwepo wayahudi ambao wanajiingiza katika kanisa la Kweli la Kristo, si kwa lengo la kumtumikia Bwana, bali kwa lengo la kuwatwika watu mzigo wa kushika sabato, na mwandamo wa mwezi na sikukuu za kiyahudi.

Hata sasa wapo watu baadhi ambao wengine wanatenda mfano wa hayo kwa kujua au kwa kutokujua, mfano mapokeo ya kushika sabato yanauua uhuru wetu katika Kristo, mapokeo ya kutahiriwa yanaua uhuru wetu katika Kristo n.k

Hivyo hatuna budi kuzipima roho, si kila pokeo ni la kupokea.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx

Mada Nyinginezo:

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).

Rudi nyumbani

Print this post

Kama Kristo alizichukua dhambi zetu na kutusamehe kwanini kila siku tunatubu?.

Jibu: Ni kweli Kristo alizichukua dhambi zetu kama biblia inavyosema katika kitabu cha Petro..

1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.

Lakini hiyo haimaanishi kuwa tumeshakamilika asilimia mia kwamba hatutakuwa na kasoro zozote kuanzia hapo na kuendelea…Kasoro chache chache na madhaifu machache chache bado tutaendelea kuwa nayo mpaka siku tutakapopata ukombozi wa miili yetu (Waefeso 4:30).

Wakati parapanda ya mwisho itakapolia hapo ndipo tutapata ukombozi wa miili yetu, na tutakuwa wakamilifu asilimia zote kwasababu tutapewa miili mingine isiyo na kasoro wala madhaifu.. lakini sasa ulimwenguni bado tupo katika mapambano, bado tupo vitani, bado ibilisi yupo, bado tutapitia vipindi vya kukosea vidogo vidogo, lakini si vya kutuangusha kabisa!!.. Kama kile Petro alichopitia wakati anakutana na Paulo kule Antiokia (Soma Wagalatia 2:11-14).

Vile vile tutapitia vipindi vya kuudhiwa, na kupata hasira, tutapitia vipindi vya kukosea kuongea, kukosea kutenda, tutapitia vipindi pia vya kuwakosa wengine pasipo kujua au kwa kujua, tutapitia vipindi vya kumkosa Mungu kwa kujua au kwa kutokujua n.k.. sasa kwa kasoro hizo zote tunazozibeba ni lazima tuwe watu wa kuomba rehema na toba mara kwa mara ili muda wote tudumu katika usafi na pia Bwana anyooshe mapito yetu..

Hiyo ndiyo sababu pia Bwana Yesu akatufundisha kuomba toba na rehema kila mara..

Luka 11:1 “Ikawa alipokuwa mahali fulani akiomba, alipokwisha, mmoja katika wanafunzi wake alimwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.

2  Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]……………….

4 UTUSAMEHE DHAMBI ZETU, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu]”.

Kwahiyo ni lazima kuomba rehema na toba kila siku, kwasababu bado tupo katika mwili, na pia ni ishara ya unyenyekevu kwa Mungu.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Fahamu Namna ya Kuomba.

JIRANI YANGU NI NANI?

Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8).

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA MKRISTO EPUKE KUENDEKEZA BAADHI YA DHAMBI

Wewe umemwaga damu nyingi,

Kuna wakati Daudi aliingiwa na wazo la kumjengea Mungu nyumba, hivyo wazo hilo likawa jema sana machoni pa Mungu, likamfurahisha sana Bwana mpaka akamwahidia Baraka tele katika ufalme wake..Lakini tunasoma Mungu alimzuia Daudi asiijenge hiyo nyumba, bali mwana wake Sulemani ndiye aje kuijenga, sio kwamba Mungu alikuwa hatamani Daudi aijenge, hapana Mungu alimpenda sana, na alikuwa kipenzi chake, lakini kulikuwa na kikwazo kilichomkwamisha..

Embu tusome…

1 Nyakati 22:7-8

[7]Daudi akamwambia Sulemani mwanawe, Kwangu mimi nia yangu ilikuwa kujenga nyumba kwa ajili ya jina la BWANA, Mungu wangu. 

