Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

Wale Nyoka waliowadhuru wana wa Israeli jangwani walikuwa wana maumbile ya moto au?. Maana maandiko yanasema walikuwa ni Nyoka wa moto, Na kama walikuwa wenye maumvile ya moto, waliwaumaje watu na walitokea wapi? Walishushwa au?

Jibu: Tusome,

Hesabu 21:6 “BWANA akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa”

Neno “moto” hapo halijatumika kuelezea maumbile (yaani miili) ya hao nyoka, kwamba wana miili iliyoundwa kwa malighafi ya moto, hapana!. Bali limetumika kuelezea “Rangi” ya hao Nyoka, kwamba wana rangi ya moto.

Rangi ya moto, inafananishwa na rangi ya “Shaba”. Mtu anaposema “sahani ile ni ya shaba” na anayesema “sahani ile ni ya moto” Ni kitu kimoja, wote wanamaanisha kitu kimoja.

Ndio maana baada ya pale utaona Musa anaagizwa atengeneze nyoka wa shaba, kuwakilisha rangi ya hao nyoka.

Hesabu 21:8 “Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi.

9 Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi”.

Nyoka hao wenye rangi ya moto, ni jamii ya Nyoka maarufu sana wenye sumu kali wanaopatikana jangwani, hadi leo wapo (Ni nyoka wa asili kabisa), maisha yao ni jangwani tu hawawezi kuishi mahali pengine, na huwa wanajificha chini ya mchanga, na kubakisha sehemu ndogo tu ya kichwa juu, hivyo si rahisi kuonekana.
Na endapo mtu akipita na bahati mbaya akakanyaga mchanga mahali ambapo nyoka huyo kajificha, basi aling’atwa na hakukuwa na matibabu.

Hivyo kwa hitimisho, walikuwa ni nyoka wa asili, isipokuwa rangi yao ni ya Moto (au shaba).

Lakini pamoja na hayo kulikuwa na ufunuo mkubwa juu ya tukio hilo lililowatokea wana wa Israeli, na huyo nyoka wa shaba, mpaka akaitwa Nehushtani.

Kwa maelezo marefu juu ya Nehushtani, unaweza kufungua hapa>> NEHUSHTANI.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Sikio lisikialo, na jicho lionalo, BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

SWALI: Huu mstari una maana gani ?

Mithali 20:12
[12]Sikio lisikialo, na jicho lionalo,
BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.


JIBU: Utajiuliza ni kwanini haijasema “Sikio na jicho” Bwana ndiye aliyeyafanya yote mawili..badala yake inasema ..

Sikio lisikialo, na jicho lionalo,
BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

Hii ni kuweka msisitizo katika kazi zao jinsi zinavyojitegemea…sikio haliwezi kuona, wala jicho kusikia, kwasababu kila moja limeundiwa mfumo wake tofauti wa kipekee..Lakini kutokufanana kwao haviwafanyi viwe na miungu miwili tofauti..bali ni Mungu yule yule mmoja aliyeviumba vyote.

Hata sasa tunapaswa tutambue kuwa Mungu ni Mungu anayeumba vitu katika mionekano tofauti tofauti..mmoja atamfanya mchina mwingine mwafrika, sio kwamba kuna itilafu au mapungufu katika jamii fulani ndio maana ikawa hivyo hapana.. ndivyo Mungu alivyotaka watu wake wasiwe na mionekano na maumbile yanayofanana, amependa tu iwe hivyo

Vilevile katika Kanisa Mungu ameweka vipawa mbalimbali..mwingine mwinjilisti, mwingine mwalimu, mwingine mchungaji..hata katikati ya hao wainjilisti au manabii bado kawatofautisha wote wasifanane..

Kutokuhubiri kwa kufoka au kwa utulivu kama yule hakukufanyi wewe usiwe na karama ile..

1 Wakorintho 12:4-6
[4]Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule.
[5]Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.
[6]Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.

Hivyo tuonapo tofauti hizi, ndani ya kanisa lake, au ulimwenguni tusinyoosheane vidole na kusema yule sio Mungu, maadamu tupo katika mstari ule ule wa imani, hatupaswi kushangaa sana au kulazimisha mambo yote yafanane..bali tukumbuke tu huu usemi..

Sikio lisikialo, na jicho lionalo,
BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

Itambue nafasi yako, Mungu aliyokuchagulia, kisha isimamie hiyo kwa bidii kwasababu vyote ni kwa utukufu wake mwenyewe.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/wp-admin/post.php?post=18939&action=edit#

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

Rudi nyumbani

Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?

