Category Archive Uncategorized @sw-tz

Kuota unasubiriwa mahali fulani uhutubie, halafu unachelewa.

SWALI: Kuota nasubiriwa mahali Fulani, nihutubie halafu mimi nachelewa, au natingwa na mambo mengine ina maana gani?


JIBU: Ndoto ya namna hii, mara nyingi huwa inaotwa na makundi ya watu ambao wanawajibika katika kuwahudumia wengine, aidha ni viongozi, au wahubiri.

Na huwa zinakuja katika sura tofauti tofauti, wengine wanaota wanasubiriwa kwenye mikutano wahutubie, lakini wanajikuta, wakicheleweshwa na mambo madogo madogo, pengine foleni, au watu, au vishughuli visivyokuwa na msingi. Wengine wanaota wanapaswa wapande madhabahuni wawahubirie wengine, lakini mara wanajiona wapo uchi, wanatafuta suti zao wavae, hawazioni, muda unazidi kwenda, mpaka mwishoni watu wanaondoka, wote na yeye bado hajatokea madhabahuni. N.k.

Hivyo ukiota ndoto ya namna hii tafsiri yake ni kuwa, wewe kama kiongozi kiwango chako cha utayari katika  nafasi hiyo Mungu aliyokuweka bado kipo chini. Na ndio maana unashindwa kufika pale, yapo mambo ambayo yanatia vikwazo kwako. Bwana anasema..

2Timotheo 4:2  “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”

Hivyo unachopaswa kufanya ni kuondoa visababu, au hivyo vizuizi vidogo vidogo, mbele yako, ambavyo pengine vinakusababishia uone huo sio wakati ufaao, kwa kumtumikia Mungu, kisha kuwa tayari, kusimama na Bwana kwa ukamilifu wote, kama askari ambaye amevitwa utayari miguuni kwa ajili ya  vita.

Waefeso 6:13  “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15  na kufungiwa miguu UTAYARI tupatao kwa Injili ya amani”

Kwa kuzingatia hayo, utakuwa umelitatua hilo tatizo, katika wito wako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuota unapigana na mtu.

KUOTA UPO KANISANI.

KUOTA UNALIA/UKIOTA UNALIA KWA UCHUNGU.

KUOTA UMECHOMWA KISU/KUOTA UMEPIGWA RISASI.

MTAWATUPIA MBWA NYAMA HIYO.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?.

Rudi nyumbani

Print this post

JIPE NAFASI KATI YA TAARIFA UNAYOIPOKEA NA MAAMUZI UNAYOYATOA.

Shalom, jina la Bwana libarikiwe.

Ni vema tukajifunza tabia kadha wa kadha za Mungu, ili na sisi tuziige hizo tuwe wakamilifu kama yeye. Leo tutajifunza tabia mojawapo ya Mungu, ambayo pengine unaweza ukastaajabu Mungu anawezaje kuonyesha angali yeye ni Mungu. Hivyo kwa kupitia hiyo tutajifunza na sisi mienendo yetu.

Kwamfano ukisoma kitabu cha Mwanzo, baada ya Mungu kumaliza uumbaji wake wote, baadaye utaona tena anasema “si vema”(Mwanzo 2:18). Sasa utajiuliza iweje aone tena si vema, kwani kazi yake hapo mwanzo ilikuwa haijakamilika? Inahitaji marekebisho.. Mpaka aanze tena uumbaji mwingine wa kumpa Adamu msaidizi?..

Jibu ni kwamba Sio kwamba hakulijua hilo? Hapana alishalijua na tayari alikuwa ameshamuumba Hawa katika akili yake tangu zamani (Soma Mwanzo 1:27). Lakini alijifanya kana kwamba amesahau, ili kutufundisha sisi pia, tuwe watu wa kupenda marekebisho. Marekebisho sio dhambi, ni karama ya Mungu..Kwani kwa kupitia hiyo tutafikia ukamilifu, ukiwa mtu wa kuridhika na maisha yaleyale, mienendo ile ile, huna maboresho yoyote, ujue tabia hii ya Ki-Mungu haipo ndani yako.

Vivyo hivyo kuna tabia nyingine, ya kushangaza aliionyesha Mungu, na leo tutajifunza. Utakumbuka wakati ule, anakwenda kuiteketeza Sodoma na Gomora, alikutana kwanza na Ibrahimu, na alipomaliza kuzungumza naye akabidi pia amweleze  Ibrahimu mpango wake, akamwambia maneno haya;

Mwanzo 18:20 “Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana, 

21 BASI, NITASHUKA SASA NIONE KAMA WANAYOTENDA NI KIASI CHA KILIO KILICHONIJIA; NA KAMA SIVYO, NITAJUA. 

22 Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za Bwana”

Tafakari kwa ukaribu hayo maneno..“nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua”.. Ni nini unajifunza hapo, kwamba huyu ni mtu asiyechukua maamuzi ya haraka kwanza bila kwenda kuthibitisha kwa undani ukweli wa tukio lenyewe.

Sio kwamba Mungu alikuwa hana uhakika wa kilichokuwa kinaendelea..Lakini alijifanya kana kwamba hajui, akaacha shughuli zake mbinguni, akateremka chini, aingie sodoma, atembee kwenye miji yake, ili apate uhakika wa taarifa zilizomfikia. Alijipa nafasi kati ya kile anachokisikia na maamuzi anayoyatoa.

Na kweli alikuta vilevile kama vilio vyao vilivyomfikia, lakini faida yake ni kuwa ndani yake alimwona mwenye haki mmoja, naye ni Lutu na familia yake, ndipo akamwokoa na ghadhabu ile. Lakini kama Bwana angetoa hukumu yake moja kwa moja kutoka kule mbinguni, pindi tu alipopokea taarifa na kusema ‘haya nyie malaika kapigeni kiberiti miji ile’.. Lutu angeonekania wapi?.

