Category Archive Uncategorized @sw-tz

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

Kwa tafsiri za kidunia mtu asiye na akili ni mtu ambaye hawezi kufiriki, kuelewa, kuwasiliana, kupanga au kutatua matatizo. Hivyo, mwanadamu mwenye mtindio wa ubongo, anajulikana kama hana akili, mtu anayefeli darasani, anajulikana kama hana akili, mtu anayeshindwa na wenzake katika maisha anajulikana pia kama asiye na akili.

Lakini je! Biblia nayo inasemaje kuhusiana na mtu asiye na akili. Sifa zake ni zipi.

Zifuatazo ndizo sifa za mtu asiye na akili mbele za Mungu, ikiwa wewe unayo mojawapo au zote, basi fahamu huna akili, haijalishi utakuwa ni wa kwanza, kimaisha, au kielimu, au kicheo. Mungu anakuona unao mtindio wa ubongo, hujakamilika. Na matokeo yake utashindwa kutumia akili zako zote kumpenda yeye kama alivyotupa maagizo katika ‘Mathayo 22:37’

1) Kutomtafuta Mungu:

Zaburi 14:2 “Toka mbinguni Bwana aliwachungulia wanadamu, Aone kama yuko mtu mwenye akili, Amtafutaye Mungu. 3 Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja, Hakuna atendaye mema, La! Hata mmoja”.

Ukishaona Mungu hana umuhimu kwako, ni uthibitisho tosha,akili zako zimepunguka kwa kiasi kikubwa mno. Ni sawa, na mbwa asiyemjua bwana wake anayemfuga siku zote. Au mtoto asiyemtambua mama yake amnyonyeshaye kila siku. Fanya bidii kumtafuta Muumba wako, kwasababu hilo ndio jaribio la kwanza alilotuumbia Mungu, ili kuthibitisha kwamba kweli sisi ni wanadamu tuliokamilika, tunaweza kumtafuta aliyetubuni.?

2) Kuwadharau wengine:

Mithali 11:12 “Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza”.

Ukishajiona wewe ni bora kuliko mtu mwingine, au unamwona mwenzako hana lolote jipya la kukufaa wewe, tambua kuwa tayari akili yako imeathirika, fanya haraka sana, kujirekebisha katika eneo hilo, ili usipoteze upeo wako wa kufikiri vema, na wa kupambanua mambo. Kamwe usimdharau mtu yeyote duniani. Hata kama ni mpumbavu wa mwisho.. Kwasababu Mungu naye hamdharau mtu aliyemuumba  japokuwa ni mnyonge (Ayubu 36:5)

3) Kuwaonea watu:

Mithali 28:16 “Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana; Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake”.

Kumuonea mtu kwasababu ya unyonge wake, au udhaifu wake, ni jambo la hatari sana. Ukimdhulumu mwenzako, au kumnyima haki yake, au kutumia hila kumwibia kisa tu hana maarifa ya jambo hilo, kumpiga mkeo, au watoto bila sababu, basi fahamu kuwa wewe ni sawa ni mjinga mbele za Mungu.. Tukae mbali na uonevu wa aina yoyote.

4) Kufanya uasherati:

Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.

Uzinzi, ni kipingamizi sio tu cha kiroho, bali pia cha kiakili. Watu wazinzi, wanajiharibia sana uwezo wao wa kupambanua mambo ya kiroho kwa sehemu kubwa sana. Kwasababu Roho Mtakatifu huwa anategemea miili yetu kutenda kazi, hivyo mwili wako unapochafuliwa, hawezi kupata nafasi ya kuwa mwalimu wako. Ndio hapo Unabaki tu kuwa wewe kama wewe, kama mnyama tu. Epuka uzinzi kwa gharama zote, ni hatari..

5) Kutokuwaza  juu ya hukumu:

Mithali 15:24 “Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini”.

Hapo biblia inatueleza wazi, mtu mwenye akili, huwaza ni jinsi gani atakavyoepukana na kuzimu iliyo chini, huwaza kwenda mbinguni, huwaza kuepukana na ziwa la moto. Lakini kinyume chake ni kweli, mtu asiyewaza hatma ya maisha yake baada ya kufa itakuwaje, badala yake yupo tu, anachowaza ni ajengeje magorofa hapa duniani, ukimweleza habari za kuzimu hata hashtuki, huyo kwa Bwana hana akili.

6) Kutopenda maagizo:

Mithali 10:8 “Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka”

Ukiwa ni mtu wa kupinga maagizo mema, unayopewa, bali unajiona upo sawa machoni pako mwenyewe, ukielezwa, uvaaji vimini ni dhambi, unasema hatupo agano la kale, unapoelezwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ni lazima, unasema sisi hatuamini hilo. Ujue kuwa unajiangamiza mwenyewe. Kila agizo lililo kwenye Neno la Mungu linapaswa lipokelewe na kukubaliwa kama lilivyo pasipo kuuliza uliza.

7) Kusahau sahau, sheria za Mungu:

Mithali 10:14 “Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa; Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu”.

Ukiwa mtu wa kutozingatia, au kutotendea kazi kile unachoambiwa au kukisikia, kuhusiana na mafundisho ya adili, yaani unasahau sahau, amri au fadhili za Mungu, unakuwa mwepesi kuanguka ovyo katika dhambi, ni uthibitisho kuwa huna akili kwa mujibu wa kibiblia. Tunapaswa tuwe watu wa kuzitafakari sheria za Mungu wakati wote, kama vile mwanafunzi akaririvyo kila siku masomo yake, ili yamsaidie kufaulu mitihani yake ya mwisho.

Mithali 3:3 “Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.

4 Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu”.

8) Uvivu:

Mithali 24:30 “Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.

31 Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake”.

Ukiwa mvivu, wa kufanya kazi ya Mungu.  Bwana anasema huna akili, yaani Ikiwa hujishughulishi na chochote, unajitafutia matitizo yako mwenyewe. Tumeumbwa, tujishughulishe, kama Mungu alivyojishughulisha..Kama huwezi mtumikia Bwana kwa kujitoa kwa asilimia zote kwenye kazi yake, ni lazima ufanye kazi ya mikono, ili ufanikiwe. Lakini tukishindwa kujishughulisha, ni kwa hasara yetu wenyewe.

