Masomo maalumu kwa wanawake.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo taa na Mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).
Je wewe ni mwanamke? Na unapenda upate kibali mbele za watu?..au je wewe ni binti na unatamani upate ndoa, tena iliyo bora na ya Baraka?, au je wewe ni mwanamke uliyeolewa na unatamani ndoa yako Bwana aibariki na pia upate kibali na heshima Zaidi katika ndoa yako?. Kama ndio basi hakikisha unazingatia mapambo!!..
Katika biblia kuna wanawake waliofanya utafiti wa mapambo yaliyo bora na mazuri na yenye mvuto mkubwa, ili kwamba wawe na mvuto wa heshima mbele za watu, wengine ili wapate ndoa nzuri na kibali kwa wenzi wao..na walipoyatumia hayo mapambo wakafanyika kuwa wanawake bora kuliko wote, na wenye kukubalika kuliko wote.
Wanawake hawa hawakutumia mapambo ya kiulimwengu kama kupaka wanja machoni au kupaka rangi mdomoni ili waolewe au waheshimiwe na waume zao, vile vile hawakuvaa nusu uchi ili wavutie mbele ya wanaowatafuta kuoa, wala hawakusuka nywele ili waonekane warembo, wala hawakupaka rangi katika kucha zao, ili wavutie mbele za watu na kupata ndoa, lakini walitumia mapambo ya aina nyingine na hayo hakawapa ndoa wanazozitafuta, yakawapa heshima wanayoitafuta, yakawapa kibali wanachokitaka n.k.
Na mapambo hayo ni yapi…..?
1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, ILIYO YA THAMANI KUU MBELE ZA MUNGU.
5 MAANA HIVYO NDIVYO WALIVYOJIPAMBA WANAWAKE WATAKATIFU WA ZAMANI, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”.
Nataka tuuangalie huo mstari wa 5 unaosema “MAANA HIVYO NDIVYO WALIVYOJIPAMBA WANAWAKE WATAKATIFU WA ZAMANI”..
Kwahiyo kumbe zamani kulikuwa na wanawake “watakatifu” na “wasio watakatifu”. Na kila kundi lilikuwa na aina yake ya mapambo ili lipate kibali na kuvutia.
Na hapa biblia inatufundisha wanawake wa zamani waliokuwa watakatifu ijapokuwa katika masomo yao kulikuwa na vipodozi vingi, kulikuwa na rangi nyingi za kucha, na za uso na za mdomoni, lakini wao kwa ufunuo waliokuwa nao hawakuchagua mojawapo wa hayo mapambo, badala yake waliona yana kasoro, hivyo wakachagua mapambo ya ndani ambayo ni UPOLE, HESHIMA, UTII NA UTULIVU.
Wakaona hayo ndio yatakayowafanya waolewe, ndio yatakayowafanya wapendwe na waume zao, ndio yatakayowafanya wapate kibali katika ndoa zao na jamii zao, ndiyo yatakayowafanya waonekane wa thamani, na si kupaka wanja, au kupaka rangi mdomoni, au kujichubua, au kuvaa nusu tupu.
Ndio maana sasa utaona biblia inasema kama vile Sara alivyokuwa mtii kwa Ibrahimu mumewe hata kufikia hatua ya kumwita Ibrahimu “bwana”, Roho hiyo ya unyenyekevu na utii, na utulivu, ndio iliyomfanya Sara awe “mama wa mataifa” na si “wigi kichwani” wala rangi mdomoni, wala hereni sikioni. Kulikuwa na wanawake wengi katika ile nchi, ambao walikuwa wanajiremba na pengine hata kukaribia kufanana na malaika, lakini Ibrahimu hakuwachagua hata mmoja wao!.
Ibrahimu alimchagua Sara kwasababu alikuwa ni mtii, na mtulivu..(alikuwa na mapambo ya ndani)
“5 MAANA HIVYO NDIVYO WALIVYOJIPAMBA WANAWAKE WATAKATIFU WA ZAMANI, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana…”
Vile vile roho ya upole na ya kujisitiri iliyokuwa juu ya Rebeka, ndio iliyomfanya apate kibali kwa Isaka, kiasi kwamba alipofikishwa kwa Isaka, alifunika kichwa chake kwa shela (Mwanzo 24:62-67), ndio iliyomfanya awe mama wa Taifa kuu la Israeli (Yakobo), na si mavazi ya vimini, au ya mgongo wazi,…Na vivyo hivyo wanawake wengine wote watakatifu walitumia mapambo hayo ili kujipatia kibali.
