Category Archive Uncategorized @sw-tz

USIOGOPE KUMWADHIBU MWANAO.

Tunaishi katika ulimwengu ambao, maadili yameporomoka sana, na bado yanaendelea kuporomoka kwa vijana na watoto..Na hiyo inatufanya tuelekeze lawama kwa watoto; tukisema watoto wa siku hizi wamebadilika sana, lakini ukweli ni kwamba wazazi ndio wamebadilika, watoto ni walewale.

Malezo ya mzazi kwa mtoto ni muhimu sana, mtoto si kama nyau, ambaye kitu pekee anachohitaji ni chakula tu na sehemu ya kulala, hata ukimwacha mwaka mzima bila kumjali kwa vingine, hakuna hasara yoyote, bado ataendelea kuwa paka..

Lakini kwa mwanadamu sivyo..yeye hafugwi, bali analelewa..na malezi ni zaidi ya chakula na nguo na mahali pa kulala.. Hapo ndipo wazazi wengi wanashindwa kuelewa.

Kwasababu mtoto atahitaji kuwa na maarifa, nidhamu, uadilifu, hekima, busara, upendo, utiifu, upambanuzi n.k. Ili aweze kuishi vema katika huu ulimwengu.

Hivi vyote hazaliwi navyo, bali anajifunza anapokuwa duniani..hivyo akikosa msaada sahihi, basi ibilisi atatumia fursa hiyo kumfundisha elimu yake na nidhamu yake hapa ulimwenguni.

Hivyo wewe kama mzazi au mlezi una jukumu kubwa sana zaidi ya lile la kumlisha na kumvisha na kumsomesha..hizo ni hatua 3 katika ya 1000, anazopaswa azijue.

Ikiwa hukupata masomo yaliyotangulia ya malezi ya watoto, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba hii, ili tuweze kukutumia chambuzi za nyuma. Au tembelea website yetu hii www.wingulamashahidi.org. au tutumie ujumbe kwa namba hizi +255693036618

Leo tutaona njia nyingine ya kumlea mtoto vema.

Na njia yenyewe si nyingine zaidi ya kutumia KIBOKO.

Lugha hii inaweza isiwe nzuri masikioni mwa wazazi lakini ni tiba nzuri kwa malezo yao. Hata ‘panadol’ haina ladha nzuri mdomoni, lakini pale inapotutibu tunaishukuru, ndio maana tunayo siku zote majumbani kwetu.

Lakini ni kwanini utumie kiboko kwa mtoto?

Sababu zipo mbili.

1) Ni kwasababu ujinga umefungwa moyoni mwake

2) Mungu naye huwa anatuadhibu sisi.

  1. Tukianzana na sababu ya kwanza biblia inatuambia..

Mithali 22:15

[15]Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.

Ni vizuri ukafahamu kuwa mtoto kama mtoto huwa ana ujinga mwingi ndani yake..yule si kama wewe, unapoona anang’ang’ania kitu fulani kisichopendeza halafu wewe kama mzazi unaamua tu kumwachia kisa anakililia, usidhani kuwa anaelewa matokeo ya kile anachokitaka..

Kumbuka yule hatafakari, wewe unatafakari, hivyo basi ukimsikia anatukana, usisubiri apumzike bali hapo hapo shika kiboko chapa. Ukiona unamwagiza kitu hatii, chapa..ukiona hawaheshimu watu wazima hata baada ya kuonywa mara nyingi..chapa..usiogope labda atakufa…biblia inasema kiboko cha adili hakiui..

Mithali 23:13

[13]Usimnyime mtoto wako mapigo; [14] Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

Hiyo itamsaidia sana kuundoa ujinga mwingi wa kipepo ambao mwingine kwa maneno tu, peke yake au kwa kufundishwa hauwezi kutoka..

  • 2) Mungu naye anatuadhibu.

Na sababu ya pili kwanini tuwaadhibu watoto wetu kwa kiboko pale wanapokosea..ni kwasababu Mungu naye anatuadhibu sisi watoto wake.

Biblia inasema hivyo..

Waebrania 12:6-7

[6]Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.

[7]Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?

Umeona..Sisi hatuna hekima ya kumzidi Mungu, tengeneza picha Bwana angekuwa anatuona tunatukana wengine halafu hachukui hatua yoyote anacheka tu..si tungaangamia..Mungu alipomuona Daudi anamchukua mke wa Huria halafu anaendelea kusema wewe ni mtumishi wangu unayeupendeza moyo wangu..Daudi leo angekuwa wapi kama sio kuzimu? Lakini Mungu alimuadhibu vikali…na baadaye akatubu akapona..

Nasi pia biblia inatuambia tutakuwa wakamilifu kama Baba yetu wa mbinguni alivyomkamilifu..(Mathayo 5:48)

Mzazi unayemtazama mwanao, anafanya ujinga, unaogopa kumchapa atalia..bado hujawa mkamilifu kama Mungu.

Hivyo anza sasa kutimiza huduma hii, ili kesho mtoto huyo afanyike baraka na neema kwa ulimwengu.

Lakini zingatia: Haimaanishi kuwa umpige pige mtoto ovyo kila saa anapokosea..hapana zipo sehemu zinastahili kiboko, zipo zinazostahili maonyo, zipo zinazostahili kuelimishwa..Zote zina umuhimu wake mkubwa bila kupuuzia hata moja.

Bwana akubariki

Shalom

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

MALEZI YA MTOTO MCHANGA.

Rudi nyumbani

Print this post

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

Mafundisho maalumu kwa waongofu wapya: Sehemu ya tatu.

Ikiwa wewe ni mwongofu mpya, yaani umeokoka hivi karibuni, basi mafundisho haya yanakufaa sana katika hichi kipindi ulichopo.

Ikiwa ulipitwa na mafundisho ya nyuma, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba zetu hizi +255693036618 tukakutumia mafundisho hayo.

Ni muhimu kufahamu kuwa, unapookoka yupo adui atakayesimama kinyume chako kukupinga wakati wote, ili uiache imani. Na huyo si mwingine zaidi ya shetani. Hivyo katika hatua hizi za awali, huna budi kufahamu silaha madhubuti za kuweza kumwangusha, Kwasababu ukizikosa ujue kuwa utakufa tu kiroho. Na silaha yenyewe tunazisoma katika vifungu hivi;

Ufunuo 12:9 “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.
10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.
11 NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA- KONDOO, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.

Jiulize hapo kwanini haijasema wakamshinda kwa mafuta ya upako, au kwa kanisa zuri, au kwa maombi ya vita.. Bali kwa damu ya Mwana kondoo na kwa neno la ushuhuda wao.
Kuna nini katika damu ya Yesu? Na ushuhuda ulionao?
Ni lazima ufahamu umuhimu wa damu yake, katika maisha yako ya wokovu.
Damu ya Yesu ilifanya mambo makuu matatu

  1. Kuondoa dhambi
  2. Kunena juu yetu
  3. kukanyaga nguvu za ibilisi

1) Kuondoa dhambi.