Hivyo tukiwa tuna mojawapo ya tabia hizo ni busara tukazidhibiti ndani yetu. Ili tuweze kuishi kwa akili Bwana anazotaka tuwe nazo.  

Zingatia: Mungu anazungumza na mtu mwenye akili timamu, rohoni. Ni lazima tufikie hapo ili Bwana aseme na sisi.

Bwana atusaidie.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?

Watu wenye ulemavu wa akili, wataenda mbinguni?

Nini maana ya ‘Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma’?

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

NI NINI BWANA ANATAZAMIA KILA TUNAPOSHIRIKI MEZA YAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

Wajibu wa wanandoa ni upi?

Mume: Kumpenda mke wake Kama mwili wake mwenyewe, ( Waefeso 5:25):  Ikiwemo kumuhudumia kiafya, kimavazi, kimalazi, na kiroho.

Mke: Kumtii Mume wake: Kumsikiliza, kumuheshimu, kukubali kuongozwa. (Waefeso 5:22).

Wote: Haki ya ndoa. (1Wakorintho 7:5)

Lakini ikitokea mmoja, ameshindwa kusimama katika nafasi yake, labda tuseme, mume hamjali mkewe, anampiga, anatoka nje ya ndoa, anamtukana, hamtimizii majukumu yake ya kimwili na watoto wake. Afanyaje?

Au mke hamweshimu mume wake, anamdharau, anafanya ukahaba, anamzungumzia vibaya kwa watu wa nje, anajiamulia mambo yake mwenyewe pasipo kumshirikisha mumewe..afanyaje?

Je! na yeye aache kutimiza wajibu wake?

Jibu ni hapana:  Embu wazia hili jambo; Ulishawahi kuishi katika nyumba ya kupanga, ambapo mnajikuta wapangaji mpo 10 mnashea umeme au maji, na kila mwisho wa mwezi bili inakuja, na mnapaswa muigawanye sawa sawa kwa kila mmoja wenu.  Kwa kawaida hapo panakuwa na ukinzani mkubwa, kwasababu wapo wengine watasema, mimi sina matumizi mengi kama ya Yule.. Na hiyo inapelekea mwingine kujiongezea  matumizi yake kwa makusudi ilimradi tu afanane na wale wengine, labda atufungulia bomba la maji ili yamwagike, ili mwisho wa mwezi utakapofika alipe sawasawa na matumizi ya wale wengine.

Lakini hajui kuwa anajiumiza yeye mwenyewe na wale wenzake, kwasababu anapoongeza matumizi ndipo gharama inapokuja juu zaidi, atalipa zaidi ya mwanzo. Ni heri angebakia vilevile akubali kuumia yeye, ili wote wapone.

Ndivyo ilivyo katika ndoa ikiwa mmoja hatimizi wajibu wake wa kindoa, suluhisho sio mwingine kujibu mapigo, bali ni kuendelea hivyo hivyo katika nafasi yake.  Ili kuinusuru ndoa. Kama mwanaume hakupendi, wewe mtii, mweshimu, msikilize, kama mwanamke hakutii, wewe mpende, mpe haki yake, ..

Na faida yake ni ipi?

  1. 1) Utamgeuza mwenzako:

Biblia inasema; .. 1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu”.

Inaendelea kusema;

1Wakorintho 7:16 “Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?

 Haijalishi itachukua miaka mingapi. Kuwa mvumilivu, timizia wajibu kwao. Hayo mengine mwachie Mungu.

  • ) Utampalia makaa ya moto kichwani:

Mithali 25:21 “Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa; 22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na Bwana atakupa thawabu.

Hili andiko linaingia pia kwa wanandoa. Wakati unaona kama wewe unaonewa, hujui kuwa Yule mwingine anateswa rohoni  anapoona hurudishi mapigo, hilo jambo linakuwa ni moto mkubwa ndani yake, na sikumoja tu, atakuja kwa machozi, na kutubu mbele zako. Ni kitendo cha muda.

  • 3) Utampa Mungu nafasi ya kulipiza kisasi yeye mwenyewe:

Unapoumizwa, usidhani kuwa Mungu haoni, lakini unapomwachia Mungu yote, basi yeye peke yake ndiye atakayeshughulika kutafuta njia ya kutatua hilo tatizo. Kiboko cha Mungu kitapita, kitamnyoosha. Hivyo unapaswa uwe mtulivu, simama katika nafasi yako. Bwana atamtengeneza yeye mweyewe.. au atatengeneza njia kwa namna nyingine. Hivyo dumu katika utakatifu.

Warumi 12:17 “Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.

18 Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.

19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana”.

Zingatia hayo, usirejeshe ubaya kwa mwanandoa mwanzako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

MJUE SANA YESU KRISTO.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

VIJANA NA MAHUSIANO.

Kwanini Bwana Yesu alie machozi, na ilihali yeye ni Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

FAMILIA TAKATIFU: Marimu na Yusufu.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WANA-NDOA; FAMILIA TAKATIFU: Marimu na Yusufu.


Karibu katika mwendelezo ya  Masomo ya wanandoa . Ikiwa wewe ni mwanandoa au unajiandaa kuingia katika ndoa, basi masomo haya ni muhimu sana kwako kuyajua.

Tulishatazama, huko nyuma jinsi ndoa ya kwanza ya wazazi wetu Adamu na Hawa ilivyokuwa, na changamoto walizokutana nazo, na jinsi walivyoweza kukabiliana nazo. Ikiwa hukupata masomo hayo, basi utatumia ujumbe inbox tukutumie.