Lakini wale wengine wa kidunia, walitumia mapambo ya nje, yaani.. vipodozi vyote walivyovitaka, waliweka pini katika pua zao, waliweka rangi kwenye kucha na kwenye kope, na midomoni, walipaka wanja machoni, na kupaka hina mwilini na kuweka nywele bandia n.k lakini wengi wa hao waliishia kutamaniwa tu na si kupendwa kama walivyotafuta,
Na wengine waliishia kuonekana kama makahaba, kama Yezebeli, (maana biblia inaonyesha Yezebeli alikuwa ni mwanamke mwenye kupaka uwanja machoni na kupamba kichwa, maana yake kusokota rasta, na kuweka nywele bandia, na ndio maana biblia ikamtaja kama mwanamke kahaba na mchawi soma 2Wafalme 9:22,30, Ufunuo 2:20-22).
Na siku zote mapambo haya mawili hayawezi kwenda pamoja!, ukitumia moja lazima lingine utalikosa…
Ukiwa unapaka uso rangi, unajichubua, unatoboa pua huwezi kuwa na unyenyekevu, utii, utulivu, au mapambo mengine yote ya ndani huwezi kuwa nayo… ni lazima tu utakuwa na kiburi, tamaa, wivu,.
Na vile vile huwezi kuwa mtii, mnyenyekevu, mpole (mapambo yote ya ndani) halafu ukavaa nusu uchi, vimini au nguo za kubana…
Ingekuwa mapambo haya mawili yanaweza kwenda pamoja (yaani ya ndani na ya nje) basi biblia isingesema wanawake wasijipambe kwa “mapambo ya nje”, badala yake ingesema “wasijipambe kwa mavazi ya nje tu pake yake bali pia wajipambe kwa mapambo ya ndani”. Lakini utaona imekosoa moja na kulihakiki lingine, ikiwa na maana kuwa mapambo haya hayawezi kwenda pamoja.
Mama, dada, binti unayetaka kwenda mbinguni?, na unayetaka kupendeza na kupata kibali.. basi zingatia kujipamba kwa mapambo ya ndani na nje jiweke katika hali yako ya asili, uone kama hutapata kazi unayoitafuta, au ndoa, au kibali popote pale uendapo kama ilivyokuwa kwa akina Sara, na wanawake wengine wa kwenye biblia, na Zaidi ya yote pia utaenda mbinguni kwasababu miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na si midoli ya matangazo ya nguo masokoni.
1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 . jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.
NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)
SWALI: Maandiko yanasema tusilaani, je! Paulo aliwalaani wagalatia na wakorintho?
Wagalatia 1:8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe. 9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe.
1Wakorintho 16:22 Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maran atha.
Mtume Paulo alipokwenda katika Galatia na kuwakuta baadhi ya watakatifu wa pale wamegeukia injili nyingine, iliyoletwa na wayahudi, inayosema ili mtu ahesabiwe haki ni lazima amwamini Kristo pamoja na sheria ya Musa, zaidi ya vile mtume alivyofundisha kwamba kinachoweza kumwokoa mtu ni Imani tu katika Kristo!. Sasa alipoona wamefikia hatua hiyo mbaya ndipo aliposukumwa kusema maneno hayo makali kwa wagalatia , kwamba “mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo waliyoipokea kwake, na alaaniwe”.
Lakini ni vema kufahamu kuwa kauli hii na ile ya 1Wakorintho 16:22 imetumiwa vibaya na baadhi ya wakristo kwa vizazi vingi, kwamba kwa ajili ya injili tunaruhusiwa kuweka laana kwa watu. Lakini je! Paulo aliwaalaani watu wale?
Jibu la! Kwasababu kama angekuwa ameruhusiwa kuwalaani maadui na wanaokwenda kinyume na , yeye basi asingesema tena maneno haya ya kubariki katika Warumi 12:14
Warumi 12:14 Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.
Na isitoshe mtume Paulo alikuwa anawaombea sana rehema ndugu zake Wayahudi waliopotoka, mbali na neema (Warumi 10:1)
Kama hakuwalaana Je! Katika vifungu hivyo alimaanisha nini?