Biblia inasema..

Waebrania 9:22 “Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo”.

Katika agano la kale Utakaso wa kila namna, ulitegemea damu za wanyama, kwasababu ndio kanuni ya Mungu ya kiroho ya kuondoa dhambi, hivyo tangu zamani zile haikupatikana damu yoyote kamilifu isiyo na hila wala mawaa itakayoweza kuondoa dhambi za mtu moja kwa moja, bila kuacha kimelea chochote. Na ndio maana kumbukumbu la dhambi lilikuwepo wakati baada ya wakati , hivyo ilimpasa kuhani mkuu kila mwaka aingie kule hemani akiwa na damu ya wanyama ili kuwapatanisha wana wa Israeli,
Lakini sasa Yesu alipokuja, damu yake ilikuwa ni kamilifu zaidi ya wanyama, yeye tu ndiye aliyeweza, kusafisha na kuondoa kabisa dhambi ya mwanadamu isikumbukwe na Mungu milele, bila kuhitaji tena kuhani kila mwaka kwenda kuomba rehema kwa dhambi zilizotangulia.


Hii ikiwa na maana gani?
Ukiukosa ufunuo huu, kuhusiana na nguvu iliyopo katika damu ya Yesu iliyomwagika msalabani, basi ni ngumu sana, kuamini kama dhambi zako za kale Mungu alishazifuta na kuzisahau kabisa kabisa.
Ni kawaida kwa waongofu wapya kuletewa mawazo haya na ibilisi kwamba, bado Mungu anawaona ni wachafu, bado Mungu anakumbuka zile dhambi walizozitenda nyuma, zile mimba walizotoa, ule uzinzi walioufanya nje ya ndoa, rushwa walizokuwa wanakula, mauaji waliyoyafanya, waganga waliokuwa wanawafuata.


Hii ndio silaha kubwa ya ibilisi kwa waongofu wapya. Wanajiona kama vile bado hawajasamehewa vizuri, bado laana zinawafuatilia, Ndugu, ujue hayo ni mawazo ya shetani, kwasababu umekosa kujua gharama Yesu aliyoingia kwa ajili ya dhambi zako. Ile damu yake kumwagika, ilikuwa ni kukomesha dhambi zako zote na laana zako kabisa kabisa..


Ndio maana hapo biblia inasema, wakamshinda kwa damu ya mwana-kondoo, na ushuhuda wao, yaani ushuhuda wa kukombolewa na Yesu. Ndio silaha kubwa sana ya kumshinda ibilisi.
Hivyo mawazo kama hayo yakikujia yakatae, sema mimi nimeshasamehewa, ya kale yamepita, tazama yamekuwa mapya. Mimi sina deni la dhambi, Ukifanya hivyo, shetani atajua umeshafahamu nafasi yako, hivyo atakukimbia, na utaishi maisha ya amani na kutojihukumu.


2) Kunena juu yetu.


Damu pia inafanya kazi ya kunena.

Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili”.

Kaini alipomuua ndugu yake Habili, Biblia inasema Mungu alimwambia Kaini sauti ya damu ya ndugu yake inamlilia kutoka ardhini (Mwanzo 4:10). Maana yake ni kuwa Mungu alikuwa anaisikia ili sauti ikinena, ikiomba, ikitaka haki itendeke, haikutulia tu.
Hata leo ukiona mtu anapitia majanga majanga fulani hivi, utasikia watu wakisema, ni kwasababu alimuua mama yake hivyo ile damu inamfuatilia..


Kuonyesha kwamba kuna uhalisia fulani katika damu ya mtu kupatiliza mema au mabaya.
Na ndivyo ilivyo kwa damu ya Yesu, inanena Mema, kuliko ile ya Habili, maana yake, hata sasa inazungumza, juu ya wale wote waliompokea yeye mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Inasema huyu anastahili kulindwa, huyu anastahili baraka, huyu anastahili furaha, huyu anastahili heshima, huyu anastahili kibali, afya n.k.


Hivyo wewe uliyeokoka ni wajibu wako kujua jambo hili, ili usiishi kama yatima hapa duniani. Ulipokuwa dhambini damu ya Yesu ilikuwa haineni juu yako, kwasababu haukuwa ndani ya agano lake. Lakini sasa upo, fahamu kuwa, Yesu anakuombea kila siku kwa Baba, hivyo kuwa na ujasiri ukijua kabisa nyuma yako ipo baraka, neema na habati wakati wote. Kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda utayathibitisha hayo yote.

Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea”.

Hivyo mishale yote ya hofu, wasiwasi, mashaka, ambayo shetani atajaribu kukutumia ili urudi nyuma, ikatae, mishale ya kesho nitaishije, nikipoteza kile kwasababu ya Yesu itakuwaje? ondoa hayo mawazo ya kuangamia, kwasababu ipo damu inayonena kwa ajili yako usiku na mchana, ili utembee katika njia salama ya uzima.

Zaburi 27:1 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?
2 Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka.
3 Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.
4 Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake”.
Lishike sana hili, ukilikosa, shetani atatumia upenyo huu kukurudisha nyuma, kama alivyofanikiwa kuwarudisha wengi.


3) Kukanyaga nguvu za ibilisi.

Utajiuliza ni kwanini Bwana Yesu, hakulisema hili neno “IMEKISHWA”, Mahali popote katika huduma yake, mpaka siku ile alipopelekwa pale msalabani? Ni kwamba alijua hakuna kuzimaliza nguvu na utawala wa ibilisi bila agano la damu timilifu.


Hivyo aliposema IMEKWISHWA, Ni kweli ilikwisha, na ndio maana aliwaambia mitume wake maneno haya;

Luka 10:18 “Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Ni lazima ujue kwa damu ya Yesu, shetani, hana nguvu yoyote juu yako. Kwamfano mwanajeshi dhaifu akitambua kuwa bomu alilonalo la nyuklia linaweza kuteketeza mji mzima, hataweza kuwa na hofu, na wanajeshi 1000 wenye nguvu, wanaomjia na bunduki zao. Kwasababu anafahamu akilituma tu kombora lake moja, kikosi chote kinakuwa jivu.


Ndivyo ilivyo kwako wewe uliyeokoka, fahamu kuwa hatua uliyopo, shetani hana nguvu zozote za kukushinda, kwasababu tayari nguvu zako ni nyingi kuliko zake, haijalishi hali yako ya uchanga kiroho. Hivyo, usiogope wachawi, usiogope mapepo, usiogope hata maadui zako. Lolote linalokuja mbele zako, uwe ni udhaifu, magonjwa, mashambulizi ya shetani, kemea kwa jina la Yesu, vitaondoka, usiwe mnyonge kwa shetani, kwasababu yule ni kama kinyago tu kinasimama hapo kukutisha, lakini hakina nguvu yoyote.
Hivyo zingatia sana kuyatafakari hayo.