SWALI: Naomba kuuliza kwamfano mimi ni mkristo mwenye uwezo wa kifedha, nikiombwa kuchangia ujenzi wa msikiti, Je! Ni halali kufanya hivyo?


JIBU: Tumeruhusiwa, kutoa misaada yoyote ile (Isiyokinzana na Neno la Mungu) kama tupendavyo kwa jinsi Bwana alivyotujalia bila kujali dini, Imani, jinsia au rangi, kabila n.k.. Kwamfano ukiombwa kujenga shule, au kutoa chakula, au kufadhili wazee wa Imani nyingine  waruhusiwa kufanya hivyo, tena ni vema Zaidi, kwasababu unaonyesha upendo ule wa ki-Mungu kwao, ambao hautoki kwa sababu Fulani.

Lakini ikiwa ni mambo yanayokinzana na Neno la Mungu  kama vile kusapoti  ujenzi wa kiwanda cha pombe, au kusapoti madhabahu nyingine tofauti na ile ya YEHOVA, tunayemwabudu katika Kristo Yesu, hapo hatujaruhusiwa.

Kwasababu upo uhusiano mkubwa sana kati ya sadaka na madhabahu. Kumbuka kiroho Sadaka ni Ibada kamili.

Mathayo 6:21 “kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako”.

Moyo wako hauwezi kuwepo katika kanisa la Kristo, na wakati huo huo uwepo katika msikiti, au katika hekalu la Buddha, au la Baniani ambao mungu wao ni ng’ombe,. Hapo utakachokuwa unakifanya ni uzinzi wa kiroho, unazini na miungu migeni, bila wewe mwenyewe kujijua.

Na biblia inasema Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu. Anatufananisha sisi na wake zake. Mungu hatazami tu pale tunapoisujudia au kuitumikia miungu migeni ndio achukizwe hapana, bali anatazama pia na sadaka zetu tuzitoazo.. Je tunazielekeza wapi? Kwake yeye, au kwa miungu migeni. Hapo tunapaswa tuwe makini sana.

Hivyo, kwa kuhitimisha ni kuwa, sisi kama wakristo, hatupaswi kuchangia ujenzi wa madhabahu za wasioamini. Ukiulizwa ni kwanini? Jibu lako ni kuwa IMANI YAKO HAIRUHUSU. Hivyo tu,

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Rudi nyumbani

Kwanini Mungu anajifanya kama hajui mambo?

  • Kwamfano ile habari ya Kaini utaona Bwana anamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?

Tofauti na tunavyomchukulia Mungu kuwa ni Mkuu sana, hana haja ya kuambiwa chochote wala kujuzwa jambo, lakini kiuhalisia Mungu mwenyewe hajachagua kujiweka katika hiyo nafasi, tabia ya Mungu ni unyenyekevu.

Ijapokuwa anajua kila kitu, lakini wakati mwingine anajishusha kana kwamba hajui,
Vile vile ijapokuwa anauweledi na hakuna anayeweza kumshauri lakini wakati mwingine anajishusha na kukubali mashauri ya viumbe wake.

Kwamfano utaona Mungu anakubali ushauri wa Musa mara kadhaa.

Kutoka 32:9 “Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu

10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.

11 Musa akamsihi sana BWANA, Mungu wake, na kusema, BWANA, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?

12 Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.

13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.

14 Na BWANA akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake”.

Kadhalika ijapokuwa Bwana anafahamu kila kitu, lakini utaona kuna wakati anajishusha na kuanza kufanya uchunguzi wa jambo mpaka analivumbua, utalithibitisha hilo katika kile kitabu cha Ayubu 28, wakati anafanya uchunguzi wa kuitafuta hekima.

Vile vile ijapokuwa anatujua wanadamu wote na matendo yetu lakini utaona kuna wakati anajishusha na kuanza utafiti kama mwanadamu kupima kiwango cha maovu duniani, utalithibitisha hilo kipindi anataka kuiangamiza Sodoma na Ghomora, kabla ya maangamizi alishuka katika mwili na kwenda kuhakiki mwenyewe kama kweli yaliyomfikia juu ndio hayo yanayoendelea chini..

Mwanzo 18:20 “BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,

21 basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua”.

Na sehemu nyingine nyingi ni hivyo hivyo. Utaona Mungu anajishusha na kuonesha tabia kama za mwanadamu, anajifanya dhaifu.. Ukitafakari sana unaweza kuona ni kama jambo lisilokuwa na maana, ni kama upumbavu hivi, lakini biblia inasema…

1 Wakorintho 1:25 “…. upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu”

Mungu amejifanya kama mdhaifu kwetu, kwa faida yetu sisi na si yake.

