MAFUNDISHO MAALUMU KWA WANANDOA: Epusha Wivu katika ndoa:
Huu ni mfululizo wa mafundisho maalumu yawahusuyo wanandoa: Ikiwa hukupata sehemu za nyuma, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba zetu zilizo chini ya somo hili, tukutumie;
Leo tutaona jinsi wivu unavyoweza kuathiri kwa sehemu kubwa mahusiano ya wanandoa.
Kibiblia wivu upo wa aina mbili:
1) Wivu wa kipepo: Ni ule wa kumuonea mtu kijicho, yaani kutotaka, mwenzako kufanikiwa kwasababu wewe hukufanikiwa kama yeye alivyofanikiwa, kutaka kile ambacho mwenzako anacho uwe nacho wewe huku hutaki yeye awe nacho. Biblia imetuonya sana dhidi ya wivu huu, kwasababu ni zao la shetani. Ndio walikuwa nao masadukayo na makuhani kwa Bwana wetu Yesu na mitume wake, pale walipoona neema ya Mungu ipo juu yao kubwa lakini kwao haipo, (Matendo 5:17, Warumi 13:13)
2) Wivu wa kimahusiano: Wanandoa, Huu ni wivu ambao ni wa asili, Mungu kauweka ndani ya mtu, huu upo katika mahusiano ya kindoa,au maagano Na ndio Wivu ambao Mungu amekiri pia mwenyewe anao.(Kutoka 20:5)..Huu ni wa kuulinda sana, hususani pale unapoingia kwenye ndoa, kwasababu madhara yake ni makubwa zaidi hata ya hasira, au ghadhabu. Biblia inasema hivyo katika..
Mithali 27:4 “Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika; Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu”.
Huu ndio umesababisha watu, kugombana, kuchukiana, kusalitiana na hata wakati mwingine kuuana, na kuwasababishia matatizo na wengine ambao hata hawahusiki.
Leo tutatazama, ni kwa namna gani, kinywa cha mwanamke, kinaweza kuwasha wivu mbaya sana, kwa upande wa pili. Na somo linalofuata tutaona tabia ambazo mwanaume anapaswa ajiepushe nazo, kuepukana na madhara ya wivu kwenye ndoa yake.
hii itakusaida, kuishi kwa amani na utulivu na kuinusuru ndoa yako, .
Sasa embu tusome kisa hichi tunachokiona katika 1Samweli 18:7. Si kisa cha kindoa lakini ni kisa kimuhusucho Daudi na Sauli, Wengi wetu tunajua sababu iliyomfanya Sauli amchukie Daudi, ambaye hapo mwanzo alimpenda ilikuwa ni Wivu. Lakini wachache sana, wanafahamu CHANZO cha wivu huo, kilikuwa ni nini?
Biblia inatupa majibu, kilikuwa ni wanawake, waliotoka na kutoa sifa zao, mahali pasipostahili kwa wakati ule. Embu Tusome.
1Samweli 18:5 “Basi Daudi akatoka kwenda kila mahali alikotumwa na Sauli, akatenda kwa akili; SAULI AKAMWEKA JUU YA WATU WA VITA; jambo hili likawa jema machoni pa watu wote, na machoni pa watumishi wa Sauli pia.6 Hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda.7 NAO WALE WANAWAKE WAKAITIKIANA WAKICHEZA, WAKASEMA, SAULI AMEWAUA ELFU ZAKE, NA DAUDI MAKUMI ELFU YAKE.8 Basi Sauli akaghadhibika sana, na maneno haya yakamchukiza; akasema, Wamempa Daudi makumi elfu, na mimi wamenipa elfu tu; kuna nini tena awezayo kupata, isipokuwa ni ufalme?9 Sauli akamwonea Daudi wivu tangu siku ile”.
1Samweli 18:5 “Basi Daudi akatoka kwenda kila mahali alikotumwa na Sauli, akatenda kwa akili; SAULI AKAMWEKA JUU YA WATU WA VITA; jambo hili likawa jema machoni pa watu wote, na machoni pa watumishi wa Sauli pia.
6 Hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda.
7 NAO WALE WANAWAKE WAKAITIKIANA WAKICHEZA, WAKASEMA, SAULI AMEWAUA ELFU ZAKE, NA DAUDI MAKUMI ELFU YAKE.
8 Basi Sauli akaghadhibika sana, na maneno haya yakamchukiza; akasema, Wamempa Daudi makumi elfu, na mimi wamenipa elfu tu; kuna nini tena awezayo kupata, isipokuwa ni ufalme?
9 Sauli akamwonea Daudi wivu tangu siku ile”.
Hicho ndicho kilichokuwa chanzo, cha vita vya Daudi na anguko la Sauli,. Wanawake wale walikuwa wanasema kweli, kwa waliyoyaona, lakini hawakutumia busara kuimba mbele ya mfalme, kwa wakati ule.. Huwenda hata Daudi, alitamani wakae kimya, wasimsifie yeye zaidi ya mfalme wake, mbele ya umati.. Lakini wale wanawake hilo halikuwa akilini mwao. Hawakujua kuwa kumbe nyimbo zao, sifa zao, maneno yao, ni panga ndani ya mioyo ya wakuu wao.
Ndio ikawa sababu ya Sauli kughahiri, hata vyeo vyote alivyompa Daudi, akampokonya na kumfukuza na kutaka kumuua kabisa, kwa kosa tu la wale wanawake. Lakini kama wale wanawake wangetumia busara, kumwimbia mfalme zaidi, basi Daudi angeendelea kustarehe na kudumishwa katika ufalme ule.
Maana yake ni nini?
Maneno yoyote ya sifa yanayotoka kinywani mwako wewe kama mwanamke, yana matokeo makubwa sana kwa upande wa pili. Sasa tukirudi katika upande wa ndoa, Wivu unatokea pale ambapo unathamini, au unasifia wanaume wengine zaidi ya mume wako. Ukiwa umeolewa tambua kuwa mume wako ndio,bora kuliko wanaume wote ulimwenguni, ndio mwenye sifa zote kuliko wanaume wote ulimwenguni.Hata kama wale wengine wamemzidi yeye kwa kiwango kikubwa kiasi gani, acha kuwazungumza zungumza mbele ya mume wako.