Na Bwana akubariki.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

KAA MAJANGWANI.

USIMPE NGUVU SHETANI.

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

Rudi nyumbani

Print this post

KAA MAJANGWANI.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Sehemu ya pili: Kaa Majangwani:

Luka 1:80 “Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu rohoni, akakaa majangwani hata siku ya kutokea kwake kwa Israeli”.

Ni kawaida ya Mungu, kuwaandalia Watoto wake, mahali maalumu pa kukulia kiroho.. Ikiwa unatamani nguvu zako za rohoni ziongozeke kwa kasi wewe kama mwongofu mpya uliyezaliwa mara ya pili, huna budi kukaa majangwani.

Mungu alipowatoa wana wa Israeli Misri, hakuwavukisha moja kwa moja na kuwafikisha Kaanani ndani ya siku moja, bali aliwapitisha kwanza jangwani, kuwalisha huko na kuwakuza kiroho, kwa muda wa miaka 40, kwasababu walikuwa bado ni Watoto wachanga, na ndipo baadaye wakaingia Kaanani, wakiwa Hodari na nguvu nyingi rohoni.

Hosea 11:1 “Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misri”.

Biblia pia inatuambia Yohana mbatizaji alipozaliwa, alikimbilia majangwani huko kuishi, na matokeo yake akakua na kuongozeka nguvu nyingi sana rohoni kwa kasi, na ndio maana hatushangai kwanini Bwana Yesu anamshuhudia na kusema katika wazao wa wanawake hakuwahi kutokea mtu aliyekuwa mkuu kama Yohana Mbatizaji.(Mathayo 11:11).. Hiyo yote ni kwasababu gani? Ni kwasababu alitumia Muda mwingi majagwani.

Sasa Kiroho jangwani ni wapi?

Haimaanishi kuwa ni sisi tukimbilie majangwani tukaishi huko, ili tukue kiroho hapana… Kama tunavyojua jangwani ni mahali ambapo hapana uwepo wa wanadamu, ni mahali pa ukiwa, pasipokuwa na huduma zozote za kijamii.. Ndivyo inavyompasa mkristo aende rohoni.

Unapaswa katika hatua zako za awali za wokovu: Kwa bidii zote uwe tayari, kuukana huu ulimwengu. Kukaa mbali na mambo yote yanayousonga wokovu wako, bila kujali unapoteza nini, au unakosa nini..

Ukiokoka, kubali kuachana na wale marafiki zako wa kale uliokuwa unakwenda nao disco, uliokuwa unakunywa nao pombe, uliokuwa unatukana nao, kubali kuwa mpweke, kwa kipindi Fulani, kwani hivyo ndivyo unavyoiponya roho yako.

Ukiokoka, kubali wakati mwingine, kupoteza hiyo kazi isiyo halali kwa Mungu, kama unafanya biashara ya pombe acha, ..wala usidhani kuwa utaangamia, kwamba Mungu atakuacha ufe, hilo wazo ondoa, uwezo wa kukulisha Mungu anao, Kama alivyofanya kwa wana wa Israeli kule jangwani, atafanya na kwako pia..

Biblia inasema..

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, AENDE ZAKE NYIKANI HATA MAHALI PAKE, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo”.

Umeona, Mungu ameshaandaa mahali pako huko nyikani, pa kukulisha kwa wakati wako na majira yako. Hivyo usiogope wewe uliyemzaa Kristo maishani mwako.

Kama wewe ni binti kubali kukaa mbali na Fashion, kubali kujisitiri na kuchoma hivyo vimini na masuruali, kubali kuonekana umerukwa na akili kwa ajili ya Kristo, hata ulimwengu mzima ukikuona mjinga, kubali hiyo hali, weka kando kila mzigo wa dhambi, kwasababu ndivyo unavyoiponya roho yako.

Je! Faida yake ni ipi?

Faida yake ni kwamba Yesu anapata nafasi ya kukupitisha katika madarasa yake, na kwasababu husongwi na mambo mengine, hivyo kasi yako ya kukua kiroho itakuwa ni kubwa sana..

Maandiko yanasisitiza hilo katika;

Isaya 40:3 “Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, Itengenezeni nyikani njia ya Bwana; Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu”.

Kuonyesha kwamba mahali pekee ambapo utamtengenezea Mungu njia, katika maisha yako ni jangwani.

Leo hii utaona watu wengi wamedumu katika wokovu kwa miaka mingi, lakini huoni mabadiliko makubwa yoyote ndani yao, bado ni wachanga kila siku wanataka wanyweshwe tu maziwa, ni kwasababu gani?

Ni kwasababu hawakumpa Kristo, nafasi ya kuwafundisha majangwani..Walilikimbia jangwa, wakakaa ulimwenguni, na hivyo Bwana akawaacha.

Ndugu/Dada uliyeokoka hivi karibuni usiipuzie hiyo sauti inayokuambia, acha hiki, acha kile, mwache Rafiki yule, acha jambo lile..usiipuuzie kabisa, fanya hivyo, ni sharti upoteze, ili upate baadaye, majira haya ni kujikana nafsi yako, kuichukia nafsi yako, na kujitwika msalaba wako kumfuata Yesu, hilo haliwezi kuepukika ikiwa unataka ukue kiroho kwa kasi anayoihitaji Kristo ndani yako.

Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.

25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.

26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?

27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”.

Kabla ya kumzalia Mungu matunda ni lazima upitishwe jangwani, kutakaswa na Mungu, hivyo kuwa mwepesi kuacha udunia wako. Umfuate Yesu.

Bwana akubariki.

Shalom.

mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA: Sehemu ya 1

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNYAKUO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

Rudi nyumbani

Print this post

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Sehemu ya kwanza: LIA NA NYONYA.

Nakusalimu katika jina kuu lenye uweza la mwokozi wetu Yesu Kristo, sifa na heshima vina yeye milele na milele.

Haya ni Makala maalumu kwa waongofu wapya, ikiwa wewe umeokoka hivi karibuni, au una ndugu/mpendwa ambaye amempokea Bwana Yesu siku za karibuni basi Makala hizi ni muhimu sana kwako au kwa yule mwingine.

Tunaposema kuokoka, tunamaanisha Kuzaliwa mara ya pili. Na mtu anazaliwa mara ya pili, kwa kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu, na pia kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi (Yohana 3:23), na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38), na kwa kupokea Roho Mtakatifu..Kwa kuzingatia hivyo vigezo, basi mtu huyo anakuwa ameshazaliwa mara ya pili.

Lakini sasa hilo peke yake halitoshi, wengi wanapotimiliza maagizo hayo wanajisahau na kudhani ndio tayari wameshatimilika, hakuna cha ziada.. Hawajui kuwa  mtu unaweza ukawa kweli umezaliwa mara ya pili lakini ni kiumbe kilicho kufa.. Utajiuliza ni kwa namna gani inakuwa hivyo?