Hebu tafakari leo hii Mungu asingejishusha na kuuvaa mwili unaiotwa Yesu, leo hii tungekuwaje?, tungemwabuduje?, tungemwelewaje, Tungepata wapi nguvu ya kumtumikia?.

Tungesema Mungu hajui maumivu yetu, hajui shida zetu, hajui mzigo aliotutwika, hajui tabu tunazozipitia, yeye ni diktekta.

Lakini yeye Mungu mwenyewe naye alijishusha na kuwa mwanadamu, na yeye akapitia umaskini, na yeye anakipitia kujifunza, na yeye akapitia kutukanwa, na yeye akapitia kudhihakiwa na kukataliwa na kuumizwa na hata kifo ili atupe tumaini sisi.

Ili pale anaposema kwamba anayajua maumivu yetu, tufahamu kuwa ni kweli anayajua, anaposema anaujua umaskini wetu tujue ni kweli anamaanisha kuujua kwasababu na yeye aliupitia, anaposema anazijua tabu zetu, iwe kweli kwasababu naye pia alizipitia alipokuwa duniani.

Anaposema atatufufua tujue ni kweli kwasababu naye pia alikufa na kuona kifo hakimstahili mtu yeyote wa Mungu.

Hivyo udhaifu wake ni faida kubwa sana kwetu, una nguvu kuliko hekima zetu, Hekima zetu zingesema Mungu hawezi kujishusha kama mwanadamu.

Wafilipi 2:4 “Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.

5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

Ni nini tunachoweza kujifunza kwa Bwana?

Kama Mungu alivyo mnyenyekevu kwa faida yetu sisi, kadhalika na sisi hatuna budi kuwa wanyenyekevu kwa faida ya wengine.

Hapo mstari wa 5 maandiko yanasema “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu”.

Umeona?..Nia ya Kristo ni kujishusha kwa faida yetu, na sisi hatuna budi kuwa hivyo hivyo..

1 Petro 5:5 “…Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

UPUMBAVU WA MUNGU.

Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

MJUE SANA YESU KRISTO.

ZIKUMBUKE FADHILI ZA MUNGU

Rudi nyumbani

Biblia inamaana gani inaposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?”

SWALI: Naomba kufahamu Bibliainaposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?” inamaana gani? Kuteka mahekalu ndio kukoje?

Warumi 2:21 “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe?

22 Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?


JIBU: Maneno hayo aliyasema mtume Paulo kwa uweza wa Roho Mtakatifu, lakini hakutoa maelezo marefu, ni kwa namna gani wayahudi walikuwa wanateka mahekalu.

Lakini kulingana na maneno yake, ni kuwa kulikuwa ni desturi mbaya kwa baadhi ya wayahudi waliokuwa wanaishi kwenye mataifa ya wapagani, ya kuvamia mahekalu yao, kisha kuiba miungu yao, ambayo haswaa ilikuwa inatengenezwa kwa vito vya thamani kubwa kama vile fedha, au dhahabu.

Hivyo wenyewe walikuwa wanaviiba  na kwenda kuviuza kama vilivyo , au wanaviyeyusha na kuviuza kama VITO kinyume chake,. Jambo ambalo si tu Mungu alilipinga, bali pia lilikuwa ni kinyume na sheria za watu wa mataifa..

Jambo kama hilo utaliona  likitajwa tena katika ile Habari ya Paulo, alipokuwa kule Efeso, wale watu walipoleta vurugu kwasababu ya Paulo kuhubiri habari ambazo zinakinzana na ibada za miungu yao. Utaona pale walipopeleka mashitaka, wale waamuzi hawakuona kosa lolote juu ya akina Paulo,..Na moja ya makosa ambayo walitazamia kuyaona kwa mitume, ni hilo la kuiba vitu vya mahekalu yao.

Matendo 19:36 “Basi kwa kuwa mambo haya hayawezi kukanushwa, imewapasa kutulia; msifanye neno la haraka haraka.

37 Kwa maana mmewaleta watu hawa, wasioiba vitu vya hekalu wala kumtukana mungu mke wetu”.

Sasa tukirudi katika swali, kwanini Mtume Paulo aliposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?”, Alimaanisha kuwa Ikiwa umeamua kutojihusisha na ibada za sanamu, iweje basi uibe vitu vyao na kuvifanyia biashara?.. Je! Kuna tofauti yoyote na wale wanaovifanyia ibada?

