Category Archive Home

Nguzo kuu za ukristo ni zipi?

Somo la nyuma tuliona msingi wa Ukristo ni nini.. kwamba Yesu Kristo Bwana wetu ndiye msingi  wenyewe..Yeye huitwa jiwe kuu la pembeni, na mwamba ambao juu yake sisi sote tumewekwa, pasipo Yesu hakuna ukristo. Yeye ndio msingi wa imani yetu.

Lakini pia kikawaida msingi ukishakaa chini, huwa nguzo zinafuata juu yake, kazi ya nguzo ni kulifanya jengo liweze kushikamana na kusimama vema toka juu kwenye paa mpaka chini kwenye msingi wenyewe.

Hivyo wewe kama mkristo ukishaweka msingi chini wa nyumba yako ya kiroho, fahamu pia moja kwa moja utanyanyua na nguzo zake, ili kuliunda jengo. Je nguzo zenye ni zipi?

Hizi ndizo nguzo kuu saba (7), za ukristo .

  1. UPENDO
  2. MAOMBI
  3. NENO
  4. USHIRIKA
  5. UTAKATIFU
  6. UINJILISTI
  7. UTOAJI

1.     UPENDO

Ni wajibu wa kila mwamini aliyekombolewa na Kristo, pindi tu alipookoka aanze kukua ki-upendo.  Hii ndio nguzo mama, kwasababu Mungu mwenyewe ni upendo (1Yohana 4:8). Zaidi sana anapaswa afahamu kuwa, upendo wa ki-Mungu sio kama ule wa kibinadamu

wa kupenda wanaokupenda, hapana ..huu ni upendo unaozidi usio na sharti wa kujitoa, ambao unapenda mpaka maadui, zaidi na kuwaombea wanaokuudhi.

Mtu asiyejijenga katika huu, haijalishi atajitaabisha vipi kwa Kristo, kazi yake itakuwa ni ya hasara siku ile ya mwisho.

1 Wakorintho 13 : 1-13

1 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi

cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama

sina upendo, hainifaidii kitu.

4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha,

zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.

2) MAOMBI

Ili   maisha ya mkristo yasimame vema, maombi ni nguzo nyingine inayomkamilisha. Biblia inasema maombi yanapaswa yawe ni jambo la daima.

Wakolosai 4:2 Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani;

Maombi ni sawa na maji mwilini, au mafuta kwenye gari, vikikosekana hivi vitu hakuna utendaji kazi wowote utakaoendelea, vivyo hivyo ukristo wako usipokuwa wa maombi, hautaendelea sana. Utakufa tu siku moja

Ili tujengeke vizuri kiwango cha chini Bwana alichotaka tuombe kwa siku ni saa moja (Mathayo 26:40). Bwana Yesu alikuwa mwombaji, mitume walikuwa waombaji, sisi yatupasaje?

3.     NENO (mafundisho)

Ukishaokoka, jambo linalofuata ni kuwa karibu na biblia yako. Katika hiyo utapata kuelewa mpango kamili wa Mungu katika maisha yako. Huku ukisaidiwa na waalimu na wakufunzi wako kwenye usomaji wako wa biblia, kama Bwana wetu Yesu alivyokuwa mdogo akifanya bidii kuwasikiliza waalimu wake.

Kujifunza na kusoma kunapaswa kuwe ni tendo la kila siku. Neno ni kama chakula na maombi ni maji. Hivi viwili ndivyo vinakukuza kiroho na kukujenga nafsi. Hupaswi kuacha kusoma.. Mkristo asiyeifungua biblia yake ni rahisi sana  kuchukuliwa na upepo wa ibilisi kwa mafundisho potofu. Kwasababu  hamjui Mungu.

Hekima, maarifa, imani, ufahamu,na  mamkala vinatoka katika kulijua Neno na mafundisho. Hivyo soma hiyo kila siku, pia sikiliza mafundisho kutoka kwa waalimu wako sahihi wa kweli, kwasababu ni muhimu sana kuvipata.

Matendo 2:41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.

42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.

1Timotheo 4:13 Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha

4.     USHIRIKA

Ushirika ni kukutana pamoja na wenzako kujengana. Ushirika ni umoja wa Roho katikati yetu.

Waebrania 10:25 wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.

Kama mtakatifu, hupaswi kujiaminisha utakuwa na utimilifu wote wa ki-Mungu ndani yako kivyako. Utahitaji kukamilishwa na wengine kwa sehemu baadhi, Ndio hapo suala la ushirika linakuja.

Ndio sababu Mungu ameweka karama tofauti tofauti ili tujengane. Katika ushirika mtaombeana, kushiriki meza ya Bwana pamoja, mtafarijiana, mtasaidiana n.k.

Na pia biblia inasema wawili walalapo watapata joto.

Mhubiri 4:9 Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.

10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!