Leo tutatazama familia nyingine takatifu. Ambayo ni ya Yusufu na Mariamu. Yapo mambo mengi sana ya kujifunza, juu ya wanandoa hawa, Na ndio maana kwanini Mungu alikusudia  mwokozi wa ulimwengu aje kwa kupitia watu hawa,  Ni Kwasababu kuna  mengi ya kujifunza kwao.  Tutaona pia utaratibu Mungu aliowawekea katika kutimiza kusudi lake hapa duniani.

1) Tukianzana na Yusufu.

Alikuwa ni mtu aliyeepuka madhara kwa wengine:  Yusufu hakuwa kama Samsoni, ambaye alipoona mwanamke aliyemchumbia amepewa rafiki yake, akakasirika, na kwenda kuchukua mbweha mia tatu, na kuwapeleka kwenye shamba la ngano la wafilisti, kuyateketeza ili ajilipizie kisasi (Waamuzi 15:1-20).

Lakini Yusufu hakuwa hivyo, yeye alipoona binti aliyemchumbua ana mimba, alitafuta njia ya kuepusha madhara kwa dada huyo, hivyo akakusudia ‘’kutomuabisha’’. Akapanga mipango yake ya kumuacha kwa siri,..huenda alipoulizwa vipi mbona humwoi msichana huyu, akawa anasema bado sijafikia muafaka, nitawapa majibu.

Mathayo 1:18 “Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

19 Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri”.

Sasa Ikiwa alikuwa na hofu ya kumwaibisha asipigwe mawe, unatazamia vipi mtu kama huyu, angeweza kumpiga mke wake hata baada ya ndoa , au awe anatoa siri za madhaifu ya mke wake kwa watu wa nje?

Mwanamke anapoteleza, sio lazima wakati wote upeleke taarifa kwa jamii, aaibike au umpige, au umfukuze, bali ni kumvumilia, kwasababu mengine yanatokea kwa sababu ambazo utakuja kuzijua mbeleni. Tabia hii alikuwa nayo Baba-wa-Yesu (kimwili)

2) Mariamu:

Alikuwa ni bikira:  Ni binti ambaye alijitunza tangu anazaliwa mpaka anakuwa mwanamke, Na hiyo ikapelekea kupata neema ya kuchumbiwa na mzao wa Daudi (Yusufu). Kumbuka ahadi ya kuzaliwa Kristo haikuwa kwa Mariamu, bali ilikuwa kwa uzao wa Daudi. Hivyo Mungu alipomuona Mariamu, na ukamilifu wake katika mwili ndipo akasema huyu anafaa kupata neema ya kukutana na Yusufu atimize kusudi la Mungu.

Maana yake ni nini, upo umuhimu sana, wa msichana kujitunza sana mwili wake, kwani hiyo itakupelekea kupata mwanaume bora, na uzao bora. Ni kweli si wote wataingia katika ndoa wakiwa bikira, lakini ikiwa umetambua sasa, wajibu wako, na umeokoka, huna budi kujitunza sana, na hata baada ya ndoa, ili hicho kitakachotoka tumboni mwako kiwe kitakatifu.

SASA BAADA YA KUONA SIFA HIZI KUU (2), WALIZOKUWA NAZO HAWA WANANDOA, TUONE UTARATIBU WA KIMAJUKUMU JINSI MUNGU ALIVYOUGAWANYA KWAO.

Malaika Gabrieli alitumwa kwa Mariamu, ili kumpa taarifa ya kupata mimba kwa uweza wa Roho na kwamba mtoto huyo ataitwa Yesu.

Lakini baada ya hapo, Mungu hakuendelea tena kusema na Mariamu moja kwa moja. Bali alimgeukia mumewe Yusufu, na kumwagiza kuwa atakapozaliwa amwite  jina lake YESU.

Mathayo 1:20 “Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao”.

Na utaona baada hapo, wakiwa kule Bethelehemu, bado Malaika anamtokea Yusufu tu, na kumwambia, mchukue mtoto na mama yake, wapeleke Misri, kwasababu Herode anataka kumuua mtoto.(Mathayo 2:13-14)

Tengeneza picha Mariamu angekuwa ni mwanamke kiburi, angesema, mbona Mungu hajasema na mimi kuhusiana na hilo?, Kwanza si wewe uliyembeba masihi, mateso huyajui, huko Misri ni nani unayemjua, nangojea Mungu anithibitishie kwanza mimi..lakini hakuwa hivyo alikubali kutii, bila kujadili jadili.

Bado utaona, akiwa kule Misri, malaika anamtokea tena Yusufu peke yake na kumwambia, mchukue mke na mtoto urudi nao Israeli kwasababu Herode amekufa. Safari tena ya mihangaiko ikaanza, huku Mariamu akisikiliza maagizo ya mumewe na kutii (Mathayo 2:19-20).. Lakini wakiwa pale Bethelehemu,  wametulia ili sasa waanze maisha, saa hiyo hiyo, Yusufu anamwambia mke wake, tuondoke hapa tuende tena Nazareti, Mungu ameniagiza hivyo (Mathayo 2:22-23).

Mariamu hakuwa na kigugumizi kumsikiliza mume wake, hakuwa na kazi nyingine yoyote zaidi  ya kupokea maagizo ya uongozi kuhusu familia au mtoto kutoka kwa mumewe.

Hii ni kufundisha nini?

Kwa mwanamke: Tambua kuwa mume ndio kichwa cha familia, Mungu atamtumia yeye, kuyalinda na kuyatamia maono yako, huwezi kufanikiwa bila yeye. Haijalishi Mungu kakuonyesha mambo makubwa kiasi gani hapo mwanzoni. Ikiwa humtii mume wako, ujue kuwa unajiharibia wewe mwenyewe. Utiifu ni muhimu sana, hata wakati ambapo unaona sehemu unapopelekwa sio pa kuvutia.

Ndio maana unawajibu sana wa kumwombea mume wako, ikiwa ni mwenye dhambi, Mungu ambadilishe. Kwasababu yeye ndio usalama wa maono yako.

