Kitabu cha Wagalatia ni moja ya nyaraka ambazo mtume Paulo aliziandika kwa makanisa aliyoyapanda. Tunaona mwanzoni kabisa mwa waraka huu Paulo mwenyewe anajitambulisha akionyesha kuwa yeye ndiye mwandishi.
Waraka huu unamwonyesha Paulo akiwastaajabia watakatifu wa kanisa la Galatia kwa kuacha Imani ambayo aliwaachia hapo mwanzo, alipokuwa analisimamisha kanisa hilo, jambo ambalo lilimfanya mpaka imani yake impelekee kufikiri kuwa wamelogwa(Wagalatia 3:1), kwa jinsi tu walivyoiacha imani kwa haraka.
Kwa mujibu wa waraka huu, tunaona Paulo alilijenga kanisa hilo katika msingi wa imani katika neema ya Yesu Kristo.Na si katika msingi wa matendo ya sheria kama kigezo cha kukubaliwa na Mungu.
Kutokana na kuwa kanisa hili lilikuwa na mchanganyiko wa wayahudi pamoja na watu wa mataifa waliomwamini Kristo.Hapo ndipo tatizo lilipoanzia baada ya baadhi ya wakristo wa kiyahudi kuanza kuwashurutisha watu wa mataifa kwa kuwaambia kwamba hawawezi kuokolewa kama hawataishika torati ya Musa, kama hawatatimiza maagizo kama tohara, kushika siku, miezi, na miaka.(Wagalatia 4:8-10)
Hivyo hiyo ikawafanya watu kuacha kuishi tena kwa Imani iliyo katika neema ya Kristo Yesu, na kuangalia matendo ya sheria kama ndio kigezo cha kukubaliwa na Mungu?
Hivyo Paulo alipojua mageuzi hayo, ndio akawaandikia waraka huo kwa ukali, akiwaambia wokovu wetu huja kwa imani iliyo katika Yesu Kristo itendayo kazi katika upendo. Na si katika matendo ya sheria. Kwasababu kama ingekuwa hivyo Kristo alikufa bure. Torati ingeendelea tu kutawala.
Wagalatia 5:6
[6]Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.
Akasema torati, haikuwahi kumkamilisha mtu, na mtu anayeishi kwa hiyo ametengwa na Kristo, bado yupo chini ya laana.
kuishi kwa sheria ni kurudia mafundisho manyonge.
Lakini Swali ambalo alitarajia lingeulizwa na wagalatia, ni hili;
Je sasa hatuna haja ya kuyatazama matendo mema, tuishi tu, kama tunavyotaka kwasababu tunahesabiwa haki kwa neema ya Kristo tu?
Mbeleni kabisa katika sura ya tano, Mtume Paulo alitolea ufafanuzi, na kuwaambia tukishaokolewa, Maana yake ni kuwa tumeusulubisha mwili pamoja na tamaa zake mbaya..Hivyo hakuna nafasi ya dhambi kupata nguvu ndani yetu.
Wagalatia 5:24
[24]Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
Je hilo inawezekanaje? kama hatuna sheria?
Linawezekana kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Ambaye tumepewa na Mungu.
Wagalatia 4:6
[6]Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.
Hivyo Paulo anaendelea kueleza ni wajibu wa kila mwamini kutembea katika Roho. Ili awasaidie Roho kuzishinda tamaa zote za mwili, na mambo maovu.
Wagalatia 5:16-21
[16]Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. [17]Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. [18]Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria. [19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, [20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, ,[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
[16]Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
[17]Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
[18]Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
,[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
Je waraka huu ulilenga hasa nini?
Kwamba kwa nguvu zetu, au dini zetu au torati kamwe hatuwezi kumpendeza Mungu bali tuitegemee neema ya Kristo ambayo kwa hiyo tumepokea Roho awezaye kutufanya wakamilifu.
Hivyo ni wajibu wako kama mkristo. Kila wakati wote kujawa Roho (Waefeso 5:18). Ambayo hiyo huja kwa kuwa waombaji, wasomaji Neno, na kufanya ibada mioyoni mwetu wakati wote..
Tukiwa watu wa namna hiyo sheria wala dhambi inakuwa haina nguvu ndani yetu. Kwasababu tunakuwa chini ya neema ya Yesu Kristo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
Ni uchafu gani unaozungumziwa katika Wagalatia 5:19?
je! Paulo aliwalaani Wagalatia na Wakorintho?
Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).
Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?
Rudi Nyumbani
Print this post
Msingi ni chimbuko, au mwanzo au kiini cha kitu fulani.
Ni wazi kuwa kila jambo lina msingi wake. taifa lina msingi wake, taasisi ina msingi wake, kabila lina msingi wake vilevile pia imani ina msingi wake.
Hivyo tukirudi katika ukristo. Msingi wa imani yake ni upi?
Msingi wa ukristo ni YESU KRISTO mwenyewe, na kazi yake aliyoikamilisha ya kufa na kufufuka kwake. Na sio kanisa, au dhehebu, au mapokeo fulani, au kikundi fulani cha wanaharakati.
Pasipo Yesu hakuna ukristo.
Yeye anafananishwa na lile jiwe kuu la pembeni, ambalo hakuna mjenzi aliyeweza kusimamisha jengo bila kuliweka hilo.
1 Petro 2:6
[6]Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.
Habari kamili za Yesu, na kazi yake aliyokuja kuifanya duniani unaipata katika kitabu kimoja tu kiitwacho BIBLIA. Hivyo huwezi kutenganisha biblia na Yesu Kristo.
Ili mtu ashawishwe kuipokea imani, ni sharti, aisikie kwanza injili yake ambayo hiyo utaipata katika Neno la Mungu yaani biblia..(Warumi 10:17)
Mpaka mtu aitwe mkristo ni lazima amtambue kwanza Kristo ni nani, na nini amekileta duniani, vinginevyo hawezi kuwa mkristo, hata kama atajiunga na kanisa, au dhehebu na kuyashika mapokeo yote aliyoyakuta huko, au kuisoma biblia yote, huyo bado hajawa mkristo.
