Category Archive Uncategorized @sw-tz

Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana,

SWALI: Je! maneno tunayoyasoma katika Mhubiri 7:24, yana maana gani?

[24]Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana, ni mtu yupi awezaye kuyatafuta?


JIBU:  Hapo Kuna vitu viwili.. 

1) Yale yaliyo mbali.

       2) Yale yaendayo chini sana.

Akimaanisha yaendayo mbali na upeo wa mwanadamu..na hayo si mengine zaidi ya mambo ya mbinguni, na kuzimu na ya maisha baada ya hapa..yatakuwa na mwonekano gani..picha yake halisi ipoje, miaka bilioni moja kutoka sasa watakatifu watakuwa wanafanya nini?..Hayo hakuna mtu anayeweza kuyavumbua isipokuwa Mungu tu peke yake.

Na yale yaendayo chini sana, maana yake ni yale yaliyositirika kama madini n.k. ambayo yenyewe yanapatikana chini sana. Hivyo vitu vilivyositirika/ siri za Mungu, ni mwanadamu gani anaweza kuzivumbua..

Kwamfano Siku ya unyakuo itakuwa lini, kabla ya uumbaji Mungu alikuwa anafanya nini,  maji yanajaaje kwenye mawingu, yaliyo hewa tu, halafu baadaye yanamwagika chini kama mvua, mifupa unajiumbaje ndani ya tumbo la mama mjamzito, mapigo ya moyo yanadundishwa kwa nishati gani, mpaka  hayachoki n.k Siri hizo anazo Mungu tu hakuna awezaye kuzivumbua..

Ayubu 11:7 inasema..

[7]Je! Wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu?  Waweza kuufikilia upeo wa huyo Mwenyezi?

Soma Kitabu cha Ayubu kuanzia sura ya 38-41, utaona Mungu anamuuliza mwanadamu maswali magumu ambayo mpaka sasa hakuna hata moja lililopatiwa jibu lake.

Hiyo ndio maana ya huo mstari;

Mhubiri 7:24

[24]Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana, ni mtu yupi awezaye kuyatafuta?

Yatosha sisi kumwamini yeye na kulitii Neno lake tu. Kwasababu hata tukijitahidi vipi kwa akili zetu kamwe hatutaweza kuzivumbua siri za ndani za Mungu wetu, isipokuwa yeye mwenyewe atufunulie.

Jina lake BWANA lihimidiwe. milele na milele. Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.

MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO

Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? (Yeremia 17:9)

Rudi nyumbani

Print this post

HUDUMA YA MALAIKA WAWILI.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, ni wasaa mwingine tena Bwana ametupa neema ya kuutafuta uso wake. Karibu tujifunze Neno la Mungu.

Lipo funzo kubwa sana Bwana anatufundisha nyuma ya wale malaika wake wawili aliowatuma sodoma kwa ajili ya kuuangamiza ule mji. Habari tunaifahamu, hakuna haja ya kulitazama tukio lote, lakini tutatazama huduma yao ya mwisho ambayo waliifanya kwa familia ya Lutu.. Hiyo itatufanya na sisi leo hii tuwe makini sana na hii neema ya Mungu tuliyopewa kwa kitambo.

Malaika wale walipomwambia Lutu atoke sodoma, maandiko yanasema,  Lutu akawa ‘anakawia kawia’,..Hata baada ya “kuhimizwa sana” bado akawa anakawia kawia..hapo ndipo ikabidi wale malaika wachukue jukumu wenyewe la kuwatoa kwa nguvu sodoma, kana kwamba ndio wao wenye shida. Tusome;

Mwanzo  19:15 Hata alfajiri ndipo malaika WAKAMHIMIZA LUTU, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. 16 AKAKAWIA-KAWIA; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, kwa jinsi Bwana ALIVYOMHURUMIA, wakamtoa wakamweka nje ya mji..

Biblia inatuambia Kwa jinsi Mungu ‘alivyomhurumia’ Lutu na familia yake, ikampelekea amtoe kwa nguvu kama katoto kanacholazimishwa kupelekwa shuleni kwa kubembelezwa.. Hivyo waliendelea kuvutwa kwa umbali mrefu kidogo.. Lutu na mke wake wakashikwa na malaika mmoja, halikadhalika mabinti zake wawili wakashikwa na malaika mwingine.. Wakati wanatembea Walikuwa wanaweza kuangalia nyuma kama watakavyo na wasiambiwe kitu. Pengine walifika mahali wakawa wanasema tumechoka, wanabembelezwa watembee tu hivyo hivyo, wanafarijiwa, wanatiwa nguvu, Kwani jukumu la wao kuokolewa halikuwa katika uwezo wa mikono yao, bali  wa wale malaika wawili.

Lakini hali hiyo haikuendelea  sana… biblia inatuambia, walipofika nje tu kidogo ya mji..Wakaachwa, na kuambiwa zamu hii, sasa kipengele kilichobakia ni juu yao wenyewe..sisi tumemaliza kazi yetu.

Mwanzo 19:17 “Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, Jiponye nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea”.