Ni nini tunajifunza?

Tumeyabomoa maisha yetu sana, tumewaharibu wakina Lutu wetu, kwa kuchukua maamuzi ya haraka kwa kila tukio/Taarifa tunayoisikia, masikioni mwetu, au kwa kila jambo linalotokea ghafla mbele yetu.

Kwamfano Umesikia ndugu yako amekusengenya, usiwe na haraka wa kurudisha majibu ya chuki. Jifanye kama hilo ulilolisikia ni la uongo hata kama umelithibitisha.. Hiyo itakupa nafasi ya wewe, kutafakari kujua chanzo cha tatizo ni nini, na hatimaye utajikuta huwenda wewe ndio ulikuwa sababu ya yeye kuwa vile, na hapo utamsamehe, au kumwombea, au kujiombea wewe rehema. Lakini ukarudisha majibu ya kumchukia, au kumsema na wewe. Utajibomoa zaidi kuliko kujijenga.

Waweza sikia taarifa mbaya, au hujapendezwa na jambo Fulani au tukio fulani  kwenye kanisa, kabla hujazira na kuondoka, pata nafasi ya kuomba, na kumshirikisha Mungu, kupitia viongozi wako wa kiroho, kama vile Mungu alivyomshirikisha rafiki yake Ibrahimu. Hiyo itakusaidia kuchukua maamuzi yaliyo ya busara zaidi.

Hata katika mambo ya maisha, kwenye familia, ukoo, pengine hata kazini kwako, ofisini, n.k, zipo taarifa nyingi zinaweza kukufikia za wafanyakazi wenzako, hupaswi kuzimeza  moja kwa moja na kuzitolea maamuzi hata kama umezithibitisha kuwa ni za kweli.. Tuliza moyo wako, tafakari, omba, ndipo baadaye Mungu akuongoze cha kutenda. Utafanya vizuri zaidi.

Ni muhimu sana, kuweka “NAFASI” Katika mioyo yetu. Kile kinachoingia, kisirudishe majibu hapo hapo. Ni heri viingie mia, kikatoka kimoja chenye majibu ya busara, kuliko kuingia 100, vikatoka vyote 100, vyenye kisasi, na maumivu, na mapigo. Ilimgharimu Bwana asiziamini taarifa zake, iweje wewe uamini za kwako, au za wanadamu wengine?

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)

Ni miaka mingapi ya njaa Daudi aliyoambiwa achague? Ni miaka 7 au miaka 3?

Rudi nyumbani

Print this post

KUWA MWOMBOLEZAJI.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WANAWAKE.

Kuwa mwombolezaji:

Yeremia 9:20 “Lakini lisikieni neno la Bwana, enyi wanawake, Na masikio yenu yapokee neno la kinywa chake; Mkawafundishe binti zenu kuomboleza, Na kila mmoja jirani yake kulia”.

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo Bwana wetu, mkuu wa uzima, karibu katika kujifunza maneno ya uzima. Huu ni mwendelezo wa mafundisho maalumu yawahusuyo wanawake.

Leo nataka tuone jambo ya kitofauti lililokuwa linawatokea wanawake wengi wa-Kimungu katika biblia. Na kwa kupitia hilo naamini lipo la kujifunza wewe kama mwanamke, uliyeokoka.

Na jambo yenyewe ni “kufungwa Tumbo la uzazi”. Ukisoma kuanzia mwanzo, wanawake wengi hodari walioitwa wacha Mungu, walifungwa matumbo yao wasiweze kuzaa, tukianzia kwa Sara, mpaka Rebeka, tukiendelea hadi kwa Raheli, na Ana-Mama yake Samweli, na  Mke wa Manoa aliyemzaa Samsoni, na  Elizabeti mama yake Yohana. Wote hawa walikuwa ni matasa. Unajua ni kwanini?

Wengi wanachukulia katika jicho la laana na mikosi, lakini ukitafakari vizuri, hakukuwa na laana yoyote juu ya watu hawa, kwasababu maandiko yanatuambia ni Mungu mwenyewe ndio aliyewafunga matumbo yao, Tengeneza picha Sara ambaye wafalme waliojaribu kumuiba wamfanye mke wao, Bwana aliwaadhibu vikali, mtu kama huyo iweje awe amebeba laana?

Hivyo lipo funzo kubwa sana nyuma yake, linalowahusu wanawake wote. Na funzo lenyewe ni kwamba Mungu anataka mwanamke yeyote, awe mwombolezaji, ili kusudi lake litimie, aulekeze moyo wake kwake kwa machozi mengi na dua, maombi, kwasababu kwa kupitia yeye, Mungu atalifanikisha kusudi  lake kubwa duniani.  Na ndio maana ilimgharimu Mungu awafunge matumbo wale wanawake wote, ambao alijua kabisa kwa kupitia wazao wao, Mungu atatukuzwa.

Ndio hapo utamwona mwanamke kama Ana, mke wa Elkana analia kama mlevi kule hekaluni, juu ya uzazi wake, yeye akidhani kwamba Mungu anasikiliza dua za tumbo lake, kumbe Mungu alikuwa anasikiliza maombi ya kuletwa mwamuzi  Samweli duniani… Kwasababu ili shujaa aje ilihitaji maombolezo mengi sana.

 Lakini kama moyo wake ungelitambua hilo tangu mwanzo, kuomba kwa bidii juu ya mwamuzi Israeli, kulikuwa hakuna sababu ya yeye kufungwa tumbo. Yanini?

Ndivyo ilivyokuwa kwa Raheli na Elizabeti, na wanawake wengine.