Ni muhimu sana kumtambua Yesu ni nani kwetu. Kumtambua Yesu kama mwana wa Mungu bado inaweza isikupe wokovu, hata kumtambua Yesu kama Mungu bado inaweza isikupe wokovu (ijapokuwa vyote hivyo ni vyeo vyake). Lakini vyeo hivyo sio kiini cha ukristo.
Yesu ni nani na ni nini alikileta duniani?
Yesu ni MKOMBOZI, kama tafsiri ya jina lake linavyojieleza( Mathayo 1:21)
mkombozi wa nini?
Alikuja kutukomboa roho zetu, nafsi zetu na miili yetu, Na kama ilivyo kanuni ya kiroho ili jambo hilo liweze kukamilika ilipasa itolewe kafara isiyo na kasoro yoyote(yaani dhambi). Na aliyeweza kukidhi vigezo hivyo ni Yesu pekee.
Ndio maana ilimgharimu afe, kama fidia ili sisi tupokee ondoleo la dhambi na msamaha wa dhambi kwa kifo chake. Hivyo yoyote anayeamini(yaani anayeupokea wokovu huo aliouleta).
kwa toba ya kweli na ubatizo, Basi anakuwa ameokoka, hivyo ile ghadhabu ya Mungu kwa wenye dhambi wote haiwi tena juu yake, tangu huo wakati anaitwa mbarikiwa, au mkristo, kwasababu dhambi zake zinakuwa zimefutwa kabisa.
Na zaidi ya hayo mtu huyu moja kwa moja anapewa zawadi ya Roho Mtakatifu, ambaye tangu huo wakati na kuendelea anakuwa ndani yake kama msaidizi, kumsaidia madhaifu yake, katika kuomba, kuijua kweli, kumkumbusha aliyoyasema Yesu, kumpasha habari ya mambo yajayo, na kumtia nguvu ya kumtumikia Mungu, pamoja na kumpa nguvu ya kushinda dhambi.
Huyu ndiye mkristo.
Swali ni je! umemwamini ipasavyo? au umempokea kwa namna ile ya kidini?
Usifikiri kuhama dini, wewe ni Kristo, au kuzaliwa kwenye familia ya kikristo wewe ndio mkristo, au kusomea theolojia, hapana hizo ni kampeni tu, ukristo halisi huja kwa kumwelewa Kristo ni nani na ni nini amekifanya kwako.
Ikiwa bado hujaokoka na unataka kumpokea leo ili upate ondoleo la dhambi zako. Basi uamuzi huo ni bora sana kwako. Wasiliana nasi namba uzionazo chini kwa mwongozo wa sala ya toba.
Ubarikiwe.
+255693036618/ +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
YESU NI NANI?
UKOMA NA UJANE ULIO NDANI YAKO, UMEUPATIA TIBA?
Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?
Biblia kitabu kikamilifu, na kitakatifu kimeandikwa na waandishi Zaidi ya 40 kwa Uvuvio wa Roho Mtakatifu. Ndani ya biblia kuna taarifa zinazohusu maisha ya watu zilizobeba sauti ya Mungu nyuma yake, pia kuna taarifa za Mataifa mbalimbali pia zenye kubeba sauti ya Mungu nyuma yake, lakini Zaidi sana kuna Nabii za wakati ujao.
Ifuatayo ni orodha ya waandishi 40 wa Biblia kuanzia Agano la kale hadi Agano jipya.
Agano la kale.
Agano Jipya.
Kwanini waandishi wapo Zaidi ya 40 na si 40 kamili?.. Ni kwasababu biblia pia imewataja wana wa Kora, ambao hatujui walikuwa ni wangapi, zaidi sana yupo mwandishi wa kitabu cha Waebrania, ambaye hajatajwa ni nani, huenda akawa ni Mtume Paulo, lakini kama si yeye bali ni mwingine, basi ataongezeka katika idadi ya walioiandika biblia.
Kumbuka tena, biblia ni kitabu cha Mungu kilichoandikwa na WATU, kwa uvuvio wa ROHO MTAKATIFU, Hivyo maneno yaliyoandikwa ndani ya Biblia, yana uzima.
2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; 17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”.
2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”.
Shalom.
KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.
Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.
Je ni Mungu au Malaika?
Mwandishi wa kitabu cha Mithali ni nani?
MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.
Swali: Je kipindi Ibrahimu anatoka Uru ya Ukaldayo, hakuwa anajua anakokwenda kwamba ni Kaanani? au alikuwa anaongozwa na Roho Mtakatifu mpaka pale alipofika, ndipo Bwana akamwambia hapo hapo atulie?…na mbona tukisoma Mwanzo 12:5 tunaona kama Abramu alikuwa anajua kabisa anakoelekea, au je biblia inajichanganya?
Jibu: Biblia, Neno la Mungu halijichanganyi kamwe..
Turejee …
Waebrania 11:8 “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka ASIJUE AENDAKO”.
Hapa ni kweli panaonesha kuwa Ibrahimu alikuwa hajui aendako, lakini hebu tusome maandiko mengine ndipo tutapata kuelewa zaidi..
Mwanzo 12:1 “BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; 2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka……………… 5 Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani”
Mwanzo 12:1 “BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;
2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka………………
5 Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani”
Hapa panaonyesha kuwa Abramu alikuwa anajua anakokwenda, kuwa ni Kaanani, Je lipi ni sahihi?
Jibu ni kwamba Abrahamu alikuwa anajua anakokwenda isipokuwa alikuwa hajui kama nchi hiyo aiendeayo (yaani ya Kaanani) kama ndio itakuwa ya ahadi..
Hivyo alienda mpaka alipofika na alipofika ndipo Mungu akamtokea na kumwambia kuwa nchi hiyo aliyopo ndiyo itakuwa milki yake (ya ahadi).
Mwanzo 12:5 “Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani. 6 Abramu akapita katikati ya nchi mpaka mahali patakatifu pa Shekemu; mpaka mwaloni wa More. Na Wakanaani siku zile walikaa katika nchi hiyo. 7 BWANA akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu BWANA aliyemtokea”
Mwanzo 12:5 “Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani.