Hilo Neno kulaani, tukisoma katika tafsiri ya awali ya biblia ya kigiriki linasomeka kama “Anathema”
Ambalo linamaanisha “mtu aliye chini ya laana/Hukumu ya Mungu”
Hivyo katika vifungu hivyo, Mtume Paulo aliposema “Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe” Alimaanisha Hivi;
Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na awe kama mtu aliye chini ya laana ya Mungu”
Na ndio maana mtume Paulo katika hiyo nyaraka yake mbeleni alieleza kwa mapana zaidi, jinsi gani watu waliokuwa wanategemea sheria ili kuwaokoa walivyokuwa chini ya laana ya hukumu. Soma;
Wagalatia 3:10 Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.
Kwa hitimisho ni kuwa, mtume Paulo hakuwalaani wakorintho au wagalatia. Bali aliwaeleza uhalisi, madhara ya kuipotosha injili ya Kristo. sisi kama wakristo hatupaswi kuwalaani watu ambao wanatupinga/ au wanahubiri injili inayopotosha, bali ni kuwaombea rehema, wageuzwe, lakini bila kuwaficha matokea ya kutenda kwao huko, Kwamba wapo chini ya laana ya Mungu na hivyo waogope! Kwasababu hukumu ipo.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?
Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).
Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?
Jibu: Jina la Bwana Yesu Kristo lisifiwe daima.
Matoleo ni Neno la ujumla linalomaanisha aidha sadaka, au michango.
Neno Matoleo linatokana na neno “Kutoa” Hivyo chochote kile mtu anachokitoa kwa Mungu wake kinaitwa Matoleo.
Lakini sadaka ni toleo rasmi ambalo linalenga moja kwa moja madhabahu, na matoleo ya sadaka tofauti na matoleo mengine kama michango ni kwamba sadaka inakuwa ni siri lakini michango mengine inaweza isiwe Siri,
Kwamfano yale matoleo Anania na Safira mkewe waliyoyatoa ya kuuza viwanja na kuleta thamani yake chini ya miguu ya mitume, hayakuwa siri, bali lilikuwa ni jambo linalowekwa wazi kwa wote.
Lakini sadaka haipaswi kuwa kitu cha kuonyesha mbele za watu, bali kinapaswa kiwe siri ya mtu na Mungu wake…kama Bwana wetu Yesu alivyotufundisha.
Mathayo 6:2 “Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu”.
3 Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;
4 sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.
Na Matoleo yote (iwe changizo au sadaka). Yana thawabu kubwa mbele za Mungu kama yakitolewa kwa nia njema na dhamiri njema na kulingana na Neno la Mungu,na Mungu anayaangalia sana.
Ukiahidi au ukipanga kumtolea Mungu kitu, basi hakiksha unatimiza kama ulivyoahidi au ulivyopanga pasipo kupunguza hata kidogo, ili isiwe kwako dhambi kama ilivyokuwa kwa Anania na Safira mkewe, ambao waimdanganya Roho Mtakatifu kwa matoleo yao.(Matendo 5:1-11).
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +25569303661
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.
Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).
YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.
Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;
2 Petro 1:3 Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe
4 Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.
Uungu ni Ile Hali ya kuwa kama Mungu.
Kwamfano mtu anayefanya vitendo viovu kama vya uuaji, utoaji mimba, uchawi, ushoga tunasema anafanya “Ushetani”.. Kwasababu anatenda kazi za shetani.
Vivyo hivyo tunaposema “Uungu”. Tunamaanisha kuwa kama Mungu, au kufanya kazi kama za Mungu, au kuwa na sifa za Mungu ndani yako.
Na Tabia ya Mungu ndani ya Mtu. Si Kila mtu anazo. Bali ni wale tu waliozaliwa na yeye. Yaani waliokoka
Hizi ni baadhi ya Tabia za kiungu.
Kitu ambacho Mungu anawakiria watu wake waliompokea ni uzima wa milele. Ambao upo ndani yake. Mwanadamu wa Tabia ya asili Hana uzima wa milele ndani yake. Akifa Hana Tumaini la kuishi. Lakini aliyezaliwa mara ya pili. Huishi milele. Kwasababu uungu upo ndani yake.
Yohana 10:34 “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu?”
Ukiwa kama mwana wa Mungu sifa hii ni lazima itaonekana ndani yako. Hakikisho la uzima wa milele, mwovu hana uzima wa milele.
Pili mtu mwenye uungu ndani yake, anatoa tabia za Mungu ndani yake, ndio zile tabia za Roho tunazozisoma katika Wagalatia 5:22, kama vile Upendo, , fadhili, uaminifu, utakatifu n.k.