Mungu alishakataza tabia kama hiyo katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati, soma;

Kumbukumbu 7:25 “Sanamu za kuchonga za miungu yao mtaziteketeza kwa moto; usitamani fedha wala dhahabu iliyo juu yao, wala usiitwae iwe yako usije ukanaswa nayo; kwa maana ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”;

Hii inatufundisha nini?

Tukikataa dhambi Fulani basi tusiwe wanafki, kuitenda katika maumbile mengine..Kwamfano,  tukisema hatunywi pombe, hatupaswi kwenda kuiba/kuchukua chupa za bia na kwenda kuziuza..Ikiwa hatuvuti sigara, hatupaswi pia kwenda kununua HISA za sigara, katika masoko ya fedha,  kisa tu zina faida kubwa. Ikiwa hatuzini, hatupaswi pia kufanya biashara za guesthouse kwa wazinzi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

Je! ni sahihi kwa mkristo kujifukiza?

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Haiwezekani kuwafanya tena upya hata wakatubu

Nini maana ya huu mstari.“Haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu” (Waebrania 6:6)

Tusome,

Waebrania 6:4 “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri”.

Kipengele cha muhimu cha kuzingatia hapo ni hicho.. “Hata wakatubu”.

Maana ya andiko hilo kwa lugha rahisi ni kwamba “watu waliopewa Nuru (Maana yake walioipokea Neema ya Wokovu) na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, kama ikitokea wakaiacha Imani, kwa makusudi, na kurudia tena mambo machafu ya ulimwengu haitawezekana kuwafanya tena WATUBU”.

Sio kwamba wataomba msamaha na Mungu hatawasamehe, hapana!…bali haitawezekana tena kuwa na huo moyo wa kutubu!..Kwasababu nguvu ya kutubu inaletwa na Roho Mtakatifu, hakuna mtu yeyote amewahi kutubu na kumgeuka kwa nguvu zake.

Yohana 6:44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho”.

Na pia maandiko yanazidi kusema..

Yohana 15:16 “Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda…”

Maana yake ni kwamba, tunatubu kwasababu ni Mungu katuwekea moyo wa toba, lakini kama tumemfedhehesha Roho Mtakatifu anayetupa moyo wa toba, na akaondoka kwetu?..Je! Tutafanyaje ili tutubu?..tutabaki tu kuendelea na maisha ya dhambi.

Hiyo ni tahadhari kwetu tuliomwamini Bwana Yesu na kusimama katika Imani, na kuvionja vipawa vya Roho, na kuona kwamba Bwana ni mwema ni lazima tuchukue tahadhari, tuangalie tusiurudie ulimwengu na kuishi tena maisha ya dhambi kama zamani.

1 Wakorintho 10:12 “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.

Mtume Petro ameliweka tena hilo vizuri kwa kusema.

2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.

21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa

22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni.”.

Pengine wewe unayesoma ujumbe huu ulikuwa umeshaanza kurudi nyuma, ingawa ulishavionja vipawa vya Mungu, Na sasa umesikia huu ujumbe na umekuogopesha na kukushtua.

Hiyo hofu iliyoingia ndani yako ni kuonesha kuwa bado Neema haijaondoka juu yako, lakini ipo mbioni kuondoka kwako kama hautageuza njia zako (Hiyo ni kulingana na maandiko).

Siku itakapoondoka hutashtushwa tena na habari kama hizi, wala hutamwona tena Yesu ni wa maana katika maisha yako, utaishia kuwa mtu wa kudhihaki na kutokujali, Toba itakuwa mbali sana nawe.

Lakini sasa bado neema ipo nawe, ndio maana sasa hivi una hofu usikiapo habari za kiMungu.

Sasa Nini cha kufanya?

Ule ulevi ambao tayari ulikuwa umeuacha usiurudie tena, ule uzinzi, uasherati, uuaji, wizi n.k ambao ulikuwa umeshauacha, usiufanye tena, kwasababu kuna hatari kubwa kuyarudia mambo tuliyokuwa tumeyaacha.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Ni kwa namna gani Bwana amekuja kuwafanya wanaoona wawe vipofu?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

ULIMWENGU WA ROHO UPO NA UNA MADHARA KATIKA MAISHA YETU! 

ULIMWENGU WA ROHO UPO NA UNA MADHARA KATIKA MAISHA YETU! 

Rudi nyumbani

WAKATI ULIOKUBALIKA NALIKUSIKIA

Maandiko yanasema kila jambo lina majira yake..