6 Abramu akapita katikati ya nchi mpaka mahali patakatifu pa Shekemu; mpaka mwaloni wa More. Na Wakanaani siku zile walikaa katika nchi hiyo.
7 BWANA akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu BWANA aliyemtokea”
Sasa swali linakuja, je ni kitu gani kilichomwelekeza Abramu aende nchi ya Kanaani na si nchi nyingine?
Tulirejea ule mlango wa 11 wa kitabu cha Mwanzo, tunasoma kuwa wazo la kuhama Uru wa Wakaldayo na kuelekea Kanaani halikuanzia kwa Abramu, bali lilianzia kwa baba yake aliyeitwa Tera, huyo ndiye aliyefikiri kuhama Ukadayo na hata kuchukua hatua ya kuhama pamoja na watoto wake wote ikiwemo Abramu.
Mwanzo 11:31 “Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko”.
Umeona hapo?..sio Abramu aliyekuwa na wazo la kuondoka Ukaldayo bali ni Tera, na sababu za kuwaondoa kule hazijulikani, kwani biblia haijaweka wazi, labda huenda ni maasi ya nchi hiyo, au sababu nyingine za kijamii au kibiashara.
Lakini katika wazo hilo la kuhama, lilikuwepo pia kusudi la Mungu ndani yake, kwamba Abramu afike Kanaani.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Abramu alijua anakoenda, lakini hakujua nchi atakayopewa mpaka alipofika.
Nini tunajifunza hapo?
Wakati mwingine Bwana anaweza kutumia wazo la mtu mwingine kukupeleka wewe mahali Mungu anapotaka uwe.
Hivyo wakati mwingine usinung’unike unapoona unahamishwa mahali ulipo, kwani pengine Mungu anakupeleka mahali anapotaka wewe uwe, na ukishafika ndipo atakuonyesha.
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Swali: Je Mungu hapendezwi na dhabihu na matoleo, kulingana na mstari huo?
Jibu: Turejee..
Waebrania 10:5 “Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari”.
Waebrania 10:5 “Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema,
Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari”.
Andiko hili limerejewa kutoka katika Zaburi 40:6, tusome ili tupate maana kamili.
Zaburi 40:6 “Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo, Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka”.
Zaburi 40:6 “Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,
Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka”.
Hapo imewekwa vizuri kuwa ni kafara na sadaka zinazotolewa kwaajili ya DHAMBI!! ndizo asizozitaka…
Sasa Dhabihu ni sadaka za kuteketezwa (ambazo ni kafara za wanyama) zilizokuwa zinatolewa kipindi cha agano la kale kwaajili ya kufunika dhambi..
Na kasoro ya dhabihu za wanyama ndio hiyo, ilikuwa haiondoi dhambi bali inafunika tu..
Kwahiyo hapo anaposema “Dhabihu na matoleo hukutaka”.. alimaanisha kuwa hizo dhabihu za wanyama hazifai katika kumwondolea mtu makosa yake na kumtakasa bali mwili wa Yesu na damu yake ndio iwezayo kumtakasa mtu na kumwondolea kabisa dhambi zake.
Ndivyo maandiko yasemavyo kuwa damu za mbuzi na mafahali haziwezi kuondoa dhambi na kumtakasa mtu bali zilikuwa zinafunika tu.
Waebrania 10:3 “Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka. 4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi”
Waebrania 10:3 “Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka.
4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi”
Lakini dhabihu ya mwili wa YESU, kupitia kumwagika kwa damu yake, unaondoa kabisa dhambi… Na hiyo ndio sadaka Mungu aliyoihitaji na sio dhabihu za kondoo na mbuzi na mafahali.
Waebrania 10:10 “Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu”.
Lakini kuhusiana na utoaji wa sadaka ni kwaajili ya shukrani, au kwaajili ya kazi ya ufalme wa mbinguni ni jambo linalompendeza Mungu na lenye baraka.
Lakini kama ni kwaajili ya dhambi (hakuna sadaka inayoweza kuondoa dhambi)..isipokuwa damu ya YESU ambayo tayari tumeshalipiwa bureee… tunachopaswa kufanya ili sadaka hiyo ifanye kazi juu yetu ni KUTUBU TU kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi!.
Tukiweza kutubu kwa kumaanisha basi tunapata msamaha na ondoleo la dhambi bure.
Je unaye YESU maishani?.
Kumbuka daima kuwa mwisho wa dunia upo, kama tu vile mwisho wa maisha ulivyo, ikiwa leo hii damu ya YESU si kitu cha thamani kwako, utasimamaje siku ile ya mwisho mbele zake?..Tafakari mara mbili.
Maran atha.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Swali: Biblia inasema kushindana kwetu ni dhidi ya pepo wachafu, je kulingana na mstari huo, wapo pepo wazuri?
Jibu: Turejee…
Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”
Biblia iliposema kuwa kushindana kwetu ni dhidi ya “pepo wabaya” haijamaanisha kuwa wapo pepo wazuri, bali inaelezea tu sifa ya hizo roho (mapepo) kwamba ni mbaya na chafu.
Ni sawa na biblia inapotaja Malaika watakatifu, (soma Mathayo 25:31, Marko 8:38 na Ufunuo 14:10) haimaanishi kuwa wapo Malaika wasio watakatifu, na kama wapo wasio watakatifu basi hawaitwi tena Malaika bali ni mapepo, vile vile hakuna mapepo wasafi na kama zipo hizo roho safi basi haziwezi kuitwa tena mapepo, bali zitaitwa Malaika.
Hivyo uzuri na usafi unaotajwa juu ya Malaika au Mapepo, ni kuelezea tu sifa zao na kazi zao, kwamba Malaika wote walioko mbinguni ni wasafi na watakatifu, na mapepo yote yaliyotupwa ulimwenguni ni machafu na mabaya.