Wagalatia 5:22-25
[22]Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, [23]upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. [24]Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. [25]Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
Mambo ambayo huwezi kuyaona kwa mtu mwenye tabia ya asili. Yeye huwa kinyume chake, au akijaribu kufanya basi ni kwa unafki, kwasababu havipo moyoni mwake.
Na pia mtu mwenye tabia ya uungu unakuwa na uwezo wa kuushinda ulimwengu(yaani dhambi) kama vile Kristo alivyoushinda ulimwengu..
1 Yohana 3:9
[9]Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.
Maana yake,dhambi inakuwa haina nguvu ndani yake. Maandiko yanasema hata wao wenyewe wakishangaa tunawezaje kuishi maisha ya mbali na dhambi (1Petro 4:4). Hawajui Ni kwasababu sisi tuna tabia za uungu ndani yetu.
Maandiko mengine yanayoeleza Neno uungu. Ni haya (Matendo 17:29, Warumi 1:20).
Bwana akubariki.
Je! Na wewe utatamani uwe na tabia za Ki-Mungu ndani yako?. Ni wazi kuwa hii ni kiu ya kila mmoja wetu. Kama ni hivyo basi, hauwezi kwa akili yako au nguvu zako, bali kwa Roho wa Mungu. Kwasababu biblia inasema wote waliompokea aliwapa UWEZO wa kufanyika wana wa Mungu (Yohana 1:12). Hivyo huu ni uwezo utokao kwa Mungu mwenyewe, na sio kwa mwanadamu. Na tunaupata kwa kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kwa kumkiri Yesu, na kumfanya kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu. kisha kumpa nafasi ya kuyatawala maisha yetu.
Hivyo basi ikiwa upo tayari siku ya leo kutubu dhambi zako, ili Bwana akufanye kiumbe kipya. Basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa Sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.
MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.
Ni kosa gani alilolifanya Eli, ilihali aliwaonya watoto wake?
Ni lazima tujue namna mbalimbali za kupambana na adui yetu (Ibilisi). Tunajua yeye ni mpinzani wetu, na mpinzani sikuzote huwa si rahisi kukubali kushindwa kirahisi, ni lazima ataleta ukinzani. Na ndio hapo suala la Kukemea linakuja wala hatumbembelezi wala hatumsihi-sihi, bali tunamkemea.
Kukemea maana yake ni kukipinga/ kukifukuza kitu kwa nguvu, kwa mamlaka uliyonayo.
Tunaona sehemu nyingi Yesu akimkemea ibilisi Pamoja na mapepo yake, ambayo yalikuwa yanawatesa watu.
Mathayo 17:18 “Yesu akamkemea pepo, naye akamtoka; yule kijana akapona tangu saa ile”.
Marko 8:33 Akageuka, akawatazama wanafunzi wake, akamkemea Petro, akasema, Nenda nyuma yangu, Shetani; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu
Hivyo na sisi tumepewa mamlaka hiyo, ya kumkemea ibilisi na mapepo yake, na uovu, na magonjwa, na vitu vya asili kwa jina la Yesu na vikatii.
Lakini pia tuna majira si lazima tufanye hivyo, Tutatumia nguvu nyingi sana! Leo tutaona silaha nyingine za Malaika ambayo wanatumia kumshughulikia shetani.. Maandiko yanatuambia wanao uwezo mkuu kuliko sisi lakini hawatumii uwezo wao wakati wote, kufanya hivyo kila wanapokutana na adui yao shetani.
Kwamfano, Wakati Fulani Malaika Mikaeli alipokutana na shetani, wakiushindania mwili wa Musa, maandiko yanasema, hakutumia uwezo wake kumlaumu, bali alisema Bwana na akukemee!.
Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee”.
Utajiuliza ni kwanini afanye vile? Sio kwasababu alishindwa, lakini alitambua SILAHA kubwa Zaidi itamfutilia mbali adui yake. Kwa namna nyingine Mikaeli alikuwa anamchonganisha shetani kwa Mungu. Na ukikemewa na Mungu unatarajia nini? Kama sio kupotelea mbali kabisa moja kwa moja.
Hivyo shetani anaiogopa vita ya Mungu Zaidi ya ile ya malaika au wanadamu.
Utaona tena jambo kama hili hili alilitenda Malaika mwingine, wakati ule wa Yoshua kuhani mkuu alipokuwa amesimama mbele za Bwana kuomba, na shetani naye amesimama kumpinga. Yule Malaika alimwambia shetani “Bwana na akukemee”.