Mtu anayezaliwa mara ya pili katika roho anafananishwa na mtoto, anayezaliwa mara ya kwanza katika dunia. Kwa kawaida mtoto huyo, ni lazima aonyeshe tabia kuu mbili. Kabla hajaweza hata kuona, au kuzungumza, au kujitambua..Ni lazima

  1. ALIE.
  2. Baadaye ANYONYE.

ALIE kwa sababu gani.. Mtoto anapotoka tumboni kwa mama yake, anakuwa kama kiumbe mfu, wanachofanya wakunga ni kumpiga kidogo, kumshutua ili atoe sauti, wakisikia analia basi wanatambua kuwa kiumbe kilichozaliwa ni hai, hivyo baada ya muda kidogo wanamsogeza katika hatua nyingine,

Ambayo ni kunyonyeshwa.

Cha kushangaza ni kwamba mtoto yule anaposogezwa katika nyonyo la mama yake, hakuna mtu yeyote anayemfundisha kunyonya, utaona ni yeye mwenyewe anajua wajibu wake, wa kula, ndio hapo utaona saa hiyo hiyo ataanza kufyonza maziwa kana kwamba alishawahi kufundishwa huko tumboni jukumu lake kabla hajafika duniani.

Sasa kiroho pia ndio ipo hivyo. Ikiwa wewe umezaliwa kweli mara ya pili, hizi ni hatua za awali kabisa ambazo utazionyesha. Na kupitia hizo sisi wengine tutathibitisha kweli wewe ni kiumbe kipya hai. Kwani  ni lazima utoe kelele fulani rohoni.. Huwezi kutulia, ambao sisi tuliokomaa kiroho tutazitambua, japo wewe hutoweza kuzielewa katika hatua yako ya uchanga rohoni..

Sisi tutaona kuhangaika kwako kutaka msaada wa kumjua Mungu, Na sisi tukishalitambua hilo, basi tunakuwa na wajibu mkubwa sana wa kukusaidia, kukosegezea matiti (Neno la Mungu) unyonye..

Hebu tujifunze kisa cha Musa, pindi anazaliwa..Biblia inatuambia, alipozaliwa, mama yake alimficha ili Farao asimuue, lakini alipoona hali imekuwa  mbaya, alimtengenezea kisafina kidogo, kisha, akamtupa mtoni.. Lakini mtoto yule alipokuwa katika kila kisafina, hakukaa kimya tu, bali alikuwa anapiga kilele, analia,sana na binti Farao aliposikia alikwenda kutazama na kufungua aone ni nini kipo ndani, akakaona katoto, wakakahurumia..Embu tusome kwa ufupi kisa hicho;

Kutoa 2:6 “Akakifungua, akamwona mtoto, na tazama, MTOTO YULE ANALIA. BASI AKAMHURUMIA, akasema, Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania.

7 Basi umbu lake mtoto akamwambia binti Farao, Je! Niende nikamwite mlezi katika wanawake wa Kiebrania, aje kwako, akunyonyeshee mtoto huyu?

8 Binti Farao akamwambia, Haya! Enenda. Yule kijana akaenda akamwita mama yake yule mtoto.

9 Binti Farao akamwambia, Mchukue mtoto huyu, ukaninyonyeshee, nami nitakupa mshahara wako. Yule mwanamke akamtwaa mtoto, akamnyonyesha.

10 Mtoto akakua, naye akamleta kwa binti Farao, akawa mwanawe. Akamwita jina lake Musa, akasema, Ni kwa sababu nalimtoa majini”.

Umeona? Mtoto yule angeangamia kama asingelia, lakini alipolia, akahurumiwa akatafutiwa msaada mapema wa kunyonyeshwa, na hatimaye akakua akaja kuwa Mkombozi wa Israeli, ndiye Musa tunayemsoma.

Ndugu/Dada uliyeokoka hivi karibuni, kutojishughulisha kwako na mambo ya Mungu, kunathibitisha kuwa wewe ni kiumbe mfu, kutoulizia kwako Habari ya ibada, kunatuambia kuwa wewe si kiumbe hai..Hupaswi kujificha, hupaswi kujiepusha na kiongozi wako wa kiimani..hupaswi kukaa mbali na wapendwa, hupaswi kupitisha siku nyingi hujulikani upo wapi, au maendeleo yako ya kiroho hayatambuliki.. kataa hiyo hali kwa nguvu zote..

Wewe tayari ni kiumbe kipya, yatamani sana maziwa ya roho.. Usisubiri kukumbushwa kumbushwa kuhudhuria mafundisho ya kuukulia wokovu, kama mtoto mchanga ambaye hafundishwi na mtu kunyonya ni wajibu wako kutafuta kufundishwa Neno la Mungu, kwa bidi zote..Sio wewe utafutwe.

1Petro 2:2 “Kama watoto wachanga wazaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili k hayo mpate kuukulia wokovu.

Hivyo anza sasa kubadilisha mwenendo wa Maisha yako.. Jifunze kuomba na wapendwa, jifunze, kusoma biblia mwenyewe kuanzia sasa, jifunze kuuliza maswali, jifunze kumshirikisha na kukuonyesha njia sahihi.

Wagalatia 6:6 “Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake up

Hivyo zingatia mambo hayo makuu mawili. Na Bwana akutie nguvu.

Shalom.

Sehemu ya pili itafuata…

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

UMEITIMIZA HAKI YOTE?

ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

kalamu yenye uongo
Wingu la Mashahidi
KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.
Loading
/

SWALI: Mstari huu una maana gani? Je, ni kweli waandishi waliweza kubadilisha baadhi ya maneno ya torati, Na hivyo inaifanya biblia isiamike hadi sasa?

Yeremia 8:8 “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.

JIBU: Hii ni hoja inayotumiwa sana na wapinga-biblia, au wapinga-ukristo. Wakisimamia mstari huu, na kusema, unaona? Biblia ilichakachuliwa, zamani na waandishi wa kiyahudi kwa kuongeza baadhi ya maneno katika torati  iliyoandikwa na mwenyezi Mungu,.. Kwahiyo hiyo inathibitisha kuwa  biblia ni kitabu chenye kasoro..

Lakini je tukisoma vifungu hivyo, vinatuambia waliibadilisha torati?

Kabla ya kuendelea kusoma zaidi, embu tuitafakari tena hiyo kauli hapo mwishoni, anasema  “kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo”. Ahaa Kumbe waandishi ndio wameifanya kuwa uongo..Lakini yenyewe kama yenyewe sio uongo.. Mfano nikikuambia, unanifanya kuwa mwongo mbele za ndugu zangu, haimaanishi kuwa mimi ni mwongo..maana yake ni kuwa, pengine ni kwasababu uliyawakilisha  maneno yangu isivyopaswa, aidha kwa kuongeza chumvi au kupunguza, na kwasababu hiyo basi, mimi nikaonekana nimeongopa, lakini sivyo, mimi nilisema ukweli mwanzo, isipokuwa wewe ndio umeniwakilisha vibaya.