Ndipo safari ya kukimbia, ikaanza..Lakini mkewe lutu, akidhani wakati huu ni kama ule wa mwanzo akageuka nyuma akidhani watakuwepo malaika tena wa kumshika mkono,na kumvuta vuta, na kumbembeleza bembeleza kama mwanzoni.. saa ile ile akageuka kuwa jiwe la chumvi.

Maana yake ni nini?

Saa tunayoishi ni wakati ambao sio tena kubembelezewa wokovu kama ilivyokuwa miaka ya kale.. Bali tunaishi ukingoni sana mwa neema ya wokovu. Wakati ambapo tunapaswa tujiokoe nafsi zetu na huu ulimwengu mbovu unaokaribia kuisha.. Pengine utasema umejuaje tupo katika zama hizo za kujiokoa nafsi zetu wenyewe, zama za kukimbia bila kuangalia nyuma, na sio za kuvutwa na Mungu? ,..Ni kutokana na kauli ya Bwana Yesu mwenyewe aliyoisema katika vifungu hivi;

Luka 17:32 “Mkumbukeni mkewe Lutu. 33 Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya”.

Maana yake ni kuwa hakuna kusubiria tena, Mungu akuambie hivi, au akuambie vile, au akufanyie hiki kwanza au kile.. Tayari alishasema na wewe kwamba usiangalie nyuma, kuna kuna kuwa jiwe la chumvi..jiokoe nafsi yako. Hivyo unapokuwa mkristo vuguvugu, unakapokuwa mkristo-jina, ujue upo hatarini sana wakati huu.. unyakuo ukipita leo au ukifa katika hali hiyo usidhani kwamba utakuwa na nafasi ya pili.

Mlango wa neema unakaribia kufungwa kwa watu wa mataifa, na hivi karibuni Yesu anarudi, dalili zote zinaonyesha huwenda kizazi tunachoishi tutayashuhudia yote. Sasa ya nini kuendelea kuufanyia mzaha wokovu,..Yanini kuendelea kuupenda ulimwengu? Ya nini kushikamana na mambo ya sodoma kama mke wa Lutu…

Usipoupokea wokovu wa kweli leo, ujue kesho itakuwa ngumu sana kwako, kuliko siku moja nyuma. Kwasababu neema ya Mungu haidumu milele kwa mwenye dhambi..litambue hilo!

Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.

29 Nao watakuja watu toka mashariki na magharibi, na toka kaskazini na kusini, nao wataketi chakulani katika ufalme wa Mungu”.

Isikize sauti ya Mungu..ikuambiayo jiokoe nafsi yako, mkumbuke mke wa Lutu.

Nyakati zetu ni za hatari sana kuliko nyakati za kale.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

USITAZAME NYUMA!

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Ni SIRI gani Paulo aliyokuwa anaimaanisha katika Waefeso 5:32?

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

Rudi nyumbani

Print this post

Miungu wasio na kikao pamoja na wenye mwili.

SWALI: Wale wachawi walikuwa na maana gani waliposema..”Miungu wasio na kikao pamoja na wenye mwili”?.

Danieli 2:11

[11]Ni neno la ajabu, hili analolitaka mfalme, wala hapana mwingine awezaye kumwonyesha mfalme neno hilo, ila miungu, wasio na kikao pamoja na wenye mwili.


JIBU: Hiyo ni baada ya Mfalme Nebukadneza kutoa mtihani mzito wa kukumbushwa na kupewa tafsiri wa ndoto aliyoiota,..lakini tunaona wale wachawi wote walishindwa kupokea taarifa yoyote kutoka kwa miungu yao..ndipo wakakiri wazi kuwa fumbo hilo, si kila aina na mungu ilimradi mungu tu anaweza kulifichua, bali ni miungu wengine isiyofanya kikao na wanadamu.

Sasa hawa wachawi walitumia neno “miungu”..kwasababu waliamini katika miungu mingi, ndio màana utaona wanatumia neno miungu na sio Mungu asiyefanya kikao na wanadamu…lakini walimaanisha Mungu mmoja ( ambaye ni Yehova) yeye peke yake, ambaye huwa hafanyi vikao na wanadamu.

Sasa aliposema…asiyefanya vikao na wanadamu” maana yake ni kuwa asiyeishi pamoja na wanadamu..yaani Mungu ambaye makazi yake si duniani, bali ni mbinguni.

Miungu yote ya kipagani, makao yao ni hapa duniani, mizimu, mapepo, vibwengo, majini, n.k. vyote hivyo vinaishi katikati ya watu, na vinawategemea watu kutenda kazi zao..vinazurura zurura huku duniani kukusanya taarifa za matukio mbalimbali…havina kitu cha ziada zaidi ya kupeleleza peleleza, kama baba yao shetani (Ayubu 1:7)..

Haviwezi kujua mambo yajayo, haviwezi kutambua siri za ndani za mioyo ya watu..wakati mwingine hata vikitaka taarifa  fulani ya mtu vitakuambia niletee kwanza unyayo, au nywele, jinsi gani vilivyo vidhaifu, havijui, wala havipo kila mahali..na ndio maana wale wachawi walitaka kwanza wasimuliwe ile ndoto..ndio walau wakisie kisie tafsiri yake..