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu”.

Maana yake ni kwamba kuna mambo ambayo unaweza kuyatamani yatokee lakini kama si majira yake hayawezi kutokea.

Kama muembe haujafika majira yake ya kuzaa maembe, haijalishi utaumwagia maji kiasi gani, au utauwekea mbolea kiasi gani, kamwe hautazaa..

Kwanini?

Kwasaababu sio msimu wa maembe, sio majira yake ya kuzaa..Lakini utakapofika wakati wake hata usipomwagiwa maji wala kuwekewa mbolea bado utazaa tu!!.

Kadhalika pia katika mambo ya rohoni, kuna vitu vinavyopatikana kwa msimu tu!. Sio kila wakati vipo, Na moja wapo ya hivyo ni NEEMA YA WOKOVU.

Tofauti na inavyofikiriwa na wengi kuwa Neema ya wokovu ni ya milele na ya wakati wote!.. Lakini kiuhalisia! Sio ya Milele, ni ya kupindi fulani tu!.

Kabla ya Bwana Yesu kuja duniani, neema hii ilikuwa haipatikani, hakukuwa na kitu kinaitwa msamaha wa dhambi, (Dhambi zote zilikuwa zinafunikwa tu).

Daudi, Musa, Eliya, na manabii wengine wote hawajawahi kuondolewa dhambi zao, badala yake zilikuwa zinafunikwa tu!, Na kila mwaka kunakuwa na kumbukumbu la dhambi.

Na hiyo si kwasababu walikuwa hawaombi sana, au hawakuwa na bidii..la! Walikuwa na bidii kuliko hata sisi (Maandiko yanasema Eliya alikuwa ni mtu wa kuomba sana kwa bidii, Yakobo 5:17).

Sasa kama ni hivyo kwanini, Hawakupewa hii Neema?.

Jibu ni kwasababu haukuwa Wakati wa Neema kuachiliwa duniani, haukuwa msimu wa Neema ya Mungu kudhihirika duniani, haijalishi wangeomba kiasi gani, bado hii Neema tuliyonayo sisi wasingeipata, kwasababu haukuwa wakati uliokubalika.

Lakini baada ya Bwana kuja duniani, ndipo majira mapya yakaanza.. Ukawa ni wakati uliokubalika wa Neema ya Mungu kumwagwa duniani.

Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema.

Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Hapo mstari wa 19, anasema “Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa”.

Hajaishia kusema tu “Mwaka wa Bwana”..bali pia “uliokubaliwa”.

Maana upo wakati uliokubalika na wakati ambao sio wa kukubalika.

Sasa tukishayajua hayo tunapaswa tufanye nini?

Biblia imetupa ushauri..

2 Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.

2 (Kwa maana asema,Wakati uliokubalika nalikusikia,Siku ya wokovu nalikusaidia; tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa.)

Hapo anasema “wakati uliokubalika nalikusikia”..na “siku ya Wokovu nalikusaidia”

Kwa lugha rahisi ni kwamba “msimu wa neema nitakusikia” “Na msimu wa kuokolewa nitakusaidia”. Maana yake msimu tofauti na huo hakuna wokovu. Kama vile misimu ya matunda ilivyo.

Ndugu hii Neema ipo ukingoni sana kuisha, na itaisha siku ile Unyakuo utakapotokea duniani, baada ya hapo hata ulieje, hakuna wokovu kwasababu sio saa ya wokovu, siku hiyo hata ufungeje kwa maombi na dua na sala hutasikiwa kwasababu sio wakati uliokubalika.

Je umeichukuliaje hii Neema leo?

Manabii wa zamani walitamani kukiona hichi kipindi tulichopo lakini hawakukiona.
Huu ndio wakati wa kusikiwa maombi yetu na sala zetu na Mungu, wakati unakuja mbingu zitafungwa.

Je umeingia ndani ya Neema leo?

Unaingiaje ndani ya neema?Unaingia kwa kumkiri Yesu na kutubu dhambi zako zote na kubatizwa kwa Jina la Yesu.

Kanuni rahisi tu hiyo, inakusogeza karibu sana na Mungu kwa viwango vingine.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Neema ni nini?

FUMBO ZA SHETANI.

MFANYE BWANA YESU MWENYEJI MAISHANI MWAKO.

Rudi nyumbani

“Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama

Nini maana ya huu mstari? Mithali 11: 15 “Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo ya dhamana yu salama”.