Kwa mwanaume: Umewekwa kama kichwa, ni lazima utambue kulinda maono mema ya mkeo, Si kila taarifa nzuri itakufikia wewe wa kwanza, Wakati mwingine inaanzia kwa mwanamke, kama ilivyokuwa kwa Mariamu, kisha wewe baadaye, hivyo uonapo hivyo, usipige vita, bali, sikiliza, tafakari, pia tendea kazi, Hapo ndipo Mungu atakapokutumia, kuijenga familia bora. Wewe kama mlinzi huna budi, kutimiza wajibu wako,wa kumtunza mkeo na kumpenda kama maandiko yanavyosema. Jambo lolote linaloihatarisha familia yako, shughulika nalo kwelikweli usimwachie mwanamke alitende.

Hivyo kwa kuzingatia mambo hayo,  Ndoa zetu zitakuwa bora, mfano wa ile ya Yusufu na Marimu. Na Bwana atatupa zawadi ya kuzaa vitakatifu kama Ilivyokuwa kwa Yesu na wadogo zake wote. Tambua wajibu wako, simama katika nafasi yako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.

KUWA RAFIKI WA DUNIA NI KUWA ADUI WA MUNGU.

VIJANA NA MAHUSIANO.

USIOGOPE KUMWADHIBU MWANAO.

Rudi nyumbani

Print this post

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

SWALI: Biblia inaposema “Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake”, ina maana gani?

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.


JIBU: Ili kuelewa neno hilo, wazia mfano huu; Mtu mmoja ameshitakiwa na mahakama kwa kosa la uchafuzi wa mazingira, hivyo, akapewa adhabu ya kulipa faini ya sh. Milioni 5 ndani ya wiki 3, au jela miaka 3. Sasa ikatokea mtu huyu akawa hana cha kulipa,.. Unadhani atakuwa katika hali gani? Ni wazi kuwa atapoteza amani yote, hawezi kuwa katika furaha, hawezi kuwa katika raha wakati wote huo kwasababu anajua hukumu ya kifungo ipo mbele.. Ili amani yake irudi, hana budi apate kiwango hicho alipe. Lakini akatokea mtu, akasema mimi nitakuchukua adhabu hiyo nitamlipia deni lake. Bila shaka furaha na amani ya yule mdaiwa itarejea tena.

Hivyo tunaweza kusema, ili kuirejesha ile amani yake ya mwanzo, alikuwa hana budi kutumikia adhabu kwanza..

Sasa tukirudi katika huo mstari ..biblia inaposema;

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Huyo ni Bwana Yesu anayezungumziwa hapo, sasa anaposema, Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”. Ni kwamba ili sisi kuipokea Amani yetu, tuliyoipoteza tangu kule edeni, ilitupasa kwanza tutumikie adhabu ya makosa.. Lakini ashukuruwe Kristo kwasababu alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, akapigwa na kuteswa ili sisi tupone. Adhabu ya amani yetu aliichukua yeye.

Na ndio maana Warumi 8:1 inasema; “Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu”.

Ukiwa ndani yake, amani yako inarejeshwa bila kulipa gharama yoyote. Lakini inastaajabisha kuona bado wapo watu hawataki kulipiwa deni zao. Wakidhani kuwa wataweza kustahimili hukumu ya Mungu siku ile. Ndugu ikiwa upo nje ya Kristo huna tumaini lolote. Ukifa ni moja kwa moja jehanamu kwenye ziwa la moto. Adhabu yako ni Mauti katika lile ziwa la moto milele.

Hiyo ndio sababu kwanini unamuhitaji Yesu Kristo leo, kwasababu ukishakufa leo hakuna tumaini, wala huna matendo yoyote ya kumshawishi Mungu, afute dhambi zako. Wasubiri nini, usimgeukie Bwana Yesu akusafishe Maisha yako angali ukiwa hai? Tubu sasa mpokee yeye. Muda ni mchache.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

Rudi nyumbani

Print this post

Nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.

SWALI: Naomba kufahamu maudhui ya mstari huu,

1Timotheo 1:20 “Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu”.


JIBU: Awali ya yote, kabla ya kufahamu ni kwanini Mtume Paulo anatoa hukumu kali kama hiyo tuangalie mistari ya juu yake ambayo inaeleza sifa, za hao watu.

Ukisoma mstari wa 19, Paulo anamuasa Timotheo, awe ni mtu mwenye Imani, lakini sio Imani tu, bali pia “dhamiri njema”.. Ni vitu vinavyokwenda sambamba.

1Timotheo 1:19 “uwe mwenye imani na dhamiri njema, ambayo wengine wameisukumia mbali, wakaangamia kwa habari ya Imani.

20 Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.”

Dhamiri ni kile kitu cha ndani kinachomshuhudia mtu kwamba anachokifanya ni sahihi au sio sahihi. Hivyo pale mtu anapokuwa na dhamiri njema, maana yake ni kuwa, anaitii nafsi yake, inapofanya kosa, pale inaposuta, anakuwa tayari kugeuka. Hivyo mtu kama huyu huwa anaishi kwa kujichunga, na kuwahurumia na kwa kuogopa hukumu pale anapojaribu kuwapotosha watu.. Kwasababu dhamiri yake njema inamshitaki.

Lakini mtu ambaye hana dhamiri njema, ni kwamba, hata anapoona jambo Fulani alifanyalo ni baya, anastahili hukumu, yeye hajali, bali anafanya atakalo, kwa maslahi yake. Atakuwa tayari kuwafundisha watu mafundisho potofu kwa makusudi kabisa akijua kabisa alifanyalo ni upotevu, lakini yeye ataendelea kufanya, kwa furaha kabisa..

Sasa ndio hapo mtume Paulo, anawatolea mfano watu hao, waliokosa dhamiri njema. Ambao ni Himenayo, na Iskanda. Watu hawa walikuwa ni wabaya, kwasababu walikuwa wanapindua Imani za watu kwa makusudi, wala sio kwa bahati mbaya wakiwafundisha kinyume na mafundisho ya mitume,.

Kwamfano huyu Himenayo, tunasoma tena, Paulo akieleza mafundisho yake potofu, ya kuwaambia watu Ufufuo wa wafu tayari umeshatokea.. Hivyo watu wengi wakaiacha Imani na kumgeukia yeye.