Hii ni kwa faida yako, na kwa wengine. Wanaume wengi wanagombana na marafiki zao vipenzi, kisa tu wake zao,wanapowasifia, wanakuwa mpaka maadui kwa sababu ndogo ndogo tu kama hizi,..Labda utasikia mmoja anasema, “mume wangu,rafiki yako huwa anapendezaga uvaaji wake, yaani navitiwa nao”..Kauli kama hizi ziepuke kinywani mwako, ili kunusuru, urafiki au ujirani wenu.
Kwa ufupi kauli zozote za sifa, zichungumze mara mbili mbili; Unaweza usione shida yoyote, au ukadhani ni jambo dogo tu, lakini upokee huu ushauri utakufaa kwa siku za mbeleni, , hilo jambo linamuathiri sana mwanaume. Usimzungumze zungumze mwanaume mwingine mbele ya mumeo, isipokuwa kwa kiasi, hata wale unaowaona kwenye tv, au unaowasiliana nao kwenye simu. Kumbuka wivu unawashwa na mambo madogo sana.
Bwana akubariki.
Je! Umeokoka? Je! Unauhakika wa maisha yako ya milele baada ya kifo? Kumbuka Kristo yupo mlangoni kurudi, dalili zote zimeshatimia, Huu si wakati wa kumbelezewa tena wokovu, ni wakati wa kujitahidi kuingia ndani ya Safina(Yesu Kristo) kwa nguvu zote, maana muda umekwisha.. Tubu dhambi zako, ukabatizwe mgeukie Bwana akupe uzima wa milele.
Maran Atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)
WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
Ndoa ya serikali ni halali?
Rudi nyumbani
Print this post
Jibu: Tusome,
Mwanzo 4:15 “BWANA akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. BWANA akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga.16 Kaini akatoka mbele za uso wa BWANA, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni17 Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe ”.
Mwanzo 4:15 “BWANA akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. BWANA akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga.
16 Kaini akatoka mbele za uso wa BWANA, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni
17 Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe ”.
“Nodi” sio jina la nchi kama vile Tanzania, Kenya au Uganda bali ni sifa ya nchi..Tafsiri ya neno Nodi ni “kutanga”. Hili ni neno la kiebrania lenye maana hiyo ya “kutanga”.
Kwahiyo biblia iliposema kuwa Kaini alienda nchi ya Nodi, haikumaanisha kuwa alienda kwenye Nchi inayoitwa “Nodi”.. La! bali ilimaanisha kuwa Kaini alienda katika Nchi ya “Kutangatanga”. Hakuwa na kikao maalumu, wala nchi maalumu sawasawa na laana Bwana Mungu aliyomlaania.
Mwanzo 4:11 “Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; 12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI”.
Mwanzo 4:11 “Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI”.
Vile vile dhambi inaweza kutufanya tusiwe watu wa vikao duniani, (tukawa watu wa kutanga tanga tu kutwa kuchwa). Tunazunguka huku na kule kutafuta unafuu wa maisha lakini hatuoni..Acha leo kutanga tanga, Suluhisho ni moja tu!, mkimbilie Bwana Yesu leo, mlilie akusamehe dhambi zako na akuokoe, kwasababu damu yake hata sasa bado inaondoa dhambi..
Na ukifanya hivyo kwa imani atakuokoa na laana ambayo imetajwa juu ya wote wamwachao Bwana..
Zaburi 107:4 “Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa. 5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao. 6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao. 7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa”.
Zaburi 107:4 “Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa.
5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.
6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa”.
Bwana Yesu akubariki.
Ikiwa utatamani kujua zaidi Mke wa Kaini alitokea wapi basi fungua hapa >>>JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?
Kaanani ni nchi gani kwasasa?
SISI NI WINDO BORA SANA, LA DHAMBI.
CHOCHOTE UMFANYIACHO KRISTO KINA THAMANI.
ANAKUJA KAMA “MWIVI” NA SI KAMA “ASKARI” FANYIKA CHOMBO CHA THAMANI.
LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.
Jina kuu la Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana lihimidiwe!. Karibu tujifunze biblia.
Je unajua maana ya kuzaliwa mara ya pili kwa Neno?.. Kupo kuzaliwa mara ya pili kwa maneno ya watu au ya mtu na pia kupo kuzaliwa mara ya pili kwa Neno la Mungu.
Neno la Mungu linasema hivi…
Yohana 3:3 “ Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO, HAWEZI KUUINGIA UFALME WA MUNGU”.
Yohana 3:3 “ Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO, HAWEZI KUUINGIA UFALME WA MUNGU”.
Umeona tafsiri ya kuzaliwa mara ya Pili kwa Neno la Mungu ni ipi?…si nyingine zaidi ya KUZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO.
Sasa unaweza kujiuliza maana ya kuzaliwa kwa maji na kwa roho ni nini?
Kuzaliwa kwa maji ni “Ubatizo wa Maji mengi”, na kuzaliwa kwa roho ni “Ubatizo wa Roho Mtakatifu” Kwahiyo unapoamini na kubatizwa kwa Maji tele (Yohana 3:23).. Na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, basi hapo unakuwa umezaliwa mara ya Pili kwa NENO LA MUNGU…(Kwasababu Neno la Mungu ndio linaelekeza hivyo).
Sasa umuhimu wa kufanya hivyo ni nini?
Ukiamini na kubatizwa na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, faida yake ya kwanza ni kwamba WOKOVU WAKO UNAKUWA NI WA KUDUMU, unakuwa sio wa kuchafuka chafuka..bali unakuwa ni thabiti siku zote mpaka siku utakapomaliza maisha yako hapa duniani.. Kwasababu Neno la MUNGU ni mbegu isiyoharibika.. Hivyo ukizaliwa kwa Neno la Mungu hilo (yaani kwa kubatizwa kwa maji na kupokea Roho mtakatifu), basi wokovu wako unakuwa imara daima…Ndivyo Neno la Mungu linavyosema..