Biblia ni kitabu pekee ambacho kinamfundisha mtu kutembea katika kanuni zote (yaani za mwilini na rohoni), jinsi ya kuishi katika roho, vilevile na jinsi ya kuishi katika mwili,  Na moja ya kitabu ambacho kinatufundisha kanuni za kutembea katika mwili na kufanikiwa ni hichi kitabu cha Mithali,

Ni kitabu ambacho kina mahusia kwa makundi yote ya watu kuanzia wanandoa, vijana, watoto, maskini,  matajiri, vilevile kina maonyo kwa viongozi, hadi kwa watumwa, Hivyo, tukirudi katika swali, kwanini Sulemani kwa hekima ya Roho alisema.. “Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo ya dhamana yu salama”.

Hapo Hakumaanisha kuwa, kumdhamini mtu yeyote, ni kosa, hapana, bali anatoa angalizo katika kutoa dhamana kwa mtu mgeni (usiyemfahamu), kunaweza kukuweka katika hatari kubwa sana ya kukumbana na shida. Kumchukulia mtu mkopo bank halafu, unaweka nyumba yako rehani, mtu ambaye umekutana naye kwa  kipindi kifupi tu, bado hujui vizuri mwelekeo wake upoje, halafu unaweka mpaka na mali zako rehani, hapo ni rahisi sana kuishia pabaya,

Hatupaswi kukurupuka kumdhamini mtu, ili mradi tu mtu kisa tunafanya tendo jema. Hapana kinyume chake biblia inaturuhusu tuchukue muda wa kumtambua, kumfahamu, kumwelewa, ndipo tumdhamini kama kuna umuhimu wa kufanya hivyo, Lakini Zaidi sana tukibaki kama tulivyo, tukamwachia Mungu asimamie mambo hayo ya kudhamini, tutakuwa katika upande ulio salama Zaidi. Kwasababu bado wakati mwingine mtu anaweza akawa ni mwema kweli, au akawa na mwelekeo mzuri lakini kwa bahati mbaya mambo yakabadilikia ghafla njiani, labda kapata hasara, hapo atakayeumia ni wewe uliyemdhamini.

Na ndio maana bado Biblia bado inasisitiza suala hilo hilo katika vifungu vingine mbeleni kidogo inasema..

Mithali 22:26 “Usiwe mmoja wao wawekao rehani; Au walio wadhamini kwa deni za watu; 27 Kama huna kitu cha kulipa; Kwani ukaondolee kitanda chako chini yako?”

Lakini maneno haya yanatufundisha nini rohoni?

Yupo ambaye hakuogopa jambo hilo, aliingia katika hii hatari ya kutudhamini, huku akijua kabisa, anaowadhamini hawawezi kulipa madeni yao hata kidogo, lakini alijiingiza katika shida zao, na kwa nguvu zake, akafanikiwa kulipa  makosa yetu yote.

Angeweza kuacha asitudhamini, kwasababu maandiko yametoa ruhusa hiyo kama tulivyosoma.. Lakini kwa upendo wake, usiopimika, alikubali kulipa madeni yetu yote. Na huyo si mwingine Zaidi ya Bwana wetu YESU KRISTO.

Hakika sifa heshima na utukufu vina yeye, milele na milele. Amina.

Ni kitendo cha kushangaza sana na cha aibu, kuona mpaka sasa kuna baadhi ya watu wapo nje ya neema yake.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.

Je! kuna madhara kuchukiwa na kila mtu kwasababu huna mali?. Kama biblia inavyosema katika Mithali 14:20?.

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

UNYAKUO.

Rudi nyumbani

NINI MAANA YA KUTUBU

Tofauti na inavyodhaniwa na wengi kuwa kutubu ni kuomba msamaha, lakini kiuhalisia kuomba msamaha kunakuja baada ya kutubu.

Kutubu maana yake ni “Kugeuka” yaani kuacha kile ulichokuwa unakifanya.
Maana yake unapojigundua kuwa wewe ni mkosaji, jambo la kwanza ni “Kuacha kile ulichokuwa unakifanya” kisichokuwa sawa. Kisha ndipo unakwenda kuomba msamaha.

Hakuna mtu anayekwenda kuomba msamahaka kabla hajaacha kile alichokuwa anakifanya.

Umemwibia mtu, au boss wako, je unaweza kwenda kumwomba msamaha huku bado unamwibia?

Jibu ni la!. Cha kwanza utakachokifanya ni kuacha kwanza wizi, kisha ndipo unakwenda kumwomba Msamaha. Maana yake matendo yako ndiyo yatakayoelezea kama kwenye kama umetubu kweli au la!, Na si maneno.