Lakini  Yehova peke yake ndiye ambaye hategemei, mwanadamu, au kiumbe chake chochote kufahamu au kutenda jambo alitakalo,  

Hii ni kutuonyesha kuwa Mungu pekee(Yehova) ndio tumaini la kweli, shetani au vipepo haviwezi kueleza hatma ya mtu. Unapotazama utabiri wa nyota, ujue kuwa umedanganyika, unapokwenda kwa waganga ujue kuwa ndio umekwenda kujitafutia matatizo, unapofanya mila na kuamsha mzimu, ujue unajifungulia milango mwenyewe wa kupelekwa kuzimu.

Zaburi 115:3-9

[3]Lakini Mungu wetu yuko mbinguni,  Alitakalo lote amelitenda.

[4]Sanamu zao ni fedha na dhahabu, 

Kazi ya mikono ya wanadamu.

[5]Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,

[6]Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,

[7]Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake.

[8]Wazifanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia.

[9]Enyi Israeli, mtumainini BWANA; Yeye ni msaada wao na ngao yao.

Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

Kuwiwa maana yake nini katika biblia?

Wasamaria walikuwa ni watu gani?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Rudi nyumbani

Print this post

Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.

SWALI: Huu mstari una maana gani?

Mithali 19:14 “Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana”.


JIBU: Mstari huo unatupa picha kuwa, kumbe vipo vitu vya kurithishwa, lakini pia kuna vitu ambavyo hatuvipati kwa kurithishwa..

Kwamfano, hapo anasema mali; kama nyumba, magari, kazi, hivi vitu mtu anaweza kuvipata kutoka kwa wazazi wake,..Lakini linapokuja suala la MKE MWENYE BUSARA.  Sio jambo la kurithishwa, au kutafutiwa na wazazi, au kupatwa kwa njia ya mali, au kwa uzuri, au kwa cheo, au kwa nguvu..Hapana, bali mke mwenye busara anatoka kwa Mungu tu! Na si sehemu nyingine.

Kumbuka hapo anasema ‘mke mwenye busara’..Sio ‘mke’…ikiwa na maana, ‘mke’ anaweza kupatikana popote tu pale, hata bar, kazini, barabarani, disco, vyuoni, mtaani, n.k. utampata.. Lakini mwenye busara, hatoki pengine isipokuwa kwa Bwana tu.

Mke mwenye busara ni yupi?

Ndio kama huyu aliyezungumziwa katika Mithali 31:10-31..Ambaye sifa zake ni; Kumcha Bwana siku zote, kuwahurumia  maskini na wahitaji, Kuishi vyema na watumwa wake, kuwa msaidizi kwa mumewe, asiye mvivu n.k. Biblia pia inasema katika 1Petro 3:1-6 mke mwenye busara ni Ni mtiifu kwa mumewe, mpole, mtulivu, ajisitiriye, aitunzaye nyumba yake.

Hivyo kumpata huyu, wala usijichoshe kwa njia za vitu au mali. Bali nenda mbele za Bwana, mwombe, mshirikishe, mpango wako, kisha yeye mwenyewe atamsogeza kwako, na utamfurahia.

Kumbuka: Kinyume chake pia ni kweli. Mume mwenye busara, hapatikani pengine popote isipokuwa kwa Bwana tu. Mume mwenye busara, ni Yule amchaye Bwana, ampendaye mke wake, kama nafsi yake mwenyewe, ailindaye familia yake, aihudumiaye nyumba yake.(Waefeso 5:25). Hivyo yakupasa umwombe Bwana, kabla ya kuchukua maamuzi ya kutafuta mke/mume.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Je! taratibu za kufunga ndoa [yaani harusi] ni agizo la Mungu au ni mapokeo tu ya kibinadamu?

MAFUNDISHO YA NDOA.

Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

KUMJUA YESU SI KUPATA UZIMA WA MILELE.

Rudi nyumbani

Print this post

NYAKATI AMBAZO NI LAZIMA TUKUTANE NAZO TU:

Katika maisha bila shaka kuna siku ambazo uliwahi kuamka asubuhi na kuona siku yako inakwenda vizuri sana, una furaha, unafanikiwa, au unautulivu, au unapokea taarifa nzuri mahali Fulani, kazini kwako, kwenye familia n,k. Lakini kuna siku ambazo unaamka huoni uzuri wowote, aidha unaumwa, unaudhiwa na watu, unapata hasara kazini, unapokea taarifa za msiba, unaibiwa, unapigwa, unapata ajali Fulani,  n.k.

Ukiwa kama mwanadamu, nyakati hizi za raha na masumbufu ni lazima ukumbane nazo, haijalishi utakuwa ni mkamilifu kiasi gani.. Na Mungu ameruhusu iwe hivyo, ili kutaka sisi tukue vema katika hali anayoitaka yeye..

Embu tafakari maandiko haya;

Mhubiri 7:14 “Siku ya kufanikiwa ufurahi, Na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote litakalofuata baada yake”.

Mungu ameyaweka hayo yaende sambamba, kwamba hili lisimuache Yule, wala Yule lisimwache huyu..Haiwezekani kila siku utakayoamka asubuhi tu iwe ya furaha,..au iwe ya huzuni tu..hapana,

Sasa kwanini afanye hivyo?