Zekaria 3:1 “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye. 2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni?”
Umeona? Hivyo si kila wakati unapopishana na adui yako uso kwa uso, ufikirie kurusha makombora, kuvunja, kuharibu na kubomoa ngome, ndio yapo majira utasimama kuomba hivyo lakini pia tulia kwasababu maandiko yanasema VITA NI VYA BWANA. Mkabidhi Bwana yote. Kwamfano shetani amekuletea majaribu ya magonjwa sugu. Mwambie Bwana yaone mateso yangu, UMKEMEE SHETANI. Arudi nyuma yangu.
Sasa Maombi kama haya, usiyaombe juu juu tu,Fahamu kanuni, Ni maombi ya kumwita Mungu aingilie tatizo hilo, amwone mtesi wako, Ili pale anapopatumia kama mlango wa kukusumbua AMKEMEE atoke. Tatizo Lililokutesa kwa muda mrefu Bwana alifutilie mbali, kwa kulikemea.
Ni maombi aliyoyafanya Esta. Alipoona adui yake Hamani, amepanga vita dhidi yake na uzao wake na ndugu zake wauawe. Hakuhangaika, kushindana na Hamani adui yake. Aliona mambo yatakuwa mengi na kuumizana kichwa. Bali alikwenda moja kwa moja kwa mfalme. Akajinyenyekeza mbele zake, akamfanyia karamu kubwa sana, tena akamwomba katika karamu hiyo aje na yule adui yake, washiriki pamoja. ndipo mfalme akamuuliza haja yako ni nini, Lakini tunaona Esta bado hakumwambia tatizo lake kwa haraka,, akamfanyia tena na mara ya pili mfalme na adui yake karamu iliyo kubwa kama ile ya kwanza, akawaalika.. Ndipo Mfalme akamuuliza tena Esta haja yako ni nini?. Ndipo Esta sasa akaeleza akasema, ni HUYU ADUI YANGU HAMANI, amepanga kuniua mimi.
Akamwachia mfalme hukumu yote. Saa ileile Hamani akaenda kutundikwa msalabani, yeye na nyumba yake yote ikauliwa. Na Habari yake ikawa imeisha pale hadi hivi leo. Wala Esta hakuita kikosi, wala hakuchukua upanga, wala hakumwambia mfame muue, mvunje shingo, mchome moto Hamani. Hakusema hayo alichomwomba mfalme ni uhai wake tu (Esta 5).
Na ndivyo Mungu atakavyofanya kwa adui yetu Ibilisi na mapepo yake, pale ambapo tutataka Bwana ashughulike na matatizo yetu, zaidi ya sisi kushughulika nayo kuyakemea. Lakini ni sharti sisi tumkaribie yeye, kwa moyo wa upendo, tumfanyie karamu, ya Kupendeza ndipo tuzikabidhi changamoto zetu kwake.
Hivyo silaha hii ukiitumia vema itakusaidia sana. Jenga ukaribu wako na Mungu, Fanya ibada nyingi, mtolee Bwana sadaka, mwimbie sifa, mtukuze sana, ruka-ruka uweponi mwake, mpendeze moyo wake..( fanya hivi Zaidi ya kurusha makombora, na maombi ya vita) kisha mwishoni ndio mwambie Bwana amkemee adui yako. . Matokeo utayaona makubwa sana, haijalishi tatizo ulilonalo limekusumbua kwa muda mrefu kiasi gani, umepambana nalo kwa muda mrefu kiasi gani, limekuja na kujirudia rudia mara nyingi kiasi gani. Ugonjwa huo hautibiki kwa namna ipi, utakwenda tu.. Safari hii halitarudi kwako tena milele.
Bwana akubariki.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?
USIRUHUSU INZI WATUE JUU YA ROHO YAKO.
Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8).
Dinari ilikuwa ni sarafu ya kirumi yenye thamani ya (utumishi wa kibarua wa siku nzima)..Kwamfano leo hii tuseme kibaru atalipwa kwa siku shilingi elfu 20, na ukawa ndio utaratibu wa nchi nzima, kuwalipa vibarua kiasi hiko kwa siku kama mshahara, basi kiasi hiko cha fedha kingekuwa na thamani sawa na Dinari kwa wakati huo.
Tutalithibitisha hilo Zaidi katika ule mfano Bwana alioutoa wakulima walioajiriwa katika shamba la mizabibu..