Na kwa Mungu ni hivyo hivyo, haangalii wingi wa maneno yetu, wala wingi wa machozi yetu, wala wingi wa majuto yetu, bali wingi wa Matendo yetu!.

Kwa Mungu “Matendo” ni Alama kubwa sana kuliko hata “Maombi”. Mtu anayetenda sana ni rahisi kufanikiwa zaidi na yule anayeomba sana bila kutenda.

Yakobo 2:17 “Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake”.

Kadhalika na Toba ni matendo si maneno.
Ili tulielewe hili vizuri hebu tujikumbushe ile habari ya Yona.

Yona 3:3 “Basi Yona akaondoka, akaenda Ninawi, kama Bwana alivyonena. Basi Ninawi ulikuwa mji mkubwa mno, ukubwa wake mwendo wa siku tatu.

4 Yona akaanza kuuingia mji mwendo wa siku moja, akapaza sauti yake, akasema, Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa.

5 Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo.

6 Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu.

7 Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu asionje kitu, wala mnyama wala makundi ya ng’ombe, wala makundi ya kondoo; wasile, wala wasinywe maji;

8 bali na wafunikwe nguo za magunia, mwanadamu na mnyama pia, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake.

9 Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe?

10 Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”

Nataka tuuone huo mstari wa 10 unaosema “Bwana akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya”…hapo haisemi “Bwana akaona kufunga kwao na kujitesa kwao, wala kulia kwao”.

Sasa sio kwamba kufunga Mungu hakuoni, anakuona lakini kunapaswa kuje baada ya mtu kuacha njia zake mbaya.

Tunapokwenda kuumaliza mwaka tulikumbuke hili, inawezekana umeomba sana Msamaha kwa Mungu kwa mambo unayoyafanya, lakini nataka nikuambie kuwa ni muda tu ulikuwa unapoteza, hakuna msamaha wowote ulioupata endapo hukuamua mwenyewe kuacha njia zako mbaya, kama hawa watu wa Ninawi.

Kama hukuamua kuacha njia ya Ulevi,uzinzi, anasa, wizi, utukanaji, uuaji, utapeli, rushwa n.k bado toba yako haikukamilika, haijalishi uliongozwa sala ya Toba na nani?, Bado mbele za Mungu hujapokea msamaha wa dhambi.
Sasa swali ni wakati gani sahihi wa kutubu?
Biblia inasema saa ya Wokovu ni sasa, wakati uliokubalika ndio huu.

2 Wakorintho 6:2 “(Kwa maana asema,
Wakati uliokubalika nalikusikia,
Siku ya wokovu nalikusaidia;
tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa.)”

Je Umetubu??..Yaani umegeuka na kuacha njia zako mbaya?. Kumbuka baada ya wewe kuamua kuacha njia zako mbaya ndipo Bwana kupitia Roho wake Mtakatifgu anakuongezea nguvu ya wewe kuweza kushinda dhambi, kwasababu Roho Mtakatifu ni msaidizi, maandiko yanasema hivyo, (kumbuka tena, Yeye ni msaidizi na si mtendaji). Watendaji ni sisi, yeye kazi yake ni kutusaidia, kutuongezea nguvu.

Sasa jiulize atamsaidiaje mtu ambaye hajaanza kufanya chochote??, Utamsaidiaje mtu aliyechoka kutembea na ilihali hata hiyo safari yenyewe hajaianza?.

Isaya 40:29 “[Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo”.

Leo kuna watu wengi wanaoshindwa na dhambi, ambao hawawezi kuacha ulevi, uzinzi, kujichua, kuiba, kusengenya n.k. Na hawajui tatizo ni nini?.

Tatizo ndio hilo, walitangulia kuomba msamaha kabla ya kuamua kuacha matendo yao.

Bwana alipofika nyumbani kwa Zakayo, alitubu wizi wake kwa matendo kwa kwenda kuwarudishia mara 4 (Luka 19:1-10) wale aliowadhulumu, na ndipo Bwana akamwambia leo wokovu umefika nyumbani kwake, hakutubu kwa maneno tu!.

Watu kama Zakayo ndio Bwana anawaongezea nguvu ya kushinda dhuluma, kwasababu wameshaanza safari ya kuacha dhuluma kwa vitendo.
Na wewe leo anza toba kamili kwa kumwacha huyo mke/mume ambaye si wako, kwa kumwacha huyo mtu mnayeishi kama girlfriend/boyfriend na ilihali hamjafunga ndoa, kwa kumrudishia mtu kitu ulichomdhulumu au kumwimbia.