Ndivyo ilivyokuwa hapo, waandishi, ambao kazi yao kubwa ilikuwa ni kufundisha na kuwaelezea watu, walianza, kutoa tafsiri zisizo sawa za torati, na kuwafundisha watu na kuwaandikia, mfano Bwana Yesu alisema, waliipindua amri ya tano;  inayosema waheshimu baba yako na mama yako, na kuwaambia watu, ikiwa kuna chochote umekiweka wakfu hupaswi kumsaidia mzazi wako, hata kama akiangamia kwa njaa ni sawa tu..Jambo ambalo Mungu hakuliagiza hata kidogo, ilikuwa ni wajibu wa kila mtu kumsaidia mzazi wake, awapo katika uhitaji (Soma Marko 7:7-13)

Umeona, sasa tukirudi kwenye ile habari ya mwanzo ili kuthibitisha hilo vizuri, ukiendelea kusoma vifungu vinavyofuata utaona Yeremia, anaeleza kwa undani jinsi kalamu za hao waandishi zilivyoweza kuipa torati tafsiri zisizo sahihi..

Yeremia 8:8 “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.

9 Wenye hekima wametahayari, wamefadhaika na kushikwa; tazama, wamelikataa neno la Bwana, wana akili gani ndani yao?

10 Basi, kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao na mashamba yao nitawapa wale watakaowamiliki; MAANA KILA MMOJA WAO, TANGU ALIYE MDOGO HATA ALIYE MKUBWA, NI MTAMANIFU; TANGU NABII HATA KUHANI, KILA MMOJA HUTENDA MAMBO YA UDANGANYIFU.

11 KWA MAANA WAMEIPONYA JERAHA YA BINTI YA WATU WANGU KWA JUU-JUU TU, WAKISEMA, AMANI, AMANI, WALA HAPANA AMANI.

12 Je! Walitahayarika, walipokuwa wametenda machukizo? La! Hawakutahayarika, wala hawakuweza kuona haya usoni; basi wataanguka miongoni mwao waangukao; wakati wa kujiliwa kwao wataangushwa chini, asema Bwana..

Umeona hapo? Anasema, hao waandishi na makuhani, wanawatabiria watu amani, amani, na kuwaambia mnaishi sawasawa na torati ya Mungu inavyosema, hivyo hamwezi kupatwa na madhara, ili hali ndani yao wanatamani, ni waovu, waabudu masanamu, wanakula rushwa n.k.. 

Wakati torati inakataza vikali vitu hivyo, wenyewe wanawatumainisha watu, Mungu anawapenda, ndio hapo anasema,  wanawaponya jeraha zao kwa juu juu tu, mwisho wa siku  wanaadhibiwa, halafu wanasema Mungu ni mwongo.. Mbona anatupiga bila sababu!.

Je! Waandishi wa namna hii wapo hadi sasa?

Jambo hili lipo hadi sasa katika kanisa la Mungu, Siku hizi za mwisho makristo na manabii wengi sana wa uongo wametokea, nao wanawaponya watu wa Mungu juu juu tu, hawawaelezi ukweli, mpaka inafikia hatua Mungu anaonekana mwongo, hasikii wala hajibu.

Wanawaambia,  utafanikiwa, utabarikiwa, kesho yako ni ya kung’ara kama jua, wanawaambia watoe sadaka nyingi, watumie maji ya upako, mafuta na chumvi, wakati mwingine wafunge mwaka mzima, Mungu atawabariki.. Lakini wanasahau kuwa hao watu wana mizigo ya dhambi, ndiyo inayowafanya wasijibiwe maombi yao.. Kama vile maandiko yanavyosema..

Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.

3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya”.

Hivyo hao watu wanataabika, januari mpaka disemba, lakini hawaona nuru yoyote, hawaona uzima wowote, ndio kwanza hali inakuwa mbaya, mwishoni wanakataa tamaa wanasema Mungu hajibu maombi, wanawageukia waganga wa kienyeji.

Ndugu, Neno la Mungu ni kweli kabisa, akisema atakuponya, atakuponya kweli, akisema atakubariki atakubariki kweli, lakini ni sharti ujue, anataka nini kwanza kwako ili hivyo vyote vikujie.. Anachotaka ni wewe uache dhambi, uache, rushwa, uache uzinzi, uache uongo, uache vimini, uache fashion za kidunia, anasa, uache ulevi, uwe mtakatifu. Ndipo hayo yote yatakapokujia..

Epuka injili zizisogusia dhambi katika maisha yako, ziepuke kama ukoma, hizo huwa zinakuja na maneno mazuri sana ya kushawishi na kufariji, lakini hazitakusaidia chochote, Mungu ni mtakatifu, kamwe hajibu maombi ya mwenye dhambi.

Je! Umeokoka?  Kweli kweli kwa kumaanisha kumfuata Kristo? Kama la! Basi huu ndio wakati wako sasa kuanza upya na Kristo. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi, waweza tupigia kwa namba uzionaza hapo chini.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAJIBU YA MASWALI YANAYOULIZWA NA WASIO WAKRISTO (Sehemu ya kwanza).

Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?

Yesu ni Mungu?, Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?

Nini maana ya “Torati na manabii”?

Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Rudi nyumbani

Print this post

ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?

Atukuzwe Yesu Kristo Bwana wetu milele na milele. Sifa na utukufu ni vyake yeye sikuzote..

Biblia inatuambia, mambo yote yaliyoandikwa katika agano la kale, yalikuwa ni kivuli cha agano jipya la rohoni. Hivyo maagizo mengi ya mwilini, unayoyasoma kule, yalikuwa ni muhtasari wa agano jipya lili bora Zaidi.

Ni sawa na mwanafunzi anayeanza chekechea, ukitaka kumfundisha  Hesabu za KUJUMLISHA na KUTOA, huwezi moja kwa moja ukamwandikia  5-3=2. Ukadhani ataelewa, ni kweli kwa upande wako ni rahisi kwasababu tayari upeo wako ulishatanuka, lakini kwa mtoto, huna budi kutumia njia ya vitendo kwa mwanzoni..

Ndipo itabidi umwekee vijiti, au mawe, ahesabu kimoja mpaka cha tano, kisha aondoe hapo vitatu, ndipo vile viwili vinavyosalia, viwe jibu. Hivyo akilini mwake anajua hesabu ni vijiti na mawe, lakini kihalisia sio hivyo.. Atakapokomaa akili, ndipo atakuwa hana haja ya vijiti, au vidole, au mawe tena.

Vivyo hivyo katika biblia, agano la kale la mwilini lilikuwa ni hatua za awali za kulielewa agano lilibora la rohoni..(Waebrania 10:1, Wakolosai 2:16-17).