Mathayo 20:1 “Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu
2 Naye alipokwisha kupatana na wakulima KUWAPA KUTWA DINARI, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu”.
Kwahiyo “ malipo ya utumishi wa kutwa nzima wa kibarua” ndiyo yaliyokuwa na uthamani wa “Dinari” na uzito wa sarafu ya Dirani ulikuwa ni “gramu 3.85”,
Kwa urefu kuhusiana na vipimo hivyo fungua hapa >>>VIPIMO VYA KIBIBLIA
Lakini tukirudi katika “Rupia”.. tunaisoma sehemu moja tu katika kitabu cha Ufunuo 6:6
Ufunuo 6:5 “Na alipoifungua muhuri ya tatu, nikamsikia yule wa tatu mwenye uhai akisema, Njoo! Nikaona, na tazama, farasi mweusi, na yeye aliyempanda ana mizani mkononi mwake.
6 Nikasikia kama sauti katikati ya hao wenye uhai wanne, ikisema, Kibaba cha ngano kwa NUSU RUPIA, na vibaba vitatu vya shayiri kwa nusu RUPIA, wala usiyadhuru mafuta wala divai”.
“Rupia” ni sarafu nyingine yenye thamani sawa na “Dinari”.. ambayo ilikuwa inatumiwa zaidi namataifa mengine tofauti na Rumi (uthamani wake ulikuwa ni sawa na mshahara wa kibarua wa kutwa)… Na mpaka sasa bado baadhi ya mataifa yanatumia Rupia!.
Lakini ni somo gani tunalolipata kutoka katika thamani hii ya fedha (Dinari na Rupia)?
Somo kubwa tunalolipata si lingine Zaidi ya lile tunalolisoma katika Mathayo 20:1-16, kuwa thawabu za Mungu hazichunguziki.
Kwa urefu unaweza kusoma hapa >>KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)
GHARAMA YA UFALME WA MBINGUNI.
SHAMBA HUWA HALIMTAMBUI WALA KUMSUBIRIA MKULIMA.
Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?
Jibu: Tusome,
Ayubu 22:12 “Je! Mungu hayuko mbinguni juu? Tena tazama umbali wa nyota, jinsi zilivyo juu!
13 Nawe wasema, Mungu anajua nini? Je! Aweza kuamua kati ya giza kuu?
14 Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione; Naye yuatembea juu ya KUBA YA MBINGU.
15 Je! Utaiandama njia ya zamani Waliyoikanyaga watu waovu?”
Kuba ni mzunguko wa Anga, Ukitazama juu utaona ncha za mbingu ni kama duara, ndio maana jua wakati wa asuhuhi ni kama “linachomoza kutoka chini upande wa mashariki” na wakati wa mchana linaonekana lipo juu kabisa (utosini) lakini inapofika jioni “linazama tena chini upande wa magharibi”..
Sasa huo mduara wa anga ndio unaoitwa “KUBA” na maandiko yanasema Bwana anatembea juu ya mduara huo, kuonyesha utukufu wake.
Ayubu 22:14 “Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione; Naye yuatembea juu ya KUBA YA MBINGU”.
Hivyo andiko hili linaonyesha utukufu na ukuu wa Mungu, kuwa yuko juu sana na mwingi wa uweza.
Je umemrudia yeye aliyezifanya Nyota na Mwezi, na anga na viumbe vyote?..
Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.
2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mada Nyinginezo:
Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?
Je unajua unapofanya mapenzi ya Mungu ni kwa faida yako na si kwa faida ya Mungu?.. Je unajua Mungu hana hasara na wala hajawahi kupata hasara kwa watu kufuata njia zao?…na vile vile hana faida yoyoyote anapata kwa wewe kuwa mkamilifu..
Zaidi sana tunapofanya mema au tunapofanya mabaya, ni kwa faida na hasara zetu wenyewe…ndivyo maandiko yanavyosema.
Ayubu 22:2 “Je! Yumkini mtu awaye yote kumfaa Mungu? Hakika yeye aliye na hekima hujifaa mwenyewe.
3 Je! Mwenyezi hupata furaha katika wewe kuwa mwenye haki? Au je, ni faida kwake, kwamba wafanya njia zako kuwa timilifu?”