Na kumbuka pia “Pepo na jini” ni kitu kimoja, isipokuwa ni lugha mbili tofuati tu!… Na hakuna jini wala pepo mzuri, wote ni wabaya na wachafu. Zipo dini zinazofundisha kuwa wapo majini (mapepo) wazuri, na kwamba watu wanaweza kuwa nao na wakawaletea mafanikio na hata kuwalinda.
Huo ni uongo wa shetani asilimia mia, kwani shetani ndiye baba wa uongo..
Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; KWA SABABU YEYE NI MWONGO, NA BABA WA HUO”.
Shetani hajawahi kuwa na urafiki wa kweli na mwanadamu, wala hajawahi kuwa na mapenzi na mwanadamu, kitu anachokipenda kutoka kwa mwanadamu ni utukufu tu!.. lakini hajawahi kumpenda mwanadamu, na hakuna unabii ya kwamba atakuja siku moja kumpenda mwanadamu, yeye ni adui wa mwanadamu wa milele.
Na Kama tu shetani asivyopendwa kuitwa shetani, bali anapendwa aitwe mungu, kadhalika hawezi kuruhusu mapepo yake yaitwe vibaya, kwa sifa mbaya?..atawatakasa tu!.. na anawatakasaje?..si kwa njia nyingine bali kwa njia za dini za uongo, zinazohubiri na kufundisha kuwa wapo mapepo wazuri.
Kwa urefu kuhusiana na pepo wachafu(majini) fungua hapa >>
MAJINI WAZURI WAPO?
Je umempokea YESU?.. kama bado ni nini kinakungojesha?
Bwana anarudi.
WhatsApp
Jibu: Habari hii inamhusu Mtume Paulo, kipindi aliposhikwa na kufungwa akiwa Yerusalemu.. sasa ili tuelewe vizuri tuanze kusoma ule mstari wa 25
Matendo 22:25 “Hata walipokwisha kumfunga kwa kamba, Paulo akamwambia yule akida aliyesimama karibu, Je! Ni halali ninyi kumpiga mtu aliye Mrumi naye hajakuhumiwa bado? 26 Yule akida aliposikia, akaenda akamwarifu yule jemadari, akisema, Unataka kufanya nini? Kwa maana mtu huyu ni Mrumi 27 Jemadari akaja, akamwuliza, Niambie, u Mrumi? Akasema, Ndiyo. 28 Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA WENYEJI HUU KWA MALI NYINGI. Paulo akasema, Na mimi ni Mrumi wa kuzaliwa”.
Matendo 22:25 “Hata walipokwisha kumfunga kwa kamba, Paulo akamwambia yule akida aliyesimama karibu, Je! Ni halali ninyi kumpiga mtu aliye Mrumi naye hajakuhumiwa bado?
26 Yule akida aliposikia, akaenda akamwarifu yule jemadari, akisema, Unataka kufanya nini? Kwa maana mtu huyu ni Mrumi
27 Jemadari akaja, akamwuliza, Niambie, u Mrumi? Akasema, Ndiyo.
28 Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA WENYEJI HUU KWA MALI NYINGI. Paulo akasema, Na mimi ni Mrumi wa kuzaliwa”.
Wenyeji unaozungumziwa hapo ni “URAIA”.. Kwahiyo hapo kiswahili kingine cha andiko hili ni hiki .. “Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA URAIA HUU KWA MALI NYINGI”.
Zamani za kanisa la karne ya kwanza, ufalme uliokuwa na nguvu duniani, ulikuwa ni ufalme wa Rumi, na ndio uliokuwa unatawala dunia chini ya Kaisari. Hivyo kutokana na nguvu ya ufalme huo, basi hata raia wake walikuwa na nguvu, na heshima.
Raia wa kirumi (yaani Mrumi) alikuwa hawezi kuadhibiwa bila kushitakiwa, na haki zake zilikuwa zinalindwa sana kuliko raia wa Taifa lingine lolote duniani,..ilikuwa ni kosa kubwa kumhukumu Mrumi kabla ya kumsikiliza.
Sasa hapa Paulo alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa lakini kwaasili ni Mwebrania (yaani muisraeli), na hapa alikuwa amevunjiwa haki yake kama raia wa kirumi, na hivyo akida pamoja na jemedari wakaogopa, kwasababu ni kosa kumhukumu Mrumi kabla ya kumpandisha kizimbani na kumsikiliza.
Sasa swali la Msingi kwanini, Jemedari aseme Uraia wake kaupata kwa mali nyingi?
Zamani ili uwe Raia wa kirumi ni aidha uwe mzawa (yaani umezaliwa katika Taifa la Rumi) au Umeununua uraia.
Sasa kitendo cha kuununua Uraia hakikuwa rasmi, bali kilikuwa ni kwa njia ya rushwa, na waliopata uraia huo waliupata wakati wa sense, ambapo majina yako yaliongezwa katika orodha ya warumi kinyume cha sheria, baada ya kulipa pesa nyingi,
Na hapa huyu Jemedari aliyeitwa Klaudio Lisia (Matendo 23:26) anaonekana kumwambia Paulo kuwa Uraia wake “Aliununua” maana yake kwa asili hakuwa mrumi, bali alikuwa kuwa mtu wa Taifa lingine, huenda Ugiriki, kwasababu hilo jina la Pili la LISIA ni jina la kigiriki, lakini Paulo yeye alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa na si kwa kununua uraia.
Upo uraia mwingine ambao ni wa Mbinguni…huo haupatikani kwa fedha, wala mtu haupati kwa rushwa bali bali kwa kuzaliwa mara ya pili.
Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu. 4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa? 5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”
Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”
Je umeupata uraia huu wa mbinguni kwa kuzaliwa mara ya pili?.. kama bado ni nini kinachokusubirisha??
Jina tukufu la Bwana YESU KRISTO libarikiwe.
Je umewahi kutafakari kwanini mapigo yote tisa (9) aliyopigwa Farao bado moyo wake ulikuwa mgumu? Na kwanini lile pigo moja la mwisho la kufa wazaliwa wa kwanza ndipo akawaruhusu wana wa Israeli?.
Sasa hakuna mahali popote maandiko yanasema kuwa “Mungu aliufanya moyo wa Farao kuwa mlaini”.