[8]Lakini neno la BWANA likanijia, kusema, Wewe umemwaga damu nyingi, na vita vikubwa umevifanya; wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu; 

Sababu yenyewe Mungu ameitoa hapo kwamba Daudi “amemwaga Damu za watu wengi”..Daudi hakujua kuuwa kwakwe watu sio jambo ambalo lilikuwa linavutia machoni pa Bwana,japokuwa Mungu alikuwa pamoja naye wakati wote, hakujua kuwa kuua kule kulikuwa kunapeleka harufu mbaya mbele za Mungu aliye mtakatifu na msafi.

Hivyo wakati anapeleka ombi lake la kumjengea hekalu, Mungu akamkataza kwasababu alimuona ananuka damu za watu wengi, Na sikuzote Mungu hawezi kuruhusu mikono yenye damu, kushiriki katika kujenga vitu vitakatifu.

Ni nini  Bwana anataka tujifunze.

Sisi kama wakristo, zipo dhambi au makosa ambayo tunayazoelea kuyafanya mara kwa mara, lakini hatujui kuwa tunamkosea Mungu, wakati mwingine tunapumbazika, kuona rehema na fadhili zake zinatufuata kila mahali, lakini ndani ya mioyo yetu tunamwaga damu kila kukicha kama Daudi.

Kwamfano, katika agano jipya, hatuui kwa Upanga au kwa mkuki, maandiko yanasema..

1Yohana 3:15  “Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake.

Kitendo tu cha kuwa na chuki, na jirani yako, au ndugu yako, kumbe rohoni unatafsirika kama mwuaji, hivyo chuki hizo zinavyoendelea na kuzidi wakati baada ya wakati, zinavyozidishwa kwa watu wengine kadha wa kadha, ndivyo mtu huyo anavyoonekana anamwaga damu nyingi.

Na madhara yake utakuja kuyaona mbeleni, wakati ambapo unamwomba Mungu kibali cha kutenda jambo Fulani jema kwa ajili yake, anakuzuia, unataka Mungu atembee na wewe katika viwango Fulani vya juu, anakuzuia, kwasababu umeendekeza makosa au dhambi hizo kwa muda mrefu.

Hivyo, tunapaswa, kila inapoitwa leo, tuangalie ni wapi tumezoelea kupafanya ambapo hapampendezi Mungu, kisha tuache mara moja, ili isije kutuletea madhara mbeleni, Kama ni katika usengenyaji, tuache mara moja, kama ni katika uongo, rushwa, udhuru,wivu, manung’uniko tuache mara moja.

Bwana atusaidie

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

NAAM, HATA WABAYA KWA SIKU YA UBAYA. 

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

KIFAHAMU KIGEZO  CHA KUSAMEHEWA NA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Ni kweli haturuhusiwi kula nyama kulingana na Isaya 66:3?


Jibu: Tusome,


Isaya 66:3 “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao”.


Mstari huo tukiusoma kama ulivyo ni rahisi kutafsiri kuwa “Biblia imekataza kuchinja wanyama na kula nyama”…lakini kiuhalisia hiyo sio maana yake kabisa…kwasababu kama hiyo ingekuwa ndio maana yake basi pia hapo imekataza matoleo… na tunajua matoleo ni jambo linalokubalika mbele za Mungu (Warumi 25:26).


Sasa tukisoma kuanzia ule mstari wa kwanza utaona Mungu anawakemea au kuwaonya wale watu ambao wanakusanya vingi na vikubwa na kwenda kumtolea Mungu, wakidhani kuwa Mungu anapendezwa na sadaka zao hizo kubwa na nyingi na huku mioyoni wapo mbali na Mungu.


Na utaona Bwana anazidi kusema.. “Mbingu na dunia ni mali yake, hakuna chochote tutakachoweza kumpa yeye ambacho kitakuwa cha kipekee”…ikifunua kuwa Mungu hana haja na vitu bali mioyo yetu, kwasababu kila kitu ni chake.