Sababu zipo tatu (3)

1) Ufurahi:

Mungu anapenda kutupa furaha, hivyo zipo nyakati utaburudishwa tu na Mungu, hata kama sio sasa wakati huo utafika tu katika maisha yako. Atakufajiri tu kwa njia zake mwenyewe anazozijua. Atakatiza furaha katika siku Fulani Fulani, au katika kipindi Fulani cha maisha, Hivyo Jifunze kumfurahia Mungu wako wakati unafanikiwa, kwa kumshukuru sana..(Yakobo 5:13)

2) Ufikiri:

Sikuzote mtu huwa anafikiri vizuri anapokuwa katika shida au mateso Fulani, anapopitia kuumwa kidogo, analazwa, hapo ndipo anapojitambua kuwa yeye sio kitu, hawezi kutenda jambo lolote kwa nguvu zake, au kwa mafanikio yake, hivyo hiyo inamfanya sikuzote tumaini lake alielekeze kwa Mungu. Kwahiyo basi ujifunze kufikiri sana unapokuwa katika matatizo au masumbufu fulani, kwasababu ndicho Mungu anachokitaka hapo, zidi kuwa mwombaji, jifunze Biblia, kaa uweponi, ukishindwa kulielewa hilo utakuwa ni mtu wa kulaumu laumu, kunung’unika nung’unika ovyo sikuzote uingiapo katika vipindi hivi.(Wakorintho 8:1-10 )

3) Uwe mnyenyekevu:

Mungu anataka uhai wetu wote, tuumimine mikononi mwake, anataka kila jambo tunalolifanya tuseme BWANA akipenda, (Yakobo 4:13-16 ), anataka tukiamka asubuhi tumwombe kibali cha siku mpya, tunapomaliza siku tumshukuru..Tunapoanza mwezi mpya tumwombe, tunapomaliza tumshukuru, tunapoongeza umri mwingine wa maisha tupeleke shukrani zetu kwake.

Ndivyo Mungu alivyokusudia tuishi. Ni vizuri tuyatambue haya mapema ili tusiwe watu wa kutokuzielewa njia za Mungu wakati mwingine. Tuendelee kumcha Mungu katika majira tuyapitiayo kwa wakati huo,

Anasema pale mema au mabaya yanapokuja tu ghafla, kwa kutokujua mwenyewe..Hiyo inakupa sababu ya kujinyenyekeza, mbele za Mungu, na kumkabidhi Mungu mambo yako yote. Kwasababu hujui kama kesho utakufa au  utaendelea kuishi..Ndio maana pale anasema “ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote litakalofuata baada yake”

Kwa kumalizia tafakari tena maandiko haya;

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;

3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;

5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;

6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;

7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani”.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

Nyakati za kuburudishwa ni zipi? (Matendo 3:19).

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.

Mego ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Mithali 17:1)

Rudi nyumbani

Print this post

HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima.

Nehemia ni mtu  aliyekusudia kutoka katika moyo wake, kwenda kuukarabati ukuta wa Yerusalemu uliokuwa umebomoka, mtu huyu hakuwa nabii, wala kuhani, wala hakujulikana popote, lakini kwa kuguswa kwake moyoni kwa habari alizozisikia kuhusiana na uharibifu ule, aliumia sana, ndipo akajitia nguvu, kumwomba Mungu kibali na baadaye akapewa, na kuweza kwenda Yerusalemu kwa ajili ya kazi hiyo ya kuukarabati. Sasa hatuna muda wa kueleza historia yote, kwa muda wako waweza kusoma habari yake tangu mwanzo hadi mwisho katika kitabu hicho.

Hivyo naamini kwa kuyatazama mapito yake, utapata funzo, hata na wewe ambaye, anataka kuingia katika kazi ya kusimama “mahali palipobomoka” ili upakarabati.

Sasa wakati Nehemia anafika Yerusalemu, ili kuanza operasheni yake ya kuujenga tena ukuta ule, ilimbidi kwanza, atembee, katika malango yote, na sehemu zote za ukuta huo ili atathimini, uharibifu uliotokea, pamoja na nguvu na gharama zitakazotumika kuukarabati tena..

Biblia inatuambia, aliondoka, usiku wakati ambapo watu wamelala, akaanza kuuzunguka ukuta ule wa mji ambao ulikuwa ni mrefu sana, Kuonyesha kuwa mpango bora wa kukarabati kusudi la Mungu, huwa hashirikishwi  kila mtu, bali watu wachache sana tena, waaminifu, ambao wanaweza kuchukua mzigo wako..Tusome

Nehemia 2:11 “Basi nikafika Yerusalemu, nikakaa huko muda wa siku tatu.

12 Kisha nikaondoka usiku, mimi na watu wachache pamoja nami; wala sikumwambia mtu neno hili alilolitia Mungu wangu moyoni mwangu, nilitende kwa ajili ya Yerusalemu; wala hapakuwa na mnyama pamoja nami, ila mnyama yule niliyempanda mwenyewe”.