2Timotheo 2:16 “Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu,

17 na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,

18 walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha”.

Na mwezake Iskanda, ambaye wengi wanaamini ndio huyu aliyezungumziwa katika vifungu hivi; Ambaye alimpinga sana Paulo katika kazi zake za kihuduma.

2Timotheo 4:14 “Iskanda, mfua shaba, alionyesha ubaya mwingi kwangu; Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake.

15 Nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu”.

Hivyo, makundi haya, Mtume Paulo hakushughulika nayo kabisa, bali kwa mamlaka aliyopewa, aliwaacha mikoni mwa shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.  Maana yake ni kuwa, ulinzi wa Mungu uliondolewa juu yao, ili shetani apate nafasi ya kuwashughulikia, ili yamkini watubu.

Aidha walikumbwa na magonjwa, au mapigo, au hata vifo hatujui.. Lakini kuwekwa mikoni mwa shetani, adhabu kali kama hizo utakumbana nazo.(Tunaona kwa ayubu pale  alivyoondolewa wigo wa ulinzi na Mungu, jinsi majangwa makali yalivyompata)..Ndivyo ilivyokuwa kwa hawa wakina Himenayo na mwenzake.

Hii ni kutufundisha  nini?

Yapo mamlaka ambayo Watakatifu wamepewa, kwa watu ambao wanauchezea ukristo, Ikiwa unafanya dhambi kwa makusudi, angali unaujua ukweli, na upo ndani ya mwili wa Kristo, kuwa makini sana, kwasababu hukumu yoyote itakayotolewa juu yako na wao lazima ikupate.. Na kama utakuwa unafanya kwa siri, kanisa halitajua, lakini Mungu atajua.. Na yeye mwenyewe atakuweka mikononi mwa ibilisi, upigwe. Ukishafikia hatua hii, waweza hata poteza Maisha yako.

Soma;

1Wakorintho 5:1 “Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.

2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo.

3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo.

4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu;

5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu”.

Bwana atupe Imani ya kweli na dhamiri safi.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

DHAMBI YA MAUTI

Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

MAZUNGUMZO MABAYA HUHARIBU TABIA NJEMA.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

Gumegume ni nini? (Isaya 50:7)

Rudi nyumbani

Print this post

Azidishaye mali yake kwa riba, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.

SWALI: Nini maana ya huu mstari; 

Mithali 28:8 “Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.


JIBU: Huyo anayezungumziwa azidishiye mali zake kwa riba na faida ni mtu ajipatiaye mali kwa njia zisizo za haki, kuwadhulumu wanyonge.

Kwamfano katika biblia Mungu aliwaangiza wana wa Israeli, wasiwatoze riba maskini, pindi wawakopeshapo, na pia wasichukue faida kutoka kwa ndugu zao, isipokuwa kwa wageni tu.

Kutoka 22:25

“Ukimkopesha mtu aliye maskini, katika watu wangu walio pamoja nawe; usiwe kwake mfano wa mwenye kumdai; wala hutamwandikia faida”.

Soma pia, Walawi 25: 35-37, kumb 23

Hivyo kulikuwa na kundi kubwa la matajiri walioihasi hii sheria ya Mungu, wakawa wanawatoza riba na kujipatia faida isivyo haki, Matokeo yake Wakafanikiwa kujikusanyia mali nyingi kama mavumbi ya ardhini.

(Ayubu 27: 13-16 ) 

Lakini bado maandiko, yanatoa matokeo au hatma ya watu kama hawa. Mwisho wa siku Mungu anawapokonya na kuligawia kundi lingine la watu lenye kuwahurumia maskini.

Utajiuliza inawezekanikaje..biblia inasema mali ina mbawa, inaweza kupaa ghafla, au ikatumiwa kwa matumizi yasiyo ya muhimu ikapukutika yote, au wewe ukafa ukamwachia mwingine. Lakini kule inapoelekea, sio popote tu ilimradi, hapana,  bali ni kwa mtu yule ambaye anawahurumia maskini.

Ndio Mungu anaweza kufanya hivyo..usipoitumia talanta yako vema. Anasema mnyanganyeni yule mwenye moja mkampe yule mwenye 10 (Mathayo 25:28),.Bwana anaweza kukunyang’anya ulichonacho. 

Hii inatufunza nini? 

Tukiwa watu wa kutenda haki na kuwahurumia maskini, kwa kuwapa vitu, basi tujue kuwa tayari kuna watu wameshaandaliwa kwa ajili ya kutuletea  hazina hizo, na watu wenyewe ndio hao waovu, wanaojilimbikizia mabilioni ya pesa katika akaunti zao za benki kwa dhuluma, na hila, na biashara haramu, na sio kwa njia halali.

Hii ni kuonyesha kuwa watu wanaopenda kuwapa wengine vitu, wanayo hazina kubwa sana hapa dunia.

Bwana atusaidie kuzifahamu hekima hizi tupende kuwasaidia watu wanyonge.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Kiburi cha Uzima ni nini? (1Yohana 2:16)

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

UBATILI.

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

SHINA LA UCHUNGU, LISICHIPUKE NDANI YETU.

DORKASI AITWAYE PAA.

Rudi nyumbani

Print this post

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

Bwana Yesu asifiwe, karibu tena tujifunze maneno ya uzima. Leo nataka tuone jambo ambalo, wengi wetu tuliookoka hatulifahamu kuhusiana na tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Ili tuelewe vema kiini cha somo, naomba tusome hivi vifungu vitatu, kwa umakini sana;

Marko 2:1
Akaingia Kapernaumu tena, baada ya siku kadha wa kadha, ikasikiwa ya kwamba yumo nyumbani.

Mathayo 13:1 “Siku ile Yesu akatoka nyumbani, akaketi kando ya bahari.