Umeona?..tunapozishika amri za Mungu ni kwa faida ya roho zetu na nafsi zetu ndio Mungu wetu anatukazania tuitafute hiyo…ili tupate uzima wa milele, lakini tunapomkataa yeye (Mungu) yeye hana cha kupoteza, kwasababu vyote vinatoka kwake…badala yake ni kwa hasara zetu na uangamivu wetu wenyewe..
Ayubu 35:6 “Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?
7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?
8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu”.
Unapozini unajiharibu mwenyewe na si Mungu…
Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”
Unapoiba unajihatarishia maisha yako mwenyewe, unapoua unajimaliza mwenyewe na mambo mengine yote yasiyofaa ni kwa hasara zetu..
Lakini Bwana anapenda kuona tunakuwa na maisha ya milele ndio maana amemtuma mwanae wa pekee kwetu, ili tunapomwamini tuokolewe na tusipotee milele.
Lakini kama tukichagua mauti kwa hiari zetu wenyewe basi hatumpunguzii kitu, zaidi sisi ndio tunaopata hasara.
Ikatae dhambi, mkubali Yesu, mgeukie Muumba wako kabla hujamaliza siku zako za kuishi na utapata faida nyingi.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Walakini ataokolewa kwa uzazi wake.
Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.
BASI NIKAOGOPA, NIKAENDA NIKAIFICHA TALANTA YAKO.
Watu wengi wanapofikia hatua ya kuomba, wanashindwa kuomba vizuri au kudumu kwa muda mrefu, sio kwamba hawana nguvu za rohoni, hapana bali wakati mwingine ni kwasababu wanakosa mwongozo wa vitu vya kuombea. Hivyo tumeona tuutoe mwongozo huu mfupi ambao utakusaidia, unapoingia katika maombi yako ya asubuhi. Zingatia: Hii sio kanuni ya daima, Zipo nyakati Roho atakuongoza cha kuombea. Lakini hapa tunakupa mambo muhimu ambayo unapaswa uyajumuishe katika maombi yako ya asubuhi kila siku .
Kiwango cha chini kiwe ni Saa moja (1).
1. SHUKRANI: Ombi la kwanza liwe ni shukrani, Kumbuka umeianza siku mpya, huna budi kutanguliza shukrani kwa Mungu wako, kwa ajili ya uzima, afya,familia,wokovu, chakula,amani n.k.
Wakolosai 3:15 “…..tena iweni watu wa shukrani”
2. MWONGOZO WA SIKU MPYA: Omba Bwana akutangulie katika siku yako mpya. Ukayatende yale yote aliyokusudia uyatende katika siku hiyo. Usitoke nje ya mpango wake. Ili siku Yako isiwe Bure Rohoni.
Mithali 16:3 “Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika”.
3. NENO LA MUNGU : Omba uwezo wa kulikumbuka na kuliishi Neno la Mungu katika siku yote mpya. Neno lake Lisidondoke moyoni mwako, Usisahau agizo lake hata moja.Uishi Kwa hilo
Zaburi 119:16 “Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako”.
4. ULIMI WAKO: Katika siku yenye masumbufu na pilikapilika ya mambo mengi, Ni busara umwambie Bwana aweke mlinzi katika kinywa chako usijikwae kwa maneno mahali popote.
Zaburi 141:3 “Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu”
5. UTUKUFU WA MUNGU: Mwambie Mungu mambo yote uyafanyao ndani ya siku mpya yawe ni kwa utukufu wake. Na sio wa adui au mwanadamu.
1Wakorintho 10:31 “Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu”
6.WAKATI: Omba Mungu akusaidie kuukomboa wakati wako, siku yako isiwe na mapengo, usipite hivi hivi hujafanya jambo la msingi katika wokovu au maisha yako kwa ujumla.
Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu”
7. INJILI YA KRISTO: Mwambie Bwana akupe ujasiri wa kuwashuhudia wengine injili, popote uwapo. Vilevile ombea injili ya Kristo ienee kwa nguvu siku hiyo ulimwenguni kote. Ombea pia watumishi wa Mungu wanaotenda kazi yake, wapewe nguvu ili waitimize huduma hiyo ya Bwana.
Matendo 4:31 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri”
8. NDUGU NA FAMILIA: Ipeleke familia yako/ ndugu zako kwa Kristo akutane nao katika siku hiyo/ waokoke/ wadumu katika wokovu. Umepewa ndugu ili usimame Kwa ajili Yao.
Warumi 10:1 “Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe”.
9. JAMII: Utakutana na watu mbalimbali, mazingira mbalimbali, Hivyo huna budi uyaombee Amani, utulivu n.k. Ili uweze kuishi pia kwa amani, katika utumishi wako Kwa Bwana.