Isaya 66:1 “BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?


2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu”.


Umeona?..Mtu mnyonge ndiye atakayemwangalia Bwana, mtu mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno lake…Maana yake mtu wa namna hii atakapoleta sadaka yake ndio Mungu atakayoikubali, lakini mtu mwovu na mwenye kiburi Mungu haitaki sadaka yake.


Sasa endapo mtu mwovu anayemkataa Mungu analeta sadaka yake mbele za Mungu, sadaka yake hiyo inaonekana kama ni sadaka ya hatia.


Kama akileta Ng’ombe na kumpeleka kwa Kuhani kama sadaka ya kuteketezwa, Bwana ataiona sadaka hiyo kama ni kafara ya Mtu sio ya ng’ombe, hivyo atajitafutia laana badala ya baraka.


Utaona maandiko yanazidi kulisisitiza hilo katika Mithali 15:8

.
Mithali 15:8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA…”

Ndio maana katika Isaya 66, Bwana anasema..


Isaya 66:3 “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao”.


Kwahiyo tunachoweza kujifunza ni kuwa, Bwana hapendezwi na matoleo mabaya, yeye alisema kulitii Neno lake ni bora kuliko dhabihu Soma (1Samweli 15:22).


Hivyo usipeleke madhabahuni fedha haramu, fedha iliyopatikana kwa rushwa, kwa wizi, kwa uuuzaji wa vitu haramu kama bangi, pombe, sigara au hata kwa uuzaji wa mwili.


Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya BWANA, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa BWANA, Mungu wako, yote mawili”


Vile vile hatupaswi kumtolea Mungu dhabihu huku hatuna mapatano sisi kwa sisi..


Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,
24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”


Bwana Yesu atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi?

HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

Rudi nyumbani

Print this post

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 25:23 Upepo wa kusi huleta mvua; Vile vile asingiziaye huleta uso wa ghadhabu.


JIBU: Maandiko yanasema Upepo wa kusi huleta mvua, hapo hasemi ‘upepo’ huleta mvua hapana bali anasema ‘Upepo wa kusi’, Maana yake ni kuwa kila aina ya upepo hubeba tabia yake, kwa mfano upepo wa Kaskazi, hauleti mvua, bali unaleta joto. Vivyo hivyo na pepo nyingine zote, hubeba tabia zao.

Hii ni kufunua nini?

Na sisi wanadamu huwa tunavumisha pepo zetu..Na ndio maana utasikia Neno “UVUMI” wa jambo Fulani, na taarifa hizo husambazwa kwa maneno ya vinywa vyetu, Hivyo kila jambo unalolitoa na kulipeleka kwa mtu mwingine au kwa jamii, huo ni upepo, na ni lazima uwe makini nao sana, kwasababu mwisho wa siku ni lazima ulete faida au madhara.

Na ndio maana hapo katika sehemu ya pili ya mstari huo anasema.. “Vile vile asingiziaye huleta uso wa ghadhabu”. Kusingizia ni neno linalojumuisha usengenyaji, au mtu anayechukua taarifa siziso za kweli na kuzipeleka kwa mwingine, Watu kama hawa, mwisho wa siku watavuna  ghadhabu tu, au kuchukiwa, au kusababishiwa madhara na wale waliotolewa taarifa zao. Kwasababu kila uvumi unamatokeo yake.

Lakini tukiwa watu wa kupeleka habari njema, watu wa kuhubiri habari za Kristo, Maana yake ni kuwa Upepo tunaovumisha ni wa heri sikuzote, hivyo tufahamu kuwa mwisho wake utakuwa ni mzuri, utatuletea neema badala ya ghadhabu, kupendwa badala ya kuchukiwa, kusaidiwa badala ya kufukuzwa.

Hivyo tuwe makini na taarifa, au maneno yanayotoka katika vinywa vyetu, biblia inasema..