11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona

moto?

12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatuhaikatiki upesi.

Muwapo pamoja kuna ulinzi wa kipekee unaongezeka juu yenu. Hivyo kamwe usijaribu ule ukristo wa kivyako-vyako. Ni lazima tuwe washirika wa kanisa. Kama kanisa la kwanza lilivyoweza kusimama kwa kanuni hiyo.

5.     UTAKATIFU

Utakatifu ni utambulisho wa ukristo. Huwezi kuwa mkristo, halafu ukawa mwovu, huwezi kupokea Roho Mtakatifu halafu sifa za utakatifu usizionyeshe ndani yako. Kwasababu maandiko yanasema Mungu tunayemtumikia ni Mtakatifu hivyo na sisi pia hatuna budi kuenenda katika utakatifu. Bwana Yesu pamoja na watakatifu wa kwanza walizingatia viwango vyote vya usafi na ukamilifu. Vivyo hivyo na sisi

1Petro 1:16 kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

 6) UINJILISTI

Ushuhudiaji unaanza pindi tu unapookoka.  Kila mkristo ameitwa kuitenda kazi ya Bwana. Na ni lazima afanye hivyo kama sehemu ya maisha yake, ili safari yake ya wokovu hapa duniani iwe imara ni lazima azae matunda.  Uwakili ni kazi yetu ya daima. Ukristo bila uinjilisti hauwezi kuwa imara. Kanisa la kwanza lilikuwa la kiinjilisti. Kila mmoja alitambua wajibu wake wa kuisambaza injili kila mahali walipokuwa wakilizingatia lile agizo la Bwana.

Matendo 8:4 Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.

.

7.     UTOAJI

Sifa ya Mungu ni utoaji, ndio maana mpaka leo tunanufanika na mengi katika ulimwengu wake. Hata tulipopotea katika dhambi alijitoa kwa ajili yetu kwa  kumtoa mwanawe awe fidia.

Na sisi kujitoa kihali na kifedha kwa ajili ya injili na kanisa la Kristo, ni nguzo muhimu sana. Unawajibu wa kuisapoti huduma inayokukuza kiroho, kwa zaka na changizo zako, pamoja na  kuwasaidia ndugu (maskini).  Kwasababu, Bwana Yesu na kanisa la kwanza lilikuwa na desturi hiyo.

1 Wakorintho

16:1 Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo

Hivyo sisi sote tukizitendea kazi nguzo hizo muhimu, basi tuwe na uhakika jengo letu la Imani litakuwa imara sana, linaloweza kustahili tufani na majaribu yote, lililoundwa vyema, kwa utukufu wa Mungu, hata siku ile ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKAE NANYI NYOTE.

USIKWEPE USHIRIKA NA MADHABAHU YA KRISTO.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini matajiri wanaambiwa walie na kupiga yowe (Yakobo 5:1-6)

Yakobo 5:1-6

Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.

Biblia inatoa angalizo na tahadhari katika eneo la watu wanaoitwa matajiri. Kimsingi utajiri si dhambi, na ni mapenzi ya Mungu watu wake wafanikiwe, (lakini si katika hila).

Hivyo biblia inafunua siri za matajiri wengi wadhalimu, na kuwaonya mapema ili wajirekebishe kwasababu kuna adhabu kali wameandaliwa mbeleni kwa ajili yao.

Biblia inafunua vyanzo vikuu vya mafanikio yao, wala sio katika uchawi kama wengi wanavyodhani,.. bali vipo kwa “wale watu wawatumikiao”, walio chini yao, au wanaowatumia kufanya shughuli zao.

Matajiri wengi, huwatumia wao kama daraja la wao kufika juu, ndio hapo hutumia njia ya kuwatumikisha zaidi ya kawaida yao, na kuwalipa mishahara midogo, au hata wakati mwingine kuwadhulumu kabisa kutowapa kitu, na kuwanyanyasa, hawajali malalamiko yao, na changamoto zao na mahitaji yao. Wanachojali ni kiasi gani kimepatikana, au kazi ngapi zimekamilika. Ili wapate fedha wakazijaze hazina zao.

Lakini Hawajui kuwa Kilio chao kinamfikia Mungu mbinguni. Ijapokuwa wao wanaweza wasione chochote. Kumbe hawajui wanajikusanyia adhabu kali siku ile ya hukumu.

Biblia imetumia mfano wa “bwana na mkulima wake” aliyemwajiri kwenye shamba lake… akiwawakilisha watu wote wenye wafanya-kazi chini yao.

Anasema..

Yakobo 5:1-6

[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.

[2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.

[3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.

[4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.

[5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.

[6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.

Umeona? wamejilisha mioyo yao utajiri, wamejinenepesha tayari kwa machinjo yao wenyewe..