Maana yake Farao aliendelea kuwa na moyo mgumu mpaka alipoingia kwenye ile bahari ya Shamu, na hapo ndio ikawa mwisho wake.
Sasa ni nini kilitokea mpaka Farao akawaachia wana wa Israeli?… Si kingine bali ni ule msiba alioupata,
Na huku bado moyo wake ukiendelea kuwa mgumu, alivunja sheria ya moyo wake na kuwafukuza wana wa Israeli kwa muda. (Lakini moyo wake bado ulikuwa mgumu tu).
Kutoka 11:1 “BWANA akamwambia Musa, Liko pigo moja bado, nitakaloleta juu ya Farao na juu ya Misri; baadaye atawapa ninyi ruhusa mtoke huku; naye hapo atakapowapa ruhusa, atawafukuza mtoke huku kabisa kabisa”
Sasa ni siri gani iliyokuwepo ndani ya wazaliwa wa kwanza wa Misri hata kumfanya Farao awafukuze wana wa Israeli?…Kwani ni wazi kuwa hata Farao angepigwa kwa mapigo gani ya asili asingewaachia wana wa Israeli.
Ila ni nini kilikuwa kwa wazaliwa wa kwanza wa kiMisri?
Kilichokuwa ndani ya wazaliwa wa kwanza wa Misri, ikiwemo mwana wa Farao si kingine zaidi ya “miungu ya kimisri”..
Hivyo kifo cha wazaliwa wa kwanza ilikuwa ni hukumu kubwa kwa miungu yao pamoja kudhalilika kwa miungu yao ambao waliamini ina nguvu nyingi.
Ndio maana MUNGU aliposhuka kuwaharibu wazaliwa wa kwanza pia alisema ataiharibu na miungu yao (ambayo kiuhalisia ilikuwa inaishi ndani ya hao wazaliwa wa kwanza).
Kutoka 12:12 “Maana nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, namij nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi BWANA.”
Zamani katika nchi ya Misri na hata katika mataifa mengine ya dunia, wazaliwa wa kwanza wa kiume waliaminika kama miungu ya familia na ya nchi.
Na wanyama wa kwanza kuzaliwa, ndio waliotumika kwa kafara za miungu yao.
Hivyo watoto wote wa kwanza wa kiume walikuwa wanabeba ukuhani wa miungu, na roho zote za miungu zilikuwa zinakaa ndani yao.
Kwahiyo kilichomwumiza zaidi Farao si msiba wa mtoto, bali ni kuhukumiwa kwa miungu yao iliyokuwepo ndani ya wale watoto!!..
Kwaufupi Farao alichanganyikiwa kidogo, hakuelewa ni nini kimetokea katika eneo lake la imani.
Na hata waMisri wote walichanganyikiwa vivyo hivyo, hakuna ambaye hakulia..wote walilia na kuhofu na kutoelewa ni nini cha kufanya, waliyeyuka mpaka kufikia hatua ya wana wa Israeli kuwateka nyara.
Kutoka 12:33 “Wamisri nao wakawahimiza watu, kuwatoa katika nchi kwa haraka, maana walisema, Tumekwisha kufa sote. 34 Watu wakauchukua unga wa mikate yao kabla haijatiwa chachu, na vyombo vyao vya kukandia wakavitia ndani ya nguo zao mabegani. 35 Wana wa Israeli wakafanya kama neno lile la Musa; wakataka kwa Wamisri vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu, na mavazi. 36 BWANA akawajalia kupendelewa na Wamisri hata wakawapa kila walichokitaka. Nao wakawateka Wamisri nyara”
Kutoka 12:33 “Wamisri nao wakawahimiza watu, kuwatoa katika nchi kwa haraka, maana walisema, Tumekwisha kufa sote.
34 Watu wakauchukua unga wa mikate yao kabla haijatiwa chachu, na vyombo vyao vya kukandia wakavitia ndani ya nguo zao mabegani.
35 Wana wa Israeli wakafanya kama neno lile la Musa; wakataka kwa Wamisri vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu, na mavazi.
36 BWANA akawajalia kupendelewa na Wamisri hata wakawapa kila walichokitaka. Nao wakawateka Wamisri nyara”
Ni ujumbe gani tunapata hapo?..au ni kitu gani kilichokuwa kimewafunga wana wa Israeli?
Si utajiri wala hazina zilizoko Misri kwamaana Bwana aliuharibu utajiri wake wote kwa zile mvua za mawe na nzige, vile vile si uzuri wa Misri, kwasababu Bwana aliharibu uzuri wake kwa zile mvua za mawe lakini bado wana wa Israeli walikuwa kifungoni.
Wala si ushujaa wa waMisri kwasababu Bwana aliwapiga kwa chawa, na majipu na aliwanyima maji ya kunywa kwa siku saba, hivyo walikuwa dhaifu..lakini bado wana wa Israeli walikuwa kifungoni.
Ni nini kilichokuwa kimewashikilia wana wa Israeli???…..jibu ni “miungu ya kimisri” iliyokuwa inaabudiwa ndani ya watu.
Hiyo ilipopigwa pamoja na makuhani wake (ambao ndio wazaliwa wa kwanza)..vifungo vikalegea, wana wa Israeli wakaachiwa.
Laiti Bwana Mungu angelileta hilo pigo mwanzoni kabla ya yote, Farao angeshaawaachia Israeli kitambo sana pamoja na moyo wake kuwa mgumu, lakini Mungu aliliruhusu liwe mwisho wa kusudi lake maalumu.
Na ukiendelea kusoma mbele utaona Bwana anawapa amri wana wa Israeli wawatakase wazaliwa wa kwanza na kwamba kila mzaliwa wa kwanza atakuwa ni wa Bwana, maana yake atakuwa kuhani wa Bwana kwa lazima (kwasababu kulikuwa na kitu katika wazaliwa wa kwanza).
Maana yake kila mzaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli alipaswa kutolewa kwa Bwana kama Hana alivyomtoa Samweli kwa Bwana (hiyo ilikuwa ni amri).