1Petro 1:23 “Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si KWA MBEGU IHARIBIKAYO, BALI KWA ILE ISIYOHARIBIKA; KWA NENO LA MUNGU LENYE UZIMA, lidumulo hata milele”
Ni kwanini leo wokovu wa watu wengi unakuwa ni wa kusuasua, unakuta mtu leo kamkiri Yesu, lakini baada ya siku kadhaa au wiki kadhaa karudi kule kule, ijapokuwa yupo kanisani na karibu na wapendwa?.. ni kwasababu huenda mtu huyo hajazaliwa mara ya pili kwa Neno la Mungu (yaani kwa kubatizwa sahihi na kupokea Roho Mtakatifu)…
Huenda baada ya kumkiri Yesu akaambiwa hakuna haja ya ubatizo, au akakawishwa kubatizwa! Na kupokea Roho Mtakatifu… Hivyo kwa mbegu hiyo aliyopandikiziwa ndani yake, hawezi kusonga mbele kwasababu ni MBEGU INAYOHARIBIKA.. Lakini kama angezaliwa mara ya pili kwa Neno la Mungu, ambalo ndio mbegu isiyoweza kuharibika basi wokovu wake ungekuwa ni imara siku zote.
Ndugu unayesoma ujumbe huu, huenda wokovu wako ni wa nusu nusu, kiasi kwamba hata wewe mwenyewe hujielewi kama Kweli Kristo yupo ndani yako au la!.. katika hali hiyo uliyopo hebu jichunguze kama kweli umezaliwa katika Neno la Mungu.. Kwasababu Neno la Mungu linasema “Ni lazima kuzaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho”.
Je! Wewe umebatizwa inavyopaswa?.. kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38)..Na ubatizo sahihi wa Roho Mtakatifu ni ule unaozaa matunda yale yaliyoorodheshwa kwenye Wagalatia 5:22. Kama vitu hivyo viwili umevikosa, basi ni vizuri ukatafuta ubatizo sahihi haraka iwezekanikavyo na vile vile ubatizo wa Roho Mtakatifu.
Ikiwa mahali ulipo unaweza kupata ubatizo sahihi basi anza kwenda kuutafuta kuanzia sasa, lakini ikiwa unapata ugumu katika kutafuta, basi unaweza kuwasiliana nasi kupitia namba zetu hapo chini, tutakusaidia kukuelekeza mahali karibu na ulipo, ambapo utaweza kupata ubatizo sahihi.
AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!
UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.
Mkomamanga ni nini? Na katika biblia unawakilisha nini?
TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
Yerusalemu, ni Neno la kiyahudi linalomaanisha “Mji wa amani” au “msingi wa amani” .
Kabla ya mji huu kupata sifa tunayoifahamu sasahivi, awali ulikuwa ni mji wa wakaanani, waliojulikana kama wayebusi, kipindi ambacho wayahudi bado hawajaimiliki nchi yao.
Hivyo baada ya wana wa Israeli kuiteka nchi ya kaanani, eneo ambalo lilikuwepo huu mji, liligawanya kwa kabila la Yuda. Lakini hawa wayebusi hawakuondolewa moja kwa moja katika mji huo wa Yerusalemu, bado ukaendelea kuwa chini ya milki yao.
Mpaka baadaye, Daudi alipouvamia na kuwaondoa wayebusi. Ndipo Mji huo ukaitwa “Mji wa Daudi”.(2Samweli 5:6-10) Baadaye akalihamishia Sanduku la Mungu la agano, mpaka mji huo, hivyo kidogo kidogo ukaanza kupokea sifa ya kuwa kiini cha dini (2Samweli 6:1-19). Daudi akaazimia kumjengea Mungu hekalu ambalo, atamwekea Mungu agano lake huko. Lakini hakuruhusiwa kwasababu ya mauaji mengi aliyoyasababisha, Mpaka mtoto wake Sulemani, alipokuja kulijenga, Hapo ndipo wana wote wa Israeli wakapafanya Yerusalemu kuwa kitovu cha kumwabudia Mungu. Na Mungu pia akapabariki na kupachagua pawe mji wake mtakatifu, kati ya miji yote, ambapo ataliweka jina lake, lijulikane kwa mataifa yote ya ulimwengu..
Japokuwa eneo la mji huu, lilibomolewa na kujengwa mara kadhaa, lakini hapo ndipo mfalme wetu Yesu Kristo atakapokuja kutawalia dunia yote katika ule utawala wa miaka 1000 kama mfalme wa wafalme na Bwana wa Mabwana, atakaporudi mara ya pili.
Lakini biblia inatuonyesha kuwa upo mji mwingine wa kimbinguni, ambao Mungu amewaandalia watu wake,..ujulikanao kama YERUSALEMU MPYA.
Umechukua jina la Yerusalemu hii ya duniani, ili kutupa picha tuelewe vizuri utakavyokuwa. Mji huo utashuka kutoka mbinguni kwa Mungu mwenyewe na kuja hapa duniani. Ndani ya mji huo maandiko yanasema “hakitaingia chochote kilicho kinyonge”. Isipokuwa watu maalumu sana wajulikanao kama bibi-arusi wa Kristo.. Kumbuka si kila atakayepokea uzima wa milele, atakuwa na daraja sawa na mwenzake..Uaminifu wako, na utumishi wako sasa, vinaeneleza wewe utastahili kukaa wapi utakapofika kule ng’ambo. Wapo ambao watastahili kukaa ndani ya mji, na wapo ambao watakaa nje ya mji huo mtakatifu. Japo wote watakuwa ni watakatifu.
Ndani ya huo mji ndio yatakuwa makao mapya ya Mungu milele (Ufunuo 21:3), Mambo yaliyopo huko ni mazuri biblia inasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia(1Wakorintho 2:9). Kwa ufupi ni kwamba kila mmoja wetu atajuta, kwanini hakujibidiisha kwa Mungu sana kwa uzuri atakaokutana nao huko.
Huu ndio mji ambao Ibrahimu aliuona..ukamfanya aishi kama mpitaji tu hapa duniani, japokuwa alikuwa na mali nyingi na utajiri mwingi..
Waebrania 11:9 “Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. 10 Maana alikuwa AKIUTAZAMIA MJI WENYE MISINGI, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu”.
Waebrania 11:9 “Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
10 Maana alikuwa AKIUTAZAMIA MJI WENYE MISINGI, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu”.
Tafakari maandiko haya;
Ufunuo 21:1 “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena. 2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. 3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. 5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli. 6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure. 7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. 8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Ufunuo 21:1 “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.
2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.
3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.
5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.
6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.