2 Wakamkusanyikia makutano mengi, hata akapanda chomboni, akaketi; na ule mkutano wote wakasimama pwani”.

Mathayo 14:13 “Naye Yesu aliposikia; hayo, aliondoka huko katika chombo, akaenda mahali pasipo watu, faraghani. Na makutano waliposikia, walimfuata kwa miguu kutoka mijini mwao.

14 Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao”.

Kama tunavyosoma hapo, kuna wakati Bwana Yesu alikaa nyumbani kwake, mahali ambapo panajulikana, kwamfano kama mtu angemuulizia angeambiwa anakaa pale kwenye kaya ile namba Fulani..Utamkuta ameketi  kwenye kochi lake, sebuleni kwake, au yupo jikoni kwake anajipikia chai, atakukaribisha na mtazungumza mengi tu.

Soma,

Yohana 1:37 “Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.

38 Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?

39 Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi”.

Lakini upo wakati aliondoka hapo, akaenda katika mazingira ambayo yana watu, lakini hayana nyumba ndio hapo unamwona anatoka nyumbani kwake anakwenda kuketi kando ya bahari.. Sasa kumpata hapa, si kurahisi kama ilivyokuwa nyumbani, Leo hii ni rahisi mtu kukwambia tuonane hoteli Fulani, au nyumba Fulani, kuliko kukwambia tuonane fukweni, wavuvi walipo. Ni ngumu kwasababu hakuna ofisi au makazi pale.

Lakini kama hiyo haitoshi, aliondoka tena huko fukweni ambapo alikuwa anakwenda mara kwa mara kuwafundisha watu, akakaa sehemu isiyokuwa na watu kabisa, maana yake nyikani/ jangwani. Huku ndiko kubaya kabisa, kwasababu hakuna upatikanaji wa mahitaji yoyote ya kijamii. Hakuna maji wala chakula, wala kivuli, ni jua tu, na vumbi..

Lakini katika sehemu zote hizi, watu waliokuwa na shida kwelikweli walimfuata, isipokuwa ni kwa ugumu sana, kwasababu iliwabidi watembee kwa miguu umbali mrefu, kama tunavyosoma hapo juu, waende mahali ambapo hawajui kama watarudi salama, au mizoga.

Na ndio maana kule nyikani, ilifikia hatua wanawafunzi wake wakamwambia Bwana awaage makutano, waende kujitafutia chakula kwasababu wamekaa naye siku tatu, usiku na mchana, bila chochote, watazimia,…Lakini Yesu alijua ni nini anakitengeneza ndani yao.

Mathayo 14:15 “Hata kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea, wakasema, Mahali hapa ni nyika tupu, na saa imekwisha pita; uwaage makutano, waende zao vijijini, wakajinunulie vyakula”.

Ndugu yangu, pindi unapookoka, ni sawa na ile hatua ya kwanza ya Yesu kukaa nyumbani kwake. Wakati huu Kristo anakuwa karibu sana na wewe, mda wowote utampata, itakuwa ni rahisi yeye kuchukuliana na wewe kwa hali zako zote.. Lakini jambo hilo halitaendelea sana..

Ataondoka nyumbani kwake na kwenda ufukweni.. Hapo ndipo itabidi umfuate. Ukikaa katika mazingira yale yale, miezi inaenda miezi inarudi, huonyeshi bidii yoyote kwa Kristo, wewe mwenyewe utashuhudia tu ukame utakaouona moyoni mwako. Utadhani kwamba Kristo amekuacha, kwasababu ile raha uliyokuwa mwanzo, au vile vitu alivyokuwa anakuonyesha mwanzo vimekata. Ukishaona hivyo, hapo ndipo unapaswa ujiongeze, zidisha bidii yako, kufanya ibada, kuomba, kusoma Neno na kujitenga na uovu. Ukizingatia hayo, utaanza kumwona tena akikufundisha..

Lakini hapo napo hatadumu kwa muda mrefu sana kama unavyodhani.. Atapiga hatua nyingine na kwenda nyikani, pasipokuwa na kitu/watu. Na huko nako huna budi kumfuata.. Hapo ndipo inapokugharimu, kuuaga ulimwengu, inapokugharimu, kupoteza nafsi yako kwa ajili yake,. Unamfuata Yesu hujui kesho yako utakula nini, hujui hatma ya maisha yako itakuwaje, unakubali kupukutika naye pale nyikani, huku ukimsikiliza tu,

Wakati huu usijijali sana, ikiwa unahaja kweli na Yesu.. Kwasababu hatua hii ya kujikana nafsi, inafikiwa na wachache, lakini huku ndipo Kristo anajifunua kwa mtu kwa viwango vingine kabisa. Utaona wale makutano walioweza kustahimili naye, siku tatu kule nyikani, bila kitu chochote, walipata faida mbili, ya kwanza ni kupokea uzima wa milele, na ya pili, ni kugawanyiwa mikate, ambayo waliila na kusaza. Sasa mikate pale inafunua, [rizki zao], maana yake ni kuwa Kristo aliwabariki, rizki zao, kule waliporudi, walipata vingi, kupita kiasi mpaka wakasaza, Kama kulikuwa na muuza genge alipata wateja mara mbili zaidi n.k..yaani kwa ufupi uchumi wao ulirekebishwa na Bwana.(Mathayo 14:19-21)

Lakini hiyo yote ilitokana na nini?

Ni kuwa radhi, kujitwika msalaba wako na kumfata Yesu. Hili haliepukiki kwa mtu yeyote anayemaanisha kumfuata Bwana Yesu. Ikiwa hauwi tayari binti kutupa vimini na suruali, na maurembo ya kidunia, kuukana ulimwengu kweli kweli, huwezi kumwona Bwana katika viwango vingine, ikiwa kijana, upo nusu nusu, vuguvugu, mizaha, na matusi, miziki ya kidunia, kubeti, mipira, punyeto, pamoja na udunia vimekutawala, hapo usiseme nimemwona Bwana.

Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.

35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.

36 Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?

37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?”

Tukizijua tabia hizi za Bwana Yesu, basi tutajifunza kuwa watu wa kupiga hatua kila siku, kumfikia yeye. Kwasababu Bwana hayupo sehemu moja. Tukatae ukristo mgando.

 Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

RABI, UNAKAA WAPI?

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Je! ni sahihi kuning’iniza picha nyumbani mwako kama ya Yesu?

“Bonde la vilio” ni nini katika biblia?(Zaburi 84:6)

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Rudi nyumbani

Print this post

SHAMBA HUWA HALIMTAMBUI WALA KUMSUBIRIA MKULIMA.

Karibu tujifunze hekima, zilizo katika Neno la Mungu, Tukisoma Mithali 24:30-34 inasema..

30 “Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.

31 KUMBE! LOTE PIA LIMEMEA MIIBA; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka.

32 Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana; Naliona, nikapata mafundisho.

33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!

34 Hivyo, umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha”.

Sulemani anaeleza, tukio alilokutana nalo katika shamba la huyu mtu ambaye alimtambua kama mvivu, Na tukio lenyewe lilimtafakarisha sana.. Yeye alidhani, kwa kulala kwake, na  kuchelewa kwake kulilima shamba lake, basi ndio litabakia vilevile, bila chochote kuwepo juu yake. Lakini kilichomstaajabisha ni kuona mazao mengi sana, tena makubwa yaliyostawi, lakini hayakuwa yale aliyoyapanda bali ni miiba.

Kuonyesha kuwa shamba halimsubirii wala halimtambui mkulima, kazi yake ni kuchepusha chochote kile kinachokuja kupandwa juu yake.. Kama ni mchicha, kama ni gugu, kama ni mwiba, kama ni mbigili, kama ni bangi, kama ni tumbaku, haijali kipandacho, hiyo ndio tabia ya shamba lolote Maandiko yanasema hivyo katika (Marko 4:26-29)

Hivyo mtu asipowajibika mwenyewe, kusafisha shamba lake, na kuhakikisha, anayatoa yale yasiyostahili, au analipalilia mara kwa mara, ajue kuwa ataangukia hasara, na mwisho wa siku kazi yake inakuwa bure. Sikuzote kazi nzito ya ukulima ipo katika kupalilia na kulitunza shamba, dhiki ya wavamizi, na magugu, na sio katika kupanda. Kwasababu kupanda kunaweza kuchukua siku moja au mbili basi. Lakini kulitunza shamba ni jambo lingine, linalomgharimu mkulima, kila siku awe anaamka asubuhi na mapema, na mara kwa mara kulitembelea shamba lake, kulitazama na kulipalilia.

Hii ikifunua nini?

Mioyo yetu ni mashamba..Chochote kinachopandwa iwe na Mungu, au ibilisi, au mwanadamu, ni lazima kimee tu, tupende  tusipende.. Hapo ndipo umakini unapohitajika sana, Hii ndio sababu kwanini maandiko yanasema, tuilinde mioyo yetu kuliko yote tuyalindayo (Mithali 4:23). Kwasababu chochote kile kinamea.

Hivyo, ikiwa huna tabia ya kuutazama tazama moyo wako, basi rohoni unatafsirika  kama mvivu wa hali ya juu, unalala,  pale unaposema, aaa, kesho nitasoma Neno, wiki ijayo, nitakwenda Ibadani, hujui kuwa shamba lako (moyo wako), unamea miiba  usiyoijua wewe na viwavi kila siku…

Ndugu kusema nimeokoka tu, hakutoshi, ni lazima kila siku uhakikishe umeongeza jambo jipya katika maisha yako ya kiroho, jiulize, je! Lile Neno ulilohubiriwa au ulilolisoma, umeliishi vipi katika siku yako, au wiki yako yote. Ni lazima ufanye hivyo kila siku.  Usijisahau, ukawa unaikumbuka roho yako, jumapili kwa jumapili, hiyo ni hatari kubwa sana,..Hata hiyo ibada haiwezi kukusaidia chochote, kwasababu magugu ni mengi kuliko ngano, hivyo utalemewa tu, ukristo wako utakuwa ni mzito sana..

Kama hujui kila inapoitwa leo shetani anaturushia mbegu zake mioyoni mwetu, unapopita barabarani na kusikia miziki ya kidunia, unapokuwa ofisini na kusikia lugha za mizaha kwa wafanyakazi wenzako, hizo ni mbegu, unapokuwa shuleni na kusikia matusi kwa wenzako, unapofungua tv, internet, whatsapp, youtube, na kuona mambo yasiyokuwa na maadili, zote hizo ni mbegu, ambazo kama usipozishughulikia mapema ndani ya siku, zitamea tu, haijalishi wewe ni nani…

Hivyo tunazishughulikia , kwa kusali kila siku, kutafakari maneno ya uzima, kujitenga na uovu, kukaa katika utulivu, kuomba rehema, na kujizuia sana. Tukizingatia haya kila siku. Basi mbegu halisi za Mungu tu, ndio zitakazokuwa zinamea mioyoni mwetu. Na matokeo yake tutakuja kula matunda yake baadaye.

Hivyo tusiwe watu, wa kukumbushwa kumbushwa habari za maisha yetu ya kiroho, tuamke usingizini, tuondoe uvivu, tukayatazame mashamba yetu kila siku. Anza sasa kuwajibika kwa kila kitu kinachoukaribia moyo wako, ikiwa hakimpendezi Mungu, hakikisha unashughulika nacho, hadi kiondoke.

Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.

15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana”.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

Rudi nyumbani

Print this post

WENYE KUHADAA ROHO ZISIZO IMARA.

SWALI: Naomba kufahamu biblia inaposema wenye kuhadaa roho zisizo imara ina maana gani? (2Petro 14)

JIBU: Tusome;

2Petro 2:14 “wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, WENYE KUHADAA ROHO ZISIZO IMARA, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana;

15 wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, aliyependa ujira wa udhalimu;

16 lakini alikaripiwa kwa uhalifu wake mwenyewe; punda, asiyeweza kusema, akinena kwa sauti ya kibinadamu, aliuzuia wazimu wa nabii yule.

17 Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa”.