Hiyo ndio sababu pale mwanzo anatangulia kwa kusema “walie, na kupiga yowe”, kwa hiyo adhabu kali inayokuja juu yao…yaani akimaanisha watubu haraka sana, ili mabaya hayo yasiwakute.

Ujumbe huu ni hata sasa?

Yaweza kuwa bado hujafikia kiwango cha utajiri wowote lakini hata ukiwa na mtu/watu uliowaajiri chini yako, bado upo kwenye mkondo huo huo wa matajiri,

hivyo wajali sana watumwa wako wape maslahi yao,.sikiliza sana malalamiko yao, kuwa tajiri usiye na lawama, mfano wa Ayubu, ambaye aliwathamini sana watumishi wake mpaka akasema..

Ayubu 31:13-15

[13]Kama nimeidharau daawa(mashtaka) ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu, Waliposhindana nami;

[14]Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini? Naye atakapozuru, nitamjibuje?

[15]Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?

Kuwa tajiri kwa kutenda mema, hapo ndipo baraka zitakapokuja.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

Rudi Nyumbani

Print this post

AKAUKAZA USO WAKE KWENDA YERUSALEMU.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya uzima. Leo napenda tujifunze tabia nyingine ya Bwana Yesu. Kwasababu yeye mwenyewe alituambia ‘tujifunze kwake’. Hivyo naamini tuna mengi ya kuyajua kuhusu yeye.

Habari hiyo tunaisoma katika vifungu hivi;

Luka 9:51  Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;

52  akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.

53  Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.

54  Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?

55  Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]

56  Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine.

Kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utakumbuka kuwa kuna wakati ulifika, ilikuwa wazi kwa watu wote, kuwa Yesu anatafutwa ili auawe, (hususani kule Yerusalemu). Na hilo lilimfanya mara kadha wa kadha asitembee kwa uwazi wote mbele ya makutano (Yohana 7:10), kwasababu, saa yake ya kuuawa ilikuwa bado haijafika.

Yohana 11:54  Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.

Lakini mambo yalikuja kubadilika baadaye,  hilo halikuendelea kwa wakati wote. Alipoona sasa kazi aliyopewa na Mungu ameimaliza, alionyesha tabia nyingine ambayo haikuwa ya kawaida. Biblia inatuambia, “aliukaza uso wake kuelekea Yerusalemu”, kule kule alipokuwa anatafutwa auawe.

Jambo ambalo lilileta mshtuko hata kwa mitume wake;

Yohana 11:7  Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.

8  Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?

9  Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

Walishangaa, ujasiri huo ni wa namna gani? Ni sawa na wanajeshi waliokwenda vitani, halafu maadui wakawaua wanajeshi wote, akabakia mmoja tu, halafu huyo mmoja anasema nitakwenda kupambana na jeshi lote hilo peke yangu sitajificha. Ukweli ni kwamba inahitaji nguvu nyingine ya ziada ndani ya huyo mtu.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, aliukaza uso wake, kwenda kututetea sisi. Embu Fikiria kama angeulegeza, na kuendelea kuzunguka mahali pengine na sio kule uyahudi(Yerusalemu), wokovu wetu tungeupatia wapi?

Ilibidi, alazamishe mambo, japo mwili wake ulikuwa hautaki, ndio maana akiwa pale bustanini, anaomwomba Baba, akisema ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, ni kuonyesha kuwa hata mwili wake ulikuwa unagoma kuwepo kule Yerusalemu,  na si mwili tu, bado mazingira pia hayakutaka,  alipokuwa anakatiza kwa Wasamaria wenyeje wa pale hawakutaka kumruhusu akae kwao, kwasababu waliona kama anawaletea matatizo, ikumbukwe kuwa watu hao  hao ndio waliokuwa wanataka kumfanya mfalme hapo mwanzo. Kuonyesha kuwa mazingira yalimgomea. Si mazingira peke yake, hata mitume wake nao, walifanya kama kumsindikiza tu, lakini mioyo yao walishajiandaa kuchukua hatua yoyote lolote litakapotokea, ndio maana pale bustanini, wale watu walipokuja kila mmoja akakimbia na njia yake.

Kwa ufupi kila kitu kilikataa, isipokuwa roho yake tu. Ndio sababu ya kwanini maandiko yanatuambia ‘aliukaza uso wake’ kwasababu haikuwa rahisi, si jambo tena la kuomba, au kubembeleza, au kushawishi, au kusubiri msimu mzuri. Bali ni kujitoa tu wote wote, katika hayo. Watu wengi tunadhani Yesu aliuchukua msalaba wake siku ile alipobebeshwa ule mti, hapana, aliuchukua msalaba wake Kwa kitendo hichi cha kuamua kuukaza uso wake, kuelekea kifoni. Hata aliposema tujitwike misalaba yetu, alilenga, eneo hilo.

Ni nini na sisi tunapaswa tukipokee kwa Bwana Yesu?