Binti, dada, Mama, bibi.. Tambua kuwa wewe umewekwa, kama  mzalisha Nuru ulimwenguni. Maombi yako, machozi yako, sala zako, maombolezo yako, ni changizo kubwa sana la Mungu kuleta mapinduzi katika kanisa, familia, na hata taifa kwa ujumla.

Usisubiri Mungu akufunge tumbo lako, ndipo uanze kulia, na kuomboleza,. Bali jitambue sasa, Kumbuka Tumbo, linaweza kuwa pia kazi yako, au  afya yako n.k ukiona hicho ndicho kinachokukosesha raha sasa, na umekiombea kwa muda mrefu bila mafanikio, basi tambua umefungwa hivyo na Mungu makusudi, ili uuelekeze moyo wako kwake.

Sasa hapo usiombe Mungu akupe mtoto au akupe kazi au akuponye huo ugonjwa, au akukombe kiuchumi, hapana omba Mungu, alete geuko kwa kanisa, kwa familia yako, kwa taifa, kwa kupitia wewe, ombea sana rehema na toba. Na hayo yaliyosalia Mungu alishakujibu siku nyingi yeye mwenyewe alishayatimiza. Kutokukujibu kwake haraka sio kwamba akutese hapana, machozi yako kwake hayajatosha, na umeyaelekeza pasipostahili.

Mwanamke usipokuwa mwombolezaji, fahamu kuwa unalididimiza kanisa, usipokuwa mwombaji, unalidhoofisha kanisa la Kristo kwelikweli. Tambua huduma hii, ili Kanisa liweze kusimama vema, wachungaji waweze kuhubiri, vipawa na karama vinyanyuke kwenye kanisa hadi kwenye familia, wewe ndio unayeweza kufungua milango hiyo.

Bwana atusaidie kujua hilo;

Yeremia 9:17 “Bwana wa majeshi asema hivi, Fikirini ninyi, mkawaite wanawake waombolezao, ili waje; mkatume na kuwaita wanawake wenye ustadi, ili waje; 18 na wafanye haraka na kutuombolezea, ili macho yetu yachuruzike machozi, na kope zetu zibubujike maji.

19 Maana sauti ya maombolezo imesikiwa toka Sayuni, Jinsi tulivyotekwa! tulivyofadhaika sana! Kwa sababu tumeiacha nchi, kwa kuwa wameangusha makao yetu.

20 Lakini lisikieni neno la Bwana, enyi wanawake, Na masikio yenu yapokee neno la kinywa chake; Mkawafundishe binti zenu kuomboleza, Na kila mmoja jirani yake kulia.

21 Kwa maana mauti imepandia madirishani mwetu, imeingia majumbani mwetu; Ipate kuwakatilia mbali watoto walio nje, na vijana katika njia kuu”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO KWA WANAWAKE.

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)

Nini maana ya kupiga Kite! Katika biblia.

Shetri ni nini kama tunavyosoma katika Marko 3:38?

Rudi nyumbani

Print this post

NIMEYATUNZA MANENO YA KINYWA CHAKE ZAIDI YA RIZIKI YANGU.

Ayubu 23:12 “

[12]Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu”,

Huyu ni Ayubu, …si ajabu kwanini Mungu alimwona ni mtu mkamilifu  aliyemcha Mungu, kuliko watu wote waliokuwa ulimwenguni wakati ule.

Kitendo cha kuyatunza maneno ya Mungu zaidi ya riziki..si jambo dogo, ni kumaanisha kwa hali ya juu sana.

Ni kawaida mtu akiamka asubuhi jambo la kwanza atakalowaza ni ale nini, anywe nini..haiwekezani mtu apitishe siku nzima bila kukumbuka kuna kitu kinapaswa kiwekwe tumboni, Au asifikirie miradi yake, au kazi zake zinakwendaje siku hiyo,. Labda awe na hitilafu katika neva za ubongo wake.

Lakini Ayubu, ilikuwa ni kinyume, chakula/rizki ilikuwa ni “B” …”A” alipoamka asubuhi alikuwa anatafakari atayatimiza vipi maagizo ya Mungu, alikuwa anawaza siku itapitaje pitaje bila kupiga hatua mpya ya ukamilifu.

Hicho ndicho kilichokuwa chakula chake, alionyesha tabia iliyokuwa kwa mkuu wake YESU KRISTO. Ambaye tunasoma wakati fulani alipofuatwa na wanafunzi wake  kuletewa chakula, aliwaambia maneno haya:

Yohana 4:30-34

[30]Basi wakatoka mjini, wakamwendea.

[31]Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.

[32]Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.

[33]Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?

[34]Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.

Ayubu alipoamka asubuhi aliwaza toba,kwa ajili ya wengine.., (Soma Ayubu 1:5)

Alihakikisha Neno la Mungu halidondoki, alifanya agano na macho yake, asiwatazame wanawake akawatamani, (Ayubu 31:1). Aliwaza kuwafundisha wengine hekima na busara na kuwasaidia waliokuwa katika dhiki na uhitaji, (Ayubu 31:16-18), mtu wa namna hii Mungu hawezi acha kumwangalia na ndio maana tunasoma Habari zake mpaka leo.

Je na sisi tunaweza kufanana na watu kama hawa ambao walikuwa na tabia sawa na sisi. Kumbuka Ayubu hakuwa myahudi, wala nabii, wala kuhani..biblia inamwita MTU tu, fulani aliyetokea  katika nchi moja iliyoitwa USI.

Na sisi, hivi hivi tulivyo tuna wajibu wa kumaanisha kuyatunza maneno ya Mungu, katika wokovu wetu, tuhakikishe tunayafanya maneno yake ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku, ili tusiwe wasahaulifu. 

Bwana Yesu alitupa amri tupendane..ni lazima tujifunze tabia hii, kila siku, alisema pia tusamehe, tusiposamehe Baba yetu naye hataweza kutusamehe makosa yetu.