Anaendelea kusema…

13 Nikatoka nje usiku, kwa njia ya lango la bondeni, nikashika njia iendayo kisima cha joka, na lango la jaa; nikazitazama kuta za Yerusalemu, zilizokuwa zimebomoka; na malango yake yameteketezwa kwa moto. 14 Kisha nikaendelea mpaka lango la chemchemi, na ziwa la mfalme; LAKINI HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

15 Kisha nikapanda usiku kando ya kijito, nikautazama ukuta; kisha nikarudi nyuma, nikaingia kwa lango la bondeni, nikarejea hivyo.

16 Wala mashehe hawakujua nilikokwenda, wala nilivyotenda; wala sijawaambia Wayahudi, wala makuhani, wala wakuu, wala mashehe, wala watu wengine waliokuwa wakiifanya kazi hiyo. 17 Kisha nikawaambia, Mnaona hali hii dhaifu tuliyo nayo, jinsi Yerusalemu ulivyo hali ya ukiwa, na malango yake yalivyoteketezwa kwa moto; haya! Na tuujenge tena ukuta wa Yerusalemu, ili tusiwe shutumu tena.

Hapo mwanzo alipoanza safari,alikuwa na mnyama wake, Ambaye ni farasi/punda.. Mnyama Yule alimsaidia sehemu baadhi tu kufika,na kuona uharibifu uliotokea katika kuta, lakini alifika mahali, ambapo mnyama asingeweza kupita katika penyo zile, bali ni mtu tu! Hapo ndipo ikabidi amwache mnyama Yule, atembee yeye kama yeye, mguu kwa mguu, kutazama sehemu za ukuta, ndogo ndogo, za mafichoni, zilizokuwa zimeharibiwa vibaya sana na maadui zao. Asingefanya hivyo, ukarabati wake ungeishia pale pale punda alipoishia, asingekarabati kote.

Ndipo alipomaliza ziara hiyo, akarejea mjini, na kuwaambia makuhani na wahusika wote, hali ilivyokuwa.

Sasa ni nini Bwana anatufundisha katika habari hii?

Bwana anasema..

Ezekieli 22:30 “Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu”.

Sikuzote kusimama mahali palipomoboka si rahisi, Mungu anatafuta watu hao mfano wa Nehemia hawaoni,,ni lazima tufahamu kuwa zipo gharama kubwa sana, za kukarabati, waweza kudhani, utakwenda na taasisi, au utakwenda na ushirika, au utakwenda na kiwango Fulani cha pesa kwenye akaunti yako.. Hapana vyote hivyo vinaweza kukusaidia kwa muda tu, bali utafika wakati hivyo vyote havitakusaidia, bali itakubidi usimame wewe kama wewe, kama ni kuomba, kama ni kuhubiri, kama ni kukemea dhambi, kama ni kuanzisha jambo..

Mnyama aliye chini yako, hataweza kuvuka nawe, ndugu zako hawataweza kutembea na wewe,katika maono hayo Mungu aliyokupa juu ya kusudi lake, .. Bali ni wewe kama wewe.

Ilimpasa Nehemia afanye hivi, japokuwa alipitia changamoto nyingi, mpaka mbeleni wakawa wanamdhihaki na kumwambia, ukuta unaoujenga jinsi ulivyo dhaifu, hata mbweha wakipita juu yake utaanguka.(Nehemia 4:3), Lakini hakuvunjika moyo, yeye aliendelea  kusimama mpaka mwisho ..

Walipokuwa wanaujenga, mkono mmoja ulishika silaha, na mwingine tofali, waliujenga katika hofu, usiku kucha, Lakini mwishoni ulikamilika, katika utukufu mwingi. Na faida yake ni kwamba hadi sasa tunaisoma habari ya Mtu huyu Nehemia, na kumbukumbu lake lipo hadi leo.(Nehemia 4: 17-23)

Ndugu zipo kuta nyingi sana zilizobomolewa na ibilisi, hadi sasa Bwana anatafuta watu watakaosimama, makanisani kujenga nyumba yake, watakaosimama kwa vijana, kuwaweka kwenye misingi ya imani, watakaosimama kwa familia na watoto kuwafundisha kumcha Bwana. Watakaosimama katika Neno la Mungu, kufundisha injili ya kweli isiyoghoshiwa, na kukemea mafundisho potofu..

Swali ni Je! Sisi tutaweza kusimama na kujenga upya?

Kama ni hivyo basi tuwe tayari hata wakati mwingine kusimama peke yetu, kama Nehemia, pale ambapo hatuona sapoti, uwe ndio wakati wa kusonga mbele, na kuitenda kazi ya Mungu, pale ambapo tunaona vita, na dhihaka, tusife moyo bali uwe ndio tuifanye kazi, usivunjike moyo wala usikate tamaa..Kwasababu Kujenga kuna gharama. Lakini faida zake ni kubwa sana mwishoni.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?

Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?

TIMAZI NI NINI

UFUNUO: Mlango wa 17

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

Neno Buruji lina maana gani katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Amali, na kila kazi ya ustadi, inatokana na mtu kupingana na mwenzake.

SWALI: Naomba kufahamu mstari huu unamaana gani?

Mhubiri 4:4 “Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.


