HUDUMA YA MALAIKA WAWILI.

HUDUMA YA MALAIKA WAWILI.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, ni wasaa mwingine tena Bwana ametupa neema ya kuutafuta uso wake. Karibu tujifunze Neno la Mungu.

Lipo funzo kubwa sana Bwana anatufundisha nyuma ya wale malaika wake wawili aliowatuma sodoma kwa ajili ya kuuangamiza ule mji. Habari tunaifahamu, hakuna haja ya kulitazama tukio lote, lakini tutatazama huduma yao ya mwisho ambayo waliifanya kwa familia ya Lutu.. Hiyo itatufanya na sisi leo hii tuwe makini sana na hii neema ya Mungu tuliyopewa kwa kitambo.

Malaika wale walipomwambia Lutu atoke sodoma, maandiko yanasema,  Lutu akawa ‘anakawia kawia’,..Hata baada ya “kuhimizwa sana” bado akawa anakawia kawia..hapo ndipo ikabidi wale malaika wachukue jukumu wenyewe la kuwatoa kwa nguvu sodoma, kana kwamba ndio wao wenye shida. Tusome;

Mwanzo  19:15 Hata alfajiri ndipo malaika WAKAMHIMIZA LUTU, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. 16 AKAKAWIA-KAWIA; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, kwa jinsi Bwana ALIVYOMHURUMIA, wakamtoa wakamweka nje ya mji..

Biblia inatuambia Kwa jinsi Mungu ‘alivyomhurumia’ Lutu na familia yake, ikampelekea amtoe kwa nguvu kama katoto kanacholazimishwa kupelekwa shuleni kwa kubembelezwa.. Hivyo waliendelea kuvutwa kwa umbali mrefu kidogo.. Lutu na mke wake wakashikwa na malaika mmoja, halikadhalika mabinti zake wawili wakashikwa na malaika mwingine.. Wakati wanatembea Walikuwa wanaweza kuangalia nyuma kama watakavyo na wasiambiwe kitu. Pengine walifika mahali wakawa wanasema tumechoka, wanabembelezwa watembee tu hivyo hivyo, wanafarijiwa, wanatiwa nguvu, Kwani jukumu la wao kuokolewa halikuwa katika uwezo wa mikono yao, bali  wa wale malaika wawili.

Lakini hali hiyo haikuendelea  sana… biblia inatuambia, walipofika nje tu kidogo ya mji..Wakaachwa, na kuambiwa zamu hii, sasa kipengele kilichobakia ni juu yao wenyewe..sisi tumemaliza kazi yetu.

Mwanzo 19:17 “Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, Jiponye nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea”.

Ndipo safari ya kukimbia, ikaanza..Lakini mkewe lutu, akidhani wakati huu ni kama ule wa mwanzo akageuka nyuma akidhani watakuwepo malaika tena wa kumshika mkono,na kumvuta vuta, na kumbembeleza bembeleza kama mwanzoni.. saa ile ile akageuka kuwa jiwe la chumvi.

Maana yake ni nini?

Saa tunayoishi ni wakati ambao sio tena kubembelezewa wokovu kama ilivyokuwa miaka ya kale.. Bali tunaishi ukingoni sana mwa neema ya wokovu. Wakati ambapo tunapaswa tujiokoe nafsi zetu na huu ulimwengu mbovu unaokaribia kuisha.. Pengine utasema umejuaje tupo katika zama hizo za kujiokoa nafsi zetu wenyewe, zama za kukimbia bila kuangalia nyuma, na sio za kuvutwa na Mungu? ,..Ni kutokana na kauli ya Bwana Yesu mwenyewe aliyoisema katika vifungu hivi;

Luka 17:32 “Mkumbukeni mkewe Lutu. 33 Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya”.

Maana yake ni kuwa hakuna kusubiria tena, Mungu akuambie hivi, au akuambie vile, au akufanyie hiki kwanza au kile.. Tayari alishasema na wewe kwamba usiangalie nyuma, kuna kuna kuwa jiwe la chumvi..jiokoe nafsi yako. Hivyo unapokuwa mkristo vuguvugu, unakapokuwa mkristo-jina, ujue upo hatarini sana wakati huu.. unyakuo ukipita leo au ukifa katika hali hiyo usidhani kwamba utakuwa na nafasi ya pili.

Mlango wa neema unakaribia kufungwa kwa watu wa mataifa, na hivi karibuni Yesu anarudi, dalili zote zinaonyesha huwenda kizazi tunachoishi tutayashuhudia yote. Sasa ya nini kuendelea kuufanyia mzaha wokovu,..Yanini kuendelea kuupenda ulimwengu? Ya nini kushikamana na mambo ya sodoma kama mke wa Lutu…

Usipoupokea wokovu wa kweli leo, ujue kesho itakuwa ngumu sana kwako, kuliko siku moja nyuma. Kwasababu neema ya Mungu haidumu milele kwa mwenye dhambi..litambue hilo!

Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.

29 Nao watakuja watu toka mashariki na magharibi, na toka kaskazini na kusini, nao wataketi chakulani katika ufalme wa Mungu”.

Isikize sauti ya Mungu..ikuambiayo jiokoe nafsi yako, mkumbuke mke wa Lutu.

Nyakati zetu ni za hatari sana kuliko nyakati za kale.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

USITAZAME NYUMA!

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Ni SIRI gani Paulo aliyokuwa anaimaanisha katika Waefeso 5:32?

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Emmanuel Kitengule
Emmanuel Kitengule
1 year ago

Barikiwa sana mwalimu kwa ujumbe NYETI,kwa kweli MUNGU na atujalie neema kuuelewa hasa na kuufanyia kazi kama alivyokusudia.