Haijalishi umekosewa mara ngapi, umeibiwa mara ngapi, umedhulumiwa mali nyingi kiasi gani, kamwe usiyasahau maneno ya Bwana Yesu.. ‘samehe mara saba sabini…’

Bwana Yesu alisema, kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni..ukilisahau hili neno ukawa ni mvivu wa kuomba walau saa moja kwa siku kama alivyosema, wewe sio mkamilifu.Ifikie hatua kama vile tukumbukavyo muda wa kula ndivyo tukumbuke muda wa maombi na ibada. Huko ndiko kuyatunza maneno yake zaidi ya riziki zetu.

Na kwa bidii hiyo Bwana atatuona na kujidhihirisha kwetu,kwasababu sikuzote anazunguka ulimwenguni kote kutafuta watu wenye kumaanisha huku kama Ayubu ajifunue kwao.

2 Mambo ya Nyakati 16:9

[9]Kwa maana macho ya BWANA hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake…”

Bwana atutie nguvu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? (Yeremia 17:9)

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

JIBU: ‘Bila kazi ya mikono’ maana yake ni kuwa pasipo kisaidizi chochote cha kibinadamu, kwamfano neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

Danieli 2:34 “Nawe ukatazama hata jiwe likachongwa bila kazi ya mikono, nalo jiwe hilo likaipiga sanamu miguu yake, iliyokuwa ya chuma na udongo, likaivunja vipande vipande”.

Huu ni utabiri unaomwelezea Yesu Kristo, jinsi atakavyokuja kuangusha ngome zote za ufalme wa huu ulimwengu, yeye ndio hilo jiwe dogo linalozungumziwa hapo, Na biblia inasema, lilichongwa bila kazi ya mikono maana yake ni kuwa lilijichonga lenyewe kutoka mwambani, lilijimegua lenyewe, likaenda na kuipigia ile sanamu, kufunua kuwa Kristo, hakuletwa na mwanadamu hapa duniani, alizaliwa pasipo baba, halikadhalika atakapokuja kuangusha hizi falme sugu za ulimwengu, hatosaidiwa na mtu, wala hata tegemea msaada wa mtu yeyote yeye mwenyewe ataupiga kwa uweza wake, na wote utaanguka kisha atauweka utawala wake usio na mwisho, ambao utaifunika dunia nzima,

Kufahamu jinsi atakavyojua kuzipiga hizi falme za dunia Soma Ufunuo 19:11-16

“11 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 NA UPANGA MKALI HUTOKA KINYWANI MWAKE ILI AWAPIGE MATAIFA KWA HUO. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA”.

Lakini pia Neno hili, utalisoma katika vifungu vingine, ambavyo vinamwelezea mtawala katili aliyetokea zamani katika ufalme wa Uyunani, aliyeitwa Antiokia Epifane, mtawala huyu alikuwa ni kivuli cha mpinga-Kristo anayekuja, kwani, alikuwa na nguvu nyingi, na kwasababu hiyo akawaua wayahudi wengi, na kama hiyo haitoshi akalitia unajisi hekalu la Mungu, ambalo hata wafalme wengine walikuwa wanaogopa kufanya matendo kama hayo, yeye hakujali hiyo alikuwa anamtukana Mungu wa Israeli hadharani, na kuchukua nguruwe na kuwaingiza hekaluni, lakini biblia inasema alivunjika, bila kazi ya mikono.

Danieli 8:25 “Na kwa mashauri yake atafanikisha hila mkononi mwake; naye atajitukuza nafsi yake moyoni mwake; naye atawaangamiza wengi katika hali yao ya salama; naye atasimama kushindana naye aliye Mkuu wa wakuu; lakini atavunjika, bila kazi ya mikono”.

Maana yake ni kuwa, Mungu hatotumia jeshi, au wanadamu, au kitu chochote kijulikanacho kumuua, bali yeye mwenyewe atampiga na kufa ghafla, na ndivyo ilivyokuwa katika historia alipatwa na ugonjwa wa ajabu na ghafla, akafa. Kama alivyokuwa Herode wakati ule alivyoliwa na chango, baada ya kujitukuza kama Mungu. (Matendo 12:23).

Hii ni kufunua nini?

Kazi zote za huu ulimwengu ni mbovu, kama Yesu mwenyewe alivyosema katika Yohana 7:7, na ndio maana atakuja kuziondosha zote.  Falme zote zitaanguka, ustaarabu wote utaondolewa, Yesu atakuja kuweka ustaarabu wake mpya wa amani hapa duniani.

Sasa jiulize, mambo unayoyasumbukia leo hii, kana kwamba ndio uzima wako yatakufaidia nini huko mbeleni? Ishi ndani ya Kristo kama mpitaji na msafiri, ukijua kuwa huna makazi ya kudumu hapa, tumia nguvu zako, kuwekeza katika ufalme ujao udumuo, hata kwa hicho unachokisumbukia.

Kumbuka mambo haya yapo karibuni kutokea, huwenda hata ndani ya kizazi chetu, tukayashuhudia haya yote.

Maran Atha.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

DANIELI: Mlango wa 8

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

DANIELI: Mlango wa 2

Je mama mjamzito anaruhusiwa kufunga?

UTAKAPOKUWA MZEE, UTAINYOSHA MIKONO YAKO. NA MWINGINE ATAKUFUNGA

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.

Rudi nyumbani

Print this post

Hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.

SWALI: Inakuwaje tunaambiwa mambo mengine tunajaliwa? Na si kwa jitihada zetu, kujaliwa ni nini kibiblia?


JIBU: Kujaliwa maana yake ni kuwezeshwa kufanya jambo ambalo wewe kwa nguvu zako kamwe huwezi kulitenda.