Yeremia 29:7 “Kautakieni amani mji ule, ambao nimewafanya mchukuliwe mateka, mkauombee kwa Bwana; kwa maana katika amani yake mji huo ninyi mtapata amani”.
10. ADUI: Mwambie Bwana akuepushe na Yule mwovu. Katika siku yako, mwovu asikujaribu katika imani, afya, kazi n.k
Mathayo 6:13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]
Ukitumia walau dakika sita (6), kuombea kila kipengele. Utakuwa umekamilisha SAA MOJA (1), La maombi. Na ukijijengea utaratibu wa kufanya hivi kila siku asubuhi, utaona mabadiliko makubwa sana ya maisha yako ya kiroho na kimwili.
WoKovu bila maombi ni sawa na gari zuri lisilo na mafuta. HUFIKI POPOTE.
Bwana akubariki. Nikutakie maombi mema.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
LITURJIA NI NINI? NA JE IPO KIMAANDIKO?
Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?
Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?(
Biblia haijatoa ‘fomula’, ya idadi ya nyakati tunazopaswa kuomba kwa siku. Ila imesema ‘tuombe kila wakati’ na sehemu nyingine imesema ‘tuombe bila kukoma’. Hiyo ni kutupa uelewa kwamba maombi yanapaswa yawe ni endelevu lakini pia yawe ya wakati wote. Na hakuna mahali maandiko yanatoa nafasi ya mwaminio kutokuomba kabisa.
Waefeso 6:18 “kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;”
1Wathesalonike 5:17 “ombeni bila kukoma”
Hivyo ni sisi kutazama, watakatifu walikuwa na desturi gani, na nidhamu gani waliyojijengea katika kuomba. Je! Walitumia vipindi vingapi kwa siku? Vilevile tutaona Bwana Yesu anasemaje kuhusiana na hilo pia. Ili na sisi tuige vielelezo vyao katika utaratibu wetu wa kusali.
DAUDI
Daudi aliomba mara tatu(3) kwa siku . Asubuhi, adhuhuri na jioni.
Zaburi 55:17 Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua, Naye ataisikia sauti yangu.
DANIELI
Danieli pia aliomba mara tatu (3), kwa siku.
Danieli 6:10 Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.
Hivyo hii ni kutuonyesha kuwa ilikuwa ni desturi ya watakatifu wa kale, kwenda magotini walau mara 3 kwa siku. Na maombi waliyoyaomba hayakuwa ‘sala’ za dakika tano (kama zile za kuombea chakula). Bali ni maombi ambayo huwenda yalizidi saa moja, kwasababu maombi ya kulalama, na kuugua, (mfano wa hayo ya Daudi) sio ya dakika chache.
YESU KRISTO.
Bwana Yesu aliomba alfajiri na usiku, na majira mengi nyakati za adhuhuri aliahirisha huduma na kwenda mahali pa utulivu kusali.
Marko 1:35 “Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko”
Na usiku
Mathayo 26:40 “Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? 41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”.
Adhuhuri
Luka 5:16 “Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba”
Hivyo tunaona pia Bwana aliomba nyakati zote. Alipopata nafasi.
Hivyo kiwango cha chini kabisa cha nyakati za kuomba kwa siku kwa sisi wakristo ni MARA MBILI. Yaani asubuhi na jioni. Unapoanza siku huna budi kuanza na Bwana kwa kumshukuru na kumwomba mwongozo wa siku hiyo, vilevile unapomaliza siku wapaswa ufanye hivyo hivyo.
Na ndio maana Bwana alisema maneno haya, kwa watu wake wanaoomba alisema;
Luka 18:7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?
Kumbe usiku na mchana tunapaswa tuombe. Walau mara mbili kwa siku. Alisema, Yeye ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Kufunua kuwa yupo katika mwanzo wetu na mwisho wetu. Hakikisha uanzapo siku unatenga muda wa kutosha wa kuingia uweponi, na umalizapo siku unafanya hivyo hivyo. Utakuwa imara sana kiroho.
Lakini zaidi sana Bwana anataka tuwe watu wa kuomba siku zote kufikia hata kukesha. Hivyo ikizidi hapo ni vema sana, kwasababu utajiwekea akiba ya maombi kwa wakati ambao utakuwa na nguvu chache.
Bwana akubariki.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.
HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA
NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?.