Kwa kuwa Roho wake naye yupo ndani yetu, hatuna budi kufahamu kuwa yapo majira katika safari yetu ya wokovu, hatutahitaji mazingira yawe mazuri, ndio tulitimize kusudi la Mungu, au  ndugu kutukubalia, au marafiki kuafikiana na sisi, au miili kutuambia sasa ndio wakati, hapana..bali ni kujitwika misalaba yetu, “kwa kukaza nyuso zetu” na kumfuata Yesu.

Tukingoja vikwazo viondoke, au viondoshwe, tutajidanganya, na tutangoja sana, kwani vita vitaendelea kuwepo mpaka mwisho, mapambano hayaishi, tutashinda tu kwa kukaza tu nyuso zetu. Na Bwana atakuwa pamoja na sisi, ijapokuwa itaonekana ni kujipoteza lakini mwisho wake utakuwa ni uzima kama ulivyokuwa kwa Bwana Yesu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

RABI, UNAKAA WAPI?

MFALME ANAKUJA.

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuota unavua samaki, kunamaanisha nini?

Jiunge  >>>  WHATSAPP  <<< kwa mafundisho.

Ikiwa ndoto hii inakujia mara kwa mara, Au imekujia kwa uzito fulani, basi hwenda Mungu anasema na wewe rohoni. Ndoto hii inaweza kuja katika maumbile mengi. Wengine wanaota wakivua samaki kwa mikono, wengine kwa ndoano, wengine kwa wavu, wengine wakivua samaki wadogo/wakubwa. n.k. Kwa vyovyote vile maadamu ni kuvua basi maudhui yake ni moja.

Kiroho, uvuvi humaanisha kuwavuta watu kwa Kristo kwa kazi ya injili.

Yesu alipokutana na wale thenashara, wengi wa hao walikuwa wakifanya kazi ya uvuvi. Hivyo hiyo ilikuwa ni njia rahisi ya Yesu kuwaeleza kusudi lake timilifu juu ya hicho wanachokifanya.

Ndio maana siku ile alipomfanyia Petro muujiza ule wa kupata samaki wengi, baada ya kutaabika usiku kucha bila kupata chochote, Yesu alimwambia usiogope tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.

Luka 5:10

[10]na kadhalika Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni.Yesu akamwambia Simoni, Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu.

Kuonyesha kuwa uvuvi wa nje, ni ufunuo wa uvuvi wa rohoni.

Utaona hata huduma ya malaika siku ile  ya mwisho ya kuwatenga watu waovu na wema inafananishwa na huduma ya uvuvi wa samaki.

Mathayo 13:47-50

[47]Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;

[48]hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa.

[49]Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,

[50]na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Hivyo kwa namna moja au nyingine ikiwa umeokoka  basi Bwana anakutaka uhihubiri injili, kwa wengine kwasababu wakati huo umefika kufanya hivyo. Usiangalie uzoefu wako, kwasababu kumshuhudia Kristo hakutegemei uzoefu bali nia ya upendo. Na Mungu mwenyewe ameahidi kukusaidia kunena uwashuhudiapo watu.

Lakini kama hujaokoka, basi Yesu anakuita na anaona wito wako kutokea mbali, kwamba ukawahubirie wengine. Hivyo ni wajibu wako kumtii na kuupokea wokovu ili kusudi hilo alilolipanga ndani yako alifanikishe juu yako, haijalishi ndoto hii umeota mtu wa dini gani au imani gani, iwe mwislamu, mhindu, mshirikina. Maana umeota msalaba. Ujue Kristo anakuita akuokoe.

Ikiwa upo tayari sasa kumpokea Yesu basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo.

>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

TENGENEZA  NYAVU ZAKO, OSHA NYAVU ZAKO.

CHAMBO ILIYO BORA.

Kuota unakimbizwa.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuota msalaba maana yake ni nini?

Jiunge  >>>  WHATSAPP  <<< kwa mafundisho.

Ikiwa wewe bado hujamjua Kristo kabisa/ hujaokoka. Fahamu kuwa ndoto hii inakujuza kuwa Kristo anakuita akuokoe.

Msalaba hufunua wokovu wa Yesu Kristo, tulioupata kwa kifo chake juu ya mti huo.

Waefeso 2:16

[16]Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba.

Hivyo fungua moyo wako upokee wokovu huu bure, Kumbuka hakuna uzima wala tumaini, wala, amani,wala raha, wala faraja nje ya Kristo. Ndio maana umeota msalaba kwasababu Kristo anakupenda, hataki uangamie. Ikiwa upo tayari kumpokea leo basi fungua hapa kwa msaada…

>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Lakini ikiwa tayari umeokoka. Kristo anakutaka kumuangalia yeye zaidi… Kuongeza kiu yako, kwake, na mawazo yako kwake, na hiyo inaambatana na kujikana nafsi.