Haya ni mambo ambayo biblia inatuambia mtu anajaliwa kuyafanya.

1) Kupokea wokovu:

Bwana Yesu alisema..

Yohana 6:65 “Akasema, Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu”.

Alisema maneno hayo, baada ya kuona wengi wa wanafunzi wake wanarudi nyuma kwa maneno yake magumu aliyokuwa anayesema, ya kuinywa damu yake na kuula mwili wake,. Hapo ndipo akasema maneno hayo. Ikiwa na maana kuwa hata sasa ukimwona mtu ameokoka kwelikweli kwa kumaanisha kumfuata Yesu na gharama zake, usidhani ni kwa nguvu zake, ameweza hivyo, hilo jambo halipo, hakuna mwanadamu mwenye asili ya dhambi anayeweza kujiamulia tu kwa akili zake kuamini mambo ya rohoni, asiyoyaona.

Alivutwa kwanza, na Mungu, kisha akapewa uwezo huo wa kukubaliana na vigezo vyake.

Yohana 6:44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho”.

2) Kujua siri za ufalme wa mbinguni:

Si kila mtu atapewa kuzielewa siri za ufalme wa mbinguni. Yesu anasema hivyo katika..

Mathayo 13:10 “Wakaja wanafunzi, wakamwambia, Kwa nini wasema nao kwa mifano?

11 Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa”.

Hiyo ni baada ya kuwapa mifano kadha wa kadha  ihusuyo ufalme wa mbinguni, bila kuwapa ufunuo wake, isipokuwa wanafunzi wake tu waliomfuata kumuuliza..ndipo akawaambia maneno hayo.

Ndugu kusoma biblia ni moja na kupokea ufunuo wa Mungu wa kweli ni jambo lingine, wapo watu wana elimu kubwa za theolojia, wanajua historia yote ya maandiko, wameirudia biblia mara 1000, kifungu baada ya kifungu, kama ilivyokuwa kwa mafarisayo na masadukayo, lakini wakashindwa kuelewa Neno dogo la ubatizo wa maji, kwamba ni lazima uwe wa kuzamishwa na kwa jina la Yesu. Au kufahamu kuwa sanamu hazipaswi kuhusianishwa ibada yoyote ya Mungu.

Hivyo ukiona wewe umepewa uelewa wa Neno la Mungu, mshukuru sana, wala usijisifu ukadhani ni kwa utashi wako, au uelewa wako mwepesi umeweza kujua hilo, Hapana bali umejaliwa  na Mungu..

3) Kuhudumu.

Kazi yoyote ya utumishi kwa Mungu, iwe ni ya madhabahuni au nje ya madhabahuni, ambayo unaifanya kwake, ujue kuwa, ni kwa nguvu ulizojaliwa na Mungu, wala si zako;

1Petro 4:11 “Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina”.

Si wote, wamepewa nguvu hizo, hivyo tumika kwa uaminifu.

4) Kutooa/kutokuolewa kwa ajili ya Bwana.

Wapo watu ambao Bwana Yesu amewapa uwezo wa kuyatawala mapenzi yao. Hivyo wanaweza kukaa bila kuoa/kuolewa na wasione shida yoyote. Sasa watu wa namna hii, sio kwa nguvu zao bali Bwana Yesu anasema ni kujaliwa.

Mathayo 19:10 “Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.

11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa”.

Hivyo, kwa kuhitimisha ni kuwa uonapo tendo lolote, la ki- Mungu lililogumu kufanyika kwa binadamu wa kawaida, ujue kuwa limetokea kwa kujaliwa na Mungu, na sio kwa nguvu za  mtu yule.

Tukiyafahamu haya, basi tutajifunza kuitii sauti ya Mungu, na kumwomba sana, na kuwa wanyenyekevu ili asitupite, kama hatutajaliwa na Mungu, haijalishi tutahubiriwa injili mara ngapi, tutaona miujiza mingi kiasi gani, tutatokewa na Yesu mara ngapi, kamwe hatuwezi kubadilika, Farao aliona miujiza mkubwa sana kutoka kwa Musa, lakini Mungu hakumpa moyo wa kutubu.

Yuda alikuwa ni mtume ambaye hakutokewa na Yesu,(linaweza likawa ni jambo dogo) bali aliishi na Yesu kabisaa kwa miaka mitatu na nusu, lakini bado ndani yake kulikuwa hakuna badiliko la dhati, na ndio maana akaja kumsaliti baadaye.

Yohana 17:12 “Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie”.

Hivyo uisikiapo sauti ya Mungu inaugua ndani yako, usiipuzie hata kidogo, chukua hatua haraka badilika. Kubali kutubu na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, Upokee kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwasababu hiyo sauti haitadumu milele ndani yako. Upo wakati itanyamaza kimya. Hivyo maanisha kumtii Mungu.

Bwana atasaidie.

Shalom.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? (Yeremia 17:9)

USIMPE NGUVU SHETANI.

Ni kweli hakuna mtu aliyewahi kuuona uso wa Mungu Zaidi ya Bwana Yesu?

Wala msimwite mtu baba duniani;..Hapo Bwana wetu Yesu anamaanisha nini kusema hivyo?

Kwanini Bwana Yesu alivikwa taji ya miiba?

Kiyama ni nini?

Je! Siku ya unyakuo watoto wachanga watanyakuliwa?

Rudi nyumbani

Print this post

KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MAENEO YA IBADA: Sehemu ya 1


KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

Kuna mambo ambayo yanaonekana madogo, lakini yana madhara makubwa sana rohoni. Watu hawafahamu kuwa wanaweza kufa kabisa kiroho kwa tabia ya kuendekeza USINGIZI ibadani..

Embu tusome habari ya Eutiko, tuone ni jambo gani Bwana anataka tufahamu nyuma ya matukio yaliyokuwa yanaendelea pale..