7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Je! Na wewe utakuwa na sehemu ndani ya mji ule?
Maran atha.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Ninawi ni nchi gani kwasasa?
Sadaka ya Amani ilikuwaje?
Israeli ipo bara gani?
JINSI MUNGU ANAVYOIPIGA NA KUIPONYA AFRIKA.
Mretemu ni mti gani?
Hisopu/ Hisopo ni nini katika biblia?(Zaburi 51:7)
Neno ‘Kima’ linamaanisha nini Katika biblia? (Mathayo 27:9 )
Uchaga ni nini? (Luka 12:24)
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujinze biblia, Neno la Mungu wetu.
Yapo mambo ambayo watu wa Mungu wanatamani kuyapata au kuyafanya kwa muda waliopanga wao, lakini pasipo kujua pia upo muda wa Mungu wa kuruhusu mtu wake apate anachokitaka au afanye analolitamani. Ni muhimu sana kujua hilo.
Kikawaida pale tunapokuwa tumeokoka, na Kristo kakaa ndani yetu, basi tunapompelekea Mungu maombi yetu, au haja zetu au mahitaji yetu, basi anakuwa anayasikia na siku ile ile anayajabu kama tumeomba sawasawa na mapenzi yake.
Lakini sasa Matokeo ya majibu hayo yanaweza kuwa ni tofauti na mategemeo yetu.. Wengi tunatamani Bwana Mungu atupatia jambo Fulani na tunataka saa hiyo hiyo tukipate kile tulichoomba, pasipo kujua kuwa Mungu hataki tuangamie katika yale tunayomwomba..
Mithali 1:32 “….Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”.
Kwahiyo Mungu kabla hajakupa kile ulichomwomba, ni lazima kwanza aondoe upumbavu ndani yako… Na upumbavu mwingi tunakuwa tunazaliwa nao, kutokana na udhaifu wa mwili, na mwingine tunaupata kutokana na maisha ya dhambi tuliyokuwa tunayaishi…..Hivyo Mungu hawezi kutupa kitu kizuri halafu hatimaye kije kutuharibu .. vinginevyo atakuwa sio Baba mzuri na mwenye hekima.. Kwahiyo kipindi cha kuondolewa kwanza upumbavu mpaka kupokea majibu ya maombi, hapo ndio pana nafasi (inaweza kuchukua kipindi kirefu sana kuondolewa upumbavu).
Ili tuelewe vizuri tutafakari mfano ufuatao..
Wewe ni mzazi mwenye uwezo (tajiri) na mwanao ambaye anasoma chekechea anakuomba umpe Gari.. Kwa mzazi mwenye upendo na hekima, huwezi kuchukua gari na kumpa pale pale, bali utamwahidia kumpa gari!, ila si wakati ule, kwasababu bado hajajua hata kusoma na kusoma, hajajua kuhesabu, atawezaje kuendesha gari barabarani?.. Hivyo utakachofanya ni wewe kumpeleka kwanza shule ili upumbavu uondoke kichwani mwake, akajifunze gari ni nini, vile vile kanuni za kuendesha gari, na sheria za barabarani ili asisababishe ajali.. Hali kadhalika akajifunze matumizi ya gari si kwaaajili ya anasa bali kwaajili ya usafiri na kwaajili ya kazi.
Sasa wakati ambao umemwahidi gari mpaka siku ya kumpa hilo gari, inaweza kuchukua hata miaka 15.. Maana yake atakuja kulipata hilo gari akiwa na miaka 25, na ili hali yeye aliliomba akiwa na miaka 10.
Sasa jiulize! Kama sisi wazazi tuna hekima kama hiyo si zaidi Mungu!.. Huwezi kumwomba Mungu akupe jambo Fulani kubwa halafu akakupa papo kwa hapo, kwa akili uliyonayo hapo!… ni lazima akutengeneze kwanza!..na kutengenezwa kunaweza kukugharimu hata miaka kadhaa!… utakapofikia vigezo anavyovitaka yeye ndipo akupe kile ulichokiomba.
Ukiona bado hujakipokea kile ulichokiomba maana yake bado hujamaliza madarasa!… endelea kumngoja Bwana.
Huwezi kumwomba Mungu akupe mali nyingi na halafu akili yako inawaza anasa!..hawezi kukupa kwa wakati unaoutaka wewe,..itakugharimu kwamba upumbavu uondolewe ndani yako ndipo akupe!… huwezi kumwomba Mungu akupe nyumba na huku kichwani unawaza kuwakomoa watu au kuwaonyesha watu Fulani au kujivuna… hawezi kukupa kwa muda huo!, bado unao upumbavu ndani yako, ambao utakuharibu wewe endapo akikupa hiko kitu kwa muda huo!… atakachofanya kwaajili yako ni kuondoa kwanza upumbavu ndani yako kupitia madarasa yake,(na wakati mwingine hata ya kupitia umasikini), ili kupitia umasikini ule ujue kuwahurumia wengine, na siku utakapopata chako uweze kuwasaidia wengine… na kama ni mwepesi wa kumwelewa Mungu na upumbavu ukawahi kutoka ndani yako, basi ahadi utaipokea mapema, lakini kama ni mgumu, basi ndivyo ahadi yako itakavyozidi kuchelewa!.
Huwezi kukwepa hayo madarasa ya Mungu (hata ufanye nini).
Huwezi kumwomba Mungu akupe karama Fulani na huku moyoni mwako unawaza kujivuna, au kuwaonyesha watu Fulani, au kuwakandamiza wengine katika mwili wa Kristo…. Ni kweli umeomba jambo jema na siku ulipoomba alikusikia lakini hawezi kukupa kwa wakati huo, ambao akili yako inawaza mabaya… Ni sharti kwanza akupeleke kwenye madarasa yake maalumu, akufundishe nini maana ya karama za roho, nini lengo la karama za rohoni ndani ya mwili wa Kristo, n.k.
Ukishayaelewa madarasa hayo, kwa vipimo vyake yeye atakuhakiki na akiona umevikidhi vigezo ndipo anakupa, kwasababu anajua utavitumia vizuri kwa faida ya wengine na si kwa faida yako binafsi.
Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo, Utakapomwomba Mungu fahamu kuwa ni lazima akuandae ndipo akupe ulichomwomba, kwasababu yeye ni Baba mwema ambaye hapendi kutupa vitu ambavyo mwishoni vitatangamiza sisi wenyewe.