Lakini sheria hiyo ilikuja kubadilika, na ukuhani wa wazaliwa wa kwanza likapewa kabila la Lawi.
Hesabu 3:12 “Mimi, tazama, nimewatwaa Walawi na kuwatoa kati ya wana wa Israeli badala ya wazaliwa wa kwanza wote wafunguao tumbo katika wana wa Israeli; na hao Walawi watakuwa wangu; 13 kwa kuwa hao wazaliwa wa kwanza wote ni wangu; katika siku ile niliyowapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri nikajiwekea wakfu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, wa wanadamu na wa wanyama; watakuwa wangu; mimi ndimi BWANA”.
Hesabu 3:12 “Mimi, tazama, nimewatwaa Walawi na kuwatoa kati ya wana wa Israeli badala ya wazaliwa wa kwanza wote wafunguao tumbo katika wana wa Israeli; na hao Walawi watakuwa wangu;
13 kwa kuwa hao wazaliwa wa kwanza wote ni wangu; katika siku ile niliyowapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri nikajiwekea wakfu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, wa wanadamu na wa wanyama; watakuwa wangu; mimi ndimi BWANA”.
Hivyo wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli wanaozaliwa ilikuwa ni sharti wakombolewe kwa sadaka ili watokane na kiapo hiko cha Bwana cha kuwa makuhani.
Na maana ya kukombolewa si kutolewa katika vifungo vya laana, kama mafundisho ya siku hizi za mwisho yanavyofundisha.
Bali ukombozi ilikiwa ni ile hali ya mtoto kutolewa katika nafasi ya kikuhani ambayo angepaswa kuitumikia maisha yake yote.
Hivyo anapokombolewa anakuwa huru kama watu wengine wasio na utumishi wa kikuhani (kwa ufupi anafunguliwa kutoka katika vifungo vya ukuhani)
Na mtoto wa kwanza asipokombolewa anabaki katika kifungo cha dhambi ya nafasi ya kikuhani.
Sasa swali je hata sasa katika agano jipya tunasheria hizo za kukomboa mzaliwa wa kwanza?.
Jibu ni la!..katika agano jipya hatuna sheria za kumkomboa mzaliwa wa kwanza au wa mwisho, kwasababu sote tuliomwamini Bwana YESU na kutakaswa kwa damu yake tunafanyika kuwa makuhani wa Bwana.
Ufunuo wa Yohana 1:6 “na kutufanya kuwa ufalme, na makuhani kwa Mungu, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina”.
Hivyo sote tunayo huduma ya kikuhani na mbele za Mungu, na ukishakuwa tu kuhani tayari ni mzaliwa wa kwanza pasipo kujali rika…Hivyo kanisa la Kristo ni wazaliwa wa kwanza.
Waebrania 12:23 “mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika”.
Kwahiyo hakuna sadaka yoyote ya ukombozi kwa wazaliwa wa kwanza kwa jinsi ya mwili.
Mafundisho na maombi ya kukombolewa kwa wazaliwa wa kwanza si ya kiMungu, bali ni ya ibilisi.
Ndio tunaweza kuwaombea wazaliwa wetu wa kwanza na kuwaweka wakfu kwa Bwana, dhidi ya roho zinazofuatilia, lakini si kuwakomboa….uwakomboe na nini?…je uwakomboe uwatoe katika ukuhani?…maana ndio lengo la ukombozi hilo kibiblia lililokuwepo juu ya wana wa Israeli juu ya wazaliwa wa kwanza.
Zaidi sana watoto wetu wa kwanza wanapaswa wawe wazaliwa wa kwanza kiroho kwa kumwamini YESU na kutakaswa ndipo wanapofanyika makuhani kama wengine wote waliomwamini YESU.
Mwisho, fahamu kuwa kilichowafuga wana wa Israeli ni miungu ya misri, iliyokuwa inaabimudiwa ndani ya kila kiumbe kilichokuwa cha kwanza.
Hali kadhalika vile vitu vinavyojiinua katika maisha yetu vilivyo vya kwanza ndivyo ni lazima tuwe navyo makini kwani hivyo ibilisi anaweza kuvitumia kama mlango wa kutufunga.
Je cha kwanza kwako ni nini?…je ni kazi uliyonayo?…au ni cheo ulicho nacho?..au ni uzuri au ni Bwana YESU?..
Ni heri BWANA YESU akawa wa kwanza kwako, kwani yeye ndiye njia, kweli na Uzima.
UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?
Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?
Waliouawa Shitimu kwa pigo walikuwa ni watu Elfu 23 au elfu 24?.
USIMWABUDU SHETANI!
SWALI: Je! tunalisoma wapi kwenye maandiko panasema ndoa inapaswa ifungwe kanisani. Utaratibu huo upoje?
JIBU: Ili kujibu swali hili tuanzie mbali kidogo.
kufahamu ndoa ni nini? aina za ndoa, kisha mahali sahihi pa kufungia ndoa ni wapi?.
Ndoa ni muunganiko kati ya watu wawili(mwanaume na mwanamke ) unaotambulika na kuheshika kijamii, au kisheria.
Pale mwanaume anapomwona mwanamke na kupatana naye waishi pamoja kama mume na mke, kwa kufuata taratibu husika za kijamii, labda kukutanishwa kwanza wazazi, au walezi, wazee wa ukoo, kupokea mahari, kisha kuidhinisha jambo hilo, au serikali kuidhinisha, hiyo tayari inaitwa ndoa.
Aina mbili za ndoa.
Ndoa za wapagani. Hizi ni ndoa lakini hazijadhibitiwa na kanuni timilifu za Mungu. Mfano wa hizi, ndio hizo kama za kijamii, na kiserikali, au za dini nyingine zote mfano wa ki-hindu, kiislamu, ki-budha n.k. zote hizi ni ndoa za wapagani.
Zingatia: (Hapa hatumaanishi zile za mashetani, kama za jinsia moja, au za wanadamu na wanyama hapana kwasababu hizo sio ndoa, bali tunazungumzia hizi za kawaida kabisa za asili).