Tusome.

Matendo ya Mitume 20:7-10

[7]Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.

[8]Palikuwa na taa nyingi katika orofa ile tulipokuwa tumekusanyika.

[9]Kijana mmoja, jina lake Eutiko, alikuwa ameketi dirishani, akalemewa na usingizi sana; hata Paulo alipoendelea sana kuhubiri, akazidiwa na usingizi wake akaanguka toka orofa ya tatu; akainuliwa amekwisha kufa.

[10]Paulo akashuka, akamwangukia, akamkumbatia, akasema, Msifanye ghasia, maana uzima wake ungalimo ndani yake.

Nataka tuyatathimini hayo mazingira..kwanza walipokuwa wanasilizia injili ni katika gorofa, na gorofa yenyewe si ya kwanza bali ni ya tatu.. 

Pili japokuwa mahali pale ilikuwa ni usiku lakini biblia inatuambia kulikuwa na taa nyingi sana..maana yake ni kuwa mazingira yote yalikuwa yanaonekana, yapo wazi hivyo mahali pa hatari palionekana, na mahali salama pia palionekana.

Lakini tunaona huyu Eutiko alichagua kwenda kukaa katika dirisha la gorofa, akijua kabisa mahali pale si salama kukaa endapo akiteleza kidogo na kuanguka..

Lakini hakujali hilo, baada ya muda kidogo akasinzia.. Na matokeo yake akaanguka kutoka katika ile gorofa ya tatu. Na alipofika chini alikuwa tayari ameshakufa..

Ni kwanini habari hii iandikwe hapa? Kumbuka kila hadhithi inayoandikwa katika biblia inafundisho kubwa sana nyuma yake.

Sasa kitendo cha kuwepo katika gorofa ya tatu.

Inamaanisha kuwa mahali popote Neno la Mungu, linahubiriwa, au ibada inaendelea, iwe ya jumapili, au fupi ya maombi au mikesha, Rohoni mnakuwa mmechukuliwa mpaka mbingu ya Tatu (ndio ile gorofa ya tatu), juu sana mahali ambapo Mungu yupo na kiti chake cha enzi kilipo.

Na huko kuna Nuru nyingi, kama tulivyoona jinsi taa nyingi zilivyokuwa pale gorofani. Ikiwa na màana kuwa wakati unajaribu kuchagua kusogea mbali na uwepo wa Mungu utatambua kabisa mahali ulipo si salama..

Tabia ya kusinzia inakutuma ukae dirishani mwa uwepo wa Bwana na sio ukumbini. Ni kuonyesha jinsi gani usivyo “siriazi” na Mungu.

Na hatimaye unaanguka kutoka uweponi mwa Bwana..na kufa moja kwa moja kiroho.

Leo imekuwa ni desturi na mtu/watu wengi kila wafikapo nyumbani kwa Mungu ni lazima wasinzie, na wenyewe wanaona ni kawaida, wanadhani pale ni sawa na ofisini kwao, au shuleni kwao, ambapo hakuna jambo lolote la rohoni linalokuwa linaendelea.

Wanasahau kuwa wamepewa neema ya kupandishwa hadi kwenye kiti cha enzi cha Mungu, lakini wanakaa madirishani.

Ndugu ikiwa wewe ni mmojawapo wacha hii tabia, ukiindekeza utaanguka na kufa kabisa kiroho. Nimeona watu wengi wenye tabii hii, wakirudi nyuma ulimwenguni, wengine wakichuliwa na mawimbi ya ibilisi.

Kuwa siriazi na Mungu wako, tambua kilichokupeleka pale, unapoona wengine hawasinzii, haimaanishi kuwa hawahisi usingizi kama wewe, wanahisi lakini watalalaje mbele ya kiongozi wao mkuu? Wanaogopa kumvunjia heshima yake. Vilevile wanataka wapokee kikamilifu kile kilichowapeleka pale,

Hivyo kataa usingizi na wenyewe utakukimbia, na hiyo inakuja kwa kuzingatia kwa makini kile  kinachoendelea pale, mawazo yako yote yakiwa pale, ukijua kabisa kila siku ni mpya nyumbani kwa Bwana, na Mungu anatembea.

Lakini kama utaenda kwa desturi na mazoea, au kukamilisha ratiba, utakuwa ni mtu wa kulala lala na siku moja utakufa kabisa kiroho kwasababu uwepo wa Mungu umekwisha kukuacha. Mheshimu Mungu.

Bwana atasaidie sana.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MIMI NI ALFA NA OMEGA.

DHAMBI YA MAUTI

YESU ANA KIU NA WEWE.

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

Sikio lisikialo, na jicho lionalo, BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

Rudi nyumbani

Print this post

Tufanyaje ili tuonekane tunampenda Mungu?

SWALI: Naomba kufahamu kumpenda Mungu kukoje, Je tufanyeje ili tuonekane tunampenda?


JIBU: Tofauti na sisi tunavyotafsiri upendo, kwamba ni kuonyesha hisia zilizo nzuri kwa mwingine, Kwamfano kuhurumia, kujali, kuthamini, kuhudumia, kusifia, kujitoa n.k.

Lakini kwa Mungu ili tuonekane tunampenda yeye, ni zaidi ya kuonyesha hisia.. Kwani waweza kuwa na hisia nzuri kwa Mungu, mpaka ukatoa machozi, unapotafakari matendo yake makuu, Unapotazama wema wake na fadhili zake, na uumbaji wake wote, vikakufanya ujihisi kumpenda sana Mungu.

Lakini hili mbele za Mungu linaweza lisihesabike, kwasababu si kile Mungu anachotaka kukiona kwetu..