Hivyo kuanzia leo ndugu yangu, tafuta kuyajua mapenzi ya Mungu, kwasababu unapoyajua mapenzi ya Mungu, basi ni rahisi kupokea majibu ya maombi yako pale tu unapoomba kwasababu kunakuwa hakuna upumbavu mwingi ndani yako… Lakini kama huyajui mapenzi ya Mungu na huyafanyi basi majibu ya maombi yako yatakawia sana, haijalishi utaombewa na watumishi wote ulimwenguni!, bado kanuni za Mungu zitabaki kuwa zile zile..
Yakobo 4:2 “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi,3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu MWAOMBA VIBAYA, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.
Yakobo 4:2 “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi,
3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu MWAOMBA VIBAYA, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.
Kama unamwomba Mungu mtoto halafu kichwani unawaza kuwakomesha maadui zako, au kuwafumba kichwa watu fulani, huenda ombi lako hilo likachukua muda kidogo kupata majibu.. Lakini kama utamwomba Mungu akupe mtoto, kwasababu tu unahitaji kulea kwa fahari yako wewe mwenyewe, na si kwa sababu ya watu Fulani wa nje au maadui zako wakuone, basi huenda maombi yako yakachukua muda mfupi sana kujibiwa..
Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?
VITA DHIDI YA MAADUI
KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.
CHAMBO ILIYO BORA.
NJIA MOJAWAPO YA KUPATA MSAADA KUTOKA KWA MUNGU.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, lihimidiwe milele.
Kwanini leo hii tunaona kama vile utukufu wa Mungu umepungua makanisani?..Tunamwita Yesu aponye lakini haponyi, tunamwita atende miujiza lakini hatendi, tunamwita afungue watu lakini hawafungui kikamilifu? Ni kwanini?
Ni kwasababu yeye mwenyewe ni mgonjwa, yeye mwenyewe ni mlemavu, ana chechemea, hana masikio, yeye mwenyewe ni kipofu, yeye mwenyewe ana kisukari, amepooza, ana saratani, na homa ya ini, sasa atawezaje kuwaganga wengine? Angali yeye mwenyewe ni muathirika wa hayo mambo?
Tunashindwa kufahamu sisi tuliookoka ni viungo vya Kristo, na kila mmoja anayo nafasi ya kuujengwa mwili huo mpaka ukamilike, ili yeye kama kichwa atakaposhuka juu ya mwili wake, awe na uwezo na nguvu za kutosha kutembea na kutimiza wajibu wake, wa kuwahudumia na kuwafungua watu wake, kama alivyofanya alipokuwa hapa duniani.
Lakini changamoto tuliyonayo, ni pale tunapodhani kuwa wote, tunaweza kuwa miguu, wote tunaweza kuwa macho, wote tunaweza kuwa midomo,..Hivyo tunaelekeza bidii zetu zote, kuwa kiungo kimojapo ya hivyo.. Na hiyo yote ni kwasababu hivyo ndivyo vinavyoonekana vina utukufu kuliko vingine, kisa tu vipo kwa nje.
Lakini tunasahau kuwa mwili, hauundwi kwa viungo vya nje tu, bali pia na vile vya ndani. Na zaidi sana vile vya ndani ndio vinaumuhimu sana, na ndio maana vimefichwa na kufunikwa na vya nje, kwasababu hivyo vikipata hitilafu tu..hata hivi vya nje haviwezi kufanya lolote.
Kwamfano moyo, ukifeli, jiulize macho yako, mikono yako, miguu yako, itakuwa na kazi gani?.. Uti wa mgongo ukifeli, mwili wote utapooza, huo mkono utawezaje kusogea?..figo zimefeli, ni nini utakachokuwa unasubiri kama sio kifo..Lakini mguu mmoja ukifeli, mwili bado unaweza kuendelea kuishi..
Biblia inasema..
1Wakorintho 12:22 “Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi.23 Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana”.
1Wakorintho 12:22 “Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi.
23 Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana”.
Si kila mtu, atakuwa mchungaji katika kanisa ndio awe kiungo bora cha Kristo, si kila mtu atakuwa mwalimu, si kila mtu atakuwa nabii, au shemasi au mwimbaji..ikiwa wewe unajiona kama huwezi kusimama katika mojawapo ya nafasi hizo, haimaanishi kuwa wewe sio kiungo, suluhisho sio kujitenga na mwili wa kristo..huwenda wewe ni moyo, au figo au ini, au uti wa mgongo.. embu angalia ni nini unaweza kukifanya ukusanyikapo na wenzako..ni nini unaweza kuchangia katika mwili huo uliowekwa na Bwana..
kama ni kufuatilia na kusimamia ratiba na vipindi vyote vya kanisani, kama ni kuhamasisha na kuwaunganisha washirika, kama ni kuchangia kwa bidii kwa mali zako, kama ni kuongoza watoto, kama ni ulinzi, kama ni usafi, kama ni kuongoza maombi na mifungo..n.k. uwapo mbali au uwapo karibu. Hakikisha unafanya kwa bidii zote na sio kwa ulegevu..
Wafilipi 4:8 “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.9 Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, YATENDENI HAYO; NA MUNGU WA AMANI ATAKUWA PAMOJA NANYI”.
Wafilipi 4:8 “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
9 Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, YATENDENI HAYO; NA MUNGU WA AMANI ATAKUWA PAMOJA NANYI”.
Lakini usikae tu, mwenyewe, na kuwa mtu wa kwenda tu kanisani na kurudi nyumbani, kama mtembeleaji tu..miaka nenda miaka rudi, utawalaumu viongozi, utalilaumu kanisani, kumbe shida ni wewe ambaye hujasimama katika nafasi yako. Kama ‘mapafu’ umejitenga kivyao,unaliangalia kanisa la Kristo likipumulia mirija.
Tubadilike, sote tujiwajibishe, ili Kristo ashushe utukufu wake kama kanisa la mwanzo. Hivyo ili Kristo atukuzwe, na aweze kutenda kazi yake, sote kwa pamoja tuje katika nia moja ya Kristo, kisha kila mtu asimame katika nafasi yake, Kristo akamilike, ndipo tuone matendo yake makuu, akiyatenda kama alivyofanya katika kanisa la mwanzo.