Sasa tukirudi katika kichwa cha somo letu. Tufanye nini ili tuonekane safi mbele za Mungu?.

Kumbuka, katika torati Mungu aliwaatenga Wanyama wote katika makundi mawili makuu.

  1. Kundi la kwanza ni Wanyama safi
  2. Kundi la pili ni Wanyama najisi

Sasa ili mnyama aitwe safi, ilikuwa ni sharti, akidhi vigezo maalumu Mungu alivyovioanisha.. Na vigezo vyenyewe zipo vitatu ambavyo ni hivi;

  1. Awe anacheua
  2. Awe na kwato
  3. Awe na kwato zilizogawanyika mara mbili

Ikiwa na maana kama hatokidhi vigezo vyote vitatu, basi huyo mnyama ni najisi, haijalishi atakuwa na kimoja au viwili kati ya hivyo. Hakuruhusiwa, kuliwa, na wengine kufugwa au  kuguswa mizoga yao.

Walawi 11:2 “Neneni na wana wa Israeli, mkiwaambia, Wanyama hawa ndio wanyama wenye uhai mtakaowala, katika hayawani wote walio juu ya nchi.

3 Kila mnyama mwenye kwato katika miguu yake, mwenye miguu ya kupasuka kati, mwenye kucheua, katika hayawani, hao ndio mtakaowala.

4 Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; ngamia, kwa sababu yuacheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.

5 Na wibari, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.

6 Na sungura, kwa sababu hucheua, lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.

7 Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu.

8 Msiile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao; hao ni najisi kwenu.

Sasa utajiuliza ni kwanini, Mungu aliwaona hawafai?

Sio kwamba aliwaona wana sumu kali, au wana madhara wakiliwa, kama wengi wanavyodhani hapana, kwasababu wengi wao wanaliwa hadi sasa, na hakuna madhara yoyote yanayowapata bali alikuwa anatufundisha jambo la rohoni, ili tutakapoingia katika agano jipya tuelewe vema, Mungu anapozungumzia unajisi anamaanisha nini.

Kwamfano, anaposema,

  1. Wasiocheua, ni najisi.

Kucheua ni nini? Ni ile hali ya mnyama kuwa na uwezo wa kukirejesha tena kile chakula alichokimeza na kukitafuta tena, kwa kawaida Wanyama kama ng’ombe, twiga, ngamia, hawa wanakuwa na tumbo la ziada, ambalo linawasaidia kurejesha na kutafuna tena kile walichokila.

Hii inafunua nini sasa katika agano jipya?. Ukiwa si mtu wa kutafakari na kukitendea kazi kile unacholishwa (Neno la Mungu), wewe ni kusikia tu kilasiku, lakini hakuna tendo lolote la ziada unalolionyesha kwa kile ulichofundishwa, huzalishi chochote, mbele za Mungu ni kama mnyama najisi, asiyeweza kucheua, Na kamwe hutoweza kuingia mbinguni (patakatifu pa Mungu), siku ukifa. Mungu anataka tutendee kazi Neno lake, pia tujifunze kuzikumbuka Fadhili zake alizotutendea huko nyuma, tusiwe hasahaulifu. Usahaulifu ni tabia ya unajisi.

Hivyo jiangalie ndani yako je! Wewe ni mtu wa kulitendea kazi Neno la Mungu? Tangu uliopoanza kusikia ni mangapi umeyatendea kazi, Kama sio, basi bado hujawa safi.

2) Awe na Kwato:

Kucheua tu haitoshi, walikuwepo Wanyama wenye uwezo huo kama ngamia, lakini walikosa kwato.. yaani ni kama nyama tu imeshuka mpaka chini, ni sawa na kusema hawana kiatu.

Awe na Kwato:

Hivyo, ni dhaifu kwa upande mmoja, kwasababu wamekosa ulinzi miguuni, ukipita msumari mrefu, basi safari yao imekwisha, hawawezi kutembea kila mahali, penye miiba, hawawezi kuruka, kwasababu miguuni ni wadhaifu.

Tofauti na mnyama  farasi,au swala, yeye ana kwato ndio maana ni mwepesi kutembea popote, ngombe anakwato, ndio maana anaweza kulima hata kwenye mashamba n.k.

Hii inatupa tafsiri gani rohoni?

Waefeso 6:14 “Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani”;

Hapo anasema, ukiwa askari wa Kristo ni lazima ujifunze kusimama ukiwa umejifungia utayari miguuni.. utayari wa nini? Utayari wa kumtumikia Mungu kwa hali zote. Na je utayari huo unatokea wapi? Unatokea kwenye kuisikia injili ya Yesu Kristo, kwa kupitia hiyo tunapokea hamasa, na nguvu na uweza wa kumtumikia yeye.

Wanajeshi, kwa kawaida ni lazima wavae viatu vigumu miguuni waendapo vitani, ili kuwasaidia kukatisha katika mazingira yoyote magumu, vinginevyo wakienda peku peku, hawataweza kwenda mbali

Halikadhalika na wewe, ukiwa umejivika UTAYARI huo wa kumtumikia Bwana katika mazingira yoyote, rohoni unaonekana kama ni mnyama mwenye kwato. Unafaa kwa kazi,

3) Mwisho, kwato ziwe zimegawanyika.

Wapo Wanyama ambao walikuwa wanacheua, walikuwa wana kwato, lakini kwato zao zilikuwa hazijagawanyika mara mbili. Hapo bado walikuwa ni najisi.

kwato zilizogawanyika

Ni kwanini, Bwana alitaka kwato za mnyama zigawanyike mara mbili, ili waonekane safi?  Ni siri gani ipo nyuma yake?

Kama tulivyotangulia, kuona kwato, Ni utayari tuupatao katika injili…

Lakini lazima tujifunze kuligawanya Neno la Mungu. Ndio maana biblia inayo agano la kale na jipya. Ili tuweze kuwa askari kamili ya Kristo, hatuna budi kufahamu kuweka injili ya Kristo kama atakavyo yeye, kwa uongozo wa Roho Mtakatifu.

Kwa kukosa, kuelewa ufunuo uliokatika agano lake, ndio inayopelekea, watu kufundisha kuwa vyakula ni najisi kwasasa..

1 Timotheo 4 : 1-5

1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.

4 Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani;

5 kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.

Wengine wanaona Ibrahimu, Daudi, wameoa wake wengi, anadhani ndio hata sasa ndivyo ilivyo, na Mungu anapendezwa navyo. Hawajui ni ufunuo gani ulikuwa nyuma yake.

Hivyo biblia inatutaka sana tujifunze kuligawanya vema Neno la Mungu. (2Timotheo 2:15).

Ni muhimu sana. Na hiyo inamuhitaji Roho Mtakatifu.

Hivyo kwa kukidhi vigezo hivi vitatu; 1) Kutendea kazi Neno la Mungu 2) Kumtumika kwa Bwana 3) Kuwa na maarifa ya Neno la Mungu. Basi utakuwa mnyama safi mbele za Mungu.