Hivyo ni vizuri kufahamu mambo haya makuu matatu (3), ambayo  ukifanya bidii kuyatenda, bila hata kuonyesha hisia Fulani kubwa,  Mungu atakuona unampenda sana, na matokeo yake atajidhihirisha kwako. Mambo yenyewe ni haya;

1). Zishike amri zake:

Amri zake ni pamoja na kukaa mbali na dhambi, halikadhalika, kupendana sisi kwa sisi.

Biblia inasema..

1Yohana 5:3 “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.

4 Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu”.

Umeona, Bado Bwana Yesu analirudia tena hilo hilo neno katika

Yohana 14:15 Mkinipenda, mtazishika amri zangu.

16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;

Na amri yake iliyo kuu aliyotupa, ni kupendana sisi kwa sisi, kama nafsi zetu (Yohana 13:34), na zaidi kuwapenda mpaka wale wanaotuchukia. Tukizingatia hayo mambo mawili, huku tukijilinda na dhambi, kwa maisha ya utakatifu, hiyo ni dalili ya kwanza inayofunua upendo wetu wa kweli kwa Mungu.

2) Uchukie ulimwengu:

Kuupenda ulimwengu kunakwenda kinyume na kumpenda Mungu, biblia inasema hivyo katika;

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

Ukisema unampenda Mungu, halafu, bado unapenda fashion, unapenda anasa, unapenda party party, na tafrija tafrija, mipira, muvi muvi kila wakati, miziki ya kidunia, kampani za wenye dhambi, vijiwe vijiwe visivyo na maana.

Basi ufahamu upendo kwa Mungu hautakaa uwepo ndani yako, Biblia inasema hivyo. Jitenge na mambo ya kiulimwengu kwa jinsi uwezavyo, tafuta ndugu katika Bwana ndio wawe watu wako wa karibu, biblia ndio iwe novel yako, nyimbo za sifa ndio ziwe mziki wako, kanisani ndio pawe kijiweni pako. Ukizingatia hayo kwa bidii, basi kidogo kidogo, upendo kwa Mungu usio wa kinafki utaingia ndani yako. Na Mungu atauona.

3) Husisha kila kitu chako chote kwa ajili ya Mungu:

Biblia inasema..

Marko 12:29 “Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;

30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote”.

Hapo hajasema, “mpende tu Bwana Mungu wako”, halafu basi, bali anasema utampenda kwa mambo yote manne, yaani roho, moyo, mwili na akili.

Mungu hataki kupendwa kwenye roho tu, bali hata kwenye akili zako, na nguvu zako. Ikiwa unafikiria Mungu anataka umtafute tu siku za ibada, umwabudu halafu basi, bado hujakamilisha kumpenda, bali anataka nguvu zako unazokwenda kuzisumbukia huko katika kutanga tanga kwako ziishie kwake, Mali zako, kujitoa kwako katika kuujenga ufalme wa Mungu, na kusambaza habari zake.

Vilevile akili yako yote uitumie kwake, ubuni utafiti ni kwa jinsi gani, unaweza kuifanya kazi ya Mungu iwe bora zaidi, kama vile unavyofikiri kila siku ni jinsi gani unavyoweza kuyafanya maisha yako kuwa bora kwake, sio tu kumwachia mtumishi Fulani,au mchungaji Fulani afanye yeye kila kitu, angali vingine vipo ndani ya uwezo wako wewe.

Kwa kuzingatia mambo hayo matatu, basi utakuwa umempenda Mungu, na yeye atalijua hilo, na matokeo yake ni kujidhihirisha kwako, na kukuhudumia. Huko ndio kumpenda Mungu.

Zaburi 91:14 “Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.

15 Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;

16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu”.

Bwana akubariki.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?

Rudi nyumbani

Print this post

Ila atapewa mara mia sasa,Ndugu wake(Marko 10:30)

SWALI: Mbona katika Marko 10:30 Bwana Yesu anasema tutapata mara mia ‘wake’? Hii si inatupa uthibitisho kuwa ndoa za mitara ni sawa?


JIBU: Tusome kwa ukaribu vifungu vyenyewe;

Marko 10:28 “ Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.
29 Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au
ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, NA NDUGU WAKE, na mama,
na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho; na wa mwisho watakuwa wa kwanza”.

Hapo hakuna mahali popote Bwana Yesu amesema tutapata mara mia ‘wake’, isipokuwa anasema tutapata mara mia  “ndugu wake”.  Akimaanisha ndugu wa KIKE, kama tu alivyosema ndugu WAUME, tutapata mara mia.

Maana yake ni kwamba mtu yeyote anayeingia gharama ya kumfuata Yesu kwa moyo wake wote, na kwa ajili ya injili yake, Bwana ameahidi kumrudishia kila kitu alichokipoteza mara100 zaidi.

Ikiwa aliwaacha dada  zake kumi(10), basi Bwana atamrudishia ndugu wadada mara mia zaidi.. yaani ndugu wadada elfu moja (1000), watakuja kuwa karibu naye.. wenye upendo kama tu ule wa wale wa kwanza   kwake.

Lakini tuseme, labda tuliacha wake zetu kwa ajili ya injili, Je! Mungu hataturudishia thawabu mara mia kwa kuwaacha wao?

Jibu ni kwamba ataturudishia pia mara mia, lakini haimaanishi kuwa tutapewa ‘wake’ tuwaoe, hapana, bali tutapewa ndugu, wenye Usaidizi kama tu wa wake.. Kumbuka, mwanamke aliumbwa kuwa msaidizi wa Adamu, hakuumbwa kuwa chombo cha starehe..

Hivyo hudumu aliyoitiwa mke duniani ni kuwa msaidizi.. Vivyo hivyo Mungu atakunyanyulia ndugu ambao watasimama kama wasaidizi kwako katika huduma, mara mia, kama wake.