Bwana awe na nasi. Bwana awe na kanisa lake takatifu.
Shalom.
Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1).
DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:
NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.
NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA
Maongeo ni nini?(Wakolosai 2:19)
USHAURI KWA MWANAMKE WA KIKRISTO.
SWALI: Nini maana ya maandiko haya?
Mithali 25:28 “Asiyetawala roho yake Ni mfano wa mji uliobomolewa, usio na kuta”.
JIBU: Mstari huu unatupa picha jinsi mtu asiyeweza kuitawala roho yake anavyoonekana rohoni.Hapo anasema, roho yake imefanana na mji uliobomolewa usio na kuta..
Zamani, miji mikubwa ilipojengwa ilikuwa ni lazima izungushiwe kuta kubwa na ndefu.. Yerusalemu ulizungushiwa kuta, Babeli ulizungushiwa kuta, Yeriko ulizungushiwa kutwa n.k. Na lengo la kufanya vile ilikuwa ni kuulinda mji dhidi ya wavamizi, na wapepelezi, wasiingie kokote tu watakako na kuushambulia mji.
Ni vijiji na vimiji vidogo tu ndivyo vilikuwa havina kuta zinazozunguka..lakini miji yote ilikuwa ni lazima iwe na sifa hiyo.
Sasa na rohoni ndivyo ilivyo, ikiwa na maana, kama wewe si mtu wa kuitawala roho yako, ni sawa na ule mji usio na kuta..Na matokeo yake ni kuwa upo hatarini kuvamiwa na kila aina ya maadui zako wa rohoni.
Ukishindwa kuizuia roho yako na tamaa za huu ulimwengu..Kwamba kila kitu unachojisikia kukifanya, wewe unafanya, kijisikia kuzini unakwenda kuzini, ukijisikia kunywa pombe unakunywa.. ukijisikia kuvaa vimini unavaa, ukijisikia kuvaa suruali unavaa, ukijisikia kutumia mkorogo unatumia, fahamu kuwa, utakuwa ni makao ya mapepo yote mabaya duniani.
Kwasababu roho yako haina ulinzi. Ndugu si kila kitu unachokiona, ukifanye, au ukiangalie, au ukisikilize, unapokesha muda wote kwenye tamthilia, kwenye simu unachati, lakini muda wa kuomba huna, muda wa kujifunza Neno huna.. Wewe ni mji usiokuwa na ukuta..
Utaombewa leo, mapepo yatatoka, lakini kesho yatarudi tena mengine mengi tu, tatizo ni hilo, umefungua malango kwa kila roho inayojisikia kukuingia ..kwasababu umeshindwa kuitawala roho yako. Leo rafiki yako anakuja kukwambia tukabeti, na wewe bila kufikiri unakimbilia huko, unatazama picha za ngono, unasikiliza miziki ya kidunia, ni lazima uvamiwe na mapepo.
Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima”.
Hivyo ni lazima tujifunze kuzitawala roho zetu, sawasawa na maandiko yanavyotasa.
JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.
Je! Ni dhambi kwa kijana aliyeokoka kuvaa suruali za kubana (model), kunyoa mitindo (mfano kiduku), ?
Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)
NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.
Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?
Ufisadi ni nini?
Swali: Katika 1Wakorintho 7:36 Mtume Paulo anafundisha kuwa Mtu akiona hamtendei vyema mwanamwali wake basi aruhusu waoane”.. Je alikuwa ana maana gani kusema hivyo? (Au kwa ujumla mstari huo unamaanisha nini)?.
Jibu: Labda tuanze kusoma kuanzia juu kidogo mstari wa 34.
“1Wakorintho 7:34 “Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe.35 Nasema hayo niwafaidie, si kwamba niwategee tanzi, bali kwa ajili ya vile vipendezavyo, tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine.36 Lakini mtu awaye yote akiona ya kuwa hamtendei mwanamwali wake vipendezavyo, na ikiwa huyo amepita uzuri wa ujana wake, na ikiwapo haja, basi, afanye apendavyo, hatendi dhambi, na awaruhusu waoane.37 Lakini yeye aliyesimama kwa uthabiti wa moyo wake, hana sharti, lakini aweza kuyatawala mapenzi yake, tena amekusudia moyoni mwake kumlinda mwanamwali wake, atatenda vema.38 Basi, hivyo na amwozaye mwanamwali wake afanya vema; na yeye asiyemwoza atazidi kufanya vema.”
“1Wakorintho 7:34 “Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe.
35 Nasema hayo niwafaidie, si kwamba niwategee tanzi, bali kwa ajili ya vile vipendezavyo, tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine.
36 Lakini mtu awaye yote akiona ya kuwa hamtendei mwanamwali wake vipendezavyo, na ikiwa huyo amepita uzuri wa ujana wake, na ikiwapo haja, basi, afanye apendavyo, hatendi dhambi, na awaruhusu waoane.
37 Lakini yeye aliyesimama kwa uthabiti wa moyo wake, hana sharti, lakini aweza kuyatawala mapenzi yake, tena amekusudia moyoni mwake kumlinda mwanamwali wake, atatenda vema.
38 Basi, hivyo na amwozaye mwanamwali wake afanya vema; na yeye asiyemwoza atazidi kufanya vema.”
Hapa Paulo kwa kuongozwa na roho anatoa USHAURI WA KITUME, juu ya watu wanaotaka kuoa na wale wasiotaka kuoa, au wa wale wanaotaka kuolewa na wasiotaka kuolewa.
Ukisoma kuanza juu zaidi utaona anashauri kuwa ni “Ni heri mtu akae bila kuoa kabisa, au kutoolewa kabisa kwaajili ya Bwana, kuliko kuoa au kuolewa”.. lakini hiyo sio sharti au Amri, bali chaguzi la mtu!!. Maana yake ni kuwa Mtu atakayeoa atakuwa hafanyi dhambi, na vile vile atakayeolewa atakuwa hafanyi dhambi… Lakini mtu ambaye atakaa bila kuoa au kuolewa, huyo ana faida mara nyingi zaidi kwasababu atakuwa atajishughulisha zaidi na mambo ya Mungu pasipo kuvutwa, au kusongwa na mambo mengine ya kifamilia.