Kiuhalisia mtu anaweza akawa katika mojawapo ya ndoa hizi, na asihesabike kuwa ni mkosaji kwasababu ndoa hasa ni jambo la kiutamaduni, ambalo huusisha wanadamu wote, bila kuchagua dini, rangi, au kabila.
Hivyo si sawa kudhani kuwa kwasababu watu fulani hawajafungishwa ndoa kikristo(kanisani) basi, zote hizo sio ndoa kwamba ni sawa tu hata kwenda kuoa tena hapo, au kuivuruga, wasiishi pamoja. Ukifanya hivyo Mungu atakuwajibisha kwa kuzivuruga ndoa za watu wengine.
Aina ya pili ya ndoa ni ndoa ya kikristo.
Hii ni ndoa inayofungwa katika kanuni timilifu za Mungu alizozikusudia tangu mwanzo.
Kanuni zenyewe ni hizi
i) Wote wawe waamini.
(1Wakorintho 7:39, 1Wakorintho 9:5, 2Wakorintho 6:14 – 16)
Kuamini si lazima muwe katika viwango sawa kiroho, lakini wote muwe upande mmoja wa Kristo, (Kwasababu hayo mengine yanaweza rekebika). Lakini mmoja ni mganga wa kienyeji, mwingine mkristo,.au mmoja ni muislamu mwingine mkristo. Hilo si sawa ni sharti wote wawe wakristo. Kwasababu hakuna ushirika wowote kati ya nuru na giza.
Kwasababu Ndoa ya kikristo ni lazima iwe katika jina la Bwana, vinginevyo, itaangukia katika lile kundi lingine.
ii) Mume mmoja, mke mmoja.
Tofauti na ndoa za wapagani. Ambazo kwao unaweza kuwa na mke zaidi ya mmoja, lakini mtu anayetaka ndoa yake itimilike mbele za Kristo, basi mume/mke atambue kuwa hana ruhusa ya kuongoza mwenza mwingine.
Mathayo 19:4-5
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, [5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? a
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? a
iii) Malazi yawe safi:
Waebrania 13:4
[4]Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.
Malazi kuwa safi maana yake ni nidhamu ya kiasi, katika kukutana kimwili. Mkristo hapaswi kuwa mtu wa hulka ambaye wakati wote anawaza zinaa, mpaka anakosa muda wa kujishughulisha na mambo ya rohoni.
1 Wakorintho 7:5
[5]Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.
Vilevile viitendo kama kuingiliana kinyume na maumbile haviruhusiwi ndani ya ndoa (1Wakorintho 6:9).
iv) Hakuna talaka.
Tofauti na ndoa za wapagani, mtu anaweza kuacha/kuachwa kwa sababu yoyote, labda mfano wamechokana, au wameudhiana, lakini katika ukristo hilo jambo halipo mtaendelea kuishi pamoja mpaka kifo kitakapowatenganisha.
Bwana alitoa ruhusa hiyo katika eneo la uasherati tu lakini ukumbuke, alisema pia ‘samehe mara saba sabini’. Hivyo kwa kauli hiyo hakuna popote tunaona wigo wa wanandoa kuachana kwa sababu yoyote ile.(1Wakorintho 7:39-40)
V) Mume ni sharti ampende mkewe.
Mume kumpenda mkewe ni amri ya kindoa, anawajibu wa kumtunza na kumuhudumia na kujitoa kwa ajili yake, kama Kristo alivyolipenda kanisa.(Waefeso 5:25-31)
Vi) Mke ni sharti amtii mumewe.
Ni amri mke amtii mumewe kwa agizo atakaloambiwa/ elekezwa. Tofauti na ndoa za wapagani ambazo hili linaweza lisiwe la muhimu. Kwenye ukristo, ni lazima utii wa mwanamke uonekane kwa mumewe.
Waefeso 5:22
[22]Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu.
Sasa vigezo hivi wakivikidhi hawa wakristo ambao wameokoka na wanatarajia kuishi kama mke na mume. Basi hiyo huitwa ndoa ya Kikristo iliyokidhi vigezo vitimilifu vya Mungu,.haijalishi imefungwa kanisani au kwenye familia, .
Swali ni je? kwanini watu wafungie kanisani? Na Je ni takwa?
Mkristo ambaye anathamini ukamilifu wote wa ki-Mungu, katika maeneo yake yote ya kiroho na kimwili, kufungia ndoa yake kanisani itakuwa ndio chaguo lake bora. Kwanini iwe hivyo?
Hizi ndio faida za ndoa kufungiwa kanisani
Biblia inatueleza mashtaka yetu, hayapaswi kutatuliwa na watu wa ulimwengu, bali ndani ya kanisa. Kwasababu kanisa ni zaidi ya mahakama yoyote, ambayo Mungu ameiheshimu mpaka akaamua malaika zake wahukumiwe katika hiyo.
Hivyo endapo kuna migogoro, au kutoelewana, au kupatiwa misaada, au mashauri, au maonyo, au maongozi, basi kanisa, limewekwa na Mungu kwa ajili yako kukusaidia katika hayo yote.
Lakini ikiwa hukuifungia ndoa yako kanisani. Fahamu kuna mambo kama hayo yatakupita, au yatakuwa magumu kwetu kutatulika.
1 Wakorintho 6:1-3
[1]Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu? [2]Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? [3]Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?
[1]Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu?
[2]Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo?
[3]Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?
2) Ushuhuda mwema.
Mungu anapenda mambo mema atufanyiayo tumtukuze mbele ya kusanyiko la watakatifu. Tunajua Ndoa ni kitu chema, hivyo tunapoweka wazi mbele za Bwana, na mbele ya kanisa lake, yeye hutukuzwa lakini pia tunapokea baraka za kanisa, Ikiwa tunapoumwa na kuponywa hatuoni sawa kukaa na shuhuda zetu ndani, tunakwenda kushuhudia mbele ya kanisa, si zaidi ndoa zetu?, ni ushuhuda mkubwa, ambao utawafariji wengine, lakini pia utaihubiri injili ya Kristo.