JIBU: Sulemani ni mtu ambaye alipewa na Mungu uwezo wa kutambua hekima ya mambo yote yanayotendeka huku duniani.. Na moja ya jambo ambalo aliliona na kutolea habari zake ni kuhusiana na chanzo cha mafanikio mengi ya watu ni nini?.. Na ndio hapo anasema..

“Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake”.

Kwamba kila utajiri, au kazi za ustadi, yaani nyumba nzuri, magari mazuri, mavazi mazuri, hatua zote za mafanikio, asilimia kubwa hutokana na mtu kupingana na mwenzake, kwa tafsiri iliyo nzuri ni kwamba hutokea mtu kushindana na mwingine..ambacho chanzo chake ni wivu.

Kwamfano, mtu atasema mbona Fulani amenunua gari, mimi sijanunua, ngoja nikakope pesa nifanye kazi juu chini na mimi mwaka huu ninunue la kwangu zuri kuliko lile.. Sasa mtu kama huyu atapata gari kweli, lakini chanzo cha gari lake sio malengo yake, bali ni kwasababu wenzake wanayo magari yeye hana.

Hata mashirika makubwa, kufanikiwa kwao ni kwa mashindano, utaona kampuni moja la simu limetoa ofa hii, kesho lingine linaiga ofa ile ile na zaidi, ili lisipoteze wateja.. Hivyo yamefanikiwa kwa njia hizo hizo, za mashindano.

Tajiri mmoja atashindana na tajiri mwenzake ili awe namba moja, hivyo atafanya kazi kwa bidii usiku kucha, ili asishindwe na mwenzake, watashindana kibidhaa n.k.. Mchungaji mmoja atashindana na mchungaji mwingine kwa wingi wa washirika, au kwa ukubwa wa kanisa,

Sasa hayo yote Sulemani ameyaona na kusema ni ubatili, ni sawa na kujilisha(kuufuata) Upepo. Maana yake ni kuwa mafanikio yanayokuja kutoka katika wivu, au mashindano, hayana afya yoyote kiroho.

Hii inatufundisha nini?

Wafilipi 2:14-15 inasema..

“14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,

15 mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu”

Kama watakatifu, hatupaswi kutafuta kitu chochote kwa kushindana, utasema mwenzangu ana neema kubwa kama ile, ngoja na mimi nikafunge na kuomba nimpite,. Hapana, bali tunapaswa tuishi kwa kumtazama Mungu,kila mmoja katika nafasi yake aliyopewa na Mungu, na kuitendea bidii hiyo, kwasababu kwa kupitia hiyo ndio Mungu atatufanikisha, na sio kwa neema za wengine..

Bwana atubariki.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali share na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Amali” na “Ijara” katika biblia?

Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

Mego ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Mithali 17:1)

Rudi nyumbani

Print this post

JE NI KUTII AU KUPATA KWANZA MAARIFA?

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo Bwana wetu, Karibu tuzidi kuyachambua maandiko;

Mwanadamu anasongwa na mambo mawili pale linapokuja  suala la kuamua hatma ya maisha yake ya milele. Je! Atii au apate maarifa kwanza?. Pale Mungu anapomwambia Usizini? Je, asifanye hivyo? Au achunguze kwanza ni nini kipo nyuma ya tendo hilo, ndipo awe huru sasa kuchagua kuzini au kutokuzini?

Ukweli ni kwamba asili ya mwanadamu ni kutaka maarifa kwanza, ya kitu ndipo baadaye atii, Lakini Je! Biblia inatufundisha nini kuhusiana na maamuzi sahihi na Salama ambayo Mungu aliyaweka kwa mwanadamu.

Tukisoma ile habari ya pale bustanini biblia inatuambia,.. Mungu alipanda miti yake, kisha alipomaliza akatoa maagizo kuhusiana nayo akasema..

Mwanzo 2:16 “Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, 17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika”.

Lakini mwanadamu akaona, hayo maelezo ya Bwana Mungu hayajitoshelezi, kwanini atuzuie tusile, hajui kuwa sisi tunataka tupate sababu kwanza, (tupate maarifa), kujua ni nini kwanza kipo nyuma ya mti huo, ndipo tuwe sasa huru kuchagua kuula, au kutoula. Ndipo wao wakauendea na kuula.

Mwanzo 3:4 “Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, 5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya. 6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni MTI WA KUTAMANIKA KWA MAARIFA, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala”.

Lakini walipofanya vile, hawakuvuna chochote, matokeo yake wakajikuta tayari wameshaingia kwenye matatizo ambayo mpaka sasa tunayashiriki, yale maarifa waliyoyategemea kuwafanya  wawe bora, yakawa mauti kwao.

Hii inatufundisha nini?

Asili yetu sisi wanadamu hatukuumbwa kwenye  kupata maarifa kwanza, ndio tuishi, bali kwenye kutii kwanza.. Ndivyo tulivyotengenezwa na Mungu.. Kwamba tukitembea katika kutii tutakuwa salama sikuzote,..hayo mengine yatakuja baadaye. Ndicho alichokifanya Ibrahimu alipoambiwa akamtoe mwanawe sadaka ya kuteketezwa alitii kwanza, hakudadisi na kusema kwanini huyu Mungu atoe maagizo ya kishetani kama haya ya kuua watu, yeye alitii, ndipo akaja kujua sababu baadaye.