Luka 9:23-24

[23]Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.

[24]Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.

Hivyo kwa ujumla wake ndoto ya msalaba, aidha umeushika au umeubeba, au umeuona, ni ishara ya kumtazama Kristo.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.

KUOTA UPO MAKABURINI.

KUOTA UMEACHWA NA GARI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuota unapewa biblia kuna maanisha nini?

Jiunge  >>>  WHATSAPP  <<< kwa mafundisho.

Biblia ni kitabu pekee chenye ukweli wote, umuhusuo Mungu, na mwanadamu, ni kitabu kinachoifunua njia ya uzima. Hivyo kuota unapewa biblia fahamu kuwa ndoto hiyo ni ya ki-Mungu, kwasababu kamwe shetani hawezi kukuongoza mahali ambapo utapata nuru ya maisha yako.

Zaburi 119:105 Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.

Hivyo ikiwa wewe bado hujamjua Kristo, basi fahamu Mungu anakupenda na hivyo anataka kukuongoza katika ukweli wote, Ndio maana umeota unapewa biblia haijalishi utakuwa mwislamu, mhindu, mpagani n.k Fahamu kuwa Yesu anakupenda, na anataka kukuokoa. Hivyo unachopaswa kufanya ni kumkubali tu maishani mwako, ili aweze kukufikisha katika ukweli wote, na majibu yote ya maisha yako.

Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo ya imani >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Baada ya hapo, tafuta kitabu hichi (BIBLIA), Haraka iwezekanavyo uanze kusoma. Huku ukisaidiwa na waalimu sahihi wa Neno la Mungu. Kumbuka Wewe kufika hapa sio bahati mbaya, tovuti hii uliyopo sasa, Bwana ameiweka kwa ajili yako ina mafundisho mengi yatakayoweza kukusaidia kuielewa biblia vizuri. (www.wingulamashahidi.org). Itembelee mara kwa mara. Yapo mafundisho mengi sana, pamoja na majibu ya maswali mengi ya biblia. Lakini pia kama unatumia mtandao wa Whatsapp basi bofya hapa >>> WHATSAPP

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUOTA UNAPEWA PESA, KUNA MAANISHA NINI?

Je! Kuota unakabwa, mara kwa mara ni ishara ya nini?

KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya jivikeni silaha ya nia ile ile? (1Petro 4:1)

SWALI: Biblia inamaana gani kusema jivikeni silaha ya nia ile ile? (1Petro 4:1)

1 Petro 4:1-3

[1]Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi. 

[2]Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. 

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;


JIBU: Tukiangalia undani wa hilo neno hapo anaposema silaha ya nia. Ni kutuonyesha kuwa kumbe  “Nia ”, inaweza kuwa silaha.

Mara nyingi tunapofikiria silaha kibiblia mawazo yetu moja kwa moja yanakimbilia zile za  Waefeso 6:10-18, silaha za haki, kama vile upanga wa Roho ambalo ni Neno la Mungu, chapeo ya wokovu, ngao ya imani, dirii ya haki n.k. 

Lakini hapa tunaonyeshwa kuwa ipo pia silaha ndani ya Nia, ambayo nayo tunashauriwa tuwe nayo, kwasababu ilikuwa kwanza ndani ya Kristo.

Na silaha  yenyewe ilikuwa ni kukubali kuteswa katika mwili ili kuiua dhambi. 

Bwana wetu Yesu Kristo alijua dhambi ina nguvu sana pale mwili unapopewa raha zake. Hivyo aliikubali Nia ya kuteswa, ili dhambi ife.

Kumbuka sababu ya yeye kuchukiwa na watu, kuudhiwa, kuwindwa auawe, kuteswa mpaka kusulubiwa ni kwasababu alitangaza uadui na dhambi, Vinginevyo asingepitia maudhi yale katika mwili. Na tunaona mwisho wake ulikuwa ni ushindi. Kwani kwa kifo chake dhambi ilihukumiwa kabisa kabisa.

Alisema..

Yohana 7:7

[7]Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu. 

Hivyo maandiko yanatuambia na sisi pia, tujivike nia ile ile ya kukubali pia mateso kwa ajili ya Kristo. Kwasababu tukifanya hivyo tunaonyesha kuwa tumeachana na dhambi(tumeihukumu dhambi).

Kwa ufupi ni kuwa ukichukia maisha ya dhambi, tafsiri yake ni kukubali dhiki katika mwili kwa ajili ya Kristo. Hivyo zipende sasa dhiki hizo kama Kristo alivyozipenda, ili dhambi isikutawale. Hiyo ni Silaha kubwa sana.

2 Timotheo 3:12

[12]Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. 

kubali shida, kwasababu umeamua kuacha ile biashara haramu, furahia kutengwa na kuonekana mshamba, kwasababu umeamua kuacha mienendo ya marafiki wabaya, penda kupigwa na kufungwa kwasababu unahubiri kweli. Hiyo ndio SILAHA YA NIA. iwezayo kuishinda dhambi.