1 Petro 2:1  Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote. 2  Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;

Epuka masengenyo, na kuwazungumzia wengine vibaya.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,

JIPE NAFASI KATI YA TAARIFA UNAYOIPOKEA NA MAAMUZI UNAYOYATOA.

IEPUKE GHADHABU YA MUNGU.

Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela.

Kwanini mtu afanye miujiza na bado asiende mbinguni?

Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

Rudi nyumbani

Print this post

Mithali 24:27 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

SWALI: Naomba nieleweshwe maana ya huu mstari

Mithali 24:27

[27]Tengeneza kazi yako huko nje, Jifanyizie kazi yako tayari shambani, Ukiisha, jenga nyumba yako.


JIBU: Zamani enzi za biblia, kilimo kilikuwa ni uti wa mgongo wa uchumi wa watu wengi kama ilivyo sasa katika  baadhi ya jamii.

Hivyo ilikuwa ni ajabu mtu kutumia rasilimali zake katika kununua au kujenga vitu visivyo na umuhimu sana, kama vile nyumba, nguo za kifahari, magari ya farasi n.k.angali shambani kwake hajajiwekeza vya kutosha.

Watu walikuwa wanakusanya kwanza chakula cha kutosha kujihakikishia shibe kwa miezi au miaka kadhaa, ndipo baada ya hapo hufikiria kutumia hazina zao katika kujenga, au kujiendeleza..lakini hawakujiendeleza kabla ya kuhakikisha mashamba yao yamewanufaisha..

Na ndio hapo Sulemani utaona anatoa ushauri ule ule..

Mithali 24:27

[27]Tengeneza kazi yako huko nje, Jifanyizie kazi yako tayari shambani, Ukiisha, jenga nyumba yako.

Yaani kwa lugha rahisi ni kwamba tengeneza kwanza mambo yako uwe imara ndipo yale mengine ya ziada yafuate baadaye.

Ni kawaida ya mwanadamu kupenda, vitu vizuri kwanza kabla hajavitaabikia..

Alikuwepo Gehazi, mtumwa wa Elisha, yeye aliona kusubiri wakati wa Mungu ni kujichelewesha, kutumika kama mtumwa asiye na faida ni kupoteza muda, hivyo, zile zawadi zenye thamani nyingi zilizoletwa na Naamani, na Elisha kuzikataa, yeye akamwona kama alikuwa hapendi mema..lakini Elisha alimwambia maneno haya..

2 Wafalme 5:26

[26]Akamwambia, Je! Moyo wangu haukuenda na wewe, hapo alipogeuka yule mtu katika gari ili akulaki? Je! Huu ndio wakati wa kupokea fedha, na kupokea mavazi, na mashamba ya mizeituni, na mizabibu, na kondoo, na ng’ombe, na watumwa, na wajakazi?

Alimuuliza Je huu ndio wakati? ..kumbe kulikuwa na wakati lakini haukuwa ule..

Watu wanataka kula vitu vya Bwana lakini hawataki kutengeneza kwanza kazi zao huko mashambani, hawana muda wa kuifikiria kazi ya Mungu, hawana muda na kuhubiri injili ya kweli,wanachokifiria ni matumbo,  na kwamba watapata faida gani..

1 Timotheo 6:5-6

[5]… huku wakidhani ya kuwa utauwa ni njia ya kupata faida.

[6]Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa.

.Vilevile hata katika maisha ya kawaida, hekima hizi zinamafunzo, mtu atataka anunue simu ya milioni 2, lakini hana shughuli yoyote ya kumwingizia kipato, badala aitumie kama mtaji, kisha kile akipatacho kama faida ndio atumie kununua hayo mengine..

Bwana atusaidie, katika kuyapangalia maisha yetu ya rohoni na mwilini

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TENGENEZA  NYAVU ZAKO, OSHA NYAVU ZAKO.

Nini maana ya vifungeni viuno vya Nia zenu? (1Petro 1:13).

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

USIWE ADUI WA BWANA

Nini maana ya Ukuta uliopakwa chokaa (Matendo23:3)?