Hii ikiwa na maana kuwa,..Kama Yesu katuambia wazinzi wote, na waongo wote, hawataurithi uzima wa milele, bali sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Tunahitaji nini tena, kutafuta uzuri uliopo nyuma ya uzinzi, mpaka tukaujaribu.au kutafuta eneo la kijeografia la jehanamu, tulione ndio tuamini?

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

Bwana Yesu anasema.. Yeye ndio njia, na kweli na uzima, mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye (Yohana 14:6), FULL STOP!..Sasa  kwanini tutafiti njia zetu wenyewe za kutupa wokovu? Kwanini uishi kwa mitazamo yako, au ya wanadamu, wanaokuambia hakuna mwisho wa dunia, au hakuna maisha baada ya kifo

Katika nyakati hizi za hatari ambazo biblia inazitaja (2Timotheo 3:1), ni lazima “tuongeze maarifa ya kulijua Neno la Mungu, na sio maarifa ya kuyadadisi maneno ya Mungu, kama Adamu na Hawa”..Tutapotea haraka sana, tukiwa watu wa namna hii, kutilia mashaka maneno ya Mungu, kila andiko tunalolisoma, tunasema kwanini iwe hivi, au iwe vile?, kwani kuna shida gani, nikinywa bia yangu na simdhuru mtu? Acha kabisa hayo mawazo ya ibilisi..Utapotea…Wewe tii sasa, sababu utakuja kuzijua mbeleni. Sayansi itakuambia haipo hivyo, ukweli ni huu, mwanadamu wa kwanza alikuwa ni sokwe, uthibitisho umepatikana, hakuna Mungu..Ndugu hapo ndio umepotea kabisa, Kumbatia Neno la Mungu.

Tunapohubiriwa tuache anasa, jambo la kwanza ni kutii, hilo Neno, haijalishi itatugharimu kiasi gani..Tunapohubiriwa tuvae mavazi ya kujisitiri, tuache vimini, tuache rushwa. Tusiulize ulize kwanini..Ni kuweka kando kwanza..Sababu tutakuja kujua huko mbeleni.

Tunusuru roho zetu…Tulipokee Neno la Mungu kama lilivyo.

Bwana atusaidie sana.

Maran Atha.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?

Maana ya watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Bilauri ni nini kibiblia?(Ufunuo 21:11,22:1)

TUYATENDE MAMBO YOTE KWA UZURI NA UTARATIBU.

Je mke wa Musa alikuwa ni Mweusi?

Rudi nyumbani

Print this post

Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

SWALI: Naomba kufahamu maana ya huu mstari;

Mithali 17:17 “Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu”.


JIBU: Huu mstari unaeleza rafiki wa kweli anapaswa aweje, pia rafiki ambaye atazidi  kuwa kama ndugu anapaswa aweje?

Anasema ‘Rafiki hupenda sikuzote’, Ndio.. hii ni tabia ya rafiki wa kweli, hupenda nyakati zote, ziwe ni nzuri , au ni mbaya, kwamfano, rafiki ambaye siku umemfurahisha anakupenda, lakini siku pia umemuudhi anakupenda, siku umempa anakupenda, lakini siku umemnyima bado anakupenda zaidi. Rafiki ambaye wakati mnawasiliana anakupenda, lakini wakati mlipopotezana kimawasiliano kwa muda mrefu bado anakupenda.

Huyo ndio rafiki wa kweli..

Lakini hapo anaposema “Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu” ..Maana yake ni kuwa Yule ambaye anakuwa na wewe bega kwa bega, katika wakati wa shida zako, na taabu zako, na misiba yako huyo si rafiki tena bali ni ndugu..

Unamwona anakujali, wakati unaugonjwa wa hali ya juu, unamwona, anakushika mkono wakati umefilisika, unamwona unakufariji sana wakati wa msiba wako, unamwona anatafuta kila mbinu, kukusogeza mahali wakati upo katikati ya mateso. Huyo ni rafiki aliyefanyika ndugu.

Kwasababu kama hapo inavyosema ‘ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu’..Maana yake ili mtu aitwe ndugu, ni lazima awe amezaliwa mahususi kwa ajili ya siku za shida zako.

Je! Na sisi tunapoitana ‘ndugu’ na ‘rafiki’ tunatambua wito wetu katika hayo?

Lakini tunamwona mmoja ambaye, ni zaidi ya rafiki, ni pia ni zaidi ya ndugu, ambaye sio tu amekuwa karibu na sisi katika shida zetu, na mateso yetu na hukumu zetu.. Lakini pia aliyatoa maisha yake yote, pamoja na uhai wake, ili kufa kwa ajili yetu.

Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”

Hivyo basi, hatuna budi na sisi kuuthamini upendo mkuu namna hii, kwa kukubali kukombolewa na yeye, ili tuoshwe dhambi zetu. Kumbuka hakuna ukombozi nje ya Yesu Kristo, vilevile hakuna uwezekano wowote wa sisi kumpendeza Mungu kwa matendo yetu wenyewe. Na ndio maana ilimpasa aje, ili atukomboe, kutoka dhambini.