Ndio maana vifungu vinavyofuata anasema..

“Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani. 

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali; 

Daima tujivike silaha hii, tukikumbuka kuwa vita vyetu si vikali tena kama vile alivyovipiga Kristo.

Waebrania 12:4

[4]Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi; 

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

NDUGU,TUOMBEENI.

DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)

KIKWAZO CHA EUODIA NA SINTIKE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

Kitabu cha Wagalatia ni moja ya nyaraka ambazo mtume Paulo aliziandika kwa makanisa aliyoyapanda. Tunaona mwanzoni kabisa mwa waraka huu Paulo mwenyewe anajitambulisha akionyesha kuwa yeye ndiye mwandishi.

Waraka huu unamwonyesha Paulo akiwastaajabia watakatifu wa kanisa la Galatia kwa kuacha Imani ambayo aliwaachia hapo mwanzo, alipokuwa analisimamisha kanisa hilo, jambo ambalo lilimfanya mpaka imani yake impelekee kufikiri kuwa wamelogwa(Wagalatia 3:1), kwa jinsi tu walivyoiacha imani kwa haraka.

Kwa mujibu wa waraka huu, tunaona Paulo alilijenga kanisa hilo katika msingi wa imani katika neema ya Yesu Kristo.Na si katika msingi wa matendo ya sheria kama kigezo cha kukubaliwa na Mungu.

Kutokana na kuwa kanisa hili lilikuwa na mchanganyiko wa wayahudi pamoja na watu wa mataifa waliomwamini Kristo.Hapo ndipo tatizo lilipoanzia baada ya baadhi ya wakristo wa kiyahudi kuanza kuwashurutisha watu wa mataifa kwa kuwaambia kwamba hawawezi kuokolewa kama hawataishika torati ya Musa, kama hawatatimiza maagizo kama tohara, kushika siku, miezi, na miaka.(Wagalatia 4:8-10)

Hivyo hiyo ikawafanya watu kuacha kuishi tena kwa Imani iliyo katika neema ya Kristo Yesu, na kuangalia matendo ya sheria kama ndio kigezo cha kukubaliwa na Mungu?

Hivyo Paulo alipojua mageuzi hayo, ndio akawaandikia waraka huo kwa ukali, akiwaambia wokovu wetu huja kwa imani iliyo katika Yesu Kristo itendayo kazi katika upendo. Na si katika matendo ya sheria. Kwasababu kama ingekuwa hivyo Kristo alikufa bure. Torati ingeendelea tu kutawala.

Wagalatia 5:6

[6]Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.

Akasema torati, haikuwahi kumkamilisha mtu, na mtu anayeishi kwa hiyo ametengwa na Kristo, bado yupo chini ya laana.

kuishi kwa sheria ni kurudia mafundisho manyonge.

Lakini Swali ambalo alitarajia lingeulizwa na wagalatia, ni hili;

Je sasa hatuna haja ya kuyatazama matendo mema, tuishi tu, kama tunavyotaka kwasababu tunahesabiwa haki kwa neema ya Kristo tu?

Mbeleni kabisa katika sura ya tano, Mtume Paulo alitolea ufafanuzi, na kuwaambia tukishaokolewa, Maana yake ni kuwa tumeusulubisha mwili pamoja na tamaa zake mbaya..Hivyo hakuna nafasi ya dhambi kupata nguvu ndani yetu.

Wagalatia 5:24

[24]Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.

Je hilo inawezekanaje? kama hatuna sheria?

Linawezekana kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Ambaye tumepewa na Mungu.

Wagalatia 4:6

[6]Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.

Hivyo Paulo anaendelea kueleza ni wajibu wa kila mwamini kutembea katika Roho. Ili awasaidie Roho kuzishinda tamaa zote za mwili, na mambo maovu.

Wagalatia 5:16-21

[16]Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

[17]Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

[18]Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

,[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Je waraka huu ulilenga hasa nini?

Kwamba kwa nguvu zetu, au dini zetu au torati kamwe hatuwezi kumpendeza Mungu bali tuitegemee neema ya Kristo ambayo kwa hiyo tumepokea Roho awezaye kutufanya wakamilifu.

Hivyo ni wajibu wako kama mkristo. Kila wakati wote kujawa Roho (Waefeso 5:18). Ambayo hiyo huja kwa kuwa waombaji, wasomaji Neno, na kufanya ibada mioyoni mwetu wakati wote..

Tukiwa watu wa namna hiyo sheria wala dhambi inakuwa haina nguvu ndani yetu. Kwasababu tunakuwa chini ya neema ya Yesu Kristo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni uchafu gani unaozungumziwa katika Wagalatia 5:19?

je! Paulo aliwalaani Wagalatia na Wakorintho?

Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).

Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?

Rudi Nyumbani

Print this post

Msingi wa imani ya kikristo ni upi?

Msingi ni chimbuko, au mwanzo au kiini cha kitu fulani.

Ni wazi kuwa kila jambo lina msingi wake. taifa lina msingi wake, taasisi ina msingi wake, kabila lina msingi wake vilevile pia imani ina msingi wake.

Hivyo tukirudi katika ukristo. Msingi wa imani yake ni upi?

Msingi wa ukristo ni YESU KRISTO mwenyewe, na kazi yake aliyoikamilisha ya kufa na kufufuka kwake. Na sio kanisa, au dhehebu, au mapokeo fulani, au kikundi fulani cha wanaharakati.

Pasipo Yesu hakuna ukristo.

Yeye anafananishwa na lile jiwe kuu la pembeni, ambalo hakuna mjenzi aliyeweza kusimamisha jengo bila kuliweka hilo.

1 Petro 2:6

[6]Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika. 

Habari kamili za Yesu, na kazi yake aliyokuja kuifanya duniani unaipata katika kitabu kimoja tu kiitwacho BIBLIA. Hivyo huwezi kutenganisha biblia na Yesu Kristo.

Ili mtu ashawishwe kuipokea imani, ni sharti, aisikie kwanza injili yake ambayo hiyo utaipata katika Neno la Mungu yaani biblia..(Warumi 10:17)

Mpaka mtu aitwe mkristo ni lazima amtambue kwanza Kristo ni nani, na nini amekileta duniani, vinginevyo hawezi kuwa mkristo, hata kama atajiunga na kanisa, au dhehebu na kuyashika mapokeo yote aliyoyakuta huko, au kuisoma biblia yote, huyo bado hajawa mkristo.

Ni muhimu sana kumtambua Yesu ni nani kwetu. Kumtambua Yesu kama mwana wa Mungu bado inaweza isikupe wokovu, hata kumtambua Yesu kama Mungu bado inaweza isikupe wokovu (ijapokuwa vyote hivyo ni vyeo vyake). Lakini vyeo hivyo sio kiini cha ukristo.

 Yesu ni nani na ni nini alikileta duniani?

Yesu ni MKOMBOZI, kama tafsiri ya jina lake linavyojieleza( Mathayo 1:21)

mkombozi wa nini?

Alikuja kutukomboa roho zetu, nafsi zetu na miili yetu, Na kama ilivyo kanuni ya kiroho ili jambo hilo liweze kukamilika ilipasa itolewe kafara isiyo na kasoro yoyote(yaani dhambi). Na aliyeweza kukidhi vigezo hivyo ni Yesu pekee.

Ndio maana ilimgharimu afe, kama fidia ili sisi tupokee ondoleo la dhambi na msamaha wa dhambi kwa kifo chake. Hivyo yoyote anayeamini(yaani anayeupokea wokovu huo aliouleta).

kwa toba ya kweli na ubatizo, Basi anakuwa ameokoka, hivyo ile ghadhabu ya Mungu kwa wenye dhambi wote haiwi tena juu yake, tangu huo wakati anaitwa mbarikiwa, au mkristo, kwasababu dhambi zake zinakuwa zimefutwa kabisa.

Na zaidi ya hayo mtu huyu moja kwa moja anapewa zawadi ya Roho Mtakatifu, ambaye tangu huo wakati na kuendelea anakuwa ndani yake kama msaidizi, kumsaidia madhaifu yake, katika kuomba, kuijua kweli, kumkumbusha aliyoyasema Yesu, kumpasha habari ya mambo yajayo, na kumtia nguvu ya kumtumikia Mungu, pamoja na kumpa nguvu ya kushinda dhambi.

Huyu ndiye mkristo.

Swali ni je! umemwamini ipasavyo? au umempokea kwa namna ile ya kidini?

Usifikiri kuhama dini, wewe ni Kristo, au kuzaliwa kwenye familia ya kikristo wewe ndio mkristo, au kusomea theolojia, hapana hizo ni kampeni tu, ukristo halisi huja kwa kumwelewa Kristo ni nani na ni nini amekifanya kwako.

Ikiwa bado hujaokoka na unataka kumpokea leo ili upate ondoleo la dhambi zako. Basi uamuzi huo ni bora sana kwako. Wasiliana nasi namba uzionazo chini  kwa mwongozo wa sala ya toba.

Ubarikiwe.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

 +255693036618/ +255789001312

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

YESU NI NANI?

UKOMA NA UJANE ULIO NDANI YAKO, UMEUPATIA TIBA?

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

Rudi Nyumbani

Print this post

ORODHA YA WAANDISHI WA BIBLIA.