1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”
1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;
33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”
Lakini Paulo hajaishia tu kutoa ushauri kwa Watu wanaotaka kuoa au kuolewa, bali alienda mpaka kwa wazazi wenye mabinti majumbani kwao ambao ni mabikira (wanawali).
Akashauri kuwa ikiwa Mzazi, anaye binti au mabinti ambao bado hawajaolewa, Na mzazi huyo anatamani mabinti wake wamtumikie Mungu pasipo kuvutwa na mambo mengine, zaidi sana na yeye mwenyewe ana uwezo wa kuyatawala mapenzi yake (Yaani sio kigeugeu, cha kutamani kupata wajukuu au kuitwa mkwe), basi anaweza kuwadumisha wanawe (mabinti wake) katika kuishi maisha ya kutotamani kuolewa, ili wamtumikie Mungu vyema, pasipo kuvutwa na mambo mengine..kama wale mabinti wane wa Filipo waliokuwa manabii, wanatabiri..
Matendo 21:8 “Asubuhi yake tukaondoka, tukafika Kaisaria, tukaingia nyumbani mwa Filipo, mhubiri wa Injili, aliyekuwa mmoja wa wale saba, tukakaa kwake.9 Mtu huyu alikuwa na binti wanne, mabikira, waliokuwa wakitabiri”.
Matendo 21:8 “Asubuhi yake tukaondoka, tukafika Kaisaria, tukaingia nyumbani mwa Filipo, mhubiri wa Injili, aliyekuwa mmoja wa wale saba, tukakaa kwake.
9 Mtu huyu alikuwa na binti wanne, mabikira, waliokuwa wakitabiri”.
Kuwalea mabinti kwa namna hiyo kuna faida kubwa sana…kwasababu biblia inasema katika Mithali 22: 6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”. Ikiwa na maana kuwa msingi ambao mtoto wako utakaomwekea tangia akiwa mdogo huo hawezi kuuacha mpaka atakapokuwa mtu mzima. Na msingi mmojawapo ambao ni mzuri ndio huo wa Kutokuja kuolewa/kuoa, ili kusudi wamtumikie Mungu pasipo kuvutwa na mambo mengine, katika siku za mbeleni.
Sasa Paulo hajatoa amri kwamba ni lazima wazazi wote wafanye hivyo kwa mabinti zao… bali ni “Ushauri tu wa kitume anaoutoa”.. Lakini pia anaendelea kusema, ikiwa mzazi anaona kuwa binti yake (Mwanamwali wake), hamtendei jinsi ipasavyo (maana yake binti yake anatamani kuolewa na yeye mzazi ni kikwazo) basi hapaswi kuendelea kumshikilia huyo binti kwa kumzuia kuolewa, bali amruhusu aolewe, na kwa kufanya hivyo pia atakuwa hatendi dhambi..
1Wakorintho 7:36 “Lakini mtu awaye yote akiona ya kuwa hamtendei mwanamwali wake vipendezavyo, na ikiwa huyo amepita uzuri wa ujana wake, na ikiwapo haja, basi, afanye apendavyo, hatendi dhambi, na awaruhusu waoane.37 Lakini yeye aliyesimama kwa uthabiti wa moyo wake, hana sharti, lakini aweza kuyatawala mapenzi yake, tena amekusudia moyoni mwake kumlinda mwanamwali wake, atatenda vema.38 Basi, hivyo na amwozaye mwanamwali wake afanya vema; na yeye asiyemwoza atazidi kufanya vema”.
1Wakorintho 7:36 “Lakini mtu awaye yote akiona ya kuwa hamtendei mwanamwali wake vipendezavyo, na ikiwa huyo amepita uzuri wa ujana wake, na ikiwapo haja, basi, afanye apendavyo, hatendi dhambi, na awaruhusu waoane.
38 Basi, hivyo na amwozaye mwanamwali wake afanya vema; na yeye asiyemwoza atazidi kufanya vema”.
Ni nini tunajifunza?
Kama mzazi, mojawapo ya mafundisho au msingi wa kuwawekea wanao ni pamoja na huo wa kutafakari au kufikiri kutokuja kuoa au kuolewa huko mbeleni (kwaajili ya Bwana).. Kumbuka “sio kumzuia mwanao kuoa au kuolewa” la! bali kumfundisha au kumwekea msingi huo, ili atakapokuja kufikia umri wake mwenyewe aone kila sababu za yeye kuishi kama alivyo kwaajili ya Bwana na utumishi wake..
Ushauri huu unaweza kuonekana kama mpya na wa ajabu lakini ndio ushauri wa kitume. (Paulo, aliye baba yetu wa kiroho alilihakiki hilo kwa msaada wa roho) hivyo na sisi tukitaka tupate faida nyingi za kiroho basi tusikilize ushauri huo. Lakini si Lazima, wala si sharti.(hatujalazimishwa)
1Timotheo 2:7 “Nami kwa ajili ya huo naliwekwa niwe mhubiri na mtume, (nasema kweli, sisemi uongo), mwalimu wa Mataifa katika imani na kweli”.
Ikiwa kama unapenda kujua zaidi kama ni Sharti mchungaji kuoa au kutokuoa katika utumishi wake basi unaweza kufungua hapa>> Je! Mtu ambaye hajaoa anaruhusiwa kulichunga kundi?
JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?
Wanafunzi wa Yesu, walimaanisha nini kusema kama “Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa”?
Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”
Hapo ndipo, atakapompa Mungu Baba ufalme wake.
JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?
Biblia inasema Bwana Yesu alifundisha kwa mifano. Naomba kuelewa hiyo mifano ni nini? Na dhumuni lake lilikuwa ni lipi?
Mifano, ni hadithi zinazoambatanishwa na habari husika, ili kueleza uhalisia zaidi wa ukweli huo.
Bwana Yesu alitumia mfumo huu, wa hadithi za kidunia ili kueleza uhalisia wa mambo ya ufalme wa mbinguni. Na takribani mafundisho yake yote yalitegemea mifano.
Mathayo 13:34 “Hayo yote Yesu aliwaambia makutano kwa mifano; wala pasipo mfano hakuwaambia neno;35 ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, Nitayatamka yaliyositirika tangu awali”.