Waebrania 2:3 “sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”;

Ikiwa upo tayari kumkabidhi Bwana Yesu maisha yako, basi waweza wasiliana nasi kwa namba zetu hizi, +255693036618/ +255789001312 kwa ajili ya mwongozo huo, bure, na hakika Bwana atayaokoa maisha yako, na kukufanya kuwa mpya tena.

Bwana akubariki.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

RAFIKI MWEMA.

JIRANI YANGU NI NANI?

KAMA VILE UMEME UTOKAVYO MASHARIKI UKAONEKANA HATA MAGHARIBI.

Mretemu ni mti gani?

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Rudi nyumbani

Print this post

WALIKUWA WAMECHOKA NA KUTAWANYIKA KAMA KONDOO WASIO NA MCHUNGAJI.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo.  Nakukaribisha tena tuzidi kuyatafakari maandiko.

Moja ya mambo ambayo, yalimuhuzunisha sana Bwana Yesu ni pale alipowatazama watu wake na kuwaona wanafanana  na kundi la kondoo wafugwao waliopoteza tumaini kabisa na kutawanyika, kila mmoja mahali pake anapopajua yeye..Ina huzunisha sana..

Embu Tusome; kwa utulivu habari hiyo; 

Mathayo 9:35-36

[35]Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.

[36]Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa WAMECHOKA na KUTAWANYIKA kama kondoo wasio na mchungaji.

Hapo biblia inasema walikuwa WAMECHOKA..na KUTAWANYIKA.

Kuchoka kunakozumgumziwa hapo, sio tu kule kwa kutembea umbali mrefu, katika kutafuta  chakula / maji…hiyo ni sehemu ya kwanza..Bali kuchoka kunakolengwa hapo hasaa kunakuja kutokana na kukandamizwa, kujeruhiwa, na kufukuzwa, kutishwa..pamoja na hofu na wasiwasi wa mashaka ya kuraruliwa na mbwa mwitu wakali.

Hii ndio hali halisi yasasa.. Watu wa Mungu WAMECHOKA. Sio kidogo bali wamechoka kwelikweli, Kutokana na kudanyanywa, kuumizwa na watumishi wa uongo, wameharibiwa, wametawanywa.., manabii wa uongo wamechukuliwa fedha zao wakiwaahidia kubarikiwa na kufunguliwa, lakini mwisho wa siku wanajikuta wapo katika matatizo zaidi, wanahangaika huku na kule kutafuta msaada wa kumkaribia Mungu, lakini hawauoni,

 badala wapewe tiba ya Neno la Mungu wanapewa maji ya upako, wanafika makanisani badala wahubiriwe Yesu, wanahubiriwa bikira Mariamu na watakatifu wa kale, na sala za wafu, badala wahubiriwe neema iliyo katika Kristo Yesu, wanahubiriwa siri zilizo ndani ya wachawi.

Imefikia hatua watu wamekata tamaa kabisa, kila mmoja anaona ni heri, asiamini kanisa lolote, ajisalie tu peke yake nyumbani..kuliko kwenda na kusikiliza madanganyo. Ni ni mbaya sana..

Ndio jambo ambalo Bwana Yesu analiona sasa hivi ulimwenguni..na kulihurumia kundi lake  jinsi lilivyotawanyika…na kuonewa sana..

Ikiwa wewe ni mhubiri, halafu hutimizi wajibu wako wa kuwaongoza watu katika njia sahihi..ujue kuwa utawajibishwa siku ile mbele za Bwana.

Kama tunaigeuza  kazi ya Mungu biashara, hatujali maisha ya kiroho ya watu wa Mungu, hata wakija watakavyo kanisani tunaona ni sawa, …tufahamu kuwa tutawajibishwa na Bwana siku ile.

Yeremia 23:1-4

[1]Ole wao wachungaji, wanaoharibu kondoo za malisho yangu na kuwatawanya! Asema BWANA.

[2]Kwa sababu hiyo BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, juu ya wachungaji wanaowalisha watu wangu, Mmetawanya kundi langu, na kuwafukuza, wala hamkwenda kuwatazama; angalieni, nitawapatiliza uovu wa matendo yenu, asema BWANA.

[3]Nami nitakusanya mabaki ya kundi langu, katika nchi zile zote nilizowafukuza, nami nitawaleta tena mazizini mwao; nao watazaa na kuongezeka.

[4]Nami nitaweka juu yao wachungaji watakaowalisha; wala hawataona hofu tena, wala kufadhaika, wala hatapotea hata mmoja wao, asema BWANA.

Tujiulize, sisi tunaosema tumeitwa kumtumikia Bwana.. Ni utumishi gani tunaoufanya? Tunadhani watu wa Mungu watapotezwa sikuzote?

Mungu anajua kuwakusanya watu wake. Na atawanyanyulia watumishi waaminifu. Sawasawa na Neno lake. Lakini sisi wengine tutawajibishwa.

Bwana atusaidie.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

JE! UNAMPENDA BWANA?

USIYADHARAU MARUDIA YA BWANA.

“Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika”,Maana yake nini?

NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post