Biblia kitabu kikamilifu, na kitakatifu kimeandikwa na waandishi Zaidi ya 40 kwa Uvuvio wa Roho Mtakatifu. Ndani ya biblia kuna taarifa zinazohusu maisha ya watu zilizobeba sauti ya Mungu nyuma yake, pia kuna taarifa za Mataifa mbalimbali pia zenye kubeba sauti ya Mungu nyuma yake, lakini Zaidi sana kuna Nabii za wakati ujao.

Ifuatayo ni orodha ya waandishi 40 wa Biblia kuanzia Agano la kale hadi Agano jipya.

Agano la kale.

  1. Amosi – Mwandishi wa kitabu cha Amosi
  2. Danieli – Mwandishi wa kitabu cha Danieli.
  3. Daudi- Mwandishi wa kitabu cha Zaburi, kwa baadhi ya Zaburi.
  4. Ezekieli- Mwandishi wa kitabu cha Ezekieli.
  5. Ezra- Mwandishi wa kitabu cha Ezra.
  6. Habakuki – Mwandishi wa kitabu cha Habakuki.
  7. Hagai – Mwandishi wa kitabu cha Hagai.
  8. Hosea- Mwandishi wa kitabu cha Hosea.
  9. Isaya- Mwandishi wa kitabu cha Isaya.
  10. Yeremia – Mwandishi wa kitabu cha Yeremia
  11. Yoeli – Mwandishi wa kitabu cha Yoeli
  12. Yona- Mwandishi wa kitabu cha Yona.
  13. Yoshua- Mwandishi wa kitabu cha Yoshua.
  14. Malaki- Mwandishi wa kitabu cha Malaki.
  15. Mika- Mwandishi wa kitabu cha Mika.
  16. – Mwandishi wa kitabu cha Esta.
  17. Musa – Mwandishi wa kitabu cha Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Kumbukumbu la Torati, Hesabu, Ayubu na Zaburi 90.
  18. Nathani (Nabii) – Mwandishi wa kitabu cha 1Samweli na 2Samweli (sehemu baadhi)
  19. Nabii Gadi- – Mwandishi wa kitabu cha 1Samweli na 2Samweli (sehemu baadhi)
  20. Nahumu- Mwandishi wa kitabu cha Nahumu.
  21. Nehemia- Mwandishi wa kitabu cha Nehemia.
  22. Obadia- Mwandishi wa kitabu cha Obadia.
  23. Samweli- Mwandishi wa kitabu cha Samweli (Sehemu baadhi)
  24. Sulemani- Mwandishi wa kitabu cha Mithali, Mhubiri na Wimbo ulio bora.
  25. Sefania -Mwandishi wa kitabu cha Sefania.
  26. Zekaria-Mwandishi wa kitabu cha Zekaria.
  27. Wana wa Kora-Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 42, Zaburi 44-49, Zaburi 84-85, na Zaburi 87-88.
  28. Asafu- Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 50, na Zaburi 73-83.
  29. Ethani – Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 89 (sehemu).
  30. Heman – Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 89 (sehemu).
  31. Aguri – Mwandishi wa kitabu cha Mithali 30.
  32. Lemueli – Mwandishi wa kitabu cha Mithali 31.

Agano Jipya.

  1. Mathayo – Mwandishi wa kitabu cha Mathayo.
  2. Marko – Mwandishi wa kitabu cha Marko.
  3. Luka – Mwandishi wa kitabu cha Luka na Matendo ya Mitume.
  4. Yohana – Mwandishi wa kitabu cha Yohana Mtakatifu na 1 na 2Yohana pamoja na Ufunuo.
  5. Yakobo – Mwandishi wa kitabu cha Yakobo.
  6. Yuda – Mwandishi wa kitabu cha Yuda.
  7. Paulo- Mwandishi wa kitabu cha Warumi, 1 na 2Wakorintho, Wagalatia, Waefeso, Wakolosai, Wafilipi, 1 na 2Wathesalonike, 1na 2Timotheo, Tito na Filemoni.
  8. Petro – Mwandishi wa kitabu cha 1 na 2Petro.

Kwanini waandishi wapo Zaidi ya 40 na si 40 kamili?.. Ni kwasababu biblia pia imewataja wana wa Kora, ambao hatujui walikuwa ni wangapi, zaidi sana yupo mwandishi wa kitabu cha Waebrania, ambaye hajatajwa ni nani, huenda akawa ni Mtume Paulo, lakini kama si yeye bali ni mwingine, basi ataongezeka katika idadi ya walioiandika biblia.

Kumbuka tena, biblia ni kitabu cha Mungu kilichoandikwa na WATU, kwa uvuvio wa ROHO MTAKATIFU, Hivyo maneno yaliyoandikwa ndani ya Biblia, yana uzima.

2Timotheo 3:16  “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.

Je ni Mungu au Malaika?

Mwandishi wa kitabu cha Mithali ni nani?

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Rudi Nyumbani

Print this post