Zaburi 35:18
[18]Nitakushukuru katika kusanyiko kubwa; Nitakusifu kati ya watu wengi.
[18]Nitakushukuru katika kusanyiko kubwa;
Nitakusifu kati ya watu wengi.
Hivyo, kwa maelezo hayo tunaweza kusema hakuna sababu ya Mkristo yoyote kuifungia ndoa yake, mbali na kanisa.
Lakini hiyo haimaanishi kuwa usipofungia kanisani, ndoa yake haitambuliwi na Mungu. Maadamu umekidhi vigezo “mama”, tulivyoviorodhesha juu. Hiyo ni ndoa.
Bwana akubariki
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
MAFUNDISHO YA NDOA.
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
Je! Ni sahihi kuoa/kuolewa na mtu uliyemzidi umri?
Swali: Je Bwana YESU alikuwa amemfunga shetani wakati wa kuzaliwa kwake Kulingana na Mathayo 12:29?
Jibu: Turejee.
Mathayo 12:29 “Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, ASIPOMFUNGA KWANZA yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake”.
Jibu ni kwamba shetani hakuwa amefungwa wakati wa kuzaliwa Bwana YESU, na hata sasa shetani hajafungwa!, kwani Ingekuwa shetani amefungwa wakati wa kuzaliwa Bwana, basi Herode asingetafuta kumwua mtoto..
Mathayo 2:13 “Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize”.
Tukio hilo linaeleweka vizuri katika Ufunuo 12:1-6.
Vile vile Ibilisi asingesimama kumjaribu Bwana kule jangwani..
Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ILI AJARIBIWE NA IBILISI. 2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa. 3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate”
Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ILI AJARIBIWE NA IBILISI.
2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa.
3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate”
Na ikiwa shetani amefungwa leo, maasi yasingeendelea kuwepo na maandiko yasingetuonya kuwa tusimpe nafasi..
Waefeso 4:28 “wala msimpe Ibilisi nafasi. 28 Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji”.
Waefeso 4:28 “wala msimpe Ibilisi nafasi.
28 Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji”.
Maandiko yametabiri shetani kuja kufungwa katika ule utawala wa miaka elfu wa Bwana wetu YESU hapa duniani. Na utawala huo utaanza baada ya dhiki kuu kuisha, na hukumu ya Mungu kwa mataifa kupita (Ufunuo 16), hapo ndipo utawala wa miaka elfu moja utakapoanza na shetani (pamoja na majeshi yake) kufungwa kwa kipindi hiko.
Ufunuo 20:1 “Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake. 2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu; 3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache”.
Ufunuo 20:1 “Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;
3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache”.
Kwahiyo shetani kwasasa yupo na hakuwahi kufungwa wakati wowote huko nyuma, lakini atakuja kufungwa baada ya hukumu ya Mungu kwa mataifa inayotajwa katika Ufunuo 16.
Sasa swali kama ni hivyo je! Maandiko hayo katika Mathayo 12:29 yana maana gani?….
Turejee tena..
Haya ni maneno ambayo Bwana YESU aliyasema, akifundisha nguvu iliyo kuu/kubwa inapoingia mahali basi inateka au inafunga ile nguvu iliyo dhaifu.
Na ukisoma kuanzia juu kidogo utaona ni wakati ambapo Mafarisayo walimwona akitoa pepo kwa uweza wa Mungu, lakini wakasema yeye hatoi kwa uweza wa Mungu bali kwa uwezo wa Pepo mkuu aitwaye Beelzebuli, ambaye ni shetani mwenyewe.
Na Bwana akawahoji, akiwauliza yawezekanaje Shetani amtoe shetani mwenzake?..jambo ambalo haliwezekani!, vinginevyo ufalme wa giza hauwezi kusimama, lakini kama wakiona pepo katolewa maana yake katolewa kwa uweza wa Mungu, kwasababu kamwe shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake.
Na ili kulifanya hilo lizidi kueleweka vizuri ndipo akatoa mfano mwingine kwamba… “Awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, ASIPOMFUNGA KWANZA yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake”
Ikifunua kuwa Bwana anapotoa pepo, kwanza anauteka ule ufalme wa giza (maana yake wote unakuwa chini ya amri yake) halafu ndipo anaamrisha pepo zitoke na kwenda atakako yeye soma Mathayo 8:28-32.
Sasa kitendo cha Bwana YESU kusimama na kuamrisha, maana yake mamlaka yake ni KUU inayoteka, na kufunga, na kuhamisha.. Na mamlaka hiyo hajabaki kwake tu peke yake, bali pia amewapa na wale wote wanaomwamini na kufanya mapenzi yake, kwamba kwa jina lake wanateka, na wanafunga na kuhamisha kila falme za giza.
2Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) 5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKIRA IPATE KUMTII KRISTO; 6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.
2Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKIRA IPATE KUMTII KRISTO;
6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.
Kwahiyo mantiki ya Bwana YESU hapo ya KUFUNGA, haikuwa ya kumfunga shetani asiwepo duniani, bali katika kuzifunga kazi za ibilisi na majeshi yake zisisimame mbele yetu. (lakini shetani yupo, na ataendelea kuwepo na kuwasumbua wale wote wasiomwamini na kumfuata Bwana YESU), lakini walio na Bwana shetani hana nguvu juu yao.
Mathayo 18:18 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni”.
Je umeokoka??..Hizi ni siku za hatari na BWANA anarudi. Na shetani anajua wakati wake uliobaki ni mchache sana, hivyo anafanya kazi kwa kasi sana kusudi asiende kwenye lile ziwa la moto peke yake.
Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”
Je bado wewe ni rafiki wa dunia?, bado ni mshabiki wa mipira, bado unacheza Kamari, bado unavaa kidunia na kuupenda ulimwengu?
1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. 16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia. 17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”
1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.
16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”
Je YUDA alikuwa ni shetani kulingana na Yohana 6:70?
NIFANYE NINI NIMSHINDE SHETANI?
Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?
Nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.
Kusujudu ni nini, na je tuna sharti la kusujudu kwa Mungu?