Lakini haimaanishi utawaoa, hapana, kama itakavyokuwa kwa ndugu mara mia atakaokupa, hawataingia kwenye tumbo la mama yako na kuzaliwa ili wawe ndugu yako, bali watatoka nje, na kusimama kama ndugu.. Vivyo hivyo na kwa watoto na mambo mengine yote.

Lakini kwanini iwe hivyo? Ni ili kulitimiza lile neno la Bwana Yesu alilosema..

 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake
kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha”.(Luka 9.24)

Bwana akubariki.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TWEKA MPAKA VILINDINI.

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000

MADHARA YA KUTOIJUA KWELI YOTE!

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUISHINDA DHAMBI INAYONITESA.

SWALI: Shalom. Naomba kufahamu nifanye nini ili niweze kuishinda ile dhambi inayonitesa.?


JIBU: Dhambi inayomtesa mtu kwa jina lingine inaitwa “dhambi izingayo kwa upesi”, ambayo tunaisoma katika;

Waebrania 12:1

[1]Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

Si kila dhambi, huwa inaondoka kirahisi ndani ya mtu pindi anapookoka..

Ni kweli asilimia kubwa ya dhambi mtu anajaliwa na Roho Mtakatifu kuziacha wakati ule anapotubu, na kudhamiria kumfuata Yesu kwa moyo wake wote, kwamfano mwingine alikuwa ni mwizi, mwongo, mshirikina, mzinzi n.k.

Lakini alipookoka hivi vyote akaviacha kiwepesi kabisa..Lakini ndani yake kukawa na shinikizo kubwa la kuendelea kufanya punyeto, au mawazo machafu kumtawala..hivyo hiyo hali ikawa inamtesa  kwa kipindi kirefu na kumfanya akose raha, wakati mwingine amejaribu kuomba sana lakini hali ipo vilevile.

Mwingine hayo yote ameweza  kuyashinda lakini dhambi ya usengenyaji imekuwa ni mzigo mzito sana kwake kuutua, mwingine ulevi, mwingine kutazama picha za ngono n.k.

Ndugu ikiwa umeokoka na unaona hiyo dhambi ni kikwazo kikubwa  kwako, nataka nikuambie huna budi kushindana nayo hadi uishinde..kwasababu usipoishinda itakupeleka jehanamu.

Kaini alikuwa na dhambi ya hasira na wivu, akaipuuzia, lakini  Mungu akamwambia, unapaswa uishinde

Mwanzo 4:6-7

[6]BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?

[7]Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

Dhambi kama hizi huwa zilishatia mizizi mrefu ndani ya mtu tofauti na nyingine, hivyo kuziondoa inahitaji nguvu ya zaida..

Na njia pekee ya kuzishinda hizi ni moja tu nayo ni “kwa Kuua vichocheo vyote vinavyokupelea kuitenda dhambi hiyo”..

Mithali 26:20 Inasema;

“Moto hufa kwa kukosa kuni;..”

Moto hauwezi kuendelea muda mrefu mahali ambapo hapana kichocheo chake kama kuni au mafuta..haijalishi utakuwa na nguvu kiasi gani, mwishowe utazima tu.

Hakuna dhambi yoyote iliyo ngumu kuishinda hapa duniani endapo vichocheo vyake vitauliwa kikamilifu.

Kwa mfano kufahamu ni jinsi gani utaweza kuishinda dhambi ya uzinzi fungua hapa..>>> MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

Kwa siku za mwanzo, utaona ni shida lakini kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda Mungu anakutia nguvu na hatimaye inakuwa ni dhambi nyepesi sana kuishinda kuliko hata zote…

Ni kawaida hata gari lililo katika mwendo kasi likichuna breki kwa ghafla, haliwezi kusimama hapo hapo…litasogea mbele kidogo, ndipo litulie japokuwa tairi tayari zilishaacha kuzunguka, kitambo kidogo.

Vivyo hivyo na wewe katika hiyo dhambi inayokuzinga kwa upesi, inayokufanya usipige mbio kwa wepesi, katika safari yako ya ukristo, kwa siku za mwanzoni itaonyesha  kama kuleta ukinzani lakini kwa jinsi unavyokaa mbali na vichocheo vyake hatimaye itakufa tu ndani yako…ni kitendo cha muda.

Kwamfano kama wewe ni mvuta sigara, kiu ya kuvuta ikija, ondoka mazingira ya upatikanaji wake, vilevile wale marafiki uliokuwa unavuta nao jitenge nao waone kama kaburi, hicho kiu kitakutesa tu kwa muda mfupi, lakini uking’ang’ana utakuja kushangaa kimetoweka tu ghafla..hapo ndio tayari kimekufa..

Shindana, hadi ushinde…usikubali kusema mimi nimeshindwa kuacha hiki au kile, usikubali hiyo hali, usiwe mnyonge wa dhambi, kwasababu wanyonge wote hawataurithi uzima wa milele biblia inasema hivyo katika Ufunuo 21:27

Ikiwa ni fashion, wewe kama mwanamke ni lazima uishinde, ikiwa ni kamari, ikiwa ni miziki ya kidunia kanuni ni hiyo hiyo…Ua vichocheo vyote. Kaa mbali nayo, ulizoea kutazama picha za ngono mitandaoni, na ulipookoka mawazo yale yanajirudia rudia kwenye fahamu zako, endelea kukaa mbali na vichocheo hivyo, acha mazungumzo mabaya, left magroup yasiyokuwa na msingi kwako, epuka kutazama au kusikiliza kitu chochote chenye maudhui ya uzinzi, marafiki wazinzi waepuke, marafiki wasiokuwa na maana wa jinsi tofauti wapeuke, utafika wakati hayo mawazo machafu yatakukimbia..

Zingatia hayo, na matokeo utayaona.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

CHUKIZO LA UHARIBIFU.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi nyumbani

Print this post