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

NAAM, HATA WABAYA KWA SIKU YA UBAYA. 

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Tomaso atake kwenda kufa pamoja na Lazaro? (Yohana 11:14-16).

Jibu: Tusome,

Yohana 11:14  “Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15  Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake.

16  Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, Twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye”

Kwa haraka ni rahisi kutafsiri kuwa Tomaso alitaka na yeye kwenda kufa pamoja na Lazaro, lakini kiuhalisia sio hivyo!.

Tomaso hakutaka kwenda kufa pamoja na Lazaro, bali hapo alimaanisha “kwenda kufa pamoja na Bwana Yesu”.

Ili tuelewe vizuri tuanze kusoma kisa hicho kuanzia juu mstari ule wa tano..(Zingatia vipengele vilivyoainishwa kwa herufi kubwa).

Yohana 11:5  “ Naye Yesu alimpenda Martha na umbu lake na Lazaro.

6  Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo.

7  Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, TWENDENI UYAHUDI TENA.

8  Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, JUZIJUZI TU WAYAHUDI WALIKUWA WAKITAFUTA KUKUPIGA KWA MAWE, NAWE UNAKWENDA HUKO TENA?

9  Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10  Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake.

11  Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.

12  Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.

13  Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.

14  Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15  Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake. 16  Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, TWENDENI NA SISI, ILI TUFE PAMOJA NAYE”

Katika kisa hiki tunaona Bwana Yesu anawapa taarifa wanafunzi wake ya kurejea tena kule Uyahudi ambapo walitaka kumpiga mawe mpaka afe!.. na taarifa hiyo ikawashitusha wanafunzi inakuwaje anataka kurudi tena huko kwenye hatari! (Maana yake si ndo anaenda kufa sasa!)

Lakini  Tomaso aliposikia wanafunzi wenzake wakimhoji hivyo, ndipo na yeye akawashauri kwamba wasimwache aende pake yake huko uyahudi, bali nao pia waende pamoja naye, ili kama ikitokea kauawa basi na wao wafe pamoja naye!.

Ni moyo mzuri aliokuwa nao Tomaso, lakini hakujua kuwa kufa kwaajili ya Kristo ni Neema na si jambo la kujiamulia tu au kujivunia kwamba linaweza kutendeka kwa uwezo wa mtu.

Mtume Petro alijaribu hilo zoezi kama la Tomaso likamshinda, kwasababu alidhani anaweza kufa ajili ya Kristo kwa nguvu zake..

Luka 22:31 “Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;

32  lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.

33  Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani AU HATA KIFONI.

34  Akasema, Nakuambia, Petro, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui”.

Zaidi sana huyu Tomaso ambaye alitaka kwenda kufa pamoja na Bwana, siku Bwana anakamatwa alimkimbia, hakuonekana!..(huenda ndo alikuwa Yule kijana aliyekimbia uchi, Marko 14:52)…na zaidi sana hata baada ya kufufuka kwake bado ilikuwa ni ngumu kuamini mpaka alipotokewa na Bwana Yesu..(huyo ndio mtu aliyetaka kwenda kufa na Yesu Yerusalemu)

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Tomaso hakutaka kwenda kufa na Lazaro, vinginevyo ingekuwa haina maana… lakini kinyume chake alitamani kwenda kufa pamoja na Bwana kwasababu aliamini huo ni ushujaa mkuu wa Imani.

Jambo tunaloweza kujifunza ni kuwa, hatupaswi kuzitumainia nguvu zetu, hatuwezi kusema tutamtumikia Mungu kwa nguvu zetu, hatuwezi kujivuna kuwa tutafanya hiki au kile kwa nguvu zetu, bali siku zote hatuna budi kuwa katika hali ya unyenyekevu, na kujishusha mbele za Bwana, kama tunatamani kufa kwaajili ya Bwana kifo cha kishujaa, basi tumalizie kwa kusema, BWANA TUSAIDIE

Na chochote kile tukifanyacho au tukikusudiacho ni lazima kumalizia kwa kusema “KWA MSAADA WA BWANA KITAFANIKIWA”.. Lakini tukijivuna kuwa tunaweza hiki au kile, tutaishia kumkana na hata kumsaliti.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti kulingana na (Zaburi 89:48)?