Na hivyo tutamkaribia Mungu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Lumbwi ni nini katika biblia?

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Bwana alimaanisha nini aliposema enendeni mkaihubiri injili kwa kila kiumbe?

Maji ya Farakano ni nini katika biblia?

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi nyumbani

Print this post

Liwali ni nani?

Liwali ni mkuu wa mji au jimbo Fulani. (Gavana).

Kwamfano katika biblia tunaona, Pontio Pilato anatajwa kama Liwali wa Uyahudi sehemu ya kusini mwa Israeli,. Hivyo eneo lote la uyahudi yeye ndiye alikuwa kama mkuu wa majimbo hayo.

Mwingine ni Yusufu, biblia inasema, Farao alimweka kama Liwali wa nchi yote ya Misri.

Mwanzo 42:6 “Naye Yusufu alikuwa ni liwali juu ya nchi, ndiye aliyewauzia watu wote wa nchi. Nao ndugu zake Yusufu wakaja, wakainama kifudifudi mbele yake”.

Hivyo kazi yao haswaa ilikuwa ni sawa na ya wakuu wa mikoa wa sasa, au majimbo, ambapo kimsingi wanakuwa na mamlaka ya kuongoza shughuli zote za jimbo hilo kwa amri yao, wala hakuna chochote kinachoweza kufanyika bila idhini yao.

Hivi ni baadhi ya vifungu vya Zaida ambavyo utaweza kukutana na hilo neno;

Mathayo 27:1 “Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua;

2 wakamfunga, wakamchukua, wakampeleka kwa Pilato aliyekuwa liwali.

Mathayo 28:14 “Na neno hili likisikilikana kwa liwali, sisi tutasema naye, nanyi tutawaondolea wasiwasi.

15 Basi wakazitwaa zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Na neno hilo likaenea kati ya Wayahudi hata leo”.

Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;

7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu”.

Matendo 18:12, 23:24, 26:30

Ni nini twaweza zingatia  kuhusu hawa maliwali?

Bwana Yesu alisema, katika utumishi wetu, utafika wakati, tutaitishwa mbele ya mabaraza ya wafalme, na maliwali, kushitakiwa.Hivyo tukijikuta  katika mazingira kama hayo hatupaswi kuogopa, kwasababu Kristo ameahidi kuwa atakuwa na sisi katika mapito yetu yote.

Mathayo 10:18 “nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”.

19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

20 Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu”.

Bwana akubariki.

Je! Umeshamkabidhi Kristo Maisha yako?. Kama jibu ni hapana, na upo tayari kuokoka leo. Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba, >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Au tutafute kwa namba zetu hapo chini, kwa msaada huo.

+255693036618/+255789001312

Mada Nyinginezo:

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?

Mjoli ni nini/ ni nani katika biblia?

Mharabu ni nani katika biblia?

Bawabu ni nani/nini?

Mapooza ni nini? Na je! Twawezaje kuepukana nayo?

Rudi Nyumbani

Print this post

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

Akida ni mkuu wa majeshi ya zamani, hususani majeshi ya kirumi. Akida mmoja alikuwa anaongoza kikosi cha askari 100,. Maakida wengi walikuwa wanachaguliwa na watalawa wao wakuu moja kwa moja toka Rumi,wengine katika mabaraza, wengine kutoka kwa maliwali, na wengine moja kwa moja kwa kupandishwa vyeo, baada ya kutumika kwa muda mrefu (miaka 15-20), katika shughuli za kijeshi.

Kazi yao kubwa ilikuwa ni kusimama mstari wa mbele katika vita kuliongoza kundi lote jeshini, pia kutekeleza mauaji ya wahalifu, au washitakiwa, mfano wa hawa ni Yule akida aliye simamia mateso na mauji ya Bwana Yesu pale Kalvari

Marko 15:39 “Basi yule akida, aliyesimama hapo akimwelekea, alipoona ya kuwa alikata roho jinsi hii, akasema, Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu”.

Pia walikuwa wanafanya kazi ya kutoa mafunzo ya kijeshi, kugawa majukumu, kusimamia ujenzi wa ngome na kuta za ulinzi za taifa. Walifanya pia kazi ya kuwalinda wafungwa na kuwahakikishia ulinzi wao pindi wasafirishwapo, Mfano wa Hawa, soma .(Matendo 23:23, 24:23, )

Pamoja na hilo, maakida wengine walikuwa ni watu wakatili, na wapenda rushwa,

Lakini ni jambo  gani Mungu anataka tujifunze nyuma ya watu hawa?

Ijapokuwa kazi hii, si kazi iliyoonekana kumrudishia Mungu utukufu, Lakini bado tunaona wapo maakida, kadha wa kadha katika biblia, waliompendeza Mungu katika utumishi wao, zaidi hata ya wayahudi wengi, waliokuwa wanajiona washika sheria na torati.

Kwamfano utaona Bwana Yesu alipokuwa katika ziara zake za kuhubiri na kufungua watu, alikutana na akida mmoja, ambaye aliustaajibisha sana moyo wake kwa imani aliyokuwa nayo, mpaka Bwana akasema hata katika Israeli,hakuna aliyekuwa na imani kubwa kama yake.

Mathayo 8:5 “Hata alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia,

6 akamsihi, akisema, Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana.

7 Yesu akamwambia, Nitakuja, nimponye.

8 Yule akida akamjibu, akasema, Bwana, mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu; lakini sema neno tu, na mtumishi wangu atapona.

10 Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, Sijaona imani kubwa namna hii, kwa ye yote katika Israeli.

11 Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;”

Utaona pia, kulikuwa na akida mwingine, aliyeitwa Kornelio, huyo alikuwa anatoa sadaka nyingi sana, na kuwasaidia watu, mpaka siku moja malaika wa Bwana anamtokea na kumpa maagizo ya kufanya ili aupokee wokovu kamili.

Matendo 10:1 “Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,

2 mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima”.

Umeona? Ni nini Mungu anataka tujue?

Ni kwamba Mungu hatazami sana mahali unapotumika, lakini anatazama uaminifu wako, moyo wako, utakatifu wako, bidii yako kwake. Unaweza ukawa unafanya kazi serikalini, lakini ukamtumikia Mungu vema, kwa kukataa rushwa, na kutenda haki, na Mungu akapendezwa nawe..Mfano wa Danieli, Maadamu, upo mahali ambapo hapakinzani na sheria ya Mungu na taifa, usijisikie vibaya kutumika unachopaswa kufanya ni kumtumikia tu Mungu kwa uaminifu wote, kuangaza nuru yako ya wokovu kwa wale watu, na kumpenda yeye na kukataa njia zote mbaya zinazokinzana na Neno lake.

Kwa kufanya hivyo Basi Mungu atakutumia kutimiza kusudi lake, alilolikusudia juu yako, na watu wake, mfano wa Kornelio na Yule akida ambayo alidhubutu hata kuwajengea wayahudi sinagogi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

ORODHA YA WAFALME WA ISRAELI.