Mathayo 13:34 “Hayo yote Yesu aliwaambia makutano kwa mifano; wala pasipo mfano hakuwaambia neno;
35 ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, Nitayatamka yaliyositirika tangu awali”.
Mpaka ikafikia wakati Fulani wanafunzi wake wanamuuliza kwanini unapenda kutumia mifano kufundisha watu?(Mathayo 13:10)
Kwamfano alipotaka kueleza habari ya madhara ya kutokusamehe, alitumia hadithi ya yule mtu aliyedaiwa talanta elfu kumi, ambaye alikuwa karibuni na kuuzwa kwa kukosa cha kulipa, lakini bwana wake akamuhurumia akamsemehe deni lote, lakini yeye alipokutana na mtumwa wake aliyemdai dinari 100 tu hakutaka kumsamehe, matokeo yake bwana wake aliposikia tabia yake hiyo akamkamata na kumtupa gerezani, mpaka na yeye atakapolipa yote(Mathayo 18:21-35).
Hivyo mtu unaposikia hadithi hiyo, inakupelekea kuelewa zaidi jinsi Mungu naye anavyojisikia pale tunaposhindwa kuwasamehe watu makosa yao .
Katika Biblia ni mifano zaidi ya 30 Bwana Yesu aliisema, lakini ni mingi zaidi ya hiyo aliifundisha, ambayo haijaandikwa kwenye biblia, (Yohana 21:25)
Madhumuni na mifano hiyo yalikuwa ni mawili:
Bwana Yesu alipoizungumza kwa waliokuwa na kiu ya kusikia, aliieleza kwa uwazi wote bila maficho yoyote.
Lakini alipokutana na kundi la watu ambao hawakuwa na nia ya kujifunza, watu wenye wivu, mafarisayo na waandishi ambao walimkufuru Roho Mtakatifu pamoja na maherodi, alikuwa anatumia mifano ya mafumbo, ili wasielewe chochote. Na alipokuwa peke yake alihakikisha anawafunulia mafumbo hayo wale ambao walikuwa na kiu ya kuujua ukweli.
Mathayo 13:13 “Kwa sababu hii nasema nao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa.14 Na neno la nabii Isaya linatimia kwao, likisema, Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona.15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya”.
Mathayo 13:13 “Kwa sababu hii nasema nao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa.
14 Na neno la nabii Isaya linatimia kwao, likisema, Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona.
15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya”.
Hivyo mfumo huu hata sasa Bwana anautumia rohoni.. ukiwa kweli na nia ya kumjua Mungu, atakufundisha sana, na kutumia hata mifano halisi ya kimaisha ili mradi tu ahakikishe unayaelewa mapenzi yake, vema na kwa ufasaha wote. Lakini ikiwa mwovu, na unajifanya unamjua Mungu, ukweli ni kwamba hutamwelewa, atakuja kwako kwa mafumbo mengi tu.. Utakuwa kila siku ni mtu wa kutomwelewa Mungu, na kumtumikia kidini tu.
Bwana Yesu atusaidie tuwe na kiu ya kweli kwake. Kwasababu hii biblia haijakusudiwa kila mtu aielewe bali wale wenye nia tu ya dhati kwa Bwana..walio maskini wa roho.
KWA WALE WALIO NJE “YOTE” HUFANYWA KWA MIFANO
MPENDEZE MUNGU ZAIDI.
Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.
MAKABURI YAKAFUNUKA; IKAINUKA MIILI MINGI YA WATAKATIFU WALIOLALA;
Ni kwanini Yesu alisema “Na wakisikia wasikie, wasielewe Wasije wakaongoka?”
Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.
KUOTA UNAPEWA PESA, KUNA MAANISHA NINI?
Swali: Katika 1Samweli 17:49, tunasoma kuwa ni Daudi ndiye aliyemwua Goliathi, lakini katika 2Samweli 21:19, tunaona biblia inamtaja mtu mwingine kabisa aliyeitwa Elhanani kuwa ndiye aliyemwua Goliathi, je kiuhalisia ni yupi aliyemwangusha Goliath kati ya hao wawili?
1Samweli 11: 49 “Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi. 50 Hivyo Daudi akamshinda yule Mfilisti kwa kombeo na jiwe, akampiga Mfilisti, akamwua; walakini Daudi hakuwa na upanga mkononi mwake”
1Samweli 11: 49 “Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi.
50 Hivyo Daudi akamshinda yule Mfilisti kwa kombeo na jiwe, akampiga Mfilisti, akamwua; walakini Daudi hakuwa na upanga mkononi mwake”
Tusome tena..
2Samweli 21:19 “Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, ALIMWUA GOLIATHI, MGITI, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji. 20 Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambako kulikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne; yeye naye alizaliwa kwa Mrefai”.
2Samweli 21:19 “Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, ALIMWUA GOLIATHI, MGITI, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji.
20 Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambako kulikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne; yeye naye alizaliwa kwa Mrefai”.
Goliathi halikuwa jina la mtu mmoja maalumu, kwamba hakuna mtu mwingine kabla ya hapo, au baada ya hapo aliyeitwa kwa jina hilo, bali lilikuwa ni jina ambalo watu wengi walikuwa wanalitumia/wanaitwa, kwahiyo huyu Goliathi aliyeuawa na Daudi ni tofauti na huyu aliyeuawa na Elhanani.. Ingawa wote wana majina yanayofanana na sifa zinazofanana.. Ni kama tu Yohana Mbatizaji na Yohana Mwanafunzi wa Yesu, walivyokuwa na majina yanayofanana na utumishi unaokaribia kufanana lakini ni watu wawili tofauti.
Kwahiyo hawa ni watu wawili tofauti wenye majina yanayofanana..Ndio maana utaona hapo kwa huyu Elhanani ni vita vingine kabisa, ambavyo tayari Daudi alikuwa ameshakuwa mfalme…” 2Samweli 21:19 “Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, ALIMWUA GOLIATHI, MGITI, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji”.
Sasa ili kujua ni nini tunaweza kujifunza kwa huyu shujaa Elhanani aliyemwua Goliathi, pamoja na mashujaa wengine wa Daudi (idadi yao 37) ambao walioangusha majitu kama alivyofanya Daudi.. basi unaweza kufungua hapa >>>LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.
NI MAONO YAPI HAYO UNAYOSUBIRIA?
Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?
Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)
Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?