Nini maana ya “mtakayoyafunga duniani, yatakuwa yamefungwa mbinguni”?

Rudi nyumbani

Print this post

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

Swali: Je mapepo yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai kama mawe, milima, bahari, maji au nyumba, na hata kubadilisha maumbile ya hivyo vitu?

Jibu ni LA! Mapepo hayawezi kuviingia vitu visivyo na uhai bali yanaweza kuvitumia vitu visivyo na uhai.. mapepo hayawezi kuyaingia mawe au maji au mchanga au maji kama vile yanavyoingia ndani ya mtu, na kuviendesha vitu hivyo kama yanavyowaendesha wanadamu… Sehemu pekee ambayo mapepo yanaweza kuingia ni ndani ya viumbe hai kama wanadamu na wanyama, basi!

Biblia imerekodi mara kadhaa mapepo kuingia ndani ya watu (Luka 8:27) na pia ndani ya wanyama soma Marko 5:12-13. Lakini hakuna mahali popote panapoonyesha mapepo yamewahi kuingia ndani ya mawe au katika maji au katika mchanga, au katika matofali au katika gari la farasi au katika chakula..

Mapepo yanachoweza kufanya ni kuvitumia tu vitu vya asili, kwamfano yanaweza kuvumisha upepo lakini si kuingia ndani ya upepo, vile vile yanaweza kutetemesha ardhi lakini si kuiingia ardhi, yanaweza kuitikisa bahari lakini si kuiingia bahari… uwezo ambao hata sisi wanadamu tunao, sisi tunaweza kuvumisha upepo tukiwa na kifaa kinachoitwa feni, lakini si kuuingia upepo, vile vile tunaweza kutengeneza mawimbi ya bahari kwa vyombo maalumu n.k, lakini hiyo haimaanishi kuwa tumeiingia bahari na kuiendesha bahari kama vile tunavyoiendesha mikono yetu au miguu yetu.

Na mapepo ni hivyo hivyo, hayana uwezo wa kuviingia vitu visivyo na uhai.

Kwahiyo tunachopaswa kufanya ili roho za mapepo zisiweze kutumia vitu vya asili kutuletea matatizo ni sisi kudumu katika usafi na utakatifu pamoja na kuomba… tukifanya hivyo shetani na mapepo yake hawawezi kutumia vitu vinavyotuzunguka kutuletea madhara, hawawezi kuzitumia nyumba zetu kama vituo vyao vya mikutano.

Lakini tusipojisogeza karibu na Mungu, basi shetani atatumia vitu vyote kutudhuru, atatumia ardhi, bahari, mabonde, na magari na hata nyumba kutuletea matatizo…

Isaya 13:21 “Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini watacheza huko”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

MAJINI WAZURI WAPO?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

Rudi nyumbani

Print this post

Je! kuna mambo ambayo Mungu hawezi kuyafanya kulingana na Waamuzi 1:19?

Jibu: Tusome,

Waamuzi 1:19 “Bwana alikuwa pamoja na Yuda; naye akawafukuza watu waliokaa katika nchi ya milimani; ASIWEZE KUWAFUKUZA HAO WALIOKAA KATIKA HILO BONDE, kwa kuwa wao walikuwa na magari ya chuma”.

Ni kweli Bwana hakuweza kuwafukuza hao watu waliokaa mabondeni… Lakini si kwamba alikuwa hana uwezo wa kuwafukuza, bali kulikuwa na kusudi kwanini hakuweza kuwafukuza..

Ili tuelewe vizuri tuanzie kuisoma habari hiyo kuanzia mstari wa 17..(zingatia maneno yaliyoanishwa kwa herufu kubwa).