Na baada ya kufanya hayo na kumwomba Bwana msamaha, utaona Amani fulani isiyoelezeka imeiingia ndani yako, hiyo itakuwa ni uthibitisho wa kwamba Toba yako imekubalika mbele za Bwana.

Na baada ya hapo Bwana atakuongezea nguvu ya wewe kushinda dhambi, ghafla utaona kiu ya kudhulumu imekufa, kiu ya kuzini imekufa, kiu ya kufanya mambo yote uliyokuwa unayafanya imekufa.

Bwana akubariki, na Bwana atubariki sote.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

NGUVU YA MSAMAHA

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA!

KIFAHAMU KIGEZO  CHA KUSAMEHEWA NA MUNGU.

Rudi nyumbani

Dhabihu ni nini?

Dhabihu kwa jina lingine ni “kafara”, zilikuwepo sadaka za kafara na vile vile zilikuwepo zisizo za kafara.

Katika agano la kale, kafara zilizokuwa zinatolewa kwa Mungu ni kafara za wanyama, kama kondoo, mbuzi na ng’ombe.

Ambapo, mtu binafsi au Taifa zima litamsogeza huyo mnyama mbele za Bwana katika hema yake, na kuhani atamchukua huyo mnyama kama ni ng’ombe, au mbuzi au kondoo na kumchinja na kutwaa damu yake na kufanya upatanisho kwa huyo mtu au kwa Taifa, na kutwaa baadhi ya viungo na kuvichoma juu ya madhabahu.

Sasa sadaka ya namna hiyo ndiyo inayoitwa dhabihu.

Zilikuwepo sadaka nyingine ambazo hazikuwa dhabihu.

Kwamfano sadaka za unga, sadaka za mazao, sadaka za fedha, sadaka za nguo, za malimbuko n.k hizo hazikuitwa dhabihu.. Dhabihu ni sadaka ya kafara inayohusisha mnyama kuchinjwa na damu kumwagika.

Leo hii tumezoea kusema “tunaenda kumtolea Bwana dhabihu tukimaanisha sadaka zetu za fedha..lakini kiuhalisia hizo sio dhabihu tunazotoa bali ni sadaka tu!. Na zina baraka zake kubwa tu!, Lakini haziitwi dhabihu, ingawa hatutendi dhambi pia kuziita hivyo.

Sasa swali ni je! Mpaka leo hii tunapaswa tutoe sadaka za dhabihu? Yaani kafara za wanyama?

Jibu ni la! Katika agano jipya hatuna tena sadaka za dhabihu za wanyama, hatuhitaji tuchinje ng’ombe ili tupate kibali fulani au baraka fulani kutoka wa Mungu.

Kadhalika hatuhitaji damu ya kuku, au ya mbuzi, kupata ulinzi fulani wa kiMungu.

Jambo hilo liliwezekanika katika agano la kale, chini ya maagizo maalumu ya Bwana.
Lakini kwa sasa Agano jipya, hatuna hicho tena,

Sasa tunayo dhabihu moja ambayo imeshatolewa inayotufanya tusiwe na haja ya dhabihu za wanyama.

Na dhabihu hiyo Mwanakondoo Yesu Kristo, ambaye alitolewa sadaka kama kafara kwa ajili yetu, na damu yake ndio inayotupa upatanisho sisi na Mungu.

Sadaka nyingine za fedha, mazao, mavazi n.k tunaweza kuzitoa, lakini dhabihu ilishatolewa, na Mungu karidhika na hiyo, na hakuna nyingine yoyote tunaweza kumtolea ikamridhisha.

Waebrania 10:3 “Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka.

4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

5 Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema,
Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari;

6 Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo;

7 Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) Niyafanye mapenzi yako, Mungu.

8 Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati),

9 ndipo aliposema, Tazama, nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi alisimamishe la pili.

10 Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu”.

Umeona hapo?. Kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu tumepata utakaso, hivyo Kristo ndio dhabihu iliyo hai leo.
Sasa swali ni kosa leo kuchinja kafara za wanyama?

Jibu ni ndio! kama wakristo hatupaswi leo kushiriki ibada zozote za kafara!. Wengi leo wanasema ni wakristo lakini vijijini kwao wanatoa kafara!..pasipo kujua kuwa wanamtolea dhabihu shetani na si Mungu.

Bwana atujalie neema yake, tuzidi kumjua yeye zaidi na mapenzi yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

Sadaka ya kutikiswa ilikuwaje?

Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?

Rudi nyumbani