Katika siku za mwisho biblia inatabiri kuwa litatokea kundi Fulani la watu mahususi, lenye kazi ya “kuhadaa roho za watu watu”.

Kuhadaa ni kudanganya, Lakini biblia bado haisemi kundi hili litahadaa kila mtu tu, hapana bali inasema, litahadaa watu “wenye roho zisizo imara”.

Hivyo lazima ujiulize roho zisizo imara ni zipi?

Kwa kawaida kitu kisicho imara ni kitu kisichoweza kudumu kwa muda mrefu, kisichoweza kustahimili mazingira ya mtikisiko, au mazingira magumu kwa muda mrefu kwasababu kimeundwa chini ya ubora. Kwamfano, ukinunua kiatu cha ngozi, na mwingine akanunua kile cha plastiki, mkavitembelea wote kwa pamoja, utaona baada ya muda mfupi kile cha plastiki, kinachakaa na kuisha kabisa, lakini kile cha ngozi kinaendelea kudumu, Kwasababu gani? Ni kwasababu kiatu kile cha plastiki sio imara.

Vivyo hivyo katika roho siku hizi za mwisho, Kuna wakristo walio imara, na wengine ambao sio imara, kuna wenye nguvu ya kudumu katika wokovu haijalishi ni mitikisiko mingapi inawakumba kwasababu hapo mwanzo walimaanisha kweli kweli kumfuata Kristo.. Hawa wana heri sana, ibilisi hawezi kuwahadaa.

Lakini kundi lililo hatarini ni hili  ambalo leo linaokoka kwa Bwana, kesho linarudi nyuma, leo ni moto kesho ni vuguvugu, leo linahudhuria mikesha, kesho linasahau, leo linaeleweka, kesho halieleweki, leo lipo ibadani wiki ijayo halifiki kabisa, likiwa na wapendwa linazungumza habari za Mungu, lakini likikaa na watu wa kidunia, linabadilika rangi, linafanana na wao. Lipo hapo katikati, Kudondoka kiwepesi katika dhambi ni jambo la kawaida kwao, ukiliuliza mbona umefanya hivi litakuambia nimepitiwa tu na shetani.

Sasa watu kama hawa ni lazima shetani atawahadaa tu,kwa hila zake, Na watakapodanganywa hawawezi kufahamu kwasababu wao ni roho zisizo imara. Kama Balaamu alipowahadaa wana wa Israeli, kwa kuwashawishi wazini, na mwisho wa siku Mungu akawapiga kule jangwani,  Pale Edeni Hawa alipodanganywa na nyoka hakujua  chochote, kwasababu moyo wake haukuwa imara kwa Mungu.

Ndugu kama na wewe ni mmojawapo tubu dhambi mgeukie Bwana, kisha maanisha kabisa kumfuata Yesu kwa gharama zozote, Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho. Watu waliovuguvugu Bwana ameahidi kuwatapika, na wewe angalia usitapikwe. Au kudanganywa na ibilisi. Simama imara kwa Bwana. Kataa ukristo feki, au wa juu juu usioingia gharama.

1Wakorintho 16:13 “Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari”.

1Wathesalonike 3:12 “Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;

13 apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

Ni mlima gani Yule Mwanamke Msamaria aliokuwa anaumaanisha? (Yohana 4:19)

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)

Rudi nyumbani

Print this post

Yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.

SWALI: Nini maana ya huu mstari? Hapo anaposema yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.

Mhubiri 10:8

[8]Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake;  Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.


JIBU: Mistari hiyo inawazumgumzia watu ambao wanasababisha matatizo kwa wenzao. Au watu wanaowakosesha wengine waliokuwa tayari katika njia sahihi.

Na ndio maana hapo anaanza kwa kusema mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake..Akiwa na maana kuwa dhara lile unalolipanga kwa mwingine limpate ndilo hilo hilo litakupata wewe.

Mfano wa watu kama hawa katika biblia ni Hamani, ambaye alikua adui wa Mordekai na wayahudi wote, mpaka akafikia hatua ya kumtengenezea msalaba Mordekai, lakini kinyume chake msalaba ule ndio ukamtundika yeye mwenyewe.

Lakini kwenye hicho kipengele cha pili anasema Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.. Maana yake ni kuwa maboma sikuzote hujengwa kwa lengo la kudhibiti maadui, tukiachilia mbali wanadamu, lakini pia wanyama wakali kama fisi, mbweha na nyoka wasivamie mifugo.

Hivyo anaposema abomoaye boma..anamaanisha aondoaye ulinzi wa mwenzake ili maadui kama nyoka wapite, wawadhuru, kinyume chake atadhurika yeye.

Hii ikifunua nini? 

Wapo watu leo hii, wanaoondoa maboma ya watu wengine kwa hila zao. Na maboma yanayomaanishwa hapo si mengine zaidi ya YESU KRISTO. Yeye ndio boma letu, Biblia inasema hivyo..

Zaburi 18:2

[2]BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu,  Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia,  Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.

Hivyo watu watu wanawakosesha kwa kuwalaghai ili ibilisi awameze, wanawazuia wasimwabudu Mungu sawasawa na mapenzi yake, wanawazuia wasimwombe Mungu wao, ili wapoe..lakini kinyume chake wao ndio watamezwa. Na Bwana atawaponya watu wake.

Mfano wa watu kama hawa,ni  wale maliwali wa Umedi waliompangia visa Danieli, ili asimwombe Mungu wake, kutwa mara tatu. Wakidhani kuwa ndio atapotelea mbali kwenye tundu la simba. Lakini kinyume chake wao ndio walimezwa na ibilisi.

Hivyo kamwe usijaribu kumkosesha mtu wa Mungu, wala usijaribu kumwondolea boma lake (Yesu Kristo), ukadhani ndio tayari atarudi nyuma. Wewe ndio utarudishwa nyuma na shetani.

Tusiwe watu wa kusababisha mabaya/madhara kwa wengine. Ndio kiini cha mistari hiyo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UBATILI.

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

Mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post