Waamuzi 1:17 “Kisha Yuda akaenda pamoja na nduguye Simeoni, na WAKAWAPIGA WAKANAANI waliokaa katika Sefathi, na kuuharibu mji kabisa. Na jina la mji huo ulikuwa ukiitwa Horma. 

18 Pamoja na haya Yuda aliutwaa Gaza pamoja na mipaka yake, na Ashkeloni na mipaka yake, na Ekroni na mipaka yake.

 19 BWANA ALIKUWA PAMOJA NA YUDA; naye akawafukuza watu waliokaa katika nchi ya milimani; asiweze kuwafukuza hao waliokaa katika hilo bonde, kwa kuwa wao walikuwa na magari ya chuma”.

Mstari wa 19, unaanza kwa kusema “Bwana alikuwa pamoja na Yuda” maana yake ni kwamba, katika vita Yuda alivyokwenda kupigana, Bwana alikuwa pamoja naye..(kumbuka Yuda anayezungumziwa hapa sio Yule mwana wa Yakobo, wala sio Yule Yuda aliyemsaliti Bwana Yesu), bali ni kabila la Yuda kwa ujumla, ambalo wakati wa kuingia katika nchi ya Ahadi lilipaswa liupiganie urithi wake kwa kuwatoa wenyeji wa Kanaani ili kusudi wapate ardhi ya kukaa wao, kama urithi wa kabila zima.

Hivyo katika harakati za kupambania urithi wao huo walikutana na makabila mengi mbalimbali, ambayo mengine yalikuwa na nguvu sana na mengine manyonge, yale yaliyokuwa manyonge Yuda walikwenda kwa ujasiri na kuyapiga na kuyapokonya ardhi, kwasababu hayakuwa na silaha zenye nguvu za kuwazidi,

Lakini yale yaliyokuwa na Nguvu nyingi za kivita, Yuda waliyaogopa, hivyo hawakudhubutu kwenda kupigana nayo, na kwasababu hiyo Mungu asingeweza kuyaondoa kwasababu Mungu kamwe hatembei na watu wasio na Imani, hivyo akawaacha,

Lakini kama wangechukua hatua ya kwenda kupambana na hao maadui zao, pasipo kutazama ni silaha za aina gani wanazomiliki, ni wazi kuwa Mungu angewasaidia katika vita hiyo, na hatimaye wangewaondoa hao watu na kuutwaa urithi wao.

Sasa baadhi ya makabila ambayo Yuda waliyaogopa ndio hao waliokuwa wanakaa mabondeni, na sababu ya kuyaogopa biblia imeitaja pale kuwa “makabila hayo yalikuwa na magari ya chuma kwaajili ya vita”..Yuda wakaogopa wasiende kupigana nayo, jambo ambalo Yoshua mtumishi wa Mungu alishawaonya kuwa wasiyaogope makabila hayo..

Yoshua 17:17 “Kisha Yoshua alinena na nyumba ya Yusufu, maana, ni Efraimu na Manase, akawaambia, Wewe u taifa kubwa la watu, nawe una uwezo mwingi; hutapata kura moja tu; 

18 lakini hiyo nchi ya vilima itakuwa ni yako; maana, ijapokuwa ni mwitu, wewe utaukata, na matokeo yake yatakuwa ni yako; kwa kuwa wewe utawafukuza hao Wakanaani, WAJAPOKUWA WANA MAGARI YA CHUMA, WAJAPOKUWA NI WENYE UWEZO”

Utaona pia hiyo sio mara ya kwanza wana wa Israeli kuyaogopa mataifa yenye nguvu kupita wao, soma pia Hesabu 13:33 na Waamuzi 4:3

Hiyo inatufundisha nini?

Tunachojifunza ni kuwa “Mungu hawezi kufanya jambo lolote kwetu pale tunapomkosea Imani” Hilo ndilo jambo ambalo Mungu hawezi kufanya!!! Na lingine ambalo hawezi kufanya ni DHAMBI!

Yakobo 1:6 “Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.

7  Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.

8  Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote”.