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Mshipi wa dhahabu matitini ni nini?

Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Rudi nyumbani

Print this post

Sifa ni nini?

Sifa ni kitendo cha kumshuhudia Mungu, au kuyasimulia matendo makuu ambayo ameyafanya au aliyonayo, na huwa inaambata na mguso wa ndani unaomfanya mtu arukeruke, acheze, afurahie, aimbe, ashangalie, apige kilele kwa nguvu, kwa hayo aliyoyaona kwa Mungu wake.

Kwamfano tunapoona jinsi, mbingu na nchi, jua na mwezi, na milima na bahari, vilivyoumbwa kwa uweza na ukuu wa ajabu, hapo tunapata sababu ya kumshuhudia Mungu, au kumtangaza kwa namna zote aidha kwa kumwimbia, kushangalia kwa sauti ya juu,

Au labda ulikuwa na shida Fulani labda ugonjwa, ukaponywa, au hitaji la kazi, nyumba, chakula ukapatiwa na yeye. Hapo ndipo unapopata sababu ya kuyatangaza maajabu yake, kwa kumwimbia kwa nguvu sana. Hizo ndio sifa.

Mungu anasema..

Zaburi 68:32 “Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, Msifuni Bwana kwa nyimbo”.

Zaburi 117:1 “Haleluya. Enyi mataifa yote, msifuni Bwana, Enyi watu wote, mhimidin.

Zaburi 147:1 “Haleluya. Msifuni Bwana; Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri”.

Biblia inatuambia viumbe vyote na uumbaji wote, vinamsifu Mungu. Kwanini na sisi tusimwimbie yeye sifa zetu?.  Embu tazama pumzi uliyopewa bure, embu tazama mapigo ya moyo yanayodundishwa ndani yako bila tozo lolote, embu tafakari jua unaloangaziwa na Yehova. Kwanini usimsifu yeye?

Bwana anaketi juu ya sifa.. (Zaburi 22:3), Na yeye pekee ndiye anayestahili kuabudiwa.

Hivyo wote wamsifuo kwa Roho na Kweli, yeye yupo juu yao. Katika sifa kuta za Yeriko zilianguka, , \vifungo vya Gereza vililegezwa Paulo na Sila walipokuwa gerezani, katika sifa maadui waliuliwa bila vita yoyote kipindi cha Mfalme Yehoshafati.  Nasi pia tukiwa watu wa sifa, ni maombi tosha ya kutuweka huru na kutufungua.

Bwana atupe macho ya kuliona hilo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)

Mwana haramu ni nani kibiblia? (Kumbukumbu 23:2).

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Kinubi ni nini katika biblia? (1Samweli 16:16, 23)

BARAGUMU NI NINI?

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Ulafi ni nini kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

Ukienda kuomba kazi yoyote halali, kikawaida huwezi kupewa majibu ya papo kwa papo na kuambiwa anza kazi leo, bila ya kutaka kwanza taarifa Fulani kutoka kwako, hata kama ni ile ndogo ya kufagia, vipo vigezo  vitaambatanishwa tu na kazi hiyo, aidha utaulizwa umri wako, au hali yako ya kiafya, au fani uliyonayo, au jinsia yako, au elimu yako n.k. Lakini ikiwa hujasoma vigezo vyao, halafu ukapeleka maombi yako kienyeji, Ni wazi kuwa barua yako itatupwa kapuni.

Vivyo hivyo na kwa Mungu, tunapopeleka maombi yetu, ni sharti tujue vigezo vya kujibiwa, vinginevyo, tutabakia kumlaumu Mungu, mbona tulifunga, na kukesha lakini hujasikia maombi yetu.

Hivi ndio vigezo vikuu vya maombi yetu kujibiwa na Mungu

  1. Kaa mbali na dhambi:

Hili ndio jambo la kwanza na la msingi; Dhambi ndiyo inayomdhoofisha Mungu, na kumdumaza kwenye eneo la kujibiwa maombi yetu.

Isaya 59:1 “”Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”.

Hakikisha unakaa mbali na mambo yote yanayomchukiza Mungu, yaliyo ndani yako, mfano uzinzi, ulevi, uongo, rushwa, wivu, matusi n.k.

  1. Omba vizuri:

Kuomba vizuri, sio kupangalia maneno katika uombaji, hapana, bali kuomba jambo linalotimiza mapenzi ya Mungu.

Yakobo 4:2 “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!

3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.

Jiulize unachokiomba je kina  lengo gani, ni ili umkomoe yule adui yako?, au ili ukaongezee mtaji wa ile biashara yako ya bar?, au ili uonekane mwanamke wa kisasa mfano wa Yezebeli? Kama sivyo  ni Ili nini?..Fahamu kuwa Mungu anachunguza mioyo. Hakikisha unachokiomba ni kwa utukufu wa Mungu. Vinginevyo hutapokea chochote.

    3. Usiombe ili utazamwe na watu unajua kuomba:

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 6:5 “Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.

6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Mawazo yako yanapaswa yamwelekee Mungu, na sio Mungu Pamoja na wanadamu. Ukilijua hilo, basi hutaona sababu ya kujionyesha kwa watu ili wakupe utukufu.

     4. Omba kwa bidii:

Ukweli ni kwamba yapo maombi utahitaji kuonyesha bidii kwa Mungu ili uyapate, na sio kuomba dakika 5 halafu basi, hapo unaweza usipokee chochote, bali yakupasa kung’ang’ana mbele za Mungu ndipo yaje kutokea.

Yakobo 5:16 “… Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.

18 Akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake.

Hivyo ongeza misuli yako ya maombi. Hata ya masafa marefu na mikesha.

    5.  Usikate tamaa:

Yakupasa ujifunze uvumilivu. Uvumilivu ni muhimu sana ikiwa hujajibiwa leo, haimaanishi kuwa Mungu hajakusikia, bali omba tena kesho, na kesho kutwa, kwasababu ipo sababu kwanini hujakipata kwa muda huo.

Luka 18 : 1-8

18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”?

    6. Jifunze kumtolea Mungu:

Ni jambo dogo, lakini linamatokeo makubwa sana rohoni. Sio kwamba Mungu anahaja na fedha zetu hapana, lakini umtoleapo unaonyesha upendo wako kwake. Ukipeleka maombi yako kwake, jijengee utaratibu pia wa kuambatanisha na sadaka, kwa kile ulichojaliwa, ikiwa ni senti mbili, au milioni 10, mpelekee Bwana. Wengi waliotenda hivi walifanikiwa.

Malaki 3:10 “”Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la”.

Hivyo kwa kuzingatia, mambo hayo sita, basi ni hakika Mungu atakujibu maombi yako. Na utamfurahia yeye.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?

Namna ya kuomba

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!

Rudi nyumbani

Print this post