Ukiamini kuwa Mungu hawezi kukuponya, basi fahamu kuwa KWELI HATAWEZA KUKUPONYA!, Ukiamini kuwa Mungu hawezi kukutendea jambo Fulani au kukupigania, basi fahamu kuwa ni KWELI MUNGU HATAWEZA KUKUTENDEA HILO JAMBO, wala KUKUPIGANIA katika hiyo vita iliyo mbele zako.

Siku zote fahamu kuwa PASIPO IMANI HAIWEZEKANI KUMPENDEZA MUNGU (Waebrania 11:6).

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu?

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao;

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

Jibu: Tusome,


Waefeso 2:20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”

Hapo maandiko yanasema tumejengwa juu ya “Msingi wa Mitume na Manabii “na si juu ya “Mitume na Manabii” .. Na pia inasema tumejengwa juu ya “Msingi” na si juu ya Misingi ya mitume na manabii. Ikiwa na maana kuwa Msingi ni mmoja tu, ambao tumejegwa juu yake, (mbele kidogo tutakuja kuuona huo msingi ni nini).


Sasa yapo maswali mawili hapo ya kujiuliza; 1) Hawa Mitume na Manabii ni akina nani na 2) Huo msingi ni nini?


1) Mitume na Manabii:


Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapa katika Waefeso 2:20 sio hawa waliopo sasa, Bali ni wale walioandika biblia, kama Musa, Yeremia, Hosea, Ezekieli na Malaki vile vile mitume wale 12 wa Bwana pamoja na wengine kama akina Paulo, ambao waliandika biblia.


Mtu yeyote aliyepo sasa, au atakayekuja kutokea na kujiita mtume au nabii, basi afahamu kuwa andiko hilo la Waefeso 2:20 halimhusu hata kidogo. Na shetani amewapandikiza watu wengi kiburi (watu wanaojulikana kama mitume na manabii wa leo), na kuanza kujivuna kuwa wao ndio Msingi wa kanisa.. Jambo ambalo si la kweli hata kidogo.


2) Msingi


Msingi ambao sisi tumejengwa juu yake ni ule waliokuwa nao Mitume, ikiwa na maana kuwa kile Mitume walichokifanya msingi, ndicho hicho hicho sisi (kanisa la Mungu) tunajengwa juu yake. Sasa ni kitu gani Mitume na Manabii wa kwenye biblia walikifanya msingi?… Hicho si kingine zaidi ya YESU KRISTO MWENYEWE!!!. Huyu ndiye Msingi wa kanisa na ndiye aliyekuwa msingi wa mitume, na ndio msingi wetu sisi na bado ataendelea kuwa msingi siku zote.


1Wakorintho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, YESU KRISTO”.


YESU KRISTO ndio Mwamba ule ambao yeye mwenyewe alisema kuwa kanisa lake litajengwa juu yake.


Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.


Umeona? Mwamba unaonenewa hapo sio Petro bali ni yeye YESU MWENYEWE!.. yaani huo Ufunuo Petro alioupata wa YESU KUWA MWANA WA MUNGU Ndio MSINGI, na NDIO MWAMBA ambao kanisa litajengwa juu yake.


Kanisa lolote leo ambao YESU sio kiini cha Imani hiyo, hilo sio kanisa la kweli, vile vile imani yoyote ile isiyomweka YESU kama msingi badala yake inawemweka mwanadamu mwingine au mnyama au sanamu basi imani hiyo ni imani ya Uongo n.k


Mahubiri yoyote yasiyomweka YESU msingi, hayo ni mahubiri kutoka kwa Yule adui.
Mtumishi yoyote Yule, awe mchungaji, mwalimu, mtume, nabii au mwinjilisti asiyemweka YESU kama kiini na kitovu cha Mafundisho huyo si wa kweli, kwa mujibu wa maandiko.
Vile vile mtu yeyote ajiitaye Mkristo na Yesu si msingi wa maisha yake, huyo ni mkristo jina tu wa uongo.
Bwana atusaidie tumweke Yesu msingi wa maisha yetu.


Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

Rudi